Professional Documents
Culture Documents
tz
Sauti ya Waislamu
Ewe MUISLAMU, Unajua kuwa anayekufa bila kuhiji hali ya kuwa aliwahi kupata uwezo anakufa Yahudi au Nasara, na Uislamu hautomtambua? Hijja ni haki ya Mola wako iliyopo juu yako! Basi mpe Mola wako haki yake kwanza kabla kuridhisha nafsi yako kwa kufanya mengine. Gharama zote ni Dola 4,300 tu. Karibu Ahlu Sunna wal Jamaa. Tafadhaliwasiliana nasi ifuatavyo: Tanzania Bara: 0717224437; 0777462022;Unguja: 0777458075;Pemba: 0776357117.7.
Haraka ya kuwaita FBI na CIA ya nini? Hakuna tulilojifunza kwa Mauricio Funes? Waislam, Wakristo wawe makini wasipotoshwe
Ni kweli Waziri Mkuu: La Waislamu gumu ila Maalim Seif akerwa na kauli ya Nchimbi
WAZIRI wa Mambo ya Ndani, Dkt. Emmanuel Nchimbi (katikati) akiwa na Kamanda wa Polisi Zanzibar, Mussa Juma. AMESEMA kweli Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda. Waislamu walijisahau wakadhani kuwa wanaweza kutoa malalamiko, madai na mashariti, serikali ikasikiliza na kutekeleza. Hilo liliwezekana kwa Wakristo ambao tunaambiwa kuwa walimpa mashariti
Ya Wakristo yametekelezwa papo hapo Waliochafua karatasi za mitihani si wajinga Ni namna ya kupinga ya Timu ya Wanga
m a g u m u Wa z i r i w a Mambo ya Ndani Mheshimiwa Emmanuel Nchimbi na akayatekeleza mara moja ila akaomba muda wa kutekeleza jambo moja tu katika mashariti matano aliyopewa. Pengine kwa kuona kuwa Wakristo wao wametoa mashariti na kukubaliwa papo hapo na serikali, Inaendelea Uk. 2
Asema Zanzibar hakuna ugaidi Wananchi wasijekamatwa ovyo JUMAZA yaonya vyombo vya habari
2
S.L.P. 55105, Simu: +022 2400786 Cel: 0784 370 208, 0713 110 148, 0755 260 087 , DSM. www.annuurpapers.co.tz E-mail: annuurpapers@yahoo.co.uk Osi zetu zipo: Manzese Tip Top Usangi House (Jengo dogo), barabara ya Morogoro, D'Salaam
Tahariri/Tangazo
AN-NUUR
Ukiacha yale malalamiko ya Wakuu wa Shule za Kiislamu mwaka jana, zipo tuhuma nyingi ambazo zinawafanya wanafunzi kutokuwa na imani na kuamini kuwa F, E na D wanazopewa zinatokana kweli na makisi walizopewa na wasahihishaji mitihani au wametunukiwa na Timu ya Wanga. Katika hali kama hii, zaweza kuwepo namna nyingi za kuonyesha kutoridhika (ku-protest) na utaratibu unaotumika kutahini. Lakini jingine ni hali iliyopo mashuleni. Zipo shule ambapo zaidi ya nusu ya wanafunzi huhama au kuacha shule kwa sababu hakuna walimu, madawati, hakuna vyoo au matatizo mengine. Unafikiri hao wachache watakaobaki hadi kufanya mtihani wa kidato cha nne au cha sita, wataandika nini kama si kuonyesha kuwa hawaridhiki na mfumo uliopo ambao umewatupa na haujali kuwa nao wanastahiki kupata eilimu bora? Kama litakuwepo kosa, basi itakuwa kwa hao walioandika matusi, lakini vinginevyo kama tunataka kutatua tatizo, basi tuwaone wanafunzi walioandika mashairi na kuwalaumu wabunge badala ya kuandika majibu, ni mashujaa. Wanaonyesha kutokuridhika kwao na hali ilivyo nchini. Shuleni hakuna walimu wala vitabu na wachache waliopo hawafundishi. Hii ndio hali halisi katika nchi hii na wala isidhaniwe kuwa ni tatizo la Wizara ya Elimu pekee. Wapi kuna nafuu? Bomba linapita mtaani, lakini hakuna maji. Umeme kila leo ni wa kukatika ovyo. Kilimo imekuwa wimbo, hakuna maendeleo yoyote. Acha mpira, hata tukiambiwa kuingia mashindano ya kucheza ngoma, hakuna tutakachoambulia. Angalia vichekesho (komedi) vya nchi jirani ulinganishe na wa hapa kwetu. Almuhimu tunasema
RABBIUL THAN 1434, IJUMAA FEBRUARI 22-28, 2013 kuwa mambo yanakwenda ovyo katika nchi hii. Nchi ndogo kama Rwanda ambayo imetoka katika machafuko hivi karibuni tu, inatuwashia taa ya kutupita kwa kasi katika kila kitu. Sisi tumo tu tunapiga porojo. Kwa mtaalamu yoyote wa elimu na utahini, hawezi kukubaliana na maelezo ya Ndalichako kuwa kuchora Mess na kuandika mashairi ndio kuliko sababisha wanafunzi kufeli zaidi ya asilimia 60. Atuambie katika hao waliopata sifuri (F), wangapi ni katika hao waliomchora Mess na kuandika single za muziki? Atuambie, katika kutoa matokeo hayo, CA zimepewa uzito gani? Na je, Kamati yake ya Kutunuku mwaka huu kwa kila somo, A, B, C na D, zimeanzia na alama ngapi na kwa nini? Lakini Swali muhimu ambalo linahitaji kujibiwa kwa uhakika ni hili: Je, matokeo haya yaliyotangazwa na Waziri Kawambwa, ni matokeo halisi yanayowakilisha ufaulu (alama) zilizotolewa na wasahihishaji? Kujua ukweli huu ni jambo jepesi sana. Karatasi za mitihani zipo, hazijachomwa moto. Zipitiwe kuhakikisha kuwa makisi zilizotolewa ndio zilizotangazwa na Baraza la Mitihani. Hizi hoja za walimu hawasomeshi, hakuna walimu, hakuna vifaa, watoto hawasomi, shule za Kata hivi na vile, ni hoja za kupotosha. Huko kunaweza kuwa na matatizo kweli, lakini sio kuzaa matokeo haya. Tatizo lipo Baraza la Mitihani na Kamati yake ya Kutunuku. Kama serikali itaona kuwa hakuna haja ya kujua ukweli juu ya matokeo haya, kwa maana ya kujua iwapo F walizopata watahiniwa zaidi ya asilimia 60 ni zao au ni zakuchakachuliwa, itabidi tuwe na wasiwasi kuwa serikali yenyewe inahusika katika mchezo huu. Ni kuku anayekunywa mayai yake au paka anayekula watoto wake. Sasa swali litabaki kwa lengo gani? Kwa masilahi gani? Ili iwe nini? Kwa sasa tusingependa kuingia katika uvumi na nadharia zinazosambaa za vurugu za mikopo kwa wanafunzi na uchaguzi mkuu 2015.
AN-NUUR
MAONI YETU
Kufeli wanafunzi Ya p o m e n g i yamesemwa juu ya kufeli sana wanafunzi wa kidato cha nne mwaka huu. Na zaidi juu ya baadhi ya wanafunzi kuandika vitu visivyo husika kama vile kuchora picha za wanamichezo maarufu na hata kuandika matusi. Sisi tuseme kuwa zipo njia nyingi za watu kuonyesha hisia zao kuwa hawaridhiki au wanapinga jambo fulani. Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania Dr. Joyce Ndalichako anasema kuwa wapo baadhi ya wanafunzi badala kuandika majibu ya
P.O. Box 55105, Tel: 2450069, 0712 974428 Fax: 2450822 D Salaam E-mail: ipcubungoislamic@gmail.com
Mlete mwanao apate Elimu bora itakayomwezesha kujiunga na Kidato cha Tano.
