You are on page 1of 17

KUKU NI DHAHABU-EV PETER KILEZU

UCHUMI NA MAENDELEO YA MKRISTO


UCHUMI WA KIBIBLIA (RELIGIUS ECONOMY)
Isaya 48:17
17 Mimi ni Bwana Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida.

1. UCHUMI
Uchumi ni namna (maarifa) ya mtu kutumia rasilimali zilizopo kwa madhumuni ya kutimiza
mahitaji na matakwa yake kwa njia nafuu /bora zaidi.

T6

Mahitaji

Matakwa

A. MAHITAJI ni mambo yote ya lazima/msingi yanayowezesha maisha ya kila siku ya


mwanadamu.
1 Timotheo 6:8 “6.Lakini utauwa pamoja na kuridhika ni faida kubwa. 7 Kwa maana hatukuja
na kitu duniani, tena hatuwezi kutoka na kitu; 8 ila tukiwa na chakula na nguo tutaridhika na
vitu hivyo. 9 Lakini hao watakao kuwa na mali huanguka katika majaribu na mtego, na tamaa
nyingi zisizo na maana, zenye kudhuru, zinazowaingiza watu katika upotevu na
uharibifu. 10 Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine
hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi”.

1
KUKU NI DHAHABU-EV PETER KILEZU

Mtaalamu ajulikanae kama MASLOW ameyatazama mahitaji ya mwanadamu katika makundi


matano ambapo kundi la kwanza limebeba mahitaji ya lazima ya mwanadamu ambayo ni
CHAKULA, MAJI NGUO NA MAKAZI.
Maslow's hierarchy of needs is a motivational theory in psychology comprising a five-tier model
of human needs, often depicted as hierarchical levels within a pyramid.
From the bottom of the hierarchy upwards, the needs are: physiological (food and clothing),
safety (job security), love and belonging needs (friendship), esteem, and self-actualization.
Needs lower down in the hierarchy must be satisfied before individuals can attend to needs
higher up.

Needs point out the something you must have for survival.


Wants refers to something which is good to have, but not essential for survival.

2
KUKU NI DHAHABU-EV PETER KILEZU

For the purpose of spending and saving money wisely, every person must know the difference
between needs and wants.
B. MATAKWA: ni yale mambo yote yanapokosekana hayakwamishi maisha ya
mwanadumu kuendelea.

2. MAENDELEO.
Maendeleo ni hali ya mtu kutoka katika kiwango cha maisha duni na kupiga hatua
kuishi katika kiwango cha maisha bora zaidi.

SWALI:
1. Kwa mtazamo wako umeelewa nini kuhusu uchumi?
2. Kwa mtazamo wako umeelewa nini kuhusu Maendeleo?

MPANGO WA MUNGU KWA MWANADAMU


Mwanzo 1:26-28 Kusudi la Mungu tangu awali, ni sisi binadamu, kuitawala dunia na
mazingira yake, na sio kutawaliwa na mazingira.

KUTAWALA MAZINGIRA TULIYOPEWA NA MUNGU KUNATUWEZESHA KUMTUMIKIA NA


KUMWABUDU MUNGU WETU KWA UHURU.
Lengo 1. Kutumia rasilimali tulizopewa na Mungu wetu ili kuinua hali ya uchumi wetu.
Lengo 2. Kuimarisha mahusiano yetu na Mungu.
Mazingira ni nini:-
 Mwanzo 1 (siku tano za kwanza Mungu alikuwa anashughulikia mazingira.
 Zaburi 24:1 (Dunia na vyote viijazavyo ni mali ya Bwana)
 Kumb 8:6-20
 Neno mazingira linajumuisha vitu vyote vinavyotunguka vikiwemo viumbe hai na
visivyo hai mf hali ya hewa, wanyama, mimea, udongo, milima, mabonde, bahari na
miundombinu.
Ni kusudi la Mungu kwa Mwanadamu awe na mahitaji ya lazima kwa wingi.

3
KUKU NI DHAHABU-EV PETER KILEZU

 2 Wakorintho 9:8-13
 Mwanzo 1:24-31
2 wakorintho 9:8-13 hapa kuna maswali matatu muhimu sana ya kujiuliza
1. Kwa nini hatuna Neema hizi kwa wingi.
2. Kwa nini hatuna Riziki za kila namna sikuzote
3. Kwa nini hatuzidi sana katika kila tendo jema
Tuangalie suala la “Mkiwa na Riziki za kila namna siku zote”
Mahitaji ya lazima kwa mwanadamu yanatazamwa kwa namna mbili kuu
1. Ki-dunia ( kama inavyoelezwa hapo juu kwenyemchoro wa pembe tatu)
2. Ki-biblia ( kama inavyoelezwa kwenye 1 Timotheo 6:8)
Tunapataje Riziki
Kuna namna nyingi za halali na zisizo za halali za mtu kujipatia Riziki. Mungu amempa
mwanadamu rasilimali nyingi tena za kutosha ili zimsaidie kujipatia riziki kwa njia za halali tu.
Mwanadamu anaweza kupata riziki ya kila namna kutoka katika vyanzo vilivyotajwa hapa
chini ingawa ni baadhi tu vyanzo hivyo:-
1. Kilimo
2. Ufugaji
3. Viwandani
4. Uchimbaji madini
5. Uvuvi
6. biashara
Muda haututoshi kuzitazama zote. Muda huu kutazama namna mojawapo ya njia ya
kujipatia Riziki ambayo ni:-
1. Njia ya asili ambayo ilibuniwa na Mungu mwenyewe
Mwanzo 1:24
Biblia inatoa ushahidi wa kutosha ya kwamba katika UFUGAJI mtu aliyesoma na asiyesoma
wote wanaweza kuwa na maisha yanayofanana yaani ya kuwa na Riziki za kila namna siku
zote kama Mungu alivyopanga hata kabla ya mwanadamu kuwepo
Mithali 27:23
 Kufanya bidi kuijua hali ya makundi yako
Hapa Mungu anamaanisha kuwa kazi ya ufugaji inahitahi usimamizi
madhubuti/makini/tumaanishe/usimamizi bora/imara kama ilivyo katika usimamiaji wa
shughuli zingine kama za miradi ya kijamiin n.k.

4
KUKU NI DHAHABU-EV PETER KILEZU

Sababu ya kufanya bidii ya kujua hali ya makundi yako ni mali huwa si ya milele

 Makundi : hapa hatuzunguzii aina moja ya wanyama wafugwao biblia imemaanisha


makundi kama yalivyotajwa kwenye AYUBU 1:3
Mungu ametuhakikishia wanadumu usalama wetu kwenye eneo la chakula na mahitaji
mengine ya lazima na yale ya Muhimu (Mithali 27:23) kuyapata kwenye mifugo kwa
mfano:-
 Kondoo- mnyama huyu anauwezo wa kumvisha mavazi mwanadamu
 Mbuzi- Mnyama huyu anauwezo wa kumnunulia mwanadamu kiwanja/shamba
 Mbuzi – maziwa
 Chakula
 Posho.

Kwa kuwa mpango huu ni mwema sana kwa Mungu, wakati mwingine mwanadamu
anakosea kama ilivyokuwa kwa wakati wa Nuhu, utaona kuwa mwanadamu muovu
aliangamizwa cha ajabu kila aliyepata Neema machoni pa Mungu alipewa nafasi ya
kuendelea kufuga mwanzo 9:10

UFUGAJI SIO KAZI YA ZIADA

Familia za wakirsto waishio kwenye umasikini zimeonesha bidii kubwa katika kuombea
hali ya uchumi wa familia zao, maombi ambayo kwa sehemu kubwa yamekosa tija kwa
kuwa familia hizi hazijawa tayari kutawala mazingira, wakati Fulani maombi yao yanadai
uchumi huu utoke mbinguni aliko Mungu, jambo ambalo si sawa. Kwani katika siku 5 wa
kwanza za uumbaji zilifanya mambo mengi pamoja na uchumi wa mwanadamu.
Tunahitaji akili tu kutambua na kuchukua hatua.

Kuishi bila hawa wanyama ni kuishi nje ya mpango na kusudi la Mungu. Tangu
mwanzo Mungu alikusudia mahali popote atakapokuwa mwandamu aishi akiwa
amezungukwa na wanyama. Ukiwakataa au kuwafukuza usidhani watakwenda porini,
watapotelea mtaani.

UFUGAJI WA KUKU WA ASILI WENYE TIJA

MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA KATIKA UFUGAJI WA KUKU WA ASILI


1. Banda bora

5
KUKU NI DHAHABU-EV PETER KILEZU

Ni muhimu kuwajengea kuku banda bora ili wapate kujikinga na mvua, baridi, wezi
na wanyama. Banda la kuku linaweza likajengwa kando kando au nyuma ya nyumba
ya kuishi. Banda la kuku linaweza kujengwa kwa kutumia raslimali za misitu
zinazopatikana kwa urahisi kwenye eneo husika.
 N.B. Jua ni muhimu katika kuhakikisha vitamini A na D zinatumika vizuri
mwilini, kwahiyo banda ni lazima lijengwe kwa mtindo ambao
unaruhusu mwanga kupita hasa nyakati za asubuhi na jioni.

