You are on page 1of 20

facebook: annuurpapers@yahoo.

com

Sauti ya Waislamu

AHLU SUNNA WAL JAMAA HAJJ AND UMRA TRUST


(5) TAJIRIKA KWA KUHIJI!

ISSN 0856 - 3861 Na. 1171 JAMADIUL AKHER 1436, IJUMAA , APRILI 3 - 9, 2015 BEI TShs 800/=, Kshs 50/=

Mtume(saw) amesema, Mahujaji


wanalipwa kwa kila walichokitumia katika
Hija, shilingi moja kwa milioni moja.
Mali ya Muislamu huongezeka anapohiji!
Unapata duniani na unafanikiwa Akhera.
Wahi sasa kuja kulipa uitakase mali yako.
Muda unakwisha! Gharama zote kwa Hijja
ni Dola 4,500. Umra ya Ramadhani ni Dola
2,300. Karibuni Ahlu Sunna Wal Jamaa kwa
huduma nzuri na uongozi bora. Wasiliana
nasi: Tanzania Bara: 0765462022;0782804480;
0717224437.

Zanzibar watishiana Albadiri


Wawakilishi nusura wazipige Barazani
Watambiana ucha Mungu, ubabe wa kisiasa

Siasa za mabeberu
Iraq na Yemen
Mashabiki wa Abu Baghdad mnasimama wapi!
Kama Iraq ni tatizo la Shia kuzuiya Khilafah
Yemen napo Waarabu wanachopigania nini?

Soma Uk. 10

Lipo Jinamizi
PICHANI juu ni siasa za Zanzibar wakijeruhiana wenyewe kwa wenyewe kwa ajili
ya mambo ya kisiasa. Picha chini mitutu ya vifaru vya Saudi Arabia vikielekezwa
Yemen. Nchi zote hizo za Kiarabu.

Tutafute ulipo mzizi wa fitna


Vijana hawa wanakwenda wapi?
Haya yanafanyika bila serikali kujua?

Soma Uk.7

Kwaheri Mahakama ya Kadhi


Ni matokeo ya Kambi ya Maaskofu Dodoma
Alisema kweli Mtwangi. Waislamu wajifunze

Soma Uk. 2

Tahariri
AN-NUUR

S.L.P. 55105, Simu: +022 2400786


Cel: 0784 370 208, 0713 110 148, 0755 260 087 , DSM.
www.annuurpapers.co.tz
E-mail: annuurpapers@yahoo.co.uk
Ofisi zetu zipo: Manzese Tip Top
Usangi House, barabara ya Morogoro, D'Salaam

Kwaheri Mahakama ya Kadhi


Ni matokeo ya Kambi ya Maaskofu Dodoma
Alisema kweli Mtwangi. Waislamu wajifunze

TAMAA ya Waislamu
kwamba siku moja
wanaweza kuwa na
Mahakama yao ya Kadhi
nchini, chombo ambacho
kingekuwa suluhu ya
hitilafu nyingi katika
kutekeleza majukumu
yao ya msingi ya kiibada
na kimaadili, sasa ifikie
kikomo.
Pamoja na kwamba
wapo watu ambao bado
wanadhani kwamba
masu al a au matatizo
ya Waislamu yanaweza
k u t a t u l i wa n d a n i ya
mfumo wa sasa wa serikali
yetu na vyombo vyake
vya kimamlaka, lakini
ukweli ni kwamba historia
inadhihirisha kwamba
katu haiwezekani jamii
ya Waislamu kutimiziwa
au kukubaliwa haja zao za
kiimani ndani ya himaya
ya watu waliofura chuki,
ambao wengi wao ndio
waliopo katika nafasi nyeti
za maamuzi.
Mwandishi mashuhuri
wa makala, Mzee wetu
Bw. Shaaban Khalid
Mtwangi, siku za nyuma
aliwahi kuandika makala
yake kuhusu Mahakama
ya Kadhi katika gazeti hili,
akisema katu haiwezekani
M a h a k a m a ya K a d h i
ikaanzishwa nchini kwa
k u wa , i l i M a h a k a m a
hiyo iweze kupata
uhalali wa kuanzishwa
na kutambuliwa na
sheria ya nchi (katiba), ni
lazima kwanza muswada
wa kuanzishwa kwake
upelekwe Bungeni na
kuridhiwa na wabunge
walio wengi.
Kwa msingi huo, Bw.
Mtwangi alisema kwa
namna ambavyo sura
ya Bunge letu ilivyo,
akimaanisha kujaa
wabunge wengi wa
imani ya Kikristo, na kwa
kuzingatia ukweli kwamba
kuna chuki kubwa ya
kiimani iliyojificha ndani
ya mioyo yao, kamwe
hawawezi kukubali
kuupitisha muswada huo
hata utakapofikishwa
mbele yao.
Mzee Mtwangi
alihitimisha kwa kusema,
Waislamu wanapoteza
muda wao kudai
mahakama hiyo ndani
ya mfuno wa sasa wa
kimamlaka na kidola

n a a k a o n a Wa i s l a m u
kuendelea kupambana
katika mazingira haya
kudumu katika matumaini
kuwa watakubaliwa kuwa
na chombo chao hicho
kikatiba, ni kupoteza muda
na nguvu za kufanya
m a m b o m e n g i n e k wa
maslahi ya Waislamu.
Yeye alishauri kwamba
kwanza uwepo mkakati
wa kuhakikisha kwamba
jamii ya Waislamu, nao
wanakuwepo kwa namba
inayoridhisha katika
vyombo vya kidola
na kimamlaka hasa
Bunge. Hapo wanaweza
kupambana uso kwa uso
kusimamia heshima na
maslahi yao ya kiibada.
Tukitizama kwa kina
alichokuwa akikieleza
M z e e M t wa n g i n d a n i
ya makala yake hiyo,
utagundua kwamba suala
la kuanzisha Mahakama
ya Kadhi nchini, ni mchezo
wa kisiasa na hadaa tupu
dhidi ya jamii ya Kiislamu
nchini lakini ukweli
wake ni kwamba haiwezi
kukubaliwa iwepo.
Suala hili limekuwa
likipigiwa kelele kwa
muda mrefu, limewahi
hata kuingizwa katika Ilani
ya CCM ya mwaka 2005.
Waziri Mkuu Mizengo
Kayanza Pinda, ambaye
ndiye hasa aliyepewa
jukumu la kusimamia
mchakato wa kuanzishwa
mahakama hii kwa upande
wa serikali, pamoja na
kujaribu kuanzisha
mchakato huo kwa kuunda
K a m a t i ya Pa m o j a ya
Viongozi wa Jumuia za
Kiislamu na serikali, bado
yalifanyika madudu kwa
kuanzisha Mahakama ya
Kadhi ya Bakwata kule
Dodoma.
Makadhi ambao
hawafahamiki kisheria
(kikatiba), ambao
walipatikana bila utaratibu
wa Kiislamu na kibaya
zaidi, yote hayo yalifanyika
bila kuwepo mawasiliano
na Kamati ya Pamoja
iliyojumuisha serikali chini
ya Waziri Mkuu, ambayo
kimsingi ndicho chombo
halali kichokubalika na
Wa i s l a m u n a s e r i k a l i
kushughulikia suala hilo
kiutaratibu.
Tu n a a m i n i k wa m b a
hadaa hii dhidi ya Waislamu

ilifanyika huku kwa namna


moja au nyingine serikali
ikihusika chini ya mwavuli
wa Makamu wa Kwanza
wa Rais.
Baadae likaja zoezi la
mchakato wa kuwa na
Katiba mpya. Waislamu
wakaona hiyo ndiyo njia
muafaka ya kuwasilisha
hoja yao ya kurejeshwa
Mahakama ya Kadhi nchini
kikatiba.
Sote tulishuhudia
namna ambavyo Tume ya
kukusanya maoni ya Katiba
Mpya chini ya Jaji Joseph
Warioba, ilivyotupilia kwa
mbali maoni ya Waislamu
juu ya kuhitaji mahakama
hiyo, ambayo yameelezewa
katika rasimu ya maoni ya
wananchi Uk. 203 hadi 206,
ambapo imeelezwa kwa
upana namna wananchi
walivyotoa maoni yao
kuhusu uanzishwaji wa
Mahakama ya Kadhi.
S e r i k a l i k wa k u o n a
hadaa imekithiri, ikaamua
kufanya mjadala kati ya
Kamati ya Viongozi wa
Kiislamu na wajumbe wa
Kamati ya Bunge, kuona
namna gani wanaweza
kukidhi vigezo vya
kuuwasilisha muswada
wa kuingizwa kipengele
cha Mahakama ya Kadhi
katika Katiba Pendekezwa.
Tuliona zoezi likifanyika
kwa mvutano mkubwa
huku Maaskofu na Mapadri
wakija juu kupinga hatua
hiyo kiasi cha kutoa
Matamko kupitia jumuia
zao. Baadhi ya Wakristo
walipinga sana kukataa
hatua hiyo. Hata hivyo
serikali kupitia Waziri
Mkuu Pinda, iliendelea
kusisitiza kuwasilisha
Bungeni mswada huo
licha ya kuwepo kauli
za kuukataa kutoka kwa
viongozi wa Kikristo,
baadhi ya Wabunge na
watu wengi wasiokuwa
Waislamu.
Baadae tukashuhudia
Maaskofu kutoka mikoa
mbalimbali ya Tanzania
wakipiga kambi kwa zaidi
ya wiki mjini Dodoma,
kuhakikisha muswada
huo hauingii Bungeni.
Tu n a a mb iwa z a id i ya
Maaskofu 4O kutoka mikoa
yote nchini, walikutana na
wabunge katika ukumbi
wa Kanisa La Kiinjili la
Kilutheli (KKKT) mjini
Dodoma kujadiliana suala
la muswada wa Mahakama
ya Kadhi. Katika mkutano
huo Maaskofu walitoa
azimio kuwa muswada
huo usiwasilishwe Bungeni
kwa kuwa kufanya hivyo
inaweza kuhatarisha
amani iliyoko nchini.
Maaskofu hao wanaounda
Jukwaa la Kikristo
Tanzania, waliwasili mjini
Dodoma tangu mwishoni
mwa wiki iliyopita
kuhakikisha wakiazimia
kuwa wanafanya lobbing
kwa wabunge Wakristo,
kuhakikisha muswada
huo uliokusudiwa
kuwasilishwa bungeni,

AN-NUUR

JAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 3-9, 2015


haufaulu.
Sote tumeshuhudia,
wabunge karibu wote wa
Kikristo kwa umoja wao,
kila ilipojitokeza hoja juu ya
muswada huo, walipinga
vikali kiasi cha kusababisha
Bunge kuvurugika licha
ya Wabunge wachache
Wa i s l a m u k u j a r i b u
kushinikiza kuingizwa
muswada huo Bungeni
hapo.
Hatimaye wiki hii Kambi
yao ilifanya kazi yake.
Wamefanikiwa kuifanya
Serikali ishindwe kuingiza
muswada bungeni. Suala
la Mahakama ya Kadhi,
ambalo lilizua mjadala
mkali kwenye Kamati za
Bunge la Bunge Maalumu la
Katiba, likaundiwa Kamati
N d o g o i l i y o o n g o z wa
na aliyekuwa Makamu
Mwenyekiti wa Bunge hilo,
Samia Suluhu Hasan, hoja
ikaishia kuondolewa.
Waziri Mkuu kutaka
muswada uingizwe
tena Bungeni ili uweze
kuingia katika Katiba
Pendekezwa, Lobbing
imefanya kazi yake,
zimezuka hoja za chuki
na hatimaye muswada
umekwama na haujulikani
utapelekwa tena au la,
n a lini . Tuna c ho we z a
kusema ni kama umezikwa
rasmi. Kambi ya Maaskofu
imefanya kazi yake na
imekamilika. Hakuna tena
muswada wa Mahakama
ya Kadhi.
Katibu wa Bunge Thomas
Kashilila, ameshasema
k u wa m u s wa a d a h u o
hautakuwepo kwenye
ratiba za Bunge, badala
yake nafasi hiyo
itachukuliwa na miswaada
mingine kujadiliwa.
Serikali inasema imeamua
kuuondoa kutokana na
hofu ya kutokea mpasuko
nchini.
Dk. Kashilila alisema
haijulikani ni lini
utawasilishwa bungeni
kwa sababu Mkutano wa
Bunge ujao unaotarajia
kufanyika Mei, utakuwa
mahsusi kwa ajili ya bajeti.
Waziri
Mkuu
alivyosema wataangalia
na kushauriana kimsingi,
alitoa maneno ya busara
tu au ilikuwa kauli ya
mtu mzima, lakini huu
muswada hautakuwapo,
alinukuliwa akisema.
Naibu Spika, Job Ndugai,
yeye amenukuliwa akisema
muswada huo hauwezi
kuletwa bungeni kutokana
na hali ilivyo. Bila shaka
hali yenyewe ni kutokana
na upinzani wa Wakristo.
H ii ni m a r a ya p i l i
tunashuhudia muswada
wa Mahakama ya Kadhi
ukiondolewa Bungeni
katika dakika za majeruhi
kutokana na upinzani
kutoka kwa baadhi ya
wabunge na Maaskofu.
Tunakumbuka kuwa

Februari mwaka huu,


muswada huo pia
uliondolewa Bungeni kwa
kile Mwanasheria Mkuu
wa Serikali alichokiita,
kwamba ni kwenda
kuonana na viongozi wa
dini kuwaelemisha juu
ya mahakama hiyo, ili
uwasilishwe tena kwenye
mkutano uliomalizika wiki
hii.
Itoshe sasa kupata funzo
kwamba, suala lolote la
Waislamu, ambalo kwa
namna moja au nyingine
litakuwa na muingiliano
na serikali, haliwezi
kukubaliwa kama litapata
pingamizi la Kanisa.
Bado tuna kumbukumbu
ya uwezekano wa Tanzania
kujiunga na Jumuia ya
k i u c h u m i ya n c h i z a
Kiislamu (OIC), ambapo
Waziri wa Mambo ya Nje
Bernad Membe alishaeleza
Bungeni kwamba halina
tatizo wala athari mbaya
kwa nchi.
Hata hivyo siku chache
baadae aliitwa na Kardinal
Polycarp Pengo na baada
ya h a p o a l i u f ya t a n a
ikaonekana kufanya hivyo
ni tatizo. Pia tunakumbuka
wakati serikali ilipotangaza
Bungeni kwamba
imeondoa misamaha ya
kodi kwa taasisi za kidini,
kwa kuwa misamaha hiyo
imekuwa ikitumika vibaya.
Maana yake ilikuwa
ni kwamba misamaha
hiyo ilikuwa ikitumiwa na
wafanyabishara kukwepa
kodi. Lakini pia taasisi za
dini pamoja na kwamba
zinasamehewa kodi katika
kuingiza bidhaa za huduma
kwa jamii, lakini huduma
hiyo imeendelea kutolewa
kwa malipo makubwa sawa
na huduma zinazotolewa
na taasisi binafsi, mfano
mzuri ukiwa ni hospitalini,
shule na vyuo.
Hapo napo Maaskofu
walikuja juu na kupinga
hatua hiyo ya serikali.
Kama kawaida, kwa nguvu
waliyo nayo, mara moja
serikali ilirejesha msamaha
huo.
Tunachoweza kusema ni
kwamba, wenye kutafakari
vizuri, sasa hakuna
kilichosalia kubaini hadaa
iliyodumu kwa muda sasa.
Sasa Waislamu nchini
washughulishwe na
m a m b o ya o m e n g i n e
katika Uislamu, lakini
ni hakika kwamba wale
wanaoendelea kusubiri
kuona Mahakama ya
Kadhi hapa nchini,
ni ndoto za mchana.
Vinginevyo, labda tusubiri
hadi hapo Masheikh wetu
nao watakapokuwa na
nguvu na thamani mbele
ya dola kama walivyo
Maaskofu, kiasi kwamba
wataweza nao kusimamia
hoja zao mbele ya serikali
na wakasikilizwa.

3
Na Salma Alghaythiyah
H A L I i n a z i d i k u wa
tete Zanzibar ambapo
sasa watu wanatishiana
kusomeana Albadiri.
Hayo yalijiri katika
kikao cha Baraza la
Wa wa k i l i s h i a m b a p o
ilipelekwa hoja binafsi juu
ya baadhi ya Wazanzibari
kunyimwa vitambulisho
vya Ukaazi.
Alikuwa Mjumbe
mmoja baada ya kuona
wenzake wa CCM
wanakuja juu kupinga
hoja madai ya baadhi
ya wanachama wa CUF
kunyimwa vitambulisho
aliposema kuwa
anakusudia kuita watoto
wa m a d r a s a k u s o m a
Albadiri kuwashitaki
CCM kwa Mungu.
Hiyo ilikuwa baada
ya k u t o k e a m v u t a n o
mkali ndani ya
Baraza la Wawakilishi
kuhusiana na hoja binafsi
iliyowasilishwa na
Mwakilishi wa Ole (CUF)
Hamad Masoud Hamad
ya kuitaka serikali ichukue
hatua za kuhakikisha
Wa z a n z i b a r i a m b a o
hawana vitambulisho vya
Mzanzibari na wana sifa,
wapewe vitambulisho
kabla ya uchaguzi mkuu.
Mvutano huo ulianza
baada ya Mwakilishi wa
Jimbo la Kwahani Hamza
Hassan Juma (CCM)
kuuchana waraka wa
hoja hiyo iliyowasilishwa
na wapinzani ambapo
baadhi ya Wawakilishi
walikasirishwa na
kitendo hicho na kuanza
kusimama na kutaka
kupigana kutokana na
kitendo cha Mwakilishi
huyo.
Kufuatia taharuki
hiyo, Spika wa Baraza
hilo Pandu Ameir Kificho,
alilazimika kusitisha
shughuli za Baraza kwa
muda wa zaidi ya saa moja
na baada kurudi tena,
hakukuwa na maafikiano
ambapo kila upande
ukivutia upande wake
wa p i n z a n i wa k i s e m a
wanadhulumiwa
huku upande wa CCM
wakisema sheria zipo
wazi wenye kutaka
vitambulisho wafuate
sheria.
Kabla ya kuahirishwa
kwa kikao hicho, mjumbe
wa Baraza hilo kutoka
CCM , Issa Haji Gavu
ambae pia ni Naibu
Wizara wa Miundombinu

Habari

AN-NUUR

JAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 3-9, 2015

Wawakilishi Zanzibar
watishiana Albadiri
na Mawasiliano na
Mjumbe wa Baraza hilo
kutoka CUF Hassan
Hamad kutaka kupigana
katika kikao hicho na
kurushiana maneno ya
jazba na kudharauliana.
Wakati Gavu akitaka
kushikana shati na Hassan
huku Hamza aliyechana
waraka huo alishikana
kwa maneno makali na
Mnadhimu na Baraza hilo
kwa upande wa upinzani
Abdallah Juma Abdallah.
Baada ya nusu saa,
suluhu iliweza kupatikana
na wajumbe wote wa
Baraza hilo kurejea na
Spika kuendeleza kikao
huku Spika akisema
kuwa hajafurahishwa
hata kidogo kutokana
na kitendo kilichotokea
katika Baraza hilo.
Kitendo hiki kwa kweli
hakikuwa cha kupendeza
na kimeleta taswira
mbaya kwa wananchi
wanaotuangalia, alisema
Kificho.
Aidha Kificho aliwataka
wajumbe wa baraza hilo
kuwa na uvumilivu
wa kisiasa, kuacha
kutukanana na kutoleana
maneno ya kashfa, kwani
wana dhamana kubwa
kwa wananchi.
Chanzo cha ugomvi
na malumbano hayo ni
pale wajumbe wa Baraza
hilo wakati wakichangia
hoja hiyo kwa jazba na
baadhi yao kuchangia
michango hiyo kutoka nje
ya mada ambapo baadhi
yao walionekana kukerwa
na dhulma inayoendelea
k wa k u n y i m wa wa t u
vitambulisho huku
baadhi yao wakiwapeleka
viongozi kuwashitaki
mbele ya Allah.
Bi Ashura Sharif Ali
kutoka nafasi za wanawake
(CUF)aliwataka viongozi
kuziheshimu nafasi
zao na kujua kwamba
wana dhamana kubwa
waliopewa na Allah na
ipo siku watarudi kwa
Mwen ye enzi Mung u
na wanayoyatenda yote
wataulizwa.

N a p e n d a
kuwakumbusha kwamba
hapa duniani tumekuja
kuishi kama wapita njia
tu, bado kuna maisha
mengine ya milele, sasa
viongozi mnaopewa
hizi dhamana mjue haya
mnayoyatenda mtakuja
kuulizwa na kuhukumiwa
mbele ya Allah, alisema
kwa uchungu Bi Ashura.
Akichangia hoja hiyo Bi
Kadija Khamis Kona wa
(CUF) alisema kwa kuwa
hatua zote wameshapitia
za kuomba vitambulisho
hivyo lakini mamlaka
zinazohusika zinafanya
kusudi kuwakatalia, basi
anasubiri kumaliza vikao
vya Baraza arudi nyumbani
kwake na kuitisha kisomo
cha watoto wa chuoni
kumshitakia Mwenyeenzi
Mungu juu ya dhulma
hiyo.
Nitawakusanya
watoto wa chuoni tusome
halalbadri kwa sababu
anayepaswa kuombwa
na kutegemewa ni yeye
Mwenyeenzi Mungu tu,
alisema Mwakilishi huyo.
Wa k i c h a n g i a h o j a
hiyo, baadhi ya wajumbe
walisema Mwenyeenzi
Mungu ni wa watu wote
na baadhi yao walionesha
kubeza visomo hivyo
kuwa hata wao wanaweza
kusoma kwa kuwa ni
miongoni mwa wacha
Mungu.
Mwakilishi wa Viti
Maalum (CCM), Wanu
Hafidh Ameri alisema
hao wenye kumuelekea
Mwenye enzi Mungu, pia
nao wana mabaya yao na
hawezi kuiunga mkono
hoja hiyo kwa sababu
Baraza la Wawakilishi
halina uwezo wa kuangalia
utaratibu wa kisheria ila
Baraza kufuata utaratibu
wa kisheria na sio kutoa
maamuzi na masharti
ya kupata vitambulisho
kwani suala la kupata
vitambulisho hivyo lipo
kisheria.
Alisema, suala la
kupata kitambulisho cha
Mzanzibari Mkaazi, ni haki
ya kikatiba na masharti

ya kupata kitambulisho
hicho yameeleza vizuri
katika ibara ya sita ya
katiba ya Zanzibar na
ibara hiyo inaeleza
kama mtu hajaridhika
katika upatikanaji wa
vitambulisho hivyo
kwenda Mahakama Kuu
na sio katika Baraza la
Wawakilishi.
Aliyewasilisha hoja hii
kama anahisi wanaotoa
vitambulisho hivi kuwa
hawawajibiki na haki
haitendeki, basi aende
mahakamani na hakuna
haja ya kuishurutisha
serikali, alisema Wanu.
Alimtaka mjumbe huyo
aliewasilisha hoja hiyo ni
vyema kuwashajihisha
wananchi kufuata
utaratibu wa upatikanaji
wa vitambulisho hivyo ili
kuweza kupatia haki hiyo.
Mohammed Aboud
Mohammed ni Waziri wa
Nchi Ofisi ya Makamo wa
Pili wa Rais, aliwaomba
Wawakilishi wasifikishane
kwa Mungu kwa kuwa
mambo ya kupatikana
vitambulisho yana taratibu
zake na kuwataka wajumbe
wafuate taratibu, kauli
ambayo ilidharauliwa na
wapinzani kwa kuwa suala
hilo serikali imeshindwa
kulisimamia huku ofisi
yake ikishutumiwa kutoa
muongozo kwa masheha
wasitoe vitambulisho.
Mwakilishi wa Jimbo
Micheweni (CUF) Subeti
Khamis Faki Abdallah
Hamad ameunga mkono
h oja hi yo na k ui t a k a
serikali kuwachukulia
hatua za kisheria
wahusika wa utoaji wa
vitambulisho hivyo ambao
wanawanyima haki yao
hiyo baadhi ya wananchi
kwa sababu zisizo na
msingi.
Alisema, suala la
kuwanyima wananchi
vitambulisho hivyo
ni mtaji wa chama cha
mapinduzi na suala hilo
limeingizwa kisiasa zaidi.
Alisema suala
h i l o l a k u wa k o s e s h a
vitambulisho wananchi
ni njama ya CCM kuweza

k u n g a n g a n i a k u k a a
madarakani na kuweza
kupata ushindi katika
uchaguzi mkuu kwa kuwa
asie na kitambulisho hicho
hatoweza kupiga kura.
Aidha, Wawakilishi
wa C U F wa l i wa t u p i a
l a wa m a m a s h e h a wa
shehia (viongozi wa mitaa)
kutokana na kuwanyima
b a a d h i ya wa n a n c h i
vitambulisho hivyo kwa
makusudi kutokana na
itikadi za kisiasa.
Mwakilishi wa
viti maalum Salma
Mohammed Ali alisema
masheha wamepewa agizo
maalum la kuwakosesha
wananchi vitambulisho
hasa wale wenye msimamo
tofauti na Chama Cha
Mapinduzi ambapo
alisema hana imani na
Masheha kwa kuwa wao
ndio chanzo cha wananchi
kunyimwa haki zao.
Awali akizungumzia
suala hilo Waziri wa Sheria
na Katiba, Abubakar
Khamis Bakari alisema
sio kwamba wananchi
hawawezi kwenda
mahakamani, lakini tatizo
liliopo wananchi hawawezi
kufika mahakamani
kutokana na vikwazo
vingi wanavyowekewa na
suala la kuambiwa sheria
inasema hivi ni mambo
ya k u h a n g a i s h wa t u
wananchi.
Waziri wa Nchi ofisi
ya Rais, Idara Maalum,
Ta wa l a z a M i k o a n a
Vikosi vya SMZ, Haji
Omar Kheir amekanusha
kauli za baadhi ya
wajumbe wa Baraza la
Wa wa k l i s h i wa l i o d a i
kuwa vitambullisho
vya Mzanzibari Mkaazi
vinatolewa kwa sababu
ya siasa.
Huku akijisifu kuwa
yeye pia ni mcha Mungu
na amekuwa akitoa sadaka
n a z a k a k i l a m wa k a
pamoja na kwenda Hijja
ambapo alisema mwaka
huu anatarajia kwenda
tena kuhiji na umra kwake
yeye ni jambo la kawaida.
Kheri alisema
vitambulisho hivyo
vinatolewa kwa mujibu wa
sheria na kama wajumbe
hao wanaona kuwa sheria
hiyo ina mapungufu, basi
waifanyie marekebisho.
Waziri huyo alisema
kama kuna mtu
ananyimwa haki hiyo
ya kupata vitambulisho,
afuate taratibu za kisheria
ili kuweza kupata haki
yake hiyo.

