Professional Documents
Culture Documents
Kwa sasa Tanzania ndio Mwenyekiti wa Umoja huo kwa kipindi cha mwaka mmoja,
baada ya kupokea Uenyekiti kutoka Jamhuri ya Zimbabwe iliyomaliza muda wake
mwezi Agosti, 2017, ambapo Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. PHILIP ISDOR
MPANGO (MB), ambae pia ni Mwenyekiti President of the Council ataongoza
Mkutano huo.
1
Katika Mkutano huo, pamoja na masuala mbali mbali yatakayojadiliwa, Serikali ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, itatumia fursa hiyo kuwasilisha Taarifa ya hatua
iliyofikia katika utekelezaji wa Mpango wa Financial Action Task Force (FATF)
ulioasisiwa mwaka 2009.
Tanzania ni miongoni mwa Nchi waanzilishi wa Umoja huo ulioasisiwa jijini Arusha,
mwaka 1999, Nchi nyingine ni Uganda, Kenya, Mauritius, Namibia, Sychelles
na Swaziland ambazo zilisaini makubaliano (Memorandum of Understanding - MOU).
Hatua ambayo ilisababisha Makao Makuu ya Sekretariati ya Umoja huo wenye nchi
wanachama (18) ambazo ni Angola, Botswana, Ethiopia, Kenya, Lesotho,
Madagascar, Malawi, Mauritius, Msumbiji, Namibia, Rwanda, Afrika Kusini,
Swaziland, Sychelles, Tanzania, Uganda, Zambia na Zimbabwe kuwa jijini
Dar es Salaam Tanzania.
IMETOLEWA NA:
KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO.