You are on page 1of 12

Sauti ya Waislamu

Mkuu wa Shule adaiwa kuhujumu wanafunzi wa Kiislamu Bagamoyo


Awapachika u-Al Qaidah apate kuwafukuza Wanafunzi Wakristo watoweka kimya kimya Mkuu wa Mkoa aingilia kati, afunga shule

ISSN 0856 - 3861 Na. 1044 Dhuul-Hijja 1434, IJUMAA NOVEMBA 9 - 15, 2012 BEI TShs 500/=, Kshs 50/=

Shari iliyokusudiwa ni kubwa mno, lakini. Wanaotamani kuona vurugu wataumbuka Sheikh Mataka, haya ya Askofu hujasikia? Uk. 6

Waislamu kuweni makini

Maaskofu Pentekoste waongo


Na Shaaban Rajab
HAKUNA Kanisa lililochomwa Yombo Dovya kama walivyodai baadhi ya Maaskofu. Uchunguzi wa gazeti hili pamoja na ule wa Serikali za Mitaa, eneo hilo, umebaini

Hakuna Kanisa lililochomwa Yombo Mishale, mikuki wanamwandalia nani? Labda somo la Rwanda bado halijaeleweka

HAYA ni Makanisa yaliyodaiwa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa yamechomwa moto huko Yombo Dovya jijini Dar. Picha ya juu ni Kanisa la Faraja International lililopo mtaa wa Uwazi, Yomnbo Dovya. Picha chini ni Kanisa la Walokole lililopo katika mtaa wa Njia Panda kwa Kombo, Yombo Dovya.

Maalim achua mambo mazito

kuwa taarifa hizo ni urongo na uzushi mtupu. Awali Maaskofu chini ya Umoja wao unaojulikana kama Baraza la Makanisa ya Kipentekoste Tanzania (PCT) walitoa taarifa wakisema kuwa wamegundua mpango Inaendelea Uk. 4

Vipigo, udhalilishaji wananchi Unguja: Amri kutoka Dodoma? Shein lawamani

2
S.L.P. 55105, Simu: +022 2400786 Cel: 0784 370 208, 0755 260 087 0713 110148, DSM. www.ipctz.org E-mail: annuurpapers@yahoo.co.uk Osi zetu zipo: Manzese Tip Top Usangi House (Jengo dogo), barabara ya Morogoro, D'Salaam

Tahariri/Habari
AN-NUUR

Dhuul-Hijja 1433, IJUMAA NOVEMBA 9 - 15, 2012

AN-NUUR

Maalim achua mambo mazito


Na Mwandishi Wetu
MAALIM Seif Shariff Hamad ametoa kauli ambayo inaashiria kuwa vipigo vilivyokuwa vikiwashukia Wazanzibari kutoka kwa Polisi na Vikosi vya SMZ, ilikuwa ni katika kutekeleza maelekezo kutoka Dodoma. Sasa haya yanayofanyika ndio matokeo ya kikao hicho (kilichofanyika Dodoma hivi karibuni) kwa sababu Polisi wanalaumiwa hawajachukua hatua, sasa hivi ndio hao wanachukua hatua lakini wanafanya udhalilishaji mkubwa sana wa ukiukwaji wa haki za binaadamu, wanawapiga watu ndani ya majumba yao, watu wanahama majumba yao kutokana na unyama wanaofanyiwa mtu anapigwa mbele ya watoto wake mbele ya mkewe na kudhalilishwa. Jee, Rais haya hayaoni? Alihoji Maalim Seif. Katibu Mkuu huyo Mkuu wa Chama cha CUF na Makamo wa Kwanza wa Rais alimshutumu Rais Kikwete na Dk. Shein pamoja na watendaji wake huku akieleza masikitiko yake ya kufanya kikao kikubwa Dodoma kinachohusu masuala ya nchi bila ya kumshirikisha yeye kwa kisingizio cha kipengele cha katiba kutomtambua. Maalim aliyasema hayo alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Kibanda Maiti na kuhudhuriwa na maelefu ya watu. Katika mkutano huo Maalim Seif amesema kuwa vipigo na hujuma wanazofanyiwa wananchi, ni moja ya njama za watu wasioitakia mema Zanzibar ambao wanataka kuharibu maelewano yaliyopo hivi sasa. Akasema kuwa mbinu za watu hao zimeshatambuliwa na kwamba kamwe Wazanzibari hawatakubali kurejeshwa walipotoka kwa kuvurugiwa kwa serikali yao. Akiwahutubia wafuasi wa chama chake alisema mpango huo hauwezi kuwa na mafanikio kwa kuwa serikali ya umoja wa kitaifa imepewa baraka zote na Wazanzibari wenyewe kwa kuichagua kwa kura nyingi za maoni na pia serikali hiyo ipo kikatiba hivyo haiwezi kuvunjika. Amesema, katika hali inayozua maswali mengi na kushangaza, vipigo na udhalilishaji wanaofanyiwa wananchi, umekuja mara baada ya kikao cha Dodoma kilichozungumzia vurugu zilitokea Zanzibar. Akasema, katika kikao hicho Polisi walilaumiwa kuwa hawakuchukua hatua za kukabiliana na vurugu zilizotokea na matokeo yake ndio hivi vipigo vinavyowashukia wananchi wasio na hatia. Viongozi wa ngazi ya juu wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa wote walikuwepo kasoro mimi, walishirikishwa kuandaa mpango huo, lakini kila likuepukalo lina kheri nalo na mimi bora nilipokuwa sikuwepo kwa sababu hata siku moja nisingebariki suala hilo. Alisema Maalim Seif akionyesha kuwa viongozi wa ngazi za juu za serikali wanahusika na idhilali inayowapata wananchi hivi sasa. Akivitaja vikundi ambavyo vinafakazi na polisi, na kutekeleza mpango wa kuvuruga Serikali ya Umoja wa Kitaifa kwa kuwadhalilisha wananchi ni pamoja na kikosi cha Janjaweed, Ubayaubaya, Kimyakimya, Mbwa mwitu na Mbwa mkali ambao wote ni vikundi vilivyopewa mafunzo na sasa vinawafunza watoto wadogo kufanya uharamia. Akizungumzia athari zilizopatikana baada ya Jeshi la Polisi kuzima vurugu zilizotokea Oktoba 17 Zanzibar, alisema kumetokea madhara ya kiuchumi, kijamii na kisiasa kwa Zanzibar kutokana na vyombo vya dola kutumia nguvu ya ziada kudhibiti vurugu hizo. Aidha, alisema hatua za kurejesha amani wakati wa vurugu hizo hazikuwa muafaka, kutokana na nguvu iliyotumika ilikuwa kubwa kupita kiasi na hatua hizo ziliwadhalilisha wananchi wasiokuwa na hatia na mali zao kuhujumiwa, huku wengine wakipoteza maisha. Tunalaani mauaji yalofanywa kwa polisi lakini pia tunalaani udhalilishaji unaofanywa na Jeshi la Polisi dhidi ya raia na hatuungi mkono kabisa unyanyasaji wanaofanyiwa wananchi hasa katika maeneo maalumu ambao yanajulikana ni maeneo ya wafuasi wa CUF kwa nini iwe hivi? Alihoji Maalim Seif. Maalim Seif alisema serikali na vyombo vya dola vitekeleze jukumu la kulinda haki za raia kwa kuwasaka wanaohusika na uhalifu bila kuwadhalilisha wananchi wasiokuwa na hatia. Alisema hakutarajia vitendo vya aina hiyo kutendeka wakati huu ambapo mfumo wa serikali ya Zanzibar unaendeshwa kwa kuzingatia maridhiano ya kisiasa baina ya CUF na CCM ambayo lengo lake ni kumaliza uhasama na chuki na kujenga amani pamoja na kuheshimu utawala wa demokrasia. Maalim Seif Sharif Hamad alitumiam mkutano huo wa mwisho wa wiki iliyopita kujenga hoja kuwa kuna mpango maalumu unaofanywa na baadhi ya watu wenye lengo la kuvuruga Serikali ya Umoja wa Kitaifa (GNU) visiwani Zanzibar. GNU is there to stay, na mimi ndio Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, mpango wao hautafanikiwa tumeshawagundua, alisema Maalim Seif huku akishangiliwa na wafuasi wake. Wale wenye ndoto kuwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa itavunjika, yagujuuu hatutoki, hatutoki na ili serikali ya umoja wa kitaifa itoke, basi kuitishwe kura ya maoni. Alisema. Maalim Seif alidai kuwa vitendo vinavyofanywa hivi sasa na Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Vikosi vya SMZ dhidi ya raia wasio na hatia, ni miongoni mwa mipango ya

MAONI YETU

Akizungumza mbele ya waandishi wa habari hivi karibuni, Katibu Mkuu wa Baraza la Makanisa ya Kipentekoste nchini Ta n z a n i a ( P C T ) , Askofu David Mwasota amewataka Wakristo kujihami kwa visu, mishale na mikuki ili kupambana na Waislamu. Askofu Mwasota amedai kuwa wana habari kuwa Waislamu wana mpango wa kuchoma makanisa nchi nzima na kwamba tayari kikosi kimoja kimetua Mbeya kwa kazi hiyo. Baadhi ya vyombo vya habari baada ya kusherehesha habari hiyo ya Askofu David Mwasota vikasema kuwa katika kutekeleza mkakati huo jijini Dar es Salaam, Waislamu walikuwa wameliteketeza kwa moto Kanisa la Kipentekoste la Faraja International Yombo Dovya, huku jingine la KKKT Yombo Dovya nalo likinusurika kuteketezwa na watu wanaojiita wanaharakati wa Kiislamu. (na kwamba) Mlinzi wa Kanisa hilo aliripotiwa kujeruhiwa. Ufuatiliaji wa karibu wa madai haya umebaini kuwa hakuna Kanisa lililochomwa moto Yombo kama ilivyodaiwa. Ni habari za kuzua. Kutokana na habari hizi za urongo, Wakristo wameambiwa na Askofu wao wajihami kwa visu, mishale, mikuki na silaha nyingine. Jaaliya katika mazingira haya anatokea kichaa tu anarusha kijinga cha moto kanisani au inatokea hitilafu ya umeme na kanisa linateketea kabisa, hali itakuwaje mitaani? Si jambo gumu kujua

Kama ni uchochezi wachochezi Ni hawa hapa, lakini Maaskofu!

hatari itakayotokana na uchochezi huu. Lakini maadhali wanaoleta uchochezi huu ni maaskofu, hilo hutasikia likisemwa. Maadhali wanaochochea chuki hizi za hatari za kidini ni Maaskofu, hutamsikia Mkuu wa Mkoa, Kamanda Kova na viongozi wa ngazi za juu wa kisiasa wakiwakemea maaskofu h a w a . Wa t a j i f a n y a hawajasikia. Lakini kwa bahati mbaya kabisa, hata Masheikh wetu wanaoona kuwa usheikh wao hauwezi kukamilika bila ya kuwashutumu mara kwa mara Waislamu wenzao ili waonekane na serikali/ maaskofu, kuwa wao ni waungwana; hutawasikia wakilani uchochezi , chuki na uhasama huu unazopandikizwa!!! Jambo moja Waislamu watie akilini: Maadhali maaskofu hawa wapo tayari kusema uwongo kuwasingizia Waislamu kuwa wana mpango wa kuchoma makanisa, hawataona vibaya pia kufanya lolote ili ile kauli yao kuwa makanisa yanateketea Yombo na Mbeya ionekane kuwa ni ya kweli. Ndio pale tukasema kuwa, wakipewa fursa kama ile ya maandamano na vurugu mitaani, wanaweza kuitumia kuchoma makanisa yao weneywe na kuwasingizia Waislamu. Ni katika mazingira haya yaliyopo hivi sasa, bado tunazidi kuwasisitiza Waislamu kutulizana na kujisaidia katika hali hii kwa Swala na Subra. Hautapita muda, wataumbuka waovu na uovu wao.

kuwavunja moyo wananchi ili wachukie serikali yao. Maalim Seif alisema kwa kuwa yeye ni kiongozi wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa hangependa kumsema Rais wake hadharani, lakini kwa kuwa amefanya jitihada za kuwasiliana na kiongozi wake na kumueleza juu ya vitendo wanavyofanyiwa raia, lakini jambo la kusikitisha Dk. Shein hajachukua hatua yoyote ya kusimamisha vitendo hivyo. Kwamba bado wananchi wanaendelea kupigwa na kufuatwa majumbani kwa kisingizio cha kutafutwa wahalifu. Leo naongea kwa masikitiko makubwa, nina huzuni kubwa kwa mambo yanayofanyika hapa nchini kwetu na niseme ni mambo ya kishenzi kabisa wanaofanyiwa raia, alisema Maalim Seif. Rais wangu Dk. Shein unatungusha kwa kuwa wewe ndiye mwenye jukumu kubwa zaidi la kulinda amani ya Zanzibar. Alisema. Katika kumkumbusha Dk. Shein ahadi yake aliyoitoa siku ambayo anatangazwa mshindi na Tume ya Uchaguzi miaka miwili iliyopita, Maalim Seif alisema Dk Shein alichukua ahadi kwa Wazanzibari wote kwamba atawalinda rai wote bila ya ubaguzi na akachukua hadi kwa Mwenye enzi Mungu kwamba atailinda Zanzibar, basi namuomba Rais wangu mpenzi akumbuke ahadi yeke. Katika mkutano huo, Maalim Seif pia alisema mbali ya lengo la kuivuruga Serikali ya Umoja wa Kitaifa, lakini wahadhina wanafanya juu shini ili kuuharibu mshikamano wa Wazanzibari ambao kwa kiasi fulani ulikuwa umeonesha nia njema. Akizungumzia lengo la tatu la wahafidhina hao alisema ni kuogopa mchakato wa katiba ambao unaonesha dhahiri kwamba Wazanzibari wanapigania mamlaka kamili ya Zanzibar na kutaka Muungano wa Mkataba jambo ambalo ni mwiba kwa baadhi wana CCM na wahadhina. Katika hatua nyengine Maalim Seif aliitupia lawama Tume ya Mabadiliko ya Katiba kwa kushindwa kuheshimu mawazo ya wananchi juu ya aina ya Muungano wanaotaka na kusema kwamba tume hiyo imekuwa ikiwalazimisha wananchi waseme kile ambacho wao wanakiamini. Maalim Seif alimshauri Mwenyekiti wa Tume hiyo Jaji Joseph Warioba kuhakikisha kuwa Tume yake inaheshimu mawazo ya makundi yote, yakiwemo yanayotaka mabadiliko katika mfumo wa sasa wa Muungano. Awali kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi, Kaimu Katibu Mkuu wa chama hicho Salim Bimani alisema Wazanzibari wamechoshwa na vitendo wanavyofanyiwa vya kudhalilishwa na kupigwa bila ya hatia. Bimani alisema ni jambo la kusikitisha kuona hakuna hatua zinazochukuliwa licha ya vitendo hivyo kuripotiwa na kuonekana hadharani.