4
Na Khalid Gwiji

KUNA methali isemayo


"mwanzo wa moto ni
cheche" ikimaanisha
kuwa ubaya mkubwa
h u a n z a k wa u b a ya
mdogo na kwamba fujo
aghlabu huanza kwa
uchokozi. Bila ya shaka
shabaha ya methali hii
ni kututahadharisha
tusidharau matatizo
madogo kwani
yakijilimbikiza
ya t a k u wa ru n d o la
matatizo na ndio
huweza kusababisha
balaa, maafa au janga
la jamii.
Watu wenye akili na
hisia za utu watalaani
kwa nguvu zote
uharamia uliofanyika
k we n ye m a e n e o ya
Fuoni Jitimai na Sheli
Maili Tano Zanzibar wa
kuvamiwa wafuasi wa
Chama cha Wananchi
- CUF na kuwajeruhi
vibaya. Kitendo hiki
kwa mazingira yake
n a k u t o k e a k wa k e ,
kinaashiria nia mbaya
waliokuwa nayo watu
wasioitakia mema
Zanzibar. Bila ya shaka
yo yote watendaji wa
kitendo hiki kiovu ni
watu wasiokuwa na
uchungu na Zanzibar
wala kufuata silka na
maadili yake.
M a t u k i o h a ya n a
mfano wake yanalenga
kuturudisha enzi zile
za siasa za chuki, fujo,
uhasama na mifarakano
ambazo tulishaapa
kuachana nazo
kupitia Maridhiano na
Serikali ya Umoja wa
Kitaifa (SUK) ambazo
zilijengeka juu ya misingi
ya kuaminiana na nia
njema miongononi mwa
viongozi na Wananchi.
Tu n a e l e w a k u w a
pamoja na sababu
kadhaa za kuzuka kwa
matukio haya, sababu
kubwa moja wapo ni
kuwepo kwa wanasiasa
U C H WA R A a m b a o
HAWAUZIKI tena katika
siasa za hoja na badala
yake wanajidanganya
kwa kuwekeza kwenye
vurugu za kuwahujumu
wanachama wa Chama
cha Wananchi - CUF,
kuchoma moto ofisi
za Chama, kupachua
bendera nk ambapo
kwao wao hayo
ndio mtaji. Hawa ni
wanasiasa waliozoea
kupata umaarufu
kwa njia za vurugu,
uhasama na mifarakano.
Wamekuwa ni sawa na
baadhi ya 'WAGANGA
WA KIENYEJI' ambao

Makala

AN-NUUR

JAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 3-9, 2015

Mnaotaka nuru ya maridhiano ififie


hamuitakii mema Zanzibar yetu !

wa Zanzibar na wa
Wa z a n z i b a r i k w a
k u t u m i k a k wa n j i a
y o y o t e i n a y o we z a
kuhujumu mshikamano,
umoja, mapenzi,
udugu na uvumilivu
baina yetu, uliojengeka
tokea kuasisiwa kwa

KATIBU Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad (kushoto) akimjulia hali mmoja wa majeruhi
aliyeshambulia katika mkutano wa Chama hicho Unguja hivi karibuni.
wanaamini kuwa bila
ya migogoro - hawana
biashara.
N i
b u s a r a
tukakumbuka na
kuzingatia eneo la
mafanikio la Serikali ya
Umoja wa Kitaifa na kwa
pamoja tukaiendeleza
kutokana na ukweli
kwamba imekuwa na
maslahi mapana kwa
wote na ni vile vile ni
muakilishi na mtetezi
wa makundi yote.
Serikali ya Umoja
wa Kitaifa kimsingi
n i n ye n z o m u h i m u
sana katika ujenzi
wa Zanzibar mpya.
Imekuja kuzika siasa
za chuki, uhasama,
vurugu zilizolenga
kufukua makaburi
na visasi na badala
yake kuleta mfumo
mpya wa mahusiano
mema miongoni mwa
Wananchi, viongozi
na Serikali yao kwa
kuyawekea maua
makaburi. Serikali hii ya
pamoja ina eneo kubwa
la Mafanikio ambayo
ni pamoja na: Kwanza,
imeleta mshikamano
miongoni mwa
wananchi kwa kuzizika
siasa za chuki na
uhasama. Pili, ilianzisha
u s t a a r a b u m p ya n a
wenye ukomavu
wa kisiasa katika
uendeshaji wa siasa za
vyama. Matumizi ya

lugha, kauli mbiu, sanaa


(nyimbo na ngoma)
hazikuwa za vijembe
kama ilivyokuwa huko
nyuma. Tatu, imerudisha
imani ya wananchi kwa
serikali yao baada ya
wananchi kujiona na
kuamini kuwa serikali
hii imetokana na
wao kufuatia kura ya
maoni (referendum)
waliyoipiga kuunga
mkono mfumo huu
wa serikali ya pamoja jambo ambalo limeipa
uhalali serikali hii.
Nne, imesaidia katika
upatikanaji wa huduma
( a f ya n a e l i m u ) n a
ustawi wa jamii (haki za
wataafu na wazee) katika
misingi ya usawa. Kwa
kiwango kizuri, haki
imekuwa ikipatikana
kwa kustahiki na sio
kwa kutizamwa we ni
nani.
Ta n o , i m e s a i d i a
Zanzibar na Wazanzibari
kufikiria nje ya chaguzi
(beyond elections).
Kwa muda mrefu,
chaguzi zimekuwa ni
chombo cha kuwagawa
Wa z a n z i b a r i . S U K
imesaidia kuonesha
kuwa chaguzi si lengo,
bali ni nyenzo kuelekea
lengo kuu ambalo ni
maisha mema, ustawi na
maslahi mapana na ya
pamoja miongoni mwa
wananchi.
Sita, SUK imesaidia

kuendeleza na
kusimamia amani na
utulivu. Saba, SUK
imesaidia kuengeza
wigo wa uvumilivu
wa kisiasa. Nane,
GNU ilisaidia serikali
kutotumia nguvu ya dola
dhidi ya wananchi kama
ambavyo pia ilisaidia
wananchi kutotumia
nguvu ya umma dhidi
ya serikali. Ilijaribu kuja
katika mrengo wa kati na
kati wa mazungumzo.
Muhimu zaidi, Serikali
ya Umoja wa Kitaifa
inahitaji kuendelezwa
kwa vile hatujawa na
demokrasia tulivu
(stable democracy)
ye n ye k u a m i n i j u u
ya m m o j a a t o k e n a
m we n g i n e a i n g i e demokrasia tulivu ya
kupokezana madaraka
na mamlaka kwa njia za
amani na ustaarabu.
Wito wetu kwa
Wazanzibari, ni muhimu
sana kuimarisha Umoja
wetu wa Pamoja,
kudumisha amani na
utulivu ndani ya nchi
yetu na kwamba harakati
zote za kuwatafuta na
kuwabaini walio nyuma
ya uovu huu ziendelee
na kuendelezwa na
Wazanzibari wote kwa
ajili ya kuthamini haki
na utu wa wenzetu
hawa.
Aidha, tusikubali
kutumiliwa na maadui

Maridhiano na Serikali
ya Umoja wa Kitaifa
(SUK) na kuipa nchi yetu
sifa njema na umaarufu
duniani.
Tusitumikie ajenda
potofu za baadhi ya
wanasiasa na watendaji
waliomo ndani ya
SUK ambao kwa wao
siasa ni biashara - na
ambao wanaamini kuwa
maslahi ya chama ni
makubwa zaidi kuliko
maslahi ya nchi na taifa
na wako tayari kuyabeza
maslahi ya nchi pale
yanapopingana na yake
ya vyama vyao.
Wengi wa wanasiasa
wa aina hii ni wakongwe
walioshindwa kufahamu
maana na umuhimu wa
SUK. Wao wamezoea
siasa za kimapinduzi
na/au ile za mfumo wa
chama kimoja. Mwisho,
t u n a t o a m k o n o wa
pole kwa wananchi
wenzetu wazalendo
waliojeruhiwa, kwa
familia, wafuasi na
wapenzi wao na
tunawaombea wapone
haraka, insha'Allah.
Mungu ibariki
Zanzibar.
Mungu wabariki
Wazanzibari.
Mungu wabariki
Watanzania

Habari za Kimataifa

AN-NUUR

JAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 3-9, 2015

Marekani yaonyesha jeuri ya Nyuklia

JESHI la Anga la Marekani


limetangaza kuwa
limefanya majaribio ya
kombora kubwa (balistiki)
linaloweza kuvuka
m a b a r a n a k wa m b a ,
majaribio hayo ni ujumbe
kwa walimwengu kuhusu
u w e z o wa s i l a h a z a
nyuklia wa nchi hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa
iliyotolewa na Jeshi
la Anga la Marekani,
kombora la MinutemanIII, lilifanyiwa majaribio
mapema Jumatatu katika
kituo cha Jeshi la Anga
cha Vandenberg huko
California.
Taarifa ya Jeshi la Anga
la Marekani imesema kuwa
Majaribio hayo ya kombola
la balestiki la nyuklia,
yanaonesha picha ya wazi
kwa walimwengu kuhusu
uwezo wa kombora ya
Minuteman-III ambalo
linaweza kulenga mahala
popote.
Kwa kutilia maanani
kwamba Jeshi la Anga
la Marekani haliwezi
kutumia makombora ya
Peace Keeper kwa mujibu
wa makubaliano ya silaha
ya START II (Strategic Arms

Yafanyia jaribio kombora la Minuteman-III

RAIS Barack Obama wa


Marekani.

RAIS Hassan Raohani wa


Iran.

Reduction Treaty), kombora


la Minuteman-III litakuwa
kombora pekee la balestiki
linaloweza kuvuka mabara
la jeshi la Marekani.
Kombora
hilo

linavishwa kichwa cha


silaha ya nyuklia aina
ya W87, ambacho kina
uwezo mkubwa wa
uharibifu. Majaribio hayo
yamefanyika sambamba

Ebola imeuwa asilimia 90 ya watoto-Utafiti


UTAFITI
mpya
umegundua kuwa Ebola,
imesababisha athari
mbaya zaidi kwa watoto
wa d o g o k u l i k o wa t u
wazima.
Asilimia 90 ya watoto
chini ya mwaka mmoja
ambao waliambukizwa
walikufa.
Utafiti huo ulifanywa
kwa ushirikiano wa
Shirika la Afya Duniani
(WHO) na chuo kimoja
cha London cha Imperial

College London.
Utafiti umeonesha
kwamba japokuwa
k i wa n g o c h a wa t o t o
walioambukizwa ni
kidogo kuliko watu
wazima, watoto na watoto
wachanga ambao walipata
ugonjwa huo walikuwa
na nafasi ndogo sana ya
kupona.
Virusi
hivyo
vinavyosababisha homa
kali na kutokwa damu
ndani na nje ya mwili,

vinaua asilimia 90 ya
watoto wachanga katika
mlipuko wa sasa.
Utafiti umebainisha
zaidi kuwa karibu asilimia
80 ya watoto wa umri
kati ya mwaka mmoja
na miaka mine, hufa
kama walivyogundua
wanasayansi.
Zaidi ya watu 23,000
waliambukizwa virusi vya
ebola na zaidi ya 10,000
walifariki dunia.(VOA).

M S E M A J I wa R a i s
Vl a d m i r P u t i n w a
Urusi, Dmitry Peskov,
amesema kuwa hakuna
kizuizi chochote cha
kisheria kitakachoizuia
serikali ya Urusi
kupeleka silaha na zana
za kijeshi nchini Syria.
Bw. Peskov, amesisitiza
kuwa hakuna kizuizi
chochote kitakachoweza
k u z u i a k u we p o p i a
mashirikiano ya kijeshi
na kiufundi kati ya
serikali za Moscow na

Damascus.
H a y o ya n a e l e z wa
katika hali ambapo
nchi za Marekani na
utawala wa Kizayuni
wa Israel, zimeingiwa
na hofu kutokana na
kuwepo uwezekano
mkubwa wa serikali ya
Urusi kupeleka nchini
Syria mfumo wa kuzuia
makombora S-300.
Msemaji huyo wa Rais
wa Urusi alisisitiza kuwa,
Moscow haijakiuka
sheria za kimataifa kwa

kuipelekea serikali ya
Syria silaha za kujihami
na kujilinda.
Hivi karibuni Rais
Bashar Assad wa Syria,
alivieleza vyombo vya
habari kwamba kuna
makubaliano mapya
ya silaha na zana za
kijeshi yaliyofikiwa kati
ya serikali yake na Urusi
na kusisitiza kwamba,
makubaliano hayo
yako katika hatua ya
utekelezaji. (irib).

Urusi wasema hakuna wa kuwazuia kupeleka silaha Syria

na mazoezi ya kijeshi
yanayoendelea kufanywa
na majeshi ya shirika
la NATO huko Ulaya
Mashariki.
Inaonekana kuwa kwa
majaribio ya kombora hilo
la nyuklia, jeshi la Anga
la Marekani linafuatilia
malengo kadhaa.
Wachambuzi wanaeleza
kuwa Marekani inataka
kuonesha misuli na uwezo
wake wa silaha za nyuklia
k wa wa p i n z a n i wa k e
wakubwa hususan Urusi.
Katika kipindi cha miaka
kama miwili iliyopita
jeshi la Urusi lilifanya
majaribio ya makombora
yanayoweza kuvuka
mabara (Intercontinental
Ballistic Missile au IBM) na
hata kurusha makombora
kama hayo kwa kutumia
nyambizi. Kwa msingi
huo Marekani ilikuwa
i k i n ye m e l e a f u r s a ya
kukabiliana na majaribio
hayo ya silaha za nyuklia
ya Urusi.
Imefahamishwa
kwamba kichocheo cha
pili cha majaribia hayo ni
kukithiri mivutano baina
ya Urusi na NATO huko
Ulaya Mashariki, ambako
kumezifanya pande hizo
mbili kujizatiti kwenye
m e d a n i ya s i l a h a n a
majeshi katika eneo hilo
na katika Bahari Nyeusi.
Hivyo inaonekana
kuwa Marekani inataka
kumuonesha adui yake
mkubwa kijeshi, yaani
Urusi, kwamba iwapo
mgogoro huo utaendelea
inaweza kutumia silaha
zake za nyuklia.
Marekani ni miongoni
mwa wamiliki wakubwa
zaidi wa silaha za nyuklia
duniani na ndiyo nchi
pekee ambayo hadi sasa
imetumia silaha hizo kuua
watu wa taifa jingine.
Nchi hiyo kinyume na
ahadi zake za kupunguza
maghala yake ya silaha za
nyuklia, bado inaonekana
kustawisha na kupanua
zaidi silaha hizo na
kuzifanyia majaribio.
Pia
inadaiwa
kuziboresha zaidi
silaha zake za zamani
za nyuklia licha ya
harakati za kimataifa za
kupunguza silaha hizo,
husuan mkataba wa NPT
unaosisitiza kupunguzwa
na hatimaye kuangamizwa
kabisa silaha hizo.

Washington imetenga
bajeti ya dola bilioni
355 ambazo zitatumika
kuboresha mitambo yake
ya silaha na kuinua juu
kiwango cha majaribio ya
silaha za nyuklia.
Aidha Marekani
imechukua hatua za
kuboresha silaha na
maghala yake ya zana
za nyuklia barani Ulaya,
yakiwemo mabomu ya
nyuklia ya B-61.
K wa u t a r a t i b u h u o
Washington, kinyume na
mikataba ya kimataifa
ya k u z u i a u z a l i s h a j i
wa silaha za nyuklia,
inaendelea kuzalisha na
kufanyia majaribio silaha
za aina hiyo, suala ambalo
linakiuka mkataba wa
NPT na wakati huo huo
kutolalamikiwa na yeyote.
Wa k a t i M a r e k a n i
ikionyesha uwezo wake
wa silaha za nyuklia,
Tauifa hilo limekuwa
kinara wa kushinikiza
mataifa mengine, hasa
ya Mashariki ya Kati
kuachana kabisa na
mpango huo.
Wiki iliyopita
mazungumzo ya Iran
na kundi la 5+1 kuhusu
miradi ya nyuklia yenye
malengo ya amani ya
Iran, yalisimama mjini
Lausanne, Uswisi
kufuatia tofauti na hitilafu
zilizopo kati ya pande za
mazungumzo hayo.
Mazungumzo hayo
yamesimama baada ya
wawakilishi wa kundi la
5+1 kushindwa kuchukua
maamuzi magumu juu
ya kuondolewa vikwazo
dhidi ya Tehran. Licha ya
Jamhuri ya Kiislamu ya
Iran kutekeleza masharti ya
makubaliano yaliyofikiwa
mjini Geneva miaka miwili
iliyopita, bado upande
wa p i l i u m e s h i n d wa
kutekeleza ahadi zake,
suala ambalo limeendelea
kuleta mvutano katika
mazungumzo hayo.
Kwa mufa mrefu Iran,
nchi ambayo imeonekana
kupiga hatua za haraka za
maendeleo ya teknolojia
n a k i j e s h i , i m e k u wa
ikiwekewa vikwazo
vya kiuchumi kufuatia
mpango wake kuzalisha
nishati ya nyklia na ajili
ya matumizi salama na
maendeleo ya Iran.

Makala

AN-NUUR

JAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 3-9, 2015

Kauli ya kutolipiza kisasi yahitaji kushereheshwa

Na Mohammed Ghassany

JIONI ya tarehe 29 Machi


2015, msafara wa wafuasi
wa Chama cha Wananchi
(CUF) waliokuwa
wakitoka Makunduchi,
kusini Unguja, kuelekea
Mjini Magharibi,
ulishambuliwa njiani
na watu wasiojulikana.
Hilo neno watu
wasiojuilikana tuliwache
hivyo hivyo kwenye alama
za mashaka, maana ni
mtazamo wangu kwamba
ni kinyume chake, yaani
ni watu wanaojuilikana
na wale wanaopaswa na
wenye wajibu wa kujuwa
mambo kama haya.
Kwa mujibu wa mmoja
wa watu waliokuwamo
kwenye msafara huo gari
ya majanjawidi ikiwa
katika mwendo wa kasi
iliupita msafara wao na
kisha kuwarushia watu
waliokuwemo katika gari
hiyo visu na nondo. Muda
mchache uliopita, Katibu
Mkuu wa CUF na Makamu
wa K wa n z a wa R a i s ,
Maalim Seif Sharif Hamad,
alikuwa amewaomba watu
wote walioshiriki mkutano
huo huko Makunduchi,
waondoke kwenye msafara
mmoja kurudi mjini.
Inaonekana alishakuwa
na wasiwasi juu ya kile
ambacho kingelitokea na
ushauri wake ulilenga,
yumkini, kukizuwia
kisitokee.
S i k u t a n o k a b l a ya
hapo, ofisi za CUF
jimbo la Dimani, mkoa
wa M j i n i M a g h a r i b i ,
zikateketezwa kwa moto
na watu wasiojuilikana
na kusababisha hasara
kubwa. Mashuhuda wa
tukio hilo, ambalo lilitokea
mtaa wa Kisauni saa 8: 00
usiku, wanasema watu
hao walifika na gari aina
ya Pick-up na kuvunja
mlango wa ofisi hizo
na kuliripua jengo hilo
kwa petroli. Kwa mujibu
wa Diwani wa wadi ya
Tomondo, Hassan Hussen
Yussuf, jengo hilo lilikuwa
na vifaa mbalimbali vya
thamani na fedha taslimu
za malipo ya uchukuaji
wa fomu za wagombea
walizolipia.
Kuchomwa kwa ofisi za
CUF Dimani kulikuja siku
tatu tu baada ya chama
hicho kufanya mkutano
kwenye eneo la jirani na
hapo kwa kile kilichosema
ni kumgotoa Mansoor
Yussuf Himid, ambaye

