You are on page 1of 14

َّ‫الس َنة امل ْي ََلدية‬

َّ ْ َ َ َْ ْ َ ْ ُ ْ ُ
ِ ِ ِ ِ ‫س‬
ِ ‫أ‬ ‫ر‬‫و‬ ‫د‬ِ ‫َل‬‫ي‬ ‫مل‬
ِ ‫ا‬ ‫د‬
ِ ِ ِ ِ ‫حكم ِإلاح ِت‬
‫ي‬‫ع‬ ‫ب‬ ‫ال‬ ‫ف‬

Hukmu Ya Kusheherekea Sikukuu Ya

Krismas Na Mwaka Mpya


Hii ni hotuba ya ijumaa iliyotolewa na Sheikh Abul Fadhli Qassim
Bin Mafuta Bin Qassim, katika Masjidul-Faaruuq, uliopo kwenye
Markaz Sheikhil Islaam Ibn Taymiyyah Pongwe-Tanga, siku ya
Ijumaa 17 Safar 1435H, sawa na 20/12/2013 A.D. Na imeandaliwa
ki-maandishi na mmoja kati ya wanafunzi wa Markaz hiyo.

Hotuba ya kwanza

Hakika sifa njema zote ni za Allah, tunamhimidi, na tunamuomba


msaada, na tunamuomba msamaha, na tunajikinga kwake
kutokana na shari ya nafsi zetu, na ubaya wa amali zetu. Yule
ambae Allah atamuongoza basi hakuna wa kumpoteza, na Yule
ambae Allah atamuacha apotee basi hakuna wa kumuongoza. Na
ninashudia ya kwamba hakuna mwenye kuabudiwa kwa haki ila
Allah. Na ninashuhudia ya kwamba Muhammad ni mja wake na
Mtume wake.

[Enyi mlioamini! Mcheni Allah ukweli wa kumcha, wala msife


ila nanyi ni Waislamu]. Suraart Aal Imraan/102.

1
[Enyi watu! Mcheni Mola wenu aliyekuumbeni kutokana na
nafsi moja, na akamuumba kutokana na nafsi hiyo mkewe. Na
akaeneza kutokana na wawili hao wanaume na wanawake
wengi. Na mcheni Allah ambaye kwaye mnaombana, na
jamaa zenu. Hakika Allah ni Mwenye kuwaangalieni] An-
Nisaa/ 1.

[Enyi mlio amini!, Mcheni Allah na semeni maneno ya


sawasawa. *** Atakutengenezeeni vitendo vyenu na
atakusameheni madhambi yenu. Na atakayemtii Allah na
Mtume wake, bila ya shaka huyo amefanikiwa mafanikio
makubwa]. Al-Ahzaab/ 71-72.

Ama Baada ya hayo:

Naitumia fursa kukunasihini, na kuinasihi nafsi


yangu.

Kama mnavyofahamu ya kwamba tupo mwishoni


mwa mwaka 2013 M, na huko mwisho kuna mambo
mengi sana, na baadhi yake tukiyapa muda mpaka
wiki ijayo itakuwa umeshapita muda wake. Kwa hiyo
nimeona jambo la sawasawa lenye kuendana na
wakati ni kuzungumzia kuhusu kadhia zilizopo katika
kipindi hiki. Hivyo basi, katika hotuba yetu ya leo
tutazungumzia: Hukmu ya kusheherekea sikukuu
ya Krismas na mwaka mpya (katika uislamu).

2
Kwa sababu sisi tunazungumzia mambo haya ndani
ya dini yetu, na yanayowahusu waislamu katika
muongozo wao, ili waislamu wajue kwamba dini yao
inawaelekeza nini katika mambo kama haya na
mfano wake.

Dini ya uislamu ni dini iliyowekwa na Allah Tabaaraka


wa Ta'alaa kupitia Mtume wake Muhammad swalla
llahu alayhi waalihi wasallam, kwa maagizo yaliyomo
ndani ya Qur’an na sunna za Mtume swalla llahu
alayhi waalihi wasallam, atakaefuata maagizo hayo
na utaratibu huo anakuwa muislamu wa sawasawa,
na atakaehalifu maagizo hayo "akaenda kinyume na
maagizo hayo" na utaratibu huo, basi uislamu wake
utapungua kwa kiasi cha kile anachokihalifu na
kwenda kinyume nacho, kwa kujua au kwa
kutokujua.