Mkuu wa Shule adaiwa kuhujumu wanafunzi wa Kiislamu Bagamoyo


Na Bakari Mwakangwale
MKUU wa Shule sekondari ya Bagamoyo, anadaiwa kupandikiza chuki za kidini huku akiwapachika ugaidi wanafunzi Waislamu wanaoswali swala tano. Mkuu huyo anadaiwa kuwaita wanafunzi hao kuwa ni Al Qaida na Al Shabab huku akijumuika na wanafunzi Wakristo akiwataka wakae mbali na magaidi hao. Kutokana na chuki iliyojengeka shuleni hapo, Mkuu wa Mkoa wa Pwani ameamua kufunga shule hiyo huku hatma ya Mkuu huyo wa Shule ya Sekondari ya Bagamoyo, Bw. Bonus Ndimbo, akiiacha mikononi mwa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi. Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Hajjat Mwantum Mahiza, amelazimika kufunga Shule hiyo mapema wiki hii, baada ya kuwepo mgogoro wa Kidini Shuleni hapo kwa muda mrefu jambo linaloashiria hali ya hatari. Akiongea na mwandishi wa habari hizi, Mkuu huyo wa Mkoa wa Pwani, baada ya kutangaza kuifunga Shule hiyo, alisema suala hilo amelikabidhi kwa Wizara husika (Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi) kwa ajili ya uchunguzi zaidi juu ya mgogoro huo na hatma yake. Hajjat Mahiza, alisema jukum lake akiwa kama Mwenyekiti wa Ulinzi na Usalama wa Mkoa, ni kuhakikisha usalama ndio maana alimechukua hatua hiyo baada ya kubaini kuna matatizo katika uongozi na wanafunzi shuleni hapo. Alisema, baada ya kufika Shuleni hapo, alibaini kuna tatizo la kiutawala kwa walimu na tatizo la nidhamu kwa wanafunzi, kwani alidai wanafunzi wengi hawakuwapo Shuleni huku uongozi wa shule haujui wanafunzi hao wapo wapi. An nuur, ilipotaka kujua uhalali wa barua ambazo walipewa wanafunzi tisa wa Kiislamu wa Shule hiyo na Bodi ya Shule kwa lengo kuwasimamisha Shule kisha wanafunzi hao kugoma kuzipokea na kusaini, alisema hilo ni miongoni mwa mambo ambayo Wizara itashughulika nalo katika uchunguzi wake na wanaotakiwa kuzitolea ufafanuzi ni Wizara husika. M i m i s i o Wi z a r a y a Elimu, zile barua zitafanyiwa kazi na Wizara ya Elimu, wao ndio wataeleza hiyo adhabu iliyotolewa na Bodi ni sahihi au la baada ya kujua chimbuko la mgogoro huo. Alisema. Kufuatia kufungwa kwa Shule hiyo, tokea jumanne wiki hii, wanafunzi wamekuwa wakiondoka kwa utaratibu maalum kurejea makwao mpaka hapo watakapotakiwa kurejea tena shuleni hapo. Kufuatia mgogoro huo wa muda mrefu Shuleni hapo baina ya Wanafuzi wa Kiislamu na Mkuu wa Shule hiyo, Bw. Bonus Ndimbo, hali ilikuwa mbaya zaidi Jumatatu wiki hii, pale ambapo Bodi ya Shule, ilipoamua kuwapa barua za kuwataka wanafunzi tisa wa Kiislamu kuondoka Shuleni hapo. Baadhi ya wanafunzi wameeleza kuwa, barua hizo zilikuwa ni za kuwasimamisha wanafunzi hao ambao miongoni mwao ni viongozi wa Waislamu Shuleni hapo, mpaka Novemba 26, mwaka huu, huku wakidai barua hizo hazikueleza sababu za msingi wao kusimamishwa. Taarifa zaidi zinasema, wanafunzi hao walipokuwa wakikabidhiwa barua hizo kisha kutakiwa kusaini, waligoma wakidai bado walikuwa wakisubiri majibu yao ya msingi kutoka kwa Mkuu wa Wilaya (Bagamoyo), Bw. Ahmed Kipozi, aliyefika Shuleni hapo siku chachache nyuma na kupokea malalamiko yao na kuahidi kuwapa majibu ya kero zao dhidi ya Mkuu wa Shule hiyo. Wanafunzi wa Kiislamu Shuleni hapo, baada ya kubaini kuwa wenzao walikuwa wanatakiwa kusimamishwa Shule, walikusanyana na kuka pale walipo wenzao mbele ya Bodi, wakitaka barua hizo za kusimamishwa wapewe wote huku wakidai tatizo ni la wanafunzi wote wa Kiislamu. Baada ya muda, viongozi wa Mkoa na Wilaya, chini ya Mkuu wa Mkoa, Hajjat. Mwantum Mahiza, walika Shuleni hapo, kisha kufanya kikao maalum baina ya uongozi na wanafuzi wa Shule, ambayo katika jumla ya mambo aliyoongea Hajjat. Mahiza, ni kusisitiza umoja na kuvumiliana. Hajjat Mahiza, alinukuliwa akisema, kama mtu anaswali swala tano na mwingine hawali swala hizo, ni vyema wakavumiliana kwani kila mmoja ndivyo imani yake inaruhusu hivyo. Baada ya nasaha zake, Mkuu huyo wa Mkoa aliamuru Shule hiyo ifungwe, ili kupisha uchunguzi ufanyike kubaini kiini cha mgogoro huo kisha hatua stahiki zichukuliwe. Awali, wakielezea chimbuko na chanzo cha mgogoro huo, baadhi ya wanafunzi wa Shule hiyo (majina tunayahifadhi) kabla na baada ya tukio la kufungwa kwa Shule hiyo, walisema tatizo ni Mkuu wa Shule, Bw. Bonus Ndimbo, kudhihirisha udini na chuki kutokana na kauli zake kwa wanafunzi wa Kiislamu shuleni hapo. Walisema, Mwalimu huyo tokea ahamie shuleni hapo amekuwa akitoa kauli za kupandikiza chuki miongoni mwa wanafunzi wa Kiislamu kwa wenzao wa Wakristo, kwa kuwaita Al-kaida, Alshabab, huku mara kwa mara akiwatahadharisha Wakristo kuwa mbali na Waislamu. Wanafunzia hao walieleza kuwa mwanafunzi yoyote wa Kiislamu anayeonekana kuwa anafuata maadili ya dini yake, mwalimu huyo hujenga chuki naye na kumuita Alshabab, huku akidai kuwa atahakikisha anawapunguza Shuleni hapo. Wanafunzi hao wanamtaja mwanafunzi El-Hakim Somji, aliye na asili ya Kihindi, kuwa miongoni mwa wanafunzi wanaoandamwa sana na Mkuu wa Shule, akimkejeli kuwa ni Al Shabab. Sikupendi na sitokupenda. Wanafunzi hao walimnukuu Mkuu wao, wakidai ni maneno aliyomwambia mwenzao Somji, huku akimshutumu kuwa ana uhusiano na Alkaida. Walisema, katika kujitete mwanafunzi Somji, ambaye pia ni Katibu wa wanafunzi wa Shule hiyo na mweka hazina kwa upande wa wanafunzi wa Kiislamu, aliwahi kumueleza Mkuu wake wa Shule kuwa, anaona hamtendei haki kumuita gaidi wa Al Qaida. Wanafunzi hao walibanisha kwamba, hali ilijiridhirisha zaidi, kipindi cha uchaguzi wa viongozi wa wanafunzi kilipoka ambapo Mkuu huyo, alibadili mfumo uliokuwa ukitumiwa miaka yote shuleni hapo, kwa kila nafasi inayogombewa ilikuwa na watu watatu, lakini kwa utaratibu mpya kila nafasi alitaka iwe na wagombea wawili, tena Mkristo na Muislamu. Walisema, siku moja kabla ya uchaguzi, Oktoba 3, mwaka huu kupitia katika sanduku la maoni Mkuu wa Shule aliwataja wanafunzi Ramadhani Bilali, na Kaiza Ruttakinikwa kidato cha Sita CBG, kuwa wanafunzi hao wanashawishi udini Shuleni hapo. Siku ya uchaguzi, (Oktaba 42012), majira ya asubuhi, Mkuu huyo inadaiwa alikwenda na karatazi hiyo ya maoni katika darsa la wanafunzi hao kisha kuisoma na kabla ya kuisoma alimtaka Ramadhani Bilali, akamsubiri osini kwake. Inadaiwa kuwa, akiwa darasani, Mkuu huyo anadaiwa kusema kuwa kuna watu wanajifanya kujua sana dini Shuleni hapo, huku akiwashawishi wanafunzi kutowasikiliza na kuwapuuza kama watu wa sokoni. Kuna watu hawapaswi kufuatwa, mfano kama hawa wanaoswali swali sana, kutwa nzima wanaswali tu. Mwenyezi Mungu ameweka siku moja tu ya kuswali. Kilisema chanzo chetu, kikimnukuu Mkuu huyo. Imeelezwa kuwa akitoa lawama hizo darasani, mwanafunzi aliyetajwa kwa jina la Japhet Kazimili (Mkristo) alipingana na Mkuu huyo, akisema kuwa huenda taarifa hizo amezipata tofauti kwani alidai, hakuna udini kama anavyodai (Mkuu). Chanzo chetu kilisema, Mkuu huyo alimtuhumu mwanafunzi Ramadhani Bilali ambaye ni kiongozi wa wanafunzi wa Kiislamu kuwa ni Alshabab na ni mdini na kuwa hayupo peke yake Shuleni hapo. Siku hiyo ya Oktaba, 4, 2012, ambayo ndiyo ilikuwa siku ya uchaguzi wa wanafunzi, wakiwa mstarini Mkuu wa Shule, aliisoma ile barua ya maoni kisha alitoa orodha ya wanafunzi Ramadhani Bilali (Kiongozi wa Daawa na taaluma kwa Waislamu), Kaiza Ruttakinikwa, El-Hakim Somji, Answaar Abdulhakim, Amin Thabit (Amir wa Jumuiya ya wanafunzi wa Kiislamu), akisema anawatahadharisha na watu hao sana Shuleni hapo, kisha aliakhirisha uchaguzi huo na kusema utafanyika siku inayofuata, Oktoba 5, 2012. Kufuatia kauli hizo za Mkuu wa Shule, wanafunzi Waislamu waliokuwa wakigombea katika nafasi mbalimbali waliandika barua za kujitoa katika uchaguzi, kwani miongoni mwa waliotajwa siku hiyo miongoni mwao ni wagombea, hivyo walidai Mkuu alidhamilia kuvuruga uchaguzi kwa kuwatangazia sifa mbaya mbele ya wapiga kura (wanafunzi). Hata hivyo uchaguzi huo uliendelea siku hiyo huku wanafuzni wa Kikristo wakinukuliwa wakitamba kuwa wanaenda kusimika Kanisa, huku Mkuu akisema, kujitoa kwa wagombea hao wametumia demokrasia yao hivyo hawezi kuahirisha uchaguzi hukuakionyesha kuridhishwa na hali hiyo. Tu l i a n d i k a b a r u a k w a Mkuu kuonyesha kuchoshwa na mwenendo wake mzima na kwamba anapandikiza mbegu za udini na kutengeneza matabaka miongoni mwa wanafunzi shuleni hapo ambao kabla ya ujio wake matatizo hayo hayakuwepo. Alisema mwanafunzi mmoja. Oktoba 15, mwaka huu, waliamua kuelekea kwa Mkuu wa Wilaya kupeleka malalamiko yao, hata hivyo njiani walikutana na Jeshi la Polisi, na kuwazuia na walipoulizwa walieleza nia yao ya kumuona Mkuu. Polisi walituomba turudi na kutuitia Afisa Elimu wa Wilaya (D.E.O), Mwl. Majoyo, ambaye tuliamini ni mtu ambaye atatusaidia kutatua matatizo yetu na Mkuu wa Shule, baada ya kutusikiliza alihaidi kulifanyia kazi na kututaka kurudi madarasani ili amsikilize na Mkuu pia kabla ya kutoa majibu ya pamoja. Alisema

Habari

Dhuul-Hijja 1433, IJUMAA NOVEMBA 9 - 15, 2012

AN-NUUR

Baada ya hapo, inadaiwa kuwa Mkuu wa Shule alianza kuwakejeli Wanafunzi hao akisema maandamano yao hayakuwa na tija kwa kuwa hawakufika walipotarajia na kuwa wamejisumbua. Oktoba, 22, Mkuu huyo inadaiwa kusimama mstarini na kusema, anawashangaa wale ambao hawamtaki, huku akidai siku zote bosi huwa sahihi na atabaki kuwa sahihi, huku akiwalaumu kwa kitendo cha Wanafunzi wa Kiislamu kulalamika kwa Asa Elimu. Akiwa mstarini hapo, Mkuu huyo alinukuliwa akisema, kuwa suala hilo, ama zake ama zao, na kwamba atahakikisha ama anaondoka yeye ama hao wanaomlalamikia. Oktoba 23, ilikuwa ni siku ya kuapishwa viongozi wapya kama alivyopanga Mkuu wa Shule, ambapo Waislamu waligoma kufanyika kwa zoezi hilo kwa kuwa hawautambui uchaguzi huo, kwa kuwa ulipandikizwa chuki miongoni mwa wanafunzi. Mkuu huyo, alipuuza rai ya Waislamu, ambapo aliendelea na utaratibu wake na ilipoka wakati wa kuwaapisha washindi, mmoja wa wanafunzi wa Kiislamu aliipora karatasi ya kulia kiapo kutoka kwa mwanafunzi mwenzake na kuichana, na kuzua zogo. Baada ya tukio hilo, alika Asa Elimu (D.E.O), kiongozi wa Bakwata, Bagamoyo, kengele iligongwa ambapo Waislamu wote waligoma kwenda mstarini wakisema wanamtaka Mkuu wa Wilaya na si D. E. O, kwa madai aliwapuuza na hawajamuona toka alipoahidi kushughulikia tatizo hilo. Walisema, kufuatia msimamo huo, Mkuu wa Wilaya, Bw. Ahmed Kipozi, alika Shuleni hapo na kufanya kikao cha pamoja, ambapo Amir wa wanafunzi Shuleni hapo Abubakar Yusuph, akiongea kwa niaba ya wenzake, alisema wamechoshwa na mwenendo wa Mkuu wa Shule kwa kupandikiza chuki za kidini miongoni mwa wanafunzi kwa kuwahusisha na Alqaida. Alisema, Mwanafunzi Somji, aliweka wazi kuwa Mkuu huyo wa Shule ameshamtamkia mara kwa mara kuwa hampendi na hatompenda kwa vile ni Al Qaidah. Wanafunzi wa Kiislamu walitanabaisha kuwa hawana ugomvi na wenzao Wakristo Shuleni hapo kama inavyo vumishwa bali ni chuki tu zinazopandizwa na Mkuu wao na kuvuruga mwenendo wa upendo na umoja uliokuwapo kabla ya ujio wake. Kwa upande wa wanafunzi Wakristo miongoni mwao

