Professional Documents
Culture Documents
tz
Sauti ya Waislamu
Dhulma ilishashtadi
Ya Escrow ni tabia
BEI TShs 500/=, Kshs 50/=
Uk. 2
Vigogo wa Mamlaka
kamili waunguruma
BAADHI ya Waislamu wakiwa nje ya Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam wakiendelea na dua wakati kesi ya Sheikh
Ponda Issa Ponda ikiendelea kuunguruma ndani ya Mahakama hiyo Novemba 26, 2014.
Wanasiasa, magazeti
wanapandikiza ugaidi
Wabaya kuliko watuhumiwa ugaidi Uk. 8
Tujifunze kutoka Kenya na ATPU yao
Kama tukifuata nyayo, tumeangamia
Tahariri/Habari
2
AN-NUUR
Dhulma ilishashtadi
Ya Escrow ni tabia
AN-NUUR
We n g i h a w a a m i n i k i
na wamejaa tamaa za fisi.
Wanapata madaraka kupitia
migongo ya Watanzania,
halafu wanatumia nafasi
tulizowapa kudhulumu ili
kukidhi tamaa zao huku
wakiwaumiza Watanzania
zaidi ya milioni 46.
Pamoja na jitihada za Bunge
kujaribu kuwabana, badi
tatizo halionekani kwisha
kwa kuwa wanaodhulumu
walishakosa mioyo ya
imani katika dini, (hawana
m w o n g o z o wa k i d i n i ) ,
wameonja tamu ya dhulma
na wameshazoea.
Katika mioyo yao, hakuna
huruma wala maadili.
Zaidi wanaonyesha wapo
kinadharia zaidi kuliko
vitendo.
Hata hivyo awali tuliona
dawa sahihi iliyoonekana
kuwa mwarobaini wa dhulma
inayofanywa na viongozi
Na Bakari Mwakangwale
wa n a z u o n i wa n a o e l e wa
masuala ya Uislamu, bali
wa n a a m i n i z a i d i m a d a
zitolewazo katika mitandao,
na fatwa anayoikuta huko
ndio unakuwa msimamo
wake.
Akasema Mwalimu Filambi
kuwa hilo ni tatizo kubwa
linaloweza kuwaangamiza
Waislamu.
Filambi alisema, Waislamu
wanapaswa kuzama zaidi
katika mafunzo ya Uislamu
kutoka kwa wanazuoni wenye
taaluma ya masuala ya dini na
si kwa tafsiri ya juu juu tu
kisha wakachukua maamuzi
na kuanza kuyafanyia kazi.
F i l a m b i , a l i s e m a k wa
kawaida watengeneza agenda
au mada za kuwagonganisha
Waislamu, huwa wanaangalia
palipo na mwanya wa
kuwagonganisha Waislamu
na hutumia njia hiyo kwa
kujinasibisha na Uislamu kwa
lengo la kuwavuruga.
Akinukuu maelezo ya
Profesa Hamza Njozi, katika
Bunge la Katiba, alisema
kwa haya yanayoendelea
nchini huivi sasa hadhani
kama Tanzania inaweza kuwa
salama, kwa sababu agenda
zinawekwa na mabwana
wakubwa hivyo Uislamu
unakuwa ni njia tu kama
daraja la kuwafikisha katika
ajenda zao.
Kwa sababu, alisema baada
ya vita na Warusi, mabwana
wakubwa hao walitangaza
wazi kuwa, vita iliyobaki ni
dhidi ya Uislamu kwa sababu
ndio dini pekee inayoweza
kuwa kikwazo katika malengo
yao.
Akitoa maoni yake
kutokana na hali ilivyo sasa
hususani kwa Waislamu
Abdallah Waziri, alisema
Uislamu ni dini ya kiutu
zaidi kwani umefundisha
kuishi na mtu hata asiyekuwa
Muislamu.
A l i s e m a , Wa i s l a m u
wanapaswa kufahamu na
kujifunza kutoka kwa Mtume
Muhammad (s a w), kwani
Habari
AN-NUUR
Na Seif Msengakamba
Makala
Na Salum Bendera
AN-NUUR
Habari za Kimataifa
AN-NUUR
Makala
AN-NUUR
Makala
AN-NUUR
HISTORIA za dini,
zinatufahamisha kuwa, kila
Mwenyezi Mungu alipoleta
Mtume au Mitume, (Manabii),
waharibifu chini ya ibilisi
wa l i i n g i l i a k a t i k u h a r i b u
miongozo ya Mwenyezi Mungu
a l i y o p i t i s h i a k wa M i t u m e
hao. Baada ya uharibifu huo,
Mwenyezi Mungu alituma
mjumbe mwingine. Na kama vile
mlezi wa mototo, humwanzisha
mtoto shule kwa darasa la
kwanza nakuendelea, ndivyo
Mwenyezi Mungu alivyowaletea
wanadamu ujumbe kulingana na
nyakati zao.
