You are on page 1of 110

MAKOSA MAKUBWA 21

YANAYOFANYWA NA
MABINTI WENGI

Brother Elihuruma Maruma

1|P a g e
Kitabu hiki kimeandikwa na Bro. Elihuruma Maruma,
hakimiliki zote ziko chini ya mwandishi.

Haki zote zimehifadhiwa. Hauruhusiwi kunakili, kurudufisha au


kutumia kitabu hiki au sehemu ya kitabu hiki bila idhini ya
mmiliki na waandaaji. Kufanya hivyo ni kuvunja sheria na haki
ya mwandishi; na ukiukwaji wa taratibu hii waweza kupelekea
mashtaka toka kwa mmiliki na waandaaji wa kazi hii.
ISBN xxxxxxxxxxxxx

Kitabu hiki pamoja na jalada lake kimesanifiwa na kupigwa


chapa na
Pathfinder Image
Simu: +255 625 990 452
+255 655 969 812

Toleo la kwanza xxxxx


Bro. Elihuruma Maruma
Mawasiliano
P.O. Box 327, Arusha
Simu: +255 752/715 307008
IG; BroElly247
FB; Brother Elihuruma Maruma
Email; ellyrealspeaker882@gmail.com

2|P a g e
YALIYOMO
DEDICATION ................................................................ 7

SHUKRANI ................................................................... 8

UTANGULIZI: ................................................................ 9

MTAZAMO SAHIHI JUU YA MAKOSA UTAKAOKUSAIDIA; .. 11

MISTAKE 1: .................................................................. 15

YOU DON’T KNOW YOURSELF! (HUJIJUI) ..................... 15

MISTAKE 2: ................................................................. 21

YOU DON’T TEST BEFORE YOU TRUST! ....................... 21

MISTAKE 3; ................................................................ 29

YOU DON’T HAVE EYES TO SEE BEYOND WHAT YOU


CAN LOOK! ............................................................ 29

MISTAKE 4: .................................................................33

YOU ARE THE FEMALE IMPALA IN HAREM SYSTEM! .....33

MISTAKE 5: .................................................................35

YOU ARE IDENTICAL TO FEMALE AFRICAN JACANA BIRD


..............................................................................35

MISTAKE 6; ................................................................. 37

YOU TALK TOO MUCH! ............................................. 37

MISTAKE 7: ................................................................. 41

YOU DON’T LIKE TO FLY ALONE! ............................... 41

3|P a g e
MISTAKE 8: ................................................................ 45

YOU PUSH OUT FATHERHOOD! ................................ 45

MISTAKE 9; ................................................................ 49

YOU ARE THE SEASONAL QUEEN!! ........................... 49

MISTAKE 10;................................................................53

YOU HAVE A DAY DREAM (Wrong Imagination) ...........53

MISTAKE 11; ................................................................ 57

YOU DON’T LIKE YOUR SWEATS! ............................... 57

MISTAKE 12; ............................................................... 63

YOU DON’T KNOW A ROMANTIC FORMULA! ............. 63

MISTAKE 13; ................................................................67

YOU WANT TO FINISH BEFORE YOU START! ...............67

MISTAKE 14; ................................................................ 71

YOU OFFER SEX AS A PROVE OF LOVE & RETURN!! ..... 71

MISTAKE 15: ................................................................ 77

YOU WANT MEN TO BE LIKE YOU! ............................. 77

MISTAKE 16; ................................................................ 83

YOU SEARCH FOR GREEN PASTURES!! .......................83

MISTAKE NO 17; ......................................................... 89

YOU FORGE TO BE WESTERN GIRL! .......................... 89

4|P a g e
MISTAKE NO 18; ......................................................... 93

YOU BELIEVE IN MORE THAN IMPOSSIBLE CHANGE. . 93

MISTAKE 19: ................................................................97

YOU THINK BOOK IS EVERYTHING!! ...........................97

MISTAKE 20: ............................................................. 101

YOU USE TO GENERALIZE MEN!! ............................. 101

MISTAKE 21; .............................................................. 105

YOU ALWAYS HAVE A PLASTIC FACE!...................... 105

5|P a g e
6|P a g e
DEDICATION
I would like to dedicate this book to: -
i. All girls whether you call yourself a lady or a woman
listen “Today is never too late to be brand new” just a
simple principle to apply “Hate the Mistake LOVE THE
LESSON”

ii. All my spiritual daughters from Ordinary level to


University you know what?
“Your best teacher is your last mistake”

iii. Daughters of Zion Network {DOZN} all over Tanzania.


Ladies “Learn from yesterday, live for today, hope from
tomorrow, the important thing is not to stop
questioning” Albert Einstein

iv. My lovely beautiful daughter “Darlene” I pray this


book will be your manual book towards being A
NOBLE GIRL in Jesus Name.

v. The girl of my life to whom I believe


COMPLIMENTARY are there I real love you and you
my Inspirer. Ukweli ni huu umenisaidia sana kuwa
nilivyo leo “Namwasi Mathayo Mjema”.

7|P a g e
SHUKRANI
Maisha ya mtu na hasa kusudi la Mungu hukamilishwa kwa
michango ya watu mbalimbali, kwangu mimi ni hekima
kuwashukuru wafuatao kwa sababu ya kitabu hiki: -
i. Yehova Mungu (Mola) ambae kwake nimeumbwa,
ninaishi, ninatembea na ninafanikiwa na kuwa na
uzima tele.

ii. Wazazi wangu na hasa Mama yangu Kipenzi Mwl.


Janeth Kisanga (Bibi), Nampenda sana.

iii. Wanoaji, Washauri, Marafiki, Wahisani na Walezi


wangu wa Kiroho, Kitaaluma, Kiuchumi na
Kimahusiano.

iv. Wadau au Wasichana wote ambao wamekuwa


sababu kubwa ya uandishi wa kitabu hiki
“Nawapenda Mashosti Mungu awabariki sana”

v. Pathfinder Image kwa kufanya kazi hii njema itoke


kwa kiwango hiki “Yehova Yire Awatangulie”

8|P a g e
UTANGULIZI:
“The person who doesn’t make mistake is unlikely to make
anything”
Paul Arden.

Makosa au kukosea ni sehemu ya maisha ya kila mwanadamu,


halikadhalika wasichana walio wengi wanakosea sana ama kwa
kutojua na wakati mwingine kwa kujua kabisa wakiendeshwa
na hisia (Feelings).
Kosa au kukosea ni kule kufanya jambo lisilo sahihi au sawa
(Doing something which is not correct) lakini pia kosa ni kule
kutambua, kuelewa au kuelezea jambo au mtu visivyo (wrongly
identified someone or something) na pia kosa ni kule kufanya
maamuzi visivyo sahihi (Making Error of judgment) maelezo
haya yote matatu wasichana wengi wanajikuta wamekosea,
1. Wanafanya mambo yasiyo sahihi
2. Yapo mambo wanayoelewa, wanayatambua, na
kuyaelewa visivyo
3. Yapo maamuzi mengi wanayoyafanya kinyume na
kanuni, na mambo yote haya yamewafanya kujikuta
wanafanya makosa mengi makubwa ambayo
yamekuwa yakiwagharimu maisha yao, malengo,
mipango na hata ndoto zao. Haijalishi kuwa wewe ni
msichana mdogo au mkubwa kiasi gani wa umri gani

9|P a g e
au kiwango gani cha elimu ila maadamu bado
hujaolewa kuna makosa kati ya 21 wanayofanya
wasichana wengi mwishoni utakubaliana nami kwamba
unayafanya au uliwahi kuyafanya.

UKUMBUKE TU KWAMBA;
“All men make mistake but only wise men learn from their
mistake”
Winston Churchill.

Ni dhahiri kwamba kila mtu anafanya makosa ila ni watu


wenye hekima pekee hujifunza kutokana na makosa yao, na
ninajua wazi kwamba maadam umepata nafasi ya kusoma
kitabu hiki moja kwa moja nakuhesabu kama msichana
mrembo mwenye hekima ambae baada ya kusoma makosa
haya 21 utajitathmini binafsi ni wapi ulikosea kisha utajifunza
kutokana na hayo makosa.

Imenigharimu takribani mwaka mzima kuandaa kitabu hiki


japo kwako kinaonekana ni kidogo tu. Mungu-Roho-Mtakatifu
alikuwa akinifundisha kwa njia mbalimbali na halisi juu ya
makosa haya 21, hivyo ninachoamini ni kwamba kuna pumzi
(Uwepo) wa Mungu kwenye hiki kitabu, na Nina Uhakika
ukisoma kwa umakini na kuzingatia yaliyomo utakubaliana
nami kwamba ukirudia haya makosa unakuwa umeamua tu.

10 | P a g e
Kwenye maisha ya msichana au binti yeyote kuna hatua za
ukuaji au mchakato ambao ni lazima aupitie kwa mfano: -
kuvunja ungo (Kupevuka) na mengine mengi. Makosa mengi
kati ya haya 21 ambayo wasichana wengi wanafanya, huwa
wanaanza mara tu baada ya msichana kupevuka na kujikuta
anaanza kuwa na hisia au mvuto na watu wa jinsia nyingine
(Ya Kiume). Hatua hii kimsingi inakuhamisha hata kama hutaki
kutoka utoto kuelekea Utu uzima. Viungo katika mwili wako
hubadilika aidha kwa kukua au hata vipya kutokea, ghafla
umbo lako linaanza kuwa na mvuto wa tofauti, ngozi inakuwa
laini na sauti kuwa nyororo wakati mwingine. Haya yote
yanachangia Usumbufu wa maombi na sifa kutoka jinsia ile
nyingine kuwa mkubwa, na hapa ndipo wengi huanza
kukosea. Hebu nisimalize huu utamu badala yake nikufundishe
kitu juu ya makosa

MTAZAMO SAHIHI JUU YA


MAKOSA UTAKAOKUSAIDIA;
Makosa kwa lugha ya kiingereza ni MISTAKES, Fatilia
uchambuzi huu: -
M- MESSAGES: that gives us feedback about life.
I - INTERRUPTIONS: that should cause us to reflect
and think.

11 | P a g e
S - SIGNPOST: that directs us to the right path.
T - TESTS: that pushes towards greater maturity.
A - AWAKENINGS: that keep us in the game
mentally.
K - KEYS: that we can use to unlock the next door of
opportunity.
E - EXPLORATIONS: that lets us journey where we
have near been before.
S - STATEMENTS: about our development and
progress.

Kwa Kiswahili kizuri tu acha nikudadavulie maana ya


uchambuzi huu mzuri wa maneno yanayotokana na neno
“MISTAKES” (Makosa), kama ambavyo Mtumishi wa Mungu
Mama Joyce Meyer alivyolichambua ili kutusaidia.

MESSAGE: (Ujumbe),
Makosa ni ujumbe unaotupa urejesho juu ya mfumo sahihi wa
maisha, tunapokosea tunajifunza namna ya kuishi.

INTERRUPTIONS: (Usumbufu/Vikwazo),
Makosa ni usumbufu au vikwazo vinavyotusukuma kuakisi na
kufikiri kwa kina.

SIGNPOST: (Kibao Elekezi),

12 | P a g e
Makosa ni kibao elekezi cha kutusaidia kwenda njia sahihi.
TESTS: (Majaribio), Makosa ni majaribio yanayotupelekea
kukua na kupevuka.

AWAKENINGS: (Uamsho),
Makosa ni uamsho unaotufanya tutumie akili ipasavyo.

KEYS: (Funguo),
Makosa ni funguo zinazotumika kufungua mlango wa fursa
nyingine.

EXPLORATIONS: (Ugunduzi),
Makosa ni ugunduzi unaotusafirisha mpaka mahali ambapo
hatukuwahi kufika kabla.

STATEMENTS: (Kauli),
Makosa ni kauli juu ya maendeleo yetu.

Hivyo basi yatazame makosa yote 21 kwenye mtazamo huo


hapo juu ili kama ulikosea, usije ukaendelea kukosea badala
yake yatumie kwa uchanya, twende sasa moja kwa moja, hatua
kwa hatua, mguu kwa mguu, na bega kwa bega, tukajifunze
juu ya makosa makubwa 21 wanayofanya wasichana wengi
kumbuka si wasichana wote.

13 | P a g e
Nakushauri sasa nikiwa kiongozi wako chukua penseli yako na
weka alama ndogo kwa kila kosa linalokuhusu kisha kwa
maarifa uliyoyapata amua kubadilika na kutokukosea tena.

14 | P a g e
MISTAKE 1:
YOU DON’T KNOW YOURSELF! (HUJIJUI)

“Knowing Yourself is the beginning of all wisdom”


Aristotle

Moja ya makosa makubwa wanayofanya wasichana wengi ni


kutokujijua. Wasichana walio wengi hawajui UBORA,
THAMANI, KIWANGO na UZURI walionao lakini pia wengi
hawajui ile asili (Nature/Origin) ya msichana kama
alivyoumbwa na Mungu. Yapo mambo mengi sana ya kiroho,
kibaolojia, kisaikolojia na kijamii yanayomhusu msichana
ambayo ni muhimu sana kwa kila msichana kuyaelewa, na
akiyaelewa inakuwa rahisi sana kujitambua na kujitunza.

Pengine tunavyoendelea mbele kwenye makosa mengine


ninaweza kukueleza kwa kina asili, tabia, uwezo, nguvu na
chanzo cha msichana LAKINI kwa sasa hebu tambua mambo
haya machache: -

1. Hukuzaliwa msichana kimakosa au kwa bahati mbaya


BALI kwa kusudi na mpango kamili wa Mungu “Kabla
mimba yako kutungwa Mungu alishakujua na alitaka
uzaliwe msichana na sio mvulana”

15 | P a g e
“Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla
hujatoka tumboni nalikutakasa; nimekuweka kuwa…”
Yeremia 1:5
Hivyo basi furahia kuzaliwa msichana na jikubali kuwa
msichana, lakini pia furahia familia yako na wazazi
waliokuzaa, hii ni sehemu muhimu ya kujitambua.

2. Sura, Umbo, Rangi, Kimo na Muonekano ulionao ndio


ambao Mungu alitaka uwe nao na anakupenda katika
namna hiyo hiyo. Hebu tazama Zaburi 139:13 “Maana
wewe ndiwe uliyeumba mtima wangu uliniunga
16
tumboni mwa mama yangu macho yako yaliniona
kabla sijakamilika…”
Mungu anajua kwa nini alikuumba hivyo, Jipende na
Jikubali binafsi, anza kujiwaza na kujiona bora na wa
kufaa.

3. Tambua ndani yako Mungu ameweka Vipaji, Vipawa,


Karama, Ubunifu, Uwezo na Nguvu za ajabu, tena za
kufanya mambo makubwa haijalishi unajionaje au watu
wanakuonaje au wanakwambia nini kukuhusu.
4.
“Lakini tuna hazina hii kwenye vyombo vya udongo, ili
adhama kuu ya uwezo iwe ya Mungu, wala si kutoka
kwetu”
2 Korintho 4:7

16 | P a g e
Ni vile hujitambui tu ila kwa taarifa yako kipaji,
kipawa, karama au uwezo wowote ulionao Mungu
alikupa ili utimize kusudi lake, na ili uishi maisha bora,
mazuri ya mafanikio. Anza kufikiri tofauti juu ya
chochote ulichonacho.

5. Tambua msichana yeyote huendeshwa na hisia zaidi


kuliko fikra (Emotional Feeler)
Ni vizuri pia kufahamu kwa namna msichana
alivyoumbwa na mfumo wa ubongo wake ulivyo
huendeshwa zaidi na hisia kuliko fikra. Hivyo kwenye
tukio lolote msichana huzungumza zaidi kwa hisia
kuliko kile anachofikiri, japo huja kufikiri baadae,
hivyo tambua hisia zako zina nguvu zaidi kuliko fikra
zako. Ni muhimu sana kuwa makini na hisia zako na
badala yake jaribu kuwa unafikiri pia kabla ya kitendo.

