Professional Documents
Culture Documents
4 Kubainisha uhusiano uliopo baina ya nadharia hizi na mchango wake katika vima
mbalimbali vya lugha
1
YALIYOMO
2
Wiki Mada Mada Ndogo Saa
Mchango wa Wanamiundo katika ngazi
ya Sintaksia
Wiki 7 (endelea) Mchango wa Wanamiundo katika miundo 3
ya kimofemiki
Mchango wa Wanamiundo na uibukaji wa
Sarufi Mpango/Msonge
Mtazamo wa Halliday na wenzake
kuhusiana na miundo ya lugha
Wiki 8 Nadharia ya Sarufi Geuza Umbo Historia ya Nadharia ya Sarufi Geuza 3
Zalishi Umbo Zalishi
Mwasisi wake na maendeleo yake
Viunzi vya Nadharia ya SGUZ
Wiki 9 Upya ulioletwa na Nadharia ya Dhana ya uzalishaji 3
SGUZ
Umuhimu wa muundo wan je na muundo
wa ndani
Mchango wa Nadharia ya SGUZ, katika
taaluma ya Fonolojia, Mofolojia, Sintaksia
na Semantiki
Wiki Maendeleo ya Nadharia ya SGUZ Jinsi Chomsky alivyopanua Nadharia ya 3
10 SGUZ – Nadharia pana sanifu (Extended
Standard Theory)
Matumizi ya data ya lugha na
ulinganishaji wa miundo mbalimbali ya
ulimwengu.
Wiki (Endelea) Nadharia ya Miundo Virai; 3
11
Uibukaji wa Nadharia ya Sarufi bia
Wiki Fonolojia zalishi kama utanzu wa Fonolojia Asilia 3
12 Nadharia ya SGUZ
Fonolojia Leksishi
Fonolojia Arudhi
Fonolojia ya Vipande Sauti
Semantiki Zalishi
Miundo ya sintaksia kwa misingi ya
nadharia ya miundo virai
3
Wiki Mada Mada Ndogo Saa
Wiki Mikondo mingine ya Uchanganuzi wa sentensi kwa kuzingatia 3
13 uchanganuzi isiyozingatia neno kuu
miundo ya virai
Semantiki ya sintaksia
Wiki Udurusu na maandalizi ya 3
14 mitihani
Mbinu za Kufundishia:
Utahini
Ili mzamili afaulu kozi hii, ni sharti apate asilimia 50 ya alama zote.
MAREJELEO MAALUMU
Borsley, R. (1999). Syntactic Theory: A Unified Approach 2nd Edition. London: Edward
Arnold.
Carnie, A. (2013). Syntax: A Generative Introduction 3rd Edition. West Sussex: Blackwell.
Chomsky, N. and Halle, M. (1968). The Sound Pattern of English. New York: Harper and
Row.
Chomsky, N. na Halle, M. (1995). The Minimalist Program. Cambridge, MA: MIT Press.
Cook, V.J. na Mark, N. (1996). Chomsky’s Universal Grammar: An Introduction. 2nd ed.
Oxford B: Blackwell Publishers Ltd
4
Crosft, D.A. (2004). Cognitive Linguistics. Cambridge: Cambridge University Press.
Goldsmith, J.A. (1990). Autosegmental and Metrical Phonology. Cambridge, Mass: Basil
Blackwell.
Haegeman, L. (1994). Government and Binding Theory 2nd Edition. Oxford: Blackwell.
Lee, D. (2001). Cognitive Linguistics: An Introduction. New York: Oxford University Press.
Massamba, D.P.B. (1996). Phonological Theory: History and Development. Dar es Salaam
University Press.
Massamba, D.P.B. (2011). Maendeleo katika Nadharia ya Fonolojia. Dar es Salaam: TATAKI.
Mathews, P. (1993). Grammatical Theory in the United States from Bloomfied to Chomsky.
Melbourne: Cambridge University Press.
5
Radford, A. (1988). Transformational Grammar A First Course. Melbourne: Cambridge
University Press.
Radford, A. (2004). Minimalist Syntax Exploring the Structure of English. New York:
Cambridge University Press.
Seuren, P.A.M. (2004). Chomsky’s Minimalism. New York: Oxford University Press.
Spencer, A. and Zwicky, A.M. (wah.) (2001). The Handbook of Morphology. John Wiley &
Sons.
Webelhuth, G. (mh.) (1995). Government and Binding Theory and the Minimalist Program.
Blackwell.
IDHINI
Dr.StanleyAdikaKevogo 04/08/2022
Mhadhiri: ............................................................Saini: ............................... Tarehe: ..................
Mudiri (COD): ....................................................... Saini: ............................. Tarehe: ..................
6
UTANGULIZI
Maana ya Isimu
Wanaisimu wameeleza maana ya isimu kwa njia tofauti. Hata hivyo, wote wanaelekea
kukubaliana kuwa Isimu ni taaluma inayochunguza lugha ya mwanadamu kisayansi.
Kwa mujibu wa Hartman (1972) Isimu ni eneo maalumu la mtalaa ambalo lengo lake ni
kuchunguza lugha. Nao Richards na wenzie (1985) wanaifasili Isimu kuwa ni mtalaa
ambao huchunguza lugha kama mfumo wa mawasiliano ya wanadamu. Besha (1994)
anaeleza Isimu kuwa ni taaluma inayochunguza na kuweka wazi kanuni ambazo ndizo
msingi wa kila lugha. Nayo Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili (1990) inaeleza Isimu
kuwa ni sayansi ya lugha.
Fasili hizi zina maelezo yanayofanana kwa kiasi kikubwa. Jambo linalosisitizwa hapa ni
kwamba Isimu hushughulikia uchunguzi wa lugha mbalimbali kwa kutumia misingi ya
kisayansi. Kwa hivyo, tunaweza kuhitimisha kuwa Isimu ni taaluma inayohakiki lugha
kisayansi. Isimu ni sayansi ya matamshi, maumbo, miundo, maana na matumizi ya
lugha. Isimu inatumia mtazamo wa kisayansi kuchambua lugha kinyume na ilivyokuwa
hapo zamani ambapo watafiti waliathiriwa na hisia na mielekeo yao.
Usayansi wa Isimu
Hili ni kusema kuwa Isimu haichunguzi lugha kiholela bali kwa utaratibu na mwelekeo
maalumu. Katika kuchunguza lugha, wanaisimu hutumia misingi ya kisayansi kama
zinavyofanya sayansi zingine kama vile Fizikia, Kemia na Bayolojia. Zipo sifa nne kuu za
uchambuzi wowote wa kisayansi. Sifa hizo ni pamaoja na:
a) Uwazi na Ukamilifu
Dhana hii ina maana kuwa masuala katika Isimu huelezwa kwa udhahiri usio na utata.
Hoja huelezwa bila shaka yoyote kimaana. Ni sifa inayomtaka mwanaisimu kujiwekea
lengo la kupima kwa uangalifu kila analofanya na kuhakikisha kuwa hoja zote anazotoa
ili kutegemeza nadharia zake au mahitimisho yake ni wazi na zinatokana na utafiti wake.
