You are on page 1of 29

KIKUNDI KIDOGO—NIA na ROHO MOJA

KIKUNDI KIDOGO
—NIA na ROHO MOJA

[Huduma na isajiliwe mbinguni]

Baadhi ya Rejea ni:


 Ellen Gould White Books
 John Mallison, The Small Group Leader: A manual to develop
vital small groups.

Vifupisho: 2ATH (Akili, Maumbile ya Tabia na Haiba, Juzuu ya 2)


(Mind, Character and Personality, Volume 2)

Musa L. Budodi
Oղe-Souɬ Audience Ӎinistry
Kagongwa, Kahama
+255-784-825-660
KIKUNDI KIDOGO—NIA na ROHO MOJA

UTANGULIZI
MWITO WETU
"Kristo hachagui malaika ambao kamwe hawajaanguka kuwa
wawakilishi wake, bali wanadamu, watu wenye hisia sawa na
zile za hao wanaotafuta kuwaokoa.” E. G. White, Tumaini la
Vizazi Vyote uk. 296.4
“Sote tumefungwa pamoja katika wando mkubwa wa
ubinadamu, na lo lote tunaloweza kufanya kuwanufaisha na
kuwainua wengine kutaakisi mibaraka kwetu wenyewe.
Sheria ya kutegemeana inafunga kila tabaka katika jamii.” E.
G. White, Wazee na Manabii uk. 534.4

Sifa za watendakazi pamoja na Mungu


 Wameitwa toka katika ubize wa shughuli za dunia hii
zinazofyonza akili na fikra zao.
 Wale ambao hawajasoma kabisa katika shule za wanadamu.
 Watokao katika kazi za chini za maisha.
 Watumishi na wenye nyadhifa kubwa katika serikali na taasisi za
wanadamu.
 Wanaojifunza kumtumikia Bwana
 Walio tayari kushiriki huzuni za wanadamu wenzao.
 Wasio na ama mashaka wala kutokuamini uweza wa Mungu.
KIKUNDI KIDOGO—NIA na ROHO MOJA

—KIKUNDI KIDOGO—
KWA AJILI YA KRISTO NA KWA AJILI YA MAISHA YA
KIMWILI
Kwa kawaida, ili kufikia lengo kwa urahisi kunategemea si idadi kubwa
ya watu bali kikundi kidogo kilichonuia na kuazimia, wanaoweza
kukutana toka katika maeneo walikotawanyika. Mungu ndiye
huanzisha hatua, na kikundi kidogo huwa hai pale Roho Mtakatifu
anapofanya kazi ndani ya kila roho inayowiwa hivyo.
‘Bwana asipoijenga nyumba Waijengao wafanya kazi bure.
Bwana asipoulinda mji Yeye aulindaye akesha bure’ (Zaburi
127:1). ‘Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, bali ni kwa roho
yangu, asema Bwana wa majeshi.’ (Zekaria 4:6).
‘Uundaji wa vikundi vidogo kama msingi wa kuwafikia
wengine umeonyeshwa kwangu na Yule asiyekosea.’—E. G.
White, Testimonies vol. 7, uk. 21, 22
‘Ni muhimu kuwa kazi hii itafanyika kwa shughuli za watu
binafsi. Ndivyo Kristo alivyofanya. Kazi yake kubwa ilifanyika
kwa njia ya mjadala wa ana kwa ana. Aliheshimu sana
mazungumzo yake pekee na mtu mmoja mmoja. Mara nyingi
kupitia kwa huyu mmoja ujumbe ulienezwa kwa maelfu.’ E.
G. White, Vielelezo vya Mafundisho ya Kristo uk. 229.1

—KWA KIKUNDI KIDOGO—

JISHUGHULISHE

Mara nyingi hisia za kuvunjika moyo hutokana na kukaa sana pasipo


kazi yo yote. Mikono na akili vinapaswa kushughulishwa, kupunguza
mizigo ya wengine; na wale waliowekwa kwa kazi hiyo
watajinufaisha wao wenyewe pia. Kukaa bila kujishughulisha na cho
KIKUNDI KIDOGO—NIA na ROHO MOJA

chote hutupa wakati wa kuwaza huzuni za kufikirika tu, na mara


nyingi wale ambao hata hawana magumu na majaribu ila tu
wanayawaza, basi wanayakaribisha katika wakati ujao. E. G. White,
The Signs of the Times, October 23, 1884. (Counsels on Health, 629).
2ATH 631.5
—KIKUNDI KIDOGO—
WAKATI WA KRISTO
‘Akaweka watu kumi na wawili, wapate kuwa pamoja naye,
na kwamba awatume kuhubiri, tena wawe na amri ya kutoa
pepo’ (Marko 3:14, 15)
Kwa njia hii, wengi walifikiwa na injili. Katika hao wachache, Yesu
alichagua kujenga ndani ya maisha ya hao wachache misingi thabiti
ambayo ingekuwa nguzo ya ufalme wake na kuweza kukabiliana na
dhoruba ambayo ingewajia. Akiwa na nia ya kuuokoa ulimwengu
wote, alitumia muda mwingi akiwa na kikundi kidogo ambacho
aliazimu kukifundisha namna ya kupendana na kutawanya habari hiyo
njema ya pendo la Mungu kwa ulimwengu.
Bwana wetu alikusanya kikundi kidogo cha watu ambao kila mmoja
alikuwa na tabia na silika anuwai. Simoni Zelote aliyekuwa mzalendo
mkali wa taifa lake, Mathayo aliyekuwa mwenye wadhifa serikalini,
Petro mwenye harara (mwepesi wa hasira), Yohana mtu wa maombi
sana, Andrea mtu mwenye imani tulivu, na Thomaso mgumu wa
kuelewa na kuamini; Kikundi hiki kilipatana tabia katika Kristo.
"Wanafunzi wote walikuwa na mapungufu makubwa sana
wakati Yesu alipowaita kuja katika utumishi wake. Hata
Yohana, aliyekuwa karibu sana na Yeye aliye mpole na
mnyenyekevu, kwa asili hakuwa mpole na mnyenyekevu.
Yeye na ndugu yake waliitwa "wana wa ngurumo." Wakati
walipokuwa na Yesu, kitendo chochote cha dharau
kilichoonyeshwa kwa Yesu kilidhihirisha hasira yao na
magomvi. Hisia ovu, kisasi, roho ya ukosoaji, vyote vilikuwa
KIKUNDI KIDOGO—NIA na ROHO MOJA

ndani ya mwanafunzi yule. Alikuwa na majivuno, na


akipenda kuwa wa kwanza katika ufalme wa Mungu. Lakini
siku kwa siku, kwa mkinzano na roho yake ya fujo, aliona
huruma na subira ya Yesu, na alisikia mafundisho yake ya
unyenyekevu na uvumilivu.” E. G. White, Tumaini la Vizazi
Vyote uk. 295.5
Machoni pa ulimwengu, baadhi walikuwa watu wenye vyeo vya juu
na wengine wa kawaida tu katika hadhi kijamii. Yesu hakutafuta
uwezo wa watu bali upatikanaji wa watu. Ingawa wengi wa
wanafunzi walikuwa vijana wa kati ya miaka 20 na 40 lakini hakujali
umri. Akiwa pamoja na kikundi hicho kidogo, alikula, alisema, alilala,
alitembea, aliabiri, alivua samaki na aliomba pamoja nao. Alitumia
muda mwingi na kikundi hicho kidogo kuliko watu wengine.
Yesu alitumia ukufunzi na uanagenzi; yaani alisimika kikundi kidogo
kuhubiri na kuwa na mamlaka; hakuiweka kazi ya uinjilisti katika
mikono yake tu bali alichagua kushirikiana huduma yake pamoja na
wengine, siyo kuikabidhi kwa watu ili wamsaidie kutambua mahitaji
ya watu, bali kuibua viongozi wa baadaye.

