Professional Documents
Culture Documents
NA MAJIBU YAKE
1. Kuingia Utu Uzima
Kitabu cha 6
2. Uhusiano kati ya Msichana na Mvulana
3. Uhusiano wa Kimwili
4. Mimba
5. Usalama katika Mapenzi
6. UKIMWI na Kizazi Kipya
7. Dawa za Kulevya
RAFIKI
8. Pombe na Sigara MWENYE ATAENDELEA
9. Haki za Uzazi UKIMWI KUWA RAFIKI
YANGU
Tanzanian German
Mkuki na Nyota Publishers Programme to Support
S. L. P. 4246 Health (TGPSH)
Kitabu hiki kimetayarishwa kwa kushirikisha
Dar es Salaam S. L. P. 65350
vijana wa Tanzania na TGPSH-GTZ
www.mkukinanyota.com Dar es Salaam
www.tgpsh.or.tz
Shukrani
Kimechapishwa na:
Tunapenda kuwashukuru vijana wote waliohusika katika kuandaa vijitabu hivi kwa
Mkuki na Nyota Publishers Ltd mchango mkubwa walioutoa. Hawa ni vijana balehe kutoka shule za msingi mbalimbali
S. L. P. 4246 za mikoa ya Lindi, Tanga na Dar es Salaam waliochangia kwa kuibua maswali ya awali,
Dar es Salaam waelimishaji rika wa vikundi kutoka Student Partnership Worlwide (SPW) na wa
UMATI ambao walipitia na kuchambua maswali ya awali pamoja na wanachuo wa Chuo
Kikuu cha Tumaini Dar es Salaam kwa mchango wao wakati wa kufanya marekebisho ya
Pepe: contact@mkukinanyota.com pili ya hivi vitabu.
Tovuti: www.mkukinanyota.com
Vilele tunatoa shukrani nyingi kwa watu wote kutoka katika makundi yote ya jamii
ndani na nje ya Tanzania amabo walisoma vijitabu hivi, na wakatupa mrejesho, kutupa
moyo na kuuliza maswali ambayo yameongeza ubora wa nakala hii.
Kwa hisani ya Serikali ya Ujerumani
Shukrani ziwaendee walimu wote wakuu wa shule za msingi ambazo zilihusika kwa
msaada wao, na kwa Bwana Walter Mbunda na marehemu Elisha Kapinga (UMATI) na
pia kwa Bwana Yassin Ally wa SPW kwa uwezeshaji.
Shukrani za pekee kwa Dkt. Regina Goergen (EvaPlan) siyo tu kwa moyo wake wa
ujasiri katika kuchochea maandalizi ya hivi vijitabu bali pia katika kusambaza wazo
hili, na kuwezesha vijitabu hivi kukubalika katika nchi 17 ulimwenguni. Vijitabu hivi
Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) vimekuwa zana mwafaka kwa maana ya njia bora ya kufikisha habari kuhusu ujinsia na
afya ya uzazi kwa vijana.
Tunamshukuru mchoraji wa katuni Nd. David Chikoko kwa mchango wake mkubwa katika
kuchora vielelezo vilivyotumika katika mfululizo huu.
Kwa njia ya pekee tunapenda kuwashukuru Meja Jenerali (mstaafu) Herman Lupogo
(aliyekuwa Mwenyekiti Mtendaji wa TACAIDS) na Bi Rustica Tembele (TACAIDS) na
Dkt. Catherine Sanga (RCHS) kwa mchango wao endelevu katika kusambaza vijitabu
hivi na bila kusahau mashirika yote yaliyosaidia katika machapisho na usambazaji wa
vijitabu hivi kwa miaka yote hiyo.
Utangulizi............................................................................................. v
Je, kuna tofauti gani kati ya neno Virusi vya UKIMWI kwa
kifupi VVU na UKIMWI?.................................................................1
Kinga ya mwili ni nini?........................................................................2
Nini kinatokea wakati Virusi vya UKIMWI (VVU) vinapoingia
mwilini na vinakwenda wapi katika sehemu ya mwili?.................2
Je, inachukua muda gani tangu mtu aambukizwe na VVU hadi
vionekane kwenye damu?..................................................................3
Je, watu wote wenye virusi vya UKIMWI watapata
UKIMWI? Na kama ndiyo, itachukua muda gani?......................3
Je, mtu mwenye kuonekana na afya nzuri, anaweza kuwa na
virusi vya UKIMWI?.........................................................................4
Je, ni tabia zipi zinazochangia kuenea kwa virusi vya
UKIMWI?............................................................................................5
Je, mwanaume akitoa uume nje ya uke kabla ya kumwaga
shahawa anaweza kuambukizwa yeye au mwanamke na
Virusi vya UKIMWI na UKIMWI?................................................6
Je, nikijamiiana na mtu mwenye virusi vya UKIMWI
bila kutumia kondomu, nitapata virusi vya UKIMWI na
UKIMWI?............................................................................................6
Je, Virusi vya UKIMWI na UKIMWI vinaambukiza kwa
kujamiiana kwa njia ya sehemu ya haja kubwa au mdomoni ?..7
Kunyonyana ulimi kunaweza kuchangia kupata virusi vya
UKIMWI?............................................................................................7
Je, nitaweza kupata virusi vya UKIMWI na UKIMWI
nikijamiiana na msichana au mvulana wa umri mdogo sana?.....8
Kwa nini nao watu wanaishi kwenye ndoa wanapata
maambukizi ya virusi vya UKIMWI na UKIMWI?....................9
Je, mtu anaweza kuambukizwa virusi vya UKIMWI na
UKIMWI iwapo atavaliana nguo na mtu mwenye Virusi vya
UKIMWI na UKIMWI?.................................................................. 10
Nikitumia nyembe kali au sindano pamoja na mtu mwenye
Virusi vya UKIMWI ninaweza kupata Virusi vya UKIMWI
na UKIMWI?..................................................................................... 10
Je, ninaweza kuambukizwa na Virusi vya UKIMWI na
UKIMWI kwa kuumwa na mbu?.....................................................11
Je, nikila na mtu mwenye Virusi vya UKIMWI,
nitaambukizwa na virusi vya UKIMWI na UKIMWI?..............11
Je, nikitoa au kupata damu hospitalini, itakuwepo hatari
ya kupata virusi vya UKIMWI na UKIMWI?............................ 12
Mama mwenye virusi vya UKIMWI na UKIMWI, anaweza
kuzaa mtoto? Na anaweza kumwambukiza mtoto aliye
tumboni au wakati wa kumnyonyesha?........................................ 12
Ni asilimia ipi ya Watanzani ambao wameambukizwa na
Virusi vya UKIMWI na UKIMWI?.............................................. 13
Hali ya maambukizi ya VVU Tanzania kimkoa............................ 14
Je, nifanye nini ili kujikinga na maambukizi ya virusi vya
UKIMWI na UKIMWI?.................................................................. 14
Je, ni kweli kwamba kufanya ngono na bikira inaponyesha
maambukizi........................................................................................ 16
Nifanye nini ili kujua kama nina au sina maambukizi ya
Virusi vya UKIMWI?....................................................................... 16
Niende wapi kupima kama nina Virusi vya UKIMWI?............. 17
ii
Je, nikiambukizwa virusi vya UKIMWI na UKIMWI
nifanye nini?...................................................................................... 18
Je, matokeo ya kupima na kukutwa huna virusi vya Ukimwi
ni yapi?................................................................................................ 19
Je , vipimo vya Virusi vya UKIMWI vinasema ukweli?........... 20
Je,niwasiliane na niishi vipi na watu wanaoishi na virusi vya
UKIMWI na UKIMWI?................................................................. 20
Ni tahadhari gani nichukue ninapomhudumia mgonjwa wa
UKIMWI?.......................................................................................... 21
iii
iv
Utangulizi
Vijana walihusishwa katika hatua zote za kukitayarisha. Kwa
njia ya kuchapisha kijitabu hiki, tunategemea tumechangia
kuinua uelewa ambao utawajengea vijana tabia ya kuwajibika
katika maswala ya uhusiano ya kimwili yasiyokuwa na matokeo
mbadala. Kumbuka haya ni juu ya mwili wako na maisha yako
kwa hiyo yathibiti kwa kuyasimamia. Kwa vijana wa Tanzania,
chukueni hii kama changamoto. Taarifa inawezesha. Tumia
uwezo huu kujenga maisha yako ya baadaye. Katika mapambano
dhidi ya maambukizo ya VVU, kila mmoja wetu ana nafasi yake
ya utendaji. Kwa asilimia kubwa VVU haiji kwako bali ni wewe
unaifuata na kujiambukiza. Tunawapa wote changamoto katika
kuwajibika na kuhimili maisha yako.
