Professional Documents
Culture Documents
Kwa ujumla kuna sababu mbali mbali zilizonipelekea kukuiandika makala hii
inayozungumzia shindiukizo la damu (presha). Baadhi ya sababu hizo ni;
Afya yako ndio jambo lenye thamani kubwa kuliko kitu chengine chochote kwani
hakuna maana yeyote ikiwa afya yako ni mbaya (Afya ni kitu muhimu na chenye
thamani kubwa kwa maisha ya mwanadamu). Katika maendeleo ya maisha
mwanadamu, afya ni kitu cha kwanza. Mwanadamu hutoweza kuishi kwa raha ki
familia ikiwa atakuwa anasumbuliwa na maradhi na kuhangaika kutafuta
matibabu.
Pamoja na kuwa uandishi sio fani yangu, lakini kwa kuzingatia kuwa shinikizo la
damu ni janga linalowakabili watu wengi, nimeona ni muhimu kwangu nitoe
mchango wangu ili uwe ni changa moto kwa watu nao waweze kutanabahi juu ya
haja ya kusaidia katika kuelimisha jamii. Pia pamoja na kuwa mimi sio mtaalamu
wa elimu ya afya lakini ni mmoja kati ya wale ambao tayari wanaogelea katika
shinikizo la damu, ni matarajio yangu kuwa makala haya yataamsha ari na kusaidia
japo kidogo katika katika kutoa miongozo kwa wale wenye matatizo ya sindikizo la
damu. Hapa nitazungumzia Presha ya juu, nategemea pia kuizungumzia Presha ya
chini siku zijazo.
Baadhi ya watu wanafikiri wao lazima wapate maradhi fulani. Wapo kwenye
mawazo hayo kwa sababu kwenye koo zao kuna maradhi kama hayo. Kupata au
kutopata maradhi ni suala la wakati, kama bado haujafika utakuawa salama na
utakapofika hutakuwa na namna ya kuyakimbia. Sote tunafahamu suala la urithi
ambalo chembechembe zetu za uhai hurithi kutoka kwa wazee wetu. Urithi huu
huwa na mchango mkubwa katika tabia, maumbile, nguvu na afya. Ukweli kuhusu
afya zetu ni kuwa, kwa kiwango kukubwa kabisa matatizo ya kiafya yanayotupata
huwa ni mchango wetu wenyewe katika miili yetu ambao hutoa ruhusa kwa huo
urithi kufanya kazi.
Utangulizi
Kwa kuwa napenda kufanya mazoezi, napenda pia afya yangu iwe nzima kwani
nikiwa na afya mbaya sitaweza kufanya au kufurahia mazoezi. Ni vizuri kuishi
maisha yaliyo huru badala ya kuishi maisha ya kifungo cha dawa na masharti ya
madaktari. Hapa nakusudia kuelezea hali ile ya mtu kulazimika kuwa na ratiba ya
kumeza dawa mara tatu, mbili au moja kila siku ili afanye shughuli zake za maisha.
Vijana wanasema mtu kama huyo haendi bila ya chaji, inabidi utie chaji ndipo
aende. Kila mara inakulazimu kuwa na dawa mfukoni, “ unatembea na betri” na
nyumbani umejaza dawa (umefungua Pharmacy). Dawa anayoitaka mtu basi
anaweza kuipata kwako. Hufika wakati ikabidi daktari akakushauri/akakupangia, “
Usile hichi, punguza hichi, kunywa maji mengi kula matunda kwa wingi ”.n k.
Ikishafika hali hii ya kuishi kwa miiko, raha ya maisha inakuwa haipo tena.
Umri wangu ni miaka 40. Nina urefu wa futi 5 inch 8 (174 cm) na uzito wa kilo 85.
Kwa sababu nilijizoesha kufanya mazoezi, ninapenda kufanya mazoezi kila
nipatapo nafasi. Kama kawaida ya watoto wanavyokuwa, na mimi nilikuwa
nikipenda kucheza mpira, kukimbia, kuruka na mengineyo mengi afanyayo mtoto.
Nilipoanza kusoma sekondari muda wa michezo ukawa haupatikani kikawaida na
idadi ya vijana tuliokuwa pamoja ilipungua. Ilibidi nifanye mazoezi ya peke yangu.
