You are on page 1of 225

BIBLIA INAFUNDISHA NINI Hasa?

BIBLIA INAFUNDISHA NINI Hasa?


KITABU HIKI NI CHA

Photo Credits: Page 7: Courtesy American Bible Society Page 19: Earth: NASA photo Pages 24-5: WHO photo by Edouard Boubat Pages 88-9: Explosion: Based on USAF photo; child: Based on WHO photo by W. Cutting

5 2005 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania Haki Zote Zimehifadhiwa
WACHAPISHAJI

Watch Tower Bible and Tract Society of South Africa 1 Robert Broom Drive East, Rangeview, Krugersdorp, 1739, R.S.A. Chapa ya 2009 Kitabu hiki hakiuzwi. Ni sehemu ya kazi ya elimu ya Biblia ulimwenguni pote inayotegemezwa kwa michango ya hiari. Isipokuwa iwe imeonyeshwa vingine, Maandiko yamenukuliwa kutoka katika Biblia TakatifuTafsiri ya Ulimwengu Mpya What Does the Bible Really Teach? Swahili (bh-SW)
Made in the Republic of South Africa Kimechapwa Katika Jamhuri ya Afrika Kusini J.G.

YALIYOMO
SURA UKURASA

Je, Hivi Ndivyo Mungu Alivyokusudia? 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 3 1. Ukweli Kumhusu Mungu 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 8 2. BibliaKitabu Kutoka kwa Mungu 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 18 3. Mungu Ana Kusudi Gani kwa Dunia? 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 27 4. Yesu Kristo Ni Nani? 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 37 5. FidiaZawadi Bora Zaidi Kutoka kwa Mungu 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 47 6. Wafu Wako Wapi? 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 57 7. Tumaini Hakika kwa Wapendwa Wako Ambao Wamekufa 9 9 9 9 9 66 8. Ufalme wa Mungu Ni Nini? 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 76 9. Je, Tunaishi Katika Siku za Mwisho? 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 86 10. Jinsi Viumbe wa Roho Wanavyohusika Maishani Mwetu 9 9 9 9 9 9 96 11. Kwa Nini Mungu Anawaacha Watu Wateseke? 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 106 12. Kuishi Maisha Yanayompendeza Mungu 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 115 13. Maoni ya Mungu Kuhusu Uhai 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 125 14. Jinsi ya Kufanya Maisha ya Familia Yako Yawe Yenye Furaha 9 9 9 134 15. Ibada Ambayo Mungu Anakubali 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 144 16. Chukua Msimamo Upande wa Ibada ya Kweli 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 154 17. Mkaribie Mungu Katika Sala 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 164 18. Ubatizo na Uhusiano Wako Pamoja na Mungu 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 174 19. Kaa Katika Upendo wa Mungu 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 184 Nyongeza 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 194

Je, Hivi Ndivyo Mungu Alivyokusudia?


KATIKA magazeti, televisheni, na redio, kuna habari nyingi kuhusu visa vya ugaidi, vita, na uhalifu. Hebu kiria pia mahangaiko yako mwenyewe. Labda unasumbuliwa na ugonjwa fulani au umewa na mtu unayempenda. Huenda ukahisi kama alivyohisi Ayubu, aliyesema kwamba maisha yake yalikuwa yamejaa masumbuko. Ayubu 10:15, Verbum Bible. Hebu jiulize: Je, hivi ndivyo Mungu alivyokusudia maisha yangu na ya wanadamu wengine yawe? Ninaweza kupata wapi msaada wa kukabiliana na matatizo yangu? Je, dunia itapata kuwa na amani? Biblia inajibu maswali hayo kwa njia ya kuridhisha.

BIBLIA INAFUNDISHA KWAMBA MUNGU ATATIMIZA MAMBO HAYA DUNIANI.


Atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena.Ufunuo 21:4

Kilema atapanda juu kama vile paa anavyofanya. Isaya 35:6

Macho ya vipofu yatafunguliwa. Isaya 35:5

Wale wote waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho watatoka. Yohana 5:28, 29

Hakuna mkaaji atakayesema: Mimi ni mgonjwa. Isaya 33:24

Kutakuwa na wingi wa nafaka duniani.Zaburi 72:16

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

FAIDIKA NA MAFUNDISHO YA BIBLIA Usidhani kwamba mambo yaliyo kwenye kurasa zinazotangulia ni ndoto tu. Mungu ameahidi kwamba atatimiza mambo hayo, na Biblia inaeleza jinsi atakavyofanya hivyo. Hata hivyo, Biblia ina faida nyingine nyingi. Inaweza kukusaidia kuwa na maisha yenye kuridhisha hata sasa. Hebu tua kidogo, ukirie mahangaiko na matatizo yako mwenyewe. Huenda yanatia ndani ukosefu wa pesa, matatizo ya familia, matatizo ya afya, au kifo cha mpendwa. Biblia inaweza kukusaidia kushughulika na matatizo leo na inaweza kukufariji kwa kujibu maswali kama haya:
Kwa nini tunateseka? Tunawezaje kushughulika na mahangaiko ya maisha? Tunawezaje kufanya maisha ya familia yetu yawe yenye furaha zaidi? Inakuwaje tunapokufa? Je, tutapata kuwaona wapendwa wetu waliokufa? Tunawezaje kuwa na hakika kwamba Mungu atatimiza ahadi zake kuhusu wakati ujao?

Je, Hivi Ndivyo Mungu Alivyokusudia?

Kusoma kitabu hiki kunaonyesha kwamba ungependa kujua yale ambayo Biblia inafundisha. Kitabu hiki kitakusaidia. Sehemu ya chini ya kurasa kuna maswali yanayoambatana na mafungu. Mamilioni ya watu wamefurahia kuwa na mazungumzo ya Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova kwa njia ya maswali na majibu. Tunatumaini kwamba wewe pia utafurahia kufanya hivyo. Mungu na akubariki unapochukua hatua hiyo yenye kusisimua na kuridhisha ya kujifunza mambo ambayo Biblia inafundisha hasa!

IJUE BIBLIA YAKO


KUNA vitabu 66 katika Biblia. Kila kitabu kina sura na mistari, ili kurahisisha usomaji. Maandiko yanapotajwa katika kitabu hiki, nambari inayofuata jina ndiyo sura ya kitabu au barua katika Biblia, nayo nambari inayofuata ni mstari. Kwa mfano, 2 Timotheo 3:16 ni barua ya pili kwa Timotheo, sura ya 3, mstari wa 16. Ukifungua na kusoma maandiko yaliyo katika kitabu hiki, utazoea kuitumia Biblia. Pia, mbona usianze kuisoma Biblia kila siku? Ukisoma sura tatu hadi tano hivi kila siku, unaweza kuisoma Biblia nzima kwa mwaka mmoja.

SURA YA KWANZA

Ukweli Kumhusu Mungu


Je, kweli Mungu anakujali? Mungu ana utu wa aina gani? Je, ana jina? Je, tunaweza kuwa na uhusiano wa karibu pamoja na Mungu?
JE, UMEWAHI kuona jinsi ambavyo watoto huuliza maswali? Wengi wao huanza kuuliza maswali mara tu wanapojua kuongea. Wanakutazama wakiwa wamekodoa macho kwa hamu na kuuliza maswali kama vile: Kwa nini anga ni bluu? Kwa nini nyota zinametameta? Ni nani aliyewafundisha ndege kuimba? Huenda ukajaribu sana kujibu, lakini mara nyingi si rahisi. Hata baada ya kuwapa jibu bora, huenda bado wakauliza: Kwa nini? 2 Si watoto peke yao wanaouliza maswali. Tunapoendelea kukua, sisi huuliza maswali. Tunauliza maswali ili tupate mwongozo, tujue hatari tunazohitaji kuepuka, au kwa sababu tu tunataka kujua. Hata hivyo, inaonekana kwamba watu wengi huacha kuuliza maswali, hasa yaliyo muhimu zaidi. Wao huacha kutafuta majibu. 3 Fikiria swali lililo katika jalada
1, 2. Kwa nini ni vizuri kuuliza maswali? 3. Kwa nini watu wengi hawajitahidi kupata majibu ya maswali muhimu zaidi?

Ukweli Kumhusu Mungu

la kitabu hiki, maswali yaliyo katika utangulizi wa kitabu hiki, au yale yaliyo mwanzoni mwa sura hii. Hayo ni baadhi ya maswali muhimu zaidi unayoweza kuuliza. Hata hivyo, watu wengi hawajitahidi kupata majibu ya maswali hayo. Kwa nini? Je, Biblia ina majibu? Watu fulani hukiri kwamba Biblia haieleweki. Wengine huogopa kuuliza maswali ili wasiaibishwe au kudharauliwa. Hali wengine huamua kwamba maswali hayo yanaweza kujibiwa tu na viongozi na walimu wa dini. Wewe unaonaje? 4 Bila shaka ungependa kupata majibu ya maswali muhimu zaidi maishani. Haikosi, nyakati nyingine wewe hujiuliza: Maisha yana kusudi gani? Je, kusudi pekee la maisha ni kuzaliwa, kuzeeka, na kufa? Kwa kweli Mungu ana utu gani? Ni vizuri kuuliza maswali kama hayo, na ni muhimu kutafuta majibu yenye kuridhisha na yenye kutegemeka bila kukata tamaa. Yule mwalimu mashuhuri, Yesu Kristo, alisema hivi: Endeleeni kuomba, nanyi mtapewa; endeleeni kutafuta, nanyi mtapata; endeleeni kupiga hodi, nanyi mtafunguliwa.Mathayo 7:7. 5 Ukiendelea kutafuta majibu ya maswali hayo muhimu, utafaidika sana. (Methali 2:1-5) Hata uwe umeambiwa nini na watu wengine, kuna majibu, na unaweza kuyapata katika Biblia. Majibu hayo si magumu, yasiyoeleweka. Isitoshe, yatakupa tumaini na shangwe. Na yanaweza kukusaidia kuishi maisha yenye kuridhisha sasa. Kwanza, na tukirie swali moja ambalo limewahangaisha watu wengi.

JE, MUNGU ANA HURUMA NA JE, ANAJALI? Watu wengi hujibu hapana. Wanasema, Ikiwa Mungu anajali, ulimwengu ungekuwa tofauti sana. Leo, ulimwengu umejaa vita, chuki, na mateso. Isitoshe, kila mmoja
6

4, 5. Ni maswali gani muhimu zaidi tunayoweza kuuliza maishani, na kwa nini tutafute majibu? 6. Kwa nini watu wengi wanakiri kwamba Mungu hajali wanadamu wanapoteseka?

10

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

wetu huwa mgonjwa, huteseka, na kuwa na wapendwa wake. Ndiyo sababu watu wengi husema, Ikiwa Mungu anatujali na kuhangaikia matatizo yetu, kwa nini hazuii mambo hayo yasitupate? 7 Isitoshe, nyakati nyingine walimu wa dini huwafanya watu wakiri kwamba Mungu hana huruma. Jinsi gani? Msiba unapotokea, wanasema ni mapenzi ya Mungu. Kwa kweli, walimu hao wanamlaumu Mungu kwa sababu ya mambo mabaya yanayotukia. Je, huo ndio ukweli kumhusu Mungu? Biblia inafundisha nini hasa? Andiko la Yakobo 1:13 linajibu: Mtu akiwa chini ya jaribu, yeye asiseme: Mungu ananijaribu. Kwa maana Mungu hawezi kujaribiwa na mambo maovu wala yeye mwenyewe hamjaribu yeyote. Kwa hiyo, Mungu hasababishi kamwe uovu ambao unaona ulimwenguni. (Ayubu 34:10-12) Ni kweli kwamba anaacha mambo mabaya yatukie. Hata hivyo, kuna tofauti kubwa kati ya kuacha jambo litukie na kulisababisha. 8 Kwa mfano, wazia baba mwenye hekima na busara aliye na mwana ambaye tayari ni mtu mzima na bado anaishi nyumbani kwa wazazi wake. Mwana huyo akiasi na kuamua kuondoka nyumbani, baba yake hamzuii. Mwana huyo anaishi maisha mapotovu na kupata matatizo. Je, baba ndiye aliyesababisha matatizo ya mwanaye? Hapana. (Luka 15:11-13) Vivyo hivyo, Mungu hawazuii wanadamu wakishaamua kufuata njia isiyofaa, hata hivyo hasababishi matatizo yanayowapata. Kwa hiyo, basi, si haki kumlaumu Mungu kwa sababu ya matatizo yote yanayowapata wanadamu. 9 Mungu ana sababu nzuri za kuwaacha wanadamu wa7. (a) Walimu wa dini wamewafanyaje watu wengi wakiri kwamba Mungu hana huruma? (b) Biblia inafundisha nini hasa kuhusu majaribu ambayo huenda yakatupata? 8, 9. (a) Unaweza kutumia mfano gani kuonyesha tofauti iliyopo kati ya kuacha uovu uwepo na kuusababisha? (b) Kwa nini si haki kumlaumu Mungu kwa kuwaacha wanadamu wafuate njia isiyofaa?

Ukweli Kumhusu Mungu

11

fuate njia isiyofaa. Akiwa Muumba wetu mwenye hekima na nguvu, hahitaji kutueleza sababu hizo. Hata hivyo, Mungu hutueleza kwa sababu ya upendo. Utajifunza kuhusu sababu hizo katika Sura ya 11. Lakini uwe na hakika kwamba Mungu hasababishi matatizo yanayotupata. Badala yake, anatupa tumaini pekee la utatuzi!Isaya 33:2. 10 Isitoshe, Mungu ni mtakatifu. (Isaya 6:3) Hilo linamaanisha kwamba yeye ni sa wala hana uovu hata kidogo. Kwa hiyo, tunaweza kumtumaini kabisa. Hatuwezi kuwatumaini wanadamu ambao nyakati nyingine wanakuwa wasadi. Hata wanadamu wenye mamlaka ambao ni wanyoofu zaidi mara nyingi hawana uwezo wa kuondoa madhara yanayosababishwa na watu wabaya. Lakini Mungu ana nguvu zote. Anaweza na ataondoa madhara yote yanayowapata wanadamu kwa sababu ya uovu. Mungu atakapochukua hatua, atakomesha uovu milele!Zaburi 37:9-11.

MUNGU ANAHISIJE KUHUSU UKOSEFU WA HAKI? 11 Mungu anahisije kuhusu mambo yanayoendelea ulimwenguni na maishani mwako? Kwanza kabisa, Biblia inafundisha kwamba Mungu ni mpenda-haki. (Zaburi 37:28) Kwa hiyo anapendezwa sana na mambo yanayofaa na kuchukizwa na mambo yasiyofaa. Anachukia ukosefu wa haki wa kila namna. Biblia inasema kwamba Mungu aliumia moyoni mwake uovu ulipokuwa mwingi duniani wakati uliopita. (Mwanzo 6:5, 6) Mungu hajabadilika. (Malaki 3:6) Bado anachukia kuona mateso yanayoendelea ulimwenguni pote. Pia, Mungu anachukia kuona watu wakiteseka. Biblia inasema, yeye anawajali ninyi.1 Petro 5:7.
10. Kwa nini tunaweza kuwa na hakika kwamba Mungu ataondoa madhara yote yanayotokana na uovu? 11. (a) Mungu anahisije kuhusu ukosefu wa haki? (b) Mungu anahisije kuhusu kuteseka kwako?

12
12

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Tunawezaje kuwa na hakika kwamba Mungu anachukia kuona watu wakiteseka? Uthibitisho mwingine ndio huu. Biblia inafundisha kwamba Mungu alimuumba mtu kwa mfano wake. (Mwanzo 1:26) Kwa hiyo, tuna sifa nzuri kwa sababu Mungu ana sifa nzuri. Kwa mfano, je, wewe husumbuka unapowaona watu wasio na hatia wakiteseka? Ikiwa unasumbuka kwa sababu ya ukosefu huo wa haki, uwe na hakika kwamba Mungu husumbuka hata zaidi. 13 Jambo moja la pekee kuhusu wanadamu ni kwamba tuna uwezo wa kuonyesha upendo. Mungu pia ana sifa hiyo. Biblia inafundisha kwamba Mungu ni upendo. (1 Yohana 4:8) Tuna upendo kwa sababu Mungu ana upendo. Je, upendo ungekuchochea kukomesha Unapotaka mateso na ukosefu wa haki unaoona mtu akujue, ulimwenguni? Kama ungekuwa na unamwambia uwezo wa kufanya hivyo, je, ungeyakojina lako, mesha? Bila shaka ungeyakomesha! sivyo? Mungu Uwe na hakika kwamba Mungu ataanatujulisha jina lake katika komesha mateso na ukosefu wa haki. Biblia Ahadi zinazotajwa katika utangulizi wa kitabu hiki si ndoto tu au matumaini yasiyo na msingi. Bila shaka ahadi za Mungu zitatimia! Hata hivyo, ili kuamini ahadi hizo, unahitaji kujua mengi zaidi kumhusu Mungu anayezitoa.
14

MUNGU ANATAKA UMJUE Ukitaka mtu akujue, unaweza ku-

12, 13. (a) Kwa nini tuna sifa nzuri kama vile upendo, nao upendo unatufanya tuwe na maoni gani kuhusu ulimwengu? (b) Kwa nini unaweza kuwa na hakika kwamba Mungu atachukua hatua kuhusiana na matatizo ya ulimwengu? 14. Mungu anaitwa nani, na kwa nini tunapaswa kulitumia jina lake?

Biblia inafundisha kwamba Yehova ni Muumba wa ulimwengu mwenye upendo

fanya nini? Utamwambia jina lako, sivyo? Je, Mungu ana jina? Dini nyingi hujibu kwamba jina lake ni Mungu au Bwana, lakini hayo si majina yake binafsi. Hayo ni majina ya heshima kama vile mfalme na rais. Biblia inafundisha kwamba Mungu ana majina mengi ya heshima. Baadhi ya majina hayo ni Mungu na Bwana. Hata hivyo, Biblia inafundisha pia kwamba Mungu ana jina lake binafsi, yaani, Yehova. Andiko la Zaburi 83:18 linasema hivi: Wewe, ambaye jina lako ni Yehova, wewe peke yako ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote. Ikiwa Biblia yako haina jina hilo, unaweza kutazama Nyongeza iliyo kwenye ukurasa wa 195-197 wa kitabu hiki ili ujue ni kwa nini. Ukweli ni

14

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

kwamba jina la Mungu linapatikana mara elfu kadhaa katika hati za zamani za Biblia. Kwa hiyo, Yehova anataka ulijue jina lake na kulitumia. Tunaweza kusema kwamba anatumia Biblia kujitambulisha kwako. 15 Mungu alijipa jina lenye maana. Jina lake, Yehova, linamaanisha kwamba anaweza kutimiza ahadi yoyote anayotoa na kufanya jambo lolote analokusudia.1 Jina la Mungu ni la pekee, halina kifani. Ni lake peke yake. Yehova ni wa pekee katika njia mbalimbali. Jinsi gani? 16 Tuliona kwamba andiko la Zaburi 83:18 linasema hivi
1 Unaweza kupata habari zaidi kuhusu maana ya jina la Mungu na jinsi linavyotamkwa katika Nyongeza iliyo kwenye ukurasa wa 195-197.
15. Jina Yehova linamaanisha nini? 16, 17. Tunaweza kujifunza nini kumhusu Yehova kutokana na majina haya ya heshima: (a) Mweza-Yote? (b) Mfalme wa umilele? (c) Muumba?

Upendo wa baba kwa watoto wake unaonyesha upendo mkubwa zaidi ambao Baba yetu wa mbinguni anatuonyesha

Ukweli Kumhusu Mungu

15

kumhusu Yehova: Wewe peke yako ndiye Uliye Juu Zaidi. Vivyo hivyo, Yehova peke yake ndiye anayeitwa MwezaYote. Andiko la Ufunuo 15:3 linasema: Matendo yako ni makuu na ya ajabu, Yehova Mungu, Mweza-Yote. Njia zako ni za uadilifu na za kweli, Mfalme wa umilele. Jina Mweza-Yote linatufundisha kwamba Yehova ndiye mwenye nguvu zaidi kuliko wote. Nguvu zake hazina kifani; ni nyingi sana. Nalo jina Mfalme wa umilele linatukumbusha kwamba Yehova ni wa pekee katika njia nyingine. Yeye peke yake ndiye amekuwapo nyakati zote. Andiko la Zaburi 90:2 linasema: Tangu wakati usio na kipimo mpaka wakati usio na kipimo [au, milele] wewe ni Mungu. Maneno hayo yanatuchochea tumheshimu, sivyo? 17 Pia, Yehova ni wa pekee kwa sababu yeye peke yake ndiye Muumba. Andiko la Ufunuo 4:11 linasema: Unastahili, Ee Yehova, naam, Mungu wetu, kupokea utukufu na heshima na nguvu, kwa sababu uliumba vitu vyote, na kwa sababu ya mapenzi yako vilikuwako navyo vikaumbwa. Kila kitu unachoweza kuwazia, iwe viumbe wa roho mbinguni ambao hawaonekani, nyota zinazotapakaa katika anga la usiku, matunda yanayokua mitini, au samaki walio baharini na kwenye mito, vyote vipo kwa sababu Yehova ndiye Muumba!

JE, UNAWEZA KUMKARIBIA YEHOVA? Kusoma kuhusu sifa za Yehova za ajabu, huwafanya watu fulani wamwogope. Wanahisi kwamba Mungu yuko juu sana wasiweze kumkaribia, nao ni duni machoni pake. Lakini je, hayo ni maoni yanayofaa? Biblia haifundishi hivyo. Inasema hivi kumhusu Yehova: Hayuko mbali sana na kila mmoja wetu. (Matendo 17:27) Hata Biblia inatuhimiza hivi: Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Yakobo 4:8.
18

18. Kwa nini watu fulani wanahisi kwamba hawawezi kamwe kumkaribia Mungu, lakini Biblia inafundisha nini?

16
19

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Unawezaje kumkaribia Mungu? Kwanza kabisa, endelea kujifunza kumhusu kama unavyofanya sasa. Yesu alisema: Uzima wa milele ndio huu, waendelee kupata ujuzi juu yako wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na juu ya yule uliyemtuma, Yesu Kristo. (Yohana 17:3) Naam, Biblia inafundisha kwamba kujifunza kumhusu Yehova na Yesu huongoza kwenye uzima wa milele! Kama tulivyoona, Mungu ni upendo. (1 Yohana 4:16) Pia, Yehova ana sifa nyingine nyingi nzuri zenye kuvutia. Kwa mfano, Biblia inasema kwamba Yehova ni Mungu mwenye rehema na neema, si mwepesi wa hasira naye ni mwingi wa fadhili zenye upendo na kweli. (Kutoka 34:6) Yeye ni mwema na yuko tayari kusamehe. (Zaburi 86:5) Mungu ana subira. (2 Petro 3:9) Yeye ni mshikamanifu. (Ufunuo 15:4) Kadiri unavyozidi kujifunza mengi katika Biblia, ndivyo utakavyozidi kujua jinsi Yehova ameonyesha sifa hizo na nyingine nyingi zenye kuvutia. 20 Ni kweli kwamba huwezi kumwona Mungu kwa sababu yeye ni roho asiyeonekana. (Yohana 1:18; 4:24; 1 Timotheo 1:17) Hata hivyo, ukijifunza kumhusu katika Biblia, utaujua utu wake. Kama mtunga-zaburi alivyosema, unaweza kuuona uzuri wa Yehova. (Zaburi 27:4; Waroma 1:20) Unapozidi kujifunza kumhusu Yehova, atakuwa halisi zaidi kwako nawe utampenda na kumkaribia zaidi. 21 Utaelewa hatua kwa hatua ni kwa nini Biblia inatufundisha kumwona Yehova kuwa Baba yetu. (Mathayo 6:9) Mbali na kwamba ametupa uhai, anataka tuwe na maisha bora iwezekanavyo, kama vile baba yeyote mwenye upendo angewatakia watoto wake. (Zaburi 36:9) Pia, Biblia
19. (a) Tunawezaje kuanza kumkaribia Mungu, nasi tutapata faida gani? (b) Ni sifa gani za Mungu zinazokuvutia zaidi? 20-22. (a) Kwa kuwa hatuwezi kumwona Mungu, je, inamaanisha kwamba hatuwezi kumkaribia? Eleza. (b) Huenda watu fulani wasio na nia mbaya wakakusihi ufanye nini, lakini unapaswa kufanya nini?

Ukweli Kumhusu Mungu

17

inafundisha kwamba wanadamu wanaweza kuwa raki za Yehova. (Yakobo 2:23) Hebu waziawewe unaweza kuwa raki ya Muumba wa ulimwengu! 22 Unapoendelea kujifunza mengi zaidi katika Biblia, huenda watu fulani wasio na nia mbaya wakakusihi uache kujifunza. Huenda wakaogopa kwamba utabadili dini yako. Lakini usimruhusu mtu yeyote akuzuie kufanya uraki pamoja na Mungu. 23 Ni kweli kwamba kuna mambo ambayo hutaelewa mwanzoni. Unyenyekevu unahitajiwa ili kuomba msaada, lakini usisite kuuliza kwa sababu ya aibu. Yesu alisema kwamba ni vizuri kuwa mnyenyekevu kama mtoto mchanga. (Mathayo 18:2-4) Kama tujuavyo, watoto huuliza maswali mengi. Mungu anataka upate majibu. Biblia inawasifu watu waliokuwa na hamu ya kujifunza kumhusu Mungu. Waliyachunguza Maandiko kwa uangalifu ili kuhakikisha kwamba mambo waliyokuwa wakijifunza ni ya kweli.Matendo 17:11. 24 Njia bora zaidi ya kujifunza kumhusu Yehova ni kuichunguza Biblia. Biblia ni tofauti na vitabu vingine vyote. Jinsi gani? Sura inayofuata itazungumzia habari hiyo.
23, 24. (a) Kwa nini unapaswa kuendelea kuuliza maswali kuhusu mambo unayojifunza? (b) Ni habari gani itakayozungumziwa katika sura inayofuata?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA Mungu anakujali.1 Petro 5:7. Jina la Mungu ni Yehova. Zaburi 83:18. Yehova anataka umkaribie.Yakobo 4:8. Yehova ana upendo, fadhili, na rehema. Kutoka 34:6; 1 Yohana 4:8, 16.

SURA YA PILI

Biblia Kitabu Kutoka kwa Mungu


Biblia inatofautianaje na vitabu vingine? Biblia inawezaje kukusaidia kukabiliana na matatizo yako? Kwa nini unaweza kuamini unabii mbalimbali ulio katika Biblia?
HEBU wazia jinsi ulivyohisi ulipopata zawadi ya pekee kutoka kwa raki yako. Haikosi ulisisimuka na kufurahi kwelikweli. Mtu anapokupa zawadi anaonyesha kwamba anakuthamini. Bila shaka, ulimshukuru raki yako kwa sababu ya zawadi hiyo. 2 Biblia ni zawadi kutoka kwa Mungu, nasi tunapaswa kuithamini kwelikweli. Kitabu hicho cha pekee hufunua mambo ambayo hatungejua kwa njia nyingine yoyote. Kwa mfano, Biblia hutuambia kuhusu kuumbwa kwa mbingu zenye nyota, dunia, hali kadhalika mwanamume na mwanamke wa kwanza. Biblia ina kanuni zenye kutegemeka zinazotusaidia kukabiliana na matatizo na mahangaiko ya maisha. Inaeleza jinsi Mungu atakavyotimiza kusudi lake na kuleta hali bora duniani. Biblia ni zawadi nzuri kama nini! 3 Pia, Biblia ni zawadi inayochangamsha moyo kwa sababu inatueleza jambo fulani kumhusu Mpaji mwenyewe,
1, 2. Kwa nini tunaweza kusema kwamba Biblia ni zawadi nzuri kutoka kwa Mungu? 3. Yehova anaonyesha nini kwa kutupa Biblia, na kwa nini hilo linatuchangamsha?

19

Biblia TakatifuTafsiri ya Ulimwengu Mpya inapatikana katika lugha nyingi

Yehova Mungu. Kwa kuwa ametupa Biblia, ni wazi kwamba anataka tumjue vizuri. Kwa kweli, Biblia inaweza kukusaidia kumkaribia Yehova. 4 Leo, watu wengi wana Biblia. Biblia imechapishwa katika lugha zaidi ya 2,300 ikiwa nzima au kwa sehemu na kwa hiyo zaidi ya asilimia 90 ya watu ulimwenguni wanaweza kuipata. Kwa wastani, Biblia zaidi ya milioni moja hugawanywa kila juma! Mabilioni ya nakala za Biblia zimechapishwa zikiwa nzima au kwa sehemu. Kwa kweli, hakuna kitabu kingine kilicho kama Biblia. 5 Isitoshe, Biblia imeongozwa na roho ya Mungu. (2 Timotheo 3:16) Jinsi gani? Biblia yenyewe inajibu hivi: Wanadamu walisema yaliyotoka kwa Mungu kama walivyoongozwa na roho takatifu. (2 Petro 1:21) Kwa mfano: Huenda babu akamwomba mjukuu wake amwandikie barua. Mjukuu huyo ataandika mawazo na maagizo ya babu huyo. Kwa hiyo, kwa kweli barua hiyo ni ya babu huyo wala si ya mjukuu wake. Vivyo hivyo, Biblia ina ujumbe wa Mungu wala si wa watu
4. Ni nini kinachokupendeza kuhusu kugawanywa kwa Biblia? 5. Biblia imeongozwa na roho ya Mungu jinsi gani?

20

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

waliotumiwa kuiandika. Kwa hiyo, Biblia kwa kweli ni neno la Mungu.1 Wathesalonike 2:13.

NI SAHIHI NA YENYE UPATANO Biblia iliandikwa kwa kipindi cha zaidi ya miaka 1,600. Walioiandika walikuwa watu wa hali mbalimbali walioishi nyakati tofauti. Baadhi yao walikuwa wakulima, wavuvi, na wachungaji. Wengine walikuwa manabii, waamuzi, na wafalme. Luka aliyeandika Injili alikuwa daktari. Licha ya malezi mbalimbali ya watu walioiandika, Biblia ina upatano tangu mwanzo mpaka mwisho.1 7 Kitabu cha kwanza cha Biblia kinatuambia jinsi matatizo ya wanadamu yalivyoanza. Kitabu cha mwisho kinaonyesha kwamba dunia yote itakuwa paradiso, au bustani. Biblia nzima inazungumzia mambo ambayo yametukia kwa maelfu ya miaka, na kila sehemu inatusaidia kuelewa jinsi kusudi la Mungu linavyotimizwa. Upatano wa Biblia hauna kifani, na hilo halishangazi kwa kuwa Biblia ni kitabu kutoka kwa Mungu. 8 Biblia ni sahihi kisayansi. Hata ilizungumzia mambo yaliyokuja kugunduliwa baadaye. Kwa mfano, kitabu cha Mambo ya Walawi kina sheria walizopewa Waisraeli wa zamani kuhusu usa na kuwatenga wagonjwa ili kuepuka maambukizo ingawa mataifa jirani hayakujua mambo hayo. Wakati ambapo watu walikuwa na maoni yasiyo sahihi kuhusu umbo la dunia, Biblia ilisema kwamba dunia ni mviringo au duara. (Isaya 40:22) Biblia ilisema kwa usahihi kwamba dunia imetundikwa pasipo na kitu. (Ayubu 26:7) Biblia si kitabu cha sayansi. Hata hivyo, inapozungumzia
6

1 Ijapokuwa watu fulani husema kwamba sehemu fulani za Biblia zinapingana, madai hayo hayana msingi. Ona sura ya 7 ya kitabu BibliaNeno la Mungu au la Binadamu? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.
6, 7. Kwa nini upatano wa Biblia ni wa pekee sana? 8. Toa mifano inayoonyesha kwamba Biblia ni sahihi kisayansi.

BibliaKitabu Kutoka kwa Mungu

21

mambo ya sayansi, hufanya hivyo kwa usahihi. Tunatarajia kitabu kutoka kwa Mungu kiwe hivyo, sivyo? 9 Pia, Biblia ni sahihi na inategemeka kuhusu mambo ya kihistoria. Inasimulia mambo hususa yaliyotokea. Mbali na kutaja majina ya watu, inaonyesha pia ukoo wao.1 Tofauti na wanahistoria wa ulimwengu ambao mara nyingi hawataji kushindwa kwa mataifa yao, waandikaji wa Biblia walikuwa wanyoofu, hata waliandika kuhusu makosa yao wenyewe na ya taifa lao. Kwa mfano, katika kitabu cha Biblia cha Hesabu, mwandikaji Musa anakiri kosa lake kubwa lililofanya aadhibiwe vikali. (Hesabu 20:2-12) Si rahisi kuona unyoofu wa aina hiyo katika masimulizi mengine ya kihistoria lakini unapatikana katika Biblia kwa sababu ni kitabu cha Mungu.

KITABU CHENYE HEKIMA Biblia ni yenye faida kwa kufundisha, kwa kukaripia, kwa kunyoosha mambo, kwa sababu imeongozwa na roho ya Mungu. (2 Timotheo 3:16) Naam, Biblia ni kitabu chenye faida. Inaeleza kinaganaga hali ya wanadamu. Hilo halishangazi kwa kuwa Mtungaji wake ni Yehova Mungu, Muumba! Anaelewa kira na hisia zetu kuliko tunavyozielewa. Isitoshe, Yehova anajua tunachohitaji ili tuwe na furaha. Anajua pia mambo tunayopaswa kuepuka. 11 Fikiria yale yanayoitwa Mahubiri ya Mlimani ya Yesu katika Mathayo sura ya 5 mpaka ya 7. Katika mahubiri hayo bora, Yesu alizungumzia mambo mbalimbali kama vile jinsi
10

1 Kwa mfano, angalia ukoo wa Yesu unaofafanuliwa katika Luka 3: 23-38.


9. (a) Biblia ni sahihi na inategemeka kihistoria jinsi gani? (b) Unajifunza nini kuhusu Biblia kutokana na unyoofu wa watu walioiandika? 10. Kwa nini haishangazi kwamba Biblia ni kitabu chenye faida? 11, 12. (a) Yesu alizungumzia mambo gani katika Mahubiri yake ya Mlimani? (b) Ni mambo gani mengine muhimu yanayozungumziwa katika Biblia, na kwa nini shauri lake lina faida sikuzote?

Isaya, mwandikaji wa Biblia alitabiri kuanguka kwa Babiloni

ya kupata furaha ya kweli, jinsi ya kutatua mizozano, jinsi ya kusali, na jinsi ya kuwa na maoni yanayofaa kuelekea vitu vya kimwili. Maneno ya Yesu yanachochea na yana faida leo kama yalivyokuwa alipoyasema. 12 Kanuni fulani za Biblia zinahusu maisha ya familia, mazoea ya kazi, na mahusiano pamoja na wengine. Kanuni za Biblia zinawahusu watu wote, na shauri lake ni lenye faida sikuzote. Kupitia nabii Isaya, Mungu anataja hekima iliyo

BibliaKitabu Kutoka kwa Mungu

23

katika Biblia: Mimi, Yehova, ni Mungu wako, Yeye anayekufundisha ili ujifaidi mwenyewe.Isaya 48:17.

KITABU CHA UNABII Biblia ina unabii mwingi, baadhi yake umetimizwa. Kwa mfano, kupitia nabii Isaya aliyeishi katika karne ya nane K.W.K., Yehova alitabiri kwamba jiji la Babiloni lingeharibiwa.1 (Isaya 13:19; 14:22, 23) Habari hususa zilitolewa kuonyesha jinsi ambavyo uharibifu huo ungetokea. Majeshi yanayovamia yangekausha mto wa Babiloni na kuingia jijini bila hata kupigana. Si hayo tu. Unabii wa Isaya hata ulitaja jina la mfalme ambaye angeshinda Babiloni, yaani, Koreshi. Isaya 44:2745:2. 14 Miaka 200 hivi baadaye, usiku wa Oktoba 5/6, 539 K.W.K., jeshi lilipiga kambi karibu na Babiloni. Ni nani aliyekuwa amiri wa jeshi hilo? Mfalme wa Uajemi anayeitwa Koreshi. Kwa hiyo, wakati ulikuwa umeka wa kutimizwa kwa unabii huo wa ajabu. Lakini je, jeshi la Koreshi lingevamia Babiloni bila kupigana kama ilivyotabiriwa? 15 Wababiloni walikuwa na sherehe usiku huo na walihisi wakiwa salama katika jiji hilo lenye kuta kubwa. Wakati huohuo, Koreshi alikuwa akigeuza kwa ustadi mkondo wa maji ya mto uliokuwa ukipita katika jiji hilo. Muda si muda maji yalikuwa yamepungua kiasi cha kwamba majeshi yake yangeweza kuvuka mto na kukaribia kuta za jiji. Hata hivyo, jeshi la Koreshi lingeingiaje Babiloni lenye kuta kubwa? Kwa sababu moja au nyingine, usiku huo malango ya jiji hilo hayakuwa yamefungwa!
13

1 Ufupisho K.W.K. humaanisha Kabla ya Wakati wa Kawaida, ambao ni sahihi zaidi kuliko K.K. (Kabla ya Kristo). Ufupisho W.K. humaanisha Wakati wa Kawaida, ambao mara nyingi huitwa A.D., au Anno Domini, ikimaanisha Katika Mwaka wa Bwana Wetu.
13. Yehova alimwongoza nabii Isaya aandike habari gani hususa kuhusu Babiloni? 14, 15. Unabii wa Isaya kuhusu Babiloni ulitimizwaje?

24
16

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Ilitabiriwa hivi kuhusu Babiloni: Hatakaliwa kamwe, wala hatakuwa na makao kwa kizazi baada ya kizazi. Na hapo Mwarabu hatapiga hema lake, na hakuna wachungaji watakaoruhusu makundi yao kulala hapo. (Isaya 13:20) Unabii huo ulitabiri hata mambo ambayo yangetokea baada ya jiji hilo kuanguka. Ulionyesha kwamba jiji la Babiloni lingeachwa ukiwa daima. Unaweza kuona utimizo wa maneno hayo. Eneo lenye ukiwa la Babiloni la kale, kilometa 80 hivi kusini mwa Baghdad, nchini Iraq, linathibitisha kwamba unabii huu wa Yehova kupitia nabii Isaya umetimizwa: Nami nitamfagia kwa ufagio wa maangamizi.Isaya 14:22, 23.1 17 Kuchunguza jinsi Biblia ilivyo kitabu chenye unabii wa kutegemeka ni jambo lenye kuimarisha imani, sivyo? Ikiwa
1 Unaweza kupata habari zaidi kuhusu unabii wa Biblia, katika broshua Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, ukurasa wa 27-29, iliyochapishwa na Mashahidi wa Yehova.
16. (a) Isaya alitabiri nini kuhusu mambo ambayo yangepata jiji la Babiloni? (b) Unabii wa Isaya kuhusu ukiwa wa Babiloni ulitimizwaje? 17. Kutimizwa kwa unabii wa Biblia kunaimarishaje imani?

BibliaKitabu Kutoka kwa Mungu

25

Yehova tayari ametimiza ahadi zake za wakati uliopita, tuna kila sababu ya kuamini kwamba atatimiza pia ahadi yake ya kuifanya dunia iwe paradiso. (Hesabu 23:19) Kwa kweli tuna tumaini la uzima wa milele ambao Mungu, asiyeweza kusema uwongo, aliahidi nyakati za zamani za kale.Tito 1:2.1

NENO LA MUNGU LIKO HAI Kutokana na mambo ambayo tumechunguza katika sura hii, ni wazi kwamba kwa kweli Biblia ni kitabu cha pekee. Hata hivyo, thamani yake haitokani tu na upatano
18

1 Kuharibiwa kwa Babiloni ni mfano mmoja tu wa unabii wa Biblia ambao umetimizwa. Mifano mingine inatia ndani kuharibiwa kwa Tiro na Ninawi. (Ezekieli 26:1-5; Sefania 2:13-15) Pia, unabii wa Danieli ulitabiri milki za ulimwengu ambazo zingetawala baada ya Babiloni. Zilitia ndani Ugiriki na muungano wa Umedi na Uajemi. (Danieli 8:5-7, 20-22) Unaweza kupata habari zaidi kuhusu unabii mbalimbali unaomhusu Masihi uliotimizwa na Yesu Kristo, katika Nyongeza iliyo kwenye ukurasa wa 199-201.
18. Mtume Mkristo Paulo anasema maneno gani yenye kuchochea kuhusu neno la Mungu?

Magofu ya Babiloni

26

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

wake, usahihi wake wa kisayansi na wa kihistoria, hekima iliyomo, na unabii uliomo unaotegemeka. Mtume Mkristo Paulo aliandika: Neno la Mungu liko hai nalo lina nguvu na ni lenye makali zaidi kuliko upanga wowote wenye makali kuwili nalo huchoma hata kukia kugawanya nafsi na roho, na viungo na urojorojo wake, nalo linaweza kutambua kira na makusudio ya moyo.Waebrania 4:12. 19 Kusoma neno la Mungu au ujumbe ulio katika Biblia kunaweza kubadili maisha yetu. Kunaweza kutusaidia tujichunguze vizuri zaidi. Huenda tukadai kwamba tunampenda Mungu, lakini jinsi tunavyoitikia mafundisho ya Neno lake, Biblia, lililoongozwa na roho kutaonyesha wazi mawazo yetu na hata mwelekeo wa moyo wetu. 20 Kwa kweli, Biblia ni kitabu kutoka kwa Mungu. Ni kitabu ambacho tunapaswa kusoma, kujifunza, na kukipenda. Onyesha kwamba unaithamini zawadi hiyo kutoka kwa Mungu kwa kuendelea kujifunza yaliyomo. Kwa kufanya hivyo, utaelewa hata zaidi kusudi la Mungu kwa wanadamu. Sura inayofuata itazungumzia kusudi hilo na jinsi litakavyotimizwa.
19, 20. (a) Biblia inawezaje kukusaidia ujichunguze? (b) Unawezaje kuonyesha kwamba unaithamini Biblia ikiwa zawadi ya pekee kutoka kwa Mungu?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA Biblia imeongozwa na roho ya Mungu na kwa hiyo ni sahihi na inategemeka.2 Timotheo 3:16. Habari iliyo katika Neno la Mungu inahusu maisha ya kila siku.Isaya 48:17. Ahadi za Mungu zilizo katika Biblia zitatimizwa hakika.Hesabu 23:19.

SURA YA TATU

Mungu Ana Kusudi Gani kwa Dunia?


Mungu ana kusudi gani kwa wanadamu? Mungu amepingwaje? Maisha yatakuwaje duniani wakati ujao?
KUSUDI la Mungu kwa dunia ni zuri ajabu. Yehova anataka dunia ijae watu wenye furaha na afya. Biblia inasema kwamba Mungu alipanda bustani katika Edeni na kuchipusha kila mti wenye kutamanika kwa macho ya mtu na ulio mwema kwa chakula. Baada ya Mungu kumuumba mwanamume na mwanamke wa kwanza, Adamu na Hawa, aliwaweka katika makao hayo mazuri na kuwaambia: Zaeni, muwe wengi, mjaze dunia na kuitiisha. (Mwanzo 1:28; 2:8, 9, 15) Kwa hiyo Mungu alikusudia wanadamu wawe na watoto, waieneze bustani hiyo duniani pote, na kuwatunza wanyama. 2 Je, unakiri kusudi la Yehova Mungu kwamba wanadamu waishi katika dunia iliyo paradiso litatimia? Mungu anasema hivi: Mimi nimesema hilo; pia nitalitimiza. (Isaya 46:9-11; 55:11) Naam, Mungu atatimiza kusudi lake! Kuhusu dunia, anasema kwamba hakuiumba tu bila sababu, bali aliiumba ili ikaliwe na watu. (Isaya 45:18) Mungu alitaka dunia ikaliwe na watu wa aina gani? Naye alitaka wakae humo kwa muda gani? Biblia inajibu: Waadilifu wenyewe wataimiliki dunia, nao watakaa milele juu yake.Zaburi 37:29; Ufunuo 21:3, 4.
1. Ni nini kusudi la Mungu kwa dunia? 2. (a) Tunajuaje kwamba kusudi la Mungu kwa dunia litatimia? (b) Biblia inasema nini kuhusu wanadamu kuishi milele?

28
3

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Ni wazi kwamba kusudi la Mungu halijatimia bado. Leo watu wanakuwa wagonjwa na kufa; hata wanapigana na kuuana. Mambo yaliharibika. Hata hivyo, hapana shaka kwamba Mungu hakukusudia dunia iwe kama ilivyo leo! Ni nini kilichotukia? Kwa nini kusudi la Mungu halijatimia? Hakuna kitabu chochote cha kihistoria kilichoandikwa na mwanadamu kinaweza kutuambia kwa sababu matatizo yalianzia mbinguni.

ADUI ATOKEA Kitabu cha kwanza cha Biblia kinataja kuhusu mpinzani wa Mungu aliyetokea katika bustani ya Edeni. Anaitwa nyoka, ingawa hakuwa mnyama halisi. Katika kitabu cha mwisho cha Biblia anaitwa Ibilisi na Shetani, anayeipotosha dunia nzima inayokaliwa. Pia anaitwa yule nyoka wa zamani. (Mwanzo 3:1; Ufunuo 12:9) Malaika huyo mwenye nguvu, au kiumbe asiyeonekana mwenye mwili wa kiroho, alitumia nyoka kuzungumza na Hawa, kama vile mtu mwenye ustadi anavyoweza kufanya ionekane kana kwamba sauti inatoka katika mwanasesere au sanamu. Bila shaka kiumbe huyo alikuwapo Mungu alipokuwa akiitayarisha dunia kwa ajili ya wanadamu.Ayubu 38:4, 7. 5 Kwa kuwa uumbaji wote wa Yehova ni mkamilifu, basi, ni nani aliyemfanya Shetani Ibilisi? Kwa ufupi, mmoja kati ya wana wenye nguvu wa Mungu aligeuka akawa Ibilisi. Jinsi gani? Leo mtu ambaye wakati fulani alikuwa mzuri na mnyoofu anaweza kugeuka na kuwa mwizi. Hilo linawezekanaje? Huenda mtu akaruhusu tamaa mbaya iingie moyoni mwake. Akiendelea kuisitawisha, tamaa hiyo inaweza kuwa na nguvu sana. Kisha akipata nafasi, anaweza
4

3. Ni hali gani zenye kuhuzunisha zilizopo duniani leo, na ni maswali gani yanayozuka? 4, 5. (a) Ni nani hasa aliyetumia nyoka kuzungumza na Hawa? (b) Mtu aliyekuwa mzuri na mnyoofu anawezaje kugeuka na kuwa mwizi?

Mungu Ana Kusudi Gani kwa Dunia?

29

kutenda kulingana na tamaa hiyo mbaya ambayo imekuwa ikisitawi moyoni mwake.Yakobo 1:13-15. 6 Ndivyo ilivyokuwa kuhusu Shetani Ibilisi. Huenda alimsikia Mungu akiwaambia Adamu na Hawa wazae watoto na kuijaza dunia. (Mwanzo 1:27, 28) Haikosi Shetani aliwaza hivi: Kwani, si wanadamu hao wote wanaweza kuniabudu mimi badala ya kumwabudu Mungu! Kwa hiyo, tamaa mbaya ikaanza kusitawi moyoni mwake. Mwishowe, akaamua kumdanganya Hawa kwa kumwambia uwongo kumhusu Mungu. (Mwanzo 3:1-5) Basi, akawa Ibilisi, jina linalomaanisha Mchongezi. Wakati huohuo akawa Shetani, jina linalomaanisha Mpinzani. 7 Kwa kutumia uwongo na ujanja, Shetani Ibilisi aliwafanya Adamu na Hawa wamwasi Mungu. (Mwanzo 2:17; 3:6) Mwishowe, wakafa kwa sababu ya uasi kama Mungu alivyokuwa amesema. (Mwanzo 3:17-19) Kwa kuwa Adamu alipoteza ukamilifu alipoasi, wazao wake wote walirithi dhambi kutoka kwake. (Waroma 5:12) Hali hiyo inaweza kulinganishwa na sufuria inayotumiwa kuoka mikate. Ikiwa sufuria hiyo imejikunja, kila mkate utakaookwa katika sufuria hiyo utakuwaje? Kila mkate utakuwa na alama, au kasoro. Vivyo hivyo, kila mwanadamu amerithi kasoro ya kutokamilika kutoka kwa Adamu. Ndiyo sababu wanadamu wote huzeeka na kufa.Waroma 3:23. 8 Shetani alipowashawishi Adamu na Hawa wafanye dhambi dhidi ya Mungu, alianzisha uasi. Alikuwa akipinga utawala wa Yehova. Ni kana kwamba Shetani alikuwa akisema: Mungu ni mtawala mbaya. Yeye husema uwongo na kuwanyima raia wake vitu vizuri. Wanadamu
6. Mmoja kati ya wana wenye nguvu wa Mungu aligeukaje na kuwa Shetani Ibilisi? 7. (a) Kwa nini Adamu na Hawa walikufa? (b) Kwa nini wazao wote wa Adamu huzeeka na kufa? 8, 9. (a) Yaelekea Shetani alidai nini? (b) Kwa nini Mungu hakuwaharibu waasi hao mara moja?

30

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

hawahitaji kutawaliwa na Mungu. Wanaweza kujiamulia yaliyo mema na mabaya. Na watakuwa na maisha mazuri zaidi nikiwatawala. Mungu angeshughulikiaje upinzani huo? Watu fulani husema kwamba afadhali Mungu angewaua tu waasi hao. Lakini je, kufanya hivyo kungetatua

Shetani angewezaje kumwahidi Yesu falme zote za ulimwengu ikiwa hazikuwa zake?

Mungu Ana Kusudi Gani kwa Dunia?

31

upinzani wa Shetani? Je, kungethibitisha kwamba utawala wa Mungu ndio unaofaa? 9 Yehova hangewaua waasi hao mara moja kwa sababu yeye ni Mungu mwenye haki kabisa. Aliamua kwamba wakati ulihitajiwa ili kutatua upinzani wa Shetani kwa njia yenye kuridhisha na kuthibitisha kwamba Ibilisi ni mwongo. Kwa hiyo Mungu akaamua kwamba atawaacha wanadamu wajitawale kwa muda fulani chini ya uvutano wa Shetani. Sura ya 11 ya kitabu hiki itaeleza sababu iliyomfanya Yehova aamue hivyo na kuruhusu muda wa kutosha upite kabla ya kutatua masuala hayo. Hata hivyo, kwa sasa ni vizuri kujiuliza hivi: Je, Adamu na Hawa walikuwa na sababu ya kumwamini Shetani ambaye hakuwa amewafanyia jambo lolote zuri? Je, walikuwa na msingi wowote wa kuamini kwamba Yehova ambaye alikuwa amewapa vyote walivyokuwa navyo, ni mwongo na mkatili? Wewe ungefanyaje? 10 Ni vizuri kukiria maswali hayo kwa sababu kila mmoja wetu anakabili masuala hayo leo. Naam, wewe una nafasi ya kuunga mkono upande wa Yehova na kumpinga Shetani. Unaweza kumkubali Yehova kuwa Mtawala na kuonyesha kwamba Shetani ni mwongo. (Zaburi 73:28; Methali 27:11) Inasikitisha kwamba, kati ya mabilioni ya watu ulimwenguni pote, ni wachache tu wanaoamua kufanya hivyo. Hilo linatokeza swali muhimu, Je, kweli Biblia inafundisha kwamba Shetani anatawala ulimwengu huu?
11

NI NANI ANAYEUTAWALA ULIMWENGU HUU? Yesu hakuwa na shaka yoyote kwamba Shetani ndiye

10. Unawezaje kuunga mkono upande wa Yehova na kumpinga Shetani? 11, 12. (a) Kushawishiwa kwa Yesu kunaonyeshaje kwamba Shetani ndiye mtawala wa ulimwengu huu? (b) Ni nini kingine kinachothibitisha kwamba Shetani ndiye mtawala wa ulimwengu huu?

32

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

mtawala wa ulimwengu huu. Pindi moja Shetani alimwonyesha Yesu kimuujiza falme zote za ulimwengu na utukufu wazo. Kisha Shetani akamwahidi Yesu: Nitakupa mambo yote haya ukianguka chini na kunifanyia tendo la ibada. (Mathayo 4:8, 9; Luka 4:5, 6) Hebu kiria: Je, Shetani angeweza kumshawishi Yesu kwa kutoa ahadi hiyo ikiwa hakuwa mtawala wa falme hizo? Yesu hakupinga kwamba serikali zote hizo za ulimwengu hazikuwa za Shetani. Bila shaka, Yesu angepinga ikiwa hazikuwa za Shetani. 12 Bila shaka, Yehova ndiye Mungu Mweza-Yote, Muumba wa ulimwengu wetu wa ajabu. (Ufunuo 4:11) Hata hivyo, Biblia haisemi kamwe kwamba Yehova Mungu au Yesu Kristo ni watawala wa ulimwengu huu. Yesu alimwita Shetani mtawala wa ulimwengu huu. (Yohana 12:31; 14:30; 16:11) Hata Biblia inamwita Shetani Ibilisi mungu wa mfumo huu wa mambo. (2 Wakorintho 4:3, 4) Kuhusu mpinzani huyo au Shetani, mtume Mkristo Yohana aliandika: Ulimwengu mzima unakaa katika nguvu za yule mwovu.1 Yohana 5:19.