—KWA KIKUNDI KIDOGO—

Mambo muhimu kuyazingatia


Ibada: Zaburi 29:2; 95:6; 103:1; Wafilipi 3:3.
Ushirika wa pamoja: Sote tunategemeana, toka kwa aliye mdhaifu
hadi kwa aliye imara. Kwa ushirika wa pamoja tunatiana moyo katika
mapitio ya maisha, tunaelekezana, tunaomba, tunajisalimisha,
tunasameheana, kusaidiana na kutiana shime. Katika kikundi kidogo,
asiachwe mtu atembee katika barabara akiwa peke yake (Waebrania
10:25).
KIKUNDI KIDOGO—NIA na ROHO MOJA

Kuleana: Maisha ya kikristo ni uzoefu endelevu wa ukuaji. Ni


uanafunzi. Ukristo ni karakana ya uanafunzi. Ni kuliishi kwa vitendo
neno la Bwana.
Utume: Tumeokolewa kutumika [kwa Kristo] (Matendo 2:38;
Mathayo 20:28; 28:16–20; Luka 4:16–21; 24:45–49; Yohana 11:4,5;
13:14,15; Wafilipi 2:5–7; Warumi 15:1; Wagalatia 6:2; Isaya 61:1–3;
Amosi 5:24.

—KWA KIKUNDI KIDOGO—

tathmini binafsi ya maisha kiroho

Ni wakati wa wote kuifanya kazi, si kuishia kupima tu sehemu ya


ubaya wa mtu mwingine, bali kila mmoja auchunguze moyo wake
mwenyewe, aungame makosa yake mwenyewe, na kuwaacha ndugu
zake kwa Bwana. Kila mtu anapaswa kujibu kwa makosa yake tu; na
huku akichunguza kwa taabu sana kung'oa magugu toka kwenye
bustani ya ndugu zake, magugu yenye sumu yanakomaa imara na
kukua vile vile ndani ya yeye mwenyewe. Hebu kila mmoja hapo
nyumbani ajitaabishe kuchunga nafsi yake mwenyewe na kuwa na
roho yenye furaha, changamfu, yenye kuvumilia, na mambo yote
yatakuwa heri. E. G. White, Letter 12, 1863. 2ATH 633.1
Kila mtu anayetii mwaliko huu atafungwa nira pamoja na
Kristo. Hatuna budi kwa wakati wote na kila mahali kudhihirisha
upole na unyenyekevu wa Kristo. Ndipo Bwana atasimama karibu na
wajumbe wake na kuwafanya vinywa vyake, na yeye aliye msemaji
wa Mungu kamwe hatatia katika midomo ya wanadamu maneno
ambayo Mkuu wa enzi ya mbinguni hangenena pale anaposhindana
na mwovu. E. G. White, Letter 38, 1894. 2ATH 634.1
Bwana ametuagiza, “Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo
ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote
yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema;
ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini
KIKUNDI KIDOGO—NIA na ROHO MOJA

hayo.” (Wafilipi 4:8). Lakini wale ambao wanashughulika sana katika


kuchambua maneno na matendo ya wengine ili kugundua yale yote
yasiyofaa wanashindwa kupambanua mambo mazuri na ya
kupendeza. Hawali chakula kinachofaa ili kukuza uhai wa kiroho na
ukuaji wenye afya. E. G. White, Manuscript 4a, 1893. 2ATH 635.2
Kuheshimiana na Kupendana—Kama akilini mwetu tutatawaliwa na
matendo maovu na dhalimu ya wengine, tutaona kuwa haiwezekani
kuwapenda vile Kristo alivyotupenda; lakini kama mawazo yetu
yakikaa kwenye pendo ajabu na huruma ya Kristo kwa ajili yetu, roho
hiyo hiyo itabubujika kwa wengine. Tunapaswa kupendana na
kuheshimiana, licha ya makosa na kasoro ambazo hatuwezi kuvumilia
kuziona. Unyenyekevu na kutojiamini vinapaswa kusitawishwa, na
kuwa na moyo wa subira kwa makosa ya wengine. Hii itaua ubinafsi
wote na kutufanya tuwe wanyoofu na wakarimu. E. G. White, Steps
to Christ, 121 (1892). 2ATH 635.3
Kutegemea Silaha za Kimwili—Bwana anajua kwamba ikiwa
tunamtazama mwanadamu, na kumtumaini mwanadamu,
tunategemea silaha za mwilini. Anatualika tumtumainie Yeye. Hakuna
kikomo kwa uweza Wake. Fikiria juu ya Bwana Yesu na matendo
Yake na pendo Lake, bali usijikite kutafuta kasoro na kuangalia makosa
ambayo wengine wamefanya. Zingatia mambo yanayostahili
kutambuliwa na kusifiwa; na ikiwa wewe ni mwepesi wa kutambua
makosa ya wengine, kuwa mwepesi zaidi kutambua wema na kusifu
wema. Utakapojikosoa mwenyewe, utaweza kupata mambo ya
kuchukiza kama vile unavyoona kwa wengine. Kisha na tufanye kazi
daima ili kuimarishana katika imani takatifu sana. E. G. White,
Manuscript 151, 1898. 2ATH 637.2
Kujaribu Kuufunika Utu wa Kale kwa Kushambulia makosa ya
wengine—Mtu yeyote na asithubutu kuficha dhambi zake mwenyewe
kwa kufichua makosa ya mtu mwingine. Mungu hajatupa kazi hii
tuifanye. Hatuna budi kuwaacha wengine wanyenyekeze mioyo yao
wenyewe, ili wapate nuru ya kumfahamu Mungu. E. G.
White, Manuscript 56, 1904. 2ATH 637.3
KIKUNDI KIDOGO—NIA na ROHO MOJA