Nikaanza kukimbia joging na kufanya mazoezi ya viungo. Utaratibu huu nilidumu
nao nikiwa high school na hata nilipokwenda chuoni. Siku moja nilikwenda
hospitali kwa matatizo mengine lakini kabla ya matibabu, nesi alinipima presha na
kuniambia ipo juu. Hata hivyo sikushughulika. Nilifanya matibabu ya lile
nililoendea na hakuna jambo lolote lililonitokezea kwenye presha. Kwetu maradhi
ya presha sio mageni, pande zote mbili yapo, na vifo vingi huja kwa sababu ya
maradhi haya.
Miaka mine baadae ( 1998) nilienda kusoma tena. Kutokana na sababu nyingi
sikuwa nikifanya mazoezi. Ndani ya miezi mitatu tu uzito wangu ulipanda na
kufikia kilo 72. Miaka miwili baadae (2000) nilioa, mfumo wa maisha ukabadilika.
Mambo yakawa mengi, muda wa kufanya mazoezi ukapungua na hata wakati kwa
ujumla ukawa hautoshi kwa ule wingi wa mambo.
Miaka tisa baadae nilijikuta nina kilo 84. Nilianza jitihada za kupunguza uzito
wangu. Niliamua kurudia zoezi la baskeli ambapo kila wiki nilifanya mara moja.
Kwa kipindi cha miezi mitatu niliweza kupunguza kilo 3 na kuwa na kilo 81. Wakati
nikiendelea na mazoezi nilipata nafasi ya kwenda kusoma chuoni ( 2009 ). Kama
mjuavyo kabla ya kwenda kusoma nje unapima afya yako, na unapofika pia
unapima tena. Vipimo vyangu havikuwa na matatizo yeyote
Nilipofika chuoni na kufanya vipimo, nikaambiwa presha yangu ipo juu kidogo
(154/97), kama ilivyokuwa miaka 19 ilopita nilipokuwa nakwenda kusoma
sikushtuka kwani niliona ndio kawaida kwa mimi. Nikiwa chuoni ndani ya mwezi
mmoja niliongeza kilo 4 na kuwa na kilo 85. Ilibidi nianze tena jitihada za
kushusha uzito, lakini kwa bahati mbaya nikapata tatizo mguu mmoja na hivyo
kushindwa kufanya mazoezi kwa kipindi cha mwezi mzima. Kilo 4 ziliongezeka
tena na kuwa na kilo 89. Baada ya kupata nafuu, ilibidi nianze na mikakati mipya
iliyonichukua miezi miwili na nusu kuweza kupunguza kilo 4 na kuwa na kilo 85
ambazo ninazo hivi sasa.
Maradhi ya shinikizo la damu ( Presha) sasa yamekuwa tatizo kubwa dunia nzima.
Maradhi haya si mageni kama Ukimwi na kwa kiasi kukubwa watu wameshayazoea
na kuhisi kuwa ni ya kawaida. Kila siku hatari za magonjwa haya zinaongezeka. Si
kwamba zanakuja hatari mpya, bali yanjulikana magonjwa mengine ambayo kwa
kuchelewa au kutoitibu presha basi yanatoke na kushtuwa watu. Hata umefika
wakati mtu mmoja anakuwa na presha, sukari, matatizo ya moyo na matatizo ya
kuona, jambo ambalo linaonaekana kuwa geni na watu hufika kusema “ndio
mwisho wa dunia”. Bila shaka kila lenye mwanzo basi lina mwisho, hili hakuna
asiyejuwa.
Kwa hofu ya maradhi haya, watu hawataki kujua kama na wao tayari
wameshakuwa na presha, jambo linalopelekea kuwa na wagojwa wengi
wanaotembea na maradhi haya (walking booms) bila kujijua na
wanapokujajulikana tayari maradhi yanakuwa yamekuwa makubwa. Kama vile
watu wengine wanavyoogopa kupima ukimwi, pia watu wanaogopa kujua presha ya
damu zao. Utasikia watu wengine hasa vijana wakisema, “presha ni maradhi wa
watu wazima, vijana hawapati” hili si kweli kwani hivi sasa maradhi haya yanzidi
kuteremka kwenye umri mdogo kuliko zamani.