Kwa mawasiliano zaidi piga namba: 0714 888557/0659 204013 Wabillah Tawiq MKUU WA SHULE
Habari
AN-NUUR
WA Z I R I M k u u , Mheshimiwa Mizengo Pinda, amejikuta akibaki ukumbini yeye pamoja na Maaskofu, katika kikao cha kutafuta muafaka wa vurugu za Wakristo kuchinja, Mkoani Geita k u f u a t i a Wa i s l a m u kutoka nje ya ukumbi. Taarifa kutoka ndani ya kikao hicho zimedai kuwa, Waislamu waliamua kuachana na kikao hicho, baada ya Waziri Mkuu kuwajibu kuwa hatoweza k u w a t o w a Wa i s l a m u wanaoshikiliwa na Polisi, kwa kuwa wana kesi ya mauaji na Maaskofu walioachiwa wana kesi ya kuchinja. Majibu hayo ya Waziri Mkuu, yanafuatia mashariti sita ya Waislamu waliyoyatoa ili kuweza kushiriki katika kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji wa Geita, Februari 17, 2013, ili kuweza kupata suluhu kati ya Waislamu na Wakristo katika sakata la kuchinja. Imedaiwa kuwa kumekuwa na manuguniko kutoka kwa Waislamu Mkoani Geita, wakidai kutotendewa haki tokea kuibuka kwa vurugu hizo, mapema hivi karibuni. Zaidi wamedai ni pale ambapo watuhumiwa Maaskofu na Wakristo, waliokamatwa katika vurugu hizo, kuachiwa kwa inayodaiwa amri ya Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk. Emannuel Nchimbi, baada ya kutekeleza msimamo wa Maaskofu kuwa hawapo tayari kuzungumza naye hadi pale wenzao waliokuwa wakishikiliwa na Jeshi la Polisi waachiwe, jambo ambalo lilitekelezwa. Sasa sisi kama Waislamu tunakutaka wewe kama Waziri Mkuu, kwamba wale wenzetu waliko ndani nao waachiwe na waletwe katika kikao hiki kama walivyotolewa wale Maaskofu ili tujadili kwa
kikimnukuu msemaji wa Waislamu katika kikao hicho. Msemaji huyo wa Waislamu aliyetajwa kwa majina ya Bw. Hamza Omari, alifafanua kwamba Waislamu katika nchi hii wameshauwawa wengi, kwa kutekeleza maagizo ya Maaskofu, yakiwemo m a u a j i y a Wa i s l a m u Mwembechai, Kijana wa Kiislamu Kakola, Shinyanga na hata Zanzibar. Bw. Omari, alisema katika mauaji yote hayo haijapata kutokea kiongozi yoyote wa Serikali kuhudhuria mazishi ya Waislamu hao, wala kiongozi wa Serikali kuomba msamaha wa aina yoyote au kutoa rambirambi kama inavyofanya kwa Wakristo. Waislamu hao wakamtaka Wa z i r i M k u u P i n d a , akubali Serikali kutoa ahadi yakulipa fidia ya uharibifu uliotokea katika Msikiti wa Buseresere, kama ilivyoahidi kulipa dia Makanisa yaliyoungua moto katika vurugu za kidini zilizotokea Mbagala Jijini Dar es Salaam. B w. O m a r i a l i s e m a kwamba, Serikali imekuwa inaegemea upande mmoja wa Wakristo, kila inapotokea mgongano baina ya dini hizo mbili, na kuwapuuza Waislamu jambo ambalo ni hatari. Alitolea mfano matukio ya Mbagala na Zanzibar kwamba baada ya kuungua moto, walionekana viongozi wa Serikali wakubwa wakiomba radhi na kuahidi kuwashughulikia wale waliofanya uharibifu huo na ahadi ya kulipa fidia, jambo ambalo ni kinyume kabisa inapotokea uharibifu Msikitini. Kwa maana hiyo kule Buseresere Msikitini, katika vurugu hizi, Wakristo wamevunja vibanda vya Msikiti na mali zingine kuteketezwa kwa moto, tunakutaka wewe Waziri Mkuu, uweze kuthibitishia, kama Serikali iliweza kuahidi na kulipa fidia Makanisa, je Serikali ipo
WAZIRI Mkuu, Mheshimiwa Mizengo Pinda tayari kuahidi na kulipa fidia mali za Msikiti wa Buseresere?, Chanzo chetu kilimnukuu Bw. Omari, akitoa hoja za Waislamu. Wa i s l a m u hao w a l i m w a m b i a Wa z i r i Mkuu Pinda, wakimtaja ofisa mmoja wa Polisi Buseresere, na askari mmoja akiwa katika sare za kazini na bunduki mkononi, kwamba walioneka katika tukio la uchinjaji Kanisani, kabla ya vurugu kuibuka. Lakini pia alidai kuna aliyempiga Muislamu risasi ya mguuni katika vurugu hizo pamoja na kiongozi mmoja wa siasa aliyekuwa kinara wa uhamasishaji Wakristo kuchinja, mpaka sasa alidai haijafahamika watu hao wote, Serikali imewachukulia hatua gani. Wa i s l a m u hao walionyesha kushangazwa na hatua zilizochukuliwa za kuwahamisha watuhumiwa wa Kiislamu kutoka Mkoa wa Geita, lilipotokea tukio na kudaiwa kupelekwa Biharamulo, ambako hakuhusiki na vurugu hizo. Wa i s l a m u pia walilalamika kitendo cha Wachungaji waliosababisha kadhia hiyo kuachiwa, kwa tamko la Waziri wa Mambo ya Ndani, (Nchimbi), baada ya Wakristo kutoa sharti la kwamba hawawezi kuzungumza naye mpaka Wachungaji walio ndani waachiwe na washiriki katika kikao hicho na Waziri alitekeleza hilo. Aw a l i m s e m a j i w a Maaskofu katika kikao hicho, alimtaka Waziri Mkuu Pinda, kutoa msimamo wa Serikali kama wachije au wala, sambamba na Serikali kumlea mjane wa Mchungaji aliyekufa. Tunachotaka kutoka kwako wewe muheshimiwa Waziri Mkuu ni kauli moja tu, tuchinje au tusichinje, lakini pia Serikali imlee mjanae wa Mchungaji aliyekufa. Kilinukuu chanzo chetu cha habari, kutoka kwa Askofu, huyo. Askofu Mussa Masanja, alieleza kuwa kwa mujibu wa vitabu vitakatifu yaani Qur an na Biblia, ni kwamba Qur an inaruhusu kula nyama iliyochinjwa na mtu wa kitabu, huku akinukuu maelezo ya Sheikh Alhad Mussa, aliyeongea mapema hivi karibuni, kupitia chombo kimoja cha Televisheni. Lakini, Askofu huyo
Inaendelea Uk. 4
Maoni
AN-NUUR
MAALIM Seif ameelezea kusikitishwa kwake na kauli iliyotolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dkt. Emmanuel Nchimbi ya kupandikiza ugaidi Zanzibar. Maalim Seif amesema hayo kufuatia kauli ya Waziri Nchimbi kwamba mauwaji ya Padri Evarist Mushi ni ugaidi. Licha ya kukiri kuwa mauwaji hayo ni uhalifu, lakini haijafikia hatua ya kuitangaza Zanzibar kuwa nchi ya kigaidi, na kwamba kufanya hivyo ni kuijengea sifa mbaya Zanzibar. Kauli kama hizi ukweli hazisaidii zaidi ya kutuvuruga, ni kweli ni kitendo kibaya na kikubwa, lakini ugaidi ni mkubwa zaidi na sisi hatujafikia na wala hatutokia hatua hiyo, alionya Maalim Seif. Amesema ni vyema kwa viongozi wanaotokea upande wa pili wa Muungano kufanya mashauriano na viongozi wa Zanzibar kabla ya kutoa kauli ambazo zinaijengea sifa mbaya na kuitia doa Zanzibar. Awali Maalim Seif Sharif Hamad amelaani vikali kitendo kwa kupigwa risasi na kuuliwa kwa Padri Evarist
MAKAMU wa kwanza wa Rais Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad Mushi wa kanisa katoliki Zanzibar na kusema kuwa kitendo hicho kimevuruga sifa njema ya Zanzibar ya
Inatoka Uk. 3 alidaiwa kusema, Biblia hairuhusu Wakristo kula nyama iliyochinjwa kwa Mungu mwingine na kwamba kwa Muislamu kuchinja ni ibada iliyokamili, akahoji iweje wao (Wakristo) walazimishwe kuabudu kupitia imani ya Kiislamu? Alisema, kwamba wao Wakristo hawapo tayari kuendelea kula nyama zinazochinjwa na Waislamu kwa sababu ya mazoea tu, kwani alidai mazoea huwa yanabadilika, hivyo alidai mazoea huwa inaka wakati yanabadilika. Askofu, huyo imedaiwa kuwa alimtaka Waziri Mkuu Pinda, kupiga marufuku
Waislamu hao. Baada ya kutolewa Buseresere, walipelekwa Chato kisha walihamishiwa Biharamulo, wakati huko ni mkoa mwingine sasa hatuelewi inafanywa hivyo kwa mujibu wa sheria gani, na hadi sasa hatuelewi kama wapo salama au la kwani miongoni mwao ni wale majeruhi walikatwa mapanga. Alisema Ust. Saleh Haruna. Ta a r i f a z a a w a l i zilifahamisha kuwa watuhumiwa watatu wameshafikishwa Mahakamini na kusomewa kosa la mauwaji na wengine makosa ya jinai ambao wa tuhuma za mauwaji wamepelekwa mahabusu Biharamulo na wengine Chato.
5
PARIS AFISA anayeshughulikia masuala ya dini katika Wizara ya Mambo ya Ndani ya Ufaransa, amesema kuwa idadi ya watu wanaoingia katika dini ya Uislamu imeongezeka mara dufu nchini humo katika kipindi cha miaka 25 iliyopita. Bernard Godard, amebainisha suala hilo katika ripoti iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Ufaransa na kuongeza kuwa, suala la watu kuingia katika dini ya Uislamu nchini Ufaransa, limekuwa jambo muhimu na kwamba ongezeko la idadi ya watu wanaoingia katika dini hiyo nchini humo hususan mwaka 2000 ni jambo linalohitaji kupewa mazingatio. Imeelezwa kuwa mwenendo mzuri wa Waislamu wa Ufaransa katika masuala mbalimbali ya kijamii na kiutamaduni, ndio unaowavutia Wafaransa wengi katika dini ya Uislamu licha ya propaganda chafu
Habari za Kimataifa
AN-NUUR
kati ya laki moja hadi mbili wameingia katika dini hiyo. Ta k w i m u h i z o zinaonesha kuwa idadi ya Wafaransa wanaoingia katika dini ya Uislamu tangu mwaka 2000, imeongezeka mara dufu ikilinganishwa na ile ya mwaka 1986 ya watu laki tano pekee kwa mwaka.
Semina ya Maimamu na Makhatibu chini ya Masheikh: Amrani Kilemile Abdallah Bawaziri Ahmed Twalib Itakayofanyika: Uwanja wa Sababa (Ukumnbi wa Wizara ya Fedha) Muda: Saa 2L30 asubuhi - 6:30 mchana. Siku: Jumamosi na Jumapili Tarehe: 23/2/2012 - 24/2/2013 Wote Mnakaribishwa
Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika mwezi Aprili mwaka huu, na Rais Muhammad Mursi, alitakiwa kuipitisha sheria hiyo Februari 25 na kutangaza tarehe ya uchaguzi. Mahakama ya Katiba ya Misri inaundwa na majaji wa wakati wa utawala uliopinduliwa wa Hosni Mubarak na baada ya mapinduzi ya wananchi wa Misri, Mahakama imekuwa ikiingilia mara kwa mara maamuzi ya serikali ya mpito na hata kulivunja Bunge.