—KWA KIKUNDI KIDOGO—


Mbegu hufa ili itoe matunda
“Chembe ya ngano isipoanguka katika nchi, ikafa, hukaa hali
iyo hiyo peke yake, bali ikifa hutoa mazao mengi” Yohana
12:24.
Katika ukristo, tunayapoteza maisha ili tuyapate maisha. Kwa kujitolea
kikamilifu kwenye huduma tunakuwa watu wa mfano kwa watu.
Kutoa ni kuishi.
Mathayo 25:14-15 “Maana (ufalme wa Mungu) ni mfano wa
mtu atakaye kusafiri (Yesu akiwa karibu kurudi Mbinguni),
aliwaita watumwa wake, akaweka kwao mali zake. Akampa
mmoja talanta tano, na mmoja talanta mbili, na mmoja
talanta moja; kila mtu kwa kadiri ya uwezo wake; akasafiri.”
Kuhusu msafiri wa nchi za mbali katika mfano huu ni Kristo ambaye
alipotoa mfano huu alikuwa karibu kutoka duniani kwenda mbinguni;
watumwa ni wafuasi wake. Talanta hizi ni kipaji cha Roho Mtakatifu
(1 Kor 12:8-11). Kabla ya kuwaacha wanafunzi wake aliwavuvia Roho
Mtakatifu (Yoh. 20:22 na 24:49) lakini Roho hakuletwa kwa ukamilifu
mpaka baada ya kupaa kwake (Yesu)...
Ni mpaka hapo, kwa njia ya imani, umoja kati yao wakiondoa tofauti
zao, maombi, walipojitolea kikamilifu na kukubali awatumie.

Mathayo 25:15 "Akampa mmoja talanta tano, na mmoja


talanta mbili, na mmoja talanta moja; kila mtu kwa kadiri ya
uwezo wake; akasafiri.”
👆Mungu wetu hutupatia vyote hivyo kwa kadiri ya uwezo wetu.
2 Wakorintho 8:12 "Maana, kama nia ipo, hukubaliwa kwa
kadiri ya alivyo navyo mtu, si kwa kadiri ya asivyo navyo.”
KIKUNDI KIDOGO—NIA na ROHO MOJA

👆Suala si kwamba tumepokea talanta ngapi bali, "ninafanyaje na kile


nilichonacho?" Ye yote ambaye hakui katika uwezo na utumishi bora
hatimizi kusudi la maisha.
Kristo mfano wetu, alikuja duniani kujitolea uhai/damu Yake Naye
alipata maumivu makali na mengi ili hatimaye ajipatie huduma zetu za
hiari; alikuja duniani kutupatia mfano wa jinsi itupasavyo kufanya
kazi, na roho ya aina gani ingetutawala kazini. Na ukamilifu wa tabia
si jambo rahisi; tabia kamilifu hairithiwi, hatuipati kwa bahati bali kwa
juhudi za kila kupitia neema ya Kristo.
👉inafanyika kwa pambano kali dhidi ya ubinafsi.

“Maisha sharti yatupwe katika mifereji ya wahitaji wa


ulimwengu. Kujipenda nafsi na kujiona sharti vivunjwe. Lakini
sheria ya kujikana nafsi ndiyo sheria ya kujiponya…Maisha
yatakayohifadhiwa ni maisha ambayo yametolewa bure kwa
huduma ya Mungu na watu” E. G. White, Vielelezo vya
Mafundisho ya Kristo uk. 86.3

—KWA KIKUNDI KIDOGO—

JIFUNGAMANISHE NA JAMII ila kwa akili

Wale walio na vipaji vingi wana wajibu kwa Mungu kuwapa, si


marafiki wao tu, bali wote wanaohitaji msaada wao. Faida za kijamii
ni talanta na hazina budi kutumiwa kwa manufaa ya wote
wanaoweza kufikiwa na mvuto wetu. E. G. White, Vielelezo vya
Mafundisho ya Kristo, 353 (1900). 2ATH 621.2
Wale waliojifungia ndani yao wenyewe, ambao hawako radhi
kuvutiwa kuwabariki wengine kwa ushirika wa kirafiki, hupoteza
mibaraka mingi; kwa maana kwa mwingiliano unaotegemeana, akili
KIKUNDI KIDOGO—NIA na ROHO MOJA

hung’arishwa na hutakaswa; kwa mwingiliano kijamii, kufahamiana


hutokea na urafiki hupatikana ambao huzaa matunda ya umoja wa
moyo na ulimwengu wa upendo unaopendeza machoni pa mbinguni.
E. G. White, Testimonies for the Church 6:172 (1900). 2ATH 621.4
Ni kupitia mahusiano ya kijamii ambapo Ukristo unawasiliana na
ulimwengu. Kila mwanamume au mwanamke ambaye ameonja pendo
la Kristo na kupokea ndani ya moyo nuru ya kimungu anahitajika kwa
Mungu ili kuangazia njia ya giza ya wale ambao hawajaijua njia iliyo
bora zaidi… Nguvu ya kijamii, iliyotakaswa na Roho. ya Kristo, sharti
idumishwe ili kuzileta roho kwa Mwokozi. E. G. White, Testimonies for
the Church 4:555 (1881). 2ATH 622.1
Tunapata hasara pale tunapopuuza fursa ya kujihusisha pamoja ili
kuimarishana na kutiana moyo katika kumtumikia Mungu. Kweli za
Neno Lake hupoteza uangavu na umuhimu wake katika akili zetu.
Mioyo yetu inaacha kuangazwa na kuamshwa na mvuto wa neno
unaotakasa, na tunapungua katika hali ya kiroho. Katika mwingiliano
wetu kama Wakristo tunapoteza mengi kwa kukosa kuhurumiana.
Yule anayejifungia ndani hajazi nafasi ambayo Mungu alimpangia.
Ukuzaji ufaao wa masuala ya kijamii katika asili yetu hutuleta katika
kuhurumiana na ni njia ya ustawi na nguvu kwetu katika kumtumikia
Mungu. E. G. White, Steps to Christ, 101 (1892). 2ATH 622.2
Maisha yote ya Mwokozi yalikuwa na sifa ya ukarimu usio na ubinafsi
na wenye uzuri wa utakatifu. Yeye ndiye kielelezo chetu cha wema.
Tangu mwanzo wa huduma Yake, wanadamu walianza kuelewa kwa
uwazi zaidi tabia ya Mungu. Alitekeleza mafundisho yake katika
maisha yake mwenyewe. Alionyesha msimamo pasipo ukaidi, wema
pasipo udhaifu, upole na huruma pasipo kuathiriwa na hisia. Alikuwa
mtu wa kuchangamana sana na jamii, lakini angali na akiba ambayo
ilikatisha tamaa mazoea yasiyofaa. Hulka yake ya kuwa na kiasi
haikuwahi kusababisha ubaguzi au ukali. Hakupatana na ulimwengu,
lakini alikuwa angali mwangalifu kwa mahitaji ya aliye mdogo kabisa
KIKUNDI KIDOGO—NIA na ROHO MOJA

