You are on page 1of 27

JINSI YA KUONGOZA IBADA YA

KUSIFU NA KUABUDU

Mwandishi: Steven K. Mattary


T.A.G – Mwembe Bamia Chamazi
Dar es Salaam Tanzania.

1|Page
SHUKURANI:
Kwa namna ya pekee kabisa namshukuru Mungu kwa msaada wa Roho Mtakatifu
aliyeniongoza kuandika kitabu hiki. Lakini pia kwa namna ya kipekee ninamshukuru
Mchungaji wangu Rev. Elia Chisawilo kwani amefanyika Baraka na msaada mkubwa sana
kwangu hasa nilipokuwa namfuata kwa maswali mengi yaliyopelekea mimi kuandika na
kukamilika kwa kitabu hiki na hakusita katika kunisikiliza na kunisaidia hata pale
alipokuwa na majukumu mengine ya kazi zake za utumishi aliacha na kunisikiliza. Pia
ninawashukuru baadhi ya wababa wa kanisa la TAG - Mwembe bamia (CMF) ambao kwa
nyakati tofauti waliweza kuchangia kwa mawazo yao nami nikayachukua na kuyafanyia
kazi, bila kusahau viongozi wote wa idara kwa michango yao hasa tulipokuwa katika vikao
vya viongozi walinipelekea kuchukua mawazo yao na kuyaingiza katika kitabu hiki.
Pengine nitakuwa sijawatendea haki wale wote kwa namna moja ama nyingine nilichukua
mawazo yao vikiwemo vyanzo mbalimbali ambavyo niliweza kuvipitia kwa muda wote
niliokuwa nikiandaa kitabu hiki ingawa naweza nisiwe na kumbukumbu ya vyanzo vyote
lakini natambua na kuthamini mchango au mawazo yao na itoshe kwa kusema asante sana
na Mungu awabariki.
Msukumo huu ulitokana na hali halisi ya mazingira niliyokuwa nikikutana nayo kwa
muda mrefu hasa linapokuja suala la kusifu na kuabudu kwa kutokuleta mguso wa ndani na
kukidhi mahitaji ya mtu (yangu) kukutana na Mungu kupitia ibada ya kusifu na kuabudu.
Yawezekana hali hii imekuwa ikiwakuta wakristo wengi na kwa kupitia kitabu hili linaweza
kuleta mabadiliko kwako wewe ambaye unaguswa katika kumtumikia Mungu kama
kiongozi wa sifa na kuabudu.
Naamini Mungu ni mwaminifu na ninaomba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu atusaidie ili
sehemu hii ya kusifu na kuabudu ilete mabadiliko makubwa na uponyaji kwa kanisa la leo
Amen.

2|Page
YALIYOMO:
1. KUSIFU NA KUABUDU NI NINI
2. NANI MWENYE SIFA NA KIONGOZI WA IBADA YA
KUABUDU
3. SIFA BINAFSI ANAZOTAKIWA KUWA NAZO KIONGOZI
WA KUABUDU
4. MOYO WA KUSIFU NA KUABUDU
5. LENGO LA KUABUDU KWETU AU KUSUDI HASA LA
KUABUDU KWETU.
6. TENDO LA KUABUDU KWA ASILI NI LA KIROHO
7. TIMU YA KUABUDU (PRAISE TEAM)
8. JE NI SAWA KIBIBLIA KUTUMIA VYOMBO VYA MUZIKI?
9. KWANINI TUNAABUDU?
10. HITIMISHO

3|Page
SEHEMU 1: KUSIFU NA KUABUDU NI NINI?
Tunapojifunza Somo hili ni vema Tukafahamu kwanza nini maana ya KUSIFU na
KUABUDU.
Kusifu na kuabudu ni tendo la “IMANI” na “Utii” kwa Mungu wetu, na wala hali hii
haitegemei hisia peke yake (Si tendo la kutegemea hisia zetu pekee) kama ambavyo
tungeweza kufikiri. Ndani ya ibada zetu hatuwezi kukwepa kuwa na utaratibu huu wa
kumwabudu Mungu lakini pia hatuwezi kutokuwa na utaratibu wa kuwa na kiongozi au
viongozi wa kusifu na kuabudu, kwani Mungu wetu pia ni Mungu wa utaratibu. Hii
itatuwezesha kuwa na utaratibu mzuri unaolenga kutukutanisha na Mungu na kupokea
kile ambacho tunakiitaji kutoka kwake, ingawa si tu kupokea lakini lazima tuelewe pia
Mungu alituumba ili tumwabudu (Worship).

SEHEMU 2: NANI MWENYE SIFA NA NI KIONGOZI WA IBADA YA KUABUDU


Hapa nitafafanua kwanza sifa anazotakiwa kuwa nazo kiongozi wa kuabudu.
Kuna sifa za kiongozi wa sifa na kuabudu anazotakiwa kuwa nazo, lakini ni vizuri
kujua sifa hizi zinatokana na nini? Si kila mtu anaweza kuwa na sifa hizi za kuongoza ibada
ya kusifu na kuabudu.
Katika Yoh 15:16 Biblia inasema; “ Si ninyi mlionichagua mimi, bali ni mimi
niliyewachagua ninyi; nami nikaweka mwende mkazae matunda; na matunda yenu yapate
kukaa ili kwamba lolote mmwombalo Baba kwa jina langu awepeni.
Katika fungu hili tunaweza kujifunza kwa ufupi jinsi Mungu anavyomchagua
kiongozi wa Ibada na kufanya maandalizi ndani yako ili uweze kuwa chombo sahihi cha
kutumika katika ibada ya kuabudu.
Pia tunaweza kujifunza hapa kidogo jinsi ambavyo Bwana aliwaandaa viongozi
wake katika Agano la kale, utaona jinsi ambavyo kuhani alipakwa mafuta ili atumike
(kuwatumikia wengine) mtazamo ambao ulikuwa ni wa kidunia na wenye kuwaaminisha
watu, maana kuhani alipakwa mafuta na Musa kwanza. Lakini pia kuhani aliweza kupakwa
mafuta na Mungu. Huu ulikuwa ni mtizamo wa Kimbingu au (Mbinguni)
Hivyo kabla sijakupeleka kujifunza sifa binafsi anazotakiwa kuwa nazo mtu, ni vizuri
pia kujiuliza je? Mungu amefanya nini ndani yako? Kama huwezi kujiuliza yawezekana
hutambui kile ambacho Mungu ameweka ndani yako na pengine anachohitaji ufanye. Haya
ni mashaka mengi walio nayo wakristo wengi juu ya kile ambacho Mungu amewapa ndani
yao ili wakitumie, hapa ndipo utakutana na mgongano wa hisia zenye mashaka kwa
waumini wengi.
Kuna mazingira ya kihisia ambayo wengi wetu tumeongozwa kwa mtazamo wa Ki-
Mungu pindi inavyokwenda tofauti tunasukuma mtazamo huo kwa shetani pasipo kupima
kama kweli unachokifanya ndicho Mungu ameweka ndani yako. Hapa ni lazima niliweka
somo Hili vizuri, watu wengi tumekosa shauku ya kumtafuta Mungu kwa kuachia uzoefu
tuliyo nao tukiamini tunafanya vema, kumbe tayari ulishatoka nje ya mstari(lengo) hivyo ni
vizuri upime na shauku yako ilete majibu sahihi ya kile ambacho Mungu ameweka na
anataka ukitumie.

4|Page
SEHEMU YA 3: SIFA BINAFSI ANAZOTAKIWA KUWA NAZO KIONGOZI WA
KUABUDU
 Hatua ya kwanza na ya muhimu sana, kiongozi wa sifa na kuabudu anatakiwa awe
amezaliwa mara ya pili (Kuokoka) na awe na Roho Mtakatifu (Kujazwa na nguvu za
Roho Mtakatifu).
 Ni mtu mwenye IBADA(MWABUDU) aliye huru mbele za watu na mnyenyekevu na
mtii mbele za Mungu.
 Anatakiwa awe makini Kiroho mwenye Roho wa Mungu ili aweze kuwaleta watu
katika uwepo wa Mungu.
 Mwaminifu, kwani kuongoza ibada ya kuabudu mara nyingi hufanywa kwa imani na
utii na siyo kwa hisia.

Hatua ya kuokoka ni muhimu sana kwa mwamini ambaye anatamani kumtumikia


Mungu katika viwango vya juu, hasa kwenye upande wa kusifu na kuabudu. Maisha
ambayo yanapelekea kuanza kuonja vipawa mbalimbali vya utumishi na kukufanya ukue
na kukomaa zaidi pale unapoingia katika huduma au kipawa kilichowekwa
(Ulichokipokea) ndani yako. Mara nyingi katika huduma yoyote ile usipozaliwa mara ya
pili kutakupunguzia ile hali ya ndani ya mwito wa Kristo Kiroho, hivyo hisia pekee yake
haiwezi kuleta mabadiliko chanya na yenye tija katika utumishi wako. Mara nyingi hisia
zinaweza kukuchukua kwa muda na mara nyingine zisiwepo kabisa hasa pale unapoamua
kufanya huduma fulani, lakini pia zina tabia ya kupunguzwa nguvu endapo hutapewa
msaada au ushirikiano wa kutosha hivyo kuharibu kusudi lenyewe na huu ndo tunauhita
uchanga wa kiimani kwani mara zote unakuwa mtu wa kukwazika na kukata tamaa.

Ili uishi maisha ya ushindi ni lazima ujue ibilisi ameshashambuliwa na kama utajua
hivyo basi utaelewa unao ushindi kiroho kwa kuwa Yesu Kristo alishakushindia. Hali hii
ni vigumu kuielewa kirahisi kama bado hujampokea Yesu huwezi kuishi na kutembea
katika hali ya ushindi bila kuwa na nguvu za ziada zinazokuonyesha kuwa mshindani
wako alishashindwa. Tunaposifu na kuabudu Mungu hushuka Ebr 2:11-13 hivyo tunatoka
kwenye kushindwa kwetu kwenda kwenye ushindi wa Kristo (1 Kor 15:57)

Na tukumbuke kuokoka ni hali ya kutubu na kuacha maisha mabaya ya dhambi


uliyokuwa unaishi, na kuanza kuishi maisha mapya chini ya utawala wa Mungu (Yesu
Kristo) 1 Yoh 1:9. Ni hali ya kubadili mwenendo na tabia, kutua mizigo
iliyokuelemea(Math 11:28-29) kwa kifupi na lugha nyepesi ni ile hali ya kupona kutoka
kwenye hatari iliyokuwa inakukabili na kuwa katika hali salama kama nilivyokwisha
sema awali, hivyo unaondoka kwenye mapungufu mengi ya kibinadamu ambayo hapo
awali yalikuletea shida nyingi, maana kabla ya kuokoka unakuwa umejawa na kila aina ya
uovu mfano uasherati, uzinzi, ulevi, roho mbaya, fitina, uchawi, uongo, husuda, ulaghai,
kuabudu sanamu, mizimu n.k, lakini unapookoka unakuwa mtu wa tofauti na hayo
yanakuwa yamevuliwa kutoka katika maisha yako. Hivyo kwa kweli kama unataka
kumtumikia Mungu katika huduma hii ya sifa na kuabudu ni vizuri uchukue hatua ya
5|Page
makusudi kuacha maisha ya dhambi na kubadili mtazamo yako, ambayo kwa ufupi
tunasema kuokoka au uwe umeokoka, kwani tendo hili la kuzaliwa upya katika Kristo
Yesu litafanya huduma yako ikue na ilete mwitikio na mafanikio makubwa kwa utakao
wainjilisha hasa kwenye huduma hii ya sifa na kuabudu.

