Professional Documents
Culture Documents
SW
Habari za UN
Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu
© WFP/Arete/Damilola Onafuwa | Mtoto wa miezi 7 akipimwa utapiamlo katika kituo cha afya cha
jimbo la Yobe nchini Nigeria
Kukimbizana na wakati
Mashirika hayo yamesema zaidi ya watu milioni 34 ulimwenguni tayari
wanakabiliwa na viwango vya dharura vya njaa kali, ikimaanisha kuwa ni
hatua kidogo tu kuwa baa la njaa.
“Kiwango cha mateso kinatisha. Na ni jukumu letu sote kuchukua hatua
sasa na kuchukua hatua haraka kuokoa maisha, kulinda maisha na kuzuia
hali kuwa mbaya zaidi ", amesema Mkurugenzi Mkuu wa FAO Qu
Dongyu.
“Katika kanda nyingi, msimu wa kupanda ndio umeanza tu au uko karibu
kuanza. Lazima tukimbizane na wakati na tusiruhusu fursa hii ya kulinda,
kuleta utulivu na hata kuongeza uzalishaji wa chakula wa ndani, kuteleza. ”
WFP/Kiyori Ueno | Sekina Hassen (kulia) na wenzake wa darasa la kwanza katika shule ya msingi ya
Udassa Repi wakinywa ui. Hupata huduma hii kila asubuhi kutokana na msaada wa WFP na hivyo
wanaweza kuzingatia masomo badala ya kushinda njaa.
Janga linalojitokeza
Kuna sababu kadhaa zinazochangia kuongezeka kwa ukosefu wa uhakika
wa chakula, na mataifa yanakabiliwa na moja au mchanganyiko wa chachu
muhimu ambayo ni pamoja na mizozo, janga la COVID-19, mabadiliko ya
tabianchi na milipuko ya nzige.
TAARIFA ZIHUSIANAZO
MAKTABA MSEMAJI WA UN
KATIBU MKUU TUPATE
KANUNI ZA MATUMIZI
CHANGIA