You are on page 1of 2

TaarifakwaVyombovyaHabari

TigonaReachforChangewazinduashindanolawajasiriamalijamii

Kilamshindikupokeadolazakimarekanimilioni20,000kwaajiliyautekelezaji
wamradiwake.
Dar es Salaam, Seeptemba 25, 2015. Tigo kwa kushirikiana na taasisi ya Reach for
Change zimezindua shindano wajasiriamali jamii liitwalo Tigo Digital Changemakers lenye lengo la kuibua mawazo ya kibunifu ambayo yatasaidia kutatuta
matatizo yanayowakabili watoto na vijana nchini.
Meneja mkuu wa Tigo Diego Gutierrez leo ametangaza uzinduzi wa shindano hilo
katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es Salaam ambapo
ametoa wito kwa watu kushiriki ili wajiweke katika nafasi ya kushinda fedha taslimu
dola za kimarekani 20,000 ambazo kila mshindi atapewa azitumie katika utekelezaji
wa mawazo yao ya kibunifu.
Tigo ikishrikiana na Reach for change itatoa tuzo ya dola za kimarekani 20,000 kwa
kila mmoja kwa washindi wawili ambao watakuwa na mawazao bunifu zaidi
kiteknolojia na kidijitali yaliyo na uwezo wa kuchangia kuleta maisha bora kwa
watoto katika jamii ya kitanzania, alisema Gutierrez.
Aliongezea kwamba, Lengo letu ni kupata mawazo ya kibunifu ya kidijitali ambayo
yataleta na kutatua matatizo yanayowakabili watoto kwa kiwango kikubwa huku
tukiendelea kuwekeza katika kukuza na kuimarisha huduma zetu za mawasiliano
katika maeneo yote nchini.
Mawazo yatakayowasilishwa kupitia shindano hili yanatakiwa kuonyesha uwezo wa
kutumia simu kidijiti tekinolojia ya habari na mawasiliano kuleta ufanisi wa
utekelezaji wa mradi husika. Watakaopenda kushiriki shindano hili wanaweza kutuma
maombi kupitia mtandao wa www.tigo.co.tz/digitalchangemakers, kwa mujibu wa
Gutierrez.
Kwa upande wake, Meneja wa Tanzania wa Reach for Change, Peter Nyanda, alisema
licha ya kupata kitita cha dola 20,000 washindi pia watapewa vifaa vya kuendeleza
utekelezaji wa mawazo yao ikiwa ni pamoja na kupata ushauri kutoka kwa
wafanyakazi waandamizi kutoka Tigo na Reach for Change. Aidha wataunganishwa

na wajasiriamali wengine ambao tayari wamenufaika kutokana na mpango huo.


Mchakato huu wa kuwapata wajasiriamali jamii wa kidigitali unaendana na mkakati
wa Tigo wa kuendeleza maisha ya kidijitali nchini. Huu ni mwaka wa nne mfulilizo
ambapo taasisi za Tigo na Reach for Change zimekuwa zikishirikiana kuwasaidia
wajasiriamali nchini. Jumla ya wajasiriamali watano wamenufaika na mpango katika
kipindi hiki ambao kwa pamoja na kupitia utekelezaji wa miradi yao wamewasaidia
jumla ya watoto zaidi ya 10,000 nchini.
Mwisho
Kuhusu Reach for Change
Reach for Change ni shirika lisilo la kiserikali lililoanzishwa nchini Sweden na
lilianzishwa na Kinnevik, mwanzilishi wa kapuni ya Millicom. Dira ya Reach for
Change ni kuhamasisha harakati za kimataifa za ubora, ujasiri na shauku kwa
mawakala wa mabadiliko, kujenga dunia iliyo bora kwa watoto. Reach for Change
inabainisha na kusaidia wajasiriamali wa kijamii barani Ulaya, Afrika na Asia.
Kuhusu Tigo
Tigo ni kampuni ya mawasiliano ya simu za mikononi yenye ubunifu mkubwa nchini
Tanzania , ikijulikana kama nembo ya maisha ya kidijitali yanayojitosheleza. Inatoa
huduma mbalimbali kuanzia huduma ya sauti, ujumbe mfupi, intaneti yenye kasi na
huduma za kifedha za kwenye mitandao ya simu za mikononi, Tigo imeanzisha
ubunifu kama vile Facebook ya Kiswahili, Kiunga cha Tigo Pesa kwa watumiaji wa
simu za Android & iOS, Tigo Music (Deezer)na huduma ya kwanza Afrika Mashariki
kutuma fedha kwa njia ya simu za mikononi nje ya nchi yenye uwezo wa kubadili
sarafu ya nchi husika.
Intaneti ya Tigo ya 3G inatoa huduma bora kwa wateja wake katika mikoa yote nchi
nzima. Kati ya mwaka 2013 na mwaka 2014 pekee kampuni ilizindua zaidi ya
maeneo mapya 500 yenye mtandao wa Tigo na kufanya kuwa zaidi ya maeneo 2000
ya mtandao na inapanga kuongeza uwekezaji wake mara mbili ifikapo 2017 katika
suala la upatikanaji wa mtandao na kuongeza uwezo wa upatikanaji wa mtandao kwa
maeneo yasiyofikika kabisa vijijini. Pamoja na kuwa na zaidi ya wateja milioni 9
waliosajiliwa, Tigo imeajiri zaidi ya watanzania 300,000 ikiwa ni pamoja na mtandao
wa wawakilishi wa huduma kwa wateja, wafanyabiashara wakubwa wa fedha za
kwenye simu za mikononi, mawakala wa mauzo na wasambazaji.
Tigo ni nembo kubwa ya kibiashara ya kampuni la Millicom, kampuni ya kimataifa
inayoendeleza maisha ya kidijitale katika nchi 12 pamoja na shughuli za kibiashara
katika Afrika na amerika ya Kusini na ina ofisi kubwa Ulaya na Marekani. Pamoja na
ujuzi Fulani walionao ambao unawafanya kubuni mara kwa mara na kuwafanya wawe
juu, Millicom anaendelea kujenga thamani kubwa kwa mbia; kutumia dhana yao ya
"mahitaji zaidi" hivi ndivyo wanafanya biashara na kurejesha nafasi yao kama
viongozi wa maisha ya kidijitale hasa katika masoko zaidi ya kipekee na yenye
changamoto.
Kwa taarifa zaidi tembelea: www.tigo.co.tz or wasiliana na:
John Wanyancha Meneja Mawasiliano

You might also like