6. Msichana yeyote hupenda kusifiwa, kupendwa kujaliwa


na kuonekana wa maana, wa thamani, na wa muhimu
(Affection).
Hii ni asili yako huwezi kuikwepa, na ndio maana
wavulana wengi huichukulia hii kama mojawapo ya
mbinu za kuwalaghai na kuwadanganya wasichana.
Anaweza kukusifia uongo, akakuonyesha wewe ni bora

17 | P a g e
na wa pekee, sababu unapenda kusifiwa na kujaliwa
na ni asili yako utajikuta unaangukia pua.
“To be beautiful means to be yourself. You don’t need
to be accepted by others, you just need to accept
yourself”

7. Mitazamo ya tamaduni, mila, desturi, dini na chochote


juu ya msichana sio muhimu sana kama mtazamo wa
Mungu juu ya maisha yako.
Ipo namna dunia, mila, desturi, dini, utandawazi na
tamaduni zetu zinapotosha kuhusu msichana na hii
imepelekea wasichana wengi kuwa wajinga. Dunia na
utandawazi inaweza kusema kuwa na boyfriend au
kufanya ngono ndio ishu, wewe tazama na komalia
kile Mungu anasema simama katika uhalisia wako,
chanzo chako na ngome yako ambaye ni Mungu.

8. Msichana yoyote anao uwezo wa kufanya mambo


mengi kwa wakati mmoja.
Mfumo wa ubongo wa msichana umeundwa katika
namna ambayo huweza kubeba mambo mengi kwa
wakati mmoja tofauti na mvulana. Hivyo msichana
anaweza kupika, kuongea na simu, kunyonyesha mtoto
na kukuelekeza kitu kwa wakati mmoja. Unaweza

18 | P a g e
kutumia huu uwezo kufanya mambo ya maana
yatakayokusaidia kufikia ndoto na malengo yako
“The more you know who you are and what you want,
the less you let things upset you” Stephanie Perkins
*Usipojijua wewe binafsi na kujikubali utaendeshwa
sana na matukio. Na kutojijua na kutojitambua ndio
huwasababishia mabinti kujikuta wanakosea kila wakati
“Ukitambua Thamani, Ubora, Uzuri, Uwezo na udhaifu
ulionao itakusaidia kujua ni kwa namna gani unaweza
kushindana na kila changamoto, mitego na mbinu za
kukuharibia maisha yako”

SWALI CHOCHEZI; Je unajifahamu na unajijua vizuri wewe


kama msichana? Na kama unajijua vizuri ni kanuni na mipaka
gani umejiwekea ili kumpendeza Mungu na kufikia malengo
yako?

Toka kwa Bro.Elly 24/7; “Jifanyie TATHMINI juu ya


Muonekano wako na Namna ulivyo, Ukijifahamu vizuri, hakuna
mtu ataweza kukwambia kuhusu wewe kuliko wewe
unavyojifahamu”

19 | P a g e
20 | P a g e
MISTAKE 2:
YOU DON’T TEST BEFORE YOU TRUST!
(HAUPIMI KABLA YA KUAMINI)

Ni dhahiri tu kwamba wasichana wengi wameumizwa kwenye


mahusiano na hata biashara na mambo mengine mengi kwa
sababu tu huamini haraka bila ya kupima wanachokiamini
kabla ya kukiamini.

JIFUNZE KWA NDEGE TAI JIKE:


Tai jike kabla ya kuanza mahusiano na tai dume humpima
kwanza ila kumuamini na kuanza nae mahusiano. Kama
ujuavyo hakuna ndege anaeweza kuruka angani juu zaidi
kuliko tai, hivyo tai jike huchukua kipande cha jani kavu na
kupaa nacho juu angani wakati huo huo Yule tai dume
humfatilia kwa karibu, basi anachokifanya Yule tai jike akifika
angani juu sana analiachia lile jani kavu na inakuwa sasa ni
kazi ya tai dume kulitafuta na kulidaka kabla halijafika chini.
Tai dume akilipata anamrudishia Tai jike na Tai jike kwa haraka
anapaa nalo tena juu sana na kuliachia tena huku
akimwangalia tai dume kama atalipata tena, Zoezi hili
hufanyika mara nyingi inavyowezekana mpaka pale tai jike
atakaporidhika na kumwamini tai dume na hatimaye kuanzisha
mahusiano na kuwa familia moja. Huyo ni ndege Tai haanzi

21 | P a g e
mahusiano mpaka amepima na kuamini. Jitahidi iga mfano
huu.

WASICHANA WA SIKU HIZI:


 Anakutana na mvulana kwenye gari anampa namba za
simu, Baada ya siku tatu bila kumjua vizuri mvulana
anaanza honey, baby, love, sweet, my love, my husband
n.k Na baada ya wiki wameshalala wote kama mara saba,
kwa nini usiumizwe?

 Unafika chuoni siku ya kwanza tu kisha kesho yake


ushampata mume na mmeamua kuishi nae

 Unachart Facebook, whatsapp, na kwenye mtandao


wowote ule siku tatu tu unatumiwa nauli unamfata aliko
mkapeane maraha.

 Mlisoma nae O-Level tu mkapotezana kisha mmekutana


kitaa mkiwa chuo, akakuomba urafiki baada ya wiki tu
umeshalala nae

 Umemuona anahubiri tu, au anaimba, au anahudumu tu


kwenye mkutano wa kiroho tayari ukamwona anafaa, siku
mbili tu “Hello! Mtumishi mume wangu” Kwanini usiumie?

22 | P a g e
SASA WEWE NA TAI JIKE NANI ANA AKILI ZAIDI?
“Trust is an expensive thing; you can’t get it to cheap people”

SHUHUDA MBALIMBALI:
“Naomba unisaidie maombi, nachukia wanaume na sitamani
hata kuolewa na nimezaliwa tarehe 1/1/1980, umri unasogea
lakini ndo hata sitamani hata kusikia neno mwanaume”

“Kuna somebody kanifanyia something bad…. I want God to


do something strange over him”

“Nimekuwa nikilala na Baba yangu mzazi tangu nikiwa darasa


la tano na kwa sasa nipo kidato cha tatu na bado nalala nae,
nikikataa anasema atajiua”

“Kuna kaka mtoto wa mamangu mdogo alinitaka kimapenzi,


sijui nifanyeje?”

“Ila….am regretting! I trusted someone a lot what he did is


unbelievable ana mambo mengi, he had other girls,
nilipokuja…. ndio haeleweki kabisaa it has resulted mimi
kupata ulcers”

23 | P a g e
TATIZO:
“Many girls confused on first impression – love at a first sight”
Siku zote usikurupuke kumwamini mvulana au mwanaume
yeyote kwenye mapenzi au mtu yoyote kwenye jambo lolote
kabla ya kumpima

Kumbuka;
“A relationship without trust is like a car without gasoline. You
can stay in it, but it won’t go anywhere”

“A real man doesn’t love million girls; he loves one girl in a


million ways”

Ni vizuri ufahamu kwamba wewe kama msichana kwenye


maisha yako unakutana na marafiki wa kike na wakiume
kwenye maeneo mbalimbali. Ni lazima ujifunze kuwatambua
hao marafiki kwenye ngazi tatu ili uweke trust yako kwa ngazi
pia.

“We will meet 3 types of friends in our life: -


1. Friend for reason - When reason accomplished they
run away
2. Friend for season – When season end they quit
3. Friend for lifetime – They are always with you

24 | P a g e
Marafiki ambao wapo kwa sababu au majira flani, sababu zao
zikiisha au majira yakikamilika huondoka, hawa sio sahihi
kuwaamini wawe wa kike au wa kiume, lakini wapo marafiki au
yupo rafiki ambae unaweza kumwamini.

NAMNA GANI UTAPIMA KABLA YA KUAMINI?


“Ukumbuke hii njia ya kupima si ya kubahatisha, kuna vitu
ataigiza ila sio hizi sifa na ishara zote”
Rejea 1 Wakorintho 13 utaona mambo haya yameelezwa,
nataka leo ujifunze kitofauti kama ifuatavyo: - Rafiki mwenye
upendo wa kweli atakuwa: -

i. PATIENT: Mvumilivu, atakuwa tayari kusubiri bila


kuchoka wala kulalamika i.e. mambo yote
atakayotakiwa kusubiri mfano: tendo la ndoa
ii. KIND: Mkarimu, ataangalia njia za kukusaidia,
kukufariji, kukutia moyo, kukuimarisha na kukuinua
mfano: - kiuchumi, kimasomo, kiroho n.k.
iii. NOT PROUD: Hana majivuno, hatakunyanyasia uwezo,
umaarufu, vipaji, huduma au nafasi aliyonayo.
iv. NOT RUDE: Hakosi adabu, atakuheshimu na kuthamini
mawazo yako lakini pia atatunza heshima yako popote
mtakapokuwa Mf; mbele za watu.

25 | P a g e
v. NOT SELF-SEEKER: Hatafuti mambo yake, hajaja kwako
kwa sababu au matarajio flani au agenda za siri,
Wenye yao utawagundua mapema Mf; Anadai ngono.
vi. NOT EASILY ANGERED: Haoni hasira upesi, na hata
unapomuudhi ukimuomba msamaha anakusamehe na
kusahau na hatakukumbushia.
vii. NOT DELIGHT IN EVIL: Hafurahii uovu au makosa
yako, unapokosea hukukemea na kukusahihisha,
unapokwenda kinyume na Mungu hukueleza wazi.
viii. REJOICES IN TRUTH: Hufurahia kweli, hata kama
utamuuma na kujitahidi daima kuwa muwazi, mkweli
na mwaminifu hana mambo ya siri.
ix. TRUSTWORTHY & HOPEFUL: Hutumaini na Huamini
yote, daima hukuamini na kuwa na matumaini na
wewe, ndoto zako na mipango yenu na zaidi
humwamini na kumtumaini Mungu.
x. PROTECTOR: Hukulinda katika Nyanja zote kimwili,
kiroho, kimahitaji, kihisia, na kijamii kuhakikisha
kwamba haudhuriki na unasonga mbele.

JE UNAEMWAMINI ANA SIFA NA ISHARA HIZI


KWAKO?

“True friendship exists when its stretched to its further extent


and doesn’t break”

26 | P a g e
Wasichana wengi wameumizwa kwa kung’ang’ania watu
ambao wanajua dhairi si waaminifu ama hawawapendi kama
wanavyofikiri, imefikia hatua ni lazima sasa useme IMETOSHA
na NG’ATUKA, maana mahusiano bila kuaminiana ni kama
gari zuri bila mafuta unaweza kukaa ndani yake ila halitaenda
popote.
Nina mifano na shuhuda za mabinti wengi ambao
waling’ang’ania mahusiano yasioeleweka kwa sababu ya hisia
zao walizoziita UPENDO wakaambulia VIDONDA.

SWALI CHOCHEZI; Je! Kwanini unamuamini unayemuamini?

Toka kwa Bro. Elly 24/7- “Mahusiano na hasa ya kimapenzi ni


jambo ambalo litagharimu maisha yako yote, na kwa hivyo hii
si sehemu ya kutumia hisia na kukurupuka kwa sababu ya
muonekano wa nje, Hakikisha unajipa muda wa kutosha
kupima ili UAMINI”

27 | P a g e
28 | P a g e
MISTAKE 3;
YOU DON’T HAVE EYES TO SEE BEYOND
WHAT YOU CAN LOOK!

(HUNA MACHO YA KUONA ZAIDI YA PALE


UNAPOANGALIA.)

“Pasipo maono, watu huacha kujizuia…….”

Mithali 29:18

MAONO ndio uwezo wa kuona zaidi ya pale macho


yanapoangalia. Wasichana wengi hawana macho ya kuona
zaidi ya pale wanapoangalia. Kwa sentensi nyepesi ni kwamba
hawana ndoto wala maono juu ya maisha yao ya baadae,
Wanaishi kwa sababu wanaishi. Mfalme Suleimani anasema
pasipo maono watu huacha kujizuia, na ndio maana
wasichana wasio na maono na mtazamo wa kina juu ya maisha
yao ya baadae hujiachia bila kujizuia kwenye mapenzi,
mavazi, maongezi na anasa za kila namna.

UNATAKIWA UONE KWA NAMNA MBILI;

1. FORESIGHT {Kuona Mbali}, Is the ability to see any


event and prepare for it before it happens i.e Uwezo
wa kuona tukio lolote na kujiandaa kulikabili kabla

29 | P a g e
halijatokea, Kwa mfano msichana ana mitihani mbele,
anajiandaa kupata kazi(ajira), kuingia kwenye ndoa na
kadhalika. Ni Muhimu msichana awe na maandalizi ya
kutosha juu ya matukio yanayokuja mbele yake na huo
ndio uwezo wa kuona zaidi ya kuangalia.

2. FARSIGHT {Kukokotoa}, Is the ability to careful


calculate the result of future outcome of present
conduct i.e Uwezo wa kukokotoa kwa umakini matokeo
ya kitakachotokea baadae kwa unachokifanya sasa.
Huu ni uwezo ambao wasichana wengi hawana na
wanakosea sana. Wengi hawana uwezo wa kuhesabu
matokeo yatakayotokea baadae kwa wanayoyafanya
sasa. Wapo ambao wanafanya ngono, wanatoa
mimba, ni wavivu hawajishughulishi, wanadanganya,
wanahongwa, wanatumia madawa makali ya kuzuia
mimba, wanatumia vipodozi vikali vya kujichubua, ni
walevi wa kupindukia, wana viburi na majivuno ILA
hawajui matokeo au madhara yatakayotokea baadae
kwa wanayoyafanya sasa.

Ni lazima msichana kuwa na maono, ndoto au malengo


ambayo atayakomalia ili awe na maisha bora na mazuri ya
baadae. Ni vizuri ukijituliza badala ya kuhangaika na mambo

30 | P a g e
mengi ambayo baadae utayajutia maana daima “UNAVUNA
ULICHOKIPANDA NA SI TOFAUTI NA HAPO”

Piga picha ya maisha yako ya baadae na yaangalie kwa kina


kisha anza kuishi leo kwa kujenga msingi bora wa maisha
hayo ya baadae kumbuka
“MAISHA NA MAAMUZI UNAYOFANYA LEO yanatoa taswira
halisi ya MAISHA YAKO YA BAADAE”.
“Your Present Faithfulness determines faithfulness of your
husband”

“Go as far as you can see; When you get there; you’ll see
further”
Zig Ziglar

SWALI CHOCHEZI; Je! Una maono na ndoto gani juu ya


maisha yako ya baadae? Na unachokifanya sasa kinachangiaje
kukamilishwa kwa ndoto au hayo maono?

Toka kwa Bro.Elly 24/7- “Msichana unayesoma kitabu hiki


fahamu kwamba chochote unachokifanya leo kiwe kizuri au
kibaya ndicho kinachojenga maisha yako ya baadae. Na amini
au usiamini utakilipia gharama baadae, ONA MBALI”

31 | P a g e
32 | P a g e
MISTAKE 4:
YOU ARE THE FEMALE IMPALA IN HAREM
SYSTEM!
(WEWE NI SWALA JIKE KATIKA MFUMO DUME)

HAREM SYSTEM:
Huu ni mfumo wa maisha ya Swala aina ya Impala ambao
dume moja la Impala humiliki kundi kubwa la impala majike.
Katika mfumo huu dume moja la impala limaweza kumiliki
mpaka majike 40 kama wake zake. Basi majike haya huwa na
dume hili kila mahali anapokwenda. Mfumo huu kwa lugha
rahisi huitwa “Polygamism” ambao mwanaume mmoja
anamiliki wanawake wengi kama wake zake.

SIKUHIZI:
Wasichana wengi tena wenye utashi, warembo na wengine
waliosoma kabisa wamejikuta kwenye huu mfumo kama wa
majike ya Impala aidha kwa kujua au kutokujua. Wapo
wanaojiita wamependa na hawako tayari kuwapoteza wavulana
wao kwa hiyo haijalishi yupo na wasichana wangapi
wanamng’ang’ania kama kupe. Wewe sio tairi la ziada (Spare
Tyre).
Sikiliza nikwambie kitu KAMWE usiruhusu heshima, thamani
na uzuri wako upotee kisa hisia, usiruhusu magonjwa ya zinaa

33 | P a g e
na mshtuko wa ubongo na presha ikupate kisa unajiita
unapenda. Zingatia mambo haya mawili kwa sababu Mungu
amekupa utashi na hekima.
“When someone treats you like an option, help him narrow his
choices by removing yourself from the equation. It’s that
simple” JITOE HARAKA

“I would rather be alone with dignity than in a relationship that


requires me to sacrifice MY SELF RESPECT”
Mandy Hale

“Its quite impossible to divide love- Ni bora kujitoa na kupata


maumivu ya muda kuliko kununua tatizo la milele mfano
watoto wa nje, wake wenza, magonjwa ya zinaa n.k.

SWALI CHOCHEZI- Je! Mpo wangapi? Upo tayari kupoteza


utu, heshima na adhi yako kisa kung’ang’ania majibu yasiyo
sahihi?

Toka kwa Bro.Elly 24/7; “Msichana kamwe usijing’ang’anize


kwa mwanaume ambaye unajua kabisa wazi kwamba ana
wasichana wengi kwenye mahusiano, Kamwe usinunue
matatizo kwa sababu eti ya hisia za kupenda”

34 | P a g e
MISTAKE 5:
YOU ARE IDENTICAL TO FEMALE AFRICAN
JACANA BIRD
(UNAFANANA NA NDEGE AFRIKAN JACANA JIKE)

AFRICAN JACANA FEMALE:


Ndege jike Afican Jacana ni ndege mwenye rangi, sura na
umbo la kuvutia, ndege huyu ndie pekee anaeitwa (Prostitute
Bird) yaani Ndege Malaya kutokana na tabia zake licha ya
uzuri wote alionao. Asilimia kubwa ya ndege ni “Monogamy”
yaani mke mmoja na mume mmoja, lakini kwa African Jacana
ni tofauti kwani ndege huyu jike hujipendekeza na kujionyesha
kwa ndege dume mpaka ampate, na baada ya kuwapata
akitaga mayai huyatelekeza na ndege dume ndio huyatunza,
na akimaliza kuyataga na kuyatekeleza huondoka na kutafuta
madume mengine tena na HII NDIO TABIA YAKE.

WASICHANA JACANA:
Siku hizi pia tuna wasichana wengi sana ambao muonekano
na tabia zao hufanana kabisa na ndege huyu wa kike Africa
Jacana. Wasichana hawa kuanzia vaa yao, tembea yao,
angalia yao na ongea yao huashiria dhairi kujionyesha na
kujipendekeza kwa wanaume wakiwataka kwa lazima. Malengo
yao ni ama kutaka pesa, umaarufu au basi tu kuwakomoa
wanaume, na inapotokea wamepata mimba na kuzaa
huwaacha watoto na bibi zao au babu zao na kisha huendelea

35 | P a g e
na tabia yao. Waswahili walisema; “KIZURI CHAJIUZA KIBAYA
CHAJITEMBEZA”

Ipo asili ambayo Mungu aliiweka kwenye maisha ya


wasichana, lakini pia zipo tabia au sifa ambazo zinajulikana
dhairi kwa mwanamke yeyote kama mama na kama mke.
Haijalishi una uzuri wa kiasi gani ila kama tabia ni kama za
African Jacana thamani, heshima na ubora wako umepotea.
BADILIKA.
Ladha ya mapenzi ya Kiafrika ni mwanaume kumfata msichana
aliyempenda, na kumuomba tena kwa kubembeleza waingie
kwenye urafiki utakaopelekea malengo mazuri ya kuja kuoana
baadae, tena chini ya kanuni za kiMungu na desturi zetu
Waafrika.

Mwanaume yeyote huwa hawezi kujisikia vizuri inapotokea


msichana amempenda na kumfata kumwambia. Ukifanya hivyo
na ukafanikiwa jua tu kwamba kuna uwezekano mkubwa sana
wa kuendeshwa kama gari bovu na hatimaye kuja kuumizwa
kwenye huo uhusiano.

SWALI CHOCHEZI; Je! Na wewe ni kama AFRICAN JACANA


BIRD? Unajisikiaje ukimfata mvulana uliyempenda na
kumwambia?
Toka kwa Bro.Elly 24/7; “Ladha ya mapenzi ya kiafrika ni
mvulana kuwa mwanzilishi wa mahusiano. Na heshima,
thamani na ubora wa msichana wa kiafrika ni kufatwa na
mvulana na kuambiwa nakupenda na nakuhitaji”

36 | P a g e
MISTAKE 6;
YOU TALK TOO MUCH!
“UNAONGEA SANA”
GIRLS FOR CONVERSATION:
Hii ni asili na haipingiki kwamba moja ya mahitaji makubwa
kabisa ya mwanamke ni MAONGEZI (Conversation), na
wataalam wamechunguza na kugundua kwamba kwa siku
mwanamke huongea takribani maneno 21,000 tofauti na
wanaume ambao huongea maneno 7,000 tu kwa siku. Na ni
wazi kwamba kuongea sana si tatizo ila tatizo ni nini
unachokiongea na unakiongeaje na ili nini?

UKUMBUKE MANENO NI UHAI (Words are Life)


“Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi….”
Mithali 18:21

“Basi umetegwa na maneno ya kinywa chako, umekamatwa


kwa maneno ya kinywa chako”
Mithali 6:2

“Kinywa cha mpumbavu ni uharibifu wake, na midomo yake ni


mtego na nafsi yake”
Mithali 18:7

37 | P a g e
“Uwe makini sana juu ya unachokizungumza juu yako na juu
ya wengine. Maana ipo nguvu ya uumbaji kwenye kinywa
chako, chochote unachozungumza kinaumbika, ukitamka
uzima, afya, kufaulu, mafanikio na chochote chema hutokea,
halikadhalika ukitamka mauti, udhaifu, kufeli, majanga na
chochote kibaya pia hutokea.

“Maneno yapendezayo ni kama sega la asali; ni tamu nafsini,


na afya mifupani”
Mithali 16:24

“Azuiaye maneno yake ni mwenye maarifa…..hata mpumbavu


akinyamaza huhesabiwa hekima; akifumba midomo yake,
huhesabiwa ufahamu”
Mithali 17:27-28

“YOU BETTER THINK BEFORE YOU TALK ANYTHING TO


YOURSELF OR TO ANYONE”

“Something you are saying to yourself is limiting or allowing


God to move in your life”
David G. Evans

38 | P a g e
ACHA KUONGEA MABAYA JUU YA WENGINE;
Wasichana hupenda kuongea sana juu ya watu kuliko vitu, na
kwa hivyo basi ni muhimu ufahamu kwamba ni hekima na
adabu kutowaongelea wengine vibaya. Maana si vema
kuwatendea wengine lile jambo ambalo usingependa
kutendewa lakini pia; “The things you say about others, also
say a lot about you”

JIFUNZE KUSIKILIZA ZAIDI KULIKO KUONGEA:


Ni vizuri pia hii sheria ya 60/40 ikusaidie ambayo
inamaanisha kwenye 100% za maongezi yoyote sikiliza kwa
60% na ongea kwa 40%. Hii itakusaidia kujifunza zaidi kuliko
kujionyesha unajua sana kuongea.

USIONGEE NA WANAUME KWA SABABU TU UNA KIU YA


KUONGEA:
Wapo wasichana wenye tabia ya kuongea na kuchart na
wanaume kwa simu na kwenye mitandao au hata uso kwa uso,
na si kwa sababu wanawapenda au wanavutiwa na hao
wavulana ila ni kwa sababu tu wanajisikia kuongea
(Conversation need). Wengi wamejikuta wameingia kwenye
mtego bila kujua kwamba IMANI chanzo chake ni KUSIKIA.
Hivyo ukimsikiliza mtu sana ipo siku utamwamini.

39 | P a g e
JIFUNZE KUZUNGUMZA UKWELI NA KUYAISHI MANENO
YAKO:
o Ni vizuri kutenda unachokisema kuliko kuzungumza
sana bila vitendo. Lakini pia jifunze kusema ukweli na
hasa mambo ambayo una uhakika nayo.
“Your words mean nothing when your actions are the
completely opposite”
“The greatest advantage of speaking the truth is that
you don’t have to remember what you said”

SWALI CHOCHEZI; Je! Na Wewe unapenda kuongea sana?,


Huwa unaongea nini na uko kuongea huwa kunakusaidiaje?

Toka kwa Bro.Elly 24/7; “Kwa sababu maneno ni uhai na


chochote unachokitamka kinaumbika, na ni ngumu sana
kuwazuia wasichana kuongea maana ni moja ya mahitaji yao
muhimu waliyoumbiwa na Mungu. Ninashauri jifunze kuongea
mambo mazuri ya kuelimisha na kujenga, epuka umbea, fitina
na masengenyo na uzushi kwenye maongezi yako”

40 | P a g e
MISTAKE 7:
YOU DON’T LIKE TO FLY ALONE!
(HAUPENDI KURUKA MWENYEWE)
Moja ya majanga makubwa waliyonayo wasichana wengi leo
ni kushindwa kujisimamia na kufanya maamuzi yao binafsi.
Maisha yao yamekuwa yakiendeshwa aidha na marafiki zao
(Mashosti), wavulana wao na hata matukio. Wengi wamejikuta
wakiangukia pua kwa sababu tu wameendeshwa na marafiki
na matukio bila kujua kuna madhara makubwa mbele. Wapo
ambao walikuwa hawana wanaume wakapata kwa sababu ya
kampani, halikadhalika wapo ambao leo wanakunywa pombe,
wanavuta sigara, wanavaa nusu uchi, wanaenda club, wanatoa
mimba, wanasengenya wengine n.k. si kwa sababu walikuwa
hivyo ila ni kwa sababu kampani na marafiki walionao
waliwasukuma kufanya hivyo.

“Stand up for what is right even if you stand alone”

TAI ndie mfalme wa ndege wote japo si kwamba ndie mkubwa


wa umbo labda kuliko ndege wote, kwa nini ni mfalme? Ni
kwa sababu anazo sifa ambazo ndege wengine hawana
ikiwemo ya kuruka angani juu sana tena akiwa mwenyewe.
Ndege karibu wote huruka kwa makundi, hutembea kwa
makundi, hula kwa makundi, na hata kwenye mtego

41 | P a g e
hukamatwa kwa makundi. Ila Tai huruka mwenyewe juu sana,
huwinda mwenyewe, hula mwenyewe n.k.
- Karibu watu wote waliofanikiwa sana hapa duniani ni wale
waliosimama kama wao kwenye ndoto zao na malengo
yao. Hawakukubali kuendeshwa na marafiki, wala
mashosti, wala matukio walisimamia misimamo yao kwa
bidii bila kujali watu wanasema nini au mazingira yakoje,
na hii iliwafanya mwanzoni kuonekana wajinga,
wanaojisikia, wanaojifanya wanajua ILA mwishoni
walifanya yasiyowezekana na walifanikiwa sana.
“Hautafanikiwa mpaka umejua kuishi kama wewe na sio
mkumbo”

“Pigeons flying in flocks but Eagles fly alone, fly higher without
limits”

Maisha ya fata mkumbo ni maisha yenye vizuizi, kufeli na


mtazamo hafifu juu ya maisha. Ni muhimu sana wewe kama
wewe msichana kuishi maisha yenye marafiki na watu sahihi,
lakini ukiwa na misimamo binafsi isiyoendeshwa na marafiki,
kampani wala matukio.

“You have only one life to live, and your own life is in your
own hand”

42 | P a g e
Na mtu yoyote asiyependa uhalisia wako au misimamo yako
ambayo hiyo ndio upenyo wa kufikia ndoto na malengo yako
HAKUFAI na achana nae. Amekukuta huvai nusu uchi, hunywi
pombe, hupendi klabu, unasoma sana, huna vinyongo na
watu AKUACHE HIVYO HIVYO na akubaliane na jinsi ULIVYO.

FAIDA YA KUJITEGEMEA BINAFSI


(Be Yourself, Fly Alone)
1. Huimarisha KUJIAMINI kwako (Self-Confidence)
2. Kutotegemea wengine sana
(Less Reliance on others)
3. Inajenga furaha na kupunguza majanga
(Promote happiness and reduce stress)
4. Hukujengea kufanya maamuzi sahihi
(Better Decision Making)
5. Huleta maendeleo binafsi na ubunifu
(Personal Improvement and Creativity)
6. Utafanya mambo wengine wanadhani hayawezekani
7. Huimarisha thamani ya ubora wako
(Improve Self-value and Self-esteem)

“Akaniambia mwanadamu, simama kwa miguu yako, nami


nitasema nawe”
Ezekiel 2:1

43 | P a g e
Simama kwa miguu yako kwenye imani, maombi, ndoto,
maono, maamuzi na maisha yako na kwa hakika
UTAFANIKIWA.

SWALI CHOCHEZI; Je ni mara ngapi umeweza kusimama


mwenyewe kwenye mambo yako? Je marafiki na kampani yako
ina nafasi gani kwenye maamuzi au misimamo yako?

Toka kwa Bro.Elly 24/7; “Msichana jifunze kutengeneza


kanuni na misimamo itakayokusaidia kufikia malengo na ndoto
yako kiroho, kimasomo, kiuchumi na kimahusiano. Usipofanya
hivyo ni rahisi sana kuendeshwa na matukio na hatma yake
utaangukia pabaya”

44 | P a g e
MISTAKE 8:
YOU PUSH OUT FATHERHOOD!
(UNAUSUKUMA UBABA)
Wasichana wengi tulionao leo wanafikiri kwa uzuri tu kuwa na
watoto wao japo si lazima waishi na baba wa hao watoto. Kwa
sababu ya mfumo wa maisha tulionao leo familia nyingi ni
familia za mzazi mmoja na hasa mama, na hii imepelekea
wasichana wengi kutowaamini sana wanaume kwa sababu tu
ya historia na maelezo waliyopewa na mama zao.
Na wakiangalia wamelelewa na mama zao tu na wakavaa,
wakala, wakasoma na hata kufikia ndoto zao. Hii huwajengea
picha ya wao vilevile kuzaa watoto na kuishi nao peke yao bila
baba zao eti kisa ni kwamba WANATAKA UHURU WAO,
HAWATAKI PRESHA, HAWATAKI USALITI, HAWATAKI
USUMBUFU n.k.

