You are on page 1of 2

WATU WA KUANGAMIA/MAISHA YA KIDINI

WIMBO:172/171

FUNGU:TITO 1:16
“Wanakiri ya kwamba wanamjua Mungu,bali kwa matendo yao wanamkana,ni wenye
machukizo,waasi,wala kwa kila tendo jema hawafai.”

“Matokeo ya kujua tu maneno ya dini pekee yake huleta chuki kwa wale walio na
imani ya kweli.Sura yenye giza zaidi ni ile inayohusu maasi makuu yaliyotokana na
wenye dini…Watu wengi hujidai kuwa ni wenye dini,lakini dini yao hiyo
isipowafanya kuwa waaminifu hasa,wenye utu
wema,wavumilivu,wastahimilivu,wenye mawazo ya Kimungu,huwa laana kwao
tu,na kwa mivuto yao huwa balaa kwa ulimwengu.”(Tumaini La Vizazi Vyote
UK,166-167)

2TIMOTHEO 3:5 “Wenye mfano wa utaua lakini wakikana nguvu Zake hao nao
ujiepushe nao.”

“Huonekana kuwa na mfano wa dini,isiyokuwa na imani,wala toba ya kweli.Hukiri


kwamba wanamjua MUNGU lakini hukana nguvu zake.Maneno Kristo aliyotamka
kwa mtini,alisema kuwa mtu anaetenda dhambi kiwazi ana heri kuliko mtu anaedai
kuwa anamtumikia MUNGU bila kuzaa matunda ya haki,yanayoonesha utukufu
Wake”(Tumaini la Vizazi Vyote UK,327)

MATHAYO 23:15” Ole wao waandishi na mafarisayo wanafiki!kwa kuwa


mnazunguka katika bahari na nchi kavu ili kumfanya mtu mmoja kuwa mwongofu;na
akiisha kufanyika,mnamfanya kuwa mwana wa jehanam mara mbili zaidi kuliko ninyi
wenyewe.”

“Niliona kundi kubwa sana la watu wakitangaza jina la kristo,lakini Mungu


hakuwatambua kama watu wake.Hakuwa na furaha nao.Shetani alionekana
kuwafanya watu waamini tabia ya kidini na alinuia sana kuwafanya watu wajidhanie
kuwa walikuwa wakristo.Alikuwa na wasiwasi kwamba watu wangeweza kumwamini
Yesu,kusulubishwa kwake na ufufuo wake.Shetani na malaika zake wenyewe
huamini kabisa haya yote kabisa na kutetemeka.Lakini imani hii isiposababisha
matendo mema,na kuwaongoza wale wanaoamini kuiga maisha ya kristo ya
kujikana nafsi,shetani anakuwa habughudhiwi,kwa maana wamejipatia jina la ukristo
tu,wakati mioyo yao bado ni ya asili,hapo shetani anaweza kuwatumia katika kazi
yake kwa ufanisi zaidi kuliko kabla ya kuamini.Wakificha sura zao bandia kwa jina la
ukristo,hawashughulikii tabia zao za asili zisizotakaswa,na tamaa zao mbaya
zisizotiishwa.Hili linawapa nafasi wasioamini kumlaumu Kristo kwa dosari zao,na
kuwafanya wale walio na dini safi na isyo na mawaa kukosa heshima.”(Maandiko Ya
Awali UK,230)

LUKA 18:9-13 “Akawaambia mfano huu watu waliojikinai ya kuwa wao ni wenye
haki,wakiwadharau wengine wote.Watu wawili walipanda kwenda hekaluni
kusali,mmoja farisayo na wa pili mtoza ushuru.Yule farisayo akasimama akiomba
hivi moyoni mwake;Ee MUNGU nakushukuru kwa kuwa mimi si kama watu
wengine,wanyang’anyi,wadhalimu,wazinzi,wala kama huyu mtoza ushuru.Mimi
nafunga mara mbili kwa juma,hutoa zaka katika mapato yangu yote.Lakini mtoza
ushuru alisimama mbali,wala hakuthubutu hata kuinua macho yake mbinguni,bali
alijipiga piga kifua akisema ,Ee MUNGU uniwie radhi mimi mwenye dhambi.”