Lakini mambo yote yanayotuzunguka ndani ya


mwaka mzima na maisha yetu kwa ujumla uislamu
umeyazungumzia, ima kwa ujumla au kwa ufafanuzi
moja baada ya jingine, iliyobaki kwa muislamu ni
kujua tu kwamba mimi natakiwa niwe katika hali gani
katika kukabiliana na jambo hili, hili linanihusu au hili
halinihusu, na wala isichukuliwe kwamba waislamu
wakizungumziwa dini yao katika baadhi ya mambo
ambayo yanapingana na dini nyengine kwamba huo

3
ni uchochezi, laa! Kama kila jambo litaachwa
waislamu wasiambiwe kwa sababu ya kuonekana
kwamba lipo kwenye sura ya uchochezi, basi dini
itakufa; kwa sababu dini ya kiislamu inapingana na
dini nyingine kwa asilimia kubwa kabisa, kwa hiyo
kila utakachokizungumza itakuwa ni dhidi ya dini
nyengine, na ushahidi wa hilo ni kauli yake Allah
Tabaaraka wa Taalaa aliposema:
َ ْ َّ َ ْ َ َّ
}‫اَّلل ِإلا ْسَل ُم‬
ِ ‫الدين ِعند‬
ِ ‫{ ِإن‬
[Hakika Dini “ya haki” mbele ya Allah ni Uislamu] Suraat Aal-Imran/19.

Maneno haya yanapingana na mtazamo wa watu


wanaosema kwamba dini zote sawa mbele ya Allah;
Kama wewe utashika njia hii, na yule akishika njia ile,
nyote nyinyi njia yenu ni moja, hapana! Katika
uislamu hilo halipo;

[Hakika Dini “ya haki” mbele ya Allah ni Uislamu] Aal-Imran/19.

Kwa maana hiyo, mtu akimuabudu Allah kupitia dini


isiyokuwa uislamu huyo hatambuliki mbele Allah
Sub'haanahu wata’laa, kama anavyosema Allah:
ْ ْ ْ ََ َ ْ َ َ
‫{ َو َمن ن ن ن ن ْنن َي ْْلاتن ن ن ن ن ِنَ ن ْ ن ن ن ن ن َ ِإلا ْسن ن ن ن ننَل ِم ِدينن ن ن ن ننا ن ن ن ن ن ْنن ُي َ ن ن ن ن ن َ ِمن ن ن ن ن ن ُ َو ُ ن ن ن ن ن َ ِ ن ن ن ن ن ِ ن ن ن ن ن َ ِ ِمن ن ن ن ن َنن‬
.}‫ين‬ َ ‫ْال َخاس‬
ِ ِ

4
[Na anayetakata (kuufanya) usiokuwa Uislamu kuwa ndiyo
dini, hatakubaliwa, na yeye huko Akhera atakuwa ni katika
wenye hasara] Suraat Aal-Imran:85.

Huo ndio uislamu na na hayo ndio mafundisho yake.

Kwa hiyo isije ikachukuliwa kwamba haya ni


mafundisho ya uchochezi, itakuwaje azungumze
mambo kama hayo ya kadha wa kadha, hapana, sisi
tuna dini yetu na ina mafunzo, labda mtwambie
uislamu basi, halafu mtupangie ule uislamu
mnaoutaka nyinyi, Uislam wa kuufuata na wala sisi
hatuutaki “uislamu huo” sisi tunautaka uislamu huu
huu wa Mtume swalla llahu alayhi waalihi wasallam
unaotupa maelekezo haya yafuatayo;-

1)Mtume swalla llahu alayhi wasallam katika


mafundisho yake ametutahadharisha sana kufuata
Mila na Desturi za wasiokuwa sisi, yaani wasiokuwa
waislamu, ameyatahadharisha hayo kupitia katika
mafundisho mbalimbali, miongoni mwake ni hadithi
ambayo ameipokea Bukhari na Muslim katika sahihi
zao “Muttafaqun alayhi” kutoka kwa Abu Said Al-
Khudriy radhia llahu a’nhu pia imepokewa kutoka
kwa Ibn Abbas kama alivyopokea imamu Al-Haakim
katika Al-Mustadrak, hadithi hiyo inasema:

5
ْ ‫َح َّتن ن ن ن ن َلن ن ن ن ن‬ ُ َ َ ً‫{ َل َت َّتن ن ن ن ن ُع َّن َس ن ن ن ن َنمن َّال ن ن ن نن‬
‫ين ِم ن ن ن ن ْنن ن ن ن ن ن ْ ك ْم ِ ن ن ن ن ن ْ ا ِب ِ ن ن ن ن ن ْ َو ِذ َراع ن ن ن ننا ِ ن ن ن ن ِنً َرا‬ ِ ِ
َ ‫َ ن ن ن ن َنار َ ن ن ن ن‬
‫نال‬
َّ
‫ل ال َو ُُ ن ن ن ن ُد َوالن‬
ْ
ِ ‫ل‬
ْ ُ َ
َ ‫لن ن ن ننو ا ْع ُت ُ ن ن ن ن ُ ْم َنن ن ن ننا َين ن ن ننا َر ُس ن ن ن ن‬ َ َ ْ ُ
‫ن‬ ‫ن‬ ‫ن‬ ‫ن‬ َ ‫ا‬ ‫ن‬ ‫ن‬ ‫ن‬ ‫ن‬
َُ َ
‫د‬
ِ
َ
}‫َ ْن؟‬

[Naapa; mtafuata nyendo za waliokuwa kabla yenu shubiri


kwa shubiri, na dhiraa kwa dhiraa, hata kama wataingia katika
shimo la Yuru (Mburu kenge) basi na nyinyi mngewafuata.
Akasema (Abu said); tukasema: ewe Mtume wa Allah,
unawakusudia Mayahudi na Manaswara “Wakristo?”,
akasema: “kama si hao” ni akina nani? “ndio hao hao”).
Bukhari/7023, na Muslim/6952.

Katika riwaya nyengine ambayo ameipokea Imamu


Al-Hakim kutoka kwa ibn Abbas radhia llahu
a’nhuma ya kwamba Mtume swalla llahu alayhi
wasallam amesema:
ُ ْ َ َ َّ ََ َ َ َ َ
}‫{ َو َح َّت ل ْ أ َّن أ َحد ُ ْم َج َام َع ْام َ أا ُ ِ الط ِ ْي ِق لف َع ت ُ ْ ُه‬

[Hata kama ikiwa mmoja wao “katika Mayahudi au


Manasara” atajamiiana “atafanya tendo la ndoa” na mkewe
barabarani, basi na nyinyi mtafanya].

Kwa maana ya kwamba, waislamu watafikia wakati


wataona kwamba maendeleo ni kuwaiga watu wa ki-
magharibi “ulaya”, maendeleo ni kuwaiga wasiokuwa
waislamu, ujanja na werevu na usasa “kwenda na
wakati” ni kufuata Mila “dini” isikuwa ya kiislamu,

6
itafikia wakati mambo yatafikia kiwango hicho, kiasi
ambacho watu watakosa haya “aibu” kama
walivyokosa wao, ikiwa mtu “Yahudi au Nasara”
amefikia kiwango cha kumuendea mke wake
barabarani basi kuna watu “miongoni mwa
waislamu” wataona hilo nalo pia ni katika
maendeleo, “kwa hiyo” wapo watakaofanya hivyo
kwa sababu ya kupenda kuiga.

Amesema imamu An-Nawawi rahimahu llahu taalaa


anasema:

[Makusudio ya Mtume swalla llahu alayhi


wasallam kutaja: Shubiri, Dhiraa na Shimo la
Mburu kenge; anakusudia kufananiza kutokana
na kuwafikiana sana na wao katika maasi na
kuhalifu “kwenda kinyume na mafundisho
sahihi”, na wala si katika ukafiri].

Wallahu taalaa Aalam.

7
Hotuba Ya Pili
Kila sifa njema ni zake yeye Mola wa viumbe vyote, mwingi wa sifa
zilo nzuri na zenye baraka ndani yake, “sifa hizo zenye” kuijaza
mbingu na ardhi, na vilivyo baina yake, na kujaza chochote
unachokitaka baada yake. Ewe mwenye sifa njema na utukufu, ni
ya haki yale aliyoyasema mja wako, na sote sisi kwako ni
watumwa; Ewe Allah! Hakuna mwenye kuzuia ulichokitoa, wala
mwenye kutoa ulichokizuia, na wala hautanufaishi kwako utajiri
wa mwenye utajiri.