Sikiliza Mungu aliyeweka mfumo wa familia kuwa na baba na


mama alijua nafasi na sehemu ya baba katika familia. Na hii ni
muhimu sana kwa watoto na mama, na ndio maana hata kama
mama angekuwa na uwezo wa kifedha na ukali wa malezi wa
kiasi gani bado pengo la baba katika familia litaonekana.
Marafiki zangu wawili waliolelewa kwenye familia ya mzazi
mmoja waliwahi kuniandikia hizi kauli hapo chini pale
walipokumbana na matatizo ya familia

45 | P a g e
“Kweli hizi familia za mzazi mmoja ni shida tupu”
“Yaani kweli baba ni mtu muhimu sana kwetu”

Nikutahadharishe kitu kimoja muhimu kwamba “Hata kama


wewe haumuhitaji mume ila watoto wako wanamuhitaji baba
yao kuliko unavyofikiri”

“You might not need a husband but your children need their
father, not his provisional but his presence”

UBABA:
Neno BABA limetokana na neno la kiebrania ‘ABBA’ na
Kiitaliano ‘PATTA’ ambayo humaanisha chanzo, mhimili,
mwanzilishi, mwendelezaji, mtoaji, mlinzi.
Hivyo basi BABA WA KWELI (Real Dad) ndani ya familia huwa
mtoa mahitaji muhimu ndani ya familia kwa Mama na Watoto,
Yeye ndio chanzo na mhimili wa familia, lakini zaidi yeye ndie
mlinzi (Protector) ndani ya familia. Huwaadabisha watoto,
huwatia moyo, huwafundisha na kuwaeleza juu ya Mungu na
maisha. Na ndio maana mama peke yake hatoshi kuwa mlezi
ndani ya familia hata kama angekuwa na uwezo wa kifedha
kiasi gani nasisitiza.

46 | P a g e
Watoto wako wa kiume wanahitaji kujifunza uanaume kutoka
kwa Baba yao, na watoto wako wa kike wanahitaji kujifunza
namna ya kuwa na Baba na Mume pia ndani ya familia.
Kamwe usilipotezee hili badala yake anza kujenga fikra ya
kuwalea watoto wako ukiwa na Baba yao yaani Mume wako
mpenzi. Na ni dhahiri kila mwanamke yaani hata wewe
unajisikia vizuri na salama unapokuwa na mwanaume wa
kusimama upande wako kwa ajili yako.

“A father is the son’s first hero and the daughter’s first


love”

Ninakubaliana na unachokiwaza kwamba ni kweli siku hizi


wanaume wengi hawaeleweki, ila ninapingana na hitimisho
lako kwamba eti siku hizi wanaume wote hawaeleweki, ni
WENGI ila sio WOTE. Na katika hao wachache
wanaoeleweka, wa kwako yupo, yaani mume wako na Baba wa
Watoto wako. Kikubwa tubu na futa maneno yote mabaya
uliyosema juu ya wanaume, kisha tulia na mwombe Mungu
kwa bidii, fuata kanuni za Ufalme za kumpata mume nae
Mungu anayekupenda sana atakupatia.

Sema Ameni basi Shosti!!!.

47 | P a g e
SWALI CHOCHEZI; Je na Wewe umewahi kuwaza
kutokuolewa na kutokuishi na mwanaume? Umewahi kufikiri
kwa kina umuhimu wa Mume na Baba katika familia?

Toka kwa Bro.Elly 24/7; “Sikiliza msichana, Si Elimu yako,


Pesa zako wala Ukali wako unaweza kuziba gap la Mume na
Baba katika familia. Wewe kama mwanamke unamuhitaji
mume, na Wanao watamuhitaji Baba yao tu haijalishi unawapa
mahitaji yote au la”

48 | P a g e
MISTAKE 9;
YOU ARE THE SEASONAL QUEEN!!
(U MALKIA WA MUDA)
Kiburi, majivuno, kujisikia na kutojali imekuwa tabia ya
wasichana wengi wa siku hizi. Kila msichana ni malkia wa
muda kwa maana hii hapa, vaa unavyovaa, ongea
unavyoongea, tembea unavyotembea, jibu unavyojibu na
angalia kwa dharau unavyoweza ILA tambua hauweza kubaki
ulivyo milele hata kama ungekuwa na uzuri na uwezo wa
kifedha au elimu ya kiasi gani.

“Alisema amin, amin, nakwambia, wakati ulipokuwa kijana,


ulikuwa ukijifunga mwenyewe na kwenda utakako; lakini
utakapokuwa mzee utainyoosha mikono yako, na mwingine
atakufunga na kukuchukua usikotaka”
Yohana 21:18

Just know; “YOU WILL NEVER REMAIN AS YOU ARE


FOREVER”

Wapo wasichana kutokana na uzuri na maumbo waliyonayo,


familia wanazotoka, elimu waliyonayo ama kipaji/uwezo flani
walionao huwaona watu wengine si kitu, huwadharau na
kuona kwamba hawana chochote cha kuwasaidia. Wamejaa

49 | P a g e
maringo, dhihaka, kiburi na majivuno. Kuna wengine hata
muda wa kusalimia hawana, na hata ukiwasalimia hawaitikii
HAYO SIO MAISHA.

Usichana, Urembo na Uzuri ulionao leo umepimwa kwenye


muda, hauwezi kubaki ulivyo milele ndio maana
nikakukumbusha tu kwamba “YOU THE SEASONAL QUEEN”

Wapo wengine ambao wametoka familia fukara na duni na


wanawalazimishia watu kuamini kwao mambo safi kwa kuishi
maisha ya kifahari ya kuigiza huku moyoni wanaumia –

YOU BETTER LOVE YOUR HOME AND MEANT TO CHANGE


THE SITUATION THAN PLAYING DRAMA.

Wapo waliobadili mpaka majina yao halisi, wakabadili na


namna zao za kuongea, kutembea, kuvaa ili tu waonekane
wao ni BORA kuliko wengine “You are just Temporary
Queen”

“Beautiful in my option has nothing to do with looks, its how


you are as a person and how you make others feel about
themselves”

50 | P a g e
MASHINDANO, Wapo ambao daima wanaishi kwa
kushindana, yaani wapo tayari kufanya chochote kuhakikisha
wanamiliki simu za gharama, wanavaa nguo za gharama na
viatu vya gharama, wanasuka nywele za gharama, basi tu
waonekane wao ni bora kuliko wengine. YOUR BETTER LIVE
YOUR LIFE.

“Look in the mirror…..that’s your competition”

BE MODESTY BUT AVERAGE, Ni vizuri kwa msichana yeyote


kupendeza, kwa kujipamba, kujiremba na kwenda na wakati.
Lakini hili linahitaji kiasi kama ambavyo mambo mengi kwenye
maisha yanahitaji kiasi. Maana siku hizi utamwona msichana
amevaa nguo fupi sana na iliyombana sana ikionyesha
maungo ya mwili wake, amejijaza “Make ups” mpaka
anapoteza uhalisia wa umbo na urembo na ubinadamu wake.
UWE NA KIASI “No amount of make up can cover an ugly
PERSONALITY”

EXHIBITIONISM, Wanasaikolojia wamegundua tatizo moja


linaloitwa Exhibitionism ambalo wasichana wengi huacha wazi
maeneo nyeti ya miili yao. Hii ni kujidhalilisha, ni muhimu kila
wakati kulinda na kuheshimu utu na heshima yako “Identity
and Dignity”.

51 | P a g e
Hebu angalia zamani wasichana walikuwa wanavaa underskirt,
baadae ikapunguzwa ikawa ni skintight, na sasa wengi huvaa
chupi tu kama nguo ya ndani, na hivi majuzi wapo walioanza
kuvaa nguo ya juu tu bila nguo yoyote ya ndani, HII NI
HATARI KUBWA SANA.

- KIBURI NA MAJIVUNO huleta ugomvi, mashindano,


uangamivu na hata laana. Hebu Badilika, Ishi kwenye
uhalisia wako, Shaurika na Heshimu kila mtu.

SWALI CHOCHEZI; Baada ya kusoma juu ya kosa hili, ni eneo


gani limekukamata? Kama lipo unadhani ni hatua gani
unazotakiwa kuzichukua?

Toka kwa Bro.Elly 24/7; “Fahamu wazi tu kwamba hauwezi


kuwa msichana milele, siku zinasonga, miaka inaenda, na siku
moja huo muonekano utaisha na hakuna atakayekuhangaikia.
Jaribu kila wakati kuwa makini na kuhesabu gharama ya kila
unachokifanya”.

52 | P a g e
MISTAKE 10;
YOU HAVE A DAY DREAM (WRONG
IMAGINATION)
(UNAOTA NDOTO ZA MCHANA)

Wasichana wengi wa leo wanaota ndoto za mchana kwa kuwa


na taswira mbovu za maisha na mahusiano, acha nikupe
mifano michache kisha utakubaliana na mimi.

WANALAZIMISHIA UKWELI WA TAARIFA:


Kwa mfano msichana anaweza kuwa kwenye mahusiano na
mvulana anayeonyesha kwamba hajatulia, ama hata
asiyempenda ILA utashangaa namna huyo msichana
atalazimishia kwamba jamaa ni mwaminifu na eti anampenda
sana. Mwisho wa siku ANAUMIA na ndoto yake ya mchana.

HUCHANGANYIKIWA NA MUONEKANO WA KWANZA WA


MVULANA:
(First Impression) Hii ni ile namna ya mwanzoni kabisa
anayoikumbuka alivyokutana na huyo mvulana, namna
alivyotabasamu, alivyomjali, alivyomsifia na alivyomshirikisha
malengo yake, hii ilimfanya huyu binti kamwe asitake
kumpoteza huyu mvulana haijalishi yukoje. Endelea na ndoto

53 | P a g e
za mchana mpaka utakapogundua unachoota hakitatokea na
utakuwa umeshaumia.

HUCHUKULIA VIJIZAWADI KUWA NDIO ISHARA YA UPENDO


WA KWELI:
Na wengi sana huchanganyikiwa na hili, akiletewa kadi, maua,
saa, simu, hela, nguo, akitolewa outing maeneo ya gharama
BASI kwenye ndoto yake ya mchana hudhani kuwa anapendwa
sana, bila kujua kwamba mvulana yupo tayari kukupa kitu
chochote ili tu apate anachokitaka, wangapi walipewa zawadi
wakadhani wamependwa mwisho wa siku wakaambulia
maumivu makali.

“You can GIVE without loving, but you never LOVE without
giving”
Victor Hugo

KUTAMBULISHWA KWA WAZAZI, MASHEMEJI, MAWIFI NA


MARAFIKI: Wengi sana waliangukia pua wakidhani
wanapendwa na wataolewa kwa hii swaga. Mvulana anaweza
kabisa kukutambulisha kama mke wake mtarajiwa kwa wazazi
wake na hasa mama, kwa dada zake, kaka zake, ndugu zake
jamaa na marafiki ili tu kukuchanganya na bado akawa
hakupendi na hana nia ya kukuoa. Utasikia baby ongea na
mama yangu, dadangu, shangazi mara mjomba kwa mkwara.

54 | P a g e
Na ndoto yako ya mchana ya kuolewa unaongea nao na ghafla
moyo wako unaamini kwamba ndoa ipo ILA kumbe mwenzako
ana lake jambo, mara amekuweka kwa facebook profile yake
ndio kabisa unachanganyikiwa kumbe mwenzio anajua
ANACHOKITAKA. Wapo wadogo zangu nimewahi kuwauliza,
Una uhakika na jamaa? Kwa mkwara wakaniandikia “I have
been introducing kwao kwa mama na ndugu zake” na mwisho
wa siku walipoteza usichana wao walioutunza muda mrefu na
kuangukia pua.

UNAWEKA MATARAJIO YALIYOZIDI NA YASIYOWEZEKANA


(OVER EXPECTATION) Hii nayo ni moja ya ndoto mbaya za
mchana wasichana wengi huwa wanaota. Utakuta msichana
anaanza kusema mimi nikiolewa ndani kwangu lazima kuwe na
sofa za milioni tano, tv flat 48”, friji labda 2, kitanda labda
cha milioni 2, kapeti sijui la milioni ngapi, na nataka mume
wangu awe hivi na hivi mara kama hana gari mi siolewi na
mengineyo mengi. Bila kukumbuka hivi vyote vinahitaji bidii
na pesa sio maneno. Ni vizuri kupanga maisha mazuri na
bora ila kwa kujishughulisha.

“Follow your heart but take your brain with you”


Zig Ziglar

55 | P a g e
SWALI CHOCHEZI; Je na Wewe huwa unaota ndoto za
mchana? Au pengine labda umewahi kuota ndoto za mchana
na yakakukuta yaliyokukuta??.

Toka kwa Bro.Elly 24/7; “Msichana achana kabisa na ndoto za


mchana ambazo daima huzaa aibu na maumivu makali.
Hakikisha kila wakati unatembea kwenye uhalisia, acha Papara
na kurukia mambo kabla hujayajua vizuri. Kumbuka watu huwa
hawapimi kina cha maji kwa miguu yote miwili”

56 | P a g e
MISTAKE 11;
YOU DON’T LIKE YOUR SWEATS!
(HAUPENDI JASHO LAKO)

Ninakubaliana na asili ya Kimungu kwamba mwanamke ni


mpokeaji (Receiver), Mwanamke alivyoumbwa ameumbwa
katika namna ambayo inamsababishia awe mpokeaji. ILA siku
hizi kuna wasichana wengi ambao hii kwao imezidi mpaka
limekuwa tatizo na wengi wamejikuta wakiingia pabaya. Na
wapo wasichana ambao hawataki kujishughulisha kabisa
kinamna yoyote ili kujipatia kipato, wanakaa tu na
wanategemea wanaume kwa 100%, hawataki kutoka jasho
kabisa.

Kibiblia mwanamke mwenye busara na hekima,


hujishughulisha kwa bidii kuhakikisha anapata kipato kwa ajili
ya maendeleo yake binafsi, familia na jamii. Hebu mwangalie
huyu mwanamke kwenye Mithali 31 kwa makini kuanzia mstari
wa 10 mpaka 31 haya ni baadhi ya maneno ya huo mstari.

“She is clothed in strength and dignity; she laughs without fear


of the future”

Unajua kwa nini anavaa katika nguvu zake na utu wake


unaheshimika, LAKINI pia anaucheka na kutouogopa wakati
ujao? NI KWA SABABU ANAJISHUGHULISHA kujipatia kipato

57 | P a g e
na wala hasubiri mpaka mume amletee kila kitu. Hasubiri
mpaka boyfriend ampe hela ya kununua kila kitu, na wala
hakai kivivuvivu akisubiri kupokea tu. Hebu iga mfano wake,
na anza kufanya kitu hata kama ni kidogo ili kujipatia kipato
kwa jasho lako.

NOTHING GOES FOR NOTHING!!

Wapo wasichana ni “Specialist Receiver” yaani hawajali wao


hupokea tu. Mvulana yeyote anaejileta upande wao na kutaka
kuwapa chochote aidha wana mahusiano nae au la wao
hupokea tu, na wana kamsemo chao “Mtu anajipendekeza
mwenyewe kukupa na hujamuomba utakataa jamani?”.

Waswahili walisema misemo mingi “Cha mtu mavi” “Vya bure


vinaua” n.k. na wanasheria wana kauli inasema; “Nothing
Goes for Nothing” maana yake “Hakuna kitu kinatolewa tu bila
kitu au bila sababu”. Kukufafanulia zaidi chochote
unachopokea kama sio kuhongwa kina sababu, hata iwe vocha
ya jero kuwa makini nayo. KIROHO kuna maana kubwa
unapopewa kitu chochote ukapokea, ni kama “Makubaliano”
tayari.

Hata kama ufahamu wako unasema KAJIPENDEKEZA


MWENYEWE SIJAMUOMBA kisha ukachukua vitu vyake, na
ukampotezea tayari umejiingiza kwenye makubaliano

58 | P a g e
yanayoweza kukugharimu baadae bila wewe kujua. Chanzo
cha migogoro kwenye mahusiano au ndoa yako ni vitu
ulivyovipokea tena ukidhani unamkomoa huyo mwanaume,
haijalishi labda ulikuwa kidato cha Pili, cha Nne, Sita au
Chuoni.

Anza kujifunza kutopokea zawadi au vitu vya “Bwerere”


maana hiyo tamaa mbaya ITAKUPONZA. Na kuna watu
wengine wakikupa kitu wanavisemea maneno, na wewe bila
kujua unapokea ukidhani unamkomoa kumbe unajiingiza
kwenye mtego mbaya sana. Ndio maana wapo wasichana
waliopokea zawadi walizopewa wakajikuta wamenaswa
kirahisi.