2. Kuchagua kuku bora wa kuendeleza kizazi.


Mafanikio zaidi katika kuchagua kuku wa kuendeleza kizazi yatapatikana iwapo
uchaguzi na uchambuzi wa kuku wanaozaliwa utafanywa mara kwa mara ili kupata
kundi la kuku litakalofaa kwa sifa zote katika uzalishaji. Sifa hizo ni pamoja na
kupevuka haraka, kutaga mayai mengi, kuwa na uzito mkubwa na nyama nyingi kwa
umri mdogo.
3. Chakula cha Kuku
Kuku wana mahitaji tofauti ya vyakula kulingana na umri (vifaranga, wanaokua,
wakubwa) na uzalishajili (utagaji au unenepeshaji). Ili kuku waweze kukua vizuri,
kunenepa na kutaga mayai mengi ni lazima wale chakula cha kutosha na chenye
ubora unaotakiwa kulingana na uhitaji wa miili yao. Lishe bora huzuia magonjwa
mengi ya kuku hivyo ni muhimu kuku wapewe virutubisho muhimu. Ubora wa lishe
ya kuku unaweza kuainishwa katika makundi ya vyakula kama ifuatavyo:
i. Vyakula vya kutia nguvu (asili ya wanga),
ii. Vyakula vya kujenga mwili (asili ya protein),
iii. Vyakula vya kuimarisha mifupa (Asili ya madini),
iv. Vyakula vya kulinda mwili (Asili ya vitamin), na
v. Maji
Makundi ya vyakula.
i. Vyakula vya kutia nguvu
Hivi ni vyakula asili ya wanga vyenye kutoa nguvu katik mwili wa kuku.
Huchangia asilimia 60-75 ya mchanganyiko wote wa chakula. Vyakula vya
mifugo vifuatavyo vipo katika kundi hili:
a. Nafaka kama vile chenga za mahindi ,chenga za mchele, uwele , mtama
na ulezi.
b. Pumba za mahindi, pumba laini za mpunga, na, pumba laini za ngano.
c. Mimea ya mizizi kama vile muhogo na viazi vitamu. Kabla ya kulisha kuku
hakikisha mizizi hiyo inalowekwa kwa muda wa saa moja au kupikwa
kabla ya kukaushwa ili kuondoa sumu ambayo kwa asili imo katika
vyakula vya aina hii. Inashauriwa kuwa  mizizi hiyo ilishwe kwa kiasi cha
asilimia 10 ya chakula chote anacholishwa kuku.
ii. Vyakula vya kujenga mwili (Protini)

6
KUKU NI DHAHABU-EV PETER KILEZU

Hivi ni vyakula vya asili ya protini na huchangia asilimia 20 hadi 30 ya


mchanganyiko wote wa chakula cha kuku.
Mfano wa vyakula katika kundi hil:
a. Mashudu: Aina zote za makapi ya mbegu za mimea aina ya mikunde na
vyakula vinavyotoa mafuta mfano alizeti, karanga, soya, mawese, ufuta
na korosho.
b. Damu ya wanyama iliyokaushwa (waliochinjwa na kukaguliwa).
c. Mabaki ya nyama, samaki/dagaa.
d. Wadudu kama vile minyoo, mchwa na mayai ya mchwa.

iii. Vyakula vya kuimarisha mifupa


Hivi ni vyakula vya madini ambavyo huhitajika kwa ajili ya kujenga mifupa na
maganda ya mayai. Huchangia 3-5 ya mchanganyiko wote. Madini ya
muhimu ni madini ya chokaa (calcium) na fosiforasi (phosphorus).
Unapoongeza madini ya fosforasi inakubidi uongeze pia madini ya chokaa
kwani uwiano wa kiasi cha aina moja ukizidi kuliko wa aina nyingine
husababisha upungufu wa kile kidogo
Kabla maganda ya mayai na nyumba za konokono havijatumika inashauriwa
yachomwe moto mkali au yachemshwe ili kuua vimelea vya maradhi. Vyanzo
vikuu vya madini:
a. Mifupa iliyochomwa na kusagwa, maganda ya mayai na konokono
yaliyosagwa.
b. Chumvi ya jikoni.
c. Madini yaliyotengenezwa viwandani kama vile dicalcium phosphate.
d. Magadi

iv. Vyakula vya kulinda mwili


Vyanzo vikuu vya kundi hili ni:
a. Mbogamboga kama vile Mchicha,mchicha pori, Chinese kabeji n.k.
b. samadi ya ng’ombe ambayo haijakaa muda mrefu.
c. Mchanganyiko wa vitamini uliotengenezwa na viwanda vya madawa
(vitamin premix).

v. Maji.
Mwili wa Ndege/Kuku umebeba 70% ya maji na yai lake lina 65%. Kuku
anahitaji maji ya kutosha kwa muda wote. Kuku anahitaji maji safi na salama
ili yamwezeshe kumeng’enya chakula, kuondoa taka mwilini na kurekebisha
hali ya joto mwilini. Ukosefu na upungufu maji kwa kuku huchangia kwa kiasi
kikubwa kudumaa na kuathilika vibaya mfuko wake wa chakula hatimaye
hufa.

