You are on page 1of 33

Kwa jina la Allah Mwingi wa Rehma Mwenye Kurehemu.

Raudhwah Time ni Jarida maalum, linalotolewa kila mwisho wa mwezi wa muandamo na


Raudhwah Islamic Group, kwa lengo la kumjenga Muislamu kumfahamu vilivyo Muumba wake
na kumpelekea kutimiza majukumu yake ya kiibada na kidini kwa ujumla, ili kuweza kupata
Radhi za Allah na kuepukana na adhabu zake.
Katika toleo la mwezi huu, tumekuandalia mada mbali mbali katika upande wa:
Afya. Ambayo itazungumzia maradhi ya Kipindupindu; ishara za mwenye maradhi haya,
tiba yake, kinga yake na mengine mengi kwa kifupi.
Jamii. Ambayo itazungumzia juu ya ujirani katika Uislamu.
Historia ya wema waliotangulia. Hapa tutamtaja kwa uchache Tabiin maarufu
anayejulikanwa kama Said bin Jubayr (rehma za Allah ziwe juu yake) na yaliyomfika
kutokana na kuukataa utawala wa Hajjaj bin Yuusuf.
Na mengine mengi yatakayokunufaisha wewe msomaji na Waislamu wote kwa ujumla.
Ni matumaini yetu kuwa Allah atatukubalia amali yetu hii na kuleta tija katika Ummah wa
Kiislamu, na kuwaongoza waliopotea na kuwaengezea istiqama walioongoka.

ii

Kila sifa njema zinamstahikia Allah Mola


wa viumbe vyote. Swala na salamu
zimuendee Mtume wetu Muhammad (swalla
Allahu alaihi wa sallam) na ahli zake na
maswahaba wake.
Leo kwa Tawfiq ya Allah nimependa
kugusia suala la ujirani katika Uislamu
ambalo wengi wetu hulipuuzia na kuliona ni
la kawaida, ima kwa kutambua au
kutotambua ukubwa wa fadhila zake.
Kama tunavyofahamu jirani ni mtu
anayeishi karibu na wewe, ima iwe
nyumbani kwako au kazini au popote pale
ulipo. Na kwa vile Uislamu ni Dini
iliyokamilika
kama
alivyotuambia
mwenyewe Allah (subhanahu wa taala): ...
Leo nimekukamiliishieni Dini yenu, na
nimekutimizieni
neema
yangu,
na
nimekupendeleeni UISLAMU uwe ndiyo
Dini ... [al-Maida (5): 3].

Mungu hawapendi wenye kiburi wanao


jifakhiri. [an-Nisai (4): 36].
Aya hii imebainisha kabisa uwajibu wa
kuwafanyia wema majirani walio karibu na
hata walio mbali kwa kadri tuwezavyo.
Sasa tumuangalie Mtume (swalla Allahu
Alayhi Wa sallam) nae anatuambia nini
kuhusu ujirani: Hakuacha Jibril ananiusia
kuhusu jirani mpaka nikadhania atamfanya
kuwa ni mmoja wa warithi wangu.
Bukhari.
Hadithi hii inatosha kabisa kutuonyesha
uwajibu wa kuishi kwa uzuri na jirani zetu
kwa sababu ni jambo ambalo alikuwa
akilitilia msisitizo Jibril (Alayhi ssalaam)
kila anapokuja kwa Mtume (swalla Allahu
Alayhi wa sallam).
Aina Za Jirani na Haki walizokuwa nazo:
1.

Uislamu haukuacha jambo lolote ila


limebainishwa na Allah (subhanah wa taala)
pamoja na Mtume wake (Swalla Allahu
Alayhi Wasallam). Katika kusisitiza hili
Allah (subhanahu wa taala) hakuacha
kulizungumzia suala la ujirani katika Qur'an
kama alivyosema: Muabuduni Mwenyezi
Mungu wala msimshirikishe na chochote.
Na wafanyieni wema wazazi wawili na
jamaa na mayatima na masikini na jirani wa
karibu na jirani wa mbali, na rafiki wa
ubavuni na mpita njia, na walio milikiwa na
mikono yenu ya kulia. Hakika Mwenyezi

2.

3.

Jirani ambaye ni ndugu yako. Huyu


ana haki tatu juu yako:
i.
Ya Uislamu.
ii.
Ya udugu.
iii. Ya ujirani.
Jirani ambaye ni Muislamu lakini sio
ndugu yako. Huyu ana haki mbili:
i.
Ya Uislamu.
ii.
Ya ujirani.
Jirani ambae si Muislamu. Huyu ana
haki moja kwako:
i.
Ya ujirani.

Hivyo ndugu zangu, lazima kila mmoja


tumpe haki anazostahiki bila ya kupunguza
chochote katika haki hizo.

Mwenye kumuamini Allah na siku ya


mwisho basi na asimuudhi jirani yake.
Bukhari.

Ewe Ndugu yangu, jilazimishe na mambo


matatu kuhusu jirani yako, utakua miongoni
mwa waliofaulu.

Hili ni himizo kwako ewe dada wa


Kiislamu, kama tunataka tuipate pepo ya
Allah, basi tujitahid kuishi vyema na
majirani zetu, kama huwezi kumfanyia
wema basi epukana na kumuudhi. Kwani
kupitia wao ndio tutaikamilisha imani yetu

1.

JIEPUSHE NA KUMUUDHI

Tukizungumzia maudhi, tunajumuisha kila


aina ya maudhi, imma ya kimaneno au
kivitendo, kwa kudhihirisha au kujificha.
Kwani hakika kuna makemeo makali kuhusu
hilo, na katika ubaya wa kumuudhi jirani
kuna khasara nyingi anazozipata mwenye
kumuudhi jirani yake ila leo nitataja mawili
makubwa kwa tawfiq ya Allah (Subhanahu
Wa taala).
a) Hawi na Imani
Hili ni kutokana na maneno ya Mtume
(Swalla Allahu Alayhi Wa sallam): Naapa
kwa jina la Allah hatoamini. Naapa kwa jina
la Allah hatoamini. Naapa kwa jina la Allah
hatoamini. pakasemwa Ni nani huyo ewe
Mtume wa Allah; akasema: Yule ambae
jirani yake hapati amani (hasalimiki)
kutokana na vitimbi vyake. Muslim.
Kina mama wengi tumekua hatujali uwepo
wa majirani na umuhimu wao kwetu.
Tumekua tukiwaudhi kwa udhia mbali
mbali. Tambua ewe ndugu yangu ya kuwa
ukamilifu wa imani yako unachangiwa na
kukaa kwa wema na jirani yako. Kama
anavyotueleza Mtume (Swalla Allahu
Alayhi Wa sallam) katika hadithi hii:

na tutaipata pepo ya Allah (Subhanahu Wa


taala). Kama alivyotuambia Mtume (Swalla
Allahu Alayhi Wa sallam): Hamtoingia
peponi mpaka muamini . Abu daud.
b) Matendo yake hubatilika
Jambo la kumuudhi jirani humsababishia
mtu kuharibika matendo yake na mwishoni
kuingizwa katika moto. Hadithi ifuatayo
inatubainishia hilo.
Siku moja maswahaba wa Mtume (Swalla
Allahu Alayhi Wa sallam) walimuuliza:
Hakika fulani anafunga mchana na
anasimama usiku kuswali na anamuudhi
jirani yake kwa ulimi wake. Mtume
akawajibu: Hamna kheri kwake nae ni
katika walio motoni wakamuuliza tena:
Hakika fulani anaswali swala za wajibu na
anafunga Ramadhani na anatoa sadaka
kidogo na wala hamuudhi jirani yake.
Mtume (Swalla Llahu Alayhi Wa sallam)
akasema: Yeye ni katika walio peponi.
Ahmad.
Hii inatupa fundisho kuwa hata kama utakua
unafanya ibada kwa wingi kiasi gani, kama

huishi na jirani yako kwa wema basi maishio


yako yatakua mabaya. (Allah Atuhifadhi).
2.

MVUMILIE MAUDHI YAKE

Hakika katika sifa za waumini wa kweli ni


wale ambao huwa na subra katika mitihani
aliyowapa Allah na wanatarajia malipo
kutokana na mitihani hiyo. Allah
(subhanahu wa taala) akikupa jirani muovu,
basi jua amekupa mtihani ndugu yangu ni
juu yako kufanya yafuatayo:
a) Kuwa na Subra
Kwani Allah (Subhanahu Wa taala)
amesema: Na ambao husubiri kwa kutaka
radhi ya Mola wao Mlezi, na wakashika
Sala, na wakatoa, kwa siri na kwa uwazi,
katika tulivyo wapa; na wakayaondoa
maovu kwa wema. Hao ndio watakao pata
malipo ya Nyumba ya Akhera. [ar-Raad
(13): 22].
b) Zuia Hasira zako na Usamehe
Atakapokuudhi jirani yako zizuie hasira
zako na jaribu kumsamehe. Kwani Allah
(subhanahu wa taala) amewasifu wenye
kufanya hivyo na amewaahidi malipo
mazuri. Allah amesema: ... Ambao hutoa
wanapo kuwa na wasaa na wanapo kuwa na
dhiki, na wanajizuia ghadhabu, na
wasamehevu kwa watu; na Mwenyezi
Mungu huwapenda wafanyao wema [alImraan (3): 134].
c) Mrekebishe na umlinganie kwa
hekima

Kwani majirani wengine hufanya makosa


kwa kutojua. Hivyo inawezekana akaongoka
kupitia wewe. Allah (Subhanahu Wa taala)
ametuambia: Waite waelekee kwenye Njia
ya Mola wako Mlezi kwa hikima na
mawaidha mema, na ujadiliane nao kwa
namna iliyo bora. Hakika Mola wako Mlezi
ndiye anaye mjua zaidi aliye ipotea Njia
yake, na Yeye ndiye anaye wajua zaidi
walio ongoka. [an-Nahli (16): 125].
d) Usimlipize bali mfanyie wema kwa
ubaya wake
Kwani hakika katika hili kuna taathira
kubwa kama alivyoeleza Allah (Subhanahu
Wa taala): Mema na maovu hayalingani.
Pinga uovu kwa lilio jema zaidi. Hapo yule
ambaye baina yako naye pana uadui
atakuwa kama rafiki jamaa wa kukuonea
uchungu. [Fusswilat (41): 34].
Nyoyo zikifanyiwa mema hujenga mapenzi,
fata maneno haya ya Allah utaona maajabu
yake.
3.

