Professional Documents
Culture Documents
Jinsi Mungu Anavyojibu Maombi
Jinsi Mungu Anavyojibu Maombi
UTANGULIZI
1. Maombi ni jambo ambalo limekuwa likisisitizwa
sana na viongozi wa kanisa. Msisitizo kuhusu maombi
ulikuwepo hata katika siku za Yesu ambapo Yesu
aliwahimiza sana wanafunzi wake kuomba.
2. Kwa mkristo jambo la maombi halikupaswa kuwa
jambo la kusisitizwa. Ni sawa na swala la kula, hakuna
mtu mzima kiafya anayesisitizwa kula chakula. Yeye
mwenyewe atapata njaa itakayomsukuma kuhitaji
chakula.
3. Vivyo hivyo hata katika afya ya kiroho ukiona mtu
anasisitizwa kufanya maombi basi kuna hitilafu katika
kiroho chake. Watu hawaombi kwa sababu aidha
hawaamini kuwa maombi hujibiwa au hawajui jinsi
Mungu anavyojibu maombi na hivyo kuwafanya
kutokuwa na imani na maombi.
4. Mkristo hapaswi kudhani kuwa Mungu hatusikii
tunapoomba bali anapaswa kufahamu kuwa kuna namna
nne ambazo Mungu hujibu maombi. Na ndiyo asubuhi ya
leo tumeona ni vyema kujifunza JINSI AMBAVYO
MUNGU ANAVYOJIBU MAOMBI.
1
I. MUNGU KUJIBU NDIYO
Mara nyingi Mungu hujibu ndiyo pale
tunapomwomba. Zaburi 118:5
5
Katika shida yangu nalimwita Bwana; Bwana
akanijibu akaniweka panapo nafasi.
Na pia Zaburi 138:3
3
Siku ile niliyokuita uliniitikia, Ukanifariji
nafsi kwa kunitia nguvu.
Zipo sababu zinaweza kumfanya Mungu kujibu
ndiyo kwenye maombi yetu. Baadhi ya sababu ni
ifuatavyo:
a. Kumtanguliza Mungu katika maisha yetu.
Mathayo 6:33
Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na
33
3
II. MUNGU KUJIBU NDIYO LAKINI SUBIRI
Kuna wakati Mungu husema ndiyo kwa maombi yetu
lakini lazima iendanae na majira yake. Mhubiri 3:1,
11
1
Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati
kwa kila kusudi chini ya mbingu. …….. 11Kila
kitu amekifanya kizuri kwa wakati wake; tena
ameiweka hiyo milele ndani ya mioyo yao; ila
kwa jinsi mwanadamu asivyoweza kuivumbua
kazi ya Mungu anayoifanya, tangu mwanzo
hata mwisho.
Hivyo wakati Mungu anasema ndiyo lakini subiri
tunaweza kudhani kuwa Mungu amesema hapana.
Kwa sababu hiyo hatupaswi kukata tamaa tunapaswa
kuendelea kumlilia. Luka 18:7
Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule
7
4
Maana Mungu si dhalimu hata aisahau
10
24
Kwa maana tuliokolewa kwa taraja;
lakini kitu kilichotarajiwa kikionekana,
5
hakuna taraja tena. Kwa maana ni nani
anayekitarajia kile akionacho?
Pale Mungu anaposema ndiyo lakini subiri ni wakati
tunapaswa kuwa wavumilivu na kutumainia neema
yake. Tunapaswa kutumainia neema ya Mungu hata
pale jibu la Mungu linakuwa vinginevyo:
III. MUNGU KUJIBU NJE YA MATARAJIO
Kuna wakati Mungu hujibu tofauti na kile
tunachotarajia. Tunapaswa kufahamu kuwa mawazo
ya Mungu na njia za Mungu ziko tofauti na zetu.
