Nukushi: 026-2322128 Ghorofa ya Nane, Baruapepe: km@habari.go.tz Makole Uhindini, Tovuti: www. habari.go.tz S. L. P 25, DODOMA. 40481. TAARIFA KWA UMMA
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison G. Mwakyembe
ametuma salamu za pole kwa familia ya aliyekuwa mwandishi wa habari nguli na Mkuu wa Wilaya za Handeni na Morogoro, Ndugu Muhingo Rweyemamu, kilichotokea jana tarehe 2 Septemba, 2017.
Waziri Mwakyembe ameeleza kupokea kwa mshituko na masikitiko taarifa za
kifo cha Muhingo ambaye mwezi Juni mwaka huu alikwenda kumjulia hali hospitali ya AgaKhan alipokuwa amelazwa na kuonyesha dalili za matumaini.
"Kifo chake ni pigo kubwa kwa wanatasnia na wadau wa habari wote na
wananchi aliowahi kuwaongoza katika uhai wake, naiombea familia ya marehemu, ndugu na marafiki waweze kupita kipindi hiki kigumu na Mungu awape nguvu na ujasiri", amesema Dkt. Mwakyembe.
Bwana alitoa na Bwana ametwaa, jina lake lihimidiwe.
Imetolewa na:
Lorietha Laurence Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo. 03/09/2017.