Na swala na salamu nyingi, zenye utimilifu zimfikie Mtume wetu


Muhammad na Jamaa zake na Maswahaba zake wote, na wenye
kuwafuata wao kwa wema mpaka siku ya malipo.

Baada ya hayo:

Jambo ambalo anatakiwa Mwislamu kulifahamu ni


kwamba, sikukuu kwa mtazamo wa kiislamu ni ibada
ambayo muislamu anajikurubisha kwayo kwa Mola
Jalla waalaa, na si jambo la sherehe tu, “hapana”! Idd
ni ibada, na ndio maana Anas bin Malik radhia llahu
a’nhu anatuelezea katika hadithi aliyopokea Imamu
Ahmad katika “Musnad/11750”, na Abu Daud katika
“Sunan/1235” anasema Anas:

8
َ
‫نان َي َع ُ ن ن ن ن ن ن ن‬
ْ
‫ن‬ ‫ن‬ ‫ن‬ ‫ن‬ ‫ن‬ َ ْ ‫َ ن ن ن ن نند َم َر ُسن ن ن ن ن ن ُل ل ن ن ن ن ن ن ل ع ين ن ن ن ن ن وسن ن ن ن ن ن م ْاملَد َين ن ن ن ن ن َنة َو َل َُ ن ن ن ن ن ْنم َي‬
‫م‬
ِ ِ ِ ِ
ْ َ َّ ُ ُ َ
‫نان ؟ ن ن ن ن ن ننال ا و نن ن ن ن ن ننا َعن ن ن ن ن ن ُنو ِ ِوُ َ ن ن ن ن ن ننا ِ ن ن ن ن ن ن‬ ‫ن‬ ‫ن‬ ‫ن‬ ‫ن‬ ‫ن‬ ‫ن‬ َ ْ ‫نال و َمن ن ن ن ن ننا َ ن ن ن ن ن ن َنًان ْال َي‬
‫م‬ َ ‫ِ وُ َ ن ن ن ن ن ننا َ َ َ ن ن ن ن ن ن‬
ِ ِ ِ
َ َ َّ َّ َ َ َّ ‫ْال َجا‬
‫اَّلل ن ن ن ن ن ن ن ن ْند‬ ‫ل ن ن ن ن ن ن ن ن ل ع ي ن ن ن ن ن ن ن ن وس ن ن ن ن ن ن ن ن م و ِإن‬ ِ
ُ ‫نال َر ُس ن ن ن ن ن ن ن ن‬
‫ل‬ َ ‫ن‬ ‫ن‬ ‫ن‬ ‫ن‬ ‫ن‬ ‫ن‬ ‫ن‬ ‫ن‬ َ ‫نة‬ِ ‫ن‬ ‫ن‬ ‫ن‬ ‫ن‬ ‫ن‬ ‫ن‬ ‫ن‬ ‫ن‬ ‫ي‬ ِِ
ْ ْ َ َ ْ َ َ ُْ ْ َ َ ْ ُ َ َ َْ
ْ ‫ألا‬
. ِ ‫ل َح َ َو َي ْ َم ال ِفط‬ ‫أ دلكم ِب ُِ ا ا ِمنُ ا و ي م‬

[Mtume swalla llahu alayhi wasallam aliwasili Madina na hali


ya kuwa watu wa Madina wana siku mbili ambazo wanacheza
katika siku hizo “watu wa Madina walikuwa na utaratibu wao
kila mwaka wana siku mbili ambazo wanashereheka”,
“Mtume swalla llahu alayhi wasallam alipowaona watu wa
Madina wanafanya hivyo” akawauliza: ni siku gani hizi?
Wakasema: sisi tulikuwa tukicheza siku hizi katika Jaahilliyya
“kabla ya kuja uislamu”, akasema Mtume swalla llahu alayhi
wasallam: Allah tabaaraka wataalaa amewabadilishia nyinyi
siku mbili hizo kwa kukupeni siku mbili nyengine zilizo bora
kuliko hizo “nazo ni” siku ya Iddi Al-Adh’ha na siku ya Idd Al-
Fitr).

Hizi ndio siku ambazo Allah amewawekeeni nyiyi ili mshereheke


katika siku hizo, na muachane na siku hizo za Jaahiliyyah.