MIONGONI mwa majeruhi wa mkasa wa kushambuliwa na watu wasiojuilikana wakati wakirudi mkutano
wa CUF, Makunduchi, tarehe 29 Machi 2015.
anarudi kugombea
uwakilishi kwa tiketi
ya CUF katika jimbo la
Kiembesamaki. Mansoor
alikuwa mwakilishi wa
jimbo hilo hapo kabla
kwa tiketi ya Chama cha
Mapinduzi (CCM), kabla
ya kufukuzwa kutokana na
msimamo wake kuelekea
Muungano wa Tanzania
na nafasi ya Zanzibar
kwenye Muungano huo.
Kwenye mkutano huo
kulizungumziwa kuwepo
kwa njama za kuiingiza
Zanzibar katika machafuko
kabla ya kura ya maoni ya
Aprili 30 mwaka huu na
kuelekea uchaguzi mkuu
wa Oktoba 25. Wito wa
wazungumzaji wa CUF
kwenye mkutano huo
ilikuwa kutochokozeka
na kutoondoshwa
kwenye mstari.
Mkutano huo nao
ulitanguliwa na mkutano
wa wazee wa CUF kwenye
ukumbi wa Salama, Hoteli
ya Bwawani Zanzibar,
ambako pamoja na mengine
mengi, Maalim Seif naye
alizungumzia mipango
hiyo ya fujo zinazopangwa
na zilizokwishafanywa
huko nyuma. Na yeye
akasogea mbele zaidi
kwa kurejelea tamko la
kutofukua makaburi lau
chama chake kitachukuwa
madaraka kamili baada
ya uchaguzi wa Oktoba.
Kwa hakika, aliwakemea
wote waliomo kwenye
chama chake, ambao

wanadhani kwamba ikiwa


CUF itaingia madarakani,
itakuwa zamu yao ya
kutesa.
Mstari wa makala
hii unapigwa hapa
ambapo nadhani pana
haja ya kushereheshwa
na sio kutafsiriwa tu.
K u s h e r e h e s h a k wa
wasioufahamu vyema
msamiati huu na asili
yake kuna maana ya
kuchambua tafsiri, wakati
kutafsiri ni kuhamisha
maana kutoka chanzo
kimoja kupeleka chengine.
Asili ya neno kusherehesha
ni kwenye madarasa ya
dini, ambako masheikh
w a n a o t a f s i r i Q u r a n
huchambuwa maana ya
kile walichokitafsiri kwa
upana na marefu.
K wa m a o n i ya n g u ,
kauli za kutochokozeka,
k u t o o n d o k a k we n ye
mstari, kutokufufua
makaburi na kutolipiza
kisasi ni za muhimu
sana katika kujenga siasa
za Maridhiano visiwani
Zanzibar na kulivuta
kundi ambalo hadi sasa
linayapinga Maridhiano
hayo kwa kuwa tu lina
wasiwasi juu ya hatima
yake, endapo CUF itaingia
madarakani. Lakini kwa
umuhimu huo huo pia,
panahitajika kuchorwa
mstari na kuwekwa vituo
ili kundi lililokwishaamua
kuiangamiza Zanzibar,
liujuwe pia ulipo mpaka
k a t i ya k i l e w e n z a o
wanachokichukulia kuwa
ni uvumilivu lakini wao
wakakiona ni ubwege.
Kwa namna yoyote

ile, sidhani ikiwa CUF


inakusudia kulipa kundi
hilo la watu wasiojulikana
hundi safi mkononi
mwao ili liijaze litakavyo,
kisha liondoke zake bila
kuguswa. Sidhani hivyo,
maana huko ni kwenda
kinyume na hata misingi
mikuu ya kuundwa kwa
CUF yenyewe, ambayo
ni haki za binaadamu
na utawala wa sheria.
CUF haivuni chochote
kwa kuwapunguzia
khofu watu hawa zaidi
ya kuwahakikishia kile
kinachoitwa impunity,
yaani uwezo wa kukwepa
sheria. Wanachofahamu
wao pale wakiambiwa
kwamba makaburi
hayatafukuliwa ni
kuwa wamepewa ruhusa
ya kuendelea kupiga,
kujeruhi na hata kuua,
wakijuwa kuwa hatimaye
hakuna mahakama wala
jela inayowasubiri. Huo
ndio uzoefu wao, maana
hawajaanza leo wala jana
kuyafanya haya.
Akili ile ile ya kutia
moto mabanda ya skuli
na vinyesi kwenye
visima, ndiyo akili ile ile
iliyounda Melody, kisha
ikaja na Janjawidi na
Mbwa Wakali na Ubaya
Ubaya. Madhara yale yale
ya miaka ya 90, ndiyo
yaliyokuwa ya 2000, 2005
na sasa 2015. Kundi hili,
lenye akili hizi, halihitaji
kuambiwa kuwa makaburi
yake hayatafukuliwa,
ikiwa bado linaendelea
k u ya t e n d a ya l e ya l e .
Makaburi yao yanapaswa
kufukuliwa na maovu

yao kuanikwa hadharani


na, zaidi kuliko yote,
kufikishwa kwenye
vyombo vya sheria.
Zanzibar ijayo baada
ya Oktoba 2015 inapaswa
kuwa ya kuvumuliana
na kushirikiana kuijenga
kiuchumi, kijamii na
kisiasa, lakini hilo
halipaswi kuwapa watu
nafasi mwanya wa
k u i c h a f u a s a l a m a ya
Wazanzibari hivi sasa,
kisha wakategemea
msamaha na kuvumiliwa
baadaye.
Kwa hivyo, ingawa
ni sahihi kabisa kujenga
moyo wa Maridhiano na
kuondosheana wasiwasi
kwa wale waliotenda
uovu katika zama za
ujahili, si sahihi hata
kidogo kuwajengea imani
waovu wa zama za leo
ambazo ni zama za
nuru. Hawa ni akina Abu
Jahl. Hakuna chochote
kitakachowabadilisha na
kuwafanya waikumbatie
salama ya Wazanzibari
wote. Hawa lazima
waelezwe kinagaubaga
kuwa kuna mahakama,
kuna jela, na kuna adhabu.
Wakati tunajitahidi
kuwazuwia vijana wetu
wasipande jazba na kuingia
kwenye machafuko, kwani
nako pia kutakuwa kwa
faida ya kundi hilo la
watu wasiojuilikana,
tunapaswa kuchora mstari
na kuweka alama zetu.
(Makala kwa hisani ya
Mohammed Ghassani
kwenye zanzibardaima.
wordpress.com.)

7
Na Omar Msangi
The Boogeyman ni filamu
ya kutisha ya Kimarekani
(American supernatural
slasher horror film)
iliyotolewa mwaka 1980.
Ikiongozwa na Ulli Lommel.
Wachezaji wakuu (stars)
walikuwa Suzanna Love,
John Carradine na Ron
James.
Filamu iliwahusu watoto
wawili, Willy na Lacey
a m b a o wa k i s h i r i k i a n a ,
walimuuwa rafiki wa kiume
wa mama yao. Willy alinyata
na kuingia chumbani kwa
mama yake ambapo alikuwa
akifanya mapenzi na rafikiye
haramu (kwa maana sio
mume wake wala baba wa
watoto wake). Kwa kutumia
kisu akamuuwa rafiki huyo
wa mama yake. Wakati hayo
yakifanyika, Lacey alikuwa
akitizama kupitia kiyoo.
Miaka 20 baadae, mpenzi
huyo wa mama yao anakuja
kulipiza kisasi katika namna
ya jinamizi, lililowahangaisha
sana watoto hao Lacey na
Willy, wakati huo wakiwa
wa t u wa z i m a . I l i k u wa
kila siku Lacey na Willy,
wanaweweseka kwa kujiwa
na mtu kama yule mpenzi
wa mama yao akiwa
na kisu mkononi akitaka
kuwashambulia. Majinamizi
kama haya (Bogeyman au
monsters), inakuwa tabu
sana kupambana nayo na
kuyashinda kwa sababu moja
tu muhimu: Sio viumbe halisi.
Inayodaiwa kuwa vita
dhidi ya ugaidi, imejaa
ma-bogey men, wengi iwe
kwa jina la Boko Haram,
Al-Shabaab, IS, Alqaidah,
Abubakar Shekau, Abu
Baghdad n.k. na kwa maana
hiyo, si vita inayotarajiwa
kumalizika kwa kutumia
polisi, makachero au
jeshi. Itamalizika tu kwa
wanaounda majinamizi haya
kuacha mchezo wao. Watu
hao kila kukicha, wanabuni
mbinu mpya ama za kubuni
majinamizi mapya au kuyapa
uhai na kuyadumisha
yaliyopo.
Oktoba 2008 ilichapishwa
habari moja katika vyombo
vya habari iliyopewa kichwa
cha habari: Beware the
Bogey Man: A new low, even
for McCain and his ignorant
supporters!
Chini ya kichwa hicho
likaelezwa tukio moja katika
mkutano wa hadhara wa
kampeni kule Minneapolis,
ambapo John McCain
alikuwa katika kampeni za
kuwania Urais wa Marekani.
Ilikuwa ni katika mkutano
h u o m wa n a m k e m m o j a
alieleza wasiwasi wake juu ya
Barack Obama akisema kuwa
hamwamini kwa sababu
amewahi kusoma mahali
kuwa Obama ni Mwarabu.
"I don't trust Obama. I have
read about him. He's an Arab."
Alisema mwanamke huyo
katika jitihada za kuonyesha
kuwa huenda John McCain
akawa Rais bora kuliko
Obama.
Katika kujibu swali la
mama huyo, John McCain
a l i p i g i l i a m s u m a r i wa
ubaguzi na kitisho cha
Muarabu na Muislamu.
Alisema:
No, maam. Hes a decent,
family man, [a] citizen that I just
happen to have disagreements
with on fundamental issues and

Makala

AN-NUUR

JAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 3-9, 2015

Lipo Jinamizi

Khadija Abubakar Abdulkadir, Maryam Said Aboud na Ummul Khayr Sadir Abdulla.
that's what this campaign is all
about."
Katika namna nyingine ni
sawa na kusema: Dont worry,
maam, Barack Obama is NOT
an Arab. Unlike Arabs, hes a
decent, family man.
Ukitizama namna zote
mbili, hapa John McCain
anachofanya ni kushindilia
tu msumari wa ubaguzi
na kitisho cha Uarabu
na Uislamu. Anamtoa
hofu muuliza swali kwa
kusema kuwa Obama ni
mtu mstaarabu, sio kama
Waarabu/Waislamu.
Kinachoelezwa na swali
la mama muuliza swali ni
kuwa jamii ya Kimarekani
imejengwa kuogopa kitisho
cha Waarabu na Waislamu,
na pengine John McCain
angeweza kusema lolote
k u s a h i h i s h a k u wa i w e
Muarabu, Mzungu, wote
ni raia wa Marekani bila
kujali asili zao. Au katika
muktadha wa dunia, kuwa
wote ni binadamu, watu
wasipimwe kutokana na
asili yao. Lakini hakufanya
hivyo. Akamwacha mama
huyo na wasilikizaji
wengine katika mkutano
huo wakibaki na ujinga wao
wa kuogopa kitisho bandia
cha Uislamu/Waislamu na
hivyo kuendeleza agenda
ya ubaguzi na vita dhidi ya
ugaidi.
Taarifa kuu na muhimu
kabisa wiki hii katika eneo letu
hili la Afrika Mashariki kwa
wiki hii, pengine zitakuwa ni
zile za kukamatwa wasichana
watatu, wakidaiwa kutaka
kuvuka mpaka kwenda
Somalia kujiunga na AlShabaab. Vyombo vya habari
vikasherehesha vikidai kuwa
wa s i c h a n a h a o K h a d i j a
Abubakar Abdulkadir,
Maryam Said Aboud na
Ummul Khayr Sadir Abdulla
waliokamatwa katika mji wa
El Wak ilikuwa wakaolewe na
Mujahidina wa Al-Shabaab
na IS. Kati ya wasichana hao,
mmoja ni kutoka Zanzibar
akitajwa kwa jina la Ummul
Khair Sadri Abdallah.
Taarifa zaidi zikafahamisha
kuwa wasichana hao
walijikuta katika mtego
wa k we n d a S o m a l i a - A l
Shabaab na kisha IS, kupitia
mawasiliano waliyokuwa

wakifanya na mwanamke
mmoja wa Syria, aliye katika
IS.
Katika jambo hili, upo
uwezekano wa namna mbili.
Moja ni kuwa inawezekana
kweli wasichana hao
walishawishiwa wakafikia
k i wa n g o c h a k u k u b a l i
kwenda kujiunga na AlShabaab. Nasema hivyo kwa
sababu ipo mifano mingi ya
watoto wa Kiislamu kuacha
shule na hata walio Vyuo
Vikuu baada ya kughilibiwa
kuwa kusoma ni kupoteza
muda, bali kinachotakiwa
ni kwenda Jihad. Lakini
hata kama itakuwa hivyo,
bado waliofanya kazi hiyo
watabaki kuwa mawakala wa
mabeberu walioandaliwa na
mabeberu kuwafanyia kazi.
Uwezekano wa pili ni
kuwa wasichana hao wapo
katika mtego alionasa Sami
Osmakac. Wakati mwingine
mawakala wanaofanya kazi
hii, ikionekana kasi yao
ndogo, makachero huingia
moja kwa moja na kuwatia
walengwa katika uhalifu
kisha kuwakamata na
kuwasukumizia tuhuma za
ugaidi. Ndiyo yaliyomkuta
Sami Osmakac ambaye hivi
sasa anatumikia kifungo cha
miaka 40 kule Marekani.
Hivi sasa kuna mikakati
ya kuhakikisha kuwa haya
mazimwi (bogey men)
yanahuishwa na namna ya
kuhuishwa ni kama hivi
kupatikana kwa watu
kama hao wakidaiwa
kwenda kujiunga na AlShabaab au IS. Namna
nyingine ni kupatikana kwa
mashambulizi ya kupanga
au kutolewa mara kwa mara
kwa tahadhari za vitisho
kama zile za wiki mbili
zilizopita kwamba magaidi
wa IS watapiga Mwanza,
Dar es Salaam, Nairobi na
Kampala.
Katika matoleo yetu
ya hivi karibuni, tuliwahi
kueleza kukamatwa watu
kule Uturuki ambao hufanya
kazi ya kunasa watu na
kuwapelekwa kwa IS na
kwamba mawakala hao
hufanya kazi kwa kutumwa
na chini ya uangalizi wa
v y o m b o v ya k i k a c h e r o
vya Magharibi na hupewa
fedha nyingi kwa kila mtu

wanayemnasa. Lengo ni
kuzidi kukoleza kitisho cha
bogey man IS.
Katika kadhia ya Sami
Osmakac, makachero wa
FBI waliunda mtego ambapo
walimnasisha kijana huyo
asiye na hatia, na kisha
kumtangazia ugaidi ambao
lau wasingekuwa wao FBI,
kijana huyo asingefanya yote
hayo aliyokuja kusingiziwa
kufanya.
Inawezekana pia kwa hawa
wasichana wakapatikana
makachero mawakala wa
mabeberu wakawachezea
akili zao na kuwanasisha
kama alivyonasa Sami
Osmakac kisha wakaibuka
na taarifa kuwa wanakwenda
Somalia kuolewa na AlShabaab.
Joseph Kibwetere
wa Uganda, aliweza
kuwaaminisha watu wake
kuwa wakijitia katika tanuri
la moto Kwa jina la Yesu,
wanaibukia upande wa pili
wakiwa Mbinguni (Peponi).
Mamia ya watu wakajitosa
wakafa. Sasa yaweza
v i j a n a wa k a t i wa i m a n i
hizi za Joseph Kibwetere
wakawaona wazazi wao
Wa i s l a m u n i m a k a f i r i
wakahiyari wakaolewe na AlShabaab, bila ya Walii maana
walii (mzazi) ashakuwa
kafiri!
Kwa
vyovyote
itakavyokuwa, kama nchi,
tunatakiwa tulitizame jambo
hili kwamba kwa asili yake,
sio la Waislamu wala AlShabaab. Ni mitengo na
mikakati ya mabeberu katika
kujihakikishia utawala na
udhibiti wa kidunia- US
World Hegemony. Kupitia
vita dhidi ya ugaidi,
kinapatikana kisingizio cha
kuingia popote kwa hoja
ya kuwafuata magaidi au
kusaidia nchi inayolengwa
kupambana na magaidi.
Tukilitizama kwa makengeza
kwamba ni tatizo la Ummul
Khair, tunajizamisha
wenyewe katika tope mithili
ya Boko Haram, ambalo
hatutaweza kutoka hata
tukitamani.
Imani yangu ni kuwa tuna
akili pevu za kuyatizama
mambo ya dunia hii kwa
mtizamo sahihi. Na niseme
hapa kuwa katika hili, akina

James Mbatia na sisi sote,


t u z i we k e p e m b e n i z i l e
chuki zetu za kidini kama
zilivyojitokeza katika ile
semina kwa wabunge juu
ya Mahakama ya Kadhi.
Haya ya Mahakama ya Kadhi
ni yetu, tutajua namna ya
kuelewena huko mbele ya
safari. Lakini hili la ugaidi
si letu na tukiruhusu
kuundiwa haya majinamizi,
wala tusijidanganye kuwa
tutakuwa na uwezo wa
kupambana nayo. Tutaumia
s o t e . N c h i i t a v u r u g wa ,
tutapigwa wala hatutamjua
anayetupiga, kama ambavyo
hatukuweza kumkamata
aliyetupiga kule Westgate
na Mandera, Kenya.
Tumebaki tunaimba AlShabaab, Samantha Louise
Lewthwaite (White Widow)
na danganya toto nyingine
kama hizo, utadhani hatuna
akili timamu.
Tukilitizama suala hili kwa
sura yake halisi, tutaacha
ushabiki wa kulifanya kuwa
ni tatizo la ugaidi wa baadhi
ya Waislamu, bali ni tatizo
la ubeberu na mbinu zake
ambapo tusipokuwa makini,
sote tutaumia.
H i v i s a s a u t a f i t i wa
haraka haraka unaonyesha
kuwa kuna vijana wengi
kule Mwanza hawajulikani
walipo. Kwa lugha
mashuhuri miongoni mwa
vijana wa Mwanza ni kuwa
wamekwenda shamba.
Wa p o wa z a z i wa n a l i a ,
hawajui watoto wao walipo.
Wapo wanawake, hawajui
walipo waume zao, mpaka
imebidi warejee makwao.
M i s i k i t i wa n a p o i b u k i a
na kwenda shamba,
inajulikana. Viongozi wao
wanaowaghilibu mpaka
kutoweka kwenda shamba,
wanajulikana.
Hapa kuna uwezekano wa
namna mbili: Moja ni kuwa
huenda Shamba ni Somalia/
Syria, kwamba wamepenya
wamekwenda huko au wapo
hapa hapa nchini wakijiandaa
kuja kuibuka kama bogey
man la mfano wa Boko
Haram.
Kwa mtu binafsi kama
ambavyo tumejitahidi
kufanya, inakuwa vigumu
sana kujua kwa uhakika,
huko shamba wanakokwenda
vijana hawa ni wapi. Lakini
tunaamini kuwa serikali
inaweza kujua na kama nchi
tukaweza kujinusuru na balaa
linaloweza kujitokeza kama
tutachelewa tukaibukiwa na
bogey man letu.
Kinachotutatiza ni kuona
sehemu zinazozalisha vijana
wa n a o k we n d a s h a m b a
zinajulikana na zinazidi
kunawiri, lakini kimyaa!
Si Masheikh, viongozi wa
Kiislamu wala wa serikali
wanaoonyesha kujali.
Inafikia mahali tunakuwa
na wasiwasi kuwa isije
ikawa tumefikishwa mbali.
Tumekuwa akina Pervez
Musharraf wa kuwasaidia
mabeberu kuunda vikosi vya
bogey men wao katika nchi
yetu. Lakini huo ni wasiwasi
tu.

Makala

AN-NUUR

JAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 3-9, 2015

Kisa cha Nabii Swaaalih sehemu ya Mitume


Na Ally Nzomkunda

NABII Swaalih alikuwa


ni Mtume katika kabila
maarufu ambalo jina
lake linatokana na jina
la babu yao Thamuud
ambaye ni katika ukoo wa
Nabii Nuuh. Kwa hivyo
jina lake ni Swaalih ibn
'Ubayd ibn Maasih ibn
'Ubayd ibn Haajir ibn
Thamuud, ibn 'Aabir
ibn Iram, ibn Saam, ibn
Nuuh.
Naye Swaalih na watu
wake wa Thamuud ni
Wa a r a b u w a l i o k u w a
wakiishi Hijr ambayo iko
baina ya Hijaaz na Tabuuk
(Kaskazini Magharibi ya
Madinah) ambako siku
moja Mtume alipita wakati
wanaelekea kwenye
vita vya Tabuuk kama
tutakavyoelezea mwisho
wa kisa hiki. Hiki ndio
kisa chake Nabii Swaalih
n a wa t u wa k e k a m a
tulivyoelezewa katika aya
mbalimbali za Qur'an.
Wa t u wa T h a m u u d
walikuwa ni watu baada
ya Nabii Huud (as) ambao
walikuwa wakiabudu
masanamu na baada ya
kuletewa Nabii Huud (as)
na kumkanusha, Allaah
(sw) aliwaangamiza.
Baada ya miaka, watu
wa Thamuud wakaibuka
na kuwa na nguvu na
ufahari. Nao pia waliabudu
masanamu, kwa hivyo
Allaah Akawatumia
mjumbe miongoni mwao
naye ni Nabii Swaalih
ambaye naye kama
k a wa i d a ya M i t u m e ,
alikuja na wito uleule
wa kuwaita watu katika
Tawhiiyd ya Allaah yaani
kumuabudu Yeye pekee
bila ya kumshirikisha na
kitu, na kuwanasihi waache
ibada ya masanamu na pia
kuwataka watubu kwa
Mola wao kwa kufuru
wanayoifanya.
Na kina Thamud
tuliwapelekea ndugu yao
Swaalih. Akasema: Enyi
watu wangu! Muabuduni
Mwenyezi Mungu. Nyinyi
hamna Mungu ila Yeye.
Yeye ndiye aliyekuumbeni
katika ardhi, na
akakuwekeni humo. Basi
mwombeni msamaha,
k i s h a m t u b u k wa k e .
Hakika Mola wangu Mlezi
yupo karibu, anaitikia
maombi. (Huud: 61)
Kwa maana kwamba:
A m e k u j a a l i e n i k u wa
makhalifa baada ya watu
wengine (kina 'Aad na

wa nyuma yao) ili mfikiri


na mtambue ubaya wao
waliotenda, na nyinyi
msiwe kama wao, na
Akakujaalieni katika hii
ardhi na kukuneemesheni
neema mbali mbali kama
za mashamba na matunda
na majumba ya fahari
mkastarehe, basi Yeye
Pekee ndiye anayestahiki
kuabudiwa bila ya
kumshirikisha, vile vile
mkabilini Mola wenu kwa
kumshukuru na kufanya
amali njema wala msjije
kumkhalifu amri Zake na
kutoka nje ya mipaka kwa
kutokumtii, basi rudini
kwake kwa kutubia na
Yeye Allaah yuko tayari
kupokea tawbah zenu.
Aya ifuatayo inaeleza
zaidi neema hizo
wa l i z o j a a l i wa n a p i a
kuonesha ukumbusho wa
Swaalih kwa hao watu wa
Thamuud kwa kuwaita
kwao kwenye dini ya haki.
N a k wa T h a m u u d
tulimpeleka ndugu yao,
Swaalih. Akasema: Enyi
watu wangu! Muabuduni
Mwenyezi Mungu.
Nyinyi hamna Mungu ila
Yeye. Hakika imekwisha
kukufikieni Ishara iliyo
wazi kutoka kwa Mola
wenu Mlezi. Huyu ni
ngamia jike wa Mwenyezi
Mungu aliye ni Ishara
kwenu. Basi mwachieni ale
kwenye ardhi ya Mwenyezi
Mungu, wala msimdhuru,
isije kukushukieni adhabu
chungu. (Al-A'araaf: 73)
Na kumbukeni
alivyokufanyeni wa
kushika pahala pa 'Aadi na
akakuwekeni vizuri katika
nchi, mnajenga majumba
ya fakhari katika nyanda
zake, na mnachonga
majumba katika milima.
Basi zikumbukeni neema
za Mwenyezi Mungu wala
msitende uovu katika nchi
kwa ufisadi. (Al-A'araaf:
74)
Kama zilivyo umma
zilizopita zilipojiwa na
Mitume, wakaamini
wachache miongoni mwao
na wengi wakamkanusha.
Na kwa kina Thamuud
tulimtuma ndugu yao
S wa a l i h k u wa a m b i a :
Muabuduni Mwenyezi
Mungu. Basi wakawa
makundi mawili
yanayogombana. (AnNaml :45)
Wa l i o m k a n u s h a
wa l i m s h u t u m u k u wa
a n a wa l e t e a s h a r i , n a
kwamba labda akili
yake haiko sawa kwani
hawakumtegemea yeye

SHEIKH Ally Bassaleh (kushoto), Sheikh Rajab Katimba (katikati) na Sheikh


Mohamed Issa (kulia).
Swaalih ambaye kwao
alikuwa ni mtu mwema
kabisa, aje kuwakataza
kuacha waliyokuja
nayo mababu zao na
kutaka wamfuate hayo
anayotaka yeye Swaalih
Wakamwambia;
Wa k a s e m a : E w e
Swaalih! Hakika kabla
ya haya ulikuwa
unatarajiwa kheri
kwetu. Je, unatukataza
tusiwaabudu waliyokuwa
wakiwaabudu baba zetu?
Na hakika sisi tuna shaka
na wasiwasi kwa hayo
unayotuitia. (Huud: 62)
Walikuwa na shaka
kubwa juu ya yale Swaalih
aliyowalingania nayo
na kuyaona ni mapya!
Swaalih akawajibu:
Akasema: Enyi watu
wangu! Mwaonaje ikiwa
ninazo dalili zilizo wazi
kutokana na Mola wangu
Mlezi, naye akawa kanipa
rehema kutoka kwake - je,
ni nani atakaye ninusuru
kwa Mwenyezi Mungu
nikimuasi? Basi nyinyi
hamtanizidishia ila
khasara tu. (Huud:63)
Akasema: Enyi watu
wangu! Mwaonaje ikiwa
ninazo dalili zilizo wazi
kutokana na Mola wangu
Mlezi.
Dalili za dhahiri zenye
uhakika kabisa kwa yale
anayowaitia kumuabudu
k w a m b a Ye y e n d i y e
Mola wa Viumbe wote
na Mola wa mbingu na
Ardhi na mwenye kupasa
kuabudiwa kwa haki.
Naye akawa kanipa

rehema kutoka kwake.