Benki ya Dunia imetangaza kuwa, ubadhirifu wa mali na ufisadi ni kikwazo kikubwa cha ustawi wa nchi zinazoendelea hasa za barani Afrika. Ripoti ya Benki ya Dunia imebainisha kuwa, nchi zinazoendelea, hususan za bara la Afrika hupata hasara ya dola bilioni 4 kila mwaka kutokana na ubadhirifu na ufisadi wa kiidara. Utafiti uliofanywa na Benki ya Dunia unaonesha kuwa, kuna uhusiano wa moja kwa moja baina ya kubakia nyuma kimaendeleo kwa nchi nyingi na suala la kuenea usadi katika nchi hizo. Aidha tathmini ya Benki hiyo inaonesha kwamba, mipango mingi ya maendeleo katika nchi zinazoendelea hasa barani Afrika, imekuwa ikikwama kutokana na ulaji rushwa, ufisadi na ubabaishaji uliokithiri na kwamba, masuala hayo ndio chanzo halisi cha kukwama juhudi za maendeleo katika nchi nyingi hasa za barani Afrika. Ukosefu wa utawala bora umeelezwa kuwa, ni kikwazo kingine cha maendeleo na ustawi katika nchi zinazoendelea.
6
Na Shaaban Rajab
MIUJIZA ya Sheikh Said John, ilianza kujitokeza tangu wakati anazaliwa katika Hospitali ya Mount Meru jijini Arusha mwaka 1989. Mzee John Edward, alimwambia mwanaye Joseph, Ulipozaliwa tu, hukutoa sauti wala kuonyesha kutapatapa (movement), ili kuthihirisha dalili ya kuwepo uhai, vipimo vya madaktari havikugundua kuwepo uhai, wakasema, haikuwa riziki, mtoto amepoteza . Mzee Hassan (John) Edward, alimwambia mwanaye Said (Joseph) John. Shariff Said John, ambaye anapenda zaidi kuitwa Sherikh Said John, akidai kuwa cheo cha Shariff ni daraja kubwa sana kumzidi, alizaliwa katika familia ya Kikristo, wazazi wake wakiwa ni waumini wa dhehebu la Pentekoste Assemblies of God. Sheikh Said anasema kuwa, mara baada ya madaktari kuthibitisha kwa vipimo kuwa amefariki, baba yake, Mzee John akashauriwa arudi nyumbani kufanya maandalizi ya kuzika kichanga. Baadae alirejea Hospitalini na wazee wawili kuchukua mwili wa mwanaye mchanga. Walimchukua kichanga na kuanza hatua za kurejea nyumbani. Lakini walipokuwa njiani, mtoto alipiga chafya na kuanza kulia, hapo hapo iliwalazimu kurudi tena hospitalini ili upata maelekezo zaidi kwa madaktari. Madaktari kwa mara nyingine wakachukua vipimo na kuthibitisha kuwa mtoto aliyezaliwa na kuthibitishwa kuwa kafa, alikuwa hai. Baada ya matibabu na kinga kwa mtoto, Mzee John na wenzake walirejea nyumbani. Baada ya siku chache kupita, mtoto alibatizwa na kupewa jina la Joseph. Hivyo jina lake rasmi likawa ni Joseph John Edward. Kwa kuwa wazazi wake Joseph walikuwa ni waumini wa Kikristo, walikuwa na kawaida ya kwenda Kanisani kila Jumapili kwa ajili ya ibada. Kwa kuwa Joseph alikuwa mchanga, waliandamana naye. Alipokuwa kanisani, aidha alilala fofofo wanapoingia kanisani au alilia sana, kiasi cha wazazi kulazimishwa kutoka nje kwani kilio cha mtoto kilivuruga ibada
Makala
AN-NUUR
Shariff Said John (katikati) akiwa nchini India katika moja ya mihadhara yake.
iliyokuwa ikiendelea. Wa z a z i w a J o s e p h hawakujua tatizo ni nini kwa kuwa mtoto haumwi na alikuwa kashiba. Wakaona ni hali hiyo inaweza kumpata mtoto mchanga. Mtoto Joseph alipotimiza umri wa miaka mitatu, akalikana jina lake la Kikristo na kujiita Saidi, na kusema yeye ni Muislamu. Akaanza kusikika akisema maneno ambayo kwa wazazi w a l i o k u w a Wa k r i s t o , hawakujua maana yake. Kwa mtazamo wao, walidhani mtoto wao amekubwa na mapepo machafu. Kufuatia hali hiyo Mzee Joseph na mkewe Rose walianza kuombea kwa jina la Yesu ili mapepo yanayomwandama mtoto wao yatoke. K a t i k a h a l i iliyowashangaza zaidi, kila wachungaji walipomfanyia maombi, mtoto Joseph alikuwa akisema hana mapepo, bali yeye ni Muislamu na aliangusha kilio kikali hadi wakati fulani kupoteza fahamu. Baada ya hali kuwa hivyo, Mzee John alipendekeza kusitishwa maombi kwa mwanaye. Lakini mama mtoto, yaani Bi. Rose, hakukubali ushauri huo na kusisitiza kuendelea kuombewa mtoto ili mashetani yamtoke. Uliibuka mzozo kati ya wazazi wawili. Mama yake Joseph yeye alihofu hali itakuwaje iwapo kanisa na majirani zake wakisikia mtoto wake kwa umri alio nao anasoma Kiarabu na anasema yeye ni Muislamu. Ukaka wakati akatishia maisha ya mtoto. Baba, yaani mzee John kuona hali hiyo, kwa kuwa wote hawawezi kuishi na mtoto wao na kumuua lisingekuwa jambo zuri, wakaona bora wamtenge. Joseph alipelekwa kwa binamu yake Maryam, ambaye ni Muislamu aliyeishi Dar es Salaam. Maryam alimpokea mtoto Joseph licha ya kuwa katika mazingira magumu. Baada ya kusikia yale maneno aliyokuwa akiyasema Joseph, alibaini mara moja kuwa ni Quran na Hadithi za Mtume (s.a.w). Hata hivyo naye alishangazwa kwa umri mdogo wa mtoto Joseph wa miaka mitatu kusoma Quran na Hadithi, huku akiwa hajafunzwa na yeyote na anatoka katika familia ya Kikristo. Bi. Maryam alimfuata Marhum Sheikh Hilal Shaweji Kipozeo na Alhad Musa, kuwaelezea jambo hilo. Nao walilipeleka kwa Waislamu. Mwaka 1995 Sheikh Said (Joseph) alianza kuhubiri mihadhara katika misikiti mbalimbali jijini Dar. Alifanya ziara mbalimba za mihadhara mikoani nchini kwa mialiko ya Masheikh. Mwanza, Dodoma, Kagera, Musoma, Tanga, Mtwara, Lind ink. Mwaka 1999 alianza ziara za mihadhara nje ya nchi hususan Malawi, ambako walifanya mihadhara nchi nzima, wilaya na vijiji isipokuwa wilaya ya Nkata Bay. Mihadhara hiyo ilimvuta hadi Rais wa nchi hiyo wakati huo Bw. Bakil Muluzi. Wakazuru Ikulu na kufanya mazungumzo naye na kuomba dua. Mwaka 2000 akafanya ziara ya mwaka mzima nchini Msumbiji. Huko nako walifanya mihadhara mikoa yote. Kama ilivyokuwa Malawi, Rais wa wakati huo wa Msumbiji, Bw. Joachim Chisano, naye alivutiwa na mihadhara ya Sheikh Saidi na kumwalika Ikulu ya Maputo na kufanya naye mazungumzo na kufanya dua. Katika ziara za mihadhara ya Sheikh Saidi John aliyofanya, watu takriban 28,000 waliweza kusilimu. Mwaka 2002 mwishoni
7
ubora wa watu katika kuwahudumia ni wazazi wawili ambao ndio sababu ya kuwepo kwetu baada ya Mwenyezi Mungu basi wao ndio wenye haki sana juu ya huduma hizi muhimu amesema mwenyezi Mungu (na wazazi wawili muwafanyie wema) na neno wema hapa na ukomo na mwisho wa neno na mwisho wa neno katika lugha ya kiaarabu inaleta faidia ya kudumu na kuthibiti na kuendelea. Na vile vile jamaa na watoto umeamrisha Uislamu kuwahudumia kwa wema na kwa ukarimu ulio nzuri amesema Mtume (S.A.W) mbora wenu mbora wenu kwa watu wake na mimi ni mbora wenu kwa watu wangu) na baada ya watu wangu ni watoto jirani umeamrisha Uislamu kuishi nao vizuri na kuacha kuwaudhi na tuwahifadhi na kuwasaidia. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu (na Muabuduni Mwenyezi Mungu na msimshirikishe na kitu chochote na wazazi wawili muwafanyie wema na wale jamaa wa karibu na mayatima na masikini
Makala
AN-NUUR
SHEIKH WAHEED MANSOOR MOHAMED SHUKRANI zote anastahiki Mwenyezi Mungu mola wa viumbe wote na Rehema na Amani zimfikie mbora wa mitume. Ama baada ya utangulizi huu. Kwa hakika Dini ya Kiislamu ndini ya kukamilisha katika mashina yake na matawi imetia nguvu dini juu ya kufafanua kwamba kuhudumiana vizuri ni msingi Mkuu wa Dini hii. Bali imekuja katika Hadithi ya Mtume (S.A.W) (Dini ni kuhudumiana) na kuhudumiana huku lazima kuwe na misingi iliyofafanuliwa nguzo zake ambazo ni:Msamaha uadilifu na upendo. Na kuhudumiana vizuri ni miongoni mwa amri za Dini yetu hii tukufu. Kwa hakika imefahamisha na kubainisha kuwa
katika kuuza na kununua na kukopesha na kudai. Amesema mtume (S.A.W) amemrehemu mola wetu mtu ambaye anapouza husamehe na anaponunua husamehe na anapodai husamehe) na katika mapokezi mengine na anapolipa neno kusamehe lina maana ya kuwa mpole laini na huruma katika kuuza kwake na kununua kwake na kulipa kwake na kudai kwake Deni na mengineyo ni wajibu awe Muislamu mpole kwa watu na usamehevu wa kulipa maana yake ulipe hali ya kuwa roho yako iwe radhi. Tunamuomba Mwenyezi Mungu aturuzuku moyo wa kuhudumia ulio mwema.
