Professional Documents
Culture Documents
Kuna Nguvu Katika Mawazo Yetu
Kuna Nguvu Katika Mawazo Yetu
(SEHEMU YA 3)
3
Kwa hiyo, hata katika suala la kuwaza au kutafakari, bila msaada
wake, hatuwezi kitu. Kama kuwaza tu kwa namna inayofaa
hatuwezi, sembuse kuyafanya hayo mawazo yetu yatupatie
shauku za mioyo yetu? Agizo la muhimu analotupa Bwana,
tunalopaswa kulizingatia ni kuwa, “Mtumaini Bwana kwa moyo
wako wote, wala usizitegemee akili zako mwenyewe.” (Mithali
3:5).
Kutofautisha nia
Ndani mwetu kuna nia za aina mbili. Biblia inasema, “Kwa kuwa
nia ya mwili ni mauti; bali nia ya roho ni uzima na amani.”
(Warumi 8:6). Kwa hiyo, kuna nia ya mwili na nia ya roho. Nia ya
mwili ni nia ambayo hujificha sana kiasi kwamba wakati mwingine
ni vigumu kuigundua. Bila shaka umeshawahi kukutana na hali
zifuatazo: