Professional Documents
Culture Documents
Uchu Mba
Uchu Mba
UCHUMBA NA MAISHA
YA NDOA
KATIKA MISINGI YA
KIKRISTO
FRANK P. KAROLI
© 2018
Haki-miliki © 2018
SHUKRANI
N
amshukuru sana Mungu na najinyenyekeza mbele Zake, kwani amenitia nguvu na
uwezo wa ajabu katika kutafiti na hadi kuikamilisha kazi yote ya kitabu hiki. Ni
kwa jinsi ya ajabu, Roho wa Mungu kanishuhudia, nami nikaona, sina budi ya
kuwashuhudia wengine kile ambacho Roho wa BWANA amekuwa akinishuhudia
kwa muda mrefu.
Sanjali na kumshukuru Mungu, napenda pia kuishukuru familia yangu ambayo kwa
sehemu kubwa nimeitumia kama sehemu ya utafiti katika kujiridhisha na kile ninachopaswa
kushiriki na Wakristo wenzangu ili niandike yaliyowazi ambayo yanawapasa Wakristo wote
na wasio Wakristo kuyafuata, kuyatenda na kuyaishi katika urafiki, uchumba, ndoa na malezi
ya vijana na watoto wao.
Shukrani za pekee ni kwa mke wangu kipenzi wa ndoa, Mariam Lucas na Mtoto
wangu Kevin Frank ambao kwao, ni sehemu ya kazi hii kutokana na maombi yao na yale
niliyojifunza kutoka kwao; hasa kwa kunivumilia na kukubali kuwa wapweke kwa wakati
nilipokuwa nikitumia muda mwingi ili kukamilisha kazi ya kitabu hiki. Siwezi kumsahau
kumpa shukrani zangu za pekee shujaa wangu miongoni mwa wanawake mashujaa
ulimwenguni; mama yangu mpendwa Koretha Karol ambaye amenilea kwa kujitoa kwa
upendo katika hali na mali hadi nilipofikia hatua ya kujitegemea katika maisha yangu.
Shukrani za pekee pia zimwendee Mchungaji Suleiman Mange aliyekuwa mlezi
wangu kipindi nilipokuwa Chuo Kikuu cha Dodoma (2009-2012). Naikumbuka kauli mbiyu
yake aliyoitumia kwa vijana wa vyuo vikuu kanda ya Dodoma iliyosema “It is not good for
man to stay alone” ikimanisha, “Si vyema mtu huyu akae peke yake”. Vivyo hivyo,
namshukuru sana Mchungaji Fransis Katengu, Mchungaji aliyenibatiza (Novemba 2011) pale
kwenye kanisa la Dodoma kati na kuniweka wakfu ili niweze kumtumikia Mungu katika
maisha yangu ya hapa duniani.
Kwa jinsi ya pekee pia, shukrani zangu zimwendee kaka yangu Japhet Ngh‟abi
ambaye aliniongoza juu ya misingi mizuri ya kumjua Mungu. Kwa namna ya pekee,
nalishukuru sana kanisa la Waadventista wa Sabato la Liwale kwa kunilea kiroho na
kunisaidia mambo mengi kwani hata mpaka nakikamilisha kitabu hiki, nilikuwa bado
mshiriki wake. Shukrani zangu za dhati zinamhusu pia Mwinjilisti Fredrick Jonathan
Sogoseye pamoja na mke wake. Namshukuru sana Mchungaji Israel Kagya kwa mafundisho
yake mazuri yaliyonijenga kiroho, na baadhi ya mafundisho yake yamo katika kitabu hiki.
Aidha, ni wengi wa kuwashukuru katika ufanikishaji wa kazi ya kitabu hiki; kwa
kuwataja baadhi ni; bwana na bibi Shamsi Kashoro, bwana na bibi Wilson Nyamanga, bwana
na bibi Paul Enock Jangu, bwana na bibi Ephraim Mmbaga, bwana na bibi Elly J. Moses,
bwana na bibi Ephraim Mwandendi, bwana na bibi Mwalimu Mbwambo, bwana na bibi
Daibrin Kibamba pamoja na Neema Erasto, ASSA-Liwale sekondari, Samson Balele, Elisha
Magoma, Graceana Makota, na wengine wengi ambao sikuwataja, natambua mchango weo,
hivyo, BWANA awabariki sana.
DIBAJI
M
iaka ya hivi karibuni, ulimwengu umekuwa ukishuhudia mabadiliko makubwa
ya ajabu katika ndoa na familia za wanadamu. Mabadiriko hayo yanachagizwa
na sababu nyingi ambazo zimepelekea familia baadhi kuyumba na kusababisha
aidha kuvunjika kwa ndoa, kuwa na migogoro isiyokoma, watoto kutokuwa na
maadili mema, usaliti kwa wanandoa, uzinzi, ngono zembe kwa vijana, magonjwa ya
kisaikolojia yatokanayo na changamoto za kifamilia au vifo miongoni mwa wanafamilia kwa
sababu ya maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi (VVU).
Nishauku yangu kumwona kijana au mwanandoa akiziepuka changamoto zote hizo
kwa kuzingatia na kuyafuata yale yaliyomo ndani ya kitabu hiki huku akimruhusu Mungu
atawale maisha yake yote. Kitabu hiki ni kazi iliyochukua muda wa miaka sita, hivyo
yaliyomo yote ni kweli isiyokuwa na mashaka maana hata Biblia inayashuhudia kwa
kuyaeleza katika utimilifu wake. Kitabu hiki ni kitabu lulu kwa wale wote walio katika ndoa,
uchumba, na vijana wote wasiokuwa katika mahusiano ya uchumba, kwani, kinamashauri juu
yao pia (vijana) ili waweze kuuelekea mwelekeo sahihi juu ya mahusiano na ndoa zao.
Ndani ya kitabu, pia pameandikwa mashauri juu ya malezi ya watoto na changamoto
zinazowakabili katika makuzi na malezi yao, na jinsi ya kuwaepusha ili waiepuke njia ile
pana ielekeayo katika upotevu. Unapokisoma kitabu hiki, yathibitishe mafungu yaliyomo
kwa kusoma Biblia yako huku ukimruhusu Roho Mtakatifu awe sehemu ya mabadiliko kwa
yale yote yaliyoelekezwa ndani ya kitabu. Kwa kuwa mwandishi wa kitabu hiki ni mwalimu
kwa taaluma na mwinjilisti, hivyo, kitabu hiki kimeandikwa kwa mtililiko na mpangilio
mzuri, unaovutia, wenye lugha rahisi, ili kumfanya msomaji aelewe kirahisi na kutochoka
pia.
Kitabu hiki chenye jina la Uchumba na Maisha ya Ndoa Katika Misingi ya Kikristo
ni kitabu ambacho kimekusudiwa kutoa elimu, ufahamu, ujuzi na maarifa katika Nyanja
zifuatazo: 1. Jinsi ya kujenga urafiki na mahusiano bora, 2. kuuelewa uchumba wa kweli na
hatua zake katika misingi ya Kibiblia; 3. Madhara ya kushiriki tendo la ndoa kabla ya ndoa
na jinsi ya kuacha au kuepuka kushiriki tendo la ndoa kabla ya ndoa; 3. Kanuni za Kibiblia
katika kujipatia mchumba anayepaswa kuwa mwenzi wa maisha; 4. Mambo ya kuzingatia
kabla ya kufanya maamuzi ya kuingia katika ndoa; 5. Utakatifu wa ndoa na makusudi ya
Mungu kuasisi ndoa kwa wanadamu; 6. Vyanzo vya migogoro katika ndoa na namna ya
kufanya ili ndoa kuwa na ustawi mzuri; 7. Jinsi ya kuwa mke au mume mwema katika ndoa
na familia; 8. Jinsi ya kuifanya familia kuwa ya kiroho na yenye furaha na amani; 9. Malezi
sahihi ya watoto katika misingi ya Kibiblia; 10. Kiasi na uwakili katika familia. Na hayo ni
kwa kutaja baadhi.
Mwandishi wa kitabu hiki ni mwalimu (wa sekondari na vyuo vya ualimu) kwa
taaluma, mwinjilisti na mwalimu wa Biblia anayemtumikia Mungu. Uzoefu alioupitia katika
makuzi, kazi, malezi, uchumba, ndoa, tafiti na maisha yake binafsi, ni miongoni mwa vionjo
alivyovitumia katika kitabu hiki, ili kushiriki na ulimwengu wote wa Wakristo na wasio
Wakristo katika kuijua hatima yao na nini wafanye ama kufuata katika “Uchumba na Maisha
ya Ndoa katika Misingi ya Kikristo”.
YALIYOMO
SHUKRANI:………………………………....................................................……..…...………………...............…… 3
DIBAJI: …..…………………………….....................................................…..……….….....…………....................… 4
UTANGULIZI: ………………………..................................................……..............……….….....…...…………….. 7
SURA YA O1:
MAMBO YA KUFAHAMU KWA VIJANA: …........................................................................…….....….…. 8
SURA YA 02:
MAMBO YA KUZINGATIA KWA MCHUMBA ILI AWE MWENZI WA MAISHA: ..........................15
SURA YA 03:
HATIMA YA UCHUMBA NA MAAMUZI YA KUOA AU KUOLEWA: ……..…................................… 28
SURA YA 04:
MPANGO NA MAKUSUDI YA MUNGU KUASISI NDOA: ……………………...........................…..….… 33
SURA YA 05:
UASI KATIKA NDOA NA FAMILIA YA KWANZA: ……………………..…........................…..........…….. 38
SURA YA 06:
CHANGAMOTO KATIKA FAMILIA ZA KIKRISTO:.........................................................................… 45
SURA YA 07:
JINSI YA KUWA MKE AU MUME MWEMA KATIKA NDOA NA FAMILIA: .................................. 53
SURA YA 08:
FUNZO KUTOKA MITHALI 31:11-31 KWA WANAWAKE-WANANDOA: ........ ...... ...................57
SURA YA 09:
UFAHAMU NA MAARIFA JUU YA NDOA YA KIKRISTO: …………....…........................................… 65
SURA YA 10:
FAMILIA YA KIROHO YENYE FURAHA: …….……............................................................................. 70
SURA YA 11:
MALEZI BORA YA KIKRISTO KWA WATOTO: .…......................................................................… 76
SURA YA 12:
SAIKOLOJIA YA TABIA NA HISIA ZA MAKUNDI YA WATU: ……….....….......................……...… 87
SURA YA 13:
TOFAUTI ILIYOPO KATI YA MWANAMKE NA MWANAMUME: .................................. 94
SURA YA 14:
UMUHIMU WA KUSAMEHEANA KWA WANANDOA: …….....…........….......................…………..... 100
SURA YA 15:
UWAKILI WA MUDA KATIKA NDOA NA FAMILIA: ……………….…........................…...………...... 104
UTANGULIZI
M
wenzi wako si mkamilifu, na wewe pia, na wote wawili hamuwezi kuwa
wakamilifu, lakini kama anaweza kukufanya ufurahi, umfikirie mara mbili na
zaidi na anakiri kuwa yeye ni binadamu anaweza akatenda makosa, basi,
mshikilie yeye na mpende kwa kadiri uwezavyo, maana, ni mtu sahihi kwako.
Anaweza kuwa hakufikirii kila sekunde katika siku, lakini anatumia sehemu ya maisha yake
kwa ajili yako. Usimbadilishe, na usitegemee makubwa zaidi ya yale awezayo kukutendea au
yale anayoyamudu. Tabasamu pale akufurahishapo, mwambie pale anapokukasirisha, na
umkumbuke (um-miss) pale anapokuwa hayupo karibu nawe. Hapo utakuwa na furaha ya
kweli katika ndoa yako.
Kwa mwanamke na mwanamume kuwa na furaha katika ndoa kunahitajika upate mtu
mnayependana, mtu atakayejali sana furaha yako kuliko hata yake, mtu atakayekuwa wa
mwisho kukufanya ulie, mtu ambaye atakupa kila unachostahili, atakayejitolea muda wa
maisha yake kuishi na wewe kama mke au mume; ambaye ni mkweli, mwaminifu, mtu asiye
na tamaa, mtu makini katika kufikiri na ajuaye anachohitaji mwenzi wake, mtu pekee ambaye
atajisikia fahari kuwa na wewe po pote na kulitetea penzi lenu kwa namna yo yote ile na
kudumisha uaminifu.
Mwanamume au mwanamke atakayekupenda kuliko wewe utakavyompenda
hapatikani kirahisi, ila tu ni kama wewe nawe utakuwa unavigezo uvitakavyo huku
ukimkabidhi Mungu atende miujiza juu yako ambapo ukiwa sehemu kubwa ya matarajio
uyatakayo. Hakuna haja ya kukata tamaa na kujiona kuwa huna thamani katika maisha yako
kwakuwa tu kila uchumba unaouanzisha hauwi na mwisho mzuri au ulioutarajia. Maisha ya
uchumba ni maisha yasiyotoa uhakika wa muda sahihi wa uwepo wa ndoa bali ni matazamio
katika kufanyiana tathimini kama mtaendana.
Ukimpata yule umpendaye kwa dhati kama lilivyokuwa tarajio lako toka ndani ya
moyo wako, mhakikishie kumpenda siku zote. Pale muda utakapowadia na utakaporuhusu
nywele zake nyeusi ziwe nyeupe, zidi kumpenda. Pale ngozi yake laini ya ujana
itakapokaliwa na ngozi iliyojikunja ya uzee, bado hitaji lako la kumkumbatia lisipotee daima.
Tena mhakikishie kuwa “pale sura yake itakapokuwa na makunyanzi anapotabasamu, bado
utampenda”.
Kwa kuyathibitisha hayo yote; kama wote, (yaani mimi na wewe msomaji) tungejua
kuwa kila mtu katika ndoa zetu anahitaji faraja na upendo, tungesema kuwa sote tupo tayari
kuwapenda wenzi wetu wa maisha kama tujipendavyo sisi wenyewe na tukavaa viatu vyao
vya magumu yote wayapitiayo katika maisha ya ndoa. Tukinuia na kuweka nadhiri kuwa siku
zote, miaka yote tutawapenda wenzi wetu, na hiyo ni kwa kuwa tu kuwapenda kwetu kwa
dhati ni amani ya mioyo yetu na ustawi wa familia zetu.
Pangekuwepo na upendo wa dhati kwa wanandoa, pasingekuwepo na matatizo ya
kifamilia kama; kesi nyingi za familia mahakamani au ustawi wa jamii, ugomvi uletao
majeraha katika mwili au vifo, usaliti, malezi mabovu ya watoto, uwepo watoto wa mitaani,
maambukizi ya magonjwa ya zinaa, migogoro ya watoto, kutengana na kuwepo kwa
magonjwa ya kisaikolojia yatokanayo na matatizo ya kifamilia. Natumaini bila hayo yote
yanayosababisha matatizo ya ndoa na familia, dunia ingekuwa mbingu ndogo.
= SURA YA 01=
1. Aliyekataliwa (Rejectee).
Aina hii ya urafiki, unakuta kundi zima, mmoja au baadhi katika kundi zima
hakubariki kwa sababu ya tabia au kutoendana na kundi zima. Utakuta kundi zima
linamtenga lakini mtu huyo anazidi kujishikamanisha katika kundi hilo bila yeye kujitambua.
Aina hii ya urafiki katika kundi hili unaitwa urafiki wa kulazimisha au kujipendekeza, na
hivyo mtu huyo atakuwa mtumwa wa kundi.
2. Anayejitenga (Isolatee).
Ni aina ya uhusiano au urafiki ambapo mtu mmoja au watu baadhi wanakuwa
wamejitenga na hawashirikishi mambo yao wengine katika kundi zima, japo ni sehemu ya
kundi hilo. Marafiki wanamna hii hunufaika na kundi, bali wao hawalinufaishi kundi maana
ni wasiri juu ya masuala yao.
3. Aliyekataa (Neglectee).
Aina hii ya uhusiano, unakuta kundi zima la marafiki linamuhitaji mtu mmoja au zaidi
lakini mtu huyo hataki kuwa sehemu na mshiriki wa kundi, hivyo hujitenga kwa sehemu
kubwa na hashirikiani na wenzie katika mambo mbalimbali ya kundi aidha, kwa sababu
mbalimbali au yeye kutotaka kwa hiali.
4. Nyota (Star).
Miongoni mwa kundi nzima yupo mtu mmoja ambaye ni maarufu, mtu mwenye
mvuto na mwenye ushawishi mkubwa sana kwa watu wengine. Katika aina hii ya uhusiano
watu wengi hujikuta wamevutwa kwa sababu ya umaarufu na ushawishi wa mtu mmoja
hivyo kila mtu anajitahidi kujenga urafiki na huyo mtu na kuwa kiungo pekee cha wengine
kufahamina.
Faida za Urafiki wa Kweli
Yampasa kijana (au mtu ye yote) kutambua kuwa urafiki wa kweli haujali jinsia.
Japokuwa yapo mabaya mengi yanayosababishwa na urafiki, lakini, yapo mengi pia yaliyo
mazuri katika urafiki wa kweli na baadhi ya faida miongoni mwa nyingi ni zifuatazo:
Kufurahishana: Urafiki wa kweli ni kuleteana furaha iliyo ya kweli miongoni mwa
marafiki na siyo kuumizana au kuleteana huzuni kwa kutendeana mabaya na usaliti.
Kukubaliana: Marafiki wenye urafiki wa kweli hukubaliana na siyo kushurutishana ili
kutekeleza jambo fulani kutoka upande mmoja wa urafiki.
