You are on page 1of 2

TAARIFA KWA MAAFISA UHAMIAJI WOTE

Nimeelekezwa na Afisa Uhamiaji Mkoa wa Mara


niwajulishe wote kuwa kuanzia sasa askari wote wa
uhamiaji wenye rank ya kuanzia konstebo hadi
sajini meja mtakuwa mnafanya gwaride (Parade)
kuanzia saa moja na nusu hadi saa mbili kasoro
robo kabla ya kuanza kazi.
Gwaride hilo kwa kuanzia litafanyika kwa siku za
jumanne na alhamisi na baadae tutarekebisha
kulingana siku zitakavyokuwa zinaenda. Afisa
Uhamiaji Wilaya atakagua gwaride hilo wiki ya
mwisho wa kila mwezi.
Hii ni kwa mujibu wa kanuni ya sheria ya Jeshi la
Polisi na Idara za Uhamiaji na Magereza namba 38
ya mwaka 2015 na notisi ya Serikali ya namba 438
iliyotolewa tarehe 2/10/2015 kifungu cha 23 (d), (n)
na (t). Yeyote ambaye hatotii kanuni hii
atachukuliwa hatua kali za kisheria kwa mujibu wa
kifungu cha 27 cha kanuni iliyotajwa hapo juu.
Shughuli hii itafanyika nje ya lango kuu la kuingilia
ndani ya ofisi hii. Nawatakia utekelezaji mwema wa
kanuni hii.

DCIS E. Mushongi

Afisa Uhamiaji Wilaya


BUNDA

You might also like