Re h m a k ut o k a k wa
Allaah kumchagua yeye
na kumpa uongofu na
kumfanya Mjumbe Wake
Allaah. Aliyemtuma kwao
kuwatoa katika upotofu.
Je, ni nani atakaye
ninusuru kwa Mwenyezi
Mungu nikimuasi?
Nikiacha kukuiteni
katika hakki ya
kumuabudu Allaah Pekee,
basi nyinyi hamtoweza
kunifaa wala kuninusuru
na adhabu yake Allaah
atakaponiadhibu, bali
itakuwa ni hasara tu na
kuangamia kwangu. Vile
vile wakamwambia:
Wakasema: Hakika
wewe ni miongoni mwa
waliorogwa. (Ashura:
153)
Mujaahid kasema;
Wamemaanisha kuwa
kaathirika na uchawi.
Wafasiri wengi wamefasiri
kwamba ina maana;
Hujui unachokisema
kutuita katika ibada ya
mungu mmoja na kuacha
miungu mingine! Hiyo
ndio ilikuwa kawaida ya
watu wa umma za nyuma,
walipojiwa na Mitume
yakawa majibu yao ni
kuwaambia hao Mitume
kuwa ni wachawi! kama
alivyoambiwa vile vile
Mtume na makafiri wa
ki-Quraysh. Vile vile ni
kawaida yao nyingine
kuwadharau hao Wajumbe
wa Allaah kwa vile wao ni
binaadamu tu kama wao.
Na wakisema:
Wewe si chochote ila ni

mtu kama sisi. (Ashura:


154)
T h a m u d i
waliwakanusha
Waonyaji. Wakasema:
Ati tumfuate binaadamu
mmoja katika sisi? Basi
hivyo sisi tutakuwa
katika upotofu na
k i c h a a ! . N i ye ye t u

a l i ye t e r e m s h i wa h u o
ukumbusho kati yetu
sote? Bali huyu ni mwongo
mwenye kiburi! Kesho
watajua ni nani huyo
mwongo mwenye kiburi.
(Al-Qamar : 23-26)
Kama kweli y eye ni

Mtume, basi wametaka


miujiza ndio waweze
kumuamini.
Wewe si chochote
ila ni mtu kama sisi.
Basi lete Ishara ukiwa
wewe ni miongoni
mwa wasemao kweli.
(Ashu'araa: 154)
Nabii Swalih
akajitenga nao kwani
alikwishakata tamaa
nao:
Basi Swaalih
akawaacha na akasema:
Enyi watu wangu!
Nilikufikishieni Ujumbe
wa Mola wangu Mlezi,
na nikakunasihini, lakini
nyinyi hamwapendi
wenye kunasihi. (AlA'araaf: 79)
Ishara au Miujiza
waliyotaka kutoka kwa
Nabii Swaalih ni ngamia
kama tutakavyoona:
(Kisa kinaendelea ...)

Makala

AN-NUUR

JAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 3-9, 2015

Ni nani hasa washenzi - Nchi za Magharibi au Waislamu?


Na Mahboob A. Khawaja

MACHI 24, 2015 Mtandao


wa Kupashana Habari Marekani na Ulaya wanaona
vita kama nyenzo ya kuweka
mamlaka na kudhibiti
rasilimali ghali za nchi
za Kiarabu na Kiislamu.
Marekani yenye hulka ya
kujiona na washirika wao
wa Ulaya wanakosa hisia
ya hatia kwa wahanga wa
uharibifu na uteketezaji wa
miaka kumi ya kuzikalia
na kuziharibu Irak na
Afghanistan. Kuinua
mahitaji ya dhamira ya
binadamu, wananchi katika
nchi za Kiarabu wanaziona
nchi hizi ni za kishenzi zaidi
kuliko watangulizi wao wa
Vita vya Msalaba vya karne
ya 12.
Kutojiweza kukiungana
na ubinafsi kichaa, hufanya
watawala wa nchi za
Kiarabu zinazozalisha
mafuta kuridhika na kufuata
maagizo ya nchi za Magharibi
licha ya changamoto za ndani
na fitina katika tawala zao.
Tamaa na ulazima wa kufanya
maovu na kushindwa kwa
uongozi wa kimaadili na
kifikra, umeweka hatarini
hali ya sasa na ya baadaye
ya dunia yote ya Kiarabu
na Kiislamu. Ukiangalia
kwa karibu kinachopita
akilini, ghadhabu na mauaji
ya kidhehebu kila siku na
kugeuza jamii ziwe za kijeshi
vimeinua taswira potofu.
Kwa kutojali kimaadili
na kifikra viongozi wa nchi
za Kiarabu na Kiislamu
wamechoka na wanangoja na
kungoja nini kitatokea baada
ya hapa, bila ubunifu na
fikra mpya kwa ulimwengu
wa udadisi na uhalisia.
Utumiaji vita wa kupanga
na ukatili unaotokana na
hali hiyo, imekuwa ndiyo
sura ya kawaida ya dunia
ya Kiarabu na Kiislamu.
Wanasubiri muujiza utokee
hivi hivi tu. Kupenda anasa
na kulea hali ya kivita
kumevuruga utamaduni
asilia wa nchi za Kiarabu na
mfumo wake wa hisia. Labda
utajiri mpito wa fedha za
mauzo ya mafuta umeleta
mafanikio na imeondoa hisia
ya hofu na aibu kwa kuwapa
uwezo wa kudiriki kufanya
uhalifu wowote dhidi ya
heshima ya binadamu na
wananchi. Mapambano ni
kati ya ubabe wa tawala
zinazoungwa mkono na nchi
za Magharibi na harakati ya
kutaka mabadiliko ya kisiasa
miongoni mwa raia wa nchi
za Kiarabu. Kila mahali watu
wanapigana. Kwa karne yote,
Waarabu wameshindwa
katika vita hivyo. Viongozi
wanaonekana kujikita katika
jahiliya mpya isiyofahamika
katika historia ya binadamu.
Kama mtu akiuliza,
wanapigana kwa ajili gani?

WAPIGANAJI nchini Yemen wakiwa na silaha zao.


Hakuna uhusiano wa mantiki
katika vita inayosimamiwa
na Marekani dhidi ya ISIL
au Iran kuendesha Shiite
kundi Al-Badr na wengine
kufanya uhalifu dhidi ya
waumini wa ki-Sunni au
wa ki-Shia walio wachache.
Hakuna maadili katika vita ya
mawakala. Matendo yote ya
kushambulia yanaamrishwa
kwa makusudi kutokana na
nia za wanaowatuma.
Dunia ya Kiarabu na
Kiislamu imeangukia katika
ukatili wa kisiasa na tope
la kudidimia. Mtu kuua
mtu mwingine, na hakuna
kujiuliza kwanini. Viongozi
na watu wanaonekana kuwa
katika ukurasa huo huo wa
umwagaji wa damu, kuzorota
kwa usalama na kupumulia
mashine katika eneo la zama
za kutatanisha linaloangukia
kusikojulikana. Hawaamini
katika chochote kile kana
kwamba dunia imezubaa,
kana kwamba hakuna Mungu
na maisha hayana tena lengo
tukufu la amani, uelewano
na kuishi pamoja. Wapanga
mikakati ya vita wa nchi za
Magharibi ni sababu muhimu
katika kuwafikisha kwenye
hali hii potofu kimaadili na
mlingano wa kibinadamu.
Katika karne ya 21 yenye
maendeleo ya juu kimaarifa,
hekima na ufahamu, watu
wanaka katika ujinga na
kiburi cha kutokufahamu
ubaya wa fikra zake. Utawala
wa kidhalilmu wa nchi
za Kiarabu na Kiislamu
ukisukumwa na taswira
yake yenyewe kufanya vita
iliyopangwa na uchokozi
dhidi ya harakati ya
kimapinduzi ya wananchi
wa Syria, Irak, Yemen, Misri,
Libya na Bahrain. Baada ya
miaka mitano, jumuiya ya
kimataifa ni mtazamaji tu
akiangalia uhalifu wa kutisha
wa wachache dhidi ya wengi.
Hakuna mamlaka ya dunia
iliyopo tayari kuwalinda
waathirika wa umwagaji

damu unaoendelea. Hakuna


sheria ya kimataifa kukataza
machafuko. Viongozi wengi
wa nchi za Kiarabu na
Kiislamu wanakosa uwezo
wa kufikiria hali ya baadaye
ya kisiasa yenye tija na
kuelewa kusudi la maisha
ya binadamu na vipaumbele
vyake ndani ya wigo wa
dunia hai na ulimwengu hai
ambako kuna uwajibikaji
makini wa mtu kuhusiana
na wakati na mahali. Ni
kwa njia gani ukatili huu
wa kutengenezwa na hali ya
machafuko kutasimamishwa
n a b i n a damu ao k o l ewa
kutoka janga la umwagaji
damu kimadhehebu
uliokolezwa kisiasa uliofikia
pabaya sana na ni vigumu
hata kufikiria matokeo yake?
Ingekuwa wanamwamini
Mungu, ubinadamu na
madhumuni ya maisha ndani
ya uwajibikaji unaoeleweka,
Dunia ingeweza kuwa mahali
pema zaidi kwa wote kuishi
kwa amani. Mgawanyiko ya
kuchukiza ya kidhehebu na
mauaji ya wa-Sunni, wa-Shia,
Wakristo na jamii nyingine
za walio wachache katika
nchi za Kiarabu imefikia
kiwango cha kutisha na janga
lisilopimika. Hivi jumuiya
ya kimataifa inayojua nini
kinatokea inataka kuona nchi
za Kiarabu kujitengenezea
ye n ye we m w i s h o wa k e
k i k a t i l i ? K u m w u a k wa
makusudi binadamu mmoja
ni kama kuua binadamu
wote. Mabwana vita wa
dunia wanawakilisha ukatili
kimawazo usioweza kuona
upande wa kibinadamu wa
dhamira iliyo hai. William
T. Hathaway ("Marekani
inashambuliwa!") ambaye pia
ni mwandishi wa Dunia ya
Maumivu na profesa mshiriki
wa elimu kuhusu nchi za
bara la Amerika, Chuo Kikuu
cha Oldenburg, Ujerumani,
amejaribu kufafanua jinsi
Marekani na Uingereza
wameifikisha dunia katika

kilele cha mauaji katika nchi


za Kiarabu za Mashariki ya
Kati:
"Marekani na Uingereza
zimefanya maovu kama
hayo katika Irak, Syria,
Lebanon, Libya, Indonesia
na Afghanistan. Tulipindua
s e r i k a l i z a o , t u k a we k a
madikteta, tukadhoofisha
u c h u m i wa o - y o t e i l i
kuimarisha maslahi yetu ya
kibiashara. Katika kila nchi
ambako sasa kuna ugaidi,
tulianza kwa kuwanyanyasa.
Marekani inashambuliwa
kwa sababu tu ilitangulia
kushambulia. Haishangazi
kuwa wanatuchukia. Fikiria
tungejisikiaje kama nchi ya
kigeni ingekuwa inatufanyia
hivi. Tungejibu mapigo kwa
njia yoyote ile tunayoweza
...... Kama watu wangefahamu
hili - wangejua jinsi ilivyo
rahisi kusimamisha ugaidi wasingetaka kupigana vita
hivi. Ndiyo maana vyombo
vya habari vinapuuza madai
ya al- Qaeda. Viongozi wa
nchi za Magharibi hawataki
watu waone kuwa nia halisi
ya vita si kusitisha ugaidi ila
kudhibiti raslimali za eneo
hlo. Kusema kweli wanautaka
ugaidi kwa sababu unawapa
kisingizio wanachohitaji tishio la adui mwovu."
Ni nani hasa washenzi,
nchi za Magharibi au
Waislamu?
"Ilikuwa chini ya ushawishi
wa Waarabu na Machotara
walioinua utamaduni na
siyo katika karne ya kumi na
tano, ambako zama mpya za
ustaarabu zilianza. Hispania
si Italia, ilikuwa ndiyo
Ulaya ilipovamiwa upya ...
Inawezekana kabisa kuwa
kama siyo kwa mchango
wa Waarabu, utamaduni
wa kisasa wa Ulaya
usingeanza kabisa; ni jambo
la uhakika kabisa kwamba
isingekuwa wao, isingekuwa
na mwelekeo ambao
u m e t u we z e s h a k u v u k a
hatua zote za mabadiliko

hadi hapa. Kwani licha ya


kwamba hakuna eneo hata
moja la kukua kwa Ulaya
ambako mchango muhimu
wa utamaduni wa Kiislamu
hauonekani, hakuna ambako
hilo liko wazi na muhimu
kama katika kuzaliwa kwa
mamlaka ambayo ni kielelezo
mahsusi cha dunia ya kisasa
na mwanzo mkuu wa ushindi
wake." (Robert Briffault,
profesa wa Chuo Kikuu
cha) Cambridge, 'Uasisi wa
Binadamu,' London. 1919
Waarabu waliwahi kuwa
waanika njia ya ustaarabu
endelevu uliojikita katika
elimu uliodumu kwa miaka
800 - kipindi kirefu zaidi cha
kuongoza kwa ustaarabu
katika historia ya binadamu.
Hivi sasa, wasomi wa nchi
za kikoloni za zamani na
wakaliaji kwa mabavu
wanawaita Waarabu na
Waislamu kama watu wa
'siasa kali' na 'washenzi.'
Katika muda wote wa karne
ya 20 na hadi kuingia karne ya
21, utajiri mafuta ulishindwa
kukabiliana na matatizo ya
kijamii, kimaadili, kifikra
na kisiasa. Badala yake,
kuingizwa mkondo wa kijeshi
wa ukanda huo, kuongezeka
kwa mauaji kunaonyesha
mkanganyiko mpana wa
kisiasa.
Uislamu uliwatajirisha
Waarabu wakawa viongozi
wa utamadunmi wenye kasi
ya maendeleo. lakini kukua
kwa haraka kutokana na
mafuta kumewabadilisha
kuwa 'waendesha mbio za
ngamia' na walengwa wa
vicheko vya kina katika meza
za chakula cha jioni katika
utamaduni wa Magharibi.
Wakati Waarabu wakiwa
na bidii ya kimisionari
ya "kukataza maovu, na
kukaribisha binadamu
wote kuyaelekea mema,"
walifanikiwa sana katika
mabadiliko ya kibinadamu,
u o n g o z i wa k i m a a d i l i ,
m a e n d e l e o ya v i t u n a
ustaarabu. Fedha haiwezi
kununua hekima, heshima
na uadilifu wa kibinadamu.
Marehemu Mfalme Abdullah
wa Saudia na Sheikh Sabah
al-Sabah wa Kuwait wote
wawili walikuwa nyororo
katika kutoa msaada wa
hali na mali kwa George
Bush mwaka 2003 wakati wa
uvamizi wa Irak na mauaji
ya watu takriban mamilioni
tatu nchini Irak wakati wa
ukaliaji nchi hiyo kwa muda
mrefu. Uwongo wa 'vita
dhidi ya ugaidi' usingetokea
iwapo viongozi wa nchi za
Kiarabu - wanaotumiwa
mstari wa mbele wa
Marekani - wangekuwa na
mwelekeo chanya wa akili,
uwezo wa kufikiri na uadilifu
kukinzana na hatua isiyo na
mantiki kabisa na ya kikatili
katika historia ya binadamu.

Inaendelea Uk. 12

10

Makala

AN-NUUR

JAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 3-9, 2015

Siasa za mabeberu Iraq na Yemen


Na Omar Msangi

WA K AT I M a r e k a n i
ilipotangaza kuwa
inawashambulia ISIS,
b a a d h i ya wa s o m a j i
wetu walituandama kwa
maneno makali wakidai
kuwa kile tulichokuwa
tukisema juu ya uhusiano
wa Abu Baghdad (ISIS)
na Marekani, ilikuwa
uwongo mtupu. Msingi
wa shutuma zao ni kuwa
wakati sisi tukijenga
hoja kuwa ISIS ni
mawakala wa mabeberu
wakitumika katika proxy
war ya kuisambaratisha
Syria, Iraq na Mashariki
ya Kati kwa ujumla, wapo
Wa i s l a m u wa l i k u wa
wakiamini kuwa ISIS
walikuwa katika Jihad
ya kusimamisha Dola
ya Kiislamu/Khilafah
(Islamic State). Sasa
i l i p o k u wa M a r e k a n i
inawashambulia ISIS,
wakaja na hoja kuwa
kama IS wangekuwa
mawakala, mamluki na
vibaraka wa Marekani,
basi isingekuwa tena
Marekani iwashambulie
IS. Baadhi ya wasomaji
hao wakaenda mbali kwa
kuja na kashfa na matusi
wakisema kuwa sisi ni
Mashia na kwamba kwa
vile jeshi la Iraq na serikali
ya Iraq inadhibitiwa na
Mashia, basi Marekani
inashirikiana na
i n a wa s a i d i a M a s h i a
kuzuia Dola ya Kiislamu
kusimama Syria na Iraq.
Sisi tulisema kuwa
mashambulizi ya Marekani
hayalengi kuwamaliza
IS, wala Marekani
haiwashambulii IS, bali
inachofanya Marekani ni
kutumia kisingizio cha
kuwashambulia IS kupiga
na kuharibu miundo
mbinu na viwanda vya
Syria, kama mkakati
wa kumdhoofisha na
hatimaye kumngoa
Bashar Assad. Lakini pia
IS kuingia Iraq, ni namna
ya kukuza mgogoro wa
Shia na Sunni (Waislamu)
n a k u a c h a wa u wa n e
wenyewe kwa wenyewe.
IS kuwepo Iraq na tangazo
na Marekani kuwa
inapeleka jeshi kuwapiga,
ni kisingizio tu cha
kurejesha na kubakisha
jeshi la Marekani katika
nchi hiyo ikizingatiwa
kuwa ilishatangaza
kuondoka. Na hadi sasa
wakati Marekani ikidai
kuwa inawapiga IS, bado

Mashabiki wa Abu Baghdad mnasimama wapi!


Kama Iraq ni tatizo la Shia kuzuiya Khilafah
Yemen napo Waarabu wanachopigania nini?

Picha Juu na chini ni wapiganaji wa Yemen waliomuondoa Rais madarakani

MAKOMBORA ya Saudi Arabia yaliyopo mpakani yakielekezwa Yemen.


Marekani inawapelekea
silaha IS na usaidizi wa
kila namna kama ambavyo
imekuwa ikifichuliwa

na hata na jeshi la Iraq


linalodaiwa kusaidiwa na
Marekani kuwapiga IS.
Pa m o j a n a u k we l i

huo, bado waliokuwa


wakitukashifu kuwa ni
Mashia na tunaungana
na Mashia (Jeshi la Iraq)

likisaidiwa na Marekani
kuzuiya Dola ya Kiislamu,
Iraq na Syria, walibaki na
msimamo wao wakisubiri
Dola ya Kiislamu
kusimama Iraq na Syria
chini ya ISIS.
Katika Yemen, kundi
linalojulikana kwa jina la
Ansar Allah (anr allh
- "Supporters of God"),
m a a r u f u k wa j i n a l a
Houthis (al-thiyyn),
likitokana na jina la
kiongozi wao wa awali
Hussein Badreddin alHouthi,
ambao ni
Mashia wa dhehebu la
Zaidi Shia, wamemtimua
madarakani Rais wa nchi
hiyo Abdrabbuh Mansour
Hadi.
Labda tuulize,
k wa wa l e wa l i o k u wa
wakisema kuwa Marekani
inawasaidia Mashia
kuzuiya kusimama Dola ya
Kiislamu ya Abu Baghdad,
katika mgogoro huu wa
Ye m e n wa p o u p a n d e
gani. Je, wapo upande wa
Saudia Arabia na Israel
wanaowapiga Houthi au
wapo upande wa Houthi.
Na je, wanachotafuta
Israel, Marekani na Saudia
Arabia, ni kuzuia Ushia
kusimama Yemen? Kama
utasema ni kuzuiya Ushia
kuchukua madaraka
Yemen, mbona katika Iraq
ni Mashia na Marekani
wa n a o wa p i g a I S . N a
je, mbona katika Syria
ni Masuni walioungana
na Marekani na Israel
kuwapiga Mashia?
Hivi sasa Saudi Arabia
ikisaidiana na Israel
(Israeli Fighter Jets Join
Saudi Arabia in War on
Yemen), inawashambulia
wapiganaji wa Houthi.
Lakini kwa upande
mwingine pia Marekani
japo haijapeleka jeshi,
lakini imetangaza kuwa
inaisaidia Saudia Arabia na
muungano unaoundwa na
nchi za Kiarabu kuwapiga
Mashia wa Houthi. Jingine
ni kuwa wakati Marekani
i n a e n d e l e a k u wa p i g a
Masuni wanaodaiwa
kuwa ni Al-Qaidah,
haiwapigi Houthi. Lakini la
ziada ambalo limejitokeza
ni kuwa wakati Marekani
inasaidiana na Israel, Saudi
Arabia na muungano wa
nchi za Kiarabu kuwapiga
H o u t h i , k wa m l a n g o
wa n y u m a i n a t a f u t a
kuwasiliana na Houthi
waliomtimua Rais wa
Yemen na kuwahakikishia
Inaendelea Uk. 11

11

AN-NUUR

Makala

JAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 3-9, 2015

Siasa za mabeberu Iraq na Yemen


Inatoka Uk. 10

kuwa watakuwa pamoja


nao.
Last week, Obama
administration officials were
scrambling to contact Houthi
leaders and assure them that
the United States doesn't
consider them an enemy.
Ndivyo linavyoripoti
gazeti la Los Angeles
Times.
We're talking with
everybody everybody who
will talk with us.
Los Angeles Times,
lilimnukuu Afisa mmoja
wa White House akisema.
(Tazama: Why the U.S. is
courting the Houthis taking
control in Yemen-By Doyle
McManus, LOS ANGELES
TIMES)
Hii tafsiri yake ni kuwa
Marekani inataka Houthi
wabakie kuwa na nguvu
kama walivyo IS kule
Syria na Iraq ili Waislamu
(Shia na Sunni), waendelee
kuuwana katika Yemen.
Katika Syria, vyovyote
utakayotizama,
wanaouwana ni Waarabu
wa Syria na Waislamu
wa Syria. Katika Iraq,
wanaouwana ni Waarabu
wananchi wa Iraq, ni
Waislamu kwa Waislamu
wanaouwana kama
ambavyo katika Somalia
wanaouwana ni Wasomali
kwa Wasomali, Waislamu
kwa Waislamu.
Katika Yemen hivi sasa
kuna hatari inayotaka
kujitokeza, kwa kuingia
Saudia Arabia kijeshi
Yemen kuwapiga Houthi
ambao inaaminika kuwa
wanasaidiwa na Iran,
ipo hatari Hizbullah
kuingia katika mgogoro
huo kuwatetea Houthi
(Mashia). Lakini ipo hatari
pia kwa Iran kuingia. Na
hiyo itakuwa ni vita ya
Waislamu kwa Waislamu.
We ukisema wale Mashia
au wale Masuni, haibadili
kuwa wanaopigana ni
Waislamu na kama ni
miji na nchi kuharibika,
inayoharibika ni miji na
nchi za Waislamu.
Taarifa kutoka Iraq
z i n a f a h a m i s h a k u wa
wapiganaji wa KishiaIraq Iraqi Militiamen,
wanajikusanya kwenda
k u p i g a n a Ye m e n
kuwasaidia Houthi
dhidi ya Saudia Arabia
na muungano wake wa
Waarabu wanaosaidiwa
na Marekani na Israel.
(Tazama: Iraqi Militiamen
Plan To Travel To Yemen To
Battle U.S.-Backed Coalition)
Tu m e w a p i g a n a

wa Kishia, wapo pamoja


na Marekani wakipigana

dhidi ya Islamic State. Sasa


katika Yemen, Marekani ipo
pamoja na Masuni wa Saudia
Arabia na Misri kupigana
dhidi ya Mashia, Houthi.
Kwa upande mwingine
litizame hivi: Katika Syria,
Marekani inampiga Bashar
Assad wakati Iran ikimuunga
mkono. Katika Iraq namna
yake ni kama Iran ipo pamoja
na Saudi Arabia na Marekani
kuwapiga IS. Inapokuja
katika Yemen, mahesabu
yanabadilika. Marekani ipo
na Saudia Arabia kuwapiga
Houthi na hivyo kuipiga Iran.
Ni kama alivyojisema
aliyekuwa kachero wa CIA
katika kikosi cha kupambana
na Osama Bin Laden, Michael
Scheuer, pale aliposema:

The thing was ideal when


IS was advancing on Baghdad
because Sunnis were killing
Shias. That's exactly what
we need. - Our best hope
right now is to get the Sunnis
and Shias fighting each other
and let them bleed each other
white."