JINSI ULIMWENGU WA SHETANI UTAKAVYOONDOLEWA 13 Ulimwengu unazidi kuwa hatari mwaka baada ya mwaka. Kuna majeshi mengi yanayopigana, wanasiasa wasadi, viongozi wa kidini wanaki, na wahalifu sugu. Haiwezekani kuubadili ulimwengu kwa ujumla. Biblia inasema kwamba hivi karibuni Mungu atauondolea mbali ulimwengu huu mbovu katika vita vya HarMagedoni. Kisha ataleta ulimwengu mpya wenye uadilifu.Ufunuo 16: 14-16. 14 Yehova Mungu alimchagua Yesu Kristo awe Mta13. Kwa nini tunahitaji ulimwengu mpya? 14. Mungu amemchagua nani awe Mtawala katika Ufalme Wake, na hilo lilitabiriwaje?

Mungu Ana Kusudi Gani kwa Dunia?

33

wala wa Ufalme au serikali Yake ya mbinguni. Biblia ilitabiri hivi zamani: Kwa maana kuna mtoto ambaye amezaliwa kwetu, kuna mwana ambaye tumepewa; na utawala wa ukuu utakuwa juu ya bega lake. Naye ataitwa . . . Mkuu wa Amani. Hakutakuwa na mwisho kwa habari ya wingi wa huo utawala wa kifalme na kwa amani. (Isaya 9:6, 7) Kuhusu serikali hiyo, Yesu aliwafundisha wafuasi wake wasali hivi: Ufalme wako na uje. Mapenzi yako na yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni. (Mathayo 6:10) Kama tutakavyoona baadaye katika kitabu hiki, karibuni Ufalme wa Mungu utaondolea mbali serikali zote za ulimwengu huu nao utatawala badala ya serikali hizo. (Danieli 2:44) Kisha Ufalme wa Mungu utaleta paradiso duniani.

ULIMWENGU MPYA U KARIBU! Biblia inatuhakikishia hivi: Kulingana na ahadi yake [Mungu] tunangojea mbingu mpya na dunia mpya, na humo uadilifu utakaa. (2 Petro 3:13; Isaya 65:17) Nyakati nyingine Biblia inapotaja dunia, inamaanisha watu wanaoishi duniani. (Mwanzo 11:1) Kwa hiyo dunia mpya yenye uadilifu ni jamii ya watu watakaopata kibali cha Mungu. 16 Yesu aliahidi kwamba katika ulimwengu mpya unaokuja, wale wanaopata kibali cha Mungu watapokea zawadi ya uzima wa milele. (Marko 10:30) Tafadhali fungua Yohana 3:16 na Yohana 17:3 katika Biblia yako, na usome yale ambayo Yesu alisema tunapaswa kufanya ili tupate uzima wa milele. Sasa ona baraka zinazotajwa katika Biblia zitakazofurahiwa na wale wanaostahili kupokea zawadi hiyo ya pekee kutoka kwa Mungu katika dunia itakayokuwa Paradiso.
15

15. Dunia mpya ni nini? 16. Ni zawadi gani yenye thamani sana ambayo Mungu atawapa wale walio na kibali chake, na tunapaswa kufanya nini ili tuipokee?

34
17

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Hakutakuwa na uovu, vita, uhalifu, na ujeuri. Mtu mwovu hatakuwako tena . . . Bali wapole wataimiliki dunia. (Zaburi 37:10, 11) Kutakuwa na amani kwa sababu Mungu atakomesha vita mpaka kwenye mwisho wa dunia. (Zaburi 46:9; Isaya 2:4) Kisha mwadilifu atachipuka, na wingi wa amani mpaka mwezi utakapokuwa haupo tenayaani, milele!Zaburi 72:7. 18 Waabudu wa Yehova wataishi kwa usalama. Nyakati zote Waisraeli katika nyakati za Biblia walipomtii Mungu, waliishi kwa usalama. (Mambo ya Walawi 25:18, 19) Litakuwa jambo zuri ajabu kufurahia usalama kama huo katika Paradiso!Isaya 32:18; Mika 4:4. 19 Hakutakuwa na upungufu wa chakula. Mtunga-zaburi aliimba hivi: Kutakuwa na wingi wa nafaka duniani; juu ya milima kutakuwa na mafuriko. (Zaburi 72:16) Yehova Mungu atawabariki waadilifu wake, na hakika dunia itatoa mazao yake.Zaburi 67:6. 20 Dunia nzima itakuwa paradiso. Kutakuwa na makao na bustani zenye kupendeza katika sehemu zilizokuwa zimeharibiwa na wanadamu wenye dhambi. (Isaya 65:21-24; Ufunuo 11:18) Kadiri wakati unavyopita, sehemu za dunia zinazokaliwa zitapanuka mpaka dunia yote iwe yenye kupendeza na kuzaa sana kama bustani ya Edeni. Na Mungu hatakosa kamwe kufumbua mkono wake na kutosheleza tamaa ya kila kitu kilicho hai.Zaburi 145:16. 21 Kutakuwa na amani kati ya wanadamu na wanyama. Wanyama mwitu na wa kufugwa watalisha pamoja. Hata
17, 18. Tunawezaje kuwa na hakika kwamba kutakuwa na amani na usalama duniani pote? 19. Tunajuaje kwamba kutakuwa na chakula kingi katika ulimwengu mpya wa Mungu? 20. Kwa nini tunaweza kuwa na hakika kwamba dunia nzima itakuwa paradiso? 21. Ni nini kinachoonyesha kwamba kutakuwa na amani kati ya wanadamu na wanyama?

36

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

mtoto mdogo hataogopa wanyama ambao ni hatari leo. Isaya 11:6-9; 65:25. 22 Magonjwa hayatakuwapo. Akiwa Mtawala wa Ufalme wa mbinguni wa Mungu, Yesu ataponya watu kwa kiwango kikubwa zaidi kuliko alivyofanya alipokuwa duniani. (Mathayo 9:35; Marko 1:40-42; Yohana 5:5-9) Hatimaye, hakuna mkaaji atakayesema: Mimi ni mgonjwa. Isaya 33:24; 35:5, 6. 23 Wapendwa waliokufa watafufuliwa wakiwa na tumaini la kuishi milele. Wote wanaolala katika kifo walio katika kumbukumbu ya Mungu watafufuliwa. Kutakuwa na ufufuo wa waadilifu na wasio waadilifu pia.Matendo 24:15; Yohana 5:28, 29. 24 Wale wanaoamua kujifunza kuhusu Muumba wetu Mtukufu, Yehova Mungu na kumtumikia wana tumaini zuri kama nini! Yesu alikuwa akizungumzia Paradiso ya wakati ujao hapa duniani alipomwahidi hivi yule mtenda maovu aliyetundikwa pamoja naye: Utakuwa pamoja nami katika Paradiso. (Luka 23:43) Tunapaswa kujifunza mengi zaidi kumhusu Yesu Kristo, atakayetumiwa kuleta baraka hizo zote.
22. Ni hatua gani itakayochukuliwa kuhusiana na magonjwa? 23. Kwa nini ufufuo utaleta shangwe mioyoni mwetu? 24. Unaonaje kuhusu kuishi katika Paradiso duniani?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA Kusudi la Mungu la kuifanya dunia iwe paradiso litatimia.Isaya 45:18; 55:11. Shetani ndiye anayeutawala ulimwengu huu. Yohana 12:31; 1 Yohana 5:19. Katika ulimwengu mpya unaokuja, Mungu atawabariki sana wanadamu.Zaburi 37:10, 11, 29.

SURA YA NNE

Yesu Kristo Ni Nani?


Yesu ana jukumu gani muhimu? Alitoka wapi? Alikuwa mtu wa aina gani?
KUNA watu wengi mashuhuri ulimwenguni. Baadhi yao wanajulikana sana katika jamii zao, majiji yao, au nchi zao. Wengine wanajulikana ulimwenguni pote. Hata hivyo, kujua tu jina la mtu fulani mashuhuri, hakumaanishi kwamba unamjua vizuri. Haimaanishi kwamba unajua malezi yake na utu wake kabisa. 2 Watu ulimwenguni pote wamesikia kumhusu Yesu Kristo, ingawa aliishi duniani miaka 2,000 hivi iliyopita. Hata hivyo, wengi hawajui kwa kweli Yesu alikuwa nani. Baadhi yao husema kwamba alikuwa mtu mzuri tu. Wengine wanadai kwamba alikuwa nabii tu. Na wengine wanaamini kwamba Yesu ni Mungu na anapaswa kuabudiwa. Je, anapaswa kuabudiwa? 3 Ni muhimu ujue ukweli kumhusu Yesu. Kwa nini? Kwa sababu Biblia inasema: Uzima wa milele ndio huu, waendelee kupata ujuzi juu yako wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na juu ya yule uliyemtuma, Yesu Kristo. (Yohana 17:3) Ndiyo, kujua ukweli kumhusu Yehova Mungu na Yesu Kristo kutakuwezesha kupata uzima wa milele katika paradiso duniani. (Yohana 14:6) Isitoshe, Yesu alionyesha kwa njia bora zaidi jinsi ya kuishi na kuwatendea
1, 2. (a) Kwa nini kujua jina la mtu mashuhuri hakumaanishi kwamba unamjua vizuri? (b) Watu wana maoni gani yanayotofautiana kumhusu Yesu? 3. Kwa nini ni muhimu ujue ukweli kumhusu Yesu?

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

wengine. (Yohana 13:34, 35) Katika sura ya kwanza ya kitabu hiki tulizungumzia ukweli kumhusu Mungu. Sasa, na tuchunguze mambo ambayo Biblia inafundisha kumhusu Yesu Kristo.

MASIHI ALIYEAHIDIWA Zamani kabla ya Yesu kuzaliwa, Biblia ilikuwa imetabiri kuja kwa yule ambaye Mungu angemtuma akiwa Masihi, au Kristo. Majina Masihi (kutokana na neno la Kiebrania) na Kristo (kutokana na neno la Kigiriki) yanamaanisha Mtiwa-Mafuta. Huyo aliyeahidiwa angetiwa mafuta, yaani, angewekwa rasmi na Mungu katika cheo cha pekee. Katika sura za baadaye
4

4. Majina Masihi na Kristo yanamaanisha nini?

Baada ya kubatizwa, Yesu akawa Masihi, au Kristo

Yesu Kristo Ni Nani

39

za kitabu hiki, tutajifunza mengi kuhusu jukumu muhimu la Masihi kuhusiana na kutimia kwa ahadi za Mungu. Pia tutajifunza kuhusu baraka ambazo Yesu anaweza kutuletea hata sasa. Hata hivyo, kabla Yesu hajazaliwa, watu wengi walijiuliza, Ni nani atakayekuwa Masihi? 5 Katika karne ya kwanza W.K., wanafunzi wa Yesu wa Nazareti walisadiki kabisa kwamba ndiye alikuwa Masihi aliyeahidiwa. (Yohana 1:41) Simoni Petro, mmoja wa wanafunzi hao, alimwambia Yesu waziwazi: Wewe ndiye Kristo. (Mathayo 16:16) Hata hivyo, wanafunzi hao wangewezaje kuwa na hakika kwamba Yesu kwa kweli ndiye Masihi aliyeahidiwa? Namna gani sisi? 6 Manabii wa Mungu walioishi kabla ya Yesu walitabiri mambo mengi kumhusu Masihi. Mambo hayo yangewasaidia watu wengine kumtambua. Kwa mfano: Tuseme umeombwa uende kwenye kituo cha mabasi chenye shughuli nyingi au kwenye kituo cha magari-moshi au kwenye uwanja wa ndege kumpokea mtu ambaye hujapata kukutana naye. Ingefaa ikiwa mtu fulani angekupa habari zaidi kumhusu, sivyo? Vivyo hivyo, kupitia manabii wa Biblia, Yehova ametueleza mambo mengi kuhusu utendaji wa Masihi na mambo ambayo yangempata. Kutimia kwa unabii huo mbalimbali kungewasaidia watu waaminifu wamtambue waziwazi. 7 Fikiria mifano miwili tu. Kwanza, zaidi ya miaka 700 mapema, nabii Mika alitabiri kwamba Yule aliyeahidiwa angezaliwa Bethlehemu, mji mdogo katika Yuda. (Mika 5:2) Yesu alizaliwa wapi hasa? Katika mji huohuo! (Mathayo 2:1, 3-9) Pili, karne nyingi mapema, unabii ulio katika Danieli 9:25 ulionyesha mwaka hususa ambao
5. Wanafunzi wa Yesu walisadiki nini kumhusu? 6. Toa mfano unaoonyesha jinsi Yehova amewasaidia watu waaminifu kumtambua Masihi. 7. Ni mambo gani mawili yaliyotabiriwa kuhusiana na Yesu ambayo yalitimia?

40

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Masihi angetokea, yaani, 29 W.K.1 Kutimia kwa unabii huo na unabii mwingine mbalimbali kunathibitisha kwamba Yesu alikuwa Masihi aliyeahidiwa. 8 Uthibitisho zaidi wa kwamba Yesu ndiye Masihi ulionekana wazi mwishoni mwa mwaka wa 29 W.K. Huo ndio mwaka ambao Yesu alimwendea Yohana Mbatizaji ili abatizwe katika Mto Yordani. Yehova alikuwa amemwahidi Yohana kwamba angempa ishara ili amtambue Masihi. Yohana aliona ishara hiyo Yesu alipobatizwa. Biblia inasimulia lililotukia: Baada ya kubatizwa Yesu akapanda mara moja kutoka katika maji; na, tazama! mbingu zikafunguliwa, naye akaona roho ya Mungu ikishuka kama njiwa, ikija juu yake. Tazama! Kulikuwa pia na sauti kutoka mbinguni iliyosema: Huyu ni Mwanangu, mpendwa, ambaye nimemkubali. (Mathayo 3:16, 17) Baada ya kusikia na kuona kilichotukia, Yohana hakuwa na shaka kwamba Yesu alitumwa na Mungu. (Yohana 1:32-34) Wakati roho ya Mungu au nguvu ya utendaji ilipomiminwa juu yake siku hiyo, Yesu akawa Masihi au Kristo, ambaye aliwekwa rasmi kuwa Kiongozi na Mfalme.Isaya 55:4. 9 Utimizo wa unabii wa Biblia na ushuhuda wa Mungu mwenyewe unaonyesha wazi kwamba Yesu ndiye Masihi aliyeahidiwa. Lakini Biblia inajibu maswali mengine mawili muhimu kumhusu Yesu Kristo: Alitoka wapi? Na alipokuwa mwanadamu, alikuwa mtu wa aina gani? YESU ALITOKA WAPI? Biblia inafundisha kwamba Yesu aliishi mbinguni

10

1 Unaweza kupata maelezo kuhusu unabii wa Danieli uliotimia kuhusiana na Yesu katika Nyongeza, ukurasa wa 197-199. 8, 9. Uthibitisho wa kwamba Yesu alikuwa Masihi ulionekanaje wazi alipobatizwa? 10. Biblia inafundisha nini kuhusu maisha ya Yesu kabla ya kuja duniani?

Yesu Kristo Ni Nani

41

kabla ya kuja duniani. Mika alitabiri kwamba Masihi angezaliwa Bethlehemu na alisema pia kwamba asili Yake ni kutoka nyakati za kale. (Mika 5:2) Mara nyingi, Yesu mwenyewe alisema kwamba aliishi mbinguni kabla ya kuwa mwanadamu. (Yohana 3:13; 6:38, 62; 17:4, 5) Akiwa kiumbe wa roho mbinguni, Yesu alikuwa na uhusiano wa pekee pamoja na Yehova. 11 Yesu ni Mwana mpendwa zaidi wa Yehovana kuna sababu nzuri. Anaitwa mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote, kwa sababu aliumbwa kwanza na Mungu.1 (Wakolosai 1:15) Kuna jambo lingine linalomfanya Mwana huyu awe wa pekee. Yeye ni Mwana mzaliwa-pekee. (Yohana 3:16) Hilo linamaanisha kwamba ni Yesu peke yake aliyeumbwa moja kwa moja na Mungu. Pia Mungu alimtumia Yesu peke yake kuumba vitu vingine vyote. (Wakolosai 1:16) Pia, Yesu anaitwa Neno. (Yohana 1:14) Hilo linamaanisha kwamba alizungumza kwa niaba ya Mungu, akiwasilisha ujumbe na maagizo kwa wana wengine wa Baba yake, yaani, malaika na wanadamu. 12 Je, Mwana huyo mzaliwa wa kwanza yuko sawa na Mungu kama wengine wanavyoamini? Biblia haifundishi hivyo. Kama tulivyoona katika fungu lililotangulia, Mwana huyo aliumbwa. Basi ni wazi kwamba alikuwa na mwanzo, lakini Yehova Mungu hana mwanzo wala mwisho. (Zaburi 90:2) Mwana huyo mzaliwa-pekee hakujaribu kamwe kuwa sawa na Baba yake. Biblia inafundisha wazi kwamba Baba ni mkuu kuliko Mwana. (Yohana 14:28;
1 Yehova anaitwa Baba kwa sababu yeye ndiye Muumba. (Isaya 64:8) Yesu anaitwa Mwana wa Mungu kwa sababu aliumbwa na Mungu. Vivyo hivyo, malaika wengine na Adamu wanaitwa wana wa Mungu.Ayubu 1:6; Luka 3:38. 11. Biblia inaonyeshaje kwamba Yesu ndiye Mwana mpendwa zaidi wa Yehova? 12. Tunajuaje kwamba Mwana mzaliwa wa kwanza halingani na Mungu?

42

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

1 Wakorintho 11:3) Yehova peke yake ndiye Mungu Mweza-Yote. (Mwanzo 17:1) Kwa hiyo, hakuna yeyote anayelingana naye.1 13 Yehova na Mwana mzaliwa wake wa kwanza walikuwa na uhusiano wa karibu mabilioni ya miaka kabla ya mbingu zenye nyota na dunia kuumbwa. Walipendana kwelikweli! (Yohana 3:35; 14:31) Mwana huyo mpendwa alikuwa tu kama Baba yake. Ndiyo sababu Biblia inamwita Mwana huyo mfano wa Mungu asiyeonekana. (Wakolosai 1:15) Ndiyo, kama vile mwana wa mwanadamu anavyoweza kufanana na baba yake katika njia mbalimbali, Mwana huyo wa kimbingu alionyesha sifa na utu wa Baba yake. 14 Mwana mzaliwa-pekee wa Yehova alikubali kuacha makao yake mbinguni na kuja kuishi duniani kama mwanadamu. Lakini huenda ukajiuliza, Iliwezekanaje kiumbe wa roho kuzaliwa kama mwanadamu? Ili kutimiza hilo, Yehova alifanya muujiza. Alihamisha uhai wa Mwana wake wa kwanza kutoka mbinguni na kuutia katika tumbo la bikira Myahudi aliyeitwa Maria. Yesu hakuwa na baba wa kibinadamu. Basi, Maria alimzaa mwana mkamilifu na kumwita Yesu.Luka 1:30-35. YESU ALIKUWA MTU WA AINA GANI? Mambo ambayo Yesu alisema na kutenda alipokuwa duniani yanatusaidia kumjua vizuri. Pia, kupitia Yesu tunapata kumjua Yehova vizuri zaidi. Kwa nini? Kumbuka kwamba Mwana huyo anamwakilisha Baba yake kika15

1 Unaweza kupata uthibitisho zaidi unaoonyesha kwamba Mwana mzaliwa wa kwanza halingani na Mungu, katika Nyongeza, ukurasa wa 201-204. 13. Biblia humaanisha nini inapomwita Mwana mfano wa Mungu asiyeonekana? 14. Mwana mzaliwa-pekee wa Yehova alizaliwaje akiwa mwanadamu? 15. Tunawezaje kumjua Yehova vizuri zaidi kupitia Yesu?

Yesu Kristo Ni Nani

43

milifu. Ndiyo sababu Yesu alimwambia mwanafunzi wake hivi: Yule ambaye ameniona mimi amemwona Baba pia. (Yohana 14:9) Vitabu vinne vya Biblia vinavyoitwa Injili, yaani, Mathayo, Marko, Luka, na Yohana, vinatuambia mengi kuhusu maisha, utendaji, na sifa za Yesu Kristo. 16 Watu wengi walimjua Yesu kuwa Mwalimu. (Yohana 1:38; 13:13) Alifundisha nini? Ujumbe wake wa msingi ulikuwa habari njema ya ufalme, yaani, Ufalme wa Mungu, serikali ya mbinguni itakayotawala dunia nzima na kuwaletea wanadamu watiifu baraka za milele. (Mathayo 4:23) Ujumbe huo ulikuwa wa nani? Yesu mwenyewe alisema hivi: Yale ninayofundisha si yangu, bali ni yake yeye aliyenituma, Yehova. (Yohana 7:16) Yesu alijua kwamba Baba yake anataka wanadamu wasikie habari njema ya Ufalme. Katika Sura ya 8, tutajifunza mengi zaidi kuhusu Ufalme wa Mungu na mambo ambayo utatimiza. 17 Yesu alifundisha wapi? Kila mahali penye watumashambani, majijini, vijijini, sokoni, na nyumbani kwao. Yesu hakungoja watu wamjie. Alienda walipokuwa. (Marko 6:56; Luka 19:5, 6) Kwa nini Yesu alijitahidi sana na kutumia wakati mwingi kuhubiri na kufundisha? Kwa sababu Mungu alitaka afanye hivyo. Sikuzote Yesu alifanya mapenzi ya Baba yake. (Yohana 8:28, 29) Hata hivyo, kulikuwa na sababu nyingine iliyomfanya ahubiri. Aliusikitikia umati wa watu waliokuja kumwona. (Mathayo 9:35, 36) Walikuwa wamepuuzwa na viongozi wao wa kidini ambao walipaswa kuwafundisha kweli kumhusu Mungu na makusudi yake. Yesu alijua kwamba watu hao walitamani sana kusikia ujumbe wa Ufalme.
16. Yesu alifundisha ujumbe gani wa msingi, nayo mafundisho yake yalitoka wapi? 17. Yesu alifundisha wapi, na kwa nini alijitahidi sana kuwafundisha wengine?

Yesu alihubiri kila mahali penye watu


18 Yesu alikuwa mchangamfu na mwenye hisia nyingi. Kwa hiyo watu walimwona kuwa mtu mwenye fadhili na uraki. Hata watoto walifurahia ushirika wake. (Marko 10:13-16) Yesu hakuwa na ubaguzi. Alichukia usadi na ukosefu wa haki. (Mathayo 21:12, 13) Aliwaheshimu wanawake ingawa wakati huo walikuwa wakidharauliwa na kunyimwa haki zao. (Yohana 4:9, 27) Yesu alikuwa mnyenyekevu kikweli. Pindi moja, aliosha miguu ya mitume wake, kazi ambayo kwa kawaida ilifanywa na mtumishi wa hali ya chini. 19 Yesu alihangaikia mahitaji ya wengine. Hilo lilionekana wazi alipoongozwa na nguvu za roho ya Mungu kufanya miujiza ya uponyaji. (Mathayo 14:14) Kwa mfano, mtu fulani aliyekuwa na ukoma alimjia Yesu na kusema: Ikiwa tu unataka, unaweza kunitakasa. Yesu alihisi

18. Ni sifa zipi za Yesu zinazokuvutia sana? 19. Ni mfano gani unaoonyesha kwamba Yesu alihangaikia mahitaji ya wengine?

45

kana kwamba yeye mwenyewe ndiye aliyekuwa akiumia na kuteseka. Alimsikitikia, akaunyoosha mkono wake, akamgusa, na kusema: Ninataka. Takasika. Na mtu huyo aliyekuwa mgonjwa akapona. (Marko 1:40-42) Je, unaweza kuwazia jinsi mtu huyo alivyohisi?

MWAMINIFU MPAKA MWISHO Yesu aliweka mfano bora wa utii mshikamanifu kwa Mungu. Aliendelea kuwa mwaminifu kwa Baba yake wa mbinguni chini ya hali zote na licha ya upinzani na magumu mbalimbali. Yesu alifaulu kupinga kwa uthabiti vishawishi vya Shetani. (Mathayo 4:1-11) Wakati mmoja, baadhi ya watu wa ukoo wa Yesu mwenyewe hawakumwamini, hata walisema kwamba alikuwa amerukwa na akili. (Marko 3:21) Hata hivyo, Yesu hakuwaruhusu wamkengeushe; bali aliendelea kufanya kazi ya Mungu.
20

20, 21. Yesu aliwekaje mfano bora wa utii mshikamanifu kwa Mungu mpaka kifo?

46

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Ijapokuwa alitukanwa na kutendewa vibaya, Yesu alijizuia, hakujaribu kuwadhuru wapinzani wake.1 Petro 2:21-23. 21 Yesu aliendelea kuwa mwaminifu mpaka alipokufa kifo cha kikatili na uchungu mikononi mwa adui zake. (Walipi 2:8) Fikiria mambo aliyovumilia usiku wa mwisho wa maisha yake akiwa mwanadamu. Alikamatwa, akashtakiwa na mashahidi wa uwongo, akahukumiwa na mahakimu wasadi, akachekwa na umati, na kuteswa na askari. Akiwa ametundikwa kwenye mti wa mateso, alivuta pumzi ya mwisho akipaaza sauti: Imetimizwa! (Yohana 19:30) Hata hivyo, siku tatu baada ya Yesu kufa, Baba yake wa mbinguni alimfufua na kumfanya hai katika roho. (1 Petro 3:18) Majuma machache baadaye, alirudi mbinguni. Akiwa huko, aliketi kwenye mkono wa kuume wa Mungu na kungoja apokee mamlaka ya kifalme.Waebrania 10:12, 13. 22 Yesu alitimiza nini kwa kuendelea kuwa mwaminifu mpaka kifo? Kifo cha Yesu kinatuwezesha kupata uzima wa milele katika dunia itakayokuwa paradiso kama vile Yehova alivyokusudia mwanzoni. Sura inayofuata itazungumzia jinsi kifo cha Yesu kinavyotuwezesha kupata uzima.
22. Yesu alitimiza nini kwa kuendelea kuwa mwaminifu mpaka kifo?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA


Utimizo wa unabii na ushuhuda wa Mungu mwenyewe unathibitisha kwamba Yesu ndiye Masihi au Kristo.Mathayo 16:16. Yesu aliishi mbinguni akiwa kiumbe wa roho kabla ya kuja duniani.Yohana 3:13. Yesu alikuwa mwalimu, mtu mchangamfu, na aliweka mfano bora wa kumtii Mungu kikamili.Mathayo 9:35, 36.

SURA YA TANO

FidiaZawadi Bora Zaidi Kutoka kwa Mungu


Fidia ni nini? Ilitolewaje? Ina faida gani kwako? Unaweza kuonyeshaje kwamba unaithamini?
NI ZAWADI gani bora zaidi ambayo umewahi kupokea? Zawadi muhimu si lazima iwe ya bei ghali. Kwa kweli, thamani ya zawadi haitegemei kiasi cha pesa kilichotumiwa kuinunua. Badala yake, zawadi inapokufurahisha au kutimiza mahitaji muhimu, basi ina thamani kubwa kwako. 2 Kati ya zawadi nyingi ambazo ungependa kupokea, kuna moja iliyo bora zaidi kuliko zote. Ni zawadi kutoka kwa Mungu. Yehova ametupatia vitu vingi, lakini zawadi bora zaidi ambayo ametupatia ni dhabihu ya dia ya Mwana wake, Yesu Kristo. (Mathayo 20:28) Kama tutakavyoona katika sura hii, dia ndiyo zawadi bora zaidi ambayo unaweza kupokea kwa sababu inaweza kukuletea furaha isiyo na kifani na kuridhisha sana. Kwa hakika, dia ndiyo wonyesho mkubwa zaidi wa upendo wa Yehova kwako.
3

FIDIA NI NINI? Kwa ufupi, dia ni njia ya Yehova ya kuwakomboa

1, 2. (a) Ni zawadi ya aina gani yenye thamani zaidi kwako? (b) Kwa nini tunaweza kusema kwamba dia ndiyo zawadi yenye thamani kubwa zaidi ambayo unaweza kupokea? 3. Fidia ni nini, na tunahitaji kuelewa nini ili tuione dia kuwa zawadi yenye thamani kubwa?

48

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

au kuwaokoa wanadamu kutokana na dhambi na kifo. (Waefeso 1:7) Ili kuelewa maana ya fundisho hili la Biblia, tunahitaji kukiria mambo yaliyotokea katika bustani ya Edeni. Tukielewa kile ambacho Adamu alipoteza alipofanya dhambi, ndipo tu tunapoweza kujua kwa nini dia ni zawadi yenye thamani kubwa kwetu. 4 Yehova alipomuumba Adamu, alimpa kitu chenye thamani sana, yaani, uhai mkamilifu. Wazia faida ambazo Adamu angepata. Kwa sababu alikuwa na mwili mkamilifu, hangekuwa mgonjwa, hangezeeka, wala kufa. Akiwa mwanadamu mkamilifu, alikuwa na uhusiano wa pekee pamoja na Yehova. Biblia inasema kwamba Adamu alikuwa mwana wa Mungu. (Luka 3:38) Kwa hiyo Adamu alifurahia uhusiano wa karibu pamoja na Yehova Mungu, kama ule wa mwana na baba mwenye upendo. Yehova alizungumza na mwanawe, Adamu, hapa duniani, akampa kazi yenye kuridhisha na kumjulisha mapenzi yake.Mwanzo 1:28-30; 2:16, 17. 5 Adamu aliumbwa kwa mfano wa Mungu. (Mwanzo 1:27) Hilo halimaanishi kwamba Adamu alikuwa na umbo kama la Mungu. Kama tulivyojifunza katika Sura ya 1 ya kitabu hiki, Yehova ni roho asiyeonekana. (Yohana 4:24) Kwa hiyo, Yehova hana mwili wa nyama na damu. Kuumbwa kwa mfano wa Mungu kunamaanisha kwamba Adamu aliumbwa akiwa na sifa kama za Mungu, kutia ndani upendo, hekima, haki, na nguvu. Adamu alikuwa kama Baba yake katika njia nyingine muhimu, alikuwa na uhuru wa kuchagua. Hivyo, Adamu hakuwa kama mashine ambayo inaweza tu kufanya kazi ambayo imepangiwa ifanye. Badala yake, angeweza kujifanyia maa4. Adamu angepata faida gani kwa kuwa na uhai mkamilifu? 5. Biblia inamaanisha nini inaposema kwamba Adamu aliumbwa kwa mfano wa Mungu?

FidiaZawadi Bora Zaidi Kutoka kwa Mungu

49

muzi, na kuchagua kati ya yaliyo sawa na kosa. Kama angechagua kumtii Mungu, angeishi milele katika Paradiso duniani. 6 Basi, ni wazi kwamba Adamu alipokosa kumtii Mungu na akahukumiwa kifo, alileta hasara kubwa sana. Kwa sababu ya dhambi aliyofanya, alipoteza uhai mkamilifu na faida zake zote. (Mwanzo 3:17-19) Inasikitisha kwamba Adamu alipoteza uhai wake mkamilifu pamoja na wa wazao wake. Neno la Mungu linasema: Kupitia mtu mmoja [Adamu] dhambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia dhambi, na hivyo kifo kikaenea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya dhambi. (Waroma 5:12) Ndiyo, sote tumerithi dhambi kutoka kwa Adamu. Kwa hiyo Biblia inasema kwamba alijiuza pamoja na wazao wake katika utumwa wa dhambi na kifo. (Waroma 7:14) Adamu na Hawa hawakuwa na tumaini kwa kuwa walikataa kumtii Mungu kimakusudi. Lakini namna gani wazao wao kutia ndani sisi? 7 Yehova alifanya mpango wa kuwakomboa wanadamu kupitia dia. Fidia ni nini? Fidia inahusisha mambo mawili ya msingi. Kwanza, dia ni bei inayolipwa ili kukomboa au kurudisha kitu. Inaweza kulinganishwa na bei inayolipwa ili kumkomboa mtu aliyetekwa nyara vitani. Pili, dia ni bei inayofunika, au kulipia gharama ya kitu fulani. Ni sawa na bei ambayo mtu hulipa anaposababisha madhara. Kwa mfano, mtu akisababisha msiba, anapaswa kulipa kiasi kinacholingana au kinachotoshana na thamani ya kilichoharibiwa. 8 Hasara kubwa aliyotuletea Adamu ingewezaje kulipwa ili tukombolewe kutoka katika utumwa wa dhambi na
6. Adamu alipoteza nini alipokosa kumtii Mungu, na hilo liliathirije wazao wake? 7, 8. Fidia inahusisha mambo gani mawili ya msingi?

50

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

kifo? Hebu tuzungumzie dia ambayo Yehova aliandaa na jinsi inavyoweza kukufaidi.

JINSI YEHOVA ALIVYOANDAA FIDIA Kwa kuwa uhai mkamilifu wa kibinadamu ulipotea, hakuna mwanadamu yeyote asiye mkamilifu angeweza kuurudisha. (Zaburi 49:7, 8) Kilichohitajiwa ni dia yenye thamani inayolingana na kilichopotezwa. Hilo linapatana na kanuni hii ya haki kamilifu inayopatikana katika Neno la Mungu: Nafsi itakuwa kwa nafsi. (Kumbukumbu la Torati 19:21) Kwa hiyo, ni nini kingeweza kulipia thamani ya nafsi au uhai mkamilifu wa kibinadamu uliopotezwa na Adamu? Kilichohitajiwa ni dia inayolingana ya uhai mwingine mkamilifu wa kibinadamu. 1 Timotheo 2:6. 10 Yehova aliandaaje dia? Alimtuma mmoja kati ya wana wake wakamilifu wa kiroho aje duniani. Lakini Yehova hakutuma kiumbe yeyote tu wa roho. Alimtuma yule aliyempenda sana, Mwana wake mzaliwa-pekee. (1 Yohana 4:9, 10) Mwana huyo alikubali kwa hiari kuacha makao yake mbinguni. (Walipi 2:7) Kama tulivyojifunza katika Sura ya 4 ya kitabu hiki, Yehova alifanya muujiza alipohamisha uhai wa Mwana huyo na kuutia katika tumbo la Maria. Kupitia roho takatifu ya Mungu, Yesu alizaliwa akiwa mwanadamu mkamilifu wala hakuwa chini ya laana ya dhambi.Luka 1:35. 11 Mtu mmoja angewezaje kuwa dia kwa ajili ya watu wengi, mamilioni ya wanadamu? Kwanza, mamilioni hayo ya wanadamu walipataje kuwa wenye dhambi? Kumbuka kwamba kwa kufanya dhambi Adamu alipoteza uhai mka9

9. Ni dia ya aina gani iliyohitajiwa? 10. Yehova aliandaaje dia? 11. Mtu mmoja angewezaje kuwa dia kwa ajili ya mamilioni ya watu?

FidiaZawadi Bora Zaidi Kutoka kwa Mungu

51

milifu wa kibinadamu wenye thamani sana. Kwa hiyo, hangeweza kuwapitishia wazao wake uhai huo mkamilifu. Badala yake aliwapitishia dhambi na kifo tu. Yesu, ambaye Biblia inamwita Adamu wa mwisho, alikuwa na uhai mkamilifu wa kibinadamu wala hakufanya dhambi kamwe. (1 Wakorintho 15:45) Hivyo, Yesu alichukua mahali pa Adamu ili atuokoe. Yesu alilipia dhambi ya Adamu kwa kudhabihu uhai wake mkamilifu na kumtii Mungu kikamili. Hivyo, Yesu akawapa wazao wa Adamu tumaini. Waroma 5:19; 1 Wakorintho 15:21, 22. 12 Biblia inaeleza kinaganaga kuhusu mateso ambayo Yesu alivumilia kabla ya kufa. Alipigwa mijeledi, akatundikwa kikatili, na kufa kwa maumivu makali juu ya mti wa mateso. (Yohana 19:1, 16-18, 30; Nyongeza, ukurasa wa 204-206) Kwa nini ilikuwa lazima Yesu ateseke sana hivyo? Baadaye tutaona kwamba Shetani alitilia shaka ikiwa Yehova ana watumishi wa kibinadamu wanaoweza kumtumikia kwa uaminifu chini ya majaribu. Kwa kuvumilia kwa uaminifu licha ya mateso makali, Yesu alijibu madai ya Shetani kwa njia bora zaidi. Yesu alithibitisha kwamba mwanadamu mkamilifu aliye na uhuru wa kuchagua anaweza kumtii Mungu kikamili hata Ibilisi afanye nini. Haikosi kwamba Yehova alifurahishwa sana na uaminifu wa Mwana wake mpendwa!Methali 27:11. 13 Fidia ililipwaje? Mungu aliruhusu Mwana wake mkamilifu asiye na dhambi auawe katika siku ya 14 ya mwezi wa Kiyahudi unaoitwa Nisani, mwaka wa 33 W.K. Hivyo, Yesu alidhabihu uhai wake mkamilifu wa kibinadamu mara moja kwa wakati wote. (Waebrania 10:10) Siku ya tatu baada ya Yesu kufa, Yehova alimfufua na kumrudisha kwenye uhai wa roho. Akiwa mbinguni, Yesu alimpa
12. Kuteseka kwa Yesu kulithibitisha nini? 13. Fidia ililipwaje?

Yehova alimtoa Mwana wake mzaliwa-pekee awe dia kwa ajili yetu

FidiaZawadi Bora Zaidi Kutoka kwa Mungu

53

Mungu thamani ya uhai wake mkamilifu wa kibinadamu uliotolewa dhabihu kama dia kwa ajili ya wazao wa Adamu. (Waebrania 9:24) Yehova alikubali thamani ya dhabihu ya Yesu kama dia ya kuwakomboa wanadamu kutoka katika utumwa wa dhambi na kifo.Waroma 3:23, 24.

JINSI FIDIA INAVYOWEZA KUKUFAIDI Licha ya hali yetu yenye dhambi, tunaweza kupata baraka nyingi sana kwa sababu ya dia. Na tuzungumzie baadhi ya faida tunazopata sasa na tutakazopata wakati ujao kwa sababu ya zawadi hiyo kubwa zaidi kutoka kwa Mungu. 15 Msamaha wa dhambi. Kwa sababu tumerithi kutokamilika, si rahisi kufanya yaliyo sawa. Sisi sote hufanya dhambi kwa maneno au kwa matendo. Lakini kupitia dhabihu ya dia ya Yesu, tunaweza kusamehewa dhambi zetu. (Wakolosai 1:13, 14) Hata hivyo, ili kupata msamaha ni lazima tutubu kikweli. Ni lazima pia tumsihi Yehova kwa unyenyekevu na kumwomba msamaha kwa msingi wa imani yetu katika dhabihu ya dia ya Mwana wake. 1 Yohana 1:8, 9. 16 Kuwa na dhamiri sa mbele za Mungu. Dhamiri yenye hatia inaweza kutufanya tukate tamaa na kuhisi hatufai. Lakini kwa sababu ya msamaha tunaopata kupitia dia, kwa fadhili Yehova anatuwezesha tumwabudu tukiwa na dhamiri sa licha ya kutokamilika kwetu. (Waebrania 9:13, 14) Hilo linatuwezesha kusema na Yehova tukiwa na uhuru. Kwa hiyo, tunaweza kumkaribia kwa uhuru katika sala. (Waebrania 4:14-16) Kudumisha dhamiri sa kunatuwezesha kuwa na amani ya akili, kujistahi, na kuwa na furaha.
14

14, 15. Tunapaswa kufanya nini ili kusamehewa dhambi zetu? 16. Ni nini hutuwezesha kumwabudu Mungu tukiwa na dhamiri sa, na dhamiri hiyo ina faida gani?

Njia moja ya kuonyesha kwamba unathamini zawadi ya dia ni kujifunza mengi zaidi kumhusu Yehova

17 Tumaini la uzima wa milele katika paradiso duniani. Andiko la Waroma 6:23 linasema: Mshahara ambao dhambi hulipa ni kifo, lakini zawadi ambayo Mungu hutoa ni uzima wa milele kupitia Kristo Yesu Bwana wetu. Katika Sura ya 3 ya kitabu hiki, tulizungumzia baraka zitakazokuwapo katika dunia itakayokuwa Paradiso wakati ujao. (Ufunuo 21:3, 4) Watu wataweza kupata baraka hizo zote za wakati ujao, kutia ndani uzima wa milele na afya kamilifu kwa sababu Yesu alikufa kwa ajili yetu. Ili tupokee baraka hizo, tunahitaji kuonyesha kwamba tunathamini zawadi ya dia.

UNAWEZA KUONYESHAJE KWAMBA UNATHAMINI FIDIA? 18 Kwa nini tunapaswa kumshukuru Yehova kwa dia? Zawadi huwa yenye thamani hasa ikiwa mtoaji ametumia wakati, jitihada, au gharama. Mioyo yetu huchochewa tunapopata zawadi kutoka kwa mtu anayetupenda kikweli. Fidia ndiyo zawadi bora zaidi, kwa sababu Mungu
17. Kwa kuwa Yesu alikufa kwa ajili yetu, tunaweza kupata baraka gani? 18. Kwa nini tunapaswa kumshukuru Yehova kwa zawadi ya dia?

FidiaZawadi Bora Zaidi Kutoka kwa Mungu

55

alijidhabihu kwa njia kubwa sana ili kuiandaa. Andiko la Yohana 3:16 lasema: Mungu aliupenda ulimwengu sana hivi kwamba akamtoa Mwana wake mzaliwa-pekee. Fidia ni uthibitisho wa pekee sana wa upendo wa Yehova kwetu. Pia, inaonyesha upendo wa Yesu kwa kuwa alikubali kutoa uhai wake kwa ajili yetu. (Yohana 15:13) Kwa hiyo, zawadi ya dia inapaswa kutusadikisha kwamba Yehova na Mwana wake wanampenda kila mmoja wetu.Wagalatia 2:20. 19 Unaweza kuonyeshaje kwamba unathamini zawadi ya Mungu ya dia? Kwanza, jifunze mengi kumhusu Mpaji huyo Mkuu, Yehova. (Yohana 17:3) Kujifunza Biblia kwa kutumia kitabu hiki kutakusaidia kumjua zaidi. Kadiri unavyozidi kumjua Yehova, ndivyo upendo wako unavyozidi kuongezeka. Kisha, upendo huo utakufanya utake kumpendeza.1 Yohana 5:3. 20 Onyesha kwamba una imani katika dhabihu ya dia ya Yesu. Yesu alisema: Yule anayemwamini Mwana ana uzima wa milele. (Yohana 3:36) Tunaweza kuonyeshaje kwamba tunamwamini Yesu? Imani ya aina hiyo haionyeshwi kwa maneno tu. Andiko la Yakobo 2:26 linasema: Imani bila matendo imekufa. Ndiyo, imani ya kweli inathibitishwa kwa matendo, yaani, jinsi tunavyojiendesha. Tunaweza kuonyesha kwamba tunamwamini Yesu kwa kujitahidi sana kumwiga kwa maneno na matendo.Yohana 13:15. 21 Hudhuria mwadhimisho wa kila mwaka wa Mlo wa Jioni wa Bwana. Jioni ya Nisani 14, 33 W.K., Yesu alianzisha mwadhimisho ambao katika Biblia unaitwa mlo wa jioni wa Bwana. (1 Wakorintho 11:20; Mathayo 26:26-28) Mwadhimisho huo pia huitwa Ukumbusho wa kifo cha Yesu.
19, 20. Unaweza kuonyeshaje kwamba unathamini zawadi ya Mungu ya dia? 21, 22. (a) Kwa nini tunapaswa kuhudhuria Mlo wa Jioni wa Bwana wa kila mwaka? (b) Ni nini kitakachozungumziwa katika Sura ya 6 na 7?

56

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Yesu aliuanzisha ili kuwasaidia mitume wake na Wakristo wote wa kweli kuzingatia akilini kwamba kupitia kifo chake akiwa mwanadamu mkamilifu, alitoa nafsi yake au uhai wake uwe dia. Yesu aliagiza hivi kuhusu mwadhimisho huo: Endeleeni kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi. (Luka 22:19) Kuadhimisha Ukumbusho hutukumbusha upendo ulioonyeshwa na Yehova na Yesu kuhusiana na dia. Tunaweza kuonyesha kwamba tunathamini dia kwa kuhudhuria mwadhimisho wa kila mwaka wa Ukumbusho wa kifo cha Yesu.1 22 Kwa kweli, dia iliyotolewa na Yehova ni zawadi yenye thamani sana. (2 Wakorintho 9:14, 15) Zawadi hiyo yenye thamani inaweza kuwafaidi hata wale ambao wamekufa. Habari hiyo itazungumziwa katika Sura ya 6 na ya 7.
1 Unaweza kupata habari zaidi kuhusu maana ya Mlo wa Jioni wa Bwana katika Nyongeza, ukurasa wa 206-208.

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA Fidia ni njia ya Yehova ya kuwakomboa wanadamu kutoka katika dhambi na kifo. Waefeso 1:7. Yehova aliandaa dia kwa kumtuma Mwana wake mzaliwa-pekee aje duniani ili afe kwa ajili yetu.1 Yohana 4:9, 10. Fidia inatuwezesha kupata msamaha wa dhambi, dhamiri sa, na tumaini la uzima wa milele.1 Yohana 1:8, 9. Tunaonyesha kwamba tunathamini dia kwa kujifunza mengi zaidi kumhusu Yehova, kuwa na imani katika dhabihu ya dia ya Yesu, na kuhudhuria Mlo wa Jioni wa Bwana.Yohana 3:16.

SURA YA SITA

Wafu Wako Wapi?


Inakuwaje tunapokufa? Kwa nini tunakufa? Je, ingefariji kujua ukweli kuhusu kifo?
WATU wameuliza maswali haya kwa maelfu ya miaka. Ni maswali muhimu. Hata tuwe nani au tunaishi wapi, tungependa kupata majibu ya maswali hayo. 2 Katika Sura ya 5, tulizungumzia jinsi dhabihu ya dia ya Yesu Kristo ilivyofungua njia ya kupata uzima wa milele. Pia tulijifunza kwamba Biblia inatabiri kuhusu wakati ambapo kifo hakitakuwapo tena. (Ufunuo 21:4) Kwa sasa, sisi sote tunakufa. Mfalme Sulemani mwenye hekima alisema: Walio hai wanajua kwamba watakufa. (Mhubiri 9:5) Sisi hujitahidi kuishi muda mrefu iwezekanavyo. Hata hivyo, tungependa kujua ni nini hutupata tunapokufa. 3 Sisi huomboleza wapendwa wetu wanapokufa. Huenda tukauliza: Wameenda wapi? Je, wanateseka? Je, wanaweza kutusaidia? Je, tunaweza kuwasaidia? Je, tutawaona tena? Dini za ulimwengu hujibu maswali haya kwa njia tofauti-tofauti. Baadhi ya dini hizo hufundisha kwamba ukiishi maisha ya uadilifu, utaenda mbinguni lakini ikiwa unaishi maisha mabaya, utateketezwa motoni. Dini nyingine hufundisha kwamba watu wanapokufa huenda kuishi katika makao ya roho pamoja na mababu zao. Na nyingine hufundisha kwamba wafu huenda
1-3. Watu huuliza maswali gani kuhusu kifo, na dini mbalimbali huyajibuje?

58

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

ahera wakahukumiwe kisha huzaliwa upya katika mwili mwingine. 4 Dini zote hizo zinafundisha jambo moja la msingi, kwamba sehemu fulani ya mwanadamu huendelea kuishi baada ya mwili kufa. Karibu kila dini, za zamani na za sasa, husema kwamba sisi huendelea kuishi milele tukiwa na uwezo wa kuona, kusikia, na kukiri. Hata hivyo, hilo linawezekanaje? Hisia zetu, pamoja na mawazo yetu, zinahusiana na jinsi ubongo wetu unavyofanya kazi. Ubongo huacha kufanya kazi mtu anapokufa. Kumbukumbu letu na hisia zetu haziendelei kufanya kazi baada ya ubongo kufa.

INAKUWAJE MTU ANAPOKUFA? Yehova, Muumba wa ubongo anajua kinachotukia tunapokufa. Anajua ukweli na katika Neno lake, Biblia, anaeleza hali ya wafu. Biblia inafundisha hivi waziwazi: Mtu anapokufa, hayupo tena. Kifo ni kinyume cha uhai. Wafu hawaoni, hawasikii wala kukiri. Hakuna sehemu yoyote ya mwili wetu inayoendelea kuishi baada ya mwili kufa. Hatuna nafsi au roho isiyoweza kufa.1 6 Baada ya Sulemani kutaja kwamba walio hai wanajua kwamba watakufa, aliandika hivi: Lakini wafu, hawajui lolote kamwe. Kisha akafafanua kweli hiyo ya msingi kwa kusema kwamba wafu hawawezi kupenda wala kuchukia na kwamba hakuna kazi, wala utungaji wala ujuzi wala hekima katika Kaburi. (Mhubiri 9: 5, 6, 10) Vivyo hivyo, andiko la Zaburi 146:4 linasema kwamba mtu anapokufa, mawazo yake hupotea.
5

1 Unaweza kupata habari zaidi kuhusu nafsi na roho katika Nyongeza, ukurasa wa 208-211.
4. Dini nyingi hufundisha jambo gani la msingi kuhusu kifo? 5, 6. Biblia hufundisha nini kuhusu hali ya wafu?

Wafu Wako Wapi?

Sisi hufa wala hatuendelei kuishi baada ya mwili kufa. Maisha yetu ni kama moto. Unapozimika, hauendi popote. Haupo tena.

MAMBO AMBAYO YESU ALIFUNDISHA KUHUSU KIFO 7 Yesu Kristo alizungumzia hali ya wafu raki yake Lazaro alipokufa. Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Lazaro raki yetu anapumzika. Wanafunzi walikiri Yesu anamaanisha kwamba Lazaro anapumzika katika usingizi kwa sababu ni mgonjwa. Walikosea. Yesu akawaambia: Lazaro amekufa. (Yohana 11: 11-14) Ona kwamba Yesu alifananisha Moto huenda wapi kifo na pumziko au usingizi. Lazaro haunapozimika? kuwa mbinguni wala motoni. Hakuwa akikutana na malaika wala mababu. Wala hakuwa akibadilika ili azaliwe tena akiwa mwanadamu mwingine. Alikuwa akipumzika katika kifo kana kwamba analala usingizi mzito usio na ndoto. Maandiko mengine pia hulinganisha kifo na usingizi. Kwa mfano, mwanafunzi Stefano alipouawa kwa kupigwa mawe, Biblia inasema kwamba alilala usingizi. (Matendo 7:60) Hali kadhalika, mtume Paulo aliwataja watu fulani katika siku zake ambao walikuwa wamelala usingizi katika kifo.1 Wakorintho 15:6. 8 Je, Mungu alikusudia watu wafe? Hapana! Yehova alimuumba mwanadamu aishi milele duniani. Kama tulivyojifunza mwanzoni mwa kitabu hiki, Mungu aliwaweka wanadamu wawili wa kwanza katika paradiso yenye
7. Yesu alifafanuaje kifo? 8. Tunajuaje kwamba Mungu hakukusudia watu wafe?

60

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

kupendeza. Aliwapa afya kamilifu. Yehova aliwatakia mema. Je, kuna mzazi yeyote mwenye upendo anayetaka watoto wake wateseke kwa sababu ya uzee na kifo? Bila shaka hakuna! Yehova aliwapenda watoto wake na alitaka waishi milele kwa furaha duniani. Biblia inasema hivi kuwahusu wanadamu: Wakati usio na kipimo [Yehova] ameuweka ndani ya moyo wao. (Mhubiri 3:11) Mungu alituumba tukiwa na tamaa ya kuishi milele. Naye amepanga jinsi tamaa hiyo itakavyotimizwa.
Yehova aliwaumba wanadamu waishi milele duniani

Wafu Wako Wapi?

61

KWA NINI WANADAMU HUFA? Kwa nini basi wanadamu hufa? Ili kupata jibu, lazima tuzingatie kilichotukia kulipokuwa na mwanamume na mwanamke mmoja tu duniani. Biblia inaeleza: Yehova Mungu akachipusha katika nchi kila mti wenye kutamanika kwa macho ya mtu na ulio mwema kwa ajili ya chakula. (Mwanzo 2:9) Hata hivyo, alikatazwa kufanya jambo moja. Yehova alimwambia Adamu hivi: Matunda ya kila mti wa bustani unaweza kula mpaka ushibe. Lakini kuhusu matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula, utakufa hakika. (Mwanzo 2:16, 17) Haikuwa vigumu kutii amri hiyo. Kulikuwa na miti mingine mingi ambayo Adamu na Hawa wangekula matunda yake. Lakini amri hiyo iliwapa nafasi ya pekee ya kuonyesha shukrani kwa Yule aliyewapa kila kitu, kutia ndani uhai mkamilifu. Utii wao ungeonyesha pia kwamba waliheshimu mamlaka ya Baba yao wa mbinguni na kwamba walitaka mwongozo wake wenye upendo. 10 Inasikitisha kwamba wenzi hao wa kwanza wa kibinadamu waliamua kutomtii Yehova. Akiongea kupitia nyoka, Shetani alimuuliza Hawa hivi: Je, ni kweli kwamba Mungu alisema msile matunda ya kila mti wa bustani? Hawa akamjibu: Tunaweza kula matunda ya miti ya bustani. Lakini kuhusu kula matunda ya mti ulio katikati ya bustani, Mungu amesema, Msiyale, wala msiyaguse ili msife. Mwanzo 3:1-3. 11 Shetani akamwambia: Hakika hamtakufa. Mungu anajua kwamba siku ileile mtakapokula matunda yake macho yenu yatafunguliwa, nanyi mtakuwa kama
9

9. Yehova alimkataza Adamu kufanya nini, na kwa nini haikuwa vigumu kutii amri hiyo? 10, 11. (a) Wenzi wa kwanza wa kibinadamu walikosaje kumtii Mungu? (b) Kwa nini kutotii kwa Adamu na Hawa kulikuwa jambo zito?