Inaendelea Uk. 4

Watuhumiwa kesi ya Ponda watoka rumande kwa dhamana


Na Mwandishi Wetu

Habari

Dhuul-Hijja 1433, IJUMAA NOVEMBA 9 - 15, 2012

AN-NUUR

WAT U H U M I WA 3 7 waliokuwa wakishikiliwa mahabusu katika gareza la Segerea wameachiwa huru Jumatano mchana baada ya hakimu katika mahakama ya Kisutu Bi. R. M Nongwa kukubali dhamana kwa watuhumiwa. Watuhumiwa waliopewa dhamana baada ya kutimiza masharti ya udhamini ni Kuluthumu Mfaume, Zainabu Mohamed, Adam Ramadhani, Selemani Abdurahaman, Salum Mzee Juma, Halima Abbas, Maua Omar Mdumila, Fatihia Habibu Abdulrahman, Hussein Ally Hussein, Shabani Ramadhani Kondo, Rashid Ramadhani, Yusuf Athumani Penza, Alawi Mussa Alawi, Ramadhani Rashid Mlali, Omary Ismail, Salma Abdullatif, Said Rashid, Feiswari Abubakar, Issa Abdulwahabu, Ally Mohamed Mussa na Abdallah Haule . Wengine ni Juma Hassani, MwanaOmary Omari Makuka, Omar Bakari, Rashidi Omar Ndimbo, Hamza Ramadhani, Maulid Namdeke, Swalehe Maulid, Jumanne Mussa Msumi, Salum Abdallah Mohamed, Hamisi Halid Mfiyome, Dite Bilali Waikela, Amiri Said Idd, Juma Yasin Ally, Thumani Rashid Selemani, Abubakar Shabani na Ally Shabani Salehe. Hata hivyo mtuhumiwa namba moja ambaye ni Sheikh Ponda Issa Ponda bado yupo mahabusu kufuatia dhamana yake bado imefungwa. Aw a l i w a k i l i w a watuhumiwa Juma Nassoro aliiomba mahakama kuwapatia dhamana watuhumiwa kabla ya kutajwa tena hapo Novemba 15 baada ya kukamilika barua za wadhamini wa watuhumiwa hao. Kesi ya jinai namba 245 ya mwaka 2012 inayomkabili Ponda na wenzake itatajwa tena hapo

Novemba 15 mwaka huu. Sheikh Ponda na Wa i s l a m u w e n g i n e walikamatwa na Polisi baada ya kupinga kuuzwa kiwanja cha Bakwata kwa mtu binafsi cha Markaz Changombe jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Mara baada ya kupewa dhamana, Bi. Detention Bilal Waikella, ambaye ni mtoto wa mwanasiasa veteran maarufu mkoani Ta b o r a M z e e B i l a l Waikela, alidai kuwa

Maaskofu Pentekoste waongo


ulioandaliwa na Waislamu wa kuchoma makanisa nchi nzima. Katika madai hayo wakasema kuwa tayari kikosi maalum cha Waislamu cha kutekeleza hujuma hiyo kilikuwa kimetua Mbeya. Akizungumza mbele ya waandishi wa habari Katibu Mkuu wa Baraza la Makanisa ya Kipentekoste nchini Tanzania (PCT), Askofu David Mwasota akawataka Wakristo kujihami kwa visu, mishale na mikuki ili kupambana na Waislamu. Baada ya kueleza na kunukuu kwa urefu yale yaliyosemwa na Katibu Mkuu wa PCT, Askofu David Mwasota, gazeti la Msema Kweli likamalizia kwa kudai kuwa wakati likielekea mitamboni, bado uchomaji moto makanisa Jijini Dar es Salaam ulikuwa unaendelea, ambapo Kanisa la Kipentekoste la Faraja International Yombo Dovya lilikuwa likiteketea, huku jingine la KKKT Yombo Dovya nalo likinusurika kuteketezwa na watu wanaojiita wanaharakati wa Kiislamu. (na kwamba) Mlinzi wa Kanisa hilo aliripotiwa kujeruhiwa. Katika taarifa yake mbele ya waandishi wa habari, Askofu David anasema kuwa kwa kushika mikuki, visu na mishale, huenda serikali itazinduka na kuwashughulikia Waislamu, kwani anasema kuwa haoni kama serikali inafanya vya kutosha kukabiliana na kitisho cha Waislamu kuchoma makanisa. Ni kufuatia taarifa hizo, An nuur ilipiga hodi Yombo ili kujua ukweli wa madai hayo. Na katika ufuatiliaji ikabainika kuwa hakuna kanisa lililochomwa moto Yombo Dovya bali habari hizo ni uzushi na uchochezi mtupu, unaolenga kuwafarakanisha Waislamu na Wakristo na wakati huo huo ukilenga kuwachongea Waislamu kwa serikali. Kwa kweli sisi hapa Yombo Dovya tumeshtushwa na habari hizi, makanisa yaliyotajwa

pamoja na kufunguliwa kesi na kuwekwa ndani, ataendela kudai haki stahiki za Waislamu dhidi ya madhalimu na kwamba anafauata nyayo za baba yake, ambaye naye aliwahi kuwekwa ndani kwa sababu ya kutetea maslahi ya umma tangu enzi za TANU. Alisema hata jina la Ditention, alipewa wakati baba yake akiwa amewekwa ndani na serikali ya Nyerere kwa sababu za kisiasa.

SHEIKH Ponda Issa Ponda (kushoto)

Inatoka Uk. 1

kuchomwa tunayafahamu, si kweli kwamba kuna kanisa lililochomwa na ni vyema umekuja mwandishi ukayaona. Alisema Bw. Shamte Mwegiro mkazi wa Yombo Dovya. Alisema kuwa baada ya kusikika habari za kuchomwa makanisa hayo hapo Dovya, taarifa ziliwafikia Wenyeviti wa Serikali za Mitaa minne ya Yombo Dovya ambayo ni mitaa ya Uwazi, Makangarawe, Dovya na Msalakala. Baada ya kupata taarifa hizo viongozi hao waliwafuata viongozi wa makanisa yaliyotangazwa kuchomwa moto pamoja na kutizama hali ya makanisa yenyewe. Taarifa zinabainisha kuwa baada ya kufika mtaa wa Uwazi lilipo kanisa la Faraja International, walikuta lipo salama. Walipomhoji muhusika juu ya kuripotiwa kuchomwa moto kanisa hilo, alijibu kuwa kanisa hilo halijaungua bali inaonekana kulikuwa na dalili za kuwepo hitilafu ya umeme. Viongozi hao walikwenda katika Kanisa la Walokole lililopo mtaa wa Njia Panda kwa Kombo, ambalo nalo liliripotiwa kuchomwa moto. Kanisa hilo lililojengwa kwa mabati na kuzungushiwa pazia, nako walilikuta ni salama. Walipohoji kulikoni kuenea habari za kuchomwa kanisa hilo, majibu yalikuwa ni moto uliokuwa umewashwa kuchoma taka zilizokuwa jirani na kanisa hilo, uliruka na kuchoma moja ya pazia la kanisa lakini uliwahiwa na kuzimwa na haukuleta madhara kanisani. Kufuatia uzushi huo, tayari viongozi wa misikiti Yombo Dovya hususan Masjid Swabrina, wametoa tahadhari kwa Waislamu kuwa makini kufuatia kuwepo propaganda za kuwapaka matope Waislamu kwa kuwazulia uhalifu.

Hata hivyo imefahamishwa kwamba yaliyotokea nchini Rwanda ndio yamekuwa m w a l i m u w a Wa i s l a m u kujihadhari na uzushi dhidi yao. Ila inavyoonekana ni kuwa wapo baadhi ya viongozi wa Makanisa, ambao bado somo la mauwaji ya Kimbari halijawaingia ndio maana wanaendesha propaganda za kuchochea chuki baina ya Waislamu na Wakristo. Uchochezi na uzushi uliofanywa na viongozi wa kanisa nchini humo ulisababisha maelfu ya raia wa Rwanda kuingia katika vita vya wenyewe kwa wenyewe. Kwa mtindo huo huo vyombo vya habari vya Kikristo, nanyo vimenogewa na staili ya Maaskofu wa Rwanda ya kueneza propaganda za uongo na uzushi ili kusababisha athari kubwa kwa watu wa imani nyingine kwa sababu ya chuki. Hivi karibuni Redio ya Kikristo ya Wapo na gazeti la Kikristo la Msema Kweli, viliripoti kwamba makanisa mawili huko Yombo Dovya yamechomwa moto na wanaodaiwa kufanya hujuma hiyo ni Waislamu. Huko nyuma iliwahi kuripotiwa kwamba kuna kiwanda cha majambia huko Mbagala, ambayo yalisadikiwa kuwa yatatumika kuleta vurugu wakati wa uchaguzi mkuu. Aidha vyombo hivi viliwahi kuripoti kwamba kuna kontena la silaha la CUF limeingia bandarini Dar es Salaam, na ilikuwa ni kipidi cha harakati za uchaguzi mkuu. Hadi leo hakijaonekana kiwanda hicho cha majambia wala kontena la silaha la CUF. Mchungaji wa Kanisa la Pentekoste, Jean Uwinkindi, ni mmoja wa viongozi saba wa dini walioshitakiwa na Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya

Kimbari ya Rwanda (ICTR) kwa kuongoza vitendo vya mauaji ya kimbari ya Rwanda ya mwaka 1994. We n g i n e n i p a m o j a n a Askofu wa kanisa la Anglikana, mchungaji wa kanisa la Wasabato na Mapandre wanne wa Kanisa katoliki. Ni mmoja tu kati ya viongozi hao wa dini ndiye aliyeachiwa huru huku mwingine mmoja akifa kabla kesi yake haijaanza kusikilizwa. Uwinkindi alizaliwa katika wilaya ya Rutsiro, Magharibi ya Rwanda. Baada ya kuwa mwalimu wa dini nyumbani kwao alikozaliwa, alipandishwa hadhi na kuwa Mchungaji kwa kutoa huduma za kiroho katika mikoa ya Bugesera na Kibungo huko Rwanda. Wakati wa mauaji ya kimbari mwaka 1994, alikuwa Mchungaji Kiongozi katika parokia ya Kayenzi. ICTR inamshita kwa mauaji ya kimbari na uteketezaji kizazi kwa madai ya kusimamia au yeye mwenyewe kushiriki katika mauaji dhidi ya Watutsi. Alhamisi Aprili 19, mwaka huu, akawa ni mshitakiwa wa kwanza wa ICTR kuhamishiwa nchini Rwanda ambako kesi yake ndiko itakaposikilizwa. Askofu wa Kanisa la Anglikana, Samuel Musabyimana ni kiongozi wa ngazi ya juu kabisa wa kanisa kuwahi kushtakiwa na ICTR, lakini alikufa Januari 2003 kabla hata kesi yake haijaanza kusikilizwa. Alikana mashitaka yaliyokuwa yanamkabili ya mauaji ya kimbari na uhalifu dhidi ya binadamu aliyodaiwa kufanya katika dayosisi yake ya Shongwe. Askofu huyo alitiwa mbaroni nchini Kenya, mwaka 2001. Naye Mchungaji wa Kanisa

Inaendelea Uk. 5

Haki itasimama tu

Habari

Dhuul-Hijja 1433, IJUMAA NOVEMBA 9 - 15, 2012


Zanzibar. Mwendesha Mashtaka kutoka Serikalini alidai mahakamani hapo kuwa upelelezi wa shitaka hilo bado haujakamilika na kuiomba mahakama ipange tarehe nyengine kwa kutajwa kutajwa tena kesi hiyo. Kwa upande wao Mawakili wa upande wa watuhumiwa Salum Tawfik na Abdalla Juma na waliiomba mahakama kutoa agizo la kupatiwa haki zinazostahiki kwa wateja wao, ikiwemo askari wa Vyuo vya Mafunzo kuruhusu kuonekana na familia zao, kupatiwa chakula, pamoja na kuwekwa katika vyumba vya pamoja na sio kama walivyo sasa ambapo baadhi yao wamo katika vyumba vya mtu mmoja mmoja na waruhusiwe kufanya ibada ya kusoma Quraan pamoja na kuweza kuletewa nguo. Kwa kweli hii sio haki na askari wa vyuo vya mafunzo wanaonekana kupindisha sheria kwa kutowatendea haki wateja wetu, inafika wakati wateja wetu wanafungiwa ndani masaa 24 na hata sisi mawakili wao haturuhusiwi kuwaona hii Mheshimiwa Hakimu haijawahi kutokea duniani kote, alisema Tawk. Hivyo waliiomba mahakama kutoa agizo kwa maafisa wa Vyuo hivyo vya Mafunzo kuwatendea haki wateja wao hao, kama sheria na katiba ya nchini zinavyoelekeza juu ya usawa wa watu wote mbele ya sheria na kulinda na kupata haki sawa kwa mtu ndani ya sheria. Mwendesha Mashitaka wa mahakama hiyo Khamis Jaffar Mfaume, Mwanasheria wa serikali kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) akitetea hoja hizo za upande wa utetezi alifahamisha kuwa, kwa upande wao hawana taarifa na suala hilo. Hata hivyo alisema kuwa, kwa upande wao hawana pingamizi za aina yoyote kwa washitakiwa hao katika suala zima la kutendewa haki kama walivyo mahabusu wengine kutokana na hilo ni haki yao kwa mujibu wa sheria. Baada ya hoja za pande hizo mbili, hakimu Ame Msaraka Pinja ameviagiza vyombo vya sheria kuzingatia wajibu wao wa kusimamia sheria, na kila chombo kinapaswa kufuata sheria kama zilivyowekwa. Mahakama haitakua na uamuzi kwani tumesikia kilichoelezwa, ila inasema kuwa vyombo vyote vya dola vina wajibu mkubwa wa kusimamia na kutekeleza sheria kama zilivyowekwa, alisema Pinja. Baada ya maamuzi hayo, Mwanasheria huyo wa serikali aliiomba mahakama hiyo kuiahirisha kesi hiyo na kuipangia tarehe nyengine kwa ajili ya kutajwa, kwa madai upelelezi wake bado haujakamilika. Hakimu Ame Msaraka Pinja, alikubaliana na hoja hizo na kuiahirisha kesi hiyo hadi Novemba 21 mwaka huu kwa kutajwa, na kuamuru washitakiwa hao wabakie rumande. Kwa upande wa jana hali ya amani na utulivu ilitawala kwa kiasi kikubwa kutokana na kutokuwepo kwa msongamano wa watu, licha ya askari polisi wa kikosi cha kutuliza ghasia (FFU), wakiwa wamevalia mavazi maalumu huku wakiwa wameshikilia silaha mikononi, na wengine wakiwa na mikanda iliyohifadhiwa mabomu ya machozi, wakiwa wamelizingira aneo zima la mahakama hiyo kwa ajili ya kuimarisha usalama. Washitakiwa waliwasili katika viunga vya mahakama hiyo majira ya saa 3:47 asubuhi, wakitokea rumande ya Chuo cha Mafunzo Kilimani wakiwa katika msafara wa magari manne yaliyosheheni askari wa FFU.