Hassan-Nasrallah, kiongozi wa Hezbollah

PICHA juu na chini ni wapiganaji wa Kishia

kuwashinda ISIS Syria,


hivi sasa tunawapiga
na kuwaangamiza ISIS
ndani ya Iraq, tutawapiga
pia Yemen, amesema
Abu Kumael, ambaye ni
mmoja wa wapiganaji wa

kundi la Kishia la Iraq


likijulikana kwa jina la
Peace Brigades.
Sisi sio wapiga porojo,
sio watu wa kusema ovyo,
tuko imara na tutawapiga
na kuwashinda Wasaudia

na washirika wao,
aliongeza mpiganaji
huyo. Kundi jingine la
Kishia ambalo linajiandaa
kuingia Yemen ni lile la
Badr Organization.
Katika Iraq, wapiganaji

(Tazama: Channel 4 Regrets


Letting Ex-CIA Agent Claim
Baghdad Massacre Would Have
Been 'Ideal')
Katika vita ya Syria na
I r a q , a m b a p o i m e k u wa
ikitangazwa kuwa IS
wamekuwa wakiuwa Mashia
na kuharibu misikiti na taasisi
zao, kiongozi wa Hizbullah,
Nasrallah alijitahisi sana
kuwazuiya wapiganaji wake
kujiingiza kwa vita hiyo kwa
sababu itakuwa ni kunasa
katika mtego wa maadui
wa Uislamu na mabeberu
wanaotaka kuisambaratisha
Mashariki ya Kati. Iran, kama
serikali, nayo ilifanya hivyo.
Inavyoelekea hili la Yemen
a m b a p o m j u m u i k o wa
Saudi Arabia, Misri, Qatar,
Jordan, Bahrein, wakisaidiwa
na Israel na Marekani
wanaw apiga Houthi, ni

katika juhudi mpya za


Mabeberu za kuwaingiza
Waislamu kwa maana ya
Mashia na Sunni, katika
vita ya wenyewe kwa
weyewe. Kama alivyosema
kachero wa CIA Michael
Scheuer, wamwage damu
zao mpaka wakauke-Our
best hope right now is to
get the Sunnis and Shias
fighting each other and
let them bleed each other
white."
Sasa sisi badala ya kukaa
kitako na kuangalia namna
ya kujinusuru na njama
hizi za makafiri, tukae tu
na tamaa za fisi kuwa Abu
Baghdad anatupigania
kusimamisha Khilafah
na akitoka huko analeta
Khilafah hiyo kwetu!

12

MAKALA

NONGWA YA MAHKAMA YA KADHI


Adayo hupendeleya, wa dinenu wapinzani,
Mazuri kuyazuiya, yenu pasi hata soni,
Kukuswibuni mabaya, wao ndilo hutamani,
UKWELI wa QUR-ANI, si kombo u dhahiriya.
Daima huwatakiya, yale yanokudhuruni,
Ya shururi huridhiya, ninyi yanokufikeni,
Ya khairati udhiya, yenu kwao ng'amueni,
UKWELI wa QUR-ANI, si kombo u dhahiriya.
Gaidhi i dhahiriya, kutoka mwao vinywani,
Vyanda wanawaumiya, kwa indazo mitimani,
Waloficha batiniya, kungaye i kwa MANANI,
UKWELI wa QUR-ANI, si kombo u dhahiriya.
Si kwamba nawazuliya, ishanena QUR-ANI,
SURA ya TATU rejeya, si nyingine IMRANI,
AYA nawakashifiya, hayo zenye kubaini,
UKWELI wa QUR-ANI, si kombo u dhahahiriya.
MIATU wa THAMANIYA, ASHARA kwa tamakuni,
Soma thuma endeleya, hadi MIA ISHIRINI,
Humo utajioneya, yote kwa wake ndani,
UKWELI wa QUR-ANI, si kombo u dhahiriya.
ALLAH alotuambiya, si dhahania yakini,
Wenyewe mwashuhudiya, yawahusu wao nini!
MAHKAMA kugomeya, ya KADHI mahakamani?
UKWELI wa QUR-ANI, si kombo u dhahiriya.
Na hofu wamewatiya, viongozi wa nchini,
Si kwa hoja usuliya, kwa pogo yao mizani,
Lengo walokusudiya, lipate kuyumkini,
UKWELI wa QUR-ANI, si kombo u dhahiriya.
Nudhumu namaliziya, kwa nyote kukuombeni,
Kujifunza kuteteya, kwa pamoja yenu dini,
'Wenzenu' huwa pamoya, kwa yao hamuwaoni?
UKWELI wa QUR-ANI, si kombo u dhahiriya.
ABUU NYAMKOMOGI-MWANZA.

SHAIRI LA BABA
Mimi nina sikitiko, limenijaa moyoni,
Nimepata fadhaiko, wa kufariji nani,
Juhudi zangu ni mwiko, wana hawazithamini,
Baba nae ni mzazi sifa anastahiki.
Kila nikijitahidi, sifa sipewi kwa nini,
Mbona hamna miadi,nyinyi ni watoto gani,
Au mwafanya kusudi, mnitoe duniani,
Baba nae ni mzazi, sifa anastahiki.
Zote mwelekeza sifa kwa mama mzazi,
Baba mi mmenibeza, hamjali yangu kazi,
Leo nawabembeleza, au niachie ngazi,
Baba nae ni mzazi, sifa anastahiki.
Mimi kwenu kama baba, nawajibika kwa mengi,
Jukumu langu ni kubwa, na tena ni la msingi,
Si tu kuleta ubwabwa, mkafaidi mitungi,
Baba nae ni mzazi, sifa anastahiki.
Mtume katuhimiza, kuwashukuru wazazi,
Hakuna alo m-beza, na kuweka pingamizi,
Japo mama ni wa kwanza, ila baba ni farazi,
Baba nae ni mzazi, sifa anastahiki.
Shime tuwapeni sifa, mababa zetu jamani,
Wamelijenga taifa, malipo yao kwa nani,
Tusisubiri wakafa, wakaenda kuzimuni,
Baba nae ni mzazi, sifa anastahiki.
Hayo tukiyatimiza, tutapunguza majonzi,
Nyoyo tutazisuuza, na kuondosha simanzi,
Mababa watatutunza, na kuboresha malezi,
Baba nae ni mzazi, sifa anastahiki.
Sasa ninahitimisha, wasia wangu jamani,
Yatosha nilokumbusha, wanangu tekelezeni,
Dharau kutozidisha, wazee tutaabani,
Baba nae ni mzazi, sifa anastahiki.
Zainab Mtima,
Mbweni- Zanzibar.
0717 165 602

AN-NUUR

JAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 3-9, 2015

Ni nani hasa washenzi - Nchi za


Magharibi au Waislamu?

Inatoka Uk. 9
Wa a r a b u wa l i u n d a
utamaduni wenye undani wa
elimu na kuonyesha njia ya
kuvumiliana, unaojumuisha
watu wa mataifa mbalimbali,
imani na lugha -hivyo kutoa
msukumo wa maendeleo
ya kila kitu kutoka hisabati
na unajimu, sayansi ya tiba,
ushairi na mawazo ya hali
ya baadaye ya ustaarabu
duniani, elimu, sheria na
haki, ubunifu majengo
unaostahimili nguvu
ya uvutano, hadi kufikia
maktaba ya kisayansi na
mengi zaidi.
Dunia ya Kiarabu na
Kiislamu ilishindwa kutoa
kiongozi yeyote mwenye
upeo na uadilifu kifikra
ili kuendana na hali
inayobadilika duniani
na masuala magumu ya
kimataifa karne ya 21.
Wakati Waarabu wakiwa
wanaongoza katika Imani
('Emaan') na maadili ya
kibinadamu, waliinua
utamaduni wa aina yake
unaokubali tofauti za
kiimani na tamaduni tofauti
za kijamii na kujenga kupitia
msingi wa umoja wa imani ya
Kiislamu kustawisha kuishi
kwa amani na maendeleo ya
binadamu. Ukiorodhesha
uvumbuzi na michango
ya wasomi wa Kiislamu,
hayahesabiki. Je, unajua
wanasayansi wengine au
wanazuoni ambao michango
yao ilitumika katika vitabu
vya kufundishia kwa
karne sita katika vyuo vya
tiba barani Ulaya? Fikiria
Muhammad Hussein bin
Ali Sina na Kanuni za
Msingi za Tiba. Wazungu
walibadili jina lake kuwa
Avicenna hivyo hakuna mtu
angejua kwamba alikuwa
mwanazuoni wa Kiislamu.
Inasemekana Ibn Sina pekee
aligundua na kuwezesha
kuthibitishwa dawa za aina
36 zinazoendelea kutumika
hadi sasa. (Angalia tungo ya
Marai Rosa Menocal - Enzi
Kuu ya Kuvumiliana: Pambo
la Dunia: Jinsi Waislamu,
Wa ya h u d i n a Wa k r i s t o
Walivyounda Utamaduni
wa Kuvumiliana katika
Hispania ya Kimwinyi,
iliyochapishwa 2003).
Anaeleza kuwa "mafunzo ya
historia, kama mafunzo ya
dini, mara nyingi hupuuza
mifano ya kuvumiliana.

Miaka elfu moja iliyopita


katika Peninsula ya Iberia
(Ulaya Kusini), mwelekeo
wenye hisia za kimaendeleo
wa Uislamu ulikuwa
umejenga utamaduni wa
hali ya juu zaidi barani Ulaya
.... Huko Cordoba, maktaba
yake ilikuwa na vitabu
400,000 wakati ambapo
maktaba kubwa katika eneo
la Ukristo wa Kilatini barani
Ulaya haikuwa na zaidi ya
vitabu 400. "
Kushusha mapipa ya
mabomu kila siku nchini
Syria, ulipuaji wa mabomu
ya kutegwa kwa gari jijini
Baghdad, uasi wa ki-Shia wa
Houthi unaofadhiliwa na Iran
nchini Yemen, mapambano
yanayosababisha vifo
vingi katika mitaa ya Cairo
na Tripoli - mamilioni
wanaondolewa na kufutika
kila sekunde kana kwamba
s i b i n a d a m u . Yo t e h i i
i n a o n ye s h a u t a m a d u n i
ulioparaganyika wa nchi za
Kiarabu wenye mwenendo
wa kutisha usioweza
kurudishwa nyuma. Hali
ya baadaye inatiwa giza na
nguvu za uovu. Utumiaji

silaha na chuki vinazamisha


kwa haraka upana wa jamii
za Kiarabu na Kiislamu
katika mawimbi ya vifo
na kuvunjiliwa mbali kwa
jamii. Takwimu za mauaji ya
kila siku hujenga kiwewe

katika vyombo vya


habari kinachoendana
na alichosema Samuel
Huntington (mada
ya "Mtafaruku wa
Ustaarabu," katika jarida
la Mambo ya Nje nchini
Marekani mwaka 1993),
akidai kuwa "Uislamu una
mipaka ya damu."
(Dk. Mahboub A.
Khawaja ni mtafiti
wa usalama, amani
na kutatua migogoro
duniani na ulinganishi wa
tamaduni za Magharibi
na Kiislamu, na ntunzi
wa m achapisho kadhaa
ikiwa ni pamoja na kitabu
cha hivi karibuni, "Amani
ya Dunia na Usuluhishi
wa Migogoro: Binadamu
na Watu Wanapotafuta
Fikra Mpya," kilichotolewa
na Lambert Academic
Publishing
nchini
Ujerumani, Mei 2012.)

KIDATO CHA TANO NA KURUDIA MITIHANI

ILALA ISLAMIC SECONDARY

USAJILI
S.2401

KWA WASICHANA TU

IPO: ILALA-AMANA-MTAA WA ARUSHA: MASJID SHAFII


SHULE YA BWENI NA KUTWA

MASOMO

Math, Phy, Chem, Bios, Geo, Civ, Eng, Kisw, Commerce,


B/keeping Islamic, Arabic na Tahfidhul Quran
COMBINATION
PCM,PCB,CDG,HGL,HGK,HGE,HKA,HEA
UFAULU 2014
KIWILAYA 3/76, KIMKOA 10/191, KITAIFA 118/2322
Kwa shule za kiislam KIWILAYA (1) KIMKOA (2) KITAIFA (5)
Zipo nafasi za kuhamia kidato cha II, III na IV, V
MAWASILIANO
Simu: 0713 007586, 0715 187515, 0714 393822,
0714 381964

DAR ES SALAAM ISLAMIC SEC.

USAJILI
S.4384

KWA WAVULANA TU

Ipo Ilala-Bungoni: Masjid Taqwa


MASOMO
Math, Phy, Chem, Bios, Geo, Civ, Eng, Kisw, Commerce, B/
keeping Islamic, Arabic na Tahfidhul Quran
COMBINATION
PCM,PCB,CDG,HGL,HGK,HGE,HKA,HEA
UFAULU 2014
Kama Ilala Islamic, imetenganishwa toka Ilala Islamic
Zipo nafasi za kuhamia kidato cha II, III na IV, V
MAWASILIANO
Simu: 0713 007586, 0715 187515, 0714 393822, 0714 381964
Ada ni nafuu na inalipwa kwa awamu nne
MLETE MWANAO APATE ELIMU NA MALEZI BORA

13
Na Khamis Haji (OMKR)

K AT I B U M k u u wa
C UF, Mhe. Maalim
Seif Sharif Hamad,
amehudhuria mazishi
ya Hemed Salum Hemed
(38) aliyefariki katika
ajali ya barabarani
iliyotokea wakati
akirudi katika mkutano
wa hadhara wa chama
hicho uliofanyika
Makunduchi Wilaya ya
Kusini Unguja.
Marehemu ambaye
ni mkaazi wa Kinuni,
Wilaya ya Magharibi
Unguja aliswaliwa
katika Msikiti Ngamia,
Kilimahewa na kuzikwa
Kianga, mkoa wa Mjini
Magharibi Unguja.
Aidha, Maalim Seif
aliwatembelea na
kuwawafariji baadhi ya
wafuasi wa chama hicho
waliojeruhiwa na watu
wasiojulikana wakati
walipokuwa wakirudi
katika mkutano huo
walipofika eneo la Fuoni.
Tukio la kujeruhiwa
wafuasi 24 wa chama
cha CUF waliokuwa
wakitokea katika
mkutano wa hadhara
huko Makunduchi,
ambao wengi wao
walikuwa ni vijana,
lilitokea hivi karibuni
kufuatia vijana
waliokuwa katika gari
eneo la Fuoni Taveta
wakiwa na mapanga,
nondo na mawe
kuwarushia mawe
Kwa mujibu wa Naibu
Mkurugenzi wa Haki
za Binadamu wa CUF
Bi. Pavu Juma, alisema
baadhi ya majeruhi
hao walipata majeraha
makubwa na wamelazwa
k a t i k a h o s p i t a l i ya
Mnazimmoja na wengine
wamesafirishwa hadi
D a r e s S a l a a m k wa
matibabu zaidi.
M a p e m a
akiwatembelea baadhi
ya majeruhi huko
Mwembemakumbi,
Katibu Mkuu huyo
wa CUF, Mhe.
Maalim Seif Sharif
Hamad, alisema watu
waliowajeruhi wafuasi
wa CUF wamefanya
hivyo baada ya chama
chao kukosa sera za
kuwaeleza Wananchi
n a s a s a wa m e a m u a
kufanya hujuma
ambazo amesema
hazitowasaidia.

HABARI

AN-NUUR

JAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 3-9, 2015

Maalim Seif ahudhuria mazishi

Awapa pole walioshambuliwa


Awasihi CUF kuwa watulivu

KATIBU Mkuu wa CUF, Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad (wa tatu kutoka kulia),
akihudhuria mazishi ya Hemed Salum Hemed (38) aliyefariki katika ajali ya
barabarani iliyotokea wakati akirudi katika mkutano wa hadhara wa chama hicho
uliofanyika Makunduchi Wilaya ya Kusini Unguja hivi karibuni.

Alirejea wito wake wa


kuwataka wanachama
na wafuasi wa CUF wawe
watulivu na kwamba,
chama hicho kinafuatilia
kwa karibu hujuma zote
zinazofanywa dhidi yao.
Awali Maalim
Seif Sharif Hamad,
aliwanasihi wanachama
wa chama hicho
kushikilia msimamo
wao wa kuendesha siasa
za kistaarabu na kuacha
kufikiria kulipiza
kisasi kufuatia hujuma
zinazofanywa dhidi ya
chama hicho.
Alisema lengo
kubwa la hujuma hizo,
zikiwemo kuchomwa
moto kwa ofisi za chama
hicho ni kutaka kukitoa
chama katika malengo
ya k e ya k u p i g a n i a
haki za wananchi na
kwamba, njama hizo
hazitoweza kufanikiwa.
Nakunasihini sana
wanachama wa CUF
msichokozeke, hawa
wanaofanya hujuma hizi
wana lengo la kututoa
katika malengo yetu ya
kupigania haki, lakini
nakuombeni musiuingie
mtego huo, alisisitiza
Maalim Seif.

Maalim Seif alitoa


nasaha hizo wakati
akihutubia mkutano wa
hadhara wa chama hicho
uliofanyika viwanja
vya Jamhuri, jimbo la
Makunduchi.
Alitumia nafasi hiyo
kuwashukuru wananchi
wa Makunduchi
k wa m wa m k o wa o
waliouonyesha katika
kukiunga mkono chama
hicho, ambapo jumla
ya wanachama wapya
584 walijiunga na
CUF katika mkutano
huo, miongoni mwao
wakiwemo makada wa
Chama Cha Mapinduzi.
Alisema hatua
hiyo inadhihirisha
jinsi wanachama wa
CUF katika maeneo
mbalimbali nchini
wa n a v y o w e z a
kuungana kwa ajili
ya kutetea haki zao
bila ya kujali maeneo
wanayotoka.
Akizungumzia
mipango ya chama hicho,
Maalim Seif, alisema
chama kinakusudia
kuleta mabadiliko kwa
kujenga uchumi imara
ambapo kila mwananchi
ataweza kunufaika na

rasilimali zilizopo.
Zanzibar inazo
rasilimali na fursa
nyingi za kiuchumi
lakini bado hazijatumika
ipasavyo kuwanufaisha
wananchi wa kipato
cha chini, endapo CUF
kitashika hatamu za
dola, kitaziibua fursa
h i z o n a k u wa f a n ya
vijana wengi kuweza
kupata ajira katika sekta
mbalimbali zikiwemo
kilimo, uvuvi, biashara,
utalii na viwanda vidogo
vidogo. Alifafanua
Katibu Mkuu huyo.
Kuhusu katiba
inayopendekezwa,
Maalim Seif ambaye pia
ni Makamu wa Kwanza
wa Rais wa Zanzibar
alisema Serikali bado
haijawahi kukaa na
kutoa msimamo juu
ya k a t i b a h i y o , n a
kufafanua kuwa hakuna
msimamo wa serikali
juu ya jambo hilo.
Alisema mawazo
yanayoendelea
kutolewa kuhusiana na
katiba hiyo, yanabakia
kuwa misimamo ya
vyama na siyo msimamo
wa serikali kama
inavyodaiwa na baadhi

ya viongozi wa kisiasa.
Mimi nikiwa
Makamu wa Kwanza
wa Rais, kama Serikali
hatujawahi kukaa
kwenye Baraza la
Mapinduzi wala kikao
chochote cha kiserikali
kujadili au kutoa
msimamo kuhusu katiba
inayopendekezwa, sasa
i n a k u wa j e we n g i n e
wanasema msimamo wa
serikali ni huu, alihoji
Maalim Seif.
Kwa upande wake
Naibu Katibu Mkuu
wa CUF Zanzibar,
Nassor Ahmed Mazrui,
alisema mwaka 2015
ni mwaka wa wana
CUF kufanya maamuzi
ya kukiweka chama
hicho madarakani kwa
kukiwezesha kupata
ushindi mkubwa katika
uchaguzi mkuu ujao.
Katika mkutano
huo, wazee wa
CUF Makunduchi
walimkabidhi Maalim
Seif, ufunguo maalum
kwa ajili ya kuifungua
Zanzibar ambayo
wamedai kuwa
imekwama kwa zaidi
ya nusu karne sasa.
Kabla ya kuhutubia
mkutano huo, Katibu
Mkuu huyo alifanya
ziara ya kutembelea
barza na matawi ya
CUF na kupata fursa
ya kuzindua na kuweka
mawe ya msingi katika
matawi na barza hizo,
zikiwemo mbili za
akinamama.
Katika ziara hiyo,
Maalim Seif ambaye
aliambana na Naibu
Katibu Mkuu wa CUF
Zanzibar, aliwahimiza
wanachama wa barza
hizo kuanzisha matawi
kamili kutoka na idadi
kubwa ya wanachama
waliyonayo.
Miongoni mwa
barza na matawi
ya l i y o z i n d u l i wa n a
kuwekewa mawe ya
msingi ni pamoja na
Barza ya Kizimkazi
D i m b a n i , B a r z a ya
Ukawa ya Nganani,
Barza ya Ismail Jussa ya
Kitundani, Fatma Ferej
Madete Barza na Tawi
la CUF Shakani.
Wanachama wapya
waliojiunga na CUF
kutoka CCM ni pamoja
na aliyekuwa mjumbe
wa Baraza la Wazazi
Wilaya ya Kusini Bw.
Yahya Mkongoa Ali na
aliyekuwa mhamasishaji
wa CCM katika eneo
hilo Bi. Kihamba Ali
Ronge.