62

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Mungu, mkijua mema na mabaya. (Mwanzo 3:4, 5) Shetani alitaka Hawa aamini kwamba angefaidika kwa kula tunda lililokatazwa. Kulingana na Shetani, Hawa angeweza kujiamulia lililo sawa na lililo kosa; angefanya atakalo. Shetani pia alidai kwamba Yehova alikuwa amesema uwongo kuhusu matokeo ya kula tunda. Hawa alimwamini Shetani. Kwa hiyo alichukua tunda hilo akala. Kisha akampa mumewe, naye pia akala. Hawakufanya hivyo kwa kutojua. Walijua kwamba walikuwa wakifanya kile ambacho Mungu aliwaambia wasifanye. Kwa kula tunda hilo, walikosa kutii kimakusudi amri rahisi na isiyodai mengi. Walimdharau Baba yao wa mbinguni na mamlaka yake. Hawakuwa na sababu ya kutomheshimu Muumba wao mwenye upendo!
Adamu alitoka mavumbini, naye alirudi mavumbini

Wafu Wako Wapi?


12

63

Kwa mfano: Ungehisije kama ungemlea na kumtunza mwana au binti ambaye angekataa kukutii na hivyo kuonyesha kwamba hakuheshimu wala hakupendi? Ungehisi uchungu moyoni. Wazia uchungu ambao Yehova alihisi wakati Adamu na Hawa walipomwasi. 13 Yehova hakuwa na sababu ya kuwaacha Adamu na Hawa wasiomtii waendelee kuishi milele. Walikufa kama Yehova alivyokuwa amesema. Adamu na Hawa wakakoma kuwapo. Hawakuendelea kuishi mahali pengine wakiwa viumbe wa roho. Tunajua hivyo kwa sababu ya yale ambayo Yehova alimwambia Adamu baada ya kuzungumza naye kuhusu uasi wake. Mungu alisema: Utarudi katika udongo, kwa kuwa ulitolewa katika huo. Kwa maana wewe ni mavumbi nawe utarudi mavumbini. (Mwanzo 3:19) Mungu alimuumba Adamu kutokana na mavumbi ya nchi. (Mwanzo 2:7) Kabla ya kuumbwa, Adamu hakuwapo. Kwa hiyo, Yehova aliposema kwamba Adamu angerudi mavumbini, alimaanisha kwamba Adamu hangekuwapo tena. Adamu hangekuwa na uhai kama vile mavumbi yaliyotumiwa kumuumba yasivyo na uhai. 14 Adamu na Hawa wangekuwa hai leo, lakini walikufa kwa sababu waliamua kutomtii Mungu na hivyo wakafanya dhambi. Tunakufa kwa sababu wazao wote wa Adamu wamerithi dhambi na kifo kutoka kwake. (Waroma 5:12) Dhambi hiyo ni kama ugonjwa mbaya sana uliorithiwa, ambao hakuna anayeweza kuuepuka. Kifo kinachosababishwa na dhambi ni laana. Kifo ni adui wala si raki. (1 Wakorintho 15:26) Tunapaswa kumshukuru Yehova sana kwa sababu ameandaa dia ili kutuokoa kutokana na adui huyu mwenye kutisha!
12. Ni nini kinachoweza kutusaidia kuelewa jinsi Yehova alivyohisi wakati Adamu na Hawa walipomwasi? 13. Yehova alisema ingekuwaje kwa Adamu wakati wa kifo, na hilo linamaanisha nini? 14. Kwa nini tunakufa?

64

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

KUNA FAIDA KUJUA UKWELI KUHUSU KIFO Mambo ambayo Biblia inafundisha kuhusu hali ya wafu yanafariji. Kama ambavyo tumeona, wafu hawahisi maumivu wala uchungu. Hatuna sababu ya kuwaogopa wafu kwani hawawezi kutuumiza. Hawahitaji msaada wetu wala hawawezi kutusaidia. Hatuwezi kuzungumza nao. Viongozi wengi wa kidini hudai kwamba wanaweza kuwasaidia wafu, na watu wanaowaamini huwapa pesa. Lakini kujua ukweli kuhusu hali ya wafu hutulinda tusidanganywe na wale wanaofundisha uwongo. 16 Je, dini nyingi hukubali mafundisho ya Biblia kuhusu hali ya wafu? Nyingi hazikubali. Kwa nini? Kwa sababu mafundisho yao yanaongozwa na Shetani. Anatumia dini ya uwongo ili kuwafanya watu waamini kwamba baada ya miili yao kufa, wataendelea kuishi katika makao ya roho. Huo ni uwongo ambao Shetani anatumia pamoja na mambo mengine ya uwongo ili kuwafanya watu wamwache Yehova Mungu. Anafanyaje hivyo? 17 Kama tulivyoona, dini fulani hufundisha kwamba mtu akiishi maisha mabaya, baada ya kifo ataenda motoni ili ateseke milele. Fundisho hilo halimletei Mungu heshima. Yehova ni Mungu mwenye upendo na hawezi kamwe kuwatesa watu hivyo. (1 Yohana 4:8) Wewe ungeonaje ikiwa mtu angemtia nidhamu mtoto asiyetii kwa kuishikilia mikono yake motoni ili aungue? Je, unaweza kumheshimu mtu huyo? Je, kweli hata ungetaka kumjua? Hapana hata kidogo! Inaelekea utamwona kuwa mkatili sana. Shetani anataka tuamini kwamba Yehova huwatesa watu motoni milelekwa mabilioni ya miaka!
15

15. Kwa nini inafariji kujua ukweli kuhusu hali ya wafu? 16. Ni nani anayeongoza mafundisho ya dini nyingi, na kwa njia gani? 17. Kwa nini fundisho la mateso ya milele halimletei Yehova heshima?

Wafu Wako Wapi?


18

65

Pia Shetani hutumia dini fulani kufundisha kwamba baada ya watu kufa wao wanakuwa viumbe wa roho ambao wanapaswa kuheshimiwa na walio hai. Kulingana na fundisho hilo, roho za wafu zinaweza kuwa raki wazuri au adui wenye kuogopesha. Watu wengi wanaamini uwongo huo. Wanawaogopa wafu, wanawaheshimu, na kuwaabudu. Kinyume cha hilo, Biblia inafundisha kwamba wafu wanalala na kwamba tunapaswa kumwabudu tu Mungu wa kweli, Yehova, Mpaji na Muumba wetu.Ufunuo 4:11. 19 Kujua ukweli kuhusu wafu hukulinda usidanganywe na uwongo wa dini. Pia hukusaidia kuelewa mafundisho mengine ya Biblia. Kwa mfano, unapojua kwamba watu wanapokufa hawaendi katika makao ya roho, ahadi ya uzima wa milele katika paradiso duniani inakuwa na maana zaidi kwako. 20 Zamani, mwanamume mwadilifu Ayubu, aliuliza swali hili: Mtu akifa, je, anaweza kuishi tena? (Ayubu 14:14) Je, mtu asiye na uhai anayelala usingizi katika kifo anaweza kufufuliwa? Biblia inafundisha jambo lenye kufariji sana kama tutakavyoona katika sura inayofuata.
18. Kuwaabudu wafu kunategemea uwongo gani wa dini? 19. Kujua ukweli kuhusu kifo hukusaidia kuelewa fundisho gani lingine la Biblia? 20. Tutazungumzia swali gani katika sura inayofuata?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA Wafu hawaoni, hawasikii wala kukiri. Mhubiri 9:5. Wafu wanapumzika; hawateseki.Yohana 11:11. Tunakufa kwa sababu tulirithi dhambi kutoka kwa Adamu.Waroma 5:12.

SURA YA SABA

Tumaini Hakika kwa Wapendwa Wako Ambao Wamekufa


Tunajuaje kwamba kutakuwa na ufufuo? Yehova anahisije kuhusu kuwafufua wafu? Ni nani watakaofufuliwa?
WAZIA kwamba unamkimbia adui mkatili. Anakushinda kwa nguvu na mbio. Unajua kwamba hana huruma kwa sababu umemwona akiwaua baadhi ya raki zako. Kadiri unavyokimbia ndivyo anavyozidi kukukaribia. Yaonekana hakuna tumaini. Hata hivyo, kwa ghafula, mtu fulani anatokea ili kukuokoa. Ana nguvu nyingi zaidi kuliko adui yako, naye anaahidi kukusaidia. Ni jambo lenye kufariji kama nini! 2 Kwa njia fulani, wewe unakimbizwa na adui wa aina hiyo. Sisi sote tunakimbizwa naye. Kama tulivyojifunza katika sura iliyotangulia, Biblia inasema kifo ni adui. Hakuna yeyote anayeweza kukishinda. Wengi wetu tumemwona adui huyo akiwaua watu tunaowapenda. Lakini Yehova ana nguvu nyingi zaidi kuliko kifo. Yeye ndiye Mwokoaji mwenye upendo na tayari ameonyesha kwamba anaweza kumshinda adui huyo. Naye anaahidi kwamba atamharibu kabisa adui huyo, yaani, kifo. Biblia inafundisha hivi: Adui wa mwisho atakayeangamizwa ni kifo. (1 Wakorintho 15:26) Hiyo ni habari njema! 3 Kwanza, tutazungumzia matokeo ya kifo. Kufanya hivyo kutatusaidia kuthamini tumaini fulani lenye kupendeza. Yehova anaahidi kwamba wafu wataishi tena. (Isaya
1-3. Ni adui gani anayetukimbiza sisi sote, na kwa nini kujifunza mambo ambayo Biblia inafundisha kutatufariji?

Tumaini Hakika kwa Wapendwa Wako Ambao Wamekufa

67

26:19) Watarudishwa kwenye uhai tena. Hilo ndilo tumaini la ufufuo.

MPENDWA WETU ANAPOKUFA


Je, umewahi kuwa? Huenda ukalemewa na uchungu, huzuni, na kuhisi kwamba huna la kufanya. Nyakati kama hizo tunahitaji kutafuta faraja katika Neno la Mungu. (2 Wakorintho 1:3, 4) Biblia hutusaidia kuelewa jinsi Yehova na Yesu wanavyohisi kuhusu kifo. Yesu aliyekuwa na hisia kama za Baba yake, alielewa uchungu wa kuwa. (Yohana 14:9) Yesu alipokuwa Yerusalemu, alikuwa akimtembelea Lazaro na dada zake, Maria na Martha, ambao waliishi katika mji wa Bethania uliokuwa karibu. Wakawa maraki wakubwa. Biblia inasema: Yesu alimpenda Martha na dada yake na Lazaro. (Yohana 11:5) Hata hivyo, kama tulivyojifunza katika sura iliyotangulia, Lazaro alikufa. 5 Yesu alihisije raki yake alipokufa? Masimulizi hayo yanaonyesha kwamba Yesu aliungana na familia na raki za Lazaro walipokuwa wakimwombolezea. Yesu alipowaona, alilemewa na hisia. Akaugua rohoni na kutaabika. Kisha masimulizi hayo yanaendelea kusema kwamba Yesu alitokwa na machozi. (Yohana 11:33, 35) Je, huzuni ya Yesu ilimaanisha kwamba hakuwa na tumaini? Hapana. Yesu alijua kwamba jambo la kupendeza lilikuwa karibu kutukia. (Yohana 11:3, 4) Hata hivyo, alihisi uchungu na huzuni ambayo hutokana na kifo. 6 Kwa njia fulani, huzuni ya Yesu inatutia moyo. Inatufundisha kwamba Yesu na Baba yake Yehova, wanachukia kifo. Lakini Yehova Mungu anaweza kumpiga na kumshinda adui huyo! Na tuone kile ambacho Mungu alimwezesha Yesu kufanya.
4

4. (a) Hisia za Yesu mtu anapokufa zinatusaidiaje kuelewa hisia za Yehova kuhusu kifo? (b) Yesu alikuwa na maraki gani wa pekee? 5, 6. (a) Yesu alitendaje alipokuwa na familia na raki za Lazaro waliokuwa wakiomboleza? (b) Kwa nini huzuni ya Yesu inatutia moyo?

68

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

LAZARO, NJOO HUKU NJE!


Lazaro alikuwa amezikwa pangoni, naye Yesu aliamuru jiwe lililokuwa kwenye mwingilio wa pango liondolewe. Martha alipinga kwa kuwa siku nne zilikuwa zimepita, na haikosi mwili wa Lazaro ulikuwa umeanza kuoza. (Yohana 11:39) Kwa maoni ya mwanadamu, hakukuwa na tumaini lolote. 8 Jiwe likaondolewa na Yesu akapaaza sauti: Lazaro, njoo huku nje! Ikawaje? Huyo mtu aliyekuwa mfu akatoka. (Yohana 11:43, 44) Je, unaweza kuwazia shangwe ya watu waliokuwapo? Iwe Lazaro alikuwa ndugu yao, mtu wa ukoo, au jirani yao, walijua kwamba alikuwa amekufa. Hata hivyo, mtu yuleyule waliyempenda, sasa alikuwa amesimama kati yao. Huenda hilo lilionekana kuwa jambo lisilowezekana. Bila shaka wengi wao walimkumbatia Lazaro kwa shangwe. Huo ulikuwa ushindi ulioje juu ya kifo! 9 Yesu hakudai kwamba alifanya muujiza huo wenye kustaajabisha kwa nguvu zake. Katika sala aliyotoa kabla ya kumwita Lazaro, Yesu alionyesha waziwazi kwamba Yehova ndiye Chanzo cha nguvu alizotumia. (Yohana 11:41, 42) Hiyo haikuwa mara ya kwanza kwa Yehova kutumia nguvu zake kwa njia hiyo. Ufufuo wa Lazaro ni mmoja tu kati ya miujiza tisa ya ufufuo iliyorekodiwa katika Neno la Mungu.1 Inafurahisha kusoma na kujifunza masimulizi hayo. Yanatufundisha kwamba Mungu hana ubaguzi, kwa kuwa waliofufuliwa walitia ndani watoto kwa watu wazima, wanaume kwa wanawake, Waisraeli na watu wasio Waisraeli. Na ni shangwe iliyoje inayotajwa katika masimulizi hayo! Kwa mfano,
7

1 Masimulizi mengine yako katika 1 Wafalme 17:17-24; 2 Wafalme 4:32-37; 13:20, 21; Mathayo 28:5-7; Luka 7:11-17; 8:40-56; Matendo 9: 36-42; na 20:7-12.
7, 8. Kwa nini huenda watu hawakukiri kwamba Lazaro angeweza kuishi tena, hata hivyo Yesu alifanya nini? 9, 10. (a) Yesu alionyeshaje Chanzo cha nguvu alizotumia kumfufua Lazaro? (b) Kusoma masimulizi ya Biblia kuhusu ufufuo kuna faida gani?

Eliya alimfufua mwana wa mjane.1 Wafalme 17:17-24

Mtume Petro alimfufua mwanamke Mkristo aliyeitwa Dorkasi. Matendo 9:36-42

Ufufuo wa Lazaro ulitokeza shangwe kubwa. Yohana 11:38-44

70

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Yesu alipomfufua msichana mdogo, wazazi wake walikuwa na shangwe kubwa. (Marko 5:42) Kwa kweli, Yehova alikuwa amewapa sababu ya kushangilia ambayo hawangesahau kamwe. 10 Bila shaka, watu waliofufuliwa na Yesu walikufa tena. Je, hilo linamaanisha kwamba hakukuwa na maana yoyote ya kuwafufua? Hapana. Masimulizi hayo ya Biblia yanathibitisha kweli muhimu na yanatupa tumaini.

MAMBO TUNAYOJIFUNZA KUTOKANA NA MASIMULIZI YA UFUFUO


11 Biblia inafundisha kwamba wafu hawajui lolote kamwe. Hawako hai wala hawaendelei kuishi mahali pengine. Masimulizi kuhusu Lazaro yanathibitisha jambo hilo. Alipofufuliwa, je, Lazaro aliwasisimua watu kwa kuwaeleza mambo aliyoona mbinguni? Au je, aliwaogopesha kwa kuwasimulia mambo yenye kutisha kuhusu moto wa mateso? Hapana. Biblia haisemi kwamba Lazaro alisema mambo hayo. Kwa siku nne alizokuwa amekufa hakujua lolote kamwe. (Mhubiri 9:5) Lazaro alikuwa amelala usingizi katika kifo.Yohana 11:11. 12 Masimulizi kuhusu Lazaro yanatufundisha pia kwamba ufufuo ni jambo halisi, wala si hadithi tu. Yesu alimfufua Lazaro mbele ya watazamaji wengi. Hata viongozi wa kidini ambao walimchukia Yesu hawakupinga kwamba muujiza huo haukutukia. Badala yake, walisema: Tufanye nini, kwa sababu mtu huyu [Yesu] anafanya ishara nyingi? (Yohana 11:47) Watu wengi walienda kumwona mtu huyo aliyekuwa amefufuliwa. Kwa hiyo, wengi zaidi wakamwamini Yesu. Kufufuliwa kwa Lazaro kuliwathibitishia kwamba Yesu alikuwa ametumwa na Mungu. Huo ulikuwa uthibitisho

11. Masimulizi kuhusu ufufuo wa Lazaro yanathibitishaje ukweli wa Mhubiri 9:5? 12. Kwa nini tunaweza kuwa na hakika kwamba kwa kweli Lazaro alifufuliwa?

Tumaini Hakika kwa Wapendwa Wako Ambao Wamekufa

71

wenye nguvu sana hata viongozi fulani wa dini ya Kiyahudi wenye mioyo migumu wakapanga njama ya kumuua Yesu na Lazaro.Yohana 11:53; 12:9-11. 13 Je, kuamini kwamba watu wanaweza kufufuliwa ni ndoto tu? Hapana, kwa kuwa Yesu alifundisha kwamba siku moja wale wote waliomo ndani ya makaburi watafufuliwa. (Yohana 5:28) Yehova ndiye Chanzo cha uhai wote. Basi, si vigumu kuamini kwamba anaweza kuurudisha uhai tena. Ni kweli kwamba Yehova atawafufua wafu walio katika kumbukumbu lake. Je, anaweza kuwakumbuka wapendwa wetu waliokufa? Kuna nyota zisizo na hesabu angani, lakini Mungu huziita zote kwa majina! (Isaya 40:26) Kwa hiyo, Yehova Mungu anaweza kukumbuka habari zote kuhusu wapendwa wetu waliokufa, naye ana uwezo wa kuwafufua. 14 Hata hivyo, Yehova anahisije kuhusu kufufua wafu? Biblia inafundisha kwamba anatamani kuwafufua. Mwanamume mwaminifu Ayubu aliuliza hivi: Mtu akifa, je, anaweza kuishi tena? Ayubu alikuwa akizungumzia kuhusu kungoja kaburini mpaka wakati ambapo Mungu angemkumbuka. Alimwambia Yehova: Utaita, na mimi mwenyewe nitakujibu. Kwa kuwa utaitamani sana kazi ya mikono yako.Ayubu 14:13-15. 15 Hebu kiria! Yehova anatamani sana kuwafufua wafu. Je, haichangamshi kujua kwamba Yehova anahisi hivyo? Lakini ufufuo wa wakati huo utakuwaje? Ni nani watakaofufuliwa, nao watakuwa wapi?

WOTE WALIOMO NDANI YA MAKABURI YA UKUMBUSHO


16

Masimulizi ya Biblia kuhusu ufufuo hutufundisha

13. Kwa nini tunaweza kuamini kwamba kwa kweli Yehova atawafufua wafu? 14, 15. Kama Ayubu alivyosema, Yehova anahisije kuhusu kuwafufua wafu? 16. Wafu watakaofufuliwa wataishi katika hali gani?

72

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

mengi kuhusu ufufuo ujao. Watu waliofufuliwa hapa duniani waliungana tena na wapendwa wao. Katika ufufuo ujao hali itakuwa bora hata zaidi. Kama tulivyojifunza katika Sura ya 3, Mungu alikusudia dunia yote iwe paradiso. Kwa hiyo, wafu hawatafufuliwa waishi katika ulimwengu wenye vita, uhalifu, na magonjwa. Wataishi milele katika dunia hii kwa amani na furaha. 17 Ni nani watakaofufuliwa? Yesu alisema kwamba wote waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho wataisikia sauti yake [Yesu] na kutoka. (Yohana 5:28, 29) Vivyo hivyo, andiko la Ufunuo 20:13 linasema: Bahari ikawatoa wale wafu waliokuwa ndani yake, na kifo na Kaburi [Hadesi, kielezi-chini] vikawatoa wale wafu waliokuwa ndani yake. Hadesi ni kaburi. (Ona Nyongeza, ukurasa wa 212-213.) Kaburi hilo litabaki tupu. Mabilioni ya watu wanaopumzika humo wataishi tena. Mtume Paulo alisema: Kutakuwa na ufufuo wa waadilifu na wasio waadilifu pia. (Matendo 24:15) Hilo linamaanisha nini? 18 Waadilifu wanatia ndani watu wengi walioishi kabla ya Yesu kuja duniani ambao tunasoma juu yao katika Biblia. Huenda ukamkiria Noa, Abrahamu, Sara, Musa, Ruthu, Esta, na wengine wengi. Baadhi ya wanaume na wanawake hao wenye imani wanazungumziwa katika Waebrania sura ya 11. Lakini waadilifu pia wanatia ndani watumishi wa Yehova wanaokufa siku zetu. Kwa kuwa tuna tumaini la ufufuo, hatuogopi kufa.Waebrania 2:15. 19 Vipi wale wote ambao hawakumtumikia wala kumtii Yehova kwa sababu hawakupata kumjua? Mabilioni hayo ya watu wasio waadilifu hawatasahauliwa. Wao pia watafufuliwa na kupewa nafasi ili wajifunze kumhusu Mungu
17. Ni nani watakaofufuliwa? 18. Waadilifu watakaofufuliwa wanatia ndani nani, na tumaini hilo linaweza kuwa na matokeo gani maishani mwako? 19. Ni nani wasio waadilifu, na Yehova amewaonyesha fadhili kwa kuwapa nafasi ya kufanya nini?

Tumaini Hakika kwa Wapendwa Wako Ambao Wamekufa

73

wa kweli na kumtumikia. Kwa kipindi cha miaka elfu moja, wafu watafufuliwa na kupewa nafasi ya kumtumikia Yehova pamoja na wanadamu waaminifu duniani. Kitakuwa kipindi kizuri ajabu! Biblia inakiita kipindi hicho Siku ya Hukumu.1 20 Je, hiyo inamaanisha kwamba kila mwanadamu ambaye amewahi kuishi atafufuliwa? Hapana. Biblia inasema kwamba baadhi ya wafu wako Gehena. (Luka 12:5) Gehena lilitokana na bonde la takataka lililokuwa nje ya jiji la kale la Yerusalemu. Mizoga na takataka ziliteketezwa humo. Wafu ambao miili yao ilitupwa humo walionwa na Wayahudi kuwa hawastahili kuzikwa wala kufufuliwa. Kwa hiyo, kwa kufaa Gehena inawakilisha uharibifu wa milele. Ingawa Yesu atashiriki kuwahukumu walio hai na wafu, Yehova ndiye Hakimu mkuu. (Matendo 10:42) Hatawafufua kamwe watu atakaowahukumu kuwa waovu na wasiotaka kubadilika.

UFUFUO WA KIMBINGU
Biblia inataja pia ufufuo wa aina nyingine. Watakaopata ufufuo huo wataishi mbinguni wakiwa viumbe wa roho. Ni ufufuo mmoja tu wa aina hiyo unaotajwa katika Biblia, yaani, ule wa Yesu Kristo. 22 Baada ya Yesu kufa akiwa mwanadamu, Yehova hakuruhusu Mwana Wake mwaminifu aendelee kukaa kaburini. (Zaburi 16:10; Matendo 13:34, 35) Mungu alimfufua Yesu, lakini si katika mwili wa kibinadamu. Mtume Petro anaeleza kwamba Kristo aliuawa katika mwili, lakini akafanywa kuwa hai katika roho. (1 Petro 3:18) Kwa kweli, huo
21

1 Unaweza kupata habari zaidi kuhusu Siku ya Hukumu na msingi wa hukumu, katika Nyongeza, ukurasa wa 213-215.
20. Gehena ni nini, na ni nani wanaoenda huko? 21, 22. (a) Kuna ufufuo gani mwingine? (b) Ni nani aliyekuwa wa kwanza kabisa kufufuliwa akiwa na mwili wa roho?

74

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

ulikuwa muujiza mkubwa. Yesu alikuwa hai tena akiwa mtu wa roho mwenye nguvu! (1 Wakorintho 15:3-6) Yesu ndiye wa kwanza kabisa kupokea ufufuo huo mtukufu. (Yohana 3:13) Lakini siye wa mwisho. 23 Akijua kwamba angerudi mbinguni baada ya muda mfupi, Yesu aliwaambia wafuasi wake waaminifu kwamba angewatayarishia mahali huko. (Yohana 14:2) Yesu alisema wale wanaoenda mbinguni ni kundi lake dogo. (Luka 12:32) Kikundi hicho kidogo kitakuwa na Wakristo waaminifu wangapi? Mtume Yohana anasema hivi katika Ufunuo 14:1: Nikaona, na, tazama! Mwana-Kondoo [Yesu Kristo] amesimama juu ya Mlima Sayuni, na pamoja naye 144,000 wakiwa na jina lake na jina la Baba yake limeandikwa juu ya mapaji ya nyuso zao. 24 Wakristo hao 144,000, kutia ndani mitume waaminifu wa Yesu, watafufuliwa wakaishi mbinguni. Watafufuliwa wakati gani? Mtume Paulo aliandika kwamba wangefufuliwa wakati wa kuwapo kwa Kristo. (1 Wakorintho 15:23) Kama utakavyojifunza katika Sura ya 9, tunaishi katika kipindi hicho cha wakati. Kwa hiyo wachache wanaobaki kati ya wale 144,000 ambao wanakufa leo wanafufuliwa mara moja na kwenda kuishi mbinguni. (1 Wakorintho 15: 51-55) Hata hivyo, idadi kubwa ya wanadamu wana tumaini la kufufuliwa na kuishi katika Paradiso duniani wakati ujao. 25 Naam, kwa kweli Yehova atamshinda adui yetu kifo, atamwondolea mbali milele! (Isaya 25:8) Hata hivyo, huenda ukauliza, Wale wanaofufuliwa na kwenda mbinguni watafanya nini huko? Watakuwa sehemu ya serikali nzuri ya Ufalme huko mbinguni. Tutajifunza mengi zaidi kuhusu serikali hiyo katika sura inayofuata.
23, 24. Kundi dogo lililotajwa na Yesu ni akina nani, na ni wangapi? 25. Tutajifunza nini katika sura inayofuata?

Tumaini Hakika kwa Wapendwa Wako Ambao Wamekufa

75

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA Masimulizi ya Biblia kuhusu ufufuo yanatupa tumaini hakika.Yohana 11:39-44. Yehova anatamani kuwafufua wafu.Ayubu 14:13-15. Wale wote walio kaburini watafufuliwa. Yohana 5:28, 29.

Katika Paradiso, wafu watafufuka na kuungana tena na wapendwa wao

SURA YA NANE

Ufalme wa Mungu Ni Nini?


Biblia inatufundisha nini kuhusu Ufalme wa Mungu? Ufalme wa Mungu utafanya nini? Ufalme huo utatimiza mapenzi ya Mungu duniani wakati gani?
MAMILIONI ya watu ulimwenguni wanajua sala ambayo wengi huiita Sala ya Baba Yetu, au Sala ya Bwana. Majina hayo mawili yanarejelea ile sala inayojulikana sana ambayo Yesu Kristo mwenyewe aliitoa kama kielelezo. Ni sala yenye maana sana, na kuchunguza mambo matatu ya kwanza katika sala hiyo kutakusaidia kujua mambo mengi ambayo Biblia inafundisha. 2 Mwanzoni mwa sala hiyo ya kielelezo, Yesu aliwafundisha wasikilizaji wake hivi: Basi, ninyi msali hivi: Baba yetu uliye mbinguni, jina lako na litakaswe. Ufalme wako na uje. Mapenzi yako na yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni. (Mathayo 6:9-13) Mambo hayo matatu yanayoombwa yanamaanisha nini? 3 Tayari tumejifunza mengi kuhusu jina la Mungu, Yehova. Na kwa kadiri fulani tumezungumzia mapenzi ya Mungu, yaani, mambo ambayo amefanya na yale atakayowafanyia wanadamu. Hata hivyo, Yesu alimaanisha nini alipotuambia tusali: Ufalme wako uje? Ufalme wa Mungu
1. Tutazungumzia sala gani inayojulikana sana? 2. Ni mambo gani matatu ambayo Yesu aliwafundisha wanafunzi wake waombe? 3. Tunahitaji kujua nini kuhusu Ufalme wa Mungu?

Ufalme wa Mungu Ni Nini?

77

ni nini? Ufalme huo utakapokuja, utalitakasaje jina la Mungu au kulifanya liwe takatifu? Na kuja kwa Ufalme huo kunahusianaje na kutendeka kwa mapenzi ya Mungu?

UFALME WA MUNGU NI NINI? Ufalme wa Mungu ni serikali iliyosimamishwa na Yehova Mungu ikiwa na Mfalme ambaye amechaguliwa na Mungu. Mfalme wa Ufalme wa Mungu ni nani? Ni Yesu Kristo. Yesu akiwa Mfalme, ni mkuu kuliko watawala wa kibinadamu na anaitwa Mfalme wa wale wanaotawala wakiwa wafalme na Bwana wa wale wanaotawala wakiwa mabwana. (1 Timotheo 6:15) Ana nguvu za kufanya mambo mengi mazuri kuliko mtawala yeyote wa kibinadamu, hata yule aliye bora zaidi. 5 Ufalme wa Mungu utatawala kutoka wapi? Kwani, Yesu yuko wapi? Unakumbuka, tulijifunza kwamba aliuawa kwenye mti wa mateso, na baadaye akafufuliwa. Muda mfupi baadaye, alirudi mbinguni. (Matendo 2:33) Kwa hiyo, huko ndiko Ufalme wa Mungu uliko, yaani, mbinguni. Ndiyo sababu Biblia huuita ufalme wa mbinguni. (2 Timotheo 4:18) Ingawa Ufalme wa Mungu uko mbinguni, utatawala dunia. Ufunuo 11:15. 6 Kwa nini Yesu ni Mfalme wa pekee? Sababu moja ni kwamba, hatakufa kamwe. Ikimlinganisha na wafalme wa kibinadamu, Biblia inamwita Yesu yeye peke yake asiyeweza kufa, anayekaa katika nuru isiyoweza kukiwa. (1 Timotheo 6:16) Hilo linamaanisha kwamba mambo yote mazuri ambayo Yesu atafanya yatadumu. Naye kwa kweli atafanya mambo mengi mazuri. 7 Hebu kiria unabii huu wa Biblia kumhusu Yesu: Roho ya Yehova itatua juu yake, roho ya hekima na ya uelewaji,
4

4. Ufalme wa Mungu ni nini, na Mfalme wake ni nani? 5. Ufalme wa Mungu unatawala kutoka wapi, nao utatawala nini? 6, 7. Kwa nini Yesu ni Mfalme wa pekee?

78

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

roho ya shauri na ya nguvu, roho ya ujuzi na ya kumwogopa Yehova; naye atakuwa na shangwe katika kumwogopa Yehova. Na hatahukumu kulingana na sura inayoonekana kwa macho yake tu, wala kukaripia kulingana tu na jambo lililosikiwa na masikio yake. Naye atawahukumu kwa uadilifu watu wa hali ya chini, atakaripia kwa unyoofu kwa ajili ya watu wapole wa dunia. (Isaya 11:2-4) Maneno hayo yanaonyesha kwamba Yesu atakuwa Mfalme mwadilifu na mwenye huruma atakayetawala watu wa dunia. Je, ungependa kuwa na mtawala kama huyo? 8 Jambo lingine kuhusu Ufalme wa Mungu ni kwamba Yesu hatatawala akiwa peke yake. Atatawala pamoja na wengine. Kwa mfano, mtume Paulo alimwambia Timotheo hivi: Tukiendelea kuvumilia, tutatawala pamoja pia tukiwa wafalme. (2 Timotheo 2:12) Naam, Paulo, Timotheo, na waaminifu wengine ambao wamechaguliwa na Mungu watatawala pamoja na Yesu katika Ufalme wa mbinguni. Ni wangapi watakaokuwa na pendeleo hilo? 9 Kama tulivyoona katika Sura ya 7 ya kitabu hiki, mtume Yohana aliona katika maono Mwana-Kondoo [Yesu Kristo] amesimama juu ya Mlima Sayuni [akiwa mfalme mbinguni], na pamoja naye 144,000 wakiwa na jina lake na jina la Baba yake limeandikwa juu ya mapaji ya nyuso zao. Hao 144,000 ni nani? Yohana mwenyewe anatuambia hivi: Hao ndio wale wanaoendelea kumfuata Mwana-Kondoo popote anapoenda. Hao walinunuliwa kutoka kati ya wanadamu wakiwa matunda ya kwanza kwa Mungu na kwa MwanaKondoo. (Ufunuo 14:1, 4) Ndiyo, ni wafuasi waaminifu wa Yesu Kristo waliochaguliwa hasa kutawala mbinguni pamoja naye. Baada ya kufufuliwa na kuenda mbinguni, watatawala wakiwa wafalme juu ya dunia, pamoja na Yesu.
8. Ni nani watakaotawala pamoja na Yesu? 9. Ni watu wangapi watakaotawala pamoja na Yesu, na Mungu alianza kuwachagua lini?

Ufalme wa Mungu Ni Nini?

79

(Ufunuo 5:10) Tangu siku za mitume, Mungu amekuwa akiwachagua Wakristo waaminifu ili kukamilisha idadi hiyo ya 144,000. 10 Mungu alionyesha upendo kwa kufanya mpango ili Yesu na wale 144,000 wawatawale wanadamu. Kwanza, Yesu amewahi kuwa mwanadamu na kuteseka. Paulo alisema kwamba Yesu si mtu ambaye hawezi kuusikitikia udhaifu wetu, bali yeye ambaye amejaribiwa katika mambo yote kama sisi wenyewe, lakini bila kuwa na dhambi. (Waebrania 4:15; 5:8) Watawala wenzake pia wameteseka na kuvumilia wakiwa wanadamu. Isitoshe, wamepambana na kutokamilika na kukabiliana na magonjwa ya aina mbalimbali. Bila shaka, wataelewa matatizo yanayowakabili wanadamu!

UFALME WA MUNGU UTAFANYA NINI? Yesu alipowaambia wanafunzi wake waombe Ufalme wa Mungu uje, aliwaambia pia waombe mapenzi ya Mungu yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni. Mungu yuko mbinguni, na sikuzote malaika waaminifu wamekuwa wakitenda mapenzi yake huko. Hata hivyo, katika Sura ya 3 ya kitabu hiki, tulijifunza kwamba malaika mwovu aliacha kutenda mapenzi ya Mungu na kuwafanya Adamu na Hawa watende dhambi. Katika Sura ya 10, tutajifunza mengi zaidi kuhusu yale ambayo Biblia inafundisha kumhusu malaika huyo mwovu, anayeitwa Shetani Ibilisi. Shetani na malaika walioamua kumfuata, wanaoitwa roho waovu, waliruhusiwa kuishi mbinguni kwa muda. Kwa hiyo, si wote waliokuwa mbinguni walikuwa wakitenda mapenzi ya Mungu. Mambo yangebadilika wakati Ufalme wa Mungu ungeanza kutawala. Mfalme mpya aliyetawazwa, Yesu Kristo, angepigana vita na Shetani.Ufunuo 12:7-9.
11

10. Kwa nini ni mpango wa upendo kwa Yesu na wale 144,000 waliofufuliwa kuwatawala wanadamu? 11. Kwa nini Yesu aliwaambia wanafunzi wake waombe mapenzi ya Mungu yatendeke mbinguni?

80
12

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Maneno yafuatayo ya kinabii yanaeleza jambo ambalo lingetukia: Nikaisikia sauti kubwa mbinguni ikisema: Sasa kumekuwa na wokovu na nguvu na ufalme wa Mungu wetu na mamlaka ya Kristo wake, kwa sababu [Shetani] mshtaki wa ndugu zetu ametupwa chini, anayewashtaki mchana na usiku mbele za Mungu wetu! (Ufunuo 12:10) Je, unaona mambo mawili muhimu yanayotajwa katika mstari huo wa Biblia? Kwanza, Ufalme wa Mungu unaanza kutawala Yesu Kristo akiwa Mfalme. Pili, Shetani anatupwa duniani kutoka mbinguni. 13 Mambo hayo mawili yamekuwa na matokeo gani? Kuhusu mambo yaliyotokea mbinguni tunasoma hivi: Kwa sababu hiyo furahini, enyi mbingu nanyi mnaokaa ndani yake! (Ufunuo 12:12) Ndiyo, malaika waaminifu walio mbinguni wanafurahi kwa sababu baada ya Shetani na malaika zake kuondolewa, wote walio mbinguni ni waaminifu kwa Yehova Mungu. Kuna amani na upatano kamili wenye kudumu. Mapenzi ya Mungu yanatendeka mbinguni. 14 Hata hivyo, namna gani duniani? Biblia inasema: Ole wa dunia na wa bahari, kwa sababu Ibilisi ameshuka kwenu, akiwa na hasira kali, akijua kwamba ana kipindi kifupi cha wakati. (Ufunuo 12:12) Shetani ana hasira kwa sababu ametupwa kutoka mbinguni na ana kipindi kifupi tu cha wakati. Kwa hasira anasababisha dhiki, au ole duniani. Tutajifunza mengi zaidi kuhusu ole hiyo katika sura inayofuata. Hata hivyo, kwa kuwa Shetani ametupwa duniani na anasababisha dhiki, tunaweza kuuliza, Ufalme huo utafanyaje mapenzi ya Mungu yatendeke duniani? 15 Kumbuka mapenzi ya Mungu kwa dunia. Ulijifunza kuyahusu katika Sura ya 3. Katika Edeni, Mungu alionyesha kwamba mapenzi yake ni kwamba dunia iwe paradiso ili12. Ni mambo gani mawili muhimu yanayotajwa katika Ufunuo 12:10? 13. Hali imekuwaje baada ya Shetani kutupwa kutoka mbinguni? 14. Hali imekuwaje tangu Shetani alipotupwa duniani? 15. Mapenzi ya Mungu kwa dunia ni nini?

Ufalme wa Mungu Ni Nini?

81

yojaa jamii ya wanadamu waadilifu na wasiokufa. Shetani aliwafanya Adamu na Hawa watende dhambi, na hilo likaathiri kutimia kwa mapenzi ya Mungu duniani, lakini kusudi lake halikubadilika. Bado Yehova anakusudia kwamba waadilifu wenyewe wataimiliki dunia, nao watakaa milele juu yake. (Zaburi 37:29) Na Ufalme wa Mungu utatimiza hayo. Jinsi gani? 16 Hebu kiria unabii ulio kwenye Danieli 2:44. Tunasoma: Katika siku za wafalme hao, Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaharibiwa kamwe. Na ufalme huo hautapewa watu wengine wowote. Utazivunja na kuzikomesha falme hizi zote, nao utasimama mpaka wakati usio na kipimo. Hilo linatuambia nini kuhusu Ufalme wa Mungu? 17 Kwanza, Ufalme wa Mungu ungesimamishwa katika siku za wafalme hao, au wakati falme nyingine zingekuwa zikitawala bado. Pili, Ufalme huo utadumu milele. Hautashindwa wala serikali nyingine haitachukua mahali pake. Tatu, tunaona kwamba kutakuwa na vita kati ya Ufalme wa Mungu na falme za ulimwengu huu. Ufalme wa Mungu utashinda. Hatimaye, Ufalme wa Mungu ndio utakaokuwa serikali pekee inayowatawala wanadamu. Kisha wanadamu watafurahia utawala bora zaidi. 18 Biblia inasema mengi kuhusu vita vya mwisho kati ya Ufalme wa Mungu na serikali za ulimwengu huu. Kwa mfano, inafundisha kwamba mwisho unapokaribia, roho waovu wataeneza uwongo ili kuwadanganya wafalme wa dunia nzima inayokaliwa. Kwa kusudi gani? Ili kuwakusanya [wafalme hao] pamoja kwa vita vya ile siku kuu ya Mungu Mweza-Yote. Wafalme wa dunia watakusanywa pamoja mahali
16, 17. Andiko la Danieli 2:44 linasema nini kuhusu Ufalme wa Mungu? 18. Vita vya mwisho kati ya Ufalme wa Mungu na serikali za wanadamu vinaitwaje?

82

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

panapoitwa katika Kiebrania HarMagedoni. (Ufunuo 16:14, 16) Kwa sababu ya mambo yanayotajwa katika mistari hiyo miwili, vita vya mwisho kati ya serikali za wanadamu na Ufalme wa Mungu vinaitwa vita vya HarMagedoni. 19 Ufalme wa Mungu utatimiza nini kupitia HarMagedoni? Fikiria tena mapenzi ya Mungu kwa dunia. Yehova Mungu alikusudia dunia ijae jamii ya wanadamu waadilifu na wakamilifu wakimtumikia katika Paradiso. Kwa nini hilo halitendeki sasa? Kwanza, sisi ni watenda dhambi na tunakuwa wagonjwa na kufa. Hata hivyo, tulijifunza katika Sura ya 5 kwamba Yesu alikufa kwa ajili yetu ili tuweze kuishi milele. Huenda unakumbuka maneno haya yaliyo katika Injili ya Yohana: Mungu aliupenda ulimwengu sana hivi kwamba akamtoa Mwana wake mzaliwa-pekee, ili kila mtu anayemwamini asiangamizwe bali awe na uzima wa milele.Yohana 3:16. 20 Tatizo lingine ni kwamba watu wengi hutenda maovu. Wanasema uwongo, wanaiba, na kujihusisha katika ukosefu wa maadili. Hawataki kutenda mapenzi ya Mungu. Watu wanaotenda maovu wataharibiwa katika vita vya Mungu vya HarMagedoni. (Zaburi 37:10) Sababu nyingine pia inayofanya mapenzi ya Mungu yasitendeke duniani ni kwamba serikali haziwatii moyo watu wafanye hivyo. Serikali nyingi hazina uwezo, ni katili, au ni zenye usadi. Biblia husema hivi waziwazi: Mwanadamu amemtawala mwanadamu kwa kumuumiza.Mhubiri 8:9. 21 Baada ya HarMagedoni, wanadamu watakuwa chini ya serikali moja tu, Ufalme wa Mungu. Ufalme huo utatenda mapenzi ya Mungu na kuleta baraka nzuri ajabu. Kwa mfano, utamwondoa Shetani na roho wake waovu. (Ufunuo 20:1-3) Nguvu za dhabihu ya Yesu zitatumiwa ili kuwaondolea wanadamu waaminifu magonjwa na kifo. Nao wataishi
19, 20. Kwa nini mapenzi ya Mungu hayatendeki duniani sasa? 21. Ufalme utatendaje mapenzi ya Mungu duniani?

Kutupwa kwa Shetani na roho wake waovu kutoka mbinguni kulileta ole duniani. Matatizo hayo yatakwisha karibuni

84

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

milele chini ya utawala wa Ufalme. (Ufunuo 22:1-3) Dunia itafanywa kuwa paradiso. Hivyo, Ufalme huo utafanya mapenzi ya Mungu yatendeke duniani na utalitakasa jina la Mungu. Hilo linamaanisha nini? Hilo linamaanisha kwamba hatimaye chini ya Ufalme wa Mungu kila mtu aliye hai atalitukuza jina la Yehova.

UFALME WA MUNGU UTACHUKUA HATUA WAKATI GANI? 22 Yesu alipowaambia wanafunzi wake wasali, Acha Ufalme wako uje, ilikuwa wazi kwamba Ufalme huo haukuwa umekuja. Je, ulikuja Yesu alipopaa kuenda mbinguni? Hapana, kwa kuwa Petro na Paulo walisema kwamba baada ya Yesu kufufuliwa, unabii huu katika Zaburi 110:1 ulitimizwa: Neno la Yehova kwa Bwana wangu ni: Keti kwenye mkono wangu wa kuume mpaka niwaweke adui zako kuwa kiti cha miguu yako. (Matendo 2:32-34; Waebrania 10:12, 13) Kulikuwa na kipindi cha kungoja. 23 Kipindi hicho cha kungoja kingeendelea kwa muda gani? Katika karne ya 19, wanafunzi wanyoofu wa Biblia walikadiria kwamba kipindi hicho kingekia mwisho mwaka wa 1914. (Kuhusu tarehe hiyo, ona Nyongeza, ukurasa wa 215-218.) Matukio ya ulimwengu yaliyoanza mwaka
22. Tunajuaje kwamba Ufalme wa Mungu haukuja Yesu alipokuwa duniani au baada tu ya yeye kufufuliwa? 23. (a) Ufalme wa Mungu ulianza kutawala lini? (b) Sura ifuatayo itazungumzia nini?

Chini ya utawala wa Ufalme, mapenzi ya Mungu yatatendeka duniani kama ilivyo mbinguni

Ufalme wa Mungu Ni Nini?

85

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA Ufalme wa Mungu ni serikali ya mbinguni inayotawaliwa na Yesu Kristo pamoja na wale 144,000 ambao wametoka duniani.Ufunuo 14:1, 4. Ufalme huo ulianza kutawala mwaka wa 1914, na tangu wakati huo Shetani ametupwa duniani kutoka mbinguni.Ufunuo 12:9. Karibuni Ufalme wa Mungu utaharibu serikali za wanadamu, na dunia itakuwa paradiso.Ufunuo 16:14, 16.

wa 1914 yanathibitisha kwamba kadirio hilo la wanafunzi wanyoofu wa Biblia lilikuwa sahihi. Utimizo wa unabii wa Biblia unaonyesha kwamba katika mwaka wa 1914, Kristo alitawazwa kuwa Mfalme, kisha Ufalme wa mbinguni wa Mungu ukaanza kutawala. Hivyo, tunaishi katika kile kipindi kifupi cha wakati kinachobaki cha Shetani. (Ufunuo 12:12; Zaburi 110:2) Tunaweza pia kusema kwa hakika kwamba hivi karibuni Ufalme wa Mungu utachukua hatua ili mapenzi ya Mungu yatendeke duniani. Je, hiyo ni habari njema kwako? Je, unaamini kwamba inawezekana? Sura ifuatayo itakusaidia kuona kwamba Biblia inafundisha mambo haya.

SURA YA TISA

Je, Tunaishi Katika Siku za Mwisho?


Ni mambo gani yanayotokea leo yaliyotabiriwa katika Biblia? Neno la Mungu linasema watu wangekuwaje katika siku za mwisho? Biblia inatabiri mambo gani mazuri kuhusu siku za mwisho?
JE, UMEWAHI kusikiliza habari kwenye redio au televisheni na kujiuliza Ulimwengu huu unaelekea wapi? Misiba hutokea ghafula na bila kutarajiwa hivi kwamba hakuna mwanadamu anayeweza kutabiri mambo ya kesho. (Yakobo 4:14) Hata hivyo, Yehova anajua mambo ya wakati ujao. (Isaya 46:10) Zamani, Neno lake, Biblia, lilitabiri mambo mabaya ambayo yangetukia siku zetu na pia likatabiri mambo mazuri ya wakati ujao. 2 Yesu Kristo alizungumza kuhusu Ufalme wa Mungu ambao utakomesha uovu na kuifanya dunia iwe paradiso. (Luka 4:43) Watu walitaka kujua wakati ambapo Ufalme huo ungekuja. Hata wanafunzi wa Yesu walimuuliza: Ni nini itakayokuwa ishara ya kuwapo kwako na ya umalizio wa mfumo wa mambo? (Mathayo 24:3) Kwa kujibu Yesu aliwaambia kwamba ni Yehova Mungu peke yake anayejua kabisa wakati ambapo mwisho wa mfumo huu wa mambo utakuja. (Mathayo 24:36) Lakini Yesu alitabiri mambo ambayo yangetokea duniani kabla tu ya Ufalme huo
1. Ni wapi tunapoweza kupata habari kuhusu wakati ujao? 2, 3. Wanafunzi walimuuliza Yesu swali gani, naye alijibuje?

Je, Tunaishi Katika Siku za Mwisho?

87

kuwaletea wanadamu amani na usalama wa kweli. Mambo aliyotabiri yanatukia leo! 3 Kabla ya kuzungumzia mambo yanayothibitisha kwamba tunaishi katika umalizio wa mfumo wa mambo, na tuzungumzie kwa ufupi vita ambavyo hakuna mwanadamu yeyote angeweza kuviona. Vilitukia katika makao yasiyoonekana ya roho, na matokeo yake yanatuathiri.

VITA MBINGUNI
Sura iliyotangulia ya kitabu hiki ilieleza kwamba Yesu Kristo alitawazwa kuwa Mfalme mbinguni mwaka wa 1914. (Danieli 7:13, 14) Muda mfupi baada ya kupokea mamlaka ya Ufalme, Yesu alichukua hatua. Biblia inasema kwamba Vita vikatokea ghafula mbinguni: Mikaeli [jina lingine la Yesu] na malaika zake wakapigana na yule joka mkubwa [Shetani Ibilisi], naye joka mkubwa na malaika zake wakapigana.1 Shetani na malaika zake waovu, yaani, roho waovu, walishindwa katika vita hivyo na kutupwa duniani kutoka mbinguni. Malaika waaminifu wa Mungu walifurahi kwamba Shetani na roho wake waovu walikuwa wametupwa nje. Hata hivyo, wanadamu hawangepata furaha hiyo. Biblia ilitabiri hivi: Ole wa dunia . . . kwa sababu Ibilisi ameshuka kwenu, akiwa na hasira kali, akijua kwamba ana kipindi kifupi cha wakati.Ufunuo 12: 7, 9, 12. 5 Tafadhali ona matokeo ya vita hivyo vya mbinguni. Kwa hasira, Shetani angeleta ole au taabu duniani. Kama utakavyoona, sasa tunaishi katika kipindi hicho cha taabu. Lakini hakitakuwa kirefu, ni kipindi kifupi cha wakati.
4

1 Unaweza kupata habari zinazoonyesha kwamba Mikaeli ni jina lingine la Yesu Kristo katika Nyongeza, ukurasa 218-219. 4, 5. (a) Ni nini kilichotokea mbinguni mara tu baada ya Yesu kutawazwa kuwa Mfalme? (b) Kulingana na Ufunuo 12:12, matokeo ya vita mbinguni yangekuwa nini?

88

Hata Shetani anajua hivyo. Biblia inakiita kipindi hicho siku za mwisho. (2 Timotheo 3:1) Tunafurahi sana kujua kwamba karibuni Mungu ataondoa matatizo ambayo Ibilisi husababisha duniani. Hebu tuchunguze mambo fulani yaliyotabiriwa katika Biblia ambayo yanatendeka leo. Mambo hayo yanaonyesha kwamba tunaishi katika siku za mwisho na karibuni Ufalme wa Mungu utawaletea baraka za milele wale wanaompenda Yehova. Kwanza, tuchunguze mambo manne katika ishara ambayo Yesu alisema ingeonyesha kwamba tunaishi katika siku za mwisho.

MATUKIO MAKUBWA YA SIKU ZA MWISHO 6 Taifa litasimama kupigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme. (Mathayo 24:7) Mamilioni ya watu wameuawa vitani katika miaka 100 iliyopita. Mwanahistoria mmoja Mwingereza aliandika hivi: Watu wengi
zaidi waliuawa katika karne ya 20 kuliko wakati mwingine wowote. . . . Katika karne hiyo kulikuwa na mfululizo wa vita, kukiwa na vipindi vifupi vichache vya wakati ambapo hakukuwa na vita mahali fulani ulimwenguni. Ripoti ya Taasisi ya Worldwatch ilisema hivi: Idadi ya watu walioathiriwa
6, 7. Maneno ya Yesu kuhusu vita na upungufu wa chakula yanatimizwaje leo?

89

na vita vya karne [ya 20] ilizidi mara tatu ile ya watu walioathiriwa na vita vyote vilivyopiganwa tangu karne ya kwanza W.K., hadi mwaka wa 1899. Zaidi ya watu milioni 100 wamekufa kwa sababu ya vita tangu mwaka wa 1914. Hata ikiwa tunahisi maumivu kwa sababu mtu mmoja tunayempenda ameuawa vitani, hatuwezi kuelewa kikamili taabu na maumivu ya mamilioni ya watu wanaowa. 7 Kutakuwa na upungufu wa chakula. (Mathayo 24:7) Watati wanasema kwamba kiasi cha chakula kimeongezeka sana katika miaka 30 iliyopita. Hata hivyo, bado kuna upungufu wa chakula kwa sababu watu wengi hawana pesa za kutosha kununua chakula au mashamba ya kukuza vyakula. Katika nchi zinazoendelea, watu zaidi ya bilioni moja ni maskini hohehahe. Wengi wao hawapati chakula. Shirika la Afya Ulimwenguni linakadiria kwamba watoto zaidi ya milioni tano hufa kila mwaka kutokana na utapiamlo. 8 Kutakuwa na matetemeko makubwa ya nchi. (Luka 21:11) Kulingana na Uchunguzi wa Kijiolojia wa Marekani, tangu 1990 kumekuwa na wastani wa matetemeko 17 ya nchi kila mwaka
8, 9. Ni nini kinachoonyesha kwamba unabii wa Yesu kuhusu matetemeko ya nchi na tauni unatimia?

