Professional Documents
Culture Documents
Dini Na Mahusiano
Dini Na Mahusiano
Neno hili, dini, likitajwa, hutaarifu uwepo wa mahusiano baina ya mwanadamu na mamlaka anayoiamini kadri
anavyoishi. Tafsiri ya neno, dini, kwa mujibu wa Kamusi ya kiswahili Sanifu,Toleo la 2004, humaanisha
yafuatayo:1.Imani inayohusianiana na mambo ya kiroho kwamba kuna muumba ulimwengu huu na
kwamba ndiye mtawala wa kila kilichomo.2.Mfumo fulani wa imani hii na njia ya kuabudu/kutii huyo
muumba,k.v.Ukristo, Uislamu au Ubuda.
Kutokana na ongezeko la maneno ya kiswahili, mengine yakiwa ni matokeo ya kutohoa, maana za neno, dini,
zinaweza kuwa zimeongezeka. Somo hili linajadili jinsi ya kudhihirisha kufaa kwa, dini ya kikristo, kama
matokeo ya mfumo wake unavyoelezwa ndani ya Biblia,ilijulikanayo kuwa ni Maandiko Matakatifu
yamtambulishayo Mungu kama Muumbaji wa ulimwengu huu aliye mtawala wa kila kilichomo.
Imani inapotumika, huwa inataarifu uhusiano wa kiibada baina ya mwanadamu na Mungu, (Yoha 4:23,24).
Tendo la kumwabudu Mungu siku zote linahusisha kuufanya mwili wa anayeabudu, utawaliwe na Roho wa
Mungu, kwa mujibu wa Warumi 12:1. Katika kumheshimu na kumtii Mungu, kunahitajika udhihirisho wa
upendo kwa Mungu, kwa njia ya kumwabudu, na hapo hapo upendo kwa wanadamu wengine, kwa njia ya
kuwahudumia majirani wa mtu wanaopitia maisha yenye dhiki. Hapa ndipo imani na matendo vinapokutana
katika kudhihirisha ukamilifu wa ibada kwa Mungu na huduma ya kuonyesha kuwajali walio wahitaji. Huduma
hii ni zaidi ya kuwasaidia walio na dhiki ya mahitaji ya kimwili. Inahusisha pia matumizi ya maneno ya faraja
kwa wanaopitia uzoefu wa msongo wa kiasi au kihisia. Hapa ndipo ulimi hutajwa kuwa, maneno yanenwayo
yasipopangiliwa vizuri ili kuwasadia walio na maumivu ya kiakili, huduma ya kuwapatia mahitaji ya
kimwili,kama vile,chakula au mavazi,au kusaidia kutibiwa maradhi ya kimwili, yote yanaweza
yasitoshe,endapo akili zao zinavurugwa na watoa huduma za kimwili. Ni katika upana huu, tunatakiwa
kujifunza jinsi ya kuoanisha yote mawili.
1
fulani aliyenipatia*, (ijapokuwa yawezekana akawa amefariki). Jingine ni kusema, *Aliyenipa aliniagiza
nisikitoe ili ajapo akione*. Mtoaji wa aina hii naye ametoa kwa masharti ya uchoyo. Hekima, Maarifa na
ufahamu, ambavyo huipatia familia nguvu ya akili ya umoja,(Mithali 24:3-6). Nguvu hizi hukosekana endapo
mmojawapo wa wazazi ni mchoyo. Mzazi wa aina hii hugawa watoto, wengine wawe wachoyo kama yeye, na
watakuwemo wakarimu kama mmoja wa wazazi alivyo.
d. MCHOYO HUSAHAU HATARI ILIYO MBELE YAKE
Mfano wa hatari ya aina hii aliutoa Yesu katika Luka 12:16-20, kisha kumhusu mchoyo kinaishia na kauli hii,
“Lakini Mungu akamwambia, Mpumbavu wewe, usiku wa leo wanataka roho yako! Na vitu ulivyojiwekea
tayari vitakuwa vya nani?