14

Makala

AN-NUUR

JAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 3-9, 2015

Mchango wa Waislmau katika maendeleo ya Dunia

Thabit Ibn Qurra (5)

Na Ben Rijal
Na Ben Rijal
MAKALA hii itamuangalia
Mwanasayansi, mjuzi wa
elimu ya nyota na hesabati
Al-Sabi Thabit ibn Qurra
al-Harrani alioishi kutika
mwaka wa 826 hadi 901.
Thabit ibn Qurra alikuwa
akifahamu lugha ya
Kiyunani vilivyo na ufahamu
wake huo ulimuwezesha
kuzitafsiri kazi mbalimbali
zilizoandikwa na Wayunani.
Thabit ibn Qurra alikuwa
ni mjuzi wa hesabati na elimu
ya nyota. Aidha akiheshimika
na uelewa wa taaluma ya
utibabu. Thabit ibn Qurra
alizaliwa katika mji wa
Harran uliokuwa ukijulikana
kwa jina la Carrhae katika
nchi ya Uturuki, anatokana
na kizazi cha waliokuwa
wakiabudu nyota katika dini
ya Sabian.
Kutokana na uelewa wake
wa lugha ya Kiarabu na
Kiyunani, Thabit Ibn Qurra
aliheshimika pakubwa
h a s a k a t i k a u wa n j a wa
wana taaluma. Alikuwa
Muhammad ibn Musa ibn
Shakir baada ya kutambua
kipawa alichokuwa nacho
Thabit Ibn Qurra alimtaka
ahamie mji wa Baghdad nchini
Iraq kwani hapo kulikuwa
ndio kiringe kikuu cha wana
taaluma wa zama hizo.
Inafahamika kuwa msomi
huyu alijishughulisha katika
maisha yake yote kujifunza
hesabati, kutizamia, elimu
ya nyota, uchawi, somo la
makenika, utibabu na falsafa.
Thabit aliishi katika uongozi
wa A b a s s i a n a a l i k u wa
mwenzani mkuu wa kiongozi
al-Mutadid alioishi kutoka
mwaka wa 899-902.
Ramani iliopo hapo
j u u i n a o n ye s h a v i g o g o
vya Kiislamu waliofanya
kazi kubwa katika midani
ya hesabati inakadiriwa
kufikisha miaka 600 tangu
ilivyochorwa.
Katika kazi za kisomi
ambazo
zilikuwa
hazifahamiki nje ya Uyunani,
ziliweza kujulikana kutokana
na Thabit Ibn Qurra, kwani
uwezo wake wa kuelewa
lugha ya Kiyunani na
Kiarabu ulikuwa mkubwa,
aliyafanyia tafsiri maandiko

THABTB Ibn Qurra

RAMANI inaonyesha sehemu ya alipozaliwa Thabit


Ibn Qurra.

ya Hellenistic na Kiyunani
na kuyaandika kwa lugha
ya Kiarabu. Utastaajabu kwa
wakati huo mtu kama yeye
kuwa na nyezo haba akiweza
kuandika miswada na tafsiri
mbalimbali za kitaaluma,
wengine walimvulia kofia
kutokana na kuweza kutafsiri
maandiko ya kale na kuyapa
ufafanuzi.
Suala la kuwa na siku
sawa katika mwaka yaani
kwenye mwaka miongo
huwa haipishani kinyume
na maeneo mengine ambayo
miongo hupishana, kiangazi
huwa mchana mrefu na usiku
mfupi wakati wa Kipupwe
huwa mchana mfupi na usiku
mrefu, Thabit Ibn Qurra
alizama kutaka kujuwa
kile kinachofanyika katika
mzunguko wa dunia kuwa
katika baadhi ya maeneo
ni kitu gani huwa miongo
haibadiliki (Equinox). Kazi
yake hio kubwa ilikuja
kuheshimika kwani katika
nyakati hizo wasomi
walikuwa wakibishana na
kuhangaika na kila mmoja
wao kuja na dhana yake,
lakini Tahbit Ibn Qurra
maandiko yake yalikuja
kukubalika katika uga wa
kitaaluma.
Thabit Ibn Qurra alifanya
utafiti wa kujua katika mwaka
kwa kufwata kalenda ya jua
mwaka unakuwaje uwe na
siku 365, kwani kuna miezi
huwa na siku 30 na miezi
kuwa na siku 31, kinyume
na mwaka unaofwata
mwezi ikiwa miezi kuwa na

siku 29 au 30 msomi huyu


alifanikiwa baada ya utafiti
alioufanya kujuwa mwaka
una siku 365, masaa 6 na
sekunde 12 kukiwa na tafauti
ndogo kabisa ya sekunde
2. Kazi hii aliifanya kwa
kulifwatilia jua kuchomoza
na kuzama kwa miaka na
baada ya hapo akachapisha
kazi yake ya kulichunguza
jua kazi ambayo kwa wakati
wake ilikuwa ni chachu ya
kufahamu wakati na siku
pamoja na kalenda. Aliweza
kuandika juu ya nyenendo
za sayari na kuhoji juu ya
maandiko ya fani hiyo ya
Arestotelian.
Ufahamu wake wa hesabati
uliokuwa mpana ulimfanya
azipinge kazi za wataalamu
na magwiji ya nyota
waliomtangulia Rosenfeld na
Gregorian. Aliweza kuandika
mswada ulioangalia kazi
za Archimedes katika
suala la mgando
na
umekanika. Thabit Ibn Qurra
inasemekana kuwa alifanya
kazi kubwa kuzipitia tafsiri
mbalimbali zilizoandikwa
kutoka lugha ya Kiyunani
na kutafsiriwa kwa Kiarabu.
Alianzisha Chuo cha kufanya
tafsiri na kukiongoza na
kutoikubali tafsiri yoyote
ile kuchapishwa kwa wakati
huo kabla ya yeye kuipitia na
kutia mkono wake.
B a a d h i ya k a z i z a k e
ambazo aliziandika kwa
mkono wake zipo hadi hii

AlJinn 72:, AlMuzzammil


73:, Al- Muddaththir 74:, AlQiyamah75:, AlInsan 76:,
AlMursalaat 77:, Annabaa
78:, Annazia'at 79:, A'basa
80:, Attakwir 81:, Al-Infit'aar
82:, Al- Mut'affifiin 83:, Al
Inshiqaaq 84:, Al Buruuj
85:, Att'aariq 86:, Al-Aa'laa
87:, AlGhaashiyah 88:,
Al Fajr 89:, Al Balad 90:,
Ash-Shams 91:, Al Layl
92:, Wadh-Dhuh'aa 93:, AshSharh' 94:, At-Tin 95:, AlA'laq 96:, AlQadr 97:, Al
Bayyinah 98:, Az-Zilzalah
9 9 : , A l - A ' a d i ya a t 1 0 0 : ,
A l - Q a a r i a ' h 1 0 1 : , At Takaathur102:, Al-A's'r103:,
Al-Humazah104:, Al
-FiiL105:, Quraish106:, AlMaau'n 107:, Al-Kawthar108:,
Al-Kafirun109:, Annas'r110:,
Al - Masad111:, AlIkhlas'112:, Al Falaq 113:,
Annas114:,
K u j i f u n z a b a a d h i ya
mambo na kuyajua
Surah zilizoteremka
Makka ni 86 na zilizoteremka
Madina 28, kuna Aya 6236
katika Quran.

Katika Quran kalima


Allah limetajwa mara 2698,
Salah imetajwa mara 700.
Quran katika mpangilio huu
tunaousoma umekusnywa
na Sahaba Syd Uthman
bin Affan na kusambazwa
katika maeneo mbalimbali.
Kwasasa kopi hizo za asili
zinapatikana mji wa Tashkent
katika nchi ya Uzbekistan na
Istanbul nchi ya Uturuki.
Mitume wanaojulikana
kwa jina la Ulul Azmi ni
Mtume Nuh, Ibrahim, Musa,
Issa na Muhammad SAW.
Surah Al Yusuf ndio Sura
pekee inayoelezea kisa kizima
cha Mtume akiwa Mtume
Yusuf kutoka mwanzo hadi
mwisho. Surat at Taha, 20:1
ndio Sura iliyomlainisha Syd
Ummar bin Khatab na ikawa
ndio sababu ya kusilimu
kwake.
Surah 6 zina majina ya
Mitume nazo ni: Surah-alYunus 10 :, Surah-al-Hood:11,
Surah-al-Yusuf 12:, Surah-alIbraheem 14:, Suah-al-Nuh
17:, Surah-al-Muhammed
47:.

Inaendelea Uk. 18

Jadweli katika Quran


Na Ben Rijal

KATIKA makala mbalimbali


zinazowasilishwa katika
gazeti letu hili huanishwa
kwa mfano Surah 2:12 au
22:15, 30:6 n.k. Baadhi ya
wa s o m a j i wa n a t a n z wa
kuelewa kinachomaanishwa.
Msahafu unaanza kuanzia
Suratul Fatha hadi Juzu ya
Ama na ina Juzuu 30.
Kwa hio inapoandikwa
2:12 ina maanisha ni SuratulBaqara Sura ya Pili na uangile
aya ya 12. Inapoandikwa
22;15 ni Sura ya Hajj aya ya
15 na 30:6 ina maanisha Sura
ta Ar-Rum aya ya 6.
Hapo chini zimeandikwa
Sura zote na mwandishi
akikuandikia utajua ufwate
vipi. Surah Sabaa aya ya 14
hio ina maana ni 34:14 na
ikiandikwa 34:14 ni Sabaa
aya ya 14
Mpangilio wa Sura:
Al-Faatih'a 1:, Al- Baqara
2:, Al-I'mran3:, An-NisaaI 4:,
AlMaida 5:, .Al-An-A'am

6:, Al-A'raaf 7:, AlAnfaal


8:, At-Tawba 9:, Yunus 10:,
Hud 11:, Yusuf 12:, Ar-Raa'd
13:, Ibrahim 14: Al-Hijr15:,
An-Nah'l 16:, Al-Israai
(Bani Israil) 17:, AlKahf
18:, Maryam19:, T'aha 20:,
AlAnbiyaa 21:, AlHajj 22:,
AlMuuminun 23:, AnNur
24:, AlFurqan 25:, AshShua'raa 26:, An-Naml 27:,
Al-Qas'as' 28:, Al-A'nkabut
29:, Ar-Rum 30:, Luqman 31:,
Assajdah 32:, Al-Ah'zab 33:,
Sabaa 34:, Faat'ir 35:, Ya-Sin
36:, Ass'affat 37:, S'aad 38:,
Azzumar 39:, Ghaafir 40:,
Fuss'ilat 41:, Ash-Shuura 42:,
Azzukhruf 43:, Addukhan
44:, AlJaathiya 45:, AlAh'qaaf 46:, Muh'ammad 47:,
Al- Fat-h'i 48:, Al-H'ujuraat
49:, Qaaf 50:, Adh-Dhaariyaat
51:, Att'ur 52:, Annajm 53:,
Al-Qamar 54:, Arrah'man 55:,
Al-Waaqia'h 56:, Al-H'adiid
57:, AlMujaadalah 58:, AlH'ashrI 59:, Al-Mumtah'inah
60:,Ass'af 61:, Al-Jumua'
62:, AlMunaafiqun 63:,
Attaghaabun 64:, Att'alaaq 65:,
Attah'riim 66:, AlMulk 67:,
AlQalam 68:, Al- H'aaqqah
69:, Al-Maa'rij 70:, Nuh' 71:,

15

Makala

AN-NUUR

JAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 3-9, 2015

Miti katika Quran na Mazingira-(3)


Na Ben Rijal
MAKALA mbili zilizopita
z i l i e l e z e a j u u ya m i t i
iliotajwa katika Quran na
baadhi ya miti ya madawa
i l i o m o k a t i k a Q u r a n .
Makala hii ya mwisho
itamurika miti inavyotoa
mchango katika maisha na
suala zima la tabia nchi.
Tu n a m a a n i s h a n i n i
maana ya tabia nchi? Ili
kuweza kuelewa maana ya
mabadiliko ya tabia nchi,
kwanza tuangalie maana
ya hali ya hewa. Kila siku
kunakuwa na mabadiliko
ya hali ya hewa mfano
tunapoamka asubuhi
hujikuta kuwa kumepoa
kwa kiasi fulani, mara jua
linapowaka tunaanza kusikia
joto, mara pepo zinavuma,
m a r a m v u a i n a n ye s h a .
Sasa huku kubadilika kwa
mabadiliko ya joto, baridi,
mara mvua, mara kuwe
shwari huitwa mabadiliko
ya hali ya hewa.
Tunapoangalia kwenye
telavisheni au kusikiliza radio
huambiwa juu ya hali ya joto,
baridi, mawingu, mvua kwa
lugha ya wataalamu wa hali
ya hewa huita, Utabiri wa
hali ya hewa katika masaa
24 yajayo.
Kuna maneno mawili siku
hizi yanakwenda sambamba
ingawa wengine huyafanya
yenye maana moja lakini
kwa kweli maneno hayo yana
maana tafauti. Ongezeko la
hali ya joto (Global warming)
na Mabadiliko ya tabianchi
(Climate change).
Hebu tuangalie ongezeko
la hali ya joto huja vipi?
Katika hewa kuna gesi
mbalimbali gesi hizo hujaalia
kuidhibiti hali ya hewa na
joto duniani, gesi ambazo
ni muhimu kabisa kwa
sayari yetu hii ni Hewa ukaa
(Carbon dioxide) Methane,
O z o n e , Wa t e r va p o u r ,
Nitrous oxide. Gesi hizo ndio
zinaochangia sayari yetu hii
kuweza kukalika, kwani jua
linapopiga kwenye sayari
yetu gesi hizi hulikinga na
kulipunguza kasi yake na
miale hio ya jua hurudi juu
na kuzunguka na kujaalia
sayari yetu hii kupozeka,
sasa zinapokuja kuongezwa
gesi kama hewa ukaa kwa
moshi unaozalishwa kutoka
viwandani, kuchoma mafuta
(Fossil fuel) au gesi ya
Methane kutoka mashamba
ya mpunga na mifugo, gesi
hizo zinapokwenda angani
hufanya kiwingu na kujaalia
ule mzunguko wa kawaida
kuwa haupo na kwa hio jua
linalopopiga duniani huja na
nguvu za ziada. Hali hio sasa
ndio tunaita ongezeko la hali
ya joto na hizo gesi huziita
gesi za Kijani za nyumbani
(Green house gases)
Baada ya kuona hali ya
hewa na kuona ongezeko la

VIWANDA vinazalisha hewa chafu na kuchafua anga.


joto sasa hali inayokuwa ya
mabadiliko ya hail ya hewa
ya siku nyingi kuanzia miaka
30 na kwenda juu huleta
mabadiliko ya hewa katika
nchi na mabadiliko hayo ndio
yanaitwa mabadiliko ya tabia
nch (Climate change.)
Mabadiliko ya tabianchi
duniani imekuwa ni
ajenda kuu duniani
kwani inamashaka ya kila
aina. Baadhi ya matokeo
mabaya yanayotokana na
mabadiliko ya tabianchi
ni mvua zisizo kuwa za
kawaida, ukame wa muda
mrefu, bahari kuvimba na
kuwafanya baadhi ya viumbe
vya baharini kushindwa
kuhimili mabadiliko hayo,
baadhi ya samaki kupotea,
maji ya chumvi kuvamia
visima vya maji matamu,
fukwe kumomongonyoka,
maeneo yaliozowea ubaridi
kubadilika na kuwa joto na
kuanza kushuhudia maradhi
yaliokuwa hayapo maeneo
hayo kuanza kujitokeza,
mfano Malaria kuonekana
katika maeneo ya Moshi,
Kilimanjaro, Mount Kenya
n.k. Viumbe vigeni ambavyo
havijakuweko kabla kuvamia
maeneo ya kilimo na bahari
na kuleta athari ya viumbe
asili kushindwa kunawiri
(Envasive species,) kilimo
kuathirika na mazao kushuka
na njaa kuingia katika nchi
nyingi za Kiafrika.
Matokeo ya mabadiliko

ya tabia nchi ni hatari na


yameweka hatima ya
walimwengu kuwa katika hali
ya hamkani. Walimwengu
walikutana katika mji wa
Kyoto uliopo Japan katika
mwaka wa 1997 mwezi wa
12 kujadili namna ya nchi
za viwanda kukubaliana
kupunguza uzalishaji wa
gesi za kijani za nyumbani
na gesi nyenginezo ambazo
huchangia ongezeko la joto
duniani na mabadiliko ya
tabia nchi. Itifaki hio ilifikiwa
makubaliano na kufanya kazi
katika mwezi wa Pili tarehe
16 mwaka wa 2005.
Itifaki ya Kyoto ni ya
kisheria kwa wale wote
walioridhia na kutakiwa
kupunguza uzalishaji wa gesi
hizo kwa asilimia 5.2%. Nchi
za viwanda ndizo zilizotakiwa
kupunguza na kuwekwa
kwenye Jaduwedi namba I
na nchi zinazoendelea wao
wakatakiwa wasaidiwe katika
kupambana na mabadiliko
ya tabia nchi na athari zake
pamoja na kusaidiwa kifedha
na kitaalamu na kupewa
teknolojia za kisasa kuweza
kuyabadilisha maisha ya
watu wao kiuchumi.
Nchi za Ulimwengu wa
tatu zikiwemo nchi za Kiafrika
wakatakiwa waingie katika
mpango wa kupanda miti ya
misitu kwa wingi ili kuweza
k u p u n g u z a h e wa u k a a
iliojaa angani pamoja na gesi
nyengine zilizokuwa hatari,

Fatilia kuandama kwa Mwezi

Leo Ijumaa ni tarehe 13 Jumada-at-Thania 1436 AH yaani


mfungo Tisa, tarehe 3 April 2015.
Tutaangalia kuandama kwa mwezi wa Rajabu tarehe April
19, 2015.
Tutaangalia kuandama kwa mwezi wa Shabana tarehe
May 18, 2015.
Tutaangalia kuandama kwa mwezi wa Ramadhani tarehe
June 16, 2015.
Kutoka leo Ijumaa ya tarehe 3 April hadi kufika Ramadhani
tumebakisha siku 84.
Mwezi utazaliwa tarehe 16 June 2015 saa 11:05 za jioni.
Juni 16 hautoonekna mwezi popote pale Duniani na tarehe 17
utaonekana kwa taklifu katika maeneo ya Kusini-Mashariki
ya Asia, Kaskazini mwa Afrika, Australia na Indonesia. Lakini
utaonekana kwa urahisi katika maeneo ya Afrika Mashariki
na sehemu mbalimbali za bara la Afrika. Ramadhani Mosi
itakuwa tarehe 18 Juni, 2015.

na mpango huo unajulikana


kama MKUHUMI (REDDReducing emissions
from deforestation and
degradation.)
Nini MKUHUMI?
MKUHUMI ni Mpango au
Mkakati wa Kupunguza
Uzalishaji wa Hewa Ukaa
itokanayo na Ukataji wa miti
ovyo na uharibifu wa Misitu.
Mpango huu ulianzishwa
na nchi zilizoendelea kama
njia moja wapo ya kutoa
motisha ya kifedha kwa
wahifadhi misitu katika nchi
zinazoendelea. Mpango
huu umebeba dhana kuu
tatu za kimsingi ambazo ni
ongezeko, uvujaji na hali ya
kudumu.
Ongezeko
Ongezeko ni shughuli
ambazo ni ongezeko kwenye
shughuli zinazoendelea
t a ya r i a u z i l i z o p a n g wa
zinakidhi kufikiriwa kupata
malipo ya Kaboni. Kwa hiyo
mdai lazima athibitishe kuwa
shughuli hizi zisingefanyika
kwa kutokuwepo mfumo wa
soko lakaboni.
Uvujaji ni ongezeko la
kiwango cha ufyekaji au
uharibifu wa misitu
kinachotokea nje ya mpaka
wa mradi na ambayo
inasababishwa na shughuli
za mradi. Uvujaji nikusema
unahifadhi kwako kisha
unakwenda kukata misitu
kwa wenzako.
Hali ya kudumu
Hali ya kudumu ni dhana
inayohusiana na muda wa
matokeo ya shughuli za
kukabiliana na mabadiliko
ya tabianchi. MKUHUMI ni
mpango ambao ukiutizama
n i m p a n g o t h a b i t i wa
kuweza kupunguza hali hii
ya ongezeko la joto lakini
wataalamu wa kizalendo
katika nchi za Ulimwengu
wa tatu wanaona ni kiini
macho, kinachohitajika
kikubwa ni nchi za viwanda
kupunguza uzalishaji wa
gesi za hatari kwa kiwango

k i l i c h o k u b a l i wa k a t i k a
itifaki ya Kyoto na vikao
mbalimbali vilivyofanyika
kutokea CopenheganDenmark, Cancun-Mexico,
Durban-Afrikak ya Kusini,
Doha-Qatar, Warsaw-Poland
na Lima-Peru na k ik ao
kijacho kitakuweko Paris
Ufaransa kuangalia namna
walimwengu watafikia vipi
upunguzaji wa hewa ukaa
na namna ya kusaidiwa nchi
zinazoendelea kupambana
na athari zitokanazo na
mabadiliko ya tabianchi.
Yanayoendelea juu ya
mpango wa MKUHUMI na
mafanikio yake :
Jee Suala la MKUHUMI
ina faida kwa Wananchi?
Hadi sasa tunaambiwa kuwa
unapopandisha miti ya misitu
unapunguza gesi ya hewa
ukaa kwahio kuna kipimo
maalumu kimeandaliwa
amabacho kitakuwezesha
kuuza gesi ukaa (Carbon
credit), mafanikio katika
uzaji wa gesi ukaa ni pale
wananchi watapokuja na
kupanda misitu ya kuwa ya
jamii, kwahio uuzaji wa gesi
ukaa utakuwa mkubwa.
Uislamu na upandaji wa miti
Imepokewa na Sahaba
Anas r.a anaeleza kuwa
Mtume SAW anasema Ikiwa
Qiyama kimewadia na moja
wenu amekuwa na mche
wa mtende basi ahakikishe
anatumia wakati huo uliobaki
kwa kupanda mti (Al-Albani)
Imepokewa kutokana na
Sahaba Anas kutoka kwa
Mtume SAW hadithi isemayo
Ikiwa Muislamu amepanda
mti au ameweka mbegu
ardhini baadaye ndege, watu
au wanyama wakafaidika
kutokana na mti ule hio huwa
ni sadaka (Bukhari)
Hadithi mbili hizi kama
Wa i s l a m u w a n g e k u w a
wamezizingatia, basi
MKUHUMI ungekuwa
umepamba moto kwa karne
katika nchi za Kislamu.
Inasikitisha leo kusikia
Muislamu tangu anazaliwa
hadi anafika kufa kuwa
hajawahi kupanda hata mti
mmoja. Waislamu katika
Misikiti, katika Maskuli
lazima wawe na mipango
maalumu ya upandaji wa
miti, ikiwa Misikiti yetu
tunaosali sala za Jamaa kuna
watu 50 tu na kila mtu kwa
mwezi anapanda miti 5
kutakuwa tumepanda miti
250 kwa mwaka miti 3,000
tuchukue kwa idadi hio hio
Misikiti 10 itapatikana miti
30,000 kwa hio waumini
tunaweza kuuza hewa ukaa
kama tutajipanga na kuitikia
wito wa Mtume SAW. Faida
tutapata ya kujipatia fedha za
halali hapa duniani na akhera
tutapata malipo tulioahidiwa.