90

ambayo yana nguvu za kutosha kuharibu majengo na kupasua ardhi. Na kwa wastani, kila mwaka kumekuwa na matetemeko yenye nguvu za kutosha kuharibu majengo kabisa. Shirika lingine lilisema: Matetemeko ya nchi yamesababisha vifo vya mamia ya maelfu ya watu katika miaka 100 ambayo imepita na maendeleo ya kitekinolojia yamepunguza vifo kwa kiwango kidogo tu. 9 Kutakuwa na tauni. (Luka 21:11) Licha ya maendeleo ya kitiba, magonjwa ya zamani na mapya yamewakumba wanadamu. Ripoti moja inasema kwamba magonjwa 20 yanayojulikana sanakutia ndani kifua kikuu, malaria, na kipindupinduyameanza tena kuenea katika miaka ya karibuni, na inazidi kuwa vigumu kuponya aina fulani za magonjwa hayo kwa dawa. Angalau magonjwa 30 mapya yamezuka. Baadhi yake ni hatari na hayawezi kutibiwa kwa dawa yoyote.

WATU WA SIKU ZA MWISHO 10 Biblia haielezi tu mambo ambayo yangetukia ulimwenguni bali pia ilitabiri kwamba jamii ya wanadamu ingebadilika katika siku za mwisho. Mtume Paulo alieleza jinsi hali ya watu kwa ujumla ingekuwa. Tunasoma hivi
10. Ni mambo gani yaliyotabiriwa katika 2 Timotheo 3:1-5 unayoona watu wakifanya leo?

91

katika 2 Timotheo 3:1-5: Katika siku za mwisho kutakuwa na nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo. Kwa sehemu, Paulo alisema kwamba watu wangekuwa

wenye kujipenda wenyewe wenye kupenda pesa wasiotii wazazi wasio washikamanifu wasio na upendo wa asili wasiojizuia wakali wanaopenda raha badala ya kumpenda Mungu wenye namna ya ujitoaji-kimungu lakini wakizikana nguvu zake
11 Je, hivyo ndivyo watu walivyo katika eneo lenu? Bila shaka. Watu walio na tabia hizo mbovu wako kila mahali. Hilo linaonyesha kwamba hivi karibuni Mungu atachukua hatua kwa kuwa Biblia inasema: Wakati waovu wanapochipuka kama majani na wote wanaotenda mambo yenye kuumiza wanapochanuka, ni ili wao wapate kuangamizwa milele.Zaburi 92:7.

11. Kulingana na Zaburi 92:7 ni nini kitakachowapata waovu?

92

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

MABADILIKO MAZURI!
Kwa kweli siku za mwisho zimejaa ole, kama vile Biblia ilivyotabiri. Hata hivyo, katika ulimwengu huu wenye matatizo mengi, kuna mabadiliko mazuri kati ya waabudu wa Yehova. 13 Kitabu cha Danieli kilitabiri hivi: Ujuzi wa kweli utakuwa mwingi. Hilo lingetimia wakati gani? Wakati wa mwisho. (Danieli 12:4) Hasa tangu 1914, Yehova amewasaidia wale ambao kwa kweli wanatamani kumtumikia wapate ujuzi zaidi wa Biblia. Wamepata kuelewa zaidi kweli kuhusu jina la Mungu na kusudi lake, dhabihu ya dia ya Yesu Kristo, hali ya wafu, na ufufuo. Isitoshe, waabudu wa Yehova wamejifunza kuwa na maisha yanayowafaidi na kumletea Mungu sifa. Pia, wameelewa vizuri zaidi jukumu la Ufalme wa Mungu na jinsi utakavyorekebisha hali duniani. Wanautumiaje ujuzi huo? Swali hilo linatukumbusha unabii mwingine ambao unatimizwa katika siku hizi za mwisho. 14 Kuhusu umalizio wa mfumo wa mambo, Yesu Kristo alitabiri hivi: Habari njema ya ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa. (Mathayo 24:3, 14) Habari njema ya Ufalme inahubiriwa duniani pote katika nchi zaidi ya 230, na kwa zaidi ya lugha 400. Habari hizo zinatia ndani: Ufalme ni nini, utafanya nini, na jinsi tunavyoweza kupata baraka zake. Mamilioni ya Mashahidi wa Yehova huhubiri kwa bidii habari njema ya Ufalme. Wanatoka katika mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na lugha. (Ufunuo 7:9) Mamilioni ya watu wanaotaka kujua yale ambayo Biblia hufundisha hasa, hujifunza Biblia pamoja na Mashahidi bila malipo. Kwa kweli, huo ni utimizo wenye kuvutia wa unabii hasa kwa kuwa Yesu alitabiri kwamba Wakristo wa kweli wangechukiwa na watu wote!Luka 21:17.
12

12, 13. Ujuzi wa kweli umekuwaje mwingi katika hizi siku za mwisho? 14. Habari njema ya Ufalme imehubiriwa kwa kiwango gani leo, na ni nani wanaoihubiri?

Habari njema ya ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa. Mathayo 24:14

94

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

UTAFANYA NINI?
Kwa kuwa mambo mengi yaliyotabiriwa katika Biblia yanatimia leo, je hukubali kwamba tunaishi katika siku za mwisho? Baada ya Yehova kuridhika na kuhubiriwa kwa habari njema, hapana shaka kwamba mwisho utakuja. (Mathayo 24:14) Mwisho ni wakati ambapo Mungu ataondoa uovu duniani. Yehova atamtumia Yesu na malaika wenye nguvu kuwaharibu wote wanaompinga kimakusudi. (2 Wathesalonike 1:6-9) Shetani na roho wake waovu hawatayapotosha mataifa tena. Kisha Ufalme wa Mungu utawaletea baraka nyingi wote wanaojitiisha kwa utawala wake mwadilifu.Ufunuo 20:1-3; 21:3-5. 16 Kwa kuwa mwisho wa mfumo wa Shetani u karibu, tunahitaji kujiuliza, Ninapaswa kuwa nikifanya nini? Unapaswa kuendelea kujifunza mengi kumhusu Yehova na mambo anayotaka tufanye. (Yohana 17:3) Jifunze Biblia kwa bidii. Uwe na mazoea ya kushirikiana kwa ukawaida pamoja na wale wanaojitahidi kufanya mapenzi ya Yehova. (Waebrania 10:24, 25) Pata ujuzi mwingi ambao Yehova Mungu amewaandalia watu ulimwenguni pote, na ufanye marekebisho yanayohitajiwa maishani mwako ili upate kibali cha Mungu.Yakobo 4:8. 17 Yesu alitabiri kwamba watu wengi wangepuuza uthibitisho kwamba tunaishi katika siku za mwisho. Waovu wataharibiwa ghafula na bila kutarajia. Siku hiyo itakuja kama mwizi wakati wa usiku na kuwashtua watu wengi. (1 Wathesalonike 5:2) Yesu alionya hivi: Kama vile siku za Noa zilivyokuwa, ndivyo kuwapo kwa Mwana wa binadamu kutakavyokuwa. Kwa maana kama vile walivyokuwa katika siku hizo kabla ya gharika, wakila na kunywa, wana15

15. (a) Je, unaamini kwamba tunaishi katika siku za mwisho, kwa nini? (b) Mwisho utamaanisha nini kwa wale wanaompinga Yehova na kwa wale wanaojitiisha kwa Ufalme wa Mungu? 16. Unapaswa kufanya nini? 17. Kwa nini kuharibiwa kwa waovu kutawashtua watu wengi?

Je, Tunaishi Katika Siku za Mwisho?

95

ume wakioa na wanawake wakiolewa, mpaka siku ambayo Noa aliingia ndani ya sana; nao hawakujali mpaka gharika ikaja na kuwafagilia mbali wote, ndivyo kuwapo kwa Mwana wa binadamu kutakavyokuwa.Mathayo 24:37-39. 18 Kwa hiyo, Yesu aliwaambia hivi watu waliokuwa wakimsikiliza: Jiangalieni ninyi wenyewe kwamba mioyo yenu isilemewe kamwe na kula kupita kiasi na kunywa sana na mahangaiko ya maisha, na kwa ghafula siku hiyo iwe juu yenu mara moja kama mtego. Kwa maana itakuja juu ya wale wote wanaokaa juu ya uso wa dunia yote. Basi, endeleeni kukesha wakati wote mkiomba dua ili mpate kufanikiwa kuponyoka mambo yote hayo yaliyokusudiwa kutukia, na kusimama [kupata kibali] mbele ya Mwana wa binadamu. (Luka 21:34-36) Tunapaswa kuyachukua maneno ya Yesu kwa uzito. Kwa nini? Kwa sababu wale walio na kibali cha Yehova Mungu na cha Mwana wa binadamu, Yesu Kristo, wana tumaini la kuokoka mwisho wa mfumo wa mambo wa Shetani na kuishi milele katika ulimwengu mpya ulio karibu sana!Yohana 3:16; 2 Petro 3:13.
18. Ni onyo gani la Yesu tunalopaswa kuchukua kwa uzito?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA Vita, upungufu wa chakula, matetemeko ya nchi, na tauni ni mambo yanayoonyesha kwamba tunaishi katika siku za mwisho. Mathayo 24:7; Luka 21:11. Katika siku hizi za mwisho, watu wengi wanajipenda wenyewe, wanapenda pesa na raha badala ya kumpenda Mungu.2 Timotheo 3:1-5. Katika siku hizi za mwisho, habari njema ya Ufalme inahubiriwa ulimwenguni pote. Mathayo 24:14.

SURA YA KUMI

Jinsi Viumbe wa Roho Wanavyohusika Maishani Mwetu


Je, malaika huwasaidia watu? Roho waovu wamekuwa na uvutano gani kwa wanadamu? Je, tuna sababu ya kuwaogopa roho waovu?
KWA kawaida kumjua mtu kunatia ndani kuijua familia yake pia. Vivyo hivyo, kumjua Yehova Mungu hutia ndani kuwajua vizuri zaidi malaika ambao ni sehemu ya familia yake. Biblia huwaita malaika hao wana wa Mungu. (Ayubu 38:7) Kwa hiyo, wana jukumu gani katika kusudi la Mungu? Je, wametimiza lolote katika historia ya wanadamu? Je, malaika wanahusika maishani mwako? Ikiwa ndivyo, jinsi gani? 2 Malaika hutajwa katika Biblia mara nyingi sana. Hebu tuchunguze baadhi ya maandiko hayo ili tujifunze mengi zaidi kuwahusu. Malaika walitoka wapi? Andiko la Wakolosai 1:16 linasema hivi: Kwa njia yake [Yesu Kristo] vitu vingine vyote viliumbwa mbinguni na duniani. Kwa hiyo, viumbe wote wa roho wanaoitwa malaika waliumbwa moja kwa moja na Yehova Mungu kupitia Mwana wake mzaliwa wa kwanza. Kuna malaika wangapi? Biblia inaonyesha kwamba mamia ya mamilioni ya malaika waliumbwa, na wote wana nguvu nyingi. Zaburi 103:20.1
1 Andiko la Ufunuo 5:11 linasema hivi kuhusu malaika waadilifu: Hesabu yao ilikuwa makumi ya maelfu ya makumi ya maelfu. Kwa hiyo, Biblia inaonyesha kwamba mamia ya mamilioni ya malaika waliumbwa.

1. Kuna faida gani kujifunza kuhusu malaika? 2. Malaika walitoka wapi, na ni wangapi?

Jinsi Viumbe wa Roho Wanavyohusika Maishani Mwetu


3

97

Neno la Mungu, Biblia, linatuambia kwamba msingi wa dunia ulipowekwa, wana wote wa Mungu walianza kupaaza sauti kwa kushangilia. (Ayubu 38:4-7) Kwa hiyo malaika walikuwako muda mrefu kabla ya wanadamu kuumbwa, hata kabla ya kuumbwa kwa dunia. Andiko hilo la Biblia linaonyesha pia kwamba malaika wana hisia kwa sababu linasema walipiga vigelegele pamoja kwa shangwe. Ona kwamba wana wote wa Mungu walishangilia pamoja. Wakati huo, malaika wote walikuwa sehemu ya familia yenye umoja iliyokuwa ikimtumikia Yehova Mungu.

UTEGEMEZO NA ULINZI WA MALAIKA


Tangu waliposhuhudia kuumbwa kwa wanadamu wa kwanza, viumbe wa roho walio waaminifu wamependezwa sana na familia ya wanadamu inayoongezeka na wamependezwa pia na kutimizwa kwa kusudi la Mungu. (Methali 8: 30, 31; 1 Petro 1:11, 12) Hata hivyo, kadiri wakati ulivyopita, malaika waliona kwamba wanadamu wengi walikuwa wakiacha kumtumikia Muumba wao mwenye upendo. Bila shaka jambo hilo liliwahuzunisha malaika waliokuwa waaminifu. Kwa upande mwingine, hata mwanadamu mmoja tu anapomrudia Yehova, shangwe hutokea kati ya malaika. (Luka 15:10) Kwa kuwa malaika hupendezwa sana na hali nzuri ya wale wanaomtumikia Mungu, haishangazi kwamba Yehova amekuwa akiwatumia malaika kuwaimarisha na kuwalinda watumishi wake waaminifu walio duniani. (Waebrania 1:7, 14) Fikiria mifano kadhaa. 5 Malaika wawili walimsaidia yule mwanamume mwadilifu Loti pamoja na binti zake waokoke kuharibiwa kwa majiji yaliyojaa uovu ya Sodoma na Gomora, kwa kuwaongoza
4

3. Andiko la Ayubu 38:4-7 linatuambia nini kuhusu malaika? 4. Biblia inaonyeshaje kwamba malaika waaminifu wanapendezwa na utendaji wa wanadamu? 5. Biblia inataja mifano gani ambayo inaonyesha jinsi malaika wanavyowategemeza watumishi wa Mungu?

98

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

kutoka katika eneo hilo. (Mwanzo 19:15, 16) Karne nyingi baadaye, nabii Danieli alitupwa katika shimo la simba, hata hivyo hakupatwa na madhara yoyote naye alisema hivi: Mungu wangu mwenyewe alimtuma malaika wake na kufunga vinywa vya simba. (Danieli 6:22) Katika karne ya kwanza W.K., malaika alimweka huru mtume Petro kutoka gerezani. (Matendo 12: 6-11) Isitoshe, malaika walimtia nguvu Yesu mwanzoni mwa huduma yake hapa duniani. (Marko 1:13) Pia, muda mfupi kabla ya kifo cha Yesu, malaika alimtokea, akamtia nguvu. (Luka 22:43) Lazima hilo lilimfariji Yesu kama nini katika nyakati hizo muhimu sana maishani mwake! 6 Leo, malaika hawawatokei kihalisi watumishi wa Mungu walio duniani. Ingawa hawaonekani, malaika wa Mungu wenye nguvu bado huwalinda watumishi wake, hasa dhidi ya madhara yoyote ya kiroho. Biblia inasema hivi: Malaika wa Yehova anapiga kambi pande zote kuwazunguka wanaomwogopa, na yeye huwaokoa. (Zaburi 34:7) Kwa nini maneno hayo yanapaswa kutufariji sana? Kwa sababu kuna roho waovu hatari, wanaotaka kutuangamiza! Ni nani hao? Wanatoka wapi? Wanajaribu kutuumiza jinsi gani? Ili kupata majibu, na tuchunguze kifupi jambo lililotokea mwanzoni mwa historia ya wanadamu.

VIUMBE WA ROHO AMBAO NI ADUI ZETU


Kama tulivyojifunza katika Sura ya 3 ya kitabu hiki, mmoja wa malaika alikuza tamaa ya kuwatawala wengine na hivyo akamwasi Mungu. Baadaye, malaika huyo akaja kuitwa Shetani Ibilisi. (Ufunuo 12:9) Kwa karne 16 tangu alipomdanganya Hawa, Shetani alifanikiwa kuwageuza karibu watu wote waache kumtumikia Mungu isipokuwa waaminifu wachache, kama vile Abeli, Enoko, na Noa.Waebrania 11:4, 5, 7.
7

6. (a) Malaika huwalindaje watumishi wa Mungu leo? (b) Tutachunguza maswali gani sasa? 7. Shetani alifanikiwa kadiri gani kuwageuza watu waache kumtumikia Mungu?

Jinsi Viumbe wa Roho Wanavyohusika Maishani Mwetu


8

99

Katika siku za Noa, malaika wengine walimwasi Yehova. Waliacha mahali pao katika familia ya Mungu ya kimbingu, wakaja duniani, na kujivika miili yenye nyama. Kwa nini? Tunasoma hivi katika Mwanzo 6:2: Wana wa Mungu wa kweli wakaanza kuwaona mabinti wa wanadamu, kwamba ni wenye sura ya kupendeza; nao wakajichukulia wake, yaani, wote waliowachagua. Hata hivyo, Yehova Mungu hakuachilia matendo ya malaika hao na usadi wao uendelee kati ya wanadamu. Alileta mafuriko duniani, akawafagilia mbali wanadamu wote waovu na kuwahifadhi watumishi wake
8. (a) Malaika fulani walikujaje kuwa roho waovu? (b) Roho waovu walilazimika kufanya nini ili kuokoka Mafuriko ya siku za Noa?

Mungu wangu mwenyewe alimtuma malaika wake na kufunga vinywa vya simba. Danieli 6:22

100

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

waaminifu. (Mwanzo 7:17, 23) Hivyo, malaika hao waasi, au roho waovu, walilazimika kuiacha miili yao yenye nyama na kurudi mbinguni wakiwa viumbe wa roho. Walikuwa wamejiunga na Ibilisi, aliyekuwa mtawala wa roho waovu. Mathayo 9:34. 9 Waliporudi mbinguni, malaika hao waasi walitengwa na familia ya Mungu, kama alivyotengwa Shetani, mtawala wao. (2 Petro 2:4) Ingawa kwa sasa hawawezi kujivika miili ya kibinadamu, bado wana uvutano mbaya sana kwa wanadamu. Shetani, akisaidiwa na roho hao waovu, anaipotosha dunia nzima inayokaliwa. (Ufunuo 12:9; 1 Yohana 5:19) Jinsi gani? Malaika hao hutumia hasa njia ambazo zinakusudiwa kuwapotosha wanadamu. (2 Wakorintho 2:11) Hebu tuchunguze baadhi ya njia hizo.

JINSI ROHO WAOVU WANAVYOPOTOSHA


Roho waovu hutumia mazoea ya kuwasiliana na pepo ili kuwapotosha watu. Mazoea hayo huhusisha roho waovu, kwa njia ya moja kwa moja au kupitia mwanadamu mwingine. Biblia hushutumu mazoea ya kuwasiliana na pepo nayo hutuonya tujiepushe na kila kitu kinachohusiana na mazoea hayo. (Wagalatia 5:19-21) Roho waovu hutumia mazoea ya kuwasiliana na pepo kama vile mvuvi anavyotumia chambo kwenye ndoana. Mvuvi hutumia vyambo vya aina mbalimbali ili kunasa samaki wa namna mbalimbali. Vivyo hivyo, roho waovu hutumia njia mbalimbali za kuwasiliana na pepo ili kuwanasa watu wa namna zote. 11 Chambo kimoja kinachotumiwa na roho waovu ni uaguzi. Uaguzi ni nini? Ni kujaribu kujua habari za wakati ujao au jambo lisilojulikana. Uaguzi unatia ndani kuangalia nyota, kusoma kadi za karata, kutazama mpira wa kioo, kusoma
10

9. (a) Ni nini kilichowapata roho waovu waliporudi mbinguni? (b) Tutachunguza nini kuhusiana na roho waovu? 10. Kuwasiliana na pepo huhusisha nini? 11. Uaguzi ni nini, na kwa nini tunapaswa kuuepuka?

Roho waovu hutumia njia mbalimbali kuwadanganya watu

viganja vya mkono, kutafuta ndege au ishara mbaya, na kufasiri ndoto. Ingawa watu wengi hukiri kwamba uaguzi hauna madhara yoyote, Biblia huonyesha kwamba wabashiri hushirikiana na roho waovu. Kwa mfano, andiko la Matendo 16: 16-18 linamtaja roho mwovu wa uaguzi ambaye alimwezesha kijakazi kufanya ufundi wa kubashiri. Lakini, roho huyo mwovu alipomtoka, alipoteza uwezo wa kubashiri. 12 Njia nyingine ambayo roho waovu hutumia kuwapotosha watu ni kuwachochea watafute habari za wafu. Mara nyingi, watu wanaoomboleza kifo cha mpendwa wao huamini mambo ya uwongo kuhusu waliokufa. Mtu mwenye uwezo wa kuwasiliana na pepo anaweza kutoa ujumbe wa pekee au anaweza kuongea kwa sauti kama ya mtu aliyekufa. Ndiyo sababu watu wengi husadiki kwamba wafu wako hai na kwamba kuwasiliana nao kutawasaidia walio hai kuvumilia huzuni yao. Lakini faraja ya aina hiyo ni ya uwongo na ni hatari. Kwa nini? Kwa sababu roho waovu wanaweza kuiga sauti ya mtu aliyekufa na kumpa mtu anayewasiliana na pepo
12. Kwa nini ni hatari kujaribu kuwasiliana na wafu?

JINSI YA KUWAPINGA ROHO WAOVU

Haribu vitu vya


kuwasiliana na pepo Jifunze Biblia Sali kwa Mungu

Jinsi Viumbe wa Roho Wanavyohusika Maishani Mwetu

103

habari kumhusu mfu huyo. (1 Samweli 28:3-19) Isitoshe, kama tulivyojifunza katika Sura ya 6, wafu hawaendelei kuishi. (Zaburi 115:17) Kwa hiyo, yeyote anayeuliza habari kutoka kwa wafu amepotoshwa na roho waovu na anatenda kinyume cha mapenzi ya Mungu. (Kumbukumbu la Torati 18:10, 11; Isaya 8:19) Basi, uwe mwangalifu usije ukanaswa na chambo hicho hatari kinachotumiwa na roho waovu. 13 Mbali na kuwapotosha watu, roho waovu huwatisha pia. Leo, Shetani na roho wake waovu wanajua kwamba wana kipindi kifupi cha wakati kabla hawajakomeshwa, na sasa ni wakatili kuliko wakati mwingine wowote. (Ufunuo 12:12, 17) Hata hivyo, maelfu ya watu ambao hapo zamani walikuwa wakiwaogopa roho waovu, sasa hawawaogopi kamwe. Ni nini kimewasaidia? Mtu anaweza kufanya nini hata ikiwa anashiriki katika mazoea ya kuwasiliana na pepo?

JINSI YA KUWAPINGA ROHO WAOVU


Biblia inatueleza jinsi ya kuwapinga roho waovu na jinsi ya kuvunja uhusiano nao. Fikiria mfano wa Wakristo wa karne ya kwanza katika jiji la Efeso. Baadhi yao walikuwa na mazoea ya kuwasiliana na pepo kabla ya kuwa Wakristo. Walipoamua kuacha mazoea hayo, walifanya nini? Biblia inasema: Hesabu kubwa ya wale waliozoea kufanya ufundi wa uchawi wakaleta pamoja vitabu vyao wakaviteketeza mbele ya kila mtu. (Matendo 19:19) Kwa kuharibu vitabu vyao vya uchawi, Wakristo hao wapya waliwawekea mfano wale wanaotaka kuwapinga roho waovu leo. Watu wanaotaka kumtumikia Yehova wanapaswa kuharibu kila kitu kinachohusiana na mazoea ya kuwasiliana na pepo. Vitu hivyo vinatia ndani vitabu, magazeti, sinema, vibandiko, na miziki inayowachochea watu kuwasiliana na pepo na kuona
14

13. Watu wengi ambao zamani waliwaogopa roho waovu wamefaulu kufanya nini? 14. Tunawezaje kuacha kuwasiliana na roho waovu kama walivyofanya Wakristo wa Efeso katika karne ya kwanza?

104

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

mazoea hayo kuwa yenye kuvutia na kusisimua. Vitu vingine ambavyo pia vinapaswa kuharibiwa ni hirizi au chochote kinachovaliwa ili kumlinda mtu asipatwe na mabaya.1 Wakorintho 10:21. 15 Miaka kadhaa baada ya Wakristo wa Efeso kuharibu vitabu vyao vya uchawi, mtume Paulo aliwaandikia hivi: Tuna kushindana mweleka . . . juu ya majeshi ya roho waovu. (Waefeso 6:12) Roho waovu hawakuwa wamekata tamaa. Bado walikuwa wakijaribu kuwanasa. Kwa hiyo, Wakristo hao walihitaji kufanya nini? Paulo alisema, Zaidi ya mambo yote, ichukueni ngao kubwa ya imani, ambayo kwa kuitumia mtaweza kuizima mishale yote inayowaka moto ya yule mwovu [Shetani]. (Waefeso 6:16) Kadiri ngao yetu ya imani ilivyo na nguvu, ndivyo tutakavyowapinga roho waovu kwa nguvu. Mathayo 17:20. 16 Basi, tunawezaje kuimarisha imani yetu? Kwa kujifunza Biblia. Ili ukuta uwe imara, ni lazima msingi wake uwe na nguvu. Vivyo hivyo, ili imani yetu iwe na nguvu ni lazima tuwe na msingi imara, ambao ni ujuzi sahihi wa Neno la Mungu, Biblia. Tukisoma na kujifunza Biblia kila siku, imani yetu itakuwa na nguvu. Sawa na ukuta imara, imani hiyo itatukinga dhidi ya uvutano wa roho waovu.1 Yohana 5:5. 17 Wakristo wa Efeso walihitaji kuchukua hatua gani nyingine? Walihitaji ulinzi zaidi kwa sababu walikuwa wakiishi katika jiji lililojaa mazoea ya roho waovu. Kwa hiyo Paulo aliwaambia hivi: Kwa kila namna ya sala na dua, endelezeni sala kila wakati katika roho. (Waefeso 6:18) Kwa kuwa sisi pia tunaishi katika ulimwengu uliojaa mazoea ya roho waovu, tunahitaji kumwomba Yehova kwa bidii ili atulinde dhidi ya roho hao waovu. Bila shaka, tunahitaji kulitumia jina la Yehova katika sala zetu. (Methali 18:10) Kwa hiyo, tunapa15. Tunahitaji kufanya nini ili kuwapinga roho waovu? 16. Tunawezaje kuwa na imani yenye nguvu? 17. Ni hatua gani nyingine tunayohitaji kuchukua ili kuwapinga roho waovu?

Jinsi Viumbe wa Roho Wanavyohusika Maishani Mwetu

105

swa kuendelea kumwomba Mungu atukomboe kutokana na yule mwovu, Shetani Ibilisi. (Mathayo 6:13) Yehova atajibu sala hizo tunazotoa kwa bidii.Zaburi 145:19. 18 Roho waovu ni hatari, hata hivyo, ikiwa tunampinga Ibilisi na kumkaribia Mungu kwa kufanya mapenzi Yake, hatutaishi kwa woga. (Yakobo 4:7, 8) Nguvu za roho waovu zina mipaka. Waliadhibiwa katika siku za Noa, nao watapata hukumu yao ya mwisho. (Yuda 6) Pia, kumbuka kwamba malaika wenye nguvu wa Yehova hutulinda. (2 Wafalme 6: 15-17) Malaika hao wangependa sana kuona tukifaulu kuwashinda roho waovu. Malaika hao waadilifu wanatushangilia. Basi, na tukae karibu na Yehova na familia yake ya viumbe waaminifu wa roho. Na tuepuke pia kila namna ya kuwasiliana na pepo na sikuzote tutumie shauri la Neno la Mungu maishani mwetu. (1 Petro 5:6, 7; 2 Petro 2:9) Tukifanya hivyo, tutashinda vita tunavyopigana na viumbe waovu wa roho. 19 Lakini kwa nini Mungu ameachilia roho waovu na uovu ambao umefanya watu wateseke sana? Swali hilo litajibiwa katika sura inayofuata.
18, 19. (a) Kwa nini tunaweza kuwa na hakika kwamba tutashinda vita dhidi ya viumbe waovu wa roho? (b) Sura inayofuata itajibu swali gani?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA Malaika waaminifu huwasaidia wale wanaomtumikia Yehova.Waebrania 1:7, 14. Shetani na roho wake waovu wanawapotosha watu na kuwafanya wamwache Mungu. Ufunuo 12:9. Ukifanya mapenzi ya Mungu na kumpinga Ibilisi, Shetani atakukimbia.Yakobo 4:7, 8.

SURA YA KUMI NA MOJA

Kwa Nini Mungu Anawaacha Watu Wateseke?


Je, Mungu ndiye anayesababisha kuteseka ulimwenguni? Ni masuala gani yaliyozushwa katika bustani ya Edeni? Mungu atakomeshaje kuteseka kwa wanadamu?
BAADA ya vita vya kikatili katika nchi moja, maelfu ya wanawake na watoto waliouawa walizikwa kwenye kaburi la ujumla lililozingirwa na misalaba. Kila msalaba ulikuwa na swali hili: Kwa nini? Nyakati nyingine swali hilo huumiza sana. Watu huuliza swali hilo lenye kuhuzunisha wakati vita, msiba, ugonjwa, au uhalifu unaposababisha vifo vya wapendwa wao wasio na hatia, nyumba zao zinapoharibiwa au wanapoteseka sana katika njia nyingine kwa sababu ya vita. Wanataka kujua kwa nini wanapatwa na misiba hiyo. 2 Kwa nini Mungu anawaacha watu wateseke? Ikiwa Yehova Mungu ana nguvu zote, ana upendo, hekima, na haki, kwa nini ulimwengu umejaa chuki na ukosefu wa haki? Je, umewahi kujiuliza maswali hayo? 3 Je, ni vibaya kuuliza kwa nini Mungu anawaacha wanadamu wateseke? Watu fulani huogopa kwamba kuuliza swali kama hilo kutaonyesha kwamba hawana imani au hawamheshimu Mungu. Hata hivyo, unaposoma Biblia utaona
1, 2. Watu wanateseka jinsi gani leo, na hilo huwafanya waulize maswali gani? 3, 4. (a) Sababu gani si vibaya kuuliza kwa nini Mungu anawaacha wanadamu wateseke? (b) Yehova anahisije kuhusu uovu na kuteseka?

107

Yehova atakomesha kabisa kuteseka

kwamba watumishi waaminifu wa Mungu waliuliza maswali kama hayo. Kwa mfano, nabii Habakuki alimuuliza Yehova hivi: Kwa nini unanionyesha jambo lenye kudhuru, nawe unaendelea kutazama taabu tupu? Na kwa nini kuna uporaji na jeuri mbele yangu, kwa nini kugombana hutokea, kwa nini mzozo huendelezwa?Habakuki 1:3. 4 Je, Yehova alimkemea nabii mwaminifu Habakuki kwa kuuliza maswali hayo? Hapana. Badala yake Mungu aliyatia maneno manyoofu ya Habakuki katika Biblia iliyoandikwa kwa mwongozo wa roho. Pia, Mungu alimsaidia kuelewa mambo zaidi na kuwa na imani zaidi. Yehova anataka kukusaidia vivyo hivyo. Kumbuka, Biblia inafundisha kwamba anakujali. (1 Petro 5:7) Hakuna mwanadamu anayechukia uovu na kuteseka kwa wanadamu kama Mungu anavyoyachukia mambo hayo. (Isaya 55:8, 9) Kwa nini basi watu wanateseka sana ulimwenguni?

KWA NINI WATU WANATESEKA SANA?


Watu wa dini mbalimbali wamewauliza viongozi na walimu wao wa dini kuhusu kinachosababisha watu
5

5. Watu fulani husema ni kwa nini watu wanateseka, lakini Biblia inafundisha nini?

108

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

wateseke sana. Mara nyingi, wanaambiwa kwamba ni mapenzi ya Mungu na kwamba ndiye aliyepanga zamani mambo yatakayowapata wanadamu kutia ndani misiba yenye kuhuzunisha. Wengi huambiwa kwamba njia za Mungu haziwezi kueleweka au Mungu husababisha vifo vya watu, hata watoto, ili wakae pamoja naye huko mbinguni. Hata hivyo, kama ulivyojifunza, Yehova Mungu hasababishi mabaya. Biblia inasema: Hasha, Mungu wa kweli asitende kwa uovu, na Mweza-Yote kutenda isivyo haki!Ayubu 34:10. 6 Je, unajua ni kwa nini watu humlaumu Mungu isivyofaa kwa sababu ya mambo yote yanayosababisha kuteseka ulimwenguni? Mara nyingi, wao humlaumu Mungu MwezaYote kwa sababu wanakiri kwamba yeye ndiye anayeutawala ulimwengu huu. Hawajui kweli ya msingi ambayo Biblia hufundisha. Ulijifunza kweli hiyo katika Sura ya 3 ya kitabu hiki. Shetani Ibilisi ndiye anayeutawala ulimwengu huu. 7 Biblia hueleza hivi waziwazi: Ulimwengu mzima unakaa katika nguvu za yule mwovu. (1 Yohana 5:19) Unapokiria hilo, je, huoni ni kwa nini ulimwengu uko jinsi ulivyo leo? Ulimwengu unaonyesha utu wa kiumbe huyo wa roho asiyeonekana, anayeipotosha dunia nzima inayokaliwa. (Ufunuo 12:9) Shetani ana chuki, ni mwongo, na mkatili. Kwa hiyo, ulimwengu ulio chini yake umejaa chuki, uwongo, na ukatili. Hiyo ni sababu moja inayowafanya wanadamu wateseke sana leo. 8 Kama ilivyozungumziwa katika Sura ya 3, sababu ya pili ni kwamba wanadamu si wakamilifu nao wamekuwa watenda-dhambi tangu uasi ulipoanza katika bustani ya Edeni. Wanadamu wenye dhambi hungangania utawala, na hilo hutokeza vita, ukandamizaji, na kuteseka. (Mhubiri 4:1; 8:9)
6. Kwa nini watu wengi humlaumu Mungu isivyofaa kwa sababu ya mambo yanayosababisha kuteseka ulimwenguni? 7, 8. (a) Ulimwengu unaonyeshaje utu wa mtawala wake? (b) Wakati na tukio lisilotazamiwa pamoja na kutokamilika kwa wanadamu kumesababishaje kuteseka?

Kwa Nini Mungu Anawaacha Watu Wateseke?

109

Sababu ya tatu ni wakati na tukio lisilotazamiwa. (Mhubiri 9:11) Katika ulimwengu usiotawaliwa na Yehova, watu wanaweza kuteseka kwa sababu ya kuwa mahali pasipofaa wakati usiofaa. 9 Inatia moyo kujua kwamba Mungu hasababishi kuteseka. Hasababishi vita, uhalifu, ukandamizaji, au hata misiba ya kiasili inayowafanya watu wateseke. Hata hivyo, tunahitaji kujua, Kwa nini Yehova anawaacha wanadamu waendelee kuteseka? Ikiwa yeye ndiye Mweza-Yote, ana nguvu za kukomesha kuteseka. Lakini, kwa nini hachukui hatua? Lazima Mungu mwenye upendo ambaye tumejifunza juu yake awe na sababu nzuri.1 Yohana 4:8.

SUALA MUHIMU LAZUKA


Ili kufahamu ni kwa nini Mungu amewaacha wanadamu waendelee kuteseka, tunahitaji kujikumbusha jinsi kuteseka kulivyoanza. Shetani alipowachochea Adamu na Hawa wamwasi Yehova, suala muhimu lilizuka. Shetani hakupinga nguvu za Yehova. Hata Shetani mwenyewe anajua kwamba nguvu za Yehova hazina kifani. Badala yake, Shetani alipinga haki ya Yehova ya kutawala. Kwa kudai kwamba Mungu ni mwongo anayewanyima raia zake mambo mazuri, Shetani alikuwa akidai kwamba Yehova ni mtawala mbaya. (Mwanzo 3:2-5) Shetani alidokeza kwamba hali ya wanadamu ingekuwa bora pasipo utawala wa Mungu. Alishambulia enzi kuu ya Yehova, haki yake ya kutawala. 11 Adamu na Hawa walimwasi Yehova. Ni kana kwamba walisema: Hatuhitaji kutawaliwa na Yehova. Tunaweza kujiamulia mema na mabaya. Yehova angetatuaje suala hilo? Angewafundishaje viumbe wake wote wenye akili kwamba waasi hao walikosea na kwamba kwa kweli njia yake ndiyo
10

9. Kwa nini tunaweza kuwa na hakika kwamba Yehova ana sababu nzuri ya kuwaacha wanadamu waendelee kuteseka? 10. Shetani alipinga nini, na jinsi gani? 11. Kwa nini Yehova hakuwaangamiza waasi hao katika Edeni?

Je, mwanafunzi ana ujuzi kuliko mwalimu?

bora? Huenda mtu akasema kwamba afadhali Mungu angewaangamiza mara moja waasi hao na kuanza upya. Lakini Yehova alikuwa ametaja kusudi lake kwamba uzao wa Adamu na Hawa ujaze dunia, naye alitaka waishi katika paradiso duniani. (Mwanzo 1:28) Yehova hutimiza makusudi yake sikuzote. (Isaya 55:10, 11) Isitoshe, kuwaangamiza waasi hao katika Edeni hakungejibu suala lililokuwa limezuka kuhusu haki ya Yehova ya kutawala. 12 Hebu tukirie mfano mmoja. Wazia kwamba mwalimu anawafundisha wanafunzi wake jinsi ya kufanya hesabu fulani ngumu. Mwanafunzi mmoja mwerevu lakini mwasi anadai kwamba mwalimu amekosea. Anadai kwamba mwalimu ameshindwa, na mwasi huyo anasisitiza kwamba anajua njia bora zaidi ya kufanya hesabu hiyo. Wanafunzi fulani wanakiri kwamba anasema kweli, nao pia wanaasi. Mwalimu afanye nini? Akiwafukuza waasi hao kutoka darasani, wanafunzi wengine wataonaje? Je, hawataamini kwamba mwanafunzi mwenzao na wale waliojiunga naye
12, 13. Toa mfano unaoonyesha ni kwa nini Yehova amemruhusu Shetani autawale ulimwengu huu na kwa nini Mungu amewaruhusu wanadamu wajitawale.

Kwa Nini Mungu Anawaacha Watu Wateseke?

111

wanasema kweli? Huenda wale wanafunzi wengine walio darasani wakaacha kumwamini mwalimu wao wakikiri kwamba anaogopa kuonyeshwa makosa yake. Basi mwalimu angemruhusu mwasi huyo awaonyeshe wanafunzi wenzake jinsi yeye mwenyewe anavyoweza kufanya hesabu hiyo. 13 Yehova amefanya kama mwalimu huyo anavyofanya. Kumbuka kwamba kuna wengi waliohusika mbali na waasi hao katika Edeni. Mamilioni ya malaika walikuwa wakitazama. (Ayubu 38:7; Danieli 7:10) Njia ya Yehova ya kushughulikia uasi huo ingekuwa na matokeo makubwa sana kwa malaika wote na hatimaye viumbe wote wenye akili. Kwa hiyo, Yehova amefanya nini? Amemruhusu Shetani aonyeshe jinsi anavyoweza kuwatawala wanadamu. Mungu amewaruhusu pia wanadamu wajitawale wenyewe wakiwa chini ya uongozi wa Shetani. 14 Katika mfano uliotolewa, mwalimu anajua kwamba yule mwanafunzi mwasi na wale wanaomuunga mkono wamekosea. Lakini pia anajua kwamba kuwapa nafasi ya kujaribu kuthibitisha madai yao kutawafaidi wanafunzi wote darasani. Waasi hao wakishindwa, wale wanafunzi wengine wote wataona kwamba ni mwalimu wao tu anayestahili kulifundisha darasa. Baadaye, mwalimu akiwafukuza waasi kutoka darasani, wanafunzi wataelewa sababu iliyomfanya awafukuze. Vivyo hivyo, Yehova anajua kwamba wanadamu na malaika wote wanyoofu watafaidika wakiona kwamba Shetani na waasi wenzake wameshindwa na kwamba wanadamu hawawezi kujitawala wenyewe. Kama Yeremia wa zamani, watajifunza ukweli huu muhimu: Ninajua vema, Ee Yehova, kwamba njia ya mtu wa udongo haimo katika uwezo wake. Mwanadamu anayetembea hana uwezo wa kuongoza hatua yake.Yeremia 10:23.
14. Kuna faida gani kwa Yehova kuwaruhusu wanadamu wajitawale wenyewe?

112

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

KWA NINI YEHOVA AMEWAACHA WANADAMU WATESEKE KWA MUDA MREFU?


Hata hivyo, kwa nini Yehova amewaacha wanadamu wateseke kwa muda mrefu? Na kwa nini hazuii mambo mabaya yasitendeke? Katika ule mfano tuliotoa, kiria mambo mawili ambayo yule mwalimu hangefanya. Kwanza, hangemzuia yule mwanafunzi mwasi kutoa madai yake. Pili, mwalimu hangemsaidia mwasi huyo kuthibitisha madai yake. Vivyo hivyo, kuna mambo mawili ambayo Yehova ameazimia kutofanya. Kwanza, hajamzuia Shetani na wale wanaomuunga mkono kujaribu kuthibitisha kwamba wanasema kweli. Ndiyo sababu ameruhusu wakati upite. Kwa maelfu ya miaka katika historia, wanadamu wamejaribu kila aina ya utawala, au serikali za wanadamu. Wanadamu wamefanya maendeleo katika sayansi na katika nyanja nyinginezo, lakini ukosefu wa haki, umaskini, uhalifu, na vita vimeongezeka sana. Sasa imeonekana wazi kwamba utawala wa wanadamu umeshindwa. 16 Pili, Yehova hamsaidii Shetani kuutawala ulimwengu huu. Kama Mungu angezuia uhalifu usitokee, je, hangekuwa anaunga mkono madai ya waasi hao? Je, watu hawangekiri kwamba labda wanadamu wanaweza kujitawala bila matatizo? Kama Yehova angefanya hivyo, angekuwa anaunga mkono uwongo, na Mungu hawezi kamwe kusema uwongo.Waebrania 6:18. 17 Lakini vipi kuhusu madhara ya uasi huo wa muda mrefu kumwelekea Mungu? Tunapaswa kukumbuka kwamba Yehova ni Mweza-Yote. Kwa hiyo, anaweza na ataondoa mambo yanayowafanya wanadamu wateseke. Kama tulivyojifunza, badala ya dunia kuendelea kuharibiwa itageuzwa iwe Paradiso. Matokeo ya dhambi yataondolewa kupitia imani
15

15, 16. (a) Kwa nini Yehova amewaacha wanadamu wateseke kwa muda mrefu? (b) Kwa nini Yehova hazuii mambo kama vile uhalifu? 17, 18. Yehova atachukua hatua gani ili kuondoa madhara ya utawala wa wanadamu na uvutano wa Shetani?

Kwa Nini Mungu Anawaacha Watu Wateseke?

113

katika dhabihu ya dia ya Yesu na ufufuo utatangua matokeo ya kifo. Hivyo, Mungu atamtumia Yesu kuzivunja kazi za Ibilisi. (1 Yohana 3:8) Yehova atatimiza yote hayo wakati unaofaa kabisa. Tunafurahi kwamba hakuchukua hatua kabla ya wakati unaofaa kwa sababu subira yake imetupatia nafasi ya kujifunza kweli na kumtumikia. (2 Petro 3:9, 10) Kwa sasa, Mungu amekuwa akiwatafuta kwa bidii waabudu wanyoofu na kuwasaidia wavumilie mambo yoyote yanayowakumba na yanayowafanya wateseke katika ulimwengu huu wenye taabu. Yohana 4:23; 1 Wakorintho 10:13. 18 Huenda wengine wakauliza, Je, mateso haya yote yangezuiwa iwapo Mungu angewaumba Adamu na Hawa kwa njia ya kwamba hawangeweza kuasi? Ili kujibu swali hilo unahitaji kukumbuka kwamba Yehova amekupa zawadi fulani yenye thamani.

UTAITUMIAJE ZAWADI AMBAYO MUNGU AMEKUPA? 19 Kama tulivyoona katika Sura ya 5, wanadamu waliumbwa wakiwa na uhuru wa kuchagua. Je, unaiona zawadi hiyo kuwa yenye thamani? Mungu ameumba wanyama wengi sana, nao wanaongozwa hasa na silika. (Methali 30:24) Mwanadamu ametengeneza mashine zinazoweza kufuata maagizo. Je, tungefurahi ikiwa Mungu angetuumba hivyo? Hapana, tunafurahi kwa kuwa tuna uhuru wa kuamua tutakuwa watu wa aina gani, tutaishi maisha ya aina gani, tutakuwa na maraki wa aina gani, na kadhalika.
19. Yehova ametupa zawadi gani yenye thamani, na kwa nini tunapaswa kuithamini?

Mungu atakusaidia kuvumilia unapoteseka

114

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Tunapenda kuwa na uhuru, na Mungu anataka tuwe na uhuru. 20 Yehova hapendi watu wamtumikie kwa kulazimishwa. (2 Wakorintho 9:7) Kwa mfano: Ni nini kinachoweza kumfurahisha mzazi zaidimtoto anaposema nakupenda kwa sababu ameambiwa aseme hivyo au anaposema hivyo mwenyewe kutoka moyoni? Kwa hiyo, ni muhimu kukiria swali hili, Wewe utatumiaje uhuru wa kuchagua ambao Yehova amekupa? Shetani, Adamu, na Hawa waliutumia vibaya uhuru wao wa kuchagua. Walimkataa Yehova Mungu. Wewe utafanya nini? 21 Unaweza kuitumia vizuri zaidi zawadi hiyo yenye thamani ya uhuru wa kuchagua. Unaweza kujiunga na mamilioni ya watu ambao wamechukua msimamo upande wa Yehova. Wanamfanya Mungu ashangilie kwa sababu wanashiriki kwa bidii kumthibitisha Shetani kuwa mwongo na mtawala asiyefaa. (Methali 27:11) Wewe pia unaweza kuchagua kuishi maisha yanayofaa. Hilo litafafanuliwa katika sura inayofuata.
20, 21. Tunawezaje kuitumia vizuri zaidi zawadi ya uhuru wa kuchagua, na kwa nini tunapaswa kufanya hivyo?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA Mungu hasababishi hali mbaya zilizo ulimwenguni.Ayubu 34:10. Kwa kudai kwamba Mungu ni mwongo na kusema kwamba Anawanyima raia zake mambo mazuri, Shetani alipinga haki ya Yehova ya kutawala.Mwanzo 3:2-5. Yehova atamtumia Mwana wake, akiwa Mtawala wa Ufalme wa Kimasihi, kukomesha kuteseka kwa wanadamu pamoja na matokeo yake.1 Yohana 3:8.

SURA YA KUMI NA MBILI

Kuishi Maisha Yanayompendeza Mungu


Unawezaje kuwa raki ya Mungu? Dai la Shetani linakuhusuje? Ni mwenendo gani unaomchukiza Yehova? Unawezaje kuishi maisha yanayompendeza Mungu?
UNGEPENDA kuwa na raki wa aina gani? Yaelekea ungependa kushirikiana na mtu aliye na maoni, mapendezi, na viwango kama vyako. Nawe ungevutiwa na mtu mwenye sifa nzuri, kama vile unyoofu na fadhili. 2 Katika historia yote, Mungu aliwachagua wanadamu fulani wawe raki zake wa karibu. Kwa mfano, Yehova alimwita Abrahamu raki yake. (Isaya 41:8; Yakobo 2:23) Mungu alimtaja Daudi kuwa mtu anayekubalika kwa moyo wangu kwa sababu alikuwa na utu unaompendeza Yehova. (Matendo 13:22) Pia, Yehova alimwona nabii Danieli kuwa mtu mwenye kutamanika sana.Danieli 9:23. 3 Kwa nini Yehova aliwaona Abrahamu, Daudi, na Danieli kuwa raki zake? Alimwambia Abrahamu: Umeisikiliza sauti yangu. (Mwanzo 22:18) Kwa hiyo Yehova huwakaribia wale wanaofanya mapenzi yake kwa unyenyekevu. Aliwaambia Waisraeli: Tiini sauti yangu, nami nitakuwa Mungu wenu, nanyi mtakuwa watu wangu. (Yeremia 7:23) Ukimtii Yehova, wewe pia unaweza kuwa raki yake!
1, 2. Taja baadhi ya wanadamu ambao Yehova aliwaona kuwa raki zake wa karibu. 3. Kwa nini Yehova huwachagua wanadamu fulani wawe raki zake?

116

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

YEHOVA HUWAIMARISHA RAFIKI ZAKE


Hebu kiria faida za kuwa raki ya Mungu. Biblia inasema kwamba Yehova anatafuta nafasi ili aonyeshe nguvu zake kwa ajili ya wale ambao moyo wao ni mkamilifu kumwelekea yeye. (2 Mambo ya Nyakati 16:9) Yehova anawezaje kuonyesha nguvu zake kwa ajili yako? Njia moja inatajwa katika Zaburi 32:8, ambapo tunasoma hivi: [Mimi Yehova] nitakufanya uwe na ufahamu na kukufundisha katika njia unayopaswa kuiendea. Nitakupa shauri jicho langu likiwa linakutazama. 5 Maneno hayo yanaonyesha kwamba Yehova anakujali sana. Atakupa mwongozo unaohitaji na kukulinda unapoufuata. Mungu anataka kukusaidia ushinde majaribu. (Zaburi 55:22) Kwa hiyo, ikiwa unamtumikia Yehova kwa moyo kamili, unaweza kuwa na hakika kama mtunga-zaburi aliyesema: Nimemweka Yehova mbele yangu daima. Kwa sababu yuko upande wa mkono wangu wa kuume, sitatikiswa. (Zaburi 16:8; 63:8) Ndiyo, Yehova anaweza kukusaidia uishi maisha yanayompendeza. Lakini, kama unavyojua, kuna adui ya Mungu ambaye anataka kukuzuia usifanye hivyo.
4

DAI LA SHETANI
Sura ya 11 ya kitabu hiki ilieleza jinsi Shetani Ibilisi alivyopinga haki ya Mungu ya kutawala. Shetani alidai kwamba Mungu ni mwongo na kudokeza kwamba Yehova alikuwa akiwakandamiza Adamu na Hawa kwa kuwanyima haki ya kujiamulia yaliyo mema na mabaya. Baada ya Adamu na Hawa kufanya dhambi na wazao wao walipoanza kujaa duniani, Shetani alitilia shaka nia ya wanadamu wote. Shetani alidai kwamba Watu hawamtumikii Mungu kwa sababu wanampenda. Ni kana kwamba alisema, Nikiruhusiwa, ninaweza kumgeuza mtu yeyote aache kumtumikia Mungu. Masimulizi kuhusu Ayubu yanaonyesha kwamba hivyo ndivyo Shetani alivyoamini. Ayubu alikuwa nani, naye alihusikaje katika dai la Shetani?
6

4, 5. Yehova anaonyeshaje nguvu zake kwa ajili ya watu wake? 6. Shetani alidai nini kuhusu wanadamu?

Kuishi Maisha Yanayompendeza Mungu


7

117

Ayubu aliishi miaka 3,600 hivi iliyopita. Alikuwa mtu mzuri, kwa kuwa Yehova alisema: Hakuna yeyote aliye kama yeye duniani, mtu asiye na lawama na mnyoofu, mwenye kumwogopa Mungu na kujiepusha na ubaya. (Ayubu 1:8) Ayubu alimpendeza Mungu. 8 Shetani alitilia shaka nia ya Ayubu kumtumikia Mungu. Ibilisi alimwambia Yehova: Je, wewe hukuweka ukuta kumzunguka yeye [Ayubu] na kuzunguka nyumba yake na kuzunguka kila kitu alicho nacho pande zote? Umeibariki kazi ya mikono yake, na mifugo yake imeenea kotekote duniani. Lakini, ili kuwe na badiliko, tafadhali nyoosha mkono wako, uguse kila kitu alicho nacho, uone kama hatakulaani wewe mbele za uso wako.Ayubu 1:10, 11. 9 Hivyo, Shetani alidai kwamba Ayubu alikuwa akimtumikia Mungu kwa sababu ya vitu alivyokuwa akipata. Pia, Shetani alidai kwamba Ayubu angemwasi Mungu ikiwa angejaribiwa. Yehova alijibuje dai la Shetani? Kwa kuwa suala hilo lilihusisha nia ya Ayubu, Yehova alimruhusu Shetani amjaribu Ayubu. Hivyo, ingeonekana wazi ikiwa Ayubu anampenda Mungu au hampendi.