MFANYIE IHSANI

Ihsani ni kila jema ambalo akifanyiwa mtu


roho yake hufurahi sawa sawa kimaneno au
kivitendo. Ewe Ndugu yangu jilazimishe na
kumfanyia ihsani jirani yako, kwani hakika
kumfanyia yeye ihsan ni miongoni mwa
sababu zitakazokufanya uipate pepo ya
Allah (subhanahu wa taala), pamoja na
kukuepusha na moto wa Allah. Na miongoni
mwa ihsan ambazo zimetajwa na Mtume
(Swalla Allahu Alayhi Wa sallam) ni:

a) Kumpa
chakula
unaoupika

katika

mlo

Amesema Mtume (Swalla Allaahu Alayhi


Wa sallam): Hajaniamini mimi mwenye
kulala hali ya kuwa ameshiba wakati jirani
yake ana njaa pembeni yake na hali yeye
anajua jambo jilo. Bukhari.

c) Kumtembelea mara kwa mara


Hakika
Allah
huwapenda
wenye
kutembeleana kwa ajili yake na ndio maana
akasema
katika
hadithi
Qudsiy:
Yamewalazimikia mapenzi yangu wenye
kutembeleana kwa ajili yangu. Ahmad.

Pia katika hadithi nyingine amesema Mtume


(Swalla Allahu Alayhi wa sallam)
kumwambia Aba Dhar: Ewe Aba Dhar!

Kwani hakika Mtume (Swalla Allahu Alayhi


Wa sallam) alikuwa akipenda kuwatembelea
majirani zake walio Waislamu na hata
wasiokuwa
Waislamu,
waliokuwa

Ukipika mchuzi kithirisha maji yake na


umpe jirani yako. Muslim.

wakimtendea wema na hata waliokuwa


wakimuudhi.

b) Pendelea kumpa zawadi


Katika hadithi Mtume (Swalla Allahu
Alayhi Wa sallam) aliwahimiza wanawake
wa Kiislamu kuwapa zawadi jirani zao.
Enyi Waislamu wa kike, asidharau jirani
kumpa jirani yake chochote hata kama ni
kipande kidogo cha nyama. Bukhari.
Na Mama Aisha (radhia Allahu anha)
alimuliza Mtume (Swalla Allahu Alayhi Wa
sallam): Hakika yangu mimi nina jirani
wawili jee ni yupi nimpe zawadi. Mtume
(Swalla Allahu Alayhi Wa sallam) akasema:
Ambae mlango wake upo karibu nawe.
Bukhari.
Mwisho napenda kumalizia nukta hii kwa
hadithi ya Mtume (Swalla Llahu Alayhi wa
sallam) aliyosema: Mwenye kumuamini
Allah na siku ya mwisho basi na amkirimu
jirani yake. Bukhari na Muslim.

d) Akiumwa
nenda
(ukamjuulie hali)

ukamtizame

Kwani kufanya hivyo utapata malipo


makubwa kama alivyotuambia Mtume
(Swalla Allahu Alayhi Wa sallam):
Mwenye kumtembelea Mgonjwa Hatoacha
kuwa miongoni mwa waliomo katika
Mabustani ya peponi. Muslim.
HITIMISHO
Huu ndio ufupisho wa mada ya ujirani
katika Uislamu kama ulivyoelezewa kwenye
Qur'an na Sunna za Mtume (Swalla Allahu
Alayhi Wa sallam). Namuomba Allah
atuonyeshe haki ilipo na atuwafikishe
kuifata na atubainishie batil na atuwafikishe
kuiacha. Amin.

Kipindupindu ni ugonjwa wa maambukizi


unaosababisha kuharisha sana kinyesi
kilicho katika mfumo wa maji maji kama
rangi ya mchele. Maradhi haya yanaweza
kusababisha upungufu wa maji mwilini na

Ugonjwa huu unatokea kwa kawaida na kwa


kiasi kikubwa katika maeneo yaliyo katika
hali duni ya usafi, msongamano wa watu,
vita, na njaa. Maeneo ya kawaida ni pamoja
na maeneo ya Afrika, Asia kusini, na

hata kifo ikiwa mgonjwa hakutibiwa


mapema. Kipindupindu husababishwa kwa
kula chakula au
kutumia maji
yaliyoathiriwa na vimelea vya bakteria
ajulikanae kwa jina la kitaalamu kama
Vibrio cholerae.

Amerika ya kati na kusini (Latin America).

Sababu za kipindupindu

i.

Kuongezeka kwa
mapigo ya moyo,

kiwango

cha

Bakteria
anaesababisha
kipindupindu,
kawaida hupatikana katika chakula au maji
yaliyochafuliwa na kinyesi kutoka mtu aliye
na maambukizi. Vyanzo vya kawaida vya
maradhi haya ni pamoja na maji ya miji,
barafu iliyofanywa kutokana maji ya miji,
vyakula na vinywaji viuzwavyo na wachuuzi
wa mitaani, mboga mboga zilizomwagiliwa

ii.

Kupungua
(elasticity),

iii.

Kukauka kwa kiwamboute (mucous


membrane) (ikiwa ni pamoja na
ndani ya mdomo, koo, pua, na kope),

iv.

Kupungua kwa shindikizo la damu,

kwa maji yaliyochafuliwa na kinyesi na


takataka za wanaadamu, samaki wabichi na

v.

Kiu kali na maumivu ya misuli.

mazao mengine ya bahari


hayajapikwa vizuri.

yaliyokuwa

Endapo mtu atatumia chakula au maji


yaliyoathirika, bakteria hutoa sumu katika
utumbo ambayo hupelekea kuharisha sana.
Dalili za maradhi
Dalili za ugonjwa wa kipindupindu
zinaweza kuanza haraka sana kama saa
chache au kwa muda mrefu kama siku tano
baada ya kuambukizwa. Mara nyingi dalili
huwa sio kali sana, lakini wakati mwengine
huwa ni mbaya sana. Takriban mmoja kati
ya
watu
ishirini
katika
watu
walioambukizwa huonyesha dalili za
kuharisha sana zikifuatana na kutapika,
ambako kunaweza kusababisha upungufu
mkubwa wa maji mwilini. Ingawa watu
wengi walioambukizwa wanaweza kuwa na
dalili chache au kutokuwa na dalili kabisa,
lakini bado wanaweza kuchangia kuenea
kwa maambukizi. Dalili na alama
za
upungufu wa maji mwilini ni pamoja na:

kwa

mkunjuko

Kama mgonjwa hakutibiwa mapema,


upungufu wa maji mwilini unaweza
kusababisha mshtuko (shock) na kifo ndani
ya masaa machache.
Kinga na tiba
kipindupindu

ya

maambukizi

ya

Ingawa kuna chanjo dhidi ya kipindupindu,


CDC na Shirika la Afya Duniani kawaida
hawaipendekezi kutumiwa, kwa sababu
inaweza kutowalinda nusu ya watu wenye
kupata chanjo hiyo na huchukua muda wa
miezi michache tu kabla kupoteza uwezo
wake wa kufanya kazi. Hata hivyo, unaweza
kujikinga na familia yako kwa kutumia maji
yaliyochemshwa vizuri au maji yaliyotiwa
dawa (chemicals) za kuua vimelea vya
ugonjwa huo, kutumia maji ya chupa
yaliyoandaliwa katika viwanda vyenye
mazingira safi.
Maji hayo huweza
kutumiwa kwa madhumuni yafuatayo:
i.

Kunywa,

ii.

Maandalizi ya chakula au vinywaji,

iii.

Kugandishia barafu,

iv.

Kusugua meno yako,

v.

Kuosha uso wako na mikono,

vi.

Kuosha sahani na vyombo ,

vii.

Matumizi ya kula au kuandaa


chakula na kuoshea matunda na
mboga.

Ili kuandaa maji yako mwenyewe, chemsha


kwa dakika zisizopungua kumi au kuyachuja
na kuongeza matone mawili ya bleach
(chlorine) au weka nusu kidonge cha madini
joto aina ya IODINE kwa kila lita moja ya
maji. Pia lazima kuepuka vyakula vibichi,
ikiwa ni pamoja na yafuatayo:

ni janga tafuta msaada wa matibabu mara


moja. Kipindupindu ni maradhi yenye
kutibika kwa urahisi, lakini kwa sababu ya
upungufu wa maji mwilini unaoweza
kutokea haraka, ni muhimu kupata matibabu
ya kipindupindu haraka sana mara tu
unapoona dalili za maradhi hayo.
Matibabu makuu ya ugonjwa huu ni
kumsaidia mgonjwa kurejesha kiwango
kikubwa cha maji ambacho amekipoteza
kwa kuharisha sana, maji yaliyopotea
yanaweza kuwekwa kwa njia ya drip katika
mishipa ya damu (intravenous). Dawa za
antibiotiki ambazo huua
vimelea vya
maradhi haya zinaweza pia kutumika katika
kupunguza kasi na nguvu ya maradhi haya.

Matunda na mboga zilizokua


hazijamenywa na kuandaliwa vizuri,

Hitimisho

ii.

Maziwa na bidhaaa za maziwa


ambazo
hazijachemshwa
au
kuhakikishwa
kuwa
vimelea
vimefariki,

iii.

Nyama iliyokua haijapikwa n.k.

sana kwa sababu athari zake zinajitokeza


katika kipindi cha muda mfupi sana baada
ya maambukizi, na vile vile huweza
kusababisha kifo ikiwa hayajatibiwa haraka
baada ya kuambukizwa, lakini maradhi haya
ni yenye kutibika na kuepukika pia. Ni
muhimu sana kutumia maji na vyakula
vilivyo katika hali ya usafi, na wagonjwa
wanashauriwa kuwahi kupata huduma za
afya endapo wataona dalili za ugonjwa huu
kwa haraka sana.

i.

Endapo utahisi dalili za kuharisha kinyesi


chenye rangi kama maji ya mchele mara
kwa mara, na kutapika sana - hasa baada ya
kula samakigamba (shellfish) wabichi au
kusafiri kuelekea nchi ambayo kipindupindu

Ugonjwa wa kipindupindu ni maradhi hatari

KUMBUKA KUWA, KINGA NI BORA KULIKO TIBA!