7
KUKU NI DHAHABU-EV PETER KILEZU

4. Kutoa Tiba na Chanjo za Kudhibiti magonjwa ya kuku


a. Magonjwa
i. Magonjwa Muhimu ya Virusi.
1. Mdondo/Kideri (Newcastle Disease)
Ni ugonjwa unaosababishwa na virusi ambao hushambulia aina
zote za spishi za ndege, ijapokuwa kuku ndio aina inayoathirika
zaidi. Binadamu na wanyama wengine pia wanaweza
kuambukizwa. Ugonjwa huathiri mifumo ya fahamu, njia ya
chakula na hewa.

Jinsi Ugonjwa Unavyoenea


 Chanzo cha maambukizi ni maji, chakula kilichochafuliwa
na kinyesi cha kuku wagonjwa.
 Pia maambukuzi huweza kupitia mfumo wa hewa kutoka
kwa kuku wagonjwa.
 Kuku, vifaa vya kazi na bidhaa zitokanazo na kuku (nyama,
mayai, manyoya na mbolea) kutoka mashamba yenye
ugonjwa zinaweza kueneza ugonjwa kutoka shamba moja
hadi jingine.
 Vifaranga wanaweza kupata maambukizi kutoka vituo vya
kutotolea vifaranga kutokana na maganda ya mayai
yaliyochafuliwa.
Dalili za kuku wenye Kideri/Mdondo
 Vifo vya ghafla vya idadi kubwa ya kuku katika
shamba/banda
 Kuku wanatetemeka na kushindwa kutembea
 Kuku hupooza miguu, mabawa na kupinda shingo; na
hujizungusha mahali alipo
 Kuku huharisha kinyesi cha kijani na wakati mwingine
chenye mchanganyiko wa rangi ya njano
 Kuku huzubaa na kuacha kula
 Kuku hukohoa, hupiga chafya na kupumua kwa shida
Vifo vinaweza kufikia asilimia 100, kutegemea na umri na aina ya ndege
Tiba :-
 Hakuna tiba ya ugonjwa huu ila kuku wapewe antibiotiki.
 Pata ushauri wa daktari.

2. Gumboro (Infectious Bursar Disease)

8
KUKU NI DHAHABU-EV PETER KILEZU

3. Mareksi (Marek’s Disease)


4. Ndui ya Kuku (Fowl Pox)
5. Saratani ya Kuku (Avian Lymphoid Leucosis)
6. Mafua Makali ya Ndege (Highly Pathogenic Avian Influenza)
7. Ugonjwa Unaoathiri Mfumo wa Fahamu (Avian Encephalomyelitis
- AE
ii. Magonjwa Muhimu yasababishwayo na Bakteria.
 Homa Kali ya Matumbo (Fowl Typhoid)
 Homa ya Matumbo (Avian Paratyphoid)
 Kuharisha Kinyesi Cheupe (Bacillary White Diarrhea)
 Kipindupindu cha Kuku (Fowl Cholera)
 Mafua ya Kuku (Infectious Coryza)
 Ugonjwa Sugu wa Mfumo wa Hewa (Chronic Respiratory Disease-
CRD)
 Kolibasilosi (Colibacillosis)
 Kampilobakta (Campylobacteriosis)
iii. Magonjwa Muhimu ya Protozoa.
 Kuhara Damu (Coccidiosis)
 Histomonasi (Histomoniasis)
iv. Minyoo ya Kuku
 Minyoo Bapa (Tape Worm Infestation)
 Minyoo ya Duara (Nematode Infestation
v. Wadudu Wanaoshambulia Ngozi
 Wadudu Wanaoshambulia Ngozi (Insect Infestation)
 Kupe Wanaoshambulia Ngozi (Acari Infestation)
vi. Upungufu wa Lishe.
 Upungufu wa Vitamini (Avitaminosis)
 Upungufu wa Madini (Mineral Deficiencies)
 Upungufu wa Protini (Protein Deficiencies)
vii. Magonjwa ya Fangasi (Fungal Diseases)
 Aspagilosi (Aspergillosis)

b. Tiba na Chanjo za kuku.


