Professional Documents
Culture Documents
Na Eleuteri Mangi-MAELEZO
Wanadamu wameumbwa kwa hulka na silika ya kuwa na uwezo wa kuwasiliana
miongoni mwao, jamii wanamoishi, taifa na hata ulimwenguni ili waweze kutimiza
nia na azma yao ya kuwasiliana.
Ili mawasiliano hayo yakamilike ni lazima yabebe ujumbe unaokusudiwa
kufikishwa katika jamii.
Ujumbe huo ili uweze kumfikia mlengwa, ni lazima iwepo njia ya kuufikisha
ujumbe huo kwa mlengwa ambao huwasilishwa kwa maandishi (magazeti), sauti
(redio) na picha (TV) pamoja na mitandao ya kijamii kupitia huduma ya inteneti.
Vyombo hivyo vya habari vinahusisha wataalamu ambao kazi yao ni kuhakikisha
jamii inapata ujumbe kwa wakati ili kuweza kujenga, kuboresha na kuimarisha
maisha yao kiuchumi, kijamii, kisiasa na kiutamaduni.
Vyombo vya habari hakika vimekuwa ndio macho na masikio ya wananchi ili
kufikisha ujumbe unaohusu mambo mbalimbali yanayofanyika ndani na nje ya
nchi.
Tunapoelekea siku ya maadhimisho ya uhuru wa vyombo vya habari duniani
ambayo huadhimishwa kila mwaka Mei 2 na 3, maadhimisho hayo mwaka huu
yataadhimishwa nchini Finland, ambapo wanahabari wote duniani wataungana
kuwakumbuka wenzao waliofariki dunia walipokuwa wakitekeleza majukumu yao
na kupanga mipango mipya ya namna watakavyoboresha kazi zao ziwe za ufanisi
zaidi.
Tanzania ikiwa miongoni mwa mataifa ya dunia hii, nayo haipo nyuma katika
suala la uwepo wa vyombo vya habari.
Ni dhahiri vyombo vya habari nchini vimekuwa kiungo muhimu katika kisaidia
Serikali kutoa taarifa mbalimbali na ajira hatua ambayo imesaidia kupunguza
tatizo la ajira nchini.
Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Shirika la Kimataifa
la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Aprili 8, 2016 imebainisha kuwa
katika maadhimisho ya Siku ya vyombo vya habari duniani mwaka huu,
mwandishi wa habari za uchunguzi kutoka Azerbaijan Khadija Ismayilova
amechaguliwa kupokea tuzo ya uandishi wa habari za uchunguzi ijulikanayo
Guillermo Cano inayotolewa na Shirika hilo.
Tuzo hiyo ina thamani ya Dola za Kimarekani 25,000, na imepoewa jina hilo kwa
heshima ya Guillermo Cano Isaza, mwandishi wa habari wa Colombia aliyefariki
Desemba 17, 1986 akiwa kazini.
Jukumu la kuenzi na kutoa tuzo ya heshima kwa waandishi wa habari duniani
linafadhiliwa na taasisi ya Cano Foundation kutoka nchini Colombia na Helsingin
Sanomat Foundation kutoka nchini Finland.
Msaidizi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mawasiliano na Habari UNESCO Frank La
Rue anasema "Uhuru wa vyombo vya habari ni muhimu kwa taarifa muhimu na
uwazi ni ambao ni mahitaji ya jamii ya kidemokrasia. Lakini leo tunaona ongezeko
la ghasia na vitisho dhidi ya waandishi ambayo mimi napendekeza nchi zote
duniani kuanzisha utaratibu wa habari na ulinzi kwa ajili ya usalama wa waandishi
wa habari"
Moja ya changamoto za kuweka utaratibu wa usalama wa waandishi wa habari ni
idadi ndogo ya mifano ya taratibu zilizopo ambayo inaweza kuwa somo ili
wengine waweze kujifunza kutokana na taratibu zilizopo.
Masuala muhimu ya kuzingatiwa wakati wa kuanzisha utaratibu huo ni pamoja na
kuwepo kwa makundi matatu ambayo ni wigo wa utaratibu, ushirikishwaji wa
wadau muhimu pamoja na taasisi kubuni na kutathmini hatua ambayo itasaidia
kufikia malengo ya kumlinda mwandishi wa habari.
Akizungumzia maandalizi ya maadhimisho kitaifa ya siku ya Uhuru wa Vyombo
vya habari nchini ambayo yanafanikia jijini Mwanza Mei 2 na 3, mwaka huu,
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya maadhimisho hayo Andrew Marawiti
amesema kuwa yanaendelea vizuri kulingana na ratiba ilivyopangwa.
Katika maadhimisho hayo, Marawiti amesema kuwa Mgeni Rasmi anatarajiwa
kuwa Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Othman Chande ambapo
Ili kufikisha ujumbe kwa jamii, Mjengwa amesema kuwa watu wote wanaofanya
kazi katika mitandao ya kijamii wanapaswa kufuata maadili ya taaluma ya habari
pamoja na sheria na taratibu za nchi husika ili kuondoa mgongano wa maslahi
katika kufikisha ujumbe kwa jamii.
Ni dhahiri haki na wajibu ni vitu ambavyo haviachani, hivyo ni jukumu la kila
mdau wa habari nchini wakiwemo Serikali, waandishi wa habari, wamiliki wa
vyombo vya habari na wananchi kuzingatia sheria, kanuni, taratibu pamoja na
maadili ya jamii.
Hatua hiyo itasaidia kuimarisha na kuhakikisha wadau hao wanakuwa sehemu ya
kujenga uhuru wa vyombo vya habari ambavyo vitakuwa chachu ya kujenga taifa
imara lenye uchumi bora kwa manufaa ya Watanzania ifikapo mwaka 2025.
Mwisho.