SUALI
Ninafanya kazi katika kampuni ya Aramco,
ambayo ina program ya kustaafisha watu
ambao wamefikia umri wa miaka khamsini
(50), na hupata matibabu bure mpaka
mwisho wa maisha yao. Jee inafaa
kubadilisha umri wangu kwa kuomba katika
idara ya kumbukumbu bila ya kulipia
chochote au kutaja umri maalum, lakini kwa
lengo la kupata matibabu ya bure, kwa
sababu nikistaafu kabla ya kufikia miaka 50
sitopata matibabu (ya bure)?
JAWABU
Sifa njema ni za Allah.
Haifai mtu kudanganya kuhusu umri wake
ili apate matibabu ya bure yanayotolewa na
kampuni. Hii inakuwa ni kusema uongo na
kuhadaa, na Mtume (swalla Allahu alaihi wa
sallam) amesema: Mwenye kutuhadaa
(kughushi/kudanganya) si katika sisi.
Imepokewa na Muslim, 101.

Pia amesema (swalla Allahu alaihi wa


sallam): Hakika ukweli unamuongoza mtu
katika wema, na wema unampeleka mtu
Peponi. Na hakika mtu huendelea kusema
ukweli mpaka akaitwa mkweli mbele ya
Allaah. Na hakika uongo unampeleka mtu
katika uchafu, na uchafu unampeleka mtu
Motoni. Na mtu huendelea kusema uongo
mpaka akaandikwa kuwa ni muongo mbele
ya Allaah. Imepokewa na al-Bukhary, 6094
na Muslim, 2607.
Anachotakiwa Muumini kufanya ni kuwa
mkweli katika maneno na vitendo. Allah
(subuhanahu wataala) amesema: Enyi mlio
amini! Mcheni Mwenyezi Mungu, na
kuweni pamoja na wakweli (katika kauli zao
na vitendo vyao). [at-Tawbah (9): 119].
Na Allah anajua zaidi.
CHANZO:

http://islamqa.info/en/126053

Kila sifa njema zinamstahikia Allah


(subhanahu
wa
taala),
Mola
wa
walimwengu wote. Swala na salamu
zimfikie Mtume wetu Muhammad (swalla
Allahu alaihi wa sallam).

1.

MAJUKUMU
YAKE

JUU

YA

NAFSI

Pia namshukuru Allah kwa kunipa fursa hii

Ewe dada wa Kiislamu, tambua ya kwamba


dunia ni mapito na akhera ndio bora na
yenye kudumu, hivyo ni lazima ujichumie
hapa duniani kila kilicho bora kwa ajili ya

ya kuizungumzia mada hii muhimu, ambayo


wengi katika kina mama wa Kiislamu
tumeghafilika nalo jambo hili.

safari ndefu uliyonayo. Na aliyebora ni yule


aliyejitambua mapema na akaufanyia kazi
umri wake katika yalio mema.

Kama tunavyofahamu ya kuwa mara nyingi


mtu mwenye akili timamu na aliefikia umri
wa baleghe lazima huwa hakosi jukumu
lolote lile ambalo humlazimu kulitekeleza.
Lakini kwa leo nimependa khaswa,
nimzungumzie
mwanamke
ambaye

Kama tunavyofahamu ya kuwa nafsi siku


zote hutuamrisha yalio mabaya isipokua zile
alizozirehem Allah (Subhanahu Wa taala).
Lakini kilicho cha wajibu kwetu ni
kuziendesha sisi katika yaliomema na sio
kuziacha zituepeleke sisi zinavyotaka.

ameshaolewa na ameruzukiwa nyumba na


watoto, kwa sababu yeye ndiye chanzo cha
maendeleo au maharibiko ya jamii iliyopo
na ijayo.

Tufahamu ya kuwa nafsi ni kama mtoto,


ukiipa kila kinachotaka mwisho hutaka hata
chenye madhara nayo. Hivyo ni lazima
tujifundishe kuzikatalia khaswa katika yalio
haramishwa na Allah na Mtume (swalla
Allahu alaihi wa sallam), kwa sababu
Muumba wa nafsi zetu ndiye mwenye
kuzifahamu zaidi kipi kina faida nazo na
kipi hakifai au kipi chenye madhara.

Mwanamke wa Kiislamu aliyeolewa ana


majukumu manne makubwa ambayo ni
lazima ayatekeleze kwa ufasaha tena kwa
mujibu wa mafundisho ya Qur'an na Sunna.
Majukumu yenyewe ni;
1.
2.
3.
4.

Majukumu juu ya Nafsi yake.


Majukumu juu ya Mumewe.
Majukumu juu ya nyumba yake.
Majukumu juu ya jamii yake.

Dunia ni sawa na jela kwa Muumini yaani


huwa na mipaka, nayo ni maamrisho na
makatazo ya Allah (subhanahu wa taala)
aliyoyaeleza kupitia katika Quraan au
Mtume (swalla Allahu alaihi wa sallam).
Ama kwa kafiri ni sawa na Pepo, kwani
huwa hana mipaka hufanya anavyotaka

mwenyewe. Hivyo lolote ulifanyalo liwe


jema au baya utalikuta mbele ya Allah
(subhanahu wa taala) kwani ametueleza:
Basi anaye tenda chembe ya wema,
atauona! Na anaye tenda chembe ya uovu
atauona! [az-Zilzalah (99): 7-8].

2.

MAJUKUMU JUU YA MUMEWE

Hivyo jukumu kubwa la nafsi yako ni


kuifanya imuelekee mola wako katika amri
zake na kuiepusha na makatazo yake ili siku

Ndoa ni pingu ya maisha na ni ahadi kubwa


ambayo huichukua mume na mke kwa kule
kukubali kuiingia ndoa. Allah (subhanahu
wa taala) ameiita ndani ya Qur'an kuwa ni
"Ahadi madhubuti". Na kwa sababu hii
tunasisitizwa sana kuijua kiundani kabla ya
kujiingiza ndani yake, jambo ambalo wengi
wetu hawalifatilii na ndio sababu tunaona

hio isiwe ni yenye kujilaumu kama ambavyo


Allah ameiapia nafsi hii ambayo itakuja

machafuko makubwa yaliyopo katika ndoa


za wakati huu kutokana na kutoijua ukweli

kujuta kwa kila baya ililolitenda. Allah


anasema: Ninaapa kwa Siku ya Kiyama!
Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu! [alQiyamah (75): 1-2].

wa kuijua.

Jee unapenda kuwa miongoni mwa watakao


jilaumu kesho akhera? Bila shaka hapana.
Basi anza leo wala usingoje kesho, ambayo
hujijui kama utafika au hutofika.
Tujiandaeni na siku ya Qiyama ambayo
Allah anatuambia: Siku ambayo kila nafsi
itakuta
mema
iliyo
yafanya
yamehudhurishwa, na pia ubaya ilio ufanya.
Itapenda nafsi lau kungekuwako masafa
marefu baina ya ubaya huo na yeye. Na
Mwenyezi Mungu anakuhadharisheni naye.
Na Mwenyezi Mungu ni Mpole kwa waja
wake. [al-Imraan (3): 30].
Mwisho napenda kumalizia nukta hii kwa
kauli ya ameer wa Waislamu Umar bin
Khattab aliyosema: "Jihisabieni nafsi zenu
kabla hamjahisabiwa na yapimeni matendo
yenu kabla hamjapimiwa."

Hivyo
nimependa
kuyazungumzia
majukumu ya mwanamke katika ndoa yake
ili kuwazindua wanawake wa Kiislam
walioolewa na ambao hawajaolewa, kwani
huenda kwa tawfiq ya Allah ikawa ni sababu
ya kizirekebisha ndoa zao au kuziendesha
vizuri watakapoziingia.
Yafuatayo ni baadhi ya majukumu ya
mwanamke kwa mumewe:
i.

Kumtii mumewe katika yalio mema

Kwa vile mwanamme huchukua jukumu la


kuwa ni msimamizi kwa mkewe badala ya
wazazi wake baada tu ya kumuoa, hivyo ni
jukumu la mke kumsikiliza na kumtii katika
kila analomuamrisha miongoni mwa yale
yaliomo katika mipaka ya kisheria ya Dini
yetu. Allah (subhanahu wa taala)
ametuamrisha ndani ya Quraan kuwatii
viongozi wetu pale aliposema: Enyi mlio
amini! Mt'iini Mwenyezi Mungu, na mt'iini

10

Mtume na wenye madaraka katika nyinyi ...


[an-Nisaa (4): 59].
Na laiti mke angelijua umuhimu wa kumtii
mumewe angejitahidi kumtii mumewe kadri
awezavyo kwani Mtume (swalla Allahu
alaihi wa sallam) amesema: Laiti
ningekuwa ninaamrisha mtu kumsujudia
mtu (mwengine) ningemuamrisha mke
kumsujudia mumewe. Tirmidhiy.
Pia

katika

masharti

manne

ambayo

humuingiza mwanamke peponi moja wapo


ni twaa ya mke kwa mumewe nayo imo
katika kuonyesha fadhila na ubora wa ibada
hii. Kama alivyotuelezea Mtume (swalla
Allahu alaihi wa sallam): Atakapo swali
mwanamke swala zake tano (za faradhi), na
akamtii mumewe, na akafunga mwezi wake
(wa Ramadhani) na akajihifadhi utupu wake
ataambiwa siku ya Qiyama ingia peponi kwa
mlango unaoupenda. Ahmad.
Jee ni uzuri ulioje wa amali hii? Lakini kwa
masikitiko makubwa wengi miongoni mwa
walioolewa inatushinda, nayo ni kutokana
na njama za iblis na majeshi yake kututaka
tusiwe miongoni mwa watakaofaulu kesho
akhera. Pamoja na kuwa mume amepewa
amri juu ya mkewe ya kuwa ni mwenye
kusikilizwa na kutiiwa, Uislamu umeweka
mipaka katika hilo kwani Allah amesema:
Na ukiwat'ii wengi katika hawa waliomo
duniani watakupoteza na Njia ya Mwenyezi
Mungu. Hawa hawafuati ila dhana tu, na
hawakuwa ila ni wenye kusema uwongo tu.
[al-An-aam (6): 116].