Kuheshimiana: Marafiki walio na urafiki wa kweli ni lazima waoneshe hali ya juu ya
kuheshimiana na si vinginevyo. Kuheshimiana kunaleta usikivu katika kushauliana miongoni
mwa marafiki.
Kusaidiana: Kusaidiana ni jambo moja la msingi katika urafiki ulio wa kweli.
Marafiki wenye urafiki wa kushibana ulio wa kweli husaidiana katika namna mbalimbali iwe
kwenye raha au changamoto mbalimbali.
Kushiriki hisia kwa pamoja: Kushiriki hisia kwa marafiki ni kielelezo cha urafiki wa
kweli. Rafiki wa kweli ni yule anayekufaa katika huzuni na raha na kwa mazingira au muda
wo wote.
Kujuana au kuelewana mapungufu: Marafiki walio na urafiki wa kweli wanajuana
mapungufu yao, hivyo wanajua jinsi ya kuishi na kurekebishana kulingana na mapungufu yao
wao kwa wao. Kujuana mapungufu na madhaifu kunasaidia kujua jinsi ya kuishi bila
kukwazana au kuumizana.
Kuaminiana: Marafiki walio wa kweli hawana haja ya kutiliana mashaka maana kila
mmoja humwamini mwenzake. Kuaminiana kunajenga ustawi mzuri wa urafiki endapo kila
mmoja atakuwa mwaminifu kwa mwenzake.
Uwazi na uhuru wa kuelezana: Kuelezana ukweli bila kufichana ni jambo la msingi
kwa marafiki maana hujenga uaminifu miongoni mwao. Mambo au masuala yakiwekwa wazi
miongoni mwa marafiki inakuwa rahisi kusaidiana au kushauriana.
mwa wanandoa, bali ni kukosekana kwa urafiki miongoni mwa wenzi katika ndoa. Kurukwa
kwa hatua ya urafiki husababisha wanandoa kutokuwa na mazingira mazuri ya urafiki. Katika
Wimbo Ulio Bora 5:16, Sulemani akiwa anamsifia mwenzi wake kwa binti za Yerusalemu
anasema “.... Ni huyu mpendwa wangu, ni huyu rafiki yangiu .....”
Hatua ya urafiki na uchumba huwa ni hatua nyeti sana kwa Mkristo anayejiandaa
kuingia katika ndoa hapo baadaye. Ni hatua ambayo haihitaji uzembe katika kuomba au
kumshirikisha Mungu; ni hatua inayotoa hatima ya aina gani ya ndoa au familia
itakavyokuwa. Itambulike kuwa: Uchumba siyo ndoa, hivyo waweza ukavunjwa au
kuvunjika na kukosea katika uchaguzi wa mchumba husababisha majuto na migogoro
isiyokoma katika ndoa na familia na hupelekea kutengana kwa wanandoa.
Nini cha Kufanya Endapo Kijana Ameshiriki Uzinzi (ngono) Kabla ya Ndoa?
Endapo kijana wa kike au kiume atakuwa ameshiriki ngono aidha kwa makusudi au
bahati mbaya (ni mara chache sana bahati mbaya hujitokeza) yampasa afanye mambo
yafuatayo ili awe safi mbele za Mungu na kujipanga kwa ajili ya kushiriki awapo ndani ya
ndoa tu:
Afanye toba ya dhati kwa Mungu kisha aache kabisa.
Abadilishe mienendo na mitindo yake yote ya maisha kwa kuacha yale yote yaliyokuwa
yakimvuta kufanya uzinzi.
Aepuke makundi rika yaliyo maovu na makundi mabaya yenye tabia mbaya na hatarishi
katika mienendo yake.
Ajilinde na vitu vinavyosababisha ama kuleta hisia za kimapenzi mfano sinema,
tamthiliya, programu za TV za mapenzi, majarida na vitabu vya mapenzi.
Aepuke kutembelea mazingira yenye ushawishi mkubwa wa kubadili hisia zako na
kutamani kufanya mapenzi.
Atenge muda mwingi kwa ajili ya kujifunza neno la Mungu kwa kusoma Biblia na
kushiriki ibada na programu mbalimbali za kanisa.
Apambane kwa kila namna ili kuzidi kuwa safi, na kupambana huko kusiwe kwa uwezo
wake pekee bali ajikabidhi kwa Yesu Kristo aliye mshindi wa dhambi na hutushindia
pia.
Achunge mdomo wake katika mazungumzo na aina ya mavazi anayovaa maana kwayo
huashiria urahisi na husadifu tabia ya mtu.
Aachane na tabia ya kuangalia picha na mikanda ya watu walio uchi au nusu uchi
maana huathiri ubongo na hisia pia.
= SURA YA 02 =
kwa kila kusudi chini ya mbingu”. Kunuia kwa mtu na kuwa tayari kutamwandaa kisaikolojia
pamoja na kujipanga kwa ajili ya azima hiyo. Kwa namna nyingine, kuingia kwenye ndoa sio
suala la kuigiza wala kujaribu, bali kunahitaji azima ya kuingia kwenye ndoa moja kwa moja.
Bidii ya Kazi
Mchumba anayefaa ni yule mwenye bidii katika kazi na siyo alichonacho, mali
alizonazo, kazi aliyonayo nk. Mtu mwenye bidii katika kutafuta anauhakika wa kufanikiwa,
hivyo mchumba huangaliwa katika kufanya kazi kwa bidii na mipango thabiti kwa ajili ya
kuyatafuta mafanikio kwa njia halali. Mithali 10:4 na Mithali 12:27; mafungu haya
yamesadiki juu ya bidii katika kazi. Kulingana na mfumo wetu wa elimu (miaka 16 na zaidi
hutumika kwa ajili ya elimu toka chekechea hadi chuo kikuu). Kumpata kijana aliyefanikiwa
kuwa na funguo tatu yaani nyumba, ofisi na gari ni nadra sana. Mara nyi watu hupata funguo
tatu uzeeni na umri wa kuoa unakuwa umepita. Hivyo, angalia mchumba aliye na bidii katika
kazi, ili muyatafute maendeleo katika ndoa kwa pamoja.
Hivyo kwa wale wanaotafuta wenzi wenye funguo tatu hasa kwa kijana, yampasa
amtafute mtu mzee, mtu aliyefiwa na mwenzi wake au kwa binti aingie katika ndoa ya
mitara. Mchumba mvivu na tepetevu na asiyejibidisha hafai kuwa mke au mume kwani dunia
ya sasa inahitaji kusaidiana katika kutafuta ili kuyafikia malengo mapema. Huu ni ushauri
wangu mwenyewe, maana uzoefu unaonesha madhara yake. Mfano baba ambaye ni mtafutaji
pindi anapofariki au kupata ulemavu wa kudumu au ugonjwa wa kudumu, familia huyumba
na kusambaratika. Hili jambo lipo hata kwa upande wa wanaume, maana wapo wasiotafuta
wala kujibidisha katika kutafuta hivyo kutegemea mahitaji yaliyo mengi kutoka kwa wake
zao (ambapo sio salama pia).
Chunguza Tabia
Kipengele hiki ni nyeti sana maana ndipo kiini cha mchumba anayefaa kuwa mke au
mume. Kipengele hiki kinabeba muktadha mzima wa mchumba mwema atokaye kwa
Mungu. kupitia tabia ndipo unaweza kupata mke mwema. Wasifu wa nje wa mtu kuutambua
ni rahisi sana kuliko wasifu wa ndani wa mtu; vivyohivyo tabia za ndani na tabia za nje kwa
mchumba. Ukikosea kuchunguza tabia ya mchumba katika kipindi cha urafiki, ni vigumu
kuzibaini tabia katika uchumba maana atazificha ili kulifikia lengo la kuolewa au kuoa.
Tabia ni sawa na ngozi, kuibadirisha ni vigumu sana (Yeremia 13:23). Usijipe moyo
kwa kusema na kufikiri “ngoja anioe au nimuoe kisha nitambadirisha tabia yake”. Japo pia
mwenye uwezo wa kumbadirisha mtu tabia ni Mungu, hivyo itahitaji maombi mengi na ya
dhati kwa kumuombea mchumba au mume au mke. Mafungu yaliyo katika Mithali 7:10-12,
Mithali 11:16 na Mithali 12:4 yanaeleza juu ya tabia bainishi zinazofaa na zisizofaa kwa mtu
anayemwabudu na kumcha Mungu wa mbinguni. Kuna aina kuu mbili za tabia na mfano
wake ni:
1. Tabia zinazojipambanua kwa nje: Tabia za nje zinajipambanua katika matumizi ya
ulimi wakati wa kuongea, mitindo au aina za mavazi anazo pendelea kuvaa (Mwanzo 3:7,
Kumb 22:5, 1pet 3:1-6), kujipamba kwake kwa sura au mwili na manukato (Hosea 2:13,
Wimbo 1:3, Ezekiel 23:40), vyakula na vinywaji apendeleavyo (Mithali 23:20-21). Tabia zote
za nje kuzibaini hazihitaji muda mrefu sana, mfano, si vigumu kumbaini mtu mchafu au
msafi.
2. Tabia zinazojipambanua kwa ndani: Tabia hizi hazionekani kwa urahisi maana ni
za ndani mno; mfano wa hizo ni wivu, upole, uchoyo, kutojali, dharau, mtazamo kwa kutaja
baadhi. Tabia za ndani huchunguzwa kwa muda mrefu sambamba na matendo ya huyo mtu.
Warumi 3:12 imezungumzia tabia njema zinatakiwa kuwa hata za moyoni. Ubainishaji wa
tabia hizi juu ya mtu, kunahitaji kiwango na ujuzi mzuri wa saikoloji. Kubadilika kwa tabia
hizi za ndani kunahitaji uwezo wa Roho Mtakatifu na utayari wa mtu baada ya kugundua
udhaifu na mapungufu yake.
Dini au Dhehebu
Dini au dhehebu katika mahusiano ni kipengele cha kuzingatia na kutilia maanani
zaidi. Inapendekezwa kuwa, wale wanaotarajia kuwa wenzi ni vyema ukawepo ufanano wa
dini au dhehebu. Kila dini na dhehebu kuna mafundisho yake (doctrines) ambayo
yanapishana kutoka dhehebu au dini moja kwenda dhehebu au dini nyingine. 1Wakorintho
1:10 na 1Wakorintho 1:12; aya hizi zinatoa umuhimu na faida za wanandoa kuwa wenye dini
au dhehebu moja, maana hawatapishana katika misingi ya mafundisho bila kuwagawanya
watoto katika imani za mafundisho. Ukitaka familia iwe chini ya kiwango katika mambo ya
kiroho, jaribu kuchanganya dini mbili tofauti miongoni mwa wanandoa katika ndoa.
Elimu
Kuna elimu ya kweli ambayo inahusu uelewa na maarifa juu ya Mungu wa kweli wa
mbinguni na elimu ya kidunia ambayo tunaipata shuleni kupitia mitaala ya masomo
mbalimbali. Nitazungumzia juu ya elimu ya kidunia ambayo inaweza ikaleta utofauti kwa
wachumba watakapo kuwa katika maisha ya ndoa. Inashauriwa kuwa wachumba
wanaotarajia kuoana wasipishane sana viwango vya elimu au walingane viwango vya elimu
ili kuleta uwiano katika mitazamo, uelewa na tafakari.
Sanjali na viwango vya elimu kuwiana au kutotofautiana, kigezo cha elimu lazima
kipewe nafasi ili kila mmoja kati ya wachumba kuridhia wao kwa wao, endapo mmoja hajui
kusoma wala kuandika au hajaenda vidato katika elimu. Suala la elimu pia laweza kutatuliwa
kwa wenzi kukubaliana katika kuendelezana katika masuala ya elimu. Mafungu yafuatayo
yanaelezea juu ya elimu ya kweli na elimu dunia: Mithali 4:13, Waefeso 5:22 na Esta 1:22.
Imani
Kipengele hiki ni sawa na kile kipengele cha dini au dhebu, lakini kinautofauti kidogo.
Suala la imani nalo ni jambo nyeti sana sawa sawa na kile kipengele cha dhehebu au dini juu
ya umuhimu wa wachumba kufanana kwa dhehebu au dini kabla ya kuoana. Yapendeza
wachumba wanaotaka kuoana wawe wa imani moja, maana kutofautiana imani huzaa
migogoro katika ndoa.
Zipo imani ambazo huruhusu kula vyakula vyote, kuoa na kuacha (kutalakiana),
kunywa pombe, kuoa wake wengi na kuvuta sigara, hivyo mwingine akiwa na masharti
katika hivyo vipengele, kutaleta migogoro mikubwa ndani ya ndoa. Sambamba na hayo, hata
taratibu za ibada kupisha kati ya imani moja na nyingine kwa wenza husababisha makwazano
miongo mwa wanandoa.
Suala lingine la msingi katika imani ni juu ya kiwango cha kiroho cha mchumba.
Inapotokea wachumba ni wa imani moja, suala la kiwango cha kiroho (imani) kwa mchumba
lafaa kuzingatiwa pia ili hapo baadaye wachumba hao watakapooana waweze kuwa na
familia yenye kiwango kizuri cha kiroho pamoja na malezi mazuri ya kiroho kwa watoto
wao.
Sio salama pia kutumia silaha ya kumtangazia mtu (mchumba) kuwa nitaolewa au
nitakuoa wewe endapo utabadiri imani yako na kuja kwenye imani yangu; kwa sababu
mchumba aweza kukubali kubadiri imani yake ili aolewe au kuoa kwa sababu ya kukidhi
hitaji lake na siyo kwa kuikiri imani.
Kitabu cha 1 Wafalme 11:4 kinasema hivi: “Maana ikawa, Sulemani alipokuwa mzee,
wake zake wakamgeuza moyo wake, afuate miungu mingine, wala moyo wake haukuwa
mkamilifu kwa BWANA Mungu wake, kama moyo wa Daudi baba yake.” Ni vyema
wachumba wanaotarajia kuoana wawaze pamoja, wanuie pamoja, watende pamoja, waamini
pamoja katika imani ili kuondoa mpasuko hapo badae wawapo kwenye ndoa yao.
Julisha Wazazi
Uchumba wa Yusufu na Mariam ulitambulika nyumbani kwao na jamii
inayowazunguka. Wakati mwingine hata urafiki utambulike kwa wazazi ili wazazi nao
wapime uaminifu wa rafiki huyo kama ilivyotokea kwa Musa (Kutoka 2:16-21). Wachumba
wanaotarajia kuoana ni vyema wakazijulisha pande zote mbili za wazazi wao ili kuweka
uwazi na kulinda uchumba wao ili kuepuka usaliti kama ambavyo wangekuwa wawili kwa
uchumba wa siri.
Huwa ni moja ya heshima kubwa sana kwa wazazi kujulishwa juu ya uchumba wa
binti au kijana wao endapo amefikisha umri wa kufanya hivyo ili nao wapate ya kushauri au
kutoa baraka zao kwa ajili ya hatua nyingine kuelekea katika ndoa.
Ulinganifu wa kiumri ni mzuri ili kubaini umri sahihi wa kuzaa pamoja na kuweza
kusimamia majukumu ya kifamilia. Kiafya inashauriwa kuwa, mwanamke asiendelee kuzaa
afikishapo umri kati ya miaka 34 hadi 36, hivyo ili mwanamke aweze kuzaa watoto watatu
wenye kutofautiana miaka mitatu; akichelewa sana mwanamke aanze kuzaa akiwa na umri
wa miaka 25 hadi 26 ili ukijumlisha miaka tisa ya tofauti ya watoto watatu, hivyo atakoma
kuzaa akiwa au kabla ya miaka 36. Jambo la kusisitiza ni kuwa si wote wanaoweza
kutendewa miujiza kama Sara alivyo zaa katika umri wa uzee (Mwanzo 17:17).
Sio vizuri pia kwa mwanamume kuchelewa kuoa, maana haipendezi kulea watoto
katika umri wa uzee, hivyo angalau mtu akichelewa sana miaka 32 awe ameoa. Sanjali na
hayo, kwa mtazamo wangu: umri wa miaka 18 hadi 25 kwa wanawake huwa ni umri wa
mabadiriko makubwa ya kimaumbile, na wengi wao hunenepa kutoka umbo la awali kwa
sababu ya mabadiliko ya kihomoni na maumbile. Umri wa miaka 25 na kuendele ndio umri
sahihi wa kutambua umbo la mwanamke maana atakuwa amepitia hatua zote za mabadiriko
ya kimakuzi.
Miliki Alizonazo Mchumba Zitambulike
Vijana wengi huwa hawana mali kwani huwa katika hatua za utafutaji wa mali.
Endapo kuna mali au miliki aidha za kurithi au kupewa na ndugu au jamaa; kunatakiwa
kuwepo ukweli na uwazi kwa wachumba juu ya mali na miliki walizonazo kwa kila mmoja
kabla ya kuoana.
Kukosekana kwa uwazi juu ya miliki au mali alizonazo mchumba kwa weza sababisha
kutoaminiana endapo siku moja miongoni mwao katika ndoa atabaini kuwa hakuwekwa
wazi. Kumficha mchumba juu ya miliki na mali hupelekea kupotea endapo mmoja atafariki
ghafla wakati wawapo katika ndoa. Uwazi wa miliki utawaweka huru wachumba wote
wanaotaka kuoana hapo baadae ili kurahisisha mipango ya maendeleo yao mapema.
Wakati mwingine mali alizonazo mchumba hujulikana bila hata kumuuliza mhusika,
kama ilivyokatika kisa cha kitabu cha Ruthu, ambapo Ruthu alitambua mali za Boazi kwa
kumuona katika usimamizi wa hiyo miliki yake (Ruthu2:3-4). Jua kuwa: Boazi alikuwa mzee
katika umri, hivyo mali zake alikuwa amezitafuta tangu enzi za ujana wake, hivyo ni tofauti
na vijana wengi ambao huwa hawana mali, kwani huwa katika mchakato wa kutafuta mali.
Ruhusa ya Wazazi
Ruhusa toka kwa wazazi huwa ni jambo la msingi sana kwa wachumba ili kuweza
kuoana. Mbaraka wa wazazi ni bora na mhimu kwa wachumba katika safari ya kuoana na
kuanzisha familia. Tena ni vyema pande zote za wazazi zikaridhia ili wachumba kuendelea
na mchakato wa kufanikisha ndoa. Kuridhia kwa wazazi hutengeneza upendo kila upande wa
wazazi wa wanandoa katika familia (soma Mwanzo 29:21-23).
Japo kunawakati pia wazazi hupinga kulingana na mila, wakati mwingine utashi wao
au imani, hivyo mtii baba na mama katika misingi ya Kibiblia na sio misingi iliyo nje na neno
la Mungu. Hekima ya wachumba katika kushauri itumike pale inapoonekana kuwa wazazi
hawako sahihi kwa yale wanayolazimisha kulingana na neno la Mungu linavyo elekeza, na
pia mazuri yaliyo mema ya wazazi wachumba wayafuate na kuyatii.
Samsoni mnadhiri wa Mungu alipingwa na wazazi wake kwa jambo jema kabisa; yeye
mwenyewe alikengeuka kwa utashi wake mwenyewe. Ukisoma Waamuzi 14:1-4 inaonesha
kuwa wazazi wake Samsoni walimpinga kwa ombi lake baya. Maamuzi yake Samsoni
yalikuwa kinyume na imani kama mnadhiri wa Mungu hivyo ilimgharimu mateso na hadi
kifo akiwa mateka katika himaya ya Wafilisti waabudu miungu.
Mianga. Mwanamke mwanandoa mtarajiwa lazima ajenge tabia ya kuvaa viatu vya matatizo
ya wengine, ahurumie na kukumbuka kuwaombea walio katika shida na changamoto.
Mwanamke ambae ni mke mtarajiwa yampasa kuwa mwangalifu ili kujipatia mume
mwenye tabia njema. Katika 1Samweli 25:1-42, mtumishi wa Mungu Daudi alipanga
kumwangamiza Nabali kwa sababu ya kukosa hekima ya maneno na fadhira juu ya yale
Daudi aliyomtendea katika kumlindia mifugo yake, lakini Abigaeli mkewe Nabali
alijishusha kwa Daudi; kwa kutumia hekima na maneno mazuri alifanikisha kumuepushia
mumewe na upanga wa Daudi.
waangalifu daima katika hatua zao za uchumba, na haina haja ya kuchelewa kuoana kama
hakuna kipingamizi cha kuwachelewesha.
kwenye gunia. Vijana wanajiaminisha kuwa upendo wa kweli huja pale wanapovuliana nguo
na kuzini. Dhambi ni dhambi hata kama itapakwa rangi au kupuliziwa pafyumu iliyokali kiasi
gani.
9.Upofu unaopelekea kutorudi nyuma wala kujitambua (Mithali 7:21-22): Kijana
anaweza kuwa ameshauriwa na viongozi wa dini, wazazi hata watu wengine wa karibu yake
juu ya mtu anayetaka kumuoa au kuolewa naye, kuwa hafai lakini kijana hasikii wala haelewi
chochote maana amekuwa kipofu wa utambuzi, hivyo, mwisho wa siku anaangukia katika
mwenzi asiyestahili.
10. Hujiaminisha kuwa watawabadirisha tabia (Mithali 7:23): Vijana hujiaminisha
kuwa watawabadirisha tabia wenzi wao wa wapo ndani ya ndoa. Kuingia na mtu katika ndoa
asiye mwenzi mwema kunaleta maumivu katika mioyo ya wanandoa, maana siyo rahisi
mwanadamu kumbadirisha mwanadamu mwenzie bali ni Roho wa Mungu na kwa msaada wa
Yesu Kristo pekee ndiye anaweza kuibadirisha tabia na mienendo ya mwanadamu.
mimba na kukataana pia. Njia hizo zote, siyo salama na ni dhambi kushiriki ngono kabla ya
ndoa.
5. Pia vijana hutumia njia ya kufanya ngono kwanza kama zawadi au kigezo cha
kufanikisha azima yao ya kuoana hapo baadae. Wanatumia kushiriki tendo la ndoa kama
sehemu ya kuthibitisha na kutakiana upendo. Mithali 6:32-33 inasema aziniye hana akili,
hivyo ni dhambi kufanya tendo la ndoa kabla ya ndoa kwa makusudi ya kumshawishi mtu
akupende kwa kumvulia nguo.
6. Njia nyingine isiyo salama inayotumiwa na vijana kujipatia wenzi ni kwa kutoa
rushwa, hususani zawadi (Mithali 18:16) ya kushawishi upendo. Rushwa au zawadi
itolewayo ili kuteka upendo wa mwingine inajumuisha kutoa pesa, vitu, tendo la ndoa na
kubeba mimba (kwa upande wa mabinti) ili kuteka upendo wa mwingine. Mambo ya Nyakati
16:19 imekataza maana hizo rushwa hupofusha macho.
7. Msukumo wa nje nao una nguvu kubwa unaotengeneza njia za kujipatia wenzi wa
maisha kwa vijana. Kijana anapendekezewa na kushawishiwa na marafiki zake juu ya mtu
fulani kuwa mwenzi. Njia hii imekuwa ikitumika hata kwa wazazi kuwachagulia wenzi wa
maisha watoto wao. Pia sio njia sahihi ya kujipatia mwenzi maana sio msukumo wa ndani wa
Roho mtakatifu.
= SURA YA 03 =
“Wewe ndiwe chemchemi ya bustani yangu, Kisima cha maji yaliyo hai, Vijito
vya Lebanoni viendavyo kasi”
Wimbo Ulio Bora 4:15
“Wakristo wote wenye shauku ya kuwa na nyumba bora ya Kikristo lazima watambue
kuwa, katika maisha ya kiulimwengu, thamani ya mtu inapimwa kwa mali aliyonayo. Lakini
vitabu vya mbinguni vinaandika thamani ya mtu inatokana na uwiano wa mema
aliyoyakamilisha kwa kutumia mali alizokabidhiwa na Mungu” [E. G. White 2 Selected
Message Vol.2, 193].
Suala la kuoa au kuolewa ni suala linalohitaji uangalifu katika kufanya maamuzi ya
kukubari kuingia katika ndoa. Siyo salama kukubari kuingia kwenye ndoa ingawa
kunamambo unayaona kwa mchumba wako hayako sawa. Katika hatua ya uchumba huwa
kuna maamuzi makuu mawili; uamuzi wa kuvunja uchumba au uamuzi wa kuendelea na
hatua za kufunga ndoa. Katika sura hii tutaona sababu zinazopelekea kuvunjika kwa
uchumba pamoja na utayari wa kuingia katika ndoa.
kunakuwa na hatia ndani ya hao wachumba kwa sababu ya kuwa wamevunja sheria ya
Mungu tayari. Kushiriki tendo la ndoa kwa wachumba husababisha kuchukiana na ule
upendo wa kweli wa awali hupotea, maana panakuwa hakuna wanachokitumainia kukipata
hpo baadaye katika ndoa yao.
Kutokudumu kuomba ili kuifikia adhima ya kufunga ndoa (2Wakorintho 11:14):
Maombi pekee yaweza kuvunja uchumba kama mchumba aliyepatikana siye sahihi kuoana
naye, maana Mungu huwaepushia changamoto wale wanaomtumainia. Wakati mwingine siyo
salama kutodumu kuuombea uchumba maana maadui na mawakala wa Shetani hawakosi
kuushambulia uchumba ili uvunjike kwani nguvu za giza pia hutawala pasi na maombi ya
dhati, hivyo uchumba unaweza ukavunjika kwa sababu ya kukosa maombi ya dhati miongoni
mwa wachumba ili kuifikia ndoa.
Kutolipa umuhimu wa kutosha suala la ndoa: Kuna watu huanzisha uchumba
ingawa hawana dira yo yote katika kuifikia ndoa kama ilivyo azima ya kuuanzisha uchumba.
Panapoanzishwa uchumba bila malengo yo yote kwa wachumba, safari ya uchumba huwa
siyo ndefu kwa sababu uchumba huo huwa hauna madhumuni yo yote ya kuifikia ndoa.
Elimu inapaswa kutolewa kwa vijana wa Kikristo ili wajue madhumuni makuu ya kuanzisha
uchumba ni yapi.
Usiri wa uchumba na kukosa washauri sahihi (Mithali 12:15): Uchumba wa kificho
bila pande mbili za wazazi kujua au mashemasi wa kanisa kujua, uchumba huo hauwezi
kuwa na washauri wa maana ili kuwepo na mwelekeo mzuri wa wachumba kuifikia ndoa.
Uchumba wa kificho huishia katika kupotezeana muda kwa wachumba kisha kuachana.
Uchumba wa namna hii ulio wa giza au wa vichakani na vichocholoni si salama na wala sio
aina ya uchumba unaofaa, maana si wawazi.
Kuamini maneno ya watu bila kutafiti (Mithali 18:21): Kushikiwa akili na mtu juu
ya kutoa taarifa sahihi bila kufanya utafiti na kujiridhisha juu ya mwenendo mzima na tabia
ya mchumba nalo ni tatizo maana si wote wanaotoa taarifa wanania njema juu ya ustawi wa
uchumba unaoendelea. Mara nyingi si kila neno linalokuja kutoka kwa watu juu ya mchumba
linaweza kupokelewe zima zima bali mhusika kulichuja na kujiridhisha mwenyewe.
Uchumba waweza kuvunjika pale tu wachumba wanapokuwa na masikio yanayosikiliza
maneno kutoka kwa watu juu ya uchumba wao.
Wachumba kukosa muda wa kuwasiliana au kuzungumza kwa pamoja:
Kukosekana muda wa mazungumzo na mawasiliano ya uhakika kwa wachumba hujenga
uchumba usiokuwa na mikakati, kukumbushana na ari ya kuifikia ndoa. Wakati mwingine
kukosekana kwa mazungumzo na mawasiliano ya karibu husababisha upendo kuchuja
miongoni mwa wachumba, kisha uchumba waweza huvunjika.
Mazoea na tabia ya kuacha au kuachwa na wachumba: Tabia iliyojengeka katika
mazoea ya kuacha au kuachwa na wachumba husababisha kujenga hali ya mazoe ya kuachwa
au kuacha. Kuizoea hiyo tabia huleta mazoea hivyo kila uchumba unaoanzishwa huvunjika
kwa sababu ya kutoona madhara au maumivu wala cha kupoteza katika kuvunja uchumba.
Kutokuwa na kazi au chanzo sahihi cha uchumi (Mwanzo 2:15): Vijana baadhi wa
kiume walio Wakristo huvunja uchumba kwa sababu ya kutokuwa na kazi itakayoweza
kuleta pesa kwa ajili ya kufanikisha kupatikana kwa mahitaji ya msingi ya kifamilia katika
ndoa. Vijana wa kike wao huvunja uchumba kwa sababu wachumba wao hawana chanzo
sahihi cha uchumi, bila kujua kuwa mafanikio na maendeleo ya uchumi katika ndoa ni
kusaidizana wote wawili.
kiasi, na kuwa safi, kufanya kazi nyumbani mwao, kuwa wema, kuwatii waume zao wenyewe,
ili neno la Mungu lisitukanwe”.
Tambua kuwa uamuzi wa kuoa au kuolewa, unaweza ukabadilisha
utumishi au wito wako kwa Mungu: Wakati mwingine ndoa inaweza ikabadirisha uelekeo
wa mtu kwa kazi aliyoitiwa na Bwana hususani kama mmoja wa wanandoa hajui umuhimu
wa kumtumikia Bwana kama moja wapo ya wito mkuu. Kitabu cha Waamuzi.16:21 (japo
siyo mfano sahihi wa aina ya ndoa) ni kisa kinachomwelezea Samsoni kutojikita katika wito
wake kwa sababu ya kuingia kwenye mahusiano na mwanamke asiye wa imani yake na
mwishowe adui wakamkamata. Fungu hilo linasema: “Wafilisti wakamkamata wakamng’oa
macho, wakateremka naye mpaka Gaza, wakamfunga kwa vifungo vya shaba naye alikuwa
akisaga ngano katika gereza”
Jua ya kuwa utaongeza marafiki au madui: Uamuzi wa kuoa au kuolewa unaweza
wakati mwingine kukuletea marafiki au maadui maana ni muunganiko wa watu wawili.
Hesabu.12:1-2 inaonesha wazi kabisa ya kwamba uoaji wa Musa ulileta mgogoro katikati
yake na ndugu zake (Miriamu na Haruni). Cha kuzingati endapo umeamua kuingi katika ndoa
jiandae vyema kuwapenda maadui na marafiki watakao kuzunguka katika familia na ndoa
kama lilivyo agizo la Biblia usiwalipe baya kwa baya bali lipa jema kwa kila baya na jema.
Jihoji kama upo tayari kuzaa, kulea na kuhudumia watoto: Je nipo tayari kuzaa,
kutunza na kulea watoto? Ni swali la msingi kujiuliza kabla ya kufanya maamuzi ya kuingia
katika ndoa. Kuwahudumia watoto na kuwalea vyema ni jambo lisilohitaji mjadala kwa
wanandoa. Lakini pia tambua kuwa kupata watoto ni mapenzi ya Mungu na siyo mapenzi ya
mwanadamu hivyo mtegemee Mungu akupatie watoto kwa uzuri wake uutakao.
Zingatia: Baada ya kufanya maamuzi sahihi ya kuingia katika ndoa jitahidi katika
kumtii BWANA (mfanye kuwa wa kwanza) na muombe akupe maisha marefu na huyo
mwenzi wako huku mkizingatia kanuni za afya katika kweli yote ya maisha yenu ya ndoa.
Fundisho Kutoka Kwenye Kitabu cha Ruthu Juu Uchumba na Hatima ya Ndoa
Ruthu alikuwa ni binti wa Kimoabu aliyeolewa katika familia ya Kiebrania. Kitabu
cha Ruthu kinatoa dondoo nyingi za kujenga katika ufahamu mpana wa mahusiano ya
uchumba na ndoa kwa Wakristo. Kitabu hicho kimejengwa na wahusika wakuu watatu yaani
Ruthu, Naomi na Bozi.
Sura ya kwanza ya kitabu cha Ruthu inaelezea uaminifu na utiifu wa Ruthu kwa
Naomi; sura ya pili inaelezea jinsi Ruthu alivyoweza kufahamiana na Boazi; sura ya tatu
inamhusu Naomi katika kumtia moyo na kumhamasisha Ruthu kuolewa na Boazi na ile sura
ya nne, Ruthu na Boazi wanaoana na kuzaa mtoto wa kiume aliyeitwa\ Obedi babu yake na
Daudi ukoo aliozaliwa Masihi Yesu Kristo.
Ndani ya kitabu cha Ruthu, yamo mambo mengi ya kuwafunza wachumba na
wanandoa kama muhtasari wa sura hii ya kitabu; hususani juu ya mambo machache
yafuatayo:
Mchumba mwema ni yule mwenye tabia ya kutii na kufuata maelekezo ya wazazi
yaliyo na tija (Ruthu 3:1-12).
Mchumba wa kweli lazima aoneshe nia ya kuoa au kuolewa naye huyo mchumba
(Ruthu 3:8-9).
Mchumba mwema ni yule mwenye kuonesha tabia ya kujali watu wengine (Ruthu
2:5).
Mchumba mwema ni yule mwenye tabia ya kuhurumia na kusaidia wengine (Ruthu
2:8).
Mchumba yampasa awe na tabia ya kuheshimu na kuonesha unyenyekevu (Ruthu
2:10).
Mchumba mwema ni yule mwenye tabia ya ukarimu (Ruthu 2:14, 16).
Mchumba mwema ni mwenye kumtumainia Mungu kwa kila jambo katika maisha
yake (Ruthu 2:20).
Mchumba mzuri ni yule aliye msafi na nadhifu na sio kwa sababu ya mapambo (Ruthu
3:3).
Mchumba mzuri ni yule mwenye washauri wema ili kufanikisha uchumba na siyo
kuubomoa (Ruthu 3:1-2).
Uchumba wa kweli hauhusishi ngono kabla ya ndoa (Ruthu 3:7-9).
Mchumba mwema ni yule aliye mwaminifu na watu wamshuhudie hivyo pia (Ruthu
3:11).
Uchumba wa kweli hauangalii vitu, talanta ama mali bali upendo ulio wa dhati (Ruthu
3:10).
Uchumba lazima uwe wa wazi kwa ndugu, jamaa na marafiki (Ruthu 4:9-11).
Uchumba wa kweli wenye uaminifu, huzaa ndoa yenye mibaraka (Ruthu 4:13).
= SURA YA 04 =
Kutiana moyo na kuonyana kwa upole: Kutiana moyo, kuonyana kwa upole
miongoni mwa wanandoa ni suala la msingi katika kunyanyuana na kuelekezana (Mathayo
27:19, 24, 2Wafalme 4:8-11).
Kulindana: Wanandoa walindane katika uaminifu, kufichiana mapungufu na
kujaliana wao kwa wao (Yeremia 31:22).
Uwepo wa utii na upendo kwa wanandoa: Wanandoa wafuate kanuni rahisi ya
kibiblia inayohusu kutii na kupenda ili kuepuka vishawishi na kudumisha amani ya ndoa.
Waefeso 5:22-25.
Uhusiano wao ujengwe katika unyenyekevu unaopatikana kwa kuongozwa na
Roho Mtakatifu: Roho mtakatifu akitamalaki katika familiya, familia itakuwa mbingu ndogo
maana Roho mtakatifu hakai katika machafuko hivyo wanandoa waombe uwepo wake Roho
Mtakatifu. Tazamama Mithali 29:23; Isaya 57:15; Wafilipi 2:1-8.
o Kila mmoja katika ndoa ajue ya kuwa hakuna aliyemkamilifu kama malaika,
bali wote wameathiriwa na dhambi na pambano kuu bado linaendelea hivyo,
wote ni wadhaifu.
o Wanandoa wasimshirikishe mtu ye yote nje ya ndoa mambo yao ya siri yaliyo
ndani ya ndoa, hususani yale yanayoonesha udhaifu wa mwingine maana
itakuwa ni kumwaibisha na kujiaibisha pia kwa anayevujisha siri.
o Kila mwanandoa afikirie katika mtazamo chanya juu ya mwenzi wake. Mara
zote imeoneka wanamume huwafikiria hasi wanawake katika ndoa; ubaguzi huu
haufai katika familia ya Mkristo.
o Yawapasa wanandoa kuvaa mavazi yanayostiri mwili vyema ili wote wawe
mfano bora kuanzia kwa watoto wao na jamii nzima inayowazunguka.
= SURA YA 05 =
Shetani amekuwa na anazidi kushambulia tasisi takatifu ya ndoa, maana anajua kuwa
akiharibu ndoa atakuwa amefanikisha kuuharibu ulimwengu wote na kuweza kuwafanya
wanadamu wengi kuanguka na kufia dhambini na kuukosa ufalme wa milele.
Ndoa ya Hawa na Adamu (mke mmoja na mume mmoja) iliyoasisiwa na Mungu
mwenyewe katika bustani ya Edeni (Mwanzo 2:18-19) iliingia hitirafu kutokana na Shetani
kuweza kuwashawishi wanadoa hao kuasi maagizo ya Mungu juu ya kutokula matunda ya
mti wa ujuzi wa mema na mabaya ambao Mungu aliwakataza wasiule (Mwanzo 2:16 -17).
Shetani alifanikisha adhima yake ya kuwaangusha wanandoa hao wa awali (Mwanzo
3:1-6) na hapo ndipo dhambi ikaingia katika ulimwengu na utukufu wa mwanadamu
ukatoweka, maisha ya umilele ya kapotea, shida, mateso na majanga ya kaanza kwa sababu
ya wanandoa hao kuasi maagizo ya Mungu.
Ndoa na familia zetu zaweza kuchangia kwa sehemu kubwa kuiharibu jamii, taifa na
ulimwengu au kuuletea amani pia. Hivyo, kama mzazi fanya sehemu yako katika kulea
watoto katika misingi ya wema na utii kwa Mungu ili hata kama watoto watakengeuka
ukubwani huko baadaye utakuwa umenawa mikono na upotevu wa roho zao Mungu
hatakudai maana ulifanya sehemu yako kama mzazi.
Mtoto aliyelelewa katika kweli yote ya Mungu kisha akakengeuka katika kuitii kweli
na maagizo ya Mungu hayuko katika familia za sasa tu bali palitokea hata katika familia ya
Hawa na Adamu hapo mwanzo kabisa. Kwa kuwa Shetani ambaye ni simba aungurumaye
hutafuta kuwapoteza wengi (1Petro 5:8) yumkini hata walio wateule ndivyo ilivyotokea
katika familia ya awali.
Chukulia kama jambo la kujifunza katika familia ya Adamu na Hawa; walizaa watoto
wawili wakiume nje ya bustani ya Edeni kama ilivyotajwa na Biblia. Swali la kujiuliza “kwa
nini familia hiyo yenye malezi katika misingi ya Mungu, Kaini aasi na Habili atii taratibu
zote za imani na ibaada?” Jua kuwa, Shetani hakomei kuwavuruga wanandoa pekee bali hata
wanafamilia yumkini hasa watoto.
Mwanzo 4:3-5 inaonesha kuwa, katika hawa watoto wawili panajitokeza mgawanyiko wa
makundi mawili ya ibada; yaani ibada ya kweli (ya Mungu kutoka kwa Habili) na ibada ya
uongo (ya Shetani kutoka kwa Kaini).
Kutokana na ukengeufu wake Kaini, Mungu anamuonya Kaini kutokana na uasi wa
taratibu za ibada alizoziweka Yeye Mwenyewe (Mwanzo 4:6-7). Wivu wa Kaini juu ya
Mungu kupokea ibada ya Habili; Kaini anaamua kumuua mdogo wake (Mwanzo 4:8).
Shetani akamshupaza shingo Kaini na akawa hamsikilizi Mungu maana alimwona si cho
chote kwake tena ambapo Kaini anakuwa jeuri hata katika majibu yake kwa Mungu
Muumbaji (Mwanzo 4:9).
Mungu anampatia Kaini laana na kumtenga ili kuwa mbali na uzao wa familia ya
watakatifu (Mwanzo 4:10-16). Tukio la Kaini kuasi; Adamu na Hawa hawakuwa na hatia
kwa Mungu maana walitekeleza malezi mpaka watoto wao walipoanza kujitegemea kwa
mambo mengi; hasa ibada, na uzalishaji. Kwa sababu hiyo Adamu au Hawa walifanya
sehemu yao mpaka walipojitambua. Ili kujua kuwa Kaini na Habili walifundishwa vyema,
wanaonekana katika ufanano ufuatao: Wote walifundishwa na wazazi wao jinsi ya utoaji wa
sadaka ya kuteketeza katika ibada zao kwa Mungu.
Wote walitengeneza madhabahu kwa ajili ya kutoa sadaka zao kwa Mungu. Wote
walisimama kama wafanya ibada mbele za Mungu wa Mbinguni. Lakini utofauti wa Kaini na
Habili unajipambanua katika mambo yafuatayo: Kaini alikengeuka na kufanya matakwa yake
badala ya maelekezo ya Mungu katika ibada. Habili alienenda katika taratibu na sheria za
Mungu katika ibada na utoaji wa sadaka ya kuteketeza. Hivyo basi, Kaini anawakilisha
kanisa au mtu asiyefuata taratibu alizoziweka Mungu. Habili anasimama kama kanisa au mtu
ambaye ni mtiifu na mfuata taratibu na sheria za Mungu.
Funzo kutoka kwa Habili na Kaini watoto wa Adamu na Hawa ni katika mambo
yafuatayo: Habili ni mfano wa wafia dini katika familia au kanisa la Mungu bali Kaini ni
muasi wa sheria katika familia na kanisa la Mungu. Wanandoa wajue ya kuwa Mungu
haangalii matukio au matendo yetu ya nyuma ili atuhesabie haki na kufuta makosa yetu ya
hivi karibuni (kama Kaini alikengeuka mwishoni na ya nyuma yote Mungu hakuyatazama
maana alijua anajua na alimuonya pia).
Watoto katika familia wafundishwe kuwa, Mungu anaangalia katika utii wa kufuata
taratibu na maagizo yake pekee. Watoto wajuzwe kwamba Mungu anapokea ibada zetu,
endapo tutaenenda kwa utaratibu na utii juu Yake Yeye pekee. Wanafamilia ambao ndio
sehemu ya kanisa wajue ya kuwa dini, madhehebu na watu watungao ibada zao wenyewe
zisizompendeza Mungu au yasiyo maagizo ya Mungu; Mungu hazipokei wala kuzitambua
hivyo, wafanya ibada bure na yaweza kuwa wanamwabudu Shetani na siyo Mungu.
Watoto wafundishwe kuwa kabla ya kumwendea Mungu, yawapasa kujua kuwa ni
kitu gani kitasababisha ibada au maombi yao yasipokelewe na Mungu. Watoto wajuzwe pia
kuwa, katika ibada Mungu aweza asijibu maombi yao kwa sababu ibada zao haziko katika
usahihi au utaratibu wa Mungu. Wanadoa na watoto wajue kuwa haiwapasi kushupaza shingo
kama Kaini ili wasije wakapotea na kupelekea kutourithi uzima wa milele.
Siku zote wanafamilia au wanandoa na watoto wao yawapasa kujitahidi kadri ya
uwezo wa Roho Mtakatifu kufanya toba wanapokosea au kutenda dhambi ili ibada zao
zipokelewe na Mungu sawasawa na mapenzi Yake. Mwisho kabisa, wanandoa na watoto wao
watambue ya kuwa, yule asiyetii juu ya sheria na maonyo, ajue Mungu huongeza laana
badala ya baraka, hivyo mkono wa Mungu huondoka juu yake.
Shetani anajua kuwa, mtoto mmoja akimwasi Mungu, hapo baadaye atakuwa na jeshi
kubwa kama alivyofanya kwa Kaini, ambapo vizazi vyake vilileta maafa kwa ulimwengu
hadi kipindi cha Nuhu. Uasi wo wote wa mwanadamu juu ya sheria na taratibu za Mungu
hufika kikomo na wamchao hupata neema Yake kama ilivyokuwa kipindi cha Nuhu
“BWANA akaghairi kwa kuwa amemfanya mwanadamu duniani, akahuzunika moyo. BWANA
akasema, nitamfutilia mbali mwanadamu niliyemwumba usoni pa nchi; mwanadamu na
mnyama, na kitaambaacho na ndege wa angani; kwa maana naghairi kwamba nimewafanya.
Lakini Nuhu akapata neema machoni pa Bwana” (Mwanzo 6:6-8).
ikigundulika huwa ni aibu ya wote (wanandoa) na wanandoa huona haya na aibu machoni pa
watu maana ni aibu kwao na wamemuaibisha Mungu.
kucheza na ndoa, tasisi aliyoiweka Mungu ili tuujue upendo wake na sisi wanadamu tutii
kwake kama ilivyo mwanamume hupenda na mwanamke hutii katika upendo wa mumewe.
Yesu alilipenda kanisa hivyo waume nao wawapende wake zao ili kanisa la Mungu liwe
takatifu na safi.
Katika jambo la kiroho, Yesu Kristo anasimama kama Bwana harusi na kanisa (na
watu wake) ni bibi harusi. Hivyo ndoa zetu zikiwa takatifu tutazalisha kanisa safi na takatifu,
na Yesu ajapo alitwae kanisa la Mungu lililo katika Ufunuo 12:1-6, ambalo ni kanisa safi na
bikira maana mafundisho yake ni safi, bali lile la Ufunuo 17:1-18 ni kanisa katika mtazamo
wa mwanamke kahaba asiye bikira maana halijatunza usafi wa mafundisho kwani limefanya
uzinzi wa kiroho.
Yesu anabisha ili aingie katika kanisa lake na ndoa zetu (Ufunuo 3:20-21) hivyo,
tumpokee ili tukaketi naye tukiwa washindi wa dhambi ndani ya kanisa ambalo ni bibi harusi
safi likifanya hukumu kwa mika 1000 na Bwana wake huko mbinguni na washiriki wake
wakiwa wamekula ule mti wa uzima na kubadirishwa tayari (Ufunuo 22:2).
= SURA YA 06 =
“Ndoa yenye mafanikio, inaupendo usiokoma kwa mwenzi yule yule kila
siku. Ndoa yenye upendo hakuna kinachoharibika”
Frank P. Karoli
Hakuna umoja katika ndoa unaopatikana bila jitihada za wanandoa kuupalilia umoja
huo. Umoja katika ndoa ni safari ambayo kila mwanandoa lazima awe na shauku na utayari
wa kuhusika. Umoja huo kwa wanandoa lazima uwe wenyekutoa nafasi ya kumilikiana wao
kwa wao, ukaribu na muunganiko wa kimapezi. Ukweli ni kwamba, ndoa siyo tu nini
tunaweza kukipata na kunufaika nacho, bali utayari wa kutoa pia. Wakati ambapo kila
mwenzi anapotoa upendo wake kwa mwenzie na mtazamo wa furaha yake kwa mwingine,
lazima patokee matunda mema ya umoja katika ustawi wa ndoa.
Familia baadhi za Kikristo zipo katika changamoto na mitikisiko mikubwa ya kila
aina, hivyo, zinahitaji msaada wa hali ya juu kutoka kwa viongozi wa kanisa na watumishi
wa Mungu walio kielelezo chema na mfano mwema kwa jamii na kanisa kwa ujumla. Kanisa
na viongozi wake wanapaswa kutambua kuwa ndoa baadhi za washiriki zipo katika
changamoto nyingi sana. Zifuatazo ni baadhi miongoni mwa changamoto nyingi zilizo katika
familia baadhi za Kikristo:
Zipo familia zimepungua katika mambo ya kiroho (imani kwa Mungu).
Zipo familia za Kikristo zimepungua katika kusoma neno la Mungu ipaswavyo.
Katika familia baadhi, elimu ya kidunia imepewa kipaumbele kuliko ya Mungu.
Zipo familia ambazo uaminifu umepungua miongoni mwa wanandoa.
Zipo familia zimeathiliwa sana na maendeleo ya utandawazi na teknolojia.
Zipo baadhi zimeugeukia ulimwengu katika mitindo na mienendo ya maisha.
Zipo ambazo kazi imekuwa kikwazo cha kutii na kutunza amri na sheria za Mungu.
Zipo familia baadhi zimo katika migogoro inayotishia ustawi wa ndoa.
Zipo familia ambazo wanandoa wanaishi kwa kuvumiliana si kwa upendo.
Familia baadhi za Kikristo zimevunjika na kuhatarisha malezi ya watoto.
Hivyo basi, kanisa na viongozi wake wafanye mambo yafuatayo ili kuzinusuru familia za
wakristo:
1. Kanisa lifundishe mafundisho mengi na nyeti juu ya kaya na familia ili kuzinusuru
ndoa na familia za Kikristo. Hivyo, Makanisa yajenge tabia za kutoa semina mara kwa mara
kwa wanandoa.
2. Programu na mafundisho maalumu juu ya mambo ya kimahusiano yatolewe
ipaswavyo kwa vijana walioko ndani ya kanisa.
Mtume Paulo naye katika 1Wakorintho 7:10 anasisitiza kuwa waliooana wasitengane
na kama watakosana wasameheane wao kwa wao na kupatana. Marko naye anasema kuwa
kilichounganishwa na Mungu, mwanadamu hawezi kukitenganisha (Marko 10:9). Katika
Mathayo 19:9 Yesu anakataza kuachana, tena kwa habari ya uasherati wanandoa wanaweza
wakaachana, lakini asioe wala kuolewa miongoni mwa waliotalakiana. Kwa misingi hiyo
basi, kuachana siyo jambo rahisi maana walioachana hawaruhusiwi kuoa wala kuolewa.
Pamoja na habari ya uasherati inatoa nafasi ya kuachana kwa wanandoa lakini
panaweza kuwepo na mashauri, uvumilivu na kuonyana ili kuiponya ndoa katika kuachana.
Hivyo, talaka au kuvunja ndoa sio jambo jepesi zaidi sana ni kusameheana na kuvumiliana
pamoja na kuruhusu hekima ya kimbingu itawale. Biblia inabainisha sababu kuu tatu (3) za
wanandoa kuachana au kukoma kwa ndoa: 1. Kifo (Warumi 7:2-3), 2. Imani (1Wakorintho
7:15) na 3. Uasherati (Mathayo 19:9).
huanza kujitangamanisha wao kwa wao bila kutatua hizo hitilafu kana kwamba
hawajakoseana chocho bali hukaa na jambo au mambo moyoni bila kuyatagfutia suluhu.
Ni kosa kubwa kwa wanandoa kuchukulia kuwa hawajakoseana na kukaa bila kutafuta
suluhu. Hali hii huwa ni hatari sana katika ustawi mzima wa ndoa, kwani huacha mioyo
ikiwa na utungu wa muda mrefu. Kila tatizo liletalo maumivu ya kihisia litatuliwe haraka na
kufutwa makosa kisha maisha ya amani na upendo katika Kristo yaendelee kama hapo awali.
Njia salama ya kuondoa hitilafu kwa wanandoa ni pale wanandoa wanapokubali kuwa:
kukoseana huwepo, hivyo, wajue kusameheana ili wapate kibali mbele za Mungu badala ya
dhambi kuzidi kuotea (Mwanzo 4:7).
Ndoa yo yote iliyojengwa katika kumtumainia Mungu na kuipa kipaumbele mipango
ya Mungu, hapawezi kuwa na migogoro ya mara kwa mara, bali amani itatawala daima
kwani wanandoa hao watakuwa wanaujua vyema upendo wa Kristo na wataudumisha
vivyohivyo katika ndoa yao (Yohana 13:17) katika kusameheana na kufutiana makosa yote.
Sara kuzaa, familia ikawa na watoto wawili ambao ni Ishimaeli kutoka tumbo la Hajiri
(mjakazi) na Isaka kutoka tumbo la Sara mke halali wa Ibrahimu.
Watoto hawa ndio chanzo kikubwa cha mgogoro uliowatenganisha makazi baina ya
Hajiri na Sara (Mwanzo 21:8-10). Hivyo basi, kupitia familia ya Ibrahimu na Sara,
kunamambo machache ya kujifunza kama wanandoa na wale wanao tazamia kuingia katika
tasisi takatifu ya ndoa:
1. Abramu ni mfano wa mwanamume mwenye kusikiliza ushauli kutoka kwa mkewe
(Mwazo 16:2-3) na mwenye kusimamia haki (Mwanzo 16:6, 21:10-11). Wakati mwingine
imeonekana kuwa mwanamke hana wazo au neno lolote lenye tija linaloweza kujenga katika
ndoa. Kwa Ibrahimu haikuwa hivyo kwa mkewe; ndivyo yawapasa wanaume kuwa katika
ndoa zao. Ikumbukwe pia kuwa, kabla ya dhambi kuingia, mwanamke na mwanamume
walikuwa wenye daraja sawa na wote waliitwa Adamu baada ya kuumbwa ili kudhihilisha
kuwa mwanamke ametokana na ubavu wa mwanamume, hivyo ni mwili mmoja (Mwanzo
5:2); bali baada ya dhambi kuingia mwanamume alipewa mamlaka ya kumtawala mwanamke
(Mwanzo 3:16), .
2. Sarai ni mfano wa mwanamke mwenye kigeugeu juu ya maamuzi yake, (Mwanzo
16:5); mwenye jeuri na asiye na subira juu ya changamoto zinazojitokeza juu yake (Mwanzo
21:8-10). Mara nyingi imezoeleka kuwa, mwanamke hufanya maamuzi ya ghafla na
kutokuwa na subira juu ya changamoto fulani. Jambo hilo si jema kwa Mkristo, hekima na
subira hutakiwa ili kufanya maamuzi sahihi kwa wakati sahihi ili kutoleta madhara yenye
athari kubwa hapo baadaye katika ustawi wa ndoa. Kuwa na subira na kutoa maamuzi sahihi
bila harara haimuhusu mwanamke pekee, bali hata mwanamume pia katika ndoa yampasa
kuzingatia hilo.
3. Mara zote, Mungu hamuachi mtu anayeonewa pasipo kutendewa haki (Mwanzo
16:6-15). Mungu hakumuacha Hajiri pekee katika majonzi na utungu baada ya kukimbia
mateso ya Sara. Kilio cha cha Hajiri kilisikika kwa Mungu na Mungu akamtuma malaika
kumpa habari njema Hajiri. Yatupasa kujua kuwa, Mungu ni mwaminifu na hakawii
kututimizia hitaji na haja zetu wakati tunapomuhitaji au kuwa katika changamoto (Mwanzo
21:15-20). Sara aliamini kuwa anamkomesha Hajiri, kumbe anamtengenezea mazingira ya
kubarikiwa uzao wa tumbo lake. Hivyo, mwanandoa usilipe baya kwa adui yako bali lipa
jema na Mungu atakuwa nawe.
4. Mungu ndiye mwenye uweza wa kuwapa watoto hata walio vikongwe endapo
tumaini la mtu lipo juu ya Mungu (Mwanzo 17:15-17). Fikara za mwanadamu hukoma, lakini
Mungu Yeye ni muweza wa yote. Mungu hutupatia hitaji zetu pale tunapokuwa tumeshindwa
katika kutumia maarifa, nguvu na uweza wetu binafsi ili tu utukufu tumulejeshee Yeye.
Mtoaji wa watoto kwa wanandoa ni Mungu na si vinginevyo. Pale wanandoa wanapokosa
mbaraka wa watoto, wavumilie na wadumu katika kumuomba Mungu. Wasitumie njia
mbadala kama kwenda kwa mganga wa kienyeji, kuzaa nje ya ndoa, kuoa mke mwingine au
wanandoa kutalakiana.
5. Japo ni mara moja Ibrahimu alifuata matakwa ya mkewe na kuacha kumtii Mungu
katika kumjua Hajiri. Haidhuru, Ibrahimu bado ni kielelezo cha baba wa familia anayefuata
maelekezo ya Mungu nje ya utashi wake binafsi (Mwanzo 21:10-12). Mungu ni wa kwanza
katika kumtii kisha wanadamu na utashi wetu hufuatia. Wakati wote yatupasa kumtii Mungu
kwanza hata kama tupo katika mazingira magumu na nyakati hatarishi. Haikuwa rahisi
Ibrahimu kumfukuza Hajiri na mwanae Ishimaeli kwa sababu ya msukumo wa Sara mkewe,
bali aliitii sauti ya Mungu bila kujali maumivu na uchungu wa moyo kwa mtoto wake
anayepaswa kutengana naye.
6. Heshima ya mama wa familia hushuka pale jukumu lake kwa mumewe
linapochukuliwa na mfanyakazi au kijakazi (Mwanzo 16:4). Kwa taswira ya sasa,
mfanyakazi wa ndani anapokabidhiwa majukumu hata yale yanayomhusu kuyatenda mama
wa familia, kutegemewe kupotea kwa heshima ya mama wa familia. Itegemewe kuwa,
ahsante zote za baba wa familia juu ya chakula, maji ya kuoga, kunyoshewa nguo,
kupokelewa mzigo, kufuliwa nguo, usafi wa nyumba na uangalizi wa watoto zitamwendea
mfanyakazi wa ndani ambapo ni halali ya mama wa familia kutoka kwa mumewe.
Udhaifu wa wazi wa mama wa familia katika kutotimiza majukumu yake kwa
mumewe au familia yake yanapotambuliwa na dada wa kazi, moja kwa moja dada wa kazi
hatakuwa na heshima au utii kwa mama wa familia; maana majukumu mazima ya familia
yapo katika uangalizi wake na ndiye msimamizi mkuu.
7. Uadui wa wazazi huhamia kwa watoto pia kwani chuki hupandikizwa juu yao
watoto (Mwanzo 21:9). Ni vibaya sana kuwashirikisha watoto uadui au chuki juu ya watu
wengine. Mazungumzo na masengenyo yo yote yasiwahusishe watoto, maana nao wanaweza
kutengeneza chuki ya moja kwa moja juu ya watu wanaosadikika kuwa ni maadui wa wazazi
wao. Ni vyema wtoto wakaambiwa kupisha pale panapooneka kuwepo kwa mazungumzo
yasiyofaa kwa watoto. Dhihaka ya Hajiri juu ya Sara ilionekana kwa Ishimaeli juu Isaka siku
ya karamu ya kuachishwa kunyonya kwa Isaka (Mwanzo 21:9). Dhambi ya chuki
iliyopandikizwa kwa watoto kutoka kwa wazazi huleta matokeo yenye madhara makubwa
miongoni mwa familia na jamii.
8. Mama (mzazi) mwenye upendo hawezi kuvumilia kumuona mtoto wake akifa huku
akiona kwa macho yake (Mwanzo 21:15-16). Ilikuwa ni vigumu kwa Hajiri kudumu
kumuona mbashara mwanae anavyopoteza uhai kwa kukosa maji ya kunywa alipokuwa
jangwani. Ndivyo ilivyo kwa mzazi ye yote mwenye mapenzi mema kwa mtoto wake
aliyemzaa; hawezi akawatelekeza au kutowapatia mahitaji ya msingi yaliyo chini ya uwezo
wake. Ndivyo pia Mungu anavyotupenda na hakutaka tuangamie dhambini, hivyo,
alitukomboa kwa damu ya thamani. Ifahamike kuwa: jambo la upendo na malezi ya watoto
linamahusiano makubwa sana na mambo ya kiroho juu ya mwanadamu na Mungu.
9. Si mpango wala maelekezo ya Mungu kwa mwanadamu kuwa na ndoa za mitala
(mke zaidi ya mmoja); bali ni maamuzi au utashi na tamaa za wananadamu. “Sarai
akamwambia Abramu, Basi BWANA amenifunga tumbo nisizae, umwingilie mjakazi wangu,
labda nitapata uzao kwa yeye. Abramu akaisikiliza sauti ya Sarai” (Mwanzo16:2). Watoto
wanaozaliwa katika ndoa za mitala huwa hawaelewani kama ilivyo kwa wake wenza. Hivyo,
ni vigumu kujenga ndoa na familia yenye furaha na amani katika ndoa za mitala.
Hata hivyo, ili kupata maelezo ya kiteolojia zaidi juu ya familia ya Ibrahimu, waweza
soma Wagalatia 4:21-31, ukioanisha na Wagalatia sura ya tatu na sura ya nne yote.
= SURA YA 07 =
“Kinywa chake kimejaa maneno matamu, Ndiye mzuri sana pia pia. Ni
huyu mpendwa, ni huyu rafiki yangu…..”
Mume mwema humheshimu mke wake: Mume ya mpasa kumheshimu mke wake.
Katika mambo mazuri, au mabaya mume lazima atumie lugha sahihi na iliyo ya staha katika
kufikisha ujumbe kwa mke wake wakati awapo peke yake au awapo mbele za watu.
Mume mwema ni mwaminifu kwa mke wake katika kila kitu: Hasa katika mambo ya
ndoa na mambo ya fedha au mali. Mwanamume yampasa kuwa wazi bila kificho wala
kudanganya juu ya matumizi na kile anachomiliki kwa mke wake wa ndoa.
Mume mwema huvaa vyema na nadhifu: Mwanamume aliye katika ndoa ni vyema
akawa safi na nadhifu katika kuvaa awapo mbele za Mungu, familia (watoto) na katika
shughuli zake za kazi au ofisini kama siyo ya kuchakalika.
Mume mwema ni yule anayeheshimu ndugu na wazazi wa mke wake na
kuwahudumia bila kuwabagua: Mwanamume aliyemume mwema asiwaongee vibaya,
kuwachukia au kuwabagua ndugu wa mke wake wa ndoa.
Mume mwema huhudumia na kutoa mahitaji yote kwa familia yake: Mume mwema
yampasa kuhudumia familia ipasavyo mfano tiba, chakula, malazi, elimu, na mengine
yaliyochini ya uwezo wake na yanayotekelezeka kulingana na uwezo wake wa kiuchumi.
Mume mwema ni yule ambaye hutenga muda wa kuwa na familiya yake:
Mwanamume katika ndoa lazima atenge muda wa kutosha wa kuwa na mkewe pamoja na
watoto ili ashiriki furaha, maumivu, majonzi, mafanikio, kushindwa, mipango na mawazo juu
ya ndoa na familia yake.
Mume mwema ni yule aliyempokea Yesu kama Bwana na Mwokozi wake: Sio wote
wanaosali wapo karibu na Mungu. mume mwema lazima amuishi Yesu na kutembea katika
njia zake. Ajue kuwa popote alipo, aendapo, atendacho Mungu anamwona maana kwake
hapana kificho.
Namna ya Kuwa Mke Mwema Katika Ndoa
Biblia inasema kuwa mke mwema hutoka kwa Bwana; ili mwanandoa awe mke
mwema yampasa kuwa mwenye sifa na tabia zifuatazo katika ndoa:
Mke mwema awe mnyenyekevu daima kwa mume wake: Awe mwenye hekima na
mwenye kumjibu vizuri kwa adiri mumewe. Kulingana na hurka ya wanaume si salama
mwanamke akampandishia sauti mmumewe, maana tabia hiyo huwa haitatui chochote au
kumjenga mwanamume (Mithali 15:1).
Mke mwenye hekima hatoi siri za ndani za udhaifu wa mumewe kwa watu
wengine: Mwanamke kutoa siri za ndani zenye kuhusu udhaifu wa mume wake haimuaibishi
mume pekee bali hata yeye mwanamke anayetoa hizo siri. Kutoa siri za ndani ya ndoa
huondoa maana kamili ya kuwa, wanandoa ni mwili mmoja katika kubebeana madhaifu
(Waefeso5:12).
Mke mwema hamfananishi mume wake na wanaume wengine: Kufanya hivyo ni
kumpunguzia nafasi yake ya upekee kwako maana wanadamu wote hawafanani hivyo ni
ishara ya kutompenda au kutobebeana naye mapungufu yake, ispokuwa ni salama sana
kumwelekeza kwa upendo pale jambo au suala fulani halipendezi huku ukizidi kumuombea
ili abadirike kwa uwezo wa Mungu anayemjua zaidi.
Mke mwema huwapenda marafiki na ndugu za mume wake: Mke mwema haimpasi
kugombana au kugombezana na watu hususani ndugu na marafiki wa mume wake; ni vyema
na kupendeza mke akawaacha waamue mambo na mume wake ili asionekane kutenda vibaya
Mke mwema ni mbunifu kwa mume wake: Mwanamke yampasa kuwa mbunifu
kulingana na mazingira na wakati. Mfano vile vitu anavyovipenda mumewe yampasa
avifanye kwa ubunifu mkubwa na avikuze siku kwa siku na asivyovipenda mumewe aviache
mara moja ili kutomkwaza. Ubunifu waweza kuwa katika upambaji wa ndani ya nyumba,
biashara, mitindo ya mavazi ya heshima yenye kuvutia n.k. ili kuleta ustawi, mvuto na
maendeleo yenye tija katika familia.
Mke mwema aepuke tamaa ya vitu vya gharama vilivyo nje ya uwezo wa kipato:
Tamaa ya vitu vya gharama vilivyo juu ya uwezo wa kipato cha wanandoa, mwanamke
mwema huviepuka kwani anajua mazingira na hali ya kipato cha ndoa yao, na haombi vitu
vya gharama kuzidi uwezo wa kipato alicho nacho mumewe.
Mke mwema hana marafiki wasio wema: Mwanamke anayejitambua hana makundi
au marafiki wasio wema katika tabia na matendo, hivyo, huwaepuka marafiki wote wenye
mawazo hasi na mitazamo na tabia mbaya zisizofaa katika kuigwa. Upendo na ukarimu wake
uwe kwa watu wote lakini si kwa kushikamana na kufanya urafiki nao wale wote wenye
mienendo na tabia mbaya zisiyofaa katika maisha ya Mkristo.
Awapende na kuwalea vyema watoto wake: Mwanamke aliye mke mwema
huwapenda na kuwalea watoto wake katika matendo mema ili wasipotee maana uzao wa
tumbo lake ni baraka kutoka kwa Mungu, hivyo hata watakapo kuwa wazee hawataicha njia
ya kweli (Mithali 22:5).
= SURA YA 08 =
Mithali 12:4
mzigo kwa mumewe, anakwamisha maendeleo ya familia na hafai kuwa mama wa kuigwa
isipokuwa kwa kukatazwa na mumewe tu.
Mwanamke katika ndoa yake daima atende mema kwa mume wake pasipo
kikomo. Mithali 31:12 inasema: “Humtendea mema wala si mabaya, Siku zote za maisha
yake”. Mwanamke mwenye hekima anayemtumainia Mungu, hapaswi kumtendea mabaya
mumewe siku zote za maisha ya ndoa. Si vyema mwanamke kumsema vibaya mume wake,
kutoa siri, mapungufu na udhaifu wa mme wake kwa watu wengine. Sio sawa kumuwazia
mabaya mume wake, wala kutomthamini wala kutomjali, au kumdharau, kumsaliti na
kumjibu kwa jeuli mume wake. Mke amtendee mema na mazuri mume wake. Pale mwana
mume anapokosea mwanamke anene naye kwa adabu na hekima.
Nashauri kwamba: Ikitokea mume wako amekukosea, jitahidi kumsamehe na
umuombee badala ya kumjengea chuki au kumuwekea kisilani na kumnunia. Epuka kuwa na
hasira juu ya mume wako. Daima tambua kuwa, wewe na mume wako ni mwili mmoja, hivyo
mnene na mnuie mamoja ili kustawisha familia yenu. Na kamwe upendo wako usipungue juu
ya mumeo. Upendo wako udumu bila kujali muda, wakati, mazingira, sehemu na hali ya
kimaisha; upendo wako juu yake utamalaki daima.
Mwanamke katika ndoa yampasa afanye kazi zake kwa moyo na bidii. Mithali
31:13 inasema: “Hutafuta sufu na kitani; Hufanya kazi yake ya mikono kwa moyo”.
Mwanamke mwenye kumtumainia BWANA, ni mwenye bidii katika kufanya kazi na
kutafuta. Hufanya kazi za nyumbani na za kiuchumi kwa moyo wa bidii, na hakomi kuonesha
bidii katika kutafuta, ilimradi yote hayo anatenda kwa sababu ya ustawi wa familia yake.
Wakati mwingine, haina haja ya mfanyakazi wa ndani endapo sehemu ya majukumu
yanayomhusu mwanamke atamtendea mume wake na familia kwa ujumla. Mwanamke
atawaliwapo na moyo wa upendo wa kimbingu, hana sababu ya kujivuna, kujiona na
kujikweza katika suala zima la majukumu ya kifamilia, na yale yote yanayohusu ustawi na
afya ya familia yake.
baa la njaa maana zilifanikiwa kuwa na chakula cha kutosha, hivyo, zilisonga mbele
kimaisha.
Mwanamke aweke akiba ya mapato yake ili asipungukiwe katika familia yake.
Mithali 31:18 inasema “Huona kama bidhaa yake ina faida; Taa yake haizimiki usiku”.
Mwanamke laziwa awe mwanauchumi; ajitahidi kuhifadhi faida iliyotokana na nguvu kazi
yake. Lakini pia, yampasa afanye mahesabu mazuri kwa kile anachotaka kuwekeza (katika
mali au bidhaa) na kufanya, na awe na uhakika ya kuwa kitamletea faida hapo badae na sio
hasara. Taa (mtaji) yake idumu kuwaka ikiwa na mafuta tele. Yaani mtaji wake uzidi
kuongezeka kila siku bila kukata. Hivyo basi, mwanamke mwenye fikra pevu, huwekeza
kwenye mambo yaletayo faida na sio yatoayo au kuleta hasara.
Mwanamke katika ndoa, mikono yake iwe shupavu katika kutenda na kufanya
kazi. Mithali 31:19 inasema kuwa: “Hutia mikono yake katika kusokota; na mikono yake
huishika pia”. Hakuna kitu kizuri kama kuona manufaa na mafanikio yatokanayo na kazi ya
miko yako. Vivyohivyo kwamwanamke kutia mkono katika kujenga maendeleo ya famila
yake huleta furaha isiyo na kifani.
Mwanamke atakuwa na amani ya umiliki na amri juu ya mali au mapato ya familia
yake maana akili na mkono wake utakuwa umechangia kuyatafuta. Mwanamke aliye katika
ndoa apende kujishughulisha kwa kutumia uwezo wa akili na mikono yake ili kufanikisha
ustawi na ukuaji wa maendeleo ya familia yake. Si vyema mke akamuachia mume wake
jukumu lote la ufanikishaji mzima wa maendeleo ya familia.
mfuatiliaji wa mambo mengi ya kifamilia kuliko baba wa familia. Hivyo basi, uhai na
usalama wa kiafya upo kwa mama wa familia hata kama kuna kunamfanyakazi wa ndani.
Mwanamke katika ndoa yake awe hodari katika ubunifu na unadhifu katika
mavazi yake. Mithali 31:22 inaelezea kuwa: “Hujifanyia mazulia ya urembo; Mavazi yake
ni kitani safi na urujuani”. Mambo ya upambaji, usafi wa nyumba na vyombo, mpangilio wa
vitu ndani, na utunzaji wa mali za ndani; ni sehemu ya jukumu la mama wa familia. Ubunifu
wa mapambo ya ndani, mfano kusuka na kufuma vitambaa, kudalizi mashuka n.k. ni jukumu
linalosimamiwa na mama wa nyumba pia.
Mama wa familia lazima ajijali katika usafi wa mwili na mavazi pia. Avae mavazi
nadhifu yenye kuvutia hata kama sio ya bei kubwa, bali mpangilio na usafi pekee ndio
kinachotakiwa. Kuolewa kwa mwanamke sio kuwa ndiyo kikomo cha kujiweka safi katika
hali ya unadhifu. Haipendezi kwa mwanamke kuvaa nguo zinazoshusha heshima, bali
yampasa avae nguo zinazostili mwili vyema. Kuvaa nguo zisizo za heshima na za kuaibisha,
ni kujiaibisha au kujidhalilisha, kujipunguzia heshima na kumdhalilisha mume na watoto pia.
Mwanamke mwenye hadhi na atendae kazi kwa nguvu, asiwaze juu ya jinsi gani
aishi kesho, bali huufurahia wakati ujao maana anajiamini katika kutafuta. Mithali
31:25 inasema: “Nguvu na hadhi, ndiyo ndiyo mavazi yake; Anaucheka wakati ujao”.
Mwanamke mchapa kazi ana amani na matumaini juu ya kesho yake na familia yake.
Kutokana na uchapa kazi, hana wasiwasi na maisha maana ana moyo wa bidii ambapo ana
amini haishi kwa kubahatisha wala hawezi kumtegemea mume wake na kukaa akiwaza juu
ya kukosa na kufanikiwa kwa mmewe. Mwanamke anayetegemea mafanikio ya mume wake,
hana matumaini kwa sababu uhakika wa kupata ama kukosa mkate wa familia upo juu ya
kupata au kukosa kwa mumewe.
amchae Mungu na mwenye hekima, hutumia upendo kama siraha ya kurejesha amani, umoja
na mshikamano katika familia yake.
Mwanamke katika ndoa awe mfano wa kuigwa kutokana na mazuri yake. Mithali
31:29 [Mume humsifu na kusema] “Binti za watu wengi wamefanya mema, Lakini wewe
umewapita wote”. Mwanamke mwenye kujua majukumu na kuisimamia familia yake, jina
lake kutajwa na kutamkwa kwa mema na mazuri, kuanzia ngazi ya familiya hadi jamii
inayomzunguka. Kwa mazuri yake, jamii imzungukayo imtolee mfano wa kuigwa; hivyo
atakuwa barua njema kwa wengine.
Mwanamke mwenye kutenda mema na mengi yaliyo mazuri, mume wake hujivunia na
hana budi kumsifia maana jina lake jema linasomeka vyema kwa familia na jamii yote
inayomzunguka. Kama mama wa familia hasomeki vizuri katika mienendo na tabia yake,
hawezi akarithisha mambo mazuri kwa watoto (binti zake), hivyo, binti zake waweza kukaa
bila kuchumbiwa au kuolewa maana tabia ya mama yao sio nzuri.
Mwanamke katika ndoa; wanafamilia na jamii imsifie kwa ucha Mungu na sio
uzuri wake. Mithali 31:30 inasema: “Upendeleo hudanganya, na uzuri ni ubatili; Bali
mwanamke amchae BWANA, ndiye atakayesifiwa”. Baadhi ya wanawake walio katika ndoa
huwa na mikogo, ujivuni au kujisikia na kujiona ya kwa kuwa ni wazuri wa sura na umbo,
hivyo, hawawezi kuheshimu, kunyenyekea kwa waume zao. Mara zote uzuri wa sura
hudanganya, hivyo huharibu tabia na matendo ya mtu. Mwanamke amtumainie na kumcha
Bwana, ndiye apatae sifa maana upendo na uzuri wa moyo watoka kwa Mungu.
Mara nyingi wanawake walio wazuri wa sura ndiyo wanaoongoza kwa roho mbaya na
matendo mabaya pia na ndiyo wanaoongoza kuleta migogoro na kuvunja ndoa, maana
anaamini kwa uzuri wake atapata mwingine. Mama mwanandoa si vyema akatumia uzuri
wake kama fimbo ya kumnyanyasa mume wake. Heri uzuri wa moyo wenye kujenga, kuliko
uzuri wa sura udanganyao na wenye kubomoa.
= SURA YA 09 =
Mithali 1:5
Waebrania 13:4 inaelezea kuwa ndoa na iheshimiwe na watu wote; hivyo ndoa ni
takatifu lazima iheshimiwe na watu wote. Kuchezea chezea ndoa nikosa na nikumkosea
Mungu aliyemwasisi wa taasisi hiyo. Ni jambo nyeti na la msingi pia kufahamu juu
mahusiano na maarifa katika ndoa.
Maarifa na ufahamu katika ndoa yapo kwenye uwepo wa Mungu katika ndoa. Maarifa
na ufahamu huo ni juu ya magomvi katika ndoa, pesa na mali katika ndoa, kusaidia ndugu
katika ndoa, afya katika ndoa, elimu katika ndoa, kanuni kuu ya maisha katika ndoa na kazi
katika ndoa.
Uwepo wa Mungu Katika Ndoa
Ndoa iliyofuata hatua zote na ikafungwa katika taratibu za Kikristo ni ndoa iliyohalali
na imekubarika mbele za Mungu kwa kuwa ndoa ni muunganiko wa mke, mume na Mungu
(Mithali 4:12). Yafuatayo ni mambo matano ya kufanya kwa wanandoa ili Mungu awepo
katika ndoa na familia yao:
Kuthamini mambo ya ibada
Wanandoa wathamini na kufanya ibada za kicho katika familia yao pamoja na
kuhudhuria na kushiriki ibada za maombi kanisani ili Mungu azidi kutamalaki na kuwepo
katika ndoa na familia yao (Waebrania 10:25).
Watoto
Jambo la kuzaa watoto linahitaji maombi ya kina juu ya mtoto anayezaliwa awe ni
mpango wa Mungu ili Mungu aanze kumwandaa toka kutungwa kwa mimba na kukua kwake
tumboni (Yeremia 1:5). Maisha ya ndoa huanza yakiwa na watu wawili pasi na watoto;
watoto huja badae katika maisha ya ndoa ukiwa kama mbaraka kutoka kwa Mungu maana sio
kwa uwezo wao wanandoa kuwapata watoto, hivyo, yaweza kuchukua muda kwa wanandoa
kupata watoto au kuwahi. Maamuzi ya kuzaa watoto wangapi na kwa kipindi gani huwa ni
makubaliano ya wanandoa wao wenyewe na si jambo la mmoja miongoni mwa wanandoa.
Wanapopatikana watoto au wanandoa wanapowazaa watoto wao yawapasa
kuwahudumia kwa pamoja bila kuwabagua, hata katika kuwapatia elimu ili kujenga
ushirikiano na umoja katika familia na miongoni mwa watoto.
Kusaidia Ndugu
Kusaidia wengine ni moja ya jambo la kiroho kwa ye yote aliye Mkristo na mcha
Mungu, maana hufungua mibaraka. Kusaidia ndugu katika familia ya wanandoa kusiwe kwa
kupendelea upande mmoja wa ndugu miongoni mwa wanandoa. Wanandoa wawasaidie
walio na uhitaji ili nao waweze kujikwamua kimaisha. Wawatendee mema wale walio ndani
ya uwezo wao, ikiwezekana wawape mtaji au kianzio (ndoano) ili nao waweze kujitafutia
riziki (samaki) zao wenyewe na sio kuwazoeza kuwapa samaki kisha wakimaliza waombe
samaki tena.
Afya Katika Ndoa
Katika kitabu cha 3Yohana 1:2, Yohana anazungumzia juu ya kufanikiwa katika afya
na roho. Afya ni jambo la msingi kwa wanandoa, hivyo, walizingatie na kulitilia mkazo hata
kwa watoto wao. Ndani ya familia, wanandoa wahakikishe kufuata kanuni zote za afya
hususani kwa kuzingatia ulaji wa vyakula vya asili vyenye ubora na vitamini na siyo vyakula
vya kutoka viwandani. Ikiwezekana, wanando wasikoboe nafaka zinazopaswa kuliwa bila
kukobolewa.
Wanandoa wazingatie mazoezi na ulaji wa mpango kwa kuwa na kiasi ili kuepuka
unene na uzito kupita kiasi; pawepo na uwiano wa urefu wa mwili na uzito wa mwili pia.
Hivyo, wanandoa wazingatie kanuni kumi na mbili za afya (yaani CELEBRATIONS;
ikimanisha SHEREHE) ambapo hapo awali zilikuwa kanuni nane za afya (yaani
NEWSTART; ikimanisha MWANZO MPYA):
1. N = Nutrition (Lishe)
2. E = Exercise (Mazoezi)
3. W = Water (Maji)
4. S = Sleep (Kulala)
5. T = Trust in God (Kumwamini Mungu)
6. A = Air (Hewa Safi)
7. R = Rest (Kupumzika)
8. T = Temperance (Kuwa na kiasi)
SHEREHE (CELEBRATIONS):
tuupate wokovu na uzima wa milele; tuonapo hali hiyo basi tuzidi kujikabidhi na
kujinyenyekeza kwake aliyetukomboa ili tusipotee milele.
Kufanya kazi kwa wanandoa kunafaida zifuatazo: huleta heshima katika jamii
inayowazunguka, ni kumbukumbu ya sabato, kuepuka kutenda dhambi ya wizi na kutamani
vitu na mali za wengine, huleta furaha maishani daima, hujenga afya maana ni sehemu ya
mazoezi, hujenga ushupavu na uwezo wa akili katika kufanya maamuzi na kufikiria mambo,
kazi inaongeza urefu wa maisha kwani hupunguza mawazo yasiyokuwa na tija na kazi yo
yote ile inafaida (Mithali 14:23 na Mithali 31:10).
Kutofanya kazi kunaleta umasikini katika familia; Mambo yanayoleta umasikin
katika familia au ndoa ni: kutomrudishia BWANA kile alichowapatia wanandoa katika
mapato yao (Mithali 10:7), uvivu uliopitiliza (Mithal 10:4), usingizi uliopitiliza (Mithali
20:13), anasa kama ulevi na urafi (Mithali 21:17, Mithali 23:20-21), kufuata mambo yo yote
ya upuuzi na yasiyofaa (Mithali 28:19), kuzurura au kutumia muda mwingi kusafiri
kutembelea ndugu bila kufanya kazi (Mithali 25:17).
= SURA YA 10 =
Mithali 15:16-17
Familia ya Kiroho
Familia ya kiroho ni familia ambayo inaishi na kutembea katika heshima na utukufu
wa Mungu chini ya mwanaye mpendwa Yesu Kristo na imejawa na Roho Mtakatifu. Ili
kutengeneza au kuunda familia ya kiroho, wanandoa wafanye mambo yafuatayo:
Kristo (Wakolosai 2:6); kwa kusoma Biblia na uthubutu wa kulitafakari neno lake (Zaburi
119:1, Wakolosai 3:16, Matendo 17:11, 1Petro 2:2).
Wanafamilia Wapate Muda wa Kutosha Katika Kuomba: Familia ya kiroho hutenga
muda wa kutosha kwa ajili ya maombi; familia ya kiroho haifanyi maombi ya yasiyokuwa na
kicho au ya harakahara. Kila mwanafamilia katika familia yampasa kupata nafasi binafsi ya
kufanya maombi (Luka 18:1, Wafilipi 4:6, 1Wathesalonike 55:17, Waefeso 6:18).
Washiriki Imani Yao na Watu Wengine: Familia ya kiroho hushiriki imani yao na
watu wengine. Wanafamilia wanaposhuhudia watu wengine imani yao juu ya Yesu kwa dhati
huwa na nguvu nyingi za kiroho, hivyo, kiwango cha kiroho hupanda kila mara wanapo
zididi kutenda hivyo (Matendo 2:42).
Wanafamilia Washiriki Shughuli na Huduma Mbalimbali za Kanisa: Familia
inayohitaji kukua kiroho, haikwepi wala haiachi kushiriki huduma na shughuli za kanisa.
Shughuli na huduma za kanisa kama vile: huduma za jamii, ushuhudiaji, kujiunga na kwaya,
kuchangia pesa katika huduma za kueneza injili pamoja na kufanya kazi za mikono
zinazohusu kanisa huvutia uwepo wa Roho Mtakatifu miongoni mwa wanafamilia kwa
sababu ya kuwa mawakili waaminifu kwa Mungu.
Wanafamilia Waepuke Dhambi: Familia inayotaka kuwa familia ya kiroho ni lazima
iepuke kutenda au kushiriki dhambi ili waishi katika kweli yote na imani ya Yesu kristo
(Warumi 22:21, Wafilipi 1:270).
Wanafamilia Huliheshimu na Kulisoma Neno la Mungu: Familia inayotaka kuwa
familia ya kiroho ni lazima ilisome na kuliheshimu Neno la Mungu pamoja na kulifanyia kazi
na kuliishi. Familia ya kiroho itafundishana, kusoma kwa sauti na kulijadili neno la Mungu
(Kumbukumbu la Torati 6:7)
Jinsi Familia ya Kiroho Ilivyo kwa Muktadha wa Waefeso 5:21 Hadi 6:9:
Wanafamilia wote ni Wakristo katika imani moja.
Familia imeundwa na baba, mama, watoto, wazazi wa wanandoa, na wafanya kazi
(extended family).
Familia ina utii na upendo kwa kila mmoja. Mwanamke anamtii mumewe na mume
anampenda mkewe.
Watoto wanawaheshimu wazazi maana wanawalea katika nidhamu na utii kwa Mungu.
Wafanyakazi wanawahudumia mabwana zao bila jicho la uangalizi; mabwana nao
wanawaonesha wafanyakazi usawa kama alivyo Bwana Yesu kwa wote.
Familia hii inamwabudu Yesu maana yeye ni kichwa cha familia na wanafamilia wote.
Kushirikishana na uaminifu
Wanafamilia wawe wawazi kila mmoja na kushirikishana kila jambo ili kuwepo
kuombeana. Kuwepo na kushirikishana katika mikakati ya maisha na maendeleo ya familia
juu ya elimu, mahali pa kujenga na vitu vya kununua, hivyo basi kushirikisha kwa
wanafamilia kutawajengea uaminifu wao kwa wao. Pia siyo salama amana ya familia
ikauzwa bila kuwasiliana au kuzungumza miongoni mwa wanafamilia (Mithali 23:20-21).
wa wao kwa wao maana hawawekeani chuki za kudumu juu yao bali huyatatua matatizo yao
kwa upole na kwa hekima ya kimbingu (Luka 11:4; Mithali 15:1).
= SURA YA 11=
Mithali 22:6
Biblia iwe mwongozo wao: Wazazi waikubali Biblia kama ndiyo njia pekee inayo
waongoza katika kutoa maelekezo ya malezi mema kwa watoto wao walio wazaa na mengine
yaliyo nje ya biblia yatumike kutokana na hekima za kimbingu baada ya kupimwa kuwa
yanafaa.
Wanandoa wapendane: Wanandoa wapendane kwanza wao kwa wao ili watoto
wajue kuwa wazazi wao wanapendana. Upendo wa wazazi utaleta picha nzuri kwa watoto ili
wayarithi na kuyaishi yale yote wanayowafundisha na kuwaonesha kwa vitendo. Wanandoa
wasineneane mabaya bali waungane katika kuleta nidhamu na maadili yaliyo mema ya
watoto kwa pamoja.
Wazazi wawapende watoto: Wazazi wawapende watoto wao kwelikweli ili waweze
kuwaonya katika adiri na wasipotee katika ukengeufu kwa kuielekea dunia.
Wazazi wawe na muda na watoto wao: Wazazi watenge muda wa kutosha wa kuwa
karibu na watoto wao ili waweze kuwalea kwa ukaribu huku wakionesha hali ya kuwajali na
kushirikiana kwa kila namna iliyo nzuri kadri iwezekanavyo.
Wazazi wa warudi watoto wao katika upendo: Wazazi wawaongoze watoto katika
njia ya kurejesha nidhamu yao kwa kutumia upendo kadri iwezekanavyo na siyo nguvu kwa
sehemu kubwa bali mara chache wawarudi kwa mapigo ili kutojenga usugu na chuki ndani
yao.
Wawatie moyo watoto: Wazazi wawasifie (commend) na kuwatia moyo (motivate
and reinforce) watoto wao pale wanapotenda mazuri na si kuwakatisha tamaa ili kuwajengea
moyo wa ubunifu na kujituma katika kutenda kwa hiari yale yote yaliyo mema na mazuri.
Wazazi wawe mfano mwema: Wazazi wajitahidi kuwa mfano mwema (role model)
kwa watoto wao ili watoto nao waishi kwa kuyaiga mambo na tabia njema za wazazi wao
badala ya kutafuta mifano toka nje ya familia ambapo yaweza kuwa siyo myema.
Wazazi wawalee watoto kulingana na falsafa ya kanisa: Watoto walelewe kulingana
na mafundisho na misingi ya kanisa ili wasipotoshwe na mafundisho yasiyofaa ya kidunia
huku wakiwaongoza kumkubali na kumpokea Yesu katika hatua za awali na hatua za makuzi
yao yote.
Wazazi wawe wanawaombea watoto wao: Maombi ya faragha yafanywe na wazazi ili
kuwaombea watoto wao kama alivyo fanya Ayubu (Ayubu 1:5) kwani huenda wakawa
wametenda dhambi pasipo wazazi kujua.
Wawafundishe nidhamu iliyobora: Watoto wafundishwe tabia ya kuwaheshimu watu
wote, kutii na kufuata mapenzi ya Mungu, kuheshimu Ibada pamoja na vitu vingine vilivyo
vitakatifu.
Baada ya kuona kanuni ambazo wazazi yawapasa kuzitumia ili kuleta malezi bora na
yenye tija kwa watoto wao, yapo pia mambo machache yanayowapasa wazazi kuyazingatia
katika kuwalea watoto wao ipasavyo:
Kazi isiwafanye wazazi kukosa muda wa kuwa na watoto wao kwa kumwamini
mfanya kazi wa ndani katika kuwalelea watoto wao.
Wazazi wajue kuwa, watoto ni mali ya Mungu siyo mali yao, hivyo, wakipotea
watadaiwa maana watoto ni kondoo wa kwanza wanaotakiwa kuokolewa kisha wengine
walio nje ya familia (zizi).
Wazazi wajue ya kwamba nidhamu mbovu ya watoto huanzia nyumbani huko nje
huwa ni nyongeza, hivyo, ni vyema matatizo ya watoto yakatatuliwa nyumbani na siyo
wayatatue watu wengine walio nje ya familia.
Wazazi watambue ya kwamba malezi ya watoto ni wajibu wake na siyo jukumu la
serikali, kanisa, ndugu au jamii maana ndiye aliyewazaa.
Wazazi wajue ya kuwa watoto anaowazaa siyo kizazi alichozaliwa yeye, hivyo,
changamoto kwa watoto zinaongezeka.
Wazazi wajuwe kuwa anazaa watoto wasiofanana katika mazuri yao na mabaya yao
hivyo wajitahidi kupalilia mazuri ya kila mtoto. Mahitaji na malezi ya watoto hutofautiana
kulingana na jinsia, vipaji, vipawa na kalama hivyo tabia zile mbaya ziondolewe na nzuri
zipaliliwe.
Wazazi wafahamu ya kuwa wasipowafundisha watoto yawapasayo, ulimwengu
utamfundisha yale yawapasayo kiulimwengu na wazazi wasiwalaumu watoto bali awarejeshe
kwa upendo.
Wazazi watambue ya kuwa uwezo wa watoto kiakili haulingani kwa kila mtoto,
hivyo, si vyema kumfananinisha au kumlinganisha mtoto wako kwa mtoto wa mwingine bali
fanya sehemu yako kupalilia na kuamusha uwezo wa mtoto wa kiaklili.
Mzazi atambue kuwa ni kawaida watoto kuomba kitu mpaka cha ziada, hivyo, kama
unajadiliana naye (mtoto) kuwa ukipata utampatia. Mtoto asipokuwa huru kwa wazazi wake
hususani katika kuwaomba mahitaji yake anaweza akajenga tabia ya udokozi au wizi.
o Mtoto hawezi kujenga kiwango cha kurizika kama hakosi wala kupungukiwa na
cho chote.
o Mtoto hawezi kujua kuwa hawezi endapo kama wote waliomzunguka ni
wakamilifu, hivyo, mtoto aachwe acheze na watoto wenzie ili kujua wapi hawezi
ili kujifunza.
o Mtoto hawezi kujifunza ubunifu kama kila kitu anakatazwa kufanya kisa
atajichafua au kuumia.
o Mtoto hawezi kujifunza ushirikiano kama kilakitu kwake anafanya peke yake bila
kushirikiana na wengine.
o Mtoto hawezi kujifunza ujasiri kama hakutani na mambo yenye kuhitaji ujasiri.
o Mtoto hawezi kujenga uking‟ang‟anizi au ukamiaji wa jambo kama kila kitu
achofanya kwake ni kirahisi tu.
o Mtoto hawezi kujiamini, kujirekebisha, na kuwa mbunifu kama hajui kushindwa.
o Watoto hawawezi kuwa na uwezo wa kujitawala wenyewe kama hawakai
wakakubaliana na wakubwa zao.
Kuwaombea Watoto
Hakuna mwanadamu aliye salama kwa siku bila maombi (Pambano Kuu uk 530).
Kila siku wazazi wanawafanyia watoto wao mambo mengi – ili kuonesha kuwa
wanawapenda na kuwajali, kuwafundisha, kuwaelekeza, kuwasaidia, kuwaongoza,
kuwawezesha, kuwatia moyo kuwalina na mengine mengi. Wazazi hutumia nyakati zao
njema ili kuwezesha maisha ya watoto wao, kuwasaidia kazi za shuleni na kuwaongoza
katika kutenda kazi. Wazazi hutumia pesa nyingi ili kufanikisha michezo ya watoto wao,
kuwapatia elimu bora ili wakue na kuwa jinsi wazazi wapendavyo, huwapatia watoto wao
misaada, fursa ili kuyafikia matamanio yao katika dunia hii.
Lakini katika nyakati za mchakaliko wa kazi nyingi katika maisha ya ulimwengu
huuu huwa tunakumbuka kuwaombea watoto wetu? Sirejerei yale maombi ya haraharaka ya
kwenda kulala au wakati wa kuagana nao asubuhi wakienda shuleni na wazazi wakienda
kazini ambayo yanaumaana kiasi kidogo tu juu yao watoto. Namanisha maombi mahususi ya
kina, yenye nguvu, yakuomba utimizwaji wa ahadi zilizoahidiwa na Mungu, pamoja na
maombi ya uvuvio wa watumaini kwa watoto. Kila mzazi hufurahia tabia njema ya watoto
wake pale wanapozidi kutembea katika kweli ya mungu. “Sina furaha iliyo kuu kuliko hii,
kusikia ya kwamba watoto wangu wanakwenda katika kweli” 3Yohana 1:4.
Hivyo, maombi yetu kwa watoto wetu hayaendi hivihivi wala kuptea bure na kufa,
bali huishi milele katika maisha ya watoto. Uhusiano wao na Yesu ni kitu pekee
kitakachowapeleka Mbinguni, na kwa hili lazima tuwaombee watoto wetu. Waombee tabia
zao, wokovu wao, ulinzi na hatima ya maisha yao ya baadaye. Marazote, mzazi naombeapo
watoto wake lazima azidai ahadi za Mungu kwa niaba yao. Hakuna kitu chenye nguvu kama
maombi ya kimyakimya ya wazazi wanapokuwa wamepiga magoti kwa unyenyekevu na
wakiwawasilisha watoto wao mbele za Mungu. Maombi yananguvu kwa sababu tunaye
Mungu ambeye hutenda hata katika mambo yasiyowezekana wakati tukimuomba (rejea
kujibiwa kwa ombi la Hana katika 1Samweli 1:27).
“Nguvu ya maombi ya mama anayeomba hayawezi kukisiwa. Anapopiga magoti
pembeni ya mtoto wake wa kiume au wa kike tangu utoto hadi ujana, madhara ya maombi
hayo hayawezi bainika mpaka wakati wa hukumu, kuwa maombi hayo yalikuwa na msaada
kwa watoto wake. Kama imani ya mama itaunganishwa na Mwana wa Mungu, maombi yake
mamlaka: 1Petro 2:17; Waefeso 2:10 ); Ujasiri (Kumbukumbu la Torati 31:6); Usafi wa
moyo (Zaburi 51:10); Wema (1Wathesalonike 5:15); Ukarimu (1Timotheo 6:18-19); Amani
(Warumi 14:19; Isaya 26:3); Uvumilivu (Waebrania 12:1; 1Wakorintho 15:58);
Unyenyekevu (Tito 3:2; Mithali 22:4); Huruma (Wakolosai 3:12; Zaburi 145:9); Wajibu
(Wagalatia 6:5; Wakolosai 3:23); Kuridhika (Wafilipi 4:12-13; 1Timotheo 6:6); Imani (Luka
17:5-6; Waebrania 11:1-40); Moyo wa utumishi (Waefeso 6:7; Warumi 12:11); Tumaini
(Warumi 15:13); Hekima (Yakobo 1:5); Shauku juu ya Mungu (Zaburi 63:8; Zaburi 42:1;
Maombolezo 3:25); Wawe waombaji (1Wathesalonike 15:17); Shukrani (Waefeso 5:20;
Wakolosai 2:7; Zaburi 107:8); Utii (Matendo 5:29) na Kuwaombe msamaha au toba kwa
Mungu (Ayubu 1:5).
= SURA YA 12 =
“Moyo wa mtu huifikiria njia yake; Bali BWANA huziongoza hatua zake.
Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu; Lakini mwisho wake ni njia
za mauti”
Mithali 16:9, 25
Wanapenda kujiamini wao pekee yao, hivyo ni watu wenye mashaka na kila mtu au
jambo.
Mitazamo yao siyo chanya mara zote.
Wapo kinadharia na siyo kivitendo zaidi.
Hawana tabia ya kuchangamana na watu, hivyo, si wepesi wa kujenga ursfiki haraka.
Wanamisimamo ya kutokubadirika daima.
Hukera kwa sababu ni wadadisi sana hata vitu ambavyo havina maana.
2. Itawasaidi kutambuwana tabia ili kurekebisha kwa upendo kwakila tabia zisizopendeza
miongoni mwa wachumba au wanandoa.
3. Itawasaidia wanandoa na wachumba kuombeana madhaifu na hulka walizonazo ili
Yesu aziondoe.
4. Itawasaidia kujuana umadhubuti wa kila mmoja hivyo kupanga namna ya kuzitumia ili
kuleta ustawi wa ndoa zao.
5. Itawasaidia wachumba kujiandaa kisaikolojia namna ya kuweza kuendana na mchumba
wake watakapokuwa katika ndoa.
6. Itawasaidia kuyakuza yale yaliyo mazuri kulingana na kundi la mtu miongoni mwa
wachumba au wanandoa ili kuleta ustawi mzu kwa familia au ndoa.
= SURA YA 13 =
“Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia
msaidizi wa kufafana naye”
Mwanzo 2:18
na walimu mashuleni. Sisi sote ni zao la kibaiolojia, utashi wa jamii zetu pamoja na
migawanyo ya majukumu kuendana na jinsi na jinsia zetu. Wanawake wanauwezo mkubwa
wa kuona kwa macho mambo mengi kwa upana. Pia, mwanamke anahisia za ndani za
kuweza kujua hisia za watoto na rafiki zao, matumaini yao, ndoto zao, hofu iliyofichika juu
ya nini wanachofikiria na kuhisi pia.
Kiwango cha kuona baina ya mwanamke na mwanamume kipo tofauti. Wanawake
wanauwezo mkubwa wa kuona pembeni (kulia na kushoto) kuliko mbele na nyuma.
Wanaume wanauwezo wa kuona vyema mbele na nyuma kuliko kiupana (upande wa kulia na
kushoto). Hivyo basi, mwanamke anauwezo wa kuona mambo mengi kwa upana kwa wakati
mmoja kuliko mwanamume. Tafiti za ajari za magari zinaonesha kuwa, kwa asilimia kubwa
wanawake hupata ajali za kugongwa au kugonga mbele au nyuma na wanaume kwa asilimia
kubwa hupata ajali za kugongwa au kugonga pembeni (upande ubavuni) wawapo katika
magari yao.
Inashauriwa kuwa, katika safari ya umbali mrefu, yampasa mwanamume aendeshe
hasa wakati wa usiku na wakati wa mchana mwanamke aendeshe gari, kwa sababu
mwanamume anaweza akatambua miondoko na aina za magari mengine yaliyo katika
barabara kwa mbele na nyuma yake. Itambulike kuwa hii ni kwa sababu jicho la
mwanamume limeumbwa na uwezo wa kuona mbali na jicho la mwanamke huona vyema
karibu na kwa upana mkubwa.
Mwanamke husikia vyema kuliko mwanamume na anauwezo mzuri wakutofautisha
sauti inapopanda na kushuka na sauti hiyo nini inaashiria. Wanawake pia wanauwezo
mkubwa wa kusikiliza na kuelewa lugha ya viongo vya mwili. Hivyo, ni vigumu sana kwa
mwanamume kumdanganya mwanamke wakiwa wanatazamana uso kwa uso. Kwa namna
hiyo, wanaume wanapohitaji kuwadanganya wake zao hutumia simu au barua wakiwa mbali,
ama taa zikiwa zimezimwa. Wanaume hutumia ubongo wa kulia tu wanapokuwa
wanasikiliza na wanawake hutumia ubongo wa kulia na kushoto kwa pamoja wakati
wanapokuwa wanasikiliza.
Mtoto wa kike mwenye umri wa wiki moja, anaweza akaitambua sauti ya mama yake
miongoni mwa sauti za wanawake wengine, ambapo mtoto wa kiume hawezi. Ubongo wa
mwanamke unauwezo wa kutenganisha na kutambua sauti na kisha kufanya maamuzi kwa
kila sauti tofauti na ubongo wa mwanamume. Mwanamume hupata shida au ugumu katika
kusikiliza mazungumzo wakati pakiwa na makelele.
Mwanamke anauwezo wa kutambua mabadiliko ya hisia ya mtu kutokana na sauti
yake ya mazungumzo, hasa kwa watoto wanapozungumza na watu wazima. Wanaume ni
wazuri kwa kuona kuliko kusikia. Wataalamu wa saikolojia wanadai kuwa, wanawake
huondokewa na misongo pale tu wanapotambua matatizo yanayowakabili. Na wakati
mwingine hupata ahuweni ya misongo pale wanapokumbatiwa na wale wanaowatia moyo.
Ngozi ya mwanamke inakiwango kikubwa cha hisia mara kumi zaidi ya ngozi ya
mwanamume. Ngozi ya mwanamke ni nyembamba sana kuliko ya mwanamume. Wanawake
hufurahia kuguswaguswa ngozi zao kuliko wanaume. Wataalamu wa tiba itokanayo na
kukumbatia (pet-patting therapy) wamethibitisha kuwa kukumbatia ni tendo la thamani
linalomsaidia mtu (hasa mwanamke) kuepuka huzuni na mtatizo mengine ya kisaikolojia.
kuzungumza nje kwa kutoa sauti. Sentensi za wanaume huwa fupi fupi sana na zenye
mpangilio kuliko za wanawake. Kwa wanandoa au wachumba, wakati mwanamume
anapokuwa amenyamaza kimya, ni rahisi kwa mwanamke kujihisi kuwa hapendwi.
Wanawake huongea huku wakisikiliza kwa wakati mmoja, lakini mwanamume
hawezi kusikiliza na kuongea kwa wakati mmoja. Kanuni ya msingi ya kuzingatia kwa
wanawake ni kwamba, wakati anapozungumza na mwanamume, aongee sentensi rahisi
zinazoeleweka na ajitahidi kumpa nafasi ya kuwa anafikiria kwa jambo moja baada ya
jingine. Sambamba na hilo, mwanamume hapendi kukatishwa wakati anapokuwa
anazungumza, ambambo ni ngumu kwa wanawake kufanya hivo.