vi
Je, kuna tofauti gani kati ya neno Virusi vya
UKIMWI kwa kifupi VVU na UKIMWI?
utaanza kuugua magonjwa nyemelezi. Magonjwa nyemelezi
hupata nafasi ya kushambulia mwili huu ambao tayari kinga
imepungua. Watu wnaoumwa UKIMWI wanaweza kupungua
uzito wa mwili, kuharisha au kupata matatizo ya ngozi. Hata
hivyo maradhi haya siyo lazima yatokane na kuwa na VVU. Ili
kuwa na uhakika, onana na mtaalamu yaani dakatari wako.
nyeupe hizi kupasuka. Virusi hivi hupata nafasi ya kuendelea
kushambulia chembechembe nyingine nyeupe za damu. Kwa
kadri chembechembe nyeupe zilizoshambuliwa zinavyoendelea
kupasuka ni kwa kiwango hicho hicho chembechembe nyeupe
zinaendelea kuharibiwa na kupungua. Matokeo yake ni kupungua
kwa kinga mwilini na mtu kuendelea kudhoofika.
kupata dalili za awali. Watoto wanaopata virusi kabla ya umri
wa miaka mitano kwa wastani wanendelea kuishi mwaka moja
hadi mitatu.
Hakuna jibu la ujumla ni miaka mingapi ataishi tena mtu
aliyeambukizwa na virusi vya UKIMWI. Idadi ya miaka ya
kuishi baada ya kuambukizwa inategemea vitu vingi, kinga
asilia inayomkinga mtu, hali ya lishe ya mtu, wakati muafaka na
usahihi katika kutibu magonjwa nyemelezi na wakati muafaka
na usahihi wa kutumia dawa za kupunguza makali ya UKIMWI
kwa Kiingereza Anti-Retro-Viral drugs (ARVS )
Je, ni tabia zipi zinazochangia kuenea kwa
virusi vya UKIMWI?
Je, mwanaume akitoa uume nje ya uke kabla
ya kumwaga shahawa anaweza kuambukizwa
yeye au mwanamke na Virusi vya UKIMWI na
UKIMWI?
Uwezekano wa kuambukizwa
na Virusi vya UKIMWI na
UKIMWI ukijamiiana na mtu
mwenye virusi vya UKIMWI bila
kutumia kondomu ni mkubwa.
Mpaka leo, kondomu ni njia pekee
ya kuzuia kuambukizwaVirusi
vya UKIMWI na UKIMWI
wakati wa kujamiiana. Kama
kondomu inatumiwa ipasavyo
na kila unapojamiiana na mtu
mwenye virusi vya UKIMWI,
uwezekano wa kuambukizwa ni mdogo sana. Kutumia kondomu
ipasavyo ina maana kutumia kondomu mpya, kuivaa vizuri uumeni
na kuitoa kabla ya uume kulegea.
Je, Virusi vya UKIMWI na UKIMWI
vinaambukiza kwa kujamiiana kwa njia ya
sehemu ya haja kubwa au mdomoni?
Je, nitaweza kupata virusi vya UKIMWI na
UKIMWI nikijamiiana na msichana au mvulana
wa umri mdogo sana?
Kwa nini nao watu wanaishi kwenye ndoa
wanapata maambukizi ya virusi vya UKIMWI
na UKIMWI?
mwingine. Kama mmoja wao au wote wawili watafanya ngono
na mpenzi mwingine (mahusiano nje ya ndoa) wanaweza kupata
maambukizi ya Virusi vya UKIMWI.
10
Je, ninaweza kuambukizwa na Virusi vya
UKIMWI na UKIMWI kwa kuumwa na mbu?
11
Hapana, ukila na mtu mwenyemaambukizi ya Virusi vya UKIMWI
huwezi kuambukizwa Virusi vya UKIMWI wala UKIMWI,
isipokuwa pale ambapo wote wawili mna vidonda mdomoni na
mnachangia kijiko kimoja. Lakini uwezekano huu ni mdogo
sana, kiasi tunachoweza kusema kwamba huwezi kuambukizwa
Virusi vya UKIMWI na UKIMWI ukila sahani moja na mtu
aliyeambukizwa na virusi.
Lakini, kufuatana na kanuni za afya, ni vizuri zaidi kila mtu
atumie vifaa vyake na baada ya kuvitumia avioshe kikamilifu.
12
Lakini siyo watoto wote waliozaliwa na
mama mwenye maambukizi watabeba
virusi. Kuwa moto ataambukizwa au
Natumaini hataambukizwa itategemea na idadi
sitapata VVU
ya virusi ambavyo viko kwenye damu
ya mama na sababu nyingine. Tafiti
zimeonyesha kwamba watoto wawili
kati ya watoto watatu waliozaliwa
na akina mama wenye maambukizi ya
Virusi huambukizwa na hivyo virusi.
Pamoja na hayo, mama mwenye
virusi vya UKIMWI anaweza kum-
wambukiza mtoto wake wakati wa
kumnyoshesha kwa sababu ya kuwe-
po virusi kwenye maziwa ya mama.
Akina mama walio na maambukizi ya
UKIMWI na UKIMWI wanashauriwa kuacha kuzaa na kutumia
njia za uzazi wa mpango.
13
Hali ya maambukizi ya VVU Tanzania kimkoa
Mkoa Asilimia
1. Mbeya 13,5
2. Iringa 13,4
3. Dar es Salaam 10,9
4. Mtwara 7,4
5. Pwani 7,3
6. Kilimanjaro 7,3
7. Mwanza 7,2
8. Tabora 7,2
9. Ruvuma 6,8
10.Shinyanga 6,5
11.Rukwa 6,0
12.Tanga 5,7
13.Morogoro 5,4
14.Arusha 5,3
15.Dodoma 4,9
16.Kagera 3,7
17.Lindi 3,6
18.Mara 3,5
19.Singida 3,2
20.Manyara 2,0
21.Kigoma 2,0
Chanzo: TACAIDS:HIV/AIDS Indicator Survey, Tanzania 2003-2004, Ukurasa 76
14
mpenzi
Kuwa na
m m o ja Acha
ifu
a mwamin kutembea
ua Zina peku
I una Ac
ha
IMW
UK
15
salama kwa upande mwingine ni kitendo cha kukaribiana ambacho
hakitahusisha uume kuingia ukeni au njia ya haja kubwa. Pia
utumiaji wa kondomu kila wakati ngono itahusisha kuingizwa
kwa umme, ukeni au njia ya haja kubwa ni njia nyingine ya
kujikinga
Twende tukapime
16
UKIMWI na UKIMWI au hapana. Njia hii ni ya kupima damu
yako katika vituo vyenye utaalamu wa upimaji.
Ni muhimu kukumbuka kuwa Virusi vya UKIMWI, vinaonekana
kwenye damu ya binadamu miezi mitatu baada ya kuambukizwa.
Kipindi hiki kati ya kuambukizwa hadi kufikia miezi mitatu kipimo
hiki hakiwezi kuonyesha kama maambukizi ya virusi yapo au
hayapo. Kipindi hiki ni cha hatari sana , kwani aliyeambukizwa
anaweza kuwaambukiza wengine bila kujua.
17
kwa sababu vyombo vinavyotumika katika upimaji ni vya gharama
kubwa na vinahitaji umeme na uangalizi mkubwa. Mpaka sasa
huduma hizi zinapatikana katika hospitali na kwa baadhi ya
mashirika yanayojishughulisha na maambukizi ya Virusi vya
UKIMWI na UKIMWI.
Jambo nzuri ni wewe kuuliza habari zaidi katika kituo cha afya
kilicho karibu nawe.
BADILI
TABIA
UKIMWI sina
18
kuzingatia kanuni muhimu za afya nzuri kama vile kula vyakula
vyenye mlo kamili na kujiweka katika hali ya usafi. Kwa mantiki
hiyo hiyo ni lazima kuharakisha kutibu maradhi mengine
yatakayojitokeza. Watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI
wanashauriwa wasitumie pombe wala kuvuta sigara, kwa
sababu vyote hivyo huchangia katika kudhoofisha mwili. Kama
watafanya ngono, ni lazima watumie kondomu ili wasiambukize
wengine.
Aliyeambukizwa, baada ya miaka kinga ya mwili wake itaanza
kupungua na atatakiwa kupata dawa za kupunguza makali ya
UKIMWI (ART).
Kama mtu aliyeambukizwa na virusi vya UKIMWI atazingatia
masharti haya, kuna uwezekano wa kuishi na kufurahia maisha
kwa miaka mingi.
19
Je , vipimo vya Virusi vya UKIMWI vinasema
ukweli?
20
wengine. Kumbuka kwamba rafiki au ndugu yako mwenye Virusi
vya UKIMWI na UKIMWI bado ni rafiki au ndugu yako!
21
Mambo ya Kukumbuka
22