You are on page 1of 2

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA MAMBO YA NDANI


JESHI LA POLISI TANZANIA
Anuani ya Simu: ‘‘POL V/NDEGE T” OFISI YA;
KAMANDA WA POLISI
Nambari ya Simu: 2844416 VIWANJA VYA NDEGE ‘T’,
Nambari ya Fax: 2842107 S.L.P 18145.
DAR ES SALAAM.

02/05/2022

TAARIFA YA JESHI LA POLISI V/NDEGE ‘T’ DSM KWA


VYOMBO VYA HABARI TAREHE 02/05/2022.

Ndugu wanahabari, nimewaita leo hapa, kwa ajili ya kutoa taarifa mbili
za ukamataji wa wahalifu.

TUKIO LA KWANZA.

Mnamo tarehe 12/04/2022 majira ya saa 10:00 hrs hapa Uwanja wa ndege
wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jengo la abiria namba tatu eneo
la kuondokea abiria sehemu ya ukaguzi wa mizigo alikamatwa abiria
mmoja Raia wa CHINA, DONG WEIJUN, mwenye umri wa miaka 44,
aliyekuwa akisafiri kwa ndege ya QATAR mruko namba QR 1499 majira
ya saa 10:00 hrs kwenda BANGKOK, THAILAND akiwa na vidani 10
na bangili moja vilivyo tengenezwa kwa meno ya tembo vyenye uzito wa
gram 110, pia alikutwa na bangili nyingine moja iliyotengenezwa kwa
manyoya ya mkia wa tembo (singa) vyote vikiwa na thamani ya tembo
mzima.
Mtuhumiwa tayari amefikishwa Mahakamani kwa hatua za kisheria.

TUKIO LA PILI,
Mnamo tarehe 29/04/2022 majira ya saa 20:30 hrs hapa uwanja wa ndege
wa Kimataifa wa Julius Nyerere Terminal three eneo la ukaguzi wa
mizigo ya abiria wanaosafiri kwenda nje ya Nchi alikamatwa abiria
mmoja Raia wa India mwenye umri wa miaka 23, akiwa na madawa ya
kulevya aina ya HEROIN yenye uzito wa Kg 17.40

Mtuhumiwa huyo aliwasili hapa Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa


Julius Nyerere kwa ndege ya Air Tanzania (ATCL) mruko namba TC 212
majira ya saa 20:30 hrs akitokea Harare – Zimbabwe, mtuhumiwa huyo
alikuwa anatarajia kuunganisha safari yake kuelekea MUMBAI INDIA
kwa ndege nyingine ya Air Tanzania (ATCL) mruko TC 400 akiwa kama
abiria wa Transit ambapo mizigo yake ilishushwa na kukaguliwa upya
kwa ajili ya kuendelea na safari na ndipo aligundulika amebeba madawa
ya kulevya aina ya HEROIN.
Upelelezi wa shauri hili bado unaendelea na mara tu utakapokamilika
mtuhumiwa atafikishwa Mahakamani.

Jeshi la polisi Viwanja vya ndege Tanzania linatoa onyo kali kwa watu
wote wanaojihusisha na kusafirisha madawa ya kulevya na nyara za
Serikali kwani watakamatwa na kuchukuliwa hatua kali za kisheria.
Polisi Viwanja vya Ndege kwa kushirikiana na vyombo vya vingine vya
ulinzi na usalama vimejipanga vizuri kuhakikisha hakuna aina yoyote ya
uhalifu utakaofanyika katika Uwanja wowote wa Ndege Nchini Tanzania.

Aidha kuelekea msimu wa sikukuu za EID EL FITRI Jeshi la polisi Kikosi


cha polisi Viwanja vya Ndege Tanzania tumejipanga vizuri katika
kuimarisha ulinzi maeneo yote ya Viwanja vya Ndege. Kutakuwa na doria
za miguu,pikipiki na magari maeneo yote ya ndani na nje ya Viwanja
vyote vya Ndege Nchini. Aidha tunawaomba wananchi wote wanaoishi
karibu na Viwanja vya Ndege waendelee kushirikiana na Jeshi la polisi
katika jukumu la ulinzi.

IMETOLEWA NA:
JEREMIA N. SHILA ACP
KAMANDA WA POLISI VIWANJA VYA NDEGE ‘T’
DAR ES SALAAM.

You might also like