Pia katika hili amesema Mtume (swalla


Allahu alaihi wa sallam): Hakuna kumtii
kiumbe katika kumuasi Muumbaji. Ahmad.
Hivyo ewe dada wa Kiislamu pupia katika
ibada hii kwa nia ya kuidumisha ndoa yako
na kupata pepo, na wala usiwasikilize
mashetani wa kijini au wa kibinaadamu pale
watakapo kuamrisha kwenda kinyume na
maamrisho mema ya mumeo kwani hakika
utakapokufa hali yakuwa mumeo yupo radhi
nawe basi pepo itakua karibu nawe in shaa
Allah.
ii.

Kujipamba kwa ajili yake

Hakika dini yetu ni nzuri na imesisitiza uzuri


katika kila nyanja. Kwani hakika Mola wetu
ni mzuri na anapenda vilivyo vizuri. Na
uzuri kulingana na dini yetu hauangaliwi
kwa mujibu wa sura wala maumbile, bali
hupimwa kwa moyo na matendo yetu kwa
ujumla. Binaadamu tumeumbwa katika
umbile la kupenda vilivyo vizuri na ndio
maana hata katika ibada Allah (subhanahu
wa taala) hupenda mja wake akifanya ibada
aifanye kwa uzuri. Katika hili la kujipamba
Muislam amesisitiziwa kujipamba na
kujipendezesha na ndio maana Mtume
(swalla Allahu alaihi wa sallam) nae akiwa
kama mfano uliobora, alikua akipenda kuvaa
vizuri na kunukia. Hili ni msisitizo kwetu
Waislamu wanaume kwa wanawake ya
kuwa Muislam anatakiwa kuwa ni mtu
mtanashati akiwa nje na ndani ya nyumba
yake.

11

Ama tukija kwa wanawake na ndio msingi


wa mada yetu, hutakiwa kujipamba lakini
kwa mipaka. Nikimaanisha anatakiwa
kujipamba mapambo yanayoendana na
sheria na kuyadhihirisha kwa mahrim zake
tu, nao ni wale wasiopasa kumuoa kama
baba, kaka, babu, mjomba n.k. Ifuatayo ni
hadithi
inayomuhimiza
mwanamke
kujipendezesha kwa ajili ya mumewe.
Amesema Mtume (swalla Allahu alaihi wa

Uislam umekemea vikali zinaa na vile vile


umeweka
makemeo
makali
khaswa
mwanamke ambaye hujizuilia na mumewe
bila ya sababu yoyote ya msingi ya kisheria.
Amesema Mtume (swalla Allahu alaihi wa
sallam): Atakapomuita mume mkewe
kwenye kitanda chake (kwa ajili ya tendo la
ndoa) halafu asimuendee, mume akalala hali
ya kuwa amemkasirikia malaika humlaani
mpaka kupambazuke. Bukhari na Muslim.

sallam): Mwanamke Bora ni yule ambae


ukimtizama anakufurahisha ... Tabrani.

Nadhani hadithi hii inatutosha kuwa ni

Ina maana mke mbaya ni yule


asiyejipendezesha kwa ajili ya mumewe,
bali hujipendezesha kwa ajili ya wengine
ambao ni haram kwake hata kuona
mapambo yake, na jambo hili ndio miongoni
mwa sababu zinazoporomosha ndoa nyingi
kwani mume karibu muda wote humuona
mkewe katika hali isiyo mvutia jambo
ambalo huondoa mvuto na mahaba katika
moyo wa mume na hatimae mume huenda
nje kwenye haram kutuliza jicho lake.
iii.

Asikatae Wito wa Mumewe

Kama tunavyofahamu kuwa mke anatakiwa


kuwa ni tulizo la macho na moyo wa
mumewe na pia mume. Khaswa katika dunia
iliyojaa machafuko ya kila aina ukiachana
na maradhi yanayozuka kila kukicha. Kwa
kuzingatia hili mke anatakiwa ajitahidi kadri
ya uwezo wake kumtuliza mumewe kwani
asipofanya hivyo madhara huwaangukia
wote.

sababu ya kutokataa wito wa waume zetu


kama kweli tunamuogopa Allah (subhanahu
wa taala).
iv.

Asimuombe talaka

Kwenye ndoa mke na mume lazima kila


mmoja awe na jitihada katika kuilinda ndoa
yake. Kwa sababu ndoa yoyote huwa haikosi
migongano ila muhimu ni subra na hawi na
subra ila mwanandoa alietimia sifa za
uumini, kwani hakika Muumini huitakidi
kuwa mwenye kupatwa na matatizo ndio
hupandishwa darja na hulipwa malipo bila
ya hisabu na kwa uchaMungu ndio Allah
(subhanahu wa taala) huleta faraja.
Kinyume na hivyo mwanandoa hushindwa
na kudai talaka jambo ambalo ni lenye
kuchukiza mbele ya Allah (subhanahu wa
taala) na lenye kufurahisha sana mbele ya
iblisi (laanatu Allahi Alayhi). Amesema
Mtume (swalla Allahu alaihi wa sallam)
katika kumzungumzia mwanamke mwenye
kupenda kudai talaka bila ya sababu
inayokubalika kisheria: Mwanamke yoyote

12

anaemuomba mumewe talaka bila ya tatizo


lolote (la kisheria) basi ni haramu kwake
harufu ya pepo. Ahmad.

wanao jilinda hata katika siri kwa kuwa


Mwenyezi Mungu ameamrisha wajilinde ...
[an-Nisaa (4): 34].

Ni khasara ilioje kuikosa hata harufu ya


pepo wakati harufu yake huipata kutoka
Masafa ya mbali kwa watakao iingia. Allah
atujalie miongoni mwao. AMIIN.

Tujitahidini sana kina mama wenzangu


kuliacha hili kwa sababu kumtolea mumeo
aibu ni sawa na kujifedhehesha mwenyewe
na mwisho tutambue ya kuwa mwenye
kumsitiri Muislamu mwenzake hapa duniani
Allah humsitiri yeye duniani na kesho

v.

Kutunza siri za mumewe

Mke na mume wakishaoana wanatakiwa


kuwa kama mwili mmoja, yani kila mmoja
aitunze aibu ya mwenziwe iwe ni kama yake
na sio kuitangaza kwa watu wa nje sawa
sawa ni kwa jamaa wa karibu au marafiki
wa mbali. Dini yetu imekataza mke
kumtolea mumewe siri zake na mume kutoa
siri za mkewe. Amesema Mtume (swalla
Allahu alaihi wa sallam): Hakika katika
watu wenye nafasi mbaya siku ya Qiyama ni
mwanamme anaemuendea mkewe au mke
anaeendewa na mumewe halafu akaeneza
siri za mwenziwe. Bukhary.
Na katika Qur'an Allah (subhanahu wa
taala) amewasifu wanawake wema kuwa ni
wale wenye kuhifadhi siri: ... Basi
wanawake wema ni wale wenye kut'ii na

Akhera na kinyume chake ukimfedhehesha


nduguyo duniani Allah atakufedhehesha
duniani na kesho akhera. Jichunguze
mwenyewe aibu zako kabla ya kuzitoa aibu
za mwenzako kama hutaki aibu zako
zijulikane usijaribu kuzitoa za wenzako
kwani ni lazima na zako zitatoka kama sio
karibu hata baadae kama hauko hai hata
ukifa.
Majukumu ya mke kwa mumewe yapo
mengi hayo ni kidogo niliojaliwa
kuyaelezea.
Kwa taufiq ya Allah tutaendelea na mada hii
katika toleo lijalo la jarida letu. Natarajia
tumefaidika nayo na tutaanza kuyafanyia
kazi in shaa Allah.

13

Alikua ni mwembamba wa mwili, mkubwa


wa akili. Aliyejawa na imani ya kufanya
mema na khofu ya kuingia katika maasi.
Alikua ni katika wachaMungu na wenye
tabia nzuri. Alikua mweusi wa sura,
mweupe wa moyo. Alikua mweusi kutokana
na asili yake ya uhabeshi, weusi wa rangi
yake haukumfanya awe dhalili, kwani
mtukufu mbele ya Allah ni yule ailyekuwa
mchaMungu. Allah anasema: ... Hakika
aliye mbora wenu mbele ya Allah ni yule
anaemcha zaidi Allah miongoni mwenu ...
[al-Hujuraati (49): 13]
NASABA YAKE
Anaitwa Said bin Jubayr bin Haashim AlAsady, Al-Kuufy, amenasibishwa na kabila
la bani-Asad ingawa hakuwa muarabu wala
hakuwa katika kabila la bani-Asad, ila
alinasibishwa nalo kwa sababu alikuwa ni
muachwa huru wa kabila hilo, alinunuliwa
kama mtumwa na baadae akaachwa huru.
KUZALIWA KWAKE
Wametofautiana

wana

tareikh

juu

KUSOMA KWAKE
Said bin Jubeyr (Rahimahu Allah) alijua
utukufu wa duniani upo kwenye kusoma, na
utukufu wa Akhera upo kwenye ibada, hivyo
akaamua kushikamana na vitu viwili hivi
mpaka mwisho wa uhai wake, elimu na
ibada. Ikawa haonekani isipokua yuko
katika moja ya hali mbili hizi, ima anasoma
na kusomesha au yuko katika ibada.
Alisoma kwa wengi katika maswahaba
akiwemo Abu-Muusa Al-Ash-ary, AbuHurayra, Abu-Said al-khudry, Abdullah bin
Umar, Bibi Aisha na wengineo katika
maswahaba (radhia Allahu anhum ajmain),
lakini zaidi alishikamana na kujilazimisha na
mwanachuoni wa umma huu na mfasiri wa
Qur-an Abdullah bin Abbaas (Radhia Allahu
anhu), akasoma kwake Qur-an na tafsiri, na
pia hadithi na lugha ya Kiarabu na
mengineyo. Mpaka akawa anamruhusu
kutoa fatwa kwa watu na alipokua akijiwa
na watu kutoka Kufah kutaka fatwa,
anawauliza jee hayupo kwenu Said bin
Jubeyr?

ya

kuzaliwa kwake, wako waliosema kuwa


amezaliwa mwaka wa 45 Hijria, wengine 46
Hijria na wengine mwaka wa 38 Hijria,
kutokana na kifo chake kilichotokea mwaka
wa 95 Hijria na kua alikufa akiwa na miaka
57 au 59. Wallahu Alam. Alizaliwa katika
mji wa Kuufah na ikapelekea kupewa laqab
ya Al-Kuufy.

