Professional Documents
Culture Documents
Mwongozo - Huduma Za Watoto Copy 2
Mwongozo - Huduma Za Watoto Copy 2
HUDUMA ZA WATOTO
KIMEANDALIWA NA
Idara ya Huduma za Watoto na
Taasisi ya Wachungaji ya Halmashauri Kuu ya
Kanisa la Waadventista wa Sabato
Kwa Kushirikiana na Idara ya Huduma za Watoto NTUC
Kimetafsiriwa na Moseti Chacha
moseti.chachc@gmail.com
YALIYOMO
Dibaji……………………………………………………….…………….… 4
Utangulizi………………………………………………………………….. 5
Sura ya 1
Filosofia ya Huduma za Watoto………………………………………….. 6
Sura ya 2
Utume wa Huduma za Watoto………………………………………….... 9
Sura ya 3
Huduma ya Yesu kwa Watoto…………………………………….………10
sura ya 4
Mashauri ya Ellen G. White juu ya Huduma za Watoto………..……….. 12
Sura ya 5
Historia Fupi ya Huduma za Watoto……………………..……………… 13
Sura ya 6
Maelezo ya kazi ya Mratibu wa Huduma za Watoto…………………… 16
Sura ya 7
Uratibu wa Kamati ya Huduma za Watoto………………………………19
Sura ya 8
Tabia Nane za Huduma za Watoto zenye Afya katika Kanisa…...…….. 22
Kuwezesha Uongozi…………..…………………………….…… 22
Huduma inayoongozwa kwa karama……………..…….………. 23
Hali ya kiroho yenye msisimko…..……………………….……… 45
Miundo inayotenda kazi………………………..………….…….. 52
Huduma za Ibada zinazovutia………………………………...…. 53
Vikundi vidogo vya ujumla……………………………………..… 54
Uinjilisti uliojikita katika mahitaji………………………………… 56
Mahusiano ya upendo…………………………………………… 59
Sura ya 9
Miongozo ya Ubatizo na Mapendekezo ya Watoto…………….....……60
Sura ya 10
Matamko ya Konferensi Kuu kuhusu Watoto…………………………..64
Matamko juu ya Ustawi na Thamani ya Watoto…………...……64
Matamko juu ya Unyanyasaji wa Watoto………………………. 65
Sura ya 11
Programuu za Huduma kwa Watoto kwa ajili ya Kanisa mahalia…..…69
Programu Zinazo Wafikia Watoto Ndani ya Kanisa………….... 70
Shule ya Sabato ya Watoto……………………...……… 70
Kanisa la Watoto…………………………………………. 71
Mkutano wa Maombi wa Watoto…………………….… 70
Darasa la Ubatizo la Watoto………………………….…. 71
Kwaya ya Watoto…………………………….………….. 72
Sabato ya Watoto……………………………………….. 72
Mkutano wa Watoto………………………………....…. 73
Mkutano wa Watoto wa Uinjilisti………………………. 73
Chama ya Wahubiri Wadogo…………………………….74
Kongamano la Muziki la Watoto…………………..…… 74
Kambi la Watoto la Uoto wa Asili………………………. 74
Programu Zinazo Wafikia Watoto Wapya…………………….. 75
Shule ya Biblia wakati wa likizo……………………….... 75
Chama cha Biblia cha Mtaa……………………………... 75
Vikundi vya Michezo……………………………….…… 76
Sanaa Mwisho wa Juma………………………………… 76
Karibu Mtoto………………………………………….… 76
Huduma ya Maktaba Inayohama………………..……… 77
Mafunzo ya Biblia Majira ya Joto……….....……………. 77
Sura ya 12
Nyenzo
zinazopendekezwa………………………………………………………79
Vitabu……………………………………….….…………………79
Magazeti………………………………….…….……………….. 80
Tovuti……………………………………….….………………... 80
Hitimisho……………………………………………..…………………. 82
DIBAJI
A
gizo la Kristo la Kulisha Kondoo (Yohana 21:5) na kuruhusu watoto
waje Kwake (Marko 10:13, 14) linatoa mamlaka kwa kanisa kufanya
uinjilisti kwa watoto na kusimamia malezi yao ya kiroho. Kitengo
cha Huduma za Watoto katika kanisa la Waadventista wa Sabato
kimejitoa kikamilifu katika kutoa nyenzo, kuwezesha na kuratibu upanuzi na
uimarishaji wa malezi ya kiroho kwa watoto katika kanisa, ili kuwaleta katika
uhusiano wenye upendo, wa kutumika na Yesu na kujikabidhi kwa kwa dhati
katika kanisa la Waadventista Wasabato.
Kitabu hiki ni mwongozo kwa wachungaji, wazee wa makanisa, viongozi
wa watoto wa kujitolea, wazazi na wengine katika makanisa mahalia ambao
wanatamani kuelewa na kujifunza jinsi ya kuratibu huduma mpya za watoto
au kutia nguvu huduma zilizopo tayari. Toleo hili dogo linatoa falsafa na
utume wa Huduma za Watoto, likifuatiwa na mapendekezo ya programu
kwa ajili ya watoto zinazoweza kujaribiwa katika kanisa mahalia. Pia
linajaribu kufanyia kazi tabia nane za kanisa lenye ustawi kama
ilivyopendekezwa na Christian Schwarz, kwa Huduma za Watoto zenye
ustawi, na kwa jinsi hiyo kutoa mtazamo uliokamilika wa Huduma za Watoto
unaopaswa kutenda kazi ndani ya huduma zote za kanisa.
Wachungaji na wazee watagundua kuwa kitabu hiki ni rahisi kutumiwa na
kuwekwa katika iutendaji wanapojihusisha katika malezi ya hali za kiroho za
watoto ndani ya kanisa. Katika ulimwengu wa leo ambapo watoto
wamejawa na mawazo na maadili yanayokinzana na yale ya Kanisa la
Waadventista, ni muhimu kwamba kila kanisa mahalia na kiongozi wake
kutafuta njia za kuwasaidia watoto wetu katika kufanya maamuzi yaliyo
sahihi kuhusu Imani yao.
Chama cha Wachungaji cha Halmashauri Kuu kinayo furaha kuunga
mkono Idara ya Huduma za Watoto ya Halmashauri Kuu ili kuchapisha
kijitabu cha maelezo ya Huduma za Watoto kwa Wachungaji na Wazee. Hii
na iwe nyenzo ya kumwezesha kila kiongozi wa kanisa na mshiriki
anayetamani kulea watoto kuelekea katika uhusiano wenye upendo, na wa
kumtumikia Yesu, na kujenga wanafunzi wadogo wa Kristo waliojikabidhi
kwa Kanisa la leo na la kesho. Hebu na tukumbuke, kujenga kanisa la kesho
kunaanzia kwa watoto wa leo.
James A. Cress, Mkurugenzi. Shirikisho la Wachungaji. Halmashauri
Kuu ya Kanisa la Waadventista wa Sabato. Silver Spring, Maryland
UTANGULIZI
W
engi wetu tunaamini kwamba watoto ndio kesho yetu. Watoto
ndio kanisa la baadae. Kwa hiyo, Kanisa, wazazi, na waalimu
wana jukumu la kuwafundisha kuwa washiriki na viongozi wa
baadae walio imara. Hata hivyo, tunasubiri tu siku za zijazo? Vipi kuhusu
wakati uliopo sasa? Je, tusingeanza mafunzo yetu sasa badala ya kubonyeza
kitufe cha subiri kwa watoto wetu?
Hata hivyo, utafiti unaonyesha uharaka wa kuwekeza muda, nguvu, na
fedha zetu kwa watoto sasa hivi badala ya wakati fulani huko mbeleni.
Utafiti wa hivi karibuni wa George Barna1 unaripoti kwamba asilimia 32 ya
wale waliofanya uamuzi wa kumkubali Yesu walifanya hivyo katika umri kati
ya miaka 5 na 12; asilimia 4 ya wale walio na umri kati ya 13 -18; na asilimia 6
kwa watu wa miaka 19 au zaidi. Kwa maneno mengine, kama watu
hawamkubali Yesu kama Mwokozi wao kabla hawajafikia umri wa
kupevuka, uwezekano wa kumkubali baadae ni mdogo sana.
Umuhimu wa kuwahusisha watoto katika mchakato huu wa kufaya
maamuzi katika miaka yao ya awali ni muhimu katika kujenga kanisa imara
leo. Tunaamini kwamba kujenga kanisa la kesho kunaanza na watoto wa leo!
Kwa hiyo, inaanzia kwa watoto katika makanisa mahalia. Inaanza na kila
kanisa kuwa na mratibu wa Huduma za Watoto ambaye atasimamia
programu zitakazowasaidia watoto kukua katika uhusiano wao na Yesu.
Kwa kuongezea, mchungaji na wazee wa kanisa ni watu muhimu ambao
wanaweza kusaidia, kutegemeza na kutia hamasa viongozi wa watoto
katika kukuza karama zao na muda wao ili kuendeleza Imani ya watoto
ndani ya kanisa. Kwa hiyo, mwongozo huu unatumika kama kiongozi kwa
Wachungaji na wazee katika kuelewa utume na jukumu la mratibu wa
Huduma za Watoto katika kanisa lao mahalia. Mwongozo huu una mawazo,
mapendekezo, na nyenzo zinazoweza kutumika katika kutekeleza
programu na shughuli za watoto.
1
Barna George. Transforming Children into Spiritual Champions. Ventura, California: Regal
Books, 2003
Sura ya 1
FALSAFA ya
HUDUMA ZA
WATOTO
H
uduma za Watoto hutafuta kuendeleza Imani ya watoto wenye
umri kati ya kuzaliwa na miaka kumi na nne. Pamoja na Shule ya
Sabato ambayo inatoa elimu ya dini kwa watoto mara moja kwa
juma, Huduma za Watoto hutafuta kutoa huduma kadhaa ambazo
zitawaongoza watoto kwa Yesu na kuwafanya kuwa wanafunzi katika
kutembea naye kila siku.
Biblia imeweka wazi sana kwamba watoto ni wa pekee kwa Mungu. Kama
utachunguza kile Biblia inachosema kuhusu watoto, utagundua sehemu
kubwa ya taswira kadhaa:2
Watoto ni zawadi kutoka kwa Mungu. Anawapa wazazi watoto kama
ishara ya upendo na utimilifu binafsi (Kum. 7:13; Zab. 127:3).
Watoto ni wa kutamaniwa. Kutoka katika uumbaji, Mungu ametuagiza
kuzaa watoto (Mwa. 9:7; Kum. 6:3).
Watoto huleta furaha na mibaraka kwa watu wazima. Mungu anatoa
faida nyingi kwa wazazi kupitia malezi ya watoto wao (Hes. 5:28; Kum
28:4, 11).
Watoto wanapaswa kufundishwa jinsi ya kuanzisha uhusiano na Mungu.
Moja kati ya changamoto zetu kuu ni kuhamisha Imani zetu na uelewa
wetu wa Mungu kwa watoto wetu (Kut. 12:26, 37; Kum. 6:1-7; Mit. 22:6).
Watoto ni wa thamani sana kwa Mungu kiasi kwamba anatuamuru
tuwalinde. Wazazi wanapaswa kuhakikisha usalama wa kiroho na wa
kimwili wa watoto wao (1 Sam. 20:42; Ezra 8:21).
Mungu anawapenda watoto kiasi cha kuhakikisha wanapata nidhamu.
(Mit. 3:11-12; 13:24; 19:18; Efe.6:4).
Mungu anafurahia asili na haiba ya watoto na anawaambia watu wazima
wajifunze kutoka kwao. Maandiko yanatambulisha tabia kama uwazi,
2
Barna George. Transforming Children into Spiritual Champions. Ventura, California: Regal
Books, 2003
unyenyekevu, urahisi, na Imani kama viwango vinavyopatikana kwa
watoto, na Mungu anathamini tabia hizi (Mat. 18:3; 19:14; Flp. 2:15).
Kama watoto wana thamani kiasi hiki kwa Mungu, basi wanapaswa
kuwa na thamani kwetu pia.
Utume Mkuu wa Yesu ni kwamba: “Enendeni mkawafanye mtaifa yote
kuwa wanafunzi wangu, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na la Mwana na la
Roho Mtakatifu.” (Mathayo 28:19). Hakika, hii inajumuisha kuwafanya
watoto kuwa wanafunzi na kuwaongoza kujitoa kwa dhati kwa Yesu.
Sura ya 2
UTUME
wa HUDUMA
ZA WATOTO
U
tume wa Huduma za Watoto ni kulea watoo ili wawe na uhusiano
wa upendo, na wa kumtumikia Yesu. Tunatafuta kutimiza utume
huu kwa kuendelezea:
W
akati wote wa huduma yake hapa duniani, Yesu alitenga muda
kuhudumia watoto. Kalamu ya Maandiko pamoja na uvuvio
vilidhihirisha wazi wazi thamani aliyoiweka kwa watoto.
Huduma yake ilijumuisha yafuatayo:
E
llen G. White amepokea wahyi kwa wingi kutoka kwa Mungu kuhusu
umuhimu wa watoto na haja ya kuwafundisha wakiwa bado wadogo
kumkubali Yesu kama Mwokozi wao. Anatetea huduma kwa watoto,
na haya ni baadhi ya mashauri yake:
Mwaka 1890 kijitabu cha “Our little Friend” kilianza kubeba masomo ya
Shule ya Sabato kwa ajili ya watoto walio katika ngazi ya msingi na awali,
kilichokuwepo kwa miaka sitini na saba. Mwaka 1957, hicho kitabu kilianza
kuwa na masomo ya Shule ya Sabato kwa ajili ya watoto wachanga pamoja
na wale wa madarasa ya awali. Masomo ya Shule ya Sabato kwa ajili ya
Watoto wa shule za msingi yalitokea katika chapisho jipya liitwalo, Primary
Treasure mwaka 1957. Lesoni za Shule ya Sabato kwa ajili ya umri wa shule
ya msingi na wa kati zilianzishwa Australia mwaka 1911 – 1913, na muda sio
mrefu lesoni zaidi zilizalishwa kwa ajili ya watoto wa ulimwengu wa
wanaozungumza Kiingereza uliobaki. Kuanzia mwaka 1933 hadi 1936
mfuatano wa matoleo matano yaliyoitwa Bible Stories for the Cradle Roll
yalitokea. Nyenzo zingine za mitaala ya watoto zilitokea kila baada ya kipindi
fulani, kutoka katika Idara ya Shule ya Sabato ya Halmashauri Kuu na kutoka
kwa waalimu walio hai wenye shauku pamoja na wafanyakazi katika shule
ya Sabato mahalia duniani kote.
Miaka ya 1960 watu kadhaa walichukua nafasi ya utendaji katika Idara ya
Huduma za Watoto: Curtis Barger, Tom Ashlock, na Ben Leibelt. Tom
Ashlock alihusika kuunda program mpya ya Shule ya Biblia wakati wa likizo,
pamoja na kazi zake za uandishi zikiwekwa katika Little Friend na Primary
Treasure.
Pamoja na kwamba kulikuwa hakuna idara rasmi kwa ajili ya watoto, lakini
katika mkutano wa Halmashauri Kuu wa 1985 uliofanyika huko New Orleans,
Idara ya Huduma za Kanisa iliundwa, ambayo iliundwa kwa kama
muunganiko wa idara nne: Shule ya Sabato/Shughuli za Walei, Uwakili na
Maendeleo, Vijana, na Huduma za Kaya na Familia. Idara hii inajumuisha
huduma na msaada kwa kazi ya Huduma za Watoto, lakini hadi mkutano wa
Dunia wa Mashauri, mwaka 1987 ndipo Huduma za watoto zilipojitokeza
kama idara mpya ndani ya Idara ya Huduma za Kanisa.
Idara hii, kwa kushirikiana na Review and Herald na Shirika la uchapishaji
la Pasific Press zilizalisha Lesoni ya Shule ya Sabato kwa ajili ya watoto. Hii
ilijumuisha Lesoni ya Shule ya Sabato ya Chekechea, Lesoni ya Msingi ya Shule
ya Sabato, Lesoni ya vijana wadogo ya Shule ya Sabato, na Lesoni ya Vijana wa
Awali ya Shule ya Sabato (sasa hivi Mahusiano) pamoja na somo la Utume
(toleo la watoto). Idara pia ilizalisha program za msaada kwa ajili ya viongozi
wa shule ya Sabato ya watoto wachanga, msingi, na vijana wadogo/vijana
wa awali.
Kuanzia 1985 – 1990, idara ya Huduma za Watoto ilipokea msukumo wake
kutoka kwenye njozi na msukumo aliokuwa nao Helen Craig, mkurugenzi
msaidizi wa Shule ya Sabato ya Watoto aliyepita, Shule ya Biblia wakati wa
Likizo, na Uinjilisti wa Watoto. Kuanzia 1990 – 1995, Virginia Smith aliongoza
kazi kwa ajili ya Huduma za watoto kama moja ya huduma zinazounga
mkono Idara ya Huduma za Kanisa.
Mkutano wa Konferensi Kuu mwaka 1995 huko Ultrecht uliasisi kipindi cha
mageuzi katika Huduma za watoto. Julai 4, 1995, A. H. Tolhurst alipendekeza
mada kwamba Idara ya Huduma za Watoto ianzishwe kama Idara tofauti na
idara zingine za kanisa. Iliungwa mkono na kupigiwa kura, na Huduma za
Watoto ikawa idara mpya kanisani, idara pekee kuanzishwa katika kikao cha
mkutano wa Halmashuri Kuu.
Mwaka 2000 mtaala mpya wa watoto uliandikwa kwa ajili ya kanisa
ulimwenguni. Huu ulikuwa matokeo ya tafakuri ya ubunifu na tathmini
iliyofanywa na watu wengi kutoka kwenye divisheni zote ulimwenguni.
Ikifahamika kama ‘Kiungo cha Neema’ (GraceLink), mtaala huu mpya
unakazia dhana nne za msingi katika Imani ya Kikristo:
K
anuni ya kanisa inapendekeza kwamba baraza la kanisa lisaidie
kutengeneza kamati ya Huduma za watoto baada ya kuchagua mtu
atakayetumika kama Mratibu wa Idara ya Huduma za Watoto.
Mratibu atafanya kazi pamoja na baraza ili kuchagua watu wengine
watakaotenda kazi katika kamati yake.
MAJUKUMU YA KAMATI
Huduma za Watoto
UTAFITI WA MCHANGANUO WA MAHITAJI
Ili tuweze kukuhudumia wewe na watoto wako kwa ubora zaidi,
tumepanga utafiti huu. Tafadhali chukua dakika kadhaa kujibu maswali
yafuatayo. Matokeo ya utafiti huu yatatumika kutusaidia katika kuratibu
programu, kutengeneza nyenzo, na kupanga malengo kwa ajili ya huduma
yetu yote kwa watoto.
1. Una watoto wangapi? ___________________________________
2. Watoto wako wana umri gani? ____________________________
3. Una mtoto mwenye mahitaji maalum? Ndiyo Hapana
Umri: _________
4. Ni programu za aina gani ungependa tutengeneze kwa ajili ya watoto
wako? (Weka alama kadiri unavyoona inafaa.)
mikutano ya faragha siku ya kazi za ustadi
mradi wa utoaji wa huduma kwaya
mapishi huduma ya wanasesere
maonyesho ya afya jaribio/mchezo wa Biblia
kambi la porini mandari (pikniki)
kikundi cha maombi chama cha kuhubiri
Mengineyo: ___________________________________________________
_____________________________________________________________
5. Ungependa turatibu programu za aina gani kwa ajili ya wazazi?
______________________________________________________________
______________________________________________________________
6. Kama ungetakiwa kuchagua program 3 zinazohitajika zaidi, ungechagua
zipi?
1) ___________________________________________________________
2) ___________________________________________________________
3) ___________________________________________________________
Sura ya 8
TABIA NANE za IDARA
ya HUDUMA za
WATOTO yenye AFYA
katika KANISA MAHALIA
C
Hristian Schwartz anonesha katika kitabu chake cha Natural Church
Development kwamba, kila kanisa linalositawi na kukua lina tabia
nane. Tabia hizi pia zinaweza zikawakilishwa katika Huduma za
watoto ili kwamba ziweze kudumisha idara inayositawi na kukua katika
kanisa mahalia. Tabia hizi nane ni:
Kuwezesha Uongozi
Huduma inayoongozwa kwa kipawa
Hali ya kiroho yenye hisia kali
Miundo inayotenda kazi
Huduma za Ibada zinazovutia
Vikundi vidogo vya ujumla
Uinjilisti uliojikita katika mahitaji
Mahusiano ya upendo
1. KUWEZESHA UONGOZI
Viongozi makini wanatilia mkazo katika kuwawezesha Wakristo wengine
kwa ajili ya huduma. Wanatoa nyenzo, wanaunga mkono, na wanatia
hamasa mtu mmoja mmoja ili wawe kile Mungu anachowataka wawe. Kwa
hiyo idara ya Huduma za watoto inawezaje kulisaidia kanisa mahalia katika
kuwezesha uongozi katikati ya washiriki wake? Hii inaweza kufanyika kupitia
programu za mara kwa mara za kufundisha uongozi ili kuwezesha watu
wenye uwezo wa stadi za uongozi kuwa viongozi na waalimu wa watoto.
Zaidi ya hayo, kutekeleza program ya wanasihi yenye matokeo bora pia
kunasaidia kuwezesha watu wenye uwezo ambao wanataka kufanya kazi
kwa ajili ya watoto.
A. KUTHIBITISHA UONGOZI
B. KUSIMAMIA WALIOJITOLEA
1. Kudahili
3. Kuwezesha
Mafunzo ya Yehoshafati
Tafakari kwa makini kile unachofanya
Kazi yako ni kwa ajili ya Mungu
Mungu yupo pamoja nawe
Hofu ya Mungu na iwe juu yako
Hakuna uonevu, wala upendeleo, au rushwa
Tumika kwa uaminifu, kwa moyo wote
Mungu ametupatia kila mmoja wetu karama na talanta. Wakati sio kila
mtu ana karama ya kufundisha na kufanya kazi na watoto, bado kuna wale
walio na ari kwa ajili yao. Ni wajibu wa kanisa kutafuta watu wa aina hiyo
wenye uwezo ambao wana karama hizi na kuwaelekeza kwenye Huduma
za Watoto.
Wakati wachungaji na wazee wanatafuta watu walio na karama na talanta
kwa ajili ya kufanya kazi na watoto, lazima pia wachuje wale wanaojitolea ili
kuhakikisha usalama wa watoto. Ni lazima watoto walindwe dhidi ya watu
ambao wanaweza kuwaumiza kimwili, kihisia, na kiroho. Huduma
inayoongozwa na karama inahusisha kazi kama kusajili, kuchuja, na
kuongoza waliojitolea.
A. KUSAJILI WANAOJITOLEA
Kusajili wanaojitolea kamwe sio kazi rahisi, lakini ni kazi ya muhimu kwa
Huduma za watoto. Watoto wanahitaji uangalizi zaidi, msaada, na uongozi
kutoka kwa watu wazima katika programu zote za watoto. Kwa hiyo, kusajili
wanaojitolea kunatakiwa kuwa ni mchakato unaoendelea kadri mratibu na
kamati ya huduma za watoto wanapotafuta watu wengine
wakuwawezesha kwa ajili ya huduma.
Majukumu ya Msajili
Anatafuta wanaojitolea wakati wote
Ana faili la wanaofaa kujitolea
Ana majukumu kwa kila kazi
Ana akiba ya fomu za usajili wa huduma
B. KUCHUJA WANAOJITOLEA
Kwa nini kuchuja wanaojitolea?
Ili kugundua wale Mungu aliowaita kwa ajili ya utume
Kuoanisha karama ya mtu na huduma
Kupima mvuto wao
Kulinda watoto
Kulinda kanisa dhidi ya madeni
Kuanzisha upatanifu wa dondoo
WAJIBU WA MFUMO
Wajibu wa kulinda watoto wote kutoka kwenye hatari
Ushiriki salama katika shughuli za kanisa au za shule
Kwamba shughuli zote zinasimamiwa na mwajiriwa au mtu anayejitolea
aliyepitia mafunzo
Matengenezo sahihi ya vifaa ili kupunguza nafasi ya hatari
Wajibu wa kufanyia kazi malezi yanayoleta maana kwa wafanyakazi
inaweza ikajumuisha:
Uchaguzi wa makini wa waajiriwa na wanaojitolea
Mafuzo sahihi kwa wafanyakazi na wanaojitolea
Usimamizi sahihi wa wafanyakazi na wanaojitolea
Tendo linalofaa ambapo ni lazima kuondoa wafanyakazi
Wajibu wa kutoa taarifa ya matukio yote ya unyanyasaji wa mtoto
kulingana na sheria
WAJIBU KWA WATOTO & WATU WAZIMA
Watu wazima wanaofahamika kuwahi kufanya matendo ya unyanyasaji
kwa watoto hapo kabla au utendaji mwingine usiofaa hawataruhusiwa
kushiriki katika program zinazofadhiliwa na kanisa katika huduma za
watoto
Hatua zinazofaa zitachukuliwa kuepuka kuwahisi watu wazima
wanaohusika na uzimamizi kupitia matumizi ya njia zifuatazo za usalama
Kanuni ya miezi sita itatumika katika kuwafahamu zaidi watu wapya
wanaojitolea
Kanuni ya watu wazima wawili itatumika katika shughuli zote
zinazofadhiliwa na kanisa
Lazima kwa wale wanaojitolea wote kushiriki katika program ya
uelewa wa unyanyasaji wa watoto kila mwaka
Kila dai linalotolewa dhidi ya mtu mzima aliyejitolea kuhusu utendaji
usiofaa litachunguzwa kwa makini na kanisa na njia sahihi za
marekebisho zitachukuliwa.
Kama mashtaka yatatolewa dhidi ya mtu mzima kuhusu utendaji usiofaa
kwa mtoto tutaheshimu haki za mtu huyo na kushughulikia masuala yote
yanayohusu suala hilo kwa siri
Tuna wajibu wa kufanya shughuli zetu kwa uwiano na ushauri wa
Mathayo 7:12
Shirika la uangalizi wa hatari linatoa miongozo hii na fomu hizi ili kusaidia maendeleo
ya programu za usalama na uangalizi wa hatari. Shirika la Waadventista la uangalizi
wa Hatari haliwajibiki katika uongozi wa shughuli zilizowekewa bima ya usalama.
Dhima ya ukomo kwa upande wa Shirika la Waadventista la uangalizi wa hatari
inakanushwa hapa
SERA NA TARATIBU ZA ULINZI WA WATOTO KATIKA
KANISA LA WAADVENTISTA WA SABATO
(MUUNDO WA MATENDO BORA)
UTUME: Utume wetu ni kutoa mazingira yaliyo salama, ya kiroho na yasiyo na
unyanyasaji kwa kila mtoto anayeshiriki programu na shughuli za Kanisa la
Waadventista wa Sabato la ___________________________
MALENGO: Ni lengo letu kuzuia kila aina ya unyanyasaji wa watoto, kimwili,
kihisia au kingono na kulinda waajiriwa wetu na watu wetu wanaojitolea dhidi
ya mashtaka ya uongo kuhusu matendo kama hayo.
TAFSIRI:
Mtoto – shule ya awali hadi shule ya msingi
Mtoto mkubwa – vijana wadogo hadi vijana waliopevuka
Unyanyasaji wa watoto – ni tendo lolote kwa mtoto linalotishia usalama wa
mtoto au linaloacha maisha yake yakiwa na makovu ya kimwili au kihisia. Ni
pamoja na matendo yote yasiyofaa kimwili, kingono au mawasiliano ya mtu
mzima yoyote kupitia matumizi ya mamlaka juu ya mtoto. Unyanyasaji pia
unaweza ukatokea kati ya watoto wawili. Hata kama ni kutokana na
kutokuelewa kwa mtoto, kutokuwa na hatia au hofu zinazoweza kuchangia ni
njia za unyanyasaji.
Unyanyasaji wa kimwili – ni jeraha lolote kwa mtoto ambalo limesababishwa
na njia zozote za ajali, pamoja na majeraha yanayoonekana kuhitilafiana na
maelezo ya jeraha hilo.
Unyanyasaji wa kihisia – ni mawasiliano yoyote ya mdomo yanayomuathiri
mtoto, kama vile kumshusha hadhi, kumdhalilisha, kumuita majina yasiyofaa,
maneno ya kumdharau, lugha ya kikatili au lugha chafu, nk.
Unyanyasaji wa kingono – kuvunja ufaragha wa jinsia ya mtoto iwe kwa
kumshika, kumsisimua kwa macho au kwa maneno. Inajumuisha kushika
sehemu zozote za binafsi za mtoto, kuingiza vitu mdomoni, sehemu za siri
au/na kinyume na maumbile, kumuambia au kumwomba mtoto kuwezesha
kujichua, kuonyesha sehemu za siri kwa mtoto, kumruhusu mtoto kushuhudia
au kuangalia namna yoyote ya shughuli za kingono, kuonyesha picha za ngono,
nk…
UTARATIBU:
Wafanyakazi wote na wale waliojitolea kufanya kazi na watoto, lazima
wajaze fomu ya wafanyakazi wa Huduma za Watoto. Hakuna mabadiliko
yanayoruhusiwa katika fomu hii bila ruhusa ya baraza la kanisa kwa ushauri
wa kisheria.
Wafanyakazi wote na wote wanaojitolea, wanakubali kufuata sera na
utaratibu wa ulinzi kwa watoto wa Konferensi ya ____________________
Washiriki wapya wanaotamani kufanya kazii na watoto na vijana lazima
wawe washiriki hai wa kainsa mahalia angalau kwa miezi sita (6) kabla
hawajaruhusiwa kufanya kazi na watoto.
Watu wazima watasiamia programu na shughuli za watoto nyakati zote. Hii
ina maana kwamba siku zote kutakuwa na angalau watu wazima wawili (2)
wanaosimamia tukio lolote ili kuepuka hali zifuatazo:
Wafanyakazi wataepuka kuwa wenyewe na watoto nyakati zote. Hii
itawalinda wote mtoto na mtu mzima kutoka kwenye hatari au
mashtaka yoyote.
Mtoto hatasaidiwa kutumia maliwato isipokuwa kuna mtu mzima wa
pili karibu na eneo hilo anayeelewa sababu ya msaada huo
Hakuna mtoto atakayeadhibiwa isipokuwa kwa kukutana na mtu
mzima mwingine ambaye anaelewa hali inayohitaji adhabu. Adhabu
zozote kali zinazuiliwa vikali.
Hakuna “mtoto” (kwa maana iliyotajwa hapo juu) atakayeachiwa kwenda
maliwatoni isipokuwa mzazi, mlezi au watu wazima wawili wakimsindikiza
Inashauriwa kwamba shughuli au programu zozote za watoto kufanyika
kwenye madarasa au ofisi zenye madirisha kwa ajili ya uangalizi rahisi.
Vyumba vyote vinapaswa kufungwa wakati wote.
Kila shughuli au programu inayofadhiliwa na kanisa inayohusisha watoto
wa umri mdogo inayofanyika nje ya kanisa lazima iwe na ukubali wa
viongozi wa kanisa.
Baraza la kanisa lazima lipitishe shughuli au safari zozote za usiku kabla
hazijafanyika. Watoto wote wa umri mdogo wanaoshiriki katika shughuli
hizi lazima wawe na ruhusa iliyosainiwa na mzazi kwa ajili ya kila safari
pamoja na barua ya dharura ya afya. Wazazi na/au waleziwatapewa taarifa
ya watu wazima ambao watahusika katika shughuli au safari hiyo.
Tabia yoyote inayoonekana kuwa ya kinyanyasaji au isiyofaa itaripotiwa
kwa kiongozi wa kanisa au mchungaji kwa ajili ya uchunguzi.
Washiriki wanaofahamu mtu yeyote aliyehukumiwa, aliyekiri bila kubisha,
au kuamuliwa kwamba alitenda unyanyasaji wa kimwili au kingono na
anashiriki ibada mara kwa mara, wanapaswa kumshauri mchungaji juu ya
taarifa hii. Uongozi wa kanisa utahusika kutoa uangalizi zaidi kwa mtu huyo
anaposhiriki katika matukio ya kanisa.
Watu ambao wamewahi kuhukumiwa au kukiri au kuashiria kuwa
wamewahi kuhusika kwa namna moja au nyingine katika unyanyasaji wa
kimwili au kingono wasiruhusiwe kushiriki katika kujitoela katika Idara ya
Huduma za Watoto inayofadhiliwa na kanisa lolote, au vijana wadogo na
wakubwa, au program ya raia wa daraja ya juu au shughuli nyingine zozote.
Imepigiwa kura na baraza la kanisa la: ___________________________
Tarehe: ___________________________
CHANZO
Kanisa la Waadventista Wasabato Beltsville na Konferensi ya Potomac
Shirika la uangalizi wa hatari linatoa miongozo hii na fomu hizi ili kusaidia maendeleo
ya programu za usalama na uangalizi wa hatari. Shirika la Waadventista la uangalizi
wa Hatari haliwajibiki katika uongozi wa shughuli zilizowekewa bima ya usalama.
Dhima ya ukomo kwa upande wa Shirika la Waadventista la uangalizi wa hatari
inakanushwa hapa
Ninahakikisha kwa ufahamu wangu kwamba taarifa nilizotoa katika fomu hii
ni sahihi. Ninaruhusu udhamini au kanisa liloorodheshwa kwenye fomu hii
kutoa taarifa yoyote kuhusu tabia yangu na uwezo wangu wa kufanya kazi na
watoto. Kwa hayo ninaachilia taasisi yoyote au mtu yoyote kutoka kwenye
deni litakalosababishwa na mimi.
FALSAFA
Nguvu nne za msukumo wa kukua kwa uzoefu wa Ukristo zinatoa msingi
wa ‘Kiungo cha Neema’. Misukumo hii ni:
MSINGI: Ngazi ya shule ya msingi ina mzunguko wa miaka minne, Ngazi hii
inapendekezwa kwa watoto wenye umri miaka 6 hadi 10. Wazazi
wanategemewa kujifunza na watoto walio wadogo. Baadhi ya maswali ya
kujifunza kila siku yatakuwa magumu kwa watoto wadogo na yanaweza
kuondolewa na wazazi. Kwa sababu ule muda wa Shule ya Sabato
umejengeka katika shughuli za vitendo, basi kila mmoja darasani anahusika.
*Imani ya ya wakati uliopo ni kifaa kingine maalum kwa ajili ya vijana wa kati (Umri miaka 12 -14)
wanapokutana tofauti na vijana wa wadogo.
4
1
Tabia ya tano ya kanisa lenye afya ni uratibu wa ibada zinazovutia kwa kila
umri. Kanisa zima litajawa na msisimko wa uhai, na furaha pale washiriki
watakapojihisi kuthaminiwa na kuhusishwa. Mratibu wa Huduma za Watoto
anafanya kazi na mchungaji ili kupanga ibada ambazo zitatimiza mahitaji ya
watoto kanisani.
Leo, vikundi vidogo vya watoto vimeongeza malengo zaidi ya yale ya kulea
ukuaji wa kiroho. Vikundi vidogo vinaweza vikahudumu kama vikundi vya
kutoa huduma kwa watoto ambaao wanateseka katika maumivu. Ni
kukutana kwa mioyo ambapo watoto wanapewa malezi ya kihisia kadiri
wanavyoongozwa kwa Yesu.
Utume wa Watoto
Anzisha programu ya watoto katika Utume
Shule au kanisa linaweza kuwa sehemu ambapo watoto watakutanika
na wazazai wao ili kwa pamoja wafundishwe jinsi ya kuwa mitume.
Wazazi wanapata mafunzo tofauti juu ya jinsi ya kuwafanya watoto wao
kuwa wanafunzi wakati watoto wanajifunza jinsi ya kufanya kazi pamoja
na wazazi wao kama timu.
Wazazi na watoto wanazungumza, wanaulizana maswali, na wanakuwa
na masomo ya Biblia (www.kid-center.org)
Upinde wa Mvua
Hiki ni kikundi cha kutoa msaada kwa watoto wanaoumia na
kusononeka, kwa sababu ya kifo cha mpendwa, kutalakiana kwa wazazi,
walio na mzazi au ndugu aliye na ugonjwa mbaya, au maumivu mengine.
Watoto wanakutanika mara moja kwa juma pamoja na mratibu wa
Upinde wa Mvua wakati wanaposhirikishana hisia, hofu na maumivu
yao.
Wanajihushisha katika shughuli iliyo ya kiuponyaji, kama vile kutoa hisia
zao, kuziandika au kuchora na kupaka rangi
Watoto wanajifunza kwamba matukio haya yanatokea sio kwa sababu
wana hatia, lakini badala yake ni mambo yaliyo nje ya uwezo wao.
Watoto wanajifunza kwamba mambo ya kutia huzuni yatapita na
mwisho wake kuna upinde. Maisha bado yana thamani, hasa pale
wanapokuwa na Yesu kama kiongozi na rafiki. www.rainbows.com
Agizo la Yesu la kupeleka injili “kwa kila kabila, lugha na jamaa” alilowapa
wanafunzi wake bila shaka linajumuisha kupeleka injili kwa watoto pia. Ellen
White anatukumbusha kwamba:
Tafiti za hivi karibuni pia zinaunga mkono dhana hii kwamba watoto chini
ya umri wa miaka 14 ni rahisi sana kukubali injili. Kwa hivyo, kanisa
linahitajika kuteka nafasii hii ili kuwafikia na kwa nguvu kuwashirikisha injili
watoto ambao hawajawahi kusikia kuhusu Yesu. Kristo alionna umuhimu wa
kuwafikia watoto:
Kwa hiyo agizo liko wazi na tunahitaji kuingia kazini katika kupanga
programu za kuifikia jamii nyingi kadiri akili zetu za kibunifu zinavyoweza
kuzalisha. Kumbuka, lengo la mwisho la kuwafikia watoto ni kuwasaidia
kumfahamu Yesu ili kwamba wajenge uhusiano wa upendo Naye.
A. AINA ZA UINJILISTI
Uinjilisti wa Urafiki
Mtazamo huu umegundulika kuwa ni moja kati ya njia zenye matokeo
sahihi katika kufanya uinjilisti kwa watoto. Watoto wote wana marafiki na
rafiki anapowaalika kuja kanisani, kuna uwezekano mkubwa wa wao
kwenda kuliko wanapoalikwa na mtu wasiyemfahamu. Uhusiano ni muhimu
katika maisha ya watoto.
Watoto wanafundishwa stadi za jinsi ya kufanya marafiki na jinsi ya kualika
marifiki.
Kadi za mwaliko. Weka tayari kadi kwa ajili ya watoto kuzitoa ili kudumisha
mawasiliano na marafiki hawa wapya. Wahimize pia kuandika na kuzichora
pia. Wapatie kadi za kuwaalika marafiki katika programu maalum kama vile
kambi la siku moja, Shule ya Biblia Wakati wa Likizo au kongamano la
uimbaji.
Kipindi cha kushirikishana Somo la Biblia Kila siku la ‘Kiungo cha Neema’
Wahimize watoto kuweka kwenye vitendo sehemu ya kujifunza ya Kiungo
cha Neema, “Wakishirikiana ujumbe” na marafiki zao. Kila juma wanapaswa
kushiriki ujumbe na mtu fulani kupitia mradi au huduma maalum.
N
i mwitikio gani tunaowapatia watoto wanapoomba kubatizwa?
Tunaanzaje kuwaanda kukubali neema ya Mungu na kutembea
kikamilifu katika mwangaza wake? Wanapaswa kuwauliza nini
kabla ya ubatizo? Ni umri gani ulio bora kwa ajili ya kubatizwa? Hatupaswi
kusita kwa muda mrefu, maana uamuzi wa mtoto unaweza ukafifia. Kama
tusipoitikia uamuzi wao wa kusisimua wa kumfuata Yesu na kubatizwa,
tunaweza tukapoteza nafasi ya dhahabu ya kufanya hivyo baadae.
Kufanya uamuzi wa kumfuata Yesu ni hatua muhimu kuelekea katika
kukua kiroho. Kanuni ya Kanisa, uk. 29 inakubali kwa kusema:
UHAKIKISHO WA IMANI
(Mfano wa Tukio hili)
…………………………………………………………………………….........
Wimbo:
Mruhusu mtoto achague wimbo anaoufahamu vyema.
Sio lazima wimbo wa kwenye kitabu cha nyimbo, unaweza
kuwa wimbo wa Shule ya Sabato.
Utangulizi:
Mtoto akae kiti cha mbele kabisa kabla ya tukio hili.
Mchungaji au rafiki katika imani ambaye anamfahamu
vyema mtoto anaweza akamtambulisha kwa washiriki.
Toa historia fupi ya ni lini, wapi na kipi kilichosukuma
uamuzi huo.
Weka mkazo kwenye maoni kuhusu huyo mtoto. Unaweza
ukasema: “ninapenda kumtambulisha kwenu Bryan hapa
kanisani. Mwezi uliopita katika Mkutano wa Watoto Bryan
alifanya uamuzi. Aliamua kumfanya Yesu kuwa rafiki yake
na anataka kuwa mmoja wa watoto wake.”
Uhakikisho:
Uhakikisho huo unapaswa kusomwa au kukaririwa na
mtoto mbele ya washiriki.
Rafiki wa Imani
Anatambulishwa:
Elezea wajibu wake.
Kwa mfano: “Kuwa na rafiki wa kukuunga mkono
kunaweza kukaleta maana ya kufanikiwa au kushindwa.
Biblia inasema kwamba, “kama mmoja akianguka, rafiki
yake anaweza akamwinua. Lakini ole wake mtu Yule
aangukaye na hakuna wa kumwinua!” (Mhubiri 4:10).
Bryan amechagua mwalimu wake wa Shule ya Sabato,
Bwana Jerry Page, awe rafiki yake wa Imani. Rafiki wa
Imani ni mtu atakayemtia moyo katika nyanja zote za
maisha yake, lakini muhimu zaidi, katika safari yake ya
kiroho pamoja na Yesu.
Rafiki wa imani anasoma agano lake kwa mtoto.
Kwa mfano: “Kama rafiki yako wa imani, ninaahidi
kukuunga mkono na kukujali. Kama wewe, ninaweza
nikatenda makosa, lakini ninafahamu kwamba Mungu
ananisamehe. Ninataka ufahamu kwamba unaweza ukaja
kuzungumza nami wakati wowote. Ninataka kuwa rafiki
yako.”
Mwitikio wa
Washiriki:
Ruhusu washiriki wahusike katika tukio hili kwa
kunyoosha mikono yao na kusimama kama ishara ya
kuunga mkono.
Kwa mfano: “Bryan, kuna watu wengine wengi hapa
ambao wanafahamu kwamba wangependa kuwa
marafiki zako wa imani. Wale kati yenu walio washiriki
ambao wangependa kuwa “rafiki” kwa Bryan tafadhali
msimame? Wale walio tayari kumtia moyo na kumuunga
mkono kwa upendo; wale wanaotaka kuweka agano la
kuwa chanya na kutomkosoa au kumhukumu, lakini kuwa
rafiki, tafadhali simameni sasa.”
Ombi:
Mchungaji anatoa ombi fupi.
Shikaneni
Mikono:
Mpatie mtoto kadi ya uhakikisho wa imani.
Imetolewa kutoka katika It’s my Choice (Ni uchaguzi wangu), na Steve Case. Hagerstown, MD: Review
and Herald Publishing Association, 1996. Sura ya 10
Sura ya 10
MATAMKO YA
HALAMASHAURI
KUU kuhusu
WATOTO
Kukosa Elimu – kukosa elimu kunafanya iwe vigumu kwa wazazi kupata ujira
wao au kuitunza familia au kumfanya mtoto afikie upeo wa uwezo wake.
KANISA LA WATOTO
KWAYA YA WATOTO
Maelezo: kikundi cha muziki kwa ajili ya watoto ambacho kinaimba hasa
kanisani lakini pia katika jamii. Unaweza ukawa ni mradi wa muda mfupi au
muda mrefu kwa ajili ya maandalizi ya kambi la vijana, makambi, au Sabato
ya watoto. Watoto katika jamii wanaweza kualikwa kujiunga na kwaya hiyo
na wazazi wao wakaalikwa kuja kutazama wakiimba, na mahusiano
kujengwa ambayo yanaweza kuwa ushuhuda mkubwa.
Maelezo: hii ni programu maalum ya kila mwaka katika kila Sabato ya tatu
ya Oktoba, ili kukuza uelewa wa mahitaji ya watoto na wajibu wetu kama
kanisa kuyatimiza mahitaji yao. Watoto wanashiriki katika huduma ya ibada,
wakipewa kazi kama vile kuomba, kusoma Maandiko, wimbo mkuu wa
ibada, kuhubiri, kukusanya sadaka, na muziki maalum.
Nyenzo: Open your Heart, Open Hands, 2003 (Huduma za Watoto Divisheni
ya Marekani); Stand Up! Stand Out! 2004 (Huduma za watoto Divisheni ya
Marekani).
MKUTANO WA WATOTO
Maelezo: watoto hukusanyika kwa siku 2-3 kwenye eneo la kambi au kituo
cha mikutano kwa ajili ya shughuli za kushirikishana kivitendo ambazo
zinaunga mkono kukua kiroho, kimwili, kijamii na kiakili. Mada maalum
zinachaguliwa na programmu inapangwa kulingana na mada hizi. Programu
zinaweza zikajumuisha uwakili, historia ya kanisa, uzoefu wa ki-Biblia, na
mashujaa wa kwenye Biblia.
PROGRAMU ZINGINE
KARIBU MTOTO
Mambo ya kipekee: Hii ni programu bora zaidi ya kuifikia jamii kwa maana
kina mama waliojifungua wanahitaji kutiwa moyo na kusaidiwa katika miezi
yao ya mwanzo. Urafiki mzuri unaweza kuanzishwa utakaowezesha
kupatikana kwa nafasi zingine za kushuhudia.
Maelezo: Kila juma gari la maktaba inayohama linasafiri katika miji maalum
ya vijijini ili kuwapatia watoto pale vitabu na nyenzo zingine za visa vya
Biblia. Kila mtoto anaweza kuazima kitabu kimoja au viwili kwa juma moja
na atavirudisha kwa ajili ya kupewa vitabu vingine gari litakaporudi juma
linalofuata. Maktaba hii inayo hama pia inatoa maonyesho ya wanasesere,
kisa cha Biblia na nyimbo za watoto kwa takribani dakika 45.
Kusudi: Kutoa nafasi kwa watoto kwa ajili ya masomo mahsusi ya Biblia.
VITABU
Allen, Steve. Growing a Healthy Children Ministry. Cincinnati, Ohio: Standard
Publishing, 2002.
Barna George. Transforming Children Into spiritual Champions. Ventura,
California: Regal books, 2003.
Bowdon, Boyce. The Child – Friendly Church; 15 Models of Ministry with
Children. Nashville, Tennessee: Abingdon press, 1999.
Calkins, Jack. Grace Is for Kids. Lincoln, Nebraska: AdventSource, 1997.
Chromey, Rick. Children’s Ministry Guide for Smaller Churches. Loveland,
Colorado: Group Publishing, Inc. 1995.
Craig, Jutila. Leadership Essentials for Children’s Ministry. Loveland,
Colorado, Group Publishing, 2002.
Dallow, Gill. Touching the Future. Oxford, England: the Bible Reading
Fellowship, 2002.
Frank, Penny. Leading Children. Nottingham, England: St. John’s Extension
Studies and Children Ministriy, 2001
Habenicht, Donna. How to Help your Child Really Love Jesus. Hagerstown,
Maryland: Review and Herald Publishing Association, 1994.
Habenicht, Donna. 10 Christian Values every kid should know. Hagerstown,
Maryland: Review and Herald Publishing Association, 2004.
Holford, Karen. 100 Creative Prayer Ideas for kids. Nampa, Idaho: Pasific
Press Publishing Association, 2003.
Hopkins, Gary and Joyce W. Hopp. It takes a Church: Every Member Guide to
Keeping Young People Safe and Saved. Nampa, Idaho: Pasific Press
Publishing Association, 2002.
Introducing GraceLink; A New Curriculum for Children’s; Sabbath Schools.
Silver Spring, Maryland: General Conference Sabbath School Department,
1999.
Irwin, Bernadine L. A Child shall Lead them: Releasing the Power of Children
as Ministers. Loma Linda, California: Millenia Publising Co.,2000.
Maspeaker, Barbara. Quick Access Ideas for Children Ministry. Lincoln,
Nebraska: AdventSource.
Robinson, Robert J. 52 Easy Program Ideas for Kindergaten Sabbath School,
Year B. Lincoln, Nebraska: AdventSource, 2003
Roehlkepartain, Jolene, ed. Children Ministry that works. Loveland,
Colorado: Group Publishing, Inc., 1991.
Tetz, Myrna and Gary Hopkins, com. We Can Keep Them in the Church.
Nampa, Idaho: Pasific Press Publishing Association, 2004.
Yount, Christine. Recruit and Nurture Awsome Volunteers for Children’s
Ministry. Loveland, Colorado: Group Publishing Inc., 1998.
MAGAZETI
TOVUTI
H
uduma za Watoto zinapaswa kuwa sehemu muhimu ya Kanisa
lolote la Waadventista Wasabato. Wewe kama mchungaji, mzee
wa kanisa, unaweza ukachukua nafasi kubwa katika kuwasaidia
watoto kukuza uhusiano wa upendo na kumtuikia Yesu. Unaweza ukatoa
nafasi za kuwafundisha na kuwashauri watoto kama viongozi wa leo na
kesho. Unaweza ukavutia kusanyiko lako kuwa na njozi ya kuongoza na
kulea watoto katika safari ya kiroho. Unga mkono programu zao, na
uwahusishe katika nyanja zote za maisha ya kanisa. Kumbuka, kujenga
kanisa la kesho kunaanzia kwa watoto wa leo!