“Its better not to receive than receiving without reasoning”


Bro. Elihuruma Maruma

“Nothing can come of nothing”


Shakespeare
LIONESS PRINCIPLE:

Hii ni “KANUNI YA SIMBA JIKE”, Simba huwa wanaishi


kifamilia yaani baba, mama, watoto, Na hii familia huitwa
“PRIDE”, Na kwa taarifa yako sasa simba jike “LIONESS” ndie
tu ambae huwinda na kuilisha familia yote yaani baba na
watoto. Hebu achana na mitazamo ya ajabu na anza kutumia

59 | P a g e
KANUNI YA SIMBA JIKE kwa kujishughulisha kujipatia kipato
ili vile vitu vizuri unavyovipenda ujinunulie mwenyewe.

Upo Chuoni au Sekondari na unataka kiwango kizuri cha


kufaulu jitume soma kwa bidii, acha kutegemea wavulana
wakufanyie “Assignment”. Kama upo kazini jitume fanya kwa
bidii na ufanisi kama unataka kupanda cheo, NA si kujiona
laini na kutafuta “Shortcut” ya kutoa utu wako kwa Boss
unampa penzi eti ili upande cheo. NIWAKUMBUSHE TU
TENA kwamba “Shortcut always is the wrong cut” na “There is
no sweet without sweat” hivyo JISHUGHULISHE. Chanzo cha
manyanyaso mengi ya wanawake hutokana na “Utegemezi
uliokithiri” “UGOLIKIPA” epuka sana sana “UVIVU, UZEMBE,
MARINGO NA UTEGEMEZI.

DON’T WISH, WORK FOR:

“You don’t get what you wish for, you get what you work for”

Jamani natamani niwe na smartphone, natamani nisuke lile


weaving la 50,000/=, natamani niwe na PHD, natamani niwe
na nyumba nzuri na gari langu zuri, yaani natamani nguo
kama ile, mara viatu, mara makeup. ILA vyote hivi haupati kwa
kusema tu unatamani, BALI unavipata kwa kuacha utegemezi
uliokithiri na kuanza kujishughulisha kwa bidii zote. Chochote

60 | P a g e
utakacho unaweza kupata kama tu utajishughulisha kwa bidii
sana.

“Mtu mvivu hataki kulima wakati wa baridi; hivyo wakati wa


mavuno ataomba, hana kitu”
Mithali 20:4

“Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito; na nafsi yake mvivu


itaona njaa”

Mithali 19:15

SWALI CHOCHEZI; Je huwa unapenda kumiliki vitu vizuri??,


Na huwa unapenda kujinunulia mwenyewe au kununuliwa?.

Toka kwa Bro.Elly 24/7; “Hakuna raha na Amani ya ajabu


kama kupokea zawadi au kitu kutoka kwa mtu unayempenda.
Ila hakuna heshima na ujasiri wa ajabu kama kujinunulia kitu
ukipendacho kwa pesa yako uliyoitafuta mwenyewe. Jifunze
kula jasho lako.”

61 | P a g e
62 | P a g e
MISTAKE 12;
YOU DON’T KNOW A ROMANTIC FORMULA!
(HUJUI KANUNI YA MAPENZI)

Wasichana walio wengi sana wanafanya hili kosa la kutokujua


kanuni ashki, hisia na hamu za kimapenzi. Na kwa wavulana
wengi kwa kujua hili wanawafanyia “DANGANYA TOTO” ndio
maana wasichana wengi wanajikuta wameingia mkenge na
kunaswa na mtego.

SAFARI MOJA HUANZISHA NYINGINE;

Usipojua safari moja ya romance huamsha nyingine utajikuta


umeshaumia. Na hii ndio maana ninaiita DANGANYA TOTO,
Unakuta watu ni wapenzi na wanakubaliana kabisa na kuweka
malengo ya kutofanya tendo la ndoa kabla ya ndoa yaani
NGONO. Wengi wanakubaliana haya kwa visingizio au
vijisababu vingi tu labda

- “Oooh bado tunasoma kidato cha pili na sisi ni


wadogo sana”
- “Oooh Mungu hapendi tendo la ndoa kabla ya ndoa”
- “Niliweka agano na Mungu na pia nilimwahidi
nitaitunza bikra yangu”
- “Nilishaahidi sintomwaribu mtoto wa mtu” n.k.

63 | P a g e
- Ila sasa inafika kipindi uzalendo unaanza kuwashinda
na hasa wavulana na hapa sasa utanielewa vizuri.
- Utamsikia mvulana anaanza na hesabu za
KURAHISISHA NA KUTOA yaani ataanza kutoa baadhi
ya misimamo mliyojiwekea na kurahisisha baadhi ya
mambo, kama sio mbaya labda, haina madhara au sio
dhambi huku akikupa mifano ya kutosha.
- Kwa mfano atakuomba akushike mkono mkiwa peke
yenu au labda akubusu na umbusu mkumbatiane tu
(hugs), na ukishakubali hii kwake SAFARI IMEANZA.
Baadae atakubusu kisha atakunyonya mdomo na
kukushika maeneo flani huku akikusisitiza si dhambi na
usipokua makini UTAJIKUTA UMEANGUKIA PUA.
- Fahamu wewe pia una hisia tena kali sana hasa
zikiamshwa kama hivyo. Na utashangaa AKILI
ZIMEHAMA na mwisho wa mchezo ndio utajua ile
ilikuwa DANGANYA TOTO kuhakikisha anakupeleka
mwisho wa safari, ASOMAE NA AFAHAMU.

HEBU ANGALIA MIFANO YA WAHUSIKA NILIO WAHOJI

“Aliniomba nikamnyima ila nikampa kiss tu”

“We only had wet kiss and zero hugging that’s all”

64 | P a g e
Wengine wakauliza;

“Hivi wet kiss (kunyonya mdomo) ni dhambi?”

“Hivi kumake love si ni dhambi?”

Watu wanashindwa kuelewa vitu rahisi sana kwamba dhambi


huanzia kwenye NIA “FIKRA” hivyo hata kama haukufanya
mpaka mwisho maadam ni kiashirio kuelekea Ngono UMEZINI
tayari.

NGONO SI YA KUCHOCHEWA NI YA KUKIMBIWA

“Nawasihi enyi binti za Yerusalemu kwa paa na kwa ayala wa


porini, Msiyachochee mapenzi wala kuyaamsha hata
yatakapoona vyema yenyewe “

Wimbo Ulio Bora 2:7

“Ikimbieni Zinaa ---------“

1 Korintho 6: 18

UNACHOCHEAJE? (KINDLING ROMANCE)

Catalysts {VICHOCHEO} ni kama;

 Kuangalia picha za ngono (pornography),


 Kusikiliza nyimbo za mapenzi,
 Kusoma hadithi za mapenzi,

65 | P a g e
 Kusikiliza radio program za mapenzi,
 Kuangalia tamthilia za mapenzi,
 Kuchati messages (ujumbe) za mapenzi,
 Kushikanashikana, Maongezi laini hasa ya usiku ya
kimahaba, Stori za waliotoka kufanya mapenzi na watu
wao. N.k

UNAKIMBIAJE? (HOW TO FLEE)

Ni kwa kuachana na hayo hapo juu ya kuchochea, epuka


faragha na mlie nae kwenye mahusiano, acha kuvaa nguo za
mitego (zinazoacha maeneo nyeti wazi). Epuka kukaa na watu
wanaoongelea ngono kila wakati. Muombe Mungu Akuhifadhi
na Akuhurumie.

SWALI CHOCHEZI; Je umewahi kufahamu kwamba hatua moja


ya tendo lolote la romantic husababisha hatua nyingine?
Jaribu kukumbuka mchakato mzima uliokupelekea kuanguka
kwenye UZINZI utagundua ilianza na hatua moja uliyoiona ni
nzuri tu tena haina madhara na si dhambi.

Toka kwa Bro.Elly 24/7; “Inawezekana hukuwahi kufahamu juu


ya kosa hili kabla, ila fahamu wavulana wanajua wazi tu
kwamba siku ya kuanza tu kulala na wewe ndio ngumu. Na
wanajua wazi ukishawakubalia hatua moja ni rahisi sana
kukupeleka hatua nyingine mpaka kumaliza mchezo. Na
baada ya hapo ni rahisi mno hiyo kuwa tabia yenu mpaka siku
atakapokuchoka na kukuacha.”

66 | P a g e
MISTAKE 13;
YOU WANT TO FINISH BEFORE YOU START!
(UNATAKA KUMALIZA KABLA YA KUANZA)

Wasichana wengi si wazuri katika kusubiri au kuwa wavumilivu


hasa kwenye mahusiano. Na hii inasababishwa na wasiwasi,
woga na hisia kali zinazo waendesha. Na ndio maana
nimesema kosa lako UNATAKA KUMALIZA KABLA YA
KUANZA. Acha nikupe vipengele vichache tu ili ukubaliane
nami taratibu tu.

 YOU ACT AS A WIFE WHO IS NOT OFFICIAL

Utakuta msichana ndio kwanza ana muda mchache sana tangu


wameanza mahusiano na huyo mvulana, ila sasa utaona hicho
kiherehere mara amtembelee mvulana kwake amfanyie usafi,
amfulie, ampikie, wakati mwingine alale naye hata wiki nzima
eti ana mapenzi ya dhati. LABDA nikusaidie tu wavulana huwa
wanavutiwa zaidi na MISIMAMO MIKALI jumlisha kumiss vitu
na daima huwa wanapata wasiwasi mkubwa na msichana
anaejirahisisha hata kama hatakwambia. Wao wanajua “Cheap
is temporary” hivyo atajiact anakupenda NA kukukubali ila
mwisho wa siku akilini mwake anajua huyu si wakuoa. Ni
vizuri ujiweke wa gharama, na usijirahisishe ukidhani

67 | P a g e
unalinda Penzi kumbe unajitengenezea mazingira ya kutumiwa
na kuchokwa.

 Waswahili wakasema;
”Haraka haraka haina Baraka”
“Pole pole ndio mwendo”
“Mvumilivu hula mbivu” I AGREE

 Na kwenye hali hii haina cha kufanya na “Na ngoja


ngoja huumiza matumbo” au “Chelewa Chelewa
utakuta mwana si wako” TULIA DADA WEWE NI WA
THAMANI NA WA GHARAMA, TULIZANA.

COMPARE FRIENDS AND HISTORY, Hii pia ndio mbaya zaidi


hapa unakuta msichana labda analazimishia utambulisho wa
haraka, au Engagement au kufanyiwa kitu flani eti kwa madai
kwamba mbona hata dada yangu alifanyiwa hivi na shemeji
yangu muda flani flani kabla hawajaoana. Mara mbona kaka
yangu baada ya miezi mitatu tu alimtambulisha wifi nyumbani,
Mara mbona rafiki yangu analalaga Kwa mchumba wake.
Mahusiano na Ndoa ni makubaliano ya watu wawili na
hayaendeshwi na historia flani au COPY-PASTE yoyote.

68 | P a g e
KULAZIMISHIA MAHUSIANO YA HARAKA NA UPENDO
{KULIPA KISASI i.e REVENGE.}

Hii ndio nyingi mno mno kwa wasichana, unakuta msichana


alikuwa na mvulana wake kisha wakaachana au kuachwa
[BREAK UP]. Ndani yake inaibuka hisia na roho ya kulipiza
kisasi kwa sababu ya maumivu ya kuachana au kuachwa,
Hivyo kwa kutaka kumkomoa au kumuumiza Yule mvulana
anaingia kwenye mahusiano ghafla na mvulana mwingine na
kuanza kufanya show off, kwamba anampenda sana na
anapendwa sana na eti anajuta kwanini hawakukutana
mapema. Bila kujua inawezekana ndo kwanza ameruka mkojo
amekanyaga mavi. Hataangaika na vijizawadi na kujali kwa
gharama zote bila kujua HISIA [Feelings] sio upendo [LOVE].
Na wengi wamejikuta wakiumizwa zaidi. UKIVUNJA
MAHUSIANO TULIA KWANZA USIWE NA HARAKA YA
KUFANYA MAAMUZI Bali jifunze kutokana na huo MVUNJIKO.

GOD’S TIMING IS THE RIGHT TIME FOR YOU!

Kamwe usisahau hili kwamba “Wakati wa Mungu ndio wakati


sahihi” Kamwe usilazimishie jambo linaloonyesha dalili na
ishara zote kwamba sio sahihi na halitafika mwisho. Wapo
ambao walishajilengesha ili walau wapate ujauzito ili waolewe
lakini bado waliangukia pua na wana watoto ila wakiwa
nyumbani kwa wazazi wao.

69 | P a g e
Kamwe usitumie nguvu nyingi na ushawishi mkubwa jumlisha
gharama kubwa kulazimishia ndoa au mahusiano. Mungu
aliyekuumba anajua umuhimu wako na upweke ulionao
LAKINI pia anajua nani anaekufaa, na atakuoa lini. Mungu ni
ALPHA na OMEGA, Mwanzo na Mwisho mpe nafasi maishani
mwako leo, mkimbilie na mtii naye ATAFANYA.

“Age and Loneliness are nothing but God’s purpose and


timing”
Bro Elihuruma Maruma

SWALI CHOCHEZI; Je una haraka yoyote juu ya mahusiano


yako?. Je kuna jambo unalotaka kulilazimishia?.

Toka kwa Bro.Elly 24/7; “Kitu chochote kinapotumika


hushuka thamani yake, na ndio maana kuna tofauti ya bei kwa
vitu vipya na vitu ambavyo tayari vimetumika. Halikadhalika na
Wewe kama msichana ukishaanza kutumika kwa mvulana
kuanzia mwili wako, kumpikia, kumfulia na chochote kile kabla
ya ndoa, thamani yako kwake huendelea kushuka na hatimaye
atakuchoka tu. Acha KUJIRAHISISHA”

70 | P a g e
MISTAKE 14;
YOU OFFER SEX AS A PROVE OF LOVE &
RETURN!!
(UNATOA NGONO KAMA ISHARA YA UPENDO NA
FADHILA)
*Hapa sasa ndio ipo shida kubwa sana hasa ya ufahamu/
Uelewa kwa wasichana wengi sana. Na hii niliifananisha na
mtu kuchimba shimo refu sana yeye mwenyewe ili hali yupo
ndani ya hilo hilo shimo na hajui ni jinsi gani atatoka (Dig a
deepest hole while your inside).

Siku zote kwa ujinga tu watu wamekuwa wakichanganya sana


UPENDO (Love) na NGONO (Sex) kwamba ni vitu
vinavyolandana kiasi kwamba mtu anaona asipopewa tendo la
ndoa kabla ya Ndoa “NGONO” (SEX) basi eti hapendwi
(Love).

Ila ukweli ni huu hapa hata kama utaukataa, UPENDO hauna


cha kufanya na NGONO (Love has nothing to do with sex) ila
UPENDO unaweza kuwepo bila NGONO (Love can exist
without sex), ILA TAMAA YA NGONO ndio haiwezi kuishi bila
NGONO (Lust cannot exist without sex).