KISA CHAKE NA HAJJAJ BIN YUUSUF


Jina la Hajjaaj si jina geni katika historia ya
Kiislamu baada ya Mtume (swalla Allahu
alayhi wassalam), amefanya aliyoyafanya na
si mada yetu ya leo kumhusu Hajjaaj. Ila
tutatizama miongoni mwa aliyoyafanya
ambayo yanamgusa Said Bin Jubeyr ambae

14

ndiye mlengwa wa mada yetu ya leo. Hajjaj


alikua ni mtawala wa Iraq, uongozi aliopewa
na Bani-Umayyah ambao ndio walikua
wanashikilia hatamu za uongozi kwa wakati
huo. Kutokana na fitna iliyokuweko wakati
huo kwa Waislamu, baadhi ya Waislamu
wakaupinga utawala wa Bani-Umayyah na
Hajjaaj akapigana na kila anayeupinga
utawala wa Bani Umayyah au kumpinga
yeye. Aliuwa wengi na kuwahiarisha baina
ya kujiita makafiri, kutokana na kitendo
chao cha kumpinga khalifa au wauwawe.
Wapo walouwawa na wapo walokubali
kuitwa makafiri hivyo wakasilimu upya, na
kumuunga mkono khalifa ili kujinusuru
maisha yao kutokana na kiongozi huyu
muuwaji. Baada ya kuona hayo Said bin
Jubeyr ambae alikua yuko Kuufah, sehemu
ambayo ndio aliyokuweko Hajjaaj akaamua
kuelekea Makka, kunusuru maisha yake
kwani alikua hana njia zaidi ya kuuwawa au
kuukubali utawala wa dhulma. Said bin
Jubeyr aliishi muda mrefu Makka kwa
kujificha ficha, huku akiendelea na darsa
zake, hadi Makka ilipopata mtawala mpya
wa Bani-Ummayyah ambae alikua dhalimu
akijulikana kwa jina la Khalid bin Abdallah
Al-Qusry. Alipoingia madarakani alimtafuta
Said bin Jubeyr, na alipomuona, aliamrisha
wanajeshi wampeleke kwa Hajjaj bin
Yuusuf. Wakati yuko njiani kupelekwa kwa
Hajjaaj (machinjioni) alisikika akiwaambia
wanafunzi wake, tulikaa usiku mmoja mimi
na marafiki zangu wawili tukamuomba
Allah tuliyomuomba, na tukamuomba
atuandikie shahada, wenzangu tayari

wameshaipata na mimi ndio naelekea.


Alipelekwa kwa Hajjaaj hali ya kua mtulivu
wa nafsi na mwenye shauku ya kukutana na
Mola wake.
KUULIWA KWAKE
Aliingia Said bin Jubeyr kwa Hajjaaj huku
akijua kua damu yake iko ukingoni
kunywiwa na Hajjaj. Alipoingia Hajjaaj
alimuuliza maswali mengi na mazungumzo
yao yalikua kama ifuatavyo:
Hajjaaj: Jina lako nani?
Said : Jina langu ni Said Bin Jubeyr (lenye
maana mwema, alieungwa).
Hajjaaj: Bali wewe ni muovu uliyevunjika
vunjika.
Said:

Mama yangu alikua akinijua zaidi

kuliko wewe ndio maana akanipa jina hilo.


Hajjaaj: Unamzungumziaje Muhammad?
Said: Unamkusudia Muhammad bin
Abdillah Mtume wa Allah (rehma na amani
ziwe juu yake)?
Hajjaaj: Ndio.
Said: Ni bwana wa watoto wa Adam, mbora
wa viumbe, mbashiriaji na muonyaji,
amebeba ujumbe na akafikisha amana na
akaunasihi Umma.
Hajjaaj: Unamzungumziaje Abubakar?
Said: Yeye ni Swiddyq, khalifa wa Mtume
(swalla
Allahu
alayhi
wassallam),

15

ameondoka akiwa mwenye kushukuriwa, na


ameishi akiwa mwenye kufurahiwa, amepita
katika muongozo wa Mtume (swalla Allahu
alayhi wasallam), hakubadilisha wala
kugeuza chochote.
Hajjaaj: Unamzungumziaje Umar?
Said: Yeye ni Faaruq, ambae Allah
ametofautisha Haki na Baatil kupitia kwake,
alikuwa ni katika vipenzi vya Allah na
Mtume wake, na amepita katika muongozo
wa waliomtangulia, akaishi akiwa mwenye
kushukuriwa na akafa akiwa mwenye
kuuliwa (shahidi).

Said: Anaeyajua hayo ni yule anaejua siri


zao na minongono yao.
Hajjaaj: Basi unanizungumziaje mimi?
Said: Unajijua zaidi nafsi yako kuliko
ninavyokujua.
Hajjaaj: Nataka unavyonijua wewe?
Said: Mimi ninavyokujua wewe ni kuwa
unaenda kinyume na kitabu cha Allah,
unafanya lile unalolipenda kwa matamanio
yako, na hayo yatakuangamiza na
kukupeleka motoni.
Hajjaj: Nitakuua.

Hajjaaj: Unamzungumziaje Uthmaan?


Said: Alikua muandaaji wa vita vilivyokuwa
vigumu (taabuk), aliyechimba kisima cha
Ruumah, aliyejinunulia nyumba peponi.
Mkwe wa Mtume (swalla Allahu alayhi
wasallam). Na ameuliwa kwa dhulma.
Hajjaaj: Unamzungumziaje Aliy?
Said: Ni mtoto wa Ami yake Mtume, wa
mwanzo kusilimu akiwa na umri mdogo,
amemuoa bibi Faatimaah na ni baba wa
Hassan na Hussein, mabwana wa vijana wa
peponi.
Hajjaaj: Ni nani katika makhlifa wa BaniUmayyah aliyekupendezesha zaidi?
Said: Aliemridhisha zaidi Mola wake.
Hajjaaj: Ni nani aliyemridhisha zaidi Mola
wake?

Said: Itakua umenifisidia dunia yangu na


mimi nimekufisidia Akhera yako.
Hajjaaj: Chagua namna gani nikuue.
Said: Chagua wewe kifo cha nafsi yako,
kwani hutoniua kifo chochote isipokua nawe
Allah atakuua kifo hicho hicho Akhera.
Hajjaaj: Hutaki msamaha?
Said : Ikiwa kutoka kwa Allah basi nautaka,
na kama kutoka kwako basi siutaki.
Akakasirika Hajjaaj na akaamrisha kukatwa
kichwa chake, na akamuona Said bin Jubeyr
anacheka, (Hajjaaj) akamuuliza kipi
kinachokuchekesha? Akasema (Said bin
Jubair): Unanishangaza ujeuri wako kwa
Allah na upole wake kwako. Akaelekezwa
kibla ili auwawe, akasoma aya ya Allah
Hakika mimi nimeuelekeza uso wangu
sawa sawa kwa aliye ziumba mbingu na

16

ardhi, wala mimi si miongoni


washirikina. [al-An-aam (6): 79].

mwa

Hajjaaj: Mgeuzeni kutoka kiblani.


Said:
Akasoma:
...
Na
popote
mtakapoelekea mtamkuta Allah ... [alBaqarah (2): 115].
Hajjaaj: Muekeni kufudifudi.
Said: Kutoka na udongo tumekuumbeni, na
huko tutakurejesheni na humo tutakutoeni
kwa mara ya pili. [Twaha (20): 55].
Hajjaaj : Mchinjeni uyo adui wa Allah
anayejidai kusoma aya za Qur-an.
Said: Ewe Mola usimsalitishe mtu yoyote
baada yangu kwa Hajjaaj. Na akauwawa hali
ya kuwa ulimi wake unamtaja Allaah.
Subhanallah ni wema gani aliouonyesha
Said bin Jubeyr, kiasi ambacho unawaombea
wenzako wasiuliwe tena na Hajjaj na yeye
ndiye awe mtu wa mwisho kuuwawa. Na

Allah aliijibu dua yake kwani haukupita


muda ila Hajjaj alisumbuliwa na maradhi na
alikua hawezi kulala kwani kila anapolala
anaota anajiwa na Said Bin Jubeyr, hadi kifo
kilipomkuta. Walimuota watu Hajjaaj
wakamuuliza, nini alichokulipa Allah
kutokana na nafsi ulizoziua? Akajibu: Kwa
kila nafsi moja ameniua mara moja, lakini
kwa nafsi ya Said bin Jubeyr ameniua mara
70.
Amekufa Said Bin Jubeyr mwezi 11
Ramadhan mwaka wa 95 Hijria sawa na
mwaka 714 Miladiyya na wako waliosema
amekufa Shaaban (Wallahu Alam).
Amekufa akiwa na umri wa miaka 59, na
kama alivyosema Imam Ahmad amekufa na
hakuna mtu katika ardhi isipokua alikua
akiihitaaji elimu yake (Rahimahu Allahu).
Allah atujaalie tuwe ni wenye kujifunza
mazuri
kutoka
kwa
hawa
wema
waliotangulia. Aamin.

17

Kila sifa njema zinamstahikia Allah


(subhanahu wa taala) Muumba wa kila
kilichomo katika ulimwengu huu. Swala na
salamu zimuendee Mtume wetu Muhammad
(swalla Allahu alaihi wa sallam).
Katika ulimwengu wetu wa sasa, ulimwengu
ambao unaitwa wa Sayansi na Teknolojia,
kwa hakika kuna kila sababu ya kumfanya
Muislamu alisahau lengo la kuumbwa
kwake hapa duniani. Hatuwezi kuzuia
mabadiliko haya yasitokee. Ila lililokuwa la
wajibu
kwetu
ni
kuhimizana
na
kukumbushana juu ya sharia za Allah
(subhanahu wa taala) na vipi mja akae
katika njia iliyosalimika. Akiwa katika njia
hiyo kiukweli kabisa, basi Allah (subhanahu
wa taala) atamridhia mja wake duniani na
kesho akhera.