Hatua ya pili ni wewe kuwa Mwabudu (mtu wa ibada) hali hii itakupa uhuru mbele
za watu, lakini pia itakupelekea kuwa mtu mnyenyekevu na mtii mbele za Mungu. Ni
vizuri sana kiongozi wa sifa na kuabudu ukapenda kuabudu, na hasa ukizoea tabia ya
kuabudu bila kujali uko peke yako au la!

Tabia ya kumwabudu Mungu itakusaidia pale unapokuja katika kipindi cha kusifu
na kuabudu tayari umefungua moyo wako kuruhusu nguvu za Mungu zitembee na
kukutana na watu. Tunaona hali ya kuzoelea kuabudu ndo ilifanya Paulo na Sila kule
gerezani kwa kufunguliwa na hili ni somo kubwa sana kwetu hivi leo. Kwani tunapoingia
katika ibada hii ya kusifu na kaubudu tunatamani Mungu akutane na vifungo mbalimbali
vya watu. Watu wengi wanakuwa kwenye vifungu vya magonjwa, huzuni, njaa, mapepo,
n.k hivyo tunategemea kipindi hiki kilete uponyaji kwa watu hawa na pengine kuliko
hatua nyingine yoyote ya vipindi vya ibada.

Kama kiongozi wa kuabudu atakuwa na maandalizi mazuri, basi hapa ndo


tunategemea umwagiko wa Roho Mtakatifu ndani ya Kanisa, na wakati huu ndo tunaweza
kuona nguvu za Roho Mtakatifu zikitembea ndani ya watu na hata wale ambao wana
kuwa hawajajazwa Roho Mtakatifu basi tunategemea kupokea Kipawa hiki cha nguvu za
Roho Mtakatifu kwa haraka sana ndani ya waamini na hapa ndo unaweza kuleta
mabadiliko kwa Kanisa maana watu watajawa na ujasiri wa kulihubiri neno la Mungu bila
hofu kwani tayari wanakuwa wamejiona tofauti na kuwa na shauku kubwa ya
kumuhubiri Yesu Kristo (Mdo 8:1-39) utaona jinsi nguvu za Roho Mtakatifu zinavyoweza
kubadili maisha ya watu.

Ni vizuri kiongozi wa sifa na kuabudu ukawa na muda wako binafsi wa kuabudu au


kumwabudu Mungu, hali hii ukiizoelea itakufanya wakati wote kuwa tayari
kuwahudumia watu, lakini pia itakufanya ukue Kiroho (Huduma yako) maana lazima
shauku yako ijengwe katika kukua na si kukaa palepale pa siku zote. Pia hali hii
itakufanya uepukane na fikira chafu ambazo zinalenga kuua huduma au Kipawa ulicho
nacho. Hivyo kukuweka katika hali ya kipekee kabisa hasa linapokuja tendo la
kumuabudu Mungu na pia unatengeneza ushawishi mkubwa kwa Kanisa na watu
wanakuwa wanapenda na kubarikiwa pale unapowahudumia.

 Kuwa mwaminifu (hali ya uaminifu au tabia ya uaminifu) kuongoza ibada ya kuabudu


inahitaji hali ya uaminifu kwani mara nyingi huongozwa na hali ya imani na utii na
wala siyo hisia pekeyake. Hapa ni vizuri nifafanue na uelewe kuwa uaminifu peke
yake hakutoshi, maana wakristo wengi wamekuwa hawatofautishi kati ya kuwa

6|Page
mwaminifu na kutembea katika tabia ya uaminifu. Wengi wetu tunaishi katika hali ya
uaminifu. Lakini tumeshindwa kutembea katika tabia ya uaminifu

Ili maisha yako yawe katika hali au tabia ya uaminifu lazima ufuate hatua hizi zifuatazo: -
1. Ni wewe na Mungu – Daniel 3;16-18
2. Ni wewe na jamii (watu) Paulo anasema sisi ni barua ya kusomwa na watu wote,
maana yake hapa kuna kuaminiwa, kukubaliwa na kuinuliwa.
3. Ni wewe mwenyewe (binafsi) maana yake dhamira yako ikushuhudie kuwa ndivyo
ulivyo. Yesu anasema yamtokayo mtu ndo yaliyomjaa (1 Samwel 12: 1- 5)
Unapoamua kuishi maisha ya uaminifu Mungu anaachilia Baraka zake – Kumb 28:1-8,
Ayubu 42:10.

Hapa tunaweza kujifunza kitu, kumbe uaminifu wako pia unatokana na unachokikiri –
Isaya 6:8 kwani umejengwa katika hali ya haki na imani yako Zab 34:15

Hivyo basi hili tuwe katika hali ama tabia ya uaminifu tunatakiwa kuwa watu wenye
haki na imani (Rum 10:10) haki na uaminifu hukaa ndani ya moyo wa mtu, na Mungu
anawatafuta wenye haki ili aweze kuwasaidia shida zao. Tunajenga msingi wa haki kwa
kuwa waaminifu ili kufike mbinguni na si kwa ajili ya watu. Lakini ni vizuri tukabeba
tabia za Bwana wetu Yesu Kristo jinsi alivyobeba tabia ya uaminifu kutoka kwa Baba
yake- Kum 7:9.

Mungu anajipambanua kuwa yeye ni mwaminifu hivyo nasi twapasa kuwa


waaminifu ili tupokee kutoka kwake na ni vema tukadumu katika hali ya uaminifu
(tunapaswa kuulinda uaminifu mpaka kufa) yaani utakatifu. Suala la kutunza utakatifu ni
la msingi sana kwa kuwa Mungu wetu ni mwaminifu na mtakatifu na anatunza agano lake
(Kumb 7:9. 32:4

Hali ya kutunza uaminifu wetu kwa Mungu kutatufanya tulipwe kutokana na tabia
hiyo, kama tunavyoweza kujifunza juu ya mfano wa taranta kwa wale watumishi (math
25.26) mwanzo sura 15 (Agano la Mungu na Ibrahimu).

Daudi anasema neno moja nimelitaka kwa Bwana nalo ndilo nitakalolitafuta, nikae
nyumbani mwa Bwana siku zote za maisha yangu niutazame uzuri wa Bwana, Na
kutafakari hekaluni mwake (Zab 27:4) Ni wazi kwamba Daudi alijua siri ya kukaa
nyumbani mwa Bwana, alitunza uaminifu na kuishi maisha ya uaminifu.

 Kuwa rafiki ni kuwa mtu wa watu mvumilivu na ujifunze kubadilika wala usiwe mtu
wa kukwazika mara kwa mara. Hapa uvumilivu kwa kweli unahitajika sana maana ni
sehemu ambayo shetani anatumia sana kuwaangusha watu wengi kwenye makwazo
na hatimaye unatoka kwenye msingi wa Mungu, hivyo uvumilivu ni muhimu sana,
jenga tabia ya kuwa na tahadhali wakati wote kwani makwazo hayana budi kuja au

7|Page
kuwepo ndani ya kanisa na hapo ni vizuri ukaibebeba imani sawa sawa kwani
kinachomfanya Ibrahimu kuwa Karimu wale wageni ni tendo la imani na pengine
alifanya hivyo si kwa sababu alitegemea kupata kitu kutoka kwao la! Bali katika hali
yake ya kutembea katika haki ya Mungu ilimsukuma kuwahudumia bila kujali wana
nini kwa ajili yake. Lakini pia tunaona anapoenda kumtoa Isack mwanae mpendwa
kama alivyoelekezwa na Mungu (mwanzo 22:7) Isack anamuuliza baba yake kuhusu
kondoo wa sadaka, majibu ya Ibrahimu kwa Isack kuwa Mungu atajipatia
mwanakondoo, pengine ni jibu ambalo mimi na wewe hatukulitegemea au na hata
Isack mwenyewe kwani ndani yake kuna imani kubwa.
Ukiwa na mahusiano mazuri na Mungu unajengwa ujasiri wa imani yako hata katika wakati
mgumu unaouendea. Mungu anakuwa na urafiki wa karibu na Ibrahimu kwa sababu
Ibrahim pia alijenga imani kubwa kwake pamoja kwamba alikuwa anaenda kumtoa
mwanae alikuwa anakabiliwa na pengine huzuni kubwa ndani yake, laikini alikumbuka
urafiki wao na Mungu na kuwa hata huyo mtoto ametoka kwake (Mungu) hivyo aliamini
bado Mungu anaweza kumletea tena furaha katika maisha yake.

 Kumbuka hapa nazungumzia sifa ya urafiki ulio katika imani. Katika Yakobo 1;5-8,
Biblia inatuambia juu ya kuwa na imani pasipo shaka yoyote, kwani imani ya kusitasita
haitakupa matokeo chanya katika Ukristo wako na hasa ukiwa kiongozi wa sifa na
kuabudu maana utakuwa ni mtu wa kukaribisha makwazo kila wakati hivyo badala ya
kukuinua unazidi kudidimia. Kama Ibrahimu angekuwa mtu wa kusitasita basi hata
Sara Mkewe asingeweza kumzaa Isack, maana mkewe Sara bila shaka jambo hili
lilikuwa gumu moyoni mwake kuzaa katika umri wake.

Hapa tunajifunza jinsi ambayo ukikaa vizuri na Mungu na kujenga imani kwake inaweza
kukuletea matokeo ambayo akili yako haina majibu nayo. Lakini imani hiyo pia itakupa
faraja ambayo hukutegemea.
Imani inaleta ujasiri (Isaya 43:1-2, Isaya 6:8) pia imani uleta Baraka mwanzo 22:17
Sifa nyingine ni kuwa mwana muziki – ni vizuri zaidi kama ukakuwa na uwezo wa
kuimba au kuwa na vionjo vizuri vya kutumia vifaa vya muziki kama utakuwa nauwezo
huo. Kwani tunaamini ukiwa na uwezo wa kupangilia vizuri vyombo vya muziki unaweza
kwa sehemu kubwa kuliweka kusanyiko katika hali nzuri ya mwitikio na hapo ndipo hali ya
kuabudu itakuwa katika mtiririko mzuri usio chosha, hivyo kuwafanya watu wahame
katoka kimwili na kuzama Kiroho zaidi.

Uwe mtu anayefundishika, mnyenyekevu mwenye moyo wa kiutumishi na uwe ni mtu


ambaye unaweza kushirikiana na wenzako yaani wanatimu.

