You are on page 1of 2

UTUME WA KWANZA :SHAMBULIZI LA FAMILIA

FUNGU KIONGOZI:WAEFESO 6:4


WIMBO:15 & 110.
=Mafungu andamizi;Yoshua 24:15 ,Torati 6:6-7 ,Mwanzo 18:19
1.Kuna mambo matatu ambayo shetani hushambulia kwa nguvu na
uhakika,ambayo;ndoa,sabato,matoleo (uchoyo wa kurudisha ZAKA na
kutoa SADAKA)
1. Ni rahisi kuhubiri nje kuliko katika familia zetu
2. Tunapata umaarufu nje kuliko katika familia zetu
3. Yesu anataka famila zetu ziongolewe na hivyo ndivyo
tutakapowavuta wengine kwa Yesu
=Mungu kupitia watumishi wake anahitaji matengenezo makamilifu na
jukumu hilo takatifu la utume wa familia limekabidhiwa kwa wazazi.Hao
watatoa hesabu kwa ajili ya ukengeufu wa familia zao.
=BWANA ameshushwa na kuvunjiwa heshima na wasioamini kwa ajili ya
mienendo mibovu ya familia zetu
=Shetani anajua kama familia zitajiweka imara katika kumtafuta MUNGU
wengi wataongolewa na kwamba atakosa mtu wa kumpoteza.
ROHO YA UNABII

=Wale ambao wanafuata mielekeo yao wenyewe,katika upendo wa


kizembe kwa watoto wao,wakiwaendekeza katika kupenda tamaa zao za
ubinafsi, na wala hawatumii mamlaka ya Mungu kukemea dhambi na
kusahihisha uovu,wanadhihirisha kwamba wanawaheshimu watoto wao
walio waovu kuliko kumheshimu Mungu.Wana hamu zaidi ya kukinga
hadhi zao kuliko kumtukuza Mungu,wanatamani zaidi kuwapendeza
watoto waokuliko kumpendeza BWANA na kutunza huduma Yake kutoka
katika kila mwonekano wa uovu (Wazee na Manabii,Uk 229).
-Mfano wa wale wanao hudumu katika mambo matakatifu unapaswa
kuwa ni ule ambao unawavutia watu kuwa na kicho kwa Mungu na hofu
ya Kumkosea (wazee na manabii uk 231)
-Hajuna laana kubwa juu ya kaya kuliko kuruhusu vijana kufanya
watakavyo.Wakati ambapo wazazi wanakidhi kila hitaji la watoto wao na
kuwaendekeza katika kile ambacho wanajua si cha kuwafaa,punde watoto
wanapoteza heshima zote kwa wazazi wao,heshima zote kwa mamlaka ya
Mungu na ya wanadamu,na wanasababishwa kuwa watumwa kama
shetani apendavyo.Athari za familia ambayo haikudhibitiwa vyema
husambaa na kuleta hasara kwa jamii.Hujikusanya kuwa wimbi la uovu
ambalo linawadhuru familia,jumuiya,na serikali mbalimbali (wazee na
manabii uk 230).

You might also like