AYUBU AJARIBIWA
Punde si punde Shetani alianza kumjaribu Ayubu katika njia mbalimbali. Baadhi ya mifugo ya Ayubu iliibiwa na mingine kuuawa. Watumishi wake wengi waliuawa. Hilo lililimletea matatizo ya kiuchumi. Halafu alipata msiba watoto wake kumi walipokufa katika dhoruba. Licha ya matukio hayo yenye kuhuzunisha, Ayubu hakutenda dhambi, wala kumhesabia Mungu jambo lolote lisilofaa.Ayubu 1:22. 11 Shetani hakukata tamaa. Haikosi alikiri kwamba ingawa
10

7, 8. (a) Ni nini kilichomfanya Ayubu awe mtu wa pekee kati ya wanadamu wa wakati huo? (b) Shetani alitiliaje shaka nia ya Ayubu? 9. Yehova alijibuje dai la Shetani, na kwa nini? 10. Ni majaribu gani yaliyompata Ayubu, naye alitendaje? 11. (a) Ni dai gani la pili ambalo Shetani alizusha kumhusu Ayubu, na Yehova aliitikiaje? (b) Ayubu alitendaje baada ya kupata ugonjwa wenye maumivu makali?

Ayubu alipata thawabu kwa sababu ya uaminifu wake

Kuishi Maisha Yanayompendeza Mungu

119

Ayubu angeweza kustahimili kupoteza mali zake, watumishi wake, na watoto wake, angeacha kumtumikia Mungu ikiwa angekuwa mgonjwa. Yehova alimruhusu Shetani amshambulie Ayubu kwa ugonjwa wenye kuchukiza sana na wenye maumivu makali. Lakini hata hilo halikumfanya Ayubu aache kumwamini Mungu. Badala yake, alisema hivi kwa uthabiti: Mpaka nitakapokata pumzi, sitajiondolea utimilifu wangu! Ayubu 27:5. 12 Ayubu hakujua kwamba Shetani ndiye aliyekuwa akisababisha matatizo yake. Kwa kuwa hakujua masuala yaliyozushwa na Ibilisi kuhusu haki ya Yehova ya kutawala, Ayubu alidhani kwamba Mungu ndiye aliyesababisha matatizo yake. (Ayubu 6:4; 16:11-14) Hata hivyo, alidumisha utimilifu wake kwa Yehova. Uaminifu wa Ayubu ulithibitisha kwamba dai la Shetani eti Ayubu alikuwa akimtumikia Mungu kwa sababu za kibinafsi, si la kweli! 13 Uaminifu wa Ayubu ulimwezesha Yehova kujibu dai la Shetani lenye kuleta suto. Kwa kweli Ayubu alikuwa raki ya Yehova, na Mungu alimthawabisha kwa sababu ya uaminifu wake.Ayubu 42:12-17.

JINSI UNAVYOHUSIKA
Suala la utimilifu kwa Mungu lililozushwa na Shetani halikumhusu Ayubu peke yake. Wewe pia unahusika. Hilo linaonyeshwa waziwazi katika Methali 27:11, ambapo Neno la Yehova linasema hivi: Uwe na hekima, mwanangu, na kuufanya moyo wangu ushangilie, ili nipate kumjibu anayenidhihaki. Maneno hayo, yaliyoandikwa mamia ya miaka baada ya Ayubu kufa, yanaonyesha kwamba bado Shetani anamdhihaki Mungu na kuwashtaki watumishi Wake. Tunapoishi maisha yanayompendeza Yehova, tunamsaidia kujibu mashtaka ya uwongo ya Shetani, na
14

12. Ayubu alijibuje dai la Ibilisi? 13. Uaminifu wa Ayubu kwa Mungu ulikuwa na matokeo gani? 14, 15. Kwa nini tunaweza kusema kwamba dai la Shetani kumhusu Ayubu linawahusu wanadamu wote?

120

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

hivyo kuufanya moyo wa Mungu ushangilie. Unahisije kuhusu hilo? Je, si pendeleo kushiriki kujibu madai ya uwongo ya Ibilisi, hata ikiwa utahitaji kufanya mabadiliko fulani maishani mwako? 15 Ona kwamba Shetani alisema: Kila kitu alicho nacho mtu atakitoa kwa ajili ya nafsi yake. (Ayubu 2:4) Aliposema mtu, Shetani alionyesha waziwazi kwamba dai lake liliwahusu wanadamu wote wala si Ayubu tu. Hilo ni jambo muhimu sana. Shetani anatilia shaka utimilifu wako kwa Mungu. Ibilisi angependa kuona ukimwasi Mungu na kuacha kuishi maisha ya uadilifu matatizo yanapotokea. Huenda Shetani akajaribuje kutimiza hilo? 16 Kama tulivyozungumzia katika Sura ya 10, Shetani hutumia njia mbalimbali kujaribu kuwageuza watu waache kumtumikia Mungu. Kwanza, yeye hushambulia kama simba anayenguruma, akitafuta kummeza mtu. (1 Petro 5:8) Hivyo, huenda uvutano wa Shetani ukaonekana wakati ambapo maraki, watu wa ukoo, au wengine wanapopinga jitihada zako za kujifunza Biblia na kuishi kulingana na mambo unayojifunza.1 (Yohana 15:19, 20) Pia, Shetani huendelea kujigeuza mwenyewe kuwa malaika wa nuru. (2 Wakorintho 11:14) Ibilisi anaweza kutumia hila kukupotosha na kukunasa uache kuishi maisha yanayompendeza Mungu. Anaweza pia kutumia mambo yanayovunja moyo, labda kwa kukufanya uhisi kwamba huwezi kumpendeza Mungu. (Methali 24:10) Iwe Shetani anatenda kama simba anayenguruma au anajifanya malaika wa nuru, dai lake ni
1 Hilo halimaanishi kwamba wale wanaokupinga wanaongozwa moja kwa moja na Shetani. Lakini Shetani ndiye mungu wa mfumo huu wa mambo, na ulimwengu wote uko katika nguvu zake. (2 Wakorintho 4:4; 1 Yohana 5:19) Kwa hiyo, tunaweza kutarajia kwamba wengi hawatafurahi kuona ukiishi maisha yanayompendeza Mungu, na baadhi yao watakupinga. 16. (a) Shetani hutumia njia gani kujaribu kuwageuza watu waache kumtumikia Mungu? (b) Ibilisi anawezaje kutumia njia hizo kukunasa?

Kuishi Maisha Yanayompendeza Mungu

121

lilelile: Anasema kwamba unapokabili majaribu au vishawishi, utaacha kumtumikia Mungu. Unaweza kujibuje dai lake na kuthibitisha utimilifu wako kwa Mungu, kama Ayubu alivyofanya?

KUTII AMRI ZA YEHOVA


Unaweza kujibu dai la Shetani kwa kuishi maisha yanayompendeza Mungu. Hilo linahusisha nini? Biblia inajibu hivi: Lazima umpende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa nguvu zako zote. (Kumbukumbu la Torati 6:5) Kadiri upendo wako kwa Mungu unavyoongezeka, ndivyo utakavyotamani hata zaidi kufanya mapenzi yake. Mtume Yohana aliandika: Kumpenda Mungu humaanisha hivi, kwamba tuzishike amri zake. Ukimpenda Yehova kwa moyo wako wote, utaona kwamba amri zake si mzigo mzito.1 Yohana 5:3. 18 Amri za Yehova ni gani? Baadhi yake zinahusu mwenendo tunaopaswa kuepuka. Kwa mfano, ona sanduku lenye kichwa Epuka Mambo Yanayomchukiza Yehova, kwenye ukurasa wa 122. Sanduku hilo lina orodha ya mambo ambayo Biblia inashutumu waziwazi. Huenda baadhi ya mazoea yanayotajwa yasionekane kuwa mabaya sana mwanzoni. Lakini baada ya kutafakari maandiko yaliyotajwa, yaelekea utaona hekima ya sheria za Yehova. Huenda kubadili mwenendo wako kukawa jambo gumu zaidi maishani mwako. Hata hivyo, kuishi maisha yanayompendeza Mungu huridhisha sana na kuleta furaha. (Isaya 48:17, 18) Huo ni mradi ambao wewe unaweza kuukia. Tunajuaje hivyo? 19 Yehova hatarajii kamwe tufanye mambo yanayopita uwezo wetu. (Kumbukumbu la Torati 30:11-14) Anajua uwezo wetu na udhaifu wetu kuliko hata tunavyojijua.
17

17. Tuna sababu gani kuu ya kutii amri za Yehova? 18, 19. (a) Taja baadhi ya amri za Yehova. (Ona sanduku kwenye ukurasa wa 122.) (b) Tunajuaje kwamba Mungu hatarajii tufanye mambo yanayopita uwezo wetu?

122

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

(Zaburi 103:14) Isitoshe, Yehova anaweza kututia nguvu ili tumtii. Mtume Paulo aliandika: Mungu ni mwaminifu, naye hatawaacha ninyi mjaribiwe kupita mnavyoweza kuhimili, bali pamoja na hilo jaribu ataifanya pia njia ya kutokea kusudi mweze kulivumilia. (1 Wakorintho 10:13) Ili kukusaidia kuvumilia, Yehova hata anaweza kukupa nguvu zinazopita zile za kawaida. (2 Wakorintho 4:7) Baada ya kuvumilia majaribu mengi, Paulo angeweza kusema: Kwa mambo yote nina nguvu kupitia yeye anayenipa nguvu.Walipi 4:13.

EPUK A MAMBO YANAYOMCHUKIZ A YEHOVA


Uuaji.Kutoka 20:13; 21:22, 23. Ukosefu wa maadili.
Mambo ya Walawi 20:10, 13, 15, 16; Waroma 1:24, 26, 27, 32; 1 Wakorintho 6:9, 10.

Jeuri.Zaburi 11:5; Methali 22:24, 25; Malaki 2:16; Wagalatia 5:20. Maneno yasiyofaa.
Mambo ya Walawi 19:16; Waefeso 5:4; Wakolosai 3:8.

Kuwasiliana na pepo.
Kumbukumbu la Torati 18: 9-13; 1 Wakorintho 10:21, 22; Wagalatia 5:20, 21.

Kuitumia damu isivyofaa.


Mwanzo 9:4; Matendo 15:20, 28, 29.

Kuabudu sanamu.
1 Wakorintho 10:14.

Kukataa kuiandalia familia.


1 Timotheo 5:8.

Ulevi.1 Wakorintho 5:11. Kuiba.Mambo ya Walawi


6:2, 4; Waefeso 4:28.

Kushiriki katika vita au katika mizozo ya kisiasa ya ulimwengu huu.Isaya 2:4;


Yohana 6:15; 17:16.

Kusema uwongo.
Methali 6:16, 19; Wakolosai 3:9; Ufunuo 22:15.

Kuvuta sigara au kutumia dawa za kulevya.


Marko 15:23; 2 Wakorintho 7:1.

Pupa.1 Wakorintho 5:11.

Kuishi Maisha Yanayompendeza Mungu

123

KUSITAWISHA SIFA ZINAZOMPENDEZA MUNGU


20 Bila shaka, kumpendeza Yehova kunahusisha mengi zaidi kuliko tu kuepuka mambo yanayomchukiza. Unahitaji pia kupenda mambo anayopenda. (Waroma 12:9) Je, huvutiwi na watu walio na maoni, mapendezi, na viwango kama vyako? Yehova huvutiwa na watu kama hao pia. Kwa hiyo, jifunze kupenda mambo ambayo Yehova anapenda. Baadhi ya mambo

20. Ni sifa gani zinazompendeza Mungu unazopaswa kusitawisha, na kwa nini sifa hizo ni muhimu?

124

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

hayo yanatajwa katika Zaburi 15:1-5, ambapo tunasoma kuhusu watu ambao Yehova anawaona kuwa raki zake. Raki za Yehova huonyesha yale yanayoitwa na Biblia, matunda ya roho. Yanatia ndani sifa kama vile upendo, shangwe, amani, ustahimilivu, fadhili, wema, imani, upole, kujizuia.Wagalatia 5:22, 23. 21 Kusoma na kujifunza Biblia kwa ukawaida kutakusaidia kusitawisha sifa zinazompendeza Mungu. Na kujifunza mapenzi ya Mungu kutakusaidia kupatanisha mawazo yako na mawazo ya Mungu. (Isaya 30:20, 21) Kadiri unavyozidisha upendo wako kwa Yehova, ndivyo utakavyotamani hata zaidi kuishi maisha yanayompendeza Mungu. 22 Jitihada inahitajiwa ili kuishi maisha yanayompendeza Yehova. Biblia husema, kubadili maisha yako ni sawa na kuvua utu wako wa kale na kujivika utu mpya. (Wakolosai 3:9, 10) Lakini kuhusu maagizo ya Yehova, mtunga-zaburi aliandika hivi: Katika kuyashika kuna thawabu kubwa. (Zaburi 19:11) Wewe pia utaona kwamba kuishi maisha yanayompendeza Mungu kunaleta thawabu kwelikweli. Kwa kufanya hivyo, utajibu dai la Shetani na kuufanya moyo wa Yehova ushangilie!
21. Ni nini kitakachokusaidia kusitawisha sifa zinazompendeza Mungu? 22. Utatimiza nini kwa kuishi maisha yanayompendeza Mungu?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA


Unaweza kuwa raki ya Mungu kwa kumtii. Yakobo 2:23. Shetani anatilia shaka utimilifu wa wanadamu wote.Ayubu 1:8, 10, 11; 2:4; Methali 27:11. Lazima tuepuke mazoea yanayomchukiza Mungu.1 Wakorintho 6:9, 10. Tunaweza kumpendeza Yehova kwa kuchukia mambo anayochukia na kupenda yale anayopenda.Waroma 12:9.

SURA YA KUMI NA TATU

Maoni ya Mungu Kuhusu Uhai


Mungu anauonaje uhai? Mungu huonaje kutoa mimba? Tunawezaje kuonyesha kwamba tunauheshimu uhai?
NABII Yeremia alisema hivi: Kwa kweli Yehova ni Mungu.
Yeye ndiye Mungu aliye hai. (Yeremia 10:10) Isitoshe, Yehova Mungu ndiye Muumba wa vitu vyote vilivyo hai. Viumbe walio mbinguni walimwambia hivi: Uliumba vitu vyote, na kwa sababu ya mapenzi yako vilikuwako navyo vikaumbwa. (Ufunuo 4:11) Alipokuwa akimwimbia Mungu wimbo wa sifa, Mfalme Daudi alisema hivi: Kwako wewe iko chemchemi ya uzima. (Zaburi 36:9) Kwa hiyo, uhai ni zawadi kutoka kwa Mungu. 2 Pia, Yehova huutegemeza uhai wetu. (Matendo 17:28) Yeye hutuandalia chakula, maji, hewa, na mahali pa kuishi. (Matendo 14:15-17) Yehova amefanya hilo kwa njia inayofanya maisha yawe yenye kufurahisha sana. Lakini, ili tufurahie maisha kikamili, tunahitaji kujifunza sheria za Mungu na kuzitii. Isaya 48:17, 18.

KUUHESHIMU UHAI Mungu anataka tuuheshimu uhai wetu wenyewe na wa wengine. Kwa mfano, katika siku za Adamu na Hawa, mwana wao Kaini alimkasirikia sana Abeli, ndugu yake mdogo. Yehova alimwonya Kaini kwamba hasira yake ingeweza
3

1. Ni nani aliyeumba vitu vyote vilivyo hai? 2. Mungu hufanya nini ili kuutegemeza uhai wetu? 3. Yehova alionaje kuuawa kwa Abeli?

TUNAUHESHIMU UHAI

kwa kutotoa mimba

kwa kuacha
kabisa mazoea machafu

kwa kuacha
kabisa kuwachukia wanadamu wenzetu

Maoni ya Mungu Kuhusu Uhai

127

kumfanya atende dhambi nzito. Kaini alipuuza onyo hilo. Alimshambulia Abeli ndugu yake, akamuua. (Mwanzo 4:3-8) Yehova alimwadhibu Kaini kwa kumuua ndugu yake.Mwanzo 4:9-11. 4 Maelfu ya miaka baadaye, Yehova aliwapa watu wa Israeli sheria zilizowasaidia kumtumikia kwa njia inayompendeza. Kwa sababu sheria hizo zilitolewa kupitia nabii Musa, nyakati nyingine zinaitwa Sheria ya Musa. Mojawapo ya sheria hizo inasema: Usiue. (Kumbukumbu la Torati 5:17) Hilo liliwaonyesha Waisraeli kwamba Mungu anathamini uhai wa wanadamu na kwamba wanadamu wanapaswa kuuthamini uhai wa wengine. 5 Namna gani uhai wa mtoto ambaye hajazaliwa? Kulingana na Sheria ya Musa, ilikuwa kosa kumuua mtoto aliye katika tumbo la mama yake. Ndiyo, hata uhai wa mtoto huyo ni wenye thamani kwa Yehova. (Kutoka 21:22, 23; Zaburi 127:3) Hilo linamaanisha kwamba ni kosa kutoa mimba. 6 Kuuheshimu uhai kunatia ndani kuwa na maoni yanayofaa kuelekea wanadamu wenzetu. Biblia inasema: Kila mtu anayemchukia ndugu yake ni muuaji, nanyi mnajua kwamba hakuna muuaji aliye na uzima wa milele ukikaa ndani yake. (1 Yohana 3:15) Ikiwa tunataka kupata uzima wa milele, tunapaswa kuacha kabisa kuwachukia wanadamu wenzetu, kwa sababu mara nyingi chuki husababisha jeuri. (1 Yohana 3:11, 12) Tunapaswa kujifunza kupendana. 7 Namna gani kuuheshimu uhai wetu wenyewe? Kwa kawaida watu hawapendi kufa, lakini watu fulani huhatarisha uhai wao ili kujifurahisha. Kwa mfano, watu wengi huvuta sigara, hutafuna miraa, au kutumia dawa za kulevya ili kujisisimua.
4. Katika Sheria ya Musa, Mungu alikaziaje maoni yanayofaa kuhusu uhai? 5. Tuoneje kutoa mimba? 6. Kwa nini hatupaswi kuwachukia wanadamu wenzetu? 7. Taja baadhi ya mazoea yanayoonyesha kwamba mtu haheshimu uhai.

128

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Vitu hivyo huudhuru mwili na mara nyingi husababisha kifo. Mtu mwenye mazoea ya kutumia vitu hivyo hauoni uhai kuwa mtakatifu. Mazoea hayo ni machafu machoni pa Mungu. (Waroma 6:19; 12:1; 2 Wakorintho 7:1) Ili kumtumikia Mungu kwa njia inayompendeza, lazima tuache mazoea hayo. Ingawa huenda ikawa vigumu sana kuacha mazoea hayo, Yehova anaweza kutupa msaada tunaohitaji. Naye huthamini tunapojitahidi kuuona uhai wetu kuwa zawadi yenye thamani kutoka kwake. 8 Ikiwa tunauheshimu uhai, tutazingatia usalama. Hatutakuwa wazembe wala kuhatarisha uhai ili kupata raha au msisimuko tu. Tutaepuka kuendesha magari ovyovyo na kushiriki katika michezo yenye jeuri au hatari. (Zaburi 11:5) Sheria ya Mungu aliyowapa Waisraeli wa kale ilisema: Ikiwa utajenga nyumba mpya [yenye paa tambarare], pia utafanya ukuta wa ukingoni kwa ajili ya dari lako, ili usiletee nyumba yako hatia ya damu kwa sababu mtu anaweza kuanguka kutoka hapo. (Kumbukumbu la Torati 22:8) Kupatana na kanuni ya sheria hiyo, ngazi za nyumba zinapaswa kuwa katika hali nzuri ili mtu asijikwae, aanguke, na kuumia vibaya. Ikiwa una gari, hakikisha kwamba ni salama kuliendesha. Makao yako au gari lako lisihatarishe kamwe uhai wako au wa wengine. 9 Namna gani uhai wa wanyama? Huo pia ni mtakatifu kwa Muumba. Mungu anaruhusu kuua wanyama kwa ajili ya chakula na mavazi au ili kuwalinda watu wasipatwe na madhara. (Mwanzo 3:21; 9:3; Kutoka 21:28) Hata hivyo, kuwa mkatili kwa wanyama au kuwaua kwa ajili ya kujifurahisha tu ni kosa na ni kutoheshimu hata kidogo utakatifu wa uhai.Methali 12:10.
10

KUHESHIMU DAMU Baada ya Kaini kumuua Abeli ndugu yake, Yehova ali-

8. Kwa nini tunapaswa kuzingatia usalama? 9. Ikiwa tunauheshimu uhai, tutawatendeaje wanyama? 10. Mungu ameonyeshaje kwamba kuna uhusiano kati ya uhai na damu?

Maoni ya Mungu Kuhusu Uhai

129

mwambia Kaini: Damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika udongo. (Mwanzo 4:10) Mungu alipotaja damu ya Abeli, alikuwa akizungumzia uhai wa Abeli. Kaini alikuwa amekomesha uhai wa Abeli, na sasa ilikuwa lazima Kaini aadhibiwe. Ilikuwa kana kwamba damu ya Abeli, au uhai wake, ulikuwa ukimlilia Yehova ili haki itekelezwe. Uhusiano kati ya uhai na damu ulionyeshwa tena baada ya Mafuriko ya siku ya Noa. Kabla ya Mafuriko hayo, wanadamu walikuwa wakila matunda, mboga, nafaka, na kokwa tu. Baada ya Mafuriko, Yehova alimwambia Noa na wanawe: Kila mnyama anayetembea ambaye yuko hai anaweza kuwa chakula chenu. Kama nilivyowapa mimea ya majani, nawapeni hao wote. Hata hivyo, Mungu alitoa amri hii: Isipokuwa tu nyama pamoja na nafsi yake [au, uhai wake]damu yakemsile. (Mwanzo 1:29; 9:3, 4) Ni wazi kwamba Yehova anahusianisha uhai na damu ya kiumbe. 11 Tunaonyesha kwamba tunaheshimu damu kwa kutoila. Katika Sheria ambayo Yehova aliwapa Waisraeli, aliamuru hivi: Na mtu yeyote . . . ambaye katika kuwinda anamkamata mnyama-mwitu au ndege anayeweza kuliwa, basi ataimwaga damu yake na kuifunika kwa mavumbi. . . . Niliwaambia wana wa Israeli: Hamtakula damu ya mwili wa namna yoyote. (Mambo ya Walawi 17:13, 14) Amri ambayo Mungu alimpa Noa karibu miaka 800 mapema kuhusu kutokula damu ya mnyama bado ilikuwa ikitumika. Maoni ya Yehova yalikuwa wazi: Watumishi wake wangeweza kula nyama ya mnyama lakini si damu yake. Walipaswa kuimwaga chini na hivyo kuurudisha uhai wa kiumbe huyo kwa Mungu. 12 Wakristo pia wanapaswa kufuata amri hiyo. Mitume na wanaume wengine waliokuwa wakiongoza kati ya wafuasi wa Yesu wa karne ya kwanza walikutana ili kuamua ni amri gani zilizopaswa kufuatwa katika kutaniko la Kikristo.
11. Mungu alitoa amri gani kuhusu damu tangu siku za Noa? 12. Ni amri gani kuhusu damu iliyotolewa na roho takatifu katika karne ya kwanza ambayo ingali inatumika leo?

130

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Waliamua hivi: Roho takatifu na sisi wenyewe tumependelea tusiwaongezee ninyi mzigo zaidi, ila mambo haya ya lazima, kuendelea kujiepusha na vitu vilivyotolewa dhabihu kwa sanamu na damu na vitu vilivyonyongwa [bila kutoa damu] na uasherati. (Matendo 15:28, 29; 21:25) Kwa hiyo, lazima tuendelee kujiepusha na damu. Machoni pa Mungu, kujiepusha na damu ni muhimu kama kujiepusha na ibada ya sanamu na uasherati. 13 Je, amri kuhusu kujiepusha na damu inahusu kutiwa damu mishipani? Ndiyo. Kwa mfano: Tuseme daktari angekuambia ujiepushe na pombe. Je, hilo lingemaanisha kwamba hupaswi kunywa pombe lakini unaweza kutiwa pombe mishipani mwako? Bila shaka hapana! Vivyo hivyo, kujiepusha na damu kunamaanisha kutoitia mwilini kwa njia yoyote ile. Kwa hiyo, amri ya kujiepusha na damu inamaanisha kwamba hatutamruhusu mtu yeyote atutie damu mishipani. 14 Namna gani ikiwa Mkristo amejeruhiwa vibaya au anahitaji kufanyiwa upasuaji mkubwa? Huenda madaktari wakasema kwamba anapaswa kutiwa damu mishipani, la sivyo atakufa. Bila shaka, Mkristo hangependa kufa. Atajitahidi kuulinda uhai ambao ni zawadi yenye thamani kutoka kwa Mungu kwa kukubali matibabu ya aina nyingine ambayo hayahusishi matumizi yasiyofaa ya damu. Hivyo, atatafuta matibabu ya aina hiyo ikiwezekana na kukubali njia nyingine za tiba zisizotia ndani damu. 15 Je, Mkristo avunje sheria ya Mungu ili aishi muda mrefu kidogo katika mfumo huu wa mambo? Yesu alisema: Kwa maana yeyote yule anayetaka kuiokoa nafsi yake [au uhai] ataipoteza; lakini yeyote yule anayeipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataipata. (Mathayo 16:25) Hatutaki kufa. Lakini tukijaribu kuokoa uhai wetu wa sasa kwa kuvunja sheria ya Mungu,
13. Toa mfano unaoonyesha kwamba amri ya kujiepusha na damu inahusu kutiwa damu mishipani. 14, 15. Ikiwa madaktari wanasema kwamba Mkristo anapaswa kutiwa damu mishipani, afanyeje, na kwa nini?

Maoni ya Mungu Kuhusu Uhai

tutakuwa katika hatari ya kupoteza uzima wa milele. Basi ni jambo la hekima kutumaini sheria ya Mungu ya uadilifu, tukiwa na hakika kwamba ikiwa tutakufa kwa sababu yoyote ile, MpajiUhai wetu atatukumbuka katika ufufuo na kuturudishia uhai ambao ni zawadi yenye thamani.Yohana 5:28, 29; Waebrania 11:6. 16 Watumishi waaminifu wa Mungu leo, huazimia kwa uthabiti kufuata amri ya Mungu kuhusu damu. Hawawezi kula damu kwa njia yoyote ile. Wala hawawezi kukubali damu kwa sababu za matibabu.1 Wana hakika kwamba Mungu, aliyeumba damu anajua kinachowafaa. Je, unaamini kwamba anajua?

MATUMIZI PEKEE YANAYOFAA YA DAMU Ikiwa daktari angekwambia 17 Sheria ya Musa ilikazia njia moja tu ujiepushe na pombe, inayofaa ya kutumia damu. Kuhusu ibaje, ungekubali itiwe da ya Waisraeli wa kale, Yehova aliamuru mishipani mwako? hivi: Nafsi ya [au, uhai wa] mwili iko katika damu, nami mwenyewe nimeiweka juu ya madhabahu ili ninyi mfanye upatanisho kwa ajili ya nafsi zenu, kwa sababu damu ndiyo hufanya upatanisho. (Mambo ya Walawi 17:11) Waisraeli walipofanya dhambi,
1 Unaweza kupata habari kuhusu matibabu yasiyohusisha kutiwa damu mishipani kwenye ukurasa wa 13-17 wa broshua Damu Yaweza Kuokoaje Uhai Wako? iliyochapishwa na Mashahidi wa Yehova. 16. Watumishi wa Mungu huazimia nini kwa uthabiti kuhusu damu? 17. Yehova Mungu alikubali damu itumiwe kwa njia gani ya pekee katika Israeli la kale?

132

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

walipata msamaha kwa kutoa dhabihu ya mnyama na kiasi fulani cha damu yake kilitiwa kwenye madhabahu katika maskani au baadaye kwenye hekalu la Mungu. Njia pekee iliyofaa ya kutumia damu ilikuwa kwa ajili ya dhabihu kama hizo. 18 Wakristo wa kweli hawako chini ya Sheria ya Musa na hivyo hawatoi dhabihu za wanyama na kuweka damu kwenye madhabahu. (Waebrania 10:1) Hata hivyo, kutumiwa kwa damu kwenye madhabahu katika Israeli la kale kuliwakilisha dhabihu ya mwisho na yenye thamani sana ya Mwana wa Mungu, Yesu Kristo. Kama tulivyojifunza katika Sura ya 5 ya kitabu hiki, Yesu alitoa uhai wake wa kibinadamu kwa ajili yetu kwa kuruhusu damu yake imwagwe ikiwa dhabihu. Kisha alienda mbinguni na kumtolea Mungu mara moja kwa
18. Tunaweza kupata baraka gani kupitia kwa damu ya Yesu iliyomwagwa?

Unaweza kuonyeshaje kwamba unathamini uhai na damu?

Maoni ya Mungu Kuhusu Uhai

133

wakati wote thamani ya damu yake iliyomwagwa. (Waebrania 9:11, 12) Kwa kufanya hivyo, aliweka msingi wa msamaha wa dhambi zetu na kutufungulia njia ya kupata uzima wa milele. (Mathayo 20:28; Yohana 3:16) Njia hiyo ya kutumia damu imethibitika kuwa muhimu sana! (1 Petro 1:18, 19) Tunaweza tu kupata wokovu kwa kuthamini damu ya Yesu iliyomwagwa. 19 Tunapaswa kumshukuru Yehova Mungu sana kwa sababu ya kutupa zawadi ya uhai kwa upendo! Je, hilo halipaswi kutuchochea kuwaambia wengine kuhusu pendeleo la kupata uzima wa milele kwa msingi wa imani katika dhabihu ya Yesu? Ikiwa tunathamini uhai wa wanadamu wenzetu kama Mungu anavyouthamini, tutachochewa kuwahubiria kwa hamu na bidii. (Ezekieli 3:17-21) Tukitimiza jukumu hilo kwa bidii, tutaweza kusema kama mtume Paulo alivyosema: Mimi ni sa kutokana na damu ya watu wote, kwa maana sikuepuka kuwaambia ninyi mashauri yote ya Mungu. (Matendo 20:26, 27) Kuwahubiria watu kumhusu Mungu na makusudi yake ni njia bora ya kuonyesha kwamba tunathamini sana uhai na damu.
19. Ni lazima tufanye nini ili tuwe sa kutokana na damu ya watu wote?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA


Uhai ni zawadi kutoka kwa Mungu. Zaburi 36:9; Ufunuo 4:11. Ni kosa kutoa mimba kwa sababu uhai wa mtoto ambaye hajazaliwa ni wenye thamani machoni pa Mungu.Kutoka 21:22, 23; Zaburi 127:3. Tunaonyesha kwamba tunaheshimu uhai kwa kutouhatarisha na kutokula damu. Kumbukumbu la Torati 5:17; Matendo 15:28, 29.

SURA YA KUMI NA NNE

Jinsi ya Kufanya Maisha ya Familia Yako Yawe Yenye Furaha


Ni nini kinachohitajiwa ili kuwa mume mzuri? Mwanamke anawezaje kufaulu kutimiza jukumu lake akiwa mke? Ni nini kinachohitajiwa ili kuwa mzazi mzuri? Watoto wanaweza kufanya nini ili maisha ya familia yawe yenye furaha?
YEHOVA MUNGU anataka familia yako iwe na maisha yenye furaha. Neno lake, Biblia, hutoa maagizo kwa kila mmoja katika familia na kuonyesha jukumu ambalo Mungu anataka kila mmoja atekeleze. Kila mmoja katika familia akitimiza jukumu lake kulingana na shauri la Mungu, familia itakuwa na furaha sana. Yesu alisema: Wenye furaha ni wale wanaolisikia neno la Mungu na kulishika!Luka 11:28. 2 Furaha ya familia inategemea hasa kutambua kwamba familia ilianzishwa na Yehova, ambaye Yesu alimwita Baba yetu. (Mathayo 6:9) Baba yetu wa mbinguni ndiye aliyeanzisha kila familia duniani na bila shaka anajua kinacholeta furaha katika familia. (Waefeso 3:14, 15) Kwa hiyo, Biblia inafundisha nini kuhusu jukumu la kila mmoja katika familia?
3

FAMILIA ILIANZISHWA NA MUNGU Yehova aliwaumba wanadamu wa kwanza, Adamu na

1. Ni nini siri ya kuwa na familia yenye furaha? 2. Furaha ya familia inategemea kutambua nini? 3. Biblia inaelezaje mwanzo wa familia ya wanadamu, na tunajuaje kwamba yale inayosema ni ya kweli?

Jinsi ya Kufanya Maisha ya Familia Yako Yawe Yenye Furaha

135

Hawa, na kuwaunganisha kuwa mume na mke. Aliwaweka katika paradiso maridadi hapa duniani, bustani ya Edeni, na kuwaambia wazae watoto. Yehova alisema: Zaeni, muwe wengi, mjaze dunia. (Mwanzo 1:26-28; 2:18, 21-24) Hii si hadithi au jambo la kukisiwa tu, kwa sababu Yesu alionyesha kwamba yale ambayo kitabu cha Mwanzo kinasema kuhusu mwanzo wa familia ni ya kweli. (Mathayo 19:4, 5) Ingawa tunapata matatizo mengi na maisha leo hayako kama Mungu alivyokusudia, hebu tuone ni kwa nini familia inaweza kuwa na furaha. 4 Kila mmoja katika familia anaweza kuchangia furaha ya familia kwa kumwiga Mungu katika kuonyesha upendo. (Waefeso 5:1, 2) Hata hivyo, tunawezaje kumwiga Mungu na hatuwezi kumwona? Tunaweza kujifunza jinsi Yehova anavyotenda kwa sababu alimtuma Mwana wake mzaliwa wa kwanza kutoka mbinguni kuja duniani. (Yohana 1:14, 18) Alipokuwa duniani, Mwana huyo, Yesu Kristo, alimwiga sana Baba yake wa mbinguni hivi kwamba kumwona na kumsikiliza Yesu kulikuwa sawa na kuwa pamoja na Yehova na kumsikiliza. (Yohana 14:9) Kwa hiyo, kila mmoja wetu anaweza kuchangia zaidi furaha ya familia kwa kujifunza kuhusu upendo ambao Yesu alionyesha na kufuata mfano wake.

KIELELEZO KWA WAUME Biblia inasema kwamba waume wanapaswa kuwatendea wake zao jinsi Yesu alivyowatendea wanafunzi wake. Fikiria mwongozo huu wa Biblia: Waume, endeleeni kuwapenda wake zenu, kama vile Kristo pia alivyolipenda kutaniko na kujitoa mwenyewe kwa ajili yake . . . Vivyo hivyo, waume wanapaswa kuwa wakiwapenda wake zao kama miili
5

4. (a) Kila mmoja katika familia anawezaje kuchangia furaha ya familia? (b) Kwa nini familia itapata furaha ikijifunza kuhusu maisha ya Yesu? 5, 6. (a) Waume wanajifunza nini kutokana na jinsi Yesu anavyolitendea kutaniko? (b) Mtu anapaswa kufanya nini ili asamehewe dhambi zake?

136

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

yao wenyewe. Yeye anayempenda mke wake anajipenda mwenyewe, kwa maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake kwa vyovyote; bali huulisha na kuutunza kwa upendo, kama vile Kristo pia anavyolitendea kutaniko.Waefeso 5:23, 25-29. 6 Upendo wa Yesu kwa wanafunzi wake ni kielelezo bora kwa waume. Yesu aliwapenda mpaka mwisho, akadhabihu uhai wake kwa ajili yao, hata ingawa hawakuwa wakamilifu. (Yohana 13:1; 15:13) Vivyo hivyo, waume wanahimizwa hivi: Endeleeni kuwapenda wake zenu nanyi msiwakasirikie kwa uchungu. (Wakolosai 3:19) Ni nini kitakachomsaidia mume kufuata shauri hilo, hasa ikiwa nyakati nyingine mke wake hatendi kwa busara? Anapaswa kukumbuka makosa yake na anachopaswa kufanya ili kupata msamaha wa Mungu. Anapaswa kufanya nini? Anapaswa kumsamehe kila mtu anayemkosea, kutia ndani mke wake. Bila shaka, mke anapaswa kufanya vivyo hivyo. (Mathayo 6:12, 14, 15) Je, unaona ni kwa nini watu fulani husema kwamba ili ndoa zifanikiwe lazima wenzi wote wawili wawe tayari kusameheana? 7 Waume wanapaswa kukumbuka pia kwamba sikuzote Yesu aliwajali wanafunzi wake. Alizingatia udhaifu wao na mahitaji yao ya kimwili. Kwa mfano, alisema hivi walipokuwa wamechoka: Njooni, ninyi wenyewe, faraghani katika mahali pasipo na watu mpumzike kidogo. (Marko 6:30-32) Wake pia wanastahili kuhangaikiwa kwa upendo. Biblia husema kwamba wao ni chombo dhaifu zaidi na waume wanaamriwa wawape heshima. Kwa nini? Kwa kuwa waume na wake pia wanashiriki pendeleo lisilostahiliwa la uzima. (1 Petro 3:7) Waume wanapaswa kukumbuka kwamba Mungu hupendezwa na uaminifu wa mtu wala si jinsia yake.Zaburi 101:6. 8 Biblia inasema kwamba mume anayempenda mke wake anajipenda mwenyewe. Hiyo ni kwa sababu mume na mke si wawili tena, bali mwili mmoja, kama Yesu alivyosema.
7. Yesu alizingatia nini, naye aliwawekea waume kielelezo gani? 8. (a) Mume anayempenda mke wake, anajipendaje mwenyewe? (b) Inamaanisha nini kwamba mume na mke ni mwili mmoja?

Jinsi ya Kufanya Maisha ya Familia Yako Yawe Yenye Furaha

137

(Mathayo 19:6) Hivyo basi, hawapaswi kufanya ngono na mtu mwingine yeyote. (Methali 5:15-21; Waebrania 13:4) Wataepuka kufanya hivyo ikiwa kila mmoja anajali mahitaji ya yule mwingine bila ubinafsi. (1 Wakorintho 7:3-5) Kikumbusho hiki pia kinafaa: Hakuna mtu anayeuchukia mwili wake kwa vyovyote; bali huulisha na kuutunza kwa upendo. Waume wanapaswa kuwapenda wake zao kama wanavyojipenda wenyewe, wakikumbuka kwamba watatoa hesabu kwa Yesu Kristo, aliye kichwa chao.Waefeso 5:29; 1 Wakorintho 11:3. 9 Mtume Paulo alizungumzia upendo mwororo alio nao Kristo Yesu. (Walipi 1:8) Wororo wa Yesu ulikuwa sifa yenye kuburudisha, iliyowavutia wanawake ambao walikuwa wanafunzi wake. (Yohana 20:1, 11-13, 16) Nao wake hutamani sana waume zao wawapende kwa wororo.

KIELELEZO KWA WAKE Familia ni kama shirika, na ili lifanye kazi vizuri, linahitaji kuwa na kichwa. Hata Yesu anajitiisha kwa Yule aliye Kichwa chake. Kichwa cha Kristo ni Mungu kama vile kichwa cha mwanamke ni mwanamume. (1 Wakorintho 11:3) Kujitiisha kwa Yesu chini ya ukichwa wa Mungu ni mfano mzuri kwa kuwa sote tuna kichwa ambaye tunapaswa kujitiisha kwake. 11 Wanaume wasio wakamilifu hufanya makosa na mara nyingi wao hupungukiwa katika jukumu lao la kuwa vichwa vya familia. Kwa hiyo, mke anapaswa kufanya nini? Hapaswi kudharau mambo ambayo mume wake anafanya au kujaribu kumnyanganya ukichwa. Mke anapaswa kukumbuka kwamba roho ya utulivu na upole ina thamani kubwa
10

9. Ni sifa gani ya Yesu inayotajwa katika Walipi 1:8, na kwa nini waume wanapaswa kuwaonyesha wake zao sifa hiyo? 10. Yesu anawawekeaje wake mfano? 11. Mke anapaswa kumwonaje mume wake, na mwenendo wake unaweza kuwa na matokeo gani?

138

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

machoni pa Mungu. (1 Petro 3:4) Akiwa na roho hiyo, itakuwa rahisi kwake kuonyesha utii wa kimungu hata katika hali ngumu. Isitoshe, Biblia inasema: Mke anapaswa kumheshimu sana mume wake. (Waefeso 5:33) Lakini vipi akikataa kujitiisha chini ya Kristo akiwa Kichwa chake? Biblia inawasihi wake hivi: Jitiisheni kwa waume zenu wenyewe, ili, ikiwa wowote si watiifu kwa lile neno, wavutwe bila neno kupitia mwenendo wa wake zao, kwa sababu wamekwisha kushuhudia kwa macho mwenendo wenu ulio sa kiadili pamoja na heshima kubwa.1 Petro 3:1, 2. 12 Mume awe ni mwamini au la, mke hatakuwa akimvunjia heshima ikiwa ataeleza maoni yake kwa njia ya busara hata kama yanatofautiana na ya mume. Huenda maoni yake yakawa sawa, na yanaweza kufaidi familia nzima ikiwa mume atamsikiliza. Ingawa Abrahamu hakukubaliana na mke wake Sara alipopendekeza jinsi ya kutatua tatizo fulani la familia, Mungu alimwambia: Sikiliza sauti yake. (Mwanzo 21:9-12) Bila shaka, mume anapofanya uamuzi ambao haupingani na sheria ya Mungu, mke wake anapaswa kuonyesha anajitiisha kwake kwa kuunga mkono uamuzi huo.Matendo 5:29; Waefeso 5:24. 13 Mke anaweza kutimiza jukumu lake kwa kutunza familia. Kwa mfano, Biblia inaonyesha kwamba wanawake ambao wameolewa wanapaswa kuwapenda waume zao, kuwapenda watoto wao, kuwa na utimamu wa akili, sa kiadili, wafanyakazi nyumbani, wema, wakijitiisha kwa waume zao wenyewe. (Tito 2:4, 5) Mke ambaye pia ni mama anayefanya hivyo, atapendwa na kuheshimiwa daima na familia yake. (Methali 31:10, 28) Lakini kwa kuwa ndoa ni muungano wa watu wasio wakamilifu, huenda hali fulani wasizoweza kuvumilia zikawafanya watengane au kutalikiana. Biblia inaruhusu kutengana hali
12. Kwa nini si kosa mke kueleza maoni yake kwa heshima? 13. (a) Andiko la Tito 2:4, 5 linawasihi wanawake ambao wameolewa wafanye nini? (b) Biblia inasema nini kuhusu kutengana na kutalikiana?

Sara aliwawekea wake mfano gani mzuri?

fulani zinapotokea. Hata hivyo, kutengana hakupaswi kuchukuliwa kivivi hivi tu, kwa kuwa Biblia inashauri: Mke hapaswi kuondoka kwa mume wake; . . . na mume hapaswi kumwacha mke wake. (1 Wakorintho 7:10, 11) Msingi pekee wa Kimaandiko wa talaka ni uasherati.Mathayo 19:9.

MFANO BORA KWA WAZAZI Yesu aliwawekea wazazi mfano bora wa jinsi ya kuwatendea watoto. Wengine walipojaribu kuwazuia watoto wadogo wasimkaribie, Yesu alisema hivi: Waacheni watoto wachanga waje kwangu; msijaribu kuwazuia. Kisha Biblia inasema kwamba aliwachukua watoto akawakumbatia na kuanza kuwabariki, akiweka mikono yake juu yao. (Marko 10:13-16) Kwa kuwa Yesu alitumia wakati pamoja na watoto, je, hupaswi kufanya hivyo na watoto wako? Wanahitaji wakati wako mwingi. Unahitaji kutumia wakati kuwafundisha kwani Yehova anawaagiza wazazi wafanye hivyo.Kumbukumbu la Torati 6:4-9. 15 Kadiri ulimwengu huu unavyozidi kuwa mbovu, ndivyo
14

14. Yesu aliwatendeaje watoto, nao watoto wanahitaji nini kutoka kwa wazazi wao? 15. Wazazi wanaweza kufanya nini ili kuwalinda watoto wao?

140

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

watoto wanavyohitaji wazazi watakaowalinda dhidi ya watu wanaotaka kuwaumiza, kama wale wanaowatendea vibaya watoto kingono. Fikiria jinsi Yesu alivyowalinda wanafunzi wake ambao aliwapenda sana na kuwaita watoto wadogo. Alipokamatwa ili auawe baadaye, Yesu alifanya mipango ili wanafunzi wake watoroke. (Yohana 13:33; 18:7-9) Ukiwa mzazi, unapaswa kuwa macho kuona njia ambazo Ibilisi anatumia kujaribu kuwaumiza watoto wako. Unahitaji kuwaonya mapema.1 (1 Petro 5:8) Huu ndio wakati ambapo hali yao ya kimwili, ya kiroho, na ya kiadili imo hatarini zaidi kuliko wakati mwingine wowote.
1 Habari kuhusu jinsi ya kuwalinda watoto zinapatikana katika sura ya 32 ya kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

Wazazi wanaweza kujifunza nini kutokana na jinsi Yesu alivyowatendea watoto?

Jinsi ya Kufanya Maisha ya Familia Yako Yawe Yenye Furaha


16

141

Usiku uliotangulia kifo cha Yesu, wanafunzi wake walibishana kuhusu ni nani aliye mkubwa kati yao. Kwa kuwa Yesu aliwapenda, badala ya kuwakasirikia, aliendelea kuwasihi kwa maneno na kuwawekea mfano. (Luka 22:24-27; Yohana 13:3-8) Ikiwa wewe ni mzazi, je, unaona jinsi unavyoweza kufuata mfano wa Yesu unapowarekebisha watoto wako? Ni kweli kwamba wanahitaji nidhamu, lakini inapaswa kutolewa kwa kiwango kinachofaa wala si kwa hasira. Hupaswi kuzungumza nao bila kukiri kama kwa upanga unaochoma. (Yeremia 30:11; Methali 12:18) Nidhamu inapaswa kutolewa kwa njia ambayo mtoto ataithamini baadaye.Waefeso 6:4; Waebrania 12:9-11.

MFANO KWA WATOTO Je, watoto wanaweza kujifunza kutoka kwa Yesu? Ndiyo, wanaweza! Kupitia mfano wake, Yesu alionyesha jinsi watoto wanavyopaswa kuwatii wazazi wao. Alisema: Kama vile Baba alivyonifundisha, ndivyo ninavyosema. Akaongezea: Sikuzote mimi hufanya mambo yanayompendeza. (Yohana 8:28, 29) Yesu alimtii Baba yake wa mbinguni, na Biblia inawaambia watoto wawatii wazazi wao. (Waefeso 6:1-3) Ingawa Yesu alikuwa mtoto mkamilifu, aliwatii wazazi wake, Yusufu na Maria, ambao hawakuwa wakamilifu. Hapana shaka kwamba hilo lilichangia furaha ya kila mmoja katika familia ya Yesu!Luka 2: 4, 5, 51, 52. 18 Je, watoto wanaweza kutambua njia wanazoweza kumwiga Yesu zaidi na kuwafurahisha wazazi wao? Ni kweli kwamba nyakati nyingine watoto huona ni vigumu kuwatii wazazi wao, hata hivyo, Mungu anataka watoto watii. (Methali 1:8; 6:20) Yesu alimtii Baba yake wa mbinguni sikuzote, hata hali zilipokuwa ngumu. Pindi moja, Mungu alipomtaka Yesu afanye
17

16. Wazazi wanaweza kujifunza nini kutokana na njia ambayo Yesu alishughulikia kutokamilika kwa wanafunzi wake? 17. Yesu aliwawekea watoto mfano bora katika njia zipi? 18. Kwa nini Yesu alimtii Baba yake wa mbinguni sikuzote, na watoto humfurahisha nani wanapowatii wazazi wao leo?

142

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

jambo gumu sana, Yesu alisema: Niondolee kikombe hiki [au takwa fulani]. Hata hivyo, Yesu alifanya mapenzi ya Mungu kwa sababu alitambua kwamba Baba yake anajua mwendo bora wa kufuata. (Luka 22:42) Kwa kujifunza kutii, watoto watawafurahisha wazazi wao na Baba yao wa mbinguni.1Methali 23:22-25. 19 Ibilisi alimshawishi Yesu, na tunaweza kuwa na hakika kwamba atawashawishi watoto pia wafanye mambo mabaya. (Mathayo 4:1-10) Shetani Ibilisi hutumia mikazo ya maraki ambayo inaweza kuwa mikali sana. Basi ni muhimu sana watoto wasishirikiane na wale wanaotenda mabaya. (1 Wakorintho 15:33) Dina, binti ya Yakobo alishirikiana na watu ambao hawakuwa wakimwabudu Yehova, na kufanya hivyo kulimletea matatizo makubwa. (Mwanzo 34:1, 2) Hebu wazia jinsi familia inavyoweza kuumia mmoja wao akihusika katika mwenendo mpotovu kingono!Methali 17:21, 25.
20

SIRI YA KUWA NA FAMILIA YENYE FURAHA Shauri la Biblia linapotumiwa, inakuwa rahisi kukabiliana
1 Mtoto ana haki ya kutotii ikiwa mzazi anamwomba avunje sheria ya Mungu.Matendo 5:29. 19. (a) Shetani huwashawishi watoto jinsi gani? (b) Mwenendo mbaya wa watoto unaweza kuwaathirije wazazi? 20. Ili kuwa na maisha ya familia yenye furaha, kila mmoja katika familia anapaswa kufanya nini?

Vijana wanapaswa kuzingatia nini wanaposhawishiwa?

Jinsi ya Kufanya Maisha ya Familia Yako Yawe Yenye Furaha

143

na matatizo katika familia. Kutumia shauri hilo ndiyo siri ya kuwa na familia yenye furaha. Kwa hiyo waume, wapendeni wake zenu na kuwatendea kama Yesu anavyolitendea kutaniko lake. Wake, tiini ukichwa wa waume zenu na mfuate mfano wa mke mwenye uwezo anayetajwa katika Methali 31: 10-31. Wazazi, wazoezeni watoto wenu. (Methali 22:6) Akina baba, simamieni nyumba zenu kwa njia nzuri. (1 Timotheo 3:4, 5; 5:8) Nanyi watoto, watiini wazazi wenu. (Wakolosai 3:20) Hakuna yeyote katika familia aliye mkamilifu kwa kuwa wote hufanya makosa. Kwa hiyo, nyenyekeeni na kuombana msamaha. 21 Kwa kweli, Biblia ina mashauri na maagizo mengi yenye faida kuhusu maisha ya familia. Isitoshe, Biblia hutufundisha kuhusu ulimwengu mpya wa Mungu na paradiso ya kidunia itakayojaa watu wenye furaha wanaomwabudu Yehova. (Ufunuo 21:3, 4) Hilo ni tarajio zuri kama nini! Hata sasa, tunaweza kuwa na maisha ya familia yenye furaha kwa kufuata maagizo ya Mungu yaliyo katika Neno lake, Biblia.
21. Tuna tarajio gani zuri, na tunawezaje kuwa na maisha ya familia yenye furaha sasa?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA


Waume wanapaswa kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Waefeso 5:25-29. Wake wanapaswa kuipenda familia yao na kuwaheshimu waume zao.Tito 2:4, 5. Wazazi wanapaswa kuwapenda, kuwafundisha, na kuwalinda watoto wao. Kumbukumbu la Torati 6:4-9. Watoto wanapaswa kuwatii wazazi wao. Waefeso 6:1-3.

SURA YA KUMI NA TANO

Ibada Ambayo Mungu Anakubali


Je, dini zote zinampendeza Mungu? Tunaweza kuitambuaje dini ya kweli? Ni nani walio waabudu wa kweli wa Mungu duniani leo?
YEHOVA MUNGU anatujali sana na anataka tufaidike na mwongozo wake wenye upendo. Tukimwabudu kwa njia inayofaa, tutakuwa wenye furaha na tutaepuka matatizo mengi maishani. Pia tutapata baraka na msaada wake. (Isaya 48:17) Hata hivyo, kuna mamia ya dini ambazo hudai kwamba zinafundisha kweli kumhusu Mungu. Lakini zinatofautiana katika mafundisho yao kumhusu Mungu na mapenzi yake. 2 Unawezaje kujua njia inayofaa ya kumwabudu Yehova? Si lazima ujifunze na kulinganisha mafundisho ya dini zote. Unahitaji tu kujifunza yale ambayo Biblia inafundisha hasa kuhusu dini ya kweli. Kwa mfano: Katika nchi nyingi kuna tatizo la pesa bandia. Unawezaje kutofautisha pesa halali na pesa bandia? Je, unahitaji kuchunguza pesa zote bandia? Hapana. Ingekuwa afadhali kama ungechunguza na kujua pesa halali. Baada ya kujua jinsi pesa halali zinavyoonekana, unaweza kutambua pesa bandia. Vivyo hivyo, tunaweza kutambua dini za uwongo kwa kujifunza kutambua dini ya kweli. 3 Ni muhimu tumwabudu Yehova katika njia anayokuba1. Tutapata faida gani tukimwabudu Mungu kwa njia inayofaa? 2. Tunawezaje kujua njia inayofaa ya kumwabudu Yehova, na ni mfano gani unaotusaidia kuelewa jambo hilo? 3. Yesu alisema tunapaswa kufanya nini ili tupate kibali cha Mungu?