Uwe mtu unayejitolea, hapo ni vizuri nieleze kwa kirefu kidogo. kiongozi wa sifa na
kuabudu lazima awe tayari wakati wote kama nilivyokwishaeleza huko nyumba, lakini
tunapenda au tungependa awe ni mtu wa kujitolea kwa Mungu kwanza, kisha familia na
kanisa kwa ujumla, maeneo haya ni muhimu sana kwa kiongozi anayetaka huduma yake
iwe nzuri na inayoleta matunda mema.
8|Page
Uwe ni mtu uliyejiandaa vizuri na mwenye muonekano mzuri katika mavazi yako na
yawe ya heshima na unadhifu yasiyoleta maswali mengi. Na hapa hata katika mitindo
mbalimbali ya mavazi yako pengine hata mifumo ya nywele kwa wale wenye kuwa na
mitindo mbalimbali ukizingatia zaidi eneo la huduma yako kuliko matokeo ya kila
ulichokibeba. Maana tumejikuta waumini wengine wanaamishia mawazo yao kwenye
mtindo wa nywele muda wote wakasahau hasa wanapaswa wamwabudu Mungu. Katika
mavazi uliyovaa yasiwe yenye kuonyesha mazingira yako yote ya mwili au mepesi kupita
ile hali ya kawaida (Trasparent) na kama kweli utakuwa makini zaidi basi wakati unaposifu
ni wakati ambao kama hukujiandaa unaweza kusababisha minong’ono mingi na fujo isiyo
ya lazima kutokana na maandalizi yako hasa kwa upande wa mavazi. Ni eneo ambalo Ibilisi
analitumia sana kuchota akili za watu ili wasimwabudu Mungu mwonekano huo ni kwa
wote yaani kiongozi wa sifa wa kiume na wa kike lakini pia ni kuhakikisha mavazi yako
yanavishikizo imara kabla ya kuingia kwenye huduma. Hii ni kukulinda pia na fedheha
inayoweza kukupata mbele za watu.

 Sifa njema: na uwe na ufahamu wa Biblia Kiongozi au timu ya kuabudu ni vema


ikawa na sifa njema ndani na nje ya Kanisa, lakini ni vizuri pia kuwa na ufahamu wa
neno la Mungu (Biblia) kwani itakusaidia uweze kutunga nyimbo zinazotokana na
neno la Mungu kwa kusudi la kuwabadilisha watu na si kuwafurahisha tu.
 Uongozi: uwe unaweza kusimamia na kuwa na ujuzi ama uzoefu wa kuwaongoza
wengine, kama kiongozi.
 Kiongozi wa sifa na kuabudu: anatakiwa awe mtii hasa kwa Mchungaji na viongozi
wengine ndani ya Kanisa, lakini awe ni mtu aliyebeba maono ya Mchungaji,
anayekubaliana na maelekezo yake. Kiongozi wa sifa kama utakuwa siyo mtii basi ni
wazi kuwa huduma hiyo haitafanya vizuri kwani utakuwa umekaribisha kiburi
ambacho kwa kweli ni hatari kwa maisha ya waamini na kanisa kwa ujumla. Hapa
ndipo panatakiwa hekima ya hali ya juu ili kuruhusu nguvu za Roho Mtakatifu zifanye
kazi ndani ya Kanisa, lakini lazima usiwe mbaguzi ukaona huyu anafaa na Yule hafai,
ni muhimu umwombe Mungu ili akutangulie juu ya huduma kwa lengo la
kuwakusanya na kuwaweka wote katika uwepo wa Mungu bila kujali tofauti zao,
rangi au Kabila hii itakupa nafasi ya juu zaidi machoni pao, hivyo Mungu ataonekana
ndani ya huduma yako hata kama utakutana na vikwazo.

SIFA ANAZOTAKIWA KUWA NAZO KIONGOZI (SEHEMU YA PILI)


Nikiwa bado katika kipengele hiki ni vema nikaongelea kitu kingine hapa kuhusu namna ya
kufikia kuwa kiongozi wa Sifa na Kuabudu yaani wito wa Mungu ndani yako.
(a) Huwa watu wengi wanatamani kuwa viongozi wa sifa na kuabudu na pengine
wanakosa nafasi kutokana na mazingira waliyopo, lakini ni vizuri kujiuliza kama
unatakiwa kweli kuongoza na hapa ni ule moyo au shauku ya kuongoza. Jambo la pili
ni uwezo ulio nao je unaweza kuongoza? Wengi wetu hapa wakijiuliza majibu yakiwa
ni hapana wanakata tamaa kwa kweli unachohitaji si uwezo tu kwani unaweza kuanza

9|Page
na hali yako uliyo nayo huku ukiendelea kutafuta fursa zaidi za kuongoza (Zakaria
4:10)

(b) Neno la Mungu linasemaje?


Jitie nguvu juu ya maneno ya Mungu (math 24:35) mbingu na nchi zitapita lakini
maneno yangu hayatapita kamwe. Anza na kuliamini neno la Mungu, na kwamba
Mungu ndiye atatenda au kuweka kitu ndani yako kwa maana Mungu uangalia Moyo
wako na Shauku uliyo nayo ya kumtumikia. Biblia katika wafilipi 3:3 inasema maana
sisi tu tohara, tumwabuduo Mungu kwa Roho, na kuona fahari juu ya Yesu Kristo,
wala hatuutumainii mwili. Kumbe tunatambua kuabudu kwetu ni kwa Rohoni na wala
si kimwili, hivyo hatuutumainii zaidi mwili ili tumwanudu Mungu. Kama ndivyo basi
ni vema au zizuri tukamtumaini Yesu na kwamba yeye ndiye ataweka kitu ndani yako
(Yoh 16:14) Biblia inasema “yeye atanitukuza mimi, kwa kuwa atatwaa katika yaliyo
yangu na kuwapasha habari. Si vema kutegemea mwili zaidi na kuanza kujionza
mnyonge na pengine ukakata tamaa, Zakari 4;6 “inasema si kwa uwezo wala si kwa
nguvu bali ni kwa Roho yangu, asema Bwana” hivyo amini tu kuwa Mungu anao
uwezo na anachokisema atakifanya kwako kama utajinyenyekeza kwake na kumtii.

(c) Jinsi ya Kuitikia wito wa Mungu.


Huitikia wito wa Mungu kwa kuonyesha tabia njema na iliyothibitika, mara nyingi
watu wanashindwa kuitikia wito wa Mungu pale wanapoamua kufanya wanachotaka
bila kuangalia kuwa wanatakiwa wafike wapi hivyo wanakuwa wanavutiwa na
taranta tu (vipawa) na kushindwa kuelewa makusudi ya Mungu ndani yao na moja ya
vitu vibaya vinavyoweza kumtokea mtu ni pale anapofanikiwa kabla ya tabia yake
kuwa tayari juu ya jambo husika.

(d) Itikia wito wa Mungu kwa kuwa mwaminifu katika vichache (Luk 16:10)
Biblia inasema “Aliye mwaminifu katika lililo dogo sana, huwa mwaminifu katika lililo
kubwa pia, na aliye dhalimu katika lililo dogo, huwa dhalimu katika lililo kubwa pia”.

Zipo fursa nyingi kutoka kwa Mungu na huja kulingana na mahitaji ya wahusika, hivyo
ni wewe kuona jinsi gani ya kutumia fursa unayoiona mbele yako hata kama si ile
uliyokusudia kwani yawezekana ikawa kipimo kwa ile huduma iliyokusudiwa ndani
yako au uliyokusudia wewe. Na hapa utajikuta wakati mwingine unatakiwa kujifunza
au kufundishwa ili uweze kufikia hatua ya kuongoza math 7:7 “ombeni nanyi
mtapewa tafuteni nanyi mtaona, bisheni nanyi mtafunguliwa”. Ukikubali kuitikia
katika vichache basi Mungu atakupandisha katika vingi pasipo wewe kujua, kwani
Mungu ndiye anaona akutumie wapi na kwa kusudi lipi.

Efeso 1:11 “huku tukichaguliwa tangu awali sawasawa na kusudi lake yeye”. Moyo wa
kitumishi uandaliwe kufanya chochote wakati ufaao na wakati usiofaa, kinachotakiwa
ni ule utayari wako hata pale unapoona si pa kukufaa (yaani pasipo na fursa) au

10 | P a g e
panawepesi au ugumu, penye kuvutia au pasipovutia wewe itikia wito wa Mungu kwa
kuwa na tumani. Ebr 13;21 “Awafanye ninyi kuwa wakamilifu katika kila tendo jema,
mpate kufanya mapenzi yake”.

Jambo la Msingi ni kufahamu msingi uliosimamia.


Kuna misingi miwili ya kweli kwa kiongozi wa kusifu na kuabudu: -
1. Umepakwa mafuta 1 Yoh 2;27 “Nanyi, mafuta yale mliyo yapata kwake yanakaa
ndani yenu, wala hamna haja ya mtu kuwafundisha, lakini kama mafuta yake
yanavyo wafundisha habari za mambo yote, tena ni kweli wala si uongo na kama
yalivyowafundisha, kaeni ndani yake’.
2. Fahamu kuwa una neema kwa sababu ya nafasi ya Ibada ya kusifu na kaubudu
(Ebe 4:16) “Basi tukikaribia kiti cha neema kwa ujasiri ili tupewe rehema, na
kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji’.

(e) Kiongozi wa ibada ya Kusifu na kuabudu anapaswa kuwa mchungaji wa Ibada ya


kusifu na kuabudu.
Unapokuwa kiongozi wa ibada ya kusifu na kuabudu lazima uelewe majukumu
uliyoyabeba kwa ajili ya watu wengine. kama hutojua hilo basi utakuwa kwenye
wakati mgumu katika kuliongoza kundi ulilopewa jukumu la kuwasimamia ili
kuwatoa na kuwavusha kwa kusudi moja kubwa la kukutana na Mungu kupitia ibada
ya kuabudu.

Kwanza kabisa utambue kuwa wewe kama kiongozi wa sifa na kuabudu lazima
ulilishe kundi au watu, hivyo lazima uchague nyimbo nzuri itakayowawezesha watu
kuingia kwenye kuabudu, na nyimbo hizi ziwe za kuwaunganisha na uwepo wa
Mungu (kukutana na Mungu) maana yake wapate chakula kizuri cha Kiroho kupitia
uimbaji. Na kwa kuwa utakuwa unalipenda kundi lazima utajitoa hasa ili ulitimize
kusudi lako kama mchungaji mwema. Yohana 15:13 Biblia inasema “hakuna aliye na
upendo mkuu kama huu wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake” na Yohana
10;11 inasema “Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo”. Kwa
misingi hiyo utaona unawajibika kuwapa kondoo wako chakula chema na
kitakachowafanya wafurahie kuwa na mtu kama wewe. Ki msingi hapa ndipo sehemu
inayohitaji maandalizi ya hali ya juu kama kweli kama utataka watu wakutane na
uwepo wa Mungu kupitia nyimbo ulizozichagua. Siku zote kondoo atategemea kupata
maelekezo mazuri kutoka kwa mchungaji wake atakayewaelekeza mazingira mazuri
ya kupata kile walichokitegemea (yaani chakula kizuri cha kiroho) tena ukisoma
katika waefeso 3;8 “inasema utajiri wa Kristo usiopimika’ hivyo malisho
wanayotegemea siyo ya kunyang’anyana bali ni yale nyenye utoshelevu katika Kristo
Yesu. Watu wale na wanywe mbele za Mungu kupitia uimbaji kiasi cha kuwatosheleza
na kuua yale mahitaji yao ya kimwili na matatizo mbalimbali, Wanayokuja nayo
kutoka mazizini mwao (nyumbani mwao).

