You are on page 1of 54

Harakati za kukandamiza fikra huru Vyuo Vikuu nchini1

1 Taarifa katika picha ni jeshi la polisi wakitumia nguvu dhidi ya wanafunzi wa Chuo Kikuucha Dar es
salaam waliokuwa wakiandamana kuelekea Ikulu ili kumuomba Mh Raisi, Jakaya Mrisho Kikwete na
serikali yake iwadhamini wanafunzi wa mwaka wa kwanza walionyimwa mikopo, Mnamo tarehe 11 no-
vemba 2011, eneo la geti maji jijini Dar es Salaam, Tanzania

Sauti za watetezi wa haki vyuoni i


VIFUPISHO

UDSM University of Dar es Salaam


UDOM University of Dodoma
CBE College of Business Education
MUHAS Muhimbili University Health and allied Science
MUHASSO Muhimbili University of Health and Allied Science
Students Organization
HELSB Higher Education Loarn Students Board
TCU Tanzania Commission of Universities
MNMA Mwalimu Nyerere Memorial Academy
MUCHS Muhimbili University college of Health Science
MSTHE Ministry of Science, Technology and Higher Education
IFM Institute of Finance Management
TIA Tanzania Institute of Accountant
SUA Sokoine University of Agriculture
DARUSO Dar es Salaam University Students Organization
DUSO Dar es Salaam Union Students Organization
TAHLISO Tanzania Higher Learning Institute Students Organization
TYL TANU Youth League
THRDC Tanzania Human Right Defenders Coalition
UVCCM Umoja wa Vijana Chama Cha Mapinduzi
CDM CHADEMA-Chama Cha Demokrasia na Maendeleo.
CCM Chama Cha Mapinduzi
CUF Civic United Front
TANU Tanganyika National Union
GN Government Notes

ii Sauti za watetezi wa haki vyuoni


YALIYOMO

Shukrani zangu 9
Historia ya Mwandishi 10
Malengo ya Kitabu 11

Sura ya Kwanza 13

Historia ya ukiukwaji wa haki za Watetezi Vyuoni 13


Utangulizi 13
Historia ya timua timua watetezi vyuoni 13
Historia ya Timua Timua Chuo Kikuu cha Dar es Salaam 1960s 1970s 14
1.2 Historia ya Timua Timua 1970s 1980s 16
1.3 Historia ya Timua Timua 1980s 1990s 16
1.4 Historia ya Timua Timua 1990s 2000s 17
1.5 Historia ya Timua Timua 2000s 2010 18
1.6 Historia ya Timua Timua Vyuo Vikuu Nchini 2011 2017 21
Hitimisho 23

Sura ya Pili 24

2.0 Vyanzo vya Kufukuzwa Watetezi wa haki za binadamu Vyuoni 24


2.1 Sababu Mbalimbali Zinazowafanya Wanavyuo Wagome 24
2.1.1 Matatizo ya Mikopo na Usiri wa Vigezo vya Ugawaji wa
Mikopo wa Bodi ya Mikopo Tanzania 24
2.1.2 Sera Mbovu za Elimu Nchini 25
2.1.3 Huduma Mbovu za Kijamii Katika Eneo la Chuo 26
2.1.4 Watetezi wa Wanafunzi Kusimamishwa Masomo,
Kufukuzwa Chuo au Kuwekwa Kizuizini 26

Sauti za watetezi wa haki vyuoni iii


2.1.5 Watawala Kutumia Mabavu na Kujenga Mazingira ya
Uhasama/Uadui Dhidi ya Wanavyuo 26
2.1.6 Wanavyuo Kupinga Madhaifu ya Sheria zinazoathiri Ustawi wa
Vyuo Vikuu Nchini. 26
2.1.7 Kukosekana kwa Mafunzo ya Vitendo na Vifaa vya Kujifunzia 27
2.1.8 Serikali Kuingilia Jumuiya na Serikali za Wanafunzi Vyuoni 27
2.2 Sababu zitolewazo na Watawala dhidi ya Watetezi Vyuoni 29
2.3 Hitimisho 29

Sura ya tatu 30

3.0 Matukio ya Ukiukwaji wa haki za Watetezi Vyuo Vikuu nchini 30


3.1Mtetezi wa Haki za Binadamu ni Nani? 30
3.2 Matukio ya Utetezi wa haki za binadamu Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam(UDSM) 31
3.3 Watetezi wa haki za Binadamu Chuo Kikuu Dododma (UDOM) 32
3.4 Matukio ya Ukiukwaji wa haki za Watetezi Chuo Kikuu cha
MUHIMBILI MUHAS 34
3.5 Taarifa za Picha za matukio ya Utetezi kutoka Vyuoni 35
3.6 Hitimisho 37

Sura ya nne 38

4.0 Mazingira na Mienendo ya Kesi za Watetezi Katika Mahakama 38


4.1 Utangulizi 38
4.2 Watetezi wa haki za Binadamu hutishiwa maisha 38
4.3 Njia Wanazozipitia Watetezi wanaporudishwa Vyuoni 40
4.4 Maisha ya Watetezi Baada ya Kurudishwa Vyuo 41
4.5 Changamoto ambazo hujitokeza baada ya Watetezi kufukuzwa Vyuoni. 42
4.6 Mienendo ya Kesi za Watetezi Mahakamani 42
4.9 Hitimisho: 43

iv Sauti za watetezi wa haki vyuoni


Sura ya tano 44
5.0 Madhara ya timua timua Watetezi Vyuo Vikuu nchini 44
5.1 Utangulizi: 44
5.I Hitimisho: 47

Sura ya Sita 48

6.0 Mapendekezo na wito 48


6.1 Utangulizi: 48
6.2 Hitimisho: 49
6.3 Wito 49
6.3.1 Utangulizi: 49
6.3.2 Asasi za Kiraia 49
6.3.3 Msaada wa Asasi Tanzania Human Righ Defender Coalition-THRDC. 50
6.3.4 Wito kwa watetezi wa haki za binadamu juu ya usalama wetu: 51
6.9 Hitimisho. 51

Sura ya Saba 52

7.0 Matokeo ya harakati za watetezi Vyuoni. 52


7.1 Utangulizi 52
7.2 Mtetezi Alphonce Lusoko akifukuzwa kwa mara ya pili UDSM 2017. 53
9.5 Hitimisho. 55

Sauti za watetezi wa haki vyuoni v


SHUKRANI ZANGU
Jitihada za matayarisho ya kitabu hiki zimechukua muda na juhudi kubwa kutoka
kwa wadau mbali mbali, asasi zisizo za kiserikali, wanafunzi wenzangu na wahadhiri
mbalimbali ili kusudi kiweze kukidhi mahitaji ya watumiaji hasa vijana ambao
wanaweza kukitumia kitabu hiki mahala popote pale nchini, ili tu kusaidiana katika
kulikomboa Taifa letu kifikra. Lakini pia kwa dhati ya moyo wangu napenda kutoa
shukrani zangu kwa asasi ya Tanzania Human Rights Defenders Coalition (THRDC)
kupitia kwa Mratibu mkuu wa taasisi hiyo Mh. Onesmo Olengurumwa kwa kujitoa kwa
dhati kushauri,kuhariri na kusaidia upatikanaji wa kitabu hiki.

Kwa namna ya pekee nawashukuru mawakili waliojitolea kuwatetea watetezi wa


haki za binadamu kutoka Kituo cha Sheria na haki za binadamu-LHRC, Chama cha
Wanasheria-TLS. Lakini vile vile nawashukuru viongozi mbalimbali wa kidini na wa
kisiasa ambao kwa namna moja au nyingine wamewagusa watetezi waliopatwa na
madhara ya utetezi vyuoni.

Kwa kutambua umuhimu wa washiriki katika uandaaji wa kitabu hiki, ningependa


kutoa shukrani zangu za dhati kwa Mwenyezi Mungu, wazazi wangu, Baba-Alphonce
Mwamwile na mama-Joyce Mwamwile, kwa kunilea katika maadili ya kupigania haki
za wanyonge, pia kwa wahadhiri wangu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam hususani
Dr. Azavery Rwaitama, Dr. Kitila Mkumbo, Mzee Matiko Matale ambaye pia ni mhanga
wa timua timua ndani ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam UDSM2. Wahadhiri hawa
wamekuwa na mchango chanya kuhakikisha kitabu hiki kinafanikiwa kuchapishwa ili
kuibua mambo wanayofanyiwa watetezi wa haki za binadamu katika vyuo vikuu nchini.

Kwa namna ya pekee, shukrani pia ziwaendee watu wote walioshiriki katika kuandika
na kushauri wakiwemo watetezi wenzangu wafuatao: Evarist Ambrose, Francis
Ndunguru, Elius Mwambapa, Wilfred Rolland, Bob Wangwe, Hellen Mushi, Hatari
Chacha, Mabirika Mawazo, Monance Baraka, Gervas Shayo, Godbless Charles,
Charles Jackson, Laizer Yonas, lema Tumsifu, Kalabamu Joseph. Wengine ni Ado
Joseph, Joel Ntile. Raymomd Abuya, Bashari Shonza, Daniel Mswelo, Michael Legan.
Pia wamo Daiel Naftal, Garubindi Gaston Odillon na wengine wengi ambao wote
ninathamini mchango wao maridhawa.

Ni matumaini yangu kuwa, kitabu hiki kitakuwa na manufaa makubwa kwa watumiaji
na kitawezesha jamii ya Kitanzania na wadau wa mbalimbali kupata zana muhimu ya
kutambua umuhimu wa watetezi wa haki za binadamu; lakini vile vile, wanafunzi wa
vyuo vikuu watapata ari mpya na hamasa ya kuendelea kutetea haki zao na za taifa
kwa ujumla wake, kwa kufuata hatua halali za kisheria.

2 UDSM-university of Dar es Salaam

vi Sauti za watetezi wa haki vyuoni


Historia fupi
ya Mwandishi

Alphonce Lusako M. Alias Emekha Ikhe, ni kijana aliyezaliwa katika kijiji cha Ipagika,
Tukuyu, Mkoani Mbeya nchini Tanzania mnamo tarehe25-11-1988, na alijiunga na
Shule ya Msingi Manga na baadaye akiwa darasa la nne kuhamia shule ya Msingi
Mapambano mkoani Mbeya kati ya mwaka 1996-2002. Alisoma katika Shule ya
Sekondari ya Samora Machel kuanzia mwaka 2003-2006 hukohuko mkoani Mbeya;
na hatimaye kidato cha tano na sita alisomea katika shule ya sekondari Sangu High
School kuanzia mwaka 2007-2009.

Baada ya hapo alijiunga na Chuo Kikuu cha Taifa University of Dar es Salaam 2009
ambako alifukuzwa chuo kwa sababu ya harakati zake za utetezi wa wanyonge.
Mnamo tarehe 14/11/2011 akiwa mwaka wa tatu alifukuzwa Chuo Kikuu cha Dar
es Salaam kwa tuhuma za kuratibu maandamano tarehe 11/11/2011 ya kuwatetea
wanafunzi wa mwaka wa kwanza ambao hawakudhaminiwa mikopo nchini.

Mwaka 2013 alichaguliwa kuwa Mkurugenzi na Katibu Mkuu wa Mtandao wa


Wanafunzi Tanzania uitwao TSNP3. Mwaka huo huo aliratibu Chama cha Wanafunzi
Watetezi waliofukuzwa vyuo vikuu nchini (UEUST4) ambacho kilifanikisha kuwarudisha
wanafunzi wengi waliofukuzwa katika Chuo kikuu cha Dodoma (UDOM) mwaka 2011.
Baada ya njia zote za kidiplomasia kushindikana kurudishwa kwake Chuoni, aliamua
kuitafuta haki yake ya elimu mahakamani lakini baada miaka mitano(5), aliamua
kuitoa kesi yake Mahakama ya Rufaa Tanzania na kumuandikia Mh. Rais John Pombe
Makufuli aingilie kati kufutwa kwake katika mfumo wa Elimu nchini, Wasaidizi wa Raisi
Ikulu katika mambo ya Elimu na Sheria, majina yamehifadhiwa walishirikiana nae na

3 TSNP-Tanzania Students Networking Program


4 UEUST: Union of Expelled University Students

Sauti za watetezi wa haki vyuoni vii


kuwasiliana na Tume ya Vyuo vikuu (TCU) na kupewa ruhusa ya kusoma tena kwa
mujibu wa Sheria, Alidahiliwa tena kusoma Shahada ya Sheria katika Chuo kile kile
(UDSM), Mnamo tarehe 30.01.2017 akiwa katika ratiba yake ya mitihani alifukuzwa
tena bila sababu yoyote ya Msingi. Lusako aliamua kupeleka malalamiko katika
Mtandao wa kutetea haki za Watetezi wa haki za Binadamu Tanzania(THRDC5) ili
asaidiwe msaada wa kisheria na namna atavyopata haki yake ya Elimu kwa wakati
aliyoitafuta takribani miaka sita sasa (2011-2017). Mtandao huu umeshaanza hatua
za awali za utetezi kisheria.

Malengo ya kitabu
Malengo ya kitabu hiki ni kuibua ukiukwaji mkubwa wa haki za watetezi wa haki za
binadamu uliotokea, unaotokea na unaoendelea kutokea ndani ya vyuo vikuu nchini,
ambapo kama taifa tukiendelea kufumbia macho suala hili, ni hatari kwa ustawi wa
amani ya nchi yetu. Hivyo kitabu hiki kina lengo la kuibua ukiukwaji husika ili jamii ya
Kitanzania wakiwemo viongozi tuliowapa dhamana, AZAKI (Asasi za Kiraia) na jamii
kwa ujumla wake, waweze kutambua ukiukwaji husika na kuchukua hatua stahiki ili
kuleta maendeleo endelevu nchini.

Lengo jingine ni kuamsha ari na hamasa ya wanavyuo katika kutetea haki zao na za taifa
kwa ujumla wake, bila kutetereka kwa njia halali za kisheria, ikiwemo maandamano na
migomo ya amani katika kushinikiza upatikanaji wa haki.

5 THRDC-Tanzania Human Right Defenders Coalition

viii Sauti za watetezi wa haki vyuoni


USULI
Kitabu hiki kinahusu harakati mbalimbali zilizofanywa na Watetezi wa haki za binadamu
Vyuo Vikuu Tanzania. Ni kitabu kinachokupa mwangaza kuhusu historia ya migomo ya
wanafunzi katika vyuo vikuu nchini. Kitabu hiki kimechambua sababu za utokeaji wa
migomo hiyo, na pia kinatoa mapendekezo ya namna ya kuizuia migomo hiyo vyuoni.