71 | P a g e
Upendo sio hisia ni kitendo na chaguo (Love is not a feeling
but choice and action) Love doesn’t go against God but LUST
does. (Upendo huwa hauendi kinyume na Mungu ila tamaa ya
ngono huwa inaenda kinyume na Mungu). LUST (Sex feelings)
is temporary but LOVE is permanent (TAMAA YA NGONO ni
ya muda tu ILA UPENDO ni jambo la kudumu)
Na ndio maana hatuwezi kuhakiki tunapendwa au tunapenda
kwa kutumia tamaa ya Ngono (We cannot prove LOVE
through SEX).
Na kama kuna ujinga na kosa kubwa ambalo wasichana wengi
huwa wanafanya ni kutoa NGONO yaani UTU/USICHANA
wao kama ishara ya UPENDO kwa wavulana ambao bado
hawajawaoa. Na wavulana wengi wamekuwa wakitumia sana
hii gia kufanikisha malengo yao ya kulala na wasichana,
utamsikia kwa hasira au ulalamishi anakwambia “NAJUA UNA
MTU NA HUNIPENDI” ndio maana hautaki kulala na mimi
(Sex), au hauniamini?

“LOVE isn’t all about flirting, hugs, kisses and sex. Love is
about having the ability to take all those things away and still
having feelings for that person”

Na wasichana wengi kwa huruma za kijinga (Pity) na kwa


kuogopa eti hataachwa (Breakup) hujikuta wamekubali na
kuingia shimoni. Na tofauti na walivyofikiri labda kwamba

72 | P a g e
akimpa ngono ndio atapendwa zaidi anashangaa inakuwa
kinyume, mara anashangaa yale matunzo, kujali, mawasiliano
taratiiibu yanaanza kupungua kutoka kwa Yule mvulana alielala
nae. Na mwisho wa siku anaweza kuanza kukuchanganya na
wasichana wengine na hata kufikia kuachana (BreakUp).
Unajua Kwa Nini? AMESHAPATA ALICHOKUWA ANATAKA
(No more business)

Hebu sikiliza kauli hizi za wasichana niliowahi kukutana nao


mahali:-
“Alinidanganya nikashea nae mara moja”

“Amenitumia sana tu ila nilipoingia 3rd year ndo


mikwaruzano ikaanza”

“I feel bitter in my heart, I feel like to cry loudly ili


hasira initoke”

“Unaamini siku hizi hakuna upendo wa kweli?”

“Amenitumia mno na sasa haoni thamani yangu tena,


nimemtamkia maneno mabaya nakwambia kamwe
hataoa”

73 | P a g e
Wote hao walikuwa na malengo ya kuhakiki WANAPENDA ila
WALIISHIA MAUMIVU.

SEX AS A RETURN;
Wapo ambao wao hawakutoa NGONO kuonyesha
WANAPENDA ila WALITOA kama KULIPA FADHILA.
Kisaikolojia wasichana wengi hudhani zawadi kubwa
wanayoweza kumpa mvulana au mwanaume aliyemsaidia sana
kwenye eneo flani maishani mwake ni NGONO. Na ndio
maana wapo waliosaidiwa ADA wakatoa NGONO kama
FADHILA, Wapo waliopewa sana matumizi na wavulana wao
au wanaume wao wakawapa NGONO kama malipo. Wapo
waliopewa ama kusaidiwa MITIHANI wakatoa NGONO kama
MALIPO. Matukio haya ni mengi sana na wasichana wengi
kwa kukosa akili wamejikuta wakiangukia pua.

MTAZAMO WA MUNGU JUU YA TENDO LA NDOA:


Niliwahi kuwauliza wasichana mahali flani nikiwa
nawafundisha. Na nilianza na kauli hii “Kama Mungu alifanya
kila kitu kwa kusudi unadhani ni kwanini aliweka bikira kwa
msichana? Ukumbi ulitawaliwa na ukimya”
*Ndani ya bikira kuna siri kubwa sana za kiroho na hata
kimwili tu, bikira ndio heshima, thamani, utu na ubora wa
msichana yeyote ambaye bado hajaolewa, Na ndio maana
Mungu aliiweka iwe ni utukufu (Glory) kwa Msichana, Na

74 | P a g e
msichana atakapoolewa pia ni ile nguvu ya upatanisho
(Gameo) (Intimacy) inapotolewa kwenye ndoa kama Agano la
ndoa. Agano halisi la ndoa limefichwa kwenye bikira na ndio
maana kibiblia anaekutoa bikira ndie mumeo halali, maana
kwa kukutoa bikira mmeingia nae agano la ndoa. Yaani nafsi
zenu zimeunganishwa ninyi tayari ni mwili mmoja. Hivyo
usifikirie BIKIRA iliwekwa tu kuna siri kubwa mno na faida
kubwa nyuma yake na ndio maana msichana akitolewa bikira
anasema ametolewa usichana wake yaani ule utu, thamani,
heshima na ubora wake unafutika. Na kwa taarifa yako
MATATIZO ya ndoa nyingi za leo yalifunguliwa mlango hapa
kwa sababu tu Mungu aliweka tendo la ndoa ndani ya ndoa,
watu wakakiuka kufanya tendo la ndoa kabla ya ndoa
“NGONO”, kama ulitolewa bikira nje ya ndoa unahitaji TOBA
na kuvunja agano batili uliloweka ili uingie kwenye ndoa
ukiwa na furaha na amani (Zingatia huu ushauri)

MADHARA YA TENDO LA NDOA KABLA YA NDOA:


o Kupoteza utukufu, nguvu ya upatanisho na mumeo
pia heshima na thamani yako
o Kuingia agano la ndoa batili
o Kutoaminiana na mumeo
o Mimba zisizotarajiwa zinazopelekea utoaji mimba
(Abortion) yaani uuaji.

75 | P a g e
o Magonjwa ya zinaa kama Ukimwi, Kisonono,
Kaswende n.k.
o Aibu kwa familia na kwa jamii
o Kutoridhishwa kimapenzi na mumeo
o Mlango kwa mapepo na nuksi kukutawala.

“Kama ulishaanza ingia kwenye TOBA, ACHA na kama


hukuwahi kufanya USIJARIBU na IKIMBIE KADRI UWEZAVYO”

SWALI CHOCHEZI; Je unadhani kutoa mwili wako kwa


mwanaume ndio ishara pekee ya kuonyesha kuwa
unampenda?
Kwa hiyo kipi ni sahihi hapa kutoa mwili wako kwa mwanaume
kumwonyesha kuwa unampenda na kuvunja mahusiano yako
na Mungu, au kukataa kutoa mwili wako kwa mwanaume na
kudumisha mahusiano yako na Mungu anaejua uhalisia na
ukweli kwamba nani ndiye mwanaume anaefaa kuwa mumeo?

Toka kwa Bro.Elly 24/7; “Ukiona unatumia mwili wako kama


ishara ya udhiirisho wa UPENDO kwa mvulana wako ujue wazi
kwamba NGONO ni appetite tu huwa haidumu wakati wote,
na hii inampa tafsiri kwake kwamba wewe ni dhaifu na kwa
hivyo ikitokea umempenda mvulana mwingine utampa pia”

76 | P a g e
MISTAKE 15:
YOU WANT MEN TO BE LIKE YOU!
(UNATAKA MWANAUME AWE KAMA WEWE)
*Hili kosa ndicho chanzo kikubwa cha migogoro na
kutoelewana kwa msichana na mvulana ndani ya jamii na hata
kwenye mahusiano. Na kama watu hawatajifunza juu ya hili,
bado na daima litaendelea kuwa tatizo.

Wasichana walio wengi huwa wanataka wavulana wawe kama


wao bila kujua na kugundua kwamba ipo tofauti kubwa sana
kuanzia kwenye uumbaji kati ya msichana na mvulana. Ingawa
tukumbuke tu kwamba mwanamke aliumbwa ili kukidhi haja ya
usaidizi ya mwanaume lakini hii haimaanishi kwamba
watafanana au kuwa sawa. Sasa leo tusaidiane tu ili wasichana
wasiendelee kufanya hili kosa lakini pia wakawaeleze na
wavulana watambue hili

Kuna utofauti mkubwa sana kati ya wanaume na wanawake


kibaolojia, kihisia, kisaikolojia, kijamii, na hata kiroho. Na leo
tunaongelea chache tu ila zile kubwa za kusaidia ili
kupunguza migogoro baina yetu.

MAHITAJI MAKUBWA 3 YA WANAUME NA WANAWAKE:

77 | P a g e
1. Mwanaume yeyote duniani anahitaji KUHESHIMIWA
(Respect), hii ndio asili yake aliyoumbiwa na Mungu,
na ukitaka mgogoro, vurugu au vita na mwanaume
yeyote usimuheshimu ila ukitaka akupende mpaka
uchanganyikiwe mheshimu.
Mwanamke yeyote duniani anahitaji KUPENDWA
(Love), hii ndio asili yake aliyoumbiwa na Mungu.
Anahitaji aonyeshwe anapendwa, anataka aonekane
yeye ni muhimu, maalum na wa pekee. Umjali na uwe
na muda nae.
Men need RESPECT, Woman needs LOVE!

2. Mwanaume yeyote anahitaji kampani


anapojistarehesha (Recreational Company), huwa
anajisikia vizuri sana anapopata kampani hasa pale
anapofanya akipendacho kama kuangalia muvie,
mpira, kusoma vitabu, kutembelea familia, na
chochote anachokipenda.
Mwanamke yeye anahitaji maongezi (Conversation), hii
ni moja ya mahitaji yake makubwa aliyoumbiwa nayo
tofauti na mwanaume. Na ndio maana wataalamu wa
utafiti wanasema inakisiwa mwanamke huongea
maneno 21,000 kwa siku tofauti na mwanaume ambae
huongea 7,000 tu kwa siku na hapa mwanamke hutaka
muongee (dialogue) na sio umuongeleshe.

78 | P a g e
Men needs RECREATIONAL COMPANIONSHIP,
Women needs CONVERSATION!

3. Mwanaume yeyote duniani kiasili moja ya mahitaji


yake makubwa mno ni TENDO LA NDOA (Sex), hili ni
jambo ambalo analihitaji kiasi kwamba wakati
mwingine wanawake huwashangaa sana wanaume na
kuwachukulia kama wanyama ama kushindwa
kuwaelewa. Zingatia sana hili kwenye ndoa na si
kwenye urafiki wala uchumba. Ila kabla ya ndoa
hakikisha unamuepushia mazingira ya kuamsha hili
hitaji maana ukifanya hivyo hutaamini hata kama
ameokokaje!
Mwanamke yeye hapa anahitaji KUSIFIWA na
KUZAWADIWA (Affection) hili ni hitaji kubwa sana
kwa mwanamke yeyote kuanzia mtoto mpaka mtu
mzima. Anahitaji kusifiwa na kuzawadiwa lakini zaidi
kumpa muda wa kukaa nae

Men needs SEX Woman needs AFFECTION


i.e. Mueshimu Mwanaume (Respect) ili akupende na kukujali
(LOVE)
Mpe kampani ya kukaa nae anapofanya anachokipenda
(Recreational Companionship) ili akupe muda wa maongezi
(Coversation)

79 | P a g e
TOFAUTI ZINGINE:
Kwenye tukio lolote fahamu kwamba mwanaume hufikiri kabla
ya kutenda na ndipo hisia juu ya jambo huja baadae, “They
are logical thinker” na ndio maana ni ngumu sana mwanaume
kuonyesha hisia yake kwa haraka kwenye jambo. Na hii ni kwa
sababu ya mfumo wa ubongo wake ILA Mwanamke hisia huja
kwanza kabla ya kufikiri, na ndio maana wanawake ni watu
wenye hisia kali sana juu ya jambo lolote, “They are Emotional
Feeler”

KWENYE TATIZO:
Wanawake wengi linapotokea tatizo kwa sasabu wao hisia
huja kwa haraka huwaona wanaume kama watu wasiojali na hii
ni kwa sababu wanaume si wepesi wa kuonyesha hisia zao,
najua leo umejua kwa nini mwanaume huonekana kama hajali,
ni kwa sasabu hisia zao zipo mbali sana.

MAONGEZI:
Daima MWANAUME huongea jambo alilolifikiri bali
MWANAMKE huongea jambo kutokana na hisia si fikra.

MUONEKANO:
Daima MWANAUME hupenda tu alivyovaa bila kujali
NYUMBA anayokaa imepangikaje au imependezaje i.e.
nyumbani mwanaume hutupa vitu shabalabagala ILA

80 | P a g e
MWANAMKE yeye hupenda nyumba ionekane nadhifu na
imepangika vizuri muda wote, mgogoro mkubwa ni pale
mwanaume anapotupa vitu ovyo.

MAKOSA MAKUBWA NI PALE MWANAMKE ASIPOGUNDUA


HIZI TOFAUTI NA KUTAKA MWANAUME AWE KAMA YEYE.

USHAURI: Badala ya kuchukia na kulalamika endelea kujifunza


tofauti iliyopo kati ya msichana na mvulana kisha msaidie pale
inapowezekana badala ya kumlaumu, kumsengenya na wewe
kujihesabia haki bila kufahamu kwamba yeye pia kuna vitu
vingi tu anavihitaji na havipati kwako.

SWALI CHOCHEZI; Je umegundua nini kuhusu utofauti uliopo


kati ya mvulana na msichana? Ni makosa gani umegundua
uliyokuwa ukifanya bila kugundua kwamba kuna tofauti kubwa
mno kati ya wavulana na wasichana?

Toka kwa Bro.Elly 24/7; “Msichana, hebu fahamu kwamba


utofauti tulionao wasichana na wavulana ndio unaoweka
thamani yako wewe kama msichana, na ndio maana
tunahitajiana ili kukidhi haja ya ukamilifu wa maisha tunayoishi
leo. Kamwe usilazimishie mvulana kufikiri na kufanya kama
wewe, Utofauti tulionao ndio thamani yetu”

81 | P a g e
82 | P a g e
MISTAKE 16;
YOU SEARCH FOR GREEN PASTURES!!
[UNATAFUTA PENYE UWEZO (UTAJIRI)]
Ni kweli kwamba karibu wasichana wote huwa wanapenda
sana ulinzi/ uhakika wa maisha (Life Security). Na hii
inatokana na jinsi walivyoumbwa, sina tatizo na hilo ILA sasa
wapo wasichana ambao wamejiwekea akilini kamwe
hawataolewa na wanaume wasio na uwezo mzuri wa kifedha.
Wapo wengi walikuwa na msimamo kama huu na walifanikiwa
kuolewa na watu wenye uwezo mzuri wa kifedha ILA mwisho
wa siku waliishia manyanyaso, mateso na utumwa. Unajua
kwanini? Ni kwa kuwa waliolewa na fedha na sio mtu mwenye
UPENDO wa DHATI kwao. Biblia inasema hivi;

“Afadhali mego kavu pamoja na utulivu, kuliko nyumba


yenye karamu nyingi pamoja na magomvi”
Mithali 17:1

“Chakula cha mboga penye wapendanao; Ni bora kuliko


ng’ombe aliyenona pamoja na kuchukiana”
Mithali 15:17

Kwa maandiko hayo hapo juu na mtazamo wa kina wenye akili


timamu ni HIVI; Ni heri kuolewa na mtu ANAEKUPENDA

83 | P a g e
KWA DHATI NA UNAEMPENDA KWA DHATI kuliko
kukimbilia mali na fedha bila kujua kwamba NDOA ni mkataba
wa maisha yako yote.

“It is a point of no return” Hivyo mpende mvulana


anaekupenda na ambae si mvivu, anapigana kujenga maisha
bora KULIKO kukimbilia maisha mazuri yatakayokutesa sana
baadae, kisha UJUTE.

SHUHUDA:
“Mamangu mdogo ameolewa na mtu tajiri sana ila mateso
anayopata ni bora na kuishi maskini, maana fedha, nyumba na
magari havimpi amani kwa jinsi mume wake anavyomfanyia”
Kijana mmoja rafiki yangu alikuwa akinihadithia
“Dadangu ameolewa na tajiri sana ila mateso anayopata
imebidi awe anatoka nje ya ndoa”
Mifano ya shuhuda nilizokupa si maigizo au hadithi za
kutunga au kudhania ni vitu halisi kabisa vinavyotokea.