Wanaiita mitandao ya kijamii, ila mimi


nitasema mitandao inayoharibu Jamii
ikiwemo facebook, tweeter, instagram,
whatsapp na mengineyo. Faida imekuwa
kwa wachache wenye kumuogopa Allah na
khasara ni kubwa mno. Jee unajua kuwa

mitandao hii ishasababisha ndoa za watu


kuvunjika? Jee unajua ndoa zinakosa utulivu
kwa sababu ya mambo haya? Jee ni yepi
yanayofanywa kwenye mitandao ya kijamii?
Namuomba Allah anijaalie tawfiq na iwe ni
sababu kwa kila atakayesoma makala hii
aweze kujirekebisha pale alipokosea na
kumuomba msamaha Allah (subhanahu wa
taala).
Kushughulishwa na mitandao hii na
kumdharau mke au mume au kusahau
majukumu ya lazima
Katika jambo muhimu analolihitaji mke au
mume ni kujaliwa na mwenzake. Endapo
ataoona mwenzake hamjali huwa hana
furaha ndani ya ndoa yake na lazima
itasababisha ugomvi mara kwa mara.
Tuchukulie mfano mume ametoka tokea
asubuhi kutafuta rizki. Anarudi usiku hana
jambo la lazima bali anakaa kwenye
mitandao hii na kuanza kuchat. Mwenzake
amemsubiri kwa hamu ila yeye amekuwa na
hamu na marafiki wake wa mitandaoni na
kumdharau mke wake. Jee hivi ni kweli
ndoa hii itakuwa na furaha? Kama kuna la
lazima basi mwambie mwenzako na ufanye
haraka kumaliza ili umpatie fursa mke wako
nae mufurahi wote.
Hebu tumuangalie mke nae. Mumewe
ametoka anaanza kuchat kutwa nzima.

18

Anayozungumza na wenzake anayajua


mwenyewe iwe ya kweli, ya uongo, ya
kuzua au ya fitina. Ushakaribia wakati wa
kuandaa chakula anaingia jikoni na kuripua
kupika. Akimaliza anarudi kwenye simu
yake. Au atasafisha nyumba yake haraka
haraka ili awahi kurudi kwenye simu yake
aendelee kuchat. Ewe dada wa Kiislamu jee
hujui kuwa mume anahitaji aone
anathaminiwa? Kwa nini usitumie muda
wako kumpikia chakula kizuri na kitamu?
Chakula kizuri na kitamu kitamsahaulisha
machofu ya kazi. Kwa nini wakati wa kula
usile nae wewe umeshika simu yako? Jee
huoni aibu nyumba yako kutokuwa safi kwa
sababu ya simu yako?
Enyi wanandoa ikiwa kukesha kwenye
mitandao ya kijamii ndio ibada kwenu hivi
hamuwaonei huruma watoto wenu? Wakati

hajatumiwa na mke wake au mume wake.


Tena huwa ni ujumbe wa mapenzi
unaoashiria kuwa mke au mume ni mwenye
kutoka nje ya ndoa yake. Mume au mke
akiwa anazungumza na mtu husema hajaoa
au hajaolewa lengo atimize lile analolitaka.
Jee kweli utulivu ndani ya ndoa utapatikana?
Inapotokea kufumwa na ujumbe huo wa
kimapenzi kwa wanandoa, wako wengine
hujifanya mafundi wa kusema uongo na
wengine huishia kutoa maneno na kukosa
jibu. Au mwanamme kujifanya yeye ndio
bwana hatakiwi kuhojiwa. Na hata wengine
huishia kupiga wake zao kwa sababu tu
atamwambia amemchunguza na kumzulia.
Hivi mke asiwe na wivu na mume wake?

watu

Kwa nini mtu ukose uaminifu kwa


mwanandoa
mwenzako?
Kwa
nini
mutumiane ujumbe wa kimapenzi na mtu
asiyekuwa mume wako au mke wako? Hivi
unadhani hesabu yako hutaikuta kwa Allah?
Tunakwenda wapi enyi umma wa Kiislamu?
Kwa nini tunazifisidi ndoa zetu kwa kufuata
matamanio ya nafsi zetu tu?

Tembelea inbox za facebook na whatsapp za


wanandoa jee kweli zitasalimika na ujumbe
wa kimapenzi? Ujumbe ambao mtu

Ewe uliyeoa au kuolewa acha tabia za


kutoka nje ya ndoa yako. Acha tabia za
kuchat mambo ya kimapenzi na asiyekuwa
halali kwako. Umeaminiwa basi na wewe
jiaminishe. Kwani hakika ni mnafik yule
anayeaminiwa akavunja uaminifu. Tambua
kuwa Allah (subhanahu wa taala) anakuona
na tambua ya kuwa hakuna la siri kwake na
ipo siku siri hiyo itatoka tena itakuwa ni siku
ya majuto makubwa na fedheha. Na mwisho

wa kuzungumza nao na kucheza nao hamna


ila wakati wa kuchat yasiyokuwa na maana
mnao? Tujirekebisheni tabia hizi kwani
zitaharibu ndoa zetu.
Mazungumzo
wengine

ya

kimapenzi

na

19

wake kuingia katika moto. Allah atuhifadhi.


Allah (subhanahu wa taala) anasema: Siku
zitakapo dhihirishwa siri. [at-Twaariq (86):
9].
Pia napenda kutoa nasaha kwa wanandoa
kuwa, unapokuta ujumbe ambao unaashiria
machafu kwa mume wako au mke wako,
basi usikimbilie kutoa maneno au kufanya
yasiyostahiki kwani huweza kuwa ni jambo

Achiliambali kusambaza, kwa nini ujirikodi


video zako za ndani? Kwa nini uzisambaze
picha zako za ndani? Munapata faida gani?
Kubwa ni kudhalilishana na kuvuana nguo
mbele za watu. Na lililokuwa baya zaidi ni
kumkera Allah (subhanahu wa taala).
Amesema Rasoul (swalla Allahu alayhi wa
sallam) katika hadithi aliyoisimulia Said
Khudry kwamba: Hakika katika watu

lililopangwa na kuzuliwa. Kwanza uliza kwa


hekima na uwe na subra, yawezekana ni

wenye nafasi mbaya siku ya Qiyama ni


mwanamme anaemuendea mkewe au mke

fitna tu imeundwa ili kukuharibieni ndoa


yenu. Na haya yapo tayari yameshavunja
ndoa za watu wengi. Allah (subhanahu wa
taala) anasema Enyi mlio amini! Akikujieni
mpotovu na khabari yoyote, ichunguzeni,
msije mkawasibu watu kwa kuto jua, na
mkawa tena wenye kujuta kwa mliyo
yatenda. [al-Hujuraat (49): 6].

anaeendewa na mumewe halafu akazieneza


siri za mwenziwe. Bukhary.

Chunguza kwanza ili baadae usije kujuta


kwa kumuingiza mwenzako kwenye makosa
yasiyokuwa yake.
Kusambaza picha zao wakati wakiwa
chumbani kwenye mitandao hii
Inawezekana ukashangaa na kujiuliza kweli
suala hili lipo? Kwanza nielezee mtindo
uliojitokeza siku hizi wa watu kujirikodi
video wakati wakifanya zinaa. Au kupigana
picha za mmoja akiwa hana nguo iwe kwa
ridhaa au bila ya ridhaa. Na kwa masikitiko
makubwa, wanandoa nao wameingia katika
tabia hizi chafu.

Jua
ewe
ndugu
yagu
Muislamu,
unapojirikodi video au picha huwa unatoa
siri zako na kuelezea ni yepi unayoyafanya
ndani. Jua makaazi yako ni mabaya siku ya
Qiyama ikiwa hutotubia kwa Allah
(subhanahu wa taala) tawba ya kweli.
Mke au mume anayesambaza video au picha
za haramu na huku anacheka akiona
anawafurahisha wenzake na kujisifia, jee
amesahau kauli ya Allah (subhanahu wa
taala) isemayo: Kwa hakika wale wanao
penda uenee uchafu kwa walio amini,
watapata adhabu chungu katika dunia na
Akhera. Na Mwenyezi Mungu anajua na
nyinyi hamjui. [an-Nnuur (24): 19].
Jee hajiulizi akifa leo watu wataangalia
video ile au picha ile kwa miaka mingapi na
ni wangapi wataangalia? Jee anajua na yeye
anapata
dhambi
kwani
alichangia
kusambaza uchafu? Allah (subhanahu wa
taala) anasema: "Na hapana shaka wataibeba

20

mizigo yao na mizigo mingine pamoja na


mizigo yao. Na kwa yakini wataulizwa Siku
ya Qiyama juu ya waliyo kuwa wakiyazua."
[al-Ankabut (29): 13].
Usiri wa kuficha password ya kwenye
mitandao na simu
Katika hali ya kustajaabisha mke na mume
kila mmoja simu yake ina password na
mwenzake haijui na hataki aijue.
Inawezekana mtu akasema kuna mambo
mengine ya siri zaidi sitaki ajue. Leo
nakujibu hakuna siri katika mitandao wala
katika simu. Jee unajua kuwa kuna program
tu zinawekwa kwenye simu na kila
unachokipata kwenye simu yako yule
alokuwekea anakipata? Jee mtu akiulizia
kwa watu wa mitandao ataweza kupata
ukweli? Jee hujui mazungumzo ya simu ya
marais na viongozi yanavujishwa? Nakupa
mifano kukwambia tu hakuna siri katika
mitandao.
Ili usimtie shaka mwanandoa mwenzako na
ujiamini katika ndoa yako basi usiogope
kutoa password yako. Hii itamtuliza
mwenzako moyo wake na kuondosha shaka
juu yako. Ila ikiwa simu ina password,
facebook yako password, ukiingia ndani
simu unazima, sio kwa sababu ya kutaka
kupumzika bali kwa kukimbia fedheha. Vipi
utaitunza ndoa yako?
Kuweka picha zao binafsi zisizofaa katika
mitandao