AN-NUUR

Sheikh Farid awaambia maafande

SHEIKH Farid Had akiwa katika karandinga la Polisi akirejeshwa rumande. Na Alghaithiyyah
SHEIKH Farid Hadi Ahmed amesema hakuna namna, lazima haki itasimama tu. Sheikh Farid alipaza sauti wakati akiingia katika karandika akisema kuwa, pamoja na vikwazo wanavyowekewa katika kupata dhamana, lakini haki lazima itasimama kwa sababu si katika maumbile kuchwa na ikachika. Amesema, maadhali wanasimama katika haki na maadhali wanapigania haki, batili haiwezi kushinda. Farid na viongozi wenzake saba wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar wanaokabiliwa na kosa uchochezi, juzi walipewa masharti magumu ya dhamana n a M a h a k a m a y a Wi l a y a ya Mwanakwerekwe Mjini Unguja. Ni kutokana na mashariti hayo na madai mengine ya kunyimwa haki za msingi kwa mujibu wa katiba na sheria, Farid amesema kuwa yote hayo yanafanyika ili kuzima nuru ya haki, lakini juhudi hizo hazitafanikiwa. Hakimu wa mahakama hiyo alisema kuwa baada ya mahakama kupitia maelezo ya pande zote mbili imeamuwa kutoa masharti magumu kwa watuhumiwa hao wakitakiwa kuwasilisha kiasi cha shilingi 1,000,000 taslim kila mshitakiwa, pamoja na kudhaminiwa na wadhamini watatu kila mmoja wadhamini ambao kila mmoja ametakiwa kuwasilisha kiwango kama hicho cha fedha taslimu. Sambamba na masharti hayo, wadhamini hao pamoja na washitakiwa wenyewe wametakiwa kuwasilisha vivuli vya hati zao za kusaria (pass port) au vitambulisho vya Mzanzibar Mkaazi. Kwa mujibu wa mahakama, wadhamini hao lazima wawe ni wafanyakazi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) wawe na vitambulisho vya kazi pamoja na barua za Sheha wa Shehia wanazoishi. Wa s h i t a k i w a w o t e wamerejeshwa rumande chini ya ulinzi mkali wa vyombo vya ulinzi na usalama kwa kuwa hata kama wangeweza kukamilisha masharti hayo ya dhamana, bado wangeendelea kuwepo rumande, kutokana na kukabiliwa na kesi nyengine katika mahakama ya Mrajis wa Mahakama Kuu Vuga, ambayo dhamana zao zimefungwa na Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) Ibrahim Mzee Ibrahim. Kesi ya Sheikh Farid na wenzake saba ilianza kutajwa Oktoba 19 mwaka huu, ambapo juzi ilikuwa ni siku ya kutoa mamuzi juu ya dhamana za watuhumiwa hao ambao wanadaiwa kutenda kosa hilo Agasti 17 mwaka huu, huko katika maeneo ya Magogoni Msumbiji wilaya ya Magharibi Unguja. Wa t u h u m i w a w e n g i n e wanaokabiliwa na shitaka hilo ni Sheikh Farid Hadi Ahmed (41) Mkaazi wa Mbuyuni, Msellem Ali Msellem (52) Kwamtipura, Mussa Juma Issa (37) Makadara, Azzan Khalid Hamdan (43) Mfenesini, Suleiman Juma Suleiman (66), Makadara, Khamis Ali Suleiman (59) Mwanakwerekwe na Hassan Bakari Suleiman (39) Tomondo. Watuhumiwa hao wote kwa pamoja wanadaiwa kutenda kosa hilo kinyume na kifungu cha 45 (1)(a) na (b) sheria namba 6 ya mwaka 2004 sheria ya Zanzibar. Imeelezwa mahakamani hapo kuwa, Agosti 17 mwaka huu, majira ya saa 11:00 za jioni huko Magogoni Msumbiji wilaya ya Magharibi Unguja, wakiwa ni wahadhiri toka Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu, walitoa matamko ya uchochezi yanayoashiria uvunjifu wa amani na kusababisha fujo, maafa mbali mbali na mtafaruku kwa Serikali ya Mapinduzi ya

Maaskofu Pentekoste waongo


Inatoka Uk. 4 wa Kitutsi wapatao 2,000 waliokuwa wanapata hifadhi ya usalama wao ndani yake waliuawa. Pandre mwingine, Emmanuel Rukundo, aliyekuwa anatoa huduma za kiroho jeshini, anatumikia adhabu ya miaka 23 jela nchini Mali. Alitiwa hatiani kwa kushirikiana na wanajeshi na wanamgambo wa Interahamwe kuwaua Watutsi waliokuwa wanapata hifadhi ya usalama wao wakati huo kwenye seminari ya Kabgayi (Rwanda Kati) na pia kumnyanyasa kijinsia mwanamke wa Kitutsi. Alitiwa mbaroni nchini Uswisi mwaka 2001. Padre pekee Mkatoliki aliyeachiwa huru ni Hormisdas Nsengimana, aliyekuwa Mkuu wa Seminari ya Kristu Mfalme, Nyanza (Kusini mwa Rwanda). Alishitakiwa kwa kusimamia mauaji ya kimbari dhidi ya Watutsi katika seminari yake na maeneo jirani, ikiwa ni pamoja na mauaji dhidi ya wanawake na mapandre wenzake. Hata hivyo, Mahakama ilimwachia huru Novemba 2009 kwa msingi ya kukosa ushahidi wa kutosha kumtia hatiani. Mwendesha mashitaka hakukata rufaa dhidi ya uamuzi huo. Alikwenda kuishi katika parokia moja nchini Italia, Machi 2010. Yeye alitiwa mbaroni nchini Cameroon miaka minane kabla ya kuachiwa huru. Padre mwingine aliyebakia kushitakiwa na ICTR ni We n s e s l a s M u n y e s h y a k a , Paroko wa Kanisa la Familia Takatifu mjini Kigali. Kesi yake ilipelekwa Ufaransa Novemba 2007 lakini yenyewe ni tofauti kabisa na kesi ya Uwinkindi kwa sababu Munyeshyaka anaishi nchini Ufaransa na hajawahi kukamatwa na ICTR. Bado yuko katika uchunguzi na wakuu wa Ufaransa. Kwa mujibu wa hati ya mashitaka ya ICTR, anashitakiwa kwa mauaji ya kimbari, mauaji, kuteketeza kizazi na ubakaji.

l a Wa s a b a t o , E l i z a p h a n e Ntakirutimana, naye pia alikufa akiwa na umri wa miaka 83, Januari 2007, muda mfupi baada ya kumaliza kutumikia adhabu yake ya kifungo cha miaka 10 jela. Kwa mujibu wa jamaa zake, alikuwa anaugua kansa kwa muda kwa miaka mingi. Alitiwa hatiani pamoja na mtoto wake wa kiume na daktari wa magonjwa ya binadamu, Gerard Ntakirutimana ambaye bado anatumikia adhabu yake jela, kwa kuhusika kwake na mauaji dhidi ya Watutsi katika eneo la kanisa lake la Mgonero, Magharibi ya Rwanda. Padre Athanase Seromba, ni mmoja wa Mapandre ambao wamewahi kushitakiwa na ICTR. Yeye anatumikia kifungo cha maisha jela nchini Benin kwa kuamuru tingatinga kubomoa kanisa lake la Nyange, Magharibi ya Rwanda katikati ya Aprili, 1994 ambapo wakimbizi

6
Na Omar Msangi NI kweli yawezekana aliyewaroga Watanzania huenda hayupo katika sayari hii kama kilivyosema kibozo cha gazeti la Majira la Jumamosi Novemba 3, 2012. Katika kibonzo hicho, msanii anaonyesha Tanzania ikilia njaa, ikinyosha mkono wa saidia masikini, huku imekalia madini, gesi na utajiri mwingine. Baada ya mamia ya maelfu, kama si mamilioni, ya tani za mchanga wenye madini kusombwa kwa miaka mingi tu kupelekwa nchi za nje, wiki hii ndio Waziri mwenye dhamana na madini anasema kuwa wapo katika mkakati wa kuandaa mchakato wa kuweka utaratibu wa kufanya uchunguzi kuona mchanga huo una madini aina gani ya thamani!!! (Rejea kipindi Dakika 45 kinachorushwa na ITV). Laiti ile hasira wangekuwa wanashushiwa wahujumu uchumi na mafisadi walafi wanaoifisidi nchi hii na kuibakisha masikini huku wao wakinenepeana. Laiti hiki kinachoonekana kuwa ni umakini wa vyombo vya dola ingekuwa unaelekezwa katika kuwatizama wanaoitwa wawekezaji wanaokuja kuwekeza katika madini na miradi mingine pakawa na mikataba mizuri ya kuifaidisha nchi! Laiti nguvu na hasira hizi za dola zingekuwa zinawashukia waliopewa madaraka ambao huwapa wawekezaji leseni na vibali vya kupora nchi bila kujali maangamizi wanayowasababishia Watanzania. Lakini kwa bahati mbaya kabisa, hasira hizi anashushiwa adui wa kubuni. Nguvu zilizopita kiasi zinazotumia rasilimia kubwa ya nchi, hufujwa kupambana na adui asiyekuwepo. Unajitisha mwenyewe unatishika, unapambana. Sawa na yule mtu anayejitekenya mwenyewe na kucheka. Yupo mzee mmoja alikuwa amejipumzisha mchana wa jua kali baada ya uchovu wa kazi. Sasa kila akitaka kulala, watoto waliokuwa wakicheza nje chini ya dirisha la chumba alimokuwa amelala, wanamghasi kwa makelele. Kila akiwafukuza, mara wamerejea tena. Yule mzee akabuni mbinu. Akatoka

Makala

Dhuul-Hijja 1433, IJUMAA NOVEMBA 9 - 15, 2012


wanaandamana, anawapa habari walio ardhini waende wakawasambaratishe. Mwisho wa yote akatamba kuwa wamefanikiwa k u w a d h i b i t i Wa i s l a m u wasiandamane. Kilichowazuiya Waislamu kuandamana sio helkopta ya Kova angani wala utitiri wa vikosi vya Polisi waliosambazwa mitaani. Waislamu hawakuandamana kwa sababu zilezile ambazo z i l i w a f a n y a Wa i s l a m u Zanzibar na Masheikh wao kutulia nyumbani na Misikitini mwao. Waislamu ni wapenda amani. Waislamu ni wazalendo. Waislamu wamegundua shari iliyoandaliwa dhidi yao na dhidi ya nchi hii. Na waligundua kuwa kuna juhudi za makusudi kuchochea ghasia na kuwachokoza Waislamu, ili wakichokozeka wakachukua hatua kama maandamano, fursa hiyo itumike kufanya hujuma dhidi ya shabaha mbalimbali na wasingiziwe Waislamu. Na likifanyika hilo, ipatikane sababu ya kuwahujumu Waislamu. Hilo Waislamu waliligundua mapema. Wakaamua kujisaidia kwa swala na subra. Lakini inavyoonekana kuna watu wamekasirika baada ya kuona kuwa Waislamu wametulia. Walichokuwa wanatamani ni kuwa baada ya kuzua uwongo na kuupamba katika vyombo vyao vya habari kuwa wakati Zanzibar kuna Al Qaida, Bara kuna Boko Haram, walitamani kuona Waislamu wanaingia mitaani, zinafanyika ghasia, kunafanyika hujuma, ili ule uwongo wao uonekane kama kweli. Ndio maana pamoja na kuwa Ijumaa iliyopita hakukuwa na maandamano wala ghasia mitaani, hali ambayo hawakuipenda kwa sababu inawaumbua; waliibuka na uwongo w a k i s e m a : Wa i s l a m u waichafua tena Dar es Salaam: Waandamana baada ya Sala ya Ijumaa. JWTZ, Polisi wajitosa kukabiliana nao. We n g i n e w a k a s e m a : Vu r u g u z a Wa i s l a m u huduma zasimama: Mabomu yarindima, vijana 19 watiwa mbaroni. Likifafanua na kuonyesha hali ilivyokuwa mbaya, gazeti la JAMBO LEO, likasema Inaendelea Uk. 7

AN-NUUR

Waislamu kuweni makini


Shari iliyokusudiwa ni kubwa mno, lakini. Wanaotamani kuona vurugu wataumbuka Sheikh Mataka, haya ya Askofu hujasikia?
nini? Babu alitaka kula pilau, sisi tunataka kupata nini? Najiuliza maswali haya baada kutangazwa katika vyombo vya habari kuwa siku ya Ijumaa iliyopita, kikosi maalum kutoka vyombo vya dola kinachohusika na mabomu pamoja na vyombo vyao vya kutambua mabomu, kilikuwa kimetumwa pale Mahakama ya Kisutu ili kuwadhibiti Waislamu. Kuja kwa makachero na wataalamu hao wa mabomu, mbwa wa kunusa mabomu pamoja na kufungwa kamera maalum, CCTV, hapana shaka hii ilitokana na hofu kwamba huenda wangekuwepo Waislamu ambao wangekuja na mabomu. Na hii inakuja baada ya kuzua uwongo wa kuwapakazia uovu Waislamu sasa tunaamini. Tumejitisha, tumetishika japo inawezekana pia kuwa huenda vyombo vya usalama kama vinafanya kazi kweli kitaalamu na kwa umakini, vitakuwa vinajua kuwa hakuna Boko Haram wala Muislamu mwenye bomu na aliyekuwa amekusudia kuingia Kisutu na bomu. Kama ni hivyo, kwa nini walijipa kazi ile kwa upole akawaambia wale watoto. Nyie mnacheza mpira hapa, wenzenu wanakula pilau kule Msikitini kuna maulidi. Watoto wakatimka kuelekea msikitini kuwahi ubwabwa. Mzee akapata fursa ya kulala. Kikapiga kitambo watoto h a w a r u d i . Yu l e m z e e aliposhtuka baada ya usingizi kumpitia, anaona watoto hawajarudi. Mh isije ikawa kweli kuna wali msikitini. Akajisemesha mzee. Akatoka kwa hatua za haraka kuelekea msitikini. Kuka anawaona watoto wanaendelea kucheza. Walipoka wakakuta hakuna wali wakaanza michezo yao pale pale. Mzee alitunga uongo, mwishowe akajidanganya kwa uwongo alioutunga yeye mwenyewe. Lakini angalau kwa mzee huyu yeye, hamu ya wali ndiyo ilimpelekea kuamini uwongo alioutunga yeye mwenyewe. Huu uwongo wa kutangaza kuwa Tanzania kuna magaidi, kuna matawi ya Boko Haram wenye uwezo wa kuunda mabomu na kulipua watu wasio na hatia, hamu yetu katika kubuni uwongo huu ni ya ziada kuhakikisha kuwa bomu halipenyi? Huenda ni katika moja ya mbinu za kusimika kitisho cha ugaidi. Mwananchi wa kawaida akisoma kuwa ilibidi kikosi maalum cha kutambua magaidi na mabomu kiletwe Kisutu, atauliza kwa nini? Jibu litakuwa kuwa kulikuwa na hofu kuwa Waislamu wangeshambulia ama kwa bomu la kujitoa muhanga au kurusha! Kwa lengo gani? Pengine kwa lengo la kumkwapua Ponda kutoka vyombo vya dola. Au ufupi wa maneno kumtoa kwa nguvu. Na hili limekuwa likisemwa sana na kupigiwa tarumbeta. Hali kama hiyo ndiyo iliyoonekana pia siku ya Ijumaa ambapo tunaambiwa kuwa pamoja na vikosi mbalimbali vya polisi, kulikuwepo pia na vikosi vya JWTZ, lakini bila sare (kama baadhi ya magazeti yalivyoripoti). Kama hiyo haitoshi Kamanda Kova naye akawa anaranda angani na helkopta huku akitamba kuwa yeye akiwa angani anatizama akiona mahali pana Waislamu