miongoni mwa wanadamu. E. G. White, Counsels to Parents, Teachers,


and Students, 262 (1913). 2ATH 622.3
Kwenye meza ya watoza ushuru aliketi kama mgeni wa kuheshimiwa,
kwa huruma na upole wake kwa jamii akionyesha kwamba alitambua
hadhi ya ubinadamu; na watu walitamani kuwa kama Yeye. Katika
mioyo yao yenye kiu maneno Yake yalianguka kwa nguvu yenye
baraka, yenye kuleta uzima. Misukumo mipya iliamshwa, na kwa watu
hawa waliotengwa na jamii kulifunguliwa uwezekano wa maisha
mapya. E. G. White, The Ministry of Healing, 26 (1905). 2ATH 623.1
Halikuwa kusudi la Mungu kwamba umaskini usiwepo kabisa
ulimwenguni. Jamii haikupaswa ifanane kamwe, kwa kuwa utofauti
wa hali ambao hutambulisha jamii yetu ni mojawapo ya njia ambazo
Mungu amepanga kuthibitisha na kudumisha tabia. E. G. White, 2ATH
626.1

—KWA KIKUNDI KIDOGO—

FUNDISHA NA IBUA VIONGOZI

Iwe kabla ya huduma au ndani ya huduma, sharti kufundishwa wale


wanaotazamiwa kuwa viongozi wa baadaye. Badiliko la mtu hadi
kuwa kiongozi linaweza kutokea pale tu linapofanyika na kuchakatwa
ndani ya roho ya akili. Ndani ya kila mtu kuna kiongozi. Si kila mtu
anaweza kuwa kiongozi wa watu lakini ye yote yule anaweza kuwa
kiongozi katika mazingira ya kipawa na kipaji chake alivyopatiwa na
Mungu. Uongozi ni matokeo ya mazingira, yaani badiliko la hali huita
watu wenye karama na vipawa. Farao alipofadhaishwa na ndoto ya
ng’ombe 7 na masuke 7, aliona rasilimali-mtu kwa Yusufu (Mwanzo
41). Hakumwona Yusufu bali aliona kipawa cha Yusufu. Vivyo hivyo
kwa Nebukadneza, baada ya hali ya mazingira kubadilika, watu wa
Babeli waliona rasilimali-mtu kwa Danieli.
KIKUNDI KIDOGO—NIA na ROHO MOJA

Hauhitaji kupandishwa cheo ndipo udhihirishe dhamiri yako katika


uongozi. Maendeleo ya hatua kwa hatua katika kuwa kiongozi
hububujika ndani ya roho ya akili yako ya kwamba wewe ni nani na
kwa nini upo duniani—hisia za utambuzi wa umuhimu wako katika
maisha haya. Uongozi si ujuzi, mtindo, au utendaji fulani bali ni
utekelezaji wa kile roho ya akili na dhamiri zinavyokuongoza.
Kujifunza kwao hakuwatoshi ikiwa bado hawajajitambua kuwa
uongozi hutokana na mafunuo ya ndani ya akili na moyo wa mtu
yanayomwongoza kutenda vile dhamiri yake inavyomwelekeza.
Mwanafunzi hawezi kubadilika mpaka anajipotambua. Unaweza
kusoma na kujifunza sana kuhusu uongozi lakini ikiwa hujatambua
utabaki kuwa tu na nadharia kuhusu uongozi. Ukitambua, akili na fikra
zako zitabadilika na matokeo yake ni kubadilika mkao na mwelekeo
wa moyo

—KWA KIKUNDI KIDOGO—


IDADI YA WANAKIKUNDI
Inategemea makusudi ya kundi lakini kundi la watu wengi ni vigumu
kuwa na uhusiano wa karibu sana miongoni mwa wanakikundi kwani
kundi kubwa ni rahisi kutawaliwa na wachache. Kikundi kinapaswa
kiwe na watu wachache ili kutoa nafasi ya kila mwanakikundi kuhusika
katika viwango vyake katika kufikia kujitolea kikamilifu kwa Kristo.
Yesu alichagua kikundi cha watu 12 tu.

—KWA KIKUNDI KIDOGO—


Kuwekeana maagano
Ni jambo zuri kuwekeana mapatano ikiwezekana kwa kuapiana (1
Samweli 18:3). Lakini maagano haya sharti msingi wake uwe katika
roho ya neema na si shuruti; katika kikundi cha watu uwezekano wa
kukosea au kuwa na mapungufu ni mkubwa. Wanakikundi
KIKUNDI KIDOGO—NIA na ROHO MOJA

waliojisimika katika ushirika wa kikristo katika roho moja wataonyana


na kukemeana kwa upendo, katika namna ya kichungaji ya upendo na
kuvumiliana, ‘kumlinda mwingine kwa upendo.’

Mifano ya Maagano
 Agano la hakikisho: (pendo lisilo na masharti—Agape); mfano,
‘hakuna chochote kitakachonifanya nikuchukie, naweza nisikubaliane
na matendo yako lakini nitakupenda kama mtu na kufanya yote
niwezayo ili kukunyanyua katika pendo la Kristo.’

 Agano la upatikanaji: Hakuna mtu aliye bize isipokuwa ni suala tu


la kipaumbele. Katika kikundi mnaweza wekeana agano kuwa,
‘niwapo na muda, nguvu na yote kwa ajili ya huduma, vyote ni kwa
ajili yetu sote. Nayatoa yote kama kipaumbele cha agano letu. Kama
sehemu ya agano hili, ninaahidi kupatikana wakati wo wote.’

 Agano la uwazi: ‘Ninaahidi kuwa muwazi ikiwa kuna jambo


linanitatiza, kunikera ama kunifurahisha. Ninawaamini katika kuwa
nami katika mahitaji ya namna zote’

 Agano la ujali: ‘Ninaahidi kujali ama kumjali ye yote kwa kadiri ya


uwezo wangu, hata kumwombea. Nitajitahidi kujua yanayomsibu kila
mmoja na kumwokoa toka katika dimbwi la mfadhaiko na kukata
tamaa.’

Faida za kuwekeana mapatano


 Mahudhurio
 Maisha ya kiroho ya kujitolea kikamilifu.
 Kuombeana na shime za kichungaji kwa kila mwanakikundi.
 Uwakili wa kikristo kwa vitendo.
 Upatikanaji wa kila mwanakikundi.
KIKUNDI KIDOGO—NIA na ROHO MOJA

—KWA KIKUNDI KIDOGO—

Jitahidi kupatana na kanisa lako


Kikundi kidogo cha watu walionuia huwa na nguvu kwa Kanisa.
Muwapo na njozi njema, upinzani hauepukiki. Hii haina maana
kwamba hamko sahihi, bali inaashiria kuwa mnatia changamoto
wengine ili wabadilike. Hiyo ndiyo fursa yenu wanakikundi ili kupima
dhamiri na kunuia kwenu katika njozi zenu. Ni afadhali mkosolewe
kwa kutenda jambo kuliko kupuuzwa kwa kukaa tu pasipo lo lote.
Ni kawaida kwa kikundi kidogo Kanisani kuleta mgawanyiko wa
washiriki na kwa msingi huu mengi mabaya huelekezwa kwa kikundi
hiki kidogo. Lakini mapatano na uaminifu vyapaswa viwe sifa ya
kikundi kidogo kwa ajili ya Kristo. Kikundi kidogo chaweza
kutengeneza wigo mpana wa ushirika katika Kanisa. Yapasa kuwepo
na mapatano kati ya viongozi wa kanisa na kikundi hiki kidogo.
Mgongano kati ya kikundi kidogo na kanisa hasa viongozi wa Kanisa,
mara nyingi hutokea pale ambapo:

1. Kanisa linakumbuka habari mbaya za nyuma juu ya vikundi


vingine vidogo vilivyowahi kuibuka. Pengine hivyo vikundi
vilikuwa na mtazamo wa viburi vya uzima au ustahimilivu hafifu
wa kuchukuliana mapungufu na mbinu za kishupavu tu za kuleana
katika kuleta mabadiliko Kanisani.

2. Pale viongozi wa Kanisa wanapohisi kuwa ikiwa hawatoweza


kuendesha masuala ya kikanisa wao wenyewe, mamlaka yao
inatishiwa. Hapa ni ukosefu tu wa uelewa. Ikiwa viongozi wa
Kanisa ni watu wa kiroho na wanaelewa vyema maana ya ukristo,
na wamejitolea kikamilifu kudumisha umoja wa mwili wa Kristo,
