You are on page 1of 35

KUTUBU KWA AJILI YA DHAMBI ZA TAIFA

SEHEMU YA KWANZA

Paulo na Sila walipofika Beroya katika Matendo 17:10, tunaambiwa kwamba watu wa Beroya walikuwa
waungwana kuliko wale wa Thesalonike kwa sababu walilipokea neno kwa utayari wote wa moyo na
wakayachunguza maandiko kila siku waone kama mambo yalikuwa ndivyo. Hakika hii ndiyo taratibu
ambayo hupendekezwa na maandiko, yaani kwamba kwanza tuone katika maandiko mafundisho
yoyote mapya kabla ya kuyaamini na kuyapokea mioyoni mwetu. Huku si kutoamini lakini inaonyesha
kuwa tunapendezwa na mambo kama hayo kama Mungu alivyoyafunua kupitia Neno lake. Tunatakiwa
kuheshimu na kumpenda Mungu kwa kuyafuata mambo yale ambayo ameyaonyesha kwetu kwa uwazi.
Hii pia ni ulinzi kwetu tutalindwa toka madhara na udanganyifu kwa kulitunza Neno lake kwa
unyenyekevu.

Vivyo hivyo, kama tukimsikia mtu anahubiri na kutuambia tuamini hili au kufanya lile, lakini hatuvioni vitu
hivyo kufundishwa katika maandiko, basi tusipokee mafundisho hayo kabisa. Haijalishi kama mafundisho
yanatufikia kupitia msemaji wa kimataifa anayetukuka, kitabu cha kikristo ambacho kimeuzwa nakala
mamilioni ulimwengu mzima, au mtu ambaye tunaweza kuwa tunamheshimu. Haijalishi hata kama
imetoka kwa Mtume au hata malaika kutoka mbinguni (Galatia 1:8), tusiamini wala kupokea kama jambo
hilo hatuwezi kuliona kwenye maandiko. Mtume Paulo alishangazwa kwamba Wagalatia walikuwa
wameiacha haraka namna hiyo Injili ambayo walikuwa wameiamini na kuipokea, na kufuata mafundisho
mengine ambayo yalikuwa mageni kabisa na yaliyokuwa kinyume na kweli. Leo, pia tunaweza
kushangazwa na jinsi watu wa Mungu wanavyopokea mambo haraka na kirahisi rahisi, ambayo
hayajafundishwa katika Biblia. Hatuchunguzi biblia kuona kama mambo hayo yako hivyo.

Hakuna kitu kipya chini ya jua. Kama ilivyo katika nyakati za Agano Jipya, ndivyo ilivyo leo kuna upinzani
kati ya ukweli wa Injili na mafundisho ambayo yanataka kututia katika kongwa la mawazo ya Agano la
kale ambayo yamemalizwa katika Kristo. Mafundisho haya si sehemu ya Agano jipya na wala hayamo
kabisa. Watu hutumia maandiko, hasa kutoka Agano la kale, na kuanza kuyajengea hoja. Mafundisho
haya hutuibia kweli, kama ilivyo katika Kristo Yesu na uhuru tulio nao katika yeye (Gal.3:1, 5:1).
Wanataka waturudishe katika mawazo ya Agano la kale ambayo yameondolewa katika Kristo na
mafanikio aliyoyapata Kalvari. Katika moyo wake na mwisho wake, mafundisho haya yote huwakilisha
mashambulizi juu ya kweli ya Injili ya Kristo naye amesulibiwa. Huvuruga kweli ya Injili na kutupofusha
tusiweze kuiona nguvu ya kweli na utoshelevu wote wa mahubiri ya msalaba. Wanaoyainua sana
mawazo hayo hawana habari kama wanapingana na kweli, lakini bado mafundisho hayo si sahihi na ya
hatari. Paulo alipigana kwa nguvu kuwafungua watu wa Mungu toka uongo kama huo na kuonyesha
kuwa waalimu kama hao walisumbua kanisa na watabeba hukumu kwa kufanya hivyo. (Galatia: 1:8,9;
5:10-12).

Sasa tufikirie juu ya wazo hili ambalo limesifika sana siku hizi kwamba tunapashwa kutubu juu ya dhambi
za nchi ambayo tunaishi ndani yake. Kufuatana na fundisho hilo, Mungu huumizwa kwa sababu ya uovu
katika nchi yetu, na uovu unamzuia Mungu asibariki nchi na watu wake kama ambavyo angependa. Na
pia nchi inakuwa chini ya laana au hukumu. Kwa sababu hiyo tunapashwa kuungama na kutubu kwa
sababu ya maovu katika nchi yetu na kwa sababu ya dhambi ambazo watu wanazifanya, ili kwamba
Mungu asamehe uovu huu na kutuma baraka zake - inabidi tupokee upatanisho kwa ajili ya nchi yetu na
watu wake. Wanaendelea kufundisha kwamba ni lazima pia kutubu kwa ajili ya dhambi zilizofanywa na
vizazi vilivyopita katika nchi yetu dhambi za kitaifa kabla Mungu hajaleta baraka kweli kweli au kuleta
uamsho. Katika insha hii ninajaribu kusema juu ya mafundisho haya. Lakini kadri mafundisho haya
yanavyoendelea kuzunguka ulimwenguni, dondoo zingine zinaimalishwa zaidi au kusisitizwa zaidi kuliko
nyingine, na yale ambayo watu huamini yanaweza kutofautiana kwa namna fulani. Kwa hiyo katika insha
hii si kwamba namjibu mwandishi mmoja tu bali jibu langu ni kwa mawazo mbalimbali ambayo
yameendelea na kupata sifa kati ya mengi ulimwenguni. Kwangu binafsi, ninaamini kuwa mtu anaweza
kwa haraka haraka na kirahisi kuonyesha kwamba mawazo haya yako kinyume na maandiko, lakini kwa
sababu watu wengine wameshawishika kwa kina sana kwa mafundisho haya mbalimbali, nimegusia
karibu kila vifungu, kama si vyote ambavyo hutumiwa katika jaribio la kuunga mkono mawazo yao, ili mtu
asije akadhani kuwa mafundisho haya yana maana yoyote ya kibiblia.

Sasa, watu wanaofundisha vitu hivi hawavileti vitu hivi kama mawazo yao au tafsiri zao lakini husema
kwamba vimefundishwa katika maandiko kwamba tunapaswa kuvifanya vitu hivi. Hili ni jambo la kutisha.

1
Ni mamlaka gani waliyonayo ya kuwabebesha wakristo mzigo huo? Tutaona kwamba hawana mamlaka
yoyote kufundisha vitu hivi. Ni utunzi wao mpya kabisa. Ni udanganyifu unaotuondoa kutoka kwenye
kweli na nguvu ya msabala. Haimtukuzi Kristo na kazi yake ya Kalvari lakini matokeo yake ni kuzitukuza
baadhi ya sehemu za sheria na kwa njia hiyo kuwaleta watu wa Mungu kwenye udanganyifu na kongwa.
Haifundishwi hasa hata katika Agano la kale, ingawa hapa ndipo wanapo kimbilia ili kuhalalisha
mafundisho haya. Wanatafuta tukubaliane na taswira za baadhi ya watu na Agano la kale kama Eliya,
Yeremia, Yona au Daniel (ingawa kuna vitu tunavyoweza kuvisifia juu yao), badala ya kutuletea mfano
wa ufunuo wa Yesu Kristo, ambaye yu juu ya hao wote, katika asili yake ya uungu na pia huduma yake.
Mafundisho haya yanataka kuturudisha katika namna ya Agano la kale ya kufikiri juu ya laana na hukumu
juu ya mataifa, badala ya kutambua, kukiri na kuutangaza kutolewa kwa msamaha katika siku hizi za
neema. Lakini zaidi ya haya, wanaishia katika kuwatumbukiza watu katika mawazo na maombi ya
kishirikina, kwa kulielewa vibaya hata Agano la kale. Hii haina maana kwamba tusiombe juu ya baadhi ya
hali za kijamii ambazo zina athiri saana jamii zetu au uenezaji wa Injili. Tutagusa juu ya jambo hili
baadaye, lakini mawazo haya ya kisasa yanaenezwa zaidi ya haya.

Swala ni rahisi tu, ni hili, kama vitu hivi vinahitajika na watu wa Mungu, yaani kuungama au kutubu
dhambi ambazo hutokea katika nchi yao, mji au sehemu, ili kwamba hukumu ya Mungu au laana juu ya
nchi iondolewe na baraka kuja, sasa kwa nini jambo hili halifundishwi kaatika Agano Jipya? Kwa nini
hakuna hata aya moja ambayo inafundisha au kuelekeza tufanye jambo hili? Hata haikutajwa wala
kuashiriwa. Kumbuka, wanataka kutuambia kwamba baraka za kweli au uamsho katika nchi yetu
huzuiliwa kama hatuungami na kutubu kwa ajili ya dhambi za vizazi vya sasa na vilivyopita! Ni kwa vipi
jambo la maana kama hili kwa ajili ya maendeleo na kuenea kwa Injili lisiwepo kabisa katika
mafundisho ya Agano Jipya? Hakuna kabisa katika Agano Jipya kitu ambacho kingetuongoza ingalau
kufikiria vitu kama hivyo. Tutaona pia jinsi ambavyo walimu hawa hulitafsiri visivyo Agano la kale katika
jaribio lao la kuhalalisha mafundisho haya.

Mitume Hawakutumia Mtazamo Huu

Fikiria matendo ya mitume. Ni wapi mtazamo huu ulikuwa mkakati wa mitume, wakifikiri au kufundisha
wasafiripo kuizunguka dunia wakihubiri Injili? Ni wapi wanawaelekeza wakristo au watu wengine wowote
watubu dhambi za nchi zao, mkoa au mji ili baraka za Mungu zije. Tunasoma wapi kuwa wao wenyewe
walifanya kitu kama hiki? Lakini haya ndiyo tunaletewa katika mafundisho haya kwamba wakristo
waungame na kutubu kwa ajili ya dhambi za ulimwengu, yaani kwa dhambi za wasioamini katika maeneo
yao, ikiwa ni pamoja na vizazi vilivyopita. Hakuna mahali popote katika matendo ya mitume jambo hili
linaonekana. Mitume na wengineo husafiri kama Mungu anavyowaongoza; kuhubiri Habari Njema kwa
watu kwamba wamesamehewa bure kwa dhambi zao zote kupitia kifo na kufufuka kwa Yesu Kristo; watu
huokolewa na makanisa kuanzishwa na wakristo hupokea mafundisho. Lakini hakuna kuungama au
kutubu kwa ajili ya dhambi za nchi yoyote au eneo na wakristo (au mtu awaye yote!) kabla ya kuipeleka
Injili mahali pale kwa uwezo bila shaka Mungu alibariki kazi na kuongeza watu wengi katika Kanisa
pasipo mafundisho haya wala hapakuwa na mafundisho kama haya yakitolewa na mitume kwa
wakristo wafanye hivyo baada ya makanisa kuanzishwa ili kazi ya Mungu kati yao istawi na kuenea.
Ilienea na kukua kwa ajabu na kulikuwa na uamsho, pasipo watu wa Mungu kujiweka katika nafasi ya
wasioamini kati yao na kutubu dhambi zao. Pia ilienea kuwa ajabu kwa neema ya Mungu pasipo wenye
dhambi kuambiwa watubu juu ya dhambi (zilizopita au za wakati huo) za miji yao mikuu au nchi zao,
kabla ya Mungu kuwabariki kweli kweli na kutenda kazi kati yao kwa nguvu! Mahali popote, mtu yeyote
aliambiwa atubu kwa ajili ya dhambi zake! Jambo hili kwa kweli ndilo fundisho na pia mfano tunaoukuta
katika Biblia yote, kama ambavyo tutaona.

Vivyo hivyo, kumekuwa na uamsho mara kadha ulimwenguni kote na Injili imeenea na kuwa na mizizi
tangu nyakati za mitume hata leo pasipo watu wa Mungu kufanya vitu hivi, kujua au kufundisha. Kwa
hiyo nani anaweza kutuambia kwa nini mafundisho haya yameonekana mara kuwa ya lazima kwa kanisa
na kwa mafanikio na kuenea kwa Injili katika siku hizi?

Mitume Hawakufundisha Juu ya Mtazamo Huu

Mafundisho haya huwezi kuyakuta mahali popote katika maandiko ya mitume katika Agano Jipya. Kitu
kama hicho hakitajwi hata kidogo. Je tunaweza kusema basi kuwa palikuwa na dhambi pungufu, uchawi
na kuabudu sanamu kupungufu katika nyakati za Agano Jipya kuliko zilizopo sasa na kwamba kwa hiyo
wakristo wa nyakati hizo hawa kuhitaji mafundisho haya kama tunavyohitaji leo. Hii ni wazi si kweli. Na
simjui mtu yeyote ambaye anayesema jambo hili. Maandiko ya Agano Jipya pamoja na kumbukumbu za
kihistoria zinahakiki wazi na kwa msisitizo kwamba kulikuwa na ufisadi mkuu na dhambi za kutisha,

2
uchawi, kuabudu sanamu na ugandamizaji katika nyakati za Agano Jipya. Kwa mfano, Mdo 8:9-11; 13:6-
8; 17:16; 19: 18,19,23-28. Tunafahamu pia toka kumbukumbu za kihistoria kwamba jiji la korintho lilikuwa
ni mahali pa uzinzi mwingi na hii inaweza kusaidia kutoa maelezo kwa nini kanisa la Korintho lilihitaji
mafundisho maalum na kukemea kwa mtume Paulo. Vita vingi vilikuwa vimetokea katika eneo hili la
ulimwengu na dhuruma nyingi zilikuwa zimetokea. Kidokezo hiki ni kikubwa kwamba hakihitaji ufafanuzi
zaidi.

Kwa hiyo kwa nini mitume hawa hawawaambii wakristo watubu kwa ajili ya dhambi ambazo nchi zao na
maeneo yao yalikuwa yametenda katika kizazi hicho ama vilivyopita? Je nchi zilikuwa hazijatenda
uonevu wowote au ugandamizaji? Bila shaka zilikuwa zimetenda lakini hakuna mahali popote mitume
waliwaelekeza watu wa Bwana waombe au watubu kwa sababu ya dhambi za Athene au kwa sababu ya
uchawi na uabdu sanamu wa Efeso au kwa sababu ya uzinzi wa jiji la Korintho, au kwa sababu ya
ugandamizaji wa Rumi juu ya nchi zingine hasa Yudea. Hakuna mahali ambapo tutaona wakitia mkazo
au kuwashinikiza wakiristo waungame na kutubu kwa ajili ya dhambi za kitaifa au za vizazi vilivyopita.
Hawawaambii wayahudi kwamba lazima waungame na kutubu kwa ajili ya dhambi za mababa zao katika
mwili; wala hawawaambii waamini wa Kirumi, Kigiriki au Waarabu au wakristo wa nchi nyingine yeyote au
eneo lolote watubu kwa ajili ya dhambi za zamani za nchi zao. Hakika wakristo mjini Rumi walikuwa na
sababu lukuki za kuungama dhambi za himaya ya Kirumi kama mafundisho haya yangekuwa kweli!
Lakini hawapewi maelezo kufanya hivyo. Hakuna aya hata moja, mkazo hata mmoja kwa wakristo
wafanye hivyo mahali popote katika Agano Jipya. Kulikuwa na dhambi nyingi mno, kuabudu sanamu,
uchawi na ugandamizaji katika siku zao na katika vizazi vilivyopita, kiasi kwamba mitume walikuwa na
kila sababu na fursa ya kutosha kuwakazia wakristo waungame au kutubu kwa ajili ya dhambi za wale
waliokuwa wamewazunguka lakini kamwe hawakufanya namna hiyo. Kwa hiyo tena tunaachiwa swali:
kama kutubu kwa ajili ya dhambi za wasioamini katika maeneo yetu au nchi ilikuwa lazima kwa ajili ya
upatanisho wa nchi na kwa ajili ya kuenea ufalme wa Mungu kwa nini mitume hawatuelekezi kufanya
hivyo? Je wamepuuza kutufundisha kitu ambacho kanisa linahitaji kujua ili Injili isitawi na kuenea? Je
walikuwa wajinga wasioweza kujua mafundisho muhimu kama hayo, kama ni mafundisho muhimu kweli?
Kama kanisa limejengwa juu ya msingi wa Kristo, mitume na manabii, Je waalimu hawa wa kisasa
wanajua zaidi ya wao? Bila shaka wasingesema hivyo na wasingetaka kuwa hivyo, lakini naweka swali
hili ili kuonyesha wazi upotofu mkuu wa mafundisho haya na hatari ambayo waalimu hawa wanajiingiza
ndani yake. Hawajengi juu ya Kristo. Wanajenga juu ya tafsiri zao juu ya Agano la kale. Wanabadilisha
imani katika kristo na dini ya ushirikina!

Yesu Hakufundisha Mtazamo Huu

Yesu mwana wa Mungu hakuwaelekeza wafuasi wake wafanye hivyo mahali popote katika Injili hata
katika ufunuo. Yesu alikuja akihubiri habari njema za ufalme wa Mungu kwa watu na kuwaambia watubu
na si kuwaambia watubu kwa niaba ya wengine! Wala hakuwaambia waungame au kutubu kwa ajili ya
dhambi za vizazi vilivyopita kama kwamba hivyo ilikuwa lazima kwa ajili yao wapokee msamaha kamili
na baraka toka kwa Mungu. Hasha. Na tuelewe kuwa kwa ajili ya Kalvari, mtu yeyote atubuye dhambi
zake, hugeuka kumwelekea Bwana na hufanyika mwana wa Mungu, dhambi zilizopita za mababa zake
au za taifa haziwezi kuweka mpaka au kuzuilia baraka kamili za Mungu katika Kristo Yesu kwa mtu huyo.
Kalvari ni kukatwa kikamilifu toka dhambi, hukumu, toka kuhukumiwa moyoni na toka Adamu wa kale, hii
ni pamoja na maisha yetu ya nyuma na mababu zetu nyuma. Mungu Asifiwe! Watu wa Mungu hawako
kwenye kongwa lolote kwa ajili ya dhambi za mababu kama wako katika kristo! Hakuna kitu kama hiki
kimafundisho ya Yesu au mitume. Angalia 2 Kor 5:17. Mawazo haya hayako ama sawasawa na maneno
au Roho wa Kristo. Neno la Mungu huja kwa watu wenyewe, moja kwa moja kuwashawishi juu ya
dhambi zao na kuwaongoza katika toba. Marko 1:14,15; 2:17 (Anawataka wenye dhambi watubu, wala si
watakatifu watubu kwa dhambi za wenye dhambi!).

Neno la Mungu sasa linakuja kwa mtu binafsi na mmoja mmoja kwa kila mtu likiwatia hatiani kwa dhambi
zao wenyewe: Luka 13:1-5; Mdo 2:38, 3:19; 8:22; 17:30; 26:20. Ni kwa njia gani wake kwa waume
husikia kuhukumiwa kwa ajili ya dhambi zao kutubu na kumgeukia Mungu kwa imani na kupokea
msamaha wa dhambi? Ni kwa njia gani baraka hii na neema ya Mungu inaloijia mioyo yao! Huja kwa
kusikia neno la Mungu linalokuja mioyoni mwao wenyewe! Rumi10:1017. Ndiyo, Yesu huwaambia
wanafunzi wake waombe lakini si kwa ajili ya dhambi za wenye dhambi katika miji mikuu, lakini badala
yake waombe Bwana wa Mavuno atume watenda kazi (kuhubiri juu ya ufalme wa Mungu ili wenye
dhambi wenyewe wasikie neno la Mungu na kwa njia hiyo kuamini na kutubu). Pia anawafundisha
waombe ufalme wa Mungu uje na kwa mapenzi yake yatimizwe hapa duniani kama huko mbinguni, na ili
kwamba tusamehewe kama tunavyowasamehe wengine. Lakini hakuna mahali popote katika Agano
Jipya na hakuna mahali popote katika Biblia tunapoambiwa kutubu kwa niaba ya wenye dhambi, au
kuungama dhambi zao ili kufanya upatanisho au mapatano kwa ajili yao kitendo ambacho kitamfanya

3
Mungu awabariki! Yesu anaweza kutambua hukumu juu ya Kapernaumu na anaweza kulia juu ya
Yerusalemu kwa sababu walifanya mioyo yao migumu kwa neno la Mungu na hawakutubu, lakini
hawaombi wafuasi wake waungame na kutubu kwa dhambi za watu hao. (Bila shaka mifano hii
inahusiana na Israeli kuikosa au kuikataa fursa ya kumpokea masihi wao).

Pia ona kwamba katika Uf.2:8-11, Bwana hakulitaka kanisa katika jiji la Smirma liombe na kutubu kwa
ajili ya maovu yaliyokuwa yakitendwa na baadhi ya watu wa Smirna ambao ni wa Sinagogi la shetani, ili
kwamba msamaha wa Mungu na baraka zake zije kwenye eneo: nasema tena, hakuna mahali popote
katika biblia watu wa Mungu wametakiwa kufanya hivyo.

Lakini watu wengine huenda hata mbali zaidi katika kufundisha kwao, kwa kuwaambia watu wa Mungu
kwamba watubu kwa ajili ya dhambi za mji au nchi, kama uchawi, uzinzi na ulevi na kuungama kwamba
wao watu wa Mungu wanahusishwa katika dhambi hizi na wamemtenda Mungu dhambi! Watakatifu
huambiwa wahusike na dhambi za wasio amini kama kwamba dhambi hizo ni zao! Huambiwa basi
watumie damu ya Yesu katika hali hiyo ili kuleta upatanisho na kuomba msamaha wa Mungu! Lakini
damu ya Yesu hutumika kwa moyo uaminio. Huwezi kuitumia damu ya Yesu kupitia maombi kwa
mwenye dhambi asiyetubu! Huu ni kama uchawi katika ukamili wake ambao hutafuta kuchukua nafasi
ya kristo ambaye ndiye mpatanishi pekee kati ya Mungu na Mwanadamu. Yesu katika jumuisho na
hitimisho amejihusisha na dhambi za ulimwengu wote pale Kalvari, kwa njia ambayo ameleta msamaha
kwa wote wanaoamini Injili. Usitafute kuongeza katika kazi ya Mungu katika Kristo.

Bila shaka wanaamini kuwa wanafuata mifano ya Agano la kale (na tutaona hayo baadaye kwa kirefu)
lakini tayari tumekwisha kuona wazi kwamba hakuna wazo kama hilo katika Agano Jipya (na hata katika
Agano la kale kama tutakavyo ona pia). Hakika sasa tunaweza kulia pamoja na Paulo na kusema,
Enyi wagalatia msio na akili, ni nani aliyewaloga, ninyi ambao Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele ya
macho yenu yakuwa amesulubiwa?
Na isitoshe, mafundisho haya yanafanana na ulozi, mwishowe watu huamini mambo ambyo, sio tu yako
kinyume na maandiko, bali pia kinyume na kufikiri ipasavyo.
Wanao ushawishi wa kiuchawi juu ya watu wa Mungu wanaoyafuata mafundisho haya pasipo
kuhakikisha kwenye Biblia. Mafundisho haya yanaonyesha yanakubalika kwa watu wengi kwa sababu
walimu wao hutumia maandiko yaliyochaguliwa kwa uangalifu sana (lakini kama walivyofanya kati ya
makanisa ya Galatia, hasa kutoka katika agano la kale) ambayo pengine huonyesha tarajio la ukweli
ambalo linalingana na la wakati ule; lakini hapo huongezea mawazo yao katika hilo. Na hii ndiyo hatari
na hila ya makosa ya aina hii, huku inatajwa kwamba wanatumia maandiko, lakini hapo hapo
wakiyakataa maandiko mengine - hivyo hujitokeza ukweli - lakini wanatafsiri vibaya mistari hiyo ya neno
la Mungu, wakiweka maana yao wao wenyewe juu yake na ndipo huishia kupata kitu fulani ambacho kwa
uhakika ni mbali na ukweli na hata huwa kinyume cha ukweli. Kwa kukataa ushuhuda wote na maandiko,
wakijenga mtindo wao wa mafundisho, ingawa huwa hawanzii na Biblia hata kidogo. Wanadai kuwa
wanao ufunuo maalum au huduma - hata mitume kutoka kwa Mungu. Wanaanza na mawazo ya aina
fulani yaliyo ya kwao ambayo wao hufikiri labda yanaweza kufanya kazi na pia ni ya kibiblia na baada ya
hapo, wanajaribu kuyatafutia mistari ya neno la Mungu, mstari wowote ambao unaweza kuonyesha
kuunga mkono mafundisho yao. Na wanapogundua kuwa kumbe biblia haiwaungi mkono kwa dhahiri,
wanaanza kujisomea maana zao wenyewe katika mistari hiyo waliyoichagua. Na wengi wamedanganyika
kwa njia hii, kwa sababu hawayachunguzi maandiko, wamesahau ile thamani ya usafi na wepesi wa
Injili ulivyotolewa kwao toka mwanzo.

Agano la Kale - Kwa Ujumla

Sasa, hebu tufikirie juu ya maandiko ya Agano la Kale, ambayo kwa hakika ni neno la Mungu lenye
uvuvio kwetu. Ndani yake tunagundua mambo ya utendaji wa Mungu kwa wanadamu na hasa kwa watu
wake aliowachagua, Israel, na maagano aliyoyaanzisha pamoja nao. Zaidi ya yote anatupatia picha ya
mambo yanayokwenda kutokea hapo baadae na kutupatia mfano wa ufufuo wa wokovu ambao Mungu
anakwenda kuuleta kwa wanadamu kupitia Yesu Kristo.

Ingawaje maandiko ya Agano la Kale yana mifano mingi inayomwonyesha Yesu katika namna yake na
wokovu atakao uleta - matarajio ya mwenendo wa maisha ya Yusufu yanamdhihirisha Yesu k.m.f. Musa
akiongoza wana wa Israel kupitia bahari ya Shamu ni picha ya ubatizo wetu katika Kristo. Lakini ili
alisimamishe Agano Jipya na kuwaingiza waume na wake ndani ya ufalme wa kiroho wa Mungu, kwa
hakika Mungu alipaswa kumleta Kristo mwenyewe na kumtuma afe katika msalaba. Kabla Kristo
hajaziondoa dhambi za ulimwengu pale Kalvari (Yoh. 1:20), Mungu asingeleta au kuzaa chochote katika
maisha ya ndani ya kiroho na uweza wa maisha yake yeye mwenyewe na ufalme. Agano la Kale
linatupatia picha ya nje ya yale ambayo Mungu alipenda kutufanyia kiroho. Kwa kweli kifo cha Yesu pale

4
Kalvari, kilikuwa ni kielelezo muhimu cha tukio la kihistoria ikiwa sio la umilele. Kifo chake kilibadilisha
mambo kwa njia ya msingi kabisa. Alilia, Imekwisha!, na papo hapo pazia la hekalu likapasuka vipande
viwili. Hii inaonyesha kuwa, watu kwa imani kupitia Kristo, sasa wangeweza kuingia patakatifu pa
patakatifu kwa damu ya Yesu; katika roho; pasipo matendo ya sheria tena. Sheria ilitolewa na Musa,
lakini neema na kweli zilikuja kwa mkono wa Yesu Kristo. Mungu habadiliki. Hata kidogo! Rehema zake
kwa ajabu kabisa zinaonyeshwa kwa matendo yake na watu katika Agano la kale. Halikadhalika, haki
yake na hukumu. Lakini sasa kwa sababu ya kifo cha Yesu pale Kalvari, uhusiano wa Mungu na
wanadamu umepitia katika msingi wa mabadiliko makubwa. Yesu alikuwa ni mwanakondoo wa Mungu
azichukuaye dhambi za ulimwengu, aliihukumu dhambi katika mwili wake hivyo kuivunja nguvu yake
ndani ya maisha ya watu, alizichukua hukumu za dhambi za wanadamu, kwa hiyo akatupatia msamaha
bure, akatupatia uzima, uzima wa milele kwa roho na haki yake (Rumi 8:1-4). Kwa ajili ya msalaba
Mungu ameweza kufanya yale ambayo sheria isingeweza kufanya, na amewapa wale wanaoamini katika
Kristo haki ya kufanywa kuwa wana wa Mungu na kuingia katika uwepo wake.

Kwa hiyo kati ya mambo mengine, mawili ya msingi na muhimu yamebadilika. Kile ambacho Mungu
amekifanya kwa ajili yetu, ni kile ambacho Mungu amekifanya ndani yetu. Katika hii ya mwanzo, watu
sasa wanashiriki haki ya Mungu kwa imani, kwa sababu ya utajiri wa neema yake na sio kwa kazi
zipatikanazo kwa sheria, na hii inatupatia sisi haki ya kufanyika kuwa wana wa Mungu.

Na kwa sababu Mungu amekwisha kutuondolea vyote viwili, dhambi na uadui wa sheria (Efeso 2:15; Kol.
2:14), sasa kunakuwa na muungano wa kweli kiroho kati ya Mungu na wanadamu. Hutufanya sisi tuwe
watoto wake kwa kutupatia roho wa mwana wake Yesu Kristo akaaye ndani yetu. Kutokana na hali hiyo
basi, sasa maisha yetu yanaonyesha tabia yake kwa njia ambayo haikuwezekana katika Agano la Kale
(2 Petro 1:3-4). Kwa hiyo, iwapo tutarudia ili kuzitunza baadhi ya sehemu ya sheria kama walivyofanya
kule Galatia, hivyo basi, tutakuwa tunaikataa imani yetu katika Kristo na wokovu wake
aliotununulia, au kama tutakuwa tunarudi kuzifuata njia za tabia za kale, ndipo basi tutakuwa tunakataa
ufunuo wa tabia yake ndani ya mioyo yetu.

Kwa mfano, katika Agano la Kale watoto wa kiume walilazimika kutahiriwa, kama ni sehemu ya agano
kati ya Mungu na watu wake. Hii ni aina au picha ya ndani ya kazi za kiroho ambazo Kristo alizikamilisha
kwa wale ambao wanamwamini yeye, (Kol. 2:11). Lakini yeye ni utoshelevu wa kweli ambao kutahiriwa
kwa nje katika agano la kale ilikuwa inaelezea (Heb.10:1). Kwa hiyo, mtu yeyote kwa sasa, iwapo
anaamini kuwa pamoja na kuamini katika Kristo, ni lazima pia kwa nje utahiriwe ili kuokoka, basi mtu wa
jinsi hiyo atakuwa anaiondoa imani yake na wokovu aliopewa (Gal. 5:3-6).

Ni ujinga ulioje jamani kuacha kitu muhimu na kubakia na kivuli chake! (Heb.10:1). Je, unaweza kula
kivuli cha tunda la ndizi? Kivuli kinaweza kukushibisha njaa yako na kukuacha hai? Ebu - jaribu kula
kivuli kwa kadiri uwezavyo. Lakini utaishia na vumbi mdomoni mwako! Na jambo hili linafanana na
mafundisho ya aina hiyo yanavyofanya. Wanayaacha ya kiroho na kungangania ya kimwili, ya mbinguni
na wanangangania ya duniani, ingawaje mtu anaamini kuwa Yesu ni mwana wa Mungu na kwamba
anao msamaha kupitia damu yake; ingawa anaamini mambo mengineyo mengi yaliyo ya kweli, bado mtu
huyo, ikiwa anatafuta kuongezea chochote kwa yale Kristo aliyoyafanya, iwapo anatafuta kuturudisha
nyuma kwenye vitu ambavyo kwa kweli Kristo alikuja kuviondosha au kutimiliza, hapo basi mtu huyo
anasababisha kuukataa wokovu wa Kristo. Kristo, na imani katika Kristo havina faida yoyote kwake mtu
huyo na hivyo imani ya mtu huyo ni bure. (Gal.4:19,20; 5:3,4). Hata kama anajifikiria kuwa anamfuata
Kristo, amejidanganya, (Gal. 3:1). Mtu wa jinsi hiyo kwa jumla, anachanganya agano la kale na jipya,
wanachanganya yale ya ndani na ya nje; kivuli na kitu halisi, ya mwilini na ya rohoni ya duniani na ya
mbinguni. Inafanana pia kama Mkristo anafikiri ni lazima kutunza sherehe za Agano la kale. Anaikataa
Imani!

Kwa mtazamo wa yote ambayo Mungu ameyafanya kwa ajili yetu kwa Kristo Yesu, haikushangaza kuona
Mtume Paulo akihuzunishwa kutoka ndani ya moyo wake, akijitahidi kadiri alivyoweza kwa maombi na
maelekezo ili kuwakomboa Wagalatia kutokana na ujinga wao wa madanganyo.

Je, unapaka damu leo katika miimo ya milango yako ili kuzuia hukumu ya Mungu? Unaleta ngombe au
mbuzi au kondoo pamoja nawe kanisani ili kumtolea Mungu kama dhabihu ya dhambi zako? Haya,
pengine labda unatabasam, kama mwitikio kwa maswali haya! Lakini makosa ya jinsi hiyo hiyo
yanafundishwa na kujitokeza siku za leo; watu wanatafuta kuturudisha nyuma kwenye fikra, na matendo
ya agano la kale. Na wengi wa watu wa Mungu wanapokea na kuyafuata mafundisho hayo. Sasa,
mafundisho tunayoyaona ndani ya makala hii yanahusiana na aina hii ya makosa.

5
Niliyoyaelezea hapo juu ni mambo ya msingi ambayo Mungu amefanya kwa ajili yetu katika Kristo -
ambaye ndiyo njia ya wokovu wetu. Sasa vipi kuhusu huduma na tabia ya Wakristo - Mungu anafanya
nini ndani yetu na kupitia kwetu. Je, mambo yanaendelea katika Agano jipya kama ilivyokuwa katika
agano la kale? Kwa kiasi tu. Lakini lazima tukiri juu ya mzizi wa mabadiliko ya msingi kwa sababu ya
Kristo na yale aliyoyafanya. Hebu fikiria Matayo 5: n.k. Sasa je, utambomoa mwenzako jino lake, kwa
sababu eti yeye amelibomoa lako? Je, utawachinja watu wasioamini kwa upanga? Kanisa lako litampiga
kwa mawe yeyote ambaye amefumaniwa katika uzinzi? Au utamwita Mungu atume moto toka mbinguni
uwajilie hao wanaompinga Mungu? Haya yote yaliruhusiwa na kutakiwa ndani ya agano la kale. Lakini
kwa sasa hatuwezi; hatuwezi kuthubutu kufanya lolote kati ya hayo. Kwa sababu sisi tumezaliwa upya
kwa roho wa Mungu na wala hakuna kati ya hayo yanayofanana na tabia yake Yesu ndani yetu.

Tunaweza kufikiri kwamba, haya yote ni rahisi na yaliyowazi kabisa, lakini ebu umchukulie Yakobo na
Yohana ambao kwa uwazi kabisa walipenda harufu ya uweza wa kuwa na Yesu aliowapa. Hata hivyo
walimwomba iwapo, angeweza kuita ili kushusha moto chini, juu ya wasamaria kwa sababu wamekataa
kumpokea Yesu. Aliwakemea mara moja, na akawaambia, hawajui ni roho ya aina gani walinayo. Wao
hawakuelewa yote mawili, kati ya tabia na huduma ya mwana wa Mungu.

Na mpaka pale tu tutakapokuwa tunatembea katika Roho ya Kristo kufuatana na neno lake, bado
tutakuwa tu tukifanya makosa hayo hayo. Na hivyo ndivyo ilivyo leo watu hawaelewi tabia ya Kristo na
wokovu wake kadhalika na huduma ya kanisa. Kutokana na uchaguzi wao kutafuta tabia ya ubinafsi wa
madaraka, baadhi ya walimu wao wamechagua maandiko kutoka katika Agano la Kale kwa kadiri
yanavyowafaa wao na vile wanavyotaka kuamini. Wanaumba mfano wa Mungu unaochipua toka katika
fikra zao, ambazo huzichochea baadhi ya nyaraka za Agano la Kale. Huu ni sawasawa na kuabudu
sanamu na hunyanganya mfano halisi wa Mungu kama ulivyofunuliwa kwetu na katika Kristo.

Kwa hiyo, hii inatokana na watu hawa ambao huja mjini, na badala ya kuhubiri Injili na utajiri
usiochunguzika wa Yesu Kristo, wanawaambia watu kwamba eti laana na hukumu za Mungu ni juu yao
na miji yao na kwamba sasa wanatakiwa kutubu kwa niaba ya dhambi za (wengine katika) miji hiyo au
taifa hilo; ili kwamba Mungu aweze kughairi na kuindoa hukumu yake na badala yake atume baraka
(watu wengine karibu wapumue moto na hukumu kama Yakobo na Yohana walivyotaka kufanya).
Tunawezaje kujua kuwa tumekwisha kuomba kwa ajili ya dhambi zote zinazotakiwa kuungamwa? Lakini
jee, watu wataendelea kutubu kwa jinsi hiyo hadi lini? Nani atakaye waambia kwamba hukumu na laana
hiyo sasa imeondolewa kwa toba ya jinsi hiyo? Wahubiri hawa hawaonyeshi kabisa kuwaambia watu bali
wanawataka tu wakristo waaendelee kutubu na kutubu na kutubu kwa ajili ya mambo ya aina zote
ambayo hao wahubiri na wapelelezi wao pamoja na waombezi wao huendelea wakitafuta makosa katika
taifa!

Kwa kawaida, wanafurahishwa sana na ushahidi wowote ule juu ya mambo yahusuyo siri za ulozi au
uchawi katika nchi hiyo. Na kisha hutangaza waliyoyagundua ndani ya makala zao na barua za maombi
kwa maelezo makubwa. Wanazingatia sana katika mambo ya aina hiyo na huzijaza akili za watu wa
Mungu kwa masomo yasiyofaa ambayo huelekea kwenye kutukuza kazi za shetani, badala ya
kuiendeleza Injili ya Bwana Yesu au kuleta baraka. Hayo ni madhara makubwa yanayowaingiza watu
katika ujinga wa kutomjua Kristo na wokovu wake wa tabia na huduma yake.

Tafadhali usielewe vibaya, hapa sisemi kuwa hatuwezi kuomba kuhusu mambo yatokezayo katika miji au
nchi zetu bali ninachosema ni kwamba tusifanye mambo ambayo hayamo katika maandiko ya neno la
Mungu; na tusiwe na mawazo ya ushirikina ambayo kwa hayo watu wengine huyachanganya na Injili ya
kweli hata kuwatumbukiza watu katika vifungo na giza kwa mafundisho yao hayo. Katika siku hizi, kwa
hakika tunaweza kuumizwa kwa yale yanayotutokea pia yanayotokea katika kanisa, na tungependa
kunyenyekea mbele za Mungu na kuomba kuwa anaweza kugeuza mioyo ili imgeukie na kuwaongoza
watu kuelekea toba. Lakini hii inatofautiana sana na aini hii ya maombi ya Ushirikina.

Agano la Kale - Daniel

Lakini sasa, kwa kadiri tunavyo yatazama maandiko ya Agano la Kale, kwa uhakika tunagundua
kwamba kumbe mafundisho ya jinsi hiyo hata hayamo humo!

Wapi katika Agano la kale ambapo Mungu au hata manabii anawainua watu wake ili kuungama na
kutubu kwa ajili ya dhambi ya yeyote yule asiyeamini au taifa lolote? Au ni wapi tunaweza kuupata
mfano wa jinsi hii katika Agano la Kale? Haupo wowote; haupo; haupo hata mmoja.

6
Daniel ambaye hunukuliwa mara nyingi, alikuwa akiishi Babel, lakini pia huko nako hatumkuti akiomba
kwa ajili ya maovu ya mji ule. Hakuna popote ndani ya Agano la Kale ambapo watu wa Mungu
wanatubu kwa ajili ya dhambi za wasiomini, ili kwamba laana ya Mungu ipate kuondolewa, na
badala yake baraka na msamaha upate kutolewa? Kwa kweli, hakuna yeyote aliyetubu kwa ajili ya
dhambi za mtu mwingine katika Biblia. Tunaona mifano ya watu wa Mungu wakiungama dhambi za
vizazi vilivyowatangulia lakini hiyo ilitokea tu wakati ule Waisraeli walipopelekwa uhamishoni na
jambo hilo lilifanyika kwa niaba ya watu wa Mungu, na kamwe sio kwa ajili ya wasioamini.

Je, Mungu amewatoa watu wengine au mataifa mengine kutoka katika baraka zake? Hapana, ndani ya
Agano la Kale tunayakuta yaleyale kama yalivyo katika agano jipya. Mungu hulituma neno lake kwa watu
wenyewe na huwainua ili kutubu juu ya dhambi zao wao wenyewe. Wao wenyewe binafsi ndio
wanaopaswa kutubu dhambi zao, ndipo Mungu hujionyesha yeye mwenyewe kuwa yeye ni Mungu
mwenye Neema isiyo na ukomo na fadhili zake na baraka zake hufuatia mara moja! Lakini ikiwa ni watu
wenye kujaa majivuno na kufanya uovu ndipo hujulikana kuwa hukumu inawangojea watu hao. Au ni kwa
kupitia imani, ushuhuda, upendo na utiifu wa watu wa Mungu katika Agano la Kale, ndipo watu huona
kuwa jina la Bwana linatukuzwa katikati ya mataifa na hivyo ndipo wengine hujiunga wenyewe pamoja na
watu wa Mungu, au huja kumwamini. Lakini wazo ya kwamba eti watu wa Mungu wanahitajika kuungama
na kutubu kwa ajili ya dhambi za mataifa yasiyoamini hivyo ndivyo iwe kama utangulizi kwa Mungu ili
aweze kubariki watu hao au taifa hilo, huo ni udanganyifu na ni mambo ya kubuni ya kibinadamu na
wala hayapatikani katika maagano yote mawili ya kale na jipya. Sio hivyo tu bali hata wazo la aina hii
linaweza kunyanganya wokovu wa bure alioununua Yesu Kristo pale Kalvari kwa ajili ya wanadamu.
Mahala ambapo alifananishwa na dhambi zao kiasi kwamba, dhambi zao zikawekwa juu yake na
akazichukua pamoja akafanywa dhambi, ili kwamba tufanywe wenye haki kwa Mungu katika yeye. (Joh.
1:29; Rum.5:8-10; 2 Wakorinto 5:19-21; 1 Joh. 2:2.). Na hii ndio sababu, katika siku hizi za Neema,
Habari Njema inapaswa ihubiriwe kwa watu wote, bure. Tumeambiwa katika sura hii kwamba,
tulipokuwa tungali wenye dhambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu, na kwamba tulipokuwa bado ni
maadui, tukapatanishwa na Mungu, kutokana na kifo cha mwanae. Haya ni maneno ya ajabu ya
wokovu wetu wa bure, ambapo Mungu alipoanzisha hatua ya kwanza, na akazishughulikia dhambi zetu
zote (wakati tulipokuwa tungali ni wenye dhambi), hata kabla hatujazijali au kuzitambua. Sasa kwa nini
basi tunahimizwa kutubu kwa ajili ya dhambi hizi za watu wasioamini ambazo kwazo Kristo alishawafia?
Kristo alizichukua dhambi zetu zote ili kwamba kulingana na mtazamo wa Mungu, haliwi tena ni kizuizi
kwake katika kutupatia wokovu na uzima wa milele. Kwa hiyo inasemwa kwamba Mungu katika Kristo
hakutuhesabia dhambi yetu! Hayo yote ni kwa sababu ya Kalvari, na sasa ni juu ya watu wenyewe
kuiamini Injili na kutubu ili kwamba waweze kujua na kupokea neema hii ya ajabu ya Mungu. Mungu
amekwisha kufanya kila kitu kwa upande wake - kwa jinsi ya ajabu na kwa fadhili zake; sehemu yetu
sasa ni kuiamini Injili na kutubu kwa ajili ya dhambi zetu binafsi na kuutafuta msamaha wa bure katika na
kupitia Kristo. Sehemu yetu sio kuzifufua dhambi za watu wengine ambazo Kristo amezifilia na tayari
amekwisha kupokea upatanisho ili kusudi tuweze kutubu kwa ajili ya hizo na kupokea upatanisho tena!
Kwa kufanya hivyo tutakuwa tumembadilisha Kristo pamoja na kifo chake kwa maombi yetu ya kutubu
kwa ajili ya Taifa!

Au, watu hawa wanatutaka tuamini kwamba Yesu alikufa kwa ajili ya dhambi za ulimwengu mzima, kwa
kila roho ndani yake, bali kwamba kifo chake pale Kalvari hakijatosha kiasi na kile wanachokiita ushiriki
wa dhambi kitaifa!? Kwa maneno mengine hapo wanataka kusema - Kalvari haitoshi kiasi kwamba ni
lazima tutake hii nyongeza maalum maombi ya upatanisho ya kanisa ili kukileta kile wanachokiita wao
suluhisho kwa taifa ambalo Yesu hakuweza kumaliza pale msalabani! Kama hivyo ndivyo ilivyo, basi
tunaona kuwa kuingiliwa kwao kwa ubunifu wao unawalazimisha zaidi kuingia ndani kabisa ya makosa
na udanganyifu. Ni kama ilivyo katika kanisa la Wagalatia - hawasemi kuwa ni Yesu tu, yeye pekee
kasulibiwa kwa wokovu wetu; bali wanasema, Yesu pamoja na kutahiriwa kwa ajili ya wokovu. Kwa
hivyo mafundisho hayo yanasema, Yesu pamoja na kushirikisha kwa maungamo na toba ili kuleta
wokovu kwa watu. Kwa hiyo wamezua wokovu katika hatua mbili - wanasema, ndiyo Kalvari kwa hakika
ni lazima lakini pia unahitaji toba ya upatanisho ili kusababisha suluhu ya kitaifa na Mungu, kabla watu
hawajapokea faida halisi ya Kalvari. Hili ni kosa kubwa sana.

Na iwapo bado, wanasema kwamba maungamo na toba ya dhambi za taifa ya aina hii kwa hakika
hayamsababishi Mungu kusamehe taifa na dhambi zake, bali kwamba inafungua tu njia ya Injili hii ya
neema ili kuwabariki watu. Bado huo nao ni udanganyifu mtupu, kwani aina hii ya maungamo na toba
wala haifundishwi kabisa katika maandiko ya neno la Mungu. Inaharibu tu ukweli uweza na wepesi wa
Injili ndani ya akili za watakatifu na wenye dhambi wote pia; inasababisha kuchanganyikiwa na ushirikina
ndani ya nchi.

7
Lakini wengine wa waandishi wao wanasema kuwa maungamo ya dhambi za kitaifa, na kuomba
msamaha, ina maana kwamba, shetani hawezi tena kuwashitaki watu hao na kwa hiyo hawezi
kuwaweka nje ya neema ya Mungu au kuwazuia kusikiliza Injili! Kwa hakika ikiwa unaweza kusadiki
hivyo, basi unaweza pia kuamini chochote kile! Ni nini? Je, shetani anayo haki ya kuiweka nchi nje ya
neema ya Mungu na kuwazuia kusikiliza Injili mpaka hapo kanisa litakapoungama dhambi za taifa na
kutafuta suluhisho kwa ajili ya dhambi hizo? Hili ni kosa lenye ubaya uliokithiri; hivi kweli hawa walimu
hawajawahi kusikia juu ya Kalvari, na uweza wake! Kwa sababu ya Kalvari, Mungu hawahesabii watu
makosa yao, bali ametia ndani yetu neno la upatanisho (2 Kor. 5:19). Amefungua mlango wazi! Yesu
amefanya njia Kalvari na shetani hana haki ya kuiweka roho nje ya neema ya Mungu, isipokuwa roho
hiyo yenyewe iasi neno la Mungu.

Ni wapi katika Agano jipya ambapo pameonyesha au kufundisha kwamba kanisa linahitaji kuungama
dhambi za mikoa ili lipate suluhisho kwa ajili ya dhambi hizo kabla Mungu hajawabariki kwa neno la
wokovu? Jambo hili linakaribia sana ya kuwa kufuru! Kwa sababu ya kifo chake Kalvari, Yesu anayo haki
kuwabariki na kuwaokoa watu sawasawa na kusudi lake na kadiri ya neema yake!

Sasa tukifuatilia jambo hilo kwa undani zaidi, wanatuambia kuwa eti kwa sababu Daniel aliziungama
dhambi za taifa lake (Daniel 9), kwa hiyo basi, sisi nasi tunahitaji kuungama na kutubu kwa ajili ya
dhambi za taifa letu - hii ni kwamba kwa ajili ya taifa lile tunaloishi, na kwa mji ule unaotuhusu.

Hakuna chochote kile kinachoonyesha kwa uwazi zaidi, kwa jinsi gani watu hawa wanaofundisha hivyo
hata wanavyochanganya mambo ya kimwili na ya kiroho; ulimwengu na kanisa. Namna wanavyosoma
ndani ya maandiko ni mawazo yao, na wala kwa kweli; hawajali kuona kuwa Biblia inafundisha nini juu ya
jambo hilo. Ndiyo, Danieli alikuwa ni Mwisrael, akiomba kwa ajili ya taifa la Israel. Lakini katika Agano la
kale Israel ni watu wa Mungu, na wanawakilisha kanisa. Na Daniel alikuwa ni mtu wa Mungu alikuwa
akiwaombea watu wa Mungu (kanisa). Na maombezi yake yanahusika na agano kati ya Mungu na
watu wake na namna ambavyo watu wa Mungu walilivunja Agano hilo na kupoteza urithi wao. Inafanana
na jinsi ambavyo watu hao wanavyonukuu mistari ya Biblia kama ile Ezekiel 22:30, na wanatuambia
kwamba, hii sasa inahusisha huduma ya kanisa katika kuomba kwa ajili ya dhambi za nchi tunamoishi.
Lakini tena mstari huo huo wa Biblia unamweleza Mungu, akitafuta mtu kati ya watu wake aombaye,
ameumizwa kwa ajili ya hali ya watu wa Mungu (kanisa) na yeye ambaye anajali vyakutosha kuhusu
heshima na utukufu wa Mungu ili aweze kuomba mbele za Mungu kutokana na hali mbaya ya watu wake
Mungu ambao kwao aliwatengenezea agano (mapatano).

Lakini, ili waweze kuyahalalisha mafundisho yao, watu hao wanaitumia vibaya mistari hiyo ya Biblia,
wakiyabadilisha maombi yao kutoka kanisa (ambalo ni watu wa Mungu waliokombolewa kwa agano na
yeye) kwa ulimwengu, kama vile hivyo ndivyo ilivyo au ingeweza kuwa sasa!

Ingawaje tunaweza au kutakiwa kuomba kwa ajili ya jamii tunayoishi, (kama vile 1Timotheo 2:1,2)
-tutaliangalia hilo hapo baadae - katika mafundisho haya, na kile tunachopaswa kukifanya, hakina msingi
wa kibiblia. Hawaupati mfano wote wa mafundisho haya ndani ya agano jipya; na kwa hiyo, wanamnukuu
kwa wingi sana kutoka katika Agano la Kale - lakini baadae tu huishia katika kushindwa katika kuitumia
mistari hiyo, na kwa ujumla kulichanganya agano, na hasa kushindwa kuelewa haswa Agano Jipya
linahusu nini!

Kwa hiyo mmoja wa waandishi wake amesema kuwa, mji na nchi eti vinawakilisha mchanganyiko wa
miili na maendeleo yao kiroho imefungwa kwa dhambi zao. Kulingana na mwandishi huyu, nchi hizo
zimepewa kanisa ili kwamba eti liwawakilishe wao mbele za Mungu na kisha kuwaongoza kwenye
kutubu na suluhisho! Anapozilinganisha nchi na miji anatumia usemi kama vile binti bikira wa Ufaransa
au binti wa New York, analinganisha Ufaransa na mji wa New York. Kwa maneno mengine anajaribu
kutumia maneno ambayo Mungu aliyatumia kwa watu wake aliowachagua, (bikira, binti wa watu , watu
wangu, binti bikira wa Israel) ambaye kwake amemwanzishia agano la uhakika na kwa yeye aliye mkiri.
Na kwa ajili yake mtumishi wake alifanya maombezi. Na mwandishi wao anatumia maneno hayo hayo
kwa nchi na miji ya ulimwengu leo! Kana kwamba leo taifa au mji huo ungeweza kutazamwa kama
vile ndio watu wa Mungu walimotendea dhambi kama ilivyo kuwa katika Agano la Kale; na kana
kwamba kanisa linapaswa kuomba kwa ajili ya mji ule au nchi kana kwamba ilikuwa ni taifa la Mungu
au watu wa Mungu! Inataka kuonekana kana kwamba kanisa linawakilisha manabii ambao huwaombea
watu wa Mungu! Je, taifa la Uingereza au Tanzania linawakilisha watu wa Mungu au kanisa la Mungu?
Na, je kanisa la Bwana leo linapaswa kutenda kama baadhi ya manabii wa Agano la Kale ili kupata
upatanisho kwa ajili ya taifa kwa kuungama na kutubu dhambi zake?! Mambo haya yote ni
mchanganyiko kabisa, na ni upotoshaji na yanalinyanganya kanisa huduma lake la kweli. Kama

8
tulivyosema tayari, matunzo na maombi kwa ajili ya jamii tuishimo ni ya muhimu (yanahitajika) na ni ya
kimaandiko. Lakini tunapaswa kufuata maandiko yanavyofundisha kuliko kufuata upotoshaji huu.

(Upo mstari mmoja katika agano la kale unaoongelea kuhusu bikira binti wa Babeli, Isaya 47:1, lakini hii
inahusu tu mambo ya hukumu na wala sio maombezi! Na kwa hakika, katika mstari wote huo, Babeli
inachukuliwa kama alama ya utawala wa kidunia au shetani, ambapo kwake hukumu ya Mungu itatujilia.
Soma Isaya sura ya 13 na 14 hasa mistari ya 4-24, hii inaweza kuelezea lugha iliyotumika katika 47:1.
Hakika hakuna mahali popote pale katika Biblia ambapo maungamo au toba vimefanywa kwa ajili ya
dhambi za watu wasioamini; Daniel na manabii wengine waliwaombea watu wa Mungu!
Wanalichanganya kanisa na ulimwengu kabisa.)

Ni nini basi, kwa sababu eti mimi ni Mwingereza, kwa hiyo ninawajibika kuungama na kutubu kwa ajili ya
dhambi ya Uingereza, kama Daniel alivyofanya kwa Israel? Ni nini basi, kutubu kwa ajili ya lile ambalo
Waingereza walilowatendea Wajerumani, Waispania, Wamarekani, Wa-Irish na wengine wengi katika
karne hii, halikadhalika miaka 100, 200, 500 na 800 ijayo? Inaishia wapi hiyo? Hii, kwa ujumla ni jukumu
lisilokuwa; wanatufundisha kwamba tunapaswa kufanya utafiti wa kihistoria kwa uangalifu sana na
uchuguzi juu ya dhambi kubwa zote, na matendo yasiyo ya haki ambayo nchi yetu imeyatenda, kwa
sababu, eti tusipofanya hivyo na kuliongoza taifa katika kuungama na kutubu kwa dhambi hizo, basi
hukumu za Mungu itaendelea kukaa juu ya nchi yetu na itazuia baraka za Mungu au uamsho kutujia kwa
kweli. (Jambo hili ni udanganyifu). Na kama tutauliza na kwenda mbali kiasi gani nyuma katika historia,
walimu hawa wanatuambia tunahitajika kwenda nyuma mpaka pale ambapo nchi yetu au taifa letu
lilipoumbwa kwa mara ya kwanza na kugundua maovu yote makubwa liliyokwisha yafanya toka wakati
huo hadi sasa. Kama ni hivyo, eti twende njia nzima nyuma mpaka kwa Adamu na kutubu kwa ajili ya
dhambi zote ambazo mwanadamu ametenda hadi kufikia wakati huu. Hii inaweza kutimiza kosa lao la
hatari na udanganyifu wao wa kufikiri ambao bado kwa namna fulani tungali (kupitia maombi ya
upatanisho) weza kufidia makosa ya wanadamu, ambayo tayari Yesu alikwisha yabeba msalabani! Na
tukiwaachilia mbali watu wa Mungu Israel, kabla ya Kalvari, ni wapi katika Agano Jipya ambapo Mungu
anahitaji taifa zima litubu? Hili ni kosa au hitilafu nyingine na udanganyifu. Kama vile wanafundisha
kwamba katika siku hizo za Injili ya Neema, Mungu anatuhitaji tuzingatie ukombozi wa mataifa kama
mataifa, wanafikiri Mungu anashughulika na mataifa leo sawa sawa na jinsi alivyofanya kwa Israel katika
Agano la Kale! Wanafundisha kuwa eti kanisa linayo haki kutumia damu ya Yesu Kristo kwa dhambi za
mataifa, na wangependa kututaka sisi tuombe kwamba Uingereza kama nchi iweze kupatanishwa na
Mungu kupitia damu yake. Tumekwisha kuona tayari kuwa hakuna kitu chochote kama hicho ambacho
kimefundishwa katika Agano Jipya. Hii si kitu kingine isipokuwa ni matumizi ya kiushirikina ya damu
ya Yesu Kristo.

