You are on page 1of 5

Wamitila, (2003).

uhakiki ni istilahi inayotumiwa kuelezea sanaa au sayansi ya uchambuzi wa


kifasihi kwa njia ya kuichanganua na kuibainisha visehemu vyake ,kuifasili kulinganisha na
kuthamini na labda hata wakati mwingine hutolea hukumu kazi hiyo ya kifasihi.

Uhakiki wa kazi ya fasihi,ni maelezo yanayo chambua maandishi na mazungumzo kwa


kufafanua mambo mbalimbali yaliyomo.

Massamba (2009:63),nadharia ni taratibu,kanuni na misingi ambayo imejengwa katika muundo


wa kimawazo kwa madhumuni ya kutumiwa kama kielelezo cha kuelezea jambo.

Hivyo nadharia ni sayansi au sanaa inayohusika na kanuni za kijumla ambazo zinatumiwa katika
uchunguzi wa jambo au kitu Fulani.

Katika kuhakiki kazi mbalimbali za fasihi,nadharia mbalimbali hutumika kama vile;nadharia ya


ulimbwende,ufeministi,udhanaishi,uhalisia na nyinginezo.Nadharia ya uhalisia ni nadharia
ambayo hutumika kuelezea hali ilivyo katika jamii husika.Nadharia ya uhalisia huongozwa na
mambo yafuatayo; maudhui ndani ya kazi husika,urahisi wa kazi husika na uhalisia ambao
hubadilika badilika kutokana na mabadiliko ya jamii husika.

Kwa kutumia tamthiliya ya KILIO CHETU iliyoandikwa na Medical Aid Foundation


(1995).Tunatumia nadharia ya uhalisia kuelezea mambo na masuala mbalimbali yanayotokea
katika jamii,mambo hayo yanaweza kuwa ya kijamii,kiuchumi,kisiasa na kiutamaduni kama
ifuatavyo;

Athari za makundi rika yasiyofaa, katika kitabu cha kilio chetu mwandishi amejaribu kuonesha
namna makundi rika yanavyosababisha matatizo mbali mbali na kuwafanya vijana kujiingiza
katika masuala ya ngono na uvutaji bangi badala ya kusoma kwa bidii ili kufikia malengo
yao.Mfano mwandishi ameonesha wahusika kama vile Joti na marafiki zake akina
Jumbe,Mwarami na Choggo kama kundi lisilofaa kwa sababu badala ya kusoma wanajiingiza
katika kuangalia picha za X vilevile wanashauriana kujiingiza katika mapenzi wakiwa bado
wadogo.Mfano katika uk20, Jumbe anasema leo si ndio siku ya picha ya x?
umesahau?.Mwishoni Joti anapata UKIMWI na Suzi kupata ujauzito.Kutokana na nadharia ya
uhalisia suala kama hili lipo katika jamii kwani wapo vijana ambao ni wanafunzi na
wanajihusisha katika masuala ya ngono na matumizi ya bangi kitu ambacho kinapelekea
matatizo katika masomo yao na jamii kwa ujumla kuathirika.

Umuhimu wa elimu ya jinsia, katika kitabu cha kilio chetu,mwandishi ameeleza juu ya
umuhimu wa kutoa elimu ya jinsia,hasa pale mwandishi alipo watumia wahusika kama Baba
Anna na Mjomba kama mfano wa kuigwa katika jamii ambapo wanaona kumpatia mtoto elimu
ya jinsia akiwa bado mdogo inamsaidia kuepukana na matatizo katika ukuaji wake.Kwa mfano
katika (uk15), Baba Anna anasema mimi bwana nitaendelea kusisitiza juu ya elimu hii watoto
wajazwe elimu.Pia wahusika kama Mama Suzi,Baba Joti wanawakilisha wahusika wanaofikiri
kuwa kumpatia mtoto elimu ya jinsia akiwa bado mdogo ni kumpotosha au kumharibu

1
mtoto.Mfano katika (uk11), Mama Suzi anasema huko si ndiko kunifundishia mwanangu
umalaya?.Hivyo basi kutokana na nadharia ya uhalisia tunaona kuwa kuna wazazi ambao bado
wanaona kuwa ,kuwapatia watoto elimu ya jinsia ni kupoteza muda na ni kuwafundisha umalaya
na tabia mbaya kama alivyosema Mama Suzi ,hali hii ndiyo hupelekea watoto au vijana wengi
kujiingiza katika mambo yasiyofaa na kuharibikiwa kabisa ,kutokana na wazazi kutokuwa na
muda wa kukaa na wanawe na kuwaasa juu ya mambo yanayoendelea katika jamii.

Suala la imani potofu, imani potofu ni uhalisia unaojitokeza katika tamthiliya hii ya kilio chetu
pale mwandishi anapomtumia mhusika Jirani alipokuwa anashauri kuwa Joti apelekwe kwa
mganga wa jadi ambaye ni Chongo kwa ajili ya kupata matibabu pindi anapoumwa.Mfano Jirani
anaposema Hivyo mie naonelea kungefanyika jitihada niwapelekeni kwa fundi mmoja
anaitwa Chongo... Mambo haya katika nadharia ya uhalisia ,yanadhihirisha uhalisia wa mambo
yanayo fanyika katika jamii na uhalisia wake,kwani katika jamii zetu suala la imani potofu
linaonekana waziwazi pale watu wanapougua hukimbilia kwa waganga wa jadi badala ya
kwenda hospitalini kwa ajili ya kupata matibabu.

