Professional Documents
Culture Documents
OFISI YA RAIS
Simu Na: +255 (026) 2963630 Menejimenti ya Utumishi wa Umma
Nukushi: +255 (026) 2963629 na Utawala Bora,
Barua Pepe: ps@utumishi.go.tz Jengo la Taaluma Na. 1,
Tovuti:http://www.utumishi.go.tz Chuo cha Masomo ya Biashara na Sheria,
Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM),
Barabara ya Mkalama,
S.L.P. 670,
40404 DODOMA.
Utangulizi
Utumishi wa Umma una wajibu wa kuleta ustawi kwa wananchi kwa kutoa huduma, ili
kuweza kufikia lengo hilo la Serikali, ni dhahiri kuwa Utumishi wa Umma hauna budi
kuendeshwa kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu; kutanguliza maslahi ya taifa na
kuzingatia Maadili katika utendaji wa kila siku. Sheria ya Utumishi wa Umma Sura 298
(Kifungu cha 34) kinaipa Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma (OR-MUU)
mamlaka ya kukuza na kufuatilia uzingatiaji wa Maadili katika Utumishi wa Umma.
Katika kutekeleza jukumu hilo, OR-MUU imekuwa ikiendelea kuunga mkono juhudi za
serikali katika suala la usimamizi wa Maadili kwa kutoa miongozo inayosimamia Maadili,
kufanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa miongozo hiyo, kutoa mafunzo na elimu kwa
umma.
1
Bidii ya Kazi;
Kutoa Huduma bila Upendeleo;
Kufanya kazi kwa Uadilifu;
Kuwajibika kwa Umma;
Kuheshimu Sheria; na
Matumizi sahihi ya Taarifa.
Utoro kazini:- baadhi ya watumishi wamejenga mazoea ya kutofika kazini bila sababu
ya msingi kinyume na Kanuni 57 ya Kanuni za Utumishi wa Umma za mwaka 2003 na
Kanuni za Maadili ya Utendaji katika Utumishi wa Umma. Tutambue kwamba kutofika
kazini kwa zaidi ya siku tano bila sababu ya msingi ni kosa na mtumishi anapaswa
kuchukuliwa hatua za kinidhamu na adhabu yake ni kufukuzwa kazi, punguzo la
mshahara/kushushwa cheo.
2
na matumizi sahihi ya taarifa. Kwa mujibu wa Sheria ya Usalama wa Taifa Na. 3 ya
mwaka 1970 na marekebisho yake, Ibara ya 5(a)&(b) , adhabu ya uvujaji wa siri ni
Kifungo kisichozidi miaka 20.
Ifahamike, lengo la Serikali si kuficha taarifa kwa wadau ila taarifa zinazotolewa
zinapaswa kupelekwa kwa ambao wanapaswa kupokea taarifa hizo (walengwa). Aidha
utoaji wa taarifa unapaswa kufuata utaratibu wa utoaji wa taarifa na zipate idhini kwa
Mtendaji wa Taasisi kabla ya kupelekwa kwa wadau.
3
Hitimisho
Usimamizi wa Maadili ni suala shirikishi hivyo kila mmoja katika nafasi yake anapaswa
kuchukua hatua ili kuleta mabadiliko na hatimaye kuboresha utoaji wa huduma.
Pili, Watumishi wa Umma wakumbuke wajibu wao kwa wananchi kwa kufanya kazi kwa
kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu zilizopo. Watumishi waache kufanya kazi kwa
mazoea na kutimiza wajibu wao kwa wananchi.
Mwisho, kwa kuwa suala la Maadili linaanzia katika ngazi ya familia, wananchi
wanaombwa kushiriki kikamilifu katika kufichua vitendo vya ukiukwaji wa Maadili katika
Utumishi wa umma kwa kutoa taarifa kwa Mamlaka zinazohusika na kutumia madawati
ya malalamiko yaliyo katika Taasisi za Umma. Pia, endapo kuna taarifa na uthibitisho
wa watumishi ambao bado wanaendelea kutumia vyeti ambavyo sio vyao au hawapo
katika vituo vyao vya kazi bila sababu ya msingi (utoro) huku wakiendelea kupokea
mshahara wa Serikali mnaombwa kuwasilisha taarifa hizo kwa Katibu Mkuu Ofisi ya
Rais- Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa hatua.