TANGAZO
VITABU VIPYA VYA MIHADHARA, MASWALI NA MAJIBU BAINA YA WAHADHIRI WA KIISLAMU NA WACHUNGAJI, PAMOJA NA MAWAIDHA YA SHEIKH NURDIN KISHKI. VINAPATIKANA MSIKITI WA MTORO (DUKANI KWA SAIMU) KARIAKOO. PIA VINAPATIKA KATIKA MADUKA YOTE YA VITABU VYA DINI JIJINI DAR ES SALAAM, KWA JUMLA NA REJAREJA. PATA NAKALA YAKO SASA. 0713 47 10 90, 0685 47 10 90, 0773 19 46 6.
TANGAZO
AN-NUUR
9
Na Omar Msangi YA P O mambo yanachefua japo inakuwa ni uhuru wa kila mtu kukiri, kusema, kutoa maoni na kutenda aonavyo inafaa. Lakini kabla ya kusema zaidi niungane na Watanzania pamoja na wapenda amani wote, kwanza kulani mauaji ya Padri Evarist Mushi na pia kutoa salamu za pole kwa ndugu na jamaa wa karibu wa marehemu Padri Mushi. Pili niseme pia kuwa ni matarajio yangu kwamba vyombo vya dola vitatekeleza wajibu wao kwa umakini, uadilifu na kwa kufuata sheria kuhakikisha kuwa wahusika wanapatikana na kuchukuliwa hatua za kisheria. Nasema kwa umakini kwa sababu zipo kauli zimetolewa na zinazoendelea kutolea ambazo zinatia wasiwasi. Moja ni pale Rais Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete aliposema kuwa ameviagiza vyombo vya dola kushirikiana na mashirika ya upelelezi ya nchi za nje katika kuchunguza mauwaji haya. Kauli hiyo ya Mheshimiwa Rais ikakolezwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mheshimiwa Emmanuel Nchimbi pale aliposema kuwa Kuuliwa Padri Mushi ni tukio la kigaidi na kusisitiza kwamba tayari keshapewa kibali na Rais Kikwete kutumia mashirika ya nchi za nje. Japo si Rais Kikwete wala Waziri Nchimbi aliyefafanua ni nchi gani itaalikwa kufanya uchunguzi, lakini mara tu baada ya kauli ya Rais na Waziri, Ubalozi wa Marekani ukatoa kauli ya kwamba ipo tayari kutoa msaada. Lakini pia ukifuatailia mijadala inayoendelea katika vyombo vya habari, kilicho katika midomo ya watu ni FBI na CIA. Gazeti moja likifurahia ujio wa FBI katika toleo lake la Jumatano Februari 20, 2013 likachekelea likisema: FBI wadaiwa kutua kisiri siri na kuwashikisha adabu wahusika wote. Wana vifaa vya kisasa vya kubaini mtuhumiwa popote.
Makala
AN-NUUR
Rais Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete Kisha gazeti hilo huku likiwa limeweka picha ya askari wa Marekani ukurasa wa mbele, likadai
TAARIFA za awali tulizo nazo zinafahamisha kuwa Al-Jazira Islamic Center, ni Kituo cha Kiislamu kilichopo Ukerewe na kilichosajiliwa na Serikali mwaka 2000 kwa Sheria ya Usajili iliyo chini ya Kabidhi Wazii kikitoa masomo ya Dini ya Kiislamu pamoja na huduma za Kijamii. Baadhi ya huduma za kijamii zilizokwisha kutolewa na taasisi hiyo imeelezwa kuwa ni pamoja na kuchimba visima vya maji sa-Visima 38 wilaya ya Ukerewe na Msoma. Pili, kutoa misaada ya vyakula na nguo na misaada mbali mbali kwa wenyeji bila kujali dini zao. Pia taasisi hiyo imejenga nyumba ya mwalimu na darasa la wanafunzi katika shule ya msingi ya Neduye na kuwachimbia kisima cha maji kwa ajili ya wanafunzi na maeneo jirani. Al Jazeera pia imechimbia kisima katika Shule ya Sekondari ya Nansio na ina mpango wa kujenga Secondari kwa ajili ya wananchi wa Ukerewe. Hiki ndio chuo ambacho hivi sasa baadhi ya magazeti yanadai kuwa ni chuo cha magaidi na kwamba kinaingiza silaha nchini bila ya serikali kujua. Likitoa shutuma hizo gazeti la Mtanzania linasema
Rais wa El Salvador, Mauricio Funes kunukuu kauli ya muumini mmoja wa Parokia ya Minara Miwili akisema: Kwa kweli tumefurahi
kusikia kuna uwezekano wa wapelelezi kutoka nje ya nchi kufika Zanzibar na kufuatilia chanzo cha mauwaji haya. Lakini zaidi ya hivyo, baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vikikoleza agenda ya ugaidi na vingine vikija na kauli kana kwamba imethibiti ugaidi upo nchini na magaidi hao ndio waliomuuwa Padri na magaidi wenyewe ni Uamsho na akina Ponda na wanachosubiri ni kuona FBI na CIA wakiwatia adabu. Nianze kwa kusema kuwa inavoonekana ni kuwa lililokuwa likitakiwa huenda limetimia. Ni aibu na msiba mkubwa. Tusubiri, balaa kubwa
Ama katika jambo la kipuuzi na la kuitukana Idara ya Uhamiaji, Polisi, Usalama wa Taifa, Vyombo vya Dola/ Sheria na Serikali kwa ujumla; ni hili la kuleta hoja kuwa kinaweza kujengwa kituo cha kufunza ugaidi kikafanya kazi kwa zaidi ya miaka 10 huku kikiingiza silaha za kivita nchini, serikali ikiwa haina habari mpaka izinduliwe katika usingizi na aliyejiita Ratifa Baranyikwa wa Mtanzania! Na ili kudramatize, inawekwa ramani kuonyesha ilivyo vigumu kufika Al Jazeera Islamic Centre. Kama vile kusema kuwa magaidi hawa wa Kiislamu wamechagua kuweka chuo chao cha kigaidi kisiwani katika ziwa Victoria mahali ambapo si rahisi Polisi, Uhamiaji na Usalama wa Taifa kuka! Hata hivyo, maadhali wanaotukanwa na kutafutiwa sababu ni Waislamu, wala hutasikia serikali ikisema kitu. Lakini maadhali jambo hili na agenda hii sio jambo la kuihusu Al Jazeera Islamic Center pekee bali Waislamu wote, itakuwa ni jukumu la Waislamu (ikiwemo An nuur), kufuatilia tuhuma na yale yote yaliyosemwa na Ratifa (Latifa?) Baranyikwa ili kujua ukweli. Mhariri
linakuja. Ila wasichojua washenga wa ajali hii ni kuwa balaa linalokuja halitachagua, mwandishi, Muislamu wala Mkristo. Nimesema kuwa ni aibu na msiba mkubwa kwa sababu tukio limetokea kabla hata polisi hawajaanza uchunguzi, serikali inatangaza kuwa haiwezi kufanya kazi hiyo bila ya msaada wa watu wa nje. Inachosema na kukiri serikali hapa ni kuwa waliohusika na mauwaji hayo si wananchi wake. Sina uhakika kwamba kuna serikali yoyote duniani ambayo ina polisi na vyombo vya dola ambavyo havina uwezo wa kuchunguza uhalifu ndani ya nchi yake. Labda Tanzania itakuwa ya kwanza. Kwa hiyo inachotuambia serikali yetu hapa ni kuwa haya si mauwaji ya kihalifu, ni mauwaji ya kupanga. Na kama ni ugaidi kama alivyosema Waziri wetu Nchimbi, basi utakuwa ni ugadi wa kupanga (False Flag Terror Attacks) na ndio maana haraka haraka serikali inatuambia kuwa itawaalika wenye agenda yao ya ugaidi wafanye uchunguzi. Kama ndio hivyo, basi tumemwelewa M h es h imiw a R ais n a Waziri wetu wa Mambo ya Ndani. Na kwa bahati nzuri wenyewe haraka haraka wakatoa kauli za kuleta watu wao utadhani walikuwa wamejiandaa wanasubiri fursa hiyo. Pengine swali linalokuja hapa ni hili, hii haraka ya kualika Watu wa nje inatoka wapi? Huyu anayealikwa, upi wasifu wake? Katika taarifa ya BBC Alhamisi Machi 25, 2010 (na vyombo vingine vya habari vya kimataifa) iliripotiwa kuwa Rais wa El Salvador, Mauricio Funes, ameomba radhi kutokana na mauaji ya Askofu Oscar Romero. Archbishop Romero aliuliwa kwa kupigwa risasi akiongoza misa Machi 24, 1980. I am seeking pardon in the name of the state. The archbishop was a victim of right-wing death squads who unfortunately acted with the protection, collaboration or Inaendelea Uk. 10
10
Inatoka Uk. 9
Makala
RABBIUL THAN 1434, IJUMAA FEBRUARI 22-28, 2013 Waziri Nchimbi wanatarajia kuwa watatua nchini muda si mrefu kutupa msaada wa kipolisi na kikachero! Na baadhi ya magazeti yanangoja kwa hamu ujio huo hata wakaona fahari kuweka picha ya askari wa Marekani katika kurasa za mbele za magazeti yao! Kwa muda mrefu katika nchi hii kumekuwa na jitihada za makusudi za kupandikiza ugaidi ili kutoa nafasi kwa wenye agenda zao wapate fursa ya kusambaza makucha yao ya kikachero na kijeshi. Ukiacha zile porojo za Al Qaida wa Kiburushi waliodaiwa kuingia nchini wakawinda Mikumi na Serengeti na kuondoka na kitoweo kuwapelekea Al Qaida wenzao kule Kandahar bila kuonekana na vyombo vyetu vya usalama (!?), hekaya za Fazul hadi usanii wa mtoto wa shule ya msingi aliyepenya ngome ya ulinzi Ubalozi wa Marekani akiwa na mabomu, sasa tunaletewa ugoro mwingine wa chuo cha Kiislamu Ukerewe kinachodaiwa kuingiza wakufunzi wa ugaidi nchini na silaha za kijeshi bila ya vyombo vya dola kujua. Na sasa ndio wanastuliwa na gazeti moja! Japo haya ni matusi makubwa na kuvidhalilisha vyombo vya dola na serikali yenyewe, lakini maadhali habari hizi zinasaidia kupalilia agenda ya kupandikiza ugaidi wa kupanga nchini kama ilivyopepewa Al Shabab Kenya, wala hutasikia kauli ya serikali kama ambavyo mpaka sasa ipo kimya kuhusu wale Wazungu wanaodaiwa kuwepo katika mhadhara wa kuhamasisha Wakristo kuchinja na kupeleka nyama sokoni kule Buselesele, Geita. Pengine ingekuwa vyema kama kuna watu washaingia mkataba wa kutoa sadaka nchi hii, wawaruhusu tu Wazungu wao waje wachukue madini watakayo, mafuta, gesi, ardhi, TANESCO na kuweka kambi zao za kijeshi. Njia wanayotaka kuchukua italeta maafa makubwa. Na hili si jambo la kufikirika. Hii imedhihirika katika nchi mbalimbali zilizokubali kulazimishwa kuwatafuna Inaendelea Uk. 11