Hapa Tanzania tunamsemo mashuhuri usemao ‘…Elimu haina mwisho’ msemo
huu unatukumbusha kuwa katika suala la Tiba na Magonjwa ya kuku tuna kazi
kubwa ya kuendelea kujifunza na kujifunza namna mbalimbali za kukabiliana na
magonjwa ya kuku. Ni dhahiri kuwa wataalamu wa ndani na wa nje ya nchi na
bara letu la Africa wamefanya kazi kubwa sana ya kutafiti na kugundua Tiba na
Chanjo zinazotusaidia leo, ukweli ni kwamba hatujafika mwisho wa ugunduzi na
utatuzi wa changamoto za kuku. Kwa kadiri mazingira yanavyoharibika (global

9
KUKU NI DHAHABU-EV PETER KILEZU

warming) ndivyo changamoto za kuku zinavyoendelea kuwa sugu. Wito wa


kwanza kwenye kukabiriana na changamoto za kuku ni kila mtu ashiriki kutunza
mazingira.
a) Kabla ya tecknolojia kukua mwanadamu alitumia njia za asili yaani miti/mimea
mbalimbali kutibia kuku. Baadhi ya miti hiyo ingali inapatikana na mingine
inapatikana ingawa kwa shida, ipo miti mingine ilikuwa mashuhuri katika kutibu
kuku lakini leo haipatikani kabisa.
Miti/ mimea iliyotumika na inayoendelea kutumia ni:-

i. MWAROBAINI (MAJANI, MIZIZI, MAGOME):

Hutibu magonjwa yafuatayo:

 Typhoid.
 Kuzuia Kideri.
 Kuhara.
 Mafua.
 Vidonda.

ii. SHUBIRI MWITU (ALOE VERA)


 Chukua majani 3-5 makubwa, katakata na loweka ndani ya maji
lita 10 kwa masaa 12 hadi 16. Wape kuku kwa siku 5 hadi 7.
Isiyotumika mwaga na tengeneza nyingine baada ya masaa 12.
Mchanganyiko huu unaweza kutibu :
 Kideri/Mdondo (Mdonde/Chikwemba/Kitoga/Chinoya/Sotoka) –
inyweshwe kabla kwa kinga.
 Homa ya matumbo (Typhoid).
 Mafua (Coryza).
 Kipindupindu cha kuku (Fowl Cholera).

iii. MTAKALANG’ONYO (EUPHORBIA)


Chukua Majani makubwa 3-5, ponda, weka katika lita 10 za maji kwa masaa 12-16, chuja na
wape kuku. Isiyotumika mwaga na tengeneza nyingine. Mtakalang’onyo hutibu:

 Kideri/Mdondo (Mdonde/Chikwemba)
 Ndui.
 Kuhara damu (Coccidiosis)

iv. MBARIKA (NYONYO)


Hutibu Uvimbe. Weka majani ya mbarika ndani ya majani ya mgomba kisha weka ndani ya jivu
la moto, kisha kanda sehemu yenye uvimbe kwa kutumia majani hayo ya mbarika.

10
KUKU NI DHAHABU-EV PETER KILEZU

v. MLONGE
Ina vitamini A na C. Chukua majani ujazo wa mikono miwili (gao mbili). Kisha yapondeponde na
kuyaweka katika lita 10 za maji na iache kwa masaa 12-16, chuja na wape kuku. Isiyotumika
mwaga na tengeneza nyingine.

Mlonge hutibu :

 Mafua.
 Kideri – inyweshwe kabla kwa kukinga
 Kipindupindu cha kuku (Fowl Cholera).
 Homa ya matumbo
 Ini.

vi. NDULELE.
 Majani hutibu Minyoo.
 Matunda hutibu Vidonda
.
vii. MAJANI YA MPAPAI

Chemsha magao mawili ndani ya maji lita 6 hadi ubakie na lita 1. Poza kisha chuja.

Hutibu: Minyoo 

Pia Majani Ya Mpapai Ni Dawa ya kutibu Kuku Kuharisha namna yoyote

Kuandaa Pata jani moja bichi la Mpapai na uliponde ponde lilainike kiasi. Kisha changanya na
maji kiasi cha lita mbili na nusu.

Kutumia (kwa tiba) – Kuku wapewe maji hayo wanywe, wasipewe maji mengine kwa ajili ya
kunywa kwa siku angalau nne au zaidi.

– Inafaa zaidi kila siku kuwaandalia dawa mpya ili dawa isiharibike.

Kutumia (kama kinga) – Hata kama kuku hawaharishi, wakizoeshwa kunywa maji yenye majani
ya mpapai yaliyopondwa angalau mara tatu kwa wiki watakingwa magonjwa mengi.

Njia nyingine ya kutumia Mpapai:

Kuandaa na Kutumia – Chukua majani ya Mpapai uyatwange upate kisamvu chake kiasi cha lita
1.

– Changanya kisamvu hicho na pumba lita 2.

– Waweza kuongezea maji kidogo na kuwapatia kuku wanaoumwa watumie chakula hicho hadi
wapone.