7
Wakati uchunguzi unapofanywa huwa kuna machukulio. Machukulio haya hubainishwa
wazi. Kwa mfano, mwanaisimu anaweza kuchunguza jinsi watu hujifunza lugha za pili
na matatizo ambayo huwakumba. Machukulio ya utafiti kama huo ni kuwa hawa watu
wana bongo imara na razini. Hili inabidi mchunguzi aweze kulibainisha.
Lugha ya taaluma ya isimu pia ina dhana mbalimbali kama vile ‘sentensi’, ‘neno’, ‘foni’,
‘fonimu’ na ‘mofimu’. Zinapotumika, dhana hizo huelezwa na mtafiti ili kupatikane
uwazi katika utafiti wake.
b) Utaratibu/Upangilifu
Utaratibu ni kufanya mambo kwa mpangilio mzuri wenye kubainika. Utaratibu unaweza
kuhusisha wakati, idadi, umuhimu na hata ukubwa. Kwa mujibu wa sifa hii, hoja za
kisayansi zinapaswa kupangwa vizuri. Taaluma yoyote ya kisayansi hufuata utaratibu
maalum na mambo yake huendeshwa hatua kwa hatua. Wanaisimu huichunguza lugha
kwa utaratibu maalumu, si kiholela.
1 Nadhariatete pia huitwa Haipothesia. Nadhariatete ni makisio au taarifa inayotabiri uhusiano baina ya vipengele
(vibadiliki) viwili katika utafiti. Inaonesha uhusiano ambao unaweza ukathibitishwa au ukakosolewa. Kwa mfano,
‘Kuna tofauti za kiisimu kati ya sarufi ya Kiswahili sanifu na sarufi ya Kimaasai’ au ‘Lugha ya Kiswahili ni ya
Kibantu’.
Kwa mfano, ikiwa mwanaisimu ameamua kufanya utafiti juu ya fonolojia ya lugha
fulani, atakuwa tayari na makisio (nadhariatete) ambayo atajaribu kuthibitisha kwa
kutoa data yake katika mawasiliano ya kila siku ya wanadamu wanaozungumza lugha
hiyo. Kisha data itakayokusanywa itachunguzwa kwa kutumia misingi maalumu ya
kinadharia ili kufikia uamuzi kuhusu nadhariatete.
8
Nadharia ni msingi au msimamo wa kuchunguza matukio fulani katika maisha ambao
unaratibu namna jambo linatakiwa kufanywa. Kupitia kwa nadharia, matokeo ya
uchunguzi huhimiliwa na ithibati tosha. Nadharia hutupa mkondo wa fikra, hutumulikia
mambo na kutuwezesha kusaili, inaupa uchunguzi misingi thabiti na inatusaidia kuona
ukweli ili tutoe fasili ifaayo. Nadharia ndiyo huongoza utafiti ikiwa inafafanua mawanda
na kutoa mwelekeo wa kufuata katika utafiti. Kuna nadharia mbalimbali za kiisimu
kama vile: Umuundo, Uchanganuzi makosa, Uchanganuzi Linganuzi, n.k.
c) Urazini/Uhoromo/Uhakikifu
Sifa hii pia inajulikana kama utonafsi au kutopendelea. Huku ni kutazama mambo
yalivyo bila kushawishiwa na hisia. Katika kuzingatia sifa hii, mwanaisimu anapaswa
kuhakikisha kuwa yale anayoyasema, pamoja na mahitimisho anayoyafikia, yanatokana
na data zilizo wazi na ambazo zinaweza kuchunguzika. Tamko lolote la kisayansi lazima
liweze kuthibitishwa na hoja.
Urazini ni sifa kuu ya sifa za usayansi. Inamaanisha kuwa wanaisimu wawe tayari
kupokea mawazo au mashauri mapya katika uchunguzi. Waiwekee nadhariatete shaka
hadi pale ushahidi kamili utakapopatikana. Wanaisimu wajitahidi kuepuka kutilia
mkazo wazo fulani kabla halijakamilika. Inawapasa kila mara kufikiria juu ya mwafaka
badalia wa tatizo hilo au hata kuwapa wenzao kazi zao wazisome na wazikosoe. Kusudi
la sifa hii ni kuondoa ubinafsi katika utafiti.
9
jarabati, yaani ya kutegemea majaribio, si ya kubahatisha. Sharti matokeo yaweze
kuthibitika. Pia inamaanisha kutumia taratibu zinazokubalika na takribani wanaisimu
wote. Hili linawezekana ikiwa wanaisimu watatumia mbinu zinazokubalika katika Isimu
kama vile jozi milinganuo finyu katika fonolojia. Hii ni mbinu inayotumiwa na
wanaisimu wanapotaka kufahamu mfumo-sauti wa lugha ngeni.
d) Iktisadi
a) Fonolojia
/b/ z -i
v
Maelezo yake: konsonanti /b/ hubadilika na kuwa /z/ au /v/ katika mazingira ya
kutangulia /i/. Kwa mfano, iba mwibi mwizi / mwivi.
b) Sintaksia
SKN+KT
Maelezo yake: sentensi hii imeundwa kwa Kundi Nomino (KN) na Kundi Tenzi (KT).
KN/KT
Yeyote anayedai kuwa anafahamu lugha lazima awe na uwezo wa kusema na kueleweka
na wale wanaofahau lugha hiyo. Hii ina maana kuwa, mtu anaweza kutoa sauti
zinazoashiria maana fulani, na kuelewa sauti hizo, na kuzifafanua. Miongoni mwa
misingi ya kiisimu kuhusu ujuzi wa lugha ni kama ifuatayo:
a) Mfumo wa Sauti
b) Maana ya Maneno
10
Kujua sauti na mfumo wa sauti ni kipengele kimoja tu cha ujuzi wa lugha. Sauti za lugha
sharti ziashirie dhana au maana fulani. Kwa mfano, neno ‘kalamu’ katika mfumo wa
Kiswahili lina maana tofauti na neno ‘karamu’.
Kwa hivyo, ujuzi wa kiisimu humwezesha mtu kutambua namna ambavyo sauti
huhusishwa na maana. Ni lazima mtu ataje na kujifunza sauti zinazowakilishwa na
herufi ili kuwasilisha dhana inayozungumziwa. Sauti katika maneno hupewa maana
katika mfumo wa lugha inamopatikana.
c) Ubunifu
Ubunifu humwezesha mtu kuweka pamoja sauti ili kuunda neno. Maneno nayo
huwekwa pamoja kuunda sentensi au tungo mbalimbali. Mwanadamu ana uwezo wa
kutaja, kubuni na kutunga sentensi tofauti tofauti kulingana na jinsi anavyotangamana
na mazingira yake.
d) Usahihi wa Sentensi
Maana ya Nadharia
11
wa kushughulikia somo au taaluma fulani. Kimsingi, nadharia ni mitazamo mbalimbali
kuhusu jambo fulani.
Watu huona jambo kwa mitazamo au mikabala tofauti. Mikabala hiyo sharti iweze
kuthibitishwa kiutafiti. Kwa mfano, wataalamu wanaochunguza masuala ya kiisimu
hutofautiana kimtazamo kwa mujibu wa misingi yao ya kinadharia. Kwa hali hiyo,
nadhari husaidia katika kueleza jambo kwa urahisi.
Aina za Nadharia
Nadharia Asilia
Nadharia Nyambuaji
Nadharia Changamano
a) Nadharia sharti iwe tabirifu, yaani inapaswa kutabiri maana fulani. Kwa mfano,
katika mfumo wa Kiswahili, maneno yanafaa kuwa na muundo fulani. Lazima
nadharia iwe na uwezo wa kutenga vipashio katika kategoria mbalimbali kama vile
nomino, vitenzi, viwakilishi, vielezi, viunganishi, vihusishi, n.k.
c) Nadharia huwa na falsafa yake. Hii ina maana kuwa lazima iwe na mtazamo fulani
wa kuelezea kile inachokieleza.
12
e) Nadharia inapaswa kueleza mambo yaliyozidi data yake. Yaani, maelezo ya nadharia
yaweze kutumika kufafanua data nyinginezo.
b) Nadharia hutoa mwongozo kwa mtafiti kueleza vipengele mbalimbali vya fasihi ili
afanye uamuzi wa kutegemewa kuhusu kazi anayoitafiti. Nadharia itamwongoza
mtafiti kuratibu uchunguzi wake katika harakati ya kuzua, kuchuja na kuweka
mikakati ya kutafitia fasihi.
c) Nadharia hutusaidia kulishughulikia somo la fasihi kitaaluma ili lifasiriwe kwa njia
mwafaka. Hii ni kwa sababu fasihi humwathiri msomaji kisaikolojia na umuhimu
wake hauwezi kupuuzwa, kuepukika wala kukwepwa.
13
SARUFI MAPOKEO
Utangulizi
Sarufi ya awali zaidi ilitungwa katika kipindi cha mbabe Alexander na Myunani
aliyeitwa Dionysus Thrax. Sarufi hiyo iliitwa Techne Grammatike (The Art of Grammar).
Baadaye Warumi walitumia mfumo wa kisarufi wa Wayunani katika lugha ya Kilatini
bila mabadiliko mengi. Kati ya karne ya 12 hadi ya 14 kikundi cha wasomi kilichoitwa
14
Modistae kilitoa kazi mbalimbali zilizojikita katika sarufi ya makisio. Mtazamo wao wa
kisarufi ulikuwa ukiitwa Grammatica Speculativa. Waliamini kulikuwepo sarufi bia moja
inayohimiliwa na uhalisia na urazini wa binadamu. Kufikia karne 17, maoni tofauti ya
kisarufi yaliendelezwa. Kufikia mwaka wa 1700, sarufi za lugha 61 zilikuwa zimeandikwa
zikiwemo zile za Kiingereza, Kifaransa, Kiarabu na Kiitaliano. Sarufi nyingi za mwanzo
ziliandikiwa kwa makusudi ya kufundishia. Pia, walitaka kuzisanifisha kupitia maandishi.
Katika kipindi hicho cha maendeleo ya sarufi, wataalamu waligawanyika kimaoni wengine
wakipendekeza sarufi fafanuzi na wengine sarufi elekezi.
Kwa ujumla, sarufi mapokeo ilisababisha kuzuka kwa makundi mawili ya wasomi.
Kundi la kwanza ni lile linalowahusu wanafalsafa na la pili ni la wanaisimu. Kimsingi,
mtazamo huu ulizingatia lugha katika mikondo na mikabala ya jadi. Inadaiwa kwamba
Plato ndiye aliyekuwa mtu wa kwanza kutafiti lugha na baadaye akafuatwa na Aristotle
aliyekuwa mwanafunzi wake. Wanaisimu watatu waliokuwa kwenye mstari wa mbele
kutafiti lugha mbalimbali ulimwenguni walikuwa wafuatao:
Wataalamu hao walitumia mbinu ambazo kwa pamoja zilifanana, kwa mfano:
15
f) Walishikilia kuwa kulikuwepo na uhusiano wa moja kwa moja kati ya neno na kile
kilichowakilishwa na neno hilo. Huu ulikuwa mtizamo wa kiuasilia, ambao pia
huitwa mtizamo wa kionamatopea. Kwa wanamapokeo, huo ndio msingi wa lugha
yoyote.
i) Walifafanua kwamba kila lugha ina kategoria za kisarufi na kileksia kama vile
nomino, vielezi, vitenzi n.k.
Dhana za sarufi mapokeo zinazofafanuliwa katika kijisehemu hiki ni: neno, sentensi,
kishazi na kirai.
Dhana ya Neno
Kwa mtazamo wa kimapokeo, neno ni kipengele cha msingi. Neno linafafanuliwa kuwa
ni kipengele cha lugha ambacho ni kidogo na huru kinachoweza kutamkika pekee yake
(Bloomfield, 1933). Maelezo haya, hata hivyo, yana upungufu. Hii ni kwa sababu
wanamapokeo waliegemea kwa lugha andishi katika fasiri yao. Ni rahisi kulitambua
neno katika muktadha wa maandishi. Kwa kuangalia nafasi kati ya neno moja hadi
lingine, ni rahisi kutambua neno katika maandishi. Hili linawezekana kwa kuangalia
nafasi inayotenganisha kipashio kimoja na kingine. Ikiwa ipo nafasi kati ya vipashio
viwili basi kila kipashio kinachukuliwa kuwa neno. Kwa mfano:
Jumba//hili//ni//zuri.
16
Katika lugha ya mazungumzo, nafasi hizi zinafikiriwa kuwa zinasimamiwa na kituo au
mtuo. Hata hivyo, ukweli ni kwamba, hatutui baada ya kutamka kila neno moja.
Tunaposikiliza lugha tusiyoielewa, hatuwezi kusema kwa uhakika ni wapi maneno
yanapoishia. Ni sawa na kusema kuwa lugha ya mazungumzo hutokea katika mfululizo
wowote bila kutua. Ijapokuwa wanasarufi mapokeo walitumia neno bila kutoa fasili
toshelevu, ukweli ni kwamba dhana hiyo ipo na inaendelea kutumiwa katika
uchanganuzi wa sarufi.
Aina za Maneno
Dhana ya Sentensi
Kwa mujibu wa wanamapokeo, sentensi ni tamko lenye fikra kamili. Maaelezo haya hata
hivyo yanadhihirisha upungufu. Kwanza, ‘fikra kamili’ ni nini? Pili, tutaitambuaje fikra
kamili na ni ipi isiyo kamili? Zaidi ya haya, hatuwezi kutambua ikiwa neno ni tamko au
kama kifungu cha maneno ni sentensi. Isitoshe, wanamapokeo hawakufafanua tofauti
iliyopo baina ya sentensi sahili, ambatani na changamani.
Njia mwafaka ya kuifafanua sentensi ni kwa kuchunguza muundo wake. Kila sentensi
huundwa kwa vipashio maalumu vilivyopangwa kwa utaratibu maalumu. Kwa kutumia
muundo wa vipshio, tunaweza kuonyesha kipashio kinachoweza au kisichoweza kuitwa
sentensi. Kwa kutumia muundo kama kigezo cha kuifafanua sentensi, sentensi basi
inakuwa kipashio kikubwa zaidi ambacho kinaweza kuwa na muundo wa kisarufi. Kwa
mfano:
Kila kipashio katika sentensi huchukua nafasi yake wala hakiwezi kuchukua nafasi ya
kipashio kingine bila kuathiri maana ya sentensi inayohusika.
Kirai
Katika sentensi, mnapatikana maneno yaliyo na dhima sawa. Maneno haya yanaweza
kuchukuliwa kama kipashio kimoja. Kwa mfano:
Vipashio vya aina hii vinaweza kuitwa virai, vikundi au vifungu. Vinapatikana kama
sehemu moja ya sentensi. Virai haviwezi kujisimamia. Kwa mfano;
17
Mti mrefu; Mtoto mzuri; Kwao nyumbani; Mara tano; n.k
Kila sentensi huwa na vikundi viwili vikuu vinavyoiunda. Hivi ni: KIRAI NOMINO na KIRAI
KITENZI. Virai hivi huchukua nafasi maalumu katika sentensi. Kila kirai lazima kiwe na
neno kuu linaloongoza mengine. KN huungozwa na nomino, ilhali KT huongozwa na
kitenzi.
Kishazi
Mkabala wa Sarufi Mapokeo una misingi yake katika sifa maalumu zinazoibainisha
sarufi hii. Nadharia ya sarufi mapokeo inajikita katika misingi ifuatayo:
f) Lugha iliyochukuliwa kuwa msingi wa sarufi ilikuwa Kilatini. Hii ni kwa sababu mambo
mengi ya kitaaluma wakati huo yalichunguzwa na kuandikwa kwa Kilatini. Lugha
ya Kilatini ilikuwa mojawapo ya lugha awali sana kuwa na maandishi. Lugha zote
zilichunguzwa kwa misingi ya Kilatini. Lugha zote ulimwenguni zilichukuliwa kuwa
na sarufi moja. Kwa muda mrefu lugha ya Kilatini ilichukuliwa kama kielelezo cha
matumizi ya kiwango cha juu kabisa cha lugha. Kwa hivyo, wanamapokeo,
walichunguza na kuishia na kanuni na sheria zilizoeleza matumizi yake. Kanuni hizo
zilichukuliwa kama kigezo cha kuchambulia lugha nyingine za ulimwengu – hata
Kiingereza. Kwa mfano, Kilatini kina sifa ya kunyambulika kwa maneno. Kwa
kutumia kigezo hiki Wanamapokeo walikiona Kiingereza kuwa na chembe za sarufi
kwani hakina sifa hii sana kikilinganishwa na Kilatini ilhali Kichina ambacho hakina
tabia hii kilisemekana kuwa hakina sarufi.
g) Sarufi mapokeo ilipendekeza kanuni za lugha. Sarufi mapokeo ilieleza kwa jinsi ambavyo
mtu anatakiwa kuongea na kuandika. Kulikuwa na kanuni ambazo zilipasa kufuatwa
18
katika kutumia lugha kwa njia sahihi. Wanamapokeo walitoa sheria zilizoelekeza
namna ya kutumia lugha.
6) Walionelea kwamba lugha ya maandishi ilikuwa bora kuliko lugha ya mazungumzo. Kwa
wanamapokeo, lugha ilikuwa ile iliyoandikwa. Maoni haya yalishikiliwa sana na
Wagiriki. Maoni yao yanafungamana na neno la Kigiriki grammar yaani sarufi
linalotokana na neno la Kigiriki grammatike linalotumiwa kwa maana ya 'kuandikwa'.
Kutokana na neno hili basi wanamapokeo wakachukulia kwamba lugha yoyote
ambayo haikuwa imeandikwa au kuandikiwa sarufi haikuwa lugha kamwe. Lugha
ya Kilatini ndiyo iliyokuwa imeandikwa wakati huo. Sarufi za lugha zote za
ulimwengu ziliegemezwa kwa lugha ya Kilatini ambayo ilikuwa lugha ya wasomi
wakati huu na tena iliyoandikwa.
19
c) Istilahi zilizobuniwa na wanamapokeo zinaendelea kutumiwa na kupanuliwa huku
zikipewa mitizamo mipya ili ziweze kutumika katika lugha nyingi iwezekanavyo.
1. Kwa kutumia kanuni za Kilatini kuwa kigezo cha uchanganuzi wa lugha, mtizamo
huu ulibainisha udhaifu kwani kila lugha ina fonimu zake mahsusi, muundo wa
maneno na sarufi ya kipekee. Takriban lugha zote duniani zinatofautiana kwa njia
mbalimbali, siyo katika kiwango cha leksia, fonolojia, sintaksia n.k. kwa mfano,
katika Kiswahili sentensi:
Aidha, dhana ya wingi huwasilishwa kwa mifumo tofauti. Katika Kiswahili kwa
mfano, kuna matumizi ya viambishi vya wingi kama vile katika msichana -
wasichana. Katika Kiingereza, girl - girls.
2. Wanasarufi mapokeo walidai kwamba Kigriki kilikuwa na hadhi ya juu kuliko lugha
nyingine za ulimwengu. Maoni haya yana udhaifu kwa kuwa lugha zote ni sawa
kihadhi. Haipo lugha inayojivunia kuwa na hadhi kiisimu kuliko lugha nyingine. Hii
ni kwa sababu kila lugha inatimiza malengo ya wazungumzaji wake kijamii na
kwamba kila lugha inajitosheleza. Kila lugha ina msamiati unaoweza kutosheleza
shughuli za maisha ya kawaida ya jamii inayohusika. Lugha inapokosa msamiati wa
kurejelea dhana zisizopatikana katika muktadha wake, si ishara kwamba lugha hiyo
ni dhaifu. Lugha zote zina uwezo wa kusharabu na kuunda misamiati mipya ili
kufidia upungufu huo.
3. Sarufi Mapokeo hupendekeza kanuni za lugha. Sarufi hii ilielekeza jinsi ambavyo
mtu alihitaji kuzungumza na kuandika lugha. Zilikuwepo kanuni zilizopaswa
kufuatwa katika matumizi ya lugha kwa njia sanifu. Msimamo huu hata hivyo
20
unadhihirisha udhaifu kwani, sarufi haipaswi kulazimishwa au kuelekezwa. Sarufi
inapaswa kuelezwa (kufafanuliwa). Wanamapokeo walisahau kuwa sarufi inastahili
kuangalia lugha jinsi ilivyo na kuieleza na siyo kuilazimisha kufuata kanuni. Istoshe,
wazungumzaji wa lugha hawatungiwi kanuni za jinsi ya kuiongea lugha yao kwani
kila mzawa wa lugha fulani anazifahamu kanuni za lugha yake pasi na kuandikiwa
kanuni.
6. Sarufi mapokeo ilisisitiza kuwa lugha andishi ilikuwa bora zaidi kuliko lugha
zungumzwa. Walieleza kuwa lugha yoyote ambayo haikuwa imeandikiwa sarufi
haikuwa lugha kamwe. Ni lugha ya Kilatini pekee iliyokuwa imeandikwa kwa
wakati huo. Msimamo huu unadhihirisha udhaifu. Ni dhahiri kuwa lugha
zungumzwa ni kongwe kuliko lugha andishi kwani maandishi yalibuniwa baadaye
tu. Mawasiliano kupitia mazungumzo yalikuwepo kabla ya maandishi. Kuandikwa
kwa lugha ni njia mojawapo tu ya kuhifadhi lugha, wala maandishi si lugha tofauti.
Aidha, zipo lugha nyingi tu duniani ambazo hazijaandikiwa sarufi. Pia zipo lugha
ambazo zinatumia tu ishara, na hati za uandishi za lugha zingine. Maandishi
yanawakilisha sehemu ndogo tu ya ukwasi wa lugha kwani hatuwezi kuhifadhi
sentensi zote za lugha katika maandishi. Mazungumzo ya watu hubadilika kila mara
na kwa mpito wa wakati. Kwa mfano, matumizi ya Kingereza nyakati za Shakespear
yalikuwa tofauti na ya nyakati hizi. Pia, lugha zungumzwa iko hai, ina ishara na
inadhihirisha hisia mbalimbali, bali ile ya kuandikwa ni kavu na haina mvuto
wowote.
Kwa hivyo, katika sintaksia, hatuna budi kutumia sifa za kimsambao katika
kufafanua aina za maneno. Msambao hurejea nafasi mbalimbali ambazo elementi za
kiisimu zinaweza kukalia katika tungo iliyoandikwa vizuri (kisarufi). Kwa mfano,
‘Nomino’ inafafanuliwa kuwa kategoria inayoungana na Vivumishi ili kuunda Kundi
21
Nomino. Pia inaweza kufafanuliwa kama neno linaloungana na kitenzi ili kuunda
Kundi Tenzi. Kwa mfano:
Vihusishi aghalabu hutangulia nomino katika ujenzi wa Vikundi Vihusishi kama vile:
katika runinga
hadi Namanga
Kwa hali hiyo, hatuwezi basi kutoa ufafanuzi wa aina yoyote ya neno bila kugusia
aina nyingine au dhana nyinginezo za kisintaksia.
Hitimisho
Somo hili limeeleza nadharia ya Sarufi Mapokeo. Historia yake, sifa zake, dhana zake,
umuhimu na udhaifu wake. Tumeeleza kwamba licha ya udhaifu uliojitokeza katika
mkabala huu wa sarufi, bado una umuhimu katika kuzifafanua sarufi mbalimbali za
lugha za ulimwengu.
22
SARUFI MIUNDO
Utangulizi
Kwa mujibu wa TUKI (1990) muundo umeelezwa kuwa mpangilio wa vipashio mbalimbali
katika lugha. Nayo Kamusi ya Kiswahili Sanifu (2004) imeueleza muundo kuwa ni:
Kwa hivyo, uchambuzi wa lugha hujikita katika uelezaji wa ruwaza hizo. Hata hivyo,
maelezo ya Sweet hayakutiliwa maanani hadi 1914 ambapo wanaisimu kama vile
Leonard Bloomfield2 waliyatetea katika kazi zao. Hii leo, kazi hizi za awali za Bloomfield
zinachukuliwa kama msingi wa Sarufi Miundo huko Marekani.
Nadharia ya isimu iliendelezwa sana Marekani kuliko Ulaya. Pande za Ulaya Sarufi
Miundo iliendelezwa na mwanaisimu wa Kiswisi Ferdinand de Saussure. Wanaisimu
23
wengine ni Franz Boas na Edward Sapir. Kazi ya de Saussure imekusanywa katika
kitabu: A Course in General Linguistics kilicholewa kwa mara ya kwanza mnamo mwaka
wa 1915. Mambo muhimu yanayoifanisha kazi yake ni kule kutenga lugha katika vitengo
maalumu yaani – langage (lugha), langue (mfumolugha) na parole (utendaji).
c Langage
e) Langue
Kwa hivyo, langue ni jumla ya sarufi, msamiati, sheria za utamkaji, pamoja na sheria za
uundaji maneno. Langue iliweza kutumiwa na mtu binafsi kama parole.
g) Parole
Parole ina ubinafsi wa yule anayeitumia katika hali halisi. Utendaji ni usemaji wa lugha
katika miktadha halisi. Ni lugha tumikizi inayotokana na sheria za jamii za langue. Kwa
mujibu wa De Saussure lugha hii ina makosa na haipaswi kutumiwa kama data ya
uchunguzi wa kiisimu.
24
Kutokana na kuvuma kwa kazi yake, wanafunzi wake waliweka misuada yake pamoja
na kukichapisha kitabu chake baada ya kufa kwake. De Saussure alieleza umbo la lugha
na muundo wake na kuonyesha kwamba vipengele vya lugha vinahusiana. Ili
kuendeleza wazo hili alitumia mfano wake maarufu wa kulinganisha vipengele vya
lugha na mchezo wa chess. Ili wachezaji wa chess wafanikishe mchezo huo, hawana budi
kusaidiana na kushirikiana.
7) Hujaribu kueleza na kufafanua lugha. Kwa hivyo, Sarufi Miundo huitwa – fafanuzi
au elezi.
8) Hueleza lugha jinsi inavyotumiwa bila kurejelea ukamilifu wake kwa kutegemea
kanuni fulani fulani kama walivyofanya wanamapokeo.
9) Wanamiundo hueleza matumizi yote ya jinsi lugha ilivyo bila kujikita kwenye
matumizi bora, safi au kufuata sheria zilizowekwa.
10) Wao hutegemea miundo au maumbo ya lugha yanayoonekana – yale ya nje (surface
structures). Haya ni yale maumbo tunayoyaona katika maandishi au kuyasikia katika
mazungumzo.
11) Kiini cha uchanganuzi wao ni muundo au umbo la lugha lakini siyo maana ya
vipengele vya lugha (kinyume na wanamapokeo: nomino nk). Walichunguza
vipengele vya isimu kutokana na data (kusanyiko la sentensi).
13) Kwao, muundo wa vipashio ni kitu cha kidhahania ambacho huonyesha kazi ya
kipashio iliyobuniwa ili kusaidia kutoa maelezo ya kile kiwezacho kusemwa au
kuandikwa katika msonge (hierachy) wa vipashio. Kwa mfano,
c) Kwa mujibu wa Wanamiundo, lugha hujengwa kwa mofu, mofu ikiwa ndiyo
kipashio kidogo chenye maana katika neno. Walichunguza jinsi vipashio mbalimbali
vinavyojenga tungo.
3
AdikaStanley Kevogo,Shule Kuu yaSayansi zaJamii,Chuo KikuuchaMount Kenya
25
katika mkabala wa maana. Wanamiundo nao walikopa dhana hizo na kuzifafanua
upya. Wanamiundo walizichukulia istilahi hizo kama vipashio vya lugha
vinavyotenda kazi kwa namna maalumu.