Lakini kwa upande mwingine, kupitia katika kitabu hiki, tunaoneshwa harakati za
kukandamiza uhuru wa kujieleza na kutoa maoni vyuoni. Hizi ni harakati zinazofanywa
na vyombo vya dola kwa kupitia viongozi wa Vyuo Vikuu nchini .

Katika kitabu hiki, tutagusia kidogo historia ya migogoro ya wanafunzi wa vyuo vikuu
ambao wamekwishawahi kusiamishwa na kufukuzwa kwa kuwa watetezi wa haki
za binadamu vyuoni.Yapo majina ya viongozi mashuhuri ambao walisimamishwa au
walifukuzwa kutokana na migogoro hiyo vyuoni, mathalani Mh. Samweli Sita, Mh.
Wilfred Mwabulambo, Mh. Chacha Zakayo Wangwe, Mh. John Mnyika, Mh. Zitto
Zuberi Kabwe, Mh. James Mbatia, Mh. Julius Mtatiro, Mh. David Silinde na Wengine
wengi ambao tunatambua na kuthamini harakati zao.

Mwandiahi wa kitabu hiki ametambua kuwa watetezi wa haki za binadamu vyuoni


wamekuwa wakikumbana na aina mbali mbali za mateso, ikiwemo; unyanyasaji,
kuharibiwa sifa kwa kushutumiwa na kusingiziwa6, kutukanwa, kubezwa, kusimamishwa
masomo kwa muda, kufukuzwa vyuoni, kufutwa katika mfumo wa elimu ya umma ndani
ya nchi, kunyimwa uhuru wa kutembea, miungano yao kupata ugumu wa kutambulika
kisheria na wakati mwingine wanaweza kupoteza maisha au kutekwa nyara.

Pia kitabu hiki kimeeleza kwa undani jinsi watetezi wa haki za binadamu wa vyuo
vikuu nchini wanavyodhulumiwa haki zao za kikatiba, wanavyokosa utetezi katika
jamii kutokana na taarifa potofu zinazotolewa na watawala wa vyuo vikuu wakati
wanawafukuza vyuoni na kutokulindwa na vyombo vya dola, kwani bado serikali
yetu imekuwa na dhana potofu dhidi ya watetezi wa haki za binadamu.Hivyo hutumia
vyombo vya dola kuwakamata na kuwapiga ili kukomesha harakati za utetezi ndani
ya vyuo vikuu nchini.

6 Gazeti la Mwananchi, TANGAZO ukurasa 14. Taarifa kwa vyombo vya habari kuhusu kufukuzwa kwa
Wanafunzi wachache Vinara wa uhalifu katika Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, kama ilivyosomwa na
Profesa Yunus D. Mgaya, Naibu Makamu Mkuu Chuo-Utawala

Sauti za watetezi wa haki vyuoni ix


Sura ya Kwanza

Historia ya ukiukwaji wa haki za


Watetezi Vyuoni
Utangulizi

Historia ya timua timua watetezi vyuoni


Kumekuwapo na historia ya kutimua watetezi katika vyuo vikuu mbalimbali hapa
nchini. Tutapitia historia hiyo katika vipindi mbalimbali, kuanzia miaka 1960s hadi
sasa kama tutakavyoonesha kwenye dondoo hapa chini.

- Historia ya timua timua vyuo vikuu nchini 1960s 1970s.


- Historia ya timua timua vyuo vikuu nchini 1970s 1980s
- Historia ya timua timua vyuo vikuu nchini 1980s 1990s
- Historia ya timua timua vyuo vikuu nchini 1990s 2000s
- Historia ya timua timua vyuo vikuu nchini 2000s Sasa

Sauti za watetezi wa haki vyuoni 1


Kumekuwa na tuhuma mbali mbali dhidi ya watetezi wa haki za binadamu
wanaosimamishwa au wanaofukuzwa vyuo vikuu au wanaofutwa katika mfumo wa
Elimu nchini kutumiwa na wanasiasa wa vyama vya upinzani. Hoja hii dhaifu itajibiwa
na historia ya timua timua vyuo vikuu nchini kwani ni dhahiri kuwa, matukio ya timua
timua watetezi wa haki za binadamu vyuoni yameanza tangu wakati wa utawala wa
chama kimoja 1960s 1990s na vile vile yameendelea hata baada ya mfumo wa
vyama vingi vya siasa nchini Tanzania, yaani kuanzia miaka ya 1990s. hivyo dhana
ya kuwa wanafunzi hugoma kwa shinikizo la vyama pinzani haina mashiko kama
ilivyodokezea hapo juu na ni hoja hafifu.

Historia hii ya timua timua imechambuliwa kwa kina katika Ripoti ya Tume ya
Uchunguzi wa Migogoro ya Wanafunzi Vyuo Vikuu Tanzania iliyoongozwa na Dr. Hawa
Sinare ya mwaka 2004.

Historia ya timua timua Chuo Kikuu cha Dar es Salaam 1960s 1970s
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (kifupisho chake UDSM kutoka Kiingereza University
of Dar es Salaam) ni Chuo Kikuu cha kwanza nchini Tanzania kilichoanzishwa mwaka
1961 baada ya uhuru wa Tanganyika, kama Chuo Kikuu Kishiriki cha Afrika Mashariki.
Kiko katika jiji la Dar es Salaam. Kilianza kuwa Chuo Kikuu mwaka wa 1970 baada ya
kutengwa kwa Chuo Kikuu cha Afrika Mashariki katika vyuo vikuu vitatu: Chuo Kikuu
cha Makerere, Uganda na Chuo Kikuu cha Nairobi, Kenya. Kwa ujumla, chuo hiki ni
chuo kikongwe chenye hadhi ya kitaifa na kimataifa ambacho kina historia kubwa
katika harakati za ukombozi wa kifikra; na mazao ya chuo hiki hayapo ndani ya nchi
tu bali yapo hata nje ya nchi katika tasnia mbali mbali.

Mnamo tarehe 22 oktoba 1966, wakati huo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kikiwa ni
Chuo Kikuu kishiriki cha Afrika Mashariki. Mh. Samweli sita akiwa kiongozi wa Serikali
ya Wanafunzi UDSM na Wanafunzi wengine waliamua kugoma na kuandamana
kupinga ulazima wa wao kujiunga na Jeshi la kujenga Taifa (JKT) na kukatwa
mishahara yao baada ya JKT. Walihoji kwanini vigogo wa Serikali na wanasiasa
wanalipwa mishahara minono na marupurupu makubwa?. Baada ya shinikizo hilo la
Wanafunzi, Mwl. Julius Kambarage Nyerere aliamua kupunguza mshahara wake wa
Tsh. 4000 bila kodi na akaagiza mishahara ya mawaziri ipunguzwe kwa asilimia mbili.
Miezi miwili baadae, Mwalimu akatangaza Azimio la Arusha (Februari 5, 1967) kuyapa
uzito malalamiko ya wanafunzi hao.

Watetezi wawili waliotolewa kafara ni Mh. Samweli Sitta na Mh. Wilfred Mwabulambo
kwa sababu walitoa maneno makali kwa Mwl. J.K.Nyerere kwamba ni heri wakati
wa Ukoloni kuliko utawala wa Mwalimu.

2 Sauti za watetezi wa haki vyuoni


Pichani kushoto ni Mh. Samweli Sita, pichani katikati upande wa kulia ni Mh. Wilfred
Mwabulambo na kulia ni Mh. Jaji Joseph Sinde Wariba, Watetezi wa Wanafunzi katika
awamu ya 1960-1970. Kwa sasa Mh. Samwel Sitta na Wilfred Mwabulambo ni Marehemu.

Mh. Samweli Sitta amesomea Shahada yake ya Sheria kwa takribani miaka saba
(7) tangu kufukuzwa kwake mwaka 1966 na ameshika nyazifa mbali mbali serikalini
ikiwemo kuwa Spika wa Jamhurui ya Muungano wa Tanzania.

Mh. Wilfred Mwabulambo na Mh. Jaji, Joseph Wariba ni watetezi walioingia katika
historia ya kuchapwa viboko baada ya mgomo wa Wanafunzi Chuo Kikuu cha Dar
es Salaam(UDSM) wa kupinga tamko la walowezi-Waingereza la mwaka 1965 la
kujitangazia uhuru Unilateral Decleration of independence wa kuongoza Rhodesia
ya Kusini(Zimbabwe). Mgomo huo uliongozwa na Mh. Jaji Joseph Warioba, Wilfred
Mwabulambo na wanafunzi wengine ambapo walitapakaa mtaani na kuvamia Ubalozi
wa Uingereza na kufanya Vurugu kubwa kuonyesha hasira zao. Mwl. J.K. Nyerere
aliwaita Ikulu na kuwaomba waombe radhi ubalozi wa Uingereza kwa niaba yake,
lakini wao walikataa. Mwalimu akaamuru wachapwe viboko7. Ndugu Wilfred amewahi
kushika nafasi mbali mbali za kiserikali ikiwepo Ukatibu Mkuu kiongozi Ikulu.

Mh. Jaji Joseph Sinde Warioba ambaye ambaye kashika nafasi mbali serikalini, kwa
mwaka 2014 alikuwa ni Mwenyekiti wa Tume ya Kukusanya na Kuratibu Maoni ya
Katiba Mpya Tanzania, na ameshawahi kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Waziri
Mkuu na Makamu wa Rais serikalini.

7 Simulizi hii ilitolewa na kuandikwa na Jaji Joseph Sinde Warioba kuhusu vuguvugu la wanafunzi nchini
kuupinga utawala wa kimabavu nchini Rhodesia ya Kusini (Sasa Zimbabwe). Maprofesa Omary na Mihyo
wanaongezea kwamba Mwalimu na Serikali yake walisukumwa kuwadhibiti wanafunzi kutokana na hali
halisi ya wakati husika. Wanayasema hayo kwenye kitabu chao kinachoitwa The Roots of Students Unrest
in African Universities (Tafsiri ni yetu):

Sauti za watetezi wa haki vyuoni 3


1.2 Historia ya timua timua 1970s 1980s
Mnamo tarehe 23 julai 1971, wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam walifanya
mgomo wa kutoingia madarasani ulioongozwa na Rais wa serikali ya wanafunzi
(DUSO8), ndugu Akivaga, ambaye aliwaongoza wanafunzi kupinga matumizi ya
Kiswahili wakati wa sherehe za kumaliza chuo graduation, lakini vile vile kupinga
uteuzi wa Kada wa Chama Tawala kuwa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam. Baada ya mgomo husika Rais wa DUSO alisimamishwa chuo na baadae
kurudishwa kuendelea na masomo9.

Mnamo Machi 1978, wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam walifanya mgomo
mkubwa wa kupinga nyongeza za posho kwa mawaziri, wabunge na maafisa wa
serikali. Watawala waliamua kuwasimamisha watetezi na wanafunzi wote waliogoma
kwa muda wa miezi tisa na kuwaacha wanafunzi wasiogoma kuendelea na masomo.
Lakini pia ikumbukwe kuwa kwa mara ya kwanza, watawala wa chuo hiki waliamua
kufuta serikali ya wanafunzi DUSO na ikawekwa chini ya uangalizi wa Kamati ya
Umoja wa vijana wa TANU ujulikanao kama TANU Youth League

1.3 Historia ya timua timua 1980s 1990s


Pamoja na ukweli kwamba kulikuwa na migombo mbali mbali katika awamu hii, Mnamo
mwaka 1985na 1986 ambapo wanafunzi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam waliamua
kufanya migomo ya kutoingia madarasani kwa sababu ya mahitaji ya vitabu vipya,
kudai posho za steshenari. Gharama kubwa ya chakula, huduma mbaya na mazingira
machafu ya Kafteria. Lakini mwaka1989, wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
walifanya mgomo mkubwa wa kutoingia madarasani uliosababishwa na wanafunzi
watetezi kuwekwa kizuizini na Jeshi la Polisi wakiwa wametoka Pyongyang Korea.

watetezi hawa walioenda korea waliongozwa na Bwana Pascal Mabiti, na sababu


ya kuwekwa kizuizini ilikuwa ya kupinga kitendo kilichofanywa na serikali ya Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania ya kuwapeleka vijana wa Umoja wa Vijana wa Chama
Cha Mapinduzi katika tamasha la wanafunzi wa vyuo vikuu, wanaotoka katika nchi
za kijamaa. Wanafunzi hawa walikataa kutoa hotuba kwa sababu nchi za wengine
zilikuja na wawakilishi wa wanafunzi wa vyuo vikuu na sio uwakilishi wa chama cha
siasa. Kamati ya baraza la chuo chini ya Prof. Godfrey Mmari, aliyekuwa Makamu
Mkuu wa UDSM wakagundua kuwa wanafunzi walioshikiliwa walishikiliwa kimakosa
na wakaiomba serikali iwaachilie watetezi husika. Baada ya maombi hayo watetezi
waliachiwa huru na mgomo ukatulia10.

8 DUSO-Dar es Salaam University Sutents Organisation.


9 The report of the probe team on students crises in higher education institutions in Tanzaniam May 2004
iliyoongozwa na Dr. Hawa Sinare.
10 The report of the probe team on students crises in higher education institutions in Tanzaniam May 2004

4 Sauti za watetezi wa haki vyuoni


1.4 Historia ya timua timua 1990s 2000s
Tangu Mnamo tarehe 12 Mei 1990 watetezi wa Wanafunzi Chuo Kikuu Cha Dar es
Salaam walianzisha rasmi harakati za kupinga Sera ya Uchangiaji Elimu ya juu (Cost
Sharing policy) kwa hoja hafifu kwamba Serikali haina rasilimali fedha hivyo muhimu
Wazazi waanze kuchangia, walipogoma Chuo kilifungwa kwa muda wa miezi 8.
Ilipofika Mwaka 1992 wanafunzi wa walifanya mgomo mzito tena wa kupinga sera ya
kuchangia gharama za elimu ya juu. Mgomo huu uliongozwa na Mh. James Mbatia,
Mh. Matiko Matale na wengineo baada ya kuona madhara ya sera husika iliyoasisi
matabaka baina ya walionacho na wasionacho. Katika mgomo huo Mh. James Mbatia
hakubahatika kurudishwa kumalizia shahada yake ya Uinjinia na akaenda kusoma nje
ya nchi, vile vile ndugu Matiko Matale ambaye mapaka leo kumbukumbu zinaonyesha
kutorudishwa masomoni.