Ujumbe wa Nabii Musa a.s
ulivurugwa mara nyigi, na
wavurugaji waliamini kuwa
wataufuta kabisa, ili sheria zao
ziwe ndizo zinazo tawala. Mfano
mdogo ni wa mfalme wa Ugiriki
na wa Rumi waliotaka imani
zao ndio zitawale. Ni pamoja
na wana wa Israeli kuibadilisha
Torati na kutengeneza kitabu
chao cha Talmudi. Hiyo ndiyo
maana Nabii Isa (Yesu) A.S. akawa
hakusomeshwa katika chuo
chochote, bali Mwenyezi Mungu
alimjuvya elimu iliyokuwa
katika Torati na ndiyo maana
hakupewa kitabu, bali alipewa
Injili (Mahubiri) yaliyotoka
kwa Mwenyezi Mungu kupitia
kichwani kwake:
Mimi siwezi kufanya neno
mwenyewe; kama nisikiavyo
ndivyo nihukumuvyo; na hukumu
yangu ni ya haki, kwa sababu
siyafuati mapenzi yangu mimi,
bali mapenzi yake aliyenipeleka.
(Yohana 5:30.)
Waandishi, Mafarisayo na
Masadukayo, walishtuka na
kukasirika baada ya kuona
kuwa anawahubiri sheria zile
zile za Torati ambazo waliamini
wamezivuruga sana, kwa kuwa
alikuwa akiwaambia kuwa:
Msidhani ya kuwa nalikuja
kuitangua Torati au Manabii la,
sikuja kutangua, bali kutimiliza.
Kwa maana, amini, nawaambia,
mpaka mbingu na nchi
zitakapoondoka, yodi moja wala
nukta moja ya Torati haitaondoka,
hata yote yatimie. (Mathayo
5:20.)
Ndiyo maana wakapanga
mbinu za kumwuuwa mapema
tu baada ya kukabidhiwa Utume
akiwa na miaka 30 kwa kuwa
walihofia kua akiendelea kuishi
wataumbuka. Na kwa kuwa Yesu
hakuwa na kitabu, mahubiri yake
ya miaka mitatu hayakuandikwa
a k i we p o , wa k i a m i n i k u wa
wakimuuwa mafundisho yake
yatakuwa ndio mwisho:
Tu n a f a n ya n i n i ? M a a n a
mtu huyu afanya ishara nyingi.
Tukimwacha hivi, watu wote
wa t a m wa m i n i ; n a Wa r u m i
watakuja, watatuondolea
Makala
8
Na Omar Msangi
NINGEPENDA kuanza kwa
kuwaombea kwa Mwenyezi
Mungu wale waliodhulumiwa
uhai wao kwa kupigwa risasi
katika tukio la mwishoni mwa
wiki kule Kenya. Katika tukio
hilo tunaambiwa kuwa watu
wanaodhaniwa kuwa ni magaidi
waliteka basi na kuuwa watu 28.
Aidha, nawapa pole wale
ndugu, jamaa na marafiki wa
marehemu ambao wamekatizwa
uhai wakiwa safarini kuelekea
Nairobi. Taarifa za vyombo
v ya h a b a r i z i n a f a h a m i s h a
kuwa basi lililokuwa likielekea
Nairobi, lilipofika katika mji
wa Mandera, ulio mpakani na
Somalia, lilivamiwa na kutekwa
na watu wenye silaha. Taarifa
zaidi zinadai kuwa watekaji hao
waliwatenganisha Waislamu
na Wakristo kisha wakawauwa
Wakristo 28, waliokuwa kati ya
abiria 60 wa basi hilo.
Waliwajua vipi Wakristo?
Baadhi ya vyombo vya habari
vikasema kuwa waliwataka
watu wote watamke Shahada
mmoja mmoja, walioshindwa
wakatambulika kuwa ni Wakristo.
Magazeti mengine yakasema kuwa
abiria waliambiwa kusoma Quran,
walioshindwa kusoma japo sura
au aya yoyote, wakatambulika
kuwa sio Waislamu.
The hijackers demanded the 60
passengers aboard recite the Shahada,
a tenet of Islam. The 28 -- 19 men
and nine women -- who were unable
to recite the passage where shot
to death. (Agence France-Presse
reported)
Wakati AFP wakisema kuwa
a b i r i a wa l i t a k i wa k u t a m k a
Shahada, BBC wao walikuwa na
haya ya kusema:
Gunmen separated out nonMuslims by asking passengers to read
from the Koran, officials and witnesses
said. Those who failed were then shot
in the head.