Athari za gonjwa la UKIMWI, tunategemea kuona au kupata matokeo ya gonjwa la UKIMWI


kutokana na madhara yake.Madhara yatokanayo na gonjwa hili la UKIMWI ni kama
vile;kifo,kupoteza nguvu kazi ya Taifa.Katika tamthiliya hii ya Kilio chetutunaona madhara
mbali mbali yanayosababishwa na UKIMWI kama pale wazazi wa Joti kupoteza nguvu kazi
baada ya Joti kufariki kwa gonjwa la UKIMWI.Tunamuona Mama Joti akiambulia kulia na
kulalama juu ya kifo cha mwanae Joti (uk.37).Hivyo basi athari za UKIMWI ni jambo ambalo
linauhalisia katika jamii zetu, kwani athari hizo tunaziona dhahiri, jamii na serikali kwa ujumla
haina budi kutoa elimu ya jinsia namna ya kujiepusha na kujikinga na hili gonjwa hatari.

Suala la umasikini, suala hili ni uhalisia unaojitokeza katika tamthiliya ya kilio chetu ambapo
mwandishi anamtumia mhusika Mama Suzi kuonesha uhalisia wa umasikini,hasa pale ambapo
analalamika kuwa anaungua mikono wakati wa kupika vitumbua ili aweze kupata pesa za
kumsomesha mwanae Suzi ambaye anaonekana kushawishika na kujiingiza katika suala la
mapenzi katika umri mdogo,ambapo matokeo yake anaambulia kupata ujauzito.Hivyo kutokana
na nadharia ya uhalisia tunaona katika jamii zetu wazazi hutafuta pesa kwa shida ili waweze
kuwasomesha watoto wao,lakini watoto hao hao hujiingiza katika suala la mapenzi kutokana na
vishawishi hata bila kujali hali ngumu wanayopitia wazazi wao katika kuhakikisha wasome na
kufikia malengo yao ya baadae.

Athari ya utandawazi, mwandishi ameonesha suala la utandawazi linavyochangia kuharibu tabia


na maadili ya vijana au watoto wengi,kwa mfano, mwandishi kawatumia wahusika kama vile;
Mwarami,Joti,Jumbe na Choggo wanajiingiza katika suala la mapenzi katika umri mdogo
kutokana na kuathiriwa na video za ngono wanazozitazama , kwa mfano Jumbe anaposema
leo si ndio siku ya picha ya X? umesahau?( uk.20).Hivyo basi tunaona jinsi uhalisia wa jambo
hili kwa vijana wengi katika jamii zetu.

2
Suala la usaliti, ni uhalisia mwingine unaojitokeza katika tamthiliya hii,kwa mfano mwandishi
anaonesha suala la usaliti kwa kumtumia Baba Joti ambaye anamsaliti mke wake na kujihusisha
kimapenzi na mwanamke mwingine,pia Joti anamsaliti Suzi kwa kuwa na wasichana wengine
kama vile;Gelda,Sikujua na Yoranda, mwandishi analithibitisha suala hili akimtumia Suzi pale
anaposema ndio maana mie nilikua nakataa Joti,nishambiwa kuwa una wasichana wengi
shuleni na mtaani kwetu(uk.21),hivyo katika jamii zetu uhalisia wa usaliti upo kwani tunaona
usaliti unapotokea baina ya wanandoa,wapenzi,marafiki na hata baina ya majirani.

Hivyo basi kutokana na matatizo mbali mbali yanayojitokeza katika jamii kama
tulivyoona,jamii haina budi kutoa elimu ya jinsia kwa watoto kuzingatia malezi bora kwa watoto
na kuachana na mila potofu kama vile kuamini waganga wa jadi zaidi kuliko mdaktari.Mbali na
hili,wazazi wanatakiwa kuwa nafasi ya kwanza katika kurekebisha tabia za watoto,kwani mzazi
ndiye mwalimu wa kwanza katika jamii.

3
MAREJELEO

1. Foundation,A.M, kilio chetu,Tanzania Publishing House,Dar es salaam(1995).


2. Massamba,Kamusi ya isimu na lugha,Falsafa ya lugha:TUKI,Dar es salaam(2009:63)

4
KITIVO : ELIMU.
IDARA : LUGHA NA ISIMU.
JINA LA KOZI : NADHARIA YA UHAKIKI NA MAENDELEO YA FASIHI YA
KISWAHII.
MSIMBO : SW125.
JINA LA MHADHILI : MUKAMA SHUKURU.
MWAKA WA MASOMO: MWAKA WA KWANZA, 2016/2017.
AINA YA KAZI : KAZI YA KIKUNDI.
MKONDO : BAED 1 A.
KUNDI : NAMBA 04.
NAMBA MAJINA NAMBA ZA USAJILI SAHIHI

1. BENSON SHILLA AM/BAED/160291


2. EMILY ERICK AM/BAED/160354
3. JUMANNE SALUMU AM/BAED/160477
4. KALITASI LIMBU SAYI AM/BAED/160482
5. BERNADI ESTER PAULO AM/BAED/160292
6. LEONARD STUMAHI AM/BAED/160567
7. CYPRIAN PIETHA AM/BAED/160330
8. ELIAS JOSEPH AM/BAED/160347
9. DAUD ELISHA AM/BAED/160337
10. ZEPHANIA VERONICA AM/BAED/15352
11. AUGOSTINO NDAYILAGIJE AM/BAED/160272
12. MVUMBA MAGRETH LAITON AM/BAED/160772
13. MASHAKA MUSA AM/BAED/160635
14. MCHEMBA MUSTAPHA AM/BAED/160685
15. MWASIKILI KELVIN AM/BAED/160801
16 MWALONGO DIGNA E AM/BAED/160787
17 RULAKUZE CHRISTINA M AM/BAED/160912
18 GEORGE SAMWEL AM/BAED/160388
Swali:

1.Hakiki kazi moja ya fasihi uliyosoma,kwa kutumia nadharia fahafu.

You might also like