11 | P a g e
 Kabla sijamaliza kwenye kipengele hiki nimeona nikuandalie maswali
yatakayokuwezesha pengine kukufungua zaidi na kukuimarisha katika huduma hii ya
kusifu na kuabudu.
1. Je haiba yako ni ipi na pengine ungependa Mungu akutumie katika hali hiyo
uliyonayo au uliyolelewa nayo na pengine iliharibu mahusiano yako na Mungu,
hivyo unaomba Mungu sasa akutayarishe upya uweze kutumika katika huduma hii
ya kumwimbia?
2. Je katika maisha yako ulishawahi kuwa na msukumo wa kumtumikia Mungu
katika huduma hii au kuna sababu nyingine uliyo nayo inayopelekea uanze na
kuchukua hatua ya kumwimbia Mungu kama kiongozi wa sifa na kuabudu?
3. Je maisha yako ya Haki, uaminifu na imani yakoje, unahisi kuna eneo ambalo
halijakaa sawa n a ungependa Mungu akutane nalo ili mwelekeo wako uwe salama
hasa pale unapoamua kuchukua hatua?
4. Je kiroho au maisha ya kiroho ukoje, unafikiri inatosha sasa kumtumikia Mungu au
wakati wako umefika wa kufanya hivyo au bado una mashaka mashaka na
huduma unayoiendea?
5. Je katika sifa nilizokwisha kuzitaja hapo nyumba unaona kabisa unakosa sehemu
ya sifa fulani na ambayo inaweza kuwa kikwazo katika huduma yako na Je
ungependa Mungu afanye nini ili uondokane na tatizo hilo?

SEHEMU YA 4: MOYO WA KUSIFU NA KUABUDU


 Kuabudu ni tendo la kujali. Mungu anajali jinsi tunavyo mwabudu, na kumfungulia
Moyo (kutoka 20:3) Biblia inasema usiwe na Miungu mingine ila mimi. Hivyo
tunapaswa kuhakikisha kuwa tunalinda mioyo yetu (mith 4:23) linda sana moyo
wako kuliko yote ulindayo, maana ndiko zitokako chemichemi za uzima “Kitendo
chetu cha kumwabudu ni kama tumemfungulia Mungu na kuingia ndani ya mioyo
yetu, hivyo tunakuwa na sehemu ya kumheshimu na kuruhusu uwepo wa Mungu
kutawala ndani yetu, na hili ni tendo la kujali kuhusiana na kuabudu kwetu.
 Tendo hili la kujali linaruhusu utawala wa Mungu katika Ibada zetu na kuweka
mwongozo mzuri wenye mawasiliano yenye tija kati yetu na yeye tunayemwabudu
kwani anakuwa amelisimamia vizuri zoezi hili ambalo kimsingi litapelekea hali ya
kumpendeza Mungu na kumridhisha, ndipo anapoweza kuamua mambo mazuri zaidi
yaje ndani ya maisha yetu.

Na ni vizuri tulenge kumwinua yeye nakuonyesha ukuu wake ama uweza wake.
Zaburi 48;1 (Bwana ndiye aliye Mkuu, na mwenye kusifiwa sana)
Ili tuelewe namna nzuri ya kuabudu lazima tuangalie mambo yafuatayo: -
(a) Ni hali ya mwonekano wetu wa kawaida na si lazima ufundishwe bali ni silica
tuliyonayo. Mfano mtoto mchanga anasilika ya kutabasamu na kucheka na
wanakuwa huru wanapofanya hivyo bila kufundishwa na mtu yeyote, lakini
unapokuja kwa watu wazima lazima watataka kutoa sauti ili watambulike au
kuonyesha mwitikio juu ya jambo fulani. Kama ilivyo kwa sura zote mbili
12 | P a g e
Mungu ametupa amri, haijalishi unajisikiaje pale anapotaka umwabudu njia ni
moja tu ya kumwabudu kwani huko ndiko tunakwenda kukutana naye.
Utayari wetu wa kumwabudu utupeleka uzimani. tunaona kusitasita kwa
Musa kulifanya akapewa msaidizi wa kuongozana naye pengine Mungu
hakupenda iwe hivyo lakini tunakuwa katika hali kama ya mtoto mchanga
tunaruhusu mambo mengi zaidi kwenye maisha yetu, hasa ya kutufanya
tutabasamu na kuwa na amani.

(b) Picha au mwonekano wa pili lazima tuelewe kuwa kumwabudu Mungu


kunatupa picha ya upendo, kama ambavyo tunamwona Ibrahimu akienda
kumtoa mwanaye kuwa sadaka (mwanzo 22:5) “Mimi na kijana tunakwenda
kule tukaabudu” ni tendola imani la kumtolea Mungu, na si tu kumtolea bali
kumtolea Mungu kilicho bora kabisa. Daudi anasema neno moja nimelitaka
kwa Bwana, nalo ndilo nitakalotafuta, nikae nyumbani mwa Bwana siku zote
za maisha yangu, Niutazame uzuri wa Bwana na kutafakari hekaluni mwake”.
Msingi wa ibada yetu ulenge kukutana na Mungu ama kukutana na uwepo
wa Mungu ambapo kwa lugha ya kiebrania ni kukutana naye uso kwa uso.

(c) Picha ya tatu ni kuonyesha thamani ya Mungu kwetu na kwa wengine pia,
kama tujuavyo Mungu wetu ni wa thamani sana na pengine ni vigumu
kuelezea thamani yake (ufunuo 4:11) “umestahili wewe, Bwana wetu na
Mungu wetu, kupokea utukufu na heshima na uweza, kwa kuwa wewe ndiwe
uliyeviumba vitu vyote, na kwa sababu ya mapenzi yako vilikuwako, navyo
vikaumbwa”. Kusifu na kuabudu kunahusiana na yale Mungu aliyoyafanya,
lakini hasa kwenye kuabudu kunamaanisha yeye ni nani.”

(d) Kuabudu ni Roho zetu kumwitikia Mungu, tunamwabudu katika Roho wa


Mungu (Filipi 3;3) na Ki-ukweli kwa asili tunapaswa kumwabudu Mungu
katika roho na kweli maana tumetokana na Roho wa Mungu.

MATOKEO YA KUMSIFU NA KUMWABUDU MUNGU


 Yapo matokeo makubwa ya kumsifu na kumwabudu Mungu moja ya matokeo hayo
ni: -
(i) Tunaweza au hali hiyo inatupa kusaidiana, kutiana moyo katika wokovu
(katika kumfuata Yesu Kristo) hata kama tunapita katika vikwazo fulani,
tutaendelea kuishi tukimtumainia Mungu.
(ii) Kusifu na kuabudu kwetu kunambariki Mungu. Mungu anatamani aone
maisha yetu ni ya kumwabudu yeye Efeso 5:19 Neno la Mungu linasema
“mkisemezana kwa Zaburi na tenzi na nyimbo za rohoni, huku mkimwimbia
na kumshangilia Bwana mioyoni mwenu” na unaweza kusoma pia Wakolosai
3:16 Biblia inasema “Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika
hekima yake, mkifundishana na kuonyana kwa Zaburi, na nyimbo na tenzi za
13 | P a g e
rohoni huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu” hivyo ni wazi
kwamba tunapomsifu na kumwabudu Mungu kwanza: -
1. Tunapona kutoka kwenye maumivi tuliyomo.
2. Tunapata furaha nafsini mwetu lakini pia tunabarikiwa na kuinuliwa zaidi
katika utumishi wetu.
3. Tunatiwa nguvu na kuishi maisha yenye amani zaidi tukifurahia au
tukifurahia wokovu wetu katika Kristo Bwana wetu, lakini zaidi ya hayo
tukitumaini uzima wa milele ambacho hasa ndicho kiini cha wokovu na
utumishi wetu.

JE KUNA VIWANGO VYA KUSIFU NA KUABUDU?


 Ukweli ni kwamba kuna viwango vya kusifu na kuabudu na hii inategemea hasa
mazingira ya maandalizi kama nilivyokwisha sema huko nyuma pia na mahusiano
yaliyopo kati ya mwabudu na mwabudiwa. Viwango vingine ni vya kibinadamu, hasa
uelewa wako wa kutumia baadhi ya vyombo vya musiki n.k na kama tunavyojua kuwa
mara nyingi sifa huongoza watu kwenye kuabudu, hivyo ni vizuri kwa kiongozi awe
na viwango vizuri kwa kweli kwenye kuwafikisha watu katika kuanudu ingawa
wakati fulani hakuna taratibu ambazo lazima zifuatwe, kwani Roho mtakatifu ni
mbunifu na mwongozaji mzuri na hafanyi kazi kwa namna moja wakati wote.
 Mahusiano yetu na Mungu yanatakiwa yajengwe kwenye misingi ya sifa na
kumwabudu Mungu na haya ndiyo yanatakiwa yawe ni maisha yetu na kwa kweli
katika maisha yetu ya kumwabudu Mungu, ni vizuri tukatambua kuwa Mungu pia
anawatafuta watu wa namna hiyo. Yoh 4;23,24 “lakini saa inakuja, nayo sasa ipo,
ambayo waabudu halisi watamwabudu baba katika roho na kweli kwa maana Baba
awatafuta watu kama hao wamwabudu. Mungu ni Roho nao wamwabudu. yeye
imewapasa kumwabudu katika roho na kweli! Siyo tu namna ya wimbo tunao
uchagua bali ni jinsi ya maisha tunayoishi, matendo yetu na nia ya moyo wetu
vikubaliane na Mungu katika hali ya utii mbele za Mungu (Rum 12;1) “itoeni miili
yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu ya kumpendeza Mungu ndiyo dhabihu yenye
maana”. Hivyo kusudi la Mungu katika maisha yetu ni kuabudu na ndiyo kutimiza
mapenzi ya Mungu katika hali ya kumwabudu.
 Na tuhakikishe kwa kweli tunakuwa waadilifu katika kuabudu. Tendo la kuwa na
uadilifu ni hali ya kutoa viungo vyetu vyote kwa ujumla na kusema kitu
kinachofanana, maana yake ukweli katika maisha yetu yawe na mahusiano tena yenye
kuunganishwa pamoja. Hivyo hafa tunapochagua nyimbo zetu lazima zikubaliane na
hali halisi ya jinsi tulivyo visitofautiane na kuleta tafasiri tofauti wakati tunapomsifu
na kumwabudu Mungu. Kwani tukifanya kinyume Mungu hachelewi kutuadhibu
(amosi 5:23, 24) Neno la Mungu linasema “niondoleeni kelele za nyimbo zenu kwa
maana sitaki kuzisikia sauti za vinanda vyenu lakini hukumu na iteremke kama maji
na haki kama maji makuu” kukubaliana kusiko sawa hudhoofisha ujasiri wetu katika
kumwabudu Mungu, kwa kuwa uadilifu unajenga ujasiri. Na ujasiri ni kitu
kinachojengwa kama hatuwezi kujenga ujasiri basi tunakuwa kwenye hatari ya
14 | P a g e
kulinda ubora tuliofikia katika kumwabudu Mungu. Kuongoza Ibada yetu ya kusifu na
kuabudu kunaimarishwa na ujasiri mkubwa tulio nao. Kama kiongozi unawasaidia
wakristo na kuwajengea ujasiri pia wa kumwabudu Mungu katika maisha yao.

Unapolinda uadilifu wako, unalinda ufanisi wa uongozi wa huduma yako ya kusifu na


kumwabudu Mungu. Kabla sijamalizia kipengele hiki ni vizuri pia ukajiuliza maswali
yafuatayo: -
1. Je? Ungetamani kumwabudu Mungu na kumfungulia moyo wako na hasa sababu ni
zipi?
2. Unajisikia vipi unaposikia kwamba Mungu anatamani wanaomwabudu
wamwabudu katika roho na kweli, na wewe ungetamani iwe hivyo?
3. Ulishawahi kufikiria Mungu ni wa thamani gani kwako?
4. Unahisi hasa ni kitu gani kinakukwamisha katika hali ya kumsifu na kumwabudu
Mungu katika maisha yako na kwanini?
5. Unahisi mbinu anazoftupa Mungu kupitia neno lake si mbinu za kawaida za
kibinadamu katika kumwabudu?

SEHEMU YA 5: LENGO LA KUABUDU KWETU KUSUDI HASA LA


KUABUDU KWETU.
 Kwanza kabisa lazima tufahamu kuwa hatuwezi kuwa na lengo au kusudi bila kuwa
na shauku ya kile tunachokilenga, ina maana shauku yetu mbele za Mungu ndicho
kitatupa msukumo wa kumwabudu Mungu. Na tutakapoonyesha shauku maana yake
Mungu ataweka ndani yetu msukumo wa kumwabudu, au shauku ya kumwabudu, na
ni shauku ambayo hakuna mtu anayeweza kuitosheleza, isipokuwa yeye Mungu
mwenyewe Zab 42:1,2. “Kama ayala aioneavyo shauku mito ya maji vivyo hivyo nafasi
yangu inakuonea shauku, ehe Mungu. Nafsi yangu inamwonea kiu Mungu, Mungu
aliye hai lini nitakuja nionekane mbele za Mungu?

Na shauku hii imejengwa katika misingi ya uimbaji. Hivyo Mungu hutupa shauku
kupitia muziki. Kwanini Mungu hutupa shauku kupitia muziki ni kwa sababu: -
1. Kupitia muziki tunaweza kuonyeshwa shauku ya kumwabudu zaidi na
kumdhihirisha zaidi Mungu ndani yetu.
2. Pia uimbaji, hasa tunapotumia vyombo vya muziki vinakuwa na mchango mkubwa
kwa watu kuwafikisha katika uwepo wa Mungu. Miili yetu inakuwa
imeunganishwa tayari na makusudi ya Mungu hivyo kuhama katika hali ya
kawaida na kumwacha Mungu atawale zaidi, na ndipo utaona mabadiliko tofauti
kama tungekuwa tunasikiliza tu maneno ya Mungu.

KWANINI TUNAMWIMBIA MUNGU


1. Kumwimbia Mungu ni kuonyesha alama ya utii kwa Mungu wetu na kwamba yeye
yuko juu ya yote, kutoka 15:1 “Nitamwimbia Bwana kwa maana ametukuka sana” na
Biblia inatuambia kuhusu kumtii Mungu Zab 68;4 mwimbieni Mungu, lisifuni jina lake.
15 | P a g e
2. Jambo la pili tunapomwimbia Mungu kwa sababu yeye ndiye aliyetuumba na ni wa
rehema na fadhili zake ni kuu kwenye maisha yetu Zab 135:3, Zab 147 :1 -20. Hivyo
tuna kila sababu ya kumwimbia Mungu.
3. Roho wa Mungu yu ndani yetu waeteso 5:18 “Bali mjazwe Roho” mkisemezana kwa
zaburi na tenzi na nyimbo za rohoni”
4. Neno la Mungu li ndani yetu ukisoma katika wakolosai 3:16 Biblia inasema “Neno la
Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote. Mkimwimbia Mungu kwa
neema mioyoni mwenu”. Hivyo tunakuwa tunaujenga mwili wa Kristo na hutusaidia
kutiana moyo, na kuimarishwa kwa imani yetu. Mazingira haya yanatufanya kila
mmoja wetu kuimarika kiroho na kuwa na mahusiano mazuri na Mungu wetu.
5. Kuimba pia kunatupa furaha mioyoni mwetu Zab 92;4 “kwa kuwa umenifurahisha
Bwana kwa kazi yako, nitashangilia kwa ajili ya matendo mikono yako. Pia kuimba ni
afya ya mwili, tunapomwimbia Mungu kunatusaidia kuachilia mwili na hisia zetu.
6. Lakini ni kuonyesha imani yetu, kuimba na kuabudu kwetu tunakuwa tunafanya tendo
la kuhushudia ulimwengu kuwa Mungu wetu ni Mungu aliye hai Zaburi 108:1
“Nitakuimbia zaburi kati ya mataifa,” mazingira haya na mengine mengi yanatuweka
kuwa watu wa tofauti na hivyo kuudhirisha kwa walimwengu wamgeukia Mungu.
7. Mungu hushuka na ukaa ndani ya sifa na kwa msingi huo tunakuwa karibu na Mungu
wetu huku tukitazamia uzima wa milele. Maisha ya uimbaji yanapunguza mawazo, na
masononeko na adha za dunia hii na kujikuta wakati wote ni watu wenye furaha na
amani ya moyo, hata kama unapitia mazingira magumu kiasi gani.

NYIMBO TUNAZOIMBA NI LAZIMA ZIWE ZAIDI YA NYIMBO: -


 Ni kule kuimba nyimbo ambazo zipo ndani ya mioyo yetu na zinadhihirisha uwepo wa
Mungu (kumgusa Mungu) lakini zieleze hasa kile tunachokifanya au kilichofanyika
ndani ya maisha yetu, ziguse mazingira tuliyo nayo au tunayokabiliwa nayo kwa
kumaanisha si tu kuimba kama nyimbo za kawaida. Ni vizuri kiongozi wa sifa na
nyimbo za kuabudu akaimba nyimbo zenye mguzo unaotokana na hali halisi
tunayopitia, ziwe ujumbe mzito unaogusa mazingira au shida za watu zenye kuruhusu
mapenzi ya Mungu yafanyike ili kuleta uponyaji kwa watu kupitia uimbaji.
 Ni vizuri ukawa na uelewa mzuri wa huo wimbo, hata kama ni mpya basi jaribu
kuwatanguliza kwa uziri kabisa ili na wao washike kwanza ndipo uendelee, unaweza
kutumia vifungu vya Biblia kukusaidia kuimba wimbo wako, lakini kuwa saidia wale
wanaoitikia pia. Ni vizuri ukaanza kuimba kwanza na kisha watu watajifunza na
kufuata kama ulivyoimba ili kuwe na muingiliano mzuri wa sauti hata kama
unashirikisha vyombo vya muziki, na ni vema wana muziki wawe wenye uzoefu wa
kutosha ili kuleta milindimo mizuri ya vyombo zitakazoendana na wimbo wenyewe
bila kuwa na makosa ya mara kwa mara kwani utakuwa unawatoa au unawashusha
kutoka pale walipofikia.
 Tumekuwa na taratibu za sifa kuwa moto na watu kuchangamka lakini tunapoingia
kwenye kuabudu tunabadili mwelekeo na kuwa wa taratibu hii hali kama
isipoangaliwa vizuri kati ya watu wanaoongoza kipindi cha sifa na kuabudu unaweza
16 | P a g e
kuwagawa watu wengine wakamwabudu Mungu na wengine wasimwabudu Mungu,
ndo maana tunashauri uwepo na muingiliano mzuri wa nyimbo pamoja na sauti ili
kuhakikisha unawabeba wote katika uimbaji, na mazingira haya yanajengwa mapema
ili kufanya ibada hii iende vizuri. Tunashauri watu wanapokuwa wamechukua jukumu
hili wawe kwa sehemu hawapishani sana ili kutokuwa kikwazo kwa watu katika
kuitikia na pengine kuwatoa nje kabisa katika ibada ya kaubudu.
 Hapa utakuwa na kiongozi wa sifa na pengine kiongozi wa kuabudu ni vema kiongozi
wa sifa akaongoza katika sifa na kiongozi wa kuabudu akaongoza katika kuabudu na
hii inatokana na jinsi alivyozoea katika uimbaji, ingawa wapo wenye uwezo wa
kuongoza sifa pamoja na kaubudu. Kama mpangilio huu ukiwa mzuri basi tunategemea
kuwa na ibada nzuri yenye mfanikio makubwa katika swala la uimbaji. Si viongozi
wote wana ujasiri katika aina zote za uimbaji, na hii inatokana na uzoefu alio nao mtu
kwenye maeneo ya uimbaji.
 Yapo mazingira ya kiongozi wa nyimbo za sifa kutotambua uwepo wa Mungu au kuona
ni kawaida, lakini pia kiongozi wa nyimbo za kuabudu kutambua uwepo wa Mungu,
hali hii ikijitokeza italeta ukinzani, lakini kama watu hawa watakuwa na sifa moja au
wanakaribiana basi tutategemea uwepo wa Mungu kwa haraka na hivyo kufanya ibada
yetu ikawa yenye mafanikio makubwa. Kitu cha msingi ni vizuri kutofautisha kati ya
kiongozi wa nyimbo au kiongozi wa kuabudu ili kusaidia namna ya kuwatumia pale
panapohitajika.
 Mara nyingi kiongozi wa kuabudu anaweza kufanya yote anayofanya kiongozi wa sifa,
lakini ana uwezo wa kutambua uwepo wa Mungu na kuhamasisha watu katika
kumwabudu Mungu, lakini pia kuwafikisha watu katika uwepo wa Mungu. Pengine hii
inatokana na uelewa wa mtu juu ya nani wanaye mwabudu au kumwimbia, mara
nyingi kiongozi wa nyimbo lazima afikiri kwa usahihi kuhusu Mungu (Ni kitu gani
kinakuja akilini mwako unapomfikiria Mungu) na ni Mungu gani tunayemwabudu? Si
watu wote wenye kujiuliza maswali kama hayo na hiyo pengine ikatokana na uelewa
mdogo wa mtu juu ya Mungu na ukuu wa Mungu. Na ndiyo maana huko nyuma
nimeeleza sifa za hawa watu ili kuleta matokeo chanya na sahihi katika ibada ya sifa na
kuabudu.
 Tunapomwabudu Mungu ni lazima tujue Mungu ni nani kwetu na ana nafasi gani
katika maisha yetu lakini hatuwezi kumwabudu Mungu bila kujua ukuu wake na ikiwa
ni pamoja na majina yake “Isaya 9:6” Biblia inasema “maana kwa ajili yetu mtoto
amezaliwa, tumepewa mtoto mwanaume. Na uweza wa Kifalme utakuwa begani
mwake, Naye ataitwa jina lake Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa
milele, mfalme wa amani”. Hivyo ni vizuri kutumia majina ya Mungu katika kuabudu.

Ibada ya Kikristo ni zaidi ya kuwa katika hisia fulani au msisimko fulani tu, bali ni
zaidi ya hayo, kwani kuabudu kwetu kumejengwa juu ya mwamba imara wa Kweli juu
ya Mungu ni nani Zab 24:10 “Ni nani mfalme huyu wa utukufu?” 1 falme 8:27 “Tazama
mbingu hazikutoshi wala mbingu za mbingu.”