AN-NUUR
participation of state agents. Ilisema taarifa ya BBC ikimnukuu Rais Funes akizindua sanamu ya Askofu Osca Romero katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa El Salvador kama namna ya kumuenzi na kumkumbuka askofu huyo. Alichosema Rais Mauricio Funes ni kuwa anaomba radhi kwa niaba ya serikali kutokana na kuuliwa askofu Oscar Romero kwa sababu askofu huyo aliuliwa na kikosi cha wauaji (death squads) ambao walikuwa wakilindwa na kushirikiana na vikosi vya serikali. Ufupi wa maneno ni kuwa waliomuuwa Askofu Mkuu Oscar Romero walitumwa na serikali. Kwa mujibu wa taarifa ya uchunguzi ya Tume iliyoteuliwa na Umoja wa Mataifa mwaka 1993 ili kutafuta ukweli, mauwaji ya Askofu Mkuu Osca Romero yalitekelezwa na Rightwing death squads? kwa maelekezo na amri ya Roberto DAubuisson, ambaye alikuwa asa wa jeshi la El Salvador. Pengine swali ni je, nani Askofu Romero? Kwa nini aliuliwa? Na ni nani hawa Right-wing death squads? Taarifa ya The New York Times, March 31, 1980, inasema kuwa Archbishop Romero, alikuwa mstari wa mbele kupinga mauwaji na mateso waliyokuwa wakifanyiwa wananchi wa El Salvador, na kutetea haki za binadamu kwa ujumla katika Latin America. Kwa hiyo ukiacha kazi zake za kidini za ki-uaskofu, Askofu Mkuu Oscar Romero alikuwa miongoni mwa wanaharakati wa El Salvador waliopinga ubeberu wa Marekani katika nchi hiyo. Alikuwa mtetezi wa masikini katika nchi hiyo na akiendesha harakati za kupinga uwepo wa makachero na wanajeshi wa Marekani katika El Salvador akisema kuwa wanasaidia askari wa nchi hiyo kuuwa wananchi wasio na hatia. Kwamba kwa msaada wao, Polisi, Jeshi na serikali ya El Salvador, ilikuwa ikiuwa watu wake wasio na hatia. Na kama ni hatia, basi ilikuwa kupinga ubeberu
General David Petraeus mwaka 2005 akinukuliwa na mwandishi Jonathan D. Tepperman (Senior Editor of the main establishment journal, Foreign Affairs of the Council on Foreign Relations) akikiri kuwa katika kulinda maslahi ya Marekani walikuwa wakiwasaidia walioitwa bad guys kuwaangamiza bad guys. Bad guys kwa maana ya watu waovu wa kwanza, ni vikundi vya kigaidi, wauwaji na watesaji. Bad guys wa pili aliowataja ni wale wote waliokuwa wakiendesha harakati za kiraia kupinga unyonyaji na ubeberu wa Marekani: Kwa maneno yake alisema: We did back the guys who went after the bad guys. And [we] dened bad guys pretty broadly. (Angalia: Salvador in Iraq: Flash Back Council on Foreign Relations, by Jonathan D. Tepperman, Senior Editor of Foreign Affairs, 5 April 2005.) Askofu Mkuu Oscar Romero alikuwa bad guy katika kundi la pili. Sasa hao ndio wanaotarajiwa kuwa katika lile kundi la watu walioombwa na serikali yetu watusaidie kumsaka muuwaji wa Padri Evarist Mushi. Hao ndio ambao baadhi ya waandishi na wananchi katika kusherehesha kwao kauli ya Rais Kikwete na
wa Marekani katika nchi hiyo. Ta a r i f a y a B B C niliyonukuu inasema kuwa mnamo Februari 1980, Askofu Mkuu Romero alimtaka Rais wa Marekani wakati huo Jimmy Carter, kuacha kuipa serikali ya El Salvador msaada kwa sababu misaada hiyo inatumiwa na wanajeshi na polisi kuuwa raia. Lakini Carter hakusikiliza kilio hicho na ndipo Machi 24, 1980 akauliwa Askofu Mkuu Romero. Gazeti la The New York Times, la October 22, 1987, Ukurasa wa 11 lina makala iliyoandikwa na Lindsey Gruson, pamoja na mambo mengine, makala hiyo inaarifu kuwa msaada wa Serikali ya Marekani wa kikachero na kipolisi kwa serikali ya El Salvador, umekuwa ukitumika kufundisha polisi watesaji wa raia, vikosi vya wauwaji (death squads) waliokuwa wakiuwa raia na vikosi vya kigaidi vilivyokuwa vikifanya ugaidi wa kupangwa na dola (statesponsored terrorism), ambao yote hayo kwa ujumla yaliisambaratisha El Salvador ikawa kama Jahannamu kwa wananchi wa nchi hiyo katika miaka ya 1980s. Ikiwa na kichwa cha habari Salvador Divided over Aid to Police, makala
hiyo ilisema kuwa The aid package is destructive b e c a u s e i t re w a rd s unrepentent torturers and members of the right-wing death squads. Na kwamba hawa death squads ndio waliohusika kuuwa maelfu ya raia katika miaka ya 1970s na 1980s. Sasa hao ndio rightwing death squads waliomuuwa Askofu Mkuu Oscar Romero kwa vile alikuwa mtetezi wa wanyonge na akipinga ubeberu wa Marekani katika El Salvador. Na kama alivyojisema Holly Burkhalter, wanapoingia watoa misaada ya kipolisi na kikachero, lengo lao kubwa ni kulinda masilahi yao na hufanya hivyo hata kama itabidi kuuwa watu kupitia serikali zao wenyewe. Were getting back in the business of helping governments crack down on their own people. Anasema Holly Burkhalter, ambaye ni mwakilishi wa Americas Wa t c h Wa s h i n g t o n . Burkhalter alikuwa akizungumzia misaada mipya kwa nchi za Latin Amerika akisema kuwa itakachosaidia misaada hiyo ni kuongeza vurugu, mauaji na mateso kwa raia. Naye Lawrence Korb, (Assistant Secretary of Defense from 1981 to 1985)
11
Makala/Tangazo
AN-NUUR
Inatoka Uk. 10
raia wake wenyewe kwa kuwapachika ugaidi. Mauwaji ya Padri Mushi yaliyofuatiwa na hizi kauli za haraka haraka za kutaka msaada wa FBI na CIA, yanaleta wasiwasi mkubwa kwamba huenda kuna jambo limepikwa kuitumbukiza nchi hii katika janga. Na kama wananchi, Waislamu na Wakristo hawatakuwa makini, wakadandia na kubebwa na hizi kauli za wanasiasa na baadhi ya waandishi wa habari, itakuja kuwa balaa. Ukiangalia mgogoro wa kuchinja kule Geita, lile la Uamsho na kutekwa Sheikh Farid na sasa hili
Je umemaliza darasa la saba au kidato cha nne na hujui la kufanya? Kituo cha mafunzo na stadi za kazi Dar es Salaam kinawatangazia OFA MAALUM ya nafasi za MAFUNZO katika kozi zifuatazo:1. Uwalimu wa Chekechea (miezi 9 ada 450,000 tu (F IV)) 2. Matumizi na ufundi wa kompyuta (miezi 4 ada 100,000 (F IV)) 3. Ushonaji na kudarizi (miezi 6 ada 100,000 (STD VII)). Ni muhimu kuwa: watakaosoma ualimu wa chekechea watasomeshwa kiingereza bure na watapelekwa masomo kwa vitendo chini ya usimamizi wa kituo. Wanafunzi watasaidiwa mbinu za kutafuta ajira watakapomaliza. wanafunzi wa Kompyuta kozi watakazosoma ni pamoja na website development, graphic designing, computer maintenance na database management. Kituo kipo Tabata karibu na Chuo cha St. Meries nyuma ya Alfaruk Sekondari School (Africa Muslim Agency) palipokuwa na chuo cha uwalimu SAFINA na Temeke Masjid Tungi. Kujiunga fika ofisi za TAMPRO magomeni au mahali chuo kilipo kuchukua fomu au piga simu 0714151532, 0767151532 au 0718807228 kwa maelezo zaidi. DAR ES SALAAM SDC TUNAKUONGOZA KATIKA MAISHA YAKO
ya Serikali yetu kuita makachero wa nchi raki, Je, tumenogewa na kutamani nasi kushiriki mchezo huu wa Ali Saleh? Alichozawadiwa Abadullah ni kuwa pamoja na kuwa aliuwa sana wananchi wake walioandamana wakitaka demokrasia, hakushutumiwa na Marekani wala kuwekewa mkakati wa kungolewa kama anavyoandamwa hivi sasa Bashar El Assad wa Syria. Je, nasi tuna wasiwasi kuwa huenda huko mbele ya safari tukakabiliwa na nguvu ya umma kama ilivyotokea kwa Ali Saleh? Je, ukaribisho huu wa haraka haraka ndio kujiandalia na kujiwekea akiba ya kulindwa na kukaribishwa White House kama Ali Saleh alivyokaribishwa Washington katika kilele cha umwagaji damu nchini mwake? Kila ambako walitiwa ujinga wakaona kuwa baadhi ya raia na watu wao ni magaidi, hakuna salama. Na balaa la mchezo huu likiingia nchini, hakuna atakaye kuwa salama. Na likiingia, ndio limeingia. Haliondoki kwa urahisi maana wenye agenda yao watataka kitisho kidumu ili kuhalalisha na kujenga hoja ya kuendelea kuwepo. Kwa hiyo itabidi matukio ya kigaidi ya kuuwana yadumishwe. Ndio yanayowakuta Pakistan, Ye m e n , I r a q , S o m a l i a , Afghanistan na Kenya. Kwa hiyo kwa wananchi, kwa Watanzania nasema kuwa kama ni watu wa kujifunza tujifunze kutokana na yale yanayokuwata waliotutangulia katika boti hii inayozama huku waliomo wakitushangaa
the bombs are ours, not yours, alinukuliwa Saleh katika mazungumzo yake na General David Petraeus, ambaye wakati huo alikuwa Kamanda wa Majeshi ya Marekani katika Mashariki ya kati. Katika haraka hii
tunavyojitahidi kuikimbilia kuingia wakati wao wapo katika taharuki wakitaka kujiokoa lakini hawaoni pa kutokea.