Mh. James Mbatia Mh. Chacha Zakayo Wangwe

Pichani kushoto ni Mh. James Mbatia ambaye miaka 1990s yeye na wenzake mathalani
Anton Kom na wengine walifukuzwa UDSM kwa kupinga sera ya kuwashirikisha wazazi
kuchangia elimu ya juu.Amekuwa Mbunge wa kuteuliwa 2010-2015 na Mbunge wa
Kuchaguliwa 2015-2020 katika Bunge la Jamhuri ya Muungano na Ni Mwenyekiti wa
Chama Cha NCCR. lakini vile vile alikuwa ni Mbunge wa Kuteuliwa mwaka 2010 2015,
hakufanikisha kumalizia shahada yake ya uinjinia katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,
UDSM. Alienda nje ya nchi baada ya nchi.

iliyoongozwa na Dr. Hawa Sinare.

Sauti za watetezi wa haki vyuoni 5


Pichani, Kulia ni Chacha Zakayo Wangwe Mtetezi wa wanafunzi ambaye alifukuzwa
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na historia inatuambua kwamba ni mmoja wa watetezi
waliokumbwa na mkasa wa kutorudisha kabisa Chuoni. Mwaka 1979 alipata cheti
cha ualimu na masomo yake ya shahada ya kwanza yalisitishwa ndani ya Chuo Kikuu
cha Dar es salaam, na hivyo akaenda kuishi Kenya kwa muda fulani. Kwa sasa ni
marehemu na Mungu airehemu roho yake. Aliwahi kuwa Mbunge wa Tarime kupitia
Chama cha Demokrasia na Maendeleo; na mauti yamemkuta akiwa mwanachama
hai wa CHADEMA. Lakini cha kusikitisha ni kwamba, mpaka mauti yanamkumba
hakuwahi kurudishwa chuo ili kumalizia shahada yake.

Pamoja na ukweli kwamba historia inatukumbusha kwamba mwaka 1994, 1995 ya


kucheleweshwa kwa malipo ya posho za vitabu.kuongezewa fedha ili kukidhi mahitaji
yao, kupunguza bei za vyakula lakini hakuna mtetezi aliyeripotiwa kusimamishwa au
kufukuzwa Vyuoni Upande wa UDSM na SUA ambako vuguvugu la mgomo lilifanyika.

1.5 Historia ya timua timua 2000s 2010


Katika awamu ya kuanzia mwaka 2000 hadi 2010, kumekuwepo na migomo mbali
mbali iliyoongozwa na Watetezi wa Wanafunzi. Madai makubwa yakilenga kuongezewa
fedha za kujikimu. mahitaji ya vifaa vya kusomea kama kikokotoleo (calculator), Mfano
Mwaka 2002, Mtetezi ndugu, Mkili alishikiliwa na jeshi la Polisi baada ya maandamano
ya kuomba kuongezewa fedha za kujikimu kutoka Tsh.1500 hadi Tsh.3000. Baada ya
Wanafunzi kufanya maandamano makubwa ya Kumtaka mtetezi wao, Jeshi la polisi
lilimuachia ndugu Mkili na kumsimamisha takribani miezi 8 masomoni.

Mwaka 2004, Mh. John Mnyika alikuwa ni mtetezi


pekee aliyetolewa mbuzi wa kafara kwa

kutetea haki za wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar


es Salaam, na mpaka sasa inasadikikika

bado hajamaliza digrii yake katika Chuo Kikuu


cha Dar es Salaam. Wakati huo alikuwa akisomea
Shahada ya Utawala (Bachelor of Adminstration)
na amewahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Ubungo;
na kwa sasa ni Mbunge wa Jimbo la Kibamba
lililopo jijini Dar es Salaam, kwa tiketi ya Chama
Mh. John Mnyika cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA.

6 Sauti za watetezi wa haki vyuoni


Mnamo mwaka 2007 na 2008, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kulikuwa na migomo
mikubwa sana. Mgomo wa mwaka 2007, uliongozwa na Mtetezi, Julius Mtatiro na Bwana
George Bush wakiwa wanadai mikopo ya wanafunzi. Lakini pia historia inatukumbusha
kuwa, mgomo wa wana-UDSM wa mwaka 2008 uliosababishwa sana na shida ya maji
katika kampasi kuu (MAIN CAMPUS), huku wanafunzi waliokuwa wanaishi kampasi
ya Mabibo wakichekelea huduma ya maji. Ndipo watetezi wakaanza kuhamasishana
Wanafunzi na kutengeneza msafara ulioelekea katika makazi ya Makamu Mkuu wa
Chuo Profesa Rwekaza Mukandala, wanafunzi wakavunja geti la nyumba ya Makamu
Mkuu wa Chuo - VC na kufanya vurugu kadhaa. Katika mgomo huu kulikuwa na
watetezi maarufu kama vile: Steven Owawa, Odong Odwar ambaye ni Mganda. Lakini
baada ya mgomo huu matenki ya maji yaliwekwa Hall II na Lifti ya Hall II iliwekwa11 pia.
Mtetezi Odong Odwar alifukuzwa Chuo na Kurudishwa nchini kwake Uganda, Watetezi
wengine walirudishwa baada ya hatua mbalimbali za kidiplomasia kufanyika.

Hawa ni wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Kampasi ya Mlimani wakiwa nje
na mizigo yao, wakiwa hawajui waelekee wapi baada ya chuo hicho kufungwa ghafla
mwaka 2008.

11 Waraka wa Wanafunzi wa Elimu ya juu kwa Serikali kuhusu migomo na maandamano ya mara kwa mara
vyuoni.
Ulioandikwa na viongozi wa serikali za wanafunzi vyuo vikuu Tanzania baadhi yao ni Debora Gabriel-Rais wa
Chuo Kikuucha Dododoma Dodoma, Musa Ndile (Waziri Mkuu Serikali yaWanafunzi Chuo Kikuucha IFM
Mboya James Katibu katika serikali ya wanafunzi Chuo Kikuucha IFM, Daniel Naftal Waziri wa mikopo Chuo
KikuuCha Dar es Salaam Mruta Julius aliyekuwa Waziri wa Elimu Chuo Kikuucha Dar esSalaam mwaka
2009/10, Lusapi Yudah-Mwakilishi kamati ya mikopo Chuo Kikuucha Arusha, Mr. Paul Makuli aliyekuwa
Waziri Mkuu mstaafu Serikali yawanafunzi Chuo Kikuucha Dar es Salaam, Rwezaula Robert-waziri mkuu
serikali ya wanafunzi Chuo Kikuucha st.John Tawi la Dar es Salaam. Nk

Sauti za watetezi wa haki vyuoni 7


Mh. Juliu Mtatiro Mh. David E. Silinde Mh. Owawa Steven

Pichani, kushoto ni Mh. Julius Mtatiro ambaye kwa sasa ni Kaimu Mwenyekiti wa Chama
Cha CUF taifa, Mh. David Silinde ni Mbunge wa Mbozi Magharibi kwa tiketi ya Chama
cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA. Mh. Steven Owawa kwa sasa ni mwajiriwa
serikalini.

Mnamo mwaka 2008-2009, Mtetezi Godbless Charles, aliyekuwa Raisi wa Serikali


ya Wanafunzi Chuo Kikuu Cha Muhimbili(MUHAS) ambaye pia historia inamuelezea
kwamba aliwahi kuwa kiongozi wa taasisi ya Vyuo Vikuu Vya umma Tanzania
(UVEJUTA) ambayo kama mtetezi aliitumia taasisi hii kupigania usawa katika elimu
kwa watoto wa kitanzania. Godbless alifkuzwa Chuo katika mgomo maarufu kama
40% ambao ulihitimishwa na serikali kwa kuridhia kozi za Sayansi kupata fursa ya
kupata elimu bila kikwazo cha uwezo wa kifedha.

Pichani kushoto ni Mtetezi Godbless Charles aliyefukuzwa MUHAS mwaka 2008, aliamua
kufungua kesi dhidi ya chuo ambayo alishinda kesi yake ya rufaa Mahakama kuu mwaka
2014 iliyosimamiwa na wakili Msomi, Prof. Abdallah Safari.

8 Sauti za watetezi wa haki vyuoni


Mnamo Mwaka 2010, wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, walifanya
mgomo mkubwa wa kuitaka serikali kuongeza kiwango cha pesa za fedha za kujikimu
boom kwa sababu ya gharama za maisha kupanda, huku pesa za boom zikiwa
zimebakia kiwango kile kile. Mgomo huu ulianzishwa na mwanafunzi wa UDSM
aliyeitwa Richard Mwita ambaye kwa mara ya kwanza aliingia kwenye historia ya
kufanya maandamano ya mtu mmoja kuelekea Ikulu, katika awamu ya uongozi wa
Rais Jakaya Mrisho Kikwete. Baada ya kukamatwa na polisi na kurudishwa chuoni,
akaongoza maandamano husika akiambatana na watetezi wenzake. Mgomo huu
ulipelekea serikali kuwaongeza wanafunzi wa vyuo vikuu nchini kiwango cha sh.
2500/= kutoka ile 5,000/= ya awali. Hivyo wanafunzi wakaanza kulipwa sh.7500/=
kwa siku wakati kabla walikuwa wanalipwa sh.5000/= kwa siku12.

1.6 Historia ya Timua Timua Vyuo Vikuu Nchini 2011 2017


Mwaka 2011 Mpaka 2017 kumekuwa na migogoro mikubwa katika vyuo vikuu mbali
mbali nchini iliyopelekea timua timua ya watetezi wa haki za binadamu, ambao ni
wanachuo. Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kikiwa ni kinara katika kuwasimamisha
na kuwafukuza idadi kubwa wanafunzi, ukilinganisha na vyuo vikuu vingine; huku
UDSM ikifuatiwa na vyuo vingine kama Chuo Kikuu cha Muhimbili (MUHAS),
MUCCOBS13, CBE14, Mwalimu Nyerere Memorial Academy, ST. JOHN, IMTU15, ST.
JOSEPH, IFM16 na TIA17. Kwa undani soma sura ya tatu inayoelezea matukio ya
ukiukwaji haki za watetezi wa wanyonge vyuoni.

Mnamo tarehe 11/11/2011, wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa niaba
ya Vyuo Vikuu vya umma nchini, tulifanya mgomo mzito dhidi ya serikali ya Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania, ili kuishinikiza serikali kupitia bodi ya mikopo (HESLB)
iwadhamini wanafunzi wa mwaka wa kwanza katika vyuo vya umma waliotelekezwa
kudhaminiwa mikopo. Watetezi walihoji uwepo wa mikopo hewa iliyokithiri ndani ya vyuo
Vikuu vya umma na kuiomba serikali kuelekeza mikopo husika kwa wanafunzi halisi na
kuwachukulia hatua za kisheria waliohusika katika ubadhirifu wa Fedha za umma.

12 Taarifa hizi zilitolewa na Baraka Monance mmoja wa watetezi walioshiriki kikamilifu katika maandamano
husika ndami ya Chuo Kikuucha Dar es Salaam wakati wa mahojiano baina yangu na yeye tarehe 20 julai
2012.
13 MUCCOBS-Moshi University College of Co-operative and Business studies.
14 CBE- College of Business Education
15 IMTU-International Medical and Technology University
16 IFM-Institute of Finance Management
17 TIA-Tanzania Institute of Accountacy

Sauti za watetezi wa haki vyuoni 9


Mgomo huu uliratibiwa na kuongozwa na watetezi wa haki za Wanafunzi akiwemo
mwandishi wa kitabu hiki na hatimaye baadaye kufukuzwa chuo. Baada ya hapo
serikali ya wanafunzi kupitia Bunge la DARUSO, waliamua kufanya mgomo mzito ili
kushinikiza utawala kuwarudisha chuoni watetezi tuliofukuzwa; lakini viongozi wote 99
akiwemo Rais wa Serikali ya Wanafunzi walifukuzwa chuoni na baada ya siku chache,
Rais wa DARUSO wa wakati huo ndugu Saimon Kilawa akarudishwa chuo18. Kuanzia
tarehe tajwa hapo juu, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam hakikutulia kwa sababu ya
matatizo ya wanafunzi kutotatuliwa kwa wakati na watawala wa Chuo hiki. Kwa hiyo,
serikali ikiambatana na watawala wa chuo wakaamua kutumia nguvu ya vyombo vya
dola kuwatuliza wanafunzi wa UDSM. Mgogoro huu ilidumu kwa takribani mwezi
mzima. Hapo chini ni baadhi tu ya picha za watetezi waliosmamishwa na wengine
kufukuzwa Chuo mwaka 2011.

Pichani ni mtetezi jasiri wa kike, Hellen P Mushi akiwahutubia wanazuoni wa Chuo kikuu
cha Dar es salaam, umuhimu wa kupinga wanafunzi wa mwaka wa kwanza kurudishwa
nyumbani kwa hoja hafifu ya bajeti haitoshi huku kukiwa na mikopo hewa lukuki Vyuoni.
Mpaka leo hii hajafanikiwa kumaliza shahada yake

18 kama Gazeti la Majira, ISSN 5086. Na. 6580. Vol 11/4590. Jumatano. Januari 11.2012 lenye kichwa cha
habari Wanafunzi 99 UDSM nao wafukuzwa Chuo. Uk. 4.

10 Sauti za watetezi wa haki vyuoni


Hellen P. Mushi Ndunguru O Francis Silayo E. Ambrose Addo Joseph

Elius Mwambapa Daniel Naftal Garubindi Gaston Christopher Mbusule

Mabirika Mawazo Legan Michael Laizer Yonas Mesaya Ismail

Pichani ni baadhi ya watetezi waliosimamishwa na wengine kufukuzwa katika Chuo Kikuu


cha Dar es Salaam mwaka 2011.

Historia inatueleza kwamba kunawatetezi hawajarudishwa kusoma tangu kufukuzwa


kwao mathalani Hellen Mushi, Bokasa Wilfred, Christopher Mbusule, Mabirika Mawazo
na Wengine wengi, wengine kuzuiliwa kujiunga na vyuo vingine vya umma akiwemo
mwandishi wa kitabu hiki. Kuna baadhi wameikimbia nchi na kuenda kusoma nchi za
nje, mathalani Elius Mwambapa ambaye wazazi wake waliamua kumsomesha Uganda
na ndugu Mwampese Hamisi ambaye alienda kuanza kusoma nchi ya Algeria .

Sauti za watetezi wa haki vyuoni 11


Je watetezi wa haki za binadamu vyuo vikuu nchini wanatumiwa na
vyama vya siasa vya upinzani?
Hili ni swali ambalo historia ya timua timua vyuo vikuu nchini inaweza ikawa jibu sahihi.
Historia hii inatukumbusha kuwa, hata wakati wa chama kimoja watetezi wa haki za
binadamu vyuoni walikuwepo na walikuwa wanasimama kutetea haki za wanafunzi
na haki za Watanzania. Hivyo suala la kusema kwamba, watetezi hawa wanatumiwa
na vyama vya siasa sio hoja ya msingi. Hoja ya msingi ni kuangalia hoja ambazo
zinafanya watetezi wasimame katika harakati kwa wakati husika na kwa njia halali
kama historia inavyopambanua19.

Hitimisho
Tathmini nzima ya historia ya timua timua Watetezi wa haki za binadamu Vyuo vikuu
Tanzania inaonyesha namna vyuo vikuu vinavyopoteza dira katika harakati za utetezi.
Watetezi wa huko Nyuma walitumia taasisi ya Chuo kikuu kupigania mambo ambayo
yanamaslahi mapana na taifa na kimataifa mathalani kupinga mishahara minono kwa
vigogo wa kiserikali, kutetea uhuru wa nchi ya Zimbabwe kinyume na sasa ambapo
watetezi wengi wamejikita katika kutetea maslahi binafsi ya wanafunzi na sio jamii
kwa upana wake Selfish Activism. Kwa sasa Watetezi Vyuoni huongoza harakati za
kutetea matumbo yao mathalani Boom likichelewa, kuongezewa fedha za kujikimu
na huoni wakijishughulisha kutetea wanyonge nje ya uanafunzi wao. Tunamfano hai,
Mchakato wa katiba Umekwama, taasisi za vyuo vikuu zilizotegemewa kusiama na
kudai katiba mpya kwa masalahi mapana ya taifa zipo kimya, hii ni hari ya hatari katika
taifa hili. Jamii inashindwa kuelewa wasomi wa sasa na hatimaye kutotuunga mkono
katika madai mbali mbali tunayoyadai. Watetezi Vyuo vikuu wanapaswa kujielekeza
katika kutetea masuala yenye maslahi mapana na wanyonge wa taifa hili.

19 Taarifa ya Mh. Philipo Mulugo bungeni aliyekuwa Naibu Waziri wa Elimu katika Gazeti la Uhuru ISSN
0876-21494 Ijumaa Mei 3, 2013 Uk. 4.

12 Sauti za watetezi wa haki vyuoni


Sura ya Pili

2.0 Vyanzo vya Kufukuzwa


Watetezi wa haki za binadamu
Vyuoni
Pamoja na ukweli kwamba historia ya timua timua vyuo vikuu nchini hususani Chuo
Kikuu cha Dar es Salaam imeelezewa kiundani katika sehemu iliyotangulia, pia zipo
baadhi ya sababu za msingi zilizopelekea na zinazopelekea watetezi wa vyuo vikuu
nchini kuendelea kuongoza migomo au maandamano. Historia inadhihirisha kuwa,
zifuatazo ni sababu za msingi zilizopelekea na zinazoendelea kupelekea migogoro
mikubwa vyuo vikuu nchini. Tutazifafanua kama ifuatavyo:

- Matatizo ya Mikopo na Usiri wa vigezo vya kutoa mikopo ndani ya Bodi ya Mikopo
- Sera mbovu za elimu.
- Ubovu wa miundombinu vyuoni
- Watetezi kuwekwa kizuizini
- Mabavu ya watawala dhidi ya wanafunzi wa vyuo vikuu
- Wanavyuo kupinga madhaifu ya kisheria ya mfumo mzima wa kuwapata watawala
wa vyuo vikuu

2.1 Sababu Mbalimbali Zinazowafanya Wanavyuo Wagome


2.1.1 Matatizo ya Mikopo na Usiri wa Vigezo vya Ugawaji wa Mikopo
wa Bodi ya Mikopo Tanzania
Mara kadhaa wanafunzi wa vyuo vikuu hugoma na huandamana kwa ajili ya kudai fedha
zao za kujikimu. Madai yao yametokana na usiri mkubwa wa vigezo vinavyotumika
kutoa mikopo kwa wanafunzi wanaodahiliwa vyuo vikuu nchini. Madai husika
yamegawika katika sehemu kuu mbali mbali: ya kwanza wanafunzi kucheleweshewa
fedha za kujikimu kama nilivyoainisha katika sura ya kwanza, kwa mfano ni mgomo
wa tarehe 4 februari 2011 katika Chuo Kikuu cha UDSM, ambapo wanafunzi walikuwa
na hoja kuu tatu. Moja ni kucheleweshwa kwa mikopo; pili wanafunzi wenye sifa na
vigezo vya kudhaminiwa mikopo kukosa fursa ya kudhaminiwa mikopo; na tatu kutaka
nyongeza ya fedha za kujikimu.

Sauti za watetezi wa haki vyuoni 13


Zifuatazo ni picha mbili zinazoonesha wanafunzi wakiandamana
kuelekea kwenye mamlaka husika ili kudai haki zao; na picha
nyingine ni ya chombo cha dola ambacho kilitumika kupambana na
wanafunzi wanaoandamana na kugoma.

Hawa ni wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Kampasi ya Mlimani wakiandamana
kuelekea Ikulu tarehe 4/02/2011 ili kushinikiza Serikali kuongeza pesa ya kujikimu, kutoka
5000/= hadi 10,000/= kwa siku. Faida ya mgomo huu ni kwamba, serikali iliongeza bumu
mpaka ikawa 7,500/=.

2.1.2 Sera mbovu za elimu nchini


Kama historia ya timua timua vyuo vikuu inavyojieleza katika sura ya kwanza, sera
mbovu nazo zimechangia kuwapo na migomo katika vyuo vikuu nchini. Mwaka
1992 wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam waligoma kupinga sera ya
kuwashirikisha wazazi kuchangia gharama za elimu ya juu cost sharing ambapo
watetezi mara kadhaa huwaongoza wanavyuo kupinga matokeo ya sera mbovu
ambazo zimeshaunda au kusababisha kuwapo na matabaka mawili katika jamii,
ambayo ni tabaka la wenye nacho na wasio nacho. Walionacho wanauwezo wa
kuchangia; wakati wasionacho wanakosa fursa ya kusoma kwa sababu ya kukosa
uwezo wa kuchangia20.

20 The report of the probe team on students crises in higher education institutions in Tanzaniam May 2004.
Ni tume iliyoongozwa na Dr. Hawa Sinare kama Mwenyekiti, Mrs. N.E. Ligate kama Makamu Mwenyekiti
na Profesa Tolly. S. A. Mbwette kama katibu mkuu wa tume husika kwa ajili ya kufanya tafiti za vyanzo vya
migogoro ya wanafunzi wa vyuo vikuu na kuja na suluhu ya kuisaidia serikali kutatua migogoro ya vyuo vikuu
Tanzania. Kubadilisha utawala wa vyuo vikuu vya umma ili kuweka mazingira mazuri ya kitaaluma ndani ya
vyuo vikuu Tanzania

14 Sauti za watetezi wa haki vyuoni


2.1.3 Huduma mbovu za kijamii katika eneo la Chuo
Kuwapo na huduma mbovu za kijamii katika eneo la chuo kama vile: uchafu wa vyoo,
kukosekana kwa huduma za maji, huduma za usafiri, kukosekana kwa lifti katika
mabweni yenye ghorofa, huduma mbaya ya kafteria kama vile uchafu wa kafteria
na gharama za vyakula kuwa juu. Mnamo mwaka 1986, wanafunzi wa Chuo Kikuu
cha Dar es Salaam waliamua kufanya mgomo mzito wa kutoingia madarasani kwa
sababu ya huduma mbaya ya kafteria, mazingira machafu ya kafteria, gharama kubwa
wanazolipia chakula katika kafteria.

2.1.4 Watetezi wa Wanafunzi Kusimamishwa masomo, Kufukuzwa


Chuo au Kuwekwa Kizuizini
Kama nilivyoeleza katika historia ya timua timua vyuo vikuu nchini katika sura ya
kwanza, mara kadhaa watetezi wa haki za binadamu hushikiliwa na jeshi la polisi
kwa sababu ya kutaka kusimamia haki za wanafunzi wa chuo. Kwa hiyo jambo
hili limekuwa ni la kawaida sana mara tu baada ya migomo kutokea. Jambo hili
linawafanya Wanafunzi waliobaki kugoma mpaka pale watetezi watvoachiwa.

2.1.5 Watawala kutumia mabavu na kujenga mazingira ya uhasama/


uadui dhidi ya Watetezi
Watawala wengi wa vyuo vikuu wamejenga hali ya kuwachukia wanafunzi wanaotetea
haki za wanafunzi wenzao na kuwaona kama maadui wao; na hivyo, hisia hizo
hupelekea utawala wa chuo husika kutumia mabavu ya vyombo vya dola kama
ionekanavyo dhahiri katika Gazeti la majira21.

2.1.6 Wanavyuo kupinga madhaifu ya Sheria zinazoathiri ustawi wa


Vyuo Vikuu nchini.
Mara kadhaa wanavyuo wamekuwa wanaandamana na kugoma kwa sababu ya
madhaifu ya sheria yanayotengeneza ubinadamu na si uwajibikaji katika utawala wa
vyuo nchini. Historia inatukumbusha kuwa, wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam, mnamo tarehe 23 Julai 1971, Rais wa Serikali ya Wanafunzi DUSO, ndugu
Akivaga aliwaongoza wanafunzi kupinga mfumo wa kuwateua makada wa chama
tawala kuwa makamu mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

21 Gazeti la Majira ISSN 0856. Na 6580. Vol. 11/4590, Jumatano Januari 11, 2012

Sauti za watetezi wa haki vyuoni 15


Lakini vile vile suala la madhaifu ya mfumo wa kuwapata watawala vyuoni limejitokeza
mwaka 2011, ambapo wanafunzi wa UDSM walilalamikia sheria husika, inayompa
madaraka Rais ya uteuzi wa mkuu wa chuo kama ibara ya 3522 ya sheria za vyuo vikuu
nchini Universities Act 2005 inavyoelezea. Sheria hii inanyima uhuru wa watawala
wanaoviongoza vyuo vikuu nchini kwani wanakosa uhuru wa kuviendesha vyuo
husika kama inavyotakiwa na kubakia kupokea mashinikizo kutoka kwa aliyewateua.

2.1.7 Kukosekana kwa mafunzo ya vitendo na vifaa vya kujifunzia


Watetezi huwaongoza wanavyuo kupinga kusoma elimu ya nadharia bila vitendo kwa
kukosa mahitaji muhimu kama vile kukosa vifaa vya kujifunzia na mazingira mabovu
ya kijifunzia. Katika historia ya timua timua ya wanafunzi katika vyuo vikuu nchini, sura
ya kwanza imeelezea kiundani migogoro iliyotokea nyakati tofauti tofauti hasa katika
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Chuo Kikuu cha Sokoine, baada ya watetezi wa
haki za binadamu kuwaongoza wanafunzi wa vyuo vikuu kudai haki husika.

2.1.8 Serikali kuingilia Jumuiya na Serikali za Wanafunzi Vyuoni


Kumekuwa na migogoro mbali mbali ya wanavyuo dhidi ya serikali au watawala
kwa sababu ya kuingiliwa na kufutwa kwa serikali na jumuiya za wanafunzi, ambazo
zipo pale kwa ajili ya kutetea haki za wanafunzi husika. Ifuatayo ni mifano ya namna
ambavyo serikali/watawala wanaingilia jumuiya na serikali za wanafunzi.

v Mnamo tarehe 12 Juni 2009, kuna muongozo wa serikali ulitolewa kutoka


Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi uliokuwa maarufu kama Sheria za
Profesa Maghembe GN 178. Muongozo husika ulitaka kubadili katiba za
serikali za wanafunzi vyuoni ili kubadili mfumo mzima wa uongozi. Mfano ni
kufuta nafasi ya Rais, Mawaziri na Manaibu Waziri na kubaki na Wenyeviti na
Makatibu wake. Mfumo huu ukarudisha mamlaka ya serikali ya wanafunzi
kwa Mshauri/Mlezi wa Wanafunzi ambaye yeye ni sehemu ya utawala na
wakati huo huo ni Rais wa wanafunzi. Wanafunzi hawakushirikishwa katika
mabadiliko husika. Sheria hizi ndizo zilizopelekea kufutwa kwa Serikali ya
Wanafunzi ya Chuo Kikuu cha Muhimbili (MUHAS23).

22 35 [1] The Chancellor of the Public University shall be appointed by the respective President.
23 Taarifa hizi alizitoa aliyekuwa Rais wa serikali ya wanafunzi MUHASO, ndugu Gervas Shayo ndani ya
Chuo Kikuucha Muhimbili mnamo tarehe 12 novemba 2012 wakati wa mahojiano naye. Yeye kama mte-
tezi ndiye aliyesimama kuwaongoza wanafunzi kupinga sheria husika kwani alikiri kwamba serikali inaingilia
uhuru wa serikali za wanafunzi ili zisitekeleze wajibu wake kwa maslahi mapana ya wanafunzi na taifa kwa
ujumla wake.

16 Sauti za watetezi wa haki vyuoni


Pichani ni mtetezi Gervas Odillo Shayo, aliyekuwa Rais wa Serikali ya Wanafunzi MUHAS
mwaka 2011, akiwa mwaka wa tano na akiwa amebakiza miezi sita kumaliza shahada ya
Udaktari alifukuzwa Chuo Kikuu MUHAS na kufutiwa udahili wake chuoni kwa sababu ya
kuwaongoza wanafunzi kupinga sheria tajwa hapo juu.

- Lakini vile vile mnamo mwaka 1978, Serikali ya Wanafunzi DUSO ilifutwa na
kuwekwa chini ya usimamizi wa Umoja wa Vijana wa TANU ulioitwa TANU YOUTH
LEAGUE TYL. Binafsi naamini hizi ni mbinu za watawala kutaka kuingilia uhuru
wa serikali za wanafunzi na kuua sauti za wasomi wa vyuo vikuu kwa kutengeneza
mifumo itakayowalinda watawala na serikali.

- Kwa muda mrefu wanavyuo wamekosa matumaini na Jumuiya ya Wanafunzi


TAHLISO kwa tuhuma za kutumiwa na Chama Tawala CCM, mfano mwepesi
ni Rais wa TAHLISO aliyekuwa mjumbe wa (U.V.C.C.M.) Ndugu Paul Makonda
jambo ambalo ni kinyume na sheria za vyuo vikuu universties charter na hivyo
chombo hiki kutotelekeza wajibu wake kwa wanafunzi. Ikumbukwe maandamano
ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam UDSM mwaka 2008 ya kudai
nyongeza ya pesa ya kujikimu kutoka 3500/= hadi 5000/=. Pia maandamano
ya 3/02/2011 kuelekea Ikulu ya kutaka kuongezwa pesa za kujikimu kutoka
Sh.5000/= hadi 10,000/= ambapo TAHLISO haikushiriki kwa namna yoyote na
cha kushangaza, Uongozi wa TAHLISO mwaka 2008, ulipinga maandamano
husika ambayo yaliyozaa matunda kwa maslahi ya wanafunzi wote mpaka leo hii.
Hata wale walioyapinga wamenufaika na matunda ya mgomo!