Ripoti ya polisi Kenya ni sawa
na ile ya AFP ambapo Mkuu
wa P o l i s i , D a v i d K i m a i y o ,
alisema kuwa waliouliwa ni wale
walioshindwa kutamka Shahada.
Taarifa ya haraka haraka ya
polisi, wanasiasa na vyombo vya
habari, zilidai kuwa wahusika wa
shambulio hilo ni Mujahidina wa
al-Shabab, wengine wakisema ni
magaidi wa al-Shabab.
Sababu zilizotolewa ni mbili,
moja ni kwamba pamoja na ile
sababu ya siku zote kwamba
wanafanya mashambulizi hayo
kulipiza kisasi kutokana na hatua
ya serikali ya Kenya kupeleka jeshi
Somalia, lakini sababu nyingine
i m e t a j wa k u wa wa n a l i p i z a
kisasi kwa tukio la wiki iliyopita
ambapo polisi walivamia Msikiti
Mombasa, wakauwa kijana mmoja
na kuwakamata wengi kwa
mamia. Katika operesheni hiyo,
iliyomalizika kwa kupigwa kufuli
misikiti minne na kuwa marufuku
kupiga Adhana na kuswali au
kufanya Ibada yoyote katika
Misikiti hiyo, polisi walidai kuwa
AN-NUUR
Wanasiasa, magazeti
wanapandikiza ugaidi
Wataalamu wa kupambana
na magaidi watatuangamiza
Na Omar Msangi
TAARIFA za wiki hii kutoka
Nigeria zinafahamisha kuwa
washambuliaji wawili wa kike
wa kujitoa muhanga (suicide
bombers), walilipua bomu katika
soko lililojaa watu katika mji
wa Maiduguri, na kuuwa kwa
uchache watu 45.
Taarifa ya Shirika la Habari la
AFP ikidai kunukuu mashuhuda
waliokuwa eneo la tukio ilidai
kuwa wasichana wadogo chini ya
miaka 20 waliokuwa wamevalia
hijabu walijilipua katikati ya watu
sokoni hapo.
Japo hakuna kikundi hadi
sasa kilichodai kuhusika na
shambulio hilo, vyombo vya
usalama vya Nigeria vinadai
kuwa watuhumiwa watakuwa ni
Boko Haram.
Tukio hilo linakuja baada ya
miaka mingi kwa serikali ya
Nigeria na vyombo vyake vya
dola kutangaza hatua kali za
kupambana na Boko Haram, lakini
pia na kuwekewa bajeti kubwa ya
9
Inatoka Uk. 8
huko nyuma na wanasiasa wetu,
ambayo ndiyo yanayopelekea
kupandikiza kitisho katika nchi
zetu. Na kikishapandikizwa,
kikakubalika kwamba kipo, hizi
kauli za polisi, jeshi, Rais wa nchi
kwamba tutapambana vikali
na magaidi, ni kauli za bure tu.
Hazina maana yoyote. Kadiri
watakavyojidai kupambana,
ndivyo na ugaidi wenyewe
utakavyoongezeka. Mfano wala
haupo mbali, upo kwa Goodluck
Jonathan na Boko Haram yake.
Aliwahi kusema aliyekuwa
Waziri wa Mambo ya Nje wa
Uingereza, Robert Finlayson
"Robin" Cook , kwamba, al-Qaida
ni magaidi wa kubuni na wa
kutumiwa na mabeberu kwa
malengo yao. Mabeberu wakiacha
mkakati huo wa kutumia magaidi
katika mipango yao, na ugaidi
unaporomoka siku hiyo hiyo.
Huo ndio ukweli. Sio kwa ATPU
au jeshi la Kenya kukaza buti
kupambana na magaidi.
Nigeria walikaza sana buti
toka Boko Haram walipokuwa
wakidaiwa kuwa wanarusha
mabomu ya mafuta ya taa na baruti
za kutengeneza kienyeji, sasa
wana magari ya kivita na mizinga
ya kutungulia ndege! Swali ni
je, wamezipata wapi silaha hizi?
Zimetoka wapi na zimeingia vipi
Nigeria hadi kuwafikia?
Al-Shabab halikuwa tatizo
la Kenya, Uganda, Tanzania
Inafahamika wazi kuwa pamoja
na matatzo waliyokuwa nayo
Somalia, vita vyao havikuwa
tatizo la Kenya, Uganda, Zanzibar
wala Dar es Salaam, ukiacha
tatizo la wakimbizi kama walivyo
wale kutoka Rwanda, Burundi
na Congo DRC. Inafahamika pia
kuwa juhudi zote za inayoitwa
Jumuiya ya Kimataifa kuleta
amani Somalia, zilikwama. Na
inafahamika kuwa ni Wasomali
weyewe hatimaye waliofanikiwa
kurejesha amani kama CCM na
CUF walivyofanikiwa kuleta
muafaka Zanzibar ikatulia,
wakati huko nyuma miafaka yote
iliyopata baraka na iliyosimamiwa
na serikali ya muungano na ile
Jumuiya ya Kimataifa, ikasainiwa
kwa mbwembwe ilikwama.