16

Makala

AN-NUUR

JAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 3-9, 2015

Muifahamu Pasaka kabla ya kuisherehekea


JUMAPILI kesho kutwa,
Wakristo wanasherehekea
sikukuu ya kukumbuka kufa
na kufufuka Yesu Kristo,
k a m a wa n a v y o i t a k i d i ,
yaani Pasaka. Kwa mujibu
wa taratibu za Kikristo za
kusherehekea sikukuu hiyo,
leo Ijumaa wanafanya ibada
ya Ijumaa kuu makanisani,
siku ambayo wanaamini
kuwa saa tisa mchana Yesu
alikufa.
Alfajiri ya siku ya Jumapili,
ambayo ndiyo siku yenyewe
y a Pa s a k a , w a n a a m i n i
kwamba ndio siku Yesu
alifufuka.
Kwa Wakristo, dhana
ya kufa na kufufuka Yesu
n i n g u z o k u b wa n a ya
msingi wanayoitegemea
kusimamisha Ukristo.
Wa k a t i t u k i s h u h u d i a
Wakristo wakijiandaa Pasaka
na kukesha Makanisani,
wakiwa na imani ya
kutekeleza utamaduni
wa kiibada wa dini yao,
k wa u p a n d e m w i n g i n e
t u m a a n i n i p i a k wa m b a
wapo wasiokuwa Wakristo,
hasa Waislamu ambao bila
shaka watakuwepo ambao
nao wanajiandaa kikamilifu
kusherehekea sikukuu hiyo.
Tena inawezekana kabisa
wakawepo Waislamu ambao
wamejiandaa vilivyo, kuliko
hata waumini wa Kikristo
ambao ndio wenye sikukuu
yao.
Hata hivyo tumeona
tumbukushane mambo
mawili matatu wakati huu wa
Pasaka, hawa kwa baadhi ya
Waislamu ambao kwa namna
moja au nyingine, wanashiriki
matukio ya kiimani bila kujua
japo kwa muhtasari maana ya
Pasaka na mantiki yake. Japo
pia wapo Wakristo wengi
ambao nao japo sikukuu ni
yao, lakini hawajui japo kwa
uchache maana halisi ya ibada
ya Pasaka na makusudio
yake.
Kwa mujibu wa maandiko
ya Biblia, tumeelezwa
kuwa Pasaka ni mnyama
anayechinjwa kukumbuka
kukombolewa Waisraeli
Misri. Hii inamaanisha
k wa m b a Pa s a k a h a l i s i
ilikuwepo kabla hata Yesu
hajazaliwa. Hata baada
ya kuzaliwa, naye alikula
Pasaka.
Pasaka hii ni kinyume
kabisa na Pasaka
inayosherehekewa sasa.
Pasaka ya leo kwa Wakristo
ina maana ya siku ya
kukumbuka kufa na kufufuka
kwa Yesu.
Kwa mujibu wa
mafundisho ya Biblia, Pasaka
ni mnyama ambaye wana
wa Israeli waliamrishwa
na Mungu wamchinje na
wamle kwa kufuata utaratibu
aliouelekeza Mungu na kwa
lengo maalum.
"Hapo ndipo Musa aliwaita
wa Israeli na kuwaambia,
nendeni, mkajitwalie wana
kondoo kama jamaa zenu
zilivyo, mkamchinje Pasaka".
(Kutoka 12:21).
"Nawe umchinjie Pasaka
B WA N A , M u n g u wa k o ,
katika kundi la kondoo
na la ng'ombe, mahali
atakapochagua BWANA
apakalishe jina lake".

(Kumbukumbu la Torati
16:2).
"Usimchinje Pasaka ndani
ya malango yako yote akupayo
BWANA, Mungu wako,
ila mahali atakapochagua
BWANA, Mungu wako,
apakalishe jina lake, ndipo
mtakapomchinja Pasaka
jioni, katika machweo ya jua,
kwa wakati kama uliotoka
Misri". (Kumbukumbu la
Torati 16:5-6).
Kulingana na maandiko
hayo juu, tunaona Biblia
inafundisha wazi kuwa
Pasaka ni kondoo au
ng'ombe ambaye Mungu
aliwaamuru wana wa Israeli
wamchinje kisha wamle.
Aidha, maandiko hayo
yanaonyesha wazi pia kuwa
amri hiyo (ya kuchinja na
kumla Pasaka) haikuwahusu
watu wa mataifa mengine
isipokuwa Waisraeli.
Pa m o j a n a wa n a wa
Israeli kuamriwa na Mungu
kumchinja Pasaka, Mungu
pia aliwawekea utaratibu
(sheria) wa kumla (Pasaka)
kama tunavyosoma katika
maandiko yafuatayo:
"BWANA akamwambia
Musa na Haruni, Amri ya
Pasaka ni hii; mtu mgeni
asimle; lakini mtumishi
wa mtu awaye yote
aliyenunuliwa kwa fedha,
ukiisha kumtahiri, ndipo
hapo atamla Pasaka. Akaaye
kwenu hali ya ugeni, na
m t u m i s h i a l i y e a j i r i wa ,
wasimle Pasaka. Na aliwe
ndani ya nyumba moja;
usiichukue nje ya nyumba
nyama yake yoyote; wala
msivunje mfupa wake uwao
wote. Na wafanye jambo hili
mkutano wa Israeli wote. Na
mgeni atakapoketi pamoja
nawe, na kupenda kumfanyia
BWANA Pasaka, waume
wake wote na watahiriwe,
ndipo hapo akaribie
na kufanya Pasaka, naye
atakuwa mfano mmoja na mtu
aliyezaliwa katika nchi; lakini
mtu yeyote asiyetahiriwa
asimle. Sheria ni hiyo
moja kwa mtu aliyezaliwa
k w e n u , n a k wa m g e n i
akaaye kati yenu ugenini.
Ndivyo walivyofanya wana
wa I s r a e l i w o t e ; k a m a
B WA N A a l i v y o wa a g i z a
Musa na Haruni; ndivyo
walivyofanya". (Kutoka
12:43-50)
"BWANA akanena na
Musa, akamwambia, mtu
wa kwenu, au vizazi vyenu,
yeyote atakayekuwa na
unajisi kwa ajili ya maiti,
au akiwako mbali katika
safari, na haya yote, ataishika
Pasaka kwa BWANA; mwezi
wa pili, siku ya kumi na nne
ya mwezi, wakati wa jioni,
wataishika watamla pamoja
na mikate isiyotiwa chachu na
mboga za uchungu; wasisaze
kitu chake chochote hata
asubuhi, wala wasimvunje
mfupa wake, kama hiyo
sheria yote ya Pasaka ilivyo
ndivyo watakavyoishika.
Lakini mtu aliyesafi, wala
hakuwa katika safari, naye
amekosa kuishika Pasaka,
mtu huyo atakataliwa
mbali na watu wake; kwa
sababu hakumtolea BWANA
matoleo kwa wakati wake
u l i o a m r i wa , m t u h u y o

PAPA Francis.
atachukua dhambi yake. Na
kama mgeni akiketi kati yenu
ugenini, naye ataka kuishika
Pasaka kwa BWANA; kama
hiyo sheria ya Pasaka ilivyo,
na kama amri yake ilivyo,
n d i v y o a t a k a v y o f a n ya ;
mtakuwa na sheria moja,
kwa huyo aliye mgeni, na
kwa huyo aliyezaliwa katika
nchi". (Hisabu 9:9-14).
Kwa kifupi, kama
maandiko hayo yanavyoeleza,
huo ndio ulikuwa utaratibu
wa Pasaka, ambao Mungu
aliwawekea wana wa Israeli.
Aidha tumeona maandiko
hayo nayo pia bado
yanatuonyesha kuwa Pasaka
ni mnyama ambaye Mungu
aliwaamuru wana wa Israeli
(peke yao) wamchinje kisha
wamle.
Pamoja na Mungu
kuwatajia wana wa Israeli
watu wanaoruhusiwa
kumla Pasaka (kama
tulivyoona katika maandiko
yaliyotangulia), tunaona
Mungu pia aliwapangia
siku na muda maalum wa
kuchinja na kumla Pasaka,
kama maandiko yafuatayo
yanavyoeleza:
"Kisha BWANA akanena
na Musa katika bara la
Sinai, mwezi wa kwanza
wa mwaka wa pili baada ya
kutoka kwao katika nchi ya
Misri, akamwambia, Tena
wana wa Israeli na washike
sikukuu ya Pasaka kwa
wakati wake ulioagizwa.
Siku ya kumi na nne kwa
mwezi huu, wakati wa jioni,
mtaishika kwa wakati wake
ulioagizwa; kwa amri zake
zote, na kama hukumu
zake zote zilivyo, ndivyo
mtakavyoishika. Kisha Musa
akawaambia wana wa Israeli
kwamba waishike sikukuu
ya Pasaka. Nao wakaishika
Pasaka katika mwezi wa
kwanza, siku ya kumi na nne
ya mwezi, wakati wa jioni,
katika bara ya Sinai, vile vile
kama haya yote BWANA
aliyomwagiza Musa, ndivyo
wa l i v y o f a n ya wa n a wa
Israeli".
(Hesabu 9:1-5)
U k a w e k wa m s i s i t i z o
"Tena, mwezi wa kwanza, siku

ya kumi na nne ya mwezi, ni


Pasaka ya BWANA". (Hesabu
28:16).
"Mwezi wa kwanza, siku
ya kumi na nne ya mwezi
wakati wa jioni, ni Pasaka
ya BWANA". (Mambo ya
Walawi 23:5).
"Mwana-kondoo wenu
atakuwa hana ila, mume wa
mwaka mmoja; mtamtwaa
katika kondoo na mbuzi.
Nanyi mtamweka hata siku
ya kumi na nne ya mwezi
ule ule; na kusanyiko lote
l a m k u t a n o wa I s r a e l i
watamchnija jioni". (Kutoka
12:5-6).
Kulingana na maandiko
hayo juu, tunaona kwamba
siku ya Pasaka ambayo
Mungu aliwapangia wana
wa Israeli kuishika ilikuwa ni
kila ifikapo tarehe 14 mwezi
wa kwanza wa mwaka wa
kutoka kwao nchini Misri.
Aidha maandiko
yanakoleza zaidi ju
ya Pa s a k a h a l i s i , p a l e
tunapoelezwa kwamba hata
Yesu mwenyewe kabla ya
kuondoka, alikula Pasaka.
"Hata siku ya kwanza
ya mikate isiyochachwa,
walipoichinja Pasaka,
wanafunzi
wake
wakamwambia, Ni wapi
utakapo tuende tukuandalie
u i l e Pa s a k a ? A k a t u m a
wawili katika wanafunzi
wake, akawaambia, Nendeni
zenu mjini; atakutana nanyi
mwanamume amechukua
mtungi wa maji; mfuateni;
na popote atakapoingia,
mwambieni mwenye
nyumba, Mwalimu asema,
ki wapi chumba cha wageni,
niile Pasaka humo, pamoja
na wanafunzi wangu? Naye
mwenyewe atawaonyesha
orofa kubwa, imeandikwa
tayari; humo tuandalieni.
Wa n a f u n z i w a k a t o k a ,
wakaenda mjini, wakaona
kama alivyowaambia,
wakaiandaa pasaka. Basi
ilipokuwa jioni yuaja na
wale Thenashara, wakila,
Ye s u a l i s e m a , A m i n ,
naawaambieni, mmoja wenu,
naye anakula pamoja nami
atanisaliti". (Marko 14:12-18).
Pamoja na Mungu
kuwawekea wana wa Israeli
utaratibu maalum wa jinsi
ya kutekeleza amri yake ya
kuchinja na kumla Pasaka,
tunafahamishwa kwamba
hakuacha pia kubainisha
lengo hasa la kutoa amri hiyo
kwa wana wa Israeli.
M a a n d i k o ya n a s e m a ,
"Utunze mwezi wa Abibu,
ukamfanyie Pasaka BWANA,
Mungu wako, kwa kuwa
ilikuwa ni mwezi wa Abibu
alipokutoa Misri usiku
BWANA; Mungu wako, Nawe
umchinjie Pasaka BWANA,
Mungu wako, katika kundi
la kondoo na la ng'ombe,
mahali atakapochagua
BWANA apakalishe jina lake.
Usimle pamoja na mikate
iliyotiwa chachu; siku saba
utakula naye mikate isiyotiwa
chachu, nayo ni mikate ya
mateso; kwa maana ulitoka
nchi ya Misri kwa haraka;
ili upate kukumbuka siku
uliyotoka nchi ya Misri,
siku zote za maisha yako".
(Kumbukumbu la Torati

16:1-3).
Kwa maandiko hayo,
tunaona kuwa lengo la
Mungu kuweka sikukuu
hiyo ya Pasaka, ilikuwa ni
kwa ajili ya kukumbuka siku
aliyowakomboa Waisrael
kuwatoa Misri chini ya
utawala ya Farao (Firauni).
Ambapo maandiko ya
Biblia yamearifu kuwa wana
wa Israeli walikaa nchini
Misri katika hali ya utumwa
kwa muda usiopungua miaka
430 (tazama Kutoka 12:40-42).
Aidha, maandiko hayo
yanaonyesha lengo lingine la
Mungu kuwawekea wana wa
Israeli sikukuu hiyo (Pasaka)
ilikuwa kama desturi yake
kujenga uhusiano mzuri
baina yake na wanaadamu
endapo watatii amri zake.
Kama tulivyoona shuhuda
nyingi za maandiko ya Biblia,
jambo la kusisitiza hapa ni
kwamba, sikukuu ya Pasaka
iliwekwa na Mungu kwa
ajili ya kumbukumbu ya
kukombolewa wana wa
Israeli kutoka nchi ya Misri.
Dhana ya kufa na kufufuka
k wa Ye s u , ya we z e k a n a
kumenasibishwa tu Pasaka
kupitia mafundisho au
taratibu za kibinadamu
ambazo wamejipanga
wenyewe kwa jinsi
wanavyoona inafaa katika
imani.
Haya ni mambo ambayo
M u i s l a m u a m b a ye k wa
namna moja au nyingine
anashiriki ibada ya pasaka,
anatakiwa kuyafahamu na
kuyafanyia uchunguzi wa
kina kabla ya kujitosa.
Ama kwa Mkristo, ana
hiari ya kutekeleza ibada
hiyo ya Pasaka kwa namna
anavyoona ni sahihi kwa
kuwa huo ni utaratibu wa
kiibada uliopo ndani ya
imani yake.
Tu s e m e t u k w a m b a
umefika wakati wa
wanaadamu kujiepusha
na kuamini bila kuwa na
ujuzi wa kimantiki wa kile
unachokiamini (ububusa),
vinginevyo mtu anaweza
kuingia katika shirki kubwa.
Quran inatuambia, "Nani
dhalimu mkubwa kuliko
yule anaye mzulia uwongo
Mwenyezi Mungu, au anaye
sema: Mimi nimeletewa
wahyi; na hali hakuletewa
wahyi wowote. Na yule anaye
sema: Nitateremsha kama
alivyo teremsha Mwenyezi
Mungu. Na lau ungeli waona
madhaalimu wanavyo
kuwa katika mahangaiko
ya mauti, na Malaika
wamewanyooshea mikono
wakiwambia: Zitoeni roho
zenu! Leo mtalipwa adhabu
ya fedheha kwa sababu ya
mliyokuwa mkiyasema juu
ya Mwenyezi Mungu yasiyo
ya haki, na mlivyo kuwa
mkizifanyia kiburi Ishara
zake." Al -An'am 6.93.
"Hawakumwua wala
hawakumsulubu." (Qur.
4:158).

17

TANGAZO

AN-NUUR

JAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 3-9, 2015

ISLAMIC PROPAGATION CENTRE


P.O Box 55105,Phone: 0222450069, 0784 267762, 0755 260087 & Fax 022 2450822, Dar es Salaam website :www.ipctz.org

NAFASI ZA KIDATO CHA TANO 2015/2016

Waislamu kote nchini mnatangaziwa nafasi za kidato cha Tano kwa shule zifuatazo:
KIRINJIKO ISLAMIC SECONDARY SCHOOL

SAME KILIMANJARO
NYASAKA ISLAMIC SECONDARY SCHOOL
MWANZA
UBUNGO ISLAMIC HIGH SCHOO L

DAR ES SALAAM

Shule hizi ni za Kiislamu zenye lengo la kuwapa wanafunzi taaluma ya hali ya juu na malezi bora ya Kiislamu.
Shule hizi ni za bweni za mchanganyiko wa wavulana na wasichana .
Zipo tahasusi za masomo (Subject Combinations) ya SAYANSI, ARTSnaBIASHARA.
Wanafunzi wote wanafundishwa Islamic Knowledge,Introduction to Arabic na matumizi ya compyuta pamoja na kutumia mtandao
(internet) katika kujifunza.
Muombaji anatakiwa awe na sifa za kujiunga na kidato cha tano ziolizotolewa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi amabazo ni :
Ufaulu wa masomo matatu (3) kwa kiwango cha Credit(yaani A,B+,B au C0 katika mtihani wa Kidato cha Nne, ns
Ufaulu usiopungua Daraja la Credit au GPA ya 1.6 katika Mtihani wa Kidato cha Nne, na
Ufaulu usiopungua Gredi D kwenye masomo yote ya tahasusi (combination).
AU
Ufaulu wa masomo matatu (3) ya tahasusi kwa kiwango cha Credit bila kujali daraja alilopata mtahiniwa
kwenye matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne.
Fomu za Maombi zinapatikana kwa gharama ya shilingi 10,000/= katika vituo vilivyoorodheshwa hapa chini.
Mwsho wa kurudisha fomu ni tarehe 15 Aprili, 2015.
Arusha

- Ofisi ya Islamic Education Panel, Jambo Plastic, Ghorofa ya 2 mkabala na msikiti Mkuu Bondeni : 0783552414/0762817640.

Kilimanjaro - Moshi: Msikiti wa Riadha :712 216490


- Same Juhudi Studio mkabala na Benki ya NMB Same: 0757 013344.

- Same: Kirinjiko Islamic Secondry School: 0784 296424/0655 697 075
- Usangi- Falhum Kibakaya : 0787 142054.
- Ugweno Kifula Shopping Centre- Yusuph Shanga : 078458776.
Tanga - Twalut Islamc Centre Mabovu Darajani : 0715 894111
- Uongofu Bookshop: 0784 982525
- Korogwe: SHEMEA SHOP : 0754 690007/071569008.
- Mandia Shop - Lushoto: 0782257533.
-Handeni Mafiga -0782 105735/0657093983
Mwanza
- Nyasaka Islamic Secondary School : 0717 417685/0786 417685.
- Ofisi ya Islamic Education Panel Mtaa wa Rufiji mkabala na Msikiti Al-Amin 0785 086 770/0714097362.
Musoma - Ofisi ya Islamic Ed Panel -Mtaa wa Karume,Nyumba Na. 05 : 0765024623
Shinyanga - Msikiti wa Majengo karibu na Manispaa ya Shinyanga Mjini :0752180426
- Kahama ofisi ya AN NUUR Karibu na msikiti wa Ibadhi : 0753 993930/0688794040
Dar es Salaam
- Ubungo Islamic High School : 0756584625/0657350172
- Ofisi ya Islamic Ed. Panel Temeke -Msikiti wa Nurul Yakin : 0655144474/0787119531
1
Morogoro - Wasiliana na Ramadhani Chale
: 0715704380.
Dodoma - Hijra Islamic Primary School : 0716 544757/0718661992
Singida
- Ofisi ya Islamic Education. Panel karibu na Nuru snack Hotel : 0786 425838/0784 928039.
Manyara
- Ofisi ya Islamic Ed. Panel Masjid Rahma: 0784491196
Kigoma
- Msikiti wa Mwandiga: 0714717727
- Kibondo Islamic Nursery School: 0766406669.
- Kasulu: Murubona Isl.SS: 0714710802.
Lindi
- Wapemba Store: 0784 974041/0783 488444/0653 705627.
Mtwara
- Amana Islamic S.S: 0715 465158/0787 231007.
Songea
- Kwa Kawanga Karibu na Msikiti wa NURU : 0713249264/0683670772.
- Mkuzo Islamic High School :0717 348375.
Mbeya
- Ofisi za Islamic Education Panel Uhindini 0785425319.
- Rexona Video mkabala na Mbeya RETICO: 0713 200209/0785425319.
Rukwa
- Sumbawanga:Jengo la Haji Said Shule ya Msingi Kizwike 0717082 072.
Tabora
- Kituo cha Kiislamu Isevya: 0784 944566/0787237342
Nzega
-Dk Mbaga-0754 576922/0784576922.
Iringa
- Madrastun Najah: 0714 522 122.
Pemba
-Wete: Wete Islamic School : 0777 432331/0712772326.
Unguja
- Madrasatul Fallah: 0777125074.
- PANDU BOOKSHOP 0777462056 karibu na uwanja wa Lumumba
Mafia
- Ofisi ya Ust. Yusufu Ally jirani na msikiti mkuu : 0773580703.
USIKOSE NAFASI HII ADHIMU WAHI KUCHUKUA FOMU SASA!
MKURUGENZI
WABILLAH TAWFIIQ

18
VIONGOZI wa makabila
katika maeneo tofauti
nchini Yemen wametoa
tangazo rasmi la vita
dhidi ya Saudia kufuatia
mashambulizi yake
yaliyosababisha zaidi ya
watu 100 kuuawa hadi
sasa. Viongozi hao kutoka
madhehebu tofauti ya
K i i s l a m u wa k i we m o
Waislamu wa Suni, alHuthi, Shia Ithnaasharia
na wengine wamewataka
vijana wao kubeba
silaha kukabiliana na
chokochoko za Saudia
dhidi yao.
Viongozi wa makabila
ya Hashid, Bakil, Khulan,
a l - Twa y ya l , A m i r ,
Hamadan, Mudh'hij,
Qahtwan na kwa pamoja
wamelitaka jeshi la Yemen
kushambulia maeneo ya
kijeshi ya Saudia ukiwemo
mji mkuu wa nchi hiyo
Riyadh na ule wa Jeddah
ikiwa ni katika kujibu kile
kilichoitwa kuwa ni jinai
za utawala wa Aal Saud.
Ta a r i f a z i n a e l e z a
kuwa jeshi la Yemen
k wa k u s h i r i k i a n a n a
Wa n a h a r a k a t i wa
Answarullah, tayari
wameweka makombora
yake ya Scud ili kujibu
hujuma hiyo.
Awali baada ya Saudia
kuanza mashambulizi
dhidi ya Yemen, Balozi wa
Saudia nchini Marekani
Adel al Jubeir, alisema
kuwa mashambulizi hayo
yanafanyika ili kuilinda
serikali aliyodai halali ya
Rais aliyejiuzulu, Abdu
Rabu Mansour Hadi huko
Yemen.
Ndege za Kikosi cha
Anga cha Ufalme wa Saudi
Arabia zilishambulia
maeneo ya Ansarullah
k a t i k a m j i m k u u wa
Yemen, San'aa mapema
siku ya Alhamisi.
Televisheni ya al Alam
iliripoti kuwa, ndege moja
ya Saudia ilitunguliwa
na jeshi la anga la Yemen
na ripoti zilionyesha
hasara kwa raia katika
mashambulizi hayo.
Balozi huyo wa
Saudi Arabia nchini
Marekani alidai pia kuwa
mashambulizi hayo
yataendelea na kwamba,
mbali na kupata baraka
kamili za Marekani,
Riyadh inashirikiana na
nchi nyingine 10 katika
operesheni hizo.
Kwa mujibu wa
balozi huyo, alisema
kuwa mashambulizi
ya Saudia dhidi ya
Ye m e n , y a n a f a n y i k a
kwa ushirikiano na nchi
kadhaa za Kiarabu. Kauli
ya balozi huyo imedaiw
akuwa inathibitisha njama
chafu dhidi ya taifa la
Yemen na eneo zima la
Masharikiya Kati kwa
ujumla.
Shirika la Habari
la Saudi Arabia (SPA)
liliripoti kuwa ukitoa