Sauti za watetezi wa haki vyuoni 17


2.2 Sababu zitolewazo na Watawala dhidi ya Watetezi Vyuoni
Ni muda mrefu kumekuwa na utamaduni wa watawala wa vyuo vikuu kutoa taarifa
potofu mbele ya umma, dhidi ya watetezi wanaosimamishwa au kufukuzwa vyuoni.
Tuhuma hizi ni kama zifuatavyo:
- Kutumiwa na wanasiasa;
- kuwapiga wahadhiri, wajawazito na wanafunzi wenzao;
- Kubaka na kuwadhalilisha wanawake kijinsia ;
- Kumwagia vyakula michanga;
- Kufanya uharibifu wa mali za chuo nk.

Tuhuma ambazo zimekuwa ni sumu kuliko tuhuma zote ni hii ya kutumiwa na wanasiasa
hasa wa upinzani, kama ilivyoonekana katika Gazeti la Mtanzania lenye kichwa cha
habari VURUGU UDSM24. Uongozi wa chuo kikuu ulidai kuwa, waliofukuzwa ni
wanasiasa, na pia habari kama hiyo ilichapishwa katika Gazeti la Uhuru25, nalo Gazeti
la Mzalendo la Jumapili tarehe 15 Januari 2012, katika makala ya 7 lilikua na habari
kama hizo.

2.3 Hitimisho
Katika sura hii, tumedondoa sababu mbalimbali ambazo zinawafanya au zimewafanya
wanafunzi wa vyuo vikuu kugoma. Ni matumaini yangu kuwa, msomaji atakayesoma
sura hii, atapata picha ya ukweli kuhusu madai ya wanavyuo ambayo yanawafanya
wagome; tofauti na taarifa potofu ambazo zimekuwa zikitolewa mbele ya jamii. Kwa
kusoma sura hii ya pili, ndugu msomaji utaanza kuelewa ukiona wanafunzi wanagoma,
kwa kuwa hutakuwa msikilizaji tu wa sababu zinazotolewa na upande wa watawala;
bali pia utapata shauku ya kusikiliza madai ya wanafunzi wanaogoma.

24 Gazeti la mtanzania ISSN 0856 - 5678 toleo namba na5842 Jumapili Januari 15, 2012 makala ya13
25 Gazeti hili liliandikwa: vurugu za UDSM: chama cha CHADEMA cha shukiwa kuwa nyuma ya mgomo
ukweli wabainika.

18 Sauti za watetezi wa haki vyuoni


Sura ya Tatu

3.0 Matukio ya Ukiukwaji haki


za Watetezi Vyuoni
3.1Mtetezi wa haki za binadamu ni nani?
Kwa mujibu wa Mwongozo wa Ulinzi na Usalama wa Watetezi wa Haki za Binadamu26,
mtetezi wa haki za binadamu ni kauli inayotumika kueleza mtu ambaye, yeye binafsi
au pamoja na wengine, anajitahidi kuendeleza na kuzilinda haki za binadamu.
Binadamu hawa wanatambulika pakubwa zaidi kwa yale wanayoyafanya na ni kupitia
kwa kuyafafanua matendo yao na katika baadhi ya maeneo wafanyayo kazi, ndipo
sasa kauli hii yaweza kupewa ufafanuzi bora zaidi. Mara nyingi mtetezi wa haki
za binadamu huwa nguzo pekee kati ya wananchi na mamlaka za nchi hasa katika
masuala yanayowataabisha watawaliwa.

Ndugu Elius Mwambapa, mmoja wa watetezi waliofukuzwa UDSM mwaka 2011


akiongoza mjadala wa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika eneo maarufu
kwa jina la Revolution Square. Pichani ni wanafunzi wa UDSM wakijadili mijadala ya kitaifa
na matatizo mbali mbali yanayowakumba wanafunzi.

26 Mwongozo mpya wa ulinzi na Usalama wa watetezi wa haki za binadamu, Umetafitiwa na kuandikwa


na Enrique Eguren na Marie Caraj, Umechapishwa na Protection International {PI} 2012, Umetafsiriwa na
Kimani Njogu.
Mwongozo huu umetolewa kwa manufaa ya wateteaji wa haki za binadamu.

Sauti za watetezi wa haki vyuoni 19


3.2 Matukio ya Utetezi wa haki za binadamu Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam (UDSM)
Habari katika picha ni wanafunzi wa UDSM wakiandamana.

Pichani kushoto ni Mtetezi wa haki za Wanafunzi ndugu, Owawa Steven J. akiwahutubia


wanafunzi eneeo la Utawala wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika maandamano
ya mwaka 2008yaliyotokana na aidha ya ukosekanaji wa maji.pichani kulia ni wakati wa
maandalizi ya mgomo husika.

Hawa ni wanafunzi wa Chuo Kikuu Kampasi ya Mlimani wakiwa katika mgomo


tarehe11/12/2011. Mgomo huu ni wa kuutaka utawala wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
uwarejeshe watetezi waliofukuzwa chuoni hapo baada ya Bunge la DARUSO kuidhinisha
mgomo rasmi.

20 Sauti za watetezi wa haki vyuoni


3.3 Watetezi wa haki za binadamu Chuo Kikuu cha Dododma (UDOM).
Mnamo tarehe 15 June mwaka 2011, Chuo Kikuu cha Dodoma kilifukuza zaidi ya
wanafunzi 9,000 wa chuo hicho (UDOM) kwa muda usiojulikana, kuanzia tarehe tajwa
hapo juu kwa madai ya kuhamasisha mgomo usio halali.

Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Idriss Kikula alithibitisha kufukuzwa kwa
wanachuo hao na kusema kuwa, suala la kuwarejesha litatokana na utaratibu
watakaoupanga baadaye27.

Ni Chuo Kikuu cha Dodoma kilipofukuza na kuwasimamisha wanafunzi zaidi ya 9000


baada ya watetezi wa haki za binadamu chuoni hapo, kuwaongoza wanafunzi wenzao
kudai haki zao kama zilivyoainishwa hapo chini kwenye ujumbe wa kwenye bango.

27 Taarifa hizi ziliripotiwa na Gazeti la Majira la tarehe 15 juni 2011. Kufukuzwa huko kulikuja siku mbili
baada ya kuanzisha maandamano yaliyoshinikiza kujiuzulu kwa viongozi waandamizi wa Serikali, Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda, Waziri wa Mambo ya Ndani, Shamsi Vuai Nahodha na Waziri wa Elimu na Mafunzo
ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa kwa madai kwamba wamewadanganya kuhusu malipo yao ya masomo
kwa vitendo kama vyuo vingine wasomavyo.

Sauti za watetezi wa haki vyuoni 21


Philipo Mwakibinga Libereus M. John Getrude Kokwenda Pascal Robert

Pichani ni watetezi waliosimamishwa na wengine kufukuzwa kabisa Chuoni. Mr.Philipo


Mwakibinga ni mtetezi aliyefukuzwa mara mbili UDOM kwa harakati zake za uetetezi.

Maandamano ya
mtetezi wa haki za
binadamu UDSM
Ndugu, Richard Mwita.

Pichani ni mtetezi wa wanafunzi Chuo


Kikuu cha Dar es Salaam mwaka 2010,
ambaye aliamua kuandamana peke yake
kuelekea Ikulu ili kumpelekea ujumbe Rais
wa nchi, kuhusu madai ya kuongeza fedha
za kujikimu kwa wanavyuo kutoka 5000/=
hadi 10,000/=.

Bw. Mwita alifikia hatua hii ya kuandamana


peke yake baada ya kuwashawishi
wanafunzi wa UDSM kwa muda mrefu
kuandamana kwa ajili ya kuitaka serikali
ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
kuongeza fedha za kujikimu maarufu kwa
jina la boom bila mafanikio. Akaamua
kujivika jukumu hilo yeye kama yeye na
kuandamana peke yake kuelekea Ikulu.

22 Sauti za watetezi wa haki vyuoni


Tukio hili lilikuwa ni la kihistoria ndani ya vyuo vikuu Tanzania, kwani baada ya
kuandamana peke yake alikamatwa na polisi na kuachiwa baada ya kuhojiwa. Mara
baada ya kuachiwa alirudi chuoni na kuwaongoza tena wanafunzi katika kuishinikiza
serikali kuongeza fedha za kujikimu. Wanafunzi waliunga mkono na hatimaye fedha za
kujikimu ziliongezeka kutoka sh.5000 hadi 750028.

3.4 Matukio ya Utetezi wa haki za binadamu Chuo Kikuu cha


MUHIMBILI MUHAS
Baada ya wanafunzi takribani 85 kufukuzwa na wengine kusimamishwa chuo kwa
sababu ya kuidai serikali yao ya MUHAS iliyofutwa, na pia kupinga agizo la Serikali la
kuwaletea GN 178 zilizokuwa maarufu kwa jina la Sheria za Maghembe29, wanafunzi
wa MUHAS walitoa wito wao kwamba, wanaomba uongozi wa chuo uwarejeshe
wanafunzi wote 85 waliosimamishwa chuo wakiwemo watetezi wao badala ya
kuwahukumu kwa kutumia matokeo ya tatizo (Sera), kama chanzo cha mgogoro wa
MUHASO ambao ni tofauti katika utekelezaji wa agizo la serikali la tarehe 12 Juni,
2009 (GN.178). Sheria hiyo ya Maghembe imefanya mabadiliko makubwa kwenye
uendeshaji wa serikali za wanafunzi katika vyuo vikuu na hivyo kuanzisha mivutano
baina ya wanafunzi na utawala katika chuo hicho na vyuo vingine nchini.

Pichani kushoto ni Mtetezi Charles Jackson akiwa anawahutubia Wanafunzi wa MUHAS,


katika sehemu ya mgomo wao wa kuushinikiza utawala wa chuo hicho, kurudishwa
serikali yao ijulikanayo kama MUHASO.Mtetezi huyu mpaka sasa bado hajarudishwa
chuoni.pichani kulia polisi wakiwatawanya wanafunzi MUHAS mwaka 2011.

28 Taarifa hizi zilitolewa na ndugu Baraka Monance, mtetezi wa haki za binadamu aliyefukuzwa na kufutwa
katika mfumo wa Elimu Tanzania katika mahojiano baina yangu nay eye mnamo tarehe 20 novemba 2012.
29 Rejea sura ya pili inayoeleza kwa kina vyanzo vya migogoro ikiwemo sababu ya serikali ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania kuingilia serikali za wanafunzi Tanzania.

Sauti za watetezi wa haki vyuoni 23


3.5 Taarifa za matukio ya Utetezi Vyuoni.

Pichani Kushoto ni Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Makumira wakiwa katika maandamano,
wakilalamikia suala la ucheleweshwaji wa mikopo yao. Jeshi la Polisi lililazimika kutumia
mabomu kuwatawanya, baada ya kuzuia barabara ya Arusha na Moshi.

Pichani kulia ni wanafunzi wa Chuo Kikuu Tumaini Tawi la Dar es Salaam, wakiwa katika
mgomo tarehe 3/01/2012. Mgomo huu ni baada ya pesa yao yakujikimu kucheleweshwa,
kufuatia utaratibu mpya wa pesa hiyo kutolewa vyuoni badala ya Bodi ya Mikopo (HELSB).

Pichani kushoto ni Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha IFM wakimsikiliza mtetezi wao (Waziri
Mkuu, ndugu. Mussa Ndile), kufuatilia mgogoro wa wanafunzi na utawala wa chuo hicho.
Mwaka 2011, wanafunzi hawa waligoma kwa ajili ya kupinga utawala kuingilia chaguzi za
serikali za wanafunzi.

Pichani kulia ni Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha IMTU wakifanya mgomo kwa niaba ya vyuo
vikuu vingine vya binafsi kuhoji uhalali wa chuo hicho kutoza ada wanafunzi kwa Dola ya
Kimarekani lakini vile vile kupandishwa kwa ada za wanafunzi kiholela holela hasa katikati
ya muhula wa masomo na hivyo wakiitaka serikali iingilie kati suala husika.

24 Sauti za watetezi wa haki vyuoni


Wanafunzi walitoa swali kwa serikali kuingilia kati suala husika, kwamba kama
mwanafunzi anaingia mwaka wa pili, mzazi wake amejifunga mkanda kumpeleka
mwanae hapo chuo cha binafsi au ndio amechaguliwa na (TCU) ghafla linatokea
ongezeko la asilimia 60% kwenye ada, je, amwachishe chuo? Kwa mfano, ada ya
Chuo Kikuu cha Tumaini ilipanda kutoka shilingi 1,500,000/= hadi shilingi 2,500,000/=
kwa mwaka! Mgomo huu ulitokea mwaka 2010/2011 na kuiomba serikali kuingilia
kati suala husika. Mpaka leo hakuna mabadiliko yoyote yaliyofanywa na serikali ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Pichani ni baadhi ya wanafunzi watetezi wa chuo cha St. Joseph waliosimamishwa


masomo yao kwa muda usiofahamika mnamo tarehe 26 Novemba mwaka 2014 baada
ya kufanya mgomo wa kudai fedha zao za kujikimu boom ambazo hawajapatiwa kwa
wakati huku mtandao wa wanafunzi Tanzania TSNP30 ukiwa umeingilia kati na kukutana
na utawala wa chuo hicho tarehe 5 Disemba 2014.

3.6 Hitimisho
Katika sura hii tumekugusia migomo iliyotokea katika vyuo vikuu mbalimbali nchini na
sababu za kutokea kwake. Kwa hakika sababu nyingi zinashabihiana na nizamsingi.

30 TSNP-Tanzania Students Networking Programme. Baada ya kuwasilisha barua ya TSNP ya kuutaka


utawala wa St. Joseph kuwarudisha chuo kabla ya Uongozi wa taasisi kuchukua hatua za kisheria dhidi yao.
Watawala waliahidi kuwarudisha wanafunzi wote ndani ya mwezi wa kumi na mbili.

Sauti za watetezi wa haki vyuoni 25


Sura ya Nne

4.0 Mazingira na mienendo ya kesi


za Watetezi katika Mahakama
4.1 Utangulizi
Watetezi wa haki za binadamu ndani ya vyuo vikuu nchini, hufanya kazi katika
mazingira tata na magumu, ambayo yana wahusika wengi tofauti na ambayo
yanaathiriwa na ushawishi mkubwa wa kisiasa katika harakati za kufanya maamuzi.
Matukio mengi aghalabu hutendeka wakati mmoja, huku kila tukio likiathiri jingine.
Ni muhimu watetezi wa haki za binadamu ndani ya vyuo vikuu nchini wayafahamu
mazingira ya harakati zao, ili wawe na uwezo wa kukabiliana na changamoto husika.

