Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii anapenda kuwatangazia wataalamu wa kada za afya kuwa bado kuna nafasi za kazi katika Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa. Wataalamu wa kada zilizoorodheshwa hapa chini wanatakiwa kuwasilisha maombi yao ili waweze kupangiwa vituo vya kazi: Madaktari Bingwa/ Madaktari Bingwa wa Meno, Madaktari/Madaktari wa Meno, Mdaktari Wasaidizi/Madaktari Wasaidizi wa Meno, Matabibu/Matabibu wa Meno, Matabibu Wasaidizi, Mteknolojia wa Meno, Wafamasia, Watenolojia wa Dawa, Wateknolojia Wasaidizi wa Dawa, Maafisa Wateknolojia wa Maabara za Afya, Wateknolojia wa Maabara za Afya, Wateknolojia Wasaidizi wa Maabara za Afya, Maafisa Wauguzi, Maafisa Wauguzi Wasaidizi, Wauguzi, Maafisa Fiziotherapia, Wafiziotherapia, wateknolojia wa Macho, Wateknolojia Mionzi, Afisa Afya Mazingira, Afisa Afya Mazingira Msaidizi, Mhandisi wa Vifaa Tiba na Mteknolojia wa Vifaa Tiba. Barua ya maombi iambatanishwe na nakala ya cheti cha kidato cha nne, cheti cha taaluma na cheti cha kuzaliwa. Waombaji wa kada zenye Mabaraza ya Taaluma wawasilishe vyeti vya usajili au leseni. Mwisho wa kuwasilisha maombi tarehe 30/6/2014
Taarifa Ya Mkuu Wa Mkoa Wa Rukwa Kwa Naibu Waziri Wa Nchi Ofisi Ya Waziri Mkuu-Tamisemi-Mhe - Aggrey Mwanri (MB) Katika Ziara Yake Mkoani Rukwa Tarehe 07 - 15 January 2013.
Orodha Ya Wanafunzi Wa Wa Uzamili Waliopata Ufadhili Wa Mafunzo Ya Uzamili/uzamivu Kupitia Wizara Ya Afya, Maendeleo Ya Jamii, Jinsia, Wazee Na Watoto 2016/17 - World Bank