Tafsiri mbaya ya maendeleo ya sayansi na teknolojia yanachangia sana tatizo la
presha kwani mifumo yote ya maisha ya zamani sasa imeachwaa kabisa. Ulaji wa
vyakula halisi na maandalizi yake umewekwa mwisho, shughuli za kuutuma mwili
zimehamia kwenye mashine, miili haipati hata zoezi dogo la kutembea kwa miguu.
Tumebadili utaratibu ulio bora wa maisha kwa utaratibu usio bora.
Watu walio wazima hawazilindi afya zao mpaka wapate maradhi. Na kwa haya
maradhi ya presha wakishakuyapata watakachojitahidi ni kutokula chumvi, kuacha
vyakula vya mafuta labda na kunywa maji, lakini mfumo wa maisha unabaki
uleule. Mambo haya yanafanya maradhi haya kuwa tishio kadri siku
zinavyoendelea.
Umefika wakati tujizatiti kupambana na maradhi haya. Watu wanaoumwa na
maradhi haya ni wengi kwani kuna wanaojulikana na wasiojulikana. Kuna idadi
kubwa ya vijana wanaotembea na maradhi haya. Napendekeza : -
a. Vijana wasiache kufanya mazoezi,
b. Wanafunzi wawe na ratiba maalum ya mazoezi kama walivyo na ratiba za
masomo.
c. Tupime afya zetu na tuvifanyie kazi vipimo tunavyovipata,
d. Tubadili mifumo ya maisha,
e. Tufuatilie maradhi haya kwani ni chanzo kikubwa cha magonjwa mengine
makubwa mwilini.
f. Kwa kuwa chanzo kimoja ni urithi kwa maradhi haya, tuchunguze afya za
watoto wetu.
Yaliyomo
Vyanzo
Jinsia na umri
Asili
Mlo
Kuzongwa na mawazo
Unywaji pombe
Magonjwa ya figo
Uzazi
Dalili
Presha kwa watoto
Maumivu ya kifua
Kuchanganyikiwa
Makelele masikioni
Kutoona vizuri
Matibabu
Tumia dawa
Hitimisho
Chakula na maradhi
Ununzi wa vyakula
SHINIKIZO LA DAMU
Shinikizo la damau ni pale pressure ya mtu inapokuwa kubwa kuliko kawaida kwa
kipindi chenye kuendelea. Presha ya kawaida inakuwa haizidi 120 juu (systolic) na
80 chini (diastolic) — huandikwa hivi 120/80 mm Hg (read 120 over 80
millimeters of mercury). Daktari atakupima kila unapokwenda kupata matibabu,
na akiona kila anapokupima presha yako ipo juu, itakuwa unapresha tayari.
Presha ya kawaida ni chini ya 120/80. Pale mtu presha yake inapokuwa kati ya
120/80 na 139/89, hali hii ni dalili ya kuwa na shinikizo la damu,
(prehypertension). Kiwango cha kwanza cha shinikizo la damu kinakuwa na
kipimo hichi 140/90 mpaka 159/99, na presha iliyo juu ya kiwango hichi, hiyo
inakuwa kiwango cha pili.
Takriban asilimia 85% mpaka asilimia 95% ya watu wenye shinikizo la damu
hazijulikani sababu zilizowapelekea maradhi hayo. Hata hivyo vipo vyanzo
ambavyoo hupelekea kuwa sababu za kupata maradhi hayo.
Vyanzo
Jinsia na Umri.
Baada ya umri wa miaka 54, wanawake wanakuwa katika hatari kubwa zaidi ya
kupata maradhi haya kuliko wanaume. Hapa tunapata funzo kuwa homoni za kike
( estrogen ) ni kinga kubwa kwa maradhi haya. Inafikiriwa kuwa homoni za kike
( estrogen ) zinasaidia kuifanya mishipa ya damu kuwa laini ( flexible). Estrogen
pia hufanya kazi na homoni nyengine na kupunguza hatari ya kupata maradhi haya
kwa wasichana.
Wanaume
Shinikizo la damu huongezeka kadri umri unavyoongezeka. Shinikizo hili huanza
kuwa kubwa kwa wanaume pale wanapovuka miaka 45, japokuwa linaweza kuwa
kubwa chini ya umri huo. Watu wenye asili ya Afrika na Amerika hupata tatizo hili
wakiwa na umri mdogo. Mafut mengi mwilini, urithi kwenye koo pia huharakisha
kujitokeza tatizo hili.