17 | P a g e
 Lazima ujue Mungu ni mwaminifu, mwema, mwenye neema, mwenye huruma
asiyebadilika, wa kushangaza, mwenye nguvu zote, anajua vyote, wa ajabu, mtakatifu,
mwenye rehema, mwenye hekima, kweli na wa milele yupo kila mahali, ni upendo
hakuna aliye kama yeye, Zab 89:6 “maana ni nani katika mbingu awezaye
kulinganishwa na Bwana? Ni nani afananaye na Bwana miongoni mwa malaika?
 Matokeo ya kujua majina na sifa za Mungu inatupa kuimarika zaidi katika imani na
kuelekeza mioyo yetu kwa Mungu hivyo kuwa na ibada nzuri ya kumwabudu Mungu
na hasa kutuongezea shauku na hali ya kumjua yeye tunayemwabudu kwa usahihi
zaidi (Yoh 4:22) tunaabudu tukijuacho
 Kama haya hayatafanyika basi maana yake tutakuwa tunadhoofisha ule ukuu wa
Mungu na kwa msingi huo dhana ya kuabudu kwetu haitakuwa na maana yoyote.
Ibada ya Sanamu ni kuwa na mawazo ya kumfikiria Mungu yasiyo ya hadhi ya Mungu.
Ili kudumisha dhana ya kuwa Mungu yuko juu ya yote na ameinuliwa sana ni lazima
kujua kwamba Mungu anaweza yote na ni kuabudiwa na kutukuzwa. Na hii si kwamba
tunamfanya yeye kuwa tu mkubwa bali lazima tumuone alivyomkubwa.

Kuabudu ni kuonyesha heshima kwa Yule aliye mkuu kuliko wewe, unapomwona aliye
mkuu kuliko wewe ndipo unaweza kuabudu, kwa kule kuelewa na kumfanya yeye
atawale maisha yako.

Baada ya kumalizia kipendele hiki ni vema ukajiuliza maswali yafuatayo: -


1. Je ni kweli unayo shauku moyoni mwako na ungependa kumwimbia au kutimiza
shauku yako kwa kumwimbia Bwana (Mungu Baba)
2. Nini kweli umeelewa tunaposema kuimba wimbo zaidi ya wimbo?
3. Unafikiri ni kitu gani kinachokujia kichwani mwako unapomfikiria Mungu.
4. Na ni jina lipi la Mungu unalolipenda katika majira ya Mungu.
5. Je ungependa kumtumikia Mungu katika huduma hii ya uimbaji au unafikiria zaidi
kuifanya biashara?

SEHEMU YA 6: TENDO LA KUABUDU KWA ASILI NI LA KIROHO


Unapokuwa kiongozi wa sifa na kuabudu ni vema au ni vizuri ukaelewa kuwa
kuabudu ni tendo la Kiroho au tendo la Roho wa Mungu. Tunapoenda kuabudu hatuendi ki
rahisi rahisi tu, ni hatua ambayo tunapaswa kujua kuwa ni muhimu sana katika maisha
yetu. Si tendo la kukamilisha tu ratiba au si tendo ambalo tunaishia kutumia akili zetu, hisia
au mwili pekeyake. Bali tunapaswa kufikiri zaidi ya hapa kwani maisha yetu yamejengwa
katika kumwabudu Mungu na wanaomwabudu Mungu lazima wamwabudu katika Roho na
kweli (Yoh 4;24) Mungu ni Roho nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika
Roho na kweli”

Ibada ya kuabudu ya kweli ni muhimu zaidi na ni ya ndani sana pengine zaidi ya kitu
kinachoonekana kwa nje, mfano muziki, mbinu za uongozi, au hata kikundi cha kuabudu.
Na hapa ndipo kiongozi wa sifa au kuabudu lazima awe makini sana na mwangalifu, kwani
18 | P a g e
yawezekana ukawa unashughulika na kulenga katika mambo nje ya kuabudu na kuacha
kushughulika na mambo ya rohoni. Maana yake unaweza kujikuta unalenga katika nyimbo
za kisasa kwa lengo la kuwafurahisha watu ili tu uonekane bora bila kutambua kuwa
kuabudu tunalenga kutatua matatizo ya watu na ndipo Mungu huonekana kwani yeye
hutazama hali ya ndani ya mioyo yetu.

JINSI YA KUCHAGUA NYIMBO ZA KUABUDU


Kwa kiongozi wa ibada ya kusifu na kuabudu anahitaji kuwa mwangalifu anapofikia
kuchagua nyimbo za kuabudu au kusifu na ndiyo maana tunapendekeza awe na maandalizi
ya kutosha, kwa sababu tendo hasa la kuabudu ni tendo linalomuhusu Roho wa Mungu na
roho zetu. Lazima uzingatie mambo yafuatayo: -
(a) Pamoja na kwamba tunaweza kuwa tunatumia vyombo vya kuabudia, lakini
vyombo hivi haviabudu, ila vinatusaidia katika kutupeleka kwenye kuabudu.
(b) Nyimbo za kuabudu hasa ndizo zinatakiwa kuwa vyombo vyenye mzigo na
kuabudu (yaani kubeba hazina za kiroho tunapoabudu).
(c) Mungu amekusudia muziki wa kuabudu ubebe vitu vyenye thamani kubwa ya
Kiroho. Na hii itatufanya kujimimina kwa Mungu wetu.

Hivyo maandalizi ya kiongozi wa sifa na kaubudu ni muhimu sana yenye orodha nzuri
za nyimbo na kwa mtiririko ulio bora katika kuabudu. Na maandalizi haya yatakupa nafasi
ya kuomba kwa Mungu na kumuuliza Mungu, juu ya mahitaji yetu ili kupata majibu kwake
ya orodha ya nyimbo utakazotu tumia katika ibada ya kuabudu. Na hii pamoja na kuomba
maombi ya pamoja na kwamba yawezekana nyimbo zikawa za kawaida lakini kitendo
chako cha kumsihi Mungu kitaleta mabadiliko makubwa katika ibada ya kuabudu, kwani
msimamizi mkuu atakuwa ni Mungu mwenyewe. Unaweza kukuta umetumia maneno
machache lakini yenye tija kubwa katika ibada ya kusifu na kuabudu. Watu wengine
hufikiri wingi wa maneno ni “vikorombwezo” vingi ndivyo vinaweza kuleta namna nzuri ya
kumwabudu Mungu na kusahau kuwa mwenye kuabudiwa ni nani, ingawa uelewa juu ya
unayemwabudu ni muhimu sana ili kujiachia kwake (mbele za Mungu).

Kwa kuwa tunakuwa tunalenga kukutana na Mungu katika Ibada ya kuabudu pengine
si vibaya kama utamuuliza mchungaji wako au msimamizi wako juu ya somo la mahubiri, si
kwamba orodha yako ya nyimbo lazima iegemee kwenye mahubiri la hasha, bali inaweza
kuwa njia nzuri ya kupanga orodha yako ya nyimbo pia, na hii hasa tunalenga watu watoke
na kitu pale wanapokuja kwenye ibada badala ya kutoka wakiwa watupu. Watu wanaweza
wasitoke na neno lakini wakatoka na wamejawa na furaha ya kumwabudu Mungu, hivyo
kutoona kama ibada ni kupoteza Muda.

WAKATI WA KUANDAA ORODHA YA NYIMBO


1. Hakikisha unaandaa orodha ya nyimbo zako za kutosha mapema ili upate nafasi ya
kufanya yafuatayo; -
(a) Hakikisha unajua nyimbo zote vizuri sana
19 | P a g e
(b) Unaweza kupanga na mchungaji au msimamizi wake
(c) Kuandaa muziki
(d) Kuandaa na kufanya mazoezi na kikundi cha Sifa na Kuabudu.

2. Baada ya maandalizi hakikisha unaendelea kujiachia na kujiamini mbele za Mungu


kwa kipindi chote katikati ya wiki kabla ya kufikia siku ya kuendesha ibada ya kusifu
na kuabudu ili kutojichanganya sana na mambo mengine na hii itakusaidia au
kutoruhusu adui kuingia katika ibada ya sifa na kuabudu.

3. Tendo hili la kuendelea kujianchia mbele za Mungu hasa katikati ya wiki kwa ajili ya
maandalizi yako, kutakufanya uwe karibu zaidi na Mungu na pengine Mungu atafunua
moyo wake wote kabla ya Ibada.

Kuna mbinu mbalimbali za kuandaa orodha ya nyimbo za kusifu na kuabudu.


Ni vizuri unapoandaa nyimbo hizi ukalenga yafuatayo: -
1. Tumia nyimbo zinazoeleweka na zinazoweza kuwasaidia watu kuweka mawazo yao
kwa Mungu.
2. Tumia nyimbo zitazowafanya watu wafurahi, washukuru waabudu na kukutana na
Mungu.
3. Tumia nyimbo zinazokazia ujumbe wa mahubiri kama itawezekana.
4. Tumia nyimbo zenye mtiririko unaofanana, zenye mtindo au mada zinazofanana
(zinazoendana)
5. Tumia nyimbo zinazojulikana na watu wote na zinaleta maana kwako, kwa timu yako
na washiriki kwa ujumla.
6. Nyimbo zinaweza kuwa mchanganyiko (yaani, tenzi, vitabu vya injili na mapambio
haijalishi ni za zamani au mpya

Mbinu ya kutumia mada inafanyika kwa kuwainisha orodha ya nyimbo na ujumbe au


kutumia mada maalumu kuandaa orodha yote ya nyimbo kwa mbinu ya upako (Yohana
2:27) “mafuta yale mliyoyapata kwake yanakaa ndani ya yenu. Habari za mafuta yake
yalivyo wafundisha kaeni ndani yake.”
- Omba Bwana hekima na umakini wa kusikia sauti yake, subiri na atajitokeza
(nyimbo zitakazojitokeza ndani ya roho yako zitaleta mgusu kwa watu na
kuwafanya wamwabudu Mungu bila shida, hivyo kuziandaa vizuri kwa ajili ya sifa
na kuabudu.
- Tafuta wimbo wa kuanzia pale ambapo Mungu anataka kuanzia (Unavyosukumwa
na Roho Mtakatifu)
- Imba na kuabudu kama ambavyo utafanya wakati wa ibada ya kusifu na kuabudu
(yaani wakati wa ibada)
- Zingatia kila Mungu alichosema nawe (roho yako) kupitia wimbo huo au nyimbo
hizo.

20 | P a g e
- Panaweza kufanyika mabadiliko kwenye orodha yako, lakini haina maana kuwa
mawazo ya mwanzo hayakustahili bali kunakuwa na hitaji maalumu pengine kwa
ajili ya watu wewe ni kuendelea na mchakato huo mpaka wakati utakapofika wa
ibada na hili ni eneo la utii ambalo litaleta mafanikio mazuri kwenye suala la ibada.
- Kama una nyimbo za ziada na pengine ungeona uzitumie basi ni vizuri kuzimaliza
mwishoni mwa ibada ingawa bado utapaswa kuzifanyia mazoezi ili ziendane na
nyimbo za awali mpaka zitakapokaa sawa, na wakati wingine Mungu anaweza pia
kurekebisha orodha hiyo wakati unapoimba.

Hapa unaweza kujiuliza maswali yafuatayo: -


1. Je ninatakiwa kufanya nini kabla ya kuandaa orodha ya nyimbo?
2. Je nyimbo zako ulizokusudia zitakuwa zimebeba hazina ya Kiroho?
3. Na je ibada ya kweli ya nyimbo za kuabudu huanza na nini?
4. Je ulijiandaa kabla ya kuandaa orodha ya nyimbo na ulijiandaaje?
5. Na tunapomsifu Mungu mara nyingi tunalenga nini kwa Yule tunayemwabudu?