Katika lugha ya Kiswahili, vipashio vingi vya kisarufi ni mofu tegemezi. Hatuwezi
kueleza maana ya sentensi kwa kutegemea maana ya maneno peke yake kama:
a-li-m-tembe-lea
Hatuna budi kuelewa utendakazi wake wa kisarufi. Kwake Fries, sentensi si kundi la
maneno tu, bali ni ruwaza ya muundo. Ruwaza hii imeundwa kwa kategoria za
maneno ambazo zinaweza kutambuliwa kwa maumbo yake pamoja na nafasi zake
katika ruwaza. Nafasi hizo ndizo hudhihirisha maana ya kimuundo ya sentensi.
Mpangilio wa maneno katika sentensi ni njia mwafaka zaidi ya kueleza au kutambua
kategoria za maneno. Maneno yanayopatikana katika nafasi sawa na yanayohusiana
na mengine kwa namna sawa yanaweza kuelezwa kuwa yanaunda kategoria moja
ya maneno. Kwa mfano:
26
Nomino Kitenzi Yambwa Kivumishi
Kitabu kiliibwa.
Nadharia ya Sarufi Miundo ni zao la Isimu Fafanuzi iliyoshamiri sana kunako karne ya
8. Nadharia hii ilianza baada ya kuchapishwa kwa kitabu: A Course in General Linguistics
chake mwanaisimu Mswizi, Ferdinand de Saussure mnano mwaka wa 1916. Kitabu
hicho ni zao la uratibishaji wa mihadhara aliyoitoa de Saussure kabla ya kifo chake.
Langue
Kwa mujibu wa Saussure, langue ni mfumo ambao kila mtumiaji wa lugha anaurejelea
katika usemaji au uandishi wake. Ni mfumo unaoigwa na kila mtu. Anaeleza kwamba
kila lugha ni mfumo ulio huru, na kwamba kutokana na hiyo langue kuna wasemaji
wengi. Aidha, langue ni mfumo ulio na kanuni zinazohusu lugha fulani, na kila lugha ni
langue kwa maana kwamba ni mfumo unaomilikiwa na wanajamii na kutokana na
mfumo huo wa kijamii wasemaji binafsi huchota na kutenda. Tunaweza kuchukulia
mfumo huo kama jumla ya kanuni na kaida zote zinazotawala au kupatikana katika
lugha fulani. Kila tunapoongea lugha, tunawajibika kuzitii kaida na kanuni za lugha
hiyo.
Parole
Katika langue kuna parole nyingi kadiri walivyo wasemaji wa lugha inayohusika.
Saussure alifafanua parole kuwa ni utendaji wa mtu binafsi katika jamii. Yaani ni upekee
wa matumizi ya lugha ya mzungumzaji wa lugha fulani. Hii inahusisha lafudhi ya
mzungumzaji wa lugha inayohusika.
27
Signife na Signifiant
Saussure pia alifafanua kwamba ishara zote ni nasibu na ni za kikaida. Katika ishara za
kiisimu isimu, signife inawakilishwa na tamko au ishara za kigrafolojia. Signifiant nayo
huwakilishwa na kile kinacho maanishwa na lile tamko ua ishara ya kigrafolojia.
i) Uhusiano wa Silisila
Katika mifano hii, sentensi (a) ni sahihi kwa sababu ishara ‘anaimba’ inaendana na
‘wimbo’ katika uhusiano wa kimlalo, lakini katika mfano wa (b), ishara ‘anasoma’ haina
uhusiano wa silisila na ‘shamba’. Hii ina maana kwamba ishara hizi mbili hazina
uhusiaono silisila kwa sababu haziwezi kubadilishana nafasi katika sentensi hizi.
28
Neno ‘huyu’ na ‘yule’ ni paradimu kwa sababu yanaweza kubadilishana katika maana au
muktadha. ‘Huyu’ linaweza kuchukua nafasi ya ‘yule’, kutokana na hali kwamba neno
‘msichana’ ni sintajimu (syntagm).
Sentensi
Kwa hivyo, sentensi ni zao la uteuzi, na uteuzi katika mahusiano hayo mawili hufanyika
sambamba.
Dhana hizi mbili husaidia katika kuchanganua nomino, vitenzi, n.k. ili tupate kwa
mfano, nomino hisivu na nomino ziso hisivu, vitenzi vielekezi na vitenzi visivyoelekeza,
n.k. Uhusiano wa kisilisila huonyesha namna vipashio vinavyopangwa katika uundaji
wa sentensi. Kuna uhusiano wa maneno yanayofuatana, ndiposa siyo kila neno linaweza
kuchukua nafasi yoyote. Uhusiano wima ni ule wa kutofautisha. Kila ishara ni zao la
uteuzi. Unapoteua kutumia ishara fulani katika nafasi fulani, unaleta tofauti za kimaana.
Kwa hivyo, uhusiano wima unadhihirisha maana katika sentensi.
Sinkronia na Daikronia
Sarufi Miundo, kwa mujibu wa Saussure, ilitenga dhana mbili muhimu katika
kuichunguza lugha kwa kurejelea wakati. Dhana hizo ni Sinkronia (Isimu Mamboleo) na
Daikronia (Isimu Historia) (Habwe & Karanja, 2004:145). Sinkronia ni utafiti wa lugha
katika kipindi kimoja maalumu. Katika mtizamo huu, lugha inafafaniliwa wakati
wowote bila kutazama historia yake. Isimu kisinkronia huiuona lugha kama kitu kilicho
kamilika katika kipindi fulani mahsusi. Kwa hivyo, sinkronia huzingatia muundo wa
lugha katika kipindi mahsusi cha wakati.
Kwa upande mwingine, daikronia ni utafiti wa lugha kwa kuzingatia vipindi tofauti
tofauti. Mtizamo huu huiona lugha kama kitu kinachobadilika kila wakati.
29
Kiambajengo Jirani
Neno ‘Juma’ liko jirani na neno ‘mfupi’ kuliko ‘kikapu’. Hivyo neno ‘ameiba’ liko jirani
na ‘kikapu’ kukiko lilivyo na ‘mfupi’. Kwa sababu hii, maneno ‘Juma’ na ‘mfupi’
hujumuika kujenga kiima huku maneno ‘ameiiba’ na ‘kikapu’ ni viambajengo
vinavyojumuika kuunda kiarifa.
Uchanganuzi Kiuambajengo
Fries alieleza aina za maneno kwa kutumia istilahi ya makundi ya maumbo (form classes)
kulingana na mahusiano yake na maneno mengine katika sentensi. Uchanganuzi
kiuambajengo ulitumiwa mwanzo katika mofolojia. Mofu hufuatana kwa namna au
ruwaza maalumu katika uundaji wa maneno. Ruwaza hizo huitwa muundo ambajengo.