Shinikizo la damu ni hatari kwani watu wengi wanakuwa nalo bila kulijua kwa
miaka mingi. Japokuwa maradhi haya hayakimbiliki, zipo njia nyingi za kukinga na
kutibu kwa kufuata maelekezo.
Watu wenye historia ya maradhi haya ndani ya koo zao, ni rahisi na wao kupata
maradhi haya.
Asili (Ethnicity).
Mlo (Diet).
Watu wanaotumia chakula chenye chumvi nyingi, hupata maradhi haya haraka.
Japokuwa zipo hali chache hutokea, mtu akawa na uzito mkubwa lakini hana
mafuta mengi mwilini na mwengine akawa na uzito wa kawaida na akawa na
mafuta mengi mwilini. Lakini hali hizi ni za kipekee.
Kwa kutumia BMI yako, jinsia na umri wako wataalamu wanaweza kufahamu
wingi wa mafuta mwilini mwako na kuweza kukushauri namnagani ya kubadili
mfumo wa maisha yako upate kuwa na afya njema. Hata hivyo ikiwa una hali ya
kupata ganzi mara kwa mara kwenye miguu au mikono na hasa unapokuwa na
uzito mkubwa inawezekana kabisa ukawa na mafuta mengi mwilini.
Bado makundi mawili ya wataalamu yanapishana katika kiwango halisi cha uzito
wa mtu kwa urefu wake. Tofauti iliyopo ni kilo 6. Lakini mimi na wewe tujue kuwa
kuwa na uzito mkubwa si salama.
Kwa kufuata makundi hayo, mtu mwenye urefu wa cm 174 anatakiwa awe na uzito
wa kilo zisizozidi 63 au 70. Itakapokuwa mtu huyu anakilo 80 au zaidi basi tayari
atakuwa na uzito mkubwa. Uzito huu utampelekea kuwa na hatari ya kupata
maradhi mengi pamoja na shinikizo la damu. Tutizame table hii katika kutuongoza
kwenye uzito ulio salama.
Wanaume Wanawake
Ukishaona una uzito mkubwa halafu mara kwa mara unapata ganzi unapokaa au
kulala ama miguuni au kichwani, kichwa kinakuuma upande mmoja na wakati
mwengine jicho linachezacheza, macho yako yanakuwa mekundu sana usipuuze,
pima presha yako. Dalili hizi ni ufikaji pungufu wa damu katika maeneo husika
kutokana na wembamba wa mishipa yako ya damu.
Lakini mtu huyu ikiwa anafanya mazoezi, anashiriki katika shughuli za kijamii
kama tayari alikuwa na shinikizo la damu basi presha yake itakuwa nafuu na
kutopanda mara kwa mara.
Hali hii ya mwili kujiandaa ilikuwa na manufaa makubwa kwa watu wa kale pale
wamapokutana na wanyama wakali kama simba au hatari nyenginezo. Lakini hata
leo mwili wako unaendelea kufanya kama ulivyokuwa ukifanya kwa watu wa kale
isipokuwa badala ya hatari zile za watu wa kale, sasa utapambana na majanga ya
moto, hatari za kwenye usafiri au mivutano kwenye makundi ya watu.
7. Unywaji wa pombe
Magonjwa ya figo
Uzazi
Ulaji mkubwa wa vitu vitamu ( sukari nyingi mwilini )
Kwa kawaida misipa ya damu ni yenye kupindika, yenye nguvu na inavutika. Ndani
ya mishipa ni laini kiasi damu inapita kwa urahisi kuelekea kwenye viungo. Ikiwa
una shinikizo la damu, presha yako itasababisha
Uharibufu wa moyo
Moyo wako hupeleka damu mwili mzima. Usukumaji wa damu usio wa kawaida
unaharibu moyo katika namna nyingi. Namna hizo ni pamoa na zifuatazo :
Kama ulivyo moyo, ubongo nao unategemea damu safi ya kutosha ili ufanye kazi
sawasawa. Shinikizo la Damu husababisha matatizo yafuatayo :
Kujua dalili za stroke ni hatu ya kwanza kuzuia isitokee. Stroke, Kwa jina jengine
"kuathirika kwa ubongo," ina dalaili zifuatazo: -
1. Kuumwa na viungo hasa miguu au mikono. Hali hii hutokea kama mtu
aliyeanguka hali hajaanguka. Watu hufikia hatua ya kuchua viungo
hivyo.
