Professional Documents
Culture Documents
Hatua zilizochukuliwa
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, kwa kushirikiana
na Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, wamefanya yafuatayo katika
kudhibiti na kuzuia athari za ugonjwa huu ikiwa ni pamoja na;
a) Kuhudumia wagonjwa hawa katika Hospitali tajwa hapo juu kwa kutenga
wodi maalum
b) Kuunda kamati mbali mbali zikiwemo za
a. Madawa
b. Matibabu
c. Uhamasishaji na utoaji Elimu
d. Maabara
c) Kupeleka timu ya mwanzo ya Wataalamu wa Afya, Wilayani Chemba na
Kondoa kwa uchunguzi wa awali. Aidha maandalizi ya timu nyingine kutoka
ngazi ya Taifa inayoundwa na Daktari Bingwa kutoka Hospitali ya Taifa
Muhimbili, Epidemiolojisti, Wataalamu kutoka Ofisi ya Mkemia Mkuu wa
Serikali, TAMISEMI na Taasisi ya Chakula na Dawa (TFDA) inawasili leo
tarehe 19/6/2016 ili kuongeza nguvu za uchunguzi zaidi. Vile vile, wataalam
wa Sekta ya Kilimo na Mifugo wanaungana na timu inayoendelea na
uchunguzi.
d) Kuchukua vipimo vya sampuli za maabara kwa ajili ya utambuzi wa ugonjwa
ambapo; Damu, mkojo, kinyesi, matapishi, Vinyama vitokanavyo na ini
vimechukuliwa. Sampuli hizi zote zimepelekwa katika Maabara ya Taifa,
Mkemia Mkuu wa Serikali na Maabara ya Kilimanjaro Christian Research
Institute (KCRI), iliyopo Kilimanjaro kwa uchunguzi zaidi.
e) Sampuli za vyakula aina ya nafaka vimechukuliwa kwa ajili upimaji.
Aidha, vipimo vya awali ambavyo vilifanywa na Maabara Kuu ya Taifa vinaonesha
kutokuwepo kwa homa ya manjano, wakati huo huo wanaendelea kufanya vipimo
vingine ikiwemo Homa ya Rift Valley (RVF). Pia tunatazamia kuanza kupata
majibu mengine kutoka kwa Mkemia Mkuu siku ya Jumanne, tarehe 21 Juni 2016.
2
Imetolewa na:
Ummy Mwalimu (Mb)
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,
Jinsia, Wazee na Watoto,
DODOMA.
19/6/2016