Kwa mfano:
a – li – kamat – w - a
Neno lenye umbo tata linaweza kugawanywa katika viambajengo vifuasi (immediate
constituents) yaani linaweza kugawika katika viambajengo viwili hadi kufikia mofu au
viambajengo ambavyo haviwezi kugawanywa tena. Hivi vinaitwa viambajengo tamati.
Kwa mfano, neno:
30
tungo. Wanamiundo hawakutolea viambajengo majina, bali waligawa tu sentensi bila
kutoa sababu au kueleza.
Uhusiano wa Karibu
Sentensi siyo mfululizo wa maneno. Inaelezwa kama viwango vya viambajengo. Hivyo
basi, upo uwezekano wa kuigawa sentensi hadi vipashio vya chini zaidi. Kwa
wazungumzaji asilia wa lugha fulani, ni dhahiri kuwa, maneno fulani ya lugha
yanauhusiano wa karibu kuliko yalivyo na mengine katika sentensi. Kwa mujibu wa
wanamiundo, sentensi imegawika kulingana na dhana hii ya uhusiano wa karibu. Kwa
mfano,
Dhana ya wingi katika sentensi ina uhusiano wa karibu na nomino paka kuliko ilivyo na
viambajengo vingine. Dhana ya wakati, -li- inahusiana sana na kitenzi. Katika tungo za
Kiswahili, ni dhahiri kuwa wingi au uchache unahusiana na nomino, ilhali, hali na
wakati unahusiana na kitenzi. Kwa mfano:
Juma anaenda.
Juma anaenda sokoni.
Juma anaenda sokoni kununua matunda.
Juma anaenda sokoni kununua matunda aliyotumwa na shangazi.
Je, walijua watakatia wapi sentensi kwa kuangalia ruwaza kama hii? Hata hivyo,
ijapokuwa vipashio hivi havikupewa majina, hadhi ya vipashio ilionekana kuchukua
hatua hizi:
31
Tathmini ya Nadhari ya Sarufi Miundo
b) Mtindo huu huonyesha hadhi ya viambajengi hadi kufikia kile cha hadhi ya chini
kabisa.
c) Kwa kiasi, mbinu hii ilikumbana na tatizo la utata wa kimuundo katika umbo la
sentensi (structural ambiguity). Kwa mfano:
32
g) Walishindwa pia kudhihirisha mahusiano muhimu kati ya sentensi za kimsingi
(basic) na zile zilizozalishwa (derived). Tazama uhusiano uliopo baina ya ile
inayoonyesha kauli tendi na ile ya kauli tendwa.
Hitimisho
Maswali ya Marudio
33
SARUFI MIUNDO VIRAI
Utangulizi
(a + b+ c+ d+... n)
(A B) + (C D)… n
Sarufi Miundo Virai (SMK) ni njia mbadala ya kuwasilisha sentensi zilizo kwenye
vielelezo tungo kwa njia ya kutumia ‘kanuni za kuandika upya.’ Katika mfumo huu,
mwanaisimu huifafanua sarufi kwa kutumia kanuni zalishi ambazo huunda muundo
sahihi wa sentensi.
Sarufi ya aina hii, mbali na kuonyesha viambajengo tamati vya sentensi kiusilisila, pia
huonyesha visehemu vidogo vidogo na viwango vya uhusiano wa vipashio. Katika
nadharia hii, mwanaismu hujishughulisha na masuala yafuatayo:
34
9 Vipashio vya kisintaksia vinavyoziunga sentensi pamoja na njia ambazo vipashio au
sehemu tofauti za sentensi huhusiana.
Kwa mujibu wa nadharia hii, Kanuni Muundo Kirai ni nyingi na zisizo na ukomo. Hii
ina maana kwamba ni vigumu mno kwa mtu kuweza kutunga kanuni muundo virai kwa
siku za maisha yake. Hata hivyo, kauli hii inadhihirisha upungufu. Mtoto anapofikia
umri wa miaka 3 au 4, huwa ameishajifunza lugha. Hali hii inatupelekea kuamini
kwamba kanuni hizi si nyingi bali zina ukomo. Kanuni muundo virai za sarufi zalishi ni
kusanyiko la uhusiano wa kiima - kiarifu na uchanganuzi wa kimapokeo wa
viambajengo vifuasi wa wanamiundo. Kanuni hizi zinafafanua uhusiano wa kimsingi
unaohusika katika umbo la ndani. Aidha, zinabainisha ni kipashio kipi kinachokitawala
kingine.
Mchoro matawi kama kielelezo cha muundo kirai wa sentensi huitwa kielelezo tungo
(phrase marker). Lengo lake ni kudhihirisha viambajengo vifuasi vilivyoiunda sentensi.
Mahali ambapo matawi mawili hukutana huitwa kifundo (node). Isipokuwa katika vistari
vya mwisho (tamati), kila kifundo huwakilisha kiambajengo ambacho kinasimamiwa na
alama kama vile: KN, KT, KH, KV n.k. na ambacho kinamiliki au kukiongoza hicho
kinachotokea chini yake.
S kifundo
KN KT kifundo
N V T E
n) Humiliki vipashio KN na KT
KN Kinamiliki vipashio N na V
KT Kinamiliki vipashio T na E
35
Baba yake ameingia ndani ya nyumba yao.
KN KT
N V T KH
H KN
N V
Vielelezo tungo vya miundo virai vinatupa maelezo kuhusu muundo wa sentensi. Hata
hivyo, havina uwezo wa kueleza ni kwa njia gani tunaweza kuzalisha sentenzi mpya.
Hili linawezekana tu kupitia Kanuni Miundo Virai.
Kanuni Miundo Virai ni kanuni zinazowezesha kuandikwa upya kwa sehemu zote za
sentensi hadi kufikia kiwango tamati cha mofimu. Kwa mfano katika:
S KN+KT
KN N
N Juma
KT T+E
T aliwasili
E jana
36
Kanuni muundo kirai huwa na ishara moja kwa upande wa kushoto na ishara moja au
zaidi kwa upande wa kulia, unaoonyeshwa na mshale.
X YZ
Kanuni hizi hufasiriwa kama maelezo ya jinsi ya kupanua au kuandika upya ishara iliyo
katika upande wa kulia wa mshale. Kwa mfano,
d KN+KT
f) Kanuni Miundo Virai zina uwezo wa kuzalisha sentensi zote za kisarufi za lugha
inayohusika.
a – na – som – a ki – tabu
Ili kuweza kutumia Kanuni Miundo Virai ipasavyo, mwanasarufi hana budi kuwa na
ufahamu wa upeo wa juu wa kategoria za kileksika za lugha inayohusika. Kiswahili
hutumia alama zifuatazo ili kutambua kategoria mbalimbali.
37
Mifano ya Kanuni Miundo Virai na Matumizi yake
1. S Ø+KT Njoo
2. S KN+KT Baba analala
3. KN N +V Mbwa mwitu
4. KN N+V+V Mwalimu wetu mzuri
5. KT t + KV (Mtoto huyu) ni mziri
6. KT T+KE anaimba vizuri
7. KT T+KN alimpiga mtoto
8. KT T+KH+KN alilala juu ya kitanda
9. KT Ts + T + KN alikuwa akisoma kitabu
10. KT T+KN+N+V alimpa mwanawe adhabu kali
Rukia analima.
Analima Rukia.
Kwa kutumia nadharia hii, inatubidi tutumie kanuni tofauti kuzifafanua licha ya
kuwa zina maana moja. Uchanganuzi wa miundo virai hauonyeshi kwamba tungo
hizi zina uhusiano wowote. Zinastahili kuchanganuliwa kama tungo mbili tofauti
ilhali tungo ya pili ni muundo mbadala wa ile ya kwanza.
h) Uchanganuzi huu wa sarufi hauonyeshi ni kwa nini karibu katika lugha zote duniani
KN hujitokeza katika nafasi sawa hivi kwamba sentensi inafafanuliwa kama:
S KN + KT na wala siyo S KT + KN
38
Hitimisho
Sarufi Miundo Virai ililenga kufafanua makundi ya kisarufi kwa kuonyesha uhusiano
kati yake. Hata hivyo, nadharia hii ilishindwa kuonyesha uhusiano uliopo kati ya
sentensi mbili tofauti katika umbo la nje lakini zilizo na umbo sawa la ndani, kwa kuwa
na maana sawa. Kwa mfano katika sentensi:
Kwa mujibu wa Sarufi Miundo Virai, sentensi hizi zingechanganuliwa kila moja
ikijisimamia kwa upekee wake. Matatizo kama haya ndiyo yaliyopelekea kuasisiwa kwa
nadharia ya Sarufi Geuzamaumbo Zalishi na Chomsky mnamo mwaka wa 1957.
39
SARUFI ZALISHI
Utangulizi
Chomsky alieleza upya umuhimu wa kazi ya sarufi na pia umbo na muundo mpya
ambao sarufi ingechukua. Alipendekeza kwamba sarufi iangaliwe kama nadharia
inayoeleza jinsi lugha inavyotumika. Sarufi hiyo mpya lazima iwe chombo cha kuunda
na kuzalisha miundo ya kisarufi ya lugha inayohusika na pia ile miundo isiyo ya
kisarufi. Alipendekeza kuwa jukumu la wanaisimu liwe ni kuunda sarufi kama hii na
kuibua njia ambazo zingetumiwa kupima na kuitathmini sarufi hii. Kabla ya sarufi hii,
wanaisimu walikuwa wakikusanya data kutoka kwa wahojiwa na baadaye kubuni sarufi
ya kisayansi iliyoandikwa kwa kutalii miundo yake bila kuzingatia maana yake. Kufikia
kipindi cha sasa, aina nyingi za Sarufi Zalishi zimefafanuliwa na kuendelezwa. Sarufi
hizo ni pamoja na:
40
e Sarufi hii hueleza sentensi ambazo ni sahihi na zile ambazo si sahihi katika lugha
inayohusika. Aidha, hueleza sentensi ambazo zina mantiki na usarufi. Sentensi hizi
hujieleza kwa uwazi kupitia sheria hivi kwamba msomaji wa sarufi hii hapaswi
kutumia makisio na ujuzi wowote kujaribu kubaini yanayoelezwa na sarufi hii.
S KN+KT
i) Kwa mujibu wa Chomsky Sarufi Zalishi inaweza kutabiri. Hailezi tu tungo ambazo
tayari zimetungwa. Inaweza kubuni kwa kutabiri tungo zote zinazowezekana
kutolewa katika lugha inayohusika, au pengine sentensi ambazo hazijawahi
kutolewa kamwe.
Umilisi
Kupitia kwa uwezo, mzungumzaji asilia wa lugha anaweza kudondoa sentensi zilizo
sahihi na zile zisizo za kisarufi. Pia, anaweza kutoa sentensi zinazowezekana kutolewa
katika lugha yake. Aidha, anaweza kutambua zile ambazo haziwezekani kutolewa, au
anaweza kutambua sentensi ambazo hajawahi kuzisikia hapo awali. Isitoshe, anaweza
kuzalisha sentensi zisizo na kipimo. Anaweza kutambua maumbo na miundo tofauti ya
tungo moja. Kwa mfano:
s) Analima Juma.
t) Juma analima.
41
Hii ni miundo tofauti ya tungo moja kwani maana ni moja, “Juma analima”. Pia mzawa
wa lugha ataweza kutambua utata wa kimuundo au wa kimaana katika sentensi.
Utendaji
i) Kwa nini sentensi mbili zinazotofautiana kijujuu (katika muundo) huwa na uhusiano
wa ndani (kimaana), kama vile katika:
Umbo Ndani
Umbo ndani huwakilisha maana ya sentensi. Umbo ndani hudhirika katika umbo nje
kupitia kwa kanuni za ugeuzaji. Katika Sarufi Zalishi kuna uwezekano wa kubadili
viambajengo kutoka nafasi moja hadi nyingine. Kwa mfano:
42
Tazama uhusiano uliopo kati ya kauli tendi (active) na kauli tendwa (passive) katika
tungo. Tungo katika kauli tendi huchukuliwa kuwa ya kimsingi ilihali ya kauli tendwa
imezalishwa na hiyo kauli tendi. Tazama mifano ifuatayo:
Umbo Nje
Umbo Nje (Surface Structure) muundo wa sentensi unaodhihirika kihalisia kupitia kwa
sauti zinazotamkwa. Umbo Nje linadhihirika tunaposema, tunapoandika au tunaposikia.
Ni umbo ambalo tayari limepitia ugeuzaji. Ni hali ya mwisho ya tungo baada ya ugeuzi
kufanywa.
Umbo Ndani
Kanuni za Ugeuzaji
Umbo Nje
Umbo nje haliwezi kufanyiwa ugeuzaji. Dhana za umbo nje na la ndani husaidia kutatua
matatizo ya utata katika sentensi. Pia hutumiwa kuhusisha sentensi mbili ambazo
pengine zingechanganuliwa kama sentensi tofauti kabisa. Uchambuaji wa Ugeuzaji
(Transformation Analysis) hujikita kwenye wazo kwamba baadhi ya tungo katika lugha ni
za msingi (Basic Sentences) ilhali zingine zote huzalishwa kutokana na hizo za kimsingi
kwa kuptia kanuni za ugeuzi.
43
Sheria ya ugeuzaji inaweza kutumiwa kuzalisha sentensi hii. Tazama mfano ufuatao:
Tanbihi: Hatuongei tukitumia umbo ndani bali umbo la nje. Zingatia mfano ufuatao:
Mitihani ilifanywa.
Ugeuzaji
Umbo ndani -> [wingi + mitihani + kiw + wkt +mzizi + kauli + kiishio]
{i} {li} {fany} {w} {a}
Hata hivyo, umbo ndani ndilo hutupa maana kamili ya tungo. Katika muundo wa ndani,
viambajengo havijabadilishwa, kudondoshwa wala kuongezwa. Umbo la nje huonyesha
tu mpangilio wa vipashio na vipengele mbalimbali vya kusintaksia kupitia sauti za lugha
zinazotuwezesha kuwasiliana kwa ujumla.
44