Ni jambo linalofahamika wazi
pia kwamba hawa wanaotoa
machozi kuwalilia Wakenya
waliouliwa na wanaosema
k u wa wa t a k u wa b e g a k wa
bega na Kenya kupambana na
magaidi, ndio waliovuruga
amani iliyochipua Somalia na
ikawa ndio sababu ya kuibuka
al-Shabab. Lakini inafahamika
wazi pia kuwa ilikoanzia alShabab, ni wananchi wa Somalia
waliokuwa wakipinga serikali
waliyoita kibaraka iliyoweka na
wale walioondoa serikali yao ya
umoja iliyoweza kurejesha amani
na usalama Somalia.
Lakini kilichotokea ni kuwa
wakati al-Shabab na serikali
ya mpito (Transitional Federal
Government-TFG), ilikuwa ni
Makala
AN-NUUR
Wanasiasa, magazeti
wanapandikiza ugaidi
Inatoka Uk. 8
tatizo la ugaidi wa Boko Haram.
Inakuwa kana kwamba kila
unapopewa msaada zaidi, ndio
ug a id i u n a v y o o n g e z e k a n a
magaidi kuwa na uwezo mkubwa
zaidi.
Tuliambiwa kuwa kule Iraq
walitumia Salvador Option na
tunafahamu kilichotokea pale
wa l i p o k a m a t wa m a k a c h e r o
wawili wa Uingereza wakijifanya
ni magaidi wa Mehdi Army wa
kujitoa muhanga. Hakuna namna
nyingine unaweza kuelewa
kitendawili hiki cha Boko Haram,
zaidi ya kutizama uhusiano wa
ugaidi wa Iraq na matukio hayo
ya Salvador Option.
Kule Mombasa tumeambiwa
kuwa polisi walivamia msikiti
kwa sababu kulikuwa na taarifa
za ki-intelijensia kuwa kuna
silaha na watu wanaojifunza
ugaidi. Ukifanya harakati kama
zile, kwa maana ya kuvamia
msikiti na kisha kuufunga na
kupiga marufuku watu kuswali,
jambo ulilo na uhakika nalo ni
kuwa litazuka zogo na vijana
(Waislamu) wanaweza kuja juu
kutaka kulipiza kisasi.
Swali ni kuwa kwa nini polisi
walifanya harakati ile wakijua
matokeo yake?
Lakini mara baada ya tukio
hilo, tunaambiwa kuwa magaidi
Wataalamu wa kupambana
na magaidi watatuangamiza
Inaendelea Uk. 10
kuthibitisha hilo.
Shambulio la Westgate
Shopping Mall Nairobi
Yapo matukio mengi ambayo
ilidaiwa kufanywa na magaidi wa
al-Shabab likiwemo lile shambulio
la Kampala tarehe 11 Julai, 2010
ambapo watu 74 walikufa na
wengine 70 kujeruhiwa wakati
wapenzi wa mpira wakitizama
mechi za kombe la dunia. Lakini
hayo tuyaache kwanza tutizame la
Westgate Shopping Mall, Nairobi.
Tuliambiwa magaidi kati ya 10 na
15 kutoka Somalia waliigia Kenya
wakiwa na gari lililosheheni silaha
wakaingia katika kituo hicho
maarufu cha kibiashara na kuanza
kuuwa watu. Walivamia tarehe
21 Septemba 2013, na kudumu
katika jengo hilo hadi 24 Septemba
ambapo ilidaiwa kuwa watu 67
waliuliwa na wengine zaidi ya 175
kujeruhiwa.
Polisi, vikosi maalum vya polisi,
Idara za Usalama za Ndani na
Nje ya Kenya na jeshi la Kenya,
w o t e h a o wa l i k u wa k a t i k a
operesheni ya kukabiliana na
magaidi hao 15 kutoka Somalia!
Vifaru na silaha nyingine nzito
za kijeshi, vikaonekana vikiranda
na kuzingira Nakumati. Na
tunaambiwa kuwa kituo hicho
cha kibiashara kinamilikiwa na
raia wa Israel. Lakini pia wapo
Wayahudi kwa uchache wanne
ambao wamekodi katika jengo
hilo wakiendesha migahawa.