Al-Majdu ibn Taymiiya rahimahu llahu anasema: [Hadithi hii


inafidisha “inatufahamisha” uharamu wa kujifananisha na
wao katika sikukuu zao, kwa sababu Mtume swalla llahu
alayhi wasallam hakuwakubalia wao katika sikukuu mbili hizi
za ki-jaahiliyyah, wala hakuwaacha wacheze katika siku mbili
hizo “kwa kufuata” kawaida yao.

9
Mtume swalla llahu alayhi wasallam akawaambia: Allah
amewabadilishieni nyinyi, na kubadilishwa kunampelekea
mtu kuacha lile alilobadilishiwa, na kufanya lile lililowekwa
badala yake; kwa sababu haiwezekani kukusanyika pamoja
jambo lililobadilishwa na lile lililowekwa badala yake
“lililobadilisha”].

Angesema: mmeongezewa siku nyengine, lakini amesema


mmebadilishiwa siku nyengine zilizo bora kuliko hizo.

Kwa hiyo sisi mbele yetu kuna sikukuu hizo ambazo


zimerasimishwa ki-serikali, na mujtamaa kwa ujumla
kwamba ni sikukuu, lakini uislamu hautukubalii
katika hili, unatwaambia hapana nyinyi sikukuu zenu
zimeshapita, Idd Al-Fitr na Idd Al-Adh-ha, kama mna
hamu ya kushereheka basi subiruni mwakani Inshaa
Allah zitakuja sikukuu hizo, na kila wiki mna sikukuu
siku ya ijumaa, na mengine yote hayatambuliki na
uislamu.

Kwa hiyo, jambo la wajibu kwa muislamu kupitia siku


hizi zilizo mbele yetu, na watu wengi wamepewa
mtihani katika siku hizo kwa kujiunga na wasiokuwa
waislamu kwa kusheherehekea. Hatusemi watu
wafanye fujo, wawapige wenye kusheherekea,
hapana! Tunazungumza kwamba wewe muislamu na
familia yako huusiki na jambo hili na wala siku hizo
hazikuhusu, siku hizo.

10
Miongoni Mwa Mambo Tunayotakiwa Kuyafahamu
1- Siku hizi zipite kwetu sisi kama zinavyopita siku nyengine, iwe
ni Krismas au mwaka mpwa; kwa sababu watu wengine ikifika
mwaka mpya “kama wanavyodai” huwa wanakuwa vichaa,
wanapita barabarani huku wakifanya makelele, na kufanya fujo,
mfano: kupiga baruti, kuendesha magari pamoja na pikipiki
kwa kasi kubwa, na wengine wanakimbia huku na kule, na
kuchoma matairi, yaani ni kichaa “uchizi” wa hali ya juu usio na
mfano, na utasikia balaa nyingi zikitokea siku hiyo, “ukiuliza”
kuna kitu gani? Aah mwaka mpya, mwaka mpya gani? Wewe
unakuhusu nini!!, utamsikia mtu wakati inapofika saa sita
6:00pm kamili usiku anasema: nimeuonaaa nimeuonaa!, je
umeona nini? Kwani jana na leo kuna tofauti gani? Au jana jua
lilikuwa linawaka na leo haliwaki? Maskini, hakuna kitu
isipokuwa ni wehu “ujinga uliotopea” wa kukosa maadili ya
dini, na pia kutofahamu misingi yake, mpaka ikawa mtu
hajielewi, anafanya mambo ya kichaa huku akidhani kuwa
amepatia, ati kwa sababu kuna fulani na wao wanafanya kama
hivyo!!!. Muislamu zingatia!.

2- Kataa kabisa jambo la kupeana pongezi na hongera za “Happy


Krismas”, na kupeana zawadi kupitia mnasaba huu, iwe
pamoja na waislamu, au wasiokuwa waislamu, ikawa mtu ana
ndugu, jamaa au rafiki, anampelekea kadi au massage kwa njia
ya Simu, au salamu kwa njia ya Redio, Tv, n.k, huo si uislamu,
bali huo ni ukristo, na jambo hilo halipo katika uislamu.