Hii kwa kweli inaleta upuuzi wa Agano Jipya na ya Injili ambayo ni uweza wa Mungu uokoao roho wa kila
roho na kila mmoja amgeukie Bwana kutoka katika nguvu za giza na kuibatiza roho hiyo iweze kuingia
katika ufalme wa kiroho wa Mungu wa uzima, furaha amani na haki. Hicho ndicho kinachoelezwa na
Agano Jipya - kuzileta roho katika uzima wa Mungu. Lakini nchi au mji hauwezi ukabatizwa katika ufalme
na uzima wa Mungu. Ndiyo, Injili inaweza kuhubiriwa kwa mataifa yote, lakini mafundisho na mafunuo ya
Agano Jipya ni kwamba mtu ataokolewa kutoka katika kila kabila na taifa. Haifundishi wala haionyeshi
kuwa mataifa hayo yataokolewa kama taifa pekee katika siku hizi za Injili kama kwamba Mungu analo
agano na Uingereza au nchi nyingine yoyote ile iwayo kama alivyofanya kwa Israel katika Agano la Kale.

Kanisa siyo ulimwengu; Uingereza siyo Kanisa; na wale wasioamini sio watu wa Mungu - Danieli
aliomba na kuungama kwa ajili ya dhambi za watu wa Mungu, na wala si kwa ajili ya dhambi za
watu wasioamini. Lakini wao wanachanganya yote pamoja.

Paulo hakwenda Mekedonia na kuliambia taifa la Mekedonia kutubu kwa ajili ya dhambi zake na vita
vilivyopita. Hakuwaita maafisa wa Serikali ili watubu kwa ajili ya dhambi za nchi yao au mji wao ili
kwamba kusababisha upatanisho kwa mji huo au nchi hiyo. Alitembelea sehemu fulani fulani katika
Mekedonia na aliwaambia watu waishio humo kuwa wanahitajika kutubu dhambi zao na kumgeukia Yesu
Kristo ambaye ndiye atakayewafanya wawe wenyeji wa nchi nyingine, yaani, mbinguni! Wataweza
kuongezwa katika kanisa la Mungu ambao ndio mwili mmoja. Paulo hakuthubutu kuweza kujaribu
kuwafanya Wakristo wa Mekedonia waweze kusababisha aina fulani ya upatanisho kwa ajili ya nchi yao.

Pasipo kuelewa wanachokifanya au nini hasa wanakisema, wanabadilisha huu wokovu wa ajabu
ambao unawaingiza wake kwa waume wengi katika uzima na uweza wa ufalme wa Mungu wa mbinguni,
kwa mawazo yao ya uanzishaji wa aina ya mambo fulani fulani ya kiinje tu ya kitaifa au ufalme wa
kikirsto.

9
Baadhi ya waandishi wao wanasema, inapotokea mkristo anatubu dhambi za taifa lake aishilo, eti hiyo ni
hatua ya mwanzo tu; kwa ujumla wasemacho hapo ni kwamba unapaswa kuwa na maombezi kama
Daniel ambaye anazitambua dhambi hizi na kisha anamuomba kwa ajili ya taifa, hii pia inapaswa
kufuatwa na ujumla wa kanisa ambalo pia linaombwa kuhusu dhambi hizi za taifa. (Wanadai kuwa hii
ililetwa na Ezra ambaye aliwaongoza watu katika maungano ya pamoja); na jambo la tatu na ambalo,
ndiyo hatua ya mwisho ni pale ambapo jamii au maafisa wa kiulimwengu katika mji ule au taifa
wanaziungama dhambi hizo hizo, na hii pia huwakilisha toba ya kweli ya kitaifa na pia kwamba, kwa taifa
hilo! (Na hii nayo wanasema eti imeletwa na Nehemia katika Agano la Kale ambaye anauwakilisha
ulimwengu au uongozi wa kiserikali!).Wanafundisha hayo ijapokuwa hakuna chochote kile kama hicho
ndani ya Agano Jipya, na kwa ujumla wanalitumia vibaya Agano la Kale katika kusudi lao la kuunga
mkono ubunifu wao. Wakiwa na nia ya kuunga mkono mambo yao mageni, inaonyesha dhahiri kuwa
upotoshaji wao hauna mwisho.

Ni janga la jinsi gani kuona viongozi wa wakristo wengi wakjidanganya wao wenyewe na tena
wakidanganya maelfu ya wengine kwa kufikiri na kufundisha kwamba eti wanasababisha aina fulani ya
upatanisho na kufungua baraka za Mungu kwa taifa lao pale wanapoungana na kutubu dhambi za taifa
lao zilizopita na zilizopo! Waumini wa Kiingereza waende Australia na kuziungama dhambi zilizopita za
waingereza walizowafanyia waumini wa Australia; kadhalika wakirsto wa Australia waje hadi Uingereza
na kuungama dhambi za Australia walizowafanyia waingereza! Wabrazil waje Uingereza, Waamerika nao
waende Japan, na Wajapan waombe msamaha toka kwa wakristo wa Marekani na hivyo kuendelea zaidi
na zaidi! Wakristo wakizunguka ulimwengu mzima wakiungama kwa wakristo wengine dhambi zilizopita
za taifa lao, ambazo kwa hakika kanisa la Yesu Kristo halina chochote cha kufanya kwake!

Enyi Wagalatia msio na akili, ni nani aliyewaloga, ninyi ambao Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele ya
macho yenu ya kuwa amesulibiwa?

Kama tulivyokwisha kuona, hakuna popote katika agano jipya ambapo mkristo anaenda akizunguka kule
na kule kuungama na kutubu kwa ajili ya dhambi za kitaifa za aina yoyote ile. Hatuuoni mfano wa jinsi
hiyo hata mmoja, na wala hayapo maagizo ya kufanya hivyo yalivyoagizwa na Yesu au hata mitume.

Wakristo toka Roma hawapaswi kwenda Mekedonia kuziungama dhambi za Warumi, wala kwa
Waathemi, kwa Wayahudi au kwa yeyote yule mwingine. Waumini toka Mekedonia, Athene, bara la Asia
au sehemu nyingine hawaendi wakizunguka kuziungama dhambi zilizopita za watu wao na kuombana
msamaha kati yao au nchi nyingine hata kama walikuwa na historia ndefu ya mapigano kati yao.
Ujumbe wa wakristo wa kirumi hawakwenda Yudea kuomba msamaha toka kwa wakristo wa
kiyahudi kule! Ni hakika kuwa kulikuwepo na mambo mabaya katika eneo lile, kama vile ilivyo katika
karne hii, lakini ukitazama jinsi ambavyo Yesu Kristo amefanya pale Kalvari, basi kwa kweli ingekuwa ni
ukichaa wao kufanya hivyo, ndio maana haishangazi kuona kuwa hatusemi chohcote cha jinsi hiyo ndani
ya Agano Jipya. Na kama ulitaka kufanya hivyo, utawezaje basi pasipo shaka yo yote kuwa na uhakika
kuwa umeungama dhambi zote ambazo nchi yako imezitenda dhidi ya nchi nyingine? Hata mtaalam wa
historia tu asingeweza kuyaelewa mambo yote ambayo yangeweza kuwa yamemchukiza Mungu.

Kama watu wa Bwana, sisi sote tu wenyeji wa mbinguni, na tunafahamu kuwa vita na matendo yasiyo ya
haki ya nchi tuishimo hayana chochote cha kulifanyia kanisa la Yesu Kristo, lakini bado utaona wakristo
wengi wakizunguka wakiomba msamaha wa wakristo wengine kwa ajili ya dhambi za ulimwengu, kwa
mfano, dhambi za mataifa yao; wakristo hao je wanaumizwa mioyoni mwao kwa yale ambayo nchi
nyingine zimelifanyia taifa lao? Kwa nini basi waumizwe? Tungepaswa kuwasamehe kama vile sisi
tulivyowasamehe iwapo tunaona kuna ugumu wowote mioyoni mwetu. Mimi sihitaji mkristo wa nchi
yoyote kuomba msamaha wangu kwa ajili ya makosa yaliyofanywa na nchi aliyotokea kuishi, wala mimi
au hata kanisa langu hatuwakilishi Uingereza kana kwamba tunao uhusiano wa kiagano maalumu na
Mungu. Ninajua kuwa wao wanafikiri kwa kufanya hivyo watakuwa wanasaidia kuleta aina fulani ya
mapatano, lakini hiyo inaishia tu kwenye maungamo mabaya kiroho na kimaandiko ya Neno la Mungu -
bila kutofautisha kati ya ulimwengu na kanisa. Hii ni tafsiri ya mwili ambayo inakataa kuudhalilisha
ukweli kuwa mimi ni uzao wa kutoka juu, tumezaliwa na Mungu na kwamba wenyeji wetu sasa uko
mbinguni (Philipi 3:20). Nimekombolewa kutoka dhambini na mimi sio wa ulimwengu huu tena, kwa
ufahamu wa ndani na ukweli; mimi sio Mwingereza na wala wewe sio Mtanzania, au Mhehe wala
Mmasai; sisi ni mali ya Mungu (watu wa Mungu). Sitajaribu kujilinganisha na ulimwengu kama vile mimi
ni wake. Hii sio kujifananisha na mahitaji ya wengine, hii ni kuchanganyikiwa, hii ni udanganyifu mtupu.
(Hata kama maelekezo ya dini yanaweza kubeba jina la ukristo, bado kama watabeba uovu na ukatili
watajionyesha kuwa hawana lolote lile mbele ya kanisa la kristo. Na katika mtiririko wa kuhubiri Injili kwa
watu fulani fulani katika maeneo fulani ya ulimwengu, ukweli huu utahitajika kutolewa wazi, lakini hii

10
haihalalishi ujumla wa mambo yasiyo ya kibiblia na ya tabia za ushirikina wa makosa haya ya kisasa.)
Kama tulivyokwisha ona, hatuoni mfano wa aina hii hata mmoja ndani ya biblia yote! Hii haimaanishi
kuwa sisi hatujali au hatuhusiki; la hata kidogo; haimanishi vilevile kwamba hatuwezi kuomba
kwa ajili ya hayo, kwa ajili ya jamii zetu au nchi. Na tutaweza kuona baadaye jinsi kanisa
linavyopaswa kuomba kwa njia za aina gani ili kwamba wale ambao hawajaamini wapate kufikiwa
na Injili! Lakini ulimwengu, na zaidi sana kanisa halisaidiwi kwa mawazo hayo potofu ya kibinadamu,
ambayo yanatumikia tu mambo magumu yasiyofahamika na kuharibu ukweli na uweza wa Injili.

Lakini waumini hao wanaendesha mikutano hii ya maungamo na kutubu, wao wanasema kuwa, eti
wametembelewa kwa macho na wanaamini kuwa eti ni Mungu anayetembea katikati yao na kuguswa
mioyo yao. Lakini wakiwa wakidanganyika kwa kuamini kwao wenyewe. Ndio maana haishangazi kuona
kuwa wanapokusanyika pamoja wanazidi kujidanganya kwa mambo yanayodhihirishwa na kujisikia. Na
kwa hakika hii ni jambo la hatari na sisemi mambo haya kiurahisi rahisi tu. Lakini aina hii ya makosa na
udanganyifu yanapatikana nyakati hizi za Agano Jipya ambapo waumini kwa kutaka kukidhi nia zao na
mawazo yao, kwa kweli kwa kufanya hivyo wanakuwa wanajifungulia wenyewe mlango ili kupokea Injili
ya tofauti, Yesu wa tofauti, na Roho wa tofauti - na wao wanafikiri kuwa hayo ni ya Bwana! Lakini mtume
Paulo anaonyesha hatari ya jambo hili kwa kusema kuwa kwa kweli wanadanganywa na malaika wa
nuru, ambaye mtume Paulo anamlinganisha na shetani (2 Kor.11:1-15). Na hivyo ndivyo ilivyo leo kwa
waumini hawa. Ni waumini, lakini wanauacha ukweli na wepesi wa Injili ya Yesu ambayo
walikwishaipokea hapo mwanzoni. Wanajiweka wazi wao wenyewe kwenye udanganyifu. Haishangazi
kuona kuwa wanaweza wakawa na aina zote za ujuzi ambao utawaendeleza kudanganywa tu. Bali
kujisikia huko wanakojisikia pamoja na kudhihirishwa kwake kunatokana na pandikizo la Injili nyingine na
roho mwingine.

Kaka zangu na dada zangu katika Kristo ninawasihini kwa ajili ya faida ya nafsi zenu ambayo kwayo
Yesu Kristo alikufa Kalvari ili kukomboa na kuwaweka huru na kutufanya tuwe wake mwenyewe:
mjihadhari na mafundisho hayo na madanganyo yake.

Biblia na kile inachosema ni cha muhimu zaidi kuliko shirika lolote kubwa la kikristo au wanenaji.
Haijalishi jinsi gani wanenaji hao wanafahamika au kujulikana. Na kama basi ni bora uchukue mwelekeo
wa Kristo, kuliko kufuata kile ambacho kinajulikana lakini na hakifundishwi katika maandiko ya neno la
Mungu, na kile unachofikiri kuwa kitatueletea umaarufu na kufahamika zaidi.

Ushahidi wa Maandiko Yao

Maandiko ya neno la Mungu kwa uhasa ni kitu gani basi? Je, hawa walimu wanatupatia sisi ili kuonyesha
kuwa kanisa linapaswa kuungama na kutubu kwa ajili ya dhambi (zilizopo na zilizopita) za nchi tuishiyo?
Tumekwisha kuona nukuu fulani kutoka Daniel. Wengine wananukuu mistari inayoonyesha fadhili za
Mungu katika kuwabariki wamataifa kwa wokovu, kama vile, Mwanzo 12:3, Zab. 22:27, Isaya 56:7, Yona
4:11 na Warumi 15: 9. Kwa hakika tungeweza hata kuongezea mistari hiyo na mingineyo inavyoonyesha,
kama vile, kwamba tokea mwanzo Mungu alipanga kuwabariki watu wote katika dunia, lakini hakuna
hata mstari mmoja kati ya hiyo, inayoonyesha kwa namna yoyote ile kwamba watu wa Mungu
wanapaswa kuungama na kutubu kwa ajili ya dhambi za mataifa hayo, kabla Mungu hajawabariki
kana kwamba hiyo ndiyo inayomfungulia Mungu mlango wa kuja kuwabariki! Ingawaje Mungu ameahidi
kupanua wokovu wake kwa watu wote, lakini jambo hili haliwakilishwi ndani ya maandiko ya neno la
Mungu kwa njia ya vifungu vipya vya kisheria kama ile ya pale Sinai na ambayo mataifa yasiyoamini
yanapaswa kuitunza - na kanisa kuombea kwa ajili yao iwapo hawayatunzi! Hapana! Makubaliano ya
Agano Jipya ambayo Mungu anayapanua kwa mataifa yote sasa, ni kwa ajili ya yeyote yule aaminiye,
waume kwa wake wanaokolewa kwa imani katika Kristo Yesu, huru kwa neema ya Mungu. Huu ndio
msingi wa Agano Jipya; toleo la Yesu Kristo ni kwa ajili ya waume na wanawake na ya kwamba, yeye
ndiye aliyesulubiwa na akafufuka ni mlango wa agano hili, wala hayapo kabisa masharti ya kutimizwa
kabla na kubarikiwa kwa wokovu wake.

Hayupo mpatanishi wa agano awaye yoyote yule na wala halipo agano lingine! (Mstari niliyoielezea hapo
juu, haiwakilishi aina fulani ya uhusiano wa agano ambapo Mungu anasema, kwa sababu nimekuahidi
kukubariki wewe kwa wokovu kupitia Kristo tangu milele (Tito 1:2) basi, sasa umo katika uhusiano wa
kiagano na mimi na kutokana na agano hilo kwa kweli huwezi kupokea wokovu kamili mpaka kwanza
nchi unayoishi itakapotubu dhambi zake, zilizopita na zilizopo).

11
Kwa hakika yapo Agano la Kale na Agano Jipya tu. Hakuna lingine! Je, wewe umo ndani ya agano lipi
kati ya hayo mawili? Aina hii ya kuomba kwa ajili ya dhambi za taifa zilizopita ni makosa, baadaye
tutaangalia kwa karibu zaidi, jinsi Mungu anavyotimiza kusudi lake ili kubariki wale wasioamini.

Wanaonyesha vidole kwa Yona, alipokuwa akihubiri kwa watu wa Ninawi, lakini hapo anathibitisha tu yale
tunayoyasema katika makala hii, yaani, ni kwa kulileta neno la Mungu kwa watu wenyewe, ndiyo
inayowapatia fursa kwa imani na toba. Yona aliongea moja kwa moja na mioyo yao na akawaambia
watubu. Nao watu wote pamoja, yaani, mji mzima, walitubu kwa ajili ya dhambi zao. Walitambua na
wakakiri dhambi zao mbele ya Mungu. Yona hakuwaambia kwamba, kwanza watubu katika ujumla wao
kwa ajili ya dhambi za wengine (wenzao waliomo mjini) kabla hajawabariki na kuwasamehe.

Wananukuu Kut.10:16-18, wakisema eti mbona Musa aliwaombea kwa Farao, na kwa hiyo kanisa nalo
linapaswa kujitambulisha na dhambi za taifa na kutubu kwa niaba yao! Ndiyo, ni kweli kwamba, Musa
aliomba kwa ajili ya Farao kwa sababu alizikiri dhambi zake na akamsihi Musa aombe kwa ajili yake.
Hiyo inatofautiana sana. Musa alikuwa hatubu kwa ajili ya dhambi za mtu asiyeamini, na cha muhimu
zaidi kwa wakati huo, Yesu alikuwa hajafunuliwa kuwa ndiye mwombezi kati ya wanadamu na Mungu.
Hivyo ilikuwa ni jambo la kawaida kuona kuwa Farao amsihi Musa ili aombe kwa ajili yake, hasa pale
ambapo Musa alipokuwa akifanya na kuongea kwa niaba ya Mungu kwa ajili ya watu (Ku. 4:16). Kwa
hiyo huu hauwezi kuwa ni mfano wa mafundisho yao hayo, agano lisilosahihi, iwapo wataendelea kana
kwamba Yesu hajafunuliwa kutoka mbinguni kuwa kama mwokozi na mpatanishi wa wanadamu. Hapa
pia tunaona jinsi mafundisho hayo yanavyojaribu kumweka mpatanishi mwingine zaidi ya Yesu Kristo
kati ya Mungu na wanadamu kwa ajili ya toleo la dhambi.

Wanafanya hivyo hivyo, pale wanapotaja kuwa Musa alipokea msamaha kwa ajili ya dhambi za Waisrael
katika (Hes.14:17-21), na wanazidi kutuambia kwamba eti kanisa linaweza kupokea msamaha wake
kupitia maungamo ya dhambi za kitaifa, kwa ajili ya dhambi za mataifa hayo, kama vile Musa alivyofanya
kwa Israel! Hapa wanajifanyia kosa la kidole, wanachanganya tena ulimwengu na kanisa, wala
hawawezi kutambua kama iwapasavyo kutambua kuwa leo yupo mpatanishi mmoja tu kati ya Mungu na
mtu, na huyo ni KRISTO YESU. Tunaelewa kuwa huduma ya Musa ilikuwa ni picha ya kielelezo cha
awali cha Kristo na kwa maana hiyo alikuwa ni wa namna ya pekee kabisa kama tunavyoona katika Kut.
4:16; Hes.12:6-8 na Kumb. 18:15.

Katika Agano Jipya, wanamnukuu Yesu, akimwomba Baba awasamehe wale waliomsulibisha
(Luka.23:34), lakini pale Yesu alikuwa hafanyi lolote zaidi ya lile alilofundisha yeye mwenyewe kufanya.;
kama vile, kuwasamehe wale wanaotutendea mabaya kwa makusudi, hasa pale wanapokuwa hawana
wazo kuwa wanatufanyia ubaya. Ninafahamu kuwa, sisi kama wakristo, sote tumemfuata Kristo katika
hili; lakini hata hivyo hii haiwakilishi ushahidi wa Agano Jipya kwamba kanisa sasa linapaswa
kujishughulisha na kutubu kwa ajili ya dhambi za miji au nchi yao! Zaidi ya kushangaza, ni pale
tunapoona wanamnukuu pia 1Yoh.1:9, tukiziungama dhambi zetu, na wanasema bila woga au hofu
ya Mungu kuwa eti mstari huo unatuonyesha kwamba, kanisa la kwanza lilikuwa linajishughulisha na
Ibada za maungamo ya dhambi za jamii! Wanadai kuwa, wakristo hapo walikuwa wanabeba mila /desturi
za Agano la Kale zilikuwa ni mfano wa pekee kwao walioufahamu na kuusikia! Zile mila ambazo
wanazizungumzia, ni mfano wa pekee wa mtu kama Danieli au Nehemia akiomba wakati ule wa
kutawanywa na kupelekwa uhamishoni kwa Israeli. Lakini hii ilihusiana tu na Israeli na kwa wakati ule wa
pekee katika historia yao! Nini? Baada ya Kalvari na baada ya kumpokea Roho Mtakatifu Wakristo
walikuwa bado hawajapata ufahamu wa ndani zaidi kuliko tukio hili la pekee la Agano la Kale? Hii
inaweza kuwa ni kweli kabisa kuhusiana na walimu hawa wa siku hizi lakini sio mitume wa kanisa la
kwanza. Hii ni aina ya rushwa ya Neno la Mungu na kwamba sisi hatulazimiki kuukubali. Lakini labda
inatosha kusema kuwa, Yohana anatumia uwingi, kama vile asemapo sisi na zetu katika barua zake
zote akimaanisha kuwa, watu wa Mungu - au je, tunapaswa kusema kwamba jamii ya watu wasioamini
wale wanaotuzunguka, wanao ushirika pamoja na Baba na Mwana? (1Yoh 1:3)!!?

Na hii ndiyo baadhi ya mistari yao muhimu sana ambayo kila mara hutolea mifano yao, au kuthibitisha
mafundisho yao. Lakini pia hii inatuonyesha sisi wazi tu kwamba, hata hao walimu hawawezi kutoa
mfano, kwa kweli hapana hawana hata mfano mmoja ambao watu wa Mungu wameonekana sehemu
fulani wakiungama au kutubu kwa ajili ya dhambi za nchi nyingine au kwa ajili ya dhambi za wasioamini
wowote wale. Sasa kumbe tunaona kwa uwazi zaidi hapa kwamba kwa hakika wanakuwa hawapendezwi
na kuelekezwa kutoka katika maandiko ya neno la Mungu katika mambo haya; bali wao wanatumia
andiko lolote lile wanalofikiri kuwa litaweza kutimiza kusudi lao, na iwapo halitimizi kusudi lao, basi wao
hulilazimisha ili liweze kutimiza, kwa kuyumbisha maana halisi ya Neno lile ili kwamba lipate kulingana na
mtindo wa mafundisho yao.

12
Baadhi ya Waraka wa Msingi

Sasa, hebu tuyaangalie mambo ambayo wao huyachukulia kama msingi wa mfumo wao wote wa kufikiri
na kufundisha kuhusiana na habari hii ya maungamo ya dhambi ya kizazi kilichopita. Mstari
wanaoupenda sana kuutumia kama msingi wa mafundisho yao, unapatikana katika Mambo ya Walawi
26:40.

Nao wataukiri uovu wao na uovu wa baba zao (Hapa unatakiwa usome sura nzima wewe
mwenyewe).

Ukitazama kwa makini. Katika sura hiyo, Mungu anatamka hukumu atakayoileta kwa Israel, iwapo tu
kama watakuwa wakirudiarudia kutomtii. Na hukumu ya mwisho itakuwa ni kuwa Mungu atawafunua
wazi kutoka katika nchi yao na kuwatawanyia katika nchi nyingine mbalimbali; lakini hata hivyo, atakuwa
bado na huruma juu yao na kukumbuka agano lake iwapo watatubu na kuziungama dhambi zao (mstari
wa 40-41).

Kwa mapana zaidi ndani ya mstari huu walimu hawa wa kisasa wanajaribu kusimamia na kutengeneza
mawazo ya upatanisho wa maungamo na toba na maungamo na toba ya dhambi za kihistoria, kwa
pamoja, wao wanafundisha kuwa, Mungu kwa hakika eti hawezi kumbariki mtu au taifa mpka kwanza
taratibu hizo ziwe zimekamilishwa. Kama vile kanisa linaongoza njia kuelekea kwenye kuungama na
kutubu kwa ajili ya dhambi za taifa na wanaamini kuwa hii itaweza kusafisha njia kwa maungamo ya
kiulimwengu kwa ajili ya hizo dhambi za kitaifa. Lakini hayo yote pengine hapa hatuna nafasi ya
kuzitazama sababu zake kwa nini iwe hivyo.

Wanawanukuu baadhi ya watu kama mifano ya aina ya maungamo na toba; haishangazi kuona
wanawataja akina Daniel, Ezra, Nehemia na Yeremiah (kama vile katika Daniel 9:;16) ambapo wote
wanazikiri dhambi za mababa zao ndani ya maombi yao. Mstari tulioutaja hapo juu unapatikana pia
katika kitabu cha Mambo ya Walawi pamoja na mifano ya maombi ya watu hao, yanawakilisha jiwe la
msingi la mafundisho hayo hayo. Lakini kwa nini tunasema, haishangazi kuona kuwa wanawanukuu watu
hawa maalumu. Ni wazi kuwa iwapo tutaisoma sura hiyo - Walawi 26 - na mistari hiyo katika mtiririko wa
habari zao, ni wazi kutoka kwa Mungu mwenyewe kwamba aina hii ya maungamo (ya dhambi za pamoja
na vizazi vilivyopita) ingeweza kutokea katika muda maalum ndani ya historia ya Israel, yaani, wakati
Mungu alipowanyanganya na kuwatapanyatapanya mbali katika nchi nyingine, (Walawi 26: 27-42). Hivyo
ndivyo tunavyogundua kwa uhakika pale, tunaposoma sura hiyo na kuiacha Biblia ijitegemee (isema
nasi) badala ya kuitumia ili kuunga mkono mawazo yetu wenyewe tu. Kwa hiyo haishangazi kuona kuwa
hawamnukuu mtu mwingine awaye yote, anayeomba kwa jinsi hiyo kabla ya wakati wa Jeremiah,
(ambaye yeye katika wakati wake, Mungu alikwisha anza kutimiliza hukumu yake dhidi ya Israel, kwa
kuwatapanyatapanya), kwa sababu hakuwepo yeyote alifanya hivyo, kwa kuwa Mungu hakutazamia
hayo kabla ya utawanyo!

Katika mazingira ya namna hii, kukataliwa na kupelekwa uhamishoni, ambavyo vinawakilisha kuvunjika
kwa agano, kungekuwa ni nini tena cha kawaida zaidi ya hii, yaani, Mungu angewataka wao
kutambua na kukiri kama vile kuungama kwa sio tu dhambi za kizazi kimoja bali kule kurudiarudia
na kutokuwa na utii kwa vizazi vingi vilivyoanzia kwa Israel wakifukuzwa kutoka katika nchi yao.
Mungu aliwataka waelewe kuwa hii haikuwa tu adhabu kali na ya ghafla kwa sababu ya kizazi
kimoja; bali kwamba vizazi vingi vinageuza migongo yao kutoka katika toleo la neema yake ya
uvumilivu wao wa muda mrefu.

Iwapo tutasoma Walawi 26 tutaweza kuona namna gani Mungu alivyokuwa mvumilivu na mwenye
rehema kwa Israel. Anawaambia kuwa ikiwa atakataa kumtii na kumfuata, ndipo atatuma aina fulani ya
hukumu juu yao. Kwa nini? Ni kama adhabu tu na laana inayoendelea? Hapana! Tunapoangalia ugumu
wa mioyo yao, Mungu angeweza kutuma hukumu kuwafanya wao wafikirie upumbavu wa njia zao na
hivyo iweze kuwapa fursa ya kutubia dhambi na uovu wao; ili yamkini, waweze kumvumilia yeye. Na
kama watakataa kuchukua tahadhari ndipo atazidisha ugumu au ukali wa hukumu hizo, katika kujaribu
kuwafanya watambue kuwa walikuwa mbali toka Mungu na baraka zake za ajabu. Hivyo, kutokana na
hukumu hizi Mungu alitaka kuona kuwa Waisrael wanarejea katika ufahamu wao kisha kurudi kwake,
kama vile yule mtoto katika Luka 15. Tazama walawi 26:14,18,21,23,27. Katika hayo yote, tunaona kuwa
hukumu zote hizo kwa kweli zilikuwa ni njia ya Mungu ya kuelezea Rehema zake, katika maana ya kuwa
alitaka kutengeneza fursa ya aina fulani kwao ili waweze kujitambua upumbavu wao (upuuzi wao) ili
watambue na watubu na kisha wamrudie yeye.

13
Kwa hiyo tunagundua hapa kuwa , kabla ya wakati wa Uhamishoni, ikiwa ikitokea mfalme yeyote wa
Israel au Yuda pamoja na watu kama vile kizazi kizima chochote, wakatubu na kurejea kwa Mungu ndipo
Mungu aliwabariki na ndipo waliweza kubarikiwa, pasipo maungamo au kutaka kuungama dhambi za
vizazi vilivyopita. (Ijapokuwa ingewezekana kuonekana kama ni jambo la kawaida kuzitaja dhambi za
aina hii kama wangekuwa wamefuta hizo dhambi zao binafsi; sio tu ili kuomba waweze kupata msamaha
zaidi au kuachiliwa, bali tu kama utambulisho wa yale yaliyowahuzunisha kwa hakika, na pengine
yalihitajika kusafishwa kutoka nchi iliyoanza mapema.) Hata hivyo, hatuoni mfano wowote wa aina hii ya
maombi kabla ya mtawanyiko, kwa mfano, nyakati za mfalme Asa, Uzia, Hezekia na Josia. Tunawaona
hapo wakimrudia Bwana pasipo hata kuzikiri dhambi za mababa, na hiyo ndiyo tunayo iona ndani ya
Biblia yote. Hii ndiyo kipimo chenyewe kuwa mtu azitubie dhambi zake mwenyewe, sio za mtu mwingine.
Na ingawaje Yeremiah anaonekana kuziungama dhambi za mababa ndani ya muda huo wa mahangaiko
ya Israel, mzigo wake mkubwa na maelezo ya ujumbe wa Mungu kwa watu wake Mungu kwa wakati huo
ni kwa ajili ya mioyo yao wenyewe, ikiwafunga, ikiwahimiza na kuwainua ili watubu na kumrudia Bwana.

Tukirudia kwenye maelezo ya mwanzoni tunaona kuwa Mungu hakuwatawanya Waisraeli kwa sababu ya
dhambi za kizazi kimoja, bali alichoshwa na vizazi vingi vilivyo mgeuzia mgongo Mungu; na mwishoni
mwake kulikuwa hakuna chochote ambacho Mungu angeweza kufanya, bali ni kuwaondoa katika nchi
kama alivyokwisha kusema. Mungu alimwita Israel, mtoto wake ambaye amemkomboa kutoka Misri
(Hosea 11:1). Naye alifanya agano pamoja nao pale Sinai, walikuwa ni taifa moja na ni watu wake, naye
alijishughulisha nao kama wana wake au kama bibi arusi wake, na alikuwa amewaahidi na akawapa nchi
ya Kanaani kama sehemu ya agano lake pamoja nao. Lakini baada ya kuvumilia dhambi na ibada yao ya
sanamu kwa muda mrefu, ilimbidi Mungu awatoe katika nchi yao. Na kwa kweli jambo hilo lilikuwa na
maana kubwa kwa sababu wao kumiliki nchi ile ilikuwa ni sehemu ya agano ambalo Mungu alikuwa
amelifanya na Israeli na sasa hili agano likawa limevunjwa na Waisraeli kukosa uaminifu. Na sasa baada
ya kuwa wametawanywa nchi nyingine, walipaswa kutambua kuwa kuendelea kwao kukosa
uaminifu kwa vizazi vingi kulikuwa kumepelekea wao kutolewa kutoka katika nchi ya ahadi. Watu
kama Daniel, Ezra na Nehemia (Ezra 9:1-10, hasa mstari 7, pamoja na Hezekiah katika 2 Mambo ya
Nyakati 30:6-9) walitambua mambo hayo, yaani, ilikuwa ni uasi wa mara nyingi wa Waisrael (wakati wa
vizazi vingi) ndio uliowapelekea kwenda uhamishoni. Na kufuatana na Walawi 26, wakaungama kule
kutokuwa na utiifu kwao kwa vizazi vingi. Aina hii ya maungamo ilionekana pia katika Kumb. 30:1-5, 1
Falme: 8:46-50, ingawaje katika sura hizo hatuoni popote wanapotaja maungamo ya dhambi za mababa.

Kwa hiyo, hapa katika Agano la Kale, walichokifanya akina Daniel na wengineo ni kuungama au kukiri
dhambi zilizopita za kisraeli zilizosababisha uhamisho na kutokumilikishwa, ambazo kwa sababu
wanazigundua wao wenyewe. Hata nyakati za Nehemia, Israel na Yuda walikuwa ni watu waliotapanywa
na ile nchi ya ahadi ilikuwa inakaliwa. Kama nilivyokwisha sema, hapo juu, kile tunachokiona katika
nyakati za misukosuko ni kuziungamia sababu ya misukosuko hiyo. Kwa hiyo tunaona kuwa kukiri uasi
uliofanywa na Waisraeli kwa vizazi vingi kulihusishwa haswa na wakati ule Waisraeli
walipotawanywa na kupelekwa uhamishoni, muda ambao waisrael walikuwa hawamiliki nchi. Hata
hivyo, wengine wao waliruhusiwa kurudi. Hii ilifanana na wakati ambapo agano lilivunjwa - agano
maalum lililofanywa kati ya Mungu na Israel, sio kati ya Mungu na mataifa nyingine!

Hebu sasa tulielewe vizuri jambo hili. Kwenye Biblia ndani ya Agano la Kale na Jipya hakuna po
pote pale ambapo watu wa Mungu wanaungama au kutubu kwa niaba ya dhambi za watu
wasioamini za zamani au za sasa, huko vijijini kwao, mjini au katika Taifa ili waweze kupata aina
fulani ya Upatanisho kwa ajili ya nchi. (Tumekwishashughulika na Musa akiomba kwa ajili ya Farao).
Hakuna mfano wo wote, hakuna maagizo yo yote ya kufanya hivyo. Hakuna mahali po pote pale ambapo
watu wa Mungu wanatubu kwa ajili ya dhambi za kizazi kilichopita, iwe kwa ajili ya waaminio au
wasioamini. Hili ni jambo lisilowezekana. Ni katika mazingira ya aini moja tu ambapo Mungu
anawategemea kuungama dhambi za vizazi vilivyopita vya watu wa Mungu na huu ulikuwa ni wakati
wa Uhamishoni na Utawanyiko. Hakuna wakati mwingine wo wote ule wala katika aina yo yote ile ya
mazingira ambapo tunasoma kuwa watu wa Mungu walipodiriki hata kuungama tu dhambi za vizazi
vilivyopita; ili kupata aina fulani ya Upatanisho au baraka. Ukweli huu pekee ni zaidi ya kutosha,
kuonyesha jinsi mafundisho haya ya kisasa yaliyokosewa na jinsi yalivyosimamia katika hila.

Fundisho la Ezekiel: Sura ya 18

Kwa nini Israel walichukuliwa uhamishoni? Je ni kwa sababu tu ya dhambi za vizazi vilivyopita? Je
walikuwa wakiadhibiwa kwa ajili ya dhambi za mababu zao? Mungu akizungumza kupitia Ezekiel katika
sura ya 18 anatuambia waziwazi kwamba walikuwa hawaadhibiwi kwa ajili ya dhambi za mababu
zao! Kupitia Ezekiel, Mungu hasa alikuwa akiwakemea watu wake kwa kufikiri na kusema kitu

14
kama hicho! Kila mtu hubeba hukumu kwa dhambi zake tu. Kama Yuda wangekuwa wametubu na
kumgeukia Bwana na moyo wao wote wakati wa Yeremia, basi Mungu angekuwa amewabakiza na
kuwabariki kama ambavyo alikuwa amefanya kabla - Yeremia 26:1-7, hasa ya aya 3. Lakini ukweli ni
huu, kwamba kizazi kile kiliendelea katika miungu na uasi kinyume na neno la Mungu, kama vile vizazi
vingine vilivyokuwa vimefanya. Ulikuwa ni uasi ulioandikwa wa vizazi vingi, ikiwa ni pamoja na hiki,
kilichosababisha uhamisho.

Lakini hata kwa Israel mwenye kurudi nyuma, Mungu katika wema wake atangaza rehema zake na
kuwataka wamgeukie na warudishwe katika nchi yao, Yeremia 3:12-14. Katika mafungu haya ya maneno
na katika mengi mengine katika Biblia yote, Mungu anasema na watu juu ya dhambi zao na jinsi gani
wazitubie njia zao na kumgeukia. Mungu hataji kamwe toba juu ya dhambi za mababu zao.
Hakuwaamuru kukiri dhambi za mababu zao kama kitu ambacho wangetakiwa kukifanya kwa kawaida.
Kama tulivyoona katika Lawi 26:40, Mungu aliwategemea kuungama dhambi zilizokuwa zikirudiwa na
zilizolundikwa kwa wingi kwa vizazi vingi ambazo zilisababisha wafukuzwe toka nchi ya ahadi. Huo
ulikuwa wakati pekee na kwa sababu maalum ambazo tayari tumezitaja.

Ilikuwa ni watu wa Israel wenyewe waliofikiri vibaya kuwa walikuwa wanabeba uovu wa babu zao -
kwamba walikuwa wanaadhibiwa kwa ajili ya dhambi za baba zao; Baba wamekula zabibu mbichi, na
watoto wakatiwa ganzi la meno. - Ezekiel 18:2. Haya ndiyo maneno Israel walikuwa wanasema, na hata
walibishana na Mungu juu ya hayo katika Ezekiel 18! Mungu hakufurahishwa hata kidogo na mawazo
yao hayo maovu. Na kila kitu ambacho tumekisema hapo juu kinaungwa mkono pia katika sura hii, na
kuwekwa hasa katika muhtasari katika mstari 19-23. Na mstari wa 20 unatangaza:

..Mwana hatauchukua uovu wa baba yake, wala baba hatauchukua uovu wa mwanae...

Na katika sura hii tunaona lile ambalo ni kweli katika Biblia yote, yaani kwamba, kila mtu anawajibika kwa
dhambi yake na anaweza tu kutubu dhambi yake. Hakuna haja ya kutubu kwa ajili ya dhambi ya babu
zetu, kwa sababu hatubebi uovu wao au hata adhabu kwa ajili ya dhambi zao. Katika Biblia hii ndiyo
kawaida kwamba watu watubu dhambi zao, na si za mwingine! Ingawa Yeremia anaungama dhambi za
mababa wakati wa kutawanywa Israel, mzigo uliolemea na kilichokuwa kwenye ujumbe kwa watu wa
Mungu kwa wakati huo ni kwa mioyo yao wenyewe, akiwataka waache ugumu wa mioyo, akiwasihi
waache dhambi yao, akiwakazia watubu na kumrudia Bwana. Haya ndiyo yaliyomo katika huduma yake -
kuonyesha Israel, wakati huo, dhambi na kutangazwa kwa rehema na hukumu ya Mungu. Na tunakuta
hili ni sawa katika Biblia yote. Ukisoma Yeremia na manabii wengine; ukisoma Wamuzi, Wafalme na
Mambo ya Nyakati; ukisoma Agano Jipya; utakuta neno la Mungu huja kupitia watumishi wa Mungu
wakiwasihi watu waliotenda dhambi warudi, au warudi kwa Bwana; neno huja kwa watu wenyewe juu ya
dhambi zao wenyewe, likiwashashiwi juu ya dhambi zao na kuwataka watubu na si kuwataka watubu
dhambi za mwingine awaye yote. Na kwa hiyo tunaona mtu mmoja mmoja na jamii wakitubu dhambi
yao na kupokea baraka za Mungu pasipo kutajwa kwa dhambi za vizazi zilivyopita wakiwa waaminio
au wasioamini! Hii ndiyo hali ya kawaida. Lakini mafundisho haya mapya yanachukua kile kisicho cha
kawaida (kilichohusu wakati wa utawanyiko), inavuruga kabisa, na kufanya iwe kanuni - inafanya iwe
sheria na kongwa kwa watu wa Mungu! Lakini tena katika hali zote hapo juu, tuone kuwa ni swala la
manabii wakiweka mkazo na kuwaombea watu wa Mungu si kwa ulimwengu, si kwa wasioamini.
Je hawa waalimu wetu wa kisasa hupata kutoka wapi mawazo yao hayo? Hasa katika Agano jipya, kifo
cha Kristo pale Kalvari kinashughulikia maisha yetu ya nyuma na kutukomboa toka wakati uliopita 2
Kor.5:17,18; Rumi 6:6; 1Pet 1:18 - tunapomgeukia na kuzaliwa mara ya pili. Msalaba wa Kristo kukatwa
kwetu kutukufu toka dhambi, toka hatia yake, hukumu kututawala katika maisha yetu, na kutoka
kuhukumiwa kote. Ni mahali pa kukatwa toka dhambi za baba zetu hadi mpaka Adamu - na hukumu
zote zinazoendana nazo. Nguvu ya msalaba ni kuu kuliko tunavyofahamu, Efeso 1:16-23. Ni nguvu ya
Mungu kila aaminiye, na hakika hakuna haja au hitaji la kutubu kwa ajili ya dhambi za baba zetu, kwa
sababu kifo cha Kristo kimeshughulikia dhambi zote na hatuwezi kujipatia upatanisho zaidi kwa toba ya
jinsi hiyo - si kwa ajili yetu na wala si kwa mji au nchi tunayoishi. Na dhambi ya mababu zetu na hukumu
kwa ajili yake haiwezi kutugusa kama sisi ni wa Kristo. Tuko huru kwa sababu Mwana ametuweka huru.
Mafundisho haya mapya yanataka tu kuturudisha nyuma kwenye kongwa.

Katika Yeremia 31:29-34, Mungu anasema kitu kilekile ambacho alisema kupitia Ezekiel 18. Mungu
anawaambia kwamba siku inakuja ambapo hawatatumia mithali hiyo tena, ambayo ni, watoto wakatiwa
ganzi la meno kwa sababu baba walikula zabibu mbichi. Mungu alitaka wasiendelee kulaumu vizazi
vilivyopita kwa ajili ya dhambi zao! Sasa Mungu anawaambia juu ya Agano Jipya ambalo anakwenda
kuweka ambapo katika hilo atasamehe uovu wao na asikumbuke dhambi yao tena. Hii ni ajabu na wazi,
lakini akizungumza kuhusu mistari hii, mmoja wa wasomi hawa wa kileo anasema kwamba Kalvari na

15
Agano Jipya haviondoi haja ya kuungama dhambi za baba zetu na zile za miji na nchi tunazoishi ndani
yake! Hata licha ya yaliyosemwa katika 1 Pet 1:18, anafundisha, sambamba na wengine, kwamba wana
na jamii bado wanaathirika na hukumu ambazo zinahusu dhambi za mababa na vizazi vilivyopita na
kwamba kwa hiyo tunaweza tu kujipatia upatanisho kamili na kupata baraka kamili za Mungu kupitia
kutubu dhambi hizi za wakati uliopita!

Msomaji mpendwa, ni nini kinachoweza kufanywa au kusemwa watu wanapompinga Mungu na kweli
yake moja kwa moja. Mungu anasema kitu kimoja nao wanasema,"Hapana si hivyo".

Kutoka 20: 3-6

Sasa tumefikia fungu lingine la maneno ambalo waandishi hawa wa kileo wanalihesabu kuwa lenye
umuhimu wa msingi wa mafundisho yao, si kuhusu kutubu dhambi za kitaifa na za mababu peke
yake, lakini pia kuhusu laana na kile wanachokiita roho za eneo. Sehemu wanayoilenga hasa ni
pale wanapozungumzia dhambi za mababa zikiwafikia wana hadi kizazi cha tatu na cha nne. Toka
fungu hili, pamoja na Lawi 26:40, wanaanzisha usemi mpya ambao haupo kwenye Biblia. Wanaita
dhambi hii, "dhambi ya vizazi". Kwa usemi huu hawafanyi rejea kwenye sheria ya dhambi na mauti
ambayo imekuwa ikitenda kazi katika kila mtu tangu anguko la Adamu, na kwa hiyo Kristo alikufa na
kutusafisha na kutuweka huru. Hapana. Kutokana na fungu hili hufundisha kuwa kama kizazi kimoja
au mtu akitenda dhambi au kuabudu miungu, basi dhambi hiyo na hukumu yake, huendelea katika
kizazi kinachofuata, kwa njia ambayo itazuia baraka za Mungu na kuleta hukumu. Na kwa sababu ya
Lawi 26:40, wanasema kwamba dhambi hizi za vizazi vilivyopita zinatakiwa zitubiwe! Wanasema
mistari hii miwili toka Kutoka na Walawi, inahusu watu wote - Myahudi au Myunani, mtakatifu au
mwenye dhambi - tangu Mungu alipoweka sheria kwa Israel pale Sinai, mpaka siku ya leo!
Wanafundisha pia kwamba Kalvari haijabadilisha hitaji la kuzitubia dhambi za vizazi vilivyopita.
Kama hatufanyi hivyo, basi dhambi za vizazi vilivyopita na hukumu zake, bado zinatuathiri na bado
zinatufanya tukose baraka kamili za Mungu na pia hutupatia msingi wa kisheria wa Ibilisi kufanya
kazi katika maisha ya watu na jamii zao! Lakini yote hii ni tafsiri isiyozekana ya mafungu haya.

Tumekwisha kuona tayari kiasi gani jambo hili ni kosa kabisa na utunzi. Tumeona pia jinsi ambavyo
wanatumia vibaya kabisa Lawi 26:40. Sasa, tunapoendelea kutazama fungu la Kutoka 20, tunakuta
hakuna amri kwa watu wa Mungu kutubu kwa ajili ya dhambi za mababa. Wazo hili wala halijatajwa
katika kutoka 20. Mungu anatangaza kwa Israel kwamba yeye ni Bwana Mungu wao aliyewatoa Misri.
Mungu anawaonya wasiwe na miungu mingine zaidi yake kwa sababu yeye ni Mungu mwenye wivu,
ambaye huwapatiliza wana mabaya ya baba zao hata kizazi cha tatu na cha nne cha wamchukiao.
Nguvu na uzito wa maana ya mstari wa tano (ang. Kumbu. 5:9), iko juu ya hao wamchukiao. Wale
wanaondelea kumkataa Mungu na neno lake kwao, na wanaochagua kufuata dhambi za baba zao. Wale
wamchukiao wamenaswa na kupotoshwa na dhambi za baba yao, na dhambi hii na uasi inaweza kuwa
matokeo na nguvu inayoongezeka kwa kila kizazi kinachofuata na kinachochagua kumkataa - na kwa
sababu hiyo, bila mashaka watahukumiwa. Lakini mtu anaweza kugeuka kutoka dhambi za mababa
zake, na kama atafanya hivyo, Mungu anaweza kumsamehe dhambi zake na kumpokea pasipo hata
kuhitaji kutubu kwa ajili ya dhambi za mababa zake.

Lakini ni muhimu sana pia kutambua kwamba haisemwi kuwa Mungu huleta adhabu au hukumu ya
dhambi za baba kwa wana! Na Ezekiel 18 inathibitisha. Wana hawauchukui uovu au adhabu ya dhambi
za baba zao, isipokuwa kama wamechagua kuendelea katika hizo. Wanapatilizwa dhambi za baba zao,
ambacho ni kitu tofauti. Ni wazi kuwa ikiwa mwana amelelewa na wazazi ambao wanatenda dhambi na
kumwasi Bwana, hapo mwana yu katika hatari ya mvuto wa maovu yao na baraka za Mungu hazipo
katika familia. Kwa hiyo dhambi ya wazazi inakuwa mtego kwa mtoto na bila shaka atajaribiwa kufuata
mfano mbaya, badala ya kumfuata Bwana. Kutoka 20 na Ezekiel 18 zinasimama katika makubaliano
kamili mmoja kwa mwingine katika kutoa kielelezo kwamba watoto wanaweza kuvutwa vibaya na
kunaswa na dhambi za baba zao. Lakini Mungu wakati wote hutuchukulia kama mtu mmoja mmoja na
humruhusu kila mmoja kufanya mwitikio wake mwenyewe kwa Mungu. Kwa hiyo, hata kama dhambi za
wazazi zitakuwa mtego kwa watoto wao, bado wana uhuru wa kuchagua - wanaweza kuchagua kuziacha
njia mbovu za baba zao na kumgeukia Bwana. Hii imewekwa wazi na Ezekiel 18 na pia na kusihi kwa
Mungu akiwasihi Israel tena na tena katika vizazi vyao vinavyofuatana waache uovu wao na uovu wa
baba zao na kurudi kwake kwa moyo wao wote. Hakuwaacha tu watu wake kwenye dhambi za baba zao.
Alilitumia neno lake kwa kila kizazi kupitia manabii wake, akiwataka watu wake wamrudie kuna mifano
mingi ya jinsi hii, kama Isaya 1:18,19. Tunaona pia jinsi ambavyo Asa, Hezekia au Yosia (2 Nyakati 14:29
na 34) walivyoacha dhambi za waliotangulia na kumrudia Mungu, ndipo watu walipobarikiwa sana na
Mungu. Uwepo wa Mungu ulikuwa pamoja nao tena, na baraka na ulinzi wake. Na hakuna wakati

16
tunapoona mmoja kati ya Wafalme hawa kabla ya utawanyiko wakikiri dhambi za baba zao. Walitubu
kwa ajili ya dhambi zao wenyewe, ambazo bila shaka zingekuwa zilezile kama za baba zao - lakini
ilikuwa ni toba yao wenyewe tu ndiyo iliyotakiwa. Na walipofanya hivi, hapo hapo na kwa wingi Mungu
aliwasamehe na kuwabariki. Na haya yote yanaendana na mstari 6 wa Kutoka 20 (ambapo tunaona
kwamba rehema ya Mungu ni kuu mno kuliko hukumu yake kwa wale wampendao na kumtii), na katika
Ezekiel 18, ambapo tunaambiwa kwamba mwana baada ya kufikiria njia mbaya za baba yake, anaweza
kugeuka toka uovu huo na kujinasua kutoka dhambi za baba yake anapomgeukia Bwana, ambaye
atawasamehe kabisa na asiwe na kinyongo chochote naye. Tunapozungumzia uhusiano wa mtu na
Mungu, Mungu haziweki dhambi za baba yake juu ya mtu huyo wala hamuadhibu kwa ajili ya hizo!
Mwana husamehewa na kubarikiwa pasipo kutubu kwa ajili ya dhambi za baba yake! Waalimu hawa wa
siku hizi wanataka tufungiwe ndani ya dhambi za baba na wahenga wetu kwa njia ambayo hata
katika Agano la kale haikujulikana, na kwamba kwa hakika haina uhusiano na Agano jipya.

Sina budi kusema kwamba fungu la kutoka 20:4,5 lina vitu ambavyo si rahisi kuvielezea, na siwezi
kusema kwamba nimeeleza kwa utimilifu. Lakini kwa kuwa Biblia ndicho kitabu peke yake chenye
fafanuzi nzuri kuliko zote juu ya Biblia, tunapoliangalia fungu hili katika mwanga wa mafungu mengine,
ingawa tutashindwa kueleza kwa utimilifu, bado kuna maandiko mengi ya kutosha ambayo yameangalia,
kuona kwamba yale yanayofundishwa na hawa waandishi wa siku hizi, ni kitu ambacho hakifundishwi na
neno la Mungu. Tafadhali rejea kwenye makala ihusuyo Laana kwa ajili ya mafindisho zaidi kuhusu sura
hii ya Kutoka 20.

Msemo wa dhambi ya kizazi umebuniwa na waandishi hawa wa kisasa kwa ajili tu ya kuunga mkono
mawazo yao ambayo si ya kibiblia. Msemo huo haumo ndani ya Biblia; huutumia kuunga mkono mawazo
ambayo hayapatikani ndani ya Biblia. Ni kweli kwamba maisha maovu na mfano wa wazazi na jamii
yanaweza kushawishi na kuathiri wengine ambao wanaendelea kukua, na kwa njia hiyo kama ambavyo
ingesaidia kufanya mioyo yao iwe migumu kwa Injili. Hii ni kawaida na hakuna jipya. Lililo jipya, ni haya
mafundisho yanayosema kwamba anapomgeukia Bwana, na pia kutubu dhambi zake, mtu au jamii
inahitaji pia kutubu dhambi za baba zao au vizazi vilivyopita.

Wanatafuta mifano ya dhambi za vizazi katika Agano jipya! Je, "uthibitisho" wa maandiko ni upi?
Wanadai ni Mathayo 23:32-35 na 1 Thesalonike 2:16! Hutuambia kuwa mistari hii huthibitisha" kuwa
Agano Jipya hufundisha juu ya dhambi ya vizazi na kwa sababu hiyo tunahitaji kutubu juu ya dhambi za
vizazi vilivyopita! Mimi sidhani hivyo. Mistari hii haitufundishi kwamba tunapaswa kutubu juu ya dhambi
za wahenga wetu! Wanarejea kwa wayahudi na jinsi wanavyochagua kupingana na Mungu. Swala si
kwamba wanalazimishwa kuendelea katika dhambi za baba zao, lakini ni kwamba wanachagua kufanya
hivyo. Hii ndiyo sababu Yesu aliulilia mji wa Yerusalemu. Alikuwa anawategemea wampokee lakini
wakachagua kutokumpokea. Hii inaweka msingi wa hukumu yao isiyokwepeka. Mstari mwingine
wanaounukuu kama uthibitisho ni ule wa I Petro1:18. Lakini mstari huu wa ajabu unathibitisha kinyume
na vile wanavyofundisha. Mstari huu unatuambia kile ambacho nimekuwa nikisema katika makala hii,
kwamba damu ya Yesu Kristo, Mwana kondoo wa Mungu, ina uwezo kamili na inatosha kutukomboa
kutoka mwenendo wetu usiofaa tulioupokea kutoka nyuma na kutoka mapokeo batili ya baba zetu.
Tumekombolewa! Tumenunuliwa na kurudishwa kwa damu ya Yesu. Hakuna tena hukumu ya adhabu juu
yao walio katika Kristo Yesu. Mungu Asifiwe! Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu? Mungu
ndiye mwenye kuwahesabia haki! Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye
aliyekufa; naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea! (Rumi 8: 33,34).

Lakini mafundisho haya mapya yangetuletea hukumu sisi sote, yakituambia kuwa si sisi wala jamii
tunazoishi ndani yake tuko huru kikamilifu toka hukumu ya Mungu mpaka hapo tunapokuwa tumetubu
dhambi za baba zetu! Hili si jambo la kushangaza. Kwa sababu kama ukimleta mtu chini ya sheria, mtu
huyo hana budi kuwa chini ya hukumu. Na hii ndiyo asili ya mafundisho haya.

Wanachanganya Kanisa na Ulimwengu

Ingawaje ni kitambo cha vizazi vingi, bado historia ya Waisrael inachukuliwa kama ni Mungu alikuwa
akishuhgulika na mtoto mmoja mmoja. Ni taifa moja pekee na historia moja. (Kanisa ni mwili mmoja
kiroho lakini linahusisha makanisa madogo madogo ya aina nyingi katika maeneo mengi mbalimbali
pamoja na watu wake, wanaotokea katika mataifa mengi ya aina mbalimbali. Na hii bila shaka
haishirikishi historia ya aina moja au maendeleo ya kiroho, kama ilivyo katika Agano la Kale - tazama
nyaraka za Agano Jipya na Ufunuo sura 2-4.)

17
Sasa, ikiwa yeyote yule kama Akani (Joshua 7:1) au Sauli (2 Samweli 21:1) alifanya dhambi, hii
ingeweza kuleta madhara kwa wote, watu pamoja na baraka za Mungu zingezuiliwa. Tena hayo
mafundisho yao mapya yanasema, Haya, unaona, kwa sababu watu hawa walifanya dhambi, Mungu
alizuia baraka zake hivyo tunahitaji kutubu dhambi za nchi yetu! Lakini kwanza, nchi yetu ipo mbinguni,
na pili nyaraka hizo hazitufundishi eti kanisa linapaswa kuungama na kutubu kwa ajili ya dhambi za
ulimwengu, kama vile nchi tunamoishi. Kinyume chake kwa urahisi tu, inamaanisha tu kuwa, iwapo watu
wa Mungu wakitenda dhambi watapata madhara katika maisha yao au katika maisha ya kanisa (Rumi 8:
13, 1Kor 5:6, Ufunuo 2:5), na kama tulivyokwisha tangulia kutaja hapo juu. Agano Jipya linatofautiana na
Agano la Kale, ndani yake kiasi kwamba, watu waliochaguo la Mungu katika Agano la Kale,
wanawakilishwa na taifa moja linalojulikana na historia yake ni moja wakati ambapo, kanisa la Agano
Jipya linahusika na watu wengi wa aina mbalimbali katika maeneo mengi mbalimbali.

Hawa walimu wanataka kulinganisha na dhambi ya Akani - jinsi dhambi ya mtu mmoja inavyoweza
kuidhuru jumuia nzima. Akani alikuwa ni mmoja wa watu wa Mungu na alifanya dhambi; dhambi yake
iliwanyima waisraeli - watu wa Mungu - ulinzi wa Mungu na baraka zake. Je, sasa wanataka
kutufundisha kwamba, ikiwa mkristo atatenda dhambi sehemu nyingine ya ulimwengu kwenye kanisa
fulani, ndipo Mungu huzuia baraka zake kwa wakristo wote ulimwengu mzima, hadi pale wote
watakapogundua nani aliyetenda dhambi hiyo, na kisha kanisa lote ulimwenguni kote litubu kwa ajili ya
dhambi ya mtu huyo? Kama ni hivyo basi, kanisa lote ulimwenguni kote litahitaji kujua na kutubu kwa ajili
ya dhambi alizokuwa akizitenda mkristo mmoja mmoja au anazozitenda, kabla hatujaweza kuishi katika
baraka zake Mungu. Mpendwa msomaji unaweza ukaona wewe mwenyewe, matatizo
yanayosababishwa na hayo mafundisho yao, jinsi yanavyojaribu kupindisha maana ya maandiko ili
kukidhi mawazo yao.

Wanachanganya mafundisho ya Biblia yahusuyo kanisa na ulimwengu. Na wala haupo mfano wowote
katika Agano Jipya ambapo kanisa likiomba kwa vizazi vingine vilivyopita; na wala haliwakilishwi na nchi
yoyote iliyopo duniani. Kanisa linahusu Roho iliyookolewa kutoka katika kila koo za makabila na mataifa.

Sasa katika makala hii nimekuwa nikitumia maneno mawili: kuungama na kutubu, kwa sababu
maneno hayo yote mawili yamekuwa yakitumiwa kwa uhuru sana katika mafundisho haya ya kisasa kana
kwamba yangeweza kutumika katika mazingira yale yale, lakini mmoja wa waandishi wao wenyewe
anakubali wazi wazi na kwa usahihi, kwamba, hakuna njia yoyote ambayo watu wowote wa Agano la
Kale kama vile Daniel au Nehemia, kwamba wangeweza kutubu kwa ajili ya dhambi za vizazi vilivyopita.
Huwezi kutubia uovu wa aina yoyote ile ambao hujahusika nao. Kwa sababu toba ni badiliko na kugeuka
kutoka katika uovu ulioutenda. Kwa hiyo, ingawa je, Daniel angeweza kutubu kwa ajili ya dhambi yoyote
aliyoitenda, lakini yeye asingeweza wala asingetubu kwa ajili ya dhambi za baba zake. Ndiyo,
asingeweza, kwa sababu, kwanza hazikuwa dhambi zake mwenyewe, (aliungama na kutubu kwa ajili ya
dhambi zake yeye mwenyewe, hata hivyo, dhambi za kumwasi Mungu hazikuwa zake). Na pili, hakuna
njia yoyote ile ambayo mtu yeyote anaweza kupokea msamaha toka kwa Mungu kwa ajili ya watu ambao
wamekufa. Hivyo kwa kweli ingeweza kuwa ni unajimu na matendo ya tabia zisizo za ki-mungu.

Sasa, ijapokuwa walimu hawa wanaweza kukubali kuwa ni kweli, lakini bado katika yote mawili, yaani
ndani ya maandiko yao pamoja na mahubiri yao, wanazungumzia kutubia dhambi za baba zetu, (jambo
ambalo haliwezekaniki), au kuimwagia damu ya Yesu katika dhambi za mji au taifa na hapo hapo eti
upokee upatanisho kwa ajili ya watu wa hapo (hii ni unajimu kama sio kufuru). Hakuna maombi yetu
yoyote ambayo yanaweza kusababisha msamaha toka kwa Mungu kwa ajili ya watu waishio au
waliokufa. Na bila shaka hatuwezi kuitumia damu ya mwokozi wetu kwa njia ya jinsi hiyo. Damu yake
Yesu sio aina fulani ya Hirizi.

Sasa yale ambayo bila shaka tunaweza kuona Daniel pamoja na wenzake wangeweza kuyafanya ni
kuumizwa juu ya dhambi za watu wa Mungu wanaomhusu. Upendo wake kwa Mungu na kwa watu wa
Mungu kwa kawaida ungeweza kumpelekea kuumizwa sana, pale aonapo kwamba Waisrael
wamemwasi Mungu, na kwamba watu wa Mungu wao wenyewe wameondolewa utajiri wa baraka zake.

Isitoshe, ule ufahamu wetu wa umoja pamoja na watu wa Mungu, ungeweza kutupelekea kuumizwa na
kujinyenyekeza wenyewe mbele za Mungu, inapotokea kanisa haliishi tena katika urithi wake ambao
Kristo Yesu alinunua kwa ajili yetu pale Kalvari. Badala ya kulihukumu kanisa, tunapaswa
kujinyenyekeza wenyewe na kuiomba rehema zake zitusaidie wakati wa uhitaji na kwa hakika hii
inaweza pia ikajulisha kuungama mambo mengine kama yalivyosababisha hitaji hili kubwa katikati yetu.
Kwa kweli, Roho wa Kristo atatuongoza katika hiyo (Rumi 8: 26,27, Efeso 6:19), lakini hii haifanani
kabisa na kutubu kwa ajili ya dhambi za wengine. Mtume Paulo aliwaombea watakatifu (Wagalatia 4:19)

18
bali yeye hakutubu kwa ajili ya dhambi zao. Alitafuta Bwana kwa ajili yao, lakini baadaye alihakikisha
wazi kabisa neno la kweli linawajia ili kuwaongoza wamrudie Kristo.

Kwa hiyo tunaona kwamba, kuungama na kutubu kwa ajili vizazi vilivyopita hata katika Agano la Kale, ili
watu waweze kuzichukua baraka za wakati huo, hakufanywi na watu wa Mungu kwa niaba ya watu
wasioamini - katika miji au taifa. Halikadhalika, aina hii ya maombi, hayakuwa na kawaida kwa watu wa
Mungu, wanapozifikiria dhambi zao wenyewe, bali aina hii ya maungamo ilikuwa inalingana tu na wakati
wa kuondoshwa kwa Waisrael na uahmishoni na inahusu Israel tu, kwa sababu ya agano zuri na Historia
yake nzuri ya matendo alivyojishughulisha nayo kwao kutokana na Agano hili. Na pengine, lililo la maana
zaidi ya yote, ni hili kwamba, aina hii ya maungamo ya dhambi za vizazi vilivyopita yalifanyika kabla ya
kifo na ufufuo wa Kristo Yesu pale Kalvari, ambaye yeye pekee ndiye mpatanishi kati ya Mungu na
mwanadamu, kwa kuwa yeye ndiye amezichukua dhambi za wanadamu wote kwa yeyote amwaminiye
(1 Yoh 2:2).

Mafundisho haya mapya yanawakilisha kitu fulani cha tofauti kwa ukamilifu wa Neema ya Mungu
ambayo imeelezwa katika kumhubiri Kristo na kuwa yeye pekee ndiye aliyesulubiwa.

Agano na Mataifa?

Kuna jambo lingine ambalo itakuwa ni vema ni kulielezea kutoka katika maandiko. Tayari tumekwisha
taja kuwa wangetutaka sisi tuamini kwamba, tunapaswa kuomba kwa ajili ya miji na nchi tuishimo
(ulimwengu) kama vile Daniel alivyofanya kwa Israel (watu wa Mungu). Na kwamba Mungu alikuwa na
maagano na mataifa ambayo yaliruhusu aina hii ya maombi; wanawezaje basi, kuruka namna hii, toka
kwa watu wa Mungu hadi kwa watu wasioamini? Wao wananukuu mistari kama Kumb.32:8 ambao
unasema kwamba Mungu, alipowapa mataifa urithi wao, alipobagua wanadamu, na hii inarejea
kwenye migawanyiko ya kijiografia katika dunia. Sasa haya mafundisho mapya yanasema kuwa Mungu
angeweza hayo tu kwa misingi ya agano la kisheria na mataifa hayo na kwa hiyo wao pia walikuwa au
wanaweza kuwa na uhusiano wa Agano na Mungu kama Israel walivyofanya nyakati za agano la kale, na
kwa hiyo kanisa linaweza kuomba kwa ajili ya dhambi zilizopita na nchi wanayoishi? Inaonyesha kuwa
huu udanganyifu haufahamu mipaka ya upotoshaji wa kweli! Yesu Kristo alileta jipya ili kuliondoa la kale
(Heb. 7:12, 18,19,22; 8:13; 10:9). Lakini walimu hao wanaanzisha maono ya kale yao wao wenyewe, na
hatua yake inalichana jipya. Oho! Enyi wagalatia msio na akili, ni nani aliyewaloga? Hayo yote kwa
kweli ni ubunifu wa ushirikina.

Tumekwisha ona kuwa maungamo ya Daniel yalihusu na uasi wa kurudiwa na Israel kinyume na Mungu,
kinyume na mafunuo yake, maalum ambayo aliwapa; pia ni kinyume na agano ambalo alilifanya maalum
kwa ajili yao kupitia Abrahamu na pale Sinai. Agano hilo haliendi sambamba na taifa lolote katika
maandiko. Mungu amepanga na kuahidi zaidi na sio tu mgawanyiko wa urithi wa dunia hii. Kwa fadhili
zake Mungu amepanga kwa ajili ya wokovu wa watu wote watakaomwamini kutoka kwa taifa au kabila la
jinsi gani lolote lile watakalo. Hii ni uwazi wa ajabu kutoka katika maandiko ya neno la Mungu na
tunafurahia katika hilo kwa mioyo yetu yote! Lakini hamna popote ambapo Mungu hata anapopataja,
achilia mbali kuwataka, wakristo au yoyete yule ahusike katika hatua za ushirikina huo wa kuungama au
kutubu kwa ajili ya dhambi za kitaifa za vizazi vilivyopita, kana kwamba hiyo inaweza kutupatia baraka za
Mungu na wokovu kwa ajili ya miji na nchi yetu.

Ni wazi kabisa kutoka katika Neno la Mungu, kwamba Mungu ametupatia baraka na wokovu kwa watu
wote kupitia kifo cha mwanae pale Kalvari. Tunaweza kuomba kwa ajili ya kueneza Injili ili kwamba watu
wapate kusikia ujumbe wa Kristo na kwamba yeye kusulubiwa ili wapate kumgeukia toka katika dhambi
zao, ambazo kwa uhuru kabisa atawasaheme.

Ule mstari halisi ambao mwandishi wao mmojawapo anaunukuu, kutoka katika Kumb. 32:8 pia
unanukuriwa na Paulo Mtume katika Matendo 17: 24-31 (mstari wa 26). Hapa Paulo Mtume anaongea
na watu wa Athene kuhusiana na ibada ya miungu yao. Hawaambii kuwa laana ya Mungu iko juu yao
kwa sababu ya Kutoka 20:5, na kwamba wanapaswa kutubu kwa ajili ya ibada ya miungu yao uliopita
kabla ya kubarikiwa na Mungu. Hapana, hasemi hivyo, isipokuwa anawaambia kuwa Mungu aliweka
mipaka ya nchi yao ili kwamba watu wapate kumtafuta Bwana (mstari wa 27). Hauelezi chochote
kuhusu uhusiano wa agano kutoka katika agano la kale, ambalo sasa linawahitaji wao watubu
dhambi zao nyingi zilizopita za miji na nchi ya Athen, vita vyake, na ibada ya sanamu yake! Hapana!
Isipokuwa yeye badala yake anawaambia kuwa, Mungu alifanya kama haoni katika enzi za ujinga
wao, lakini sasa anawaagiza watu wote watubu. Ndipo anaanza kuwaelezea kuhusu Yesu na ufufuo
wake.

19
Inafanana pia na katika Matendo 14:16, ambapo watu wa Listra walitaka kumtolea dhabihu Paulo na
Barnaba, wala Paulo hakuwakaripia na kuwaambia kuwa walikuwa chini ya laana ya Mungu, kwa sababu
ya ibada ya sanamu yao mbaya na hivyo walitakiwa watubu dhambi za mababa zao kwanza, kabla
Mungu hajawabariki wao bali pamoja na nchi yao; Hapana! Aliwaambia kuwa yeye alikuwa ni mtu kama
wao, na kwa uwazi kabisa lakini kwa fadhili aliwahitaji wageuke na kuyaacha mambo hayo ya ubatili
wamrudie na kumwelekea Mungu aliyehai, ambaye Mtume Paulo anasema .ambaye zamani
zilizopita aliwaacha mataifa yote waende katika njia zao wenyewe, lakini hakujiacha pasipo
ushuhuda; kwa kuwa alitenda mema akiwapa mvua kutoka mbinguni, akiwashibisha mioyo yenu
chakula na furaha. Hii ingeweza kuwa ni fursa ya pekee kwa Mtume Paulo kuweza kuhalalisha
mafundisho haya mapya; lakini badala yake, hafanyi chochote cha aina hiyo, wala hazunguki huko na
huko akihubiri laana na hukumu kwa sababu ya dhambi za vizazi ambavyo watu wanahitaji kuungamia
na kutubuia; mpendwa msomaji wangu; tafadhali angalia jinsi ambavyo maandiko ya Neno la Mungu
yanavyowakilisha karibu ni kinyume kabisa cha picha halisi ya yale mafundisho wanayoyatengeneza
wao.

Katika mipangilio ya kuhubiri Injili, Mungu haweki majukumu yoyote juu ya taifa kwa ajili ya dhambi za
vizazi vilivyopita (Rumi 3:24). Kwa kweli Mtume Paulo anasema, Mungu alifanya kama haoni katika
nyakati zao za ujinga, ni vema kuliko kuongelea kuhusu ujumla wa mibaraka za Mungu ambazo kwa
fadhili zake Mungu ameendelea kuzitoa chini ya nyakati zote kwa watu wote.

Na hii haishangazi kwa sababu kinyume na hayo mafundisho yao mapya, Mungu hajajifunua mwenyewe
kwa namna ya pekee kwa mataifa kabla ya Kristo, kama alivyofanya kwa Israel. Hajafunua kwa mataifa
haki yake na tabia yake takatifu kupitia sheria zake za manabii, na alijitokeza kwa mafunuo maalum.
Hajalianzisha agano pamoja nao, ambalo kwa hilo sasa aweza kuwahukumia. Hapana, mbali ya
kutambua uasili ambao unapaswa kuwa ndani ya moyo wa mume na mwanamke, kumhusu Bwana wao
(Rumi 1: 19,20), kimsingi, walikuwa hawajapata mafunuo maalum kuhusiana na tabia ya haki yake na
matakwa ya haki yake; na kwa hiyo Mungu kwa ujumla alikuwa hawakabi kuhusika na yaliyopita (yeye
aliyepewa machache, machache yatahitajika) kinyume chake, anaendelea kuwa mwema kwao na
anawabariki. Lakini kama Mtume Paulo alivyosema, sasa anawaagiza wote watubu dhambi zao wao
wenyewe, na kumrudia Mungu aliye hai! Haleluya! Hii ndiyo Injili!

Mstari maalum wanaoutumia ili kufunga mkono mafundisho (Kumb. 32:8), unanukuliwa na kuelezwa na
Mtume Paulo, kufundisha kinyume cha mawazo yao!

Wanasema unapaswa kuungama na kutubu kwa ajili ya dhambi za nchi yako kwa sababu eti ya
uhusiano wa Agano (!?) kati ya Mungu na nchi ile, kabla Mungu kwa hakika hajakubariki wewe na nchi
yako. Mtume Paulo anasema kuwa, Mungu alijua kuwa mataifa yalikuwa katika ujinga kwa tabia yake na
haki, na kwa hiyo katika wema wake na rehema yake alifanya kama haoni, zilikuwa ni kama vizuri kwao,
lakini kwa sasa anawaagiza wote kutubu, kwa sababu ya wokovu unaotolewa katika Kristo Yesu!

Hii ndiyo neema, maajabu na wepesi wa Injili. Hebu tuipokee hazina hii, tuitunze na kuitangaza.

Sasa tunaweza kuona jinsi wanavyofanya makosa makubwa. Msingi halisi wa mafundisho yao
umesimikwa juu ya makosa ya kuwabadilisha au kuwachanganya watu wa Mungu na wasioamini.
Wanawajali wenye dhambi na wasioamini kana kwamba ni watu wa Mungu waishio chini ya Agano la
Kale ambapo kanisa linapaswa kuomba kwa ajili ya ulimwengu kama vile Danieli alivyofanya kwa ajili
ya Waisraeli! Kwa hiyo wanatenda makosa mawili makubwa na ya kumsingi. Kwanza, wasioamini sio
watu wa Mungu waliokombolewa na hawawezi kutendewa au kuhesabiwa kama hivyo katika mahubiri
au kuomba (ijapokuwa kwa vyo vyote vile tunapaswa kuomba na kuihubiri Injili kwao). Jambo la pili, Yesu
Kristo alipokufa pale Kalvari alilia Imekwisha! Hii ililijumlisha na Agano la Kale. Imekwisha, kwa kuwa
Kristo ametukomboa kutokana na sheria (Rum 7:6). Torati na manabii vilikuwapo mpaka kipindi cha
Yohana, lakini sasa Ufalme wa Mungu unahubiriwa (Mt 11:12,13; Luka 16:16) au angalau ingekuwa hivi.
Hatupo chini ya Agano la Kale tena, lakini hapo ndipo wangependa kutuweka sisi kama wangeweza
kufanya hivyo! Mbaya zaidi, yale wanayoyafundisha ni mtindo wa uchafu wa Agano la Kale. Tumekwisha
kuona jinsi ambavyo mafundisho yao yote yalivyo; yanapatikana kutokana na tafsiri yao wenyewe ya
kitabu cha Kutoka 20:3-5 na Walawi 26:40. Je huo ni ufunuo wa Agano Jipya? Hapana!

SEHEMU YA PILI

20
Tukiangalia kwa makini maandiko yasemavyo:

Injili

Kama vile ilivyokuwa huko Galatia, vivyo hivyo leo mafundisho ya aina hii yanapora mahubiri ya
Msalaba, uweza wake na utimilifu wake. Hii ni kasoro ya aina ya kizamani sana ni ya kienyeji. Inapotosha
ukweli wa Injili, na inaturudisha nyuma hadi kwenye mtazamo wa aina ya Agano la Kale; wakielezea kwa
jinsi hiyo, kwa uhakika, inawakilisha mashambulizi dhidi ya Injili ya Kristo na kile alichokipata pale
Kalvari. Inatuondolea mtazamo wetu mbali na Kristo na inalikuza Agano la Kale. Hali kadhalika inafunua
ukosefu wa ufahamu wa kile kilichomo ndani ya Agano Jipya. Ili kuonyesha kuwa hivyo ndivyo ilivyo,
litakuwa ni jambo la faida kwetu sasa iwapo tutayatazama maandiko yanasema nini juu ya baadhi ya
mambo haya. Tumekwisha onyesha wazi kuwa Agano Jipya halina hata mfano mmoja wa aina hii mpya
ya mafundisho.

Hebu basi tuone katika Agano Jipya linatufundisha nini katika 2 Kor 5:19, tumesoma kuwa,

Mungu alikuwa ndani ya Kristo, akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake, asiwahesabie makosa
yao

Warumi 5:8 inasema, ...bali Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo
alikufa kwa ajili yetu tulipokuwa tungali wenye dhambi.

Waefeso 2:11 nayo inatuambia, akawapatanisha wote wawili na Mungu, katika mwili mmoja kwa
msalaba, akishaufisha ule uadui kwa huo msalaba. Akaja akahubiri amani kwenu ninyi mliokuwa mbali,
na amani kwao wale waliokuwa karibu.

Hii ni mistari ya thamani na ya muhimu, kwa sababu inafunua moyo halisi wa Injili, msingi wa wokovu
wetu na neema ya Mungu ya ajabu kwetu sisi katika Kristo Yesu. Tulipokuwa bado tungali wenye
dhambi, kabla hata hatujaweza kufikiria juu ya Mungu au kujali juu yake au hata juu ya amri zake, kabla
hatuja mkaribisha kwa njia yoyote ile; yeye mwenyewe Mungu Baba, kupitia mwanawe Yesu, alikusudia
kutujia na kwa niaba yetu kupokea msamaha wa dhambi hizo katika maisha yetu na kuziondoa hukumu
zake juu ya maisha yetu kwa ajili ya hizo dhambi zilizopita, (Rumi: 3:24-28). Hivyo ndivyo alivyofanya
pale Kalvari. Pasipo gharama yoyote alizichukua dhambi zetu na kuziharibu nguvu zake. Hili halikuwa tu
ni wazo la baadae isipokuwa hayo yote yalitokea kulingana na kusudi lake la milele na kufurahishwa
kwema kwa nia yake. Mungu asifiwe!

Mungu alitimiza yote kwa niaba yetu pasipo hata kutaka tulipe gharama (ni bure). Ni kwa neema, na kwa
sababu ya neema ya Mungu, watu wanasamehewa na kuokolewa. Ilifanywa kwa ajli yao, hata walikuwa
wafu katika makosa na dhambi, (Efeso 2:4-9). Na sasa Mungu huwapa haki watu wasio wanyofu kwa
imani peke yake (Rumi 5: 4,5). Na pasipo hata kujitahidi kwa watakatifu wenyewe ili kujaribu kupata
msamaha na upatanisho kwa ajili ya wenye dhambi, miji au Taifa; kwa kutubu kwa ajili ya dhambi zao.
Kwa maneno mengine, pasipo hata kuwataka watakatifu kuongezea chochote kile juu ya neema na kazi
za Mungu aliyoipata pale Kalvari kupitia Kristo!

Tumekombolewa kutoka katika mwenendo usiofaa ambao tuliupokea kutokana na mila na desturi
za mababa zetu, kupitia damu ya thamani yaa Yesu Kristo; hapa sio kwa kupitia maombi ya
watakatifu wala maungamo yao, (1 Petro 1:18,19). Hatuoni haja yoyote ya kuendelea kuzichambua
dhambi zilizopita, yaani za mababa zetu ili kwamba sisi tupate kupokea wokovu huu kamili na ili tupate
kuwa huru kabisa! Ni nini au ni nani atakayetuhukumu, atakayetushitaki, au kutuweka katika
vifungo? Je, ni dhambi za mababa zetu? Hapana! Damu ya Kristo imetukomboa! Kwa maana damu
ya Kristo imetufaa kabisa na ni kwa wakati wote; na wokovu wake upo wazi na ni kamili kwa yeyote
atakayetubu na kuamini. Baadhi ya hao walimu wao wa kisasa wanasema kuwa, eti mstari huu
unaopatikana katika Petro wa kwanza unathibitisha mawazo ya dhambi za vizazi, na kwamba, kwa hiyo
sisi twapaswa kuungama na kutubu kwa ajili ya dhambi hizo za mababa zetu! Lakini katika sura ile, Petro
hawaelekezi kufanya jambo lolote la aina ya mawazo yao hayo. Ni wapi basi anapokazia hitimisho lake,
kwamba tunapaswa kuomba kwa ajili ya hilo, na kutubu kwa ajili ya dhambi za mababa zetu? Kwa
hakika, hapo anatufundisha kinyume kabisa cha dhana ya mapokeo yao. Yaani, hapo anatufundisha
kwamba, damu ya Kristo imefanya kazi yake, ametukomboa sisi kutokana na mila na desturi za mababa
zetu. Kwa hiyo, mapokeo na maelekezo yao, kwa hakika ni mapokeo yanayoendeleza mashambulizi juu
ya utimilifu wa uhuru ambao Mungu ameutoa katika huyo Kristo kwa ajili ya wanaume na wanawake
wote.

21
Ukweli huu, uhusuo wokovu wetu kamili unafafanuliwa vizuri zaidi katika Warumi 5:15-21, ambapo
tunasoma kwamba, dhambi na hukumu iliyowajilia watu wote kwa sababu ya Adamu wa kwanza, sasa
kwa Kristo ambaye ndiye Adamu wa pili ametuondolea pasipo malipo yoyote; bali ni kwa kifo chake pale
Kalvari, akitupatia msamaha na haki kwa wote watakaomwamini. Kwa maneno mengine, tungeweza
kusema kuwa dhambi zao zote zisingeweza kuwashikilia kwa kuwa Kristo amewaondoa mzigo wa
uwajibikaji kwa ajili ya hilo, kama vile Isaya anavyotutaarifu, katika ile sura ya 53. Na hii ndiyo maana
halisi ya 2 Kor 5:19.