“Dini ya farisayo haigusi roho.Hatafuti kuwa kama MUNGU katika tabia yake,moyo
uliojawa na upendo na rehema.Analotaka ni dini ihusikanayo tu na mwonekano wa
nje.Haki yake ni ya kwake mwenyewe binafsi matunda ya kazi zake mwenyewe na
zikipimwa kwa vipimo vya kibinadamu…Farisayo na mtoza ushuru huonesha
makundi makuu mawili ya wale wanaokuja kumwabudu MUNGU.”(Lulu Za Uzima
UK,98-99)

“Sheani daima anatafuta kuwadanganya watu na kuwaongoza kuiita dhambi kuwa


haki na haki kuwa dhambi.Ni kwa kiasi gani kazi yake imekuwa ikifanikiwa!Ni mara
ngapi lawama na shutuma zinatupwa kwa watumishi wa Mungu waaminfu kwa
sababu wanasimama kwa ujasiri kuutetea ukweli! Watu ambao ni mawakala tu wa
shetani wanasifiwa na kupongezwa,na hata kutazamwa kama wafia dini,wakati wale
ambao wangepaswa kuheshimiwa na kutegemezwa kwa ajili ya uaminifu wao kwa
Mungu,wameachwa kusimamama peke yao,katika lawama na tuhuma.Kazi ya
kuifanya bandia kuwa kweli,na uongo kuwa utakatifu bado inaendelea kutenda kazi
yake ya udanganyifu.Roho ile ile inadhihirika kama ilivyokuwa katika nyakati za
Luther kwa kutumia mitindo mbali mbali kuzipotosha akili kutoka kwenye maandiko
na kuwaongoza watu kufuata mawazo ,fikra na maono yao wenyewe badala ya kutoa
utii kwa sheria ya Mungu.Hii ni mbinu mojawapo za shetani zenye mafanikio
makubwa sana za kushutumu utakatifu na ukweli.”(Pambano Kuu UK,192-193)

“Kuna wengi leo ambao wako katika udanganyifu unaofanana na huo,kwa maana
huku wakiwa na mwonekano wa utakatifu mkuu,sio watendaji wa neno la
Mungu.Nini kinaweza kufanyika ili kuwafungua macho watu hawa wanaojidanganya
wenyewe isipokuwa kuwadhihirishia ,mfano wa ucha Mungu wa kweli na sisi
wenyewe tusiwe wasikiaji tu bali watendaji wa amri za Bwana,hivyo kuakisi nuru ya
usafi wa tabia kwenye njia yao.”(Imani Na Matendo UK,117)

UFUNUO 3:15 “Nayajua matendo yako,ya kuwa hu baridi wala hu moto,ingekuwa


heri kama ungekuwa baridi au moto.”

“Wakristo nusu nusu ni wabaya mno kuliko makafiri;maana maneno yao


yadanganyayo na msimamo wao usioelekea upande wowote huwafanya wengi
kupotea.Kafiri anaonesha msimamo wake.Mkristo aliye na uvuguvugu anadanganya
makundi yote mawili.Yeye si mlimwengu mzuri,wala yeye si mkristo mzuri,shetani
anamtumia kufanya kazi ile asiyoweza kufanya mtu mwingine yeyote.”…(7BC 963)

WITO
“Tunahitaji kuongoka kama walivyofanya wayahudi.Kama ukiona nuru
ndogo,hupaswi kurudi nyuma na kusema,nitasubiri mpaka ndugu zangu wawe
wameiona.Kama ukifanya hivyo utaendelea kuwa gizani.”( Imani Na Matendo UK,78
)
“Injili haifanyi maafikiano na uovu.Haiwezi kutoa udhuru kwa dhambi.Dhambi za
siri lazima ziungamwe kwa Mungu kwa siri;bali kwa dhambi za wazi toba ya wazi
huhitajika.”(Tumaini La Vizazi Vyote UK,458)

You might also like