Mwanamme nae anaamua kupiga picha


akiwa amevaa bukta tu au yuko tumbo wazi
anaweka katika mitandao. Jua unaleta fitna
kwa wanawake wengine. Kutamani ni
maumbile ya wanaadamu wote. Jua sehemu
hizo hazidhihirishwi ila kwa mke wako tu na
sio wengine wasiokuwa halali kwako.
Mwanamke amepiga picha yake akiwa
amejipamba vizuri. Anachukua picha ile na
kuiweka katika facebook au whatsapp ili
awaonyeshe watu wengine. Tena picha
nyengine huonyesha ni jinsi gani
alivyoumbwa na Allah (subhanahu wa taala)
kwa sababu amevaa nguo yenye kubana. Jee
unajua ewe dada wa Kiislamu kuwa uzuri
huo hutakiwi kuudhihirisha isipokuwa kwa
mume wako tu? Halafu unalaumu watu
hawana adabu wanakutongoza na wewe ni
mke wa mtu. Sasa kwa nini umeiweka? Yote
hayo yatakukuta kwa sababu umevunja
sheria Allah (subhanahu wa taala). Allah
anasema: "Ewe Nabii! Waambie wake zako,
na binti zako, na wake za Waumini
wajiteremshie nguo zao. Hivyo ni karibu
zaidi kuweza kutambulikana wasiudhiwe.
Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye
kusamehe, Mwenye kurehemu." [al-Ahzaab
(33): 59].
Allah (subhanahu wa taala) ameshasema
lengo la hijaab ni mtu asiudhiwe.
Ukiondosha sheria hii basi jua tayari
unakaribisha madhambi na maudhi kutoka
kwa watu. Ama hukmu ya kuweka picha
hiyo tayari ilishaelezwa katika toleo la
kwanza kabisa la jarida letu hili

21

(https://www.dropbox.com/s/kc7uyruai1wn7
91/TOLEO%20LA%20KWANZA.pdf?dl=0
).
Kwa hakika mada hii ni refu na ina mifano
mingi sana. Naomba niishie hapa na nitoe
nasaha zifuatazo: Matamanio ya nafsi zetu
yasituhadae hadi tukawa tayari kumuasi
Allah (subhanahu wa taala) na kuvunja ndoa
zetu, na tusipochunga matamanio yetu
yatatupeleka pabaya siku ya Qiyama.
Tumuogopeni Allah (subhanahu wa taala).
Hebu kaa na utafakari ni muda gani
unautupa katika mitandao hii kwa kuchat?
Jee muda huo ungeweka maalum kwa ajili
ya mola wako na mume wako au mke wako

na hata watoto wako ungepata faida kiasi


gani? Tambua unatumia neema ya wakati.
Allah (subhanahu wa taala) atakuja
kukuuliza juu ya neema hiyo.
Ewe mwanandoa muogope mola wako na
itunze ndoa yako. Usiwe tayari kuiharibu
kwa sababu ya mitandao hii michafu. Dunia
ni hadaa na hesabu zetu zote tutazikuta
mbele ya Allah (subhanahu wa taala).
Na tuikumbuke aya ya Allah (subhanahu wa
taala) isemayo: Na iogopeni Siku ambayo
mtarudishwa kwa Mwenyezi Mungu, kisha
kila nafsi italipwa ilicho chuma. Nao
hawatadhulumiwa. [al-Baqara (2) : 281].

22

Kila sifa njema zinamstahikia Allah


(subhanahu
wa
taala),
Mola
wa
walimwengu wote. Swala na salamu
zimfikie Mtume wetu Muhammad (swalla
Allahu alaihi wa sallam).
Ndugu wa Kiislamu, Allah (subhanahu wa
taala) ametuwekea sherehe maalum za Eid
kila baada ya kumalizika kwa ibada ya
mfungo wa Ramadhaan na ibada ya Hijjah.
Watu wa Madina walikuwa wakisherehekea
Eid zao, lakini Mtume (swalla Allahu alaihi
wa sallam) aliwataka waachane nazo na
badala yake washerehekee Eid mbili tu
ambazo ni Eid al-Adhwha na Eid al-Fitri.
Kama kawaida ya sherehe yoyote ile huwa
kuna furaha na watu hujiburudisha kwa vitu
mbali mbali ikiwemo vyakula na vinywaji.
Ni wajibu wa kila Muislamu kujichunga
kwanza juu ya suala zima la kutofanya israfu
katika kusherehekea Eid hizi. Pia ni sunnah
kufanya yafuatayo katika siku ya Eid ili
kuzidi kupata faida ya ibada tulizozifanya
ima katika mfungo wa Ramadhaan au
Hijjah.
Kukoga kabla ya kwenda kuswali swala ya
Eid
Ni mustahab (inapendeza) kukoga kabla ya
kwenda kuswali swala ya Eid na kujitia
manukato mazuri kwa wanaume, kwani hivi
ndivyo walivyokuwa wakifanya watu wema
waliotangulia. Imesimuliwa hadithi sahihi

katika Al-Muwatta na kwengineko kuwa


Abd-Allah ibn Omar alikuwa akikoga
asubuhi ya Fitri kabla ya kwenda sehemu ya
kuswali.
Kula kabla ya kwenda kuswali katika Eid
al-Fitri na baada ya kuswali katika Eid alAdhwha

Ni katika sunnah kula tende kwa idadi ya


witri kabla ya kwenda kuswali Eid al-Fitri
au chochote kile cha halali ikiwa
itakosekana tende, kwani huo ndio ulikuwa
utaratibu wa Mtume wetu (swalla Allahu
alaihi wa sallam) kama ilivyoripotiwa na
Imam Bukhari kutoka kwa Anass ibn Malik
ambae amesema kuwa Mtume wa Allah
(swalla Allahu alaihi wa sallam) alikuwa
hatoki asubuhi kwenda kuswali Eid al-Fitri
mpaka ale tende ... ambazo alizila kwa idadi
ya witri.
Ama katika Eid al-Adhwha ni vyema mtu
kutokula mpaka baada ya kuswali, ili aje ale
katika kichinjo alichokichinja kwa ajili ya

23

Allah, lakini kwa asiyechinja hakuna ubaya


kwake kula kabla ya kwenda kuswali.
Kuleta takbira

Kama ilivyosimuliwa katika Musannaf wa


Ibn Abi Shaibah kwa sanadi sahihi kutoka
kwa Ibn Masoud (radhi za Allah ziwe juu
yake) kwamba alikuwa akisoma takbira
katika siku za Tashriq: Allaahu akbar,
Allaahu akbar, laa ilaaha ill-Allaah, wa
Allaahu akbar, Allaah akbar, wa Lillaah ilhamd (Allaah ni Mkubwa, Allaah ni
Mkubwa,
Hapana
Mola
anayepasa
kuabudiwa kwa Haki Ila Allaah, Allaah ni

Hii ni katika sunnah kubwa za siku ya Eid


kwani Allah (subhanahu wa taala) anasema:
... Mwenyezi Mungu anakutakieni yaliyo
mepesi wala hakutakieni yaliyo mazito, na
mtimize hiyo hisabu, na mumtukuze
Mwenyezi Mungu kwa kuwa amekuongoeni
ili mpate kushukuru. [al-Baqara (2): 185].
Takbira huanza kutolewa pale tu mtu
anapotoka nyumbani kwake kuelekea
sehemu ya kuswalia. Na ni sunnah kwa
wanaume kuileta kwa sauti kubwa na kwa
wanawake kwa sauti ndogo isiyosikika.
Imesimuliwa kwamba al-Walid ibn Muslim
alisema: Nilimuuliza al-Awzaai na Malik
ibn Anas kuhusiana na kuleta takbira kwa

Mkubwa, Allaah ni Mkubwa Na Shukrani


Zote ni za Allaah).
Imesimuliwa pia na Abi Shaibah katika
sehemu nyengine kwa sanad sawa ila tamko
la Allaahu akbar limejirejea mara tatu
(badala ya mara mbili).
Ama ile takbira refu tuliyoizoea wengi:

sauti kubwa katika Eid mbili. Wakasema;


Ndio, Abd-Allah ibn Omar alikuwa
akiisema kwa sauti kubwa katika Eid al-Fitri
mpaka anapokuja Imam (kuswalisha).

, , , ,

, ,

Katika Eid al-Fitri takbira huanza baada ya


kuonekanwa mwezi muandamo na humaliza
baada kumalizika kwa swala ya Eid, ama
katika Eid al-Adhwha takbira huanza mwezi
tisa Dhulhijjah mpaka laasiri ya siku ya
mwisho ya Tashriq.

Na maneno ya takbira ni:

, , ,
.

, ,
,

24

Kwa vile haijathibiti namna maalum


aliyoifundisha Mtume (swalla Allahu alaihi
wa sallam), ni rai yetu kuwa hakuna tatizo
kuisoma takbira hii, na Allah Anajua zaidi.
Kupongezana
Pia ni katika sunnah kupongezana katika
siku za Eid kwa kusema Taqabbala Allaah
minna wa minkum (Allah azikubali (amali
nzuri) kutoka kwetu na kwako) au Eid
mubaarak au kwa namna nyenginezo
zinazokubalika.
Imesimuliwa kwamba Jubayr ibn Nufayr
amesema: Wakati maswahaba wa Mtume
(swalla
Allahu
alaihi
wa
sallam)
wanapokutana katika siku ya Eid, walikuwa
wakisema kuambiana, Allah azikubali
(amali nzuri) kutoka kwetu na kwako.
Amesema Ibn Hajar sanad yake ni hasan.

ambayo ilitengenezwa kwa hariri na ilikuwa


ikiuzwa kwa bei ya takhfifu sokoni, aliileta
kwa Mtume (Swalla Allaahu alayhi wa
aalihi wa sallam) na akasema: "Ewe Mtume
nunua hii na uvae kwa ajili ya Eid na
watakapokuja wageni" Mtume (Swalla
Allaahu alayhi wa aalihi wa sallam)
akasema: "Hizi ni nguo za yule ambaye hana
sehemu akhera. Al-Bukhaariy.
Hadithi hii inaonyesha kuwa, katika kuvaa
vizuri huko ni lazima pia kuchunga mipaka
ya mavazi, yaani wanaume wasivae mavazi
ya kike na wanawake wasivae mavazi ya
kiume wala kusivaliwe mavazi ambayo
yanayoshabihiana na ya makafiri. Na kwa
vile wanaume wamekatazwa kuvaa hariri
ndio maana Mtume (swalla Allahu alaihi wa
sallam) akalikataa vazi lile aliloletewa.
Kuswali swala ya Eid

Kuvaa mavazi mazuri


Ni sunnah kuvaa mavazi mazuri na
kujipamba kwa wanaume wanapokwenda
kuswali Eid. Ama kwa wanawake
watakaokwenda kuswali Eid hawatakiwi
kujipamba wala kujitia mafuta mazuri kwani
hawatakiwi kuyafanya hayo kwa wasiokuwa
maharimu wao. Imesimuliwa na Jabir (radhi
za Allah ziwe juu yake) kwamba: Mtume
(swalla Allahu alaihi wa sallam) alikuwa na
jubba ambalo alilivaa katika Eid mbili na
siku ya Ijumaa. Sahih Ibn Khuzayma.
Pia Abd-Allaah bin Omar (radhi za Allah
ziwe juu yake) amesema: Omar alichagua
jubbah (nguo refu inayovaliwa juu ya kanzu)

Swala ya Eid ni katika sunnah muakkadah


(zilizokokotezwa), hivyo ni wajibu wa kila
Muislamu kuihuwisha sunnah hii na sio
kukimbilia kwenye kula tu asubuhi ya siku
ya Eid.