11
KUKU NI DHAHABU-EV PETER KILEZU

Kama kuku ni wachache, andaa chakula wanachoweza kumaliza kwa siku moja ili kisibakie na
kuharibika kabla hawajakimaliza.

viii. MAJANI YA MWEMBE


Majani magao mawili, ponda na chemsha ndani ya lita 6 za maji hadi ibaki lita 1.

Wape kwa siku moja.

 Mwembe hutibu:
 Homa ya matumbo.
 Mafua.
 Kinga ya Kideri/Mdondo.

ix. PILIPILI KICHAA


 Pondaponda kiasi kisha changanya na maji na wawekee kuku
wawe wanakunywa kwa muda wao. Inasemekana inasaidia
kutibu Mdonde (lakini mapema kabla maradhi kuingia).
 Chukua pilipili 5 za kichaa au ndefu au mbuzi kama ukikosa zote,
twanga weka kwenye maji lita 4,wape baada ya kula. Wape kwa
siku 5 _Hutibu aina zote za mafua

x. KITUNGUU SWAUMU:

Hutibu Mafua, Typhoid, Kuharisha kinyesi cheupe

Jinsi ya kutumia Unakitwanga kisha uchanganye kwenye maji chuja kwa chujio ili kuondoa nyuzi
na uchafu.

Kiwango cha kuwapa kitategemeana na idadi ya kuku. Huu ni ushuhuda wa mfugaji aliewahi
kutumia kitunguu swaumu kwa kuku wake

TEKNOLOGIA

Imetusaidia kuja na suluhisho la changamoto za kuku kama

- Chanjo za maji na vidonge


- Pia antibiotic kama vile OTC n.k

5. Faida za kuku
a) Ufugaji hauhitaji mtaji mkubwa kuuanzisha.
b) Ni rahisi kuusimamia.
c) Faida inapatikana mapema.

12
KUKU NI DHAHABU-EV PETER KILEZU

d) Mali ghafi nyingi zinazohitajika zinapatikana kwa urahisi katika mazingira ya


vijijini.
e) Kwa kipindi cha hivi karibuni, uzoefu unaonyesha kuwa soko la kuku wa
kienyeji linakua na linaelekea kwenye kutokutosheleza wateja
f) Chakula – nyama ya kuku na mayai hutumika kama chakula muhimu cha
wanadamu, chenye protini.
g) Chanzo cha kipato – mkulima hupata fedha akiuza kuku au mayai.
h) Chanzo cha ajira – ufugaji wa kuku hutoa ajira kwa jamii.
i) Kuku hutumika kwenye shughuli za ndoa kama vile kutoa mahari na pia ni
kitoweo muhimu katika sherehe hizo.
j) Gharama nafuu za kuanzisha na kuendesha mradi huu.
k) Mbolea – kinyesi cha kuku kinaweza kutumika katika kurutubisha mashamba
ya mazao na mabwawa ya samaki.
l) Soko lipo la uhakika, ukilinganisha na kuku wa kisasa kwani nyama na mayai
yake hupendwa zaidi na walaji.
m) Manyoya ya kuku hutumika kama mapambo, pia huweza kutumiaka
kutengenezea mito ya kulalia na kukalia.
n) Mayai yenye mbegu ya jogoo hutumika katika kutengeneza dawa za chanjo.
o) Magamba ya mayai yanaweza kutumika katika utengenezaji wa vyakula vya
wanyama.
p) Kiini cha njano cha mayai kinaweza kutumika kutengeneza mafuta ya
kuoshea nywele (shampoo).

Mungu akupe NEEMA unapochukua hatua za kuanza kufuga makundi mbalimbali ya


wanyama.

13
KUKU NI DHAHABU-EV PETER KILEZU

KUTAWALA MAZINGIRA TULIYOPEWA NA MUNGU KUNATUWEZESHA KUZITAWALA NGUVU


KUU MBILI ZINAZOTAWALA DUNIA NA KISHA KUMTUMIKIA NA KUMWABUDU MUNGU
WETU KWA UHURU.
YESU alianza vibaya kwa kuzaliwa kwenye mazingira duni yaani kwenye hori/zizi la ng’ombe
lakini alimaliza kazi yake vizuri na kuzikwa kwenye kaburi zuri la tajiri mmoja ili atufanyie
maisha yenye utoshelevu yaliyojaa Neema za kila namna kwa wingi. Sababu mojawapo ya Yesu
kuzaliwa kwenye hori la ngo’mbe ni kipato duni, kazi ya Yusufu ya uselemala inaonesha
haikumpa kipato kizuri ndiyo maana Yesu alipokufa huoni Yusufu akisemwa kwenye shughuli na
harakati za mazishi ya Yesu.
UTAJIRI NA UMASKINI ni nguvu mbili zinazotawala dunia nzima, wakati wa uumbaji Mungu
hakukusudia kuwa na Nguvu ya Umaskini kwa sababu ya maasi yaliyozaa laana ndipo chipukizi
la UMASKINI LIKAPATIKANA na sasa linatawala dunia kwa nguvu kubwa sawa na UTAJIRI.
MHUBIRI 10: 15 …………… Mstari huu unatueleza wazi wazi kuwa UMASKINI ni UANGAMIVU
Kama Umaskini una UA mtu, unawezaje kuufurahia, kuuendekeza na kufanya urafiki nao.
UTAJIRI
Tunaposema Utajiri hapa hatuhusianishi wala kutazama vitu visivyozalisha kama Gari, fanicha
n.k ila vitu kama miradi ya uzalishaji mifugo n.k
MHUBIRI 7:12 ………………… FEDHA NI ULINZI/USALAMA inalinda watu, utu pia inalinda na
NAFASI zao.
MHUBIRI 10:19 ………………. FEDHA NI JAWABU LA MAMBO YOTE