Isaya 55: 8 – 9:
8
Maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala
njia zenu si njia zangu; asema Bwana. 9Kwa
maana kama vile mbingu zilivyo juu sana
kuliko nchi, kadhalika njia zangu zi juu sana
kuliko njia zenu, na mawazo yangu kuliko
mawazo yenu.
Kwa mfano unaweza ukamwomba Mungu nguvu na
uvumilivu lakini Mungu akakupitisha kwenye
mapito. Wafilipi 1:29 – 30.
29
Maana mmepewa kwa ajili ya Kristo, si
kumwamini tu, ila na kuteswa kwa ajili yake;
30
mkiwa na mashindano yale yale mliyoyaona
kwangu, na kusikia kwamba ninayo hata sasa.
6
Mapito ya majaribu hayo hukujengea nguvu na
uvumilivu ambao ulimwomba Mungu. Rumi 5: 3 – 4.
3
Wala si hivyo tu, ila na mfurahi katika dhiki
pia; mkijua ya kuwa dhiki, kazi yake ni kuleta
saburi; 4na kazi ya saburi ni uthabiti wa moyo;
na kazi ya uthabiti wa moyo ni tumaini;
Hatupaswi kumwekea Mungu mipaka kama
tunavyowaza katika mawazo yetu. Hii ni kwa sababu:
a. Mungu ana uwezo wa kufanya zaidi ya
tuwazavyo kama tunavyoweza kusoma katika
Waefeso 3:20
20
Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya
mambo ya ajabu mno kuliko yote
tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya
nguvu itendayo kazi ndani yetu;
b. Lakini pia sisi hatujui kuomba
inavyotakiwa:
26
Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu
wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi
itupasavyo, lakini Roho mwenyewe
hutuombea kwa kuugua kusikoweza
kutamkwa.
7
Kumwekea Mungu mipaka katika kujibu
maombi yetu ni sawa na kujiwekea mipaka ya
majibu yetu. Mfano pale tunapoomba kwa ajili
ya wagonjwa. Je huwa tunaomba Mungu
afanikishe matibabu ya mgonjwa? Kama
tukiomba hivyo tunakuwa tunampangia Mungu
namna ya kufanya ambapo yeye ana njia zaidi ya
tuwazavyo. Ni vizuri kumwomba Mungu
awafanye uponyaji kwa namna atakavyo yeye.
Tunapomwomba Mungu, inatupasa tutumaini kuwa
atafanya katika namna anavyoona inafaa. Hata hivyo
tunapaswa kuendelea kumtumaini Bwana hata
pale…..
IV. MUNGU KUJIBU HAPANA
Kuna wakati Mungu hujibu hapana kwa maombi yetu
Yakobo 4:3
Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu
3
10
HITIMISHO
Wapendwa zipo namna mbalimbali ambavyo Mungu
hujibu maombi yetu baadhi namna hizo ni hizi ambazo
tumejikumbusha leo; kwamba hujibu ndiyo, Mungu
hujibu ndiyo lakini subiri, Mungu kujibu nje ya matarajio
yetu na pia Mungu kujibu hapana.
Vyovyote Mungu atakavyojibu maombi yetu tunapaswa
kufahamu kuwa majibu yake kwa ajili ya mema kwetu.
Hivyo basi hatupaswi kukakta tamaa katika kumwomba
Mungu maana yeye ni Mwema na atatupatia mema kwa
ajili ya ustawi wetu. Zaburi 6:6;
9
Bwana ameisikia dua yangu; Bwana
atayatakabali maombi yangu.
11
Wimbo:
Unaweza kufanya, Unaweza kutenda, Mambo makubwa
zaidi ya niombavyo x 2
Mambo makubwa zaidi ya niombavyo x 2
Zaidi ya niombavyo, zaidi nitakavyo unaweza kufanya,
unaweza Yesu
Zaidi ya tarajio, zaidi ya niombavyo unaweza kufanya
unaweza Yesu.
Mambo makubwa zaidi ya niombavyo x 2
12