You are on page 1of 16

www.annuurpapers.co.

tz

Facebook:annuurpapers@yahoo.com

Sauti ya Waislamu

Wizara ya Elimu yatakiwa kuwa na sera ya madrasa


Wito wa Maalim Seif maulidini Alabama Hazina ya maadili, historia itiliwe mkazo

Mauwaji Msikitini: Makubwa yafichuka


Usiombe kuingia anga ya polisi wa ugaidi Sheikh alingolea macho, sehemu za siri Mchezo wa danganya toto jinga waendelea

ISSN 0856 - 3861 Na. 1112 RABIUL THAN 1435, IJUMAA , FEBRUARI 14-20, 2014 BEI TShs 500/=, Kshs

Uk. 16

Baraza Kuu, Ulamaa kuteuwa Makadhi


Na Bakari Mwakangwale J U M U I YA n a Ta a s i s i za Kiislamu (T) chini ya Ha-y-at Ulamaa, i m e wa t a k a Wa i s l a m u waliohitimu Digrii ya Sharia za Kiislamu, kuwasilisha wasifu wao (CV), ili kuingizwa katika mchakato wa kuwapata Makadhi.

Balozi mdogo wa Marekani nchini Sudan, Joseph D. Stafford (mwenye kilemba cha kijani na picha ndogo chini) akiwa nchini Sudan.

Profesa Jeffrey-kutoka Ukatoliki hadi Uislamu

DHULKIFLI A. Rogo. Habari Uk. 8

RAHMA Hassan mke Sheikh Said Mohammed Njiro.

Waislamu wenye taaluma ya Shariah waitwa


Akiongea na An nuur, Jumatano wiki hii, Amiri wa Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu, Alhaj Mussa Yusuph Inaendelea Uk. 3
PROFESA Jeffrey Lang. Soma habari yake Uk. 6.

2
S.L.P. 55105, Simu: +022 2400786 Cel: 0784 370 208, 0713 110 148, 0755 260 087 , DSM. www.annuurpapers.co.tz E-mail: annuurpapers@yahoo.co.uk Ofisi zetu zipo: Manzese Tip Top Usangi House (Jengo dogo), barabara ya Morogoro, D'Salaam

Tahariri/Makala
AN-NUUR
v i t a d h i d i ya u g a i d i lishafanyiwa kazi sana. Hakuna kiongozi wa nchi leo anaweza kuwa na udhuru wa kusema kuwa alikuwa hajui. Ukiacha haya yanayoelezwa hivi sasa juu ya Al Qaida na Al Shabab, wanaweza kurejea katika historia waone wenzao walivyofanyiwa katika nchi za Nicaragua, Guaetamala, El Salvador, Chile, Cuba na Panama. Nchi zilivurugwa magaidi wa kuundwa wakifanya mauwaji ya

RABIUL THAN 1435, IJUMAA FEBRUARI 14-20, 2014


kutisha huku vikosi vya serikali navyo vikiuwa. Nchi zikawa taabani huku mabeberu wakipora mali. Kwa nini hatujifunzi katika historia hiyo? Hivi kama tunaridhia kutumiwa kijinga na kirahisi namna hii, tunachowaeleza hao wanaotutumia nini? Ujumbe gani tunawapa? Kwamba sisi si binadamu kamili na wenye akili kama wao? Sisi tunaamini kuwa Mungu katuumba sote katika hali ya usawa kiakili na uwezo wa kufikiri. Ndio maana tunao maprofesa wa taaluma mbalimbali walioko Marekani na Ulaya wakisomesha katika vyuo vikuu na hata kutumikia taasisi nyeti na muhimu za nchi hizo. Kama ni kuzidiana, inatokana na mtu mwenyewe anavyoitumia akili yake. Hebu tutumie akili zetu vizuri tuepukane na mabalaa haya ya kuletwa na binadamu wenzetu kwa tamaa zao za kupora na

AN-NUUR

Vita dhidi ya ugaidi:

Tusijidharaulishe wenyewe wala tusilaumu mabeberu


KUTOKANA na tafiti mbalimbali za wataalamu na wanazuoni mahiri na hata kutoka katika ndimi za mabeberu wenyewe, vita dhidi ya ugaidi ni vita bandia. Ni vita ya kupanga iliyolenga kutafuta adui ili kuhalalisha mambo kadhaa. Tafiti hizo zinasema kuwa makundi ya k i g a i d i ya l i u n d wa n a asasi za mabeberu na kwamba hadi sasa yanasaidiwa na kufanywa yaendeleekuwepo na asasi hizo. Aidha inaelezwa kuwa kundi la Al Qaeda liliundwa na mabeberu hao toka kipindi cha vita ya kiitikadi kati ya Marekani na Urusi na linaendelea kupewa misaada kwa siri. 'Vita ya kimataifa dhidi ya u g a i d i ' i n a e l e z wa kuwa ni mkakati wenye miingiliano mingi na ya kijasusi na kwamba ni nyenzo ya kueneza ukoloni ambao unaelekeza kuhujumu mataifa huru. Makundi ya kigaidi ya k i s h a u n d wa , h u t u m i k i s h wa k a t i k a kuleta ghasia na machafuko katika nchi lengwa na hatimaye kuidhoofisha. Ufupi wa maneno na kwa lugha nyepesi tunafahamishwa kuwa magaidi ni adui wa k u u n d wa k u h a l a l i s h a utoaji misaada ya kikachero na kijeshi, na hivyo kuwezesha nchi kukaliwa kijeshi na mabeberu. N c h i i k i s h a i n g i z wa katika mchezo huu mchafu, itakuwa ikiandamwa na mashambulizi ya kigaidi kila uchao. Watu wake wakiuliwa na magaidi na polisi/jeshi la nchi nalo likiuwa watu kwa mtizamo wa kupambana na magaidi. Hali hii itakuwa ya kuendelea ili kuhalalisha wito wa kupewa msaada wa kikachero na hata jeshi. Matokeo yake ni kuwa mnajikuta, kwanza mnauwana wenyewe kwa wenyewe. Pili, nchi inakuwa katika machafuko, hakuna maendeleo na

hatimaye mnajikuta mmekaliwa na mtandao wa kikachero na kijeshi kutoka kwa mabeberu. Hamfanyi jambo mpaka muelekezwe la kufanya. Rasilimali zenu zinaporwa na mnakuwa hamna kauli ila kwa yale mnayoruhusiwa kufanya. Kwa nchi zetu za Afrika Mashariki, ukiacha Al Qaidah, hivi sasa tumeletewa adui mwingine, Al Shabab. Wote hawa ni katika ule mkakati kwamba adui anahitajiwa kuwezesha agenda ya kijeshi ifaulu ambayo inakuwa ni kuwafuata Al Qaida na Al Shabab. Katika mchezo huu, tunahadaiwa tunaletewa m a g a i d i , wa n a t u u wa na kuharibu mali. Kisha tunapewa mafunzo (polisi) ya kupambana na magaidi. Tunajazwa ukatili wa kutuwezesha kumlaza mwananchi mwenzetu kitandani na kumpiga risasi kichwani tukiwa tumemfunga pingu. Tunajazwa mafunzo ya kututoa ubinadamu wetu kuwa baada ya kumuua mwananchi mwenzetu asiye na hatia kwa kumpiga r i s a s i s i t a k i c h wa n i , tunakosa soni bali tunavaa uso wa kihayawani kumsingizia kuwa ni gaidi hatari tuliloliuwa baada ya kutushambulia kwa risasi. Alipotukosa, tukamuwahi. H a y a n d i y o y a n a y o w a k u t a wa n a o t u h u m i wa k wa u g a i d i n c h i n i K e n ya hivi sasa. Haya ndiyo wanayofanya askari wa ATPU Kenya. Hatima ya yote haya, ni vurugu na kuuwana Wakenya kwa Wakenya. Analohakikisha beberu ni kuwa watuhumiwa wa ugaidi hawakosekani kila uchao, na askari katili wa ATPU wanazidi kupewa mafunzo na posho zao kupitia msaada wa mamilioni ya dola kutoka kwa mabeberu kila mwaka. Ya p o m a m b o m t u unaweza kufanya kwa ujinga. Lakini hili la

Uislamu katika mizani


Na Dr. Ahmed Abdulatif
SHUKRANI zote anastahiki Mwenyezi Mungu ambaye amemuumba Binadamu na akamfundisha ubainifu (Uwazi) na akainyanyua mbingu na akaweka mizani. Ama baada ya utangulizi huu mfupi, kwa hakika ulimwengu umeuweka Uislamu kwenye mizani ili wauhukumu lakini mizani inatofautiana na kauli zinazogongana tunaikuta hukumu juu ya Uislamu ni kinyume na ni kuuludhumu na ni kuvuka mipaka ya haki. Uhakika wa mambo ya Dini ya Kiislamu imeepukana na hayo yote. Kwani dini ya Kiislamu ni Dini ya Amani na Usalama Dini ya upole na utulivu. Dini ya ukati na kati, uwastani na uadilifu (Usawa) na Dini iliyompa kila mtu haki yake na ni Dini ya kimaumbile ya binadamu na Dini nyepesi na tabia njema na mwenendo mzuri. Na wenye kudhibitika na ni Dini ya Elimu na utamaduni na bidii na kufanya kazi na ni Dini ya maendeleo na ni Dini ya ushindi na utukufu na ni dini ya afya na usafi. Nayo ndio Dini ya Mwenyezi Mungu Mtukufu na ni Dini ya kila nabii na mitume (a.s) SUALI moja ninajiuliza mimi Mwenyewe, kwanini dini hii tukufu inatuhumiwa kwa tuhuma hizi zote ambazo ni uongo mtupu? NA JIBU: Kwa hakika wao sababu na wao kuuweka Uislamu katika mizani mbovu na ya dhuluma kwani baadhi yao wana uhukumu Uislamu kwa kuwatazama baadhi ya Waislamu ambao wanajinasibisha na Dini hii katika zama hizi wakawakuta baadhi yao watu wa dhuluma wengine masikini wengine wanatengana na wengine maadui na wengine wanatisha kwa tabia zao za kinyama isipokuwa waliorehemewa ujinga tu walionao kwamba dini yao ya Kiislamu ndio sababu ya hayo yote. Ninaapa kwa Mwenyezi Mungu, Uislamu yaliyotajwa katika matusi yao kwa yale wanayoyaona kwa baadhi ya hali ya waumini wake kwani hawa wanakwenda kinyume na mafunzo ya Uislamu na wameacha vyanzo vya Diini na misingi yake na hawakuyafanyia kazi kwa upande wa maisha yao na muamala wao wengine wanauweka Uislamu katika mizani ya upande wa ugaidi pale walipowaona wanaoliunga hilo kwa ujinga wao upande wa Dini pamoja na kujinasibisha na Dini hiyo kwa ujinga wao wanajiingiza katika kazi ya ugaidi kwa kuwaua wasio na hatia wala makosa. Kwa wanayoyafanya watu hawa makosa watu hawa kwani Uislamu unaamrisha Amani amesema Mwenyezi Mungu Enyi mlioamini ingieni katika sheria za Uislamu zote na wala msifuate nyayo za shetani kwani yeye kwenu ni adui wawazi. Surat AlBakarat aya ya (208). Na miongoni mwao wapo wanaochuma makosa ya makusudi na kuuzushia Uislamu hayo yote kwa dhuluma na kwa uadui kama kwamba wanataka kuizibia njia ya Mwenyezi Mungu n a wa k a we k a u s h a h i d i juu ya madai yao kwamba Uislamu unahimiza jihadi pale unapofanyiwa uadui kwa kuchukua dalili kauli yake Mwenyezi Mungu Na atakayekufanyieni uadui, basi wafanyieni uadui. Albakarat (194) Na tunajiuliza na kukaa pembeni ni kujibu uadui? Na ajabu jambo hilo lakini sisi tunajisifu kwa kuwa dini yetu inatuamrisha tulipize Uadui

vile vile na hii nikuonyesha wazi uadilifu na utukufu wa dini hii amesema Mwenyezi Mungu (na piganeni katika njia ya Mwenyezi Mungu wale ambao wanaopigeni nyinyi na wala msivuke mipaka hakika mwenyezi Mungu hawapendi wavukao mipAka). Surat Al-bakarat aya ya (190) Jee, hapo kuna ugaidi? Bali wengine wanaotaka kujibu uadui kwa kuuweka Uislamu kwenye ncha ya ugaidi basi mizani yao imegeuka kwani magaidi ni wale ambao wanaovuka mipaka duniani kwa kuzifanyia uadu ardhi nafsi na rasilimali bila ya haki. Na miongoni mwao wa p o wa n a o i g a a m b a o wanawasikiliza wanaoutaka Uislamu bila ya kuilazimisha nafsi yake kutafuta uhakika wa Uislamu na wanakiri na kujitambulisha kutokana na vyanzo vya asili na wala hawazigeukii kauli za wana chuoni wasio Waislamu katika Elimu nyingi na matunda ya elimu toka katika Qur ani na suna na wanatosheka na wanayoyasikia toka kwa wa n a o t u k a n a d i n i wa l e ambao wana malengo yao na maslahi katika kuupakazia Uislamu mabaya. Bali hakika Dini ya Uislamu nayo ni Dini ambao amekuja nayo nabii wote nabii Nuhu amesema (Na nimeamrishwa niwe miongoni mwa Wa i s l a m u ) n a I b a h i m u amesema (nimenyeyekea kwa Mola wa Ulimwengu) amesema Nabii Yakubu kuwambia watoto wake (hakika Mweneyezi Mungu amekuchagulieni Dini musife isipokuwa mufe Waislamu) amesema Suleimani (na nijilieni mimi Waislamu) na Issa (Wamesema (na shuhudilieni kwamba mimi ni Muislamu) na akasema Mussa (na kwa Mwenyezi Mungu tegemeeni ikiwa nyinyi ni Waislamu) na aya nyingine za Qur-an zinashuhudia juu ya hilo. Mwenyezi Mungu ndiye muwezeshaji.

Habari

RABIUL THAN 1435, IJUMAA FEBRUARI 14-20, 2014

AN-NUUR

Inatoka Uk. 1 Kundecha, amesema mchakato huo utawahusu Makadhi watakaofanya kazi chini ya Jumuiya na Taasisi za Kiialamu. Tu n a wa o m b a wa l e wote waliohitimu masomo ya Shariya (Digrii ya Sharia) katika vyuo mbalimbali kuwasilisha vyeti na wasifu (CV) katika Ofisi za Baraza Kuu na Ha-y-at, wakati tukielekea katika mchakato wa kuanzisha vituo vya Kadhi kwa mujibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu. Amesema Amir Kundecha. Na Hassan Kombo

Baraza Kuu, Ulamaa kuteuwa Makadhi


Alisema, hatua hiyo imefikiwa katika kikao kilicho wakutanisha v i o n g o z i wa J u m u i ya na Taasisi za Kiislamu pamoja na wale wa Ha-y-at Ulamaa, Jumamosi ya wiki iliyopita Kariakoo Jijini Dar es Salaam. Amir Kundecha, alisema kwamba baada ya zoezi la kupokea wasifu wa wanataaluma hao katika fani ya Sharia ya Kiislamu, watawaita tayari kwa usaili (Interview). Alisema, zoezi hilo la kupokea wasifu kutoka kwa Waislamu litakoma Februari 28, 2014, hivyo aliwataka wale wote wenye sifa na vigezo vinavyo kidhi haja kuwahi kuwasiolisha vyeti vyao katika ofisi za Hay-at Ulamaa na Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu (T). A l i s e m a , wa m e f i k a maamuzi hayo kutokana na kwamba Serikali imeshawaruhusu Waislamu kuendelea na zoezi hilo katika Taasisi zao juu ya jambo hilo. Kwa maana hiyo Amir Kundecha, alisema wanaimani kwamba hata Ofisi za Ha-y-at na Baraza Kuu nazo pia zinawajibika kuwa na jambo la namna hiyo, kwani aliongeza kusema huduma hiyo inatakiwa itolewe kwa kiwango cha kutosha na haitoshi kuwa katika eneo moja tu. Amir Kundecha, alifafanua kuwa kwa muda wote huo tokea Serikali itoe amri hiyo, walikuwa katika mchakato wa kujipanga kwa kuandaa Ofisi na vituo katika Mikoa na Wilaya, jambo ambalo tayari limekamilika na hatua inayofuata ni kutafuta wenye sifa na

KUNA mfuko wa Rais Bush wa Kupambana na Ugaidi Afrika Mashariki (President Bushs East African Counterterrorism Initiative). Pia kuna Scholarship za B a l o z i k wa wa s i c h a n a (The Ambassadors Girls Scholarship Program). Usisahahu pia Mfuko wa elimu Afrika (African education initiative). Unajua misaada na mifuko hii inavyowaathiri Waislamu na Dini yao? Wanazitumia pesa hizo kuwasomeshea Wa a l i m u wa K i i s l a m u , kuandaa mitaala na vitabu, kuwalipa mishahara waalimu, na viongozi wa jamii, na kusaidia pia kipesa watoto wa masikini. Wameanzisha pia Kituo cha Vitabu vya rejea vya madrasa Zanzibar (The Zanzibar Madrasa Resource Centre). Misaada hiyo Marekani kwa kupitia mradi wa MKEZA (Mradi wa Kuendeleza Elimu Zanzibar) imekwisha kujenga madrasa 16 (mpaka mwaka 2007) moja ya madrasa hizo aliyotembelea mke wa Bush, Laura, Julai 2005. Na kwa mujibu wa USAID wenyewe M a r e k a n i n i wa f a d h i l i wakubwa kwenye nyanda ya elimu huko Zanzibar. Kwa upande wa Tanzania bara, USAID kwa kushirikiana n a B A K WATA wa m e t o a kitabu cha Mwongozo wa kufundishia walimu wa Kiislamu. USAID pia imetoa mafunzo kwa walimu 54 wa madrasa ya kuwafundisha watoto wa Kiislamu namna ya kupambana na UKIMWI. Mwongozo huo wa vitabu 2,500 uligawanywa kwa walimu wa madarasa Dar es Salaam na Iringa. (Taarifa hizi zote zimepatikana kutoka katika tovuti ya USAID/

