Professional Documents
Culture Documents
VYA HABARI
Ukizingatia kwamba nyaraka za Tanzania yenyewe za sera zinatambua PPP kama ni chombo muhimu cha
kuvutia uwekezaji mpya, ripoti hiyo badala yake inataka pawepo na mwelekeo mpya thabiti tofauti na
mambo kama kawaida, na inatoa kwa muhtasari vipengele muhimu vya kuzingatiwa na serikali katika
kujenga muundo wa PPP ambao unafaa kwa madhumuni haya. Hivi ni pamoja na kutoa mwongozo wa
kimkakati na uongozi wa programu ya PPP; kuhakikisha matumizi ya mbinu za ushindanishi ili kupata
PPP; kutoa rasilimali za kutosha kuelekea kuainisha na kutayarisha PPP na kukuza njia za wazi katika
kutoa msaada wa Serikali kwa PPPs.
Ukizingatia usimamizi imara wa uchumi ambao umesaidia kuendeleza mtazamo thabiti wa sasa wa
asilimia saba, Toleo la 8 linazitaka mamlaka kuendelea kufuatilia viwango vya deni la nchi kwa namna
makini ili kuhakikisha uendelevu wa kifedha na deni unaoendelea.
Hali ya Uchumi wa Tanzania ni ripoti inayochapishwa na Benki ya Dunia mara mbili kwa mwaka kwa lengo
la kukuza mjadala wa sera unaojenga baina ya wadau na watunga sera na kuchochea mdahalo kwenye
masuala muhimu ya uchumi ndani ya nchi.
Mawasiliano:
Washington: Aby Toure, (202) 473-8302, akonate@worldbank.org
Dar es Salaam: Loy Nabeta, (255) 216-3246, lnabeta@worldbank.org
Kwa habari zaidi kuhusu kazi za Maendeleo za Benki ya Dunia na Taasisi zake katika Afrika, tafadhali
tembelea tovuti: www.worldbank.org/africa