You are on page 1of 11

MPANGO WA LUGHA

Kupanga ni tendo la binadamu linalotokana na hali ya kupata suluhisho kwa


shida fulani. Tendo hili linaweza kuwa (limepangwa na) la makusudi au liwe
limetokea tu bila mpango kamili. Linaweza kutekelezwa na watu binafsi au
linaweza kuwa rasmi.
 
Buliba .A na wengine na Kimani Njogu na Mwihaki .A (2006), wanasema
upangaji lugha unamaanisha harakati zenye utaratibu zinazonuia utatuzi wa
matatizo ya lugha katika kiwango cha taifa.

Iribemwangi P.Lna Mukhwana A. (2011) Wakimnukuu Das Gupta na Jernudd


wanasema kuwa upangaji lugha ni shughuli ya kisiasa na kiutawala ambayo
hutatua matatizo ya lugha.

Mathooko P.M (2007) akimnukuu Haugen (1966) anasema kuwa upangaji


lugha ni tathmini ya mabadiliko ya lugha. Ni shughuli ya kutayarisha tahajia,
sarufi na kamusi sanifu, kuwaongoza wazungumzaji katika jamii lugha anuai
(yenye lugha tofauti tofauti).

Rubin na Jernudd (1971) wanaonelea kuwa ni juhudi za kimakusudi za kuleta


mabadiliko katika lugha ya maandishi au ya mazungumzo au zote mbili
zinazochukuliwa na taasisi zilizoundwa kutekeleza jambo hili. Upangaji lugha
hunuia kumaliza matatizo ya lugha kwa kuchukua uamuzi ulio bora zaidi.

Rubin (1971) anasema kuwa upangaji lugha unamaanisha maendeleo,


utekelezaji na utathmini wa mbinu maalum za kutatua matatizo mahsusi ya
lugha.

Weinstein(1990) anaelezea upangaji lugha kama shughuli inayoamrishwa na


serikali ili kuleta mabadiliko katika lugha na kutatua matatizo ya
kimawasiliano.
1
Cooper (1980), anashikilia kwamba sio lazima serikali ihusishwe; kulingana
naye upangaji lugha ni juhudi za kimakusudi za kuathiri tabia ya wengine
kuhusu kujifunza, miundo na majukumu ya lugha.

Kulingana na fafanuzi hizi basi upangaji lugha ni shughuli inayonuia kutatua


matatizo yanayotokana na lugha ili kuleta mabadiliko katika matumizi ya
lugha fulani yawe mabadiliko ya kijukumu na kimtindo.

Majukumu ya kupanga
Moshe Nahir (1977) anapendekeza kwamba upangaji wa lugha una majukumu
matano bainifu.
(i) Uchujaji na utakaso wa lugha (Language purification). Kueleza matumizi
sahihi na kuhifadhi usafi wa lugha. (Korean language (1949) Maneno
mkopo ‘hanja’ Korea waliondoa maneno ya kijapani na kuyafanya
Kiswahili sanifu.)
(ii) Ufufuaji lugha, hasa lugha ya kale na kuweka katika hadhi yake ya
zamani. Uhaishaji wa lugha iliyokufa. (Hebrew language 1980-1914).
(iii) Ugeuzaji na urekebishaji lugha (Language reform) kuwezesha
matumizi ya lugha kupitia usahihishaji au urahisishaji wa msamiati na
tahajia yake.
(iv) Usanifishaji kuwa lugha (Standardisation). Kuhakikisha kuwa lugha
moja au lahaja moja katika eneo au taifa fulani inakubaliwa kama lugha
kuu.
(v) Uingizaji usasa au upya wa msamiati (Lexicomodernisation). Kujaza
pengo kati ya msamiati wa lugha na istilahi mpya zinazotokana na
teknolojia ya kisasa.