12
Kalamu leo nashika, ya kwangu kuyaandika, Moyoni yalochika, na huzuni kuiweka, Leo nataka pasuka, na uwazi kuuweka, Kumi na moja yaka, Ndalichako tahadhari.
AN-NUUR
Kweli mmekithirisha, kwa yale mnayofanya, Waislamu kufelisha, matokeo kudanganya, Shule zenu kupandisha, kwa njia zenu za panya, Kumi na moja yaka, Ndalichako tahadhari. Vijana wajitahidi, kitabu kukomalia, Tena wafanya juhudi, na uzembe kwao doa, Ilikuwa yao budi, tokea kufurahia, Kumi na moja yaka, Ndalichako tahadhari. One zao mwangaza, na four mkazijaza, Ziro mkaziongeza, na two kuzipoteza, Shule zenu zikajaza, kwa one za kuingiza, Kumi na moja yaka, Ndalichako tahadhari. Kichwani yatuzunguka, yale ya mwaka wa jana, Ndugu zetu kuanguka, na vyuo kutoviona, Ziro kwao kuziweka, na one mkazibana, Kumi na moja yaka, Ndalichako tahadhari. Kumi na moja yaka, tarehe iliyopangwa, Ya vijana kujiweka, kwa namba walizopangwa, Darasani kujazika, mtihani kuupiga, Kumi na moja yaka, Ndalichako tahadhari. Vijana wamejipika, vyema wamejiandaa, Peni zao kuzishika, kwa vyuo kuendeleza, Dhuluma msijeweka, one zao kuzitoa, Kumi na moja yaka, Ndalichako tahadhari. Kwa hiyo haina budi, A zao kuziweka, Kwa hii yao juhudi, kwao hazina mashaka, Msijefanya hurudi, kwa f kuzibandika, Kumi na moja yaka, Ndalichako tahadhari. Kalamu nchini naweka, ya kufelishwa, Hakuwa patashika, waislamu kufelishwa, Haki sasa twaitaka, usawa kusimamisha, Kumi na moja yaka, Ndalichako tahadhari. Hussein J.B Gombeye Mwanafunzi Nyasaka Islamic Sec School.
VIWANJA VILIVYOPIMWA KONGOWE KIBAHA TOWNSHIP REGISTERED PLAN No. 70995 BLOCK H
PLOT HATUA ENEO MRABA GHARAMA TSH
50 x 29 32 x 32 50 x 30 37 x 30 50 X 45 33 x 37 60 x 45 50 x 40 67 x 50 70 x 45 90 x 50 59 x 40
1341 Sqm 1136 Sqm 1470 Sqm 1115 Sqm 2259 Sqm 1566 Sqm 2423 Sqm 1984 Sqm 3564 Sqm 2842 Sqm 3780 Sqm 2292 Sqm
4,023,000/= 3408000/= 4410000/= 3345000/= 6750000/= 4695000/= 7269000/= 5952000/= 10692000/= 8526000/= 11340000/= 6876000/=
Vipo Barabara ya Kongowe-Soga Kilomita moja toka barabara ya Morogoro. Simu No.0755 090 754/0715 090 754.
kusimamia serikali ni kubwa. Lakini unaonekana kuingilia uhuru wa mahakama. Umeeleza kwa mujibu wa taarifa zako zilizoandikwa ndani ya gazeti lililotajwa hapo juu, Ponda alihusika na vurugu za Zanzibar, na amehusika kumuua Sheikh katika vurugu za Mombasa nchini Kenya. Na anahusika na kundi la Al- Ashabaab kule nchini Somalia na kwamba, Ponda Issa Ponda si raia halali wa Tanzania. Ni Vema ukaujulisha Ummah wa Watanzania kwani Serikali ina Idara za kiusalama na uhamiaji nchini, zenye majukumu ya kubainisha mambo ya mtu mapema kabla ya mtu kutuhumiwa na mashitaka mengine. Ama suala la vurugu za Mombasa limepita zaidi ya miezi miwili sasa, kwa nini polisi na DPP msubiri kumkamata Ponda kwa mambo ya kiwanja cha Markaz Changombe halafu baada ya miezi mitatu, ndio mnatuletea hoja za mashitaka kama haya? Ponda kahusika vipi kumuua Sheikh wa Mombasa? Ndugu DPP, una taarifa zozote zilizokukia zinazoonyesha kuwa Sheikh Ponda aliwahi kuwa na uhasama na Sheikh mwenzake wa Mombasa? Idara ya Uhamiaji ndio inayotambuwa watu wote wanaoingia ndani ya nchi na kutoka nchini, Bw. Eliazer Feleshi, unazo taarifa ni mara ngapi kasari Ponda kutoka Tanzania kwenda Somalia na kurudi? Ili upatikane uhakika unaothibiti kuueleza umma kuwa ni al-Shabaab? Au uhamiaji wana taarifa juu ya Al Shabab walioingia nchini na kukutana na Ponda? Kama ndio, mbona hawakukamatwa? Au wakati huo Polisi, Uhamiaji, Usalama wa Taifa na serikali kwa ujumla ilikwenda likizo? Kuhusu vurugu Zanzibar, kwa jinsi hali ilivyo na maneno aliyonukuliwa kuyatoa, DPP anaashiria kuwa ni mtu wa Kanisa na anatumia vitengo walivyo navyo kuwachongea Waislamu. Tafuteni waliohusika na vurugu Zanzibar. Acheni kuwasingizia Waislamu na viongozi wao ili kuwakamata, kuwatesa na Inaendelea Uk. 13
13
MAKALA
AN-NUUR
KWELI wanafunzi wengi wanaposhindwa kufaulu m t i h a n i w a Ta i f a , i n a t i a uchungu. Bila shaka uchungu unaopatikana sasa, ni funzo tosha kwa wale wanaopuuza malalamiko yanayotolewa na wenye uchungu wa kufelishwa watoto wao, lakini malalamiko yao yasimguse yeyote. Na hata inapotokea jamii fulani ya watu kudhulumiwa, wanapolalamikia dhulma, huishia kupuuzwa na kukejeliwa. Wakorofi, walalamishi. Hata baada ya shinikizo, ukweli unapobainika, kudaiwa ni makosa ya komputa! Safari hii inaonekana ladha ya uchungu wa kushindwa imewagusa wengi na kilio kimekuwa cha wengi pia. Sote tunafahamu kuwa maisha bila elimu katika ulimwengu wa sasa, ni maisha yasiyokuwa na uhakika. Elimu ndio dira sahihi ya maisha ya kila mtu. Elimu inaweza kulikomboa taifa au kuliangusha taifa. Elimu ndio matumaini si kwa taifa tu, bali hata kwa familia na mtu mmoja mmoja. Elimu ndio urithi pekee wa uhakika ambao mtu anaweza kumwachia mwanaye au ndugu yake, ili iweze kumfaa katika maisha yake ya kila siku. Taifa la watu wasio na elimu, ni taifa linalovutia hatari na lisilokuwa na matumaini wala matarajio mema kwa watu wake. Ni taifa linalosubiri watu wake kugawana umaskini, udhalili na aibu. Wakati wazazi wengi na watoto wao wakigugumia uchungu wa matokeo mabovu ya kidato cha nne, lipo tabaka la wazazi ambao wanachekelea na kufurahia kufaulu vizuri watoto wao. Huwezi kumkuta mtoto wa vigogo wa serikali, Mkurugenzi, Katibu Mkuu wa Wizara, Waziri, Mkuu wa Mkoa, Wilaya, Mbunge au mfanyabiashara tajiri, mwanaye anasoma katika shule za Kata. Shule ambazo hazina walimu, na kama wapo hawana sifa. Shule ambazo hakuna vifaa vya kufundishia, hakuna vitabu, madawati ya kugombania, hakuna maabara. Shule ambazo walimu wanadai mafao serikalini miaka nenda. Wanafundisha wakiwa wamekata tamaa na ajira zao. Wanaingia darasani kutimiza wajibu na kujiondokea kusaka maisha kwenye biashara ndogondogo au kufundisha tuition. Katika mazingira haya, watoto wa wakubwa tangu chekechea hadi kidato cha sita wanasoma shule za binafsi za gharama kubwa. Mtoto anapelekwa na kurudi shule kwa gari. Shule ambazo zina walimu bora wanaolipwa sawia. Zina kila vifaa va kutosha vya kufundishia, mwalimu anafundisha kwa matumaini.
Kabwela hadhubutu kumpeleka mtoto wake huko, kwa kuwa hana ubavu wa kulipa ada ya milioni tano kwa mwaka. Matokeo yake ni kwamba, watoto hao wanaosoma wa St. kwa mamilioni, ndio wanaopata elimu nzuri na kufaulu. Hawa ndio watakaohitimu hadi vyuo vikuu na kuja kuchukua nafasi za wazazi wao. Wale wa Kata ndio wale wanaomaliza darasa la saba hawajui kusoma wala kuandika. Kwa kuwa nafasi za shule za sekondari za kata ni kwa ajili yao, husombwa vivyo hivyo kwenda kidato cha kwanza hadi cha nne na kumaliza na daraja sifuri. Matokeo ya kidato cha nne 2012, yanadhibitisha mazingira haya. Kwa mfano, katika shule ishirini bora zilizotajwa na Waziri wa Elimu Dk. Shukuru Kawambwa, ni shule mbili tu za serikali zilizoingia katika orodha hiyo. Ni Mzumbe sekondari ya Morogoro na Kibaha sekondari ya Pwani. Tena shule zenyewe ni zile ambazo zinafahamika kuwa ni zile za vipaji maalum. Kama si kwa sababu ya kuchukua wanafunzi wenye vipaji maalum, bila shaka shule hizi za serikali nazo zingeangukia pua. Hakuna shule hata moja ya Kata iliyopenya hapa. Zaidi ni kwamba, matokeo haya yameonyesha shule za Kata, wanakosoma makabwela zikitamba kwa kushindwa vibaya. Wanafunzi 240,903 sawa na asilimia 60.6 wamepata daraja 0. Tunatarajia hawa watakwenda wapi. Wanafunzi 103,327 sawa na asilimia 26.02 wamepata daraja la nne. Katika hawa ni wachache sana watakuwa
na alama 27 zinazoweza kuwafanya kwenda vyuo vya ualimu. Waliosalia watakwenda wapi? Baada ya hapo huzagaa mitaani kusaka kazi za vibarua, umachinga, kupiga debe, kuokota chupa za maji nk. Na
baadhi wakiamini kuwa nafasi pekee ya kumudu maisha yao ni kujaribu kuingia kwenye usanii. Baadhi watapotea kabisa kwa kujihusisha na matumizi ya mihadarati na uhalifu. Kwa ujumla watabakia kuwa
tabaka la watawaliwa dhidi ya tabaka la watawala, ambalo wazazi wao ambao ni watawala, walimudu kuwasomesha katika shule hizo bora za gharama kubwa za binafsi na kuhitimu. Wanafunzi waliofaulu ni 23,520 sawa na asilimia 5.16. Bila shaka wengi katika hawa ndio wale wa shule za seminari na nyingine za binafsi za gharama kubwa. Huku kabwela haki. Hili ni daraja la watoto wa vigogo, matajiri. Hali ikiendela hivi, tabaka la hawa litashika hatamu za mamlaka na kuendelea kuneemeka. Wa n a f u n z i w a l i o f a n y a mtihani walikuwa ni 456,137, lakini waliokuwa shuleni ni 397,136 na wa kujitegemea walikuwa 68,806. Labda katika mazingira haya, inawezekana kuwa sababu ya wenye dhamana ya elimu serikalini, ambao ndio wasimamizi wa sekta nzima ya elimu nchini, wamekuwa sio wasikivu na wasiojali wala kuguswa, pale wananchi wanapolalamikia elimu mbovu katika shule za Kata na zile za serikali pamoja na utendaji unaotia mashaka wa Baraza la Mitihani Nchini (NECTA). Tumeona namna ambavyo Mh. Mbatia alivyozodolewa Bungeni. Pamoja na nia yake sa, bado wasioguswa na athari wanazopata makabwela katika elimu wakaizima hoja. Kile walichokitetea dhidi ya hoja za Mh. Mbatia, ni sehemu ya matokeo tuliyoyapata sasa.
14
Makala
AN-NUUR
M AT O K E O y a k i d a t o cha nne yametangazwa na Waziri wa Elimu na Mafunzo vya Ufundi Dr. Shukuru Kawambwa, matokeo hayo yapokelewa kwa hoja na sababu mbali mbali kwa vile idadi ya wanafunzi waliopata divisheni zero ni asilimia sitini ambayo ni kubwa ukilinganisha na miaka yote ya nyuma! Wa s h i k a d a u w e n g i wamechangia mawazo yao na kila aliyechangia amekuwa na mtizamo wake: wengine wamesema Wizara ya Elimu ihamishiwe Ofisi ya Rais; wengine wamesema walimu ni watoro kwa vile hawalipwi vizuri; wengine wamesema walimu hawahusishwi na utaratibu wa kupangwa mitaala; wengine wamesema mitaala ni mibovu; na wengine wamesema Waziri na uongozi wake wote wa juu wajiuzulu! Na mimi kama mdau wa elimu nitakuwa sijawatendea Watanzania wenzangu haki kama mjadala huu utapita bila ya kuchangia maoni yangu. Mimi nina mtizamo tofauti kidogo na wadau wenzangu ambao wamechangia katika tatizo hili la kufeli mitihani kwa wanafunzi wa kidato cha nne: Napenda nianzie mbali na nichambue kila sababu ili tuweze kujua kwa nini tumepata matokeo mabaya; nawaombeni muangalie suala zima la maisha ya kila siku jinsi tunavyoishi hapa nchini, tunaishi katika matabaka: tabaka la watawala na watawaliwa; tabaka la matajiri na masikini; na katika matabaka haya mawili makubwa ni kwamba kila tabaka lina mfumo wake wa elimu kuanzia ngazi ya chekechea hadi kidato cha nne; watawala na matajiri wapo katika tabaka moja; na tabaka lingine ni lile la watawaliwa na masikini nao hawa wapo kwenye tabaka lao, lakini pamoja na kwamba matabaka haya yana mifumo tofauti kuanzia chekechea hadi kidato cha nne, lakini wanafanya mtihani mmoja bila ya kujali kwamba umesomea kwenye mfumo gani! Watoto wa watawala na matajiri wanasoma kwenye shule maalumu ambazo hujulikana kama akademi kuanzia chekechea hadi kidato cha nne, ni shule ambazo zina walimu wazuri wanaojituma kwa vile wanalipwa vizuri na pia wanajitahidi sana kuwafundisha vizuri watoto wa watawala na matajiri ili waendelee kulipwa vizuri. Watoto wa watawaliwa na masikini wanasoma shule za serikali na shule za kata ambazo
Je, pesa hizo zisingeweza kuwalipa walimu mishahara minono wakajituma kikamilifu kama wanavyojituma wenzao wa shule za akademi!? Wa c h a n g i a j i w e n g i wanaangalia tu matokeo ya mitihani lakini hawaangalii chanzo cha kusababisha matokeo hayo; tukianza kumsakama Dr. Kawambwa na uongozi wake wote wa juu kwamba wajiuzulu kwa vile ni chanzo cha tatizo la kufeli kwa wanafunzi tutakuwa hatujatatua tatizo, kwa vile hata wakija akina Profesa Kawambwa wengine hawabadilisha matokeo ya kufeli kwa wanafunzi kwa vile tatizo halipo wizarani! Kama nchi imeshindwa kudhibiti rasimali zake kwa manufaa ya raia wake, kwa kuhakikisha kwamba walimu wanalipwa mishara minono na pia kuhakikisha kwamba shule zote za serikali na zile za akademi zinakuwa na viwango sawa na mfumo mmoja wa elimu ili wanafunzi wapimwe kiuwezo katika mazingira sawa, lakini wanafunzi wamegawanywa katika matabaka mawili: tabaka la wanaopendelewa na kufaidi rasimali za taifa; na tabaka lingine ni lile la wanafunzi wa masikini waliotelekezwa kama vile siyo raia wa nchi hii! Sasa mwanafunzi wa shule ya kata ambaye ametelekezwa na serikali akipata divisheni zero unamlaumu waziri!? Ulitaka waziri atoe pesa yake mfukoni awalipe walimu mishahara minono? Au ulitaka waziri atoe mshahara wake azinunulie shule za kata zote Tanzania nzima vifaa vya maabara? Au ulitaka waziri na uongozi wake wote wa juu waende wakafundishe huko shule za kata ili watoto wafaulu mitihani? Tatizo letu hapa ni mfumo mbovu wa ugawanyaji wa pato la taifa, mfumo ambao umekumbatia hulka za kisadi, hivyo kumlaumu aliyetangaza matokeo ya mtihani tutakuwa hatupo sahihi kabisa! Tatizo ni mfumo wa usadi! Mfumo unaojali wachache na kugandamiza waliowengi. Waziri ni mtu mdogo sana kutatua au kubadilisha mfumo wa nchi, mfumo wa nchi haubadilishwi na waziri, labda kama tunafanya siasa tu ambazo hazina tija kwa taifa. Tunachotakiwa hapa ni kumfanya kila mmoja wetu aelewa kwamba rasimali zote zilizopo hapa nchini ni mali ya Watanzania wote, na kila Mtanzania ana haki sawa na mwingine kuhusu mgawanyo wa rasimali hizo. Tukifanikiwa kulitekeleza hilo, tutakuwa tumetatua tatizo la kuzorota kwa elimu na matatizo mengine mengi yanayozikabili wizara zetu zote na yanayoikabili nchi hii kwa ujumla.
15
TANGAZO
AN-NUUR
1.