Makala/Habari

AN-NUUR

JAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 3-9, 2015

Ni vita vya Yemen na Saudia Kesi ya Waislamu


Makabila ya wapiganaji serikali waungana
yaahirishwa tena

Oman, nchi nyingine zote


wanachama wa Baraza
la Ushirikiano la Ghuba
ya Uajemi zimekubali
kushiriki kwenye
operesheni hiyo.
K wa
u p a n d e
wake, Ansarullah
wameshatangaza
mapema kuwa watajibu
kwa silaha mashambulizi
yanayofanywa dhidi yao,
kama ambavyo huko
nyuma waliwahi kufanya
mashambulizi dhidi ya
Saudi Arabia, baada ya
nchi hiyo ya kifalme
kuanza kuyashambulia
maeneo ya kundi la al
Houthi huko Kaskazini
mwa Yemen.
Kiongozi
wa
Answarullah Abdul Malik
al Houthi, ameeleza kuwa
wapiganaji wa harakati
hiyo wakishirikiana na
wananchi na jeshi la taifa
watakabiliana vilivyo na
uchokozi wa Saudi Arabia
na madola mengine ya
Kiarabu.
Aliongeza kuwa nchi
za Kiarabu zilizoamua
kushirikiana kwa lengo
la kuishambulia kijeshi
Yemen kuwa ni vikaragosi
vya madola ya Magharibi
yakiongozwa na Marekani
na kwamba, njama za
madola ya Magharibi ni
kutaka kuigawa Yemen na
kuvuruga utulivu ulioko
nchini humo.
Aidha Kiongozi huyo
wa kundi la Answarullah
nchini alilaani vikali
shambulio hilo la kijeshi
lililofanywa na jeshi la
anga la Saudi Arabia
dhidi ya ardhi ya Yemen
na kusisitiza kwamba,
mashambulizi hayo
yametekelezwa kwa
maslahi ya Marekani na
utawala wa Kizayuni wa
Israel.
Alisisitiza kuwa,
u t a wa l a wa k i f a l m e
wa Saudi Arabia ni wa
kidhalimu na wala hauna
hata chembe ya utu na
ubinadamu.
Tayari bei ya mafuta
imeripotiwa kupanda
kufuatia operesheni hizo
za kijeshi za Saudia nchini
Yemen.
Maelfu ya wananchi
wa Ye m e n A l h a m i s i
ya wiki iliyopita
walifanya maandamano
makubwa katika maeneo
tofauti ya taifa hilo,
wa k i t a n g a z a k u u n g a
mkono Wanaharakati
wa Answarullah na
muungano wa wananchi
wa n c h i h i y o k a t i k a
kuilinda nchi yao.
Msemaji wa Wizara ya
Mambo ya Nje ya Iran
Bi. Marzieh Afkham,
amelaani mashambulizi

hayo ya Saudia dhidi ya


Yemen na kuitaka jamii
ya kimataifa kuishinikiza
nchi hiyo kusitisha mara
moja kile kilichoitwa ni
chokochoko .
Bi. Marzieh alisema
kuwa mashambulizi dhidi
ya nchi hiyo ya Kiarabu,
yatasababisha hali ya
m a m b o k u wa m b a ya
zaidi.
Wiki iliyopita
wapiganaji wa kikundi
cha Answarullah nchini
Ye m e n , wa l i r i p o t i wa
kuwateka wanajeshi 40
wa Saudi Arabia katika
eneo la mpaka wa nchi
hizo mbili.
Taarifa zilisema kuwa,
hatua ya wapiganaji wa
Answarullah ya kuwateka
nyara wanajeshi hao,
ilitokana na shambulizi
la kijeshi lililofanywa na
majeshi ya Saudi Arabia
ardhi ya Yemen.
Ilielezwa kuwa
wapiganaji hao wa
Answarullah walifanikiwa
kuteka maeneo kadhaa
yaliyoko katika mkoa wa
Najran nchini Saudia,
baada ya kutokea
mapigano makali kati ya
majeshi ya Saudi Arabia
na wapiganaji hao wa
Yemen.
Mapigano makali
bado yanaendelea
kati ya wapiganaji wa
Answarullah na wanajeshi
wa Saudia katika mpaka
wa nchi hizo mbili.
Wakati huohuo, Waziri
wa Mambo ya Nchi za
Nje wa Algeria Ramtane
Lamamra, amesema kuwa
Wa a r a b u wa n a p a s wa
kutatua matatizo yao
wenyewe kwa kutumia
njia za mazungumzo ya
amani.
Lamamra alisisitiza
kuwa, njia ya kutumia
kijeshi na mabavu
imepitwa na wakati na
wala haiwezi kutatua
migogoro iliyopo.
Naye Mkuu wa Sera
z a K i g e n i wa U m o j a
wa Ulaya, Federica
Mogherini, amekosoa
vikali uingiliaji wa kijeshi
wa Saudia nchini Yemen
na kusisitiza kwamba
mgogoro wa nchi hiyo
unapasa kutatuliwa kwa
njia za mazungumzo.
Kwa upande mwingine,
Rais Omar Hassan al
Bashir wa Sudan yeye
amedai kuwa, hakuna
chaguo jingine isipokuwa
k u t u m i wa n g u v u z a
kijeshi nchini Yemen. Rais
al Bashir amesema kuwa,
Sudan iko tayari kutuma
jeshi la nchi kavu kwa
lengo la kupambana na
harakati za wananchi wa
Yemen.

Na Mwandishi Wetu

KESI ya Waislamu 23
wanao tuhumiwa
kwa ugaidi akiwemo
Sheikh Farid Had na
Sheikh Mselem Ali,
imeahirishwa tena hadi
Apili 13 mwaka huu.
Kesi hiyo inayo sikilizwa
k a t i k a M a h a k a m a ya
Hakimu Mkazi Kisutu
Jijini Dar es Salaam,
iliahirishwa Jumatano
wiki hii, Mahakamani
hapo, kwa maelezo kuwa
kesi hiyo imekatiwa rufaa
Mahakama Kuu.
Waendesha Mashitaka
walisema shauri lipo katika
hatua ya Rufaa kwa hiyo
waliomba siku nyingine,
hivyo imepangwa kurudi
April 13, 2015 kwa ajili
ya kutajwa. Imeelezwa
Mahakamani hapo.
Kutokana na hali hiyo,
Hakimu anaye sikiliza
kesi hiyo Mhe. Janet
Kaluyenda alilazimika
kuahirisha kesi hiyo hadi
Apili 13 mwaka huu.

A wa l i , k e s i h i y o
ambayo iliahirishwa
katika siku zilizopita
kufuatia upande wa
mashitaka ukiongozwa
na Wakili Pita Njike,
ulipoarifu Mahakama
kuwa, kesi hiyo ipo
Mahakama ya Rufaa na
wanasubiri kupangiwa
siku ya kusikilizwa.
N a y e Wa k i l i w a
u p a n d e wa u t e t e z i
Abdulfattah Abdallah,
akizungumza na
Wandishi wa habari
Mahakamani hapo
alisema, leo (Jumatano
wiki hii) Kesi hiyo
ilifikishwa hapo (Kisutu)
kwa ajili ya kutajwa
na washitak iwa wote
walikuwepo Mahakamani
hapo.
Wa k i l i A b d a l a h
alisema, kinachosubiriwa
Mahakama Kuu ni
mwenendo wa kesi na
wapo katika mchakato wa
kuhimiza suala hilo liende
haraka ukizingatia wateja
wao wapo ndani hawako
huru.

Thabit Ibn Qurra (5)


Inatoka Uk. 14
leo ingawa inasemekana
kazi zake nyingi zimepotea.
Katika kazi zake ambazo
zimehifadhiwa hadi hii leo
ni katika midani ya hesabati,
elimu ya nyota na utibabu,
kazi hizo baadhi zipo katika
lugha ya Kiarabu na baadhi
zimeandikwa kwa lugha ya
Syriac.
Kutoakana na umahiri wa
taaluma za hesabati na nyota,
baadhi ya maandiko yake
yalifanyiwa tafsiri kwa lugha
ya Kilatino na Gehrrard
wa Cremona. Kazi zake
nyengine zimefanyiwa tafsiri
katika lugha mbalimbali za
nchi za Ulaya. Inaaminika
kuwa Thabit Ibn Qurra
aliweka msingi wa kuifanyia
kazi elimu ya nyota kwa
utaalamu wa Ptolemaic.
Kazi zake ziliweka msingi
wa kuunganisha taaluma za
kidunia na mafungamano
ya utamaduni wa Kiislamu
ambao katika Uislamu
hautenganishwi huwekwa
kuwa kitu kimoja, kinyume
na Ukiristo, ambao dini
h u wa m b a l i n a e l i m u
ya dunia mbali. Katika
Uislamu vitu viwili hivyo
hufunganishwa kwa pamoja

na ndio utaona miaka hiyo ya


nyuma Waislamu walipata
mafanikio makubwa.
Ta n g u k u k u b a l i
kuingia katika mtego wa
kuvitenganisha vitu viwili
hivyo, ndio utaona Waislamu
wamekosa kupata vigogo
kama hao ninaowaelezea
katika makala hizi. Vigogo
hivi imani yao ya dini
ilikuwa kubwa na ndio
iliowapelekea kuzama katika
sayansi na wengi walikuwa
na unyenyekevu mkubwa
wa Mola wao na kuweza
kupata mafanikio.
Tahabit Ibn Qurra alifariki
katika mji wa Baghdad,
mjukuu wake Ibrahim Ibn
Sinan alifwata nyao za babu
yake na alifanya kazi kubwa
ya kutumia chombo cha
Sundial, chombo ambacho
hutumika kujua wakati
k a t i k a s i k u wa k a t i j u a
linawaka, aliitanua kazi hii
kwa upana kabisa.
Makala ya wiki ijayo
itamzungumzia Abu Bakar
Al-Razi, Mfursi alikuwa
gwiji wa somo la kemia
na falsafa. Aidha alikuwa
tabibu mahiri anayelezewa
katika historia.

19

Makala ya Mtangazaji

AN-NUUR

JAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 3-9, 2015

Israel Arrests ICC Membership Asserts International


16 Palestinians Responsibility towards Palestine, Says PLO
in West Bank,
East Jerusalem
WEST BANK, (WAFA)
Israeli army and police
Wednesday conducted mass
arrests during predawn
and night raids across the
West Bank and Jerusalem,
with at least 16 Palestinians
reported arrested in the past
24 hours, according to local
and security sources.
In Jerusalem, Israeli police
arrested eight local residents,
who, according to Prisoner
Support and Human Rights
Association (ADDAMEER),
were identified as Foad
Ebeid, Omar Wazzouz,
Hazem Dejani, Malek
S h w e k i , Yo u s e f A b u
Shousha, Aziz Abu Sarhan,
Morad Abu Sarhan and Ali
Abidiya.
A c c o r d i n g
t o
ADDAMEER, the latest
arrests push up the number
of those who were arrested
during the past 48 hours
to 38 Palestinians in the
Jerusalem governorate alone.
Meanwhile in Jenin,
19-year-old Ahmad Salim
Noursi was injured with
a live bullet in the right
leg during confrontations
with Israeli army, which
broke into the adjacent Jenin
refugee camp. The army
raided and searched several
homes before arresting two
Palestinians in the camp.
They were identified as
Ahmad Quraini, 21, and
Abdal-Karim Abul-Fouz, 19.
Security sources said the
army force, which raided
the camp, used three locals,
including a woman, as a
human shield during their
house raids.
In the meantime, army
broke into Hebron and
arrested four residents,
including three students of
the Palestine Polytechnic
University, after raiding and
searching their homes and
sabotaging the furniture. The
four were identified as Raed
Sharabati, 44, Asad Imam,
24, Anas Abu Hadid, 21, and
Abder-Rahman Khatib, 22.
Another army force also
stormed the nearby towns
of Yatta, Sair and finally
Idna, where they raided
and searched the house of
Mohammad Abu Jehesha,
a member of the Palestine
Legislative Council.
Meanwhile in Bethlehem,
Israeli army stormed the
village of Hosan, west of the
city, and arrested Ahmad
Sabatin, 16.
Israeli forces also broke
into the town of Azzoun, east
of Qalqilia, before arresting
18-year-old Anas Salim, after
raiding and sabotaging the
furniture of his home.

Over 30 detained
in Jerusalem in
last 3 days

RAMALLAH, (WAFA)
- PLO Executive
Committee Member and
Head of the International
Criminal Court (ICC)
Higher National
Committee Saeb Erekat
said the occasion serves
as a reminder to the
international community
of its responsibilities
under international law,
in order to achieve a just
and lasting peace, and put
an end to the prolonged
Israeli Occupation.
In a press statement
on Palestine's official
accession to the ICC,
Erekat explained that
on the Palestinian level
the membership reflects

Palestine's commitment to
justice, international law,
and human rights.
Our determination
to protect our people
against the injustice of
those responsible for war
crimes is underscored
by our nation's accession
to the Rome Statute and
submission to the ICC's
jurisdiction.
Describing the
membership as historic,
Erekat called upon the
international community
to support the inalienable
rights of Palestinians,
including the right to
self-determination, by
supporting the peaceful
movement to end decades

of impunity, occupation,
and exile.
He renewed the
Palestinian authoritys
calls upon all nations of
conscience to recognize
the State of Palestine on
the 1967 border, with East
Jerusalem as its capital.
In a closed and special
ceremony, the ICC
officially accepted the
membership of the State
of Palestine accession to
the international legal
body making it the 123
of ICC's state parties.
However, Palestinians
might have to wait years
before actually opening a
full investigation against
Israel.

BETHLEHEM, (WAFA)
A number of Palestinian
students Tuesday suffered
suffocation by tear gas as
Israeli soldiers assualted
them while they were
heading to their schools in
the town of Taqou to the East
of Bethlehem, according to
security sources.
Sources told WAFA that
Israeli forces intercepted
students while they were
heading to their schools in
the early morning hours,
firing tear gas canisters and
stun grenades toward them,
causing many to suffer from
tear gas suffocation.
Israeli army previously
carried out numerous
attacks, with the deliberate
and reckless use of force,
against schools and

educational facilities across


the West Bank, in a serious
violation of international
law and students right to
pursue education in a safe
environment.
An increasing number
of unarmed and peaceful
Palestinians were either
killed or seriously injured
as a result of Israels constant
use of tear gas against
Palestinians.
To be noted, Defense
for Children International
(DCI) described the year
2014 as the most difficult
year for Palestinian children
due to the ongoing Israeli
violations, mainly the 2014
summer aggression on the
Gaza Strip.
M e a n w h i l e , S AWA ,
a Palestinian non-

governmental institution
working for women's and
children's rights stated in a
press release issued in July
2014 that, Children have the
right to life and survival, nondiscrimination, education,
recreation, and safety.
In the meantime, a special
report issued by Al-Mizan
Center for Human Rights
said that Israel deliberately
targeted intellectual property
during its recent onslaught
on Gaza in the summer of
2014. Jean Gough, UNICEFoPt Special Representative
said that, Every child has
the right to learn and grow
in an environment where
their health and safety are
paramount.

JERUSALEM (Ma'an) -Israeli forces detained three


Palestinians from the Jabal
al-Mukabbir village of East
Jerusalem late Tuesday
claiming they possessed an
"explosive device."
Sources told Ma'an
that Israeli forces closed
the "tunnel checkpoint" in
southern Jerusalem City
for more than two hours
after allegedly finding 3
explosive devices in a car
after searching it.
The three detainees in
the vehicle were identified
as Aziz Abu Sarhan,
Murad Abu Sarhan and Ali
Ubeidiya, and taken to the
Russian compound police
station for interrogation.
An Israeli army
spokeswoman did not have
immediate information but
told Ma'an she was looking
into the incident.
Israeli forces then carried
out a detention raid in
Jerusalem early Wednesday.
Lawyer of the Addameer
Prisoners Support and
Human Rights Association,
Muhammad Mahmoud, said
that Israeli forces detained
five youths after raiding their
homes in neighborhoods
across Jerusalem, identified
as Malik Shweiki, Hazem
al-Dajani, Omar Wazwaz,
Fouad Obeid, and Youssef
Abu Shusha.
The Israeli authorities
h a ve d e t a i n e d o ve r 3 0
Pa l e s t i n i a n s , i n c l u d i n g
women and minors,
throughout during the past
week, 15 of which were
banned from entering the
Al-Aqsa mosque compound
for periods between 12 to 90
days.

RAMALLAH, (WAFA)
The Palestinian cabinet, in
its weekly session Tuesday,
rejected Israels unilateral
decision to transfer the
Palestinian Authoritys tax
revenues after deducting
almost 300 million shekels
($75 million).
The cabinet reiterated
its utmost rejection to
Israels repeated act
of withholding PAs tax
revenues and deducting 300
million shekels, describing
it as a premeditated crime,
a collective punishment
against Palestinians, and
a blatant violation of
previously agreed upon
agreements and international
resolutions.
It urged the international
community to pressure Israel
to release the entire sum, and
to put an end to this illegal
action.
Israels decision to deduct
millions of shekels from
Palestinians came under

the pretext of paying for


accumulated debts for
services provided to the
Palestinian population,
including electricity, water
and hospital bills.
However on March 27,
Israel decided to release
hundreds of millions of
dollars in Palestinian tax
revenues, which has been
withheld since last January
following PAs accession to
the International Criminal
Court.
I s r a e l i
P r i m e
Minister Benjamin
Netanyahus approved the
recommendation of his
Defense Minister, Moshe
Yaalon, and of the Israeli
military and Shin Bet
internal security agency to
transfer the withheld funds.
Netanyahu explained that
the decision came, based on
humanitarian concerns and
in overall consideration of
Israels interests at this time.
In the meantime, the

Palestinian Finance Ministry


stated that the deductions
made by Israel to cover
services provided to the
Palestinians havent been
bilaterally discussed or
agreed upon and constitute
an unjustified and illegal
procedure that could cause
complications.
The ministry affirmed that
transferring the tax revenues
is not a favor done by the
Israeli government and that
the Palestinian government
rejects any unilateral
deductions outside the
appropriate calculation
mechanism.
Israel has frequently
resorted to halting the
transfer of Palestinian tax
revenues and exploited it as a
political instrument intended
to punish the Palestinians
for their political choices
and attempts to secure
the establishment of their
state through international
diplomatic means.

As a result of the Israeli


measure, the PA has been
incapacitated from fully
paying approximately
170,000 public servants on its
payroll, which costs between
$160 and $170 million a
month.
Under the Protocol on
Economic Relations signed
in 1994, Israel transfers $127
(175) to PA each month
in customs duties levied
on goods destined for
Palestinian markets that
transit through international
borders.
Acting to address the
financial crisis it is gripped
with, the PA has borrowed
from local banks to partially
pay 60% of the public
servants, December, January
and February wages.
Meanwhile, the cabinet
expressed its gratitude to all
efforts exerted by various
countries to get Israel to
release its frozen revenues.

Israeli Soldiers Attack Students with Tear Gas, Suffocate Many

Cabinet Rejects Israeli Unilateral Deduction of PAs Tax Revenues

AN-NUUR

20

MAKALA

20

Na Mwandishi Wetu
MAKAMU wa Kwanza
wa Rais wa Zanzibar,
Maalim Seif Sharif
Hamad, amemtembelea
kijana Shamsi Ali
Khamis nyumbani kwao
Mwembemakumbi.
Shamis ni mmoja kati
ya watu waliojeruhiwa
wakati msafara wao ukiwa
njiani kutoka mkutano
wa Chama cha Wananchi
(CUF) katika jimbo la
Makunduchi, Unguja
Kusini.
K i j a n a
h u y o
aliyejeruhiwa jicho la kulia,
alitarajiwa kusafirishwa
juzi kuelekea Dar es
Salaam kwa matibabu
zaidi.
Watu
kadhaa
walijeruhiwa baada ya
msafara wa wanachama
wa CUF waliokuwa
wakitoka katika mkutano
kushambuliwa na watu
wasio julikana.
Shambulio hilo linakuja
wakati siku zikiyoyoma
kuelekea uchaguzi mkuu
hali inayoleta wasiwasi
kuwa huenda hali isiwe

JAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA MACHI 27-APRILI 2, 2015

MAHAKAMA Kuu ya
Ta n z a n i a , i m e m t a k a
Mwanasheria wa
Serikali kujibu haraka
hoja za Masheikh walio
fungua kesi kupinga
m p a n g o wa S e r i k a l i
kuipa BAKWATA uwezo
kisheria kusimamia
mambo ya Waislamu.
Amri hiyo imekuja baada
ya Mwanasheria huyo
kuiomba Mahakama Jijini
Dar es Salaam, Jumanne
wiki hii wapewe muda
wa siku 14, ili waweze
kujibu hoja za Masheikh
h a o wa l i z o wa s i l i s h a
Mahakamani hapo,
mapema wiki iliyopita.
Upande wa Jamhuri
ukiongozwa na Wakili
Malata, uliomba wapewe

Safari ya Hijja Hijiria 1436

Tanzania Muslim Hajj Trust, uandikishaji unaendelea,


gharama za Hijja ni US Dollar 4400, tarehe za Safari ni:
11 na 13 Septemba, kurudi 7 Oktoba, 2015.
Wahi kujiandikisha sasa
Kwa mawasiliano:
+255 222181577
+255 222 182370
0786 383820
0754 261910; 0717 000065
0713 764636
0784 272723

Maalim Seif atembelea


majeruhi wa Janjaweed

KATIBU Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad (kushoto) akimjulia hali mmoja
wa majeruhi aliyeshambulia katika mkutano wa Chama hicho Unguja hivi karibuni.
shwari huko mbeleni.
Hii ni hali iliyokuwa
ikijiri huko nyuma kila

unapokaribia uchaguzi
mkuu hadi kupatikana
matokeo na hata

Mwanasheria Mkuu atakiwa


kujibu hoja za Masheikh
Na Mwandishi wetu.

AN-NUUR

JAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 3-9, 2015

siku kumi na nne, kuanzia


siku waliyopokea Samansi,
ili wakaandae majibu zaidi
ya Shauri lililowasilishwa
Mahakamani hapo.
M wa n a s h e r i a wa
Serikali, aliomba wapewe
m u d a wa s i k u k u m i
na nne waweze kujibu,
M a h a k a m a b a a d a ya
kusikiliza hoja ilikubali
lakini iliwataka wajaribu
k u wa h i z a i d i k u t o a
majibu hayo. Alisema
Wakili wa Masheikh hao
Juma Nassoro.
Awali, Wakili Juma
Nassoro, alisema upande
wa Serikali, kisheria
wana haki ya kujibu ndani
ya siku kumi na nne
tokea siku waliyopokea
Samansi, ndio maana
akasema, Mwanasheria
huyo wa Serikali aliomba
wapewe muda huo.

Mahakama ilikubalina
nao, lakini iliwaambia
kwa sababu hii Kesi ina
umuhimu mzito ingefaa
wajibu kabla ya siku hizo
14, sasa kwa maelezo
hayo ya Mahakama
wanatakiwa wajibu April
2 ,2015 siku ya Alhamisi
(jana) na sisi tutachukua
hayo majibu yao April
8, hivyo tutaanza kuja
kuanza kusikiliza Kesi
rasmi, utaratibu ni huo.
Alisema Wakili Nasoro.
Sheikh Rajabu Katimba,
n a w e n z a k e wa t a t u ,
mapema wiki iliyopita
walifungua kesi namba 17
ya 2015, katika Mahakama
Kuu ya Tanzania, kupinga
m p a n g o wa S e r i k a l i
kupitia hoja ya kuipa
BAKWATA uwezo rasmi
wa Kisheria kusimamia
mambo ya Waislamu na
kuteua Makadhi nchini.

baada, jambo ambalo


halikutarajiwa kutokea
tena baada ya kupatikana

kwa Serikali ya Umoja


wa Kitaifa.
Hata hivyo, katika
masiku ya hivi karibuni
kumekuwa kukitolewa
matamshi ya kuikataa,
kuibeza na kutaka
Serikali hiyo kuvunjika.
Wa l i o t a j wa k u wa
vinara wa kutoa kauli
hizo ni katika makada
wa CCM katika kundi
la wahafidhina.
Hata
hivyo,
wakongwe wengine
wa CCM, kama
Mzee Nassoro Moyo,
wamekuwa wakihimiza
amani na kusema kuwa
Wazanzibar wasikubali
kuvunjwa kwa Serikali
ya Umoja wa Kitaifa
ambayo imeleata amani
na maelewano Visiwani.
Akasema kuwa
wanaotaka ivunjike
Serikali hiyo na
kurejea zama za chuki
na uhasama, ni watu
wabinafsi wasio itakia
mema Zanzibar na
Wazanzibari.

ISLAMIC PROPAGATION CENTRE (IPC)


TANGAZO
MABADILIKO YA TAREHE YA KURUDISHA
FOMU ZA KIDATO CHA TANO KWA SHULE ZA IPC
MWISHO WA KURUDISHA FOMU NI
TAREHE 15 APRIL 2015 BADALA YA
15 MEI 2015 ILIYOKUWA
IMETANGAZWA AWALI.
WALE WOTE WALIOKIWISHA
KUCHUKUA NA WANAOENDELEA
KUCHUKUA FOMU HIZO WANATAKIWA
KUZINGATIA TAREHE HII MPYA.
WAHI KUCHUKUA NA KURUDISHA FOMU
YAKO SASA!
WABILLAHI TAWFIQ
MKURUGENZI

Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na POA Printing Works LTD, S.L.P. 4605, Dar es Salaam.

You might also like