Zaidi ni kwamba, Kenya ina
makubaliano na Israel ya kiulinzi
na hivyo makachero wa mwanzo
kuingia katika operesheni hiyo ya
kukabiliana na magaidi 15 kutoka
Somalia, walikuwa makachero wa
MOSSAD. (Tazama: International
Business Times)
Hata hivyo, vikosi vyote hivyo
havikufanikiwa japo kukamata
au kuuwa hata gaidi mmoja
n a k u o n y e s h a m a i t i ya k e !
Magaidi wakafanya waliyofanya,
wakajiondokea zao wakaacha
huku nyuma wanajeshi,
serikali na wananchi wa Kenya,
wakiparurana kuwa badala ya
kupambana na magaidi, wanajeshi
walikuwa wakipora mali na
kulewa. Picha zikasambazwa
kuonyesha walichokuwa
wakifanya wanajeshi hao wakiwa
ndani ya Nakumati. (Pflanz, Mike.
"Kenyan army admits that soldiers
looted Westgate during siege".
London. Retrieved 29 October
2013.)
Taarifa za kuingia magaidi
Nakumati, Westgate, Nairobi,
zilipambwa na kusindikizwa na
visa vyingi vilivyonogeshwa zaidi
na vyombo vya habari vikiwa vile
vilivyopigiwa zumari kuonyesha
jinsi magaidi hao al-Shabab
walivyokuwa katili kwa Wakrsito.
TV na magazeti yakaandika na
kupamba kwamba magaidi hao
walikuwa wakiwapa mateka wao
mtihani, anayefaulu kuthibitisha
kuwa ni Muislamu anaachwa,
a n a y e f e l i a n a p i g wa r i s a s i
Inaendelea Uk. 10
10
Inatoka Uk. 9
kichwani. Lakini tukaambiwa
pia kuwa hata watoto wadogo
wakithibitika kuwa ni Wakristo,
walikuwa wakibamizwa vichwa
vyao katika ukuta au mikono yao
kukatwa ikachongwa na kufanywa
kalamu za kuandikia huku damu
ikifanywa wino. Vyombo vya
habari vikasherehesha sana habari
hizi.
K wa h i y o , m p a k a t u k i o
linamalizika, ishawekwa
ushahidi kuwa wapo magaidi
wanaoitwa al-Shabab weye uwezo
wa kushinda polisi, Idara ya
Usalama ya Kwenya na Jeshi
lote la Kenya likipewa msaada
kutoka Israel na Uingereza!
Lakini maadhali tuliambiwa kuwa
walikuwepo makachero wenye
silaha nzito wa MOSSAD na wale
wa Uingereza (na Marekani?), ni
kwamba tukio liliweka muhuri pia
kuwa magaidi hao ni hatari mno
kiasi kwamba hata wazito hao wa
kidunia katika vita na ukachero,
hawana ubavu wa kukabiliana
nao!
Maadhali ushaweka msingi
huo, na maadhali ushakubali
kuwa una kitisho hicho cha
ugaidi wa kiwango hicho, katika
ulimwengu huu wa Vita dhidi
ya Ugaidi, yaliyosalia au tuseme
yatakayokuja kufanyika baadae
ili kuendeleza vita ya wenyewe
mabeberu dhidi ya ugaidi, wala
hutakuwa na udhibiti nayo. Huo
ndio ukweli. Ndio pale nikasema
kuwa kauli ya Rais Uhuru Kenyatta
na mwenzake William Ruto, wala
hazina maana yoyote. Silaha
zitaendelea kupatikana Misikitini,
iwe ni kwa njia ya kupandikizwa
(dubious terrorism sting tacticsDubious Entrapment ), kwa maana
ya kughilibu baadhi ya watu au
kuwanunua na kuwafanyisha
vitendo vitakavyothibitisha kuwa
kuna ugaidi. Na kwa sababu
hiyo, matukio yanayodaiwa
ya Wakristo kutenganishwa
na Waislamu, kisha Wakristo
kuuliwa, yataendelea kuwepo.
Ile kukubali propaganda
kuwa al-Shabab wanaopambana
n a m a j e s h i ya u va m i z i ya
Ethiopia yaliyovamia nchi yao
na kuweka serikali kibaraka,
ni magaidi hatari kwetu; kosa
namba moja. Vile tulivyopokea
shambulio la Westgate, pamoja
na utata wote ulioligubika kama
inavyoelezwa katika ile makala
ya Jicho Pevu (KTN), kosa la
pili la msingi. Mtu anadaiwa
kupigwa risasi ya mgongoni,
lakini picha inamwonyesha hana
damu inayotiririka, bali doa tu
jekundu inakodaiwa kupita risasi.
Lakini zaidi anatembea. Ajabu
ya mambo. Kwa ujasiri mkubwa
tv zinaonyesha na magazeti
yaliandika na kusherehesha, ikiwa
ni pamoja na yule aliyedaiwa
kupigwa risasi ya kisigino, lakini
soksi haina damu na anatembea
mwenyewe!
Kuuliwa Masheikh
Kenya yamefanyika mauwaji
Makala
Wanasiasa, magazeti
wanapandikiza ugaidi
Wataalamu wa kupambana
na magaidi watatuangamiza
Inatoka Uk. 9
Columbia Law School, wamefanya
utafiti na kutoa ripoti ya kurasa
214 waliyoipa jina "Illusion of
Justice: Human Rights Abuses in US
Terrorism Prosecutions.
Ndani ya ripoti hiyo
wanaonyesha jinsi FBI
wanavyotumia njia mbovu na
zisofaa (Dubious Entrapment
Arrests/terrorism sting tactics.)
kuwatia katika jinai ya ugaidi
watu ambao wala hawakuwa na
mawazo ya kufanya uhalifu huo.
Ripoti hiyo inaeleza kwa
undani jinsi serikali ya Marekani
inavyowahujumu Waislamu na
kuwachonganisha na jamii ya
Wakristo. Na hiyo ni kwa sababu
ya kuwafanyia vitendo vingi vya
entrapment na kuwatangaza
kuwa ni magaidi.
The report also shows how
government tactics are antagonizing
American Muslims. "The U.S.
government has on the one hand
claimed that American Muslim
communities are essential partners,
while at the same time placing them
under surveillance and treating them
as suspects. The impact of those
practices has been quite serious,
alienating some communities and
leading to fear and suspicion in places
like mosques and community centers
that should be places of refuge."
(Andrea Prasow, deputy Washington
director for HRW)
Kama tutakumbuka vizuri
katika matukio yote yaliyowahi
AN-NUUR
11
Makala
Na Mwandishi Wetu
AN-NUUR
12
Barua/Mashair
AN-NUUR
Wataalamu wa kupambana
na magaidi watatuangamiza
Inatoka Uk 10
ni kuwatafuta vijana
maadhura walio
punguwani kidogo, kama
wavuta bangi vile na
wenye matatizo ya kipesa.
Hawa hujazwa fikra za
ugaidi, kulipua mabomu
na Jihad feki halafu
ndio baadae hukamatwa
ikadaiwa kuwa ni magaidi
Waislamu.
Sasa kwa mtindo huu,
kama tutakwenda na
mtiz a m o k uwa ha wa
vijana ndio maadui hatari
wa amani ya nchi yetu,
kadiri tutakavyofanya
operesheni
za
kuwakamata na kuwatesa,
haitatusaidia sana.
Haitatusaidia kwa sababu
tuta kuwa tunahangaika
a j i l i ya k u p a m b a n a n a
makafiri au Wakristo au
hata kwenda Somalia, mtu
huyu anasimama katika
misikiti miwili, mitatu na
a n a d u m u k wa m a s i k u
kadhaa, bila ya vyombo
husika kuchukua hatua,
kwa nini Waislamu wasiwe
na wasiwasi kuwa ni katika
zile zile mbinu za marafiki
zetu FBI za dubious
entrapment? Rejea ile ripoti
ya HRW iliposema: The
government came up with the
crime, provided the means, and
removed all relevant obstacles."
Kama walivyosema HRW,
Sting Op erations hizi
Operations za ki-FBI,
hakuna wa kuwasaidia
wala wasitafute mchawi.
13
TANGAZO
AN-NUUR
Waislamu kote nchini mnatangaziwa nafasi za kidato cha Kwanza kwa shule zifuatazo:
Mkuzo Islamic High School - Bweni tu - SONGEA
Kirinjiko Islamic Sec. School - Bweni tu SAME - KILIMANJARO
Nyasaka Islamic Sec.School - Bweni tu - MWANZA
Ubungo Islamic High School - Kutwa tu DAR ES SALAAM
1. Shule hizi ni za Kiislamu, zenye lengo la kuwapa watoto elimu bora na kuwalea kwa malezi mazuri ya Kiislamu.
2. Masomo yanayofundishwa ni haya yafuatayo:
Elimu ya Dini ya Kiislamu, Usomaji Quran na mafunzo yake, Hadithi za Mtume(s.a.w), Lugha ya Kiarabu, Kiswahili, English, Basic Mathematics, Physics, Chemistry, Biology, Geography,
History, Civics, Book keeping na Commerce.
3. Patakuwa na mtihani tarehe
29/11/2014 saa2:00asubuhi katika vituo mbali mbali kote nchini. Muombaji anaweza kufanyia mtihani katika kituo chochote.
Arusha
Kilimanjaro
Tanga
Mwanza
Dar es Salaam
- Ubungo Islamic High School : 0712974428/0712033556.
- Ofisi ya Islamic Ed. Panel Temeke -Msikiti wa Nurul Yakin : 0655144474.
Morogoro
- Wasiliana na Ramadhani 1
Chale : 0715704380.
Dodoma
- Hijra Islamic Primary School : 0716 544757/0718 661992.
Singida
- Ofisi ya Islamic Education. Panel karibu na Nuru snack Hotel : 0786 425838/0784 928039.
Manyara - Ofisi ya Islamic Ed. Panel Masjid Rahma: 0784 491196
Kigoma
Lindi
Mtwara
Songea
Mbeya
Tabora
Iringa
Pemba
Unguja
- Madrasatul Fallah: 0777125074.
Mafia
- Ofisi ya Ust. Yusufu Ally jirani na msikiti mkuu : 0773580703.
Handeni - Nassoro Mafiga: 0782 105735/ 0657 093983
14
Makala
AN-NUUR
15
MAKALA/TANGAZO
AN-NUUR
AN-NUUR
16
16
16
MAKALA
AN-NUUR
Soma
gazeti la
AN-NUUR kila Ijumaa
Na Bakari Mwakangwale
MWENYEKITI wa Taasisi
ya Kiislamu ya DaarulHijra ya Mjini Morogoro,
S h e i k h Wa z i r i A m a n i
Maduga, ameachiwa huru
na Mahakama ya Wilaya
ya Morogoro baada ya
kukamatwa kwa tuhuma
za Ugaidi.
Mbali ya Sheikh
Maduga, pia Mahakama
hiyo imewaachia Waislamu
Na Seif Msengakamba
KESI dhidi ya watuhumiwa
wa ugaidi ambayo awali
iliwasilishwa katika
Mahakama ya Hakimu
Mkazi Kisutu kwa zaidi
ya mwezi mmoja uliopita,
imefikishwa Mahakama
Kuu ya Tanzania Jumatatu
wiki hii Novemba 24 ikiwa
chini ya Jaji Twaibu Faudhi.
Hata hivyo kesi hiyo
imeahirishwa hadi Desemba
4 mwaka huu, baada ya
mawakiliwa wa upande wa
Jamhuri kuiomba mahakama
hiyo kuwapa muda wa
kuleta majibu ya maombi
yaliyoletwa na upande wa
utetezi katika mahakama
hiyo.
Jaji Faudhi alikubaliana na
hoja ya upande wa Jamhuri
na kuwaamuru kuleta majibu
yao Novemba 28.
Wakili wa upande wa
utetezi, Abubakari Salim,
alimwelezea mwandishi
wa gazeti hili baada ya
kuahilishwa kwa kesi hiyo
kuwa, upande wa Jamhuri
ulioongozwa na wakili
Peter Njike, awali waliomba
kupewa muda zaidi wa
kuleta majibu ya maombi
ya u p a n d e wa u t e t e z i
yaliyowasilishwa mahakami
hapo.
Wamepewa tarehe 28
Novemba walete majibu
yao na sisi kama tuna hoja
za nyongeza, tumetakiwa
kuleta Desemba 1 na shauri
litasikilizwa Desemba 4
mwaka huu. Alisema Wakili
na mawakili wenzake
waliokuwa Dar es Salaam
ambao walimhakikishia
kwamba Sheikh Msellem
alikuwa salama.
Taarifa hizo za mitandao
ya simu na kijamii ni za uzushi
na uvumi unaoenezwa bila
kuchunguzwa. Niwatoe hofu
Waislamu juu ya afya ya
Sheikh Mselemu, afya yake
ni safi na imeimarika na
inaendelea vizuri.
W a k i l i
h u y o
aliwahakikishia Waislamu
a k i wa o m b a wa t u l i e n a
kuwataka kutosikiliza taarifa
zisizokuwa rasmi na ambazo
hazijachunguzwa.
Kila mmoja atakufa, ya
nini umzushie mwenzako
hali ya kuwa yu hai, alihoji
Wakili Juma.
Alisema watuhumiwa
wote walifika mahakamani
na afya zao zinaendelea vizuri
hivyo kuwataka Waislamu
kuendelea kuwa na subra.
bali ni watuhumiwa
kwamba Serikali ilikuwa
inawatuhumu tu na wao
ni wajibu hoja kujitetea.
Alisema Sheikh. Mwinge.
Kiongozi huyo wa
Waislamu Mkoani humo,
alisema ilibainika Mahakana
hapo kuwa Waislamu hao
walikamatwa na watu wa
uchunguzi wa mabomu
wa Kimataifa, ambao ndio
wanaendelea na zoezi hilo
kwa sasa hata hivyo hakuna
ushahidi wowote uliotolewa
kwa tuhuma hizo.