25

Na ni juu ya kila Muislamu kuhakikisha


kuwa ameshatoa zakatul Fitri kabla ya
kwenda kuswali Eid kwani anayetoa baada
ya swala huwa ametoa sadaka tu na sio
zakatul Fitri tena.

makaburi kutaibadilisha furaha hii na


kuifanya kuwa huzuni na huu si katika
utaratibu wa Mtume wetu Muhammad
(swalla Allahu alaihi wa sallam).

Kubadilisha njia ya sehemu ya kuswalia


Ni sunnah vile vile kuenda kwenye sehemu
ya kuswalia Eid kwa njia moja na kurudi
kwa kutumia njia nyengine. Jaabir bin AbdAllaah (radhi za Allah ziwe juu yake)
ameripoti kuwa: Mtume (Swalla Allaahu
alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa
akibadilisha njia siku ya Eid. al-Bukhari.
Ndugu wa Kiislamu hayo ni katika ya
sunnah tunayotakiwa kujihimu kuyafanya
katika siku ya Eid. Lakini kwa vile katika
jamii zetu kuna mambo mengi ambayo
hufanyika katika siku za sherehe hizi, ni
vyema kuwanasihi ndugu zetu khasa wazee
na walezi wa familia kuwa, wazingatie sana
nyenendo za vijana wao, kwani wengi katika
vijana huzigeuza sherehe hizi kuwa ni siku
walizoachiwa huru kufanya kila aina ya
maasi wayatakayo.
Pia ni vyema Waislamu wote tukajichunga
na kutofanya yafuatayo, ili kutoharibu ibada
yetu ya mwezi mzima wa Ramadhaan.
Kuzuru makaburi
Kuzuru makaburi katika siku ya Eid ni
kitendo kinachokwenda kinyume na lengo
zima la kusherehekea Eid, kwani siku ya Eid
ni
siku
ya
furaha,
kutembeleana,
kupongezana na kupeana zawadi. Kuzuru

Kuacha swala za jamaa


Wengi wetu katika kutekeleza sunnah ya
kutembeleana hujisahau na kuwacha wajibu,
kwani hufikia baadhi ya watu kukosa nafasi
ya kwenda kuswali jamaa na wengine
hufikia hata kuacha kuswali katika siku ya
Eid. Hili si jambo zuri hata kidogo kwani
swala ni nguzo ya Dini na lengo la funga ni
kutufanya kuwa wachaMungu. Sasa
tutalifikiaje lengo hili ikiwa tutaiacha swala
siku ya kwanza mara tu baada ya kuisha
Ramadhaan? Mtume (swallah Allahu alaihi
wa sallam) amesema: Tofauti iliyopo baina
yetu na wao (makafiri) ni swala, mwenye
kuiacha basi amekufuru. Tirmidhy na AnNasai.
Kuchanginyika wanawake na wanaume
sehemu moja

26

Hili tunalishuhudia sana katika viwanja vya


Eid, na watu huliona kama ni jambo la
kawaida, matokeo yake huamsha hisia
mbaya kwa vijana wabaya na kupelekea
kuwabaka
wasichana
wadogo,
kuwanyanganya vitu vyao vya dhahabu na
hata kuwavunjia heshima wazee wa kike.
Pia michanganyiko hii huzaa fitna nyingi na
huengeza vishawishi vya kufanyika zinaa.
Hivyo ni bora kuliepuka hili na
alhamdulillah
baadhi
ya
misikiti
wameanzisha
viwanja
vyao
vya
kusherehekea Eid katika mazingira ya
Kiislamu, kwa hivyo tunawashauri wazazi
na walezi kuwapeleka watoto wao katika
viwanja vyenye kuendeshwa kwa maadili ya
Dini yetu tukufu.
Kutoka pasi na kutimiza hijab kwa
wanawake
Imekuwa ni kawaida ya wanawake wengi
kuhisi kuwa siku ya Eid ni siku ambayo
wameruhusiwa kutoka bila ya kuchunga
sheria ya hijab. Hili ni kosa na haifai kwa
mwanamke yeyote yule kutoka nje ya
nyumba yake hali ya kudhihirisha mapambo
yake kwa wasiokuwa maharim wake. Allah
anasema: Na waambie Waumini wanawake
wainamishe macho yao, na wazilinde tupu
zao, wala wasionyeshe uzuri wao isipo kuwa
unao dhihirika. Na waangushe shungi zao
juu ya vifua vyao, wala wasionyeshe uzuri
wao ila kwa waume zao, au baba zao ...
[an-Nur (24): 31].

Pia katika kutilia mkazo namna ya uvaaji wa


shungi, ni kama tunavyoona katika aya kuwa
shungi inatakiwa ishuke hadi chini ya kifua
na sio kujizonga kichwa tu na kifua chote
kikawa wazi (style ya kiandazi) kama
wafanyavyo wengi katika dada zetu siku
hizi.
Hivyo ni juu ya waume na wazee kwa
ujumla kuwachunga na kuwasimamia wake
na mabinti zao, kwani hilo ni jukumu lao
kama Allah anavyosema: Wanaume ni
wasimamizi wa wanawake ... [an-Nisaa (4):
34].
Kusikiliza na kupiga miziki pamoja na
kuenda madisko
Ni uwazi usio na shaka yoyote ile kuwa
miziki na madisko ni jambo lilio haramu
katika Dini yetu. Kuiaga Ramadhaan kwa
mambo kama haya itathibitisha kuwa
mfanyaji hakuwa akifunga kwa ajili ya
Allah na kulipata lengo la kufunga ambalo
ni uchaMungu. Pia tunashuhudia kuwa
wengi hudhurika kwa kuenda kwenye
madisko, kwani baadhi yao huibiwa vitu
vyao na wasichana wengine hufikia mpaka
kubakwa kutokana na shari ipatikanayo
humo. Ni vyema kwa ndugu zetu wa
Kiislamu kujiepusha na mambo kama haya
ili kupata radhi za Allah (subhanahu wa
taala).
Kucheza kamari na mambo mengine ya
bahati nasibu

27

Kamari na vyenye kufanana nayo ni haramu


katika Uislamu kwa kauli ya Allah
(subhanahu wa taala) isemayo: Enyi mlio
amini! Bila ya shaka ulevi, na kamari, na
kuabudu masanamu, na kupiga ramli, ni
uchafu katika kazi ya Shet'ani. Basi
jiepusheni navyo, ili mpate kufanikiwa. [alMaida (5): 90].
Michezo ya kamari hushamiri sana katika
viwanja vya Eid, ni jukumu la kila
Muislamu
kumkataza
na
kumnasihi
mwenziwe kujiepusha na mambo kama hayo
ili kuepukana na adhabu za Allah
(subhanahu wa taala) kwani hakuna
anayeweza kustahamili adhabu hizo.
Ndugu wa Kiislamu, yafaa kujiuliza jee
tumejifunza nini katika mwezi wa
Ramadhaan? Jee kuisha kwa Ramadhaan
ndio kuachwa wazi kwa mlango wa kufanya
maasi? Jee kuisha kwa Ramadhaan ndio
turudie
katika
maasi
tuliyokuwa
tukiyafanya?

Bila ya shaka jawabu ni hapana, hivyo ni


vyema tukajihimu kuyaendeleza yale yote ya
kheri tuliyokuwa tukiyafanya katika mwezi
wa Ramadhaan kama kusimama usiku kwa
swala na ibada nyengi, kuwa wakarimu kwa
majirani na ndungu zetu, kuwa na huruma
na kuwasaidia mayatima, wajane, wagonjwa
na masikini. Pia kujihimu katika kuendelea
kuswali jamaa misikitini, kwani ni jambo
lenye kusikitisha kuona kuwa Ramadhaan
inapoisha, misikiti hupwaya kutokana na
vijana wengi kutoendeleza kuswali jamaa.
Tunamuomba Allah Mtukufu azikubali
funga zetu na amali zetu nyengine
tulizozifanya katika mwezi mzima wa
Ramadhaan na atuwafiqishe kuziendeleza
katika miezi mingine na atuwezeshe kuingia
katika Pepo yake katika mlango wa Rayaan.
Amin.

28

Twakuomba Mtukufu - Aso kijana na kufu


Mola wetu maarufu - Allahu ulo Karima
Mikono tumeinuwa - Mola wetu watujuwa
Taqabali zetu dua - Utupe lilo na wema
Mola machozi yatoka - Hakika yabugujika
Tumetubu kwa hakika - Waja wako tumekoma
Ya Rabbi tupe elimu - Utupe njema fahamu
Ya kutambua vigumu - Vya Dini yako Karima
Utupe matunda yake - Tuisome tusichoke
Mola elimu iweke - Moyoni mahala pema
Rabbi ijapo hukumu - Isiwe kwetu ni ngumu
Tusiweze kudhulumu - Tukuche wewe Karima
Utupe na kupendana - Sisi na wetu vijana
Mapenzi yaso khiana - Yalo mazuri daima
Tutuze mijini mwetu - Tuqidhie deni zetu
Kabla ya kuja kwetu - Mjumbe wa mauti mwema
Kila ajae na shari - Waijua yake siri
Ivunde yake dhamiri - Asiweze kusimama
Rabbi sala na salamu - Zimfikie Hashimu
Na swahabaze kiramu - Na aali na kila mwema
Amina Rabbi amina - Amina Rabbi amina
Amina Rabbi amina - Ya Rabbi watusikia

29

You might also like