SHEIKH Khamis Mataka akiongea na waandishi wa habari

7
Inatoka Uk. 6 kuwa Maosa wa usalama kikiwemo Kikosi cha Ulinzi c h a J e s h i l a Wa n a n c h i Tanzania (JWTZ), Jeshi la Polisi na askari kanzu walionekana wakivinjari katika maeneo mbalimbali ya Dar es Salaam. Nalo gazeti la Mtanzania likieleza hali ilivyokuwa mbaya likasema: JWTZ waingia mitaani..(kwamba) kutokana na vurugu (za Waislamu), Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), lililazimika kuingia mitaani huku askari wake wakiwa wamevalia kiraia. Kama askari hao walikuwa wamevalia kiraia, mwandishi wa Mtanzani aliwajuaje kuwa ni JWTZ? Anaeleza akisema kuwa: Mtanzania (gazeti) iliwashuhudia askari hao, huku mmoja wao akijikuta katika hali ngumu baada ya kitambulisho chake cha kazi kudondoka kutokana na vurugu hizo. Sijui kitambulisho changu kimedondoka wapi, ni cha jeshi maana duh sasa hii imeshakuwa kazi, ahaaa kumbe kipo katika soksi nimekibana. Alisikika askari huyo wa JWTZ akimwambia mwenzake. Akionyesha jinsi askari wa JWTZ walivyofanya kazi kubwa Mtanzania likashangaa na kuwasifu likisema kuwa: Katika hali ya kushangaza, askari wa JWTZ waliweza kufanya kazi ya ziada huku wakilazimika kutimua mbio kukimbizana na waandamanaji hao na kufanikiwa kuwatia mbaroni baadhi yao. Kwa waliokuwa Dar es Salaam Ijumaa iliyopita wanajua kuwa hapakuwa na maandamano ya Waislamu wala mabomu yaliyorindima. Hata taarifa ya Kamanda Kova inasema kuwa hao vijana 19 wanaodaiwa kukamatwa, walikamatwa wakiwa nje ya Msikiti wa Idrisa, sio wakiandamana. Na mabomu mawili matatu yaliyopigwa, hawakupigwa watu waliokuwa wakiandamana. Yalirushwa eneo la Msikiti wa Idrisa askari wakitaka waumini watawanyike haraka mara baada ya swala. Na waumini waliondoka. Tulipewa taarifa kuna vijana nje ya Msikiti wa Idrisa, nasi tuliwamrisha kuondoka, wakakaidi nasi tukawakamata. Hiyo ndiyo taarifa ya Kamanda wa Polisi, Kanda Maalum ya Dar es

Makala

Dhuul-Hijja 1433, IJUMAA NOVEMBA 9 - 15, 2012


Sasa hapa lazima Wa i s l a m u w a j i u l i z e , wajifunze na watanabahi: Kama kuwepo kikundi cha watu kinachodaiwa kuwa ni cha waumini wa Dini ya Kiislamu kilichoonyesha dalili ya kutaka kuanzisha maandamano, kilipelekea risasi za moto kurindima na vyombo vya habari kudai kuwa Waislamu waichafua tena Dar es Salaam, je, wangeandamana kweli, hali ingekuwaje? Hivi wametulizana majumbani mwao na Misikitini kwao, lakini wanaambiwa wamechafua Dar es Salaam hali iliyolazimisha kikosi maalum cha JWTZ kupelekwa kupambana nao, wangetoka na kusema wanaelekea Ofisini kwa Waziri Mkuu, hali ingekuwaje? Hapana shaka haya yaliyojiri na yaliyosemwa, yamewathibitishia Waislamu kuwa ule uamuzi waliochukua kumeza hasira na kujisaidia kwa swala na subra, hawakuwa wamefanya makosa. Imekuwa ni sababu ya Allah kuwaletea nusra na kuwaacha waliopanga njama za kuwahujumu wakiumbuka. kadhaa tunaowana wakiwa katika vikao vya pamoja? Na kama wanakubaliana na Askofu David kuwa kundi la Waislamu lilishushwa mkoani Mbeya kwa ajili ya kuchoma moto makanisa, je, ile kukaa kimya na kuacha kundi la Waislamu hao likapambane na Wakristo waliojihami kwa visu, mishale na mikuki, ndio kulinda na kudumisha amani ya nchi hii? Lakini ukiacha taarifa hiyo, uongozi wa Kanisa Katoliki la Mtakatifu Augustino, M w an za, u med ai k u w a Paroko wake, Padiri Andreas Buhembo ametumiwa ujumbe wa kumtangazia kifo. Kwamba, wakati kimbunga cha kuchoma makanisa kinaendelea, sasa Waislamu wanatangaza mpango wa kuuwa Mapadiri. Padiri Buhembo anasema kuwa yeye amekabidhiwa ujumbe unaotishia kumuuwa na Mapadiri wengine na kwamba ujumbe huo umeandikwa kwa Lugha ya Kiarabu. Padiri Andrea Buhembo anadai kuwa akitumia mbinu za kikomandoo kwa kuvaa sawa na mavazi ya wahudumu wa Kanisani kwake, mtu (Muislamu) mwenye ujumbe huo ulioandikwa Kiarabu, aliingia na kumkabidhi Inazendelea Uk. 8

AN-NUUR

MAGARI ya jeshi yakiwa yamebeba askari wa jeshi hilo wakipita mitaa ya Kariakoo, jijini Dar es Salaam Salaam, Suleiman Kova. Sasa hizi taarifa nyingine kwamba polisi walitumia mabomu ya machozi na risasi za moto kutawanya Waislamu waliokuwa wakiandamana zinatoka wapi? Lakini Waswahili wana msemo wao, njia ya mwongo fupi. Hata hao walioibuka na vichwa vya habari kuwa risasi za moto zilirindima kutawanya maandamano ya Waislamu, bado katika maelezo yao ukisoma wanasema kuwa, baada ya kikundi cha watu wa dini ya Kiislamu waliokuwa katika Msikiti wa Idris kuonyesha dalili ya kutaka kuanzisha maandamano ndipo Askari wa Jeshi la Polisi walipolazimika kufyatua mabomu ya machozi.

Sheikh Mataka, Khalifah Hamisi haya ya Maaskofu hamjayasikia?


Maaskofu wametoa taarifa rasmi wakidai kuwa Waislamu wana mkakati wa kuchoma makanisa nchi nzima. Na kwamba katika hatua za awali za kutekeleza mkakati huo, wamepata habari kwamba kundi la Waislamu lilishushwa mkoani Mbeya kwa ajili ya kuchoma moto makanisa. Akizungumza mbele ya waandishi wa habari Katibu Mkuu wa Baraza la Makanisa ya Kipentekoste nchini Tanzania (PCT), Askofu David Mwasota amewataka Wakristo kujihami kwa visu, mishale na mikuki ili kupambana na Waislamu waliodhamiria kuchoma makanisa. Askofu David anasema kuwa kwa kushika mikuki, visu na mishale, huenda serikali itazinduka na kuwashughulikia Waislamu, kwani anasema kuwa haoni kama serikali inafanya vya kutosha kukabiliana na kitisho cha Waislamu. Katibu Mkuu huyo wa PCT anamshutumu Rais Jakaya Mrisho Kikwete kuwa amekuwa akitoa matamko mepesi tu badala ya nguvu n a h as ir a zote za do la kuwaangukia Waislamu. Zilipotokea vurugu Mbagala baada ya lile tukio la Quran kunajisiwa, ilidaiwa kuwa kuna makanisa yalichomwa moto. Kwa vile waliotoka kuandamana walikuwa Waislamu na kwa kuwa Waislamu ndio waliokuwa na hasira kufuatia kitendo cha kukojolewa Quran, wakawa ndio watuhumiwa namba moja kuwa ndio waliohusika kuharibu makanisa hayo. Kufuatia tukio hilo, wapo Masheikh ambao walitoa kauli za shutuma wakiwashutumu Waislamu waache vurugu na waache kuchoma makanisa. Ile kuwa kanuni ya Uislamu ni kuwa laiti watu wangeaminiwa kwa kauli zao tu, kuna watu wangedai damu za watu na mali zao (hivyo ni juu ya mwenye kuleta tuhuma kuja na ushahidi utakaothibiti mbele ya mahakama), haikuwashughulisha Masheikh wetu hawa. Wao wakakimbilia kuwashutumu Wa i s l a m u . I l e k u w a mwongozo wa Quran ni kuchunguza kabla ya kuamini jambo na kuchukua hatua, waliona itawachelewesha kujisajili kwamba nao wamewashutumu Waislamu. Lakini hebu tujaaliye kuwa kuna Waislamu walihusika katika kadhia hiyo inayodaiwa ya kuchoma makanisa, na tujaaliye kuwa nia ya Masheikh waliowakemea Waislamu ilikuwa kulinda amani ya nchi kama walivyojieleza: Swali ni je, haya ya Maaskofu kutoa wito kwa Wakristo kujihami kwa visu, mishale na mikuki hawajayasikia? Mbona kimya? Je, wanakubaliana na Maaskofu kwamba kuna kikosi cha Waislamu kimetumwa Mbeya tayari kuanza kazi ya kuchoma moto makanisa? Kama hawaamini, mbona hatuwasikii wakiwasema Maaskofu hao ambao mara

8
Inatoka Uk. 7 mkononi wakati akiendesha ibada bila kushtukiwa na waumini. Katika maelezo yake Padiri Buhembo hakueleza iwapo anajua Kiarabu kwa hiyo aliposoma, alifahamu kilichoandikwa au alikwenda kutafuta mkalimani baadae baada ya kumaliza Misa. Ila anachosema ni kuwa walimkamata na kumhoji lakini wakamuacha akaondoka bila ya kumdhuru! Kama hiyo haitoshi, uongozi huo wa Kanisa Katoliki Mwanza ukadai tena kuwa walikuja mabinti wawili waliovalia Hijabu na kutaka kuingia kanisani lakini wakazuiwa. Labda niulize tena, Masheikh wetu ambao kawaida yao imekuwa ni kushutumu tu Waislamu, taarifa hii ya Padiri Andreas, hawajaipata? Je, wanakubaliana na madai yake kuwa kuna Waislamu wamempelekea ujumbe wa kumtangazia kifo? Kama nilivyotangulia kusema, upo utamaduni mzuri tu ambapo Masheikh hukaa katika vikao pamoja na Maaskofu kuzungumzia masuala ya kinchi. Je, wameshakaa na kiongozi mwenzao huyu wa kidini na kumtaka atoe ushahidi wa madai yake haya? Au kimya chao kieleweke kuwa nao wanakubaliana na Padiri huyo kuwa kuna wasichana wa Kiislamu wanavamia Makanisa na hijabu zao (kufanya nini? Kuyalipua?) na kuwatumia ujumbe wa kifo mapadiri? Kwa maana hiyo tusubiri kuwasikia wakiibuka na kauli za kuwashutumu Waislamu kuwa waache kuwatisha mapadiri?!!! Ukitizama yale madai ya Askofu David Mwasota na haya ya Padiri Andreas Buhembo, kubwa wanachofanya ni kupiga propaganda ya kuwapakazia uovu Waislamu na hasa kujaribu kuisimika ikae na ikubalike kuwa nchini kuna kitisho cha Boko Haram kama ilivyokwisha kutajwa katika baadhi ya magazeti. Ukijua kuwa mengi ya makanisa haya ni yale yaliyoanzia Marekani au kufadhiliwa na taasisi za Kimarekani, matamshi ya Maaskofu hawa hayakupi shida sana. Lakini niseme yafuatayo, ili kupitisha sheria ya Patriot Act, ilibidi kitumike kitisho cha kweli cha shambulio la kimeta (Anthrax Terror Attack), wakafa watu saba wasio na hatia. Kitisho cha Al Qaida na Usam Bin Laden, kimeonekana kweli baada ya

Makala

Dhuul-Hijja 1433, IJUMAA NOVEMBA 9 - 15, 2012


watuambie, wapo tayari kutoa gharama kiasi gani? Wapo tayari kuona watu wangapi wasio na hatia wakiuliwa? Na kwa vile propaganda hapa ni Boko Haram, ni Waislamu, Swali ni je, Askofu Mwasota na Padiri Andreas, wapo tayari kuona Wakristo wangapi wakiuliwa ili hilo wanalotamani litimie? Na mimi nasema, watakaouwa Wakristo na watakaolipua Makanisa ili kudai kuwa ni Waislamu, ni hawa hawa wanaodai k u w a k u n a Wa i s l a m u walioshushwa Mbeya kulipua Makanisani hawa hawa wanaodai kuwa wametumiwa ujumbe wa kifo. Nasema hivyo kwa sababu wanayodai ni urongo mtupu. Ni uchochezi. Ni usanii. Na wanafanya hivi bila ya wasiwasi kwa sababu wanajua kuwa hawatakamatwa kwa idhilali kama wanavyofanyiwa viongozi wa Kiislamu. Labda tujiulize, Muislamu anaingiaje kanisani anakupa ujumbe wa kukutishia kukuwa, halafu humkamati na kumpeleka polisi? Imekuwa kama ule usanii tulioambiwa kuwa kuna vijana wametekwa na wanaharakati wa Kiislamu Arusha wakateswa na mmoja wao akakatwa masikio, lakini katika picha waliyopigwa wote wana masikio yao yakiwa mazima!

AN-NUUR

Sheikh Mataka, Khalifah Hamisi haya ya Maaskofu hamjayasikia?