Ibada Ambayo Mungu Anakubali

145

li. Watu wengi huamini kwamba dini zote zinampendeza Mungu, lakini Biblia haifundishi hivyo. Hata haitoshi tu kudai kuwa Mkristo. Yesu alisema: Si kila mtu anayeniambia, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni, bali yule anayefanya mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni ndiye atakayeingia. Kwa hiyo, ili tuwe na kibali cha Mungu, lazima tujifunze mapenzi ya Mungu na kuyafanya. Yesu aliwaita wale wasiofanya mapenzi ya Mungu wenye matendo ya uasi-sheria. (Mathayo 7:21-23) Dini ya uwongo haina thamani yoyote kama vile pesa bandia zisivyo na thamani. Isitoshe, dini hizo ni hatari. 4 Yehova anampa kila mtu duniani nafasi ya kupata uzima wa milele. Hata hivyo, ili tuishi milele katika Paradiso, ni lazima tumwabudu Mungu kwa njia inayofaa na tuishi maisha yanayompendeza. Inasikitisha kwamba wengi hukataa kufanya hivyo. Ndiyo sababu Yesu alisema: Ingieni kupitia lango jembamba; kwa sababu barabara inayoongoza kwenye uharibifu ni pana na kubwa, na wengi ndio wanaoipitia; lakini lango ni jembamba na barabara inayoongoza kwenye uzima ina nafasi ndogo, na wachache ndio wanaoipata. (Mathayo 7:13, 14) Dini ya kweli inaongoza kwenye uzima wa milele. Dini ya uwongo inaongoza kwenye uharibifu. Yehova hataki mwanadamu yeyote aharibiwe na ndiyo sababu anawapa watu wote nafasi ya kujifunza kumhusu. (2 Petro 3:9) Hivyo basi, uhai wetu unategemea jinsi tunavyomwabudu Mungu.

JINSI YA KUITAMBUA DINI YA KWELI Barabara inayoongoza kwenye uzima inaweza kupatikanaje? Yesu alisema kwamba dini ya kweli ingetambuliwa kwa matendo ya wafuasi wake. Alisema: Kwa matunda yao mtawatambua. Kila mti mzuri huzaa matunda mazuri.
5

4. Yesu alimaanisha nini alipozungumzia zile barabara mbili, na kila moja inaelekea wapi? 5. Tunawezaje kuwatambua wafuasi wa dini ya kweli?

146

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

(Mathayo 7:16, 17) Yaani, wale wanaofuata dini ya kweli wangetambuliwa kwa mafundisho na matendo yao. Waabudu wa kweli hujitahidi kufanya mapenzi ya Mungu wakiwa kikundi ingawa hawajakamilika na wanakosea. Hebu tuzungumzie mambo sita yanayowatambulisha wafuasi wa dini ya kweli. 6 Watumishi wa Mungu hutumia Biblia kama msingi wa mafundisho yao. Biblia yenyewe inasema hivi: Andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu nalo ni lenye faida kwa kufundisha, kwa kukaripia, kwa kunyoosha mambo, kwa kutia nidhamu katika uadilifu, ili mtu wa Mungu awe na uwezo kamili, akiwa na vifaa kamili kwa ajili ya kila kazi njema. (2 Timotheo 3:16, 17) Mtume Paulo aliwaandikia hivi Wakristo wenzake: Mlipolipokea neno la Mungu, ambalo mlilisikia kutoka kwetu, mlilikubali, si kama neno la wanadamu, bali, kama vile lilivyo kwa kweli, kama neno la Mungu. (1 Wathesalonike 2:13) Hivyo, mafundisho na matendo ya wafuasi wa dini ya kweli hayategemei maoni au desturi za wanadamu. Yanategemea Neno la Mungu, Biblia, lililoongozwa na roho. 7 Yesu Kristo aliweka mfano mzuri kwa kutumia Neno la Mungu kama msingi wa mafundisho yake. Katika sala kwa Baba yake wa mbinguni alisema: Neno lako ni kweli. (Yohana 17:17) Yesu aliamini Neno la Mungu, na mambo yote aliyofundisha yalipatana na Maandiko. Mara nyingi Yesu alisema: Imeandikwa. (Mathayo 4:4, 7, 10) Kisha Yesu alinukuu andiko. Vivyo hivyo, watu wa Mungu leo hawafundishi maoni yao wenyewe. Wanaamini kwamba Biblia ni Neno la Mungu, nao hutegemeza kwa uthabiti mafundisho yao katika yale inayosema. 8 Wafuasi wa dini ya kweli humwabudu Yehova peke yake
6, 7. Watumishi wa Mungu huionaje Biblia, na Yesu aliwekaje mfano mzuri kuhusiana na jambo hilo? 8. Kumwabudu Yehova kunatia ndani nini?

WALE WANAOMWABUDU MUNGU WA KWELI

hutumia Biblia kama msingi wa mafundisho yao humwabudu Yehova peke yake na kuwajulisha watu jina lake wanapendana kikweli wanakubali kwamba Mungu anamtumia Yesu kuwaokoa si sehemu ya ulimwengu wanahubiri kwamba Ufalme wa Mungu ndio tumaini pekee la wanadamu

148

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

na kulijulisha jina lake. Yesu alisema: Yehova Mungu wako ndiye unayepaswa kumwabudu, na yeye peke yake ndiye unayepaswa kumtolea utumishi mtakatifu. (Mathayo 4:10) Kwa hiyo, watumishi wa Mungu humwabudu Yehova peke yake. Ibada hiyo inatia ndani kuwajulisha watu jina la Mungu wa kweli na sifa zake. Zaburi 83:18 inasema: Wewe, ambaye jina lako ni Yehova, wewe peke yako ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote. Yesu aliweka mfano kwa kuwasaidia wengine wamjue Mungu, kama alivyosali: Nimelifunua jina lako kwa watu ulionipa kutoka ulimwenguni. (Yohana 17:6) Vivyo hivyo, waabudu wa kweli leo huwafundisha wengine kuhusu jina la Mungu, makusudi yake, na sifa zake. 9 Watu wa Mungu wanapendana kikweli bila ubinafsi. Yesu alisema: Kwa jambo hili wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu, mkiwa na upendo kati yenu wenyewe. (Yohana 13:35) Wakristo wa zamani walipendana kama Yesu alivyosema. Upendo huo unaotegemea kanuni za Biblia, hauzuiwi na tofauti za kikabila, kijamii, na kitaifa nao huwavuta watu pamoja katika kifungo cha kudumu cha undugu wa kweli. (Wakolosai 3:14) Wafuasi wa dini za uwongo hawana undugu kama huo wenye upendo. Tunajuaje? Wanauana kwa sababu ya tofauti za kitaifa au kikabila. Wakristo wa kweli hawatumii silaha wala kuwaua ndugu zao Wakristo au mtu mwingine yeyote. Biblia inasema: Watoto wa Mungu na watoto wa Ibilisi ni wazi kwa jambo hili: Kila mtu ambaye haendelei kufanya uadilifu hatokani na Mungu, wala yeye ambaye hampendi ndugu yake. . . . Tunapaswa kupendana; si kama Kaini, aliyetokana na yule mwovu akamuua ndugu yake.1 Yohana 3:10-12; 4:20, 21. 10 Bila shaka, kuwa na upendo wa kweli hakumaanishi tu kutowaua wengine. Wakristo wa kweli hutumia wakati, ngu9, 10. Wakristo wa kweli huonyeshana upendo katika njia zipi?

Ibada Ambayo Mungu Anakubali

149

vu, na mali zao kusaidiana na kutiana moyo bila ubinafsi. (Waebrania 10:24, 25) Wanasaidiana wakati wa taabu na hawadhulumiani. Wao huishi kulingana na kanuni ya Biblia inayosema tuwatendee wote mema.Wagalatia 6:10. 11 Wakristo wa kweli hukubali kwamba Mungu anamtumia Yesu Kristo kutuokoa. Biblia inasema: Hakuna wokovu katika mwingine yeyote, kwa maana hakuna jina lingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu ambalo kupitia hilo lazima sisi tupate kuokolewa. (Matendo 4:12) Kama tulivyoona katika Sura ya 5, Yesu alitoa uhai wake kuwa dia kwa wanadamu watiifu. (Mathayo 20:28) Isitoshe, Yesu ni Mfalme aliyewekwa rasmi na Mungu katika Ufalme wa mbinguni ambao utatawala dunia yote. Na Mungu anataka tumtii Yesu na kufuata mafundisho yake ikiwa tunataka kuishi milele. Ndiyo sababu Biblia inasema: Yule anayemwamini Mwana ana uzima wa milele; yule asiyemtii Mwana hataona uzima.Yohana 3:36. 12 Waabudu wa kweli si sehemu ya ulimwengu. Alipokuwa ameshtakiwa mbele ya Pilato, mtawala Mroma, Yesu alisema: Ufalme wangu si sehemu ya ulimwengu huu. (Yohana 18:36) Katika nchi yoyote ile wanamoishi, wafuasi wa kweli wa Yesu ni raia wa Ufalme wake wa mbinguni na hivyo hawajihusishi kamwe na siasa za ulimwengu huu. Hawaungi mkono upande wowote. Hata hivyo, waabudu wa Yehova hawawazuii wengine kujiunga na chama cha kisiasa, kugombea kiti cha kisiasa au kupiga kura. Waabudu wa kweli wa Mungu wanatii sheria hata ingawa hawajihusishi na siasa. Kwa nini? Kwa sababu Neno la Mungu linawaamuru wajitiishe kwa mamlaka zilizo kubwa za kiserikali. (Waroma 13:1) Matakwa ya kisiasa yanapopingana na matakwa ya Mungu, waabudu wa kweli huiga mfano wa mitume
11. Kwa nini ni muhimu kukubali kwamba Mungu anamtumia Yesu Kristo kutuokoa? 12. Kutokuwa sehemu ya ulimwengu kunahusisha nini?

150

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

ambao walisema: Lazima tumtii Mungu kuwa mtawala kuliko wanadamu.Matendo 5:29; Marko 12:17. 13 Wafuasi wa kweli wa Yesu wanahubiri kwamba Ufalme wa Mungu ndio tumaini pekee la wanadamu. Yesu alitabiri: Hii habari njema ya ufalme itahubiriwa katika dunia
13. Wafuasi wa kweli wa Yesu wana maoni gani kuhusu Ufalme wa Mungu, na hivyo wanachukua hatua gani?

Utafaidika sana ukimtumikia Yehova pamoja na watu wake

Ibada Ambayo Mungu Anakubali

151

yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakapokuja. (Mathayo 24:14) Wafuasi wa kweli wa Yesu Kristo hutangaza Ufalme wa mbinguni wa Mungu kuwa tumaini pekee la wanadamu badala ya kuwatia watu moyo wategemee utawala wa kibinadamu kusuluhisha matatizo yao. (Zaburi 146:3) Yesu alitufundisha kusali kwa ajili ya serikali hiyo kamilifu aliposema: Ufalme wako na uje. Mapenzi yako na yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni. (Mathayo 6:10) Neno la Mungu lilitabiri kwamba Ufalme huo wa mbinguni utazivunja na kuzikomesha falme hizi zote [zilizopo leo], nao utasimama mpaka wakati usio na kipimo.Danieli 2:44. 14 Kulingana na mambo ambayo tayari tumezungumzia, jiulize: Ni dini gani inayotumia Biblia kama msingi wa mafundisho yake yote na kuwajulisha watu jina la Yehova? Ni dini gani huonyesha upendo jinsi Yehova anavyotuagiza, ina imani katika Yesu, si sehemu ya ulimwengu, na hutangaza Ufalme wa Mungu kuwa tumaini pekee la wanadamu? Kati ya dini zote duniani, ni dini gani inayotimiza matakwa hayo? Uthibitisho unaonyesha wazi kwamba ni Mashahidi wa Yehova.Isaya 43:10-12.

UTAFANYA NINI? Huwezi kumpendeza Mungu kwa kudai tu kwamba unamwamini. Kwani, Biblia inasema kwamba hata roho waovu wanaamini kwamba Mungu yuko. (Yakobo 2:19) Hata hivyo, ni wazi kwamba hawafanyi mapenzi ya Mungu na hawana kibali chake. Ili tukubaliwe na Mungu, haitoshi tu kuamini kwamba yeye yuko, ni lazima tufanye mapenzi yake. Ni lazima pia tujitenge kabisa na dini za uwongo na kukubali ibada ya kweli.
15

14. Ni dini gani inayotimiza matakwa ya ibada ya kweli? 15. Mungu anataka tufanye nini mbali na kuamini tu kwamba yeye yuko?

152
16

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Mtume Paulo alisema kwamba hatupaswi kushiriki katika ibada ya uwongo. Aliandika: Tokeni katikati yao, na mjitenge, asema Yehova, na mwache kugusa kitu kilicho najisi; nami nitawakaribisha ndani. (2 Wakorintho 6:17; Isaya 52:11) Kwa hiyo, Wakristo wa kweli wanaepuka kitu chochote kinachohusiana na dini za uwongo. 17 Biblia inaonyesha kwamba dini zote za uwongo ni sehemu ya Babiloni Mkubwa.1 (Ufunuo 17:5) Jina hilo linatukumbusha jiji la zamani la Babiloni, ambako dini za uwongo zilianzia baada ya Mafuriko ya siku ya Noa. Mafundisho na mazoea mengi ambayo ni ya kawaida katika dini za uwongo yalianza zamani huko Babiloni. Kwa mfano, Wababiloni waliabudu miungu mitatu-mitatu. Leo, Utatu ni fundisho kuu katika dini nyingi. Lakini Biblia inafundisha wazi kwamba kuna Mungu mmoja tu wa kweli, Yehova, na kwamba Yesu Kristo ni Mwana wake. (Yohana 17:3) Wababiloni waliamini pia kwamba wanadamu wana nafsi isiyoweza kufa ambayo huendelea kuishi baada ya mwili kufa na ambayo inaweza kuteseka motoni. Leo, dini nyingi hufundisha kwamba nafsi au roho haiwezi kufa na inaweza kuteseka motoni. 18 Kwa kuwa ibada ya Babiloni ya zamani ilienea duniani pote, Babiloni Mkubwa ya leo inaweza kuitwa kwa kufaa milki ya ulimwengu ya dini za uwongo. Na Mungu ametabiri kwamba milki hiyo ya dini za uwongo itaharibiwa ghafula. (Ufunuo 18:8) Je, unaona kwa nini unapaswa kujitenga na kila sehemu ya Babiloni Mkubwa? Yehova Mu1 Unaweza kupata habari inayoeleza kwa nini Babiloni Mkubwa inawakilisha milki ya ulimwengu ya dini za uwongo katika Nyongeza, ukurasa 219-220. 16. Tunapaswa kuwa na maoni gani kuhusu kushirikiana na dini za uwongo? 17, 18. Babiloni Mkubwa ni nini, na kwa nini ni muhimu kutoka kwake haraka?

Ibada Ambayo Mungu Anakubali

153

ngu anataka utoke kwake, yaani, Babiloni Mkubwa, haraka kabla ya kuchelewa.Ufunuo 18:4. 19 Huenda baadhi ya watu wakaacha kushirikiana nawe kwa sababu ya uamuzi wako wa kuacha kushirikiana na dini ya uwongo. Hata hivyo, utafaidika sana ukimtumikia Yehova pamoja na watu wake. Kama wanafunzi wa zamani wa Yesu ambao waliacha vitu vingine ili wamfuate, utakuwa na ndugu na dada wengi wa kiroho. Utakuwa sehemu ya familia kubwa ya ulimwenguni pote yenye mamilioni ya Wakristo ambao wanakupenda kikweli. Nawe utakuwa na tumaini zuri la kuishi milele katika mfumo wa mambo unaokuja. (Marko 10:28-30) Huenda wale ambao walikukataa kwa sababu ya imani yako wataona yale ambayo Biblia inafundisha na kuwa waabudu wa Yehova. 20 Biblia inafundisha kwamba hivi karibuni Mungu ataharibu mfumo huu mbovu wa mambo na kuleta ulimwengu mpya wenye uadilifu chini ya utawala wa Ufalme wake. (2 Petro 3:9, 13) Huo utakuwa ulimwengu mzuri ajabu! Na katika mfumo huo mpya wenye uadilifu, kutakuwa na dini moja tu, aina moja ya ibada ya kweli. Je, si jambo la hekima kuchukua hatua zinazofaa ili kujiunga na waabudu wa kweli sasa hivi?
19. Utafaidikaje ukimtumikia Yehova? 20. Washiriki wa dini ya kweli wanatazamia nini wakati ujao?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA Kuna dini moja tu ya kweli.Mathayo 7: 13, 14. Dini ya kweli inatambuliwa kwa mafundisho na matendo yake.Mathayo 7:16, 17. Mashahidi wa Yehova wanamwabudu Mungu kwa njia anayokubali.Isaya 43:10.

SURA YA KUMI NA SITA

Chukua Msimamo Upande wa Ibada ya Kweli


Biblia inafundisha nini kuhusu kutumia mifano katika ibada? Wakristo huzionaje sikukuu za kidini? Unaweza kuwaelezaje wengine imani yako bila kuwaudhi?
NAMNA gani ukipata habari kwamba eneo lenu lote limetiwa sumu? Mtu fulani amekuwa akitupa kisiri takataka zenye sumu katika eneo lenu na maisha ya watu yamo hatarini sasa. Utafanya nini? Bila shaka utahama ikiwezekana. Hata hivyo, baada ya kuhama, bado utakiria swali hili kwa uzito, Je, nimeathiriwa na sumu hiyo? 2 Ndivyo ilivyo kuhusiana na dini za uwongo. Biblia inafundisha kwamba ibada kama hiyo imechafuliwa na mafundisho na mazoea machafu. (2 Wakorintho 6:17) Ndiyo sababu unapaswa kutoka katika Babiloni Mkubwa, ambayo ni milki ya ulimwenguni pote ya dini za uwongo. (Ufunuo 18:2, 4) Je, tayari umefanya hivyo? Ikiwa ndivyo, unastahili kupongezwa. Hata hivyo, kuna mambo mengi ambayo unahitaji kufanya mbali na kujitenga au kujiuzulu kutoka katika dini ya uwongo. Baada ya kutoka, unapaswa kujiuliza, Je, bado mimi ninashikilia mambo fulani niliyozoea kufanya nilipokuwa katika dini ya uwongo? Fikiria mifano kadhaa.
1, 2. Baada ya kutoka katika dini ya uwongo, unapaswa kujiuliza swali gani, na kwa nini ni muhimu?

155

KUABUDU SANAMU NA MABABU Watu fulani wamekuwa na sanamu au vihekalu katika nyumba zao kwa miaka mingi. Je, wewe ni mmoja wao? Ikiwa ndivyo, huenda ukaona kwamba ni vigumu au ni vibaya kusali kwa Mungu bila kutumia vitu vinavyoonekana. Huenda hata unavipenda sana baadhi ya vitu hivyo. Lakini Mungu ndiye anayesema jinsi anavyotaka aabudiwe, na Biblia inafundisha kwamba hataki tutumie sanamu. (Kutoka 20:4, 5; Zaburi 115:4-8; Isaya 42:8; 1 Yohana 5:21) Kwa hiyo, unaweza kuchukua msimamo upande wa ibada ya kweli kwa kuharibu vitu vyovyote ulivyo navyo ambavyo vinahusiana na ibada ya uwongo. Kwa vyovyote vile, vione vitu hivyo jinsi Yehova anavyoviona, yaani, ni vitu vinavyochukiza.Kumbukumbu la Torati 27:15. 4 Katika dini nyingi za uwongo, mababu pia huabudiwa.
3

3. (a) Biblia inasema nini kuhusu kutumia sanamu, na kwa nini huenda ikawa vigumu kwa wengine kukubali maoni ya Mungu? (b) Unapaswa kufanya nini ikiwa una vitu vinavyohusiana na ibada ya uwongo? 4. (a) Tunajuaje kwamba kuabudu mababu ni kazi bure? (b) Kwa nini Yehova aliwaonya watu wake wasiwasiliane na pepo kwa njia yoyote?

156

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Kabla ya kujifunza kweli ya Biblia, watu fulani waliamini kwamba wafu wanaishi katika makao yasiyoonekana ya roho na kwamba wanaweza kuwasaidia au kuwaumiza walio hai. Labda ulikuwa ukijitahidi sana kuwatuliza mababu zako waliokufa. Lakini kama ulivyojifunza katika Sura ya 6 ya kitabu hiki, wafu hawana fahamu wala hawaishi popote. Kwa hiyo, ni kazi bure kujaribu kuwasiliana nao. Ujumbe wowote ambao inasemekana unatoka kwa mpendwa aliyekufa, kwa kweli unatoka kwa roho waovu. Kwa hiyo, Yehova aliwaonya Waisraeli wasijaribu kuongea na wafu au kuwasiliana na pepo kwa njia yoyote ile.Kumbukumbu la Torati 18:10-12. 5 Ikiwa zamani ulikuwa ukitumia sanamu au kuabudu mababu, unaweza kufanya nini? Soma na utafakari maandiko ya Biblia yanayoonyesha maoni ya Mungu. Sali kwa Yehova kila siku kuhusu tamaa yako ya kuchukua msimamo upande wa kweli, na umwombe akusaidie uwe na maoni kama yake. Isaya 55:9.

KRISMASI HAIKUSHEREHEKEWA NA WAKRISTO WA ZAMANI 6 Ibada ya mtu inaweza kuchafuliwa na dini za uwongo kupitia sherehe zinazopendwa. Kwa mfano, kiria Krismasi. Inasemekana kwamba Krismasi ni ukumbusho wa kuzaliwa kwa Yesu Kristo, na karibu dini zote zinazodai kuwa za Kikristo husherehekea Krismasi. Hata hivyo, hakuna lolote linalothibitisha kwamba wanafunzi wa Yesu walisherehekea sikukuu hiyo. Kitabu Sacred Origins of Profound Things kinasema: Kwa miaka 200 tangu Kristo alipozaliwa, hakuna mtu aliyejua siku hususa ambayo alizaliwa, na ni watu wachache tu waliotaka kujua.
5. Unaweza kufanya nini ikiwa zamani ulikuwa ukitumia sanamu au kuabudu mababu? 6, 7. (a) Krismasi inasemekana kuwa ukumbusho wa nini, na je, wafuasi wa Kristo wa karne ya kwanza waliisherehekea? (b) Wakati wa wanafunzi wa kwanza wa Yesu, sherehe za kuzaliwa zilihusianishwa na nini?

Chukua Msimamo Upande wa Ibada ya Kweli


7

157

Hata kama wanafunzi wa Yesu wangejua tarehe hususa ya kuzaliwa kwake, hawangeisherehekea. Kwa nini? Kwa sababu, kama vile kitabu The World Book Encyclopedia kinavyosema, Wakristo wa zamani waliona kusherehekea sikukuu ya kuzaliwa kwa mtu yeyote kuwa desturi ya kipagani. Sikukuu pekee za kuzaliwa zinazotajwa katika Biblia ni zile za watawala wawili ambao hawakumwabudu Yehova. (Mwanzo 40:20; Marko 6:21) Pia, sikukuu za kuzaliwa zilisherehekewa ili kuheshimu miungu ya kipagani. Kwa mfano, mnamo Mei 24, Waroma walisherehekea kuzaliwa kwa mungu wa kike aliyeitwa Diana. Siku iliyofuata, walisherehekea kuzaliwa kwa mungu-jua aliyeitwa Apollo. Hivyo, sherehe za kuzaliwa zilihusianishwa na upagani wala si Ukristo. 8 Kuna sababu nyingine ambayo ingewafanya Wakristo wasisherehekee kuzaliwa kwa Yesu. Inaelekea wanafunzi wake walijua kwamba sherehe za kuzaliwa zilihusiana na ushirikina. Kwa mfano, Wagiriki na Waroma wengi wa kale waliamini kwamba roho fulani ilikuwapo wakati wa kuzaliwa kwa kila mwanadamu na ilimlinda maisha yake yote. Kitabu The Lore of Birthdays kinasema kwamba, roho hiyo ilikuwa na uhusiano wa kichawi pamoja na mungu ambaye siku ya kuzaliwa kwake ililingana na siku ya kuzaliwa kwa mtu huyo. Bila shaka, Yehova hawezi kufurahishwa na sherehe yoyote ambayo inamhusianisha Yesu na ushirikina. (Isaya 65:11, 12) Basi, watu wengi walianzaje kusherehekea Krismasi?

KRISMASI ILIANZIA WAPI? Watu walitenga Desemba 25 kuwa siku ya kusherehekea kuzaliwa kwa Yesu mamia ya miaka baada ya yeye kuishi duniani. Lakini Yesu hakuzaliwa siku hiyo, inaonekana alizaliwa mwezi wa Oktoba.1 Basi, kwa nini Desemba 25
9

1 Ona Nyongeza, ukurasa 221-222. 8. Kuna uhusiano gani kati ya sherehe za kuzaliwa na ushirikina? 9. Desemba 25 ilichaguliwaje kuwa siku ya kusherehekea kuzaliwa kwa Yesu?

158

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

ilichaguliwa? Inaelekea kwamba baadaye watu fulani waliodai kuwa Wakristo walitaka tarehe hiyo ipatane na sherehe ya kipagani ya Waroma ya kuzaliwa kwa jua lisiloshindwa. (The New Encyclopdia Britannica) Wakati wa majira ya baridi kali, jua lilipoonekana kuwa hafu zaidi, wapagani walifanya sherehe ili kulifanya jua lirudi na kuwaletea joto na nuru. Walidhani kwamba jua lilianza kurudi Desemba 25. Katika jitihada za kuwafanya wapagani wawe Wakristo, viongozi wa kidini waliikubali sherehe hiyo na kujaribu kuifanya ionekane kuwa ya Kikristo.1 10 Tangu zamani imejulikana kwamba Krismasi ilitokana na wapagani. Kwa kuwa ilitokana na chanzo kisichopatana na Maandiko, Krismasi ilipigwa marufuku katika karne ya 17 nchini Uingereza na pia katika koloni kadhaa za Amerika. YeJe, unaweza yote ambaye hakwenda kazini siku kula peremende ya Krismasi alitozwa faini. Hata ambayo hivyo, punde si punde, desturi hizo imeokotwa za kale zikarudi, na nyingine mpya katika mtaro? zikaongezwa. Kwa mara nyingine tena Krismasi ikawa sikukuu kubwa, na hivyo ndivyo ilivyo leo hii katika nchi nyingi. Hata hivyo, kwa sababu Krismasi inahusianishwa na dini za uwongo, wale wanaotaka kumpendeza Mungu hawaisherehekei wala
1 Sherehe ya Saturnalia pia ilichangia kuchaguliwa kwa Desemba 25. Sherehe hiyo inayomheshimu mungu wa kilimo wa Waroma ilifanywa Desemba 17 hadi 24. Katika sherehe hiyo ya Saturnalia, watu walikula na kunywa, walijitumbuiza na kupeana zawadi. 10. Kwa nini watu fulani hawakusherehekea Krismasi nyakati zilizopita?

Chukua Msimamo Upande wa Ibada ya Kweli

159

hawasherehekei sikukuu nyingine yoyote iliyotokana na ibada ya kipagani.1

JE, VYANZO VYA SIKUKUU NI MUHIMU? Watu fulani hukubali kwamba sikukuu kama vile Krismasi zilianzishwa na wapagani, hata hivyo, wanahisi kwamba si vibaya kuzisherehekea. Kwani, watu wengi wanaposherehekea sikukuu hizo hawakirii ibada ya uwongo. Pia, pindi hizo huwezesha familia kuwa pamoja. Je, hivyo ndivyo unavyohisi? Ikiwa ndivyo, huenda sababu inayokufanya uone ugumu kuchukua msimamo upande wa ibada ya kweli ni upendo wako kwa familia wala si kwa dini ya uwongo. Uwe na hakika kwamba Yehova aliyeanzisha familia anataka uwe na uhusiano mzuri na watu wako wa ukoo. (Waefeso 3:14, 15) Hata hivyo, unaweza kuimarisha vifungo hivyo kwa njia ambayo Mungu anakubali. Mtume Paulo alisema hivi kuhusu jambo lililo muhimu zaidi maishani mwetu: Endeleeni kuhakikisha lile linalokubalika kwa Bwana.Waefeso 5:10. 12 Huenda unahisi kwamba leo watu hawaadhimishi sikukuu kwa sababu ya vyanzo vyake. Je, vyanzo vya sikukuu ni muhimu? Ndiyo! Kwa mfano: Tuseme umeona peremende kwenye mtaro. Je, utaiokota na kuila? Haiwezekani! Peremende hiyo ni chafu. Sawa na peremende hiyo, huenda sikukuu hizo zinaonekana kuwa zenye kuvutia, hata hivyo, zimeokotwa mahali pachafu. Ili kuchukua msimamo upande wa ibada ya kweli, tunapaswa kuwa na maoni kama ya nabii Isaya, aliyewaambia hivi waabudu wa kweli: Msiguse kitu chochote kilicho najisi.Isaya 52:11.
11

1 Unaweza kupata habari zaidi kuhusu maoni ya Wakristo wa kweli juu ya sikukuu nyingine zinazopendwa na watu wengi, katika Nyongeza, ukurasa 222-223. 11. Kwa nini watu fulani husherehekea sikukuu, hata hivyo, ni jambo gani lililo muhimu zaidi kwetu? 12. Eleza ni kwa nini tunapaswa kuepuka desturi na sherehe zenye vyanzo visivyofaa.

160

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

TUMIA UTAMBUZI UNAPOSHUGHULIKA NA WENGINE 13 Magumu yanaweza kutokea unapoamua kutosherehekea sikukuu. Kwa mfano, huenda wafanyakazi wenzako wakataka kujua ni kwa nini husherehekei sikukuu fulani zinazofanywa kazini. Vipi ukipewa zawadi ya Krismasi? Je, ni vibaya kuikubali? Vipi ikiwa mwenzi wako wa ndoa ana imani tofauti? Unaweza kuhakikishaje kwamba watoto wako hawahisi kwamba wamekosa kitu fulani kwa kutosherehekea sikukuu hizo? 14 Unahitaji utambuzi ili kushughulikia kila hali inayotokea. Mtu akikupa salamu za sikukuu, unaweza tu kumshukuru kwa kukutakia heri. Lakini vipi ikiwa wewe humwona au kufanya kazi na mtu huyo kila siku. Basi, huenda ukaamua kumweleza mengi zaidi. Vyovyote vile, tumia busara. Biblia inashauri: Maneno yenu na yawe yenye neema sikuzote, yenye kukolezwa chumvi, ili mjue jinsi mnavyopaswa kumjibu kila mtu. (Wakolosai 4:6) Uwe mwangalifu usije ukawavunjia wengine heshima. Badala yake, waeleze msimamo wako kwa busara. Waeleze waziwazi kwamba hakuna ubaya wa kutoa au kupokea zawadi na kuwa na sherehe, hata hivyo ungependa kufanya mambo hayo wakati mwingine. 15 Vipi ikiwa mtu anataka kukupa zawadi? Inategemea hali mbalimbali. Huenda mwenye kukupa zawadi akasema: Najua kwamba husherehekei sikukuu. Hata hivyo, ningependa kukupa zawadi hii. Basi, huenda ukaamua kwamba kupokea zawadi hiyo si sawa na kushiriki katika sikukuu. Bila shaka, ikiwa mwenye kukupa zawadi hajui imani yako, unaweza kumtajia kwamba wewe husherehekei sikukuu hiyo. Hilo litamsaidia kuelewa ni kwa nini ingawa unakubali kupokea zawadi yake, hutampa zawadi yoyote. Kwa upande
13. Ni magumu gani yanayoweza kutokea usiposherehekea sikukuu? 14, 15. Unaweza kufanya nini ukipewa salamu ya sikukuu au ikiwa mtu anataka kukupa zawadi?

Chukua Msimamo Upande wa Ibada ya Kweli

161

mwingine, huenda isifae kupokea zawadi ikiwa yule anayekupa zawadi hiyo anataka kuonyesha kwamba hushikamani na imani yako au kwamba unaweza kuvunja imani yako ili kupata vitu vya kimwili.

NAMNA GANI WASHIRIKI WA FAMILIA? Namna gani ikiwa washiriki wa familia wana imani tofauti? Unapaswa kuwa na busara. Hakuna haja ya kubishania kila desturi au sherehe ambayo watu wako wa ukoo wanaamua kusherehekea. Badala yake, heshimu maoni yao, kama vile ungependa waheshimu maoni yako. (Mathayo 7:12) Epuka mambo yoyote ambayo yangefanya uonekane kwamba unasherehekea sikukuu. Lakini utumie busara katika mambo ambayo hayahusiani moja kwa moja na sherehe za sikukuu. Bila shaka, sikuzote unapaswa kutenda kwa njia itakayokuacha ukiwa na dhamiri njema.1 Timotheo 1:18, 19. 17 Unaweza kufanya nini ili watoto wako wasihisi kwamba wamekosa kitu fulani kwa sababu ya kutosherehekea sikukuu isiyopatana na Maandiko? Inategemea sana mambo unayofanya nyakati nyingine. Wazazi fulani hutenga nyakati za kuwapa watoto wao zawadi. Mojawapo ya zawadi bora zaidi ambazo unaweza kuwapa watoto wako ni kuwa pamoja nao na kuwaonyesha upendo.
16

UNGA MKONO IBADA YA KWELI Ili kumpendeza Mungu, lazima ukatae kushiriki ibada ya uwongo na kuchukua msimamo upande wa ibada ya kweli. Hilo linatia ndani nini? Biblia inasema hivi: Acheni tukiriane ili kuchocheana katika upendo na matendo mazuri, bila kuacha kukusanyika pamoja sisi wenyewe,
18

16. Unawezaje kutumia busara unaposhughulikia mambo yanayohusiana na sikukuu? 17. Unawezaje kuwasaidia watoto wako wasihisi kwamba wanakosa kitu fulani wanapowaona wengine wakisherehekea sikukuu fulani? 18. Kuhudhuria mikutano ya Kikristo kunawezaje kukusaidia kuchukua msimamo upande wa ibada ya kweli?

162

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

kama vile wengine walivyo na desturi, bali tutiane moyo, na kufanya hivyo zaidi kwa kadiri mnavyoona siku ile kuwa inakaribia. (Waebrania 10:24, 25) Mikutano ya Kikristo ni pindi za furaha ambazo unaweza kumwabudu Mungu kwa njia anayokubali. (Zaburi 22:22; 122:1) Kwenye mikutano hiyo, kuna ubadilishanaji wa kitia-moyo kati ya Wakristo waaminifu.Waroma 1:12. 19 Njia nyingine ya kuchukua msimamo upande wa ibada ya kweli ni kuwaambia wengine mambo ambayo umejua baada ya kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Kwa kweli, watu wengi wanaugua na kulia kwa sababu ya uovu unaotendeka ulimwenguni leo. (Ezekieli 9:4) Huenda unajua watu fulani wanaohisi hivyo. Unaweza kuzungumza nao kuhusu tumaini lako la wakati ujao linalotegemea Biblia. Unaposhirikiana na Wakristo wa kweli na kuzungumza na wengine kuhusu kweli nzuri za Biblia ambazo umejifunza, utaona kwamba tamaa yoyote ya kushiriki desturi za dini ya uwongo ambayo huenda bado ikawa moyoni mwako itatoweka hatua kwa hatua. Uwe na hakika kwamba utakuwa na furaha sana na utapata baraka nyingi ukichukua msimamo upande wa ibada ya kweli.Malaki 3:10.
19. Kwa nini ni muhimu kuzungumza na wengine kuhusu mambo uliyojifunza katika Biblia?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA Ibada ya sanamu na ibada ya mababu haipatani na ibada ya kweli.Kutoka 20:4, 5; Kumbukumbu la Torati 18:10-12. Haifai kushiriki katika sherehe zilizoanzishwa na wapagani.Waefeso 5:10. Wakristo wa kweli wanapaswa kutumia busara wanapowaeleza wengine kuhusu imani yao.Wakolosai 4:6.

Kuunga mkono ibada ya kweli huleta furaha ya kweli

SURA YA KUMI NA SABA

Mkaribie Mungu Katika Sala


Kwa nini tunapaswa kusali kwa Mungu? Ni lazima tufanye nini ili Mungu asikilize sala zetu? Mungu hujibuje sala zetu?
DUNIA ni ndogo sana inapolinganishwa na ulimwengu wote mzima. Kwa kweli, Yehova, Mtengenezaji wa mbingu na dunia, anayaona mataifa ya wanadamu kuwa kama tone dogo la maji katika ndoo. (Zaburi 115:15; Isaya 40:15) Hata hivyo, Biblia inasema: Yehova yuko karibu na wote wanaomwitia, wote wanaomwitia yeye katika ukweli. Atawatimizia wale wanaomwogopa tamaa yao, naye atakisikia kilio chao cha kuomba msaada. (Zaburi 145:18, 19) Hebu wazia! Muumba mweza-yote yuko karibu nasi naye atatusikiliza tukimwitia yeye katika ukweli. Tuna pendeleo lililoje la kumkaribia Mungu katika sala! 2 Hata hivyo, ikiwa tungependa Yehova asikilize sala zetu, ni lazima tusali kulingana na mapenzi yake. Hatuwezi kufanya hivyo tusipojua mambo ambayo Biblia inafundisha kuhusu sala. Ni muhimu tujue yale ambayo Maandiko yanasema kuhusu hilo kwa sababu sala inatusaidia kumkaribia Yehova.
3

KWA NINI TUSALI KWA YEHOVA? Sababu moja muhimu inayotufanya tusali kwa Ye-

1, 2. Kwa nini tunapaswa kuiona sala kuwa pendeleo kubwa, na kwa nini ni muhimu tujue mambo ambayo Biblia inafundisha kuhusu sala? 3. Taja sababu moja muhimu inayotufanya tusali kwa Yehova.

165

Mtengenezaji wa mbingu na dunia yuko tayari kusikiliza sala zetu

hova ni kwamba anatuhimiza tufanye hivyo. Neno lake linatutia moyo: Msihangaike juu ya kitu chochote, bali katika kila jambo kwa sala na dua pamoja na kutoa shukrani maombi yenu na yajulishwe Mungu; na amani ya Mungu yenye ubora unaozidi kira zote itailinda mioyo yenu na nguvu zenu za akili kwa njia ya Kristo Yesu. (Walipi 4:6, 7) Kwa kweli, hatupaswi kupuuza uandalizi huo wenye fadhili kutoka kwa Mtawala Mkuu wa ulimwengu! 4 Sababu nyingine ni kwamba tunaposali kwa ukawaida, uhusiano wetu na Yehova unaimarika. Maraki wa kweli hawawasiliani tu wanapohitaji kitu fulani. Badala yake, maraki wazuri huhangaikiana, na uraki wao huimarika wanapozungumza kwa uhuru kuhusu maoni yao, kueleza hisia zao, na mahangaiko yao. Kwa njia fulani, ndivyo uhusiano wetu pamoja na Yehova Mungu ulivyo. Kitabu hiki kimekusaidia kujua mambo mengi ambayo Biblia inafundisha kumhusu Yehova, utu wake, na makusudi yake. Umejua kwamba yeye ni
4. Kusali kwa ukawaida kunawezaje kuimarisha uhusiano wetu na Yehova?

166

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Mungu halisi. Sala hukuwezesha kumueleza Baba yako wa mbinguni mawazo na hisia zako za moyoni. Unapofanya hivyo, unamkaribia zaidi Yehova.Yakobo 4:8.
TUNAPASWA KUTIMIZA MATAKWA GANI? Je, Yehova husikiliza sala zote? Fikiria yale aliyowaambia Waisraeli waasi katika siku za nabii Isaya: Hata mjapotoa sala nyingi, mimi sisikilizi; mikono yenu imejaa umwagaji wa damu. (Isaya 1:15) Kwa hiyo, matendo fulani yanaweza kumfanya Mungu asisikilize sala zetu. Basi, ili sala zetu zisikilizwe na Mungu, ni lazima tutimize matakwa fulani muhimu. 6 Takwa moja muhimu ni kuwa na imani. (Marko 11:24) Mtume Paulo aliandika: Bila imani haiwezekani kamwe kumpendeza [Mungu] vema, kwa maana yule anayemkaribia Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko na kwamba yeye huwa mthawabishaji wa wale wanaomtafuta kwa bidii. (Waebrania 11:6) Mbali na kuamini kwamba kuna Mungu anayesikiliza na kujibu sala, mengi yanahitajiwa ili kuwa na imani ya kweli. Imani huthibitika kwa matendo yetu. Maisha yetu ya kila siku yanapaswa kuthibitisha kwamba tuna imani.Yakobo 2:26. 7 Pia Yehova anataka wale wanaosali, wafanye hivyo kwa unyenyekevu na unyoofu. Tuna kila sababu ya kuwa wanyenyekevu tunapozungumza na Yehova, sivyo? Kwa kawaida, watu huzungumza na mfalme au rais, kwa he5

5. Ni nini kinachoonyesha kwamba Yehova hasikilizi sala zote? 6. Ili Mungu asikilize sala zetu, tunapaswa kutimiza takwa gani muhimu, na tunawezaje kufanya hivyo? 7. (a) Kwa nini tunapaswa kuonyesha heshima tunapozungumza na Yehova katika sala? (b) Tunawezaje kuonyesha unyenyekevu na unyoofu tunaposali kwa Mungu?

Mkaribie Mungu Katika Sala

167

shima, wakitambua cheo chake cha juu. Basi, tunapaswa kumheshimu Yehova hata zaidi tunapozungumza naye. (Zaburi 138:6) Kwa kweli, yeye ni Mungu Mweza-Yote. (Mwanzo 17:1) Tunaposali kwa Mungu, tunapaswa kumkia kwa njia inayoonyesha kwamba tunatambua kwa unyenyekevu hali yetu mbele zake. Unyenyekevu huo utatuchochea kusali kwa unyoofu kutoka moyoni mwetu, na kuepuka sala za kidesturi au za kurudia-rudia.Mathayo 6:7, 8. 8 Ikiwa tunataka Mungu atusikilize, tunapaswa kutenda kulingana na sala zetu. Yehova anatarajia tujitahidi kadiri ya uwezo wetu kutenda kulingana na sala zetu. Kwa mfano, tukisali Utupe leo mkate wetu kwa ajili ya siku hii, ni lazima tufanye kwa bidii kazi yoyote tunayoweza kufanya. (Mathayo 6:11; 2 Wathesalonike 3:10) Tukisali atusaidie kushinda udhaifu fulani wa kimwili, ni lazima tuwe waangalifu na kuepuka mambo au hali zinazoweza kututia majaribuni. (Wakolosai 3:5) Mbali na matakwa hayo muhimu, kuna maswali kuhusu sala ambayo tungependa kujibiwa.
KUJIBU MASWALI FULANI KUHUSU SALA Tunapaswa kusali kwa nani? Yesu aliwafundisha wafuasi wake wasali kwa Baba yetu aliye mbinguni. (Mathayo 6:9) Hivyo, sala zetu zinapaswa kuelekezwa kwa Yehova Mungu peke yake. Hata hivyo, Yehova anataka tutambue cheo cha Mwana wake mzaliwa wa pekee, Yesu Kristo. Kama tulivyojifunza katika Sura ya 5, Yesu alitumwa duniani ili awe dia na kutukomboa kutoka katika dhambi na kifo. (Yohana 3:16; Waroma 5:12) Yeye ndiye Kuhani Mkuu na Hakimu aliyewekwa rasmi.
9

8. Tunawezaje kutenda kulingana na sala zetu? 9. Tunapaswa kusali kwa nani, na kupitia nani?

168

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

(Yohana 5:22; Waebrania 6:20) Hivyo, Maandiko yanatuagiza tutoe sala zetu kupitia Yesu. Yeye mwenyewe alisema: Mimi ndiye njia na kweli na uzima. Hakuna anayekuja kwa Baba ila kupitia kwangu. (Yohana 14:6) Ili sala zetu zisikiwe, ni lazima tusali kwa Yehova tu kupitia Mwanaye. 10 Je, ni lazima tuwe katika hali fulani hususa tunaposali? Hapana. Yehova hahitaji tufanye jambo fulani hususa tunaposali. Biblia inafundisha kwamba tunaweza kusali tukiwa katika hali mbalimbali. Tunaweza kusali tukiwa tumeketi, tumeinama, tumepiga magoti, na tukiwa tumesimama. (1 Mambo ya Nyakati 17:16; Nehemia 8:6; Danieli 6:10; Marko 11:25) Jambo muhimu si kukaa katika hali fulani hususa ili tuonwe na wengine, bali ni kuwa na mwelekeo unaofaa. Isitoshe, tunapokuwa katika shughuli zetu za kila siku au tunapokabili hali ya dharura, tunaweza kusali kimyakimya popote tulipo. Yehova husikiliza sala kama hizo hata ingawa hazisikiwi na watu walio karibu nasi.Nehemia 2:1-6. 11 Tunaweza kusali kuhusu nini? Biblia inaeleza: Hata tukiomba nini kulingana na mapenzi yake, yeye [Yehova] hutusikia. (1 Yohana 5:14) Basi tunaweza kuomba chochote kulingana na mapenzi ya Mungu. Je, ni mapenzi yake tusali kuhusu mahangaiko yetu? Ndiyo, bila shaka! Kusali kwa Yehova ni kama kuongea na raki wa karibu. Tunaweza kuongea waziwazi, tukimimina moyo wetu mbele za Mungu. (Zaburi 62:8) Tunapaswa kuomba roho takatifu, kwa sababu itatusaidia kufanya mambo yanayofaa. (Luka 11:13) Tunaweza pia kuomba mwongozo wa kufanya maamuzi ya heki10. Kwa nini hatuhitaji kuwa katika hali fulani hususa tunaposali? 11. Ni mahangaiko gani ya kibinafsi tunayoweza kusali juu yake?

Mkaribie Mungu Katika Sala

169

ma na nguvu za kukabiliana na magumu. (Yakobo 1:5) Tunapofanya dhambi, tunapaswa kuomba msamaha kwa msingi wa dhabihu ya Kristo. (Waefeso 1:3, 7) Lakini hatupaswi kusali tu kuhusu mambo ya kibinafsi. Tunapaswa kusali kwa niaba ya watu wengine kama vile familia yetu na pia waabudu wenzetu.Matendo 12:5; Wakolosai 4:12. 12 Katika sala zetu, tunapaswa kutanguliza mambo yanayomhusu Yehova Mungu. Bila shaka tuna kila sababu ya kumsifu na kumshukuru kutoka moyoni kwa sababu ya wema wake wote. (1 Mambo ya Nyakati 29:10-13) Katika sala ya kielelezo iliyo kwenye Mathayo 6:9-13, Yesu alitufundisha tusali jina la Mungu litakaswe, yaani, lionwe kuwa takatifu. Kisha tusali Ufalme wa Mungu uje na mapenzi yake yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni. Baada ya kuzungumzia mambo hayo muhimu kumhusu Yehova ndipo Yesu alipotaja mambo ya kibinafsi. Sisi pia tunapomtanguliza Mungu katika sala zetu, tunaonyesha kwamba hatuhangaikii tu mambo yetu wenyewe. 13 Sala zetu zinapaswa kuwa na urefu gani? Biblia haisemi sala zinazotolewa faraghani au hadharani zinapaswa kuwa na urefu gani. Tunaweza kutoa sala fupi kabla ya kula au sala ndefu faraghani tunapomweleza Yehova mambo yaliyo moyoni mwetu. (1 Samweli 1: 12, 15) Hata hivyo, Yesu aliwashutumu watu waliojiona kuwa waadilifu ambao walitoa sala ndefu ili waonekane na watu. (Luka 20:46, 47) Sala za aina hiyo hazimpendezi Yehova. Jambo muhimu ni kusali kutoka moyoni. Hivyo, sala zinazokubalika zinaweza kuwa na urefu mbalimbali ikitegemea hali na mahitaji.
12. Tunawezaje kumtanguliza Baba yetu wa mbinguni katika sala zetu? 13. Maandiko yanasema nini kuhusu urefu wa sala zinazokubalika?

170
14

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Tunapaswa kusali mara ngapi? Biblia inatutia moyo tusali sikuzote, tudumu katika sala, na tusali bila kuacha. (Mathayo 26:41; Waroma 12:12; 1 Wathesalonike 5:17) Bila shaka, maandiko hayo hayamaanishi kwamba tunapaswa kusali kwa Yehova kila dakika. Badala yake, Biblia inatuhimiza tusali kwa ukawaida na kumshukuru Yehova daima kwa sababu ya wema wake kwetu na kumwomba atuongoze, atufariji, na kutuimarisha. Je, haitii moyo kujua kwamba Yehova haweki mipaka kuhusu urefu au mara ambazo tunaweza kuzungumza naye katika sala? Ikiwa tunathamini kikweli pendeleo la sala, tutapata nafasi nyingi za kusali kwa Baba yetu wa mbinguni. 15 Kwa nini tunapaswa kusema Amina mwishoni mwa sala? Neno amina humaanisha bila shaka, au iwe hivyo. Mifano ya kimaandiko inaonyesha kwamba tunapaswa kusema Amina mwishoni mwa sala za kibinafsi na za hadharani. (1 Mambo ya Nyakati 16:36; Zaburi 41:13) Tunaposema Amina mwishoni mwa sala zetu, tunaonyesha kwamba maneno yetu yanatoka moyoni. Tunaposema Amina kimyakimya au kwa sauti baada ya mtu fulani kutoa sala hadharani, tunaonyesha kwamba tunakubaliana na sala hiyo.1 Wakorintho 14:16.
JINSI MUNGU ANAVYOJIBU SALA ZETU Je, kweli Yehova hujibu sala? Bila shaka! Tuna sababu thabiti ya kuamini kwamba Msikiaji wa sala hujibu sala zinazotolewa na mamilioni ya wanadamu wanyoofu. (Zaburi 65:2) Yehova anaweza kujibu sala zetu kwa njia mbalimbali.
16

14. Biblia inamaanisha nini inapotuhimiza tusali sikuzote, na kwa nini hilo linatufariji? 15. Kwa nini tunapaswa kusema Amina mwishoni mwa sala za kibinafsi na za hadharani? 16. Tunaweza kuwa na uhakika gani kuhusu sala zetu?

Mkaribie Mungu Katika Sala


17

171

Yehova hutumia malaika wake na watumishi wake duniani kujibu sala. (Waebrania 1:13, 14) Kuna watu wengi ambao walisali kwa Mungu ili wapate msaada wa kuielewa Biblia na muda si muda wakatembelewa na mmoja wa watumishi wa Yehova. Mambo kama hayo yanaonyesha kwamba malaika wanaongoza kazi ya kuhubiri juu ya Ufalme. (Ufunuo 14:6) Yehova anaweza kumchochea Mkristo mwenzetu atusaidie tunaposali wakati
17. Kwa nini tunaweza kusema kwamba Mungu hutumia malaika na watumishi wake duniani kujibu sala zetu?

Mungu anaweza kusikia sala zako wakati wowote

Yehova anaweza kujibu sala zetu kwa kumchochea Mkristo mwenzetu atusaidie

wa uhitaji mkubwa.Methali 12:25; Yakobo 2:16. 18 Yehova Mungu pia hutumia roho yake takatifu na Neno lake, Biblia, kujibu sala za watumishi wake. Tunapoomba msaada wa kukabiliana na majaribu, anaweza kutujibu kwa kutuongoza na kutuimarisha kwa roho yake takatifu. (2 Wakorintho 4:7) Mara nyingi Biblia hujibu sala zetu za kuomba mwongozo. Yehova hutusaidia kufanya maamuzi ya hekima kupitia Biblia. Tunapojifunza Biblia kibinafsi na tunaposoma vichapo vya Kikristo kama kitabu hiki, tunaweza kupata maandiko yanayoweza kutusaidia. Tunaweza kukumbushwa habari za kimaandiko kwenye mikutano ya Kikristo au na mzee wa kutaniko anayetuhangaikia.Wagalatia 6:1. 19 Tukihisi kwamba Yehova anachelewa kujibu sala zetu, haimaanishi kwamba hawezi kujibu. Badala yake, tunapaswa kukumbuka kwamba Yehova hujibu sala kupatana na mapenzi yake na kwa wakati wake. Anajua mahitaji yetu na jinsi ya kuyatimiza kuliko tuwezavyo. Mara nyingi yeye huturuhusu tuendelee kuomba, kutafuta, na kupiga hodi. (Luka 11:5-10) Tunapoendelea
18. Yehova hutumiaje roho yake takatifu na Neno lake kujibu sala za watumishi wake? 19. Tunapaswa kukumbuka nini tunapohisi kwamba sala zetu hazijibiwi nyakati nyingine?

173

kufanya hivyo, tunamwonyesha Mungu kwamba tunatamani sana jambo tunaloomba na tuna imani ya kweli. Isitoshe, Yehova anaweza kujibu sala zetu kwa njia isiyo ya moja kwa moja. Kwa mfano, anaweza kujibu sala yetu kuhusiana na jaribu fulani kwa kutupa nguvu za kuvumilia badala ya kuliondoa jaribu hilo.Walipi 4:13. 20 Tunapaswa kushukuru kwamba Muumba wa ulimwengu huu mkubwa yuko karibu na wote wanaomwitia kwa njia inayofaa katika sala. (Zaburi 145:18) Na tutumie kikamili pendeleo lenye thamani la sala. Tukifanya hivyo, tutapata shangwe ya kumkaribia zaidi Yehova, ambaye ni Msikiaji wa sala.
20. Kwa nini tunapaswa kutumia kikamili pendeleo lenye thamani la sala?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA


Kusali kwa ukawaida kwa Yehova hutusaidia kumkaribia.Yakobo 4:8. Ili sala zetu zisikiwe na Mungu, ni lazima tusali kwa imani, unyenyekevu na unyoofu. Marko 11:24. Tunapaswa kusali kwa Yehova tu kupitia Mwana wake.Mathayo 6:9; Yohana 14:6. Yehova, Msikiaji wa sala, hutumia malaika wake, watumishi wake duniani, roho yake takatifu, na Neno lake kujibu sala zetu. Zaburi 65:2.