Hii ni habari njema ya Injili na sasa wanaume kwa wanawake wanaitwa ili kuziamini habari njema hizi
na kugeuka kutoka katika dhambi zao. Imani hii ndiyo wokovu wao; kwa sababu hiyo tunasoma kwamba,
Mungu alikuwa ndani ya Kristo, asiwahesabie makosa yao (kwa vile yeye mwenyewe angeyaondoa).
Kwa hiyo, Yesu alimwambia mtu yule aliyepooza ambaye alipelekwa kwake kwa ajili ya kuponywa, (kama
ilivyo katika Injili ya Luka 5), kwamba, dhambi zake zimesamehewa pasipo malipo (bure) kwa sababu tu
aliamini. Katika Injili ya Yohana sura 8 anamwambia mwanamke aliyefumaniwa katika uzinzi, kwamba,
hamhukumu, isipokuwa aende zake na asifanye dhambi tena. Katika Injili ya Yohana 4, anatoa maji ya
wokovu bure kwa mwanamke Msamaria - kwa hakika msamaha sasa uilikuwa ni bure, na Mungu
mwenyewe alikuwa akipatanisha wanaume na wanawake na nafsi yake mwenyewe. Kwa sababu
alikuwa akienda kuliondoa lile pingamizi kuu la dhambi, ambalo limewashikilia watu wote katika vifungo
vya dhambi na mauti; kuanzia wakati ule wa Adamu. Misingi yote ya mambo ilikuwa inaenda kubadilika
kwa sababu ya Kalvari - ... kwa maana manabii wote na torati walitabiri mpaka wakati wa Yohana,
Mathayo 11:13. Katika Luka 13:1-5, Yesu analiweka wazi zaidi kwa hao anaoongea nao, kwamba
hawapo watu wengine ambao wao ni watenda dhambi wakubwa kuliko wengine; bali wote wamekufa
katika makosa na dhambi; hata kama kwa nje wanaonekana wanatenda dhambi nyingi au kidogo; hapo
hakuna tofauti, hali ya kila mmoja wao ni (Rumi 3:10,12,23). Sio wingi wa yale wanayoyafanya watu,
isipokuwa ni ile hali yao. Hali ya watu wote (wanaume kwa wanawake) ni moja, ni ya dhambi na kifo na
kutengwa kutoka kwa Mungu. Jambo hili halikufunuliwa kwa uwazi zaidi ndani ya Agano la Kale, kwa
sababu hapakuwepo na matengenezo kwa ajili ya hali hii ya dhambi katika wakati ule. (Gal.3:22-25 ; 4:3-
5; Rumi 3:19-22; Heb 1:1-2 ; 9:6,9 ; 10:1 ; 4:9,10). Lakini kwa sasa, kutokana na kujidhihirisha kwa Yesu,
ukaja ufunuo wa kudumu, wenye kina cha uozo wa mwanadamu, kwa sababu, Mungu sasa alikuwa
akitoa matengenezo kamili juu ya hali hiyo na alikuwa akifanya hivyo bure nje ya upendo na neema yake
isiyo na ukomo.

Yesu hakuja kuwahukumu kwa ajili ya dhambi zao ambazo alipaswa kufa kwa ajili ya hizo (Yohana 3:17;
12:4), bali kuwapatia wokovu bure wale wote watakaotubu na kuamini Injili. Hii ndiyo maana halisi ya ile
mistari mikuu inayopatikana katika Yoh. 3:16 18. Mungu alifahamu wazi kuwa watu wote walikuwa
katika vifungo kwa dhambi na kwamba kifo kilitawala ndani yao kwa sababu ya dhambi. Alikuwa
hawalaumu kwa jambo hilo kwa maana hayo yote yalikuwa ni matokeo ya dhambi ya Adamu, na yeye
Yesu, alikuwa anaenda kuzibeba dhambi hizo zote pamoja na hukumu zake pale Kalvari. Kuendelea
kungangania juu ya dhambi moja na kuukataa msaada wa bure wa msamaha na wokovu; jambo hili
linawakilisha dhambi ambazo watu watahukumiwa nazo.

Kile ambacho kinafanywa na mafundisho hayo yao mapya ni kuzifufua dhambi zile ambazo Yesu
alikwisha mwaga damu yake kwa ajili ya hizo, na wakati huo huo kuwataka watakatifu kuomba kwa ajili
ya dhambi hizo! Walimu hao wa kisasa wangekataa hizo; lakini wao hawajali madhara ya mafundisho
yao. Hii inatoa mifano pia ya jinsi wanavyotumia vibaya ile 2 Kor 5:19. Wao wanasema kuwa, huduma hii
ya upatanisho ni sehemu muhimu ya huduma ya kanisa.

Ndiyo, kwa kweli ni sawa, lakini je, maana yao hasa ni nini? Wanaharibu maana halisi ya sura hiyo; pale
wanaposema kuwa ni sehemu ya huduma ya kanisa, kuupatanisha ulimwengu (mji, au nchi inayotuhusu)
kwa Mungu! Na ni kwa jinsi gani basi? Kwa kuungama na kutubu dhambi za Nchi yetu na kujitwalia
damu ya Yesu kwa dhambi hizo? Lakini maana hii waitoayo, hatupewi popote pale na Mtume Paulo!
Hasemi kuwa Mungu yupo katika kanisa na akiwaongoza watakatifu leo kuungama na kutubu kwa ajili
ya dhambi za jumuia ili kwamba apate kuwasamehe! Isipokuwa yeye anasema kuwa, Mungu alikuwa
ndani ya Kristo na katika huyo Kristo alikuwa akiupatanisha ulimwengu na yeye mwenyewe
asiwahesabie makosa yao; sasa kwa nini kuzifufua dhambi ambazo Mungu hazihesabii kwa
ulimwengu? Ili kwamba eti kanisa liweze kutubu na kuungama kwa ajili hizo? Huu ni utata na
mkanganyiko mkubwa! Katika sura hiyo yote tokea ule mstari wa 14 mpaka wa 21 kimsingi inaelezwa
yale ambayo Mungu aliyafanya kupitia Kristo pale Kalvari kwa niaba ya wanadamu. Imefanywa!
Mungu amefanya! Imekwisha na wala hakuna yeyote awezaye kuongezea lolote lile juu ya hilo!

Katika ule mstari wa 18 anatuambia kuwa Mungu alitupatanisha na yeye mwenyewe kupitia mwanae
Yesu Kristo; wala kamwe haikuwa ni kanisa lililofanya hilo kwa kupitia maombi ya kuungama na kutubu!
22
Mafundisho hayo yanajaribu kuongeza au kupunguza utimilifu wa Kalvari kupitia ubunifu wa hizi kazi zao
za upatanisho, ambazo kanisa lililazimika kutimiliza kupitia kile wanachokiita wao maombezi ya
utambulisho. Lakini Paulo haungami wala kutubu kwa ajili ya dhambi za yeyote yule katika waraka huu!
Hii ni nini basi Neno au huduma ya neno ya upatanisho ile ambayo mtume Paulo ameitaja katika
mstari ule wa 18,19? Ni sawa kuwa anatuambia sisi, naye alitupa huduma ya upatanisho yaani,
Mungu alikuwa ndani ya Kristo akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake asiwahesabie makosa yao.
Tangazo la ujumbe huu ni Nenoau huduma ya upatanisho - kutangaza kwa watu kile ambacho
Mungu amekifanya katika Kristo kwa niaba yao, ni ujumbe wa neema uletao amani, kuwa upatanisho
wanaume kwa wanawake kwa Mungu. Tazama kwa makini kile ambacho Paulo amekifanya ndani ya
waraka huu, tunaona kuwa hajaribu kupata upatanisho kwa ajili ya tabia za kimwili walizo nazo
wakorintho kwa kupitia maombi ya toba kwa niaba yao.

Tunamwona Mtume Paulo akitangaza kwa wakorintho kile ambacho Mungu amekwisha kifanya ndani ya
Kristo kwa niaba yao, na ili baadae waweze kuelewa kuwa yawapasa kuwa ni watu wa aina gani katika
hali ya ukweli huu wenye utukufu; ndipo sasa anawaagiza kupatana na Mungu, kana kwamba Mungu
alikuwa akiwasihi (sio kuomba maombi ya toba kupitia kwetu sisi).tunawasihi mpatanishwe na
Mungu. Ametangaza neno la Mungu lenye neema kwao ili kwamba ikibidi wapate kurejea na kutubu.

Hebu basi tuangalie kwa ufasaha zaidi jambo hili. Ni kweli kwamba unaweza kuhuzunishwa hadi kufikia
kutoka machozi na maumivu ndani ya maombi, pale tuonapo ndugu zetu wakitenda dhambi au wakienda
mbali na Mungu, 2 Kor 2:4; Gal 4:19; kwa ujumla tunapaswa kuguswa na mambo yale yanayoumiza
mwili wa Kristo na hivyo kuombeana mbele ya kiti cha enzi cha neema ya Mungu na wema wake upate
kuwaongoza wale waliofanya dhambi wapate kutubu na kwamba rehema zake zipate kurejesha tena
mioyo yao kwake. Lakini sasa, jambo hili lipo tofauti kabisa na hayo mafundisho yao ya kisasa. Wao
wanatusihi tuyafanye yale wanayotufundisha, kwamba wanatutaka tutubu kwa ajili ya dhambi za dunia,
yaani, dhambi za watu wasioamini! Lakini kwa chochote kile tunachoweza kuombea, tusisahau kabisa
kwamba yupo mpatanishi mmoja tu kati ya Mungu na wanadamu, na huyo ndiye mwanadamu Yesu
Kristo; na sasa hayo mafundisho yao ya kisasa yanapoteza mwelekeo wao katika ukweli huu.

Tunaliona hili mara nyingi katika Biblia kwamba neno la kweli la Mungu huja kwa mtu binafsi likimtaka
kugeuka toka dhambini kwenda kwa yeye; na katika Agano Jipya hili ni neno lenye utukufu, limejaa
neema na kweli, likiwataka waume kwa wake wokovu wa bure katika Kristo. Dhambi zao zilizopita
haziwezi kuwatenga wala kuwazuia katika kupokea wokovu. Mungu hawahesabii tena dhambi hizo
zilizopita ndani yao (kwa sababu ya Kalvari). Lakini kwa hakika sehemu ya wokovu huu mkuu ni
kwamba, watu wanapokea msamaha wa dhambi zao zote zilizopita kupitia damu ya Kristo, pale tu
wanapokea habari hii ya upatanisho.
(Rumi10:9-10, ukisoma kwa makini katika mistari hiyo, utaona kuwa Mungu anamtaka mtu binafsi
amwamini Yesu na kumpokea moyoni mwake ili aweze kuokolewa; na wala si vinginevyo).

Lakini ili kuendelea na ujumbe wetu; tatizo halisi hapa sio kwamba watu wanafanya wizi, kuua n.k. bali
tatizo ni kwamba, kuhukumiwa kwao ni kuwa mtu haiamini habari njema na hachukui hatua ya
kuondoka kutoka katika giza. Katika Injili ya Yohana 16:9 tunasoma kwamba, hivyo Roho Mtakatifu
atakapokuja atauhakikishia ulimwengu kwa habari ya dhambi. Sasa ni jambo la maana sana kugundua
na kuelewa kuwa, ni kwa nini auhakikishie ulimwengu kwa habari ya dhambi?

Kwa hatua ya kwanza, haiwi hivyo kwa sababu ya kudanganya, kuiba, uchawi, uzinzi na kuua, bali Roho
Mtakatifu atawashawishi juu ya dhambi kwa sababu hawakuamini. Hivyo ndiyo sababu ya msingi
inayowazuia watu kuokoka - kule kutokuamini kwao. Ufahamu kuwa, Kalvari imekwishaishughulikia
dhambi pamoja na nguvu yake. Waache watu sasa watubu na kuamini Injili. Mafundisho hayo yahusuyo
kutubu kwa ajili ya dhambi za wenye dhambi, yanashambulia na kudhalilisha ukweli - iwapo mtu atakuwa
amejihusisha katika uchafu, ulevi au uchawi, atahitaji pia kupata ukombozi maalumu ili kuondokana na
mambo hayo; katika namna ambayo sio lazima wote waipitie hiyo. Mambo hayo yanaweza na yanafanya
madhara makubwa na uharibifu katika maisha ya mtu iwapo atayaendea na kuyafanya. Lakini jawabu la
hilo sio, kwa wengine kuanza kutubu kwa ajili ya dhambi za hao, badala yake ni kuomba, kwa mfano,
mlango wa kuingia Injili upate kufunguliwa kwa ajili ya watu hao - hilo tu linalotupasa kufanya kwa ajili
yao.

Katika Agano Jipya tatizo kubwa lililokuwepo la kueneza na kuipokea Injili, haionyeshi kuwa ni dhambi
ya watu, dhambi zile wanazozitenda watu! Isipokuwa ni kule kutokuamini kwao. Katika Injili, tunaona
kuwa, ilikuwa ni watenda dhambi ndio waaliokuwa wakimiminika kwenda kwa Yesu: wanyanganyi,
makahaba, watu wachafu na wale waliopagawa na mapepo; na wala sio watu wenye dini; hawa watu
walikuwa ndio wale ambao hawakumuamini! Ndani ya mji wake mwenyewe, Yesu hakuweza kabisa

23
kufanya miujiza mingi, sio kwa sababu ya uovu wa mji ule, isipokuwa ni kwa sababu ya kutokuamini
kwao (Mty 13:58).

Tunaona pia katika Matendo ya Mitume, kwamba, kimsingi haikuwa ni kwa sababu ya dhambi za watu
kama vile uchawi wao, ulevi wao na uuaji, ambavyo viliwakilisha kuzuiwa kwa Injili. Kwa mapenzi ya
Mungu mwenyewe, Mtume Paulo na wengineo walitembea moja kwa moja katika mazingira ya miji ya
jinsi hiyo, kama vile mji wa Samaria na Efeso, na Mungu alifanya kazi ya ajabu huko (wala pasipo hata
kuomba au kuhubiri kwamba mmoja anapaswa kutubu kwanza kwa ajili ya dhambi za mji ule). Tatizo
lililokuwa hapo ni kutokuamini, ugumu wa mioyo kuelekea ukweli, mara nyingi kutoka kwa watu wa dini;
haijalishi kama wao walikuwa ni Wayahudi au kutoka kwa hao waliojishughulisha na kuabudu sanamu.
Unapoendelea kusoma Matendo ya Mitume utagundua kuwa tatizo halikuwa ni dhambi ya watu,
isipokuwa ni ugumu wa mioyo yao kuelekea ukweli - kutokuamini (kwa ajili ya sababu yoyote ile iwayo).
Ndilo litakalo wahukumu watu siku hiyo, sawasawa na kazi zao kama maandiko ya Neno la Mungu
yaonyeshavyo - kwa uwazi sana; na watu wanapaswa kuambiwa hayo. Lakini kwa mujibu wa tangazo la
Injili tunapaswa kuanza kueleza kwa watu wote ule msamaha wa Mungu utolewao bure kwa njia ya
Kristo ambaye alifufuliwa kutoka kwa wafu kwa ajili ya haki yao. Kutokuamini na kutokupokea. Hiyo ndiyo
dhambi ya wanadamu.

Katika uwazi wa ukweli huu wote na ufunuo, mitume wangewezaje basi kutubu au kuwaambia
wengine ili watubu kwa ajili ya dhambi za wasioamini katika nchi na miji yao? Yesu Kristo tayari
alikwishawafia kwa ajili ya dhambi zao, na amekwisha lipa bei ya upatanisho wao (1Yoh.1:2)! Msamaha
wa wokovu tayari umekwisha patikana katika Kristo, watu wanapaswa sasa kuamini habari njema, na
wao wenyewe, yaani wao binafsi, ndio wenye dhambi zao. Kristo aliteswa mara moja kwa ajili ya dhambi,
na sasa je, tunafikiria kuongelea chochote juu ya kazi yake aliyoimaliza kwa kutubu kwa ajili ya dhambi
hizo mbele za Mungu na kuomba msamaha kwa damu ya Yesu Kristo wakati ambapo damu yake
iliyomwagika pale Kalvari tayari imepokeo hayo?

Je, mateso yetu tunayo yapata tuombapo na kutubu yanaweza kutupatia msamaha zaidi kwa ajili ya
wenye dhambi? Au tunadhani kuwa toba yetu kwa ajili ya dhambi zao kwa namna nyingine, labda sasa
inamwezesha Mungu kuibariki mikoa na miji yetu pamoja na watu wake kwa Injili? (Watu wanaweza
kudhani kuwa wao ni kama Daniel, wafanyapo hayo, lakini kwa masikitiko makubwa na kwa ubaya zaidi
wamekosea). Ni nini? Mungu aliwasamehe waume kwa wake bure pale Kalvari; kisha eti watakatifu
watubu kwa ajili dhambi hizo hizo ndani ya maombi yao ili kwamba Mungu apate kuwasamehe na
matendo yao maovu? (Afanye hivyo kwa mara nyingine tena?). Na kwamba hii eti imzuie Mungu kuibariki
miji au mikoa ili kwamba wenye dhambi wenyewe wapate tena kuzitubia dhambi hizo hizo na kupokea
msamaha pia. (Je, mara nyingine tena?). Ni mchanganyiko wa jinsi gani huu? Ni aina gani ya
mchanganyiko wa mawazo yasiyo na afya ya Agano la Kale na Jipya, ambayo yanaweza tu
kuwadanganya watu kuhusiana na ukweli? Linaloshangaza zaidi, ni ule ukweli kuwa baadhi ya wahubiri
wanasafiri huko na huko katika miji na kuhubiri hadharani kwa watakatifu pamoja na wenye dhambi,
wakiwaeleza kwamba ni lazima watubu kwa ajili ya dhambi za nchi zao badala ya kuwapatia ukweli wa
Injili wale wasioamini - kuwapa pia ujumbe wa Kristo na kwamba yeye ndiye aliyesulubiwa, kwamba
Kristo alikufa na amefufuka kutoka kwa wafu na ameziondoa dhambi zetu zote, kwa ajili ya kutupatia
msamaha na haki!

Wanatujia kwa mtindo wa baadhi ya manabii wa Agano la Kale, kama vile Yona au Yeremia wakiitangaza
hukumu ya Mungu juu ya Taifa kwa ajili ya dhambi zake; wakati ambapo tumekwishaelezwa kwa uwazi
kabisa kuwa nyakati za zamani Mungu aliongea na baba zetu kwa vinywa vya manabii; nyakati hizi za
mwisho ameongea nasi kwa njia ya Mwana wake. Waebr.1:1,2. Sio tu kwamba Mungu amemchagua Mtu
wa tofauti kabisa na wapokee mtu halisi wa kutuunganisha; bali ni kwamba ujumbe na huduma sasa ni
mpya kabisa kwa sababu ya Mtu mwenyewe aliyechaguliwa na Mungu - Yesu Kristo, na kile
alichokwisha kukifanya! Torati ilitolewa na Musa, lakini neema na kweli zilikuja kwa njia ya Kristo Yesu.
Lakini hawa wahubiri wengineo wanahubiri kitu cha tofauti kabisa, na kitu kingine ambacho kipo jirani
kabisa na torati na hukumu kuliko Injili na neema. Hata kama katika suala la Yona, yeye aliwaambia watu
wa Ninawi wao wenyewe watubu, (wao binafsi). Hakuwataka kutubu kwa ajili ya dhambi za watu wengine
katika mji ule! Na bila shaka Yona hakutubu kwa ajili ya dhambi zao.

Hebu niseme hapa, kwa vyovyote vile tunaweza na pengine tumehuzunishwa na yale yanayoendelea
kufanyika katika jamii zetu au jamii na kwa hiyo tunaweza kuomba kuhusiana na vitu vya namna hiyo
ambavyo ni vya wazi na vinavyotuhuzunisha na ambavyo vinaweza kutumika pia kama vizuizi vya watu
kuisikia na kuipoke Injili. Na kwa hakika, tunaweza pengine kufikiri kuwa mambo yameenda mbali zaidi
kiasi kwamba tunafikia hatua inayoonyesha kuiva kwa hukumu ya mwisho ya Mungu juu ya dunia. Na
kwa hivyo, hiyo inaweza kutushurutisha kuomba kwa bidii sana, kwa ajili ya hali na huduma ya kanisa

24
kwa ulimwengu huu uliopotea na wenye machukizo, hivyo kutangaza kwa bidii haja ya waume kwa wake
kutubu. Hata hivyo, hiyo nayo tena hailingani kabisa na haya makubaliano ya kisasa yanayopenda
kututaka sisi tufanye; katika kutubu kwa ajiliya dhambi za ulimwengu na katika jamii yenye kushutumiwa
kama baadhi ya manabii wa Agano la Kale na wakiwasihi wauamini kutubu kwa ajili ya dhambi za jamii
yao, kana kwamba jamii ni kama Israel ya Agano la Kale. Tunapaswa kuendelea kuhubiri Injili ya Yesu
Kristo hadi mwisho utakapotujia.

Watu wanapokea msamaha na wokovu ambao tayari Kristo amekwishaununua kwa ajili yao, pale
wanaposikia na kuamini habari njema. Lakini kabla watu wenyewe hawajatubia dhambi zao na kusikia
habari njema, maombi yetu wala toba haviwezi kumshawishi kusamehe dhambi hizo, au kuleta
upatanisho kwa ajili yao au kwa ajili ya nchi yao. Kuyafikiria hayo au kuyatenda, huu ni ushirikina wa
kidini na wala sio vinginevyo! Hayana msingi wowote katika neno la Mungu. Ni sawa, Mungu
amewasamehe dhambi zao katika Kristo kwa sababu ya Kalvari, lakini hata kama ni hivyo, hiyo haileti
manufaa yoyote katika maisha yao mpaka tu pale watakapotubu na kuaimini Injili.

Kwa hiyo, hebu basi kwa hakika tuombe, ili kwamba Mungu atume watenda kazi wake ili Neno la Mungu
lipate kuletwa kwa waume kwa wake na kuwaongeza katika kanisa lake. Tuombe kwamba Mungu
afungue mlango wa usemi kwa wale wadumuo kwa jina lake, kwamba Injili hiyo ipate kuifikia mioyo ya
watu wengi na kuwarejesha kwa mwokozi.

Ni jambo moja la kuombea nalo ni kwamba Bwana wa mavuno apeleke watenda kazi katika mavuno
yake (Luka 10:2); au kuwawezesha watumwa wake kuihubiri ile siri ya Injili kwa ujasiri (Efeso 6:19), au
kwamba aweze kufanya maajabu kupitia watu wake ili wasioamini waweze kufikiwa (Mtd 4: 29,30); au
kuhuzunishwa kwa sababu ya ugumu wa mioyo ya wale tunaowajua na wengineo pia na kwa hivyo
kuomba ili kwamba Mungu aweze kuwaokoa (1 Tim 2:3,4; Rumi 9:1-3; 10:1); au kujinyenyekeza
wenyewe na kuomba na kuombea katika kiti cha neema kwa ajili ya rehema ya Mungu iweze kuwafikia
na kurejesha mioyo yao kwake pale ambapo wengine hutenda dhambi au kupotelea mbali (Gal. 4:19).
Hayo yote ni mambo ambayo tunaweza na tunapaswa kuyafanya; lakini badala yake tunaona ni jambo la
kinyume kabisa, pale tunapoanza kutubu kwa ajili ya dhambi za wenye dhambi na wakati huo huo kufikiri
kuwa labda tunaweza kupokea msamaha na upatanisho kwa ajili yao na kwa nchi yetu pia!

Ni mchanganyiko wa kimawazo na upuuzi wa jinsi gani huu! Tumepotelea mbali kiasi gani na Biblia na
mawazo yake. Kwanza, eti tuombe kwa jambo ambalo tayari Mungu amekwisha lifanya - kwa mfano,
amewasamehe watu katika Kristo, na hii ameifanya bila malipo, bure - na kisha kujaribu tena na
kusababisha msamaha huu ndani ya maisha yao kwa njia ya ujumla isiyofaa, kwa mfano, kwa kupitia
maungamo na toba ya ushirikishwaji! Je, tunamjaribu Mungu kwa kulikataa neno lake na kupinga ukweli
wake? Je, sio kwamba ni watu kwa makusudi kabisa ndio wanaoupinga ukweli wa Mungu lakini bila
mashaka yoyote yale, hayo ni matokeo na mambo yaliyo sababishwa na mafundisho; pale
wanapoongezea maombi yao ili kupata msamaha kwa ajili ya wenye dhambi.

Kwa ujumla, wanaushambulia ukweli huu, kuwa msamaha ulikwishapatikana kwa ajili ya wanaume na
wanawake katika Kristo, kadhalika kwa kufanya hivyo wafanyavyo, wanapotosha ukweli juu ya asili ya
dhambi na ukamilifu wa msamaha wa Mungu ndani ya Kristo, wanapofikia kuwa ni dhambi mbaya kama
vile uchafu, uchawi, n.k. ambavyo ndiyo inayozuia Injili kuenezwa katika mkoa, kuliko kutambua kuwa:

1. Watu wote wamekufa katika makosa na dhambi.


2. Kristo amekwishazishughulikia dhambi hizo kikamilifu na bure na kwa hiyo kimsingi ni
kutangaza habari njema kwamba watu wameletwa katika uzima na toba; kuliko kutujia na kuihubiri
hukumu juu ya dhambi za watu kama ilivyokuwa kwa baadhi ya manabii wa Agano la Kale; na tena papo
hapo kuwataka watu watubu kwa ajili ya dhambi za watu wengine, hata kama ni mjini au nchi na
kwamba.
3. Ni kule kutokuamini, hiyo ndiyo dhambi ambayo watu watahukumiwa nayo na ndiyo
inayowazuia watu kupokea msamaha na wokovu.

Ni ipi basi iliyo njia ya Mungu ya kuleta ukweli wa msamaha katika maisha ya watu? Ni kwa njia ya
kuhubiri Injili - Kristo ndiye aliyesulibiwa - akiwataka watu kutubu na kuamini Injili. Hapa, tunaweza labda
wote kusema kuwa hii ni wazi zaidi, ni pale watu wengine wanashindwa kuona kuwa mafundisho hayo
mapya, yanaondoa ukweli uliopo kutoka katika Agano Jipya na kujaribu kutubatiza ndani ya fikra za
kiagano la kale. Lakini hata hayo mawazo yao nayo, hayajatafsiriwa kwa usahihi. Kwa hiyo, ulinganifu
huu unawapa wasio amini sura potofu ya Injili.

25
Injili ina maana gani? Ina maana kuwa ni Habari njema au Ujumbe mwema. Bwana asifiwe! Hivyo
ndivyo anavyouelezea ujumbe wa Agano Jipya kwa wenye dhambi! Na msisistizo wake ni kuihubiri Injili.
Katika Biblia zetu kuhubiri Injili inatafsiriwa kwa neno moja la kigiriki (uangelizo), ambalo linaweza
kutafsiriwa zaidi kama kuelezea, kutangaza, au kuhubiri habari njema. Tangu mwanzo, Yesu alipofika
hapa duniani, malaika walitangaza ujio wake kuwa ni habari njema yenye furaha kuu, (Luka 2:10). Yesu
mwenyewe anaianza huduma yake kwa kutangaza habari njema ya ufalme wa Mungu, (Luka 4: 43),
kisha anaendelea kuihubiri habari hii njema kwa wakati wote wa huduma yake, (Luka 8:1). Na
anawaamuru wanafunzi wake kuitangaza kwa kila kiumbe. Na katika Agano Jipya lote, Neno hili kweli,
linafananishwa kama ni habari njema, Efeso 1:13, na linatangazwa kwa wote - Kolosai 1: 5,6; 2 Tim 4:17.
Na katika Injili hiyo, Mtume Paulo wala hakuona aibu kuitangaza kwa sababu ni uweza wa Mungu uletao
wokovu kwa kila aaminiye, (Rumi 1:16). Mtume Paulo yupo wazi na dhahiri kabisa na jambo hili
anawaambia Wakorintho kwamba, Kristo hakunituma ili nibatize, bali nihubiri habari njema, wala sio
kwa hekima ya maneno, msalaba wa Kristo usije ukabatilika. (1Kor: 1:17). Hivyo alidhamiria asijue kitu
chochote kingine, isipokuwa Yesu Kristo naye amesulibiwa. Kote alikokuwa akizunguka alieleza hayo.
Kwa sababu yeye anaeleza kuwa, mahubiri ya msalaba ni uweza wa Mungu kwa hao wanaookolewa (1
Kor 1: 18-22). Hivyo, kwa nini basi watu hawakomi kutujia nakuhubiri kwa mtindo wa baadhi ya manabii
wa Agano la Kale wakitangaza laana na hukumu juu ya miji na nchi kwa sababu ya dhambi. Kwa nini
pia hawakomi kuongezea ujumbe wao wenyewe juu ya Injili na ambao unatolewa tu kulingana na
matakwa na busara zao wenyewe ambao kwa huo huunyanganya ukweli na uweza wa Injili mioyoni
mwa jamii. Kwa nini wanahubiri Injili hii nyingine?!

Katika magazeti ya aina mbalimbali na kwenye mikutano ya hadhara, badala ya kutuhubiria Kristo, wao
wanajaribu kudhihirisha maovu ya jamii na kisha kuwaambia watu watubu kwa ajili ya dhambi za jumuiya
ili kusudi Mungu apate kuiondosha laana na hukumu kutoka katika mikoa yao. Aha! Ni upuuzi wa jinsi
gani huu jamani! Aha! Ni madanganyo gani ya jinsi gani hayo? Aha! Jamani, ni huzuni ya jinsi gani hiyo?
Tangaza jambo hili juu ya paa la nyumba, ili kila mmoja apate kusikia na kuelewa ya kwamba Yesu
amekwisha kuziondoa laana zote na hukumu zake kwa niaba yetu sote. Sasa, tunapokea msamaha na
wokovu bure iwapo tu, tutaamini na kutubu - dhambi zetu wenyewe. Toba yetu tuifanyayo kwa ajili ya
dhambi za watu wasioamini, haiwezi kutusaidia kupata aina yoyote ya upatanisho na Mungu wala
msamaha, zaidi ya lile ambalo damu ya Kristo imeupata pale Kalvari. Mty 13:38,39; Rumi 5:18; Kol 2:13-
15.

Katika mahubiri ya mwanzoni yaliyonakiliwa na Mtume Paulo katika Matendo ya Mitume 13, anawaambia
kwamba, Mungu ametuma, Neno la wokovu huu kwao, (Mstari wa 26). Hawaombi Wayahudi watubu
kwa ajili ya ugumu wote wa viongozi wao waliopo kule Yerusalem na sehemu nyinginezo; hali kadhalika
hawaambii wacha Mungu wasio wa kiyahudi kutubu kwa ajili ya dhambi za kule Antiokia, kusudi kwamba
Mungu apate kuwabariki pamoja na mikoa yao! (Hebu niseme hapa kitu kidogo; ijapokuwa ni kitu kingine
kidogo pale inapotokea mtu wa Mungu anakuja kulionya kanisa linapaswa kujisafisha lenyewe; basi
inapotokea jinsi hiyo, ndipo tunayo mifano ya kutosha ndani ya Agano Jipya).

Kutoka katika maandiko mengi ya Neno la Mungu, tunaona kuwa kiini cha Injili hii ni, Kumhubiri Yesu
Kristo kwa watu, Mt 5:42; Mdo 8:12,25; 11:20, na kuutangaza ufufuko wake kama msingi na uthibitisho
wa msamaha wa Mungu na wokovu. Mtd 2: 22,23; 4:410-12; 5:30,31; 10:40-43; 13:30-33; 17:18. Hii
ndiyo Injili, huu ndiyo utume wa mfano wa Agano jipya. Ni kifo na ufufuo wa Kristo ndiyo kiini na uzima
halisi wa ujumbe wa Injili, kwa sababu watu wamepata msamaha kutokana na hilo tu. Hatari kubwa
inayoonekana na hapo, ni pale mtu mwenyewe (binafsi) anapokataa kuamini kuzipokea habari njema.
Mtd 13:40, 41-46. Lakini Injili hii inaleta ujumbe wa amani mioyoni mwa waume kwa wake, Mtd 10:36. Ni
Injili ya Neema ya Mungu, Mtd 20-24; na inatangazwa kuwa ndiyo Injili ya wokovu wetu, Efeso 1:17. Ni
Injili halisi na ni yenye neema ya ajabu inayotupatia uweza wa uzima wa milele, 2Thes 1:9,10. Ni Injili
yenye utukufu wa kweli 1Thes 1:11; kwa hakika, Injili ni Injili ya Mungu, 1Thes 2: 2,9, na ya Mwana
Wake, Bwana wetu Yesu Kristo - 2 Kor 2: 12; 9:13?! Lakini watu sasa, wanaibadili na kuifanya ni
ujumbe wa sheria, laana za ushirikina.

Kutokana na maandiko ya Neno la Mungu yote hayo, tunaweza sasa kuona kuwa ujumbe wa Injili ni
tangazo la neema na rehema za Mungu isiyo nakifani kwa wanadamu wote ambayo walipatiwa kabla ya
misingi ya ulimwengu huu, (2 Timotheo 1:19), na sasa inadhihirishwa wazi kwa kufufuliwa kwake
mwokozi wetu Yesu Kristo Mwanae. Kwa sababu hiyo, wao pia ni habari za furaha. Na huu ndio
ujumbe, huu ndio mkazo wake kwamba kwa kadri tupatavyo nafasi (fursa) twapaswa kulitangaza hilo
kwa wanadamu wote - kwamba tunapaswa kutubu na kumwamini Kristo ambaye amewakomboa
kutokana na dhambi na hukumu; na kule kutokuamini ni dhambi kuu inayostahili hukumu ya binafsi
ambayo kwa kweli ndiyo watakayohukumiwa kwayo.

26
Sasa inaweza kusemwa kuwa haya yote tayari yaeleweka lakini ni ukweli na Injili hii ndivyo
vilivyopotoshwa (Gal1:7), na imetiwa giza kwa mafundisho mengineyo ya kisasa. Wanatuletea ujumbe
wenye laana na hukumu wanawahusisha watu mizigo ya uongo; wanawaelekeza watu kwenye mambo
yasiyofaa kabisa yasiyo ya kibiblia kwa makusudi na uchunguzi usio na mwisho wa dhambi na maovu
katika jumuia zao, miji na nchi zao. Kisha wanaweka matangazo ya uovu huu ndani ya nyaraka za
maombi yao na mara zote wanajisikia kuwa kwa hakika wanapata maendeleo fulani pale wanapofanikiwa
kuzigundua nyendo fulani za kiuchawi na unajimu ambapo baadae wanaendelea kufafanua na kutoa
mifano yenye ujumbe wenye kupotosha maana katika maandishi yao. Wanakimbilia kuijaza mioyo ya
watakatifu na akili zao kwa mambo hayo yasiyofaa na hatimaye hupenda kuishikilia mioyo yetu pia, kwa
kututaka tutubu na kuomba juu ya maovu haya kana kwamba ni dhambi zetu wenyewe (binafsi) na
kuiweka damu ya Yesu katika mazingira ya jinsi hivyo ili kuleta upatanisho ili kwamba laana ya Mungu na
hukumu zipate kuondolewa. Hayo yote ni matendo ya ushirikina zaidi kuliko hata ilivyo Injili yenyewe. Ni
vitendo vya kuwabatiza watu katika mazingaombwe yenye mawazo ya kidini ambayo huwaondoshea
mbali ule ukweli uliomo ndani ya Kristo.

Inaonekana wazi kuwa siku hizi yapo makundi ambayo yanatafuta njia mpya ya kuieneza Injili kwa
mafanikio zaidi, lakini matarajio yao nayo ni ya kupita kiasi, kwa ajili ya mafanikio na ufanisi pamoja na
utayari wa kupokea kwa urahisi (mambo yao) uzoefu wao usio wa kawaida; hata kama ni vipawa kama
inavyoitwa; au aina tofauti ya maono - imewapatia kwa haraka roho zidanganyazo. Hivyo wanapenda
kuzingatia maandiko machache ya neno la Mungu, yanayoonyesha kuwa pengine yanaweza kuunga
mkono mambo ya kihisia, wakati huo huo wakiukataa ushuhuda mzima wa maandiko ya neno la Mungu;
hivyo katika kufanya hivyo wanawasilisha kitu kilicho tofauti na Injili. Hata hivyo Injili tunayohubiriwa
hailingani na matakwa ya kibinadamu (Gal.1:16), mwanadamu hawezi kuibuni, wala hawezi kuibadilisha,
wala hawezi kuongeza chochote juu yake au kugundua mandari mpya ya Injili. Ni Injili ya Mungu na ni
ya kudumu.

Ikiwa watu wa Mungu watajinyenyekeza wenyewe mbele za Mungu na kuomba mbele zake kwa bidii, je,
hataweza kufanya kazi yake katikati ya watu hawa, hata kama mawazo na maneno halisi ya maombi yao
siyo sahihi? Historia yote kurudi nyuma imeonyesha wazi jinsi Mungu alivyotembea; lakini kutembea
huko kwa Mungu hakuonyeshi kwamba kila kitu ambacho wakristo walikifanya katika kukuza kule
kutembea kwa Mungu kuwa kilikuwa ni sahihi. Lakini hebu tuseme hivi kwa haraka; kwamba ingawa hao
wanaoamini kanuni hizo za kisasa, wanatumia pesa nyingi, muda na nguvu nyingi katika kukuza mawazo
yao na kujaribu kuonyesha jinsi gani mipango yao imeweza kufanikiwa ulimwenguni, lakini bado
uthibitisho wake sio kamili na wala sio wa mwisho. Kinyume chake, ndio sababu makala hii
imeandikwa. Katika nchi nyingine tofauti na zile nyingine, mafundisho haya ya kisasa
yanasababisha kuchanganyikiwa na ghasia bila kugeuza mageuzo ya mkondo wa uovu kwa
namna yoyote ile. Na katika maeneo mengine mengi hayaleti faida yoyote ila isipokuwa ni
kuwafadhaisha watakatifu kutoka katika wito wa kweli. Wanachukua mahala pa Injili kuihuibiri kwa
watu wote sehemu za hadhara kwa wasioamini na kwa watakatifu makanisani; matokeo yake ni
kuwa, akili za wote, watakatifu pamoja na wapagani zinajazwa mawazo yenye maagano ya
kisheria, hukumu na laana, ambazo huwaongoza kuingia katika aina ya ushirikina na toba isiyo
na manufaa na vijitabia vya udanganyifu. Injili ya Bwana wetu Yesu Kristo hapo inabadilishwa.

Siamini kuwa watu wanayafanya hayo kwa makusudi, wala sisemi kuwa walimu hao sio watu wa Mungu.
Mtume Paulo aliwaandikia watu wa Mungu katika makanisa kule Galatia na Korintho, wao waliamini
katika mambo ya msingi ambayo sisi sote tunayaamini kuhusiana na Kristo na damu yake. Lakini wao
baadae walipokea vingine, nyongeza ya mafundisho (Galatia) au walizingatia zaidi katika mambo ya nje
wakiwa na nia ya kimwili kwa ajili ya kupata uwezo wa madaraka na utukufu (Wakorintho). Paulo
amewaandikia akijaa huzuni ya kweli kwa jili yao, anapowaona wakiwa nje ya Imani kwa Mungu na kweli
yake ndipo anawaonya kuwa, wanakaribia kuiacha Imani ya kweli, ambapo Kristo kwao sio wa faida
tena, (Gal 3:4 ;4:11. 20:5:4). Anawaonya wakristo wa huko Korintho kuwa, kutokana na tabia zao za
kimwili na kupeana utukufu wao kwa wao, wapo ukingoni kabisa kuelekea kudanganywa na shetani
katika kumpokea Yesu mwingine, roho nyingine, na Injili nyingine; kwa sababu hata shetani hujigeuza ili
afanane na malaika wa nuru, basi sio neno kubwa watumishi wake nao wakijigeuza wawe mfano wa
watumishi wa haki. Kwa ajili ya hilo wakorintho walikaribia ukingoni mwa kudanganywa! (2 Kor. 11:1-20).
Ikiwa mambo yaliweza kuwa hivyo katika kanisa la mwanzo; haitatushangaza sisi leo, kuona yanatukia
pia ijapo kuwa yatatuhuzunisha sana. Na mambo hayo yanatokea siku hizi - watu wamo ukingoni kabisa
kupokea Injili nyingine, Yesu mwingine na Roho mwingine - inawezekana kuwa tayari wamekwisha
kuzipokea! Basi na hii makala ndogo hata kama haijawa kamilifu, ni kilio cha kurejea kwa wepesi uliomo
katika Kristo, na kwa tangazo la umilele, Injili ya Mungu isiyobadilika, ambayo ni uweza utupatiao
wokovu, ambao hutolewa bure kwa wanadamu!

27
Hebu tujikumbushe, ni nini mafundisho haya yasemavyo; ili kwamba asiwepo mtu atakayeelewa vibaya
yale tunayoyasema hapa.

Mafundisho hayo yanawaambia wakristo kuwa wanalazimika kuungama na /au kutubu kwa ajili ya
dhambi (zilizopo na zilizopita) za wenye dhambi wanaowazunguka katika miji na maeneo yao pamoja na
nchi yao. Na hata kuungama kuwa wamemtenda Mungu dhambi za kwa ajili ya dhambi hizo.
Wanapaswa kufanya hivyo ili kupokea msamaha wa Mungu na kuleta upatanisho kwa ajili ya nchi; kwa
maneno mengine, wanataka kutuambia kuwa, kanisa linapaswa kutubu kwa ajili ya dhambi za ulimwengu
na hata kuziungama dhambi hizo kana kwamba ni zao binafsi ili wapate msamaha wa Mungu!
Vinginevyo eti laana ya Mungu na huku yake itaendelea kubakia juu ya nchi. (Mafundisho haya
yanaweza kutofautiana kidogo kati ya nchi na nchi).

Sasa tunaelewa kuwa, kumbe Mungu hutazama mioyo, na bado anasikia kilio cha mioyo yetu hata kama
ufahamu wetu na maneno yetu katika maombi tuombayo hayako sawa, lakini hiyo siyo sababu ya
kuruhusu akili zetu zijawe mawazo ambayo kwa hakika siyo ya kibiblia katika kutupofusha ili tusione
ukweli kama ulivyo katika Kristo Yesu. Hakuna lolote lile ndani ya Agano Jipya ambalo lingeweza
kutuongoza ili tufikiri au kuamini lolote lile la mawazo hayo.

Maombi Katika Agano Jipya

Agano Jipya linatufundisha nini kuhusu maombi? Tunaipata mifano gani pale? Hebu basi tuanze na
mwana wa Mungu mwenyewe. Katika Yoh.17 Yesu anaomba mambo ya ndani kabisa moyoni mwake,
hata tunaweza kusema kuwa ni mambo fulani ya moyo wa Mungu yanafunuliwa katika maombi hayo.
Tukiangalia kwa makini sana katika maombi hayo tutagundua kuwa, Yesu haombi mahitaji mengi hapo,
isipokuwa moja ya mambo anayoyasema ni hili:
Mimi siuombei ulimwengu bali hao ulionipa

Je, umewahi kumsikia mtu yoyote yule akihubiri juu ya jambo hili? Ni mstari ambao mara nyingi
unapuuzwa, lakini unayo maonyo yenye maana yaliyozungumzwa na Kristo mwenyewe. Yesu alikuwa
akiwaombea wale ambao Mungu amempa Wafuasi wake. Alikuja kuwaita watu wenye dhambi ili watubu,
na alikuwa akienda kufa kwa ajili ya dhambi za ulimwengu. Baba aliupenda ulimwengu kiasi kwamba
alimtoa mwanae pekee, kwa sababu hakusudii yeyote aangamie, (1 Tim.2:4). Kwa hiyo tunaona kuwa
Mungu anao moyo unaojihusisha na wanadamu wote. Yesu alipokuwa akiomba kwa Babaye alikuwa
haombi kwa ajili ya walimwengu hata kidogo, bali alikuwa akiomba kwa ajili ya wale walio wa Mungu. Hii
ndiyo ilikuwa ni haja yake kubwa pale alipokuwa akiomba na inabakia kuwa haja yake kubwa siku ya leo
pia. Yesu Kristo anafanya nini pale alipoketi kuumeni mwa Baba yake? Katika Warumi 8:34, tunaelezwa
kuwa anatufanyia maombezi sisi - watakatifu. Na katika Waebrania 7:25 tunaambiwa kuwa yu hai siku
zote ili awaombee wao wamjiao Mungu kwa yeye. Hiki ndicho kielelezo cha huduma yake yenye
kuendelea katika maandiko, sio tu kwamba ni jambo ambalo alilifanya katika Injili ya Yohana 17. Lakini
cha kushangaza, leo tunao walimu ambao wanatuambia kuwa, tuwe tunaendelea kuomba na kutubu kwa
ajili ya dhambi za ulimwengu! Kwa hakika jambo hili ni kinyume kabisa!

Yapo maandiko mengine ambayo kwa hakika yatupasa kuyaangalia ili tupate picha pana kuhusu mstari
wa Yohana 17 ili usimame na mistari mingine, au sijaribu kuweka tafsiri nyembamba (hafifu) juu yake
kana kwamba kulikuwa na jambo moja tu la kuomba; sifanyi hivyo hata kidogo! Bali hebu tuangalie
maandiko mengine zaidi yanasemaje kuhusu hilo na nini hasa mwelekeo na mkazo wake mkuu; ndipo
itatuweka katika nafasi nzuri ya kuyafahamu mambo haya na msingi wake na nini, na ni kipi hakipo
hivyo.

Tunafahamu nini basi juu ya huduma ya Roho Mtakatifu ndani ya maombi? Kumbe, kama ilivyo pamoja
na Yesu Kristo ndivyo ilivyo pamoja na Roho Mtakatifu.Tunasoma katika Warumi 8:26,27,34, kwamba
Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa. Mtume Paulo anaendelea kutuambia
kuwa Roho Mtakatifu huwaombea watakatifu kama apendavyo Mungu.

Lolote liwalo laweza likawa ni kweli, maandiko ya Neno la Mungu yanatufunulia kwamba huduma kuu ya
Mwana na ya Roho Mtakatifu katika maombi ni kwa ajili ya watakatifu. Ni vipi kuhusu watakatifu
wenyewe? Wanapaswa kuomba kwa ajili ya nini? Jambo la kwanza na lililo kuu, kulingana na maandiko
ya Neno la Mungu tunalolipata katika somo hili, tunaona watakatifu wanaomba, na pia wanapaswa
kuombeana wao kwa wao kama vile Mwana na Roho Mtakatifu wanavyofanya. Katika Waefeso 6:10-18,
tunaambiwa kuwa, Tuzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake, kwa maana
kushindana kweli sisi si juu ya damu na nyama, bali ni juu ya falme na mamlaka n.k., kwa maneno
mengine yule adui sio wa kimwili bali ni wa kiroho. Ikiwa hivyo ndivyo ilivyo, mtume anatutaka tufanye

28
nini? Je, hapo anatuambia kuwa, kwa hiyo tuwe tunaomba dhidi ya mamlaka na uweza, dhidi ya
ulimwengu huu na dhidi ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho na kuwafunga? Hapana!
Huo sio ushauri wake! Sio hivyo hata kidogo! Hafundishi hivyo mahala hapa wala sehemu nyingine
yoyote ile ndani ya nyaraka zake kwa watakatifu. Hali kadhalika Petro naye, hafundishi hivyo. Yakobo na
Yohana hawawaagizi wakristo kufanya hivyo kwa sababu wanajua kuwa adui yako ni mwenye nguvu za
kiroho. Mtume Paulo anawaagiza waumini kuvaa silaha zote za Mungu, hiyo ni kwamba, wanahitajika
kuishi na kutembea kiroho wakiwa na silaha za kiroho. Katika sura hiyo tunafundishwa kuwa, kwa
sababu adui yetu ni wa kiroho, kwa hiyo mwendo wetu, maisha yetu ya kila siku yawe ni ya kiroho ili
kwamba tupate kusimama kinyume na hila zote za shetani na mapepo yake, ambayo yanataka kutujaribu
ili tuwe mbali katika kumtegemea na kumwamini Mungu; ili yeye (shetani) aweze kupata nafasi ya
kupanda mbegu za mashaka, kukata tamaa, uongo na tamaa mbaya mioyoni mwetu.

Tunapaswa kuishi katika utii wa Imani na upendo kwa Mungu, tukiukataa uongo wote wa yule adui toka
mioyoni na akilini mwetu. Hii ni vita ya kiroho; kwa hiyo sasa, tukiwa tumezivaa silaha za kiroho, Paulo
anatuagiza tuombe juu ya nini pale katika mstari wake wa 18? Je, juu ya uweza na mamlaka n.k.?
Hapana! Anatuambia tunapaswa kuomba kwa maombi na sala zote kuwaombea watakatifu wote.
Kusimama tukiwa tumevaa silaha zetu, yaani, kuishi na kutembea kiroho ili tuweze kuombeana
wenyewe kwa wenyewe kwa utaratibu na kwa mafanikio. Katika mienendo yetu binafsi mbele za Mungu,
tunapaswa kuyapinga majaribu ya shetani, kusita juu ya Mungu au kuwekwa naye mbali; na kutokana na
kukaa katika mwenendo huo ndipo tunawezeshwa kuomba vizuri kwa ajili ya watakatifu. Hayo ndiyo
mafundisho yake, lakini watu wanatupoteza kwa kutufundisha vitu vingine; wakituhimiza kuzingatia
kuomba dhidi ya mamlaka na uweza au kutubu kwa ajili ya dhambi za ulimwengu, jambo ambalo hiyo
siyo maana ya Mtume Paulo kabisa, katika jambo hilo hapa. Kwa Mtume Paulo hili ni jambo muhimu
sana, hatuagizi kuomba tu kwa ajili ya watakatifu, isipokuwa, kukesha katika jambo hilo kwa bidii na
kudumu katika sala, kwa maana nyingine, tunapo ombeana, tunatakiwa kuwamacho na kuwa
waangalifu kwa mahitaji ya watakatifu na matokeo ya maombi yetu kwao (watu wengine wangependa
kututaka tuendelee kuwa macho na makini kwa kila aina ya uovu, dhambi na matendo ya uchawi
yanayotuzunguka).

Paulo mwenyewe binafsi anafanya nini? Anaombaje? Zaidi sana anaomba kwa ajili ya watakatifu
akidumu kuomba kwamba wapate kukua na kuongezeka katika upendo na ufahamu wa urithi wao wa
wokovu katika Kristo jinsi ulivyo; karibu maombi yake yote katika Agano Jipya ni ya tabia hii. Hivyo
anawaambia Wafilipi kuwa, anawakumbuka kila wakati anapoomba, na anapowaandikia wanawajulisha
juu ya maombi yake kwa Mungu kwamba upendo wao upate kuwa mwingi sana, (Wafilipi 1:4-9). Huo
ndio ushuhuda wake wa kawaida uhusuo maombi yake, kama tunavyoweza kuona kutoka katika mistari
ifuatayo: Rumi 1:9; Gal.4:19; Efeso 1:16-20, 3:14-19; Kolosai 1:3,9-11; 2:2,3; 1Thes.1:2,3; 3:10; 2Thes
1:3, 11,12; 2Tim.1:3; Philemon 1:4. Epafra anaomba maombi ya jinsi hiyo hiyo (Kol. 4: 12).

Kwa hiyo tunaona kwa uwazi kuwa, mifano na kumbukumbu nyingi za maombi katika nyaraka za Agano
Jipya yanajishughulisha na maombi kwa ajili ya watakatifu kutoka kwao ndani ya Kristo na kwa ajili ya
huduma ya kanisa kwa wengineo. Iko mistari mingine ambayo ni kama mausia ya maombi - kama vile
Kol.4:2 na 1Thes.5:17; wengine wanafanya marejeo kwa mambo maalum kwa ajili ya kuwaombea, na
tutaangalia katika jambo hilo kwa karibu zaidi. Lakini tena hapo napo hatuoni hata andiko moja ambalo
linatusihi tuungame au kutubu kwa ajili ya dhambi za wasioamini katika maombi yetu.

Hii sasa inatupeleka mbali zaidi katika jambo lingine ambalo Kristo aliomba katika Yoh. 17:20,

wala sio hao tu ninaowaombea, bali na wale watakaoamini kwa sababu ya neno lao.

Kwa hiyo, Yesu anaendelea kuomba sio tu kwa ajili ya wanafunzi wake, bali na kwa wale watakaoamini
kwa neno lao, hapo anawaombea wale ambao baadae wataongezeka kwa kanisa. Kwa hiyo Kristo
anategemea kuona wengine wakiokolewa pia kwa kupitia huduma ya watumishi wake. Hadi kufikia
mwisho bado anawasihi kuomba kuwa, Bwana wa mavuno atume watenda kazi, na kwa hakika yeye
mwenyewe anawaagiza kuihubiri Injili kwa kila kiumbe, Luka 24:46-47 na Mark 16:15-16. Na pale
yanapotokea matatizo tunaliona kanisa likiomba sio dhidi ya mamlaka na uweza wala sio kuzitubia
dhambi za hao waliomo katika miji hiyo, isipokuwa ni kulingana na mfano wa Yesu Kristo mwenyewe
katika Yohana 17 - wanaomba ili Bwana awape ujasiri kulinena neno lake, na kuwa Bwana atende
ishara na maajabu katikati ya watu (Mtd. 4: 29-30). Katika Warumi 15:30-32, Paulo anawaomba wakristo
wa kirumi kuungana naye katika kuomba kwa ajili ya kazi ya huduma na kwamba ili apate kuokolewa
kwa ajili ya wasioamini katika Yudea.

29
Hakuna sehemu yoyote inayotaja kutubu kwa ajili ya wanaoipinga Injili. Angalia kwa makini sana hapo,
utaona kuwa sio hapo wala penginepo popote pale katika nyaraka zake kwa Warumi (pamoja na sura ya
9-11) ambapo Paulo anajaribu hata kuelekeza tu wale wakristo wa kirumi kwamba eti watubu kwa ajili ya
dhambi za Rumi na ufalme wake - ambao umeshinda na kukaliwa na nchi ya Israel na sasa wanaitawala.
Katika nyarak zake hizo, alikuwa na fursa ya kifalme ya kuwaambia kuwa Rumi imetenda dhambi dhidi
ya watu wa Israel, na kwamba kama lilikuwa ni jukumu lao la kiroho, kama wenyeji wa Rumi, kuzitambua
dhambi za nchi yao na kisha kuzitubia dhambi hizo dhidi ya Israel. Zaidi ya hayo yote, bila shaka kama
ilivyo kwa ye yote yule anayajua maandiko ya Agano la Kale yahusuyo toba na umuhimu wa taifa la
Israeli, lakini Paulo bado hawaagizi wakristo wa kirumi watubu kwa ajili ya dhambi za Warumi au
za wengine - hafanyi hivyo hata kidogo! Hatuioni kabisa aina hii ya mafundisho yao ndani ya nyaraka
zake, kama vile ilivyo ndani ya Agano Jipya lote, hivyo, kwa sababu ingekuwa ni udanganyifu kufanya
hivyo. Anawaonya kwa uangalifu sana wasio na watu wenye kujivunia akili, kinyume na wayahudi (sura
11), lakini bado hakuwaomba watubu kwa ajili ya dhambi za watu wengine. Sasa iwapo mitume
wenyewe hawafundishi hivyo, je, hawa walimu wa kisasa wanachukua kutoka wapi hizi mamlaka
na ufunuo huo? Kwa masikitisho makubwa, hawaupati toka kwa Mungu.

Mtume Paulo anapowaandikia Wakorintho, anawaandikia katika moyo huo huo (2 Kor 1:11), anawaomba
wamwombe yeye mwenyewe pamoja na wale wote walio naye. Tumekwisha kuona katika Efeso 6 jinsi
Mtume Paulo anavyowasihi ili waombe kwa ajili ya watakatifu. Kadhalika katika ule mstari wa 19
(kulingana na kielelezo au moyo wa Yesu unaopatikana katika Yoh.17), anawaomba kuwa apate kupewa
usemi ili kuihubiri Injili yenye nguvu, anayaomba makanisa mengine kuomba vivyo hivyo. Kwa mfano,
kuomba kwa ajili yake na huduma ya Neno la Mungu lipate kuendelea. Wafilipi 1:18,19; Kol. 4: 2,3;
1Thes.5:25; 2Thes3:1. Tafadhali, hapa usijaribu kufikiria kuwa labda tunatafuta tu baadhi ya mistari
michache, tuliyoichagua. Mafunzo haya yanahusiana na karibu kusihi kote kwa maombi katika Agano
Jipya. Zaidi ya yote kumbukumbu zote zinazohusiana na toba hazielezei chochote kile kuhusu eti
mwamini atubu kwa ajili ya dhambi za kitaifa au miji. Hali kadhalika anawaelezea wafilipi kuwa
wayafanye mambo yote pasipo manunguniko na kushutumiana. Kwa nini basi anafanya hivyo? Ili
kwamba wawe ni watu wasiolaumiwa na wasio na madhara, wana wa Munguwale waliomo katikati
ya taifa linaloenda kombo na lenye ukaidi, ambamo ninyi mnawaka kama nuru ulimwenguni, mkilishika
kwa ukamilifu lile neno la uzima.