2. Kuwa dhaifu au kukosa hisia usoni, mikononi au miguuni upande mmoja
tu wa mwili.
3. Kupoteza uwezo wa kuona au kutoona vizuri jicho moja au yote mawili.
4. Kutoweza kusema, kusema kwa tabu au kutofahamu
kinachozungumzwa.
5. Kuanza ghafla kuumwa sana na kichwa bila kuwepo na chanzo chochote.
6. Kushindwa kutembea au kutembea kwa kuyumbayumba.
2. Kuchanyikiwa
3. Makelele masikioni
Hatua muhimu katika kuzuia na kutibu presha ni kuishi kwa kufuata taratibu za
kiafya. Unaweza kushusha presha yako kwa kubadilika katika hali zifuatazo:
Njia za kupunguza uzito zipo nyingi, lakini hapa nitazitaja 16 ambazo unaweza
kuzitumia katika kupunguza uzito.
5. Kula nafaka
Kula vyakula vya nafaka isiyo kobolewa kunasaidia sana kupunguza uzito.
6. Kuacha kunywa chai nzito asubuhi
Punguza chakula kwa kutumia sahani ndogo badala ya kutumia sahani kubwa kwa
kulia. Hivyo hivyo unaweza kupunguza hata glasi yako kubwa kwa vinyaji vitamu
hasa vya viwandani.
16. Unguza mafuta mwilini kwa zaidi ya Calories 100 kila siku
Jenga mazoea ya kutembea kwa miguu, kukimbia joging, kushughulikia bustani,
kufagia kiwanja cha nyumbani, kufanya kazi za usafi za ndani ya nyumba kama
kupiga deki, kukosha choo kupanga ukumbi na nyenginezo.
Utafiti wa kiafya unaonyesha kuwa, uvutaji sigara unaathiri moyo na mapafu. Pia
huongeza hatari ya kupata baadhi ya kensa. Kwa sababu hizi ni vizuri kuacha
uvutaji wa sigara.
Matokeo
Unapovuta sigara, pumzi zako huwa kidogo na mapafu yako hujaa moshi. Uvutaji
sigara huingiza mwilini mwako sumu ya nicotine na tar.
Moshi wa sigara
Moshi wa sigara unakuwa na gesi ya carbon monoxide. Gesi hii huchukua nafasi
na kuingia katika damu yako kama ambavyo oxygen inavyoingia ndani ya damu.
Kumbuka kuwa carbon monoxide ni sumu.
Nicotine
Hii ni dawa inayoongeza presha yako ya damu na mapigo yako ya moyo.
Inapunguza mwendo wa damu kwenye mikono na miguu na pia hupunguza kasi ya
kuyeyusha chakula mwilini.
Tar
Huu ndio ukungu unaobakia katika mapafu yako baada ya kumaliza kuvuta sigara.
Ukungu huu hujijenga hata ukasababisha oxygen kidogo kupita na kuingia katika
mishipa yako ya damu.
Madawa mengine
Moshi wa sigara una zaidi ya madawa 4,000. Baadhi ya hayo ni pamoja na
formaldehyde, arsenic, na lead. Mengi ya haya madawa yaliyomo husababisha
kansa.
Jambo hili si lenye kujulikana sana kwa vavutaji wa sigara na wasiovuta sigara
lakini huu ndio ukweli na wavutaji sigara walifahamu hili ili waweze kuchukua
jitihada za ziada kuepukana na uvutaji wa sigara.
Hakuna mtu aliyetayari kupoteza uwezo wake wa kuona, labda na jambo hili liwe
kichocheo kwa vavutaji sigara kuacha haraka uvutaji wa sigara.
iii. Kula vyakula kwa maelekezo (kula matunda kwa wingi, mbogamboga, na
kupunguza kula mafuta kwa wingi).
Kula matunda kila siku ni jambo muhimu sana na hapa nitazungumzia tunda moja
kama mtu hapati matunda mchanganyiko basi hili litatosheleza.
Mafuta mengi, chumvi nyingi na kula chakula kingi kunaharibu afya yako. Hizi ni
baadhi ya njia za kutumia ili kuepuka utumiaji wa mafuta mengi katika vyakula.
a. Chakula kiandaliwe kwa mafuta ya matunda badala ya samli au mafuta
mengineyo.
iv. Kupunguza kiwango cha chumvi katika chakula chako unachokula kwa siku
kufikia 2,300 milligrams (kiasi kijiko kimoja kidogo cha chai) kwa siku au
pungufu zaidi .
