Professional Documents
Culture Documents
Tabia Zisizompendeza Mungu Zinazofanywa Na Vijana Katika Mahusiano
Tabia Zisizompendeza Mungu Zinazofanywa Na Vijana Katika Mahusiano
MUNGU ZINAZOFANYWA NA
VIJANA KATIKA MAHUSIANO
KABLA NA BAADA YA NDOA
Utangulizi:
Ziko baadhi ya tabia ambazo zimezoeleka na zimekomaa ambazo vijana wengi
huzifanya wengine wakiwa wanajua na wengine wakiwa hawajui kuwa ni
mbaya katika mahusiano na hazimpendezi Mungu kabisa. Miongoni mwa tabia
hizo ni kama ifuatavyo;
1. Tabia ya kukaa mda mrefu mpaka usiku wa manane.
Biblia inasema; “Kazi yenu ni bure, mnaoamka mapema, Na kukawia kwenda kulala…” Zaburi 127:2.
Roho ya unabii inasema; “Tabia ya kukaa muda mrefu hata usiku wa manane imezoeleka,lakini haipendezi Mungu,
hata kama ninyi nyote ni Wakristo.” UKV sura 149, uk. 407 aya 2.
Swali, Kwa nini Mungu hapendi kukaa hadi usiku wa manane? Roho ya unabii inasema; “Saa hizi zilizoendelea sana
huathiri afya,hufanya akili isijiandae kwaajili ya majukumu ya siku inayofuata, na zinamwonekano wa uovu.” UKV, uk.
407. pia 3T. 44,45.
USHAURI WA MUNGU KWAKO: “Ndugu yangu,ninatumaini utajiheshimu kiasi cha kutosha kuachana na uchumba wa
aina hii. Ikiwa kusudi lako ni kumtukuza Mungu,utatembea kwa uangalifu mkubwa…” 3T.44,45. UKV uk. 407 aya ya 2.
Vijana wengi leo wamejikuta katika mahusiano ya kuchati masuala ya mapenzi usiku na mchana na kupoteza muda ambao
wangeutumia kwa masomo, kazi za mikono au kwa shughuli zingine za maana.
5. Tabia ya kufanya urafiki na binti bila kuwahusisha wazazi. Si tendo jema Mungu anachukia. Uchumba wa
Siri haufai.
Tangu zamani uchumba wa Wazao wa wazee wetu wa Imani katika Biblia ulikuwa wa wazi bila kificho.
Roho ya unabii inasema; “Kijana wa kiume anayepata na kufurahia urafiki na binti bila kuwajulisha wazazi
wake,hatendi tendo jema Kikristo kwa binti huyo wala kwa wazazi wake. Kwa njia ya mawasiliano na mikutano ya siri
kijana wa kiume anaweza kuwa na mvuto juu ya akili ya binti;lakini kwa kufanya hivyo kijana wa kiume haoneshi
uungwana wala uadilifu wa roho ambayo kila mtoto wa Mungu anapaswa kuwa nayo.Ili kutimiza lengo lao,watenda
tendo lisilokuwa la kweli na wazi na lisilokidhi viwango vya Biblia,na kuonekana kuwa wasiokuwa wakweli kwa wale
wanaowapenda na wanaojaribu kuwa walinzi wao waaminifu….” UKV Sura 151, uk. 412,413.
Cont…
Nabii anasema; “Uchumba wa uongo unaendeshwa,na mawasiliano ya siri hufanyika, mpaka mapenzi ya binti
asiyekuwa na uzoefu,na mabaye hajui mwisho wa mapenzi hayo,kwa kiwango Fulani huhamishwa kutoka kwa wazazi
wake na kuwekwa kwa mwanaume ambaye mambo yake yanaonyesha baadaye kuwa hakustahili mapenzi yake. Biblia
inalaumu kila aina ya kukosa uaminifu, na inadai utendaji sahihi katika mazingira yote..” UKV ,uk.413 aya 3.
ZINGATIA SANA HILI; “Kama kuna suala ambalo linapaswa lifikiriwe
kwa tafakari tulivu na
uamuzi usiokuwa na msisimko, ni suala la ndoa.Ikiwa kuna wakati ambao Biblia
inahitajika kama mshauri, ni Wakati kabla ya kuchukua hatua inayounganisha watu
pamoja Maisha yao yote.” Nidhambi kuchezeana mioyo kwa kudanganyana. Mungu
hapendi ni tabia mbaya inayokuharibia utu na heshima yako.