11
Amesema ibnul Qayyim rahimahu llahu katika kitabu
“Ahkaamu Ahlid Dhimma”:
[Ama kupeana hongera kwa kupitia nembo “alama” za
ukafiri zenye kuwahusu wao, ni haramu kwa makubaliano
ya wanachuoni, mfano: mtu kuwaa hongera na pongezi
kwa ajili ya sikukuu zao, na funga zao, mfano mtu
akasema: “iwe ni” sikukuu yenye baraka kwenu, Happy
Krismas, n.k, maneno haya ikiwa msemaji atasalimika na
ukafiri basi atakuwa hajasalimika na kutenda jambo la
haramu; kwa sababu haya ni katika mambo
yaliyoharamishwa, mfano wake ni sawa na Yule aliyempa
hongera mtu kwa sababu ya kusujudia msalaba, “hongera
bwana umesujudia sana msalaba mwaka huu!!”, bali
mwenye huyo mwenye kutoa pongezi ana madhambi
makubwa zaidi, na anachukiwa zaidi mbele ya Allah kuliko
Yule anaempongeza mtu kwa ajili ya kunywa pombe, au
kuiua nafsi, au kufanya zinaa, ….. lakini kama mfano mtu
yupo katika mazingira magumu ambayo hawezi
kudhihirisha uislamu wake sikuwa kwa kujipendekeza
kwao, ikawa anawaambia kwa dhahiri hali ya kuwa moyoni
mwake kuna imani, basi mtu huyo atakuwa ana afadhali).
lakini wewe unagopa nini mpaka ukaingia huko?.
3- Haifai kuacha kufanya kazi katika siku hizo, wala si kwa ajili ya
masomo “zikafungwa shule au madrasa n.k)”, au kazi binafsi
sawa iwe ni kazi binafsi au ya kuajiriwa.

12
4- Haifai kwa wafanyabiashara kuuza kitu chochote
kinachowasaidia makafiri katika Idd yao, mtu asije akaona ya
kwamba huu ndio msimu wa kuuza maua, au nguo, n.k.
amesema ibnul Haajj Allah amrehemu:

[Haifai kwa Muislamu kumuuzia Naswara “mkristo” kitu


chochote chenye maslahi ya dini yake, (ama siku za
kawaida muuzie mtu yeyote, ni sawa awe Yahudi au
Naswara, kwa kuwa ni biashara ya halali basi hakuna
tatizo, lakini ukiona kuna ishara ya kwamba kitu hicho
kinafungama na ibada fulani basi usimuuzie), si nyama,
wala ngozi, wala nguo, na wala hawaazimwi hata kipando
“mfano akasema: niazime kipando chako kwa ajili ya
kwenda kwenye mkesha, beach, au kanisani n.k”, kwa
sababu kufanya hivyo ni kuwasaidia wao juu ya ukafiri
wao, na inatakikana kwa watawala wa kiislamu wawazuie
waislamu juu ya mambo hayo). “Fatawa ibn Hajar Al-
Hathamiy: j 4, uk 228”.
Kwa hiyo ndugu zangu waislamu, kuna mengi yametajwa na
wanachuoni kuhusu mambo haya ya kusheherekea sikukuu ya
Mwaka Mpya na Krismas, na sikukuu nyengine za makafiri na
washirikina. Na jambo kubwa kabisa linalotajwa na maulamaa
katika kuacha kushirikianana na watu hawa na sherehe zao ni;
kujenga msingi wa al-walaa wal-baraa “kupendana na
kuchukiana kwa ajili ya dini”, na huo ndio uislamu.

13
Haina maana umfanyie dhulma kafiri, mfano: ukaenda kwenye
Krismas ukaanza kuwashambulia, kuwalipua na kuwapiga,
hapana! Dini yetu haitufundishi hivyo, na wala huo si utaratibu
wa dini.
Kwa hiyo tunachotakiwa sisi ni kuwafundisha watoto wetu ya
kwamba utaratibu huu sisi hautuhusu. Sisi tunakwenda kwenye
madrasa zetu, biashara zetu, na shambani kama kawaida,
isipokuwa kama mtu anafanya kazi sehemu kwa kafiri na
akamwambia leo hakuna kazi, basi atarudi. Na hili hasa
linawahusu vijana, kwa sababu wao ndio hujifanya hawaelewi,
pamoja na wazazi wao wanaowaruhusu katika mambo hayo ya
batili.
Kwa hiyo sitorefusha sana, haya niliyoyasema kwenu
yanatosha, kitu cha msingi ni kuyazingatia na kuyafanyia kazi.

Na swala na salamu zimfikie Mtume wetu Muhammad na


Jamaa zake na maswahaba zake.

Abu Abdil alim Arafat bin Mahmoud


19 Safar 1435 H – 22/12/2014 A.D
Pongwe/Tanga- Tanzania.

14

You might also like