Ni jambo la muhimu kwa Mtume Paulo kwamba anapaswa kumweleza Kristo kwa namna zote mbili, kwa
tabia yao na kupitia ushuhuda wao. Hayo yote yanafanana na maombi ya Yesu katika Yoh.17 ambapo
anaomba kuwa wapate kutakaswa kwa ile kweli kama vile yeye alivyotumwa hapa ulimwenguni, ili
wengine wapate kuamini kupitia Neno lao (mstari ule wa 17-20), na kwamba wote wapate kuwa kitu
kimoja.

Kama vile nilivyokwisha eleza hapo mwanzoni, kuwa kuna mistari mingine ambayo inatuagiza zaidi jinsi
itupasavyo kuomba. Katika 1Tim 2:1-4, tunasihiwa kuwaombea watu wote, na Mtume Paulo anawataja
rasmi, kuwaombea wale waliopo katika mamlaka na kadhalika anataja kusudi la maombi ya jinsi hiyo,
sala na maombezi yaani tunapaswa kuwa na tabia za aina hiyo, za kijamii, ambayo itatupelekea sisi
kuishi maisha ya kimungu katika amani. Mstari wa 3 na wa 4 inaoonyesha kuwa tunapaswa kuomba kwa
mtinndo huo, kwa sababu itawezesha pia kujenga nia ya kuieneza Injili kwa wanaume na wanawake.

Hivyo inatupasa kuwaombea wale walimo katika mamlaka serikalini, kwamba tuwapate watu wa jinsi hiyo
ambao wanaweza kukuza uaminifu, haki na hali ya amani ambavyo ni msaada mkubwa katika kuenenza
Injili ili kuifikia mioyo ya watu; kuliko kuwa na mashambulizi, vita na masharti mengi yasiyo ya haki.
(Ijapokuwa tunaelewa kutoka katika kitabu cha matendo ya mitume kuwa tunapaswa kuieneza Injili hata
katika hali ya mateso).

Kwa hali hiyo, naona ni vema kuitaja Warumi 13:1-7, na Tito3:1,2, ambapo sehemu zote mbili
tunasisitiziwa kujinyenyekeza kwa wenye mamlaka na kuwapa heshima wanayostahili, na wala tusinene
mabaya juu ya mtu yeyote, ijapokuwa mtiririko wa aya hizo zinaweza kutofautiana kidogo, hata hivyo
mstari unaopatikana kutoka katika 2 Petro2:10-12 umebeba mambo yanayofanana hapa pia; katika
ukweli kwamba mafungu yote mawili ya maneno yanatusisitizia na kutuonya tusiwakemee na
kuwashutumu wale waliomo katika mamlaka. Kwa maneno mengine, usijifikirie kuwa wewe unayo haki
ya kuja na kusuta, kulaumu na kutamka hukumu dhidi ya hao waliomo katika mamlaka kama
walivyofanya baadhi ya manabii wa Agano la Kale, eti kwa sababu tu wewe ni mkristo na wao ni watu wa
dunia. Tena, hitilafu nyingi na michanganyiko inatujia kutoka kwa watu wanaoitumia vibaya mifano ya
Agano la Kale - wao wanafikiri kuwa kama manabii wa Bwana walivyowakemea watu wa Bwana katika
Agano la Kale, kwa hiyo wakristo wanaweza kuwakemea walio kwenye mamlaka na walio katika jamii.
Mitume wa Bwana hawakufanya hivyo!

30
Lakini hayo yote, kwa ujumla ni mambo ya kulichanganya kanisa na ulimwengu, neema na sheria.
Haupo mstari au mfano wowote wa Agano Jipya, wala hayapo mafundisho yoyote yatakayo tupeleka sisi
na kufanya au kusema kwa jinsi hiyo. Hebu ujifunze kitabu cha Matendo ya Mitume kwa wakati wako
mwenyewe, utagundua kuwa kulikuwepo na uovu na udhalimu mwingi katika jamii katika siku hizo; lakini
je, watakatifu walijiheshimu namna gani? Kwa hakika, hebu tuihubiri Injili, lakini tuwe macho sana na hao
wanaochanganya matengenezo ya jamii na Injili. Msingi mkuu wa huduma ya kanisa kwa ulimwengu ni
kuleta mabadiliko ya ndani kwa waume na wake; kutoka katika mauti kuelekea uzimani. Kutoka katika
dhambi kuelekea haki. Lakini iwapo utazidisha kukazia zaidi juu ya matengenezo ya jamii, watu
watashindwa kuelewa kuwa Injili inahusu nini hasa?

Bila shaka tunaweza kuchagua kuzitumia haki zetu za kidemokrasia, ikiwa tunazo na dhamira zetu na
imani; lakini kuhubiri na uwasilishaji wa Injili nyakati hizi za neema ni, na inapaswa kuwa tofauti kutoka
katika namna ambayo manabii wa Agano la Kale walikuja kulisema neno la Mungu. Zipo siku nyinginezo
ambapo wanayachanganya mambo haya na kutaka kuturudisha nyuma kwenye njia za kufikiri na
kutenda za kiagano la kale; ambazo kwa hakika hizo zilikwisha kuondolewa katika Kristo. Hapa sisemi
kuwa tusiwaambie watu juu ya hukumu inayokuja, isipokuwa ninachokisema hapa ni kuwa hakuna
awezaye kutushurutisha kufanya lolote lile ambalo hatuamriwi kulifanya katika maandiko ya neno la
Mungu. Kwa mfano, si Yesu wala Mitume waliipinga mamlaka ya utawala kwa ajili ya matengenezo
ya kisiasa au jamii ijapokuwa kulikuwa na maovu mengi nyakati hizo. Watu wengine wanadai kuwa
eti hawakuweza kufanya upinzani huo, kwa vile kulikuwa hakuna uhuru wa kufanya hivyo wakati huo.
Lakini iwapo hilo ni jukumu la Mkristo kufanya kampeni kwa ajili ya kuleta mabadiliko, je, lisingekuwa ni
jukumu la mitume kufanya hivyo pia kwa hali yoyote iwayo kwa jamii? Hata hivyo, cha muhimu zaidi ya
hilo ni kwamba hatulioni agizo lolote lile kutoka kwa Bwana Yesu mwenyewe, wala kutoka maandishi yao
mitume wenyewe (kwa ajili ya kizazi chochote kijacho ambacho kitakuwa na uhuru zaidi wa kupinga)
kiasi kwamba tunapaswa kufanya kampeni kwa ajili ya matengenezo ya kijamii au kuwashutumu wale
waliomo madarakani. Hapa sisemi kuwa wakristo hawawezi kujishughulisha na matengenzo ya kijamii
wanapopata fursa ya kufanya hivyo; lakini kile nisemacho ni kwamba, hakuna yeyote yule aliye na haki
au mamlaka kutoka katika Agano jipya linalosema kuwa Mkristo anapaswa kujihusisha katika
siasa kwa jinsi hiyo. Kila mtu ashawishike na dhamira yake mwenyewe na hivyo atende ipasavyo
pasipo kulazimishwa na kuhukumiana. Bila shaka katika mambo makubwa zaidi pale ambapo uovu wa
haki au watu waovu wanaweza kutushurutisha kufanya mambo kinyume kabisa na mapenzi ya Mungu,
lazima tuweke msimamo. Katika tukio lolote lile nia yetu kuu iwe ni kuwaona watu waume kwa wake
wakizaliwa katika ufalme wa Mungu wa haki, furaha na amani; ambayo historia pia imeonyesha kuwa
ni mambo yenye mafanikio makubwa katika kuibadilisha jamii kuliko aina yo yote ile ya kampeni
ilivyoweza kufanya.

Mwisho hebu tutazame katika maelezo ya Mtume Paulo kwa Warumi, (Warumi 9:1-3 na 10:1). Hapa
anaelezea hamu yake waziwazi, ya kusikia kuwa Israel inaokolewa na kwamba anayo huzuni nyingi
isiyokoma kwa sababu ya ugumu wa ndugu zake kwa jinsi ya mwili wanaosimama kinyume na Injili.
Huzuni zake ni kubwa kwa sababu ya wao waliofanywa kuwa wana wa ule utukufu na maagano (mstari
wa 4). Na kwa sababu hiyo, vile vifungo vyake na huzuni yake kwa ujumla zingeweza kuwa ni kubwa
kuliko ambavyo raia yoyote wa nchi nyingine angeweza kujisikia kwa ajili ya watu wa nchi yake, ambao,
kwao kule kufanyika wana wa maagano haikutumika mwanzoni kama vile ilivyofanywa kwa Wayahudi.

Ili kwamba watu wapate kuokolewa ni jambo jingine tena lililo wazi katika mioyo yetu - linaonyesha nia
yake Mungu ndani ya mioyo yetu - hasa kwamba kuomba kwa ajili ya watu walio jirani nasi kwa namna
fulani inaweza kuwa ni familia au jumuia. Lakini tafadhali uangalie hapa kuwa, hakuna sehemu yoyote ile
ambayo Mtume Paulo anaonyesha akitubu kwa ajili ya ugumu wao, kule kukaa kwao kinyume na Injili.
Ijapokuwa hilo limehuzunisha, bado yeye maombi yake ni kwamba, ili wapate kuokolewa. Angalia
tena tafadhali, kwamba Paulo angeweza kupata fursa nzuri sana hapa ya kuwasihi wauamini katika
Urumi, kutubu kwa ajili ya dhambi za mji wao mkuu na viongozi wao, ambao majeshi yake yalikuwa
yakikalia mji wa Israel pamoja na maeneo mengine ya ulimwengu. Lakini bado hatuoni fununu yoyote
ya mafundisho ya jinsi hiyo hapa wala katika Agano Jipya. Jambo moja tu linalopatikana hapa kwa
ajili ya Wayahudi ni kuomba wapate kuokolewa, ambapo kwa ajili ya hilo Biblia inatupatia sababu za
kutosha kutuwezesha kufanya hivyo.

Lakini ni jambo la tofauti kabisa leo kuwaambia watu kwamba wanapaswa kuunga mkono Serikali ya
kisiasa ya Israel. Hakuna mstari hata mmoja katika Agano Jipya unaotusihi tufanye hayo. Niko
mwangalifu sana juu ya maandiko ya neno la Mungu, na mistari mingi iliyomo ndani ya Agano la Kale
ihusuyo Israel; lakini jambo Mungu mwenyewe alipendezwa nalo ni vile uhusiano wake yeye mwenyewe
na Israel, kwamba wawe ni watu watakatifu, wamtumikie yeye pekee. Israel waliposhindwa kutimiza hilo

31
Mungu naye hakuweza kuuheshimu unyoofu wa Taifa lao. Wakati ambapo manabii wengine walipokuwa
wakitoa unabii nyakati zile za Yeremiah alisema kuwa kwamba Israel watakuwa na amani, na wala
hawataona vita. Bali Yeremiah alisema maneno ya Mungu kwao kama vile, Taifa lao litaangamizwa na
kwamba watatapanywa mbali utumwani (lakini baadae baadhi yao wangerudi kulingana na neema yake).
Kwa hiyo, tunaona wazi kuwa hata katika nyakati hizo Mungu hakuwa akiunga mkono Serikali ya nje ya
kisiasa wakati ambapo mioyo yao ilipokuwa mbali naye.

Jambo hili halitofautiani kabisa na nyakati hizi za leo, lakini tena watu wengine nyakati hizi hizi za leo
wanachanganya kwa matamko yao kuelewa kwao juu ya Agano Jipya na Agano la Kale, hali kadhalika
hawafahamu jinsi gani Kalvari ilivyobadilisha mambo haya, lakini wao wangetamani kuwataka watu leo,
ili waombe na kufanya mambo yanayounga mkono mambo ya kimwili ya kiinje ya serikali ya kisiasa ya
Israel ambayo wala haimtambui Mungu. Ni taifa la kidunia tu; wapo pia Wayahudi wa Othodox ndani ya
Israel ambao wanakataa kulitambua taifa la kisiasa la Israel ni kutokana na sababu hiyo ya msingi wao
wanafanya hivyo. Wanaamini kuwa, kwa vile Mungu amewarejesha katika nchi yao, hata hivyo
atawashughulikia tu - iwapo wataweka matumaini yao kwake Mungu na sio katika nchi nyingine.
Ninarudia tena kusema kuwa, ni jambo moja tu tupaswalo kuomba nalo ni kwamba wapate kuweka
matumaini yao katika Kristo ya kwamba ni mwokozi wao. Lakini, badala yake, sasa tunawaongoza watu
waende mbali na Mungu pale tunapojaribu kuwaambia kuwa eti wanapaswa kuunga mkono taifa la
kisiasa la Israel.

Je, Yehoshaphat hakukemewa na manabii wa Mungu kwa ajili ya sababu hiyo? Kama pale
alipounga mkono ndugu zake waisrael wakati ambapo kwa kupitia kwa Ahabu walikuwa wamempa
Mungu mgongo, 2Nyk.18:3 na 19:2 - uaminifu wa kimwili kwa kweli unapingana na kusudi la Mungu. Siyo
kwamba najihusisha katika mjadala kuhusu kanisa na Israel, bali jambo pekee ambalo ninalifanya kwa
kiasi fulani ni hili kwamba; wazo kuwa tunapaswa kuunga mkono Serikali ya kisiasa ya kiinje ya taifa la
Israel, halijawahi kufundishwa na Yesu wala manabii. Kulingana na Injili, ni sawa kuwa tunaweza kuomba
kwa ajili ya Wayahudi, lakini ukienda ndani zaidi hadi kufikia hatua ya kuunga mkono serikali yao ya
kisiasa ambayo ni ya kiinje tu, basi hapo yakupasa uwe mwangalifu ili kuona kuwa huungi mkono kitu
ambacho kinakataa kumtambua Mungu na kujikabidhi katika kweli na neema yake.

Tafadhali sana, unaweza kwenda sana katika maombi yako kadiri unavyoamriwa na maneno ya Mungu,
lakini uwe makini kuona kuwa huvuki mipaka ya maandiko ya neno la Mungu na bila shaka
usiwashurutishe watu wa Bwana na kufanya hivyo. Pia ukumbuke kupambanua kuwa yeye ni Myahudi
aliye Myahudi kwa ndani, na sio Myahudi aliye Myahudi kwa nje. Rumi 2:28,29. Usije ukachanganya
mwili na Roho, ulimwengu na kanisa, Agano la Kale na Agano Jipya.

Mambo ya Kufikiria Mwishoni

Mwisho, hebu tuangalie ni jinsi gani fundisho hili, kwa kweli, linavyoiinua torati ya Agano la Kale juu ya
neema ya Agano Jipya, na linavyotafuta kutuweka kwenye utumwa kwa hoja zinazopingana na Injili.
Labda kwa kutambua kuwa hii hoja ya dhambi za vizazi na kuzitubia haifundishwi katika Agano Jipya,
mwalimu mmoja anajaribu kuhalalisha fundisho hili kwa njia ya ajabu kabisa. Na haya yafuatayo ndiyo
majibu yake akisema, Inapaswa kuwa wazi kuwa hatujaokolewa kwa kutunza torati ya Agano la Kale,
isipokuwa tumeokolewa kwa imani na kwa toleo la damu yake Yesu kwa ajili ya dhambi zetu. Anaendelea
kusema zaidi kuwa, hii haimaanishi kuwa chimbuko la kina la amri kumi zilizotajwa katika Kut. 20:3-17 na
Kumb. 5:7-21, ilibatilishwa kwa imani katika Kristo. Wanadai kuwa Mtume Paulo anatuonyesha hayo yote
kwa uwazi kabisa katika Warumi 3:31, pale ambapo Paulo anasema, hatuibatilishi sheria bali
tunaithibitisha sheria kwa imani katika Kristo; na hivyo huyo mwandishi wao anahitimisha kuwa imani ya
Agano Jipya inatilimilizwa na kuthibitisha chimbuko la kina la sheria ya Agano la Kale (torati) kama ilivyo
katika Rumi 8:4, 13:8! Na ni chimbuko gani la kina la Agano la Kale ambalo Agano Jipya linatimiliza
sasa?

Kwanza kabisa, katika makala hiyo yake ijapokuwa ananukuu hizo sehemu 3 za maandiko ya Agano la
Kale, kimsingi na kama sio kipekee, mwandishi huyo anahusika kabisa na kule kuyathibitisha mawazo ya
dhambi na vizazi; ambayo imejitokeza tu katika mstari mmoja ndani ya kila habari kama nilivyokwisha
kutangulia kusema hapo juu. Hupenda kuthibitisha yale mawazo yake tu ya dhambi za vizazi, kama vile,
kwamba eti, dhambi inaweza kuendelea toka kizazi hadi kizazi na kwa hiyo inatupasa kuungama na
kutubu kwa ajili ya dhambi hizo ili kwamba tupate kuachiliwa kutoka katika laana na hukumu. Hapo
haelezi mengineyo (uhakika au utukufu) yahusuyo tabia ya Mungu anapo ya Mungu kumbushia katika
nyaraka hizo. Hivyo anachotaka kutueleza hapa ni kwamba, kutokana na Warumi 3:31 na 8:4, imani
katika Kristo inathibitisha kweli ya dhambi za vizazi na ushirikishwaji! Imani ya Agano Jipya inathibitisha

32
torati; na dhambi za vizazi zimetajwa katika torati; kwa hiyo dhambi ya vizazi ni sehemu ya kweli ya
Agano Jipya! Eti hiyo ndiyo sababu yake ya msingi anayoitoa. Tohara ilikuwa ni sehemu ya torati, na
iwapo imani ya Agano Jipya inaithibitisha torati kwa namna anavyosema, je, si sote tunapaswa
tutahiriwe?! Je, unaweza kufikiria kuwa Paulo alikuwa anawaza hivyo alipokuwa akiandika mistari hiyo
katika waraka wa Warumi? Ikiwa ndio hivyo, kwa nini fundisho hili haligusiwi hata kidogo mahali popote
katika maandishi yake?

Jambo la pili: Je, umewahi kusikia kuhusu chimbuko la ndani kabisa lihusulo tabia ya Mungu ambayo
ilijitokeza katika Agano la Kale na jinsi ilivyolinganishwa na ile iliyomo katika Agano Jipya? Je, hii ina
maana gani? Mpendwa msomaji, napenda kukualika usome Amri kumi katika Kut. 20; kisha usome
Matayo sura ya 5 mpaka ya 7. Unafikiri nini hapo? Je, ni sura ipi ambayo inakupatia kwa kina zaidi juu ya
ukuu na zaidi ya yote pamoja na utukufu wake - ule mwanga wa tabia ya Mungu pamoja na torati? (Ikiwa
tunatumia neno torati hapa kwa ukweli ambao Yesu anauelezea ndani ya sehemu yake katika Mathayo,
huo ni mwanga wa kutosha wa maisha halisi ya Mungu ndani ya mtu; sio maisha yale ambayo mtu
anayapata kwa kujitahidi kwake mwenyewe katika kutunza torati. Hii ndiyo sababu inasemwa kwamba
torati ilikuja kupitia Musa, lakini kweli na neema imekuja kupitia Yesu Kristo). Yesu alisema, Yeyote
anionaye mimi amemwona Baba. Je, kulifunuliwa nini kwa sehemu au kwa aina, na zaidi sana kwa nje
katika Agano la Kale? Jambo hili kwa sasa limefunuliwa kwa utukufu zaidi na kwa njia ya ukamilifu
kupitia Kristo, ambaye hutupatia utukufu huu na ukamilifu ndani yetu kwa Roho. Ni kweli tunayo kila
sababu ya kumshukuru Mungu na kuitukuza Injili yake ya neema na kweli.

Hebu sasa utazame katika, 2Wakor.3:6-18; 4:6; Wakol.1:27; 1Petro1:10-12; Waebr.1:1-3; 7:18,19;10:1.
Kutokana na maandiko hayo, wanawezaje kusema kuwa Agano la Kale linayo hali yenye kina zaidi
ihusuyo tabia ya Mungu kuliko Agano Jipya? Mungu habadiliki, na upendo wake, upole na uvumilivu
wake, hali kadhalika na hukumu zake zimejitokeza wazi kabisa katika Kristo, utukufu wa tabia yake,
neema ya kusudi lake la umilele kwa ajili yetu na kina cha wokovu imefunuliwa kwa njia yenye utukufu na
ya ndani zaidi. Paulo anatuambia kwamba utukufu wa Agano Jipya ni mkubwa zaidi kuliko ule wa
zamani, ndiyo kusema kuwa kwamba ya zamani haina utukufu kwa kulinganishwa!

Jambo la latu: wananukuu warumi 8:4 ili kusudi kuhakikisha kuwa mawazo ya dhambi za vizazi katika
torati yametimilizwa au kuthibitishwa ndani ya Agano Jipya; pengine hakuna chochote kinachoweza
kuonyesha kwa uwazi jinsi ambavyo, siyo tu kwamba hawaelewi Agano Jipya bali pia hulinyanganya
uweza wake na maana yake halisi, kwa kupitia mafundisho hayo yao. Warumi 8 inayo mistari muhimu na
yenye utukufu katika Agano Jipya, ukijumlisha mstari 1-4 kwa kupitia kifo na ufufuko wa Kristo - sasa
tumewekwa huru kutokana na sheria ya dhambi na mauti. Ni mara ya kwanza katika historia ya
mwanadamu; toleo la sheria halikuweza kutupatia haki, isipokuwa kwa ujumla liliweza tu kututhibitishia
kwamba sisi hatuna haki; na kisha tupo katika vifungo vya dhambi, hivyo hatuna uwezo wa kukaribia
katika uwepo wa Mungu (Rumi 3: 10-12,19,20; 7: 7-11; Gal 3:19; Heb 9:8); na kwamba tuna haja ya
wokovu, njia pekee ya kutupatia uzima. Uzima wa milele ni kutufanya tuwe wenye haki; hakuna tofauti ya
hakika kati ya uzima kama ulivyo katika Mungu na haki (Gal. 3:21; Rumi 5:21). Basi tena kwa kupitia
Adamu wengi walifanywa kuwa wenye dhambi, hali kadhalika kwa kutii kwake Kristo wengi walifanywa
wenye haki, kwa sababu Mungu alimfanya kuwa dhambi ili kwamba tupate kufanywa wenye haki kwa
Mungu katika yeye. Rumi 5:19; 2Kor.5:21. Huo ndiyo uwezo na utukufu wa Habari Njema!

Ni sehemu gani ya sheria katika Agano la Kale ambayo Mungu alipenda kuikamilisha ndani yetu? Sio
sehemu za wonyesho wa Ibada! Wala hakuna chochote kiwezacho kuleta laana na hukumu! Ilikuwa ni
haki ya sheria - hiyo ndiyo iliyotuletea mwanga wa hali yake ya utukufu na haki ya ile tabia yake. Hicho
ndicho alicho nacho toka katika umilele. Alipenda kukileta kwetu, kama vile, ile haki yake yeye
mwenyewe na maisha ya utukufu wake! Ilikuwa ni njia pekee ya kutupatia uzima wa umilele kutufanya
kuwa wana wake kulingana na tabia yake yeye mwenyewe. Ni Injili ya jinsi gani hiyo? Je, ni neema ya
jinsi gani hiyo? Ni upendo wa jinsi gani huo? Tazama ni upendo wa jinsi gani ambao Baba ametupatia
kwamba tuitwe wanawa Mungu, 1Yoh. 3:1; na pia tazama Gal.3: 21; Efeso1:4,5; Rumi 8: 15-17; 29;
2Kor 4:10 ,11; 2Tim 1: 9; Heb 12:10, 1Petro 1:15, 16; 2Petro 1:3,4; 1Yoh. 4:17.

Mpendwa msomaji, ukiitazama mistari hiyo hapo juu kwa makini sana, utagundua kuwa hii ndiyo ile,
ambayo Rumi 8:4 inaelekeza yale ambayo torati haikuweza kuyatimiza, yale ambayo damu ya
mafahari ya ngombe na mbuzi hayakuweza kuyafanya; yale ambayo jitihada nzuri kabisa za watu wazuri
kabisa hawakuweza kuyafanya - Mungu ameyafanya sasa ndani ya Mwana wake; mwanakondoo wa
Mungu ameziondoa dhambi zetu, akihukumiwa katika mwili wake na hivyo pia hakiharibu uweza wake na
mashutumu yake juu yetu ili kwamba ile haki inayopatikana kwa sheria ipate kutimilizwa ndani yetu

33
sisi ambao hatuenendi kwa sheria bali katika Roho. Hii ina maana kwamba, uzima wake upate
kudhihirishwa ndani yetu, pamoja na haki yake, neema yake, upendo wake, upole na uvumilivu wake.

Hivyo ndivyo inavyohusika na ile Warumi 8, kama vile, kuwa na uzima wake Yesu ndani yetu. Nashangaa
wanawezaje basi kuchukua mstari huu wenye utukufu wa namna hii na kuanza kuutumia vibaya namna
hii, ili tu kukidhi udanganyifu wao! Naona bila shaka hawafanyi hivyo kwa kusudi, hata hivyo wanahusika
kwa ajili ya kuyakataa na kuyapinga yale ambyo yanaelezwa na maandiko ya neno la Mungu, kama
wafanyavyo katika mafundisho yao kama tulivyoeleza katika makala hii. Hakuna chochote kile
kinachoelezea kwa undani kama Kalvari wala hakuna lolote lenye ukuu kama Kalvari; katika matukio
yote yaliyopo ya kihistoria pamoja na mafunuo ya Mungu kwa wanadamu Kalvari inaelezea kila kitu na
kwa kweli imepata kila kitu.

Tafsiri zao katika mistari hii ya Warumi, pamoja na kufasiri kwao bado inaonyeshwa wazi jinsi
wanavyozingatia maandiko ya Agano la Kale, wakiyatengeneza na kuyatukuza zaidi kinyume na Agano
Jipya. Wanatangaza mistari ya Agano la Kale kiasi kwamba inadharirisha na kuuharibu ukweli wa Agano
Jipya -sawa sawa kabisa kama ilivyokuwa katika makanisa ya wagalatia!

Hii ni hitilafu na udanganyifu wa aina ile ile ya wagalatia; hii ni ulozi. Hata kama wanakubali ukweli
mwingineo juu ya Yesu Kristo kama walivyofanya wale walimu waa uongo kule Galatia, hata hivyo yale
wanayoyaongezea katika ukweli, kwa hakika waliutangua ukweli.

Na hii ndiyo sababu ya kuandikwa kwa makala hii. Watu ambao walisumbuliwa, walichanganywa au kwa
kiasi fulani kusita kuhusishwa na mafundisho haya waliniomba niweke kitu fulani katika maandishi ili
kuwaelezeni mambo hayo jinsi yalivyo kutokana na maandiko ya neno la Mungu. Ni matumaini yangu
kuwa nimefanya itoshayo kuonyesha wazi kuwa mafundisho haya mapya hayana nafasi yoyote katika
Agano Jipya (na wala hayatakuja kuwa na nafasi yoyote katika nyakati zijazo hata milele) na kwa hiyo,
yasipewe nafasi yoyote katika mioyo yetu. Tumeweza kugusia sehemu za ndani na kubwa kuhusiana na
somo hili (kama vile mambo ya maombi, maombezi na wokovu) ndani ya makala hii. Lakini hatukufanya
hivyo kwa nia ya kutoa ufahamu wa undani wa mafunzo juu ya kila mmoja wapo, bali kusudi haswa la
makala hii ni kutazama kwa kina juu ya maandiko ili kuona yanavyoenda pamoja na mambo
yanayohusiana na muungano, maombi na toba; kisha kuyapambanua kwa uwazi zaidi kuwa yanasema
kitu tofauti sana na mawazo yale wanayoyafundisha katika mafundisho yao ya kisasa.

Kungekuwa na mambo mengi sana ya kusema juu ya somo hili, na kwa hakika sijaelezea kila jambo
moja moja ambayo hawa walimu wa kisasa huyafanya - kama nisingefanya hivyo ingebidi makala hii
kuwa ndefu zaidi kuliko ilivyo sasa, lakini bila hata kuongezea kitu chohote juu ya yale mambo ya
kimsingi ambayo ninaamini nimeweza kuyaelezea.

Mpendwa, naomba nikuachie mstari kutoka katika Gal. 5:1,

kwa hiyo simameni wala msinaswe tena chini ya kongwa la utumwa.

Neema ya Bwana Wetu Kristo iwe nanyi!

David Stamen 2002 somabiblia.com

34
35

You might also like