SURA YA KUMI NA NANE

Ubatizo na Uhusiano Wako Pamoja na Mungu


Ubatizo wa Kikristo hufanywaje? Unapaswa kuchukua hatua zipi ili ustahili kubatizwa? Mtu hujiwekaje wakfu kwa Mungu? Ni sababu gani ya pekee inayomfanya mtu abatizwe?
TAZAMA! Maji; ni nini kinachonizuia nisibatizwe? Swali hilo liliulizwa katika karne ya kwanza na osa Mwethiopia wa makao ya kifalme. Mkristo aliyeitwa Filipo, alikuwa amemthibitishia kwamba Yesu alikuwa Masihi aliyeahidiwa. Akiwa amechochewa
1. Kwa nini osa Mwethiopia wa makao ya kifalme alitaka kubatizwa?

Ubatizo na Uhusiano Wako Pamoja na Mungu

175

na yale aliyokuwa amejifunza katika Maandiko, Mwethiopia huyo alichukua hatua. Alionyesha kwamba anataka kubatizwa!Matendo 8:26-36. 2 Ikiwa umejifunza kwa makini sura za kwanza za kitabu hiki na mmoja wa Mashahidi wa Yehova, huenda ukauliza, Ni nini kinachonizuia nisibatizwe? Kukia sasa umejifunza kuhusu ahadi ya Biblia ya uzima wa milele katika Paradiso. (Luka 23:43; Ufunuo 21:3, 4) Pia umejifunza ukweli kuhusu hali ya wafu na tumaini la ufufuo. (Mhubiri 9:5; Yohana 5:28, 29) Huenda umekuwa ukihudhuria mikutano ya Mashahidi wa Yehova na umejionea upendo walio nao ambao hutambulisha ibada ya kweli. (Yohana 13:35) Zaidi ya yote, huenda umeanza kusitawisha uhusiano wa karibu pamoja na Yehova Mungu. 3 Unawezaje kuonyesha kwamba unataka kumtumikia Mungu? Yesu aliwaambia hivi wafuasi wake: Nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, mkiwabatiza. (Mathayo 28:19) Yesu mwenyewe alituwekea kielelezo alipobatizwa katika maji. Hakunyunyiziwa wala kumwagiliwa maji kidogo kichwani. (Mathayo 3:16) Neno batiza linatokana na neno la Kigiriki linalomaanisha zamisha. Kwa hiyo, ubatizo wa Kikristo unamaanisha kuzamisha, au kutumbukiza kabisa ndani ya maji. 4 Kila mtu anayetaka kuwa na uhusiano pamoja na Yehova Mungu anapaswa kubatizwa katika maji. Ubatizo huonyesha waziwazi kwamba unataka kumtumikia Mungu. Pia unaonyesha kwamba unatamani kufanya mapenzi ya Yehova. (Zaburi 40:7, 8) Hata hivyo, ili ustahili kubatizwa, ni lazima uchukue hatua fulani.
2. Kwa nini unapaswa kukiria kwa uzito kuhusu ubatizo? 3. (a) Yesu aliwapa wafuasi wake amri gani? (b) Ubatizo wa maji hufanywaje? 4. Ubatizo wa maji huonyesha nini?

176

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

UNAHITAJI IMANI NA UJUZI Tayari umeanza kuchukua hatua ya kwanza. Jinsi gani? Labda kwa kujifunza Biblia hatua kwa hatua na kuendelea kupata ujuzi kumhusu Yehova Mungu na Yesu Kristo. (Yohana 17:3) Hata hivyo, kuna mengi ya kujifunza. Wakristo wanataka wajazwe ujuzi sahihi wa mapenzi yake [Mungu]. (Wakolosai 1:9) Kuhudhuria mikutano ya Mashahidi wa Yehova kutakusaidia kufanya hivyo. Ni muhimu kuhudhuria mikutano hiyo. (Waebrania 10:24, 25) Kuhudhuria mikutano kwa ukawaida kutakusaidia kuongeza ujuzi juu ya Mungu. 6 Ni kweli kwamba si lazima ujue kila jambo katika Biblia ndipo ustahili kubatizwa. Yule osa Mwethiopia wa makao ya kifalme alikuwa na kiasi fulani cha ujuzi, hata hivyo, alihitaji kusaidiwa ili kuelewa sehemu fulani za Maandiko. (Matendo 8:30, 31) Vivyo hivyo, wewe pia unahitaji kujifunza mengi zaidi. Kwa kweli, hutakia mwisho wa kujifunza kumhusu Mungu. (Mhubiri 3:11) Hata hivyo, kabla ya kubatizwa, unahitaji kujua na kukubali mafundisho ya msingi ya Biblia. (Waebrania 5:12) Mafundisho hayo yanatia ndani kweli kuhusu hali ya wafu na umuhimu wa jina la Mungu na Ufalme wake. 7 Ujuzi peke yake hautoshi kwa maana bila imani haiwezekani kamwe kumpendeza [Mungu] vema. (Waebrania 11:6) Biblia inatuambia kwamba watu fulani wa jiji la kale la Korintho waliposikia ujumbe wa Kikristo walianza kuamini na kubatizwa. (Matendo 18:8) Vivyo hivyo, kadiri unavyozidi kujifunza Biblia, ndivyo unavyopaswa kuwa na imani zaidi kwamba hiyo ni Neno la Mungu lililo5

5. (a) Kabla ya kubatizwa, mtu anapaswa kuchukua hatua gani kwanza? (b) Kwa nini mikutano ya Kikristo ni muhimu? 6. Mtu anapaswa kuwa na ujuzi wa Biblia kiasi gani ili astahili kubatizwa? 7. Kujifunza Biblia kunapaswa kuwa na matokeo gani kwako?

Ubatizo na Uhusiano Wako Pamoja na Mungu

177

ongozwa na roho. Kujifunza Biblia kunapaswa kukusaidia kuwa na imani katika ahadi za Mungu, na kuamini kwamba dhabihu ya Yesu inaweza kukuokoa.Yoshua 23:14; Matendo 4:12; 2 Timotheo 3:16, 17.
KUZUNGUMZA NA WENGINE KUHUSU KWELI ZA BIBLIA 8 Kadiri unavyozidi kuwa na imani, ndivyo utakavyoona ikiwa rahisi kuzungumza na wengine mambo ambayo umejifunza. (Yeremia 20:9) Utachochewa sana kuzungumza na wengine kuhusu Mungu na makusudi yake. 2 Wakorintho 4:13. 9 Unaweza kuanza kuzungumza na wengine kuhusu kweli za Biblia kwa kuanzisha mazungumzo kwa busara pamoja na watu wa ukoo, maraki, majirani, na wafanyakazi wenzako. Baada ya muda, huenda ukataka kuhubiri rasmi pamoja na Mashahidi wa Yehova. Ukikia hatua hiyo, mjulishe Shahidi anayekufundisha Biblia. Ikiwa unastahili kuwa mhubiri, mipango itafanywa ili wewe na mwalimu wako mwe na mazungumzo pamoja na wazee wawili wa kutaniko. 10 Kufanya hivyo kutakuwezesha kuwafahamu wazee Wakristo wanaolichunga kundi la Mungu. (Matendo 20:28; 1 Petro 5:2, 3) Wazee hao wakiona kwamba unaelewa na kuamini mafundisho ya msingi ya Biblia, unaishi kupatana na kanuni za Mungu na kwa kweli unataka kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova, watakujulisha kwamba unastahili kushiriki katika huduma ukiwa mhubiri ambaye hajabatizwa wa habari njema.
8. Ni nini kitakachokuchochea kuzungumza na wengine mambo ambayo umejifunza? 9, 10. (a) Unaweza kuanza kuwahubiria nani kweli ya Biblia? (b) Unapaswa kufanya nini ikiwa unataka kushiriki katika kazi ya kuhubiri pamoja na Mashahidi wa Yehova?

178
11

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Kwa upande mwingine, huenda ukahitaji kurekebisha maisha na mazoea yako ili ustahili kuwa mhubiri. Hilo linaweza kutia ndani kuacha mazoea fulani mabaya. Kwa hiyo, kabla ya kuomba kuwa mhubiri ambaye hajabatizwa, unahitaji kuacha kabisa dhambi nzito kama vile ukosefu wa adili katika ngono, ulevi, na kutumia dawa za kulevya.1 Wakorintho 6:9, 10; Wagalatia 5:19-21.
KUTUBU NA KUGEUKA Kuna hatua nyingine zinazotangulia ubatizo. Mtume Petro alisema: Tubuni na mgeuke ili dhambi zenu zipate kufutwa. (Matendo 3:19) Kutubu ni kusikitika kikweli kwa sababu ya jambo ulilofanya. Mtu anapaswa kutubu ikiwa aliishi maisha yasiyo ya adili na hata yule ambaye amekuwa akiishi maisha sa kiadili anapaswa kufanya hivyo pia. Kwa nini? Kwa sababu wanadamu wote ni watenda dhambi na wanahitaji msamaha wa Mungu. (Waroma 3:23; 5:12) Kabla ya kujifunza Biblia, hukujua mapenzi ya Mungu. Kwa hiyo hungeweza kuishi kulingana na mapenzi yake. Basi, unapaswa kutubu. 13 Baada ya kutubu, lazima ugeuke. Haitoshi tu kusikitika. Unahitaji kukataa maisha yako ya zamani na kuazimia kabisa kufanya yaliyo mema kuanzia sasa na kuendelea. Ni lazima utubu na kugeuka kabla ya kubatizwa.
12

KUJIWEKA WAKFU Kuna hatua nyingine muhimu inayopaswa kuchukuliwa kabla ya ubatizo. Ni lazima ujiweke wakfu kwa Yehova Mungu.
14

11. Huenda watu fulani wakahitaji kufanya marekebisho gani ili wastahili kuwa wahubiri? 12. Kwa nini mtu anapaswa kutubu? 13. Kugeuka kunamaanisha nini? 14. Kabla ya kubatizwa, unahitaji kuchukua hatua gani muhimu?

Ubatizo na Uhusiano Wako Pamoja na Mungu


15

179

Unapojiweka wakfu kwa Yehova Mungu katika sala inayotoka moyoni, unamwahidi kwamba umejitoa kwake peke yake kwa umilele wote. (Kumbukumbu la Torati 6:15) Hata hivyo, kwa nini ujitoe kwake? Tuseme kwamba mwanamume ameanza kumchumbia mwanamke. Kadiri anavyozidi kuona sifa zake nzuri ndivyo anavyozidi kuvutiwa naye. Kwa kawaida, baada ya muda atamwomba wafunge ndoa. Ni kweli kwamba kufunga ndoa kutamwongezea majukumu. Hata hivyo, upendo utamchochea kuchukua hatua hiyo muhimu. 16 Baada ya kumjua na kumpenda Yehova, utachochewa kumtumikia bila kusita wala masharti yoyote kuhusiana na ibada. Yeyote anayetaka kumfuata Mwana wa Mungu, Yesu Kristo, lazima ajikane mwenyewe. (Marko 8:34) Tunajikana wenyewe kwa kuhakikisha kwamba mapendezi na miradi yetu binafsi haituzuii kumtii Mungu kikamili. Basi, kabla ya kubatizwa, ni lazima jambo kuu maishani mwako liwe kufanya mapenzi ya Yehova Mungu.1 Petro 4:2.
KUTOOGOPA KUSHINDWA Watu fulani husita kujiweka wakfu kwa Yehova kwa sababu wanaogopa kuchukua hatua hiyo muhimu. Huenda wakaogopa kuwajibika mbele za Mungu wakiwa Wakristo waliojiweka wakfu. Kwa kuwa wanaogopa kumkosea na kumkasirisha Yehova, wanaona ni afadhali wasijiweke wakfu kwake. 18 Unapoendelea kujifunza kumpenda Yehova, utachochewa kujiweka wakfu kwake na kujitahidi kuishi
17

15, 16. Kujiweka wakfu kwa Mungu kunamaanisha nini, na ni nini humchochea mtu kufanya hivyo? 17. Kwa nini huenda watu fulani wakasita kujiweka wakfu kwa Mungu? 18. Ni nini kinachoweza kukuchochea ujiweke wakfu kwa Yehova?

Kupata ujuzi sahihi kuhusu Neno la Mungu ni hatua muhimu ambayo mtu anapaswa kuchukua ili astahili kubatizwa

Imani inapaswa kukuchochea uzungumze na wengine kuhusu mambo ambayo umejifunza

kulingana na wakfu huo. (Mhubiri 5:4) Baada ya kujiweka wakfu, bila shaka utajitahidi kutembea kwa kumstahili Yehova kwa kusudi la kumpendeza yeye. (Wakolosai 1:10) Kwa sababu unampenda Mungu, haitakuwa vigumu kwako kufanya mapenzi yake. Bila shaka utakubaliana na mtume Yohana, aliyeandika: Kumpenda Mungu humaanisha hivi, kwamba tuzishike amri zake; na bado amri zake si mzigo mzito.1 Yohana 5:3. 19 Haimaanishi kwamba unahitaji kuwa mkamilifu ili ujiweke wakfu kwa Mungu. Yehova anajua uwezo wako naye hatarajii kamwe ufanye mambo usiyoweza. (Zaburi
19. Kwa nini hupaswi kuogopa kujiweka wakfu kwa Yehova?

Ubatizo na Uhusiano Wako Pamoja na Mungu

181

103:14) Anataka ufanikiwe naye atakutegemeza na kukusaidia. (Isaya 41:10) Bila shaka, ukimtumaini Yehova kabisa, atanyoosha mapito yako.Methali 3:5, 6.
KUONYESHA WAKFU KWA KUBATIZWA Kukiria kwa uzito mambo ambayo tumezungumzia kwaweza kukusaidia kuamua kujiweka wakfu kwa Yehova katika sala. Kila mtu anayempenda Mungu kikweli lazima
20

20. Kwa nini mtu anapaswa kuonyesha hadharani kwamba amejiweka wakfu kwa Yehova?

Je, umejiweka wakfu kwa Mungu katika sala?

Ubatizo humaanisha kufa, au kuacha maisha ya zamani, na kuanza maisha mapya ya kufanya mapenzi ya Mungu

182

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

pia afanye tangazo la hadharani kwa ajili ya wokovu. (Waroma 10:10) Mtu hufanyaje tangazo hilo? 21 Mjulishe mratibu wa baraza la wazee la kutaniko lenu kwamba ungependa kubatizwa. Atapanga wazee fulani wapitie nawe maswali kadhaa yanayohusu mafundisho ya msingi ya Biblia. Wazee hao wakiona kwamba unastahili, watakujulisha kwamba utabatizwa katika kusanyiko linalofuata.1 Kwa kawaida hotuba inayoeleza maana ya ubatizo hutolewa katika makusanyiko hayo. Kisha msemaji huwaomba wote watakaobatizwa wajibu maswali mawili rahisi ikiwa njia moja ya kutoa tangazo la hadharani la imani yao. 22 Ubatizo ndio unaoonyesha hadharani kwamba umejiweka wakfu kwa Mungu na sasa wewe ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Wanaobatizwa huzamishwa kabisa majini ili kuonyesha hadharani kwamba wamejiweka wakfu kwa Yehova.
MAANA YA UBATIZO WAKO Yesu alisema kwamba wanafunzi wake wangebatizwa katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu. (Mathayo 28:19) Hilo linamaanisha kwamba anayetaka kubatizwa anatambua mamlaka ya Yehova Mungu na Yesu Kristo. (Zaburi 83:18; Mathayo 28:18) Pia anatambua kazi na utendaji wa roho takatifu au nguvu ya utendaji ya Mungu.Wagalatia 5:22, 23; 2 Petro 1:21. 24 Hata hivyo, ubatizo si kutumbukizwa majini tu. Una23

1 Ubatizo hufanywa kwa ukawaida katika makusanyiko ya Mashahidi wa Yehova ya kila mwaka. 21, 22. Unawezaje kutoa tangazo la hadharani la imani yako? 23. Inamaanisha nini kubatizwa katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu? 24, 25. (a) Ubatizo huonyesha nini? (b) Ni swali gani linalohitaji kujibiwa?

Ubatizo na Uhusiano Wako Pamoja na Mungu

183

wakilisha jambo fulani muhimu sana. Kuzamishwa majini huonyesha kwamba umekufa, au umeacha maisha yako ya zamani. Na kuibuka kutoka majini huonyesha kwamba sasa umeanza maisha mapya ya kufanya mapenzi ya Mungu. Kumbuka pia kwamba umejiweka wakfu kwa Yehova Mungu mwenyewe wala si kwa kazi fulani, mradi fulani, mtu fulani, au tengenezo fulani. Kujiweka wakfu na kubatizwa ni mwanzo wa kuwa na uhusiano wa karibu sana na Mungu.Zaburi 25:14. 25 Ubatizo haukuhakikishii wokovu. Mtume Paulo aliandika: Endeleeni kuufanyia kazi wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka. (Walipi 2:12) Ubatizo ni mwanzo tu. Kwa hiyo basi, Unawezaje kukaa katika upendo wa Mungu? Sura ya mwisho ya kitabu hiki itajibu swali hilo.
MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA Mkristo hubatizwa kwa kuzamishwa kabisa majini wala si kunyunyiziwa maji.Mathayo 3:16. Hatua zinazoongoza kwenye ubatizo huanza kwa kupata ujuzi, kisha kuwa na imani, halafu kutubu, mwishowe kugeuka na kujiweka wakfu kwa Mungu.Yohana 17:3; Matendo 3:19; 18:8. Ili kujiweka wakfu kwa Yehova, lazima ujikane mwenyewe kama watu walivyojikana wenyewe ili kumfuata Yesu.Marko 8:34. Ubatizo huonyesha kwamba umekufa, au umeacha maisha yako ya zamani, na umeanza maisha mapya ya kufanya mapenzi ya Mungu.1 Petro 4:2.

SURA YA KUMI NA TISA

Kaa Katika Upendo wa Mungu


Kumpenda Mungu kunamaanisha nini? Tunawezaje kukaa katika upendo wa Mungu? Yehova atawathawabishaje wale wanaokaa katika upendo wake?
WAZIA kwamba unatembea barabarani siku yenye dhoruba kali. Mawingu yanazidi kutanda. Radi inapiga na ngurumo zinasikika, kisha mvua kubwa inanyesha. Unakimbia huku na huku ukitafuta mahali pa kujikinga. Halafu, ngambo ya barabara unaona mahali pa kujikinga. Ni mahali imara, pakavu, na penye kuvutia. Unafurahi kama nini kupaona mahali hapo! 2 Tunaishi katika nyakati zenye msukosuko. Hali za ulimwengu zinaendelea kuzorota. Hata hivyo, kuna mahali salama, kimbilio linaloweza kutukinga. Ni wapi tunapoweza kupata kimbilio hilo? Biblia inafundisha hivi: Nitamwambia Yehova: Wewe ni kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye nitamtegemea. Zaburi 91:2. 3 Hebu wazia! Yehova, Muumba anayeutawala ulimwengu mzima, anaweza kuwa kimbilio letu. Anaweza kutulinda kwa kuwa
1, 2. Tunaweza kupata wapi kimbilio salama leo? 3. Tunawezaje kumfanya Yehova kuwa kimbilio letu?

Je, utamfanya Yehova awe kimbilio lako katika nyakati hizi zenye msukosuko?

Kaa Katika Upendo wa Mungu

185

yeye ana nguvu nyingi kuliko yeyote au chochote kinachoweza kutuumiza. Hata tukiumizwa, Yehova anaweza kuondoa madhara yote mabaya. Tunawezaje kumfanya Yehova kuwa kimbilio letu? Tunahitaji kumtumaini. Isitoshe, Neno la Mungu linatusihi: Jitunzeni katika upendo wa Mungu. (Yuda 21) Ndiyo, tunahitaji kukaa katika upendo wa Mungu kwa kudumisha kifungo cha upendo pamoja na Baba yetu wa mbinguni. Ndipo tunapoweza kuwa na hakika kwamba yeye ni kimbilio letu. Tunawezaje kudumisha kifungo hicho?

ZINGATIA UPENDO WA MUNGU NA KUTENDA KUPATANA NAO 4 Ili tuendelee kukaa katika upendo wa Mungu, tunapaswa kutambua jinsi Yehova ametuonyesha upendo wake. Fikiria baadhi ya mafundisho ya Biblia ambayo umejifunza katika kitabu hiki. Akiwa Muumba, Yehova ametupatia dunia iwe makao yetu yenye kupendeza. Ameijaza chakula na maji mengi, mali za asili, wanyama wenye kuvutia, na mandhari maridadi. Akiwa Mtungaji wa Biblia, Mungu ametujulisha jina lake na sifa zake. Isitoshe, Neno lake husema kwamba alimtuma Mwana wake mpendwa duniani na kuruhusu ateseke na kufa kwa ajili yetu. (Yohana 3:16) Zawadi hiyo ina maana gani kwetu? Inatupa tumaini la kuwa na maisha mazuri wakati ujao. 5 Pia tumaini letu la wakati ujao linategemea jambo fulani ambalo Mungu amefanya. Yehova amesimamisha serikali ya kimbingu, Ufalme wa Kimasihi. Karibuni itakomesha mateso yote na kuifanya dunia iwe paradiso. Hebu wazia! Tunaweza kuishi humo tukiwa na amani na furaha milele. (Zaburi 37:29) Kwa sasa, Mungu ametupa mwongozo wa kuishi maisha bora zaidi sasa. Pia ametupa zawadi ya sala, inayotusaidia kuwasiliana naye wakati wowote. Hizo ni baadhi ya njia chache tu ambazo Yehova ameonyesha
4, 5. Taja baadhi ya njia ambazo Yehova ameonyesha upendo kwetu.

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

upendo kwa wanadamu wote kwa ujumla na kwako wewe binafsi. 6 Hebu kiria swali hili: Nitaonyeshaje kwamba ninathamini upendo wa Yehova? Huenda wengi wakajibu, Kwa kumpenda pia. Je, hivyo ndivyo unavyohisi? Yesu alisema kwamba hii ndiyo amri kuu zaidi: Lazima umpende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote. (Mathayo 22:37) Bila shaka una sababu nyingi za kumpenda Yehova Mungu. Lakini je, kuhisi tu kwamba una upendo huo kunatosha kuonyesha kwamba unampenda Yehova kwa moyo, nafsi, na akili yako yote? 7 Kama Biblia inavyoonyesha, kumpenda Mungu si hisia tu. Ingawa ni muhimu kuhisi kwamba unampenda Yehova, huo ni mwanzo tu wa kumpenda kikweli. Mti wa matunda hutokana na mbegu. Ikiwa unataka kula tunda, je, utatosheka tu mtu akikupa mbegu ya tunda hilo? Hapana! Vivyo hivyo, kuhisi kwamba unampenda Yehova Mungu ni mwanzo tu. Biblia inafundisha: Kumpenda Mungu humaanisha hivi, kwamba tuzishike amri zake; na bado amri zake si mzigo mzito. (1 Yohana 5:3) Ili tumpende Mungu kikweli, lazima tuzae matunda mazuri. Ni lazima tuonyeshe kwa matendo kwamba tunampenda.Mathayo 7:16-20. 8 Tunaonyesha kwamba tunampenda Mungu tunaposhika amri zake na kufuata kanuni zake. Si vigumu kufanya hivyo. Sheria za Yehova si nzito bali zimekusudiwa kutusaidia kuishi maisha mazuri, yenye furaha, na yenye kuridhisha. (Isaya 48:17, 18) Tunapoishi kupatana na mwongozo wa Yehova, tunamwonyesha Baba yetu wa mbinguni
6. Unawezaje kuonyesha kwamba unathamini upendo ambao Yehova amekuonyesha? 7. Je, kumpenda Mungu ni kuwa na hisia tu? Eleza. 8, 9. Tunawezaje kuonyesha upendo na shukrani kwa Mungu?

Kaa Katika Upendo wa Mungu

187

kwamba tunathamini kikweli yale yote ambayo ametufanyia. Inasikitisha kwamba ni watu wachache ulimwenguni leo wenye uthamini kama huo. Hatutaki kukosa uthamini kama watu fulani walioishi wakati Yesu alipokuwa duniani. Yesu aliwaponya watu kumi wenye ukoma, lakini ni mmoja tu aliyerudi kumshukuru. (Luka 17:12-17) Bila shaka tungependa kuwa wenye shukrani kama yule mtu mmoja wala si kama wale wengine tisa wasio na shukrani! 9 Ni amri gani za Yehova tunazopaswa kutii? Tumezungumzia amri kadhaa katika kitabu hiki, hebu tujikumbushe chache. Kutii amri za Mungu kutatusaidia kukaa katika upendo wa Mungu.

MKARIBIE YEHOVA ZAIDI Kujifunza juu ya Yehova ni hatua muhimu ya kumkaribia. Ni hatua inayopaswa kuendelea daima. Tuseme unaota moto wakati wa usiku wenye baridi, je, ungeuacha moto huo ue na kuzimika? Hapana. Utaendelea
10

10. Eleza kwa nini ni muhimu kuendelea kupata ujuzi juu ya Yehova Mungu.

Kama moto, upendo wako kwa Yehova unahitaji kuchochewa ili uendelee kuwaka

188

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

kuongeza kuni ili moto uendelee kuwaka. Huenda uhai wako unautegemea! Sawa na vile kuni huchochea moto, ndivyo kumjua Mungu kunavyoimarisha upendo wetu kwa Yehova.Methali 2:1-5. 11 Yesu alitaka wanafunzi wake waendelee kuimarisha upendo wao kwa Yehova na Neno lake la kweli lenye thamani. Baada ya kufufuliwa, Yesu aliwafundisha wanafunzi wake wawili baadhi ya unabii ulio katika Maandiko ya Kiebrania ambao ulitimizwa maishani mwake. Matokeo yakawaje? Baadaye walisema hivi: Je, mioyo yetu haikuwa ikiwaka alipokuwa akisema nasi barabarani, alipokuwa akitufungulia Maandiko?Luka 24:32. 12 Ulipojifunza kwa mara ya kwanza mambo ambayo Biblia inafundisha hasa, je, hukufurahi sana, ukawa na bidii na upendo mwingi sana kumwelekea Mungu? Bila shaka. Wengi wamehisi hivyo. Kazi kubwa sasa ni kuendelea kukuza na kuimarisha upendo huo. Hatutaki kuuiga ulimwengu. Yesu alitabiri hivi: Upendo wa walio wengi zaidi utapoa. (Mathayo 24:12) Unawezaje kuendelea kumpenda Yehova na kweli zake zilizo katika Biblia? 13 Endelea kupata ujuzi juu ya Yehova Mungu na Yesu Kristo. (Yohana 17:3) Tafakari au kiria kwa uzito mambo unayojifunza katika Neno la Mungu, na ujiulize: Mambo hayo yananifundisha nini juu ya Yehova Mungu? Yananisaidiaje kumpenda Yehova zaidi kwa moyo, akili, na nafsi yangu yote? (1 Timotheo 4:15) Kutafakari juu ya mambo hayo kutakufanya umpende Yehova zaidi. 14 Njia nyingine ya kuimarisha upendo wako kwa Yehova ni kusali kwa ukawaida. (1 Wathesalonike 5:17) Katika
11. Mafundisho ya Yesu yalikuwa na matokeo gani kwa wanafunzi wake? 12, 13. (a) Upendo wa watu wengi ulimwenguni kumwelekea Mungu na Biblia ukoje? (b) Tunawezaje kuendeleza upendo wetu? 14. Sala inawezaje kutusaidia kuendelea kukaa katika upendo wa Yehova?

Kaa Katika Upendo wa Mungu

189

Sura ya 17 ya kitabu hiki tulijifunza kwamba sala ni zawadi yenye thamani kutoka kwa Mungu. Kama vile uhusiano kati ya wanadamu husitawi kwa sababu ya kuwasiliana kwa uhuru na kwa ukawaida, uhusiano wetu na Yehova hukua na kuimarika tunaposali kwa ukawaida. Hatupaswi kusali kidesturi tu, tukirudia-rudia maneno yaleyale bila hisia wala maana yoyote. Tunapaswa kuzungumza na Yehova kama vile mtoto anavyozungumza na baba anayempenda. Bila shaka, tunataka kuzungumza kwa heshima, lakini waziwazi, kwa unyoofu, na kutoka moyoni. (Zaburi 62:8) Ndiyo, funzo la Biblia la kibinafsi na sala inayotoka moyoni ni mambo muhimu katika ibada yetu, nayo hutusaidia kuendelea kukaa katika upendo wa Mungu.

UWE NA SHANGWE KATIKA IBADA Funzo la Biblia la kibinafsi na sala ni matendo ya ibada ambayo tunaweza kufanya faraghani. Hata hivyo, na tuchunguze sehemu moja ya ibada yetu tunayofanya hadharani, yaani, kuzungumza na wengine kuhusu imani yetu. Je, tayari umezungumza na watu fulani kuhusu kweli za Biblia? Ikiwa ndivyo, haikosi umefurahia kufanya hivyo. (Luka 1:74) Tunapozungumza na wengine kweli ambazo tumejifunza juu ya Yehova Mungu, tunatimiza mgawo muhimu sana ambao Wakristo wote wa kweli wamekabidhiwa, yaani, mgawo wa kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu. Mathayo 24:14; 28:19, 20. 16 Mtume Paulo aliiona huduma yake kuwa yenye thamani sana, aliiita hazina. (2 Wakorintho 4:7) Kazi bora unayoweza kufanya ni kuzungumza na watu juu ya Yehova Mungu na makusudi yake. Yeye ndiye Bwana bora zaidi, na kumtumikia huleta faida zisizo na kifani. Kwa kufanya kazi hiyo, unawasaidia watu wenye mioyo minyoofu wamkaribie Baba yetu wa mbinguni na kutembea katika
15

15, 16. Kwa nini tuione kazi ya kuhubiri Ufalme kuwa pendeleo na hazina?

190

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

barabara ya uzima wa milele! Hakuna kazi yenye kuridhisha kama hiyo. Isitoshe, kuhubiri juu ya Yehova na Neno lake huongeza imani yako na kuimarisha upendo wako kwake. Na Yehova anathamini jitihada zako. (Waebrania 6:10)
Yehova angependa upate uzima ulio wa kweli. Je, utaupata?

Kaa Katika Upendo wa Mungu

191

Kufanya kazi hiyo kwa bidii kutakusaidia kuendelea kukaa katika upendo wa Mungu.1 Wakorintho 15:58. 17 Tunapaswa kukumbuka kwamba kazi ya kuhubiri Ufalme ni muhimu sana. Biblia inasema: Lihubiri neno, fanya hivyo kwa bidii. (2 Timotheo 4:2) Kwa nini ni muhimu kufanya hivyo leo? Neno la Mungu linatuambia: Ile siku kuu ya Yehova iko karibu. Iko karibu, nayo inaharakisha sana. (Sefania 1:14) Ndiyo, wakati wa Yehova kuharibu mfumo huu wote wa mambo unakaribia sana. Watu wanapaswa kuonywa! Wanapaswa kujua kwamba huu ndio wakati wa kumchagua Yehova kuwa Mwenye Enzi Kuu wao. Mwisho hautachelewa.Habakuki 2:3. 18 Yehova anataka tumwabudu pamoja na Wakristo wa kweli. Ndiyo sababu Neno lake linasema hivi: Acheni tukiriane ili kuchocheana katika upendo na matendo mazuri, bila kuacha kukusanyika pamoja sisi wenyewe, kama vile wengine walivyo na desturi, bali tutiane moyo, na kufanya hivyo zaidi kwa kadiri mnavyoona siku ile kuwa inakaribia. (Waebrania 10:24, 25) Tunapokusanyika pamoja na waamini wenzetu katika mikutano ya Kikristo, tuna nafasi nzuri ya kumsifu na kumwabudu Mungu wetu tunayempenda. Pia tunajengana na kutiana moyo. 19 Tunaposhirikiana na waabudu wa Yehova, tunaimarisha vifungo vya upendo na uraki kutanikoni. Tunapaswa kuzingatia wema wa wengine, kama Yehova anavyozingatia wema wetu. Usitazamie waamini wenzako wawe wakamilifu. Kumbuka kwamba wote wamekia viwango tofauti vya ukomavu wa kiroho, na kwamba kila mmoja wetu hufanya makosa. (Wakolosai 3:13) Jitahidi kufanya uraki na wale wanaompenda Yehova sana, nawe utafanya maendeleo ya kiroho. Ndiyo, kumwabudu Yehova pamoja na ndugu na
17. Kwa nini huduma ya Kikristo ni muhimu leo? 18. Kwa nini tumwabudu Yehova pamoja na Wakristo wa kweli? 19. Tunawezaje kuimarisha vifungo vya upendo katika kutaniko la Kikristo?

192

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

dada zako wa kiroho kutakusaidia kukaa katika upendo wa Mungu. Yehova huwathawabishaje wale wanaomwabudu kwa uaminifu na kukaa katika upendo wake?

JITAHIDI KUPATA UZIMA ULIO WA KWELI Yehova huwathawabisha watumishi wake waaminifu kwa kuwapa uzima, au uhai. Hata hivyo, ni uhai wa aina gani? Je, kweli uko hai sasa? Wengi wetu wangejibu, Ndiyo. Kwani, si tunapumua, tunakula, na kunywa? Bila shaka, tuko hai. Na tunapokuwa na furaha, huenda tukasema, Haya ndiyo maisha! Hata hivyo, Biblia inaonyesha kwamba, katika maana halisi, hakuna mwanadamu yeyote ambaye ana uzima wa kweli. 21 Neno la Mungu linatuhimiza tuushike imara uzima ulio wa kweli. (1 Timotheo 6:19) Maneno hayo yanaonyesha kwamba tuna tumaini la kupata uzima ulio wa kweli wakati ujao. Ndiyo, tutakapokuwa wakamilifu, tutakuwa na uzima wa kweli, kwa maana tutaishi kama Mungu alivyokusudia tuishi. Tutakapoishi katika paradiso duniani tukiwa na afya kamili, amani, na furaha, ndipo tutakapofurahia uzima ulio wa kweliuzima wa milele. (1 Timotheo 6:12) Je, hilo si tumaini zuri? 22 Tunawezaje kushika imara uzima ulio wa kweli? Akizungumzia jambo hilohilo, Paulo aliwahimiza Wakristo wafanye mema na wawe matajiri katika matendo mazuri. (1 Timotheo 6:18) Basi, ni wazi kwamba tunahitaji kutumia kweli ambazo tumejifunza katika Biblia. Lakini je, Paulo alimaanisha kwamba uzima ulio wa kweli ni malipo ya kutenda mema? Hapana, kwa maana tumaini hilo zuri hutegemea fadhili zisizostahiliwa kutoka kwa Mungu. (Waroma 5:15) Hata hivyo, Yehova anapenda kuwathawabisha wale wanaomtumikia kwa uaminifu. Angependa upate
20

20, 21. Uzima ulio wa kweli ni nini, na kwa nini tumaini hilo ni zuri? 22. Unawezaje kushika imara uzima ulio wa kweli?

Kaa Katika Upendo wa Mungu

193

uzima ulio wa kweli. Wale wanaokaa katika upendo wa Mungu ndio watakaopata uzima huo wa milele, wenye furaha na amani. 23 Kila mmoja wetu anapaswa kujiuliza, Je, ninamwabudu Mungu kupatana na maagizo yake yaliyo katika Biblia? Ikiwa tunafanya hivyo kila siku, basi tunatembea katika njia inayofaa. Tunaweza kuwa na hakika kwamba Yehova ni kimbilio letu. Atawaokoa watu wake waaminifu katika siku hizi za mwisho zenye taabu za mfumo huu wa kale wa mambo. Pia, Yehova atatukomboa na kutuingiza katika mfumo mpya mtukufu ulio karibu. Tutakuwa na shangwe iliyoje kuishi wakati huo! Na tutakuwa na furaha iliyoje kwa kuwa tulifanya maamuzi yanayofaa katika siku hizi za mwisho! Ukifanya maamuzi yanayofaa sasa, utapata uzima ulio wa kweli, uzima ambao Yehova Mungu alikusudia, kwa umilele wote!
23. Kwa nini ni muhimu kukaa katika upendo wa Mungu?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA Tunaonyesha kwamba tunampenda Mungu kikweli tunaposhika amri zake na kufuata kanuni zake.1 Yohana 5:3. Kujifunza Neno la Mungu, kusali kwa Yehova kutoka moyoni, kuwafundisha wengine kumhusu, na kumwabudu katika mikutano ya Kikristo kutatusaidia kukaa katika upendo wa Mungu.Mathayo 24:14; 28:19, 20; Yohana 17:3; 1 Wathesalonike 5:17; Waebrania 10:24, 25. Wale wanaokaa katika upendo wa Mungu wana tumaini la kupata uzima ulio wa kweli.1 Timotheo 6:12, 19; Yuda 21.

NYONGEZA
HABARI UKURASA

Jina la MunguMaana na Matumizi 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 195 Jinsi Unabii wa Danieli Ulivyotabiri Kutokea kwa Masihi 9 9 9 197 Yesu KristoMasihi Aliyeahidiwa 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 199 Ukweli Kuhusu Baba, Mwana, na Roho Takatifu 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 201 Kwa Nini Wakristo wa Kweli Hawatumii Msalaba Katika Ibada? 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 204 Mlo wa Jioni wa Bwana Maadhimisho Yanayomletea Mungu Heshima 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 206 Maneno Nafsi na Roho Yanamaanisha Nini Hasa? 9 9 9 9 9 208 Sheoli na Hadesi Zinamaanisha Nini? 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 212 Siku ya Hukumu Ni Nini? 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 213 1914Mwaka Muhimu Katika Unabii wa Biblia 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 215 Yule Malaika Mkuu Mikaeli Ni Nani? 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 218 Kumtambulisha Babiloni Mkubwa 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 219 Je, Yesu Alizaliwa Desemba? 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 221 Je, Tusherehekee Sikukuu? 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 9 222

195

Jina la Mungu Maana na Matumizi


ANDIKO la Zaburi 83:18 limetafsiriwaje katika Biblia yako? Biblia TakatifuTafsiri ya Ulimwengu Mpya husema hivi: Ili watu wajue kwamba wewe, ambaye jina lako ni Yehova, wewe peke yako ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote. Biblia nyingine hutumia maneno yanayofanana na hayo. Hata hivyo, tafsiri nyingi hazitumii jina Yehova, badala yake zinatumia majina ya heshima kama vile Bwana au Mwenyezi. Ni jina gani linalopaswa kutumiwa katika mstari huo? Jina la heshima au jina halisi Yehova? Mstari huo unazungumzia jina halisi. Katika Kiebrania cha awali ambacho kilitumiwa kuandika sehemu kubwa ya Biblia, jina halisi la pekee linatumiwa katika mstari huo. Linaandikwa hivi katika heru za Kiebrania LYHWHMD Katika KiswahiliE mara nyingi jina hilo hutafsiriJina la Mungu wa Yehova. Je, jina hilo hupatikana katika katika heru mstari mmoja tu wa Biblia? Hapana. Liza Kiebrania napatikana katika maandishi ya awali ya Maandiko ya Kiebrania karibu mara 7,000! Jina la Mungu ni muhimu kadiri gani? Fikiria ile sala ya mfano ambayo Yesu Kristo aliwafundisha wanafunzi wake. Inaanza kwa kusema: Baba yetu uliye mbinguni, jina lako na litakaswe. (Mathayo 6:9) Baadaye, Yesu alisali hivi kwa Mungu: Baba, litukuze jina lako. Mungu akajibu kutoka mbinguni, akisema Nimelitukuza na pia nitalitukuza tena. (Yohana 12:28) Ni wazi kwamba jina la Mungu ni muhimu sana. Kwa nini basi watafsiri fulani wameliondoa jina hilo katika Biblia wanapotafsiri na kutumia majina ya heshima badala yake? Inaonekana kuna sababu mbili kuu. Kwanza, wengi wao hudai kwamba jina hilo halipaswi kutumiwa kwa sababu hakuna yeyote leo anayejua jinsi lilivyokuwa likitamkwa zamani. Kiebrania cha awali hakikuandikwa kwa kutumia irabukama vile a, e, i, o, u. Kwa hiyo, hakuna yeyote leo anayeweza kusema kwa uhakika jinsi watu wa nyakati za Biblia walivyotamka jina YHWH. Hata

196

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

hivyo, je, hilo lituzuie tusitumie jina la Mungu? Katika nyakati za Biblia, huenda jina Yesu lilikuwa likitamkwa Yeshua au hata Yehoshuahakuna yeyote anayejua kwa hakika. Hata hivyo, leo watu ulimwenguni pote wanatumia namna mbalimbali za jina Yesu, wakilitamka jinsi linavyotamkwa kwa ukawaida katika lugha yao. Hawasiti kulitumia jina hilo eti kwa sababu hawajui jinsi lilivyokuwa likitamkwa katika karne ya kwanza. Pia, ikiwa ungesari kwenda nchi nyingine, huenda ukaona kwamba jina lako mwenyewe linatamkwa kwa njia tofauti kabisa katika lugha nyingine. Kwa hiyo, kutojua jinsi jina la Mungu lilivyokuwa likitamkwa zamani si sababu ya kutolitumia. Sababu ya pili ambayo hutolewa mara nyingi inayowafanya watafsiri fulani waliondoe jina la Mungu katika Biblia inahusisha mapokeo ya kale ya Wayahudi. Wengi wao huamini kwamba jina la Mungu halipaswi kutajwa. Inaonekana imani hiyo inatokana na kutoelewa vizuri sheria ya Biblia inayosema: Usilitumie jina la Yehova Mungu wako kwa njia isiyofaa, kwa maana Yehova hatamwacha bila kuadhibiwa yule anayelitumia jina lake kwa njia isiyofaa.Kutoka 20:7. Sheria hiyo inakataza kulitumia jina la Mungu kwa njia isiyofaa. Lakini je, inakataza kulitumia jina lake kwa heshima? Hapana. Waandikaji wote wa Maandiko ya Kiebrania (Agano la Kale) walikuwa wanaume waaminifu waliotii Sheria ambayo Mungu aliwapa Waisraeli wa kale. Hata hivyo, walilitumia jina la Mungu kwa ukawaida. Kwa mfano, walilitia katika zaburi nyingi zilizoimbwa na umati wa waabudu kwa sauti. Yehova Mungu hata aliwaagiza waabudu wake waliitie jina lake, na wale waliokuwa waaminifu walifanya hivyo. (Yoeli 2:32; Matendo 2:21) Kwa hiyo, Wakristo leo hawasiti kulitumia jina la Mungu kwa heshima, kama Yesu alivyofanya.Yohana 17:26. Wanapoliondoa jina la Mungu na kutumia majina ya heshima badala yake, watafsiri wa Biblia hufanya kosa kubwa. Wanamfanya Mungu asijulikane, na hali Biblia inawahimiza wanadamu wasitawishe uraki wa karibu pamoja na Yehova. (Zaburi 25:14) Ikiwa ungekuwa na raki ambaye hujui jina lake, uhusiano wenu ungekuwa wa karibu kadiri gani? Vivyo hivyo, watu wasipojulishwa jina la Mungu, Yehova, wanawezaje kumkaribia?

Nyongeza

197

Isitoshe, watu wasipolitumia jina la Mungu, hawawezi kuelewa maana muhimu ya jina hilo. Jina la Mungu linamaanisha nini? Mungu mwenyewe alimweleza mtumishi wake mwaminifu Musa maana ya jina lake. Musa alipomwuliza Mungu jina lake, Yehova alimjibu: Nitakuwa kile nitakachokuwa. (Kutoka 3:14) Tafsiri ya Rotherham inatafsiri hivi maneno hayo: Nitakuwa chochote Nipendacho kuwa. Kwa hiyo, Yehova anaweza kuwa chochote kinachohitajika ili kutimiza makusudi yake. Hebu wazia kwamba ungeweza kuwa chochote ambacho ungependa kuwa. Ungewafanyia nini raki zako? Ikiwa mmoja wao angekuwa mgonjwa sana, ungeweza kuwa daktari stadi na kumtibu. Ikiwa mwingine angelisika, ungeweza kuwa tajiri na kumsaidia. Hata hivyo, ukweli ni kwamba wewe huna uwezo wa kuwa chochote ambacho ungependa kuwa. Hakuna yeyote kati yetu aliye na uwezo huo. Unapoendelea kujifunza Biblia, utafurahi kuona jinsi Yehova huwa chochote kinachohitajika ili kutimiza makusudi yake. Naye anapenda kutumia nguvu zake kwa niaba ya wale wanaompenda. (2 Mambo ya Nyakati 16:9) Wale wasiojua jina la Yehova hawawezi kuuona uwezo wake wa kuwa chochote anachopenda kuwa. Ni wazi kwamba, jina Yehova linapaswa kuwa katika Biblia. Kujua maana yake na kulitumia kwa uhuru katika ibada yetu kunaweza kutusaidia sana kumkaribia Baba yetu wa mbinguni Yehova.1
1 Unaweza kupata habari zaidi kuhusu jina la Mungu, maana yake, na sababu za kulitumia katika ibada kwenye broshua Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, iliyochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

Jinsi Unabii wa Danieli Ulivyotabiri Kutokea kwa Masihi


NABII Danieli aliishi zaidi ya miaka 500 kabla ya kuzaliwa kwa Yesu. Hata hivyo, Yehova alimpa Danieli ujumbe ambao ungefanya iwezekane kujua wakati hususa ambapo Yesu angetiwa mafuta

198

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

au kuwekwa rasmi kuwa Masihi au Kristo. Danieli aliambiwa hivi: Ujue na ufahamu kwamba tangu kutolewa kwa lile neno la kurudisha na kujenga upya Yerusalemu mpaka Masihi aliye Kiongozi, kutakuwa na majuma 7, pia majuma 62.Danieli 9:25. Ili kujua wakati ambapo Masihi angetokea, kwanza tunahitaji kujua mwanzo wa kile kipindi ambacho Masihi angetokea mwishoni mwake. Kulingana na unabii huo, kingeanza wakati ambapo lile neno la kurudisha na kujenga upya Yerusalemu lingetolewa. Neno hilo lilitolewa wakati gani? Kulingana na Nehemia, mwandishi wa Biblia, neno la kujenga upya kuta za Yerusalemu lilitolewa katika mwaka wa 20 wa Mfalme Artashasta. (Nehemia 2:1, 5-8)

MAJUMA 70
Miaka 490

Majuma 7
(Miaka 49) 455 406

Majuma 62
(Miaka 434) & K.W.K. W.K. ) 29

Juma 1
(Miaka 7) 33 36

Lile neno la kurudisha . . . Yerusalemu

Masihi atokea

Masihi akatiliwa mbali Mwisho wa yale majuma 70

Yerusalemu lajengwa upya

Nyongeza

199

Wanahistoria wanathibitisha kwamba mwaka wa 474 K.W.K., ndio uliokuwa mwaka wa kwanza wa utawala wa Artashasta. Kwa hiyo, mwaka wa 20 wa utawala wake ni mwaka wa 455 K.W.K. Kwa hiyo, kile kipindi cha unabii wa Danieli kuhusu Masihi kingeanza mwaka wa 455 K.W.K. Pili, Danieli anaonyesha urefu wa kipindi hicho ambacho Masihi aliye Kiongozi angetokea. Unabii huo unataja majuma 7, pia majuma 62jumla ya majuma 69. Kipindi hicho kina urefu gani? Tafsiri kadhaa za Biblia zinaonyesha kwamba hayo si majuma ya siku saba, bali ya miaka. Yaani, kila juma linawakilisha miaka saba. Wayahudi wa kale walizoea kuhesabu majuma ya miaka, au vipindi vya miaka saba. Kwa mfano, kila mwaka wa saba ulikuwa mwaka wa Sabato. (Kutoka 23:10, 11) Kwa hiyo, yale majuma 69 ya unabii yalikuwa vipindi 69 vya miaka 7 kila kimoja, au jumla ya miaka 483. Sasa tunachohitaji ni kupiga hesabu tu. Tukihesabu miaka 483 kuanzia mwaka wa 455 K.W.K., tutaka mwaka wa 29 W.K. Huo ndio mwaka hususa ambao Yesu alibatizwa na kuwa Masihi!1 (Luka 3:1, 2, 21, 22) Je, huo si utimizo wenye kustaajabisha wa unabii wa Biblia?
1 Kuanzia mwaka wa 455 K.W.K. hadi mwaka wa 1 K.W.K. ni miaka 454. Kuanzia mwaka wa 1 K.W.K. hadi 1 W.K. ni mwaka mmoja (hakukuwa na mwaka sufuri). Na kuanzia mwaka wa 1 W.K. hadi mwaka wa 29 W.K. ni miaka 28. Tukijumlisha miaka hiyo tunapata jumla ya miaka 483. Yesu alikatiliwa mbali alipouawa mwaka wa 33 W.K., katika juma la 70 la miaka. (Danieli 9:24, 26) Unaweza kupata habari zaidi kuhusu unabii huo katika kitabu Sikiliza Unabii wa Danieli! sura ya 11, na Insight on the Scriptures, Buku la 2, ukurasa wa 899-901 au Etude Perspicase, Buku la 2, ukurasa wa 995-997. Vitabu hivyo vimechapishwa na Mashahidi wa Yehova.

Yesu Kristo Masihi Aliyeahidiwa


ILI kutusaidia kumtambua Masihi, Yehova Mungu aliwaongoza manabii wengi wa Biblia waandike habari kuhusu kuzaliwa, huduma, na kifo cha Mkombozi aliyeahidiwa. Unabii wote huo

200

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

UNABII KUMHUSU MASIHI


TUKIO UNABII UTIMIZO

Azaliwa katika kabila la Yuda Azaliwa na bikira Mzao wa Mfalme Daudi Yehova amtangaza kuwa Mwanawe Akosa kuaminiwa Aingia Yerusalemu akiwa amepanda punda Asalitiwa na mtu wa karibu Asalitiwa kwa vipande 30 vya fedha Akaa kimya mbele ya waliomshtaki Mavazi yake yapigiwa kura Atukanwa akiwa kwenye mti wa mateso Hakuna mfupa wake uliovunjwa Azikwa pamoja na matajiri Afufuliwa kabla ya mwili wake kuharibika Akwezwa kwenye mkono wa kuume wa Mungu

Mwanzo 49:10 Isaya 7:14 Isaya 9:7 Zaburi 2:7 Isaya 53:1 Zekaria 9:9 Zaburi 41:9 Zekaria 11:12 Isaya 53:7 Zaburi 22:18 Zaburi 22:7, 8 Zaburi 34:20 Isaya 53:9 Zaburi 16:10 Zaburi 110:1

Luka 3:23-33 Mathayo 1:18-25 Mathayo 1:1, 6-17 Mathayo 3:17 Yohana 12:37, 38 Mathayo 21:1-9 Yohana 13:18, 21-30 Mathayo 26:14-16 Mathayo 27:11-14 Mathayo 27:35 Mathayo 27:39-43 Yohana 19:33, 36 Mathayo 27:57-60 Matendo 2:24, 27 Matendo 7:56

wa Biblia ulitimizwa maishani mwa Yesu Kristo. Unabii huo ni sahihi sana na una habari kamili. Kwa mfano, hebu tuchunguze unabii mbalimbali uliotabiri kuzaliwa kwa Masihi na maisha yake ya utotoni. Nabii Isaya alitabiri kwamba Masihi angetokea katika ukoo wa Mfalme Daudi. (Isaya 9:7) Kwa kweli, Yesu alizaliwa katika ukoo wa Daudi.Mathayo 1:1, 6-17.

Nyongeza

201

Mika, nabii mwingine wa Mungu alitabiri kwamba hatimaye mtoto huyo angekuwa mtawala na kwamba angezaliwa Bethlehemu Efratha. (Mika 5:2) Wakati ambapo Yesu alizaliwa, kulikuwa na miji miwili huko Israeli iliyokuwa ikiitwa Bethlehemu. Mji mmoja ulikuwa karibu na Nazareti, kaskazini mwa nchi hiyo, nao ule mwingine ulikuwa karibu na Yerusalemu huko Yuda. Mji wa Bethlehemu, uliokuwa karibu na Yerusalemu, ulikuwa ukiitwa Efratha zamani. Yesu alizaliwa katika mji huo, kama vile tu unabii ulivyokuwa umetabiri!Mathayo 2:1. Unabii mwingine wa Biblia ulitabiri kwamba Mwana wa Mungu angeitwa kutoka Misri. Mtoto huyo, Yesu, alipelekwa Misri. Alirudishwa kutoka huko baada ya kifo cha Herode, na hivyo, unabii huo ukatimia.Hosea 11:1; Mathayo 2:15. Katika ukurasa wa 200, maandiko yaliyoorodheshwa chini ya kichwa Unabii yanaeleza mambo mengi zaidi kumhusu Masihi. Tafadhali linganisha maandiko hayo na yale yaliyo chini ya kichwa Utimizo. Kufanya hivyo kutaimarisha zaidi imani yako katika ukweli wa Neno la Mungu. Unapochunguza maandiko hayo kumbuka kwamba maandiko yenye unabii yaliandikwa mamia ya miaka kabla ya kuzaliwa kwa Yesu. Yesu alisema: Mambo yote yaliyoandikwa katika sheria ya Musa na katika Manabii na Zaburi juu yangu lazima yatimizwe. (Luka 24:44) Biblia inaonyesha wazi kwamba unabii huo ulitimia kabisa!