Pesa ni kitu chenye nguvu sana , kama mtu hana pesa anaweza kudhalilika n ahata kupoteza
UTU wake
Mf :-
1. wanawake walioajiliwa kwenye bandi za mziki
2. kufanya Ngono na Mbwa
3. Kufanya ngono ya jinsia moja kwa lengo la kupata ufadhili wa masomo
4. vyombo vya habari vya hapa nchi viliwahi kuripo matukio ya kutweza UTU wa
WATU chuo kikuu kimoja wanafunzi wake waanza kufanya rekodinging za
ngono na kusambaza kwenye mitandao na tovuti
suala la kuwa uchi wa mnyama pekee liliwashinda ADAMU na EVA baada ya
kukosa/kuasi kiasi kwamba walihangaika kushona majani majani kama nguo

14
KUKU NI DHAHABU-EV PETER KILEZU

zao ili tu kutunza UTU wao. Je, kufanya ngono na kusambaza dunia nzima
kwa video na picha kisa unasaka tonge/pesa.
5. Migogoro ya familia za wakristo MAHALI FLANI (KIGOMA) baraza la wazee
tukakutana ili kugawana majukum
6.
Namna hii inawashushia heshima, wanadhalilika, kwa sababu hawana ULINZI/USALAMA
Unayeniskia mahali hapa au mahali pengene kamwe usijaribu kufanya hayo wakati wowote
kwenye maisha yako ama kwa kuisifu kwa sababu ya PESA

UMASIKINI ni nini?
Ni ukosefu au upungufu wa rasilimali vitu au Pesa.
Katika dunia hii MATAJIRI ndio huweka mipango na MASIKINI ndio huikamilisha mipango hiyo.
Mtu akitaka kutawaliwa basi akose fedha.
Mf:-
1. Delila na Samson
Delila alikuwa mwanamke mzuri kwa sura na kwa umbo, Delila
hakuwa mwanamke mbaya. Ubaya wa Delila unajitokeza kwenye
umaskini wa Nyumbani kwao, kama si Pesa asingemsalti Samsoni
mpenzi wake ambaye naye alikuwa mwenye mvuto mkubwa kwa sura
na umbo.
Wafiliti walikuwa tayari kufadhili masomo yake na kuwasaidia wazazi
wake kama tu angewasaidia kujua asili ya nguvu za SAMSONI
2. YESU alipokuwa kwenye chakula cha usiku na wanafunzi wake
aliwaambia mmoja wenu atanisaliti
Wote walikana Je, ni mimi bwana ! mimi kweli! Kamwe
haitawezekana hata Yuda Mwanzoni alikana.
Lakini pamoja na shetani lakini pesa ndiyo ilimuua Yesu baada ya
Yuda kushirikishwa na wakuu wa makuhani, baada ya usaliti huu
aliujutia na kuchukua hatua za yeye kujiua
Kuna watu wanatenda mabaya si kwa kupenda, wengine wapo hapa
ni wanandoa kwa sababu ya umasikini wanasalti ndoa zao.
3. Wakuuu wa makuhani wale wale waliotoa pesa kwa Yuda amsaliti
Yesu hao hao walitoa pesa tena kuufuta ukweli wa tukio la kufufuka
kwa Yesu. MATHAYO 28:11-15
4. Shetani anatumia fedha katika kuwalaghai na kuwaaminisha watu
kuwa fedha ni mali yake LUKA 4: 5-7 Jambo ambalo si kweli.

