Professional Documents
Culture Documents
Leo
hii
tunapokea
wajumbe
wapya
kuendeleza
yale
nyumba yake ya kuishi, usafi katika eneo lake la kazi, usafi katika vyombo
vya usafiri, usafi katika sehemu za biashara, usafi katika nyumba za kulala
wageni, usafi katika sehemu zinazouza vyakula, usafi na usalama wa
vyakula na maji, usafi katika viwanda, migodi, mashamba, taasisi na nk.
Aidha, ni ukweli usiopingika kuwa kila sehemu inahitaji kuwekwa katika hali
ya usafi na endelevu ili kudumisha kanuni za afya mazingira.
Ndugu Wananchi,
Katika ya miaka hivi karibuni, Serikali imefanya maboresho katika sekta ya
afya nchini ambayo yanalenga katika kuimarisha na kudumisha huduma
bora za afya ya msingi kote nchini. Miongoni mwa masuala muhimu ni
kuweka msingi na taratibu za kuhakikisha watoa huduma za afya
wanazingatia sheria, kanuni, miiko na maadili ili waweze kutoa huduma
kwa ufanisi na ubora wa hali ya juu. Pamoja na mambo mengine Serikali
imetunga Sheria ya Kusimamia na Kudhibiti Utendaji wa Wataalamu wa
Afya ya Mazingira ya mwaka 2007, na kutengeneza Kanuni za Ujumla za
Sheria zinajulikana kwa jina la kiingereza The Environmental Health
Practitioners (General) Regulations 2011. Kanuni ya 3, 4 na 5
zinazungumzia suala la Usajili, kuorodheshwa na kuandikishwa kwa
Wataalam wa Afya ya Mazingira Nchini. Aidha Kanuni ya 12 ya Kanuni za
Ujumla za Usajili inasisitiza kusajiliwa kwa wataalam wote wenye taaluma
ya Afya Mazingira kote nchini.
Ndugu Wananchi,
Napenda kutoa msisitizo juu ya suala hili kwa kuzitaja huduma za afya ya
mazingira
Ndugu Mwenyekiti,
Taaluma ya Afya ya Mazingira ni muhimili muhimu katika kupambana na
magonjwa ya mlipuko. Shirika la Afya Ulimwenguni ambapo Tanzania ni
miongoni mwa mwanachama, lilitengeneza Kanuni za Afya za Kimataifa
(The International Health Regulations) kwa mujibu wa Kanuni hizi
wataalamu wa Afya Mazingira ndio wasimamizi wakuu wa Kanuni hizi na
wana wajibu wa kuhakikisha kuwa wageni wote wanaoingia nchini kupitia
katika mipaka yetu wanakaguliwa kwa kusudi la kuzuia magonjwa
yanayoripotiwa Kimataifa. Nchi nyingi zinazoendelea hivi leo zinakabiliwa
na changamoto ya wataalamu wa afya mazingira kukosa tekinolojia ya
kisasa na endelevu, vitendea kazi duni, mazingira duni yasiyoridhisha
kiafya, hali mbaya ya uchumi, soko la ajira, uzembe na uzururaji, Rushwa,
ushindani wa kitaaluma, mabadiliko ya tabianchi (kuongezeka kwa joto
duniani), matumizi ya kemikali na viuatilifu yasiyozingatia misingi ya afya
mazingira.
Katika sekta ya Afya, kuna changamoto nyingi zikiwemo za ongezeko la
magonjwa ya milipuko yatokanayo na uchafuzi wa mazingira, hususan
ugonjwa hatari wa kipindupindu. Aidha, Afya Mazingira ni suala mtambuka
ambalo linahusisha wadau wengi katika kulitekeleza. Ni muhimu katika
utekelezaji wa majukumu yake, Baraza lishirikishe kwa karibu wadau
mbalimbali kutoka sekta mbalimbali ili kutoa matokeo chanya yenye tija na
ubora wa hali ya juu kwa taifa letu. Ni matumaini yangu kuwa tutafanya
bayana
adhabu
zitakazotolewa
kwa
wataalamu