Tunavurugwa bila kujua


Tanzania). Kwa mujibu wa hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali (SMZ) kuhusu makadirio ya mapato na matumizi ya fedha ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali kwa mwaka wa fedha 2013/2014: Elimu ya madrasa na vyuo vya Quran Anasema, Mheshimiwa Spika, Idara hii inashughulikia j u m l a ya m a d r a s a / v y u o vya Kur- ani 2,251. Aidha zipo skuli za maandalizi za madrasa 84, Unguja na Pe m b a z i n a z o s i m a m i wa na kuhudumiwa kupitia Kituo cha Zanzibar Madrasa Resource Centre (ZMRC), ambazo ufundishaji wake unafuata misingi ya dini ya Kiislamu. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, Wizara kwa kushirikiana na Shirika la UNICEF inakusudia kutoa mafunzo kwa walimu wa madrasa/vyuo vya Kur-ani 350, Unguja 200 na Pemba 150. Pia itaendelea kufanya ziara mbali mbali za kikazi katika madrasa na vyuo vya Kur-ani pamoja na kusaidia kutatua changamoto zinazowakabili pamoja na kushajiisha kufanya ziara za pamoja za kubadilishana uzoefu. Je, unadhani watu hawa, wa f a d h i l i h a wa k u t o k a Marekani, wana jema lolote kwa misaada yao hii kwa madrasa zetu? Wakoloni wa Kiingereza na maeneo mengineo hawakukata tamaa na k u w a a c h i a Wa i s l a m u waendelee kujitawala wenyewe katika maeneo yao wala hawakukusanya misahafu na kuitia moto, bali waliweka mikakati ya kuitoa Quran katika maisha ya Waislamu. Waliweka Mitaala katika mifumo yao ya elimu iliyo wahakikishia k u wa k i z a z i k i t a k a c h o elimishwa kupitia mitaala hiyo kitatoa Waislamu wengi wasio na haja hata ya kuisoma Quran, wachache watakao penda kuisoma wasielewe, watakaoielewa wasiingize katika maisha yao ya jamii bali iishie katika kuiendea kwenye ibada maalumu za swala, zakat, swaumu hija nk.k na wale wachache watakaoingiza Quran katika maisha ya jamii wapigwe vita na kusalitiswa na Waislamu wenzao na kuitwa wazushi, siasa kali, magaidi n.k. Kwa marejeo haya ya historia itoshe kuona kuwa hali waliyonayo Waislamu, takribani ulimwenguni kote, katika suala la kuiendea Quran sio jambo lililotokea kwa bahati nasibu, bali ni mikakati ya makusudi i l i y o f a n y wa n a n c h i z a kitwaaghuut katika harakati za kuitawala dunia kinyume na Mwongozo wa Allah (Subhaanahu wa Taala). Matatizo yote tuliyokuwa nayo tumeyapata baadaya kuiacha Quran na kuwafuata maadui zetu (Matwaaghuut) na hawaa za nafsi zetu. Iweje leo tuweze kuwa na matatizo hali kuwa tunao muongozo wa kutuwezesha kupata suluhisho la matatizo yetu, ni baada ya kuiacha kuingiza Qurani katika mfumo wa maisha yetu. Amesema Mwenyezi Mungu, K wa h a k i k a wa n a y o yakataa mawaidha haya yanapo wajia (wataangamia), na haya bila ya shaka ni Kitabu chenye nguvu na utukufu (Fuss'ilat 41:41) Hautakifikia upotovu mbele yake wala nyuma yake. Kimeteremshwa na Mwenye hikima, Msifiwa (Fuss'ilat 41:42) Hii Quran tumeletewa ili tuweze kuisoma kwa kuizingatia na kuitekeleza kwa kile ambacho imetuelekeza. Amesema Allah (Sw), Na hiki Kitabu, tumekuteremshia wewe, kimebarikiwa, ili wazizingatie Aya zake, na wawaidhike wenye akili. ( Saad 38:29) Ama mimi nimeamrishwa nimuabudu Mola Mlezi wa mji huu aliye ufanya ni mtakatifu; na ni vyake Yeye tu vitu vyote. Na nimeamrishwa niwe miongoni mwa Waislamu, wenye kunyenyekea.(Naml 27:91 ) Na niisome Qur'ani. Na mwenye kuongoka, basi ameongoka kwa faida ya nafsi yake; na aliye potea basi sema: Hakika mimi ni miongoni mwa waonyaji. .(Naml 27:92 ) Kwa kutoifuata Quran na kuwafuata matwaaghuut na Hawaa za nafsi zetu, Wa i s l a m u n d i o s a b a b u inayotufanya kuweza kupata tabu na mateso katika mfumo mzima wa maisha yetu ya kibinafsi na kijamii, na hili ni angalizo ambalo tumepewa kwenye Quran. Amesema Allaah (Sw): A k a s e m a : O n d o k e n i humu nyote, hali ya kuwa ni maadui nyinyi kwa nyinyi. Na ukikufikieni uwongofu kutoka kwangu basi atakaye ufuata uwongofu wangu, hatapotea wala hatataabika (TaHa 20:123) Na atakaye jiepusha na

watakaokidhi haja katika taaluma hiyo. Sasa kinachofuata ni kutafuta Makadhi katika utaratibu unaokubalika kisheria kasha tutafanya nao semina tayari kwa kuanza kazi rasmi kwa mujibu wa Jumuiya na Ta a s i s i z a K i i s l a m u . Alisema. Alisema, zoezi hilo litasimamiwa na Msheikh kutoka Hay-at Ulamaa katika mchakato wa kuwachuja Makadhi hao, ambao watakuwa wakifanya kazi chini ya Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu (T).
mawaidha yangu, basi kwa yakini atapata maisha yenye dhiki, na Siku ya Kiyama tutamfufua hali ya kuwa kipofu. (TaHa 20:124) Amesema Allah (Sw): Na Mtume alikuwa akisema: Ee Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wameifanya hii Qur'ani ni kihame. (Al Furqan25:30) Baadhi ya maswahaba wa l i s h a n g a a u k u u l i z a vipi wameihama (Kuipa mgongo) Quran hali yakuwa wanaisoma? Alisema Mtume (Saw) Umekuwa mzigo kwa mama yako ewe! Ziad, nilikuwa ninakuona kuwa ni mtu m we n ye u f a h a m u z a i d i katika Maddina (Je, Nyinyi sio kama) Mayahud na Manasara ambao mkononi mwao wana Tourati na Injili wala hawanufaiki navyo nachochote. (Ahmad) K wa h i v y o p a m o j a n a kuwa nayo Quran lakini hatunufaiki nayo kibinafsi wala kijamii, kama sawa na Mayahud na Manasara. Katika hali halisi tuliyo nayo viongozi wa kitwaaghuut ambao hawana ufunuo kutoka kwa Allaah (Subhaanahu wa Taala) ndio ambao ambao wanaotuundia mfumo wa maisha yetu vile wao wanavyoataka tuwe. Pamoja na kwamba matwaaghuut wana mchango mkubwa wa kutufanya tuweze kuipa mgongo Quran, lakini sisi wenyewe kwa sehemu kubwa pia tunao mchango wetu kwa kufuata hawaa za nafsi zetu kwa kuisaliti Quran. Hivyo inatupasa kujiuza na kupatia majibu mambo yafuatayo; Je, pale tunapoisoma au kuisikiliza Quran kwenye swala nk. Tunakuwa tupo hadhiri na kufahamu kile Inaendelea Uk. 7

4
Na Shaban Rajab
A M A k we l i M we n ye z i Mungu humjaalia amtakaye neema zake, kwa vigezo a m b a v y o n i s i r i ya k e mwenyewe muumba. Wakati mwingine utajiri si kwa uhodari, akili nyingi au ujanja wa mtu, bali ni kwa hiari yake mwenyewe Allah (sw). Hata hivyo lililo dhahiri k wa m wa n a d a m u k wa mujibu wa mafundisho ya Mwenyezi Mungi, ni kwamba utajiri au ukwasi, ni mtihani mkubwa kwa mwanadamu. Kwamba rizki za watu wengine kwa namna moja au nyingine, zimehifadhiwa ndani ya utajiri wa mtu. Hata hivyo, rizki na haki za wengine zilizohifadhiwa k wa m k wa s i , z i n a we z a zikapatikana iwapo aliyepewa dhamana hiyo na Mwenyezi Mungu, atatambua hadhi ya aliyempa utajiri huo, yaani Mwenyezi Mungu, akawa mwadilifu na mwenye busara katika kuutendea haki ukwasi aliojaaliwa, ili na wengine waweze kupata rizki zao wa l i z o p a n g i wa k u p i t i a ukwasi huo. Kinyume cha tajiri kushindwa kufanya uadilifu katika mali yake, basi ni kuangukia katika majaribu n a m i t i h a n i m i k u b wa , ikiongozwa na kibri, fahari, israafu, ria, dhulma, dharau nk. Alhaj Aliko Dangote, alizaliwa April 10, 1957 katika jimbo la Kano lililopo Kaskazini mwa Nigeria. Dkt. Dangote ambaye maskani yake yapo jijini Lagos, alipata taaluma ya biashara katika Chuo Kikuu cha Al-Azhar cha jijini Cairo nchini Misri. Kwa sasa ndiye mmiliki, Mwenyekiti na Mtendaji M k u u wa k a m p u n i ya Dangote Group. Inaelezwa kwamba utajiri wa D k t . D a n g o t e h a d i kufikia Novemba mwaka jana (2013) ulikuwa ni dola za Kimarekani bilioni 20.8, kiasi kilichomfanya kuwa tajiri namba moja Afrika kwa muda wa miaka mitatu mfululizo, kwa mujibu wa jarida maarufu la Fobes. Alhaj Dangote ni mtoto wa mzee Mohammed Dangote na mama Mariya Sanusi Dantata. Amelelewa na wazazi wake katika maadili kamili ya Kiislamu. Familia ya Dangote ni miongoni mwa familia zilizokuwa na uwezo huko Kano. Kampuni ya Dangote Group iliyoanzishwa mwaka 1977, shughuli zake zikiwa ni kuuza bidhaa mbalimbali nchini Nigeria, hususan bidhaa za vyakula. Le o k a mp u n i h i y o si ya kuuza bidhaa tu, bali ni kampuni inayomiliki

Mkwasi namba moja Afrika Alhaj Dkt. Aliko Dangote


Utajiri ulianza kwa kuuza pipi

Makala

RABIUL THAN 1435, IJUMAA FEBRUARI 14-20, 2014


watu wengi zaidi Afrika Magharibi. Pamoja na kujishughulisha na biashara hizo, pia kampuni ya Dangote imeingia katika biashara ya sekata ya mawasiliano na imeshaanza ujenzi wa njia za mawasiliano (fibre optic cables) kilometa 14,000 ili kukidhi mawasiliano kwa nchi nzima ya Nigeria. Matokeo yake, Dangote Group ilitunukiwa tuzo Januari 2009 kwa kuongoza kwa kutoa ajira katika sekta ya ujenzi nchini Nigeria. "Let me tell you this and I want to really emphasize it...nothing is going to help Nigeria like Nigerians bringing back their money. If you give me $5 billion today, I will invest everything here in Nigeria. Let us put our heads together and work." Amenukuliwa akisema Alhaj Dangote, akisisitiza falsafa yake kuwekeza zaidi nchini mwake na kuwataka Wanigeria kuingiza zaidi mitaji nchini humo na kushirikiana kufanya kazi pamoja. Itakumbukwa 23 Mei 2010, gazeti la Daily Mirror la Uingereza liliripoti kuwa Alhaji Dangote alikuwa akitaka kununua asilimia 16 za hisa za klabu ya soka ya A r s e n a l z i l i z o k u wa zinamilikiwa na Lady Nina Bracewell-Smith. Hata hivyo Alhaji Dangote alikana tetesi hizo. Novemba 14, 2011, Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan alimtunukiwa Alhaj tuzo maarufu heshma ya juu nchini Nigeria ya Grand Commander of the Order of the Niger (GCON). Alhaj Dangote amekuwa akijitolea sehemu ya mali yake kusadia wasiojiweza, waliothiriwa na majanga kama mafuriko, ukame nk. Aidha imekuwa ikiripotiwa kwamba amekuwa kishiriki katika hafla za kugawa zaka nchini Nigeria. Hata hivyo kuna mashaka iwapo mali yake inatolewa zaka kama inavyotakikana, maana hata hapa kwetu hatujawahi kusikia wakwasi wakishiriki katika kutoa zaka kwa kiasi cha mali zao, zaidi ya misaada isiyokidhi katika jamii, hususan siku za Ijumaa.

AN-NUUR

Alhaj Dkt. Aliko Dangote,


n a k u e n d e s h a v i wa n d a vya kutengeneza bidhaa mbalimbali katika nchi kadhaa za Afrika, hususan katika nchi za Benin, Cameroon, Togo, Ghana, Afrika Kusini na Zambia. Alhaji Dangote, ambaye mwaka jana alizuru nchini, hivi sasa kampuni yake ndiyo inajenga kiwanda kikubwa cha saruji nchini mkoani Mtwara, kiwanda ambacho kitakuwa kikubwa zaidi cha kuzalisha saruji kwa Afrika Mashariki na Kati. Kwa mujibu wa viwango vya utajiri vya jarida la Forbes, Dangote anashika nafasi ya kwanza ya utajiri barani Afrika huku akiwa tajiri wa 43 katika matajiri wakubwa kabisa duniani. Tangu awali akiwa kijana mdogo kabisa, inaelezwa kwamba Alhaj Dangote a l i k u wa n a m v u t o wa kibiashara. Labda kutokana na historia ya wazazi wake kuwa watu wa biashara. Mwenyewe alinukuliwa na gazeti la The Nation la Nigeria akisema, "I can remember when I was in primary school, I would go and buy cartons of sweets and I would start selling them just to make money. I was so interested in business, even at that time." Yaani anasema, Naweza kukukumbuka nilipokuwa nasoma shule ya msingi, nilimudu kununua katoni ya pipi na kuanza kuziuza ilimradi tu nipate pesa. Nilikuwa ninavutiwa sana na kufanya biashara tangu kipindi hicho. Baada ya kumaliza shahada yake ya biashara katika chuo kikuu cha Al-Azhar Cairo, Misri, alirejea nyumbani Nigeria na kuomba mkopo kutoka kwa mjomba wake aliyeitwa Sanusi Abdulkadir Dantata. Naye alimpatia mtoto wa dada yake huyo kiasi cha fedha za Nigeria Naira 500,000 na kuanza shughuli za biashara, wakati huo Dangote alikuwa na umri wa miaka 21. Kwa sasa Dangote Group imepanua zaidi shughuli zake za biashara kuanzaia viwanda vya kusindika vyakula (food processing), kutengeneza saruji, kusafirisha shehena (freights), kutengeneza na kusambaza sukari, kutengeneza na kusambaza vinywaji baridi, mikate, biashara ya mafuta na gesi, usafirishaji wafanyakazi huko Nigeria nk. Kwa ujumla kampuni hiyo inashika karibu asilimia 70 ya soko la bidhaa na huduma zake nchini Nigeria. Inaelezwa kuwa Dangote Group ndio kampuni kubwa zaidi ya kutengeneza na kusambaza bidhaa za vyakula bara la Afrika na inashika nafasi ya tatu katika huduma hizo kwa dunia nzima, ikizalisha jumla ya tani 800,000 za sukari kila mwaka. Mbali na hilo Dangote Group inamiliki viwanda vya kutengeneza chumvi, unga na ndio kampuni kubwa ya kuingiza mchele, samaki, tambi, mbolea na saruji nchini Nigeria. Kampuni hiyo pia husafirisha pamba, korosho, cocoa, mbegu za sesame, tangawizi katika nchi kadhaa za nje. Pia kampuni imewekeza katika sekta ya fedha na ardhi na viwanda vya nguo. K a m p u n i ya k e i m e a j i r i watu 11,000 na kuifanya kuwa kampuni iliyoajiri

Aidha kuna haja ya Taasisi za Kiislamu z i na z o a m i ni k a , k uwa na utaratibu rasmi wa kutoa zaka, ambao utawashirikisha pia wakwasi ili kufikia malengo yanayotakikana. Tukirejea katika enzi za Khalifa Umar (ra)

kuhusu suala la zaka, hakika tutafika pale kila Muislamu anapopatamani kufika, kuikomboa jami ya Kiislamu dhidi ya umaskini na ufukara.

Habari za Kimataifa

RABIUL THAN 1435, IJUMAA FEBRUARI 14-20, 2014

AN-NUUR

BANGUI Mashirika ya kutoa misaada Jamhuri ya Afrika ya Kati yameonya kuwa endapo Waislamu nchini humo wataendelea kulihama taifa hilo, njaa itawamaliza raia wa Taifa hilo. Taarifa kutoka Bangui zinaeleza kwamba tayari masoko nchini humo yameanza kuwa matupu na bidhaa za vyakula kuwa haba. Mashirika ya kutoa misaada ya Oxfam na lile la Action Against Hunger, yamesema kuwa ni chini ya maduka kumi ya jumla ndiyo yaliyosalia katika mji mkuu wa nchi hiyo huku wa f a n ya b i a s h a r a we n g i wakiendelea kutoroka taifa hilo. Umoja wa Mataifa umekadiria kwamba watu milioni 1.3, ikiwa ni zaidi ya robo ya idadi ya watu nchini humo wanahitaji msaada wa haraka wa chakula kufuatia machafuko ambayo jamii ya kimataifa nayo imeonekana kushindwa kudhibiti hali na wafanyabiashara wakiwa wameondoka na biashara zao. Immeelezwa kuwa Waislamu ndio wanaomiliki sehemu kubwa ya biashara katika nchi hiyo kutoka nchi za jirani, na ndio ambao wamekuwa wakisambaza huduma muhimu za bidhaa za vyakula kama sukari, unga wa mahindi na ngano, sabuni, mafuta ya kupikia na vitoweo kwa watu zaidi ya 800,000 wa mji wa Bangui na miji mingine nchini humo. Bei za bidhaa za vyakula zimepanda kwa asilimia ishirini tangu Novemba, huku bei ya nyama ikiwa imepanda zaidi ya mara mbili ya bei iliyokuwepo awali kufuatia wafugaji kukimbilia porini na mifugo yao. Katika soko la Petevo, lililopo karibu na ukingo wa mto Oubangui Kusini mwa mji wa Bangui, limebaki tupu huku huduma ya kitoweo ikififia tangu kuondoka Waislamu, ambao ndio waliokuwa wanamiliki biashara za mifugo kutoka Chad. Imeelezwa kwamba kitoweo pekee kilichopo ni nyama ya nguruwe ambayo ni kidogo sana kutokana na nguruwe kufugwa kwa uchache na wenyeji. Kwa sasa kuna upungufu mkubwa wa nyama kwa sababu wafugaji wamekimbilia msituni na wakati wanapochinja mifugo yao, bei huwa ghali sana. Tuna mashaka makubwa s a n a k wa s a b a b u i wa p o upungufu huu utaendelea kidogo tu, tutakufa kwa njaa, alinukuliwa akisema

Kuondoka Waislamu Afrika ya Kati kwaleta njaa


Nadege Kodo, mama aliyekuwa akitafuta bidhaa za nyumbani. Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na shirika la Oxfam na Action Contre la Faim, usambazaji wa bidhaa za majumbani Bangui kutoka kwa wafanyabiashara wakubwa wa jumla ambao walikuwa wakiingiza bidhaa nchini humo, umepungua sana kufuatia wafanyabiashara hao kuondoka na inakisiwa wamebaki kumi tu, ambao muda wowote nao wataondoka iwapo hali ya usalama haitaimarishwa. Ta ya r i k u n a u h a b a mkubwa wa chakula Jamhuri ya Afrika ya Kati na hali inatarajiwa kuendela kuwa mbaya zaidi, alisema Steve Cockburn, Meneja wa Kanda wa Oxfam. Kufuatia hali hiyo, mashirika hayo yameonya kuwa chakula kinapungua kwa kiasi kubwa nchini humo na kwamba bei za vyakula huenda zikapanda mara dufu na kuna uhaba mkubwa. Umoja wa Mataifa unakadiria kuwa zaidi ya asilimia tisini ya raia wa nchi hiyo, wanaishi kwa kula mlo mmoja kwa siku na kwamba hali hiyo huenda ikawa mbaya zaidi. Shirika la World Food Programme lina malori 27 yaliyobeba mahindi na mchele lakini yamekwama katika mpaka wa Cameroon huku madereva wakikataa kuendelea na safari. Sasa shirika hilo linapanga kusafirisha kwa ndege tani 90 za chakula kwa siku kutoka Cameroon mwezi ujao na gharama yake ikiwa ni zaidi ya mara tano ya gharama ya kusafirisha kwa malori. Hatuna namna nyingine," alisema mfanyakazi mmoja wa WFP, Alexis Masciarelli. Taifa hilo limegawanyika zaidi kufuatia vita vilivyoanza mwaka uliopita kati ya Wakristo ambao ni wengi nchini humo na Waislamu k u f u a t i a m a p i n d u z i ya serikali. Maelfu ya Waislamu tayari wametoroka nchini humo na kutafuta hifadhi katika mataifa jirani ya Cameroon na Chad. Wa i s l a m u we n g i waliofukuzwa na Wakristo wa l i k u wa wa k i c h a n g i a sehemu kubwa katika uchumi wa taifa hilo. Umoja wa Mataifa umesema kuwa ikiwa imesalia chini ya mwezi mmoja kabla ya msimu wa kilimo, zaidi ya asilimia tisini na sita ya wakulima hawana mbegu. Ghasia zinazoendelea zimezuia vyakula kuingizwa nchini humo na ripoti

WAISLAMU nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati wakihama nchi hiyo kuelekea nchi jirani za Chad na Cameroon. zinasema kuwa mamia ya Shirika la Medecins Sans ya Makosa ya Jinai ilisema malori yaliyosheheni chakula Frontiers (MSF) limesema siku Ijumaa iliyopita kwamba yamekwama katika mpakani za hivi karibuni limewatibu i n a k u s u d i a k u f u n g u a mwa nchi hiyo na Cameroon, watu 100 majeraha ya risasi mashataka ya awali kutokana kwa sababu madereva wengi na mapanga katika kambi n a k u we p o u we z e k a n o ambao ni Waislamu, wana iliyopo jirani na uwanja wa mkubwa wa makosa ya kivita wasiwasi wa kushambuliwa. ndege wa Bangui ambako katika machafuko hayo. Shirika hilo la Oxfam, kuna wakimbizi 100,000. Umoja wa Mataifa limesema kuwa endapo Watu wanakuja hapa umesema kuwa zaidi ya watu raia waliosalia hawatapewa bila pua, masikio, chuchu, 2,000 wameuliwa na zaidi ulinzi wa kutosha, hali nchini alisema Lindis Hurum, ya elfu 800,000 wamekimbia Jamhuri ya Afrika ya Kati msimamizi miradi wa MSF nchi, huku nusu ya watu hao huenda ikawa mbaya zaidi. Mahakama ya Kimataifa wakitoka mji wa Bangui.

KHARTOUM Balozi mdogo wa Marekani nchini Sudan, Joseph D. Stafford, amefutwa kazi ghafla mara tu baada ya kusilimu na kuingia katika dini tukufu ya Kiislamu. Hata hivyo msemaji wa ubalozi wa Marekani mjini Khartoum, amedai kuwa balozi huyo aliamua kujiuzulu yeye mwenyewe na kuachia nyadhifa zote za kisiasa. Habari zilizochapishwa na World Bulletin, zimeeleza kuwa Bw. Joseph D Stafford, alijiuzulu nafasi yake baada ya kuamua kusilimu na kuwa Muislamu. Lakini vyanzo vya vyombo vya habari nchini Sudan vimesema kuwa Balozi huyo wa Marekani alilazimishwa kujiuzulu baada tu baada ya kubainika taarifa zake za kusilimu. Stafford mwenyewe ameieleza Idara ya Mambo ya Nje ya Marekani kuwa ameamua kujiuzulu kwasababu zake binafsi, lakini vyanzo vya habari nchini Sudan vimedai kuwa balozi huyo alilazimishwa kujiuzulu baada ya kuamua

Marekani yamtimua balozi baada ya kusilimu

Aliyekuwa Balozi mdogo wa Marekani nchini Sudan, Joseph D. Stafford. kusilimu. Vyanzio hiyo vilibainisha kwamba Bw. Stafford alikuwa akirekodiwa kila alipokuwa anatembelea Makao Makuu ya Ansar alSunnah nchini Sudan, ziara ambazo ziliweza kuanzisha uhusiano wa karibu na idadi

kubwa ya viongozi wa dini ya Kiislamu kufuatia ziara za mara kwa mara za balozi huyo. Idara ya Mambo ya Nje ya Marekani haijatoa maelelzo yeyote kuthibitisha ama kukanusha habari za kusilimu na kuacha kazi Bw. Joseph Stafford. Mara baada ya kujiuzulu, Bw. Stafford aliandika habari katika jarida la Sudan Tribune akisema, "Mke wangu na mimi tumekuwa na bahati ya kukutana na watu wengi wazuri hapa Sudan, ambao tulikuwa na nia na lengo muhimu la kuimaridha jamii zao. Siku zote tutawakumbuka na nchi yenu nzuri, na natambua kuwa mtaendelea kufanya kazi kwa bidii kwa ajili ya kufikia maisha bora, kama mnavyosema kila siku 'Fi Kulu Harakah Baraka' kila hatua ina Baraka zake. Marekani haijawahi kuteua balozi kamili katika Ubalozi wake wa Khartoum nchini Sudan tangu mwaka 1998 na kwa muda wote huo, shughuli zote za kibalozi n c h i n i h u m o z i l i k u wa zikisimamiwa na balozi mdogo (charge daffaires).

6
DAD, do you believe i n h e a ve n ? H i l o n i swali ambalo kijana mdogo Jeffrey siku moja alimuuliza baba yake wakati wakiwa katika matembezi na kupunga upepo ufukweni (beach). Swali hili kwa lugha na msamiati wa Kiislamu ni sawa na kumuuliza je, unaamini kuwa kuna Pepo? M u u n d o wa s wa l i ukilinganishwa na umri wake wakati huo, ulidhihirisha jambo moja: kuwa ni mdadisi na mtu wa logic na haikushangaza wengi alipokuja kuwa profesa wa hesabu akiwa muhadhiri katika Chuo Kikuu cha Kansas. Dr. Jeffrey Lang ni Profesa wa hesabu katika Chuo Kikuu cha Kansas (University of Kansas), moja ya vyuo v i k u u v i k u b wa s a n a katika Marekani. Safari yake ya kutafuta dini ya haki inaanzia Januari 30, 1954, alipozaliwa katika familia ya Kikatoliki huko Bridgeport, Connecticut. Katika miaka 18 ya kwanza ya maisha yake aliitumia katika shule za Kikatoliki (Catholic schools), hata hivyo, masomo katika shule hi zo, yal i mwac h a n a maswali mengi badala ya kupata majibu na kwa hakika kumchanganya zaidi kuhusu dhana ya Mungu na uhusiano wake na binadamu au viumbe kwa ujumla. Kama kuna Mungu, na huyu Mungu ni Mungu wa upendo na mwenye huruma, kwa nini anawaacha baadhi ya watu wanaishi maisha ya tabu hapa duniani, magonjwa, njaa na hata kuonewa na wanadamu wenzao ( k a m a wa l i v y o k u wa Wa m a r e k a n i We u s i wakibaguliwa na kuonewa na Wazungu wa Marekani). Kwa nini asituchukue tukaishi huko mbinguni tukaepukana na tabu za dunia hii? Kwa nini aumbe watu ili wataabike? A n a s e m a , m a s wa l i kama haya, yaligonga akili yake kila siku na hakupata majibu. Anasema, akiwa sekondari-Notre Dam Boys High, alikuwa akihoji sana juu ya Mungu na wakati mwingine kukataa majawabu aliyokuwa akipewa na walimu na wachungaji akisema kuwa hayana mantiki wala hayakubaliani na akili ya

Profesa Jeffrey-kutoka Ukatoliki hadi Uislamu

Makala

RABIUL THAN 1435, IJUMAA FEBRUARI 14-20, 2014


Hivyo, kila akisoma, anakuta swali lililokuwa kichwani linajibiwa kabla hajauliza. The Quran was always way ahead of my thinking; it was erasing barriers I had built years ago and was addressing my queries. I was being led, working my way into a corner that contained only one choice. Dr. Jeffrey Lang anasema, Quran ilikuwa muda wote imetangulia fikra na mawazo yake na kila akisoma ilikuwa i k i o n d o a v i k wa z o n a kutosheleza kiu yake ya mambo yaliyokuwa yakimtatiza kwa muda mrefu. Mwisho anasema, alijikuta amewekwa katika kibano ambapo, hana jingine ila kusalimu amri. Alikuwa hana namna nyingine ila kusilimu. Katika miaka ya 1980s, kulikuwa na Waislamu wachache sana katika Kampasi ya Chuo Kikuu, University of San Francisco. Wanafunzi w a c h a c h e Wa i s l a m u waliokuwa Chuoni hapo, walikuwa wakiswali swala tano katika chumba kidogo ndani ya Kanisa la Chuo. Kichumba hicho amekitaja kama a small place at the basement of a church. Anasema, alijipa moyo, alipiga moyo konde, siku m o j a a k a wa t e m b e l e a wa n a f u n z i Wa i s l a m u wakati wa swala, aliporejea tayari alikuwa ni mmoja wao. Alikuwa ametamka shahada. Kwa mara ya kwanza aliposwali swala ya jamaa, anasema Imam alikuwa kijana akiitwa Ghassan. Akiwa kavaa kanzu na kofia, kasimama mbele peke yake, huku wengine wa k i wa n y u m a ya k e katika mistari iliyonyooka wakimfuta kila anapotoa takbira ya kuhama, anasema alishtuka sana. Anasema hali hiyo ilimkumbusha ndoto ambayo alikuwa akiiota mara kwa mara zamani wakati huo akiwa haamini kwamba kuna Mungu. Anasema, alikuwa akiota ameingia katika chumba kidogo kuna watu wamesimama katika mistari, lakini mmoja wao yupo mbele peke yake kavaa kanzu na kofia. Wengine wote wapo kimya, yeye tu ndiye anazungumza, wengine wanamsikiliza. Anasema, ndoto hii i l i k u wa i k i m j i a m a r a kwa mara, japo akiamka alikuwa akijiuliza, nini Inaendelea Uk. 7

AN-NUUR

Jeffrey Lang ni Profesa wa hesabu katika Chuo Kikuu cha Kansas (University of Kansas)

kawaida. K a d i r i a l i v y o f a n ya mjadala na Mchungaji wa shule (school Priest), wazazi wake na wanafunzi wake, hawakuweza kabisa kutosheleza kiu yake ya k u m j u a M u n g u . K wa hiyo, kwa mshangao wa mchungaji na wazazi, akatangaza kuwa yeye s a s a h a a m i n i j u u ya M u n g u . Wa k a t i h u o alikuwa na umri wa miaka 18. Na akabaki hivyo kwa miaka 10. Kwa maana mpaka alipokuwa na umri wa miaka 28, alikuwa haamini juu ya kuwepo kwa Mungu wala alikuwa hashughuliki na kwenda kanisani si Jumapili, Krisimasi, Pasaka wala mwaka mpya. Akiwa anafundisha katika Chuo Kikuu cha San Francisco (University of San Francisco), alikutana na mwanafunzi Muislamu akiitwa Mahmoud Qandeel akiwa mmoja wa wanafunzi wake

akiwafundisha hesabu. Alijikuta akiwa karibu sana na mwanafunzi huyu na kuwa marafiki hasa kutokana na mwenendo wake. Urafiki wa Profesa na mwanafunzi wake ukapelekea urafiki kuingia katika familia zao. Hata hivyo, katika muda wote walipoanza urafiki wa kifamilia, kila familia hizi mbili zilipokutana, dini haikuwa kabisa moja ya mada katika mazungumzo yao. Hata hivyo, baadae kabisa familia ya Kiislamu ya mwanafunzi wake, walimzawadia Dr. Jeffrey Lang Quran. Japo hakuwa na hamu ya dini, lakini akaona ngoja tu asome kama kitabu kingine chochote. You cannot simply read the Quran, not if you take it seriously. You either have surrendered to it already or you fight it. It attacks tenaciously, directly, personally; it debates, criticizes, shames, and

challenges. From the outset it draws the line of battle, and I was on the other side. Hayo ni maelezo yake baada ya kuipitia Quran kidogo. Anasema, ukiisoma Quran, utakuta ikikushambulia (kama unafanya mambo yasiyo kubalika), ikijadiliana na wewe juu ya mambo mbalimbali, ikikulaumu, ikikupa changamoto na nasaha, na hata kukuaibisha kwa matendo yako. Kwa hiyo anasema, alijikuta akiwa vitani na Q u ra n . A n a p a m b a n a nayo. I was at a severe disadvantage, for it became clear that the Author knew me better than I knew myself. Hata hivyo anasema kuwa alijikuta akizidiwa nguvu kwani ilielekea kana kwamba mwandishi wa Quran alikuwa akimjua vizuri pamoja na maswali yake yote aliyokuwa nayo kichwani.

7
Inatoka Uk. 6 maana yake, lakini mara akipuuza na kuiacha kama ilivyo. Hivi naota tena au nipo macho, anasema alijuliza akiwa ndani ya swala ilipomjia ile picha ya ndoto aliyokuwa akiota zamani ikiwa sawasawa na jinsi watu walivyokuwa katika chumba kile kidogo wakiswali naye akiwa mmoja wao. Ni kutokana na ndoto hii na historia yake kupitia kwenye Ukatoliki hadi kukanusha Mungu, Dr. Lang anasema, hawezi kusema kuwa amefanya juhudi kubwa sana kutafuta ukweli juu ya Uislamu, ila anamshukuru Mwenyezi Mungu kuwa ndiye pekee a l i ye m w o n g o z a h a d i kusilimu. Mtoto kama baba Baba kwa nini tunaswali (Daddy, why do we pray)? Hili ni swali ambalo binti wa Dr. Lang aitwaye Jameellah akiwa na miaka minane (8), siku moja alimuuliza baba yake baada ya kumaliza swala ya dhuhuri. Sikutarajia kuulizwa swali hili kutoka kwa mtoto wa miaka minane na kwa hiyo sikuwa na jawabu la haraka. Anasema Dr. Lang, hata hivyo akisema kuwa swali la binti yake huyo mdogo, linamkumbusha swali la kiudadisi kama hilo ambaye naye alimuuliza baba yake Mzee Lang. Yeye alimuuliza, unaamini kuwepo kwa Pepo? Anasema, swali kama hilo la kimantiki na kitafiti, l i n a m p a f a r a j a k u wa huenda binti yake huyo akawa msomi wa kiwango cha hali ya juu. Wasomi wa kiwango cha juu kabisa katika fani mbalimbali, ndio wanatakikana katika ulimwengu wa leo kufanya D a wa h n a h a o n d i o watakaouhuisha Uislamu ukarejesha heshma yake. Baada ya kutafakari k wa m u d a , a l i m j i b u : Tunaswali kwa sababu Mwenyezi Mungu anatutaka tuswali. Jameellah akauliza tena, lakini kwa nini? Kwa nini Mungu atuamrishe kuswali? Swala ina faida gani kwetu? M a s wa l i ya l i k u wa mazito na uzito wake unakuwa kwamba Dr. Lang alikuwa akipata tabu ni kwa vipi na kwa maelezo gani mepesi atatumia binti yule wa umri mdogo apate

kuelewa. Binti yangu ninaye kupenda sana, ni vigumu kueleza kwa mtoto mdogo kama wewe ukaelewa. We endelea tu kuswali swala tano kila siku, nina uhakika itafika siku utaelewa kwa n i n i t u n a s wa l i . H a t a hivyo, ngoja nijaribu kukufahamisha. Huku akimshika kichwa kwa upendo akasema: Honey Binti yangu, si unaona nakupenda, lakini Mungu ndiye chanzo cha upendo, huruma, ukarimu, hekma, busara na uzuri wa kila kitu kinachotuzunguka katika maisha. Kama unavyoona, jua ndio chanzo cha mwanga tunaouona wakati wa mchana. Lakini Mungu ndiye chanzo cha vyote hivyo na vingine usivyovijua. Kwa hiyo, upendo nilio nao kwako, kwa dada zako na kwa mama yako, unatoka kwa Mungu, ni Mungu kanipa. Tunajua kuwa Mungu ni mkarimu sana kwa kutupa yote mazuri katika maisha yetu. Tunaposwali tunapata hisia za upendo wa Mungu na ukarimu wake kwetu kwa namna ya kipekee kabisa na yenye athari kubwa katika mioyo yetu. Binti yangu, chukua mfano huu: unajua k u wa m a m a ya k o n a mimi tunakupenda sana na tunafanya kila tuwezalo kukuhudumia, kukuhurumia na kukulinda. Lakini tunapokukumbatia na kukubusu, bila shaka unapata hisia za upendo wa hali ya juu na za ndani kabisa jinsi tunavyokupenda. Ni vivyo hivyo, tunajua Mungu anatupenda sana na ni mkarimu kwetu, lakini tunaposwali, tunapata hisia za ndani kabisa na za kipekee juu ya upendo, huruma na ukarimu wake kwetu. Hayo yalikuwa maelezo ya Dr. Lang kwa binti yake Jameellah aliyetaka kujua ni kwa nini tunaswali. Does praying make you a better daddy? Je, swala inakufanya kuwa baba mwema zaidi, inakufanya kuwa baba mzuri zaidi (kwetu na kwa mama?) Jameellah alimuuliza tena

Profesa Jeffrey-kutoka Ukatoliki hadi Uislamu


baba yake. Kwa ufupi maelezo ya Dr. Lang yalikuwa kwamba unapomjua Mungu, ukawa unaswali, unakuwa katika nafasi ya k u o n a h u r u m a ya Mungu kwako, upendo wa Mungu kwako, neema za Mungu kwako kwa hiyo ukizingatia jinsi Mungu anavyokupenda na kukuhurumia, lazima nawe utakuwa na huruma kwa binadamu wenzako ukianzia na watu wa familia yako. Lazima utataka ile huruma ya M u n g u k wa k o n a w e umfanyie mkeo na watoto wako. U m e n i e l e w a Jameellah? Je, mimi si baba mwema kwako? Jibu la Jameellah lilikuwa kumkumbatia baba yake na kumwambia: I love you, Daddy! (nakupenda baba yangu.) I love you too, sweetie pie. I love you too. Alijibu Dr. Jeffrey Lang kurejesha jawabu la upendo kwa binti yake.

Makala

RABIUL THAN 1435, IJUMAA FEBRUARI 14-20, 2014


uhakika wala majibu ya wazi, hupata tabu sana. Ni kutokana na msingi huu wa ufanyaji kazi wa akili yake, alishindwa kumeza baadhi ya maelezo aliyokuwa akipewa katika maisha yake ya awali katika dini. Kwa upande mwingine anasema, Uislamu ni dini ya kutumia akili toka kwenye kuamini. Uislamu unakutaka utafakari juu ya maumbile na mambo mbalimbali kutambua ukweli. Kwa sasa yeye ndiye mshauri wa wanafunzi Waislamu katika Chuo Kikuu anakosomesha na pia wa Chama cha Wa n a f u n z i Wa i s l a m u katika Vyuo Vikuu, Marekani. Akiwa mwakilishi wao katika mambo yanayohitaji kuwasiliana na uongozi wa vyuo. Dr. Jaffrey Lang ameoa mke kutoka Saudi Arabia na ana watoto watatu. Wote mabinti. Ameandika vitabu vingi juu ya Uislamu. Kitabu kimoja amekipa jina Even Angels ask; A journey to Islam in America. Katika kitabu hiki pamoja na mambo mengine anahimiza u t u m i a j i wa a k i l i n a kuhoji. (Imekusanywa n a wa a n d i s h i wa A n n u u r k u t o k a v ya n z o mbalimbali.)

AN-NUUR

B a a d a ya k u s i l i m u Dr. Lang anajitahidi kufuata Uislamu kama unavyoagiza. Anaswali swala tano na anasema, hakuna sakina, utulivu wa nafsi, burudani na faraja anayopata kama ile anayopata akiswali na kusoma Quran. Anasema, hata asiyejua tafsiri ya Quran, akiisoma kwa imani na kwa utulivu, n a ye h u p a t a u t u l i v u na sakina kama mtoto mchanga anapokumbatiwa na mama yake. Dr. Lang ana Shahada ya Uzamili na ya Uzamivu ( m a s t e r s a n d d o c t o r a l degrees) katika hesabu kutoka Chuo Kikuu cha Purdue (Purdue University). Lang anasema, anapenda sana hesabu kwa sababu Maths is logical. Kwamba hesabu ni logiki. Ni kutafuta ukweli na majibu sahihi na ya wazi yasiyo na utata. Na kwamba, kwake yeye anapokutana na mambo yasiyo na maelezo ya

Tunavurugwa bila kujua


kinachoendelea. Bali tulio wengi achilia mbali swala za jamaa hata swala ya mtu akiswali peke mpaka mtu akitoa salamu haelewi amesoma sura gani wala kuwa ameswali rakaa ngapi? Mathalani, miongoni mwa nguzo za swala ni mtu kuwa na Khushui (Unyenyekevu) au Tumanina (Kutulizana) akiwa yupo ndani ya swala. Lakini jambo hilo halipatikani kwa watu wengi bali hupatikana kwa mtu anapokuwa yupo kwenye kutizama TV/Runinga. Kwani msanii mwenye kuilingania hadhira hugusa hasa moyo kile kitu inachokipenda. Hivyo hufunguka na kupokea chochote kile kiwe ni cha heri au shari bila ya kuchuja. Leo mtu ili kulithibitisha hili ajifanyie tathimini yeye mwenyewe pindi anapokuwa yupo kwenye swala mawazo yote

Inatoka Uk. 3

na hata kuelewa kuwa imamu alisoma sura gani baada ya kusoma Suratul Fatiha. Lakini jiulize jinsi unavyoweza kueleza kwa ufasaha mara baada kumalizika mpira u liok u wa uk i ut i z a ma katika TV/Runinga, na mtu akitokea na kukuuliza ni timu ipi iliyoshinda? Utajibu kwa ufasaha kabisa timu iliyoshinda, mfungaji wa goli, aliyempatia pasi, dakika Fulani na beki au
kipa wa adui aliyesababisha makosa yaliyopelekea timu yao kufungwa au jiulize jinsi unavyoweza kuelezea Filamu na wakati mwingine hata hiyo lugha inayozungumzwa huifahamu bali utaweza

na akili itakuwa yapo nje ya swala na inafikia mahali hata hufahamu upo kwenye rakaa ya ngapi na bali utashituliwa na imamu akitoa salamu ndio utakumbuka kwamba ulikuwa upo kwenye swala,

kutaja wahusika wakuu na wadogo na kila mtu nafasi au dhima yake ilikuwa ni ipi. Au hata wanafunzi wengi wanapokuwa mbele ya mwalimu ni tofauti kabisa

na wanavyokuwa mbele ya kioo cha TV/Runinga. Je, kwa muda wa mwaka mzima tumeisoma Quran aya ngapi na kuzifanyia kazi? Je, kwa muda wa mwaka mzima kwenye matatizo yetu ambayo ya m e t u t o k e a k we n ye Nyanja ya siasa, uchumi, maadili na mizozo yetu nk. Tumeweza kuirejea Quran mara ngapi ili kuweza kututatulia matatizo yetu? S wa l i l a m s i n g i l a kujiuliza wapi tunakwenda na mustakabali wetu dunia na akhera ni upi? Kwa mantiki hiyo ni ukweli halisi kwamba tumeidhara Quran na tuko mbali nayo kabisa.

Makala

RABIUL THAN 1435, IJUMAA FEBRUARI 14-20, 2014

AN-NUUR

Mauwaji Msikitini: Makubwa yafichuka


Na Omar Msangi SAA hi yo nilikuwa nimepigwa risasi, wakati natolewa kwa uchungu nilikuwa nikililia Laailaha ilallah, laailaha ilallah. Sasa yule jamaa alikuwa kwa strecha (machela ya kubebea wagonjwa), nafikiri naye alikuwa Muislamu kwa sababu nikisema laailaha ilallah, husema Muhammadu r a s u u l u l l a h nikaingizwa kwa ambulance (gari ya wagonjwa) bado nasema laailaaha ilallah aliyekuwa akinipatia first aid (huduma ya kwanza), naye husema Muhammad rasuulullah-ndio jamaa (askari) akauliza nani anasema hiyo? Huyo ni wetu au wa upande gani? Sasa nikashangaa nikasikia jamaa wa n a s e m a s u s p e c t , suspect (mtuhumiwa, mtuhumiwa). Huyo ni Ali Gitonga ambaye aliwekwa rumande kwa wiki tatu na mateso makali akituhumiwa kwa ugaidi. Katika siku alizokaa ndani, NAAM! Mtazamaji nakuomba umakinike na uniazime masikio ya k o m a w i l i , k wa n i taarifa tutakazokupa sasa zitakushangaza na hata kukufungua macho hata zaidi. Iwazie hali ya wanawake kuachwa wajane na watoto kuachwa yatima na hata familia kukosa mtu anayetafuta riziki ya kila siku. Kisa na sababu, yeye kuhusishwa na ugaidi. Kinachofuatia ni yeye kufungwa bila ya kufunguliwa mashitaka na hatimaye kuuwawa katika hali ya kutatanisha. Hayo ndiyo masaibu waliyopitia Wa k e n ya ( Wa i s l a m u ) wengi kwa kuhusishwa na ugaidi. Kwa waliobahatika kuishi, wamesalia kama wafungwa ndani ya n c h i ya o . H a ya y o t e yanatokana na kitengo kinacholaumiwa vikali cha ATPU (Anti Terrorism Police Unit-yaani polisi wa kupambana na ugaidi) miongoni mwa asasi za usalama zinazolaumiwa

Usiombe kuingia anga ya polisi wa ugaidi Sheikh alingolea macho, sehemu za siri Mchezo wa danganya toto jinga waendelea

KHUBAIB A. Rogo, mtoto wa Marehemu Abdul Rogo. alihojiwa na kutishwa wakiwemo wale wa FBIAwali serikali ya Kenya n a m a k a c h e r o we n g i Wazungu. ilikuwa imetangaza kuwa

A l i G i t o n g a a l i k u wa mmoja wa magaidi wa Al Shabab waliovamia Westgate Shopping Mall na kwamba alikuwa amejeruhiwa katika mapambano na polisi. Hata hivyo Ali Gitonga alikuwa kijana dereva aliyekuwa ameajiriwa na tajiri mmoja Nairobi na kwamba siku ya tukio, alikuwa amewapeleka watoto wa tajiri yake katika duka la Nakumatt kufanya manunuzi. Aliposikia risasi zikirindima ndani, ilibidi aingie ndani kujaribu kuwaokoa watoto wa tajiri yake na ndio akapigwa risasi na kujeruhiwa na magaidi. Kama alivyojieleza hapo juu, wakati anatolewa katika ile hali ya uchungu, na akidhani ndio anakufa, akawa anashahadia. Askari waliposikia anatamka Laailah ilallah, wakasema huyu ni gaidi. Serikali ya Kenya ikamtangaza kuwa ni gaidi aliyejeruhiwa. Akasota ndani wiki tatu. Haya ni baadhi ya mambo a m b a y o ya m e f i c h u k a Inaendelea Uk. 9 Muda mfupi baadae maafisa wa polisi (ATPU) walimlaza Sheikh Said k i t a n d a n i m wa k e n a kumpiga risasi sita kichwani akiwa amelala kifudifudi na pingu mikononi. Hivyo ndivyo anavyosimulia mchunguzi wa KTN kutokana na maelezo aliyopewa na mke wa marehemu pamoja na shemeji yake, Twalha Hassan. Katika taarifa ya uchunguzi wa KTN wanasema kuwa baada ya kufanya mauwaji hayo, askari hao wa ATPU, walizidisha unyama wao kwa kumkamata m k e n a m t o t o wa k e mdogo eti nao magaidi kando na kuwa silaha haramu. Silaha ambazo ni za kumbambikizia na kumkamatisha mkononi. Akisimulia kisa hicho cha kusikitisha mke wa marehemu anasema, yeye binafsi walimpiga sana kabla hawajamuuwa Inaendelea Uk. 9

kufanya mauwaji kinyama na kuepuka (mkono wa sheria kutokana na) maovu hayo. Hivyo ndivyo mwendesha kipindi anavyofungua makala ya Jicho Pevu cha televisheni ya K T N , m a d a i k i wa Wagigisi wa Mauwaji. Mwendesha kipindi katika ufafanuzi wake alisema kuwa wagigisi wa m a u wa j i n i wa t u wanaojifanya kuwa wao ni walinzi wa usalama wa raia (Polisi), lakini hao hao ndio wanaofanya mauwaji ya kutisha na ya kinyama, halafu hakuna hatua zozote wanazochukuliwa kwa mujibu wa sheria za nchi. H u k u akiwatahadharisha watazamaji kuwa makala hiyo itakuwa na picha za kutisha, hasa

Wagigisi wa mauwaji
kutokana na maiti za Masheikh waliouliwa kikatili, akafungua mada kwa kueleza masaibu ya Waislamu wa Mombasa katika hiki kinachoitwa vita dhidi ya magaidi. Kisa cha kwanza k ue lezwa ni k il e cha k u u l i wa S h e i k h S a i d Mohammed Njiro wa Kiembeni, Mombasa. Makala inafunguka kwa kuonyesha chakula k i s h a t e n g wa m e z a n i . Kama ilivyo kawaida ya wanawake wa Pwani, mkewe Sheikh Said kafunika chakula kwa kawa imeandikwa, Siringi ni tabia yangu. Kwa vile wakati wa dhuhri ulishakaribia, Sheikh Said akamwambia mkewe kwamba anakwenda kwanza msikitini kuswali halafu atakula akirejea. Lakini

Sheikh Said Mohammed Njiro, hakuwahi kula chakula hicho kilichoandaliwa na mkewe kipenzi, Rahma Hassan, wa l a h u k o m s i k i t i n i hakuwahi kufika. Askari wa kikosi cha ATPU walimkamata njiani, wakamfunga pingu na kumrejesha nyumbani. Kwa mujibu wa maelezo ya majirani waliokuwa katika eneo la tukio akiwemo msichana Agnes Kanga, ili kuficha ushahidi, polisi walifukuza watu wote walio jirani na eneo hilo. Baada ya kupekuwa nyumba nzima na kukosa silaha walizodai kuwa zipo katika nyumba hiyo, wa l i m c h u k u a S h e i k h wakamlaza kitandani kwake kifudifudi wakiwa wamemfunga pingu wakampiga risasi sita kichwani.

Makala

RABIUL THAN 1435, IJUMAA FEBRUARI 14-20, 2014

AN-NUUR

Inatoka Uk. 8 wakati tukifuatilia tukio la kuvamiwa Waislamu waliokuwa masjidi Mussa, Mombasa na watu kadhaa kuuliwa. Awali katika taarifa zetu tulikuwa tukisema kuwa hakukuwa na picha za kamera zilizo wanasa waliodaiwa kuwa magaidi. Hata hivyo, pamoja na picha nyingi kuharibiwa na kufichwa, lakini jicho la uchunguzi la kituo kimoja cha televisheni, Kenya kimepata picha nyingi zikionyesha tukio hilo, na hasa magaidi hao walivyofanikiwa kutoroka huku jengo likizingirwa na jeshi la Kenya-Kenya Defense Force (KDF). Kama itakavyoonekana katika makala hii huko mbeleni, mtafaruku uliotokea baina ya polisi n a wa n a j e s h i k a t i k a operesheni ya Westgate, huenda ndio uliopelekea baadhi ya polisi kutoa picha hizo kwa baadhi ya waandishi wa habari zilizokuwa zimedhibitiwa ili kulipiza kisasi kwa wanajeshi. Lakini jingine ambalo tumelipata katika ufuatiliaji wetu tukio la Masjid Mussa ni kuwa unyama wa kutisha hadi sasa umeshafanywa dhidi ya Waislamu wa Inatoka Uk. 8 mumewe. Wa l i n i p i g a s a n a mpaka nikafura uso (uso ukavimba). Wakanilazimisha nilale chini. Kulikuwa na begi la nguo za mtoto wangu. Walichukua silaha wakatia silaha (katika begi ile) wakanyanyua wakaniuliza, we mama waona hii nini? Nikawaambia mimi sijui. Wakanitoa wakaniweka sitting room wakaniambia nikae hapo hapo nisiinuke, nikiinuka wataniuwa baadae wakanipeleka ndani wakaniambia twende ukaone, tumemuuwa (mumeo). Baada ya kukamilisha operesheni hiyo, tunaambiwa kuwa polisi h a o wa l i f a n ya k a m a walivyozoeya. Kuita waandishi wachache wa magazeti,

Mauwaji Msikitini: Makubwa yafichuka

Kenya katika zile jitihada za serikali hiyo kujisajili kwa Marekani kwamba inapambana na magaidi. Taarifa za uchunguzi zilizokusanywa na kituo cha televisheni KTN, katika kipindi chake maarufu Jicho Pevu, zinaonyesha kuwa waliomuuwa Sheikh Aboud Rogo ni polisi wa kikosi cha kupambana na magaidi-Anti Terrorism Police Unit (ATPU) na kwamba aliuliwa jirani kabisa na kituo cha polisi cha Bamburi. Na baada ya mauwaji hayo polisi wawili waliomuuwa waliingia katika kituo hicho cha

POLISI wa Kenya walipovamia Masjid Mussa, Mombasa


polisi kurejesha bunduki walizotumia na wengine wawili wakaelekea baharini. Mkusanya habari wa KTN baadae aliwahoji watoto wa Sheikh Rog o, nao wak aeleza jinsi wanavyotishwa na kubambikiziwa tuhuma za ugaidi. Kijana Khubaib Abdu Rogo anasema, moja ya picha wanazo tumia polisi hao kumtisha ni za Samir K h a n . H u mw o n ye s h a wakati yupo hai na kisha humwonyesha zile picha za kutisha baada ya kuuliwa. Huyu Samir Khan alitekwa

redio na runinga w a n a o a m i n i k a kutumikia maofisa wa polisi wanaochapisha taarifa bandia na porojo kama wanavyotakiwa zinazochapishwa na kitengo hicho na kutumwa kwa wanahabari hao. K wa h i y o , k u p i t i a wanahabari hao, polisi wakasema kuwa wamemuuwa mtuhumiwa wa ugaidi Sheikh Said Mohammed katika mapambano makali ya kurushiana risasi na polisi!!! Mke na mtoto wake kwa muda wa siku sita akawa yupo rumande katika gereza la Shimo la Tewa, kisha akapelekwa

Wagigisi wa mauwaji
mahakamani akituhumiwa kuwa yeye ni gaidi hatari anayemiliki silaha. Kutokana na kilio cha mama huyo, Bi Rahma Hassan, mahakama ikampa dhamana, lakini bado akibaki na tuhuma za ugaidi na kukutwa na silaha (silaha ambayo alikamatishwa na polisi). Mwingine kufikwa na mkasa kama huu ni Sheikh Mohamed Aboud Rogo. Huyu aliuliwa tarehe 27 Agosti, 2012. Akisimulia kisa cha mauwjai yake, Mohammed Ali anasema: A g o s t i 2 7 , 2 0 1 2 ndiyo siku ambayo familia, ndugu, jamaa na marafiki wa Sheikh Mohammed Aboud Rogo,

Mombasa na siku kadhaa baadae, aliokotwa katika msitu wa Tsavo, maiti yake ikiwa imenyofolewa macho na sehemu zake za siri. Walioshuhudia tukio la kutekwa kwake wanasema, alitekwa na polisi wa ATPU mara tu alipovuka kivuko cha Likoni. Wananiambia tutakufanya kama huyu. Awali polisi walikuwa wa m e k a n u s h a k a b i s a kuhusika na kumteka Samir na kisha kumuuwa. Lakini sasa wanatumia picha za Samir baada ya kufanyiwa unyama

kuwatisha watoto wa Sheikh Aboud Rogo. Pengine nitaje hapa tena kisa cha kuuliwa Sheikh Said Mohammed. Huyu aliuliwa Mombasa. Polisi wa l i m k a m a t a wa k a t i akielekea msikitini kuswali dhuhri, wakamrejesha nyumbani. Wakapekua wakidai wanatafuta silaha, walipokosa kitu wa k a m f u n g a m i k o n o kwa nyuma wakamlaza kifudifudi kitandani mwake na kisha kumpiga risasi sita kichwani. Taarifa ikadai kuwa aliuliwa akipambana na polisi. (Yote haya ni kwa mujibu wa taarifa za Jicho PevuKTN). Na hayo ni baadhi tu ya matukio ya mauwaji ya kutisha waliyofanyiwa Waislamu kabla ya hili la juzi la Masjid Mussa. Pengine sasa tuangalie lile shambulio la Westgate Shopping Mall, ili tutizame linahusiana vipi na matukio kama haya ya kuvamia misikiti na kushambulia Waislamu. Mpaka sasa yapo maswali mengi ambayo bado hayajapatiwa majibu kufuatia shambulio la kigaidi pale Westgate Shopping Mall, Nairobi. Moja ya maswali hayo ni hili: Kama magaidi waliuliwa, maiti zao ziko Inaendelea Uk. 10 ni polisi wa kikosi maalum walijitokeza nje kidogo ya barabara wakamfyatulia risasi. Maelezo ya mtafiti wa KTN yanasema kuwa waliomuuwa ni watu wa kikosi maalum wanaopewa mafunzo kutoka Marekani, Uingereza na Israel na kwamba kikosi hicho kina kambi zake Nairobi, ila kukiwa na operesheni kama hiyo, hupewa ndege wakaingia Mombasa wakafanya kazi yao na kurejea Nairobi b i l a ya k u t a m b u l i k a . KTN katika Jicho Pevu wanasema, katika operesheni chafu kama hizo, Marekani, Uingereza na Israel, hucheza kadi zao kinyumenyume ili wasigundulike. Wa n a o i n g i a k a t i k a orodha hii ni watu wengine sita ambao nao wameuliwa Inaendelea Uk. 10

hawataisahau kamwe. Siku ambayo kiongozi wa dini aliyekuwa na ufasaha na ustadi wa kusema na kuvutia hadhira, alizimwa kwa mtutu wa bunduki. Je, aliuliwa vipi? Maelezo yanatolewa kuwa aliuliwa kiasi mita 200 kutoka kituo cha polisi cha Bamburi. Baada ya yeye kupita eneo fulani kukaribia kituo hicho cha polisi, polisi walikuwa wamepangwa kana kwamba kulikuwa msafara wa Rais. Njia zote zikafungwa. Hakuna gari inayokuja mbele yake wala nyuma yake katika barabara ya MalindiMombasa. Hapo ndio watu wanaodaiwa kuwa

10

Mauwaji Msikitini: Makubwa yafichuka


Inatoka Uk. 9

Makala

RABIUL THAN 1435, IJUMAA FEBRUARI 14-20, 2014

AN-NUUR

wapi? Pili, magaidi hao ni akina nani? Tatu, kwa nini polisi wa kawaida na vikosi maalum waliondolewa ghafla na badala yake likaletwa jeshi (KDF)? Kwa nini jeshi halikuingia kuanza mashambulizi bali likasubiri usiku kucha muda ambao unadhaniwa ndio waliotumia magaidi kutoka? Taarifa ya uchunguzi wa K T N i n a o n y e s h a kuwa hadi kufikia jioni ya siku ya shambulio, polisi walikuwa wamefanikiwa kuwaokoa watu wote, kwa hiyo ndani kukabaki magaidi peke yao. Na taarifa hiyo inaonyesha jinsi ndani kulivyokuwa kupitia kamera za C C T V. Wa n a o n e k a n a watu (magaidi) wanne tu wakiwa na silaha zao wakirandaranda bila hata ya kuwa na wasiwasi. Mohammed Ali, mchunguzi na mtayarishaji kipindi wa KTN, anasema kuwa pamoja na mafanikio hayo, lakini jambo lisilokuwa la kawaida na lisilokuwa limetarajiwa likafanyika. Ilitangazwa k u wa j e s h i l i n a i n g i a kuongoza operesheni. Kilichotokea ni kuwa walijikuta wakiuwana Inatoka Uk. 9 kinyama wakituhumiwa kwa ugaidi. Mmoja wao ni Sheikh Samir Hashim Khan, Imam wa msikiti. Huyu alitekwa na maofisa wa polisi akiwa na Sheikh Mohamed Kassim (kipofu). Walitekwa katika kivuko cha Likoni muda wa saa 6 mchana tarehe 10 Oktoba, 2012. Siku sita baadae mwili wa Sheikh Samir uliokotwa katika msitu wa Tsavo ukiwa na majeraha ya kuteswa, macho pamoja na sehemu za siri zikiwa zimenyofolewa. Aidha, uso ulikuwa umeharibika ikidhaniwa kuwa alimwagiwa tindi kali katika kuteswa au baada ya kuuliwa. Hadi makala haya ya Wagigisi wa Mauwaji inakamilika, Kassim alikuwa hajapatikana, si maiti au japo kusikia yupo wapi. Pengine nimalizie kwa masaibu yanayowakuta watoto wawili wa kiume wa marehemu Sheikh Aboud

POLISI wa Kenya walipovamia Masjid Mussa, Mombasa


wenyewe kwa wenyewe. Wanajeshi wakauwa na kujeruhi polisi. Mmoja wa Polisi aliyeuliwa ametajwa kwa jina la Martin Munene Kithinji. K ufuatia h a li h iy o, makamanda wa polisi waliondoa vikosi vyao wakilalamika kudharauliwa. Lakini hata wanajeshi nao, hawakuingia ndani mpaka kesho yake. Taarifa ya KTN kupitia kamera za video walizopata, zinaonyesha magaidi hao wanne wakiwa ndani bila ya wasiwasi. Ilipofika usiku wanaonekana magaidi wa l e wa k i s wa l i k wa zamu, anaswali mmoja mmoja huku wengine wakishika zamu. Kisha baada ya hapo wakafanya m a wa s i l i a n o k u p i t i a simu na kisha mmoja kutoka nje na kuangalia hali ikoje. Mara wote wakatoka wakatokomea kusikojulikana. Hiyo ilikuwa ni saa 4 na dakika 54 usiku. Kwa hiyo, usiku ule KDF, walibaki wamezingira jengo huku magaidi waliokuwa ndani walishatokomea kusiko julikana. Taarifa ya Jicho Pevu inasema kuwa ilipofika a s u b u h i ya J u m a p i l i ndio wanajeshi waliingia katika jengo hilo. Lakini na weyewe wakajikuta wakiumizana wenyewe kwa wenyewe. Taarifa hiyo ya KTN i n a o n ye s h a r u n d o l a chupa za ulevi na kisha inawaonyesha wanajeshi

Rogo. Hawa ni Khubaib A Rogo na Dhulkifli Aboud Rogo. Katika maelezo yao vijana hawa wanasema kuwa polisi wamekuwa wakiwajia na kuwasumbua mara kwa m a r a wa k i wa t u h u m u kuwa wanaficha silaha na kwamba wao walishakwenda Somalia na kujifunza ugaidi. Katika kuwatisha huwa wakiwaletea picha ya baba yao na masheikh wengine waliouliwa na miili yao kuharibika vibaya, kisha huwaambia kuwa watawafanya kama hao au kuwafanyia vibaya zaidi. Waliniwekea bunduki juu ya meza wakaniambia niifungue,wakati wakinitisha, wananiletea picha ya Samir wakati n i m z i m a n a wa k a t i

Wagigisi wa mauwaji
washamchoma kwa asidi, washamuuwa, wakasema unaona vile tulimfanya huyu, basi na wewe tutakufanya hivi au kukufanyia unyama zaidi. Baada ya hapo wakaniletea picha ya baba yangu wakati yupo hai, wakaniuliza wamjua huyu, nikawaambia ndio baba yangu, kisha hunionyesha picha wakati washampiga risasi. Hayo ni maelezo ya K h u b a i b a k i e l e z a alivyokuwa akipata wageni mara kwa mara kutoka kikosi cha ATPU wakiongozwa na kamanda wa kikosi hicho Mombasa, Elijah Rop, mara baada ya baba yake kuuliwa na hata sasa. Khubaib anasema katika mambo ambayo hatayasahau, ni kauli ya Elijah Rop alipomwambia kuwa wao, ATPU, ndio waliomuuwa baba yake. Kisha akamwambia, naye akileta kidomodomo watamuuwa kama walivyomuuwa baba yake. Khubaib anasema, yeye hajawahi kwenda Somalia na wala hana mpango huo, ila yeye ni Mwana Sunna. Ni Muislamu. Sasa kama atauliwa kwa ajili hiyo, hana la kusikitika. Ila anasema, akiitwa katika kituo chochote cha polisi, hatakwenda. Kama ni kumuuwa waje wamuue mbele ya mama yake, k a m a wa l i v y o m u u wa baba yake mbele ya mkewe (mama yake Khubaib). Mama yake ajue kwamba mwanawe kauliwa na polisi.

hao wakiingia wakiwa wa m e s h i k a b u n d u k i , lakini wanapotoka kila mmoja kashika mifuko ya Rambo utadhani wanatoka kufanya manunuzi (shopping). Katika tukio moja wanaonekana wakielekezana duka la kuingia kupora kwa hiyo wakati wanatoka, kila mmoja anaingia hapo na kuchukua kitu kabla ya kutoka. Katika kilele cha operesheni hiyo, wakati wa na nchi wa k i jiul i z a ilikuwaje jeshi likaitwa na nini kinaendelea ndani ya Westgate, ukaonekana moshi mzito ukitokea duka la Nakumatt. Waziri wa Usalama akasema kuwa hao walikuwa magaidi waliokuwa wamechoma magoro kutaka k u wa b a b a i s h a a s k a r i na kwamba moto huo ungezimwa mara moja. Hata hivyo, haukupita muda ikaonekana kuwa haukuwa moto wa magodoro bali ulikuwa u k i wa k a n j e s e h e m u ya juu ya kuegesha magari na mara jengo likaporomoshwa kutoka ghorofa ya tatu mpaka chini. Wa k a t i h a l i i k i z i d i kutatiza, mara jina la Samantha Louise Inaendelea Uk. 12 Maelezo ya mtoto Dhulkifli nayo ni ya namna hiyo hiyo. Naye anasema AT P U wa n a m wa m b i a kuwa yeye ni komandoo la magaidi waliohitimu mafunzo Somalia. Katika tukio la kuvamiwa Masjid Mussa wiki mbili zilizopita, Dhulkifli anaonekana mbele ya msikiti akiwa kashikishwa bendera ya Al Shabab huku polisi wenye silaha wakimzingira. Katika picha moja iliyopigwa kupitia simu ya m k o n o n i , a m b a y o nimeishuhudia na kuisikiliza, mtoto huyo wa Sheikh Rogo anasikika a k i l a l a m i k a k wa m b a kashikishwa bendera hiyo na polisi. Na katika mahojiano yake na KTN anasema, afya yake ni mgogoro mtupu, kama anavyoonekana (unene usio wa kawaida). Kisha anahoji, hivi na mwili huu mazoezi gani ya kijeshi/kigaidi naweza kufanya.

11
Mohammed Makimu K U J I H U S I S H A na madh-hab flani imekuwa ni dhana na itikadi inayoshadidiwa miongoni mwa Waislamu walio wengi. Kwa dhana hi yo, i m ef ikia hatua mtu kuwaaminisha waislamu wasiojitambua na kuufahamu Uislamu sahihi na wale ambao si Wasilamu waamini kwamba bila kuwa na dhehebu katika Uislamu wewe si Muislamu. Ni seme t u kwamba dhana hii ni dhanifu na daima haikubaliki katika Uislamu. Suala la kuwa na dhehebu flani, ni wazo na zao la mtu binafsi (Personal and Private opinions). Mwenyezi Mungu (SWT) na Mtume wake, hawakutuamrisha tujitenge kimakundi kama tulivyojitenga sasa hivi. Kwa kuangalia ubaya wa jambo hili, Mwenyezi Mungu (SWT) hakuacha kutuonya tusifanye hivi pale aliposema ndani ya Quran: Nyenyekeeni Kwake na mcheni, na simamisheni swala wala msiwe katika washirikina. Katika wale walioitenga dini yao na wakawa makundi, kila kikundi kinafurahia kilichonacho (30:30-31). Kwa kuirejea aya hiyo na nyingine ambazo sijazinukuu katika makala haya, hakuna mahala suala la madhehebu limebainishwa. Na si lazima kuwa mfuasi wa Hanafi, Shafii, Maliki au Hanb ali. Hawa ni wanazuoni na maimamu waliofanya na kuonesha juhudi zao katika dini na hawakuwaamrisha watu watengeneze makundi na kupigana ima kutukanana kama tufanyavyo sisi. Na waliweza kuhitilafiana lakini hawakugombana, kuzomeana, kutukanana, kukufurishana na kufanyiana uhasama na uadui kama tufanyavyo sisi leo hii. Jambo moja la msingi la kufuata si Shekhe wala Imam Fulani, bali ni kuitafuta njia iliyobainishwa kwetu kama Wa i s l a m u . M we n ye z i Mungu anasema ndani ya Quran: Sema: Hii ndio njia yangu, ninaita (ninalingania) kwa Mwenyezi Mungu k wa u j u z i wa k we l i , mimi (nafanya hivi) na (kila) wanaonifuata. Na Mwenyezi Mungu ametakasika na kila

Makala/Tangazo

RABIUL THAN 1435, IJUMAA FEBRUARI 14-20, 2014


Mtu mmoja akasema Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu inaonekana kama huu waadhi wa kutuaga, ni kitu gani unachotupa kwa sasa? Mtume akasema Nakuusieni kumcha Mwenyezi Mungu na muwe ni wasikivu na wenye kutii hata kama atakujieni Mhabeshi Mtumwa (madhali anakupeni ujumbe utokao kwa Mwenyezi Mungu na Mtume wake). Kwa wale watakaoishi baada ya kufa k wa n g u , wa t a s h u h u d i a ikhtilafu nyingi. Mnatakiwa mshikamane (pindi muda huo zikitokea hizo ikhtilafu) na Sunnah zangu na zile za Makhalifa waongofu. A l i y o ya t a b i r i M t u m e ndiyo haya yanatokea sasa. Jambo la msingi ni kuiingiza hadithi hii katika utendaji wa maisha yetu. Hakuna haja ya kuwa mfuasi wa madhehebu fulani wakati dhehebu hilo halipo katika asili ya Uislamu. Na anachokupeni Mtume basi pokeeni, na anachokukatazeni jiepusheni nacho. (Qu.an 59:7) (mohdmak@hotmail.co.uk)

AN-NUUR

upungufu, wala mimi sio miongoni mwa wanaomshirikisha (Mwenyezi Mungu) (12:108). Mwenyezi Mungu (SWT) ametuamrisha tushikamane na kuwa kitu kimoja (3:103). Na ametoa tahadhari kwamba iwapo tusipokuwa pamoja na letu likawa moja kama Waislamu tunaomfuata Mtume mmoja nini kitatufika. Na mtiini Mwenyezi Mungu na Mtume wake wala msizozane (msigombane), msije mkaharibikiwa na kupotea nguvu zenu, na vumilieni (mstahamiliane). Bila shaka Mwenyezi Mungu yu pamoja na wanaovumilia Quran (8:46) Katika miongoni mwa kauli za Imam Maliki anasema mawazo a u m t a z a m o wa m t u yeyote waweza kubalika pale yakiendana na Quran na Hadithi na yanaweza kupingwa pale yanapokuwa kinyume ispokuwa ya huyu aliyelazwa hapa kaburini. (Akaashiria kaburi la Mtume Muhammad s.a.w). Maimam wote wane wa Fiq-hi wamesema katika kauli zao kwamba kama Hadithi sahihi itabainika kuliko haya maoni yangu, hivyo basi hiyo itakuwa ndio madhehebu yangu (Idhaa swah-hal-hadiith fahuwa madh-habii). Hii ina maana kwamba hadithi sahihi ikibainika katika masala wanayoyafutu, ndio i t a k u wa n j i a ya wa o kufuata. Si maoni yao tena. Na walihimiza na kusisitiza s a n a wa t u wa ya p i m e maneno na mitazamo yao kwa uzani wa Quran na Sunnah, ikibainika wao kwenda kinyume, watu wasiwafute kwa ushabiki kwa kuwa wanawapenda, bali wayaachilie mbali maneno yao. Ugonjwa unaowasibu Waislamu wengi sasa hivi ni kuifuata dini kibubusa na kuwa washabiki wa dini. Suala la umaamuma katika Uislamu linaishia katika swala tu. Na hata katika umaamuma katika swala, ni lazima na wewe un ayes walis h wa u ju e namna ya kuswali. Sio kwamba anatakiwa kujua

Madhehebu
Imam pekee. Kama ilivyo wajibu kwa Imamu kusoma Suratul Fatha na kujua taratibu zote za swala, ndivyo hivyo anavyotakiwa kuwa maamuma. Kwa hiyo, kila Muislamu anawajibu wa kuusoma na kuufahamu Uislamu sahihi k u t o k a k we n ye v ya n z o vyake (Quran na Sunnah) si kushabikia. Waislamu walio wengi wamekuwa ni wafuasi wa madhehebu mbalimbali. Mbaya zaidi hakuna lolote wanalojua juu ya huyo wanayemnasibisha na dhehebu wanalolifuata. Si Shafii, Hanbali, Maliki wala Hanafi. Hakuna wanachokifahamu wafuasi wa madhehebu hayo zaidi ya kujua jina tu ima huyu ni Shafii, Maliki, Hanbali au Hanafi. Ukiwauliza kipi unafahamu juu ya yale yaliyozungumzwa na Imam

huyu, hana jibu la msingi. Ndugu zangu katika dini hii iliyofundishwa na Mitume wote, bado inatutaka tuitumikie kama inavyotufundisha. Tu i r e j e e k i l a k i p e n g e l e chake kimatendo. Huu ni muda wa kuacha tofauti zetu kwa kuangali Uislamu unafundisha nini si watu wanasemaje. Ishi na Muislamu mwenzako kama ndugu yako, penda yamfike mambo ya kheri kama wewe mwenyewe unavyopenda katika nafsi yako. Nihitimishe makala yangu kwa kuirejea hadithi iliyosimulia na Irbad bin Sariya katika SahihtTirmidh. Anaeleza kwamba Siku moja Mtume (s.a.w) alituawaidhi waadhi ambao ulishtua nyoyo za watu baada ya swalat Fajr ambao ulibubujisha watu machozi, na nyoyo zikapatwa khofu,

CHUO KIKUU CHA WAISLAMU CHA MOROGORO KINATANGAZA NAFASI ZA MASOMO KWA NGAZI ZA DIPLOMA NA CERTIFICATE KWA MWAKA WA MASOMO 2014/2015 MASOMO YA TOLEWAYO NI:1) Diploma and Certificate in Science and Laboratory Technology 2) Diploma and Certificate in Journalism 3) Diploma and Certificate in Islamic Banking and Finance 4) Diploma and Certificate in Procurement and Logistics Management 5) Diploma and Certificate in Law and Shariah 6) Diploma and Certificate in Islamic Studies 7) Certificate in Medical Laboratory Technology 8) Certificate in Information Technology 9) Certificate in Chinese Language 10) Certificate in Sign Language 11) Certificate in Arabic Language SIFA ZA KUJIUNGA:KWA NGAZI YA DIPLOMA. MWANAFUNZI ANATAKIWA AWE NA FORM SIX ONE PRINCIPLE PASS NA SUBSIDIARY, SIFA ZA MUOMBAJI ZIENDANE NA KOZI ANAYOOMBA. AU AWE NA NTA LEVEL 4 CERTIFICATE YA KOZI INAYOFANANA NA IWE YA CHUO KINACHOTAMBULIKA NA SERIKALI. KWA NGAZI YA CERTIFICATE. AWE NA ANGALAU D NNE ZA KIDATO CHA NNE ZINAZOFANANA NA KOZI ANAYOOMBA AU AWE NA VETA LEVEL 3 CERTIFICATE INAYOFANANA NA KOZI ANAYOOMBA FORM ZA KUJIUNGA NA CHUO ZINAPATIKANA MUSLIM UNIVERSITY OF MOROGORO AU KATIKA WEBSITE YA CHUO, www.mum.ac.tz AU KUPITIA MAWAKALA WETU. MASOMO YATAANZA RASMI TAREHE 12/05/2014. MWISHO WA KUPOKEA MAOMBI NI TAREHE 31/03/2014 KWAMAELEZO ZAIDI NA KWA KUPATA ORODHA YA MAWAKALA WALIPO KARIBU YAKO PIGA SIMU AU TUMA UJUMBE MFUPI KWA NAMBA ZIFUATAZO: - 0712277598, 0655003744 AU 0785330002 IMETOLEWA NA NAIBU MAKAMU MKUU WA CHUO TAALUMA CHUO KIKUU CHA WAISLAMU CHA MOROGORO

12

Mashairi/Makala

Mhariri samahani, niweke japo pembeni, Nitoe yangu maoni, kwa wananchi nchini, Katiba ninabaini, jadidi mada mezani, Katiba mpya si hoja, hoja ni uadilifu !

BUNGE LA KATIBA (KATIBA MPYA SI HOJA!)

Bunge lile tambueni, la katiba li njiani, Wajumbewe kwa yakini, wiki jana si zamani, Amiri-Jeshi nchini, wote aliwabaini, Katiba mpya si hoja, hoja ni uadilifu ! Si kwa majina kwa nduni, baadhi nakujuzeni, Wanasiasa kundini, pamwe na wanazuoni, Kadhalika wa kidini, viongozi nao ndani, Katiba mpya si hoja, hoja ni uadilifu ! Juma lijalo nadhani, yumkini li hewani, Bilhaki kwa yakini, wengi mwalitumaini, Kwa mengi matumaini, tena yaso na kifani, Katiba mpya si hoja, hoja ni uadilifu ! Kwa finyu wangu uoni, sina nalotumaini, kutoka humo bungeni, la utendi si uneni, Yanenwayo katibani, matendoni siyaoni, Katiba mpya si hoja, hoja ni uadilifu ! Mifano nitakupeni, toka ile ya zamani, Kwa ibara katibani, msijedhani nabuni, Tisashara namba 'wani', 'UHURU WA KIIMANI', Katiba mpya si hoja, hoja ni uadilifu ! Waminywa huu na nani, uhuru wa kiimani, Katiba au insani, jibu mnalo vichwani, Hapo ina kosa gani, katiba nijulisheni, Katiba mpya si hoja, hoja ni uadilifu ! Kadhalika rejeeni, moja tatu namba 'wani', 'USAWA WA SHERIANI', haki ya kila insani, Nao waminywa na nani, katiba au insani, Katiba mpya si hoja, hoja ni uadilifu ! Shekhe pale kizimbani, kupandishwa kulikoni, Mchungaji mitaani, yu 'apeta' ni kwanini, Hapo ina kosa gani, katiba nijulisheni, Katiba mpya si hoja, hoja ni uadilifu ! Moja nane kwa makini, kifungu 'a' durusuni, Waandishi kitanzini, watiwa sasa kwanini, Mwigamba muulizeni, vyema atakujuzeni, Katiba mpya si hoja, hoja ni uadilifu ! Pamwe na wenza safuni, walikamatwa kwanini, Japo kesi 'waliwini', wiki ya juzi kotini, Kilichowaminya nini, katiba au insani, Katiba mpya si hoja, hoja ni uadilifu ! Aidha likumbukeni, 'MWANAHALISI' si geni, 'linasota' kifungoni, hadi leo ni kwanini, 'UHURU WA KIMAONI', wa 'Bongo' u mashakani, Katiba mpya si hoja, hoja ni uadilifu ! Japo sasa i hewani, kifungoche dhukuruni, Redio yetu 'IMANI', 'ilisota' gerezani, Kwa ghaidhi ya insani, si sheria katibani, Katiba mpya si hoja, hoja ni uadilifu ! Mwisho nakukumbusheni, cha Njozi mwanazuoni, KITABU kilobaini, mauaji ya insani, Dawamu marufukuni, kwa amri yake 'Beni', Katiba mpya si hoja, hoja ni uadilifu ! Usuli au kiini, cha tatizo katibani, Adala na si uneni, ya insani matendoni, Kwa yangu mimi maoni, jipya hasa silioni, Katiba mpya si hoja, hoja ni uadilifu ! Kwa kina tafakarini, kuhusu yangu maoni, Yapimeni 'kwa mizani', si 'kwa alosema nani', Kaditama kwaherini, wa Bara na Visiwani, Kalamu naweka chini, mwisho wa yangu maoni. ABUU NYAMKOMOGI - MWANZA.

Inatoka Uk. 10 Lewthwaite, maarufu White Widow, likaanza kusikika katika vinywa vya wanahabari na serikali k wa m b a a l i h u s i k a n a shambulio hilo. Wakenya walijisahau wakashika hilo. K T N i n a s e m a k u wa kuletwa jina la Samantha ilikuwa namna nyingine ya danganya toto jinga k u w a f a n y a Wa k e n y a wasihoji mambo ya msingi kwani japo mama huyo alishawahi kufika Kenya huko nyuma, lakini madai ya kushiriki mashambulio hayo ilikuwa ni porojo tupu. Katika kuhitimisha kadhia hiyo, Waziri wa Usalama akatangaza kuwa k u l i k u wa n a m a g a i d i 10 mpaka 15. Naye Rais Uhuru Kenyatta siku ya Jumanne, siku moja baada ya kutolewa tangazo kuwa operesheni imekamilika, alisema kuwa magaidi wa l i o u l i wa wa l i k u wa watano na 11 walikuwa wamekamatwa na kushikiliwa na polisi. Hata hivyo, picha za kamera za CCTV ambazo hatimaye zilifika mikononi mwa waandishi wa habari, zilionyesha kuwa kulikuwa na magaidi wanne tu. Lakini jingine la kutaja hapa ni kuwa japo taarifa ya serikali ilitangaza kuwa m a g a i d i 5 wa l i u l i wa , haikuweza kuonyesha picha za maiti hao. Aidha, hadi leo haikuweza pia kuonyesha hao magaidi 11 waliokamatwa na kushikiliwa na polisi. Kinyume chake, kama ilivyoripotiwa katika gazeti la Daily Nation la Jumatatu iliyopita Februari 10, 2014, serikali sasa inasema magaidi waliouliwa eti toka wakati huo, maiti zao zinashikiliwa na FBI wakizifanyia uchunguzi!!! Ajabu ya mambo! Akitoa taarifa hiyo Mkuu wa Jeshi la Kenya, Generali Julius Karangi, anasema: Here it from me, these fellows were killed on Monday morning. It happened on Saturday. We f i n i s h e d t h e m o n Monday morning and their bodies are with the FBI somewhere. Swali ni je, iweje magaidi wauliwe na jeshi la Kenya, serikali ishindwe k u o n ye s h a m i i l i ya o , lakini muda wote huo toka Septemba mwaka

Mauwaji Msikitini: Makubwa yafichuka


jana 2013 mpaka leo, ndio i n a s e m wa k u wa m i i l i hiyo inachunguzwa na FBI. Kenya haina uwezo wa kuchunguza maiti? Hiyo Jumatatu anayosema Generali Julius, hakukuwa na mtu yoyote ndani kwani wa t u w o t e wa l i k u wa washaokolewa. Kwa hiyo waliobaki ni magaidi na kwa hiyo hakukuwa na utata wowote kutambua nani waliuliwa. Ukitizama simulizi hizi, ambazo zimefichuka baada ya kufanyika uchunguzi, zinaacha maswali mengi bila ya majibu. Kama alivyosema mchunguzi wa KTN, nyingi ya taarifa za Westgate zimekuwa ni porojo za danganya toto jinga. Ndio hapa unaweza k u o n a k u wa p e n g i n e katika kutafuta namna nyingine ya kuendeleza hii danganya toto jinga, lazima matukio kama haya ya Masjid Mussa yatokee ili kuwashibisha Wakenya na walimwengu kuwa ni kweli magaidi wapo na magaidi hawa ni Al Shabab na Waislamu waliopata mafunzo Somalia. Na katika danganya toto jinga hii, tufahamu kuwa michezo ya entrapment itafanyika sana ili kuwakamatisha Waislamu na silaha au jambo lolote linaloweza kusaidia kuwapakazia ugaidi Waislamu na kufunika yale maswali ya Westgate yasiyo na majibu. Kabla ya tukio la Masjid Mussa, vipeperushi vilisambazwa kuhimza watu wahudhurie. Na ili kuhakikisha kunakuja vijana wengi, hata wazamiaji wa mitaani, ikatangazwa kuwa kutakuwa na ubwabwa. Sasa pengine ni suala la kutafiti, nani alitoa kipeperushi hiki? Nani waliandaa ubwabwa huu? Nani alikuwa azungumze? Je, naye alikamatwa? Nani alikuja na kupachika bendera za Al Shabab katika msikiti huo? Ta a r i f a y a K T N inaonyesha kuwa serikali ya Kenya inapokea mamilioni ya dola kila mwaka kwa ajili ya kupambana na ugaidi. Sasa lazima Kenya ionyeshe kuwa inafanya k a z i . Wa l a h a i t a k u wa jambo la kushangaza hapo baadae ikigundulika kuwa hata ubwabwa ulioliwa pale Masjid Mussa ulitoka

RABIUL THAN 1435, IJUMAA FEBRUARI 14-20, 2014

AN-NUUR

katika hizi dola kutoka Marekani. Ambalo kila wakati la kujikumbusha ni kuwa vita hii dhidi ya ugaidi ina malengo makuu mawili. Kwanza ni kwa ajili ya kuendeleza agenda ya mabeberu ya kuzitia utumwani nchi mbalimbali duniani ili zipate kudhibitiwa na kuwatumikia mabeberu. Pili, ni kuhujumu Uislamu. Wanapouliwa Masheikh na vijana wa Kiislamu, Uislamu unahujumiwa kwa kuporwa nguvu kazi yake. Lakini unapowaonyesha magaidi kama wale pale Westgate, eti wanaswali Isha, baada ya kuuwa watoto wachanga na wanawake wasio na hatia, unahujumu Uislamu kwa kutangaza kuwa ni dini inayofundisha ukatili na hivyo unahalalisha hatua zozote zinazoweza k u c h u k u l i wa k u u p i g a v i t a U i s l a m u . Ta t u , u n a p o f a n ya n j a m a z a entrapment, unawafanya vijana wa Kiislamu na nguvu kazi ya Waislamu, badala ya kufanya kazi za kimaendeleo kwa ajili ya dini yao na dunia yao, wabaki kila mara ni watu wa kupambana na polisi na kufanya ghasia mitaani. Unapouwa Sheikh, unawatia ghadhabu Waislamu na hasa vijana, kwa hiyo unawafanywa wawe na msimamo mkali zaidi dhidi ya serikali na hata wasio Waislamu. Wanabaki kuwa watu wa kuongozwa na hasira za kujihami badala ya kukaa kupanga na kufanya mambo ya maendeleo. Matokeo yake ni kuwaingiza katika chambo na ndoano ya Free Islamic Army, kwa maana ya jeshi la mujahidina lisilo na malengo maalum ya nchi maalum wala kuwa na udhibiti wa serikali yoyote duniani. Wao wakisikia mahali kuna vita wanatafuta hoja za kujiridhisha (kujidanganya) kuwa ni jihad, wanakwenda. Kwa mtindo huu ndio linaibuka tatizo jingine la hatari la kuwaangamiza Waislamu: Kutumiwa kama jeshi huru la kimataifa la kupigana proxy war ya mabeberu. Ndio walioko Afghanistan, Iraq, Libya, Pakistan, Somalia na sasa Syria.

13

Makala

RABIUL THAN 1435, IJUMAA FEBRUARI 14-20, 2014

AN-NUUR

Serikali tatu ni hatua ya ukombozi kwa Zanzibar


Na Alghaithiyyah, Zanzibar
Kilichosababisha Mzee Jumbe kulazimisha kujiuzulu kutokana na msimamo wake wa kujenga hoja za kisheria akisaidiwa na aliyekuwa mwanasheria Bashir Swanzy juu ya kuvurungwa kwa mambo ya muungano wa serikali mbili na Nyerere. Katika kitabu hicho mzee Jumbe anabainisha wazi kuwa suala la mvurugiko katika muungano wa serikali ni njama za dhahiri za kuwamaliza Wazanzibari na zilianza baada ya kupitishwa katiba ya mwaka 1977 inayotumika hadi leo ambayo ilipitishwa na wafuasi wasiotetereka wa Chama Cha Mpainduzi. Hili la katiba ya mwaka 1977 kutogusia suala la shirikisho pia lilielezwa na aliyekuwa mwanasheria wa serikali ya Muungano Joseph Warioba ambaye alinukuliwa na gazeti la Daily News la Machi 16 mwaka 1982 alipokuwa akijibu hoja za Prof. Srivastava. Akinukiliwa alisema, Nina wasiwasi kuwa Profesa alikuwa akitizama katiba ya mwaka 1977 katika mtazamo wa kishirikisho ambapo ungeweza kuwa na serikali tatu tofauti. Nina hakika waliotunga katiba ya 1977 hawakuwa na mawazo hayo vichwani mwao. Lakini pia kilichomponza mzee Jumbe ni unafiki waliokuwa nao Wazanzibari kwamba aliandika barua ambayo ilikuwa iwasilishwe kwa Nyerere kwenye vikao halali, lakini cha kushangaza barua hiyo ilitua mikononi mwa Julius Nyerere wakati yeye mwenyewe ameiacha kwenye kabati la Ikulu ya Zanzibar. Nyerere kama kawaida yake katika kikao cha NEC wakati anataka kummaliza mzee Jumbe aliisoma barua hiyo maeneo ambayo yalikuwa na faida kwake, kwamba hakutoa nafasi ya Jumbe kujitetea wala wajumbe wa NEC kupewa nakala za barua hiyo kuisoma na kukifahamu kile kilichokuwa kidaiwa na Jumbe. Kama wapo wenye kukumbukumbu basi wakumbuke katika mwaka 1995 katika viwanja vya Malindi akihutubia mkutano mkubwa wa hadhara, Dk. Salmin Amour Juma alivyochoshwa na visa vya Nyerere na muuungano kwa ujumla alimfuata Butiyama kumuuliza kama anataka Muungano uendelee au hataki. Ghadhabu za Dk. Salmin zilikuwa wazi hadi kufikia kusema hakuna cha baba wa taifa wa babu wa taifa. Sishangai UVCCM wakati ule walikuwa ama hawajazaliwa au hawajui kitu lakini basi ata kuisoma historia pia hamtaki. Kwa upande mwengine wapo wanaohofia Wazanzibari watakufa njaa endapo tutatoka katika mfumo wa serikali mbili. Swali, kwani Watanganyika ndio walipewa ufunguo

MWAKA 2013 ulimalizika kwa kali ya aina yake katika medani za siasa hapa nchini Tanzania, hasa baada Tume ya Mabadiliko ya Katiba kutoa Rasimu ya Pili ya Katiba mpya ambayo ina ibara 271. Katika ripoti ya tume hiyo ambayo ilikabidhiwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete na Rais wa Zanzibar Ali Mohamed Shein, hakuna kitu kilichovuta hisia za watu wengi na kusubiriwa kwa hamu kama suala la mundo wa Muungano wa Tanzania. Mwenyekiti wa Tume hiyo Jaji Warioba katika hotuba yake fupi aliyoitoa katika viwanja vya Kareemje, alikiri kuwa suala la muundo wa Muungano wa Tanzania ndilo lililoipasua kichwa Tume hiyo. Kwa kauli yake Tume hiyo ilichukua muda mrefu katika kuyafanyia uchambuzi maoni ya wananchi yaliyokusanywa na Tume hiyo juu ya suala la muundo wa muungano na kulazimika kufanya utafiti zaidi. Kama hiyo haitoshi katika kujiridhisha juu ya suala la muundo wa muungano, Tume hiyo ililazimika kupitia ripoti za tume na kamati mbalimbali zilizoundwa na kutoa mapendekezo juu ya suala la muungano, kama vile Tume za Jaji Kisanga, Tume ya Amina, Tume ya Shelukindo na nyenginezo. Jaji Warioba alihitimisha kutoa matokeo ya maoni ya Watanzania juu ya muundo wa m u u n g a n o a m b a p o kwa Zanzibar asilimia 0.1 (ambazo ni sawa na watu 25) walipendekeza serikali moja, asilimia 34 walipendekeza serikali mbili na asilimia 60 walipendekeza serikali ya mkataba. Kinachoshangaza ni kwamba wapo baadhi ya watu ambao kwa fikira zao na wanavyojihisi kuwa wao ni Wazanzibari zaidi kuliko wengine huku wakisema suala la serikali tatu katu asilan, abadan haliwezekani, h u k u wa k i a p a k u l i n d a mfumo wa serikali mbili uliopo, ambao umechokwa na Wazanzibari. Kinachosumbua kila ukiwafikiria watu hawa unajiuliza masuala mawili mawili, hivi kweli wana udhati wa kuipenda Zanzibar? Ama wanashikilia suala la serikali mbili kuendeleza maslahi yao binafsi na wale wanaowatuma kufanya hivyo? Wakati Rais Jakaya Kikwete akihitimisha matembezi ya maadhimisho ya miaka 50 ya mapinduzi, yaliyoratibiwa na Umoja wa Vijana wa CCM pale katika viwanja vya Maisara, viongozi wa umoja huo walikula yamini kuendelea kulinda mfumo wa serikali mbili. Nilikuwa pembeni kusikiliza kwa makini sababu za vijana hao kwanini waseme

HAYATI Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. tuendelee na serikali mbili, lakini nilikuja kubaini kuwa wao ni makuwadi wa kisiasa ni watumwa wa kundi fulani ambalo linapenda liendelee k u wa m a d a r a k a n i k wa manufaa binafsi kama vile suala la ulua limekuwa teule kwao kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Nathubutu kuwaita makuwadi wa kisiasa kwa sababu ni mambumbu, wenye ufinyu wa mawazo, uwezo na upeo mdogo wa kifikiri, kwa ujumla nilibaini wanaugua maradhi yaitwayo ufinyu wa mawazo. Katika ripoti yake Jaji Warioba ameainisha sababu kadhaa za kimantiki na sio zile za kiporojo kwanini Tanzania iwe na mfumo wa serikali tatu na sio mbili kama ilivyo hivi sasa au serikali moja ambayo maoni yake hapa Zanzibar yalitolewa na watu 25 tu, sina shaka hawa ni watu wenye asili ya Tanzania bara. Sikuwa na shaka k u wa U V C C M n a wa l e wanaowatuma hapa Zanzibar wanaugua gonjwa la uoni finyu, kwani dalili kubwa ya kuugua ugonjwa huu ni kushindwa kutoa sababu za kimantiki ambazo tutazikubali Wazanzibari kwanini tuendelee muundao wa serikali mbali. Ipo hoja nyengine inayoendelea kutumiwa na wahafidhina wanaotaka serikali mbili nayo ni kutokwenda kinyume na m a wa z o ya m a r e h e m u walioasisi muungano mzee Abeid Amani Karume na Mwalimu Nyerere. H i i n i h o j a ya k a m a wale waliopigiwa mifano katika kur-ani, hawajui wanachokifanya au waliodai kufuata waliyowakuta nayo babu zao wakaambiwa na Kuran, hata kama babu zao walikuwa wajinga au hawajui kitu? Hivi jamani mpaka lini tukiwa katika karne hii tutaongozwa na fikra za tuliokwisha kuwazika na sasa ni hitma tu juu yao? Wanasahau kuwa mzee Karume alipokuwa akielezea madhila ya muungano wa serikali mbili aliwahi kutamka kuwa koti likikubana livue, akimaanisha uwezekano wa kujitoa kwenye muungano wa serikali mbili wenye mizengwe. Kwa upande wake marehemu Nyerere wakati alipokuwa hana jinsi ya kuzima kasi ya wabunge waasi G55 mwaka 1993 waliokuwa wanataka Tanganyika yao, aliwatuliza kwa kile kilichoelezwa kuwa muelekeo ni kutoka serikali mbili kuelekea moja. Lakini ni sababu zipi hasa zinazotufanya tuendelee kuyaabudu, kuyaenzi, kuyanyenyekea na kuyaendeleza mawazo ya wafu? Wazanzibari wamechoka na mfumo wa serikali mbili kwa sababu hautoi haki, inakuwaje Muungano ujipanue unavyotaka kuchota mamlaka ya Zanzibar, wakati Zanzibar ikigusa tu wanakuja juu, suala la muungano huu pia limewakera baadhi ya viongozi wa Zanzibar. Nimepitia kitabu cha Rais wa Pili wa Zanzibar Mzee Aboud Jumbe Mwinyi kiitwacho The Partner Ship , katika kitabu hicho i n a o n e k a n a wa z i m z e e huyo hakuwa muumini wa serikali mbili na amebainisha wazi kuwa katiba ya muda ya mwaka 1965 ilikuwa na vipengele vilivyoeleza Tanzania kuwa nchi ya shirikisho kwamba kuna s e r i k a l i ya M u u n g a n o , serikali ya Zanzibar na serikali ya Tanganyika.

wa riziki za Wazanzibari? Mbona wanatuuzia mchele wa Kiyela ghali kuliko ule unaotoka Thailand, Pakistan, India na China. Mbona saruji inayotoka Oman na Urusi rahisi kuliko ya Wazo Hill ama kiwanda cha Tanga Cement. Mbona vitunguu thomu vya India rahisi kuliko vya Tanzania bara. Nguzo ya uchumi wa visiwa duniani ni uingiza bidhaa zaidi importation kulikokusafirisha e x p o r t a t i o n . K wa n i n i liwasumbue vichwa enyi wenye mawazo mgando? Mwanafalsafa Aristotle, alipokuwa akitoa tafsiri ya maana neno ujinga, alisema ujinga ni kutokuwa na habari za undani juu ya kitu fulani ama to be a mere lack of information, hili ndilo tatizo la UVCCM na CCM kwa ujumla wake. Dunia imebadilika na hii si jamii ya Wazanzibari ambao wanatosheka na sababu kuambiwa waendelee na mfumo wa serikali mbili eti kwa sababu tu sera na ilani zinaeleza hivyo. Wazanzibari wanafahamu kuwa sera na ilani sio misahafu kutoka kwa Mungu. Hawaoni jinsi Zanzibar ilivyokaliwa shingoni kama ngoma ya kimanga haupumui kwa kila kitu si kwa uchumi, siasa, utamaduni, diplomasia. Mbona wanaCCM wenyewe wanalalamika chini kwa chini kulichoka suala la Rais wa Zanzibar kuchaguliwa Dodoma? Sera ya amani na utulivu si ya CCM, hiyo ni sera yenye uasili wa Wazanzibari tangu zama za kale nashangaa hivi sasa kuwa kufanywa ndio dira. Msingi wa amani na utulivu unatokana na wananchi na sio nguvu za kisiasa. Angalizo liliopo ambalo linapaswa kungaliwa kwa makini ni kwamba hata Zanzibar iwe na siasa safi kiasi gani, hata iwepo amani na utulivu kiasi gani, bila ya uchumi imara ambao mizizi na mihimili yake imekaliwa na serikali ya muungano ipo siku amani na utulivu h u o u t a t o we k a b i l a ya kipingamizi. Suala la uchumi ni muhimu na likiwezekana hilo ndipo amani na utulivu utakapodumu lakini kama mnasisitiza amani na utulivu mnajilia kuku huku wananchi wakishinda hata kupata kishina cha muhogo hapo litatokezea tatizo. Tungalie kwa makini majanga yanayotunyemelea ikiwemo lile la kujaliwa kuwa na vijana ambao hawana ajira, na haiwezekani vijana hao kupata ajira endapo uchumi utataendelea kuwa na serikali mbili. Kwa wale wanaodhani kuwa Wazanzibari wamelala wanakosea, Wazanzibari wanaona mbali, Wazanzibari wanaona mbele na sio kama ngombe anayeona mbele haoni mbali.

14
H A PA N A S H A K A kila aliyesoma au kusikiliza ile simulizi ya mama wa Kiislamu aliyekuwa Masjid Mussa, Mombasa atasikitika na kupandwa na ghadhabu. Maelezo ya mama huyo t u l i ya c h a p i s h a w i k i iliyopita ukurasa wa 3 ikiwa na kichwa cha habari, M a m a a l i ye k u we p o Masjid Mussa aeleza kilichotokea. B a a d a ya k u e l e z e a kwa urefu kilichojiri na yaliyosemwa na vyombo v ya d o l a v ya K e n ya , sasa hebu tuangalie upande wa pili. Kwa maana ya kutumia jicho pevu kufanya tathmini, uchambuzi na kuona iwapo Waislamu walipatia au kuna tatizo. Siku kadhaa kabla ya kufanyika muhadhara huo ulioleta maafa makubwa kwa Waislamu, kulisambazwa kipeperushi kuhimiza watu kufika. Katika sehemu moja kipeperushi hicho kinasema: Alhamdulillah Jihad haiko mbali sasa, na Inshaallah maadam maIkhwa wameshaanza kuwauwa majasusi, dalili ya kuanza Jihad Kenya zaanza kudhihiri. Kisha kipeperushi kikaeleza kuwa vijana wa Jihad wamemuuwa adui wa Uislamu (Ahmed Abdullah Bahshuweiny.) Juu ya kipeperushi hicho ikachapishwa picha ya Ahmed Abdullah Bahshuweiny, waliyedai kuwa adui mkubwa wa Waislamu na hivyo ikatajwa kuwa aliuliwa na Mujahidina na kwamba mkusanyiko wa Masjid Mussa siku ya Jumapili, ilikuwa ni katika kujenga umoja wa vijana wanaopenda Jihad na kuweka mikakati na mipango ya kuwauwa makafiri na maadui wa Uislamu. Moja ya mada zitakazozungumzwa ikatajwa kuwa ni A h k a m u l - J i h a d . Nyingine ni Hukumu ya Shaheed. Kipeperushi kikaandika chini ya picha ya Ahmed Abdullah kuwa Allah awahifadhi (vijana wapenda Jihad) wenye k u f a n ya k a z i h i i ( ya kuwauwa watu kama Ahmed) na awape nguvu juu ya makafiri. Ili kuhakikisha wanapatikana watu wengi, kipeperushi kikatoa motisha, kikasema:

Makala

RABIUL THAN 1435, IJUMAA FEBRUARI 14-20, 2014


ya kuuwa polisi zaidi na maadui wengine wa Uislamu: Ukienda utasema hiyo ni akili au ujinga? Utasema uliendea Jihad/Uliitiwa jihad au maangamizi? Sasa haya ndiyo mambo tunayotahadharishana kwamba ujinga ni mzigo. Na kutokana na ujinga mwingi, Waislamu wanajikuta wakinaswa kwa wepesi na kujiletea maafa kwa mikono yao wenyewe. Masjid Mussa pale vijana wabichi, nguvu k a z i wa n a o t e g e m e wa na familia zao na U i s l a m u wa m e u l i wa . Watoto wadogo kabisa wamejerujiwa. Wanawake wameumizwa na kusota r u m a n d e . Wa i s l a m u wamepata nini? Uislamu umepata nini? Kama askari yule alikuwa kauliwa na watu wa biashara za madawa ya kulevya kama wengine wanavyotuhumu, kwa tukio la kipeperushi na Waislamu kuitikia wito wa kipeperushi, sasa wauwaji wa polisi ni Waislamu. Na inawaweka katika mazingira magumu zaidi kutokana na propaganda za kuwatangazia ugaidi. Ya p o y a l e y a kuwabambikizia Waislamu silaha, mtu unaweza kujitetea na Wa i s l a m u w e n z a k o watasimama nawe na hata wapenda haki duniani kote. Sasa na hili la kuitwa na kipeperushi Muislamu unajitetea vipi? Hebu tujitizame madhaifu yetu na matatizo yetu ya ndani, na hasa hili la elimu na ufinyu wa uelewa mambo. Jazba na mihemko hailipi. Mtu atakutangaziaje kuwa katika Jihad anayofanya kauwa polisi, na unajua ni kweli kuna polisi kauliwa na watu wanasakwa na Muislamu mwenzenu mmoja kashauliwa kwa sababu hiyo, anakuita ndani ya msikiti muweke mikakati ya kupambana zaidi na polisi, halafu unakwenda!!! Je, huo utaita ujasiri au ujinga? Hiyo itakuwa jihad au maangamizi? Ukiyatizama yote haya utaona kuwa makachero wa serikali, wametumia tukio la kuuliwa Ahmed Abdullah Bahshuweiny, k u wa n a s a Wa i s l a m u , kufanya hujuma na kujenga hoja ya kuendelea kuwabamiza Waislamu.

AN-NUUR

Huu ni ujasiri au ujinga

POLISI wa Kenya walipovamia Masjid Mussa, Mombasa.


Vijana wamejitahidi kupatikane chakula cha saa sita kwa kila atakayehudhuria. N a k we l i p i l a u n a ubwabwa kwa wapenda wali mweupe ukapatikana ukivutia vijana na watoto wadogo wengi. Na wote hawa wamekombwa na kuwekwa ndani wakiitwa magaidi ukiacha wale waliouliwa na wengine kuondoka na vilema kutokana na risasi. An nuur imejitahidi kupata habari za huyu Ahmed Abdullah Bahshuweiny. Taarifa za ndugu zake wa karibu na marafiki zake zinasema kuwa huyu bwana Ahmed Abdullah Bahshuweiny, ni afisa wa ngazi ya juu wa polisi kituo cha Malindi na kwamba alikuwa akikaribia kustaafu (taarifa nyingine zinasema alishakuwa katika orodha ya askari wa akiba). Lakini pia anatajwa kuwa ni Muislamu aliyek uwa a k ijita h id i kutekeleza Uislamu wake wa nguzo tano. Sifa yake kubwa ni kuwa alikuwa akiwabana sana watu wa unga (madawa ya kulevya) na majambazi walioingia eneo la Malindi. Watu wa karibu yake wana mawazo kwamba yawezekana aliuliwa na hao watu wa unga na majambazi kulipiza kisasi. Hili linapewa uzito na watu wengi japo hakuna ushahidi. Ila polisi wao wameligeuza kuwa ni Mujahidina waliomuuwa, japo hakukuwa na kikundi cha Waislamu waliokiri kuhusika mpaka kiliposambazwa kipeperushi cha kuita Waislamu Masjid Mussa. Lakini zipo taarifa za uhakika pia kuwa alikuwa akitumikia Idara za Kikachero za FBI na Polisi wa Kupambana na Ugaidi Kenya (ATPU). Mr Ahmed Bakswein, (6 1 ) a liu liwa s ik u ya Jumanne ya tarehe 28 Januari katika mji wa Malindi. Alikuwa ndani ya gari yake, watu wawili wa l i o k u wa n a s i l a h a wakiendesha pikipiki, wakampiga risasi wakati wanapita gari lake. Kwa nafasi hiyo ya k u f a n y i a k a z i z a ukachero idara za ATPU na FBI, inadaiwa kuwa amehusika katika operesheni zilizofanyika kuwaandama vijana wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa Al Shabab katika mji wa Malindi. Kwa mujibu wa taarifa ya Kamanda wa Polisi, Malindi, Kiprono Langat Mr Bakswein a l i s h a m b u l i wa a k i wa katika mzunguko (round about) wa barabara ya Malindi-Garsen na kwamba washambuliaji hao walikuwa na bastola. Kufuatia tukio hilo, kijana mmoja wa Kiislamu aliyetajwa kwa jina la Ali M o h a m m e d a l i u l i wa kwa kupigwa risasi na polisi ikidaiwa kuwa ni katika waliohusika kumuuwa Ahmed Abdalla Bakshueni. Anti-terror police unit (ATPU) wanadai kuwa Ali Mohammed Delawa mkazi wa Msambweni, ni katika watu muhimu katika kundi la Al-shabab na Al-Qaeda. Sasa labda tujiulize: k a m a wa l i o i t a d a r s a na muhadhara ule ni katika waliopanga na kutekeleza mauwaji ya Afisa wa Polisi, Ahmed Abdullah Bahshuweiny; mtu mwenye akili timamu na anayejua analolifanya, anaweza kufanya mauwaji kama yake halafu akatangaza katika kipeperushi kwamba ndiye aliyehusika na kuitangazia polisi na serikali kwamba atakuwa msikiti fulani siku fulani? Kama suala ni ujasiri na kwamba haogopi, kwa nini basi baada ya kuuwa asikae hapo na kusubiri polisi waje wamkamate au apambane nao? Je, alichokusudia mtu huyo au walichokusudia watu hao katika kuita Waislamu Masjid Mussa, na kuwahamasisha kwa pilau; ni kuwaelimisha juu ya Uislamu/Jihad au kuwakamatisha? Vi p i Wa i s l a m u waliohudhuria! Wewe mtu anakutangazia kuwa kauwa polisi, kwa sababu yoyote itakayo kuwa, halafu anakutangazia kuwa uje ili mpange mikakati na kuhamasishana namna

15

Omar Bin Abdul-Aziz


akiwatahadharisha magavana wake katika utumiaji wao wa mali na akiwanasihi hata katika utumiaji wa kalamu na mishumaa inayowashwa bila sababu. Alihakikisha kuwa kila dirham inatumika mahala pake bila ubadhirifu, na kwa njia hii akaweza kuzibadilisha nyuso za huzuni za watu masikini na kuzifanya ziwe za furaha, kwani haukupita muda mrefu tokea pale alipotawala, Wizara ya Mali ya Waislamu (Baytul m a a l ) i k a f u r i k a k wa wingi wa mali, na Omar akawaandikia magavana wake barua na kuwataka kutekeleza yafuatayo. Kila mtu lazima awe na nyumba ya kulala, farasi wa kupanda, vifaa vya nyumbani (furniture), mwenye deni alipiwe deni lake, watumwa na mateka wote wakombolewe, mayatima wadhaminiwe maisha mema, asiyeoa aozeshwe, na ikiwa mali itatosha basi ni vyema, ama isipotosha nijuulisheni nipate kukutumieni mali zaidi ili muweze kutimiza haja za Waislamu. Akatoa amri ya kuwatosheleza maulamaa kwa kila wanachokitaka ili waweze kujishughulisha na kazi ya kuwafundisha watu dini yao. Ikafika hadi matajiri wakati mwingine wanatoka na mali yao ya Zaka na hawapati masikini wa k u m p a m a l i h i y o wala hawapati mtu wa kunyoosha mkono wake kupokea mali hiyo. Na hii ni kwa sababu Uadilifu wa Omar haukuondoa umasikini tu, bali uliwaletea watu heshima ya nafsi zao, wakawa wanaona haya kunyanyua mikono yao kwa ajili ya kupokea mali ya Zakaa au kuwa ombaomba. Alikuwa akisema; Wallahi kama haki haiwezi kusimama na batili kuondoka ila ikatike mikono yangu na viungo v ya n g u n a m a t u m b o yangu, basi nitafanya hivyo nami nikiwa mwenye furaha. Na akasema pia Wa l l a h i l a u k a m a nitaishi nanyi kwa muda wa miaka hamsini, basi sitojishughulisha na jingine isipokuwa kuusimamisha uadilifu.

Makala

RABIUL THAN 1435, IJUMAA FEBRUARI 14-20, 2014


wale wenye watoto wengi wasiokuwa na chakula cha kuwatosha na wengine wa mfano wao waliojaa duniani. Nimewaza juu ya hao wote nikatambua kuwa Mwenyezi Mungu ataniuliza kuhusu hao siku ya Kiama, na atakayewatetea hao dhidi yangu ni Mtume wa Mwenyezi Mungu Muhammad (Swalla Llaahu alayhi wa sallam). . Nimewaza yote hayo nikaogopa hoja isije ikathibiti dhidi yangu siku ya kiama, kwa ajili hiyo ninalia. Viongozi wetu wanalia kwa kuwafikiria masikini waliopo Tanzania? Kule kuneemesha watu wote katika utawala wa Omar ibn Abdul Aaziz, kuliwafanya watu wasiwe na uhitaji, na kufanya Zaka inayokusanywa isiwe na maskini wakupewa, na kwa hivyo zikatumika Z a k a k wa m a m b o ya maendeleo. Nimalizie kwa kuwakumbusha a ya h i i ya Q u r a a n , nafikiri itawanufaisha Waislamu na wasiokuwa Waislamu Hiyo nyumba ya akhera tutawafanyia wale wasiotaka kujitukuza katika ardhi wala (kufanya) ufisadi, na mwisho (mwema) utawathibitikia wacha mungu. {Al qasas 83}

AN-NUUR

Aliondoa umasikini kwa miaka miwili

Na Rashid Abdallah, MUM WAANDISHI wote wa historia wameshuhudia j u u ya U c h a M u n g u wake, uadilifu na huruma yake, pamoja na uwezo wake mkubwa wa kuongoza kwa haki na kuibadilisha hali ya umma kutoka katika umasikini uliopindukia na kuiweka katika hali njema inayoendelea kuzungumziwa mpaka wakati wetu huu. H u y o s i m we n g i n e ila ni Omar bin Abdull Aziz, ambaye baadhi ya wanazuoni wanamuita kuwa ni Khalifa wa tano baada ya wale wanne wakubwa, ambao ni Abuu Bakar, Omar, Othman na Ally (Rehema za Allah ziwe juu yao). A l i k u w a

Inatoka Uk. 16 Mwezi wa Ramadhani ulipokwisha nilipata muda wa kutosha kufikiri na kujiuliza, kwanini navaa hijab katika mwezi wa Ramadhani pekee na sio muda wote? Kuanzia hapo nilianza mwenyewe kujizoesha kuvaa hijab kila nilipotoka nyumbani. Siku hizi siwezi hata kutoka nje bila kuwa na hijab na sijisikii raha nikiikosa. Hijab imekuwa sehemu ya maisha yangu na inanipa hamasa na ufahamu mimi ni nani na nini lengo la kuumbwa kwangu hapa duniani. Nilikuwa nikivaa kama wanavyovaa wanawake wengi wanavyovaa katika mji. Nimekulia jijini Dar es Salaam. Nilihisi naonekana wa kisasa (up to date) kwa fasheni, lakini nimekuja kutambua

Jinsi nilivyoweza kuwa mwanamke wa Hijaab


kwamba nilikuwa napiga hatua kwenda nyuma kwa kuendekeza msemo wa kijinga FREEDOM lakini uhuru bila nidhamu ni vurugu. Nilikuja kugundua kwamba hijab inamweka mwanamke huru dhidi ya dhana ya kuonekana kama chombo cha matamanio na starehe au kuthaminishwa kwa jinsi anavyoonekana, au umbo lake badala ya fikra na weledi wake. Leo siwezi tena kuwa mtumwa wa utumiwaji. Hijab imenistaarabisha kutoka mtu wa kuiga yasiyowiana na uhalisia, unyanyasaji na kupewa majina machafu na taswira zinazoenezwa na vyombo vya habari. K u v a a h i j a b kumeonyesha kuwa kuvaa vizuri na kufunika nywele zangu, kumeondoa usumbufu wa kimapenzi katika maeneo mengi ambayo nachanganyika na watu wa jinsia tofauti. N a z i j u a b a a d h i ya familia au wanawake wanaofuata tamaduni wanalazimishwa kuvaa hijab lakini hii si njia sahihi. Qur'an imeeleza wazi kwamba katika dini hakuna kulazimishana (Q 2:256). Wanawake wanaoamua kuvaa hijab wamekuwa hawafanyi uamuzi huo kirahisi. Hakika wanawake wengi wanathibitisha kwamba wamekuwa wakikumbana na upinzani mkubwa kutoka katika familia zao ziwe za Waislamu au zisizokuwa za Kiislamu, pale wanapoamua kujistiri. Duniani kote kumekuwa na mifano kadhaa ya wanawake wakitetea haki yao ya kuvaa hijab. Lakini natakiwa kukumbuka na kufikiri mara kwa mara kwamba hijab haitakiwi ionekane k a m a n i n g u o t u ya kufunika kichwa changu. Bali ni alama ya utu na sio nguo tu kwa ajili ya kujipendezesha. Maana yake inapanuka zaidi hadi kuhusu tabia yangu. Siwezi wala sijawahi kufikiri kwamba i m a n i ya m wa n a m k e kwa Mungu wake mmoja inapimwa kwa vazi lake, lakini sasa natambua raha na uhuru wa kweli ninaopatiwa na Hijab. Hijab inatulinda kuliko kitu chochote na nina furahia sana kuivaa kuliko ilivyokuwa hapo awali. Siku ya hijab duniani ni wazo zuri kwasababu wanawake wanawajibika katika hijab. Tunaipenda na tunafanya hivyo kwa ajili ya Allah (SWT). Ni jukumu letu kwa imani yetu, kwa Muumba wetu na bwana wetu. Inafahamika vyema

Huyo ndiye Omar Bin Abdull Aziz, cha kushangaza kama si kufurahisha hayo yote aliyafanya ndani ya miaka MIWILI TU. Historia hii ya Omar ni nzuri sana kwa viongozi wa sasa wa Tanzania na hata Duniani haijalishi uwe Muislamu ama siyo Muislamu. Chakuzingatia ni kuwa aliyeondosha umasikini k wa m i a k a m i w i l i ni Binaadamu kama wewe. Siku moja Fatima binti Abdul Malik mke wa Omar bin Abdul Aziz alipoingia chumbani na kumkuta mumewe akiwa juu ya msala akilia. Alimuuliza; 'Mume wangu una nini mbona unalia namna hii? Omar akamjibu; Ewe Fatima! Mimi nimepewa jukumu kubwa katika jambo hili. Nawaza juu ya fakiri mwenye njaa na mgonjwa asiyejiweza, na yule asiyekuwa na nguo ya kuvaa, na yatima asiyekuwa na wa kumtazama, aliyedhulumiwa asiyeweza kujitetea, mgeni asiyekuwa na pa kulala na mateka na wazee na vizuka na

kwamba sisi wanawake wa Kiislamu ni viumbe wanaovutia. Mwenyezi Mungu anapenda tujihifadhi kwa hijab zetu. Hijab ni ulinzi wetu wa nje dhidi ya uovu wa maisha. H a k u n a m t u anayetukandamiza na dunia inahitaji kuona kuwa hatuhitaji kuokolewa au kuwekwa huru. Ndio maana msingi huu ni bora kabisa na ninauunga mkono kwa asilimia mia m o j a n a u t a wa s a i d i a wanawake wasiokuwa Wa i s l a m u k u o n a n i namna gani tunajisikia hasa kwa kuvaa vazi hili tulilolichagua kulivaa. N i k i wa m wa n a m k e wa Kiislamu ninatambua kuwa vazi hili sio nguo tu ya kuvaa, lina maana nyingi kwetu na tunatumaini litawasukuma wanawake wengine kuelekea katika hali ya kujiweka vizuri wenyewe, Insha Allah. Mrs. Mwanaidi Mohamed Ali.

16

AN-NUUR
MAKALA

RABIUL THAN 1435, IJUMAA FEBRUARI 14-20, 2014

16

RABIUL THAN 1435, IJUMAA FEBRUARI 14-20, 2014

Soma AN-NUUR kila Ijumaa

AN-NUUR

Jinsi nilivyoweza kuwa mwanamke wa Hijaab


M W A N A I D I M o h a m m e d Ali (pichani), ni mwanamke anayejitambua, anayejiheshimu na anayethamini jinsia yake ya kuwa mwanamke na kujihifadhi. Kutokana na kujitambua kwake barabara na kujua t h a m a n i ya k e , B i . Mwanaidi aliona kuwa anastahili heshma na utu. Fikara yake inafikia katika vazi la hijab. Vazi la kumstiri, kumthamini na kumletea heshma mwanamke mahali popote awapo. Kifuatacho ni kisa chake juu ya vazi la hijab alichokibainisha katika mtandao wake wa Tmarkturn na Jiko langu Blog. Kisa chake hiki chatosha kuwa somo na funzo kwa wanawake wengine wa Kiislamu na wasiokuwa Waislamu katika suala zima la umuhimu wa vazi la hijab. Februari mosi ilikuwa siku ya Hijab duniani. Na hii ni habari yangu jinsi gani nilianza kuvaa hijab. Nilianza kuvaa hijab mwaka 2011, wakati huo ulikuwa ni katika mwezi mtukufu wa Ramadhani na hata hivyo, lilikuwa jambo la manufaa zaidi ambalo sikuwahi kulifanya katika maisha yangu. Nilikuwa katika pandembili za shilingi. Kama mwanamke ambaye amezaliwa na kukulelewa katika jamii ya kisasa kama walivyo Waislamu

MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, amesema wakati umefika kwa Wi z a r a ya K a t i b a na Sheria kuandaa sera itakayozingatia maslahi ya walimu wa madrasa, ili kuthamini juhudi zao za kuwafundisha watoto. Maalim amesema, walimu wa madrasa wana kazi kubwa ya kuisaidia jamii katika malezi na kuwajenga wa t o t o k i m a a d i l i , hivyo hakuna budi kuthaminiwa kwa kazi hiyo ambayo muda wote wamekuwa wakiifanya kwa kujitolea. Akizungumza katika hafla ya maulid ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (SAW) yaliyoandaliwa na madrasatMuumin Islamiya ya M u e m b e s h a u r i , Maalim Seif amesema hatua hiyo itasaidia kuwapa moyo walimu hao na kuzidisha ari ya kufundisha. Kwa upande mwengine Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar amesisitiza suala la umoja na mshikamano miongoni

Wizara ya Elimu yatakiwa kuwa na sera ya madrasa


Wito wa Maalim Seif maulidini Alabama Hazina ya maadili, historia itiliwe mkazo
m wa wa n a n c h i , n a kuwashauri viongozi wa k i j a m i i k u a c h a tabia ya kutoa kauli zinazoweza kuchochea chuki miongoni mwa wanajamii. Aidha amesisitiza haja kwa wanajamii kuhimizana na kukumbushana juu ya kulinda mila, silka, kuuenzi na kuuendeleza utamaduni wa Zanzibar. Amefahamisha kuwa katika kuuenzi utamaduni na silka za Wazanzibari, hakuna budi kwa wazazi kuwasomesha vizuri watoto wao, ili wajue elimu zote pamoja na historia ya utamaduni wao. Ameonya kuwa iwapo juhudi hizo za kuwaelimisha watoto hazitoungwa mkono na jamii nzima hasa katika ngazi za familia, jamii

itaendelea kushuhudia mporomoko mkubwa wa maadili, ikizingatiwa kuwa sehemu kubwa ya

malezi iko katika ngazi ya familia. Katika kuunga mkono juhudi za madrasa hiyo, Maalim Seif ameahidi kutoa kompyuta mbili pamoja na mifuko ya saruji kwa ajili ya kuiendeleza madrasa hiyo. Mapema akisoma risala ya madrasa hiyo ustadh Baiya Maulid, amesema madrasa hiyo iliyoanzishwa mwaka 1995, kwa sasa inakusudia kuanzisha miradi itakayosaidia kukidhi mahitaji ya kuendeleza madrasa yao. Amesema tokea kuanzishwa kwa madrasa hiyo wameweza kupata mafanikio mbali mbali ikiwa ni pamoja na kuimarisha jengo la madrasa, kuhifadhisha kuran, pamoja na kukuza mashirikiano baina ya walimu na wazazi. Hata hivyo wamesema bado wanakabiliwa na changamoto nyingi zikiwemo uchakavu wa vifaa vyao vya ofisi pamoja na kutaka kunyanyua jengo lao. H i v y o wa m e i o m b a serikali pamoja na wahisani we n g i n e

MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar. Maalim Seif Sharif Hamad

kuweza kuungana nao katika kutatua kero hizo, ili kuwawezesha watoto kusoma katika mazingira mazuri.

wote, dini mara zote imekuwa ufunguo katika familia yangu, lakini nikuwa navaa hijab katika siku za sherehe za kidini pekee kama sherehe ya ndoa au kwenye Maulid n.k. B a a d a ya k u o l e wa mwaka 2009 nilijaribu kuvaa hijab na jambo la kufurahisha, ni mume wangu ambaye alikuwa kila mara akinieleza kuwa nikivaa hijab naonekana mwanamke mzuri zaidi na mwenye heshima. Inaendelea Uk. 15

Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na POA Printing Works LTD, S.L.P. 4605, Dar es Salaam.

You might also like