Hapa kuna maana zaidi ya kutia chumvi katika chakula. Hapa ni kuondoa chumvi
mezani, kuchukua tahadhari na vyakula vyenye asili ya chumvi ( Ng’onda ).
Ikiwezekana chakula chako kisitiwe chumvi kinapopikwa ili utie mwenyewe.
v. Kufanya mazoezi ( kutembea kwa miguu kiasi cha dakika 30 kila siku).
Mazoezi ya viungo kama kuinua vitu vizito ni muhimu kimipango kwa kuuweka
mwili katika hali imara, mazoezi haya husaidia sana kuweka presha yako sawa kwa
kule kutumia hewa iliyo ndani ya mapafu yako na kuufanya moyo wako upige
harakaharaka.
Lakini zoezi lazima liwe na malengo ya kutimiza si pungufu ya nusu saa kwa zoezi la
taratibu na ikiwa ni la kasi basi unaweza kukisia muda kwa uzoefu. Ni vizuri zoezi liwe
lenye kuendelea sio la kukatisha katisha ili kupata athari za zoezi mwilini.
Namna gani pombe inaathiri ubongo na nini athari za kunywa pombe sana.
Khofu na unyonge
Kwa muda mfupi tu pombe ndio hukuondolea mawazo mazito na hali mabya
ambayo unajisikia. Hii ndio sababu baadhi ya wanywaji hutumia pombe
kujisahaulisha matatizo yao , lakini baadae pombe huyafanya matatizo kuwa
makubwa na ya kudumu. Kumbuka kitendo cha mtu kuwa katika hali ya khofu na
unyonge kinamsababishia mwili wake kuwepo katika hali ya kukabiliana na hatari
ambazo ubongo unafikiri zitatokea. Mapigo ya moyo wa mywaji huongezeka muda
wote akiwa katika hali hii. Hali hii humuweka katika hatari ya kupata shinikizo la
damu.
Ni muhimu sana kwa vijana hasa wenye umri wa miaka 18 au 19 kwa sababu bado
ubongo wao unaendelea kukua. Vijana wanaoanza kunywa umri mdogo sana wana
hatari ya kupata maradhi ya akili.
Kunywa Maji
Wingi wa kunywa maji ni kinga ya magonjwa mengi, hata hivyo madaktari
wanasema watu wenye maradhi wanahitaji kunywa lita moja (Glasi 5) zaidi ya watu
wazima, ambao wao lazima wapate si pungufu ya lita mbili (glasi 10) za maji kwa
siku. Hii ndio kusema wagonjwa ni muhimu kwao kupata kiasi cha lita tatu (glasi
15) za maji kila siku.
Unywaji wa maji kwa mtu mwenye afya unategemea mambo mengi kama, hali ya
hewa, kiasi cha kazi azifanyazo, kiasi cha afya yake, ukubwa wa mwili wake, na hata
chakula anchokula. Mahitaji a maji mwilini yanaongezeka kutokana na wingi wa
shunguli azifanyazo na hali ya hewa. Katika hali hiyo, watu wengine watahitaji
marambili ya kiwango cha maji ambacho watu hunywa katika mazingira yao.
Watu wanashauriwa kunywa lita mbili (glasi 10) za maji kwa siku kwa sababu
kiwango chengine wanakipata kwenye maziwa, kahawa, chai, matunda,
mbogamboga na vyakula vinginevyo. Ni vizuri ukafahamu kuwa maji mwilini
hayapatikani kwa kunywa maji yenyewe tu bali ni katika vyakula vinginevyo pia, na
hapa utaona kuwa mwili unahitaji maji mengi kwani ikiwa maji mengine huingia
kwa njia nyinginezo na bado mtu mwenye afya kamili analazimika kunywa lita
mbili za maji, basi aliye na maradhi anahitajika kuongeza lita moja ya ziada.
Sambamba na hili, wale watu waliopoteza maji mengi ikiwa kwa kutapika, au
kuharisha wanahitajika kunywa maji mengi zaidi ili kutoa madini ya sodium
ambayo ni chanzo cha upungufu wa maji mwilini. Kundi la wazee lazima lizingatie
sana unyaji wa maji kwani wazee wengi hawahisi kiu sana kitendo ambacho
kinawaweka katika hali ya kuwa na upungufu wa maji mwilini.
