Professional Documents
Culture Documents
Barabara ya Luthuli,
P.O Box 5380,
Dar es Salaam.
TANZANIA.
17/4/2016
"lakini tukiwatuliza kwenye mambo yao wana maji, wana umeme, wana
chakula, mtoto anaenda shule vizuri, anapata afya, akienda zahanati dawa
zipo, watatulia tu."
Alisema kwa hivi sasa kuna tatizo la watumishi hewa na wengine wamediriki
kumdanganya mkuu wao wa kazi na hayo ndiyo mambo ambayo hayaleti
picha nzuri katika serikali.
Aliwataka wakuu wa mikoa na wilaya nchini kuunga mkono jitihada hizo za
serikali ili kurejesha nidhamu na uwajibaikaji kwa watumishi wote.
Wakati huo huo, Makamu wa Rais jana alitembelea kiwanda cha kutengeneza
nguo cha Mazava ambapo aliutaka uongozi wa kiwanda hicho kuzingatia
masharti ya ajira na wafanyakazi kuchapa kazi kwa bidii ili Taifa liweze
kupata kodi na wao wapate mapato.
Akizungumza na wafanyakazi, Samia aliuhakikishia uongozi wa kiwanda
hicho kuwa serikali itazifanyia kazi changamoto za eneo na ukosefu wa ujuzi
kwa kuwapeleka vijana wengi kwenye Vyuo vya Ufundi Stadi (VETA) kujifunza
ushonaji.
Alisema Serikali ya Awamu ya Tano imeweka mkazo kwenye viwanda na
kusisitiza kwamba kupitia mpango wa EPZ viwanda vingine vinatarajiwa
kujengwa mkoani humo jambo ambalo litaongeza ajira kwa vijana.
Kiwanda hicho ambacho kilianza uzalishaji mwaka 2010 kina wafanyakazi
zaidi ya 2,000 na kwamba asilimia 100 ya nguo zinazozalishwa kiwandani
hapo zinauzwa nje ya nchi ambapo soko kuu liko Marekani.
Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
Morogoro
17/4/2016