Ukweli Kuhusu Baba, Mwana, na Roho Takatifu


WATU wanaoamini Utatu husema kwamba kuna Mungu Baba, Mungu Mwana, na Mungu Roho Mtakatifu. Wote wanasemekana kuwa sawa, wenye nguvu zote, na hawana mwanzo. Kwa hiyo, kulingana na fundisho la Utatu, Baba ni Mungu, Mwana ni Mungu, na Roho Mtakatifu ni Mungu, hata hivyo, Mungu ni mmoja tu.

202

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Wengi wanaoamini fundisho la Utatu hukubali kwamba hawawezi kulieleza. Lakini, huenda wakakiri kwamba hilo ni fundisho la Biblia. Ni muhimu kutambua kwamba neno Utatu halipatikani kamwe katika Biblia. Lakini je, wazo lenyewe linapatikana katika Biblia? Ili kujibu swali hilo, hebu tuchunguze andiko ambalo wanaounga mkono fundisho hilo hutumia kutetea Utatu.
NENO ALIKUWA MUNGU Andiko la Yohana 1:1 linasema: Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. (Union Version) Baadaye, katika sura hiyohiyo, mtume Yohana anaonyesha waziwazi kwamba Neno ni Yesu. (Yohana 1:14) Hata hivyo, kwa kuwa Neno anaitwa Mungu, watu fulani hukata kauli kwamba Mwana na Baba ni Mungu yuleyule. Kumbuka kwamba mwanzoni sehemu hiyo ya Biblia iliandikwa katika Kigiriki. Baadaye, mstari huo wa Kigiriki ulitafsiriwa katika lugha nyingine. Hata hivyo, watafsiri fulani wa Biblia hawakusema Neno alikuwa Mungu. Kwa nini? Kulingana na ufahamu wao wa lugha ya Kigiriki iliyotumiwa kuandika Biblia, watafsiri hao walikata kauli kwamba maneno Neno alikuwa Mungu yalipaswa kutafsiriwa tofauti. Jinsi gani? Kuna mifano michache hapa: Logos [Neno] alikuwa na sifa za kimungu. (A New Translation of the Bible) Neno alikuwa mungu. (The New Testament in an Improved Version) Neno alikuwa pamoja na Mungu na alikuwa na utu kama wake. (The Translators New Testament) Kulingana na tafsiri hizo, Neno si Mungu mwenyewe.1 Badala yake, kwa sababu ya ukuu wake miongoni mwa viumbe wa Yehova, Neno anaitwa mungu. Hapa, jina mungu linamaanisha mwenye nguvu. PATA HABARI ZAIDI Watu wengi hawajui Kigiriki kilichotumiwa kuiandika Bib1 Kwa habari zaidi kuhusu Yohana 1:1, ona gazeti la Mnara wa Mlinzi la Novemba 1, 2008, ukurasa wa 24-25, lililochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

Nyongeza

203

lia. Basi unawezaje kujua alichomaanisha mtume Yohana? Fikiria mfano huu: Mwalimu anawafundisha wanafunzi jambo fulani. Baadaye, wanafunzi wanakuwa na maoni tofauti kuhusu jambo walilofundishwa. Wanafunzi hao wanaweza kutatuaje tofauti zao? Wanaweza kumwomba mwalimu awape habari zaidi. Bila shaka, kupata habari zaidi kutawasaidia kuelewa jambo hilo vizuri zaidi. Vivyo hivyo, ili kuelewa maana ya Yohana 1:1, unaweza kutafuta habari zaidi kuhusu cheo cha Yesu katika Injili ya Yohana. Kupata habari zaidi kutakusaidia kujua ukweli. Kwa mfano, kiria yale ambayo Yohana aliandika katika sura ya 1, mstari wa 18: Hakuna mwanadamu amemwona Mungu [Mweza-Yote] wakati wowote. Hata hivyo, wanadamu wamemwona Mwana, yaani, Yesu kwa kuwa Yohana alisema: Neno [Yesu] alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake. (Yohana 1:14, UV) Basi, Mwana angewezaje kuwa ndiye Mungu Mweza-Yote? Yohana anasema pia kwamba Neno alikuwa pamoja na Mungu. Basi, mtu anawezaje kuwa pamoja na mtu mwingine na wakati huohuo awe ndiye mtu huyo? Isitoshe, katika Yohana 17:3, Yesu anaonyesha waziwazi tofauti iliyopo kati yake na Baba yake wa mbinguni. Anamwita Baba yake Mungu wa pekee wa kweli. Kisha Yohana anasema hivi mwishoni-mwishoni mwa Injili yake: Haya yameandikwa ili mpate kuamini kwamba Yesu ndiye Kristo Mwana wa Mungu. (Yohana 20:31) Ona kwamba Yesu anaitwa, Mwana wa Mungu, wala haitwi Mungu. Habari hiyo ya ziada iliyo katika Injili ya Yohana inatusaidia kuelewa andiko la Yohana 1:1. Yesu, yule Neno, ni mungu katika maana ya kwamba ana cheo cha juu lakini siye Mungu Mweza-Yote.
CHANGANUA UTHIBITISHO Ukirie tena ule mfano wa mwalimu na wanafunzi. Wazia kwamba baadhi ya wanafunzi wangali na shaka, hata baada ya kusikiliza maelezo ya ziada ya mwalimu wao. Wafanye nini? Wanaweza kumwomba mwalimu mwingine awape habari zaidi kuhusu suala hilo. Mwalimu huyo wa pili akiunga mkono maelezo ya yule wa kwanza, wanafunzi wengi wataridhika. Vivyo

204

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

hivyo, ikiwa huna uhakika kuhusu alichomaanisha mwandishi wa Biblia Yohana alipoandika kuhusu uhusiano kati ya Yesu na Mungu Mweza-Yote, unaweza kupata habari zaidi kutoka kwa mwandishi mwingine wa Biblia. Kwa mfano, hebu kiria aliyoandika Mathayo. Kuhusu mwisho wa ulimwengu huu, anamnukuu Yesu akisema: Kuhusu siku ile na saa ile hakuna mtu anayejua, wala malaika wa mbinguni wala Mwana, ila Baba tu. (Mathayo 24:36) Maneno hayo yanathibitishaje kwamba Yesu si Mungu Mweza-Yote? Yesu anasema kwamba Baba anajua mambo mengi kuliko Mwana. Hata hivyo, ikiwa Yesu angekuwa ndiye Mungu Mweza-Yote, angejua mambo yote anayojua Baba yake. Kwa hiyo, basi, Mwana na Baba hawalingani. Hata hivyo, wengine wanadai: Yesu ana nyutu mbili. Hapa anazungumza akiwa mwanadamu. Na hata kama hilo lingekuwa kweli, namna gani roho takatifu? Ikiwa hiyo pia ni Mungu yuleyule ambaye ndiye Baba, mbona Yesu hasemi kwamba roho hiyo inajua mambo anayojua Baba? Unapoendelea kujifunza Biblia, utaona maandiko mengine mengi ya Biblia yanayohusiana na habari hii. Yanathibitisha ukweli kumhusu Baba, Mwana, na roho takatifu.Zaburi 90:2; Matendo 7:55; Wakolosai 1:15.

Kwa Nini Wakristo wa Kweli Hawatumii Msalaba Katika Ibada?


MSALABA unapendwa na kuheshimiwa na mamilioni ya watu. Kitabu The Encyclopdia Britannica kinasema kwamba msalaba ni ishara kuu ya dini ya Kikristo. Hata hivyo, Wakristo wa kweli hawatumii msalaba katika ibada. Kwa nini? Sababu kuu ni kwamba Yesu Kristo hakufa kwenye msalaba. Kwa kawaida neno la Kigiriki linalotafsiriwa msalaba ni stauros . Neno hilo linamaanisha mti au nguzo iliyo wima. The Companion Bible inasema hivi: [Neno stauros ] halimaanishi kamwe vipande viwili vya mbao vilivyokingamana kwa njia yo-

Nyongeza

205

yote ile . . . Hakuna jambo lolote katika [Agano Jipya] lugha ya Kigiriki linalodokeza vipande viwili vya mbao. Katika maandiko kadhaa, waandishi wa Biblia wanatumia neno lingine kurejelea kifaa ambacho Yesu alia juu yake. Ni neno xy lon la Kigiriki. (Matendo 5:30; 10:39; 13:29; Wagalatia 3:13; 1 Petro 2:24) Neno hilo linamaanisha mbao au kijiti, rungu, au mti. Kikieleza kwa nini ni mti tu wa kawaida uliotumiwa mara nyingi kuwatundikia waliohukumiwa kifo, kitabu kimoja kinasema: Miti haikupatikana kila mahali ambapo palichaguliwa kuwatundikia watu waliohukumiwa kifo. Kwa hiyo, nguzo zilisimamishwa ardhini. Mara nyingi wahalifu walitundikwa kwenye nguzo hizo, mikono yao ikiwa imeinuliwa juu na mara nyingi miguu yao ikiwa imefungwa au kupigiliwa misumari. Kitabu Das Kreuz und die Kreuzigung, kilichoandikwa na Hermann Fulda. Hata hivyo, Neno la Mungu linatoa uthibitisho wenye kusadikisha zaidi. Mtume Paulo alisema: Kristo kwa kutununua alituachilia huru kutoka katika laana ya Sheria kwa yeye kuwa laana badala yetu, kwa sababu imeandikwa: Amelaaniwa kila mtu aliyetundikwa juu ya mti. (Wagalatia 3:13) Hapa Paulo ananukuu andiko la Kumbukumbu la Torati 21:22, 23, ambalo kwa wazi linarejelea mti wala si msalaba. Kwa kuwa watu waliouawa kwa njia hiyo walionwa kuwa laana, haifai Wakristo kupamba nyumba zao kwa sanamu za Kristo akiwa ametundikwa. Hakuna uthibitisho wowote unaoonyesha kwamba wale waliodai kuwa Wakristo walitumia msalaba katika ibada kwa muda wa miaka 300 baada ya Kristo kufa. Hata hivyo, katika karne ya nne, Maliki mpagani Konstantino alijiunga na Wakristo waasi-imani na kuutetea msalaba kuwa ishara yao. Hata Konstantino awe alikuwa na nia gani, msalaba haukuwa na uhusiano wowote na Yesu Kristo. Kwa kweli, msalaba ulibuniwa na wapagani. Kitabu New Catholic Encyclopedia kinakiri hivi: Msalaba ulitumiwa na watu walioishi kabla ya enzi za Ukristo na wale ambao hawakuwa Wakristo. Watu fulani maarufu wamesema kwamba msalaba unahusiana na ibada ya viumbe na desturi za kipagani za ngono.

206

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Kwa nini basi ishara hiyo ya kipagani ilienezwa? Yaelekea ilienezwa ili kufanya iwe rahisi kwa wapagani kukubali Ukristo. Hata hivyo, Biblia inashutumu waziwazi matumizi ya ishara yoyote ya kipagani. (2 Wakorintho 6:14-18) Biblia inakataza pia kila namna ya ibada ya sanamu. (Kutoka 20:4, 5; 1 Wakorintho 10:14) Hivyo basi, Wakristo wa kweli wana sababu nzuri za kutotumia msalaba katika ibada yao.1
1 Ili kupata habari zaidi kuhusu msalaba, ona ukurasa wa 211-215 wa kitabu Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko, Chapa ya 2004, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

Mlo wa Jioni wa BwanaMaadhimisho Yanayomletea Mungu Heshima


WAKRISTO wanaamriwa waadhimishe Ukumbusho wa Kifo cha Kristo. Maadhimisho hayo yanaitwa pia mlo wa jioni wa Bwana. (1 Wakorintho 11:20) Maadhimisho hayo yana umuhimu gani? Yanapaswa kufanywa wakati gani na jinsi gani? Yesu Kristo alianzisha maadhimisho hayo usiku wa Pasaka ya Kiyahudi mwaka wa 33 W.K. Pasaka ilikuwa maadhimisho yaliyofanywa mara moja tu kila mwaka, siku ya 14 ya mwezi wa Nisani katika kalenda ya Kiyahudi. Ili kukadiria tarehe hiyo, inaonekana kwamba Wayahudi walisubiri hadi sikusare (Machi 21) ya wakati wa majira ya kuchipua. Hiyo ndiyo siku ambayo mchana na usiku zinalingana. Mwezi wa Nisani ulianza wakati mwezi mpya ulipoonekana kwa mara ya kwanza karibu na Machi 21. Maadhimisho ya Pasaka yalifanywa siku 14 baadaye, baada ya jua kutua. Yesu aliadhimisha Pasaka pamoja na mitume wake, kisha baada ya kumfukuza Yuda Iskariote,

Nyongeza

207

akaanzisha Mlo wa Jioni wa Bwana. Mlo huo ulichukua mahali pa Pasaka ya Kiyahudi na hivyo unapaswa kuadhimishwa mara moja tu kwa mwaka. Injili ya Mathayo inasema: Yesu alichukua mkate na, baada ya kutoa baraka, akaumega, akawapa wanafunzi, akasema: Chukueni, mle. Huu unamaanisha mwili wangu. Pia, akachukua kikombe na, akiisha kushukuru, akawapa, akisema: Kinyweeni, ninyi nyote; kwa maana hii inamaanisha damu yangu ya agano, ambayo itamwagwa kwa ajili ya wengi kwa msamaha wa dhambi. Mathayo 26:26-28. Watu fulani huamini kwamba Yesu aligeuza mkate kuwa mwili wake na divai kuwa damu yake. Hata hivyo, mwili wa Yesu ulikuwa kamili alipowapa mkate huo. Je, kweli mitume wa Yesu walikuwa wakila mwili halisi na kunywa damu yake? Hapana, kwa kuwa kufanya hivyo kungekuwa kuvunja sheria ya Mungu iliyokataza kunywa damu. (Mwanzo 9:3, 4; Mambo ya Walawi 17:10) Kulingana na Luka 22:20, Yesu alisema: Kikombe hiki kinamaanisha agano jipya kwa msingi wa damu yangu, ambayo itamwagwa kwa ajili yenu. Je, kikombe hicho kilikuwa agano jipya kihalisi? Hilo halingewezekana kwa kuwa agano ni makubaliano wala si kitu halisi. Hivyo, mkate na divai ni mifano tu. Mkate huwakilisha mwili mkamilifu wa Kristo. Yesu alitumia mkate uliobaki baada ya mlo wa Pasaka. Mkate huo uliokwa bila chachu, au hamira. (Kutoka 12:8) Biblia hutumia chachu kuwakilisha dhambi au kuharibika. Kwa hiyo, mkate unawakilisha mwili mkamilifu ambao Yesu alidhabihu. Haukuwa na dhambi yoyote.Mathayo 16:11, 12; 1 Wakorintho 5:6, 7; 1 Petro 2:22; 1 Yohana 2:1, 2. Divai nyekundu inawakilisha damu ya Yesu. Damu hiyo inafanya agano jipya liwe halali. Yesu alisema kwamba damu yake ilimwagwa kwa msamaha wa dhambi. Hivyo, wanadamu wanaweza kuwa sa machoni pa Mungu na kuwa katika agano jipya pamoja na Yehova. (Waebrania 9:14; 10:16, 17) Agano au mkataba huo huwawezesha wale Wakristo waaminifu 144,000 kwenda mbinguni. Watakuwa wafalme na makuhani mbinguni na kuwaletea wanadamu wote baraka.Mwanzo 22:18; Yeremia 31:31-33; 1 Petro 2:9; Ufunuo 5:9, 10; 14:1-3.

208

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Ni nani wanaopaswa kula mkate na kunywa divai wakati wa Ukumbusho? Ni wale tu walio katika agano jipya, yaani, wale walio na tumaini la kwenda mbinguni. Roho takatifu ya Mungu huwasadikisha kwamba wamechaguliwa kuwa wafalme mbinguni. (Waroma 8:16) Wako pia katika agano la Ufalme pamoja na Yesu.Luka 22:29. Namna gani wale walio na tumaini la kuishi milele katika Paradiso duniani? Wanatii amri ya Yesu kwa kuhudhuria Mlo wa Jioni wa Bwana, lakini wao huwa watazamaji wenye heshima wala hawashiriki mifano. Mara moja kila mwaka, Mashahidi wa Yehova huadhimisha Mlo wa Jioni wa Bwana mnamo Nisani 14 baada ya jua kutua. Ingawa ni watu wachache tu ulimwenguni wanaodai kuwa na tumaini la kwenda mbinguni, maadhimisho hayo yanathaminiwa na Wakristo wote. Ni pindi ambayo wote wanaweza kukiria juu ya upendo usio na kifani wa Yehova Mungu na Yesu Kristo.Yohana 3:16.

Maneno Nafsi na Roho Yanamaanisha Nini Hasa?


MANENO nafsi na roho yanamaanisha nini kwako? Wengi huamini kwamba maneno hayo yanamaanisha kitu fulani kisichoonekana na kisichoweza kufa kilicho ndani yetu. Wao hukiri kwamba mtu anapokufa kitu hicho kisichoonekana hutoka ndani ya mwili wa binadamu na kuendelea kuishi. Kwa kuwa fundisho hilo limeenea sana, watu wengi hushangaa wanapogundua kwamba si fundisho la Biblia. Basi, Neno la Mungu linasema nafsi na roho ni nini?
FUNDISHO LA BIBLIA KUHUSU NAFSI Kwanza, tuzungumzie nafsi. Huenda unakumbuka kwamba mwanzoni Biblia iliandikwa katika Kiebrania na Kigiriki. Waandishi wa Biblia walitumia neno ne phesh la Kiebrania au psykhe la Kigiriki walipoandika kuhusu nafsi. Maneno hayo mawili yanapatikana zaidi ya mara 800 katika Maandiko, na

Nyongeza

209

Tafsiri ya Ulimwengu Mpya huyatafsiri yote kuwa nafsi. Unapochunguza jinsi neno nafsi linavyotumiwa katika Biblia, utaona kwa wazi kwamba neno hilo humaanisha (1) watu, (2) wanyama, au (3) uhai wa mtu au mnyama. Na tuzungumzie baadhi ya Maandiko yanayoonyesha mambo hayo matatu. Watu. Katika siku za Noa . . . watu wachache, yaani, nafsi nane, walichukuliwa salama kupitia maji. (1 Petro 3:20) Kwa wazi neno nafsi katika andiko hilo linamaanisha watu, yaani, Noa, mkewe, wanawe watatu, na wake zao. Andiko la Kutoka 16:16 lina maagizo kwa Waisraeli kuhusu kuokota mana. Waliambiwa: Okoteni kiasi chake . . . kulingana na hesabu ya nafsi ambazo kila mmoja wenu anazo katika hema lake. Kwa hiyo, kiasi cha mana kilichookotwa kilitegemea kiasi cha watu katika kila familia. Maandiko yafuatayo ya Biblia yanaonyesha matumizi ya neno nafsi kumaanisha watu, Mwanzo 46:18; Yoshua 11:11; Matendo 27:37; na Waroma 13:1. Wanyama. Tunasoma hivi katika masimulizi ya Biblia kuhusu uumbaji: Mungu akaendelea kusema: Maji na yajawe na nafsi hai na viumbe vinavyoruka viruke juu ya dunia kwenye uso wa anga la mbingu. Mungu akaendelea kusema: Dunia na itokeze nafsi zilizo hai kulingana na aina zake, mnyama wa kufugwa na mnyama anayetambaa na mnyama-mwitu wa dunia kulingana na aina yake. Ikawa hivyo. (Mwanzo 1:20, 24) Katika andiko hilo, samaki, wanyama wa kufugwa, na wanyama-mwitu wote wanaitwa kwa neno lilelilenafsi. Ndege na wanyama wengine wanaitwa nafsi kwenye Mwanzo 9:10; Mambo ya Walawi 11:46; na Hesabu 31:28. Uhai wa mtu. Wakati mwingine neno nafsi humaanisha uhai wa mtu. Yehova alimwambia Musa: Watu wote waliokuwa wakiiwinda nafsi yako wamekufa. (Kutoka 4:19) Adui za Musa walikuwa wakiwinda nini? Walitaka kumuua Musa. Raheli alipokuwa akimzaa mwanawe Benyamini, nafsi yake ilitoka (kwa sababu alikufa). (Mwanzo 35:16-19) Wakati huo Raheli alipoteza uhai wake. Fikiria pia maneno ya Yesu: Mimi ndiye mchungaji mwema; mchungaji mwema huitoa nafsi yake kwa ajili ya kondoo. (Yohana 10:11) Yesu alitoa nafsi au

210

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

uhai wake kwa ajili ya wanadamu. Katika maandiko hayo ya Biblia, ni wazi kwamba neno nafsi linamaanisha uhai wa mtu. Utapata mifano mingine yenye maana hiyo ya neno nafsi kwenye 1 Wafalme 17:17-23; Mathayo 10:39; Yohana 15:13; na Matendo 20:10. Unapoendelea kujifunza Neno la Mungu utaona kwamba hakuna popote katika Biblia ambapo neno nafsi linahusianishwa na kutoweza kufa au kuishi milele. Badala yake, Maandiko yanasema kwamba nafsi inaweza kufa. (Ezekieli 18: 4, 20) Kwa hiyo, katika Biblia mtu ambaye amekufa huitwa nafsi iliyokufa.Mambo ya Walawi 21:11. MAANA YA ROHO Hebu tuzungumzie jinsi Biblia inavyotumia neno roho. Watu fulani hukiri kwamba roho ni neno lingine linalomaanisha nafsi. Lakini, si kweli. Biblia inaonyesha wazi kwamba roho na nafsi ni vitu viwili tofauti. Vinatofautianaje? Waandishi wa Biblia walitumia neno la Kiebrania ru ach au neno la Kigiriki, pneu ma waliporejelea roho. Maandiko yenyewe yanaonyesha maana ya maneno hayo. Kwa mfano, andiko la Zaburi 104:29 linasema: [Yehova] ukiiondoa roho [ru ach] yao, wanakata pumzi, na kurudi katika mavumbi yao. Andiko la Yakobo 2:26 linasema kwamba mwili bila roho [pneu ma] umekufa. Katika andiko hilo roho inamaanisha kile ambacho huupa mwili uhai. Bila roho, mwili umekufa. Kwa hiyo, katika Biblia neno ru ach halitafsiriwi tu roho bali pia nguvu au kani ya uhai. Kwa mfano, Mungu alisema hivi kuhusu Mafuriko ya siku ya Noa: Ninaleta gharika ya maji duniani ili kuharibu kutoka chini ya mbingu wote wenye mwili walio na nguvu [ru ach] za uhai ndani yao. (Mwanzo 6:17; 7: 15, 22) Hivyo, roho inarejelea nguvu isiyoonekana, inayotendesha viumbe vyote vilivyo hai. Nafsi na roho hutofautiana. Mwili unahitaji roho kama vile redio inavyohitaji umeme ili kufanya kazi. Kwa mfano, unapotia betri katika redio na kuiwasha, nguvu zilizo katika betri huiwezesha redio kufanya kazi. Hata hivyo, redio haiwezi kufa-

Nyongeza

211

nya kazi bila betri. Hali kadhalika, redio ambayo imeondolewa kwenye umeme haiwezi kufanya kazi. Vivyo hivyo, roho ni nguvu ambayo hutendesha mwili wetu. Kama umeme, roho haiwezi kuhisi wala kukiri. Ni nguvu isiyo na utu. Lakini bila roho au kani ya uhai, tunakata pumzi na kurudi kwenye udongo, kama mtunga-zaburi alivyosema. Andiko la Mhubiri 12:7 linasema hivi linapozungumzia kifo cha mwanadamu: Mavumbi [mwili wake] huirudia nchi kama yalivyokuwa, nayo roho yenyewe humrudia Mungu wa kweli aliyeitoa. Roho au kani ya uhai inapoondoka mwilini, mwili hufa na kurudi ulipotoka, yaani, kwenye udongo. Vivyo hivyo, nguvu ya uhai hurudi ilipotoka, yaani, kwa Mungu. (Ayubu 34:14, 15; Zaburi 36:9) Hiyo haimaanishi kwamba nguvu ya uhai huenda mbinguni kihalisi. Badala yake, inamaanisha kwamba mtu akifa, tumaini lolote la kuishi tena linamtegemea Yehova Mungu. Ni kana kwamba uhai wake uko mikononi mwa Mungu. Ni kupitia nguvu za Mungu tu ndipo roho au nguvu ya uhai inaweza kurudishwa ili mtu aweze kuishi tena. Inafariji kama nini kujua kwamba hivyo ndivyo Mungu atakavyofanya kwa wote wanaopumzika ndani ya makaburi ya ukumbusho! (Yohana 5:28, 29) Wakati wa ufufuo, Yehova atamfanyizia mwili mpya yule anayelala katika kifo na kuuhuisha kwa kutia roho, au nguvu ya uhai ndani yake. Itakuwa siku ya shangwe sana. Ikiwa ungependa kupata habari zaidi kuhusu maneno nafsi na roho kama yanavyotumiwa katika Biblia, ona broshua Ni Nini Hutupata Tunapokufa? na ukurasa wa 221-226 katika kitabu Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko, Chapa ya 2004, vilivyochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

212

Sheoli na Hadesi Zinamaanisha Nini?


KATIKA lugha za awali, Biblia inatumia neno la Kiebrania she ohl na neno la Kigiriki hai des zaidi ya mara 70. Maneno yote mawili yanahusiana na kifo. Tafsiri fulani za Biblia hutumia maneno kaburi, kuzimu, au shimo. Hata hivyo, katika lugha nyingi hakuna maneno yanayoweza kutoa maana halisi ya maneno hayo ya Kiebrania na Kigiriki. Biblia TakatifuTafsiri ya Ulimwengu Mpya hutumia maneno Sheoli na Hadesi katika vielezi-chini. Maneno hayo yanamaanisha nini hasa? Hebu tuchunguze jinsi yanavyotumiwa katika maandiko mbalimbali ya Biblia. Andiko la Mhubiri 9:10 linasema: Hakuna kazi, wala utungaji wala ujuzi wala hekima katika Kaburi [Sheoli, kielezi-chini], mahali unapokwenda. Je, hilo linamaanisha kwamba Sheoli ni kaburi hususa, au la mtu mmoja ambamo huenda tumemzika mpendwa wetu? Hapana. Biblia inapozungumzia kaburi hususa, inatumia maneno mengine ya Kiebrania na Kigiriki, wala si she ohl na hai des. (Mwanzo 23:7-9; Mathayo 28:1) Pia, Biblia haitumii neno Sheoli kurejelea kaburi ambamo watu wengi wamezikwa pamoja, kama vile kaburi la familia.Mwanzo 49: 30, 31. Kwa hiyo, basi, Sheoli ni mahali pa aina gani? Neno la Mungu huonyesha kwamba maneno Sheoli, au Hadesi, hayamaanishi kaburi kubwa la watu wengi. Kwa mfano, andiko la Isaya 5:14 linasema kwamba Sheoli imepanua sana nafsi yake nayo imepanua kinywa chake kupita mipaka. Ingawa Sheoli tayari imemeza wafu wengi, nyakati zote huonekana kwamba haitosheki. (Methali 30:15, 16) Tofauti na mahali hususa pa kuzikia, ambapo ni watu kadhaa tu wanaoweza kuzikwa humo, Sheoli hapatosheki. (Methali 27:20) Yaani, Sheoli hapajai kamwe. Hapana mipaka. Hivyo, Sheoli, au Hadesi, si mahali halisi. Badala yake ni kaburi au mahali pa mfano ambapo watu walio wengi hulala usingizi katika kifo. Fundisho la Biblia kuhusu ufufuo hutusaidia kuelewa vizuri zaidi maana ya Sheoli na Hadesi. Katika Neno la Mungu, She-

Nyongeza

213

oli na Hadesi huhusianishwa na kifo cha watu watakaofufuliwa.1 (Ayubu 14:13; Matendo 2:31; Ufunuo 20:13) Neno la Mungu linaonyesha pia kwamba wale waliomo Sheoli, au Hadesi, si wale tu ambao walimtumikia Yehova bali pia wengi ambao hawakumtumikia. (Mwanzo 37:35; Zaburi 55:15) Kwa hiyo, Biblia hufundisha kwamba kutakuwa na ufufuo wa waadilifu na wasio waadilifu. Matendo 24:15.
1 Tofauti na hilo, inasemekana kuwa wafu ambao hawatafufuliwa wako Gehena wala si Sheoli, au Hadesi. (Mathayo 5:30; 10:28; 23:33) Kama ilivyo kuhusu Sheoli na Hadesi, Gehena si mahali halisi.

Siku ya Hukumu Ni Nini?


UNA maoni gani kuhusu Siku ya Hukumu? Watu wengi hukiri kwamba mabilioni ya watu watasimamishwa mmojammoja mbele ya kiti cha enzi cha Mungu. Kisha kila mmoja wao atahukumiwa. Baadhi yao wataishi kwa raha mbinguni, na wengine watateswa milele. Hata hivyo, masimulizi ya Biblia kuhusu hukumu ni tofauti kabisa. Kulingana na Neno la Mungu, si wakati wenye kutisha bali ni wakati wa tumaini na kurudisha hali nzuri. Mtume Yohana anafafanua hivi Siku ya Hukumu katika Ufunuo 20:11, 12: Nikaona kiti cha ufalme kikubwa cheupe na yeye aliyeketi juu yake. Dunia na mbingu zikakimbia kutoka mbele zake, na mahali popote hapakupatikana kwa ajili ya hizo. Nami nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya kile kiti cha ufalme, na vitabu vya kukunjwa vikafunguliwa. Lakini kitabu kingine cha kukunjwa kikafunguliwa; hicho ni kitabu cha uzima. Na wafu wakahukumiwa kutokana na mambo yale yaliyoandikwa katika vile vitabu kulingana na matendo yao. Hukumu hiyo itatekelezwa na nani? Yehova Mungu ndiye Hakimu au Mwamuzi mkuu wa wanadamu. Hata hivyo, ana mwakilishi wa kufanya hukumu.

214

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Kulingana na Matendo 17:31, mtume Paulo alisema kwamba Mungu ameweka siku ambayo katika hiyo anakusudia kuihukumu kwa uadilifu dunia inayokaliwa kupitia kwa mwanamume ambaye amemweka rasmi. Hakimu huyo aliyewekwa rasmi ni Yesu Kristo aliyefufuliwa. (Yohana 5:22) Hata hivyo, Siku ya Hukumu itaanza lini? Itakuwa na urefu gani? Kitabu cha Ufunuo kinaonyesha kwamba Siku ya Hukumu itaanza baada ya vita vya HarMagedoni, wakati ambapo mfumo wa Shetani utaharibiwa.1 (Ufunuo 16:14, 16; 19:1920:3) Baada ya HarMagedoni, Shetani na roho wake waovu watafungiwa katika abiso kwa miaka 1,000. Wakati huo, wale 144,000 watahukumu na kutawala wakiwa wafalme pamoja na Kristo kwa miaka elfu. (Ufunuo 14:1-3; 20:1-4; Waroma 8:17) Siku ya Hukumu haitakuwa tukio la haraka la saa 24. Itachukua miaka 1,000. Katika kipindi hicho cha miaka 1,000, Yesu Kristo atahukumu walio hai na wafu. (2 Timotheo 4:1) Walio hai watakuwa umati mkubwa utakaookoka HarMagedoni. (Ufunuo 7:9-17) Mtume Yohana aliwaona pia wafu . . . wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi cha hukumu. Kama alivyoahidi Yesu, waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho wataisikia sauti yake [Kristo] na kutoka. (Yohana 5:28, 29; Matendo 24:15) Watahukumiwa kwa msingi gani? Katika njozi, mtume Yohana aliona vitabu vya kukunjwa vikifunguliwa na wafu wakahukumiwa kutokana na mambo yale yaliyoandikwa katika vile vitabu kulingana na matendo yao. Je, vitabu hivyo vya kukunjwa ni rekodi ya mambo ambayo watu walifanya zamani? Hapana, watu hawatahukumiwa kulingana na mambo ambayo walifanya kabla ya kufa. Tunajuaje? Biblia inasema: Yeye ambaye amekufa ameondolewa hatia ya dhambi yake. (Waroma 6:7) Hivyo, ni kana
1 Kuhusu HarMagedoni, tafadhali angalia Insight on the Scriptures, Buku la 1, ukurasa wa 594-595, 1037-1038 au Etude Perspicase, Buku la 1, ukurasa wa 1073-1075, Buku la 2, ukurasa wa 63-64; na sura ya 20 ya kitabu Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli, vilivyochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

Nyongeza

215

kwamba wale watakaofufuliwa wataanza upya. Kwa hiyo, vitabu vya kukunjwa vinawakilisha matakwa mengine ya Mungu. Ili waishi milele, wale watakaookoka HarMagedoni na wale watakaofufuliwa watahitaji kutii amri za Mungu kutia ndani matakwa yoyote mapya ambayo huenda Yehova akafunua katika ile miaka 1,000. Hivyo, watu watahukumiwa kulingana na yale watakayotenda katika Siku ya Hukumu. Wakati wa Siku ya Hukumu, mabilioni ya watu watapata fursa ya kujifunza kwa mara ya kwanza mapenzi ya Mungu na kuishi kupatana nayo. Hivyo, kutakuwa na kazi kubwa ya kuwaelimisha watu. Wakaaji wa nchi yenye kuzaa hakika watajifunza uadilifu. (Isaya 26:9) Hata hivyo, si wote watakaofanya mapenzi ya Mungu. Andiko la Isaya 26:10 linasema: Hata mwovu akionyeshwa kibali, yeye hatajifunza uadilifu. Atatenda isivyo haki katika nchi ya unyoofu, naye hatauona ukuu wa Yehova. Waovu hao wataangamizwa milele wakati wa Siku ya Hukumu.Isaya 65:20. Mwishoni mwa Siku ya Hukumu, wale wanadamu wengine watakuwa hai kikamili kwa sababu watakuwa wakamilifu. (Ufunuo 20:5) Hivyo, katika Siku ya Hukumu, wanadamu watarudishwa katika hali ya ukamilifu waliyokuwa nayo mwanzoni. (1 Wakorintho 15:24-28) Kisha kutakuwa na jaribu la mwisho. Shetani atafunguliwa kutoka katika abiso na kuruhusiwa ajaribu kuwapotosha wanadamu kwa mara ya mwisho. (Ufunuo 20:3, 7-10) Wale watakaompinga wataona utimizo kamili wa ahadi hii ya Biblia: Waadilifu wenyewe wataimiliki dunia, nao watakaa milele juu yake. (Zaburi 37:29) Ndiyo, Siku ya Hukumu itakuwa baraka kwa wanadamu wote waaminifu!

1914Mwaka Muhimu Katika Unabii wa Biblia


MIAKA mingi mapema, wanafunzi wa Biblia walitangaza kwamba mambo muhimu yangetukia mwaka wa 1914.

216

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Ni mambo gani hayo, na ni uthibitisho gani unaoonyesha kwamba mwaka wa 1914 ungekuwa mwaka muhimu? Kulingana na Luka 21:24, Yesu alisema: Yerusalemu litakanyagwa-kanyagwa na mataifa, mpaka nyakati zilizowekwa za mataifa zitimie. Yerusalemu lilikuwa jiji kuu la taifa la Kiyahudikiti cha utawala cha nasaba ya wafalme wa nyumba ya Mfalme Daudi. (Zaburi 48:1, 2) Hata hivyo, wafalme hao walikuwa tofauti na viongozi wa mataifa mengine. Waliketi juu ya kiti cha ufalme cha Yehova wakimwakilisha Mungu mwenyewe. (1 Mambo ya Nyakati 29:23) Kwa hiyo, Yerusalemu liliwakilisha utawala wa Yehova. Hata hivyo, utawala wa Mungu ulianza kukanyagwa-kanyagwa na mataifa jinsi gani na wakati gani? Mwaka wa 607 K.W.K., Yerusalemu liliposhindwa na Wababiloni. Kiti cha ufalme cha Yehova hakikuwa na mtu, nayo nasaba ya wafalme wa uzao wa Daudi ilikatishwa. (2 Wafalme 25:1-26)

NYAKATI SABA
Miaka 2,520 Miaka 606 1/4
Oktoba 607 K.W.K. hadi Desemba 31, 1 K.W.K. 607 & K.W.K. W.K. )

Miaka 1,913 3/4


Januari 1, 1 W.K. hadi Oktoba 1914 1914

Yerusalemu litakanyagwakanyagwa na mataifa

Atakapokuja yule aliye na haki ya kisheria

Nyongeza

217

Je, lingekanyagwa-kanyagwa milele? Hapana, kwa kuwa unabii wa Ezekieli ulisema hivi kuhusu Sedekia, mfalme wa mwisho wa Yerusalemu: Kiondoe kilemba, na kulivua taji. . . . Hakika hili halitakuwa la mtu yeyote mpaka atakapokuja yule aliye na haki ya kisheria, nami nitampa yeye. (Ezekieli 21:26, 27) Kristo Yesu ndiye aliye na haki ya kisheria ya taji la Daudi. (Luka 1:32, 33) Kwa hiyo, kukanyaga-kanyaga kungeisha wakati ambapo Yesu angekuwa Mfalme. Tukio hilo kuu lingetokea wakati gani? Yesu alionyesha kwamba Mataifa yangetawala kwa muda fulani uliowekwa. Masimulizi ya Danieli sura ya 4 yanatusaidia kujua urefu wa muda huo. Yanataja ndoto ya kinabii ambayo Mfalme Nebukadneza wa Babiloni aliota. Aliona mti mkubwa uliokatwa. Kisiki chake hakingeweza kukua kwa sababu kilikuwa kimefungwa kwa pingu ya chuma na ya shaba. Malaika alitangaza hivi: Nyakati saba zipite juu yake.Danieli 4:10-16. Katika Biblia, nyakati nyingine miti huwakilisha utawala. (Ezekieli 17:22-24; 31:2-5) Kwa hiyo, kukatwa kwa mti huo wa mfano kunaonyesha jinsi utawala wa Mungu, uliowakilishwa na wafalme wa Yerusalemu, ungekatishwa. Hata hivyo, maono hayo yaliashiria kwamba kukanyagwa-kanyagwa kwa Yerusalemu kungekuwa kwa muda fulanikipindi cha nyakati saba. Kipindi hicho kina urefu gani? Andiko la Ufunuo 12:6, 14 linaonyesha kwamba nyakati tatu na nusu zinatoshana na siku 1,260. Kwa hiyo, nyakati saba zingekuwa mara mbili ya kipindi hicho, au siku 2,520. Lakini Mataifa hayakuacha kukanyaga-kanyaga utawala wa Mungu siku 2,520 tu baada ya kuanguka kwa Yerusalemu. Basi, inaonekana kwamba unabii huo ulizungumzia muda mrefu zaidi. Kwa kutegemea andiko la Hesabu 14:34 na Ezekieli 4:6, yanayotaja siku moja kwa mwaka mmoja, zile nyakati saba zingekuwa miaka 2,520. Miaka hiyo 2,520 ilianza Oktoba 607 K.W.K., Yerusalemu lilipoangushwa na Wababiloni na mfalme wa uzao wa Daudi akaondolewa katika kiti cha ufalme. Kipindi hicho kiliisha Oktoba 1914. Wakati huo, nyakati zilizowekwa za mataifa ziliisha, na Yesu Kristo akawekwa kuwa Mfalme wa

218

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

mbinguni aliyechaguliwa na Mungu.1Zaburi 2:1-6; Danieli 7:13, 14. Kama Yesu alivyotabiri, matukio ya pekee ulimwenguni, kama vile, vita, njaa, matetemeko ya nchi, na tauni, yanaonyesha kuwapo kwake akiwa Mfalme mbinguni. (Mathayo 24:3-8; Luka 21:11) Matukio hayo yalitoa uthibitisho wa kwamba kwa kweli Ufalme wa mbinguni wa Mungu ulizaliwa mwaka wa 1914 na siku za mwisho za mfumo huu mbovu wa mambo zikaanza.2 Timotheo 3:1-5.
1 Tangu Oktoba 607 K.W.K. hadi Oktoba 1 K.W.K. ni miaka 606. Kwa kuwa hakuna mwaka wa sufuri, kuanzia Oktoba 1 K.W.K. hadi Oktoba 1914 W.K. ni miaka 1,914. Tukijumlisha miaka 606 na miaka 1,914, tunapata miaka 2,520. Unaweza kupata habari kuhusu kuanguka kwa Yerusalemu mwaka wa 607 K.W.K., katika makala Chronology katika In sight on the Scriptures au Chronologie katika Etude Perspicase, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

Yule Malaika Mkuu Mikaeli Ni Nani?


KIUMBE wa roho anayeitwa Mikaeli hatajwi mara nyingi katika Biblia. Hata hivyo, kila mara anatajwa akitenda jambo fulani. Katika kitabu cha Danieli, Mikaeli anapigana na malaika waovu; katika barua ya Yuda, anabishana na Shetani; na katika Ufunuo, anapigana na Ibilisi na malaika wake waovu. Anapoutetea utawala wa Yehova na kupigana na adui za Mungu, Mikaeli anatenda kupatana na maana ya jina lakeNi Nani Aliye Kama Mungu? Lakini Mikaeli ni nani? Nyakati nyingine, watu huitwa majina mbalimbali. Kwa mfano, mzee wa ukoo Yakobo aliitwa pia Israeli, na mtume Petro aliitwa Simoni. (Mwanzo 49:1, 2; Mathayo 10:2) Vivyo hivyo, Biblia inaonyesha kwamba Mikaeli ni jina lingine la Yesu Kristo, kabla na baada ya maisha yake duniani. Hebu tuone sababu za Kimaandiko zinazotufanya tukate kauli hiyo. Malaika Mkuu. Neno la Mungu linamwita Mikaeli yule malaika mkuu. (Yuda 9) Ona kwamba Mikaeli anaitwa yule malaika

Nyongeza

219

mkuu. Hilo linaonyesha kwamba kuna malaika mmoja tu aliye mkuu. Isitoshe katika Biblia, jina malaika mkuu linatumiwa katika hali ya umoja tu, wala si kwa wingi. Zaidi ya hayo, Yesu anahusianishwa na wadhifa wa malaika mkuu. Kuhusu Bwana Yesu Kristo aliyefufuliwa, andiko la 1 Wathesalonike 4:16 linasema: Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni akiwa na mwito wenye amri, kwa sauti ya malaika mkuu. Kwa hiyo sauti ya Yesu inafafanuliwa kuwa sauti ya malaika mkuu. Basi, andiko hilo linadokeza kwamba Yesu mwenyewe ndiye Mikaeli yule malaika mkuu. Kiongozi wa Jeshi. Biblia inasema kwamba Mikaeli na malaika zake walipigana na yule joka mkubwa na malaika zake. (Ufunuo 12:7) Kwa hiyo, Mikaeli ni Kiongozi wa jeshi la malaika waaminifu. Pia kitabu cha Ufunuo kinamtaja Yesu akiwa Kiongozi wa jeshi la malaika waaminifu. (Ufunuo 19:14-16) Naye mtume Paulo anamtaja kihususa Bwana Yesu na malaika zake wenye nguvu. (2 Wathesalonike 1:7; Mathayo 16:27; 24:31; 1 Petro 3:22) Kwa hiyo, Biblia inataja Mikaeli na malaika zake na Yesu na malaika zake. (Mathayo 13:41) Kwa kuwa Neno la Mungu halionyeshi popote kwamba kuna majeshi mawili ya malaika waaminifu mbingunimoja likiongozwa na Mikaeli na lingine likiongozwa na Yesuni wazi kwamba Mikaeli si mwingine ila ni Yesu Kristo akiwa katika wadhifa wake mbinguni.1
1 Unaweza kupata habari zaidi zinazoonyesha kwamba jina Mikaeli linamhusu Mwana wa Mungu katika Insight on the Scriptures, Buku la 2, ukurasa wa 393-394 au Etude Perspicase, Buku la 2, ukurasa wa 280-281, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

Kumtambulisha Babiloni Mkubwa


KITABU cha Ufunuo kina majina ambayo yana maana ya mfano. (Ufunuo 1:1) Kwa mfano, kinataja mwanamke ambaye jina Babiloni Mkubwa limeandikwa katika paji la uso wake. Kinasema kwamba mwanamke huyo ameketi juu ya umati na mataifa. (Ufunuo 17:1, 5, 15) Kwa kuwa hakuna mwanamke

220

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

halisi anayeweza kufanya hivyo, lazima Babiloni Mkubwa awe mwanamke wa mfano. Kwa hiyo, kahaba huyo wa mfano anawakilisha nini? Kwenye Ufunuo 17:18, mwanamke huyohuyo wa mfano anatajwa kuwa lile jiji kubwa lililo na ufalme juu ya wafalme wa dunia. Jina jiji linarejelea kikundi cha watu. Kwa kuwa jiji hilo kubwa linaongoza wafalme wa dunia, lazima yule mwanamke anayeitwa Babiloni Mkubwa awe shirika lenye uvutano ulimwenguni pote. Linaweza kuitwa milki ya ulimwengu. Milki ya aina gani? Ya kidini. Ona jinsi maandiko mengine katika kitabu cha Ufunuo yanavyotusaidia kukia uamuzi huo. Milki inaweza kuwa ya kisiasa, ya kibiashara, au ya kidini. Mwanamke anayeitwa Babiloni Mkubwa si milki ya kisiasa kwa sababu Neno la Mungu linasema kwamba wafalme wa dunia, au wanasiasa wa ulimwengu huu, walifanya uasherati naye. Uasherati wake ni mapatano ambayo amefanya na watawala wa dunia na ndiyo sababu anaitwa kahaba mkubwa.Ufunuo 17:1, 2; Yakobo 4:4. Babiloni Mkubwa hawezi kuwa milki ya kibiashara kwa sababu wanabiashara wa dunia, watamlilia atakapoharibiwa. Isitoshe, wafalme na wanabiashara watamwangalia Babiloni Mkubwa wakiwa mbali. (Ufunuo 18:3, 9, 10, 15-17) Kwa hiyo, ni wazi kwamba Babiloni Mkubwa, si milki ya kisiasa wala ya kibiashara, bali ni milki ya kidini. Hilo linathibitishwa na ile taarifa ya kwamba Babiloni Mkubwa anapotosha mataifa yote kwa mazoea yake ya kuwasiliana na pepo. (Ufunuo 18:23) Kwa kuwa mazoea yote ya kuwasiliana na pepo hutokana na roho waovu, haishangazi kwamba Biblia inamwita Babiloni Mkubwa makao ya roho waovu. (Ufunuo 18:2; Kumbukumbu la Torati 18:10-12) Pia, milki hiyo inapinga vikali dini ya kweli, ikiwatesa manabii na watakatifu. (Ufunuo 18:24) Kwa kweli, Babiloni Mkubwa anachukia sana dini ya kweli hivi kwamba anawatesa kikatili na hata kuwaua mashahidi wa Yesu. (Ufunuo 17:6) Hivyo, ni wazi kwamba mwanamke huyo anayeitwa Babiloni Mkubwa anawakilisha milki ya ulimwenguni pote ya dini ya uwongo, inayotia ndani dini zote zinazompinga Yehova Mungu.

221

Je, Yesu Alizaliwa Desemba?


BIBLIA haisemi Yesu alizaliwa wakati gani. Hata hivyo, inatupa sababu za kutosha kukata kauli kwamba hakuzaliwa Desemba. Fikiria hali ya hewa wakati huo wa mwaka huko Bethlehemu, ambako Yesu alizaliwa. Mwezi wa Kislevu katika kalenda ya Kiyahudi (unaolingana na miezi ya Novemba/Desemba) ulikuwa mwezi wa baridi na mvua. Mwezi unaofuata ulikuwa mwezi wa Tebethi (Desemba/Januari). Huo ndio mwezi uliokuwa na baridi kali zaidi, mara kwa mara kukiwa na theluji katika nyanda za juu. Hebu tuone Biblia inasema nini kuhusu hali ya hewa ya eneo hilo. Mwandishi wa Biblia Ezra anaonyesha kwamba Kislevu ulikuwa mwezi wenye baridi na mvua nyingi. Baada ya kueleza kwamba umati ulikuwa umekusanyika Yerusalemu katika mwezi wa 9 [Kislevu] siku ya 20 ya mwezi huo, Ezra anasema kwamba watu walikuwa wakitetemeka . . . kwa sababu ya manyunyu ya mvua. Kuhusu hali za hewa wakati huo wa mwaka, watu waliokuwa wamekusanyika walisema: Haya ni

Yesu alipozaliwa, wachungaji na makundi yao walikuwa malishoni wakati wa usiku

222

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

majira ya manyunyu ya mvua, wala haiwezekani kusimama nje. (Ezra 10:9, 13; Yeremia 36:22) Basi, haishangazi kwamba wachungaji walioishi karibu na Bethlehemu walihakikisha kwamba wao wenyewe na mifugo yao hawakuwa nje malishoni mwezi wa Desemba ulipoka! Hata hivyo, Biblia inasema kwamba wachungaji walikuwa malishoni wakilisha makundi yao usiku ambao Yesu alizaliwa. Isitoshe, mwandishi wa Biblia, Luka anaonyesha kwamba wakati huo wachungaji walikuwa wakiishi nje, wakichunga makundi yao usiku karibu na Bethlehemu. (Luka 2:8-12) Ona kwamba wachungaji hao walikuwa wakiishi nje, si kwamba walikuwa wakitembea-tembea nje wakati wa mchana. Walikuwa na makundi yao malishoni usiku. Je, wangeweza kuishi nje wakati wa baridi na mvua huko Bethlehemu mwezi wa Desemba? Hapana. Kwa hiyo, matukio hayo ya wakati wa kuzaliwa kwa Yesu yanaonyesha kwamba hakuzaliwa Desemba.1 Neno la Mungu linatuambia waziwazi wakati ambapo Yesu alikufa, lakini halielezi mengi kuhusu wakati ambapo alizaliwa. Hilo linatukumbusha maneno ya Mfalme Sulemani: Jina ni bora kuliko mafuta mazuri, na siku ya kufa kuliko siku ya kuzaliwa kwa mtu. (Mhubiri 7:1) Basi, haishangazi kwamba Biblia ina habari nyingi kuhusu huduma na kifo cha Yesu lakini inataja mambo machache tu kuhusu wakati wa kuzaliwa kwake.
1 Unaweza kupata habari zaidi kwenye ukurasa wa 275-279 wa kitabu Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko, Chapa ya 2004, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

Je, Tusherehekee Sikukuu?


SIKUKUU za kidini na sikukuu nyingine zinazopendwa na watu wengi ambazo husherehekewa sehemu nyingi za ulimwengu leo, hazikutokana na Biblia. Basi, sikukuu hizo zilianzia wapi? Ikiwa unaweza kufanya utati katika maktaba, unaweza kujifu-

Nyongeza

223

nza mengi kuhusu sikukuu zinazopendwa na wengi katika eneo lenu. Fikiria mifano michache. Ista. Katika Agano Jipya, hakuna lolote linaloonyesha kwamba Ista ilisherehekewa, yasema The Encyclopdia Britannica. Ista ilianzaje? Ilitokana na ibada ya kipagani. Ingawa inasemekana kwamba sikukuu hiyo ni ukumbusho wa kufufuka kwa Yesu, desturi zinazohusiana na sikukuu ya Ista si za Kikristo. Kwa mfano, The Catholic Encyclopedia inasema hivi kuhusu yule sungura wa Ista: Sungura huyo ni mfano wa kipagani na sikuzote huwakilisha nguvu za uzazi. Sherehe za Mwaka Mpya. Tarehe na desturi zinazohusiana na sherehe za Mwaka Mpya hutofautiana katika nchi mbalimbali. Kuhusu chanzo cha sikukuu hiyo, The World Book Encyclopedia inasema: Mtawala Mroma Kaisari Yulio aliteua Januari 1 kuwa Siku ya Mwaka Mpya katika mwaka wa 46 K.W.K. Waroma walitenga siku hiyo kwa ajili ya Yanu, mungu wa malango, milango, na mianzo. Mwezi wa Januari ulipata jina lake kutoka kwa Yanu, aliyekuwa na nyuso mbilimmoja ukiangalia mbele na mwingine ukiangalia nyuma. Kwa hiyo, sherehe za Mwaka Mpya zinatokana na mapokeo ya kipagani. Mkesha wa Siku ya Watakatifu Wote (Halloween). The Encyclopedia Americana inasema: Desturi fulani-fulani zinazohusiana na Mkesha wa Siku ya Watakatifu Wote zilitokana na sherehe za kidini za Kiselti za kabla ya enzi za Ukristo. Waselti walikuwa na sikukuu kwa ajili ya miungu wawili wakuu mungu-jua na mungu wa wafu . . . , ambaye sikukuu yake ilikuwa Novemba 1, mwanzo wa Mwaka Mpya wa Kiselti. Pole kwa pole, sikukuu hiyo ya wafu ikaingizwa katika desturi za Kikristo. Sikukuu Nyingine. Haiwezekani kuzungumzia sikukuu zote ulimwenguni. Hata hivyo, sikukuu zinazowatukuza wanadamu au mashirika ya kibinadamu hazimpendezi Yehova. (Yeremia 17:5-7; Matendo 10:25, 26) Pia, kumbuka kwamba Mungu hupendezwa au kuchukizwa na sikukuu za kidini ikitegemea vyanzo vyake. (Isaya 52:11; Ufunuo 18:4) Kanuni za Biblia zilizotajwa katika Sura ya 16 ya kitabu hiki zitakusaidia kujua maoni ya Mungu kuhusu sikukuu zisizo za kidini.

Je, ungependa kupata habari zaidi?


Unaweza kuwasiliana na Mashahidi wa Yehova katika www.watchtower.org.

You might also like