MMOJA wa askari wakimkatama mama mmoja katika kamatakamata ya Polisi iliyofanyika Kariakoo jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Septemba 11 ambapo watu sio kama kweli waliopiga u c h a w i w e n y e w e k w a takriban 4,000 walikufa. Kampla walikuwa Al Shabab wenyewe. Lakini wakati huo Uganda ilikuwa hivyo au la. Ila tu tusisahau kuwa walilokusudia lishatimia. Sasa labda kwa wale hivyo. Watu kama 70 hivi k a t i k a A n t h a x Te r r o r Watanzania wenye hamu ya walikufa ili kitisho cha Al A t t a c k w a l i t u a m b i a Shabab kionekane kuwa ni kuwa ni Al Qaidah, lakini kuona kitisho cha Waislamu real, cha kweli. Hapa hoja haukupita muda wakashikana kinakuwa real, cha kweli,

Mkuu wa Shule adaiwa kuhujumu wanafunzi wa Kiislamu Bagamoyo


Inatoka Uk. 3 walikiri kuwa hakuna ugomvi kati ya Waislamu na Wakristo, huku mwanafunzi anayejulikana kwa jina la George Mnyaru, alitoboa mbele ya Mkuu wa Wilaya akisema hutumwa na mwanafunzi Emannuel Mmali, kuwafatilia Waislamu kisha kumpa taarifa na yeye huzipeleka kwa Mkuu wa Shule, na kwamba wenye kazi hiyo si yeye pekeyake bali wapo wengi. Mwanafunzi Boniface Chaki, alitoa hoja akitaka Shule hiyo ifungwe, kutokana na Waislamu kumkataa Mkuu wa Shule, na kwamba kutofanya hivyo wanaweza kuzua tatizo Shuleni hapo, jambo ambalo Mkuu wa Wilaya hakuliaki, na kuwataka wanafunzi kutompa muda maalum katika kulitafutia ufumbuzi suala hilo. Pamoja na kikao hicho Waislamu waliendelea na mgomo wao wa kutokuingia madarasani wala msitarini, wakitaka Mkuu wa Shule aondolewe. Taarifa zinasema, katika hali ya kushangaza, usiku wa tarehe 24 kuamkia 25, Oktoba, palivumishwa taarifa kuwa wanafunzi wa Kiislamu watafanya tukio shuleni hapo, taarifa hizo zilienea kwa wanafunzi wa Kikristo pekee. Ambapo ilipoka majira ya saa sita usiku, kengele iligongwa, na kushangaza walipotoka nje waliona miongoni mwa wanafunzi wa Kikristo wakiwa na mapanga na mbo, wengine wakiwa wameshavaa nguo kama vile wameshajiandaa kwa kitu fulani. Tuligundua kuna mchezo unatengenezwa, tulichofanya tuliwaambia mabinti wa Kiislamu kuingia Msikitini na sisi tulienda huko, ambapo Mwanafunzi Seuri Kisambo, alisikika akitangaza kuwa kuna tukio linataka kufanyika. Lakini cha ajabu Mkuu wa Shule hakuonekana kabisa muda huo na wala hutukuona Polisi wakija kama ilivyo kawaida yake kuita Polisi tunaposigana naye, tukawa tunajiuliza kuna nini? Alisema Mwanafunzi mmoja wa Kiislamu. Taarifa zinasema, Oktoba, 25, wanafunzi wa Kikristo wakawa wanashinikiza waruhusiwe kuondoka shuleni hapo, lakini inadaiwa kuwa Mkuu wa Shule alikuwa akiwaambia kuwa hakuna cha kuogopa kwa kuwa wao (Wakristo) wapo wengi kuliko Waislamu. Kuanzia siku hiyo, Wakristo walianza kuondoka shuleni, wakijenga hoja kutatokea vurugu na kuwa kuna Alqaida na Alishabab shule na mpaka Oktaba 27, wanafunzi wapatao 350, walikuwa wametoweka shuleni kati ya wanafunzi 740, wa shule nzima. Kilisema chanzo chetu. Novemba 1, mwaka huu, Bodi ya Shule ilikutana na kutoa majibu ya wanafuzni wa Kiislamu kuwa Mkuu wa Shule Bw. Bonus Ndimbo, ataendelea na wadhifa wake, na kwamba madai na mgomo wa wanafunzi wa Kiislamu ni batili, ili hali Serikali ya wanafunzi iliyochaguliwa itaendelea, marekebisho ya dosari zilizopo yatafanyika katika uchaguzi ujao. Baada ya maamuzi hayo, Bodi hiyo iliwataka wanafunzi kurejea madarsani, huku Mkuu wa Shule akiomba samahani kwa yaliyotokea huku akimalizia kwa kusema Mbwa Mzee hafundishwi mawindo. Majibu hayo kwa ujumla yaliamsha upya hasira za Waislamu, ambapo Novemba, 2, walilazimika kwenda kwa Mkuu wa Wilaya, kutaka kujua kama msimamo wa Bodi ndiyo majibu aliyowaahidi. Mkuu wa Wilaya, alisema hatambui hayo na kututaka tuendelelee kuwa na subira kwani susla hilo linashughulikiwa kwa kina, na matokeo yake watayapata kwani amebaini matatizo mengi shuleni kwetu. Alisema Mmoja wa wanafunzi hao. Taarifa zinasema, wanafunzi hao walipoendelea na mgomo wao, baada ya maamuzi ya Bodi, ndipo Bodi ilipoibuka tena na maamuzi ya kuwapa barua za kuwasimamisha baadhi ya wanafunzi wa Kiislamu Shuleni hapo, jambo ambalo lilipingwa vikali wakitaka wote wapewe barua, na kulazimika Mkuu wa Mkoa kufika shuleni hapo na kuamuru shule hiyo kufungwa. Juhudi za kumpata Mkuu wa Shule hiyo Bw. Bonus Ndimbo, kupata maelezo yake hazikufanikiwa baada ya kulezwa kuwa ametoweka nyumbani kwake akihofia maisha yake, na hata alipotafutwa kwa simu yake ya kiganjani ilikuwa haipo hewani.

9
Said Rajab
NI vyema Serikali ikatambua wazi kwamba kukamata viongozi wa Waislamu kwa lengo la kuwafanya wasalimu amri, haitasaidia kuzima jitihada za Waislamu wa Tanzania kudai haki zao. Kwa kifupi hiyo inazidisha tu imani ya Waislamu na kuwafanya wawe madhubuti zaidi kupigania haki zao. Wala usidhani Mwenyezi Mungu ameghafilika na haya wanayofanya madhalimu. Hakika Yeye anawaakhirisha tu mpaka siku ambayo macho yao yatakodoka (yatoke nje kwa hofu). Wawe wanakwenda mbio, vichwa juu, na macho yao hayapepesi, na nyoyo zao tupu Qur ( 14:42:43). Mfumo na muundo wenyewe wa dini ya Kiislamu ndiyo unaowafanya Waislamu wasikubali kudhulumiwa. Kama dhulma dhidi ya Waislamu itaendelea katika jamii yoyote ile, lazima atapatikana kiongozi madhubuti, aliye tayari kujitoa muhanga, ili kukomesha dhulma hiyo. Hilo ni jambo la kimaumbile tu. Mwenyezi Mungu Mtukufu ndiye aliyeumba maisha haya na akayewekea mfumo maalumu ambao hauwezi kubadilishwa hata kidogo, kama mwenyewe alivyobainisha ndani ya kitabu chake: Hii ni kawaida ya Mwenyezi Mungu iliyokuwa kwa wale waliopita zamani; wala hutapata mabadiliko katika kawaida ya Mwenyezi Mungu Qur(33:62). Mahali pengine Mwenyezi Mungu anasema: Wala hutapata mabadiliko katika desturi yetu. Qur (17:77). Sehemu ya mfumo huu wa Mwenyezi Mungu ni mapambano baina ya Haki na Dhulma. Haitakuja kutokea duniani Haki ikavumilia Dhulma, wala Dhulma ikakubali Haki. Mapambano baina ya Haki na Dhulma yataendelea tu mpaka siku ya Kiyama, na yanaweza kuchukua sura mbalimbali kisiasa, kidini, kiutamaduni na hata mapigano. Ndipo wanapokuja watu madhubuti kama Sheikh Ponda Issa Ponda. Sheikh Ponda, mara zote amekuwa mstari wa mbele katika kupigania haki za Waislamu Tanzania. Amepata misukosuko mingi sana kutoka serikalini kwa sababu ya msimamo wake usiyoyumba wa kupigania haki za Waislamu zinazodhulumiwa. Kuna baadhi ya watu, wengine ni ndugu zetu, wanamuona Ponda ni mtu hatari, anayepanga kuleta vurugu katika nchi. Wao ni vipaza sauti vya propaganda za madhalimu. Uhodari wao uko katika kukosoa tu harakati zinazofanywa na Ponda, lakini siyo wao kupanga harakati hizo! Waislamu wa Tanzania wanahitaji viongozi kama Sheikh Ponda Issa Ponda katika mazingira yaliyopo sasa. Yaani viongozi wakweli, waadilifu, wanaoweza kujitoa muhanga na walioungana kihisia

Makala

Dhuul-Hijja 1433, IJUMAA NOVEMBA 9 - 15, 2012


mpaka haki ipatikane. Jambo la kuzingatia ni kwamba Waislamu wasije wakapoteza dira yao kutokana na matukio yaliyotokea siku chache zilizopita. Wajue kwamba Haki na Dhulma kamwe haviwezi kukaa pamoja. Jitihada kubwa zinafanywa na maaskofu, wanafiki, Serikali, wanasiasa na vyombo vya habari kuwatia ujinga Waislamu wa Tanzania, wasitambue ukweli wa kimaumbile kwamba kuna mgongano wa kudumu kati ya Haki na Dhulma, kama ulivyo mgongano kati ya Imani na Kufru au Ukweli na Uongo. Na huo mgongano ndiyo uhalisia tunao ushuhudia leo kati ya Waislamu na Serikali hapa nchini. Kama tulivyoona awali, mbinu, mikakati na miundo wa kupigania haki zinazoporwa ni tofauti sana. Kuna baadhi ya Waislamu wanaweza kuona Sheikh Ponda amefanya jambo lisilo na faida wala tija kuhamasisha Waislamu kuchukua haki yao kwa mikono yao wenyewe. Wamejitakia wenyewe matatizo yaliyowakuta. Ningependa kuwakumbusha Wa i s l a m u k w a m b a h a k i huchukuliwa haiombwi. Na Uislamu una mtazamo tofauti sana kuhusu faida au tija. Kwa mujibu wa dini ya Kiislamu, faida huzunguka kwenye Sheria na Kanuni za Mwenyezi Mungu tu, na siyo mawazo nyu ya kibinadamu. Kila palipo na Uislamu, basi faida hupatikana na siyo kinyume chake. Waislamu wanapaswa kutekeleza maagizo ya Kiislamu, bila kuzingatia faida au hatari inayoweza kupatikana. Faida ni ile iliyozungumzwa na Sheria ya Mwenyezi Mungu tu. Kwa maneno mengine, faida kwa Waislamu ipo katika kumtii Mwenyezi Mungu na kufuata Uislamu. Mwenyezi Mungu anasema: Mmelazimishwa kupigana vita (kwa ajili ya dini). Nalo ni jambo zito kwenu. Lakini huenda mkachukia kitu, nacho ni kheri kwenu. Na huenda mkapenda kitu nacho ni shari kwenu. Na Mwenyezi Mungu ndiye anayejua, (lakini) ninyi hamjui Qur (2:216). Aya hii inaonyesha wazi kwamba Mwenyezi Mungu ameamrisha vitu ambavyo vinaweza visionekane kama faida kwa jicho la kibinadamu, ambavyo Waislamu wanapaswa kuvitekeleza bila ya kuzingatia maoni yao kuhusu vitu hivyo. Uwezo wa kuamua lipi jema na lipi baya, lipi lenye tija na lipi lisilo na tija kuhusu vitu hivyo siyo wa kibinadamu. Kwa hiyo Sheikh Ponda na Waislamu wengine wanapoamua kuondoa munkari kwa mikono yao, jambo ambalo wengine hatuwezi kwa sababu ya woga; na kisha kupata misukosuko waliyopata kutoka Serikalini, hatupaswi kuwaona wamefanya jambo baya lisilo na tija.

AN-NUUR

Mapambano ya kudai haki yako pale pale


na umma wanaouongoza. Ukipitia Sira ya Mtume wa Mwenyezi Mungu haraka haraka, utaona alipambana vikali dhidi ya dhulma. Kule Makkah, Mtume alikuwa akifumua imani za Washirikina na kushambulia mfumo wao wa maisha, bila woga wala kulegeza msimamo. Kiukweli, Mitume wote wa Mwenyezi Mungu wamefuata njia hii, na wote walipingwa vikali na mamlaka zilizokuwa zikitawala maeneo yao. Mimi sioni taabu sana iwapo Sheikh Ponda ataandamwa na viongozi wa Serikali inayokandamiza Waislamu. Au akiandamwa na Maaskofu, au Bakwata au vyombo vya habari vinavyotumikia Mfumo - Kristo. Ila naumia sana ninapoona watu wenye majina ya Kiislamu nao wakimshambulia Ponda! Wa n a t u m i k a t u d h i d i y a Waislamu wenzao. Kama tulivyoona awali, ingawa mapambano dhidi ya dhulma ni sehemu ya ukweli wa kimaumbile, lakini mbinu zake, mikakati yake na miundo yake hubadilika. Kwa mfano, kuna baadhi ya watu wanaona njia iliyotumiwa na Sheikh Ponda, kuchukua kwa nguvu kiwanja cha Waislamu kilichouzwa kinyemela haikuwa sahihi. Wanadhani mchakato wa kisheria ungetumika zaidi kukia lengo kuliko matumizi ya nguvu. Wengine wanaona njia za kidiplomasia zingetumika, yaani kukaa meza moja na Bakwata, waliouza kiwanja kinyemela, na kuzungumza nao mpaka muafaka upatikane. Sijui kama kuna diplomasia ya kuzungumza na wahalifu, au huenda nimeelewa vibaya. Lakini, katika medani ya diplomasia, huwezi kufanya mazungumzo ya pande mbili zinazovutana, iwapo upande mmoja hauna negotiating power . Mazungumzo ya Waislamu na Bakwata hayawezi kuleta tija, kwa sababu Bakwata imedhibiti kila kitu, na Waislamu hawana kila kitu. Ni sawa na mazungumzo ya Wapalestina na Mayahudi. Hayana maana yoyote kwa Wapalestina! Pia mchakato wa sheria hauwezi kuleta jawabu. Ni vyema ikaeleweka vizuri kwamba wakati mwingine sheria zipo kwa ajili ya kulinda uhalifu. Tangu lini haki za Waislamu wa Tanzania zikapatikana kupitia mchakato wa sheria bila ya shinikizo? Askofu Mwingira wa kanisa la Efatha amevamia kiwanda na kuharibu mali pale Mwenge, lakini mpaka leo yuko huru, ila Sheikh Ponda akivamia eneo ndiyo sheria inakuwa na macho! Sheria za nchi hii zinawashughulikia tofauti Sheikh na Askofu kwa kosa lile lile! Ni ukweli unaofahamika vyema kwamba historia haijawahi kushuhudia hali ambayo viongozi wa jamii fulani ya watu wanakuwa mawakala wa maadui wa watu wao. Zamani, viongozi wa watu mara zote walikuwa pamoja na watu wao dhidi ya maadui. Hata kama wakishindwa, viongozi watafanya harakati za kujikomboa wakiwa bega kwa bega na watu wao dhidi ya maadui. Lakini leo hali ni tofauti kwa Waislamu nchini Tanzania. Bakwata inayojitapa kuwa taasisi kiongozi ya Waislamu wa Tanzania inatumia rasilimali za watu wake, kuwanufaisha maadui wao! Bakwata ndiyo imekuwa silaha kali ya maadui dhidi ya Waislamu. Ni msiba mkubwa sana unaotukabili ndugu zangu - hili dude Bakwata! Angalia wale viongozi wenye uchungu na Waislamu, mara zote wamekuwa wakiwasihi waumini wenzao kutuliza munkari na kufanya lile lenye manufaa zaidi, ikiwemo kuepusha maafa yasiyokuwa ya lazima. Watu mashuhuri, kama Prof. Ibrahim Lipumba, ingawa si kiongozi wa kidini, lakini alifanya jitihada kubwa za kuwatoa ndani viongozi wa Waislamu waliokamatwa, kisha akatembelea vyombo vya habari jioni ile ile kuwasihi Waislamu wasiandamane baada ya Swala ya Ijumaa ili kuepusha maafa. Waislamu kwa busara kubwa waliona mantiki ya kutoandamana. Prof. Lipumba alikuwa ameungana kihisia na Waislamu wanaolalamika na ndiyo maana wakamuelewa na kumtii. Hii ndiyo sifa ya kiongozi. Kama ujumbe ule wa kuwataka Wa i s l a m u w a s i a n d a m a n e ungetolewa na Bakwata, wanaojifanya kuwa viongozi wa Waislamu, kupitia masheikh wao, Alhad Mussa Salumu au Issa Shaaban Simba, nina hakika Waislamu wasingewatii. Kwa sababu, kama ilivyo kawaida yao, wangeanza na kejeli na vitisho, jambo ambalo Waislamu hawalipendi kabisa. Lakini pamoja na yote yaliyotokea, ajenda ya Waislamu wa Tanzania kudai haki zao zinazokandamizwa na Serikali iko pale pale. Mapambano ya kudai haki huwa hayakomi