Mawanda/Aina za Upangaji Lugha

2
(a) Upangaji Lugha Kifahari (Prestige Planning). Upangaji lugha kifahari
hulenga katika kutoa mielekeo chanya ya kisaikolojia ambayo ni
muhimu ikiwa kutakuwepo na ufanisi wa muda mrefu katika upangaji
lugha; mfano mzuri ni fahari kuu ambayo Kiebrania kilikuwa nayo kama
lugha ya kidini ilisababisha kutokuwepo na haja ya kuwa na upangaji
kifahari. Upangaji kifahari huwa muhimu pale ambapo lugha ambayo
imeteuliwa ilikuwa ya hadhi ya chini (kama ilivyo katika diglosia). Ili
watu wakubali hadhi ya lugha hiyo iliyotwazwa, kuna haja ya kuboresha
na kuendeleza ufahari wa lugha hiyo. Hivyo basi, upangaji kifahari
aghalabu hutangulia upangaji kihadhi.
(b) Upangaji Lugha Kiurithi (Acquisition Planning). Hizi ni juhudi za
kusambaza ujifunzaji wa lugha. Hapa tunaona taasisi za kitamaduni
zinazosambaza na kuendeleza lugha mbalimbali. Kwa mfano, Britishi
Council, French Cultural Center, Japanese Cultural Center na
kadhalika. Taasisi hizi hutoa mafunzo ya mara kwa mara kwa walimu
wanaofundisha lugha hizi.
(c) Upangaji Lugha Kihadhi (Status Planning). Upangaji huu hurejelea utoaji
wa dhima kwa lugha (kama vile kutumia lugha hiyo kufunzia shuleni au
kama lugha rasmi). Jambo hili huathiri dhima ya lugha katika jamii.
Kwa mfano, uamuzi wa kutumia Kiebrania kama lugha ya mafunzo
katika shule za Wayahudi kule Palestine. Kabla ya hapo, Kiebrania
hakikuwa kikitumiwa katika mawasiliano ya kila siku ila katika maombi
na maandishi ya kidini na kiusomi. Hadhi ya Kiswahili nchini Kenya
imeinuliwa kwa njia hiyo, matumizi ya Kiingereza nchini Rwanda,
Kiswahili nchini Tanzania na Uganda.
(d) Upangaji Lugha Kiukongoo (Corpus Planning). Kongoo ni kusanyiko la
data za semi zilizoandikwa au kunukuliwa ambazo hutumiwa kama
kianzio cha ufafanuzi wa kiisimu. Upangaji lugha kiukongoo unahusika
na muundo wa ndani wa lugha. Mambo yanayozingatiwa ni pamoja na
kuunda othografia kwa lugha ambazo bado hazijaandikwa, kuanzisha

3
mabadiliko katika tahajia, kubuni maneno mapya na kuchapisha vitabu
vya sarufi. Jambo la kimsingi katika aina hii ya upangaji lugha ni
usanifishaji wa lugha. Huu hueleweka kuwa ni uanzishaji na uendelezaji
wa kaida za kiisimu.
Majukumu ya Lugha katika Jamii
(i) Lugha rasmi hutumiwa katika miktadha ya kitaifa na inaunganisha
watu kisiasa na kitamaduni. Aghalabu hadhi hii huwa imetangazwa
kwenye katiba.
(ii) Mawasiliano mapana; matumizi ya lugha kama chombo cha
mawasiliano kinachovuka mipaka ya lugha mbalimbali katika nchi
moja. Hii ni kama lingua franka; kwa mfano Kiswahili nchini
Tanzania, Kihindi, Kiingereza n.k.
(iii) Mawasiliano ya kimataifa (Lugha ya Kimataifa); kwa mfano
Kiingereza, Kifaransa, Kiswahili, Kiarabu, n.k.
(iv) Kuendeleza elimu; katika shule na taasisi za elimu.
(v) Dini
(vi) Vyombo vya habari
(vii) Kazini
(viii) Fasihi
Mchakato wa Upangaji Lugha
Haugen (1966, 1972, 1987) alisema kuwa mchakato wa upangaji lugha unazo
hatua nne ambazo zinaweza (ingawa si lazima) kufuatana;
1. Uteuzi (Selection)
2. Ukuzaji msimbo (Codification)
3. Utekelezaji (Implementation)
4. Upanuzi (Elaboration)
Uteuzi
Upangaji lugha huanza kukiwepo na uwezekano wa kuchagua moja kati ya
vibadala vingi vya kiisimu. Uteuzi huu utatokea baada ya watu kutambua
kwamba kuna shida fulani ya kiisimu. Basi lahaja au lugha moja kati ya zile

4
zinazotumika katika jamii husika huchaguliwa kuwa msingi wa usanifishaji.
Uteuzi ni ule uchaguzi wa lugha au lahaja ili ipewe dhima fulani katika jamii;
kwa mfano iwe rasmi, ya kufunzia, ya dini, n.k. Hii ina maana kwamba lugha
au lahaja ya fahari zaidi ndiyo inayochaguliwa. Uchaguzi unazingatia
umuhimu wa lahaja hiyo kijamii, kisiasa, kibiashara, kielimu, n.k.