SEHEMU YA 7: TIMU YA KUABUDU (PRAISE TEAM)


Timu ya kuabudu (Praise team) ni chombo cha kuwandaa na kuwatumia watu katika
kanisa ambao Mungu amewaita na kuwapa vipawa vya kulihudumia Kanisa katika eneo la
kusifu na kuabudu.
Kila mtu anaweza kuwa na mtazamo wake ni jinsi gani timu ya kusifu na kuabudu
inatakiwa iwe, lakini tunapokuja kwenye malengo hasa tunatakiwa yawe yenye mtazamo
mmoja wa kuwaunganisha watu na Mungu wanayemwabudu
Tunatambua kuwa uongozi wa timu kwa kawaida lazima uwe chini ya mchungaji
husika, lakini pia zipo faida nyingi Kanisa linapokuwa na timu ya kuabudu (worship team).
(i) Wanatoa msaada wa muziki na pia Kiroho, hivyo kuongoza washirika katika
kuimba na kumwabudu Mungu.
(ii) Timu inayoongoza sifa na kuabudu inakuwa inahamasisha washirika katika
kumwabudu Mungu na kuwaunganisha pamoja kitu ambacho kitaleta mvuto
na mwamko mkubwa kwa Kanisa katika ibada ya kuabudu.

MUUNDO WA TIMU YA KUSIFU NA KUABUDU


Kama nilivyokwisha elezea hapa nyuma kuna mawazo tofauti ya jinsi ya kuanzisha
timu hii ya kusifu na kuabudu. Mara nyingi timu hii uteuliwa na uongozi wa Kanisa, na hapa
itategemea hali halisi iliyopo, ingawa mtu yeyote anaweza kuanzisha timu ya kuabudu,
lakini lazima kuwepo na majadiliano mazuri Kati ya uongozi na huyo muhusika. Baada ya
kuanzisha tunategemea kati ya uongozi na huyo muhusika. Baada ya kuanzisha
tunategemea uongozi utakuwa hasa umelenga watu wale wenye uwezo au vipaji vikubwa
katika uimbaji na ambao watakuwa tayari kujiunga na team ya kuabudu. Ingawa mtu
21 | P a g e
yeyote anaweza kujiunga na timu ya kuabudu, itategemea hasa msukumo alio nao wa
kumwimbia Mungu katika idara hii ya kusifu na kuabudu. Na kabla ya kuanzisha ni vizuri
watu (washirika) wapate taarifa juu ya uanzishwaji wa timu ya kuabudu.

Lakini pia ni vizuri utafute taarifa zao kabla kwa kila mtu atakayetaka kujiunga na
timu ya kuabudu na hapa ni vizuri uzingatie historia yao Kiroho ili kama kuna marekebisho
basi yaweze kufanyika mapema. Na si vibaya kama utawajulisha watu wanaotaka kujiunga
ni kitu gani au sifa zipi wanatakiwa kuwa nazo, kwani si kila mtu mwenye msukumo
anaweza kujiunga na timu hii. Lazima uwaonyesha matarajio yanayotakiwa watakapokuwa
wamejiunga na timu na baada ya mchakato mzima wa kufahamiana vizuri basi ni vema
utaratibu uanze mara moja wa kuanza mazoezi na pengine hata elimu ambayo wengi wao
hawakuwa nayo kuhusu jambo hilo.

Waandaliwe Kiroho na kimwili yaani mwenekano wao katika uvaaji, tabia ili
wanapokuwa katika huduma hii na nje ya huduma wawe ni watu wa mfano wa kuigwa
wakiwa wamevaa Sura nzuri ya Ukristo (yaani wenye mauhusiano mazuri na Mungu).
Kama watakuwepo wenye ujuzi wa kutumia vyombo basi ni vema kama hawapo bado
wanaweza kuandaliwa ili waweze kutumia vyombo vya muziki vizuri na kwa weledi wa
hali ya juu katika kuwaunganisha watu na muziki.

SEHEMU YA 8. A: JE NI SAWA KIBIBLIA KUTUMIA VYOMBO VYA MUZIKI?


Pengine wapo watu wanaoweza kujiuliza swali hili, nah ii inatokana na baadhi ya
mafundisho yaliyopo sasa juu ya utumiaji wa vyombo vya muziki katika ibada au uimbaji
kwa ujumla.

Ukisoma katika biblia utakutana na neno “Zaburi” ni kitabu kimojawapo ndani ya


Biblia. Neno Zaburi ni muhimu sana na linapatikana katika Agano la kale’ na pia katika
Agano jipya.” Linamaanisha wimbo unaoimbwa au kwa kutumia vyombo vya Muziki. Na
sehemu nyingine limetumika kama kupiga kwa kutumia nyuzi za chombo”.

Katika Agano la kale, ukisoma zaburi 150 utaona pameorosheshwa baadhi ya


vyombo vya muziki vinavyoweza kutumika kama vile: - Tarumbeta, Kinubi, Zeze, matari,
nyuzi, filimbi, kinanda, matoazi n.k. lakini pia Katika Agano Jipya kila mara neno Zaburi
linapotumika, linaonyesha ni wimbo au nyimbo zinazoimbwa kwa kuchezwa
(kuchanganywa) na vyombo vya muziki. Unaweza kupitia vifungu hivi uone jinsi vyombo
vilivyotumika katika Biblia 1 Kor 14:26, 1 Kor 14:15, Yakobo 5:13, Efeso 5:19 na Kolosai
3:16. Hivyo kusema kuwa vyombo vya muziki havitakiwi bila shaka tutakuwa tumepungua
katika kutafasiri maandiko.

22 | P a g e
B: NAMNA YA KUWAFUNDISHA WANA TIMU AU KIKUNDI CHA KUSIFU NA
KUABUDU (PRAISE TEAM)
Tunaamini ufundishaji wowote una kanuni zake, hivyo hata kufundisha muziki
lazima ufuate kanuni au taratibu za kufundisha muziki, na hasa tungependa kuona kiongozi
wa kikundi cha Kusifu na Kuabudu kwa sehemu kubwa akiwa ni mwalimu na mtaalamu
wa muziki. Na kama hayupo basi wateuliwa wachache ambao watajifunza ili waweze kuja
kuwasaidia kikundi cha kuabudu. Pengine kuwa na wataalam ni vizuri zaidi ili waweze
kutoa maelekezo makini juu ya wakati gani unaofaa kucheza au kutocheza, na kwa weledi
zaidi pia kutoenda nje ya mtiririko wa vyombo. Ni vizuri kuwa na watu tofauti na vyombo
tofauti katika timu ili kuleta radha tofauti tofauti ya muziki na hii inaweza kuleta
muunganiko mzuri sana kati ya wahusika na washirika.

Lakini ni vizuri zaidi kwa kiongozi uliyepewa jukumu hilo la kukifundisha kikundi
cha kuabudu ukakumbuka jinsi Mungu alivyo mwema kwako (kumbuka Bwana ndiye
Mchungaji wangu) wakati unapofundisha. Zaburi 23:1 na katika Zaburi 78:72 tunaona ama
tunasoma Daudi kama mchungaji wa watu, kwa msingi huo Zaburi hizi zinaelezea jinsi
Mungu alivyomtunza na kumchunga Daudi na jinsi ambavyo Daudi alivyochunga watu
wake. Katika kujenga timu nzuri ya kuabudu lazima wawe ni watu wanaofamiana vizuri na
wenye umoja wa hali ya juu nje na ndani ya huduma, hii itajenga umoja mzuri katika
kufanya mazoezi, na umoja huu kama utakuwa wazi sana basi tunategemea kukua na
kujenga kikundi ambacho ni imara katika Kanisa. Lakini umoja wa ‘Kiroho” ni wa muhimu
zaidi na unakamilishwa kwa hatua ya pamoja ya kupata muda wa zaida wa kumwabudu na
kumwomba Mungu pia kusoma Biblia kwa pamoja.

Timu ya kuabudu lazima iwe na mwelekeo mmoja kama ambavyo Farasi ni lazima
wavute kuelekea upande mmoja au jinsi ilivyo kwa mme na mke lazima wafanye kazi kwa
mwelekeo na malengo yanayofanana, vinginevyo hakuna kitakachofanyika. Hivyo
tunaamini kama timu ya kuabudu itafanya kama hii mifano basi tunaamini itakuwa ni timu
bora na yenye nguvu katika kuwainjilisha watu katika huduma hii ya kusifu na kuabudu.

Kama tutachukua mfumo wa Bwana wetu Yesu Kristo basi tunaamini huduma hii
itakuwa yenye Baraka sana katika kuwaimarisha watu na kuvuna roho za watu wengi
ambao bado hawajamjua Mungu, lakini pia italeta uponyaji kwa watu wengi. Soma vifungu
vifuatavyo kukusaidia ni jinsi gani unatakiwa uwe: mark 10:45, wafilipi 2:5 math 20:25, 26

C. MAZOEZI YA TIMU YA KUSIFU NA KUABUDU


Kwa kuwa kila jambo ni lazima liwe na utaratibu wake ili liweze kwenda vizuri, basi
hata timu yetu ya kusifu na kuabudu ni vema ikawa na miongozo inayoiongoza au
kuongozwa.
(i) Ni vizuri ukawekwa muda ambao utafaa kwa ratiba ya watu walio wengi
(wanakikundi)

23 | P a g e
(ii) Mahudhurio kwenye mazoezi ni muhimu sana ili kuweza kuwa na
maandalizi mazuri au yaliyoshiba kwa ajili ya ibada.
(iii) Ni vizuri kwa kiongozi wa ibada kuwa na muda wa ziada wa kujiandaa
mwenyewe na mahali pakufanyia mazoezi, hivyo itakulazimu ufike mapema
kabla ya wanatimu ili kufanya maandalizi.
(iv) Mazoezi ni vizuri yakazingatia muda au ratiba mtakayokuwa mmejiwekea
kama kikundi ili kutoingilia ratiba nyingine kwa sehemu husika au ratiba
nyingine za makundi mengine katika Kanisa.
(v) Kiongozi lazima uwe na orodha ya wanakikundi ili kuweza kubaini ambaye
atakuwa hajaudhuria na jambo hili ni jema na la msingi ili kuwasiliana naye
pengine ni mgonjwa au amepata shida hivyo kuona namna ya kumsaidia.
Lakini pia ni taadhali kwa siku ya ibada kwani kama hakuwepo kwenye
mazoezi ni ukweli kwamba mnaweza kupishana katika uimbaji au mpangilio
mliyojiandaa wakati yeye hayupo.
(vi) Lisha kudni lako kwa kuomba kuabudu na kusoma neon la Mungu na
wajulishe matamanio yako kutokana na mazoezi.
(vii) Ni vizuri siku zote ukamaliza mazoezi kwa wakati na ukumbuke
kumshukuru kila mtu (mwanakikundi) kwa ajili ya kuwa mwaminifu
kutenga muda wake kwa ajili ya timu mwisho mmalize kwa kumshukuru
Mungu kwa maombi na kutawanyika.