15
KUKU NI DHAHABU-EV PETER KILEZU

a. Anataka kuwaaminisha wakrist kuwa Uchumi ni Mali yake


b. Anataka kuhakikisha anawatoa kwenye mzunguko wa kumiliki
uchumi
Yesu alipokufa alikuwa na wanafunzi wake wote, kwa kuwa miongoni mwao hakuwepo mweny
kaburi walitoroka, mtu mmoja tajiri na mfuasi kwa siri wa Bwna Yesu alijitolea kwa fedha yake
kushugulikia mazishi ya mwili wa yesu kwnye kaburi jipya tena na kuuomba mwili wake Yesu
kwa Herode kwani alikuwa na fedha. Yesu akazikwa na kufufuka kwenye kaburi la Kitajiri ili iwe
sababu ya sisi kuturudishia heshima ya kutwala na kumiliki UTAJIRI.

WITO WA YESU/WITO WA MBINGUNI


Msingi mkubwa wa WITO wa mbinguni ni TOBA
--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------

BARAKA ZA BWANA
Mungu anazo Baraka kwa ajili ya watu wake,Baraka hizi si vitu vinavyoshikika
MITHALI 10:22 Baraka za Bwana hutajirisha wala hachanganyi huzuni nayo
Kubarikiwa na Bwana haina maana ya moja kwa moja kwamba una MALI na wala si lazima
uipime kwa kuwa na PESA
 Lakini Baraka ya Bwana ina uwezo wa kufanya/kuwezesha kuwa
tajiri
 Baraka ya Bwana ni kama nyenzo inayokuwezesha wewe kuwa
tajiri
 Unaweza kuwa umeberikiwa na Bwana lakina maisha yako
yakaendelea kuwa ya umaskini.
Leo tuzungumie kidogo kuhusu UKUBWA WA ENEO ambalo Baraka za Bwana zinachukua
Baraka za Bwana zinaweza kuenea kwa umbali gani yaani zinachukua eneo kubwa kiasi gani
KUMBU 28:1-8 hapa tunaona utajiri wa Baraka za Bwana, unaziona kwa urefu wake upana na
kimo chake vizuri.
1. Eneo la Kwanza:
Baraka za Bwana zimeenea maeneo ya mjini na vijijini hii inamaana kuwa hazina mipaka.
Katika mazingira halisi yanaweza kuonesha kasoro Fulani Fulani hasa katika maeneo ya
vijijini ila katika mpango wa Mungu hakuna eneo lisilokuwa na Baraka za Bwana.

16
KUKU NI DHAHABU-EV PETER KILEZU

Kwenye UCHUMI wa Mungu hakuna eneo hata moja lisilokuwa na Baraka za Mungu.
Kama ni Africa au Ulaya Baraka za Bwana zi kila mahali kwa utimilifu.
2. Eneo la Pili:
Baraka za Bwana zimeenea kwenye UZAO wote wanaotoka kwenye viuno/tumbo lako
lakini pia hata wale unaoishi nao wanauhusiano na wewe kwa namna moja au nyingine.
Aina hii ya Baraka ni ya vizazi vyote, Baraka ya ajabu maana inawagusa hata wale
wasiokuwa kwenye agano moja na wewe
 Mf: ibrahimu ni mtu aliyebarikiwa na Bwana lakini Luthu mpwae hakuwa kwenye
agano lakini alibarikiwa kwa sababu ya Baraka ya mjomba wake Ibrahimu.
3. Eneo la Tatu:
Baraka zimeenea kwenye maeneo ya uzalishaji kwenye vitu tunavyolima na kuzalisha
4. Eneo la Nne:
Baraka za Bwana zimeenea kwenye safari zote za ndani ya nchi, nje ya nchi, ukiamua
kubaki hapa nchini utabarikiwa ukisafiri kwenda nje ya nchi utabariki kwa sababu Eneo
halitazuia Baraka za bwana. 2 SAMWEL 8:14, 2 SAMWEL 19:2
 Mf: Yusufu alibarikiwa alipokuwa nyumbani kwa babaye, alipoenda kwa potifa,
gerezani n ahata ikulu alibarikiwa.
Ukiwa na usafiri wako utabarikiwa.
5. Eneo la Tano:
Baraka za Bwana zimeenea kwenye eneo la VITA chochote kitakachokuja kinyume chako
Baraka hii itakiondoa. Masha ya mtu yamezungukwa na vita kama huna vita basi, wewe
si kiumbe hai. Vita kama magonjwa n.k yatakuja juu yako yakiwa yamejipanga
yataondolewa mbele yako bila utaratibu. Mungu anapigana kwa ajili yako. 2 NYAKATI
23:6
6. Eneo la Sita:
Kwenye eneo la STOO YA CHAKULA CHA NYUMBANI KWAKO Hautakusanya na
usivitumiwe mwenyewe wala havitapeperushwa. Ukivuna au Benki na uwekezaji Baraka
za bwana zitafika huko.

Hii ni package kubwa sana ya Baraka za Bwana hii inatosheleza maeneo yote ya maisha
ya mtu
Chini ya Baraka za Bwana umebarikiwa popote utakapokuwa

17

You might also like