SHEIKH Ponda Issa Ponda (kushoto)

10

Makala

Dhuul-Hijja 1433, IJUMAA NOVEMBA 9 - 15, 2012

AN-NUUR

Maendeleo ya Uislam vijijini


na kwenda kubatizwa. Huyu Padri Yusufu alikuwa akijaribu sana afanikiwe kufanya hivyo. Mji mdogo wa Uvinza nao ni kama hivyo hivyo. Kwa miaka zaidi ya mia moja umekuwa ni mji wa Kiislamu. Katika miaka ya arobaini na mwanzoni mwa hamsini kanisa lilikuwa likijulikana kama CMS (Church Missionary Society) ambalo sasa linajulikana kuwa ni Kanisa Anglikana walijaribu kufungua misheni yao hapo Uvinza. Ilibidi wahame kwa kukosa mafanikio. Baadae Kanisa Katoliki nao walika na kujenga kanisa lao hapo. Walichofanikiwa ni kupata jambo la kusikitisha kuwa hivi sasa hali imebadilika kabisa. Uislamu uko mashakani. Huko nyuma palikuwa na kanisa moja tu la Katoliki pale Ujiji zee la zamani na baadae katika miaka ya hamsini walijenga lingine Kigoma mjini. Leo hii hali haiko hivyo kiasi kwamba Uislamu uko mashakani. Ujiji tu peke yake sasa kuna makanisa takriban matano ya madh-hebi mbali mbali. Uvinza napo pameingiliwa pakiwa na makanisa zaidi ya sita. Wale walioshindwa kueneza dini yao, miaka hiyo ya nyuma, CMS na Katoliki, leo wapo kwa kasi kabisa. Sita katika kimji kidogo cha watu takriban thelethini na tano wanahamia Dar es Salaam tu wale wa BAKWATA wao ni wanasiasa wa CCM zaidi ya kuwa masheikh. Bahati nzuri ni kuwa pale Uvinza kwa mfano kuna Alim vijana ambao wanakerwa na mamabo haya. Mmoja ni Ustadh Majaliwa Issa Ndagojwe ambaye katika Khutba ya siku ya LJumaa alidokeza kuwa wakati akisafiri kwa treni akienda Tabora alikaa karibu na wachungaji wawili wa kanisa moja la Pentecoste. Aliwasikia wachungaji hao wakijigamba jinsi gani walivyoweza kuusimamisha Ukristo katika vijiji vingi katika mkoa wa Kigoma hasa vile vilivyo kati ya Uvinza na Nguruka. Wakijigamba kwamba tayari wamekwisha jenga makanisa kote huko na kuna wachungaji wenzao wakieneza dini yao. Huyu Ustadh Majaliwa Issa Ndagijwe hakusita kuwakosoa viongozi wa dini hasa wa BAKWATA kuwa wao wamelala usingizi tu wakati Uislamu unapigwa vita. Bahati mbaya sana mji mdogo wa Uvinza unakosa maendeleo ya maana kwa sababu kutokuwepo na uchumi wa kuaminika. Kiwanda kidogo cha chumvi kilichoko hapo hakitoshelezi kuwawezesha wenyeji kuweza kujikimu vya kutosha. Hivyo maendeleo ya kila aina ni duni san. Waislamu wa hapo hawana uwezo mkubwa wa kujiendeleza wenyewe. Pana misikiti mitatu ambao mmoja, Masjid Taqwa ndio shina la dini hapo kwa vile ulijengwa takriban miaka mia moja iliyopita. Jamii ya Kihindi ya KiPunjabi (leo hii wanaitwa wa Pakistani) ndio walianzisha harakati za kuujenga msikiti huo. Vizazi vya WaPunjabi hawa viko hapo mpaka leo

Na Khalid S Mtwangi

K U M E K U WA na malalamiko ya muda mrefu sana kuwa maendeleo makubwa ya Uislamu yamekuwemo katika miji mikubwa tu. Ni jambo la kusikitisha kuwa hata vile vijiji ama miji midogo iliyokaribu na miji hiyo mikubwa, nao wamesahauliwa. Huko nyuma katika gazeti hili kulitolewa mfano wa ustadh mmoja aliyetembelea kijiji kilichoko karibu ya Tabora ambako alishindwa kuendelea na swala ya L J u m a a k w a s a b a b u alivyokuwa akiboronga yule Imam ambaye ndiye alikuwa khatib pia. Hakika Tabora pamekuwa ni mji wa mashina ya Uislamu kwa muda mrefu sana na wapo Alim wengi tu hapo mjini. Shida ni kwamba hawa Alim wanajishughulisha na malumbano mijini na kujigamba nani kasoma zaidi ya mwenzake. Hali kama hiyo ya kusikitisha nayo inapatikana vitongoji vinavyizunguka Ujiji na Kigoma yote kwa jumla. Hakuna asiyefahamu sifa ya Ujiji katika nyanja ya ilm ya dini ya Kiislamu. Kwa sababu hiyo ni sawa kabisa kutegemea kuwa takriban mkoa wote wa Kigoma ungekuwa nao ni ngome ya Uislamu. Huko nyuma kulikuwepo wamishionari wa Kikristo kama aliyekuwa akijulikana kama Padri Yusufu wa pale misheni Kagera. Huyu alikuwa ni raki wa kila mtu pale Ujiji. Lilikuwa ni jambo la kawaida kabisa kumkuta kijiweni katika kundi la waSwahili naye akinywa nao kahawa na akipiga domo. Alikuwa akiijuwa lugha ya Kiha kuliko hata wale watu wa mjiji Ujiji. Alipofariki takriban mji mzima wa Ujiji ulihudhuria mazishi yake ingawa yalikuwa ndiyo yale ya Kikatoliki. Ni jambo la kujivunia kuwa mpaka alipofariki hakuwahi kumrubuni hata mtu mmoja, awe kijana ama mzee, aliyekubali kupotea

Kanisa Katoliki Uvinza

Masjid Takwa ulio na umri wa karibu miaka mia moja

Hawa waislamu wa Uvinza wanahitaji misaada sana kwa sababu uwezo wa Waislamu na wenyeji wote kwa jumla ni duni sana. Wengi hujikimu kwa kufanya vibiashara vidogo vidogo tu ambavyo husaidia kupata chakula tu. Huko nyuma Uvinza palikuwa ni mapanda njia ya mizigo na watu kwenda Mpanda kulikokuwa na migodi ya dhahabu na madini nyingine. Kweli wakati huo uchumi wa Uvinza ulikuwa mzuri lakini hivi sasa wenyeji hujishughulisha sana na vibiashara vidogovidogo tu Kweli pana kiwanda cha chumvi ambacho kimekuwepo kikizalisha chumvi tangu wakati wa Utawala wa Kidachi (Jeremani) na hata wakati wa WaArabu. Lakini uzalishaji wa kiwanda hicho na ajira inayopatikana kutoka kiwanda hicho haikidhi kabisa kuendesha maisha bora ya wenyeji. Wameshindwa hata kuendeleza msikiti mdogo ulio Kibaoni ambaho ni kitongoji cha mji huo. Hali ya kimsikiti hicho ni aibu sana kwa vile jirani yake pana kituo kikubwa tu cha Kanisa Katoliki ambacho maendeleo yake ndiyo yanaaibisha nguvu ya Waislamu. Waislamu wa Uvinza wamejaribu sana kuomba misaada kurekebisha hali hii ya aibu. Maombi yamepelekwa kwa taasisi za Kiislamu nchini na nje ya nchi kujaribu kuuhami Uislamu. Ni jambo la kusikitisha sana kuwa taasisi hizo zimekuwa kimya. Wakati huo huo Kanisa Katoliki na hata makanisa mengine wamo mbioni kuwaghilibu vijana wa Kiislamu na wasio Waislamu kujiunga na dini ya Kikristo. Waislamu wa Tanzania tunawezaji kuuokoa Uislamu??

Msaada wa Kuchimbwa KISIMA


Msikiti Kibaoni, kitongoji cha Uvinza. Hapa ni upande wa wananawake
utalii wa ndani tu kutembelea daraja la kamba suspension bridge walilojenga kuvuka Mto Ruchugi. Hivyo baadae nao walihama. Hiyo ilikuwa katika miaka ya sabini. Hivyo ndivyo Uislamu ulivyojenga mizizi hapo Uvinza na Kigoma/Ujiji kwa jumla. Bahati mbaya sana na ni elfu. Hata yale makanisa ya walokole, kama ya Bishop Kakobe, yanayo ongozwa na mitume kama Apatha, Church of God nayo yamejikita hapo. Baya zaidi ni kuwa Waislamu wao wamelala usingizi tu wala hawaoni kuwa Uislamu katika sehemu hizo uko mashakani. Masheikh wa Kigoma wengi

Msikiti wa KIBUTA- Kitondwe B Munga- Kisarawe Wanaomba Msaada wa Kuchimbwa KISIMA cha Maji. Kwa Mawasiliano Piga No. 0656 092 436 au 0685 171 221

11
(Imewekwa kwenye mtandao Februari 27, 2012) NI kweli maajabu hayaishi, hasa nchini Nigeria. Kuna usemi wa siku nyingi kuwa ni rahisi zaidi kumshawishi mtu achome nyumba yake kuliko kumshawishi aache upendeleo wake wa asili. Sikudhani hata siku moja kuwa usemi huo ungekuwa kweli kama ulivyo, hadi niliposoma kuwa wapiga mabomu tisa, wanaoaminika k u w a n i Wa k r i s t o , walikamatwa wakijaribu kulipua Kanisa la Kristo la Nigeria (COCIN) lililoko Miya Barkate, kilomita 20 katika barabara ya JoshBauchi jimbo la Bauchi. Watuhumiwa wa ulipuaji ni Lamba Goma, Filibus Danasa, Joshua Ali, Danjuma Sabo, Joseph Audu, Simon Gabriel, Bulus Haruna, Yohanna Ishaya na Daniel Ayuba (aliyekuwa Katibu wa PDP chama kilichoko madarakani, Peoples Democratic Party cha Rais Dk. Goodluck Jonathan) katika kata ya Tilden Fulani, wilaya ya Toro, jimbo la Bauchi. Wa t u h u m i w a h a o n i wanachama wa kanisa hilo la COCIN eneo al Unguwar Rimi, makazi madogo mapya ya Wakristo kati ya Tilden Fulani na vilima vya Shere. Watuhumiwa hao ambao walipigwa vibaya na wananchi waliokolewa na polisi na halafu kufungiwa katika kituo cha polisi cha tarafa ya Toro kabla ya kuhamishiwa kituo kikuu cha polisi jimbo la Bauchi. Wakati huo huo katika jimbo la karibu la Plateau, mlipuko wa bomu uliripotiwa katika makao makuu ya kanisa hilo la COCIN katika ibada ya Jumapili. Mchungaji wa kanisa lililolengwa la COCIN katika eneo la Bauchi ni Ishaya Izam, ambaye alianza kazi katika kituo hicho kutoka makao makuu ya COCIN mjini Jos, ambako bomu lililipuka (asubuhi hii). Hakuna uhakika kama milipuko hiyo ya mabomu inahusiana. Taarifa kuhusu tukio hilo katika jimbo la Bauchi ilikuwa haijatolewa na polisi. Kwa mujibui wa Shirika la Habari la Ufaransa, AFP, watu watatu waliripotiwa kuuawa katika mlipuko wa Jos. Shambulio hilo lilisababisha vurugu zilizofanywa na vijana wa Kikristo ambao walianza kuua watu ovyo. Waislamu takriban wawili waliuawa na kundi hilo la vijana wa Kikristo. Watu hao walivutwa kutoka kwenye pikipiki zao baada ya kusimamishwa

Makala

Dhuul-Hijja 1433, IJUMAA NOVEMBA 9 - 15, 2012


Nigeria vimelishukia gazeti la The Sun kwa kupendelea upande mmoja katika matukio ya Jos, na kwingineko kuonyesha kuhusishwa isivyopasa kwa kundi la Boko Haram na pia hatari kwa Waislamu wanaokaa jimbo la Delta (ufukwe wa mto Niger wenye visima vya mafuta na uharibifu wa mazingira) kutokana na magadi wa Kikristo. Kama matukio hayo ya kushangaza yanavyoonyesha, Boko Haram tayari imetangaza kuhusika na milipuko ya Jos. Aliyedaiwa ni msemaji wa Boko Haram, Abul Qaqa, ambaye amewekwa kizuizini na SSS (Idara ya Usalama wa Taifa) alidai kuhusika kwa niaba ya kundi hilo. Tulifanya shambulio dhidi ya kanisa COCIN mjini Jos leo na tulifanya tulichofanya kama sehemu ya nia yetu ya kulipiza kisasi mauaji na udhalilishaji wa Waislamu katika Jos katika miaka 10 iliyopita. Ni vipi Abul Qaqa alihakikisha kuwa ilikuwa ni kundi lake lililohusika? Nina uhakika kama wapiga mabomu wa Kikristo wangefaulu Bauchi, angetangaza kuhusika na ulipuaji huo pia. Hivi kuna shaka gani kuwa uongozi wa Boko Haram hauna uwezo wa kuhakikisha vitendo vya wanachama wake wote. Boko Haram inaweza kuwa haihusiki na baadhi ya mashambulio ambayo wamedai kuhusika nayo.