3. Matumizi ya Dawa
Ukihisi dawa unazotumia zinakuletea matatizo, fanya utafiti kuona kama ni hizo
dawa unazotumia au ni kitu chengine. Hii ni muhimu kwa dawa yeyote
utakayotumia, sio kwa dawa za presha tu. Japokuwa maelekezo mengi ya dawa
yatakufahamisha namna inavyofanyakazi mwilini. Hii inamaana kuwa dawa si
hatari kutumia kama inavyoonekana na kusikika na watu wengi, kwani ufanyaji
kazi wa dawa (kama kuumwa na kichwa, kutia usingizi, uchovu, kutaka kutapika,
nk.) hutokea kwenye dawa za uwongo (feki). Hata hivyo, fuata maelekezo ya
daktari na unapoona jambo lolote basi urudi tena kwa daktari wako kwa ushuri na
maelekezo mengine. Hakikisha siku zote unamuona daktari ili akupe maelekezo
kamili kabla ya kubadili mwenendo wa matumizi ya dawa aliokupangia, kuanza
matumizi ya dawa nyengine au kuacha kutumia dawa alokupa. Jenga uhusiano wa
karibu na daktari wako ili upate maelekezo ya mara kwa mara.
Unaweza kuishusha presha yako kwa kutumia dawa zilizo nzuri. Dawa inategemea
na mwili wako. Dawa hiyohiyo yaweza kuwa inawafaa sana watu wengine lakini
wewe isikufae, ndio kusema kwa wewe itakuwa si nzuri. Italazimika ubadilishiwe
nyengine.
Uchaguzi wa dawa ya Presha.
Uchaguzi wa dawa ya presha ni jambo gumu. Ni jambo la kujaribu ili kupata dawa
inayokufaa.
Kuna dawa chungunzima za kutibu presha hivi sasa ambazo zina hasara zake na
faida zake katika matumizi. Kwa kutegemea kiwango chako cha presha , daktari
atakupatia aina moja au mbili za dawa kwa matibabu. Kwa mtu yeyote ambae
tayari ana shinikizo la damu au anahatari ya kupata shinikizo la damu, kubadilisha
utaratibu wa maisha kama ambavyo tumeelezea kutasaidia sana. Kabla ya kuanza
matumizi ya dawa ni vizuri kufahamu hali tofauti zilizopo.
Kwa wenye presha ya juu na wale ambao wameanza kupata dalili za kuwa nayo
(120/80 to 139/89)
Hata ikiwa daktari atakupa dawa kutibu presha yako, bado atapendelea ubadili
utaratibu wa maisha yako kwani kufanya hivyo kutasaidia kupunguza au kuacha
kabisa kutumia dawa. Mabadiliko haya ya maisha ni pamoja na :
e. Kufanya mazoezi kwa dakika 30 kila siku. Hata ikiwa utapumzika pumzika
lakini lengo liwe ni kutimiza muda wa dakika 30.
Huhitajiki kutumia dawa ikiwa presha yako ndio kwanza inaanza, lakini ikiwa pia
una na kisukari, maradhi ya figo au maradhi a moyo daktari atakupatia dawa ili
kuishusha na kuiweka katika hali ya kawaida.
Katika hali hii utalazimika kutumia dawa na kubadili mfumo wako wa maisha. Kwa
mtumiaji wa mara ya kwanza, daktari atakupa dawa moja tu. Inashauriwa dawa
utakayoanza nayo uendelee nayo. Usibadilishebadilishe dawa. Na wakati mzuri wa
kumeza dawa ni asubuhi (saa 1 – 4). Nyakati hizi maranyingi presha hupanda au
kushuka. Kumbuka presha yako huongozwa na mapigo ya moyo, na ndio sababu
kukawa na mapendekezo kuwa asubuhi ni wakati mzuri wa kumeza dawa za
presha.
HITIMISHO
a. Chakula na maradhi
b. Ununuzi wa chakula
Kutokana na uzito wa tatizo lenyewe la presha, kuna haja ya kuelekezana sio kula
tu bali hata namna ya kununua hivyo vyakula.
Kupatana sana kunaweza kukutoa katika malengo ya kupata chakula kilicho bora.