FAMILIA YANGU, JAMAA, NDUGU NA MARAFIKI


WATANICHUKULIAJE?
Wapo wasichana wengi ambao wapo kwenye mahusiano na
wanaume wenye vipato vya chini au vya kati na wanaogopa
sana kusema wapo tayari kuolewa nao japo WANAWAPENDA
eti kisa nyumbani hawatamkubali, wazazi watanionaje,

84 | P a g e
wakubwa zangu watanicheka, na yanayofanana na hayo.
Badala yake huachana nao na kwenda kuolewa na watu
wasiowapenda ila wenye uwezo ili tu kuwafurahisha wazazi,
kanisa, ndugu, jamaa, na marafiki, jambo ambalo ni ujinga tu
kama ujinga mwingine.

KUMBUKA; Atakaeenda kuishi na huyo mwanaume ni wewe


binafsi na si wazazi wako, ndugu, jamaa na marafiki zako.
Ukishawafurahisha wao, mziki wa ndani utaenda kuucheza
mwenyewe kwa kadri ulivyo, tena maisha yako yote.

JIRANI YANGU; Huko nilipozaliwa kulikuwa na jirani yetu


mmoja ambae alijaaliwa kupata mabinti karibu wote wazuri
sana maumbo na sura. Huyu jirani alikuwa na tabia ya
kuwalazimisha watoto wake kuolewa na watu wenye uwezo
tena anaowataka yeye. Mabinti walikuwa wanalia sana lakini
mwisho wa siku wanakubali kuolewa na hao watu wenye
uwezo aliowataka mzazi wao na sio wale waliowapenda wao.
Kati ya mabinti wote takribani wanne walioozeshwa kwa lazima
karibu wote wameshaachana na wale wanaume aidha
wakarudi nyumbani au wakaolewa tena na wanaume wengine.

MTAZAMO WA MZAZI & MTAZAMO WA BIBLIA:

85 | P a g e
Mtazamo wa wazazi wako wanapokataa usiolewe na fukara au
mtu asiye na uwezo au ambae hajasoma sawasawa ni
kukuwekea UHAKIKA, ULINZI, WA MAISHA YAKO (Life
Security), KUTUNZA HESHIMA YA FAMILIA (Family Respect)
i.e. Mtoto wetu kaolewa na jamaa mwenye uwezo flani na
elimu flani, KULINDA UANACHAMA / USHIRIKA WA
KANISA e.i. usiolewe na watu dhehebu flani wao hawajaokoka
sawasawa hivyo hatuchangamani nao, na katika haya yote wala
hakuna cha unampenda au la au hata wajiulize kuna kusudi la
Mungu hapo, au mmejipangaje kuishi.

MTAZAMO WA MUNGU; Ni rahisi na inaeleweka japo watu


wanaichakachua ni hivi; “Mtu” (Msichana) ataachana na
babaye na mamaye ataambatana na mumewe……” hapa
Mungu hakusema mumewe mwenye elimu gani, uwezo gani,
dhehebu gani, n.k. Ninakubaliana na watu wa imani moja na
msimamo mmoja kuoana na ni vizuri na nashauri iwe hivyo
ILA wawe wamependana na kukubaliana wao bila msukumo
wa mtu wa nje.

Watu wakikubaliana wao binafsi na kuambatana bila kuangalia


elimu, uwezo, Familia wanaotoka, Ila wana imani moja ya
kumcha Mungu na wanapendana waoane. Oana na
mwanaume wa ndoto yako na UNAYEMPENDA KWA DHATI
na si mume wa ndoto za wazazi wako au ndugu, jamaa,

86 | P a g e
walezi au marafiki. Na KAMWE usiolewe na elimu, umaarufu,
pesa, nyumba na magari, Olewa na mume umpendaye.
Nyuma ya kupendana na kukubaliana kwa dhati huku mkimcha
Mungu na kuishi kwenye mahusiano yenye USHUHUDA kuna
Baraka za Mungu haijalishi mkoje.

WEWE NDIO HITIMISHO, You are the Final Say/Conclusion.


Mwanzo24:57-58 “Wakasema, na tumwite huyo msichana
tumuulize mwenyewe. Wakamwita Rebeka wakamuuliza, Je!
Utakwenda na mtu huyo? Akasema, NITAKWENDA”

Kibiblia, wewe ndie mwenye maamuzi ya mwisho kuolewa na


unayempenda wao wanapaswa kukushauri na
kukutahadharisha tu na mwisho wa siku wakuulize
UNAOLEWA? Ukisema ‘NDIO’ ni ‘NDIO’, ‘SIO’ ni ‘SIO’.
Mungu Akusaidie.

SWALI CHOCHEZI; Je upo tayari kuolewa na mwanaume


yeyote kisa tu awe na mali au uwezo wa kifedha hata kama
hujampenda? Je upo tayari kuachana na chaguo la moyo wako
na kuolewa na mwanaume ambaye wazazi na kanisa
limekuchagulia??

87 | P a g e
Toka kwa Bro.Elly 24/7; “Ukifahamu kwa kina maana ya
NDOA na yaliyomo ndani ya NDOA, utamuangalia Zaidi
anayekuoa kuliko alichonacho anayekuoa”

88 | P a g e
MISTAKE NO 17;
YOU FORGE TO BE WESTERN GIRL!
(UNALAZIMISHIA UZUNGU)
Wasichana wengi tulionao ni wazuri sana kwenye kuiga
mambo yanayofaa na hata yasiyofaa {Imitation} toka kwa
wanawake wa Magharibi i.e Ulaya na Amerika. Yale mazuri
kama kujituma kusoma na kufanya kazi kwa bidii ni faida
kubwa kwetu tukiiga, LAKINI pia ipo mitindo ya mavazi na
nywele ambayo hayakudhalilishi wala hayaharibu utu wako si
mbaya ukiiga. Ila sasa wanachovaa wengi wa wasichana ni
majanga, aibu na kujidhalilisha kwa maisha ya mwanamke wa
kiafrika. Tukubaliane tu kwamba mazingira yote duniani au
maeneo yote duniani yanaongozwa na namna flani ya
utamaduni, na kwenye hilo eneo ukiishi kulingana na
utamaduni wao hakuna atakaekulaumu wala kukushagaa, ILA
ukienda kinyume na utamaduni wa eneo husika kila mtu ndani
ya eneo hilo atakushangaa, atakulaumu, atakusema na
pengine watakuchukulia hatua ya kinidhamu.
Yapo mambo wanayofanya wasichana wengi siku hizi
yanayotokana na KUIGA NJE ambayo yamewafanya kuonekana
vituko na balaa ndani ya jamii. Na wapo wengine ambao
walizidisha hayo mambo kiasi cha kufundishwa adabu na
heshima kwa kudhalilishwa. Kwa mfano; Nimewahi kuona
baadhi ya wasichana waliovaa mavazi yanayoonyesha sehemu

89 | P a g e
nyeti za miili yao wakikamatwa na kuchaniwa nguo pamoja na
kuchapwa. Mifano hii ni mingi sana, na kumbuka wapo ambao
walitolewa kanisani na kuonywa huku wakipewa kanga
wajisitiri.

HEBU TUKUBALIANE MAMBO YAFUATAYO;


Don’t Imitate Everything {Usiige Kila Kitu}
Haijalishi umekipenda hicho kitu kiasi gani ILA kabla ya kuiga
kilinganishe na utamaduni wako, na wewe kama mkristo
kilinganishe na Neno la Mungu na maadili ya kikristo kisha
upate jibu kama kinafaa kuiga au hakifai AMA Uliza watu
waelewa.

Understand It’s Source and Reason {Elewa Chanzo Chake Na


Sababu Zake} Ipo mitindo ya nguo, viatu, nywele na
kujipamba {make up’s} nyingi tu ambayo vyanzo vyao ni
viashiria flani vinavyohamasisha uovu flani au ambavyo vinakiri
vitu flani ambavyo ni kinyume na Mungu. Kwa mfano kuna
baadhi ya mitindo ya nywele ni viashiria vya watu
wanaompinga Kristo. SO Elewa kila kitu kina chanzo na
sababu USIIGEIGE TU.

Study Environment {Soma Mazingira}, Wasichana wenye akili


nzuri kabla hawajaiga chochote husoma kwanza mazingira na
kuelewa kipi kinafaa wapi na kwanini. Kwa mfano kuna nguo

90 | P a g e
za kuvaa wakati wa kulala hizo hazifai kutembea nazo mtaani,
zipo nguo watu wanavaa nyumbani wakiwa na wapenzi wao
au honeymoon, hizo hazivaliwi barabarani au kanisani.
Wenzetu wanavaa nguo fupi sana wakija Africa ni kwa sababu
wamezoea baridi kali huko kwao na hapa ni joto kali ndio
maana inabidi wavae hizo ili wapunguze joto. Wewe unaona
UNAIGA ili tukuite umeendelea au umekua mzungu.

Crazy Role Models {Kuiga Watu Wasiyo Na Ushuhuda}


Ni ajabu sana lakini hili hasa ndio tatizo kubwa zaidi kwa
wasichana kuiga. Wapo wasichana wanaowapenda
wanamuziki, waigizaji, watangazaji na watu maaarufu flani
flani ndani na nje ya nchi, Na kwa hivyo huwaiga kila kitu
kuanzia namna wanavyoongea, wanavyotembea, wanavyovaa
na walivyoweka nywele, tabia zao n.k Kwa mfano niliwahi
kusikia mwanamziki mmoja akihojiwa akasema hua havai
chupi na ghafla leo ama sikuhizi tunawaona wadada
wanaotembea na hawavai chupi ila nguo ya juu tuu. Ukweli ni
kwamba kuiga hakukubadili wewe kuwa kabila flani, toka kijiji
flani na nchi flani zaidi ya kujidhalilisha tu. Hata ungeiga kiasi
gani wala hutaitwa Rihana wala Ciara au Beyonce au Nikki
Minaji.

SWALI CHOCHEZI; Je huwa unawaza na kufikiri kwa kina


kabla ya kuiga chochote? Je kuna mtu maarufu unaempenda

91 | P a g e
na kumuhusudu na hata kutamani kuwa kama yeye? Kwa nini
na unafaidikaje?
Toka kwa Bro.Elly 24/7; “Vitu vyote na watu wote ambao
dunia imewapa thamani ni wale ambao walikuwa halisi kwenye
mambo yao na hawakuiga toka kwa wengine. Japo walijifunza
kutoka kwa watu wengine bado walibaki halisi na hawakuiga
kutoka kwao. Ukitaka thamani na heshima kuwa halisi na wa
kipekee”

92 | P a g e
MISTAKE NO 18;
YOU BELIEVE IN MORE THAN IMPOSSIBLE
CHANGE.
{UNAAMINI KATIKA BADILIKO LISILOWEZEKANA KABISA}
Wasichana wengi ni wazuri kwenye kulazimishia mambo
wanayoyapenda. Halikadhalika kwenye mahusiano ndio kabisa
wana imani kubwa isiyo na matendo tena katika
lisilowezekana. Labda nitoe mifano mizuri tu ili ikusaidie
kugundua nini maana ya kuamini katika badiliko
lisilowezekana.

MFANO 1; UNA UHUSIANO WA KIMAPENZI NA MUME WA


MTU WA NDOA
“I know He will marry me” hii kauli yakuamini mume wa mtu
anaweza kukuoa labda kama wewe si Mkristo ni wa imani
nyingine, Ila kama ni Mkristo tambua UNAHANGAIKA NA
KUPOTEZA TU MUDA.
Otherwise UTABAKIA KIMADA AMA ATAKUZALISHA TU,
ACHANA NAE.

MFANO 2; UPO KWENYE UHUSIANO NA MVULANA


AMBAYE HAJAOKOKA.
“I believe he will be born again and marry me” tena
unamkumbusha kabisa “USIPOOKOKA HUTANIOA” kama

93 | P a g e
kwenye huo uhusiano kuna KUSUDI LA MUNGU njia itafanyika
LAKINI tofauti na hapo ataigiza ameokoka na kanisani ataenda
na haitoshi atanena kwa kugha ILA akishakupata kwa kuwa
ALIKUOKOKEA na ameshapata alichokitaka utaona rangi zote
za Misri. Tena wengine huwa wanasema ukitaka kunioa
HAMIA KANISANI KWETU ni kweli atahamia ila mwisho wa
siku akitimiza lengo ATARUDI ALIPOTOKA. Na ukumbuke si
jambo jepesi sana kufahamu kama kuna kusudi la Mungu au la
ikiwa tayari umeshaingia kwenye hisia za kimapenzi na
mahusiano.

USHUHUDA: Siku moja nilikwenda kununua nguo mahali


nikakutana na kijana mmoja muuzaji wa nguo, ghafla wakati
tunaendelea kuuziana nguo na kupeana stori moja mbili,
ALIANZA kunielezea namna ambavyo wenzake wengi
walifanikiwa kuwaoa mabinti wa kanisa flani kwa kuigiza
wokovu.
Hii ni kwa sababu sheria ya hilo kanisa ni kwamba
hauruhusiwi kuoa au kuolewa nje ya kanisa hilo, hivyo njia
pekee ni kuwa muumini wa hilo kanisa. Akaniambia wengi wa
marafiki zake walienda hapo wakaokoka, wakaimba na kwaya
na baada ya miezi sita wakaoa TENA akaniambia na sherehe
kanisa ndio lillilogharamikia.
Nikamuuliza baada ya kuoa waliendelea na wokovu na
KANISA? Akaniambia WALA! YESU TUSAIDIE MWENYE

94 | P a g e
KUSOMA NA AELEWE maana INAUMIZA. Hebu PIGA PICHA
YA HATMA YA HIYO NDOA!

MFANO WA 3: UPO KWENYE UHUSIANO NA MLEVI,


MVUTA BANGI AMA MVULANA MWENYE WANAWAKE
WENGI.
“I know he will change”
Hapa ndipo unaweza kuwashangaa wasichana na misemo yao
LOVE is BLINDNESS, kama wanajua hata LOVE maana yake
nini zaidi tu feelings zao zilizopitiliza. Hauwezi kutumbukia
kwenye shimo unaloliona mbeleni halafu useme LOVE IS
BLINDNESS. Sina mengi ILA fahamu ya kwamba;

“Some people will never fit in your life no matter how much
you want them to”

MFANO 4: KULAZIMISHIA PENZI KWA MCHUMBA WA MTU


AU MVULANA ASIYEKUPENDA:
“He must love me one day, I won’t give up”
Hii ndio kabisa hata kama ungemvaliaje na kumtega kiasi
gani, tambua wavulana wasipopenda huwa wanamaanisha
labda kama akudanganye akuchezee kisha akuache, au
umshawishi alale na wewe lakini ni hakika baada ya tukio
atajuta sana na kukulaumu, hatakupenda na atarudi

95 | P a g e
alipopenda. HAKUNA JAMBO LINALOUMIZA NA KUTESA
KAMA KUMPENDA MTU ASIYEKUPENDA. “You better quit
faster”

“If you could love the wrong person that much, imagine how
much you could love the right one”
“We may love the wrong person and cry over the wrong
person, but one thing is for sure. Mistakes help us find the
right person”

SWALI CHOCHEZI; Wewe huwa unalazimishia nini msichana?


Unaamini katika nini katika hayo yaliyosemwa?

Toka kwa Bro.Elly 24/7; “Msichana nisikilize vizuri, maisha ni


jambo la kuwa makini nalo sana. Kamwe usijinunulie matatizo
kwa utu wako mwenyewe. Kila wakati mwamini Mungu kuliko
hisia na fikra zako”

96 | P a g e
MISTAKE 19:
YOU THINK BOOK IS EVERYTHING!!
(UNADHANI KUSOMA NDIO KILA KITU)
*Ili pia ni moja katika makosa makubwa wanayoyafanya
wasichana wengi. Wapo wasichana wanadhani KUSOMA
SANA ndio kila kitu kwenye maisha bila kujua KUSOMA ni
sehemu moja tu ya maisha na MAHUSIANO au KUFANIKIWA
ni sehemu nyingine ya maisha. Na ndio maana wapo
waliosoma sana lakini mpaka leo wana MAISHA DUNI, lakini
pia wapo waliosoma sana lakini bado MAHUSIANO na NDOA
zao zinawatesa si kawaida. Kwenye hili ni vizuri tusaidiane
kwa kina ili usiendelee kufikiri unavyofikiri na mwisho wa siku
ukateseka sana. Wengi wa wasichana wanawaza hivi.

1. NIKISOMA SANA HAKUNA MWANAUME


ATAKAETHUBUTU KUNIDANGANYA:
Kimsingi kama nilivyosema hapo juu hakuna uhusiano kati
ya kusoma kwako na kutodanganywa na wanaume. Ni
kweli kwamba wapo baadhi ya wanaume wanawaogopa
wasichana waliosoma sana ILA pia wapo wanaume ambao
tena wala hata hawajasoma kabisa ila wanajua funguo za
mapenzi, hawa wanathubutu na wanaweza kukudanganya
ukaingia mkenge na mwisho wa siku ukaumizwa na PHD
(Doctorate) au Masters yako.

97 | P a g e
2. NIKISOMA SANA NITAKUWA NA MALI ZANGU NA
HAKUNA MWANAUME ATAKAENITAWALA WALA
KUNIENDESHA:
Dhana nyingi potofu inayowatesa sana wanawake wasomi
wa leo ni hii ya kudhania kwa sababu ya elimu na mali
walizonazo basi hakuna mwanaume anaweza kumtawala
wala kumuendesha hata kama ni mume wake.
Nikukumbushe tu kwamba moja ya hitaji kubwa alilonalo
mwanaume yeyote alilopewa na Mungu ni kutaka
HESHIMA (Respect). Mwanaume ameumbwa kuwa kichwa
cha mwanamke, na hii ni asili ya kiMungu. Na ndio maana
unaweza kumtawala kwa muda ILA siku akikubadilikia
hutaamini kitakachotokea.
Hii ndio sababu kubwa ya familia za wanawake wasomi
wengi kuwa na migogoro ama hata ndoa kuvunjika.
Mungu akusaidie sana hata kama utasoma kwa kiasi gani
utambue nafasi na heshima ya mume wako ndani ya
familia bila kujali ana elimu gani au uwezo wa fedha kiasi
gani.

3. NIKISOMA SANA NITAMPATA MWANAUME YEYOTE


NINAEMTAKA:
Na hii pia ni mojawapo ya ndoto za mchana waotazo
wasichana wengi wasomi. Takwimu zinaonyesha ndoa na

98 | P a g e
mahusiano karibu 80% zina matatizo na migogoro
mikubwa, Na wapo waliokua na ndoto kama yako LAKINI
waliangukia kwa wanaume wasiojielewa na wengine
wanazeeka hawajapata bado wanaume waliowataka.
USIJIDANGANYE.

4. UNAMUHITAJI MUNGU SANA KULIKO ULIVYOWAHI


KUWAZA:
Elimu pekee haiwezi kukupa mafanikio ya kimaisha na
ndio maana wapo watu waliosoma sana na mpaka leo
wana maisha duni ya ajabu.

Elimu haiwezi kukupa mwanaume mwaminifu, furaha na


amani kama unavyotaka, na ndio maana ndoa za wasomi
wengi leo ni majanga.

Elimu haiwezi kukuepusha na presha, kisukari, uoga,


udhaifu, kutojikubali, na kukosa amani na ndio maana
wasomi wengi ni wagonjwa na hawajiamini.
-
“HIVYO NI MUHIMU KUSOMA ILA ELIMU/KUSOMA SIO KILA
KITU”

Unamuhitaji Mungu ambae yeye ndiye kila kitu, unamuhitaji


sana kwenye kila eneo la maisha yako kuanzia elimu, uchumi,

99 | P a g e
afya, mahusiano na chochote kile. UKIMPATA YEYE NA
KUMPOKEA KWA UAMINIFU UMEPATA VYOTE, MPOKEE
LEO, MWITE YEYE ATAITIKA, YU KARIBU SANA KULIKO
UNAVYOFIKIRI.

SWALI CHOCHEZI; Unadhani Elimu yako ndio ufunguo wa


kumfahamu mwanaume mwaminifu au asiye mwaminifu?
Unafikiri kusoma sana ndio kunaweza kubadili uhalisia
kwamba wewe ni mwanamke?

Toka kwa Bro.Elly 24/7; “Kusoma sana ni jambo jema na la


kufaa, ila kamwe usisome ukifikiri unaweza kubadili kanuni na
mtazamo halisi juu ya mfumo wa Ndoa ambao Mungu
mwenyewe aliuumba na kuutangaza tangu mwanzo. Na hivyo
kusoma sana hakumbadilishi Mungu kuwa Mungu wala kanuni
za kiMungu kwenda unavyotaka wewe”.

100 | P a g e
MISTAKE 20:
YOU USE TO GENERALIZE MEN!!
(WANAUME WOTE NI SAWA TU)
Mojawapo ya mambo yanayowaangusha wasichana wengi
kwenye mahusiano ni kitendo cha kudhania kwamba wanaume
wote ni sawa tu. Kiasi kwamba tabia ya mwanaume flani ndio
tabia ya wanaume wote, kwa hiyo kwa sababu wanaume
wengi ni waongo basi wanaume wote si waaminifu. Inaweza
kuwa True but not Truth, na inaweza kuwa Real but not Reality.

Na kinachochosha zaidi ni kauli inayotamkwa sana na


wanawake eti kwamba “WANAUME WOTE NI WATOTO WA
MAMA MMOJA NA BABA MMOJA” kwa maana nyingine
wanafanana. Kwa mfano kama msichana alikutana na mvulana
fulani akamwambia vitu flani kama njia ya kumpata na baadae
hakutimiza na wakaachana ANAJENGA akilini mwake kwamba
mvulana yeyote anaekuja na kusema maneno kama yale au
yanayofanania ni MUONGO PIA. Yapo mazingira mengi na
njia nyingi wanazotumia wavulana/wanaume waongo ndio
hizo hizo hutumiwa na wanaume waaminifu wanaomaanisha
wanachokisema UNAHITAJIKA TU KUWA MAKINI NA
KUTOKUAMINI KWA HARAKA na hasa unamuhitaji sana
Mungu kabla ya maamuzi ya mwisho. Unahitaji ushauri sahihi
kabla ya maamuzi ya mwisho.

101 | P a g e
Lakini pia WASICHANA wengi hudhani kwamba kila mvulana
anaekuonyesha kutaka kukuuliza kitu au kuwa karibu na wewe
eti ni njia ya kukutaka na wengine hii imewatesa sana nafsini,
kiasi cha kudhania labda huyu mvulana anaogopa kumwambia
au si mzima labda, BILA kujua wapo wavulana wanaotaka
urafiki wa kawaida ambao hauna cha kufanya na mapenzi.

Anaweza akatembea na wewe maeneo mazuri na salama


(Outing), mkawa mnasoma pamoja, mnakula pamoja, mnakaa
mnapiga hadithi pamoja, mnaenda fellowship wote na
anakupa hata zawadi kama rafiki wa kawaida tu na si mpenzi.
KAMA UNA TABIA YA KUFIKIRI wanaume wote ni sawa na hizi
ndio njia zao utateseka bure na mwisho wa siku ukiugundua
ukweli utajiona mjinga sana. Kwa mfano hata kwenye
mitandao ya kijamii wapo ambao wakiona “friend request” au
message ya salamu toka kwa mwanaume akilini mwake ghafla
anajua tu huyu mvulana ananitaka, inawezekana ni wengi
wapo hivyo ila sio wote JIFUNZE KUTOKUKARIRI.

KINGINE- UNATAKA MWANAUME ANAEFANANA NA BABA


AU KAKA YAKO
Hii imewatesa wasichana wengi sana, unakuta msichana yupo
kwenye mahusiano ya urafiki, uchumba, au ndani ya ndoa
anataka mvulana wake, au mume wake amfanyie yale ambao
aidha baba yake alikuwa akimfanyia au kaka yake alikuwa

102 | P a g e
anamfanyia au afanyiwe kama baba yake anavyomfanyia mama
yake au kaka yake anavyomfanyia wifi yake. Utasikia “MBONA
DAD WANGU HAFANYAGI HIVYO KWA MAMY?” “MBONA
KAKA YANGU HAMFANYIAGI HIVYO WIFI YANGU?” Sikiliza
hili na likufae

“Sikia, Binti, Utazame, Utege sikio lako, uwasahau watu wako


na nyumba ya baba yako”
Zaburi 45:10

Maana yake ni nini? Si kwamba msiwapigie simu au


usiwatembelee la hasha maana yake ni kwamba achana na
tabia, desturi na mifumo ya nyumbani kwenu aidha ya baba,
mama, kaka, au dada yako badala yake kubaliana na mwenza
wako mkijadiliana kuishi maisha yenu, ni kweli yapo mambo
tunaweza kuiga kwa wazazi na ndugu LAKINI sio lazima na
pia sio yote CHUKUA TAHADHARI MAPEMA.

SWALI CHOCHEZI; Je una mtazamo gani juu ya wanaume na


hasa kwenye mahusiano? Ni mambo gani ungependa
yafanyike kwenye ndoa yako ambayo pia hufanyika nyumbani
kwenu, na yana faida gani?

103 | P a g e
Toka kwa Bro.Elly 24/7; “Si kila unachokifikiri na kukisikia
kuhusu wanaume kinaweza kuwa sahihi kwa kila mwanaume.
Halikadhalika wapo wanaume waaminifu na wanaojielewa tena
wenye hofu ya Mungu japo hawapatikani kirahisi mpaka
umetengeneza mazingira sahihi ya kiMungu kuwapata. Na
ifahamike wazi hautowapata mpaka umeamini kwamba wapo
na ukamuomba Mungu akukutanushe na wa kwako.”

104 | P a g e
MISTAKE 21;
YOU ALWAYS HAVE A PLASTIC FACE!
(U MZURI WA KUIGIZA) (Pretending)

“A real woman avoid drama, she knows her time is precious


and she is not wasting it on unimportant things”

Wasichana walio wengi huwa ni wazuri wa kuigiza na si


wawazi kwenye mambo yao. Wengi huvaa uso wa plastiki
ambao sio uso wao halisi kwenye mambo mengi tu. Wapo
tayari kuutetea uongo hata kwa machozi wakikushawishi
ukubaliane nao ili hali wanajua wazi si kweli. Angalia hii hapa:

“Being truth to yourself is better than being a liar just to


impress everyone”

Kwa Mfano; KWENYE MAHUSIANO; Unaweza kukuta


msichana ana mtu kabisa kwenye mahusiano lakini akaulizwa
akasema “SINA” na hii imekua inazaa utata mwingi sana.
Swali la msingi ni kwanini uingie kwenye mahusiano ambayo
huweza kuyatetea kwa kuyakubali mbele za watu. Ama haupo
kwenye mahusiano na unasema una mtu just sema SINA MTU
NA SIPO TAYARI KUINGIA.

105 | P a g e
“Don’t be in a relationship, if you’re going to act single”

“Being in relationship is a full time job, so don’t apply if


you’re not ready”

Hapa kwenye mahusiano wasichana wanadanganya mno,


‘mara sikuwahi kuwa na mtu wewe ndio mwanaume wangu wa
kwanza’, ‘mara mimi bado ni bikira ili hali anajua hana’, ‘upo
peke yako tu, na kumbe amepanga foleni’ SIKU HIZI MSHIKA
MAWILI, YOTE HUMPONYOKA.

KWENYE WOKOVU; Hapa ndio inauma zaidi maana wengi


wanadhani wanaweza kumdanganya Mungu kumbe
wanajidanganya wao. “Nimeokoka Nampenda Yesu,” Bwana
Yesu Asifiwe; “Shalom” hizi ndio kauli zao wakiwa na
wapendwa ILA sasa wanabadilika na mazingira, hamna kweli
ndani yao. Wanaweza kuomba na kuimba huku machozi
yakiwatoka lakini umbea, fitina, kutopendana wao kwa wao,
wivu mbaya, uongo, uzinzi, ulevi, uzushi na faraka umewajaa
ndani yao. Kumbuka MUNGU HADHIHAKIWI, Upandacho
Ndicho Uvunacho

*MAMBO MENGINE; Msichana anaweza kucheka na kusema


nimekusamehe na akawa bado na kinyongo si cha kawaida,
anaweza kukubali na kufanya jambo kwa shingo upande huku

106 | P a g e
ndani ana maumivu makali anaweza akakwambia “FANYA
UTAKAVYO” ili ndani yake anateseka mno.

“When you say “Yes” to others make sure you are not saying
“NO” to yourself”
Paulo Gelho

“Sometimes it’s easier to pretend that you don’t care, than to


admit its killing you”

TUNAKUVUA SASA USO WA BANDIA KWA KUKUSAIDIA


YAFUATAYO: -
5 Deadly Terms Used by A Woman;
1. FINE; This is the word women use to end an argument
when she knows she is right and you need to shut up
2. NOTHING; means something and you need to be
worried
3. GO AHEAD; this is a dare, not permission, do not do
it
4. WHATEVER; A woman’s way of saying screw you
5. THAT’S OKEY; she is thinking long and hard on how
and when you will pay for your mistakes.

HAYA YOTE NI MATESO YA NAFSI, JIFUNZE KUWA MKWELI


NA MUWAZI

107 | P a g e
BE A WOMAN OF INTEGRITY;
“Integrity is doing the right thing when no one is watching”
Myles Munroe

SWALI CHOCHEZI; Je na wewe unaigiza kwenye mambo


mangapi maishani mwako? Mara ngapi umeumia na kuteseka
mno kwa sababu tu uliigiza upo sawa kumbe kuna jambo
linalokutesa?

Toka kwa Bro.Elly 24/7; “Dadangu mpendwa, ni muhimu sana


kuwa halisi na wazi kwenye maisha yako yote. Hakuna jambo
linalogharimu kama kuigiza maisha na kuficha uhalisia.
Fahamu kwamba Uhalisia na Uwazi Unalipa mno”

MISTAKES HELPFUL QUOTATIONS;


1. “You cannot travel back in time to fix your mistakes but you
can LEARN from them and FORGIVE YOURSELF for not
knowing better”
“Forget what hurt you but never forget what it taught you”
“Don’t carry your mistakes around with you instead place them
under your feet and use them as stepping stones to rise above
them”

108 | P a g e
 Jisamehe wewe binafsi, samehe wengine, sahau
makosa, jifunze kutokana na makosa NA yatumie haya
makosa kwenda kiwango kingine.

2. “Cry as much as you want to, but just make sure when your
finished you never cry for the same reason again”
“Nothing wrong with apologizing but saying
“I’M SORRY” does NOTHING when you continue to
make the same mistakes”
“You can NEVER MAKE SAME MISTAKES TWICE….
Because the second time its not a mistake…...its a
CHOICE”

 Kamwe usirudie kosa, daima kufanya kosa si kosa bali


kurudia kosa, na unaporudia kosa inakuwa umechagua
kurudia kosa.

3. “I may have been broken……but I’m still beautiful”


“May be its not always about trying to fix something
broken. May be its about starting over and creating
something better”
“Forgive others, not because they deserve forgiveness,
but because you deserve peace”
 Na anza upya kwa bidii zote.

109 | P a g e
110 | P a g e

You might also like