Uteuzi huu unaweza kutanguliwa na mijadala mikali kati ya watu hadi pale
wanapokubaliana, au wanaweza kuamuliwa na viongozi K.mf uteuzi wa hijai
ya Kituruki kutoka kwa Kiarabu hadi Kiroma. Uteuzi huu hutekelezwa na jamii
kupitia kwa viongozi wao na wanaohusika katika uteuzi huu si taasisi za
serikali bali ni watu binafsi, vikundi kama makanisa, vyama vya kisiasa, mikoa
na nchi yote.

Lahaja au lugha fulani inapochaguliwa, inapendelea watu wanaoizungumza


kwa inawapa fahari na hawapotezi muda kujifunza. Uteuzi mbaya unaweza
kusababisha mgawanyiko katika nchi.

Wakati mwingine wapangaji lugha huunganisha lahaja mbalimbali k.mf,


usanifishaji wa Basque, lugha inayozungumzwa kusini magharibi mwa
Ufaransa na kaskazini magharibi mwa Uhispania. Basque sanifu iliundwa
miaka ya 1960 kwa kuweka pamoja lahaja zake zote nne.

Ukuzaji Msimbo
Sehemu hii hutekelezwa na wanaisimu au wataalamu wa lugha. Lahaja
iliyoteuliwa huwekewa kanuni au utaratibu za matumizi. Huku ni kukuza
mfumo wa lugha hiyo k.v fonolojia (othografia na matamshi), sarufi, msamiati
na maana.
Ukuzaji msimbo ni uundaji wa kiwangogezi (norm or standard) cha kiisimu
kwa msimbo fulani wa kiisimu. Shughuli hii hufanywa kupitia kwa hatua
zifuatazo;

5
(a) Kukuza mfumo wa maandishi (graphisation)
(b) Usarufishaji (grammatication)
(c) Uleksikishaji (lexicalilsation)
Kukuza mfumo wa maandishi. Ikiwa lugha husika ilikkua ya mikazungumzo
tu, basi inatayarishiwa mfumo wa maandishi. Wakati mwingine
kinachofanyika ni kwamba wataalamu wanakopa mfumo wa kimaandishi wa
lugha nyingine. Wataalamu wanamua mfumo wa maandishi utakaoifaa lugha
hiyo. Ni ule wenye msingi wa sauti (vokali na konsonanti), silabi au maneno?
Kwa mfano lugha ya Kiswahili kwanza iliandikwa kwa herufi za Kiarabu kabla
ya kutumia zile za Kirumi.
Usarufishaji. Hii ni sehemu nyingine ya mchakato wa upangaji lugha. Inahusu
kuunda kanuni za kisarufi. Wanaamua maumbo na miundo ambayo itakuwa
sanifu. Hali hii hupunguza vibadala au tofauti katika matumizi ya kisarufi.
Vitabu vya sarufi hutayarishwa.
Uleksikishaji. Hurejelea uchaguzi na utayarishaji wa msamiati unaofaa.
Kimsingi, hatua hii inahusu kuamua maneno fulani yatumiwe katika mitindo
ipi. Mara nyingi, uleksikishaji hushughulikia uondoaji wa maneno yenye asili
ya kigeni kutoka kwa lugha. Kamuzi za lugha hiyo hutayarishwa kama
ilivyokuwa wakati Kihindi kiliposanifishwa kwa kutumia maneno ya mkopo
kutoka Kiajemi, Kiingereza, n.k.

Utekelezaji
Utekelezaji unahusisha shughuli za waandishi, taasisi, na serikali katika
kuitumia na kuisambaza lugha ambayo imeteuliwa na kukuziwa msimbo. Hili
linafanyika kwa kutoa au kuchapisha vitabu, majarida, magazeti, na makala
katika lugha hiyo iliyokuziwa msimbo. Wenye mamlaka huhakikisha kwamba
lugha hii inatumiwa pia kwenye vyombo vya habari kama redio, televisheni na
magazeti.
Huku wanaisimu wakihusika sana na sehemu ya ukuzaji msimbo, sehemu hii
ya utekelezaji hushughulikiwa na dola/taifa. Inabidi kuwepo na mbinu za

6
kibiashara za kusambaza lugha hii. Waaandishi wanachapisha vitabu kwa
lahaja hii sanifu wanatuzwa, wafanyakazi serikalini wanaoifahamu lahaja hii
sanifu wanapandishwa vyeo kazini, na lugha au lahaja hii inatangazwa sana.
Wakati mwingine kunawekwa sharia ambazo zinahimiza matumizi yake.

Lugha hii inahitaji kupata ukubalifu katika jamii. Ikiwa itakubalika,


itawaunganisha watu wanaozungumza lugha tofauti. Kuhusu Kiswahili,
kamati ya lugha (Kiswahili) ya Afrika Mashariki iliandaa mashindano ya
kuandika insha na vitabu katika Kiswahili sanifu na washindi walituzwa.
Kunakuweko pia na tume mbalimbali za elimu ambazo zinapendekeza sera
mbalimbali za lugha k.mf, Ssenteza Kajubi Education Report (1987)
iliyopendekeza kufundishwa kwa lugha ya Kiswahili kama somo la lazima
kuanzia ngazi ya shule za msingi nchini Uganda, Mackey (1981) iliyopendekeza
kuanzishwa kwa mfumo wa 8-4-4 nchini Kenya na katika mfumo huo wa
elimu, Kiswahili ni somo la lazima katika shule za msingi na sekondari na
linatahiniwa.

Upanuzi
Hii inarejelea ukuzaji wa istilahi na mitindo ili lugha iliyokuziwa msimbo
itemize mahitaji ya kisasa ya mawasiliano katika ulimwengu unaoendelea
kisayansi na kiteknolojia. Huku ni kuendelea tu na utekelezaji wa kiwangogezi
ili kutimiza dhima za lugha katika ulimwengu wa kisasa. Sehemu hii ya
upanuzi lugha ni hiyo ya kuunda na kusambaza istilahi mpya, na kuhakikisha
kuwa kuna mbinu mbalimbali za kuundia msamiati; hali hii inaweza
kukamilika kwa kukopa kutoka lugha zingine, kupanua maana ya istilahi, na
kubuni maneno mapya.

Upanuzi wa lugha huendelea kila wakati. Hii ni kwa sababu lugha inahitaji
kujengwa upya kila siku kwani kuna dhana na vyombo vipya vinavyojitokeza

7
kila siku. Kuna haja ya kuwa na taasisi za kushughulikia upanuzi wa
msamiati.

Kwa mujibu wa Haugen (1987), ukuzaji msimbo na upanuzi ni sehemu ya


upangaji lugha kihadhi (pia kifahari na kiurithi). Kielelezo hiki cha upangaji
lugha cha Haugen ni cha kiduara kwani upangaji lugha kihadhi unaweza
kutokana na upangaji lugha kiukongoo. Upangaji kiukongoo ukifaulu au la,
utaathiri upangaji lugha kihadhi.

Lingua Franka
Lugha hii hutumiwa na watu walio na lugha tofauti kwa ajili ya mawasiliano.
Mfano mzuri ni Kiswahili ambayo ni lingua franka katika eneo la Afrika
Mashariki.
Sababu za kuzuka kwa Lingua Franka
Zipo sababu tofauti tofauti, ambapo kwa mujibu wa Iribemwangi (2011),
ametoa sababu zifuatazo:
Lingua Franka huibuka kwa sababu ya Hali ya kutaka ushirikiano.
Ushirikiano unaotafutwa kupitia Lingua Franka ni ule wa kisiasa, kibiashara,
kiutamaduni na kielimu. Mfano Tukirejelea Kiswahili, lugha hii imetumika
katika kujenga, kuendeleza na hata kudumisha uchumi, biashara na umoja
miongoni mwa watu wa Afrika Mashariki.
Aidha Lingua franka huzuka kutokanana kuleta umoja miongoni mwa
watumiaji wake. Hii humaanisha kuwa miongoni mwa watu walio na
utamaduni mbalimbali, lingua franka ndiyo inayotumika kuwaleta pamoja.

Jinsi Lingua Franka inavyoenea

Iribemwangi (2011), anaeleza jinsi Lingua Franka inavyoweza kuenea kupitia


mambo mbalimbali, baadhi ya mambo hayo ni kama yafuatayo;

8
Vita, mfano kupitia vita lugha ya Kigiriki iliweza kuenezwa. Pia Kifaransa
kiliweza kuenea hasa enzi ya utawala wa Napoleon Bornaparte. Pia katika
lugha ya Kiyunani iliweza kuenea kupitia vita, ambapo tawala zilizoshindwa
zililazimika kutimia lugha ya mtawala wao mpya. Hivyo basi kupitia vita lingua
franka iliweza kuenea maeneo mbalimbali.

Biashara, kupitia njia hii lingua franka huwezwa kuenezwa . Mfano Lugha ya
Kiswahili na Kihausa zimeweza kuenea kutokana na dhima zao za Kibiashara.
Hivyo sio ajabu kupata watafiti kadhaa wakiziita Lingua franka kwa lugha za
biashara.

Shughuli za Kikoloni, Lugha za Kifaransa, Kiingereza na Kireno zimeweza


kuenea kupitia kwa nyenzo hii ya ukoloni.
Shughuli za Kisiasa, lugha ya Luganda nchini Uganda imeweza kuenea
kutokana na nguvu kisiasa za watu wa Buganda.

Elimu, kama lugha ya kiingereza imeweza kuenea kupitia elimu.Hali hii


inawezekana katika maeneo ambapo lugha fulani hutumika katika kutolea
mafunzo.

Nguvu ya sayansi na teknolojia, kwa Marekani na Uingereza shughuli za


Sayansi na teknolojia zimechangia kuenea kwa lugha ya Kiingereza kote
ulimwenguni hasa istilahi mpya zinazoibuka kila uchao.

Sifa za Lingua Franka ni kama zifuatazo:

1. Hukiuka mipaka ya kitamaduni.


2.  Hukutanisha watu wa asili mbalimbali.
3. Hukiuka mipaka ya kimaeneo kwa kuwa hutumika katika eneo pana
zaidi.

9
4. Hutumiwa na watu ambao lugha mame zao ni tofauti.
5. Ni lugha ya mawasiliano kati ya watu wenye lugha zaidi ya moja.
6. Yaweza  kuwa lugha ya kwanza au ya pili ya mzungumzaji na kwa
wengine lugha ya kigeni.

Lugha ya Taifa

Hii ni lugha ya asili ya kikabila inayozungumzwa katika nchi fulani mathalan


baadhi ya lugha zinazozungumzwa nchini Kenya ni kama vile: Kikikuyu,
Kiluhya, Kikamba nchini Kenya.

Nchini Tanzania kuna lugha kama vile: Kihaya, Kisukuma, Kibondei.

Pijini (Pidgin)

Massamba na Wenzake (2009),wanafasili Pijini wakimnukuu Decamp (1971)


na Hall (1972), wanasema kuwa ni lugha yenye mfumo uliorahisishwa sana
ambao hutumiwa na wazungumzaji wenye lugha tofauti katika mazingira
maalum baina yao na kwamba pijini siyo lugha mama kwa mzungumzaji
yeyote. Aidha kuhusu mazingira ndiyo kichocheo cha kuzuka kwa lugha za
Pijini.

Wanaisimu- jamii wengi wanakubaliana kuwa Pijini ni lugha iliyozuka katika


miktadha ya kibiashara na biashara ya Utumwa. Kama asemavyo
Kwa ujumla Pijini ni lugha ambayo huzuka pale ambapo makundi mawili ya
watu wenye lugha mbalimbali yanapokutana na haja ya mazungumzo kutokea.
Mara nyingi ni lugha za kibiashara hasa.

10
Hii ni lugha inayobuniwa na kutumiwa kwa mawasiliano baina ya watu ambao
lugha zao ni tofauti na hawana lugha moja wanayoielewa kwa pamoja.

Sifa za pijini ni kama zifuatazo:

1. Haina wazungumzaji wazawa.


2. Huzuka baina ya lugha tofauti kabisa kitamaduni.
3. Huwa na miundo hafifu ya kisarufi.
4. Ina msamiati finyu sana.
5. Huwa lugha ya hadhi ya chini inayopigwa vita ili ife.
6. Msamiati mwingi wa pijini hutegemea sana mojawapo katika lugha
zinazo wakutanisha watu.
7. Huwa na fonimu chache.
8. Hutumia ishara kwa wingi kwa sababu ya uhaba wa msamiati.

Marejeo

Chimera, R. (2000) Kiswahili: Past, Present and Future Horizons. Nairobi.


Nairobi University Press.

Haugen, E.(1956) Bilingualism in the Americans. University of Alabama Press.

Kingie, G. (2001) Matatizo ya matumizi ya lugha katika vyombo vya habari:


Mifano kutoka Kenya, katika Swahili Forum VII German. University of Koln
Uk. 45-56.

Mbaabu, I. (1996) Language Policy in East Africa, Educational Research and


Publication; Nairobi.

11

You might also like