KIRINJIKO ISLAMIC SECONDARY SCHOOL NYASAKA ISLAMIC SECONDARY SCHOOL UBUNGO ISLAMIC HIGH SCHOO L
Shule hizi ni za Kiislamu zenye lengo la kuwapa wanafunzi taaluma ya hali ya juu na malezi bora ya Kiislamu kwa gharama nafuu. Shule hizi ni za mchanganyiko wa wavulana na wasichana na zinapokea wanafunzi wa bweni tu. 2. Masomo yanayofundishwa ni Islamic knowledge, Combinations za SAYANSI, ARTS, BIASHARA pamoja na COMPYUTA. 3. Muombaji awe na Crediti 3 au zaidi na angalau D ya Elimu ya Dini ya Kiislamu katika matokeo ya kidato cha nne. Ikiwa ana F au hakufanya Elimu ya Dini ya Kiislamu, basi awe tayari kusoma programu maalum ya Maarifa ya Uislamu atakapokuwa kidato cha tano. 4. Mwisho wa kuchukua na kurudisha fomu ni tarehe 18 /05 /2013 5. Fomu za Maombi zinapatikana kwa gharama ya shilingi 10,000/= katika vituo vilivyoorodheshwa hapa chini. 6. Arusha Kilimanjaro Tanga Mwanza Musoma Kagera Shinyanga Osi ya Islamic Education Panel Jambo Plastic Ghorofa ya 2 mkabala na msikiti Mkuu Bondeni - 0763 282 371/ 0784 406 610 Moshi: Msikiti wa Riadha 0654 723 418 Same: Kirinjiko Islamic Secondry School: 0784 296424/0655 697 075 Uongofu Bookshop: - 0784 982525/ Mandia Shop - Lushoto: 0782257533 Nyasaka Islamic Secondary School 0717 417685/0786 417685 Osi ya Islamic Education Panel - Mwanza - Mtaa wa Ruji mkabala na Msikiti Al-Amin 0785 086 770 Duka la Kansolele -Stendi ya zamani sokoni - 0714587193 Bukoba: Alhuda Caf Kwa mzee Kinobe karibu na osi za TRA. - 0688 479 667 Msiikiti wa Majengo-0718866869 Kahama osi ya AN NUUR Karibu na msikiti wa Ibadhi: 0753 993930 Ubungo Islamic High School 0754 260 241/0712033556 Osi ya Islamic Ed. Panel Temeke -Msikiti wa Nurul Yakin 0655144474 Wasiliana na Ramadhani Chale :0715704380 Hijra Islamic Primary School : 0716 544757/0712 325086 Osis ya Islamic Ed. Panel karibu Nuru snack Hotel 0714285465 Babati: Shule ya Msingi Hangoni: 0784 667575 Msikiti wa mwanga Kigoma: 0753 355224 Kibondo Islamic Nursery School: 0784 442860 Kasulu: Murubona Isl.SS. 0714710802 Wapemba Store: 0784 974041/0786 959663 Amana Islamic S.S 0786 729 973 Kwa Kawanga Karibu na Msikiti wa NURU 0715 681701/0716791113 Mkuzo Islamic High School. 0716 791113 Duka la vifaa vya Kiislamu nje ya Msikiti wa Uyole 0713 200209 Rexona Video mkabala na Mbeya RETICO: 0713 200209 Sumbawanga: Masjid TAQWA 0717082 073 Kituo cha Kiislamu Isevya: 0784 944566 Madrastun Najah: 0714 522 122 Wete: Wete Islamic Education Center: 0777 432331 Madrasatul Fallah: 0777125074Osi ya ust. Yusufu Ally jirani na msikiti mkuu 0653705627
Dar es Salaam Morogoro Dodoma Singida Manyara Kigoma Lindi Mtwara Songea Mbeya Rukwa Tabora Iringa Pemba Unguja Maa -
Pia Fomu zinapatikana kwenye Tovuti: www.ipctz.org. Ikumbukwe kuwa watakaopata fomu kupitia tovuti (download) watatakiwa kuzilipia wakati wa kuzirejesha. USIKOSE NAFASI HII ADHIMU WAHI KUCHUKUA FOMU SASA! Wabillah Tawiq MKURUGENZI
16
AN-NUUR
16
AN-NUUR
Na Bakari Mwakangwale
MASHAHIDI upande wa Mashitaka, katika kesi inayomkabili Sheikh Ponda Issa Ponda, na wenzake wamejikuta wakijichanganya katika kutoa ushahidi wa watuhumiwa hao. Kesi hiyo ambayo wiki hii imesikilizwa kwa siku tatu mfululizo, mbele ya Hakim Mkazi Kisutu, Bi. Victoria Nongwa, Jijini Dar es Salaam, ilishuhudia mashahidi ambao ni maasa wa Polisi wapelelezi wakibabaika kujibu maswali ya jopo la Mawakili wa washitakiwa. Akitoa ushahidi wake kwa upande wa mashitaka Mahakamani hapo, shahidi namba nane, Sajenti Mkombozi (46), wa kituo cha Polisi, Mbagala, alidai kuwa watuhumiwa walikiri kosa la kuchukua vitu vilivyopo katika eneo la kiwanja cha Markazi. Hata hivyo alipoulizwa n a Wa k i l i N a s s o r o , walivipeleka wapi vitu hivyo, Afande Mkombozi alisema kwamba walivitumia kujengea Msikiti katika kiwanja hicho palepale. Sajenti Mkombozi alifafanua kuwa kufanya hivyo ni wizi, kwa maana wizi ni kuhamisha kitu kutoka sehemu kilipokuwa na kukipeleka sehemu nyingine kwa matumizi binafsi. Wa k i l i N a s s o r o akimuhoji shahidi huyo kwa kutumia maelezo ya Ustadh Mukadamu aliyoyatoa akiwa kituo cha Polisi Kikuu cha Polisi (Central Police Station) baada ya kukamatwa, kwamba nini haswa kosa la Mukadam, afande alisema, anatuhumiwa kwa kosa la kuingia kwa jinai (katika kiwanja hicho). Alipoulizwa kama anamfahamu mmiliki wa eneo la kiwanja hicho, afande huyo alijibu kuwa katika upelelezi wake alibaini kuwa mmiliki wa eneo hilo anaitwa Hadhi.
SHEIKH Ponda Issa Ponda (kulia) akiwa na Ustadh Swaleh Mukadam katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam. Kwa upande wake, Sajenti yake kufuatia maswali ya ardhi nyingine iliyopo Juma, kutoka kituo cha Wakili Nassoro, alidai Kisarawe. Lakini pia shahidi Polisi Changombe, akitoa kuwa mmiliki wa eneo la ushahidi wake Mahakamani kiwanja cha Markazi ni mtu huyo alifafanua kuwa h a p o , a k i o n g o z w a n a anayejulikana kwa jina la alibaini kwamba wapo Wakili wa Serikali, Tumaini Bw. Suleimani, na kusisitiza wanaodai kuwa kiwanja Kweka, alisema kuwa kesi kuwa Hafidhi, alikuwa ni hicho ni cha Waislamu na inayowakabili Ponda na mtoa taarifa aliyekuwa Bakwata hawana uwezo wenzake, ilifunguliwa a k i t u m w a n a m w e n y e wa kukigawa, kukiuza au na mlalamikaji Hafidhi, kiwanja (Suleiman). kukifanyia mabadiliko N a a l i p o t a k i w a yoyote. ambaye alilalamika kuwa Kwa maelezo hayo, ameingiliwa kwa jinai kuthibitisha na Wakili wa upande wa utetezi kwamba Wakili Nassoro, alimuuliza katika kiwanja chake. Sajenti Juma, alisema, ni karatasi au nyaraka zipi kuwa kwa maana hiyo w a l i m t a k a H a f i d h i , a m b a y o i n a y o o n y e s h a hapo kuna hoja mbiIi awasilishe nyaraka za uhalali wa Suleimani, kuwa zinazokinzana, baina ya kuthibitisha kuwa kiwanja mmiliki wa eneo hilo, alidai pande mbili kuhusu ardhi kile ni mali yake, jambo kuwa hakumbuki. hiyo, Afande, Juma alikiri Akijibu swali la wakili kuwa pande hizo zipo. ambalo alifanya hivyo Unafikiri Polisi na n a k u j i r i d h i s h a k u w a Nassoro, Sajent Juma, kiwanja ni mali yake alisema kwamba aligundua Mahakama ya Hakimu (Hafidhi), sambamba na katika upelezi wake wa kadhia Mkazi Kisutu wanamamlaka kuthibitishiwa na Afisa ya kiwanja hicho, kuwa kwa mujibu wa sheria Ardhi wa Halmashauri ya Bakwata, hawakuliuza eneo ya kutatua mgogoro wa hilo, bali wamebadilishana ardhi? Alihoji Wakili Manispaa ya Temeke. Hata hivyo katika majibu k w a k u p e w a e n e o l a Nassoro, ambapo Sajenti
Juma, alijibu Hapana Na hata alipoulizwa ni vyombo gani vinavyoshughulikia migogoro ya ardhi, Sajenti Juma, alijibu kuwa ni Mahakama ya Ardhi. Je katika Mahakama hii (Kisutu), inaweza kusema kuwa ni nani mmiliki halali wa eneo lenye mgogoro? Shahidi huyo, alipiga kimya! Wa k i l i N a s s o r o alimuuliza Sajent Juma baada ya kusoma maelezo (waraka) ya Sheikh Ponda, kwamba maelezo hayo yanahusika vipi na kesi inayo wakabili wateja wake, ambapo Asa huyo wa Polisi mpelelezi, alijibu kuwa ni kushawishi watu kuingia sehemu kwa jinai, hiyo alidai ni kwa mujibu wa taarifa za kiitelejensia. Je, katika maelezo ya Sheikh Ponda, uliyoyasoma mbele ya Mahakama, aliyoyatoa Polisi, kuna sehemu inayoonyesha alieleza alihamasisha watu kuvamia eneo hilo? Alihoji wakili Nassoro, na Mpelelezi huyo wa Jeshi la Polisi, alijibu Hapo, hamana. Katika hatua nyingine Mahakamani hapo, Wakili wa upande wa utetezi Nassoro, alidai kuwa karatasi ya maelezo ya mahojiano kati ya Sheikh Mukadam na Polisi, ambayo, ilizua mabishano ya kisheria, katika muda wa kumhoji mtuhumiwa, kisheria, ilighushiwa. Wakili Juma alisema katika karatasi hiyo, awali (asubuhi ya Jumatatu na Jumanne) ilikuwa imeandikwa muda tu yaani 11:15, lakini haikuainisha ni jioni au asubuhi, lakini muda huu (saa saba, mchana, Jumanne) imeongezewa hrs. Mheshiwa Hakimu, kuna kosa limefanywa na wenzetu, kulikuwa na maelezo ya muda iliandikiwa 11:15, haikuwa haifahamiki ni jioni au asubuhi, lakini sasa tumerudi kuna nyongeza ya hrs, mwanzo hayakuwepo sasa hivi yapo, wenzetu wamefoji. Alisema wakili Juma.
Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na Business Printers Limited, S.L.P. 78495 Dar es Salaam.