Alipoulizwa kama
Waislamu hao walipata
nafasi ya kujitetea juu
ya tuhuma hizo, Sheikh
Mwinge, alisema, kutokana
na upande wa mashitaka
kuweka wazi kuwa haikuwa
kesi hawakuwa na papara
ya kutafuta Wakili kwa ajili
ya utetezi au wao wenyewe
kujitetea.
Waislamu
hao
wameachiliwa kwa mashariti
kadhaa kufuatia upande
wa mashitaka kuiomba
Mahakama, miongoni mwa
mashariti hayo kuwataka
wasifadhili Magaidi,
wasiwasaidie na wasitoe
msaada wa kifedha kuwapa
magaidi.
Aidha, Mahakama hiyo
iliombwa iwatake Waislamu
hao kuwa walinzi wa amani
kwa muda wa miaka mitatu,
sambamba na mashariti
magumu ambayo yatatolewa
na Mahakama.
Mashariti mengine
yametajwa kuwa, kila mjibu
m a o m b i ( m t u h u m i wa )
alitakiwa kusaini mkataba
wa udhamini wenye thamani
ya Shilingi Milioni tatu,
sambamba na wadhamini
watatu huku wakitakiwa
kuripoti kituo cha Polisi kwa
RCO, kila baada ya miezi
mitatu.
Sheikh Mwinge, alisema
mashariti yote yalitimizwa
k wa wa t u h u m i wa h a o
kwa kusaini mkataba wa
kulinda amani na dhamana
ya shilingi milioni tatu kwa
maandishi pia walipatikana
wadhamini watu kwa kila
mmoja siku hiyo hiyo
Mahakamani hapo, baada
ya Mahakama kukubaliana
na upande wa mashitaka.
Lakini Mahakama
ilipinga muda wa miaka
mitatu na badala yake
ikawapa miaka miwili.
K wa h i y o k wa m u j i b u
wa makubaliano hayo ya
kimahakama, wataanza
kuripoti kwa RCO, kuanzia
Februari 25, 2015, kwa hiyo
tokea jana (Jumatatu wiki
hii) wakawa huru. Alisema
Shkh. Mwinge.
A k i z u n g u m z i a
k a m a t a k a m a t a h i y o ya
Serikali na kuwahusisha na
Ugaidi, Sheikh Muwinge,
alisema hayo ni matunda
y a Ta n z a n i a k u u n g a
mkono sheria ya Ugaidi,
kwa madai ya kupiga vita
Ugaidi bila kujua gaidi
wanayemkusudia ni nani.
Mchakato ule wa sheria
ya Ugaidi matokeo yake ndio
haya na kwa kutokana na
hali ya Waislamu tuliyonayo
sasa na kanuni za sheria
h i y o , n i wa z i k wa m b a
Waislamu tupo katika kuti
kavu ndani ya nchi yetu.
Alisema Muwinge.
Kubwa niseme kwamba
utulivu unahitajika, subra
inahitajika hekma inahitajika
katika suala zima la kufikisha
u j u m b e wa M w e n y e z i
Mungu, vinginevyo
tunaweza kujikuta tunaingia
katika mitego iliyokusudiwa
kwetu. Alisema na
kutahadharisha.
Sheikh Waziri Maduga,
n a Wa i s l a m u w e n g i n e
wanne walikamatwa usiku
wa J u m a t a t u k u a m k i a
Jumanne ya wiki iliyopita,
kisha walisafirishwa
hadi Jijini Dar es Salaam,
ambapo Novemba 23, 2014
( Jumapili) walirudishwa
Mjini Morogoro na hatimaye
Novemba 24 (Jumatatu wiki
hii) walifikishwa Mahakama
ya Wilaya ya Morogoro.
Waislamu
hao
walikumbwa na kadhia hiyo
ni Sheikh Waziri Amani
M a d u g a ( K i o n g o z i wa
Kiislamu), Othman Saidi
Masanga (Dereva SUA),
Shabani Ramadhani Mussa,
Ally Ahmada Kahena
(wafanyabiashara Sokoni
Morogoro) , Msagomora
Faraji Msagomora, wote
wa k i wa n i wa k a z i wa
Morogoro.
Sheikh Waziri Maduga,
ni Mwenyekiti wa Taasisi ya
Daarul Hijra iliyopo Mafisa
Mjini Morogoro, ambayo
inaendesha na kusimamia
Shule za Awali na Msingi
za Taasisi hiyo, pia Shekh
Maduga, ni muhadhiri wa
Dini ya Kiislamu.