Ubongo wa mwanamke umejengwa katika uchakatuaji (process-oriented) na ndiyo
maana wanawake wengi hupenda na kufurahia mchakato wa mazungumzo katika
mawasiliano. Sentensi zote zilizo katika hali au kauli ya taarifa hujenga mazingira rafiki kwa
wanawake pale wanapokuwa wanawasiliana wao kwa wao, ila hazifanyi kazi kwa wanaume,
kwa sababu, mwanamume hupenda sentensi zenye kauli ya moja kwa moja. Sentensi nyingi
za wanaume katika mazungumzo huwa ni za moja kwa moja na zimejikita katika kutoa
suluhisho au utatuzi wa tatizo zinapokuwa zinahitimishwa au kufika mwisho.
Ili kupata nafasi ya mwanamume kukusikiliza vyema yakupasa mtu ampe taarifa
kabla, mahali patakapofanyikia mazungumzo na mada husika itakayo tawala mjadala.
Ikitokea mwanamke anapenda kuongea sana na mtu fulani hasa jinsia ya kiume, jua ya kuwa
anamfurahia, na kama haongei naye jua yupo katika tatizo naye. Kuelezea na kutoa maana ya
neno kwa mwanamke si jambo la msingi kwake, maana yeye anajikita na sauti pamoja na
namna sauti inavyopanda na kushuka kulingana na hisia ya mzungumzaji sambamba na lugha
ya viungo vya mwili.
Mwanamke husoma kile kilichosemwa kutokana na sauti ya mzungumzaji, hivyo,
sura ya mwanamke huendana na hisia za msimuliaji au tukio husika linalotendeka kwa
wakati huo. Ili mwanamume kuuteka usikivu wa mwanamke yampasa sura yake na lugha ya
mwili kuendana na kile anachokizungumza au kusilikiliza. Tofauti na wanaume, wanawake
huwa na muonekano wa aina sita hadi saba katikanyuso zao wanapokuwa wakitazama au
kusiliza: sura ya huzuni, furaha, kuchukia, hofu, shauku, hasira, kushangaa na kurudia au
kusisitiza kile alichokiona au kukisikia.
Wanawake hupenda urafiki na kushirikiana, wanaume hupenda mamlaka na hadhi.
Wanaume hushindana, wanawake hushirikiana. Wanawake hupenda kuongelea chakula,
mavazi, urafiki, ndoa, watoto, haiba na matendo ya watu wengine. Wanaume hupenda
kuzungumzia michezo, kazi zao, habari na matukio, ujuzi na teknolojia. Jedwali lifuatalo
linaonesha tafiti iliyofanywa juu ya asilimia ya mazungumzo baina ya wanawake na
wanawake na wanaume kwa wanaume kwa njia ya simu katika kampuni moja ya simu huko
Uingereza mwaka 1999 kwa watumiaji wa simu 1, 000:
Aina ya mazungumzo Wanaume Wanawake
Marafiki 30% 53%
Mapenzi/mahusiano 18% 22%
Kazi 25% 11%
Michezo 16% 2%
Tafiti hiyo ilionesha pia, moja ya tatu ya wanawake wote mawasiliano yao yalidumu
angalau kwa dakika 15 na nusu ya wanaume mawasiliano yao yalidumu chini ya dakika 5.
Hivyo basi, wanawake huthamini mahusiano, wanaume huthamini vitu na kazi.
Mwanamke anaweza akamuacha mwenzi wake si tu kwa sababu hampatihii mahitaji
bali kwa sababu mwenzi huyo hatimizi hitaji la hisia kwa mke wake. Na mwanamume
anaweza akamuacha mwenzi wake kwa sababu ya kuona mwenzi huyo hana furaha kwa
sababu ya mahitaji anayotoa. Mwanamke anahitaji upendo, mahaba na mazungumzo. Hivyo,
mwanamume inampasa kuonesha mahaba, upendo na kumsikiliza mwenzi wake pale
anapokuwa anaelezea hisia zake badala ya kukimbilia kutuo suluhisho.
Mwanamume hapendi kukosolewa au kuonekana amekosea kwa sababu hujihisi kuwa
hajafanya jukumu lake impasavyo. Na hii ndiyo sababu ambayo humfanya mwanamume
kuwa mgumu kusema „samahani‟. Mwanamume huona kuwa anajihukumu moja kwa moja
kuwa anamakosa na ameshindwa. Ili kukabiliana na tatizo hilo, mwanamke inampasa
kutomfanya mwanamume kujihisi mkosaji anapojadili matatizo na yeye. Jambo hili kwa
wanaume huenda mbali sana, hata kwa kumpatia msaada mwanamume hujihisi ama
kutafasiri kuwa hayuko vyema sana au hajiwezi.
Mwanamume anachukulia kukosolewa, na ndio maana hupenda kuoa wanawake
ambao wanawazidi umri au ambao hawako juu yao kiuwezo aidha wa kielimu na kipato.
Wanaume hawapendi kujisalimisha kwa wenzi wao kuwa wameshindwa maana huhisi
wanaweza wasipendwe, lakini kiuhalisia mwanamke humpenda mwanamume ambaye
husema pale anaposhindwa. Mwanamume huficha hisia zake akimanisha kutoonesha wazi
wazi udhaifu wake. Kiasili mwanamume ni mtu mwenye mashaka, ushindani, kujihami na
anayejaribu kuzificha hisia zake.
Kwa mwanamume kuonesha hisia zake wazi wazi, hujiona kama ameshindwa
kujimudu. Tabia hii kuwa imejengeka tangu utoto wake kwa sababu ya maneno aliyokuwa
akiambiwa “wanaume hawalii”, “onesha sura ya kiume”, “kuwa na sura ya kazi”. Kwa
mwanamke, ubongo wake umeunganishwa kwa kuwa wazi, kuamini, kushirikiana, kuonesha
hisia. Kwa hoja hii, wanawake na wanaume hukutwa na changamoto kwa pamoja hasa kwa
kila mmoja kuchanganywa na mwenzake juu ya kutoelewa hali na hisia ya mwenzake.
Changamoto nyingine kwa wanaume ni kutokubali ama kuchukia kupewa ushauri. Hii
ni kwa sababu, mwanamume hujihisi kuwa anauwezo wa kutatua matatizo na kuona kuwa,
kuyajadili matatizo yake na wengine ni kuwaongezea mzigo wengine, labda huyo mtu awe na
jibu zuri zaidi. Kwa mwanamke kuweka wazi matatizo yao hujihisi kuwa na ahueni kutoka
kwenye msongo. Wanawake hawahitaji utatuzi wa matatizo yao, bali wanahitaji kuongea
matatizo yao na kusikilizwa tu. Mwanamke kushiriki tatizo lake na mtu mwingine ni
kuonesha ishara ya uaminifu katika urafiki au uhusiano wao.
Tofauti na mwanamke, mwanamume anapokuwa na msongo hawezi akaongea.
Wanaume huongea kwa ndani kwa sababu ubongo wao (wa kulia) hauna sehemu imara ya
mazungumzo kama ilivyo kwa wanawake. Kwa sababu hiyo, mwanamume hawezi akawa
anatatua tatizo huku anaongea. Kwa utofauti huo: mwanamke ni mwongeaji na mwanamume
= SURA YA 14 =
mwenzi katika ndoa kunajenga hali ya kulipa kisasi, maana kisasi ni kulipa baya kwa jinsi yo
yote ile kwa mtu aliyekukosea (Warumi 12:19; Yakobo 4: 12).
inayokataza kuua hivyo hutenda dhambi (1Yohana 3:15, 1Yohana 3:11-12, Mathayo 5:21-
22.)
Kutosamehe Huongeza Maadui na Uadui: Kutosamehe kunakopelekea kulipa kisasi
huongeza maaudui na uadui miongoni mwa wanandoa pamoja na watu baki. Kulipa baya kwa
baya huwa hakuleti suluhu juu ya migogoro katika ndoa au jamii, bali huongeza uadui na
maadui kwa sababu ya kukosekana kwa upande au mtu anaye weza kujishusha katika, hivyo,
kulipizana mabaya hufanyika kwa ushindani wa kila upande.
= SURA YA 15 =
Zaburi 77:11-12
HITIMISHO
Mithali 25:11
Ndoa ni sawa na maisha, ambayo hutupa changamoto ili kupima ujasiri wetu na
utayari wetu wa kubadilika. Katika muda huo, hakuna nafasi ya kujifanya kwamba hakuna
linalotokea au kusema kuwa hauko tayari kuipokea hiyo changamoto; maana changamoto za
ndoa hazisubiri utayari wa mwanandoa. Ndoa ni maisha uliyoyaanza ambayo hayaangalii
nyuma, ni kama sheria mpya inayotungwa juu ya jambo fulani, huwa inaanzia pale
iliposainiwa.
Ili uwe huru pale unapoamua kuingia katika kifungo cha ndoa, lazima ujifunze
kusamehe na kusahau na kuacha mambo mengine yapite. Acha kuhusika na mambo
madogomadogo katika maisha ya ndoa bali acha yaende kwa kusamehe na kusahau. Tupa
woga unapoamua kuzikabili changamoto za ndoa, acha kuzisumbukia kumbukumbu za
nyuma juu ya nini kilitokea katika magumu ya ndoa. Kubali kuanza upya ili kuijenga
thamani ya ndoa aliyokupatia Mungu.
Kushindwa kupanga ni kupanga kushindwa. Kanuni ya mafanikio katika maisha ya
ndoa ni sawa na jambo lo lote binadamu afanyalo ambalo huwa ni kuwa na mpango thabiti
unaoelekeza ni wapi mwanandoa anataka kufika na kwa kiwango gani. Mipango ya
mafanikio yetu katika ndoa hupangwa na vichwa vyetu pamoja na fikra tulivu zinazotawala
mioyo yetu huku tukiomba msaada toka kwa Mungu. Tukiwa na mipango, kinachofuatia ni
mikakati; hii huwa ni njia ya utekelezaji wa mipango yetu ndani ya ndoa.
Ukijua uendako katika ndoa ni rahisi sana kupata njia sahihi ya kukufikisha; hata kama
utachelewa kiasi gani, lakini uhakika wa kufika unao. Yaweza kuwa ulichelewa sana katika
kumpata mwenzi sahihi au kuingia katika ndoa, bali, jua ya kuwa, nafasi ya kuyafikia
malengo uwapo ndani ya ndoa bado unayo maana maisha ya ndoa hayakuhitaji uwe na elimu
kubwa sana ili ufanikiwe, bali kinachotakiwa ni kujitambua, kuweka mipango iliyo na
mikakati mizuri yenye vipaumbele, kujiamini na kusimamia unayo yaamini sambamba na
mapenzi ya Mungu.
Uwapo katika ndoa, kumbuka kuwahudumia na kuwalisha watoto wote bila ubaguzi
maana wote ni watoto wako na wana haki sawa katika kuyapata mahitaji yao. Kumjua mtu au
kutokumjua hakukupi sababu ya kumdharau au japo kumuamini sana; hivyo, watoto ambao
BWANA atakupatia uwapo katika ndoa jitahidi kuwafundisha kuto wadharau watu juu ya
kile wazazi au wao walichonacho ambacho huyo mtu hana, bali wajue kuwa kila mtu ni
muhimu kwao na ni muda tu haujafika au Mungu hajapanga wala hawajamkosea.
Ukiwa na Yesu utayaweza mambo yote yaliyo katika ndoa bila kujali kuwa umetoka
kwenye familia ya aina gani na wala haijalishi maisha yako ya zamani yalikuwaje kabla ya
sasa (soma Wafilipi 4:13). Uamuzi wako utakaoufanya sasa juu ya nini unataka kukitilia
mkazo na nini maana ya vitu fulani kwako katika ndoa, aina ya mafanikio uyatakayo na jinsi
ambavyo utafanya ili kuyafikia ndicho kitakachokupa mwanga wa mtu wa aina gani utakuwa
hapo badaye katika ndoa na familia yako.
Kila kitu duniani chenye mafanikio kilianzishwa na mtu fulani, ndivyo hata katika
familia, wazo laweza kuwa kichwani mwa mmoja wa wanandoa na yeye atakapomshirikisha
mwenzi wake atahesabika kuwa yeye ndiye aliyeleta jambo hilo japo ustawi wa familia
utakaopatikana ni manufaa ya wote katika ndoa. Kila mtu mwenye mafanikio alikuwa na
ndoto kabla, akazichambua ndoto zake na kuziishi huku akifanya kila njia kuzileta kwenye
uhalisia kwa kushirikisha wengine, hivyo, mwanandoa mmoja mmoja ananafasi ya kuifikisha
familia yake pale atakapo kama wote wawili watamshirikisha Mungu kwa kila hitaji na lengo
lao.
Kifo ni hatua ya mwisho ya muda wa binadamu katika dunia; haijarishi ni muda gani
utachukua kuwa hapa duniani ila jua tu kwamba ipo siku na wewe utakufa. Cha kujiuliza ni
kitu gani katika maisha ya uhai kitakacho kutambulisha baada ya kifo chako. Ni kitu gani
kitakufanya usimame ukiwa mwenye haki mbele za Muumba wako utakapokuwa ukifanyiwa
hesabu ya matendo yako ya imani katika siku ya hukumu? Hivyo, kufa hakuhitaji uwe
mgonjwa au upate ajali, ili ufe inahitajika siku yako iwe imefika.
Watu waliofanikiwa zaidi katika ndoa zao ni wale walioyajua matatizo, waliozijua
harakati za maisha na ndoa zao, waliokumbana na misukosuko na taabu, waliokutana na
majaribu bila kukata tamaa, lakini mwisho wa siku waliyakabili na kusonga mbele. Lo lote
ambalo haliwezekani leo, unaweza kulifanya liwezekane kesho, kama tu utaamua juu ya
mustakabali wa njia uipitayo huku ukimwalika Yesu atembee katika ustawi wa familia yako.
Umaskini wa fikra ni mbaya zaidi kuliko umasikini wa kipato. Fikra sahihi kwa wakati
sahihi ndio njia ya kupata suluhu ya kila limfikalo mwanandoa. Hekima ya kweli ni kumjua
Mungu ili uwe mwenye haki mbele zake; lakini upumbavu ni kuyajua yote ya dunia na raha
zake za kitambo kisha mwisho wa ulimwengu unadharauliwa milele huku ukilipwa ujira
wako sambamba na uliyo yatenda. Walee watoto katika hekima ya kumjua Mungu na siyo
hekima za kiduni ambazo haziwavushi ng‟ambo ya kaburi. Fanya sehemu yako kama mzazi
ili usije ukadaiwa kondoo wa nyumbani mwako ambao BWANA alikupatia nafasi ya
kuwalea na kuwatunza katika misingi inayostahili ili waurithi uzima wa milele.
Si vyema ukajisahau na kurizika kama bado hujafanikiwa kuurithi uzima wa milele.
Pamoja na familia yako, panga namna ya kuyakabili mashambulizi ya Shetani kwa kuwa
yeye ameshapanga namna ya kukukabili toka mwanzo wa uasi wake. Jiulize, kwa nini
unahali ile ile ya kiroho iliyo chini ya kiwango. Jiulize ulivyokuwa mwaka jana na ulivyo
mwaka huu upo sawa, au umepungua zaidi kwa sababu ya kuheshimu sanamu za maisha
kuliko Mungu. Je, kwanini hakuna tofauti ya mafanikio yako ya kiroho japo kuna ongezeko
la umri katika ndoa? Gundua kipaji chako, taranta na karama (kipawa chako) yako na uitumie
kwa ajili ya kazi ya Mungu. Elimu yako si kitu pia kama haina mchango katika kazi ya
BWANA hapa duniani.
Upendo wetu juu ya wengine hutufumba macho na kutufanya tusahau kuwa tuna
jukumu la kujitazama wenyewe pia, pale wengine wanaposhindwa kujali hisia na majonzi
yetu. Bwana atutie nguvu, hekima, uwezo, maarifa na upendo uliojengwa kuto kwake. Yesu
aponye ndoa zetu ili ziwe mbingu ndogo hapa duniani. Yesu atamalaki na kuzulu familia zetu
huku akizilinda na kuziepusha na mishale ya Shetani mwenye uhitaji wa ajabu katika
kuiangamiza tasisi ya ndoa.
REJEA
Andrews, S,. & Little, B: (2000). Anatomy of Desire: The Science and Psychology of
Sex, Love and Marriage.
Allen, L.S., Richey, MF., Chai, Y.M. & Gorski, R.A: (1991). Sex differences in the
corpus callosum of the living human being, Journal of Neurosdence 11, 933-942.
Beatty, W.W: (1988). „A Fargo Map Test: A Standardized Method for Assessing
Remote Memory for Visuospatial Information’ Journal of Clinic Psychology 44, 61-
67.
Bailey, J.M. & Bell, A.P: (1995). Familiality of Female and Male: Cambrigde
University Press.
Daniel, G: (2000). Change Your Brain, Change Your Life: The Breakthrough
Program for Conquering Anxiety, Depression, Obsessiveness, Anger and
Implsiveness. Times Book.
DeAngelis, B: (1997). Sectrets About Men Every Women Should Know. New York:
Norton
Pease, A. & and Pease, B: (2001). Why Men Don’t Listen and Women Can’t Read
Maps: Great Britain. Orion Publishing Group.
United Bible Societies (1952). The Holy Bible Version in Kiswahili. Union Version:
Published as Biblia Mandiko Matakatifu. Dodoma: The Bible Society of Tanzania.
Vishala, M: (2006). Guidance and Counseling: For Techers, Parents and Students.
New Delhi: Schand & Company Ltd.
White, E. G: (1980). The Adventist Home. Tailend and UK: The Estnaborougs Press
Ltd.
White, E. G: (1970). Conflict and Courage. E. Publication: Ellen G. White Estate Inc.