 Hapa ningependa pia ujiulize maswali yafuatayo;


1. Je unafikiri ni njia ipi uliyogungua yenye kuleta ufanisi na umoja katika timu ya
kuabudu?
2. Je nje ya mitazamo hii niliyoielezea katika sura hii unafikiri una mtazamo au
ungependa kuongeza kitu kingine ambacho unaona ni bora zaidi katika kuleta
ufanisi katika timu ya kusifu na kuabudu?
3. Unafikiri upo umuhimu wa kuwa na timu ya kusifu na kuabudu au la?
4. Je kama wewe ni kiongozi wa kuabudu ungependa kutafuta njia mpya
unayoweza kuitumia katika kuitumikia timu yako kama Yesu alivyowatumikia
watu wake?
5. Kuna mitazamo miwili katika kuabudu: -
(1) Mtazamo wa asili: -
(i) waimbaji ndio uongozi ulio mbel, wachungaji, viongozi wa ibada na
timu ya kuabudu
(ii) Mrekebishaji (mrekebishaji ukumbini anaesaidia waimbaji wawe
katika utaratibu) ni Mungu
(iii) Watazamaji ni washiriki wanaotazama na kuitikia.

(2) Mtazamo wa Kifalme:


(i) Waimbaji wa washirika
(ii) Mrekebishaji ni uongozi

24 | P a g e
(iii) Mtazamaji ni Mungu Je wewe ungependelea mtazamo upi katika hii?

SEHEMU YA 9: KWANINI TUNAABUDU: -


Yawezekana kabisa yakawepo maswali kama haya miongoni mwetu juu ya kuabudu
na sababu hasa ya kumwabudu Mungu. Hapa nitaeleza kwa ufupi baadhi ya sababu za
msingi ni kwanini tunamwabudu Mungu
(i) Kwanza ni kuwasaidia watu kufika katika uwepo wa Mungu (kukutana na
Mungu kupitia ibada ya kumwabudu Mungu) maana kwenye kumwabudu
Mungu huwa anashuka.
(ii) Kuishangilia kazi iliyokamilishwa na Yesu Kristo pale msalabani kwa
kumtukuza na kumfurahia milele.
(iii) Kusaidia na kuwaandaa watu ili neno la Mungu liingie akilini na ndani ya
mioyo yao.
(iv) Kuchochea Karama za Roho Mtakatifu.
(v) Lakini tunamwabudu Mungu ili kumshinda adui wa roho zetu na kuimiza
umoja katika Kanisa na kuwakumbusha waamini matokeo ya siku za mwisho
ili kuwa tayari wakati wote.
(vi) Ni tendo la kumheshimu Mungu, kwani ndilo kusudi la kuumbwa kwetu.
 Lakini ni vema pia nigusie mahusiano Kati ya mchungaji na kiongozi wa Kusifu na
kuabudu (Praise team).
Kiongozi Mkuu wa Ibada ya Kuabudu
(i) Mchungaji ni msimamizi mkuu wa uhai wa ibada kuabudu katika Kanisa (ndani
ya Kanisa)
(ii) Kiongozi wa Praise Team yeye yuko chini ya mamlaka ya Mchungaji na ni
lazima awe anaweza kufanya kazi kwa karibu sana na Mchungaji kwa ajili ya
uhai wa Kanisa.
(iii) Mchungaji anatakiwa kumwelewa kiongozi wa ibada ya kuabudu na kiongozi
vivyo hivyo kwa kumshukuru Mchungaji na wito wake pia si vibaya hata
ukilijumlisha Baraza lake la wazee, hii ni njia ya kujenga mahusiano mazuri kati
yenu kwa ajili ya hii huduma na kanisa kwa ujumla.

Kama mambo haya yatakuwa ya kushirikishana basi tunategemea kwa sehemu


kubwa kuleta ufanisi mkubwa na uhai wa kiroho katika Kanisa. Kwani mara zote Mchungaji
anakuwa na matazamio kwa kiongozi wa ibada ya kuabudu na angependa yalete matokeo
chanya kila wakati hasa pale Kiongozi atakapotembea katika maono ya Mchungaji. Kiongozi
wa kuabudu wakati fulani anatakiwa aelewe kuwa yeye ndiye amebeba upako na maono ya
Mchungaji kwa kuwajibika kwa washirika chini ya maongozi ya Roho Mtakatifu ili kuleta
uhai kwa waamini kupitia uimbaji.

Na ndiyo maana nimetangulia kusema kuwa Kiongozi anapaswa kuwa na maandalizi


ya ziada yake binafsi lakini pia hata kuhakikisha vyombo vyote viko sawa kimziki na tayari
kwa kutumika katika ibada ili kuhakikisha kuwa kweli watu watakutana na Mungu. Kama
25 | P a g e
kutakuwa na wasiwasi wa vyombo kunaweza kukuweka katika wakati mgumu wakati wa
kuabudu, ingawa tunashauri maandalizi hasa ya Kiroho yakifanyika vizuri utakuwa katika
wakati mzuri hata kama kutatokea na shida fulani ya vyombo, kwani Mungu atakupa
uelekeo mzuri na ufahamu wa kutosha ili ujue unakoelekea au unapopaswa kuelekea.
Tunajua wakati mwingine wasiwasi unaohusiana na maisha yetu binafsi unaweza kuwa
kikwao, lakini lazima uelewe hasa unaemwendea katika kumwabudu ni nani hata katika
hali hiyo ya msongo wa mawazo. Tafakari na mshirikishe Roho Mtakatifu ili akupe ujasiri
kama tunvyoweza kusoma katika 1 Pet 5:7. Mungu atakupatia neema unayohitaji katika
kuongoza hata katika masumbufu hayo. Mungu atatumia hali hiyo kujidhihirisha na kukupa
ujasiri kwa kukujengea tabia ili uweze kushikilia zaidi uzima wake na upako kwa
kumtanguliza yeye ili ashughulike na matatizo yako.

MISINGI KWA AJILI YA HUDUMA YA KUSIFI NA KUABUDU


1. Umtegemea Mungu
(i) Fanya kazi na Roho mtakatifu ili kuwa na nyakati za ibada zilizojaa uzima na
Mungu.
(ii) Uombe na ujinyenyekeze mbele zake na umililie Mungu ili ashuke, ukijua kwa
sababu kuu ya kukusanyika ni kukutana na Mungu.
(iii) Unapaswa kuelewa kuwa kuabudu si tu kwa ajili ya kuwaingiza watu ibadani au
kuwandaa kwa mahubiri bali ni kuleta uponyaji kwa washirika ukijua ni hatua
ambayo pia ya kukutana na Mungu.

MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA KABLA YA KUANZA KWA IBADA YA


KUABUDU
(i) Mara zote unashauriwa kuwasiliana na Mchungaji kuhusu wanachotaka kwa ajili ya
ibada, hii ni vizuri kwani itakupa ufahamu kuwa ni wakati gani atataka ibada
irudishwe kwako badala ya kutegemea muda uliotengwa kwa ajili ya ibada ya
kuabudu na ni heshima pia kwa kiongozi wako (yaani Mchungaji)
(ii) Jiandae kwa ajili ya watu kumwabudu Mungu (Isaya 57:14)
(iii) Ni vizuri ujitahidi sana kuondoa vitu vile ambavyo vinaweza kuwaondoa watu
wasimwabudu Mungu (kwenye uwepo wa Mungu)
(iv) Andaa mazingira ya Kiroho kwa kuwaandaa watu katika kumwabudu Mungu
(v) Kwa kuwa utakuwa umeomba kabla na kuliweka eneo lote la kufanyia ibada pia
kuviweka vyombo vitakavyotumika vya muziki tunaamini utakapoanza ibada ya
kuabudu italeta uwepo wa Mungu na hivyo Mungu kukutana na watu.

KUHUSU NYIMBO ZA KUABUDU


 Hapa nianze kwa mfano huu: -
Kuendesha ndege ni sawa sawa na kuongoza wimbo wa kuabudu. Mfano (a) kupaa
kutoka uwanjani (b) kuwa angani (c) mwishoni ni kutua kwa ndege aridhini.

26 | P a g e
Hivyo kupaa ni ile hali ya utangulizi yaani kuanzisha wimbo na hali ya kuwa angani ni
kule kuimba wimbo na kutua kwa ndege aridhini ni kumalizia wimbo. Kama kiongozi
wa nyimbo za kuabudu atachukua mfano huu na kuufanyia kazi basi unaweza
kupangilia vizuri zaidi na kufikisha zaidi lengo la kuabudu kwa watu.

NAMNA YA KUFUNDISHA WIMBO MPYA


Ni vizuri kwa Kanisa na team ya kuabudu kuwa na nyimbo mpya lakini si vizuri sana
ukauweka kuwa wa kwanza katika arodha zako za nyimbo na ni vizuri uendelee mara kwa
mara ili watu wauzoee kabla ya kuleta wimbo mwingine mpya.

Tunajihusisha na ulimwengu usioonekana tunapokuwa tunaongoza ibada ya


kuabudu. Hivyo imani ni ya lazima 2 kor 4;18. (Tusiviangalie vinavyoonekana bali
visivyoonekana) uwezi kuviona, lakini umeitwa ili uviongoze na vionekane kupitia mioyo
yetu (imani). Nyimbo ni Jukwaa (chombo) cha kutuingiza kwenye kuabudu na kuipeleka
mioyo yetukatika ushirika na Mungu. Shirikiana na Mungu katikati ya nyimbo, kwani
kuabudu kunakuwa na kusudi la kuzungumza na Mungu. Mara nyingi Mungu hufunua
mipango yake “Kwa sehemu” mpaka atakapotaka kutuonyesha tena kulingana na
utaratibu unaouona yeye kwa mara nyingine. Na mengine zaidi huja hasa tunapotembea
naye yani mahusiano yetu na yake. (mith 16:9) inasema moyo wa mtu hufikiria njia yake,
bali Bwana huziongoza hatua zake. Mungu hatafuata njia zako au mipango yako hivyo ni
lazima sisi tufuate mipango yake hata kama utafanya mazoezi kwa sehemu kubwa
unatakiwa umruhusu Bwana kuongoza hatua zako.

NJIA NA KAZI ZA ROHO MTAKATIFU


(i) Fahamu kile anachokifanya Mungu na jihadhali, kuhusu kushikilia ajenda zako na
kukosa kile Mungu anachokifanya au anachokusudia kukifanya kwako.
(ii) Kubaliana na kile Mungu anachokifanya na uwe makini kwa uongozi wa Roho
Mtakatifu, kubali uongozi wa Roho Mtakatifu Isaya 30:21 “na Masikio yako yatasikia
neno nyuma yako, likisema njia ni hii ifuateni, mgeukapo kwenda mkono wa kulia na
mgeukapo kwenda mkono wa kushoto”

SEHEMU YA 10: HITIMISHO


NJIA ZA MUNGU
 Baadhi ya ajenda za Mungu tunazifahamu mapema na tunaweza kuziwekea mipango, na
baadhi ya mengine hatuwezi kuyafahamu mapema, lakini tunakuja kuzifahamu na
kuzikubali kadri mambo yanavyoendelea na kufunuliwe kwetu wakati wa ibada.
Baadhi ya mambo Mungu huyafanya kupitia sisi bila sisi kuwa na ufahamu.
 Mambo mawili ya kufanya baada ya ibada kumalizika: -
1. Kumbuka kuna vitu vinavyoathiri ibada ya kuabudu, baadhi ya vitu hivyo viko
katika uwezo wetu na baadhi haviko katika uwezo wetu.
2. Kumbuka kumshukuru Mungu na kumpa utukufu bila kujali ibada ya kuabudu
ilivyoenda, mtumaini Bwana na umwachie yeye matokeo. Amina.
27 | P a g e

You might also like