You are on page 1of 4

BIBLIA NA WEMA WA BINADAMU

Sehemu ya Kwanza

Pd. Titus Amigu


Yaliyomo
Dibaji
Utangulizi …………………………………………………………………………
Sura ya Kwanza: Upendo ………………………………………………………..
Sura ya Pili: Furaha ………………………………………………………………
Sura ya Tatu: Amani ……………………………………………………………..
Sura ya Nne: Uvumilivu ………………………………………………………….
Sura ya Tano: Utu wema ……………………………………………………………
Utangulizi
Baada ya vitabu vyangu kuhusu makosa ya binadamu katika Biblia, nisingeliitendea haki
Biblia kama nisingeliandika kuhusu wema wa binadamu. Ninasema hivyo kwa sababu si
vyema kuiangalia Biblia kwa jicho lililokaa senta. Asikwambie mtu, Biblia ni neno la
Mungu lenye lengo maalum na neno la Mungu limekusudiwa kuwaadilisha watu ili
waishi maisha ya kikamilifu hapa duniani ili mwishowe wajiunge na Mungu katika uzima
wa milele. Kwa ukweli huo, Biblia inarekodi kwa ajili yetu yote mabaya na mema ya
mwanadamu kusudi wanadamu waoneshwe katika picha yao kamili.
Pande hizo mbili ndizo nilizozichukua kindakindaki. Ndipo katika kitabu BIBLIA NA
MAKOSA YA BINADAMU (Sehemu I-III) nilieleza kwa mapana makosa ya binadamu
ili binadamu tunaopumua sasa hapa duniani tusirudie upumbavu wa wenzetu anaokataza
Mungu wetu. Ndiyo kisa basi nikachambua kwa urefu orodha za maovu zilizomo katika
Marko 7:20-23; Rum 1:29-31 na Gal 5:19-21.
Lakini Mungu wetu ni mkamilifu na anataka sana tuwe wakamilifu kama yeye (Kum
18:13; 2 Sam 22:31; 1 Nya 28:9; Mt 5:48; Ebr 13:21). Hata hivyo ukamilifu wetu utakuja
kwa mazoezi. Ukamilifu wa Mungu hauna mashaka, isipokuwa ni huo wetu unaotiwa
majaribuni mara kwa mara hata Waswahili wakasema: “Hujafa, hujaumbika” yaani
wakati tunaishi chochote kinaweza kutokea. Kumbe basi ni hapo inapotujuzu binadamu
tualikane tupige jaramba tuwe wakamilifu. Kwa hali hiyo ninapaswa nigeukie upande wa
pili wa mambo kwa kitabu hiki BIBLIA NA WEMA WA BINADAMU (Sehemu I-III)
kusudi binadamu tunaopumua sasa hapa duniani tujifunze kila jema litakalotupatia
matunda yenye kudumu nyumbani kwetu kwa Mungu.
Basi kwa kukidhi lengo la kitabu hiki, awali ya yote nimeichukua orodha ya Gal 5: 22-23
panapotajwa mema yafuatayo: upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili,
uaminifu, upole na kiasi. Kishapo nikaioanisha orodha hiyo na orodha ya Flp 4:8 na 2
Pet 1:5-6. Nadhani sikufanya vibaya.
Katika Flp 4:8 tumeandikiwa na Paulo hivi, “Hatimaye, ndugu zangu, mambo yoyote
yaliyo ya kweli, yoyote yaliyo ya staha, yoyote yaliyo ya haki, yoyote yaliyo safi, yoyote
yenye kupendeza, yoyote yenye sifa njema, ukiwapo wema wowote, ikiwapo sifa nzuri
yoyote, yatafakarini hayo”.
Katika 2 Pet 1:5-6 tunasoma, “Kwa upande wenu katika imani yenu tieni wema, na katika
wema wenu maarifa, na katika maarifa yenu kiasi, na katika kiasi chenu saburi, na katika
saburi yenu utauwa, na katika utauwa wenu upendano wa ndugu na katika upendano wa
ndugu, upendo”.
Lakini katika orodha hiyo ya tatu limetokea neno lingine la ajabu ambalo kwalo ninapata
nguvu ya kuwahimizeni wote mnaomtafuta Mungu kutoacha tabia ya kujisomea na
kujielimisha katika mambo ya imani. Ni kwa neno hilo usomalo, “Katika imani yenu
tieni wema, na katika wema maarifa (2 Pet 1:5). Kwa kauli hiyo, kumbe haishauriwi
kumfuta Mungu katika umbumbumbu wa imani. Tusome, tusome tukajiongezee maarifa
katika imani yetu. Kwa ufupi, Biblia inatuambia imani na maarifa havipingani hata kwa
dawa.
Karibu basi usome kitabu hiki kusudi uujue vyema upana wa uwanja wa mazoezi ya
kuwa mkamilifu kwa kutenda wema pasipo kulegea.
Padre Titus Amigu,
Septemba 2010

Katika Flp 4:8

kweli
staha
haki
safi
kupendeza
sifa njema
wema

Katika 2 Pet 1:5-6

imani
wema
maarifa
saburi
utauwa

You might also like