Ni ukweli usiofichika kuwa panaweza kuwepo na nchi ambazo serikali zinatoa tishio
la kijumla dhidi ya kazi zote zinazohusiana na utetezi wa haki za binadamu. Lakini
pia nchi yetu imekuwa na shughuli za kutishia watetezi wa haki za binadamu kupitia
matamko mbali mbali kwa mfano kauli ya Waziri Mkuu, Mh. Mizengo Peter Pinda
aliyoitoa ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mnamo tarehe 27 Juni
2012, kwamba, Serikali itatoa tamko la hatua itakazochukua kuhusiana na mgomo
wa madaktari nchini na litakalokuwa na liwe31. Huu ulikuwa ni wakati wa mgomo
wa madaktari ulioongozwa na Dr. Steven Ulimboka. Hii ina maana kwamba, watetezi
wote wanaweza kukabiliwa na hatari.

Lakini najua pia kwamba, watetezi wengine wanakabiliwa zaidi na hatari kuliko wengine
kwa sababu ya misimamo yao. Tunaweza kusema kuwa, timua timua ya watetezi
wa haki za binadamu ndani ya vyuo vikuu ni jambo la kawaida, lakini pia linaweza
kushangaza tunapofanya uchunguzi wa sababu zinazopelekea kuwepo kwa hali
kama hii ili tuwe na ufahamu bora na hata kuyashughulikia matatizo yanayowakabili
watetezi. Kiwango cha hatari kinacholikabili kundi la watetezi wa haki za binadamu
vyuo vikuu kinaongezeka kulingana na vitisho wanavyovipokea, uwezekano wao wa
kudhuriwa, na pia uwezo wao wa kukabiliana na vitisho mbali mbali.

31 kama ilivyoripotiwa na Gazeti la nipashe la 28 juni 2012 katika Mgomo wa Madaktari ulioongozwa na
Steven Ulimboka.

26 Sauti za watetezi wa haki vyuoni


4.2 Watetezi wa haki za binadamu hutishiwa maisha

- Vitisho ni nini?
Maana kamili ya vitisho ni uwezekano kwamba mtu fulani atamdhuru mtu mwingine
kimwili, au kimaadili ama kimali kupitia kwa fujo za kimakusudi, na za kila mara32.
Tathmini ya hatari au matishio ndani ya vyuo vikuu nchini imezidi kukithiri kwani
watetezi wengi wamekuwa wakidhuriwa na watawala wa vyuo vikuu nchini na baadhi
ya viongozi katika sekta ya elimu. Kuwadhuru huku ni kwa kuwachafua watetezi hao
mbele ya vyombo vya habari na hivyo kuchafua sura yao na maadili yao kwa umma.
Katika mazingira kama haya, watetezi huanza kujihami na watetezi chipukizi huogopa
kuendelea kudai haki za binadamu wenzao. Watetezi pia wanaweza kukumbana na
matishio mbalimbali katika hali ya mgogoro. Kwa mfano mwaka 2011 utawala wa Chuo
Kikuu cha Dar es Salaam, UDSM, ulitoa tamko dhidi ya watetezi kuwa, wamefutwa
katika mfumo wa elimu nchini na kuwatishia waliobaki kwamba, watakaojihusisha na
harakati za utetezi (ambazo wao wanazibatiza kuwa ni vurugu) watafukuzwa mara
moja33.

- Kufukuzwa, kusimamishwa masomo na hufutwa katika mfumo


wa elimu nchini:
Watetezi wa haki za binadamu vyuoni husimamishwa masomo kwa muda
usiofahamika. Kumekuwa na namna mbali mbali ambazo watawala wa vyuo vikuu
hutumia kuwaadhibu watetezi wa haki za binadamu, mara nyingi hupewa barua za
kusimamishwa kwa muda usiofahamika, kufukuzwa kabisa na wengine kufutwa
katika mfumo wa elimu nchini, kitu ambacho kinarudisha nyuma harakati za watetezi
vyuoni. Pia watetezi hupigwa na kuteswa34.

32Tafsiri husika imetolewa na Mwongozo wa Usalama wa Watetezi wa haki za binadamu uliotafitiwa na


kuandikwa na Enrique Eguren na Marie Caraj pia kuchapishwa na Protection International (PI) mwaka 2012.
33 Rejea historia ya timua timua watetezi vyuo vikuu Tanzania tangu uhuru wan chi yetu katika sura ya
kwanza ambayo imeeleza kwa kina namna ambavyo watawala wa vyuo vikuu wanavyowasimamisha na
kuwafukuza watetezi wanaposimama kudai haki za binadamu
34 Taarifa hizi zilitolewa na ndugu Lugiko Mathias ambeye ni mtetezi aliyepigwa sana na jeshi la polisi ndani
ya Chuo KikuuUDSM eneo la geti maji mnamo tarehe 11/11/2011 na kupelekwa katika kituo cha polisi cha
Ostabay kilichopo Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Sauti za watetezi wa haki vyuoni 27


Jeshi la polisi likitumia nguvu dhidi ya wanafunzi wa UDSM waliokuwa wakiandamana
kuelekea Ikulu, wakidai mikopo ya wanafunzi wa mwaka wa kwanza ambao
hawakudhaminiwa mikopo katika vyuo vya umma nchini mnamo tarehe 11 novemba
2011.

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu


cha Dar es Salaam, UDSM
Prof. Rwekaza Mkandala na
Profesa Yunus Mgaya- Naibu
Makamu Mkuu wa Chuo Utawala
wakiongea na vyombo vya
habari.

Viongozi hawa wa UDSM walikuwa wanatoa tamko katika mkutano na waandishi


wa habari juu ya maamuzi ya Baraza la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kuridhia
uamuzi uliotolewa na uongozi wa chuo hicho, wa kuwafukuza wanafunzi 13 na
kuwasimamisha wengine 86 kwa madai ya kuhusika katika matukio mbalimbali ya
vurugu na uhalifu chuoni hapo. Tamko hili lilisomwa tarehe 13/11/2011 kwa niaba
yake na Naibu Makamu Mkuu wa Chuo (Taaluma), Profesa Makenya Maboko kwa
waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

28 Sauti za watetezi wa haki vyuoni


4.3 Njia wanazopitia Watetezi wanaorudishwa Vyuoni
Ifahamike kuwa, kunabaadhi ya watetezi ambao baada ya muda fulani hurudishwa
chuoni kwa sababu mbali mbali. Sababu ya kwanza ni pale ambapo watawala wa
vyuo vikuu wamefikiria kuwa hawakutenda haki na kwa sasa huenda mioyo ya
watetezi husika imekufa, na kuhisia kuwa, kwa adhabu waliyopewa wanaweza kuwa
wamejisahihisha na kuachana na harakati zao.

Sababu ya pili, ni pale watetezi wenyewe wanapoamua kujisalimisha mbele ya


watawala na kukiri makosa wasiyotenda na kukubali kushusha utu wao, ili tu kuinusuru
elimu yao. Na watawala huitumia fursa husika ili kuwashinikiza kuandika barua za
kuomba misamaha kama sharti la wao kurudishwa chuoni na kuwapa masharti ya
vitisho35.

Sababu ya tatu ni pale ambapo watetezi wa haki za binadamu wanarudishwa kwa amri
ya mahakama baada ya wao kwenda kudai haki zao katika mhimili wa mahakama.
Kwa mfano, wanafunzi wa UDSM waliofukuzwa chuoni mwaka 2011 walirudishwa
masomoni kwa amri ya mahakama36.

- Zifuatazo ni hatua ambazo watetezi wa haki za binadamu


wanaofukuzwa vyuoni huchukua ili kuhakikisha wanapata haki zao:
Watetezi wa haki za binadamu ambao hufukuzwa vyuoni, hutumia hatua kadha wa
kadha ili kuhakikisha wanapata haki zao. Miongoni mwazo ni hatua za ndani na hatua
za nje. Hatua za ndani ya chuo ni:

1. Kuchukua hatua mbali mbali za kidiplomasia ili kutatua mgogoro husika.


2. Kukata rufaa dhidi ya maamuzi ya kufukuzwa kwao chuoni.
3. Kuomba Baraza la Chuo University Council kupitia upya maamuzi
yaliyofanyika ya kuwafukuza watetezi.

35 Taarifa hizi zilitolewa na Wilfred Mwalusanya mtetezi aliyefukuzwa UDSM mwaka 2011 ambaye alirud-
ishwa na chuo kwa kukubaliana na masharti ya watawala tumepewa masharti kadhaa kama kutafuta cheti
cha hati ya tabia nzuri kutoka kwa wakuu wetu wa wilaya-Certicificate of clean character. Barua za kututisha
endapo tutarudia tena harakati za utetezi
36 CRIMINAL CASE NO. 270/2011, REPUBLIC VERSUS MWAMBAPA ELIUS & 49 OTHERS-ACCUSED,
iliyoamuliwa katika mahakama ya hakimu mkazi Kisutu mnamo tarehe 30/08/2012 na kuamuru wanafunzi
wote kurudishwa chuo.

Sauti za watetezi wa haki vyuoni 29


Hatua za nje ya chuo:
1. Kwenda katika AZAKI (Asasi Zisizo za Kiserikali) zinazojihusisha na kutoa misaada
ya kisheria ili kuomba ushauri wa kisheria; lakini vile vile ni kuomba msaada wa
kupatiwa wakili au mawakili watakaowasaidia kusimamia haki zao37.

2. Kupeleka madai ya watetezi katika mhimili wa mahakama katika ngazi tofauti


tofauti ili kutatua mgogoro husika kisheria.

4.4 Maisha ya Watetezi baada ya kurudishwa Vyuo


Maisha ya watetezi hawa baada ya kurudishwa chuo yanakuwa chini ya uangalizi
mkali sana na kuundiwa sheria zinazowataka wasifanye harakati zozote za utetezi
katika eneo la chuo husika; na pia kuwapa usumbufu wa kila namna ili wajutie
harakati walizozitenda. Hivyo ni uhalisia kuwa watetezi wanakuwa katika mazingira
hatarishi mno38. Lakini pia kuna watetezi ambao hawakubali kushusha utu wao na
wana msimamo na kitu walichokisimamia. Mara nyingi watetezi hawa wa mrengo
wa pili, husimama haki zao mpaka mwisho na kupambana na hali halisi. Wengi wao
huchukua mkondo wa kisheria dhidi ya maamuzi waliyofanyiwa ili kuhakikisha haki
zao zinapatikana kupitia katika mahakama za nchi hii.

4.5 Changamoto ambazo hujitokeza kwa Watetezi baada ya


kufukuzwa
Zipo changamoto mbalimbali zinazowakabili watetezi wa haki za kibinadamu baada
ya kufukuzwa chuo. Miongoni mwa changamoto hizi ni kama zifuatavyo:

- Kupata misaada ya kisheria;


- Kutengwa na wazazi ndugu na jamaa na hata wadau wa maendeleo;
- Kesi za watetezi kutoisha kwa muda katika mahakama zetu.

37 THRDC, LHRC, TLS.


38 Mtetezi Ismail Mesaya aliyebahatika kurudishwa chuo UDSM alisema tunakuwa katika uangalizi mkali
sana kwa mfano ndugu Daniel Mwakyusa alijitokeza kugombea nafasi ya URais wa serikali ya wanafunzi
DARUSO 2013/2014 , alipigiwa simu na Naibu makamu mkuu wa chuo-utawala, Profesa Yunus Mgaya
kumuuliza kwa nini amegombea wakati sheria ziko wazi kwa watetezi wote waliowahi kufukuzwa chuo
kutoruhusiwa kugombea

30 Sauti za watetezi wa haki vyuoni


Pamoja na ukweli kwamba watetezi huchukua njia za kisheria ili wapate haki zao,
kumekuwa na changamoto nyingi sana za kimahakama ambazo sina budi kuzielezea
kwa niaba ya watetezi wenzangu. Nitazielezea kama ifuatavyo:

4.6 Mienendo ya kesi za Watetezi Mahakamani


Kesi za watetezi Huchukua muda mrefu mahakamani kwa kuahirishwa mara kwa mara.
Mara nyingi kesi za wanafunzi watetezi huchukua muda mrefu bila sababu zozote za
msingi, kitu ambacho kinatupelekea kutoamini mhimili wa mahakama. Mfano: tathmini
fupi kwa watetezi waliofukuzwa UDSM, MUHAS na UDOM, toka 2011 hadi sasa 2014
kesi zao zimekuwa zikisua sua na kutoamuliwa kwa wakati, wakati zilifunguliwa chini
ya hati ya dharura undercertificate of Urgency. Kinyume na baadhi ya kesi za kisiasa
zinazoisha hata kabla ya mwaka mmoja ambazo hazikuonesha udharura wowote.

4.7 Watetezi UDSM wakiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi


Kisutu

Baadhi ya wanafunzi watetezi wa kike na wa kiume waliofukuzwa UDSM mwaka


2011 kwa sababu ya kuratibu maandamano ya kuwatetea wanafunzi wa mwaka wa
kwanza walionyimwa mikopo. Pichani wakitoka kwenye kesi iliyokuwa inawakabili katika
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu39.

Tukiwa Mahakama ya Mwanzo katika kesi iliyokuwa inamkabili Mtetezi wa wanafunzi


Mesaya Ismail kwa kosa la kuingia Mabibo hostel bila ruhusa (Trace pass) baada ya
kufukuzwa kwake Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam.

39 THE RESIDENT MAGISTRATES COURT OF DSM AT KISUTU CRIMINAL CASE NO. 270 OF 2011
REPUBLIC VERSUS MWAMBAPA ELIUS & 48 OTHERS- ACCUSED.

Sauti za watetezi wa haki vyuoni 31


Pichani ni Watetezi wakiwa Mahakama ya Mwanzo Kimara, Dar es Salaam, Tanzania
katika kesi iliyokuwa inamkabili mtetezi aliyefukuzwa UDSM mwaka 2011, ndugu Ismail
Mesaya mwenye shati jeupe katika picha40.

4.9 Hitimisho:

Hivi ndivyo changamoto ambazo watetezi wa haki za binadamu huwa


tunakumbana nazo mahakamani. pamoja na ukweli kwamba mara nyingine
tunapata misaada ya kisheria kutoka kwa mawakili wasomi lakini kadri muda
unavyoenda mawakili wengi wanashindwa kutoa ushirikiano. Kwa Mfano
Kesi ya Mtetezi Gervas Odillo Shayo aliyefukuzwa Chuo Kikuu Muhimbili
(MUHAS) mwaka 2011 ilishindwa kufika mwisho kwa sababu ya wakili wake
aliacha kutoa ushirikiano na kushindwa kufika mahakamani mara kadhaa.