AN-NUUR

Boko Haram walipogeuka Wakristo


katika kizuizi cha magari kilichowekwa na vijana hao wa Kikristo, polisi walisema. Pia maduka mengi ya Waislamu yalichomwa moto, mwandishi wa AFP aliyekuwa eneo hilo alisema. Taarifa kutoka Jos (asubuhi hii) inaonyesha kuwa Waislamu wanane waliuawa bila sababu na kundi hilo la vijana. Mjini Bauchi, msemaji wa kamandi ya polisi, Hassan Mohamed, alithibitisha tukio hilo lakini akasema atatoa maelezo ya kina wakati mwingine. Wa t u h u m i w a w a k o makao makuu ya polisi lakini tutatoa maelezo ya kina baada ya wapelelezi kupata mwanga wa kutosha wa hali ilivyokuwa, alisema. Hata hivyo hiyo si mara ya kwanza ambako Wakristo wamehusishwa na mashambulizi dhidi ya makanisa na Wakristo. Itakumbukwa kuwa Mkristo, Wi s d o m K i n g s , a k i w a amevalia kama Muislamu, alikamatwa akiwa anajaribu kuchoma moto kanisa huko Yenagoa, jimbo la Bayelsa. Pia, katika jimbo la Adamawa Yola, wiki kadhaa kabla, watu watatu waliuawa katika kanisa na Waislamu walisemwa ndiyo walihusika. Lakini uchunguzi wa polisi ulionyesha kuna mgogoro mkubwa ndani ya familia moja ya Kikristo. Mwaka jana mwanamke wa Kikristo, Lydia Joseph, alikwenda katika kanisa la parokia yake mjini Bauchi na kujaribu kuliwasha moto. Katika jimbo la Plateau, mtu anayesemakana ni Mkristo alikamatwa akijaribu k u l i p u a k a n i s a . Wa t u wenye silaha waliwapiga risasi kundi la Wakristo waliokuwa wakikutana kanisani, halafu ikajulikana kuwa waliokamatwa ambao wako katika kuhojiwa siyo Waislamu na yote inatokana na mifarakano ya ndani. Kama kawaida na kama ilivyotazamiwa, vyombo vya habari vinapuuzia tukio la Bauchi kwa sababu haliendani na mielekeo yao iliyosukwa tayari ya propaganda dhidi ya Waislamu na dini ya Uislamu. Wakristo hawawezi kuwa magaidi, ugaidi ni kitu cha Kiislamu, ndiyo wanavyodhani, wakati vielelezo vyote vinaelekea kinyume chake. Gazeti la Vanguard nchini Nigeria na mengine makubwa yanaripoti tukio hilo kama ushindani kati ya wanachama wa kanisa hilo. Lini wanachama wa Kanisa walianza kutumia milipuko kumaliza migongano? Tunaweza kuwa sahihi kusema kuwa tukio la ulipuaji bomu la Mandala siku ya Krismasi na

MMOJA wa watuhumiwa waliokamatwa wa Boko Haram anayedaiwa kuwa ni Mkristo

mashambulio mengine dhidi ya makanisa, likiwemo lile la Jos, yalifanywa kutokana na migongano katika jumuia ya Kikristo? Vyombo vya habari vya

Lipumba alivyoepusha shari Ijumaa iliyopita


Inatoka Uk. 12

Kikwete, kupitia wasaidizi wake ili amfahamishe mantiki na sababu ya hatua alizochukua ili na yeye atumie uwezo wake alionao ili Sheikh Ramadhan Sanze na wenzake waachiliwe, kwa mustakabali wa Taifa, hata hivyo alisema hakuweza kumpata, Rais (Jakaya) kwa wakati muafaka. Alisema, katika kuhangaika zaidi ili viongozi hao waachiliwe, siku ya Ijumaa (iliyopita) alipata fursa ya kuzungumza na IGP na kumfahamisha sababu

hawajaachiwa. Niliwasiliana na RCO na nikabaini kuwa suala hilo haliko tena chini ya uamuzi wake na litakamilishwa siku ijayo, (Ijumaa). Alisema. Alisema, juhudi zake hazikuishia hapo kwani siku hiyo hiyo usiku wa Alhamisi kuamkia Ijumaa (wiki iliyopita) alijaribu kuwasiliana na Rais

ya juhudi alizochukua na mategemeo kuwa Sheikh Sanze na wenzake wangeachiwa toka siku ya Alhamisi. Ninakiri kuwa katika mazungumzo ya simu, IGP Mwema alikuwa msikivu na mkarimu sana katika kauli yake. Alinishukuru kwa kauli niliyoitoa katika vituo vya televisheni na kuwa atafuatilia suala nililomueleza. Hatimaye Sheikh Ramadhan Sanze na wenzake waliachiwa siku ya Ijumaa. Alisema. Prof. Lipumba alisema, baada ya mlolongo wote huo na juhudi zake za kusimama kati ya Waislamu na Jeshi la Polisi, anaamini kuwa Waislamu wengi na wananchi kwa ujumla walipokea vizuri wito wake na hawakushiriki katika maandamano, japo kwamba wapo waliohoji hatua yake hiyo.

AN-NUUR
12
Na Bakari Mwakangwale
WAKATI wanasiasa na wakuu wa vyombo vya dola na hata baadhi ya Masheikh wakitoa kauli za vitisho na kejeli kwa Waislamu, Profesa Ibrahim Lipumba, wiki iliyopita alifanya juhudi kubwa kuepusha shari ambayo ingewasibu Waislamu na wananchi wa Dar es Salaam. Katika jitihada zake, Prof. Kipumba alisimama kati kama msuluhishi wa Polisi na Waislamu huku akipigania kupewa dhamana viongozi waliokuwa wamekamatwa. Hata hivyo, baadhi ya watu wamemshutumu Lipumba hali ambayo imempelekea kutoa ufafanuzi akisema kuwa ndani ya Tanzania kuna Watanzania wengi, miongoni mwao ni Waislamu ambao nao pia wanastahiki kutendewa haki na kusikilizwa. Profesa Lipumba, aliye Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF), Taifa, ametoa kauli hiyo mbele ya waandishi wa habari mwishoni mwa wiki hii, akijibu wale waliohoji sababu za yeye kuingilia kati mvutano baina ya Waislamu na Jeshi la Polisi nchini. Katika majibu ya hoja hizo, Prof. Lipumba, alisema kwamba CUF inasimamia Haki Sawa kwa Wananchi Wote, kwani miongoni mwa Watanzania wamo Waislamu, ambao nao wanastahiki kupata haki katika nchi yao. Kuna Watanzania wengi ambao miongoni mwao ni Waislam na wao pia wanastahiki kutendewa haki katika nchi yao. Amesema Prof. Lipumba. Ama kuhusu hoja kwamba katika mikutano ya CUF, hujaa balaghashia na hijabu, utadhani kuna mawaidha, Prof. Lipumba, alisema ni vyema wanaohoji suala hilo wakasoma historia ya nchi hii ambayo hata picha zinaonyesha umati wa watu waliokuwa katika mikutano ya kupigania Uhuru, iliyokuwa ikihutubiwa na Mwalimu Nyerere, wengi wao walikuwa wamevaa balaghashia na baibui, hivyo haoni kama ni tatizo. Kuhusu balaghashia na baibui ni vyema vijana wakatazama histori, zipo picha za umati wa watu ukihutubiwa na Mwalimu Nyerere wakati wa kupigania Uhuru wa nchi hii. Picha hizo zinaonyesha waliokuwa wakipigania Uhuru wengi walikuwa wavaa balaghashia na baibui, hata Mwalim Nyerere alipewa zawadi nyingi za balaghashia na akaamua kuwa anazivaa. Alibainisha Prof. Lipumba. Prof. Lipumba, alitanabahisha kwamba, kushamiri kwa demokrasia ya kweli mahala

Dhuul-Hijja 1433, IJUMAA NOVEMBA 9 - 15, 2012

Usikose nakala yako ya AN-NUUR kila Ijumaa na Jumanne


kuachiliwa kwa viongozi wa Kiislamu waliowakamata . Prof. Lipumba, alisema kuwa walifahamishwa kuwa itabidi wafanyiwe mahojiano na baadaye wataachiliwa isipokuwa Ust. Mkadam Swalehe, ambaye walielezwa kuwa ana faili jingine pale Polisi linaloendelea kufanyiwa upelelezi. Tulifahamishwa kuwa nitume mtu saa 10:30 jioni ili aweze kufuatilia utaratibu wa kuachiliwa watuhumiwa watatu akiwemo Sheikh Ramadhan Sanze, Sadik Gogo na Mzee Abdillah. Alisema. Alisema, taarifa za kukamatwa kwa Sheikh Ramadhan Sanze na wenzake zilikuwa zinaenea kwa kasi na kupandisha hasira za Waislamu wengi, jambo ambalo lilimpa wasiwasi kuwa munkar huo unaweza kupelekea Waislamu wengi kuandamana baada ya sala ya Ijumaa. Alisema, aliamini kwamba ikiwa Sheikh Ramadhan Sanze na wenzake wataachiwa na Waislamu wakapata taarifa hiyo, inaweza kusaidia kupunguza hamasa na watu wasishiriki maandamano baada ya sala ya Ijumaa. Niliwasiliana kwa simu na kuzungumza na RCO na nikiamini kuwa Sheikh Ramadhan Sanze, Sadik Gogo na Mzee Abdillah, wataachiwa baada ya kukamilisha mahojiano, na wakati huo ilikuwa inakaribia majira ya

Lipumba alivyoepusha shari Ijumaa iliyopita

PROF. Ibrahim Lipumba


popote msingi wake mkubwa ni amani na utulivu na kwamba amani ya kweli haipatikani bila kuwepo haki miongoni mwa makundi katika jamii. Akizungumzia kushikiliwa kwa Sheikh Ponda Issa Ponda na kunyiwa dhamana alisema, Kiongozi huyo wa Waislamu ana haki ya msingi ya kupatiwa dhamana hata kama kauli zake zinaichefua Serikali. Alisema, kesi ya Sheikh Ponda, msingi wake ni madai ya kiwanja, hivyo kimsingi kesi ya madai yanayomkabili ilipaswa kusuluhishwa na Mahakama ya Ardhi. Prof. Lipumba, alisema anasikitishwa kuona viongozi wa Serikali kushindwa kutumia njia za busara na juhudi za makusudi za kukutana na kuzungumza na Maimam wa Misikiti na viongozi wa Jumiya za Kiislamu, ili kupunguza munkari kwa Waislamu, badala yake kumekuwa na kauli za vitisho na kamatakama kwa viongozi hao. Nasikitika sana katika kipindi hiki tete, viongozi wa Serikali wameshindwa kuchukua juhudi za makusudi kuzungumza na Maimam wa Misikiti na viongozi wa asasi za Kiislam. Badala yake wameachia kauli za vitisho vya Kamanda Kova, ndiyo viwe mawasiliano kati ya Serikali na Waislam. Amesema Prof.

SHEIKH Ramadhan Sanze


Lipumba. Akitoa rai kwa Serikali na Jeshi la Polisi, Profesa Lipumba alisema, ni vyema Serikali ikatumia busara na kuwasiliana na Maimamu wa Misikiti na viongozi wa asasi za Kiislam kusikiliza hoja na malalamiko yao kisha wazifanyie kazi. Kwa upande wake alisema, atafanya juhudi za makusudi kuzungumza na viongozi wa asasi za Kiislamu pamoja na viongozi wa Makanisa ya Kikristo. Alisema, madhumuni ya mazungumzo hayo ni kuwafahamisha mantiki ya juhudi zake katika kumaliza mivutano na kushauriana misingi muhimu ya Waumini wote kuheshimiana na kuvumiliana ili kujenga Tanzania yenye haki sawa kwa wote. Aidha alisema, amefanikiwa kuongea na Rais Jakaya Kikwete, juu ya suala hilo, akidai kwamba hali hiyo Rais, pia inamsononesha bila shaka alidai, huenda akaitafutia suluhisho la kudumu. Hatimaye nimepata fursa ya kuzungumza na Mheshimiwa Rais (Kikwete) hivi leo asubuhi na nikamueleza juhudi nilizozichukua kuweza kupunguza msimamo na kuwaomba Waislam wasishiriki kwenye maandamano baada ya sala ya Ijumaa. Ni wazi hali hii ya mtafaruku ndani ya jamii inamsononesha

IGP Said Mwema


sana Mheshimiwa Rais na ninaamini atajitahidi kwa uwezo wake wote kutafuta suluhisho. Alisema Prof. Lipumba. Hata hivyo Prof. Lipumba, alisema katika kutafuta suluhu ya mtafaruku huu, ataendelea na jitihada zaidi za kutafuta fursa ya kukutana na Rais Kikwete, ili aweze kubadilishana mawazo katika masuala hayo. Awali, Prof. Lipumba, aliwaambia waandishi wa habari kwamba alistushwa na kamatakama ya Jeshi la Polisi kwa viongozi wa Kiislamu, na kuhofia kwamba huenda ikazidisha hasira miongoni mwa Waislamu na kuvuruga mani. Alisema, siku ya Alhamisi (iliyopita) alisikia kwamba Sheikh Ramadhan S. Sanze, Sadik Gogo, Ustadhi Mukadam na Mzee Abdillah wamekamatwa na wamefikishwa Central Police Station. Nilistushwa na kamata kamata hii na nikahoa kuwa inaweza kuongeza jazba miongoni mwa waumini wa Kiislam, nikampigia simu Mkurugenzi wa Haki za Binadamu na Mahusiano ya Umma, Abdul Kambaya, tukutane kituo cha Polisi kuangalia kama tunaweza kuwawekea dhamana. Alisema Prof. Lipumba. Alisema, walipoka kituoni hapo walizungumza na RPC Suleiman Kova na RCOMsangi, kuhusu uwezekano wa

saa 12 jioni. Alisema Alisema, baada ya hapo, alifanya juhudi ya kuwasiliana na vyombo vya habari (Televisheni) kwa lengo la kuongea na Waislamu na akiwasihi wasiandamane baada ya sala ya Ijumaa, na kuwaahidi kuwa atalishughulikia suala hilo na viongozi wao wataachiwa. Hata hivyo, alisema, mambo hayakwenda kama alivyokuwa amekubaliana na Makamanda hao wa Polisi, kwani alidai baada ya kutoa taarifa katika vituo vya Televisheni na Radio Iman, kuwa Sheikh Ramadhan Sanze na wenzake wataachiliwa lakini hawakuachiliwa. Baada ya kuwasihi Wa i s l a m u w a s i s h i r i k i maandamano baada ya sala ya Ijumaa nilimpigia simu Abdul Kambaya kuulizia kama naweza kuzungumza na Sheikh Ramadhan Sanze. Kambaya akanieleza mambo yamebadilika na Inaendelea Uk. 11

Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na Business Printers Limited, S.L.P. 78495 Dar es Salaam.

You might also like