40 Kesi namba KMR/4923/2012.

32 Sauti za watetezi wa haki vyuoni


Sura ya Tano

5.0 Madhara ya timua timua


Watetezi Vyuo Vikuu nchini.
5.1 Utangulizi:
Kuna madhara mbalimbali yanayotokana na athari za kuwatimua wanavyuo.
Miongoni mwa madhara hayo ni:

- Kushuka kwa hadhi ya vyuo vikuu nchini.


- Kuzika vyuo vikuu.
- Hasara kwa taifa.
- Wanafunzi wa kigeni kupata shuruba.
- Wanafunzi kupoteza nafasi zao za masomo.
- Kukosa rasilimali watetezi wa haki za binadamu vyuoni.

Tutazifafanua moja baada ya nyingine ili tuweze kueleweka


barabara.
- Kushuka kwa hadhi ya vyuo vikuu nchini:
Kitendo cha kuwatimua wanafunzi kutoka vyuoni kinashusha hadhi ya vyuo vikuu
nchini ambavyo vinahusika na tukio hili. Hii ni kwa sababu vyuo vikuu vinachangia
katika kuzima fikra huru za watetezi wa haki za binadamu; wakati Hayati Mwalimu
Julius Kambarage Nyerere aliwahi kusema kuwa Chuo Kikuu ni mahali pa kufikiria.
Kwa hiyo, inatarajiwa chuo kikuu kuwepo na fikra huru ambazo watawala wanajitahidi
kuzizima kwa nguvu zote.

- Kuzika vyuo vikuu visiwe visima vya fikra huru think tank of the nation.

Kupitia timua timua ya watetezi wa haki za binadamu, ni dhahiri kuwa imeua ari ya
wanafunzi wa vyuo vikuu kulitumikia taifa lao kufa na kupona, kwa kukemea kwa
vitendo serikali yao, na kuikosoa na kuishauri inapokosea. Watawala wa vyuo vikuu
wanataka wanafunzi wa vyuo vikuu wasihoji, wasishauri na wasiikosoe serikali au
mamlaka ya chuo pale inapobidi.

Sauti za watetezi wa haki vyuoni 33


- Hasara kwa taifa.
Hasara kubwa ambayo taifa hili imeipata ni kuua na kupoteza rasilimali watetezi
wa haki za binadamu ndani ya taifa letu. Watetezi wa haki za binadamu ni rasilimali
adimu na muhimu katika taifa lolote lile duniani. Aghalabu, watu huzungumza
kuhusu rasilimali madini, misitu, wanyama n.k. na kusahau kuwa hakuna rasilimali
muhimu kama watetezi wa haki za binadamu kwa sababu wao ni nguzo pekee kati
ya watawaliwa na watawala. Mfano kwa mujibu wa takwimu za UEUST-Chama cha
Watetezi waliofukuzwa UDSM ni zaidi ya wanafunzi 154 walifukuzwa vyuoni kati ya
2011-201441.

- Kupuuza rasilimali fedha za wananchi kodi za wananchi.

Kwa mujibu wa takwimu za Umoja wa Watetezi Waliofukuzwa Vyuo Vikuu Nchini


UEUST ni zaidi ya wanafunzi 9289 walisimamshwa masomo yao; na watetezi 154
waliofukuzwa vyuoni kati ya mwaka 2011 mpaka 2014. Hivyo ni zaidi ya watetezi 154
anaowafahamu waliofukuzwa vyuo vikuu tangu uhuru42.

Nitadadavua hasara ilipayo taifa kwa kumfukuza mwanachuo kwa kutumia wastani
wa wa mwanafunzi mmoja kwa mwaka 2011.

Na Huduma Maelezo ya mchanganuo wa fedha

1st year 2nd year 3rd year JUMLA


1 Ada 1,500,000 1,500,000 1,500,000 4,500,000
Fedha ya
2 450,000 450,000 450,000 2,700,000
chakula
Fedha ya
3 200,000 200,000 200,000 600,000
steshenari
Mazoezi kwa 7,500/= kwa
4 450,000
vitendo siku x siku 60

5 Jumla kuu 8,250,000/=


Jumla ya shilingi milioni nane laki mbili na elfu hamsini zinapotea kama mchanganuo

41 Taarifa hizi zinapatikana kwa kina katika Gazeti la Mtanzania ISSN 0856-5678. Toleo Na. 7308. Jumatano
mei 6, 2013. UK.3
42 Taarifa hizi zilitolewa na mwenyekiti wa chama cha watetezi waliofukuzwa vyuo vikuu Tanzania-UEUST

34 Sauti za watetezi wa haki vyuoni


unavyoonesha hapo juu, kwa mwanafunzi aliyekuwa anasoma miaka mitatu. Hivyo
ni wastani wa zaidi ya sh.8,250,000/= za Kitanzania zinapotea bila sababu za
msingi. Hivyo ni zaidi ya 1,237,500,000.00 zimetupwa au zimepotea kwa sababu ya
kuwafukuza watetezi wa haki za binadamu nchini, ambao ni wasomi kutoka katika
vyuo vyetu vya umma.

- Wanafunzi wa kigeni kupata shuruba:


Timua timua ya watetezi vyuo inaambatana na mushkeli mkubwa kutokana na matumizi
ya nguvu kutoka kwa vyombo vya ulinzi pale utawala wa chuo husika unapotangaza
kufungwa kwa chuo. Wanafunzi wa kigeni wanakosa mahala pa kukimbilia kwani wao
ni wageni, wanabaki kutaabika na shuruba mbali mbali katika nchi ya kigeni.

- Wanafunzi wengi hupoteza nafasi zao za masomo kwa masharti magumu


yanayotolewa warudipo vyuoni.
Kuna baadhi ya wanafunzi wa vyuo vikuu wanashindwa kuendelea na masomo yao
kwa sababu ya masharti magumu wanayopewa, kama vile kurudishwa kwa sharti
la kulipa ada yote ya muhula. Watetezi au wanafunzi wanaotoka katika familia za
kimaskini hushindwa kulipa ada husika kwa mkupuo ukizingatia watetezi husika
hunyimwa mikopo kwa ajili ya kumudu gharama za maisha wakiwepo chuoni43.

Nasema haya kwa niaba ya watetezi walio wengi ambao tumeteswa, tumenyanyaswa,
tumebezwa, tumepuuzwa, tumeshutumiwa, tumesingiziwa, tumetukanwa vya kutosha
kama utafiti wa kitabu hiki unavyojitanabaisha.

5.I Hitimisho:
Mambo ambayo yanatendeka ya uvunjwaji wa haki za kibinadamu kwa watetezi wa
wanyonge vyuoni, hayana budi kukomeshwa kwani yakiachwa yaendelee kwani
kuna hatari kubwa huko mbele ya safari tunakokwenda. Itafika sehemu wanyonge
hatutaona thamani ya sheria za nchi yetu, kwa sababu sheria si msumeno na
zinawalenga tabaka la wavujajasho, hivyo hatutaona thamani ya kuishi na hivyo
kukubali kupambana kwa ajili ya vizazi vijavyo! Wanyonge hatutathamini uhai wetu
zaidi ya mapambano na tutakuwa tayari kujitoa mhanga kwa ajili ya faida ya vizazi
vijavyo. Wanyonge tutaamua kuweka historia yetu kwenye taifa letu kwa mapambano
dhidi ya waliotuonea kwa muda mrefu.

43 Taarifa hizi alizitoa mtetezi aliyefukuzwa UDOM mwaka 2011, ndugu Lema Tumsifu alipo nipigia simu
juu ya kutafuta namna ya kutatua tatizo la mtetezi Philipo Mwakibinga aliyekuwa anatakiwa alipe ada yote
1500,000 mara baada ya kurudishwa chuo UDOM mwaka 2014.

Sauti za watetezi wa haki vyuoni 35


Sura ya Sita

6.0 Mapendekezo na Wito


6.1 Utangulizi:
Nawasihi sana watawala wa vyuo vikuu pamoja na serikali kwamba, suluhu ya
migogoro vyuoni sio mabomu, risasi na virungu; sio kuwapeleka watetezi magerezani;
sio kushughulikia matokeo ya matatizo, bali ni kushughulikia vyanzo vya matatizo.
Suluhu ya wanafunzi ni kuonana nao na kujadiliana nao kuhusu changamoto
zinazowakumba kwa pamoja, na sio kusubiri mpaka pale wanapogoma.

Katika kuwasihi watawala wa vyuo na serikali, wazingatie mambo yafuatayo:

- Serikali iwarudishe watetezi wote waliosimamishwa na kufukuzwa vyuoni kwani


wana haki ya kupata elimu kikatiba, na kutoendeleza utamaduni husika ili
kuepusha migogoro inayoweza kujitokeza kwa wanavyuo kushinikiza tawala za
vyuo na serikali.

- Serikali isipuuze rasilimali watetezi ambao wamesomeshwa kwa kodi za


wananchi kwa sababu za kisiasa au kulinda maslahi ya viongozi ndani ya serikali
wanaosababisha migomo na maandamano vyuoni.

- Mikopo itolewe kwa asilimia mia moja (100%) kwa kila mwanafunzi anayepata
fursa ya kuchaguliwa kuwa mwanafunzi wa chuo kikuu.

- kufanywa marekebisho ya sheria zinazoipa nguvu Bodi ya Mikopo [HESLB] ya


kubadili na kufanya mabadiliko ya sera mara kwa mara kwa wanafunzi wa elimu
ya juu nchini.

- Kiundwe chombo maalum ndani ya Wizara ya Elimu kitakachokuwa na jukumu


la kutathimini na kufanya tafiti za hali halisi za gharama za maisha na pesa
wanayokopeshwa wanavyuo, ili kufanya maboresho kwa kushauriana na Wizara
ya Fedha na Hazina ya Taifa, na sio kusubiri wanavyuo wagome na kuandamana.

- Serikali na watawala wa vyuo vikuu kujishughulisha na utatuzi wa vyanzo vya


migogoro na sio matokeo ya migogoro husika.

36 Sauti za watetezi wa haki vyuoni


- Serikali ifungue ofisi za Bodi ya Mikopo katika kanda mbali mbali ndani ya nchi,
kwani wanafunzi wengi wanahitaji huduma za bodi hii ya mikopo huko mikoani
kwao.

- Mikataba kati ya Bodi ya Mikopo na mwanafunzi uwe wazi katika vigezo vya
mwanafunzi mwenye sifa ya kudhaminiwa mikopo, kwa sababu, kuna usiri
mkubwa sana wa utoaji mikopo kwa wanavyuo. Hakuna kanuni formular
maalumu inayoweza kutuwezesha sisi waombaji mikopo kutambua ni kiasi gani
tutalipa kulingana na hali halisi ya mwombaji.

- Serikali ifungue akaunti maalum ya Bodi ya Mikopo kwa ajili ya wanafunzi wa elimu
ya juu ili kuondoa ukiritimba wa ucheleweshaji wa pesa kutoka Hazina kwenda
Bodi ya Mikopo. Pia Bodi ya Mikopo iingie mkataba na benki nyingine kama NBC,
NMB kuliko kutegemea kupitisha pesa kwenye Benki moja tu ya CRDB pekee;
na hao CRDB kusambaza fedha taratibu kwenye benki nyingine. Kitendo hiki
kinachosha na hufanya wanafunzi wenye akauti tofauti na CRDB kuchelewa zaidi
ya siku 4 ili kupata pesa zao wakati wenzao waliomo kwenye akaunti ya CRDB
wakiwa wameshapata na hivyo kuleta vurugu kwa wenzao.

- Serikali pamoja na vyama vya siasa visiingilie jumuiya na serikali za wanafunzi


vyuoni ili kupandikiza vibaraka wao kupitia uchaguzi wa serikali za wanafunzi. Kwa
mfano, mwaka 2009, miongozo iliyotolewa na serikali (GN 78) kama nilivyoelezea
katika vyanzo vya migogoro vyuoni, ilikuwa na lengo la kuingilia uhuru wa serikali
za wanafunzi vyuoni.

- Watetezi ndani ya vyuo vikuu wapewe uhuru wa kujadili masuala ya kitaifa,


kinyume na sasa ambapo, watawala wa vyuo husika hunyima uhuru wanafunzi
kukusanyika na kuwa na uhuru wa kutoa maoni, ili vyuo vikuu viwe ni visima vya
fikra huru katika taifa (think tank of the nation).

- Suluhu ya migogoro ya vyuo vikuu sio nguvu ya vyombo vya dola: mabomu na
risasi, virungu; lakini vile vile sio kuwasimamisha na kuwafukuza watetezi vyuo
vikuu, ila suluhu ni kutatua matatizo yanayowakabili au mambo wanayoyadai kwa
wakati sahihi.

- Watawala wa vyuo vikuu waondoe utamaduni wa uadui na wanavyuo, bali waweke


utamaduni wa kushirikiana katika matatizo yanayowakumba wanafunzi na jamii
kwa ujumla wake.

Sauti za watetezi wa haki vyuoni 37


- Uwekwe utaratibu maalumu wa wanafunzi wa vyuo vikuu kushiriki siasa wakiwa
vyuoni, kwani vyuo vikuu ni sehemu muhimu ya kuwazalisha viongozi wa taifa
letu, na ni sehemu muhimu kwa wanafunzi wa vyuo vikuu kujifunza siasa. Nchi
za wenzetu ikiwemo Uganda imeweka utaratibu wa wanafunzi wa vyuo vikuu
kushiriki siasa kwa utaratibu maalumu.

6.2 Hitimisho:
Kama tulivyojitahidi kuelezea katika sura hii, tumetoa mapendekezo kadha wa kadha
ambayo serikali, Bodi ya Mikopo, na watawala katika vyuo vikuu nchini hawana budi
kuyazingatia, ili kujenga jamii bora ya vijana wasomi kwa manufaa ya kizazi cha leo
na kesho.

6.3 Wito
6.3.1 Utangulizi:
Katika sehemu hii, nitatoa wito wangu kwa makundi mbalimbali yaliyopo katika jamii,
ili kila mmojawao ajue wajibu wake na majukumu yake katika mazingira ya kutetea
haki za watu wanyonge wa taifa hili. Wito ni kama ufuatavyo:

6.3.2 Asasi za Kiraia


Ninaomba asasi za kiraia zisisite kutusaidia watetezi wa haki za binadamu mara baada
ya kusimamishwa au kufukuzwa vyuoni. Watetezi tulichukua jukumu la kuzunguka
katika asasi mbali mbali za kijamii ili kuwaeleza ukweli juu ya kufukuzwa kwetu;
Kinyume na taarifa potofu ambazo watawala wa vyuo vikuu walizitoa kupitia vyombo
vya habari, zenye lengo la kuchafua taswira yetu mbele ya jamii.

Ninasisitiza na kuomba kuwa, AZAKI mbali mbali kama vile: Kituo cha Sheria na
Haki za Binadamu Legal Human Rights Center (LHRC); THRDC44, TGNP45; TLS46;
TAMWA47; TAWLA48; JUKATA49 na FORDIA kuendelea kujitolea kuwatetea watetezi wa
haki za binadamu.

44 Tanzania Human Right Defenders Coalition


45 TGNP-Tanzania Gender Networking Programme
46 TLS-Tanganyika Law Sociaty
47 TAMWA-Tanzania Media Womens Association
48 Tanzania Women Lawyers Association
49 JUKATA-Jukwaa La Katiba

38 Sauti za watetezi wa haki vyuoni


6.3.3 Msaada wa asasi Tanzania Human Rights Defenders
Coalition-THRDC.
Shukrani kwa asasi hii kwa kunisaidia msaada wa kisheria mara baada ya kufukuzwa
kwangu mara ya pili Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Ni imani yangu kwamba asasi
hii itaendelea kusaidia misaada ya kisheria kwa watetezi wa haki za binadamu kwani
imekuwa ikijitoa sana katika matatizo yanayowakumba watetezi wa haki za binadamu.

Huyu ni Mr. Onesmo


Olengurumwa, Mratibu
Taifa na Mkurugenzi Mkuu
katika Taasisi hii ya Kutetea
Haki za Watetezi wa Haki
za Binadamu na ndiye
aliyekukubali kudhamini
kitabu hiki, kilichobeba
hali ya ukiukwaji wa haki
za watetezi vyuoni nchini
Tanzania.

Mh. Hellen Kijo Bisimba Mh. Mabere Marando Mh.Kibatara

Pichani, Picha Mbili kulia ni mawakili waliojitolea kutetea haki za wanafunzi watetezi
waliofukuzwa Vyuoni tangu 2011-2017. Picha moja kushoto ni Mkurugenzi wa Kituo Cha
Sheria na Haki za Binadamu-LHRC , Mh. Hellen Kijobisimba ambaye alisaidia sana kutoa
msaada wa kisheria kwa watetezi tuliofukuzwa vyuo.

Sauti za watetezi wa haki vyuoni 39


6.3.4 Wito kwa watetezi wa haki za binadamu juu ya usalama wetu:
Pamoja na ukweli kwamba, Azimio la Watetezi wa Haki za Binadamu lililoanzishwa
rasmi 1998 linasisitiza kuwa, nchi/dola ndiyo ya kwanza katika kuwalinda watetezi
wa haki za binadamu. Mlinzi wa kwanza wa mtetezi yoyote ni mtetezi mwenyewe
lakini hatuna budi kutengeneza mtandao wetu wa ulinzi ili kujilinda na mashambulio
ya namna yoyote dhidi yetu. Nasema haya kwa kuwa bado serikali yetu inahitaji elimu
ya kutosha juu ya jukumu lao kama dola, kuwalinda na kuwatetea watetezi wa haki za
binadamu TANZANIA.

6.4 Wito
Napenda kutoa wito jumuishi kwa makundi mbalimbali ambayo wakati wa mapito
yetu watetezi tumepata kuyafikia ili kuomba kuingilia kati uonevu tuliofanyiwa
mathalani Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jeshi la polisi, watawala wa
Vyuo Vikuu Tanzania, Serikali za Wanafunzi Vyuoni, Jumuiya ya Wanafunzi TAHLISO,
taasisi za kidini, Vyama vya Siasa, Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
watu binafsi na jamii kwa ujumla wake. Kutokuwa na mitazamo hasi dhidi ya Watetezi
wa haki za binadamu. Watetezi ni nguzo pekee kati ya watawala na watawaliwa na
dhamira yao kuu ni kusaidia kuwasemea walioonewa.

6.9 Hitimisho.
Mwandishi anahitimisha sura hii kwa kusisitiza kwamba, elimu juu ya haki za
binadamu haina budi kutolewa kwa kila mtu ili tujenge jamii ya watu wanaozilinda
na kuzitetea. Nashauri Azaki zote zinazojihusisha na masuala ya utetezi wa haki za
binadamu zifanye harakati shirikishi na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
ili ziwekeze kikamilifu katika kutoa elimu juu ya haki za binadamu.

40 Sauti za watetezi wa haki vyuoni


Sura ya Saba

7.0 Matokeo ya harakati


zilizofanywa na Watetezi Vyuoni.
7.1 Utangulizi
Pamoja na ukweli kwamba watetezi tulitolewa mbuzi wa kafara baada ya kuibua
ufisadi wa fedha za mikopo ya wanafunzi mwaka 2011 ambapo baada ya siku mbili tu
Serikali kupitia Bodi ya Mikopo (HESLB) iliwadhamini mikopo wanafunzi wengi ndani
ya vyuo vikuu vya umma nchini. Mnamo tarehe 17 .08.2016 baada ya miaka mitano (5)
Waziri wa Elimu, Prof. Joyce Ndalichako alivitaka Vyuo Vikuu takribani 31 kati ya 81,
kurejesha fedha walizozipokea ambazo ni za wanafunzi hewa. Haya yote ni matokeo
ya uhojaji wa watetezi tangu mwaka 2011. Lakini vile vile alifanya maamuzi dhidi ya
wakurugenzi wanne wa bodi ya mikopo kwa sababu ya madhaifu yao ya kiutendaji.

Pichani kushoto ni ni Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa


Joyce Ndalichako aliyevunja mkataba wa Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Mikopo ya Elimu
ya Juu (HESLB) nchini, George Nyategi na kuwasimamisha kazi wakurugenzi wengine
watatu huku akitaka uchunguzi ufanyike haraka.

Pichani upande wa kulia ni wanafunzi wakitawanywa na mabomu yaliyopigwa na Jeshi


la polisi lililotanda eneo la geti maji ndani ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwaka 2011
wakati wa Maandamano ya Wanafunzi kuelekea Ikulu, ili kumpelekea taarifa za uwepo
wa mikopo hewa na madhaifu ya kiutendaji ya Bodi ya Mikopo Mh. Raisi, Jakaya Mrisho
Kikwete.

Sauti za watetezi wa haki vyuoni 41


7.2 Mtetezi Alphonce Lusoko akifukuzwa kwa mara ya pili UDSM
2017.
Mnamo tarehe 30.01.2017, Mtetezi Alphonce Lusako akiwa katika ratiba yake ya
mitihani alifukuzwa tena na Utawala wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM)
baada ya miaka sita kuruhusiwa kusoma tena.

Pichani kushoto ni Alphonce Lusako akitafakari uonezi dhidi ya haki yake ya kupata Elimu
kwa takribani miaka sita sasa, pichani kushoto akiondoka ndani ya Chuo Kikuu cha Dar
es Salaam baada ya kufukuzwa kwake

Pichani ni Mtetezi Alphonce Lusako alipoamua kuwaeleza watanzania kupitia vyombo vya
habari uonezi unaomkabili katika harakati za kupata elimu ndani ya Nchi yake. Alisema :

42 Sauti za watetezi wa haki vyuoni


Kabla ya kueleza, undani wa sakata la kufukuzwa kwa mara ya pili Chuo Kikuu cha Dar
es Watanzania, jueni kwamba ninaonewa, ni takribani miaka sita sasa, napambana
kuitafuta haki yangu ya kusoma bila mafanikio, nimezunguka nchi hii, kuomba,
Viongozi wenye mamlaka na Elimu wanipatie haki yangu ya kusoma bila mafanikio.

Kihistoria(Hatua Tulizozichukua)
Watetezi tuliofukuzwa kwa sababu ya mgomo tuliouratibu wa kupinga kuwarudisha
wanafunzi wa mwaka wa kwanza nyumbani kwa hoja hafifu kwamba bajeti haitoshi
huku kukiwa na mikopo hewa lukuki, tulianza kufanya hatua za ndani ya Chuo,
tukakata rufaa dhidi ya maamuzi ya kutufukuza na kutufuta katika mfumo wa elimu,
Tukaomba baraza la Chuo (UDSM) Lirejee maamuzi husika yenye lengo la kupoka haki
yetu ya kusoma katika vyuo vya umma nchini. Baraza la chuo lilikataa maombi yetu.

Tulishitakiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika Mahakama ya


Hakimu Mkazi kisutu (Criminal case No. 270 ya 2011). kwa makosa makuu mawili,
mosi, Kufanya Mkusanyiko usio halali, pili kukaidi amri halali ya polisi iliyotutaka
tutawanyike. Mnamo tar. 30.08.2012, Tulishinda kesi hii kwa Mahakama kutupilia mbali
shitaka husika. Tuliporudi Chuoni, Wanafunzi takribani 12 kati ya 51 tukabaguliwa bila
sababu za msingi na hatukurudishwa.

Tukaanza njia za kidiplomasia tena, tulizunguka nchi hii kwa kila kiongozi mwenye
mamlaka na sekta ya Elimu, tukiomba huruma yao ya kuturudisha Chuoni tumalize
shahada zetu. Tuliandika barua kwa Mkurugenzi wa Vyuo vikuu, Waziri wa Elimu, Mh.
Shukuru Kawambwa kwa wakati huo, Waziri Mkuu, Mh. Mizengo Pinda, Waziri wa
Mambo ya Ndani, Mh. Nahodha vuai kwa wakati huo ambaye tulimuomba atusaidie
suala letu la kesi mahakamani. Tuliomba Tume ya Utawala bora na haki za Binadamu
iingilie kati, Tuliomba Bunge La jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia kamati
maalumu iliyokuwa inaongozwa na Mh. Magreth Sitta, kuingilia kati. Hatua zote hizi
hazikuleta suluhisho.

Baada ya hatua zote hizo kushindikana, tuliona kutafuta haki yetu Mahakamani ndio
njia pekee. Tuliomba msaada katika taasisi zinazotoa msaada wa kisheria, Kituo cha
Sheria na haki za binadamu (LHRC) na Tanganyika Law Sociaty (TLS), tukapatiwa
mawakili ambao wamepambana miaka yote kututea (takribani miaka 5) mahakamani
ili tupate haki yetu ya kusoma bila mafanikio, tulianza Mahakama ya Hakimu Mkazi
kisutu, tukakata rufaa mahakama kuu, tukakata rufaa mahakama ya Rufaa (Appeal
Court of Tanzania). Ilipofika mwaka 2016, nikaona niachane na masuala ya kesi kwani
ni muda mrefu nipo mahakamani. Nikatoa faili langu mahakamani.

Sauti za watetezi wa haki vyuoni 43


Nikaamua kuingia katika diplomasia tena. tukamuandikia Mh. Raisi (John Pombe
Makufuli) kuomba aingilie kati mgogoro huu ili tupate haki yetu ya kusoma nchini.
Tukashukuru Mungu, Wasaidizi wa Mh. Raisi katika masuala ya Elimu na Sheria
walionyesha Ushirikiano, tumekaa vikao mara kadhaa Ikulu, wakamshirikisha
Mkurugenzi wa Vyuo vikuu, wakaishirikisha wizara ya Elimu na Mkurugenzi Mtendaji
wa Tume ya Vyuo Vikuu (TCU), wakati huo akiwa ni Prof. Yunus Mgaya.

Mnamo tar 12. 02. 2016, TCU waliwaandikia barua rasmi Chuo (UDSM) kwamba kwa
mujibu wa sheria ya vyuo vikuu [Universities reguration 43(1) GN 226 ya mwaka 2013,
Mwanafunzi aliyefukuzwa Chuo kwa masuala ya kinidhamu anaruhusiwa kuomba
Chuo kwa mara nyingine tena baada ya miaka miwili kupita, katika chuo hicho hicho
au vyuo vingine tangu kufukuzwa kwake (Barua imeambatanishwa), hivyo akakiomba
Chuo kitupe Ushirikiano.

Kutokana na Ushauri husika, mwaka 2016 nikaomba udahili katika Vyuo vikuu vitatu
ikiwemo UDSM. TCU wakanichagua nisome UDSM shahada ya Uchumi (Economics)
kipaumbele changu cha pili baada ya Sheria, kwa kuwa ndoto yangu ni kusoma
shahada ya Sheria, nikaanza hatua za kubadilisha kozi kuelekea Shahada ya Sheria,
Utawala wa UDSM, Ulinipa Ushirikiano kwa kugonga mihuri ya kukubali kubadilisha
kozi yangu, hadi DVC Undergraduate UDSM, alithibitisha uhamisho wangu.

Baada ya miezi minne kupita tangu aanze masomo yake, katika hali ya sintofahamu
mnamo tar 30.01.2017akiwa katika ratiba yake ya mtihani akapewa barua ya
kusimamishwa uanafunzi wake kwa kile kinachodaiwa kwamba alidahiliwa kimakosa
na hivyo kusimamishwa rasmi masomo katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
Sio siri, nilishtushwa na niliumizwa sana kibinadamu ni masuala magumu sana ila
namuachia Mungu anitetee alisema Lusako

Alisisitiza kwamba Prof. Rwekaza Mkandala atambue, Kumnyima mtoto wa masikini


elimu, ni sawa na kumpiga risasi afe katika nchi yake. Hakuna dhambi kuu niliyoitenda
nchi hii, nikastahili adhabu ya kupokwa kabisa haki yangu ya kusoma milele. Lusako
alisema:

Chuo kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), ni chuo kikuu cha umma, ni chuo kilichojengwa
na kodi za watanzania, ni chuo kilichojengwa na jasho la kila mtanzania. Hivyo kila
mtanzania mwenye sifa kwa mujibu wa kanuni, taratibu na sheria, anapaswa kusoma
katika chuo hiki bila kubaguliwa. Natamani kuona nchi hii inaongozwa kwa mujibu wa
katiba na sheria . Tukiendelea kuongoza vyuo vikuu , kwa visasi, kwa chuki binafsi,
neno la mtu likawa sheria, watawala wa vyuo vikuu wakawa juu ya sheria, tutaliingiza
taifa hili katika gharama za machafuko.

44 Sauti za watetezi wa haki vyuoni


9.5 Hitimisho.
Kwa tafiti alizozifanya mwandishi, watetezi wengi kwa asilimia kubwa huwa
hawafanikiwa kudhaminiwa ili wamalizie shahada zao au waanze upya shahada
ziingine. Ninaomba wadau wa maendeleo na wanaoamini kuwa watetezi wa haki za
binadamu ni nguzo pekee kati ya wananchi na serikali, na kwamba ni watu muhimu
katika kutetea haki za bianadamu, wajitolee pale wanapoona watetezi wa haki za
binadamu wanapokwa haki yao ya msingi, kwa sababu ya kutetea haki za binadamu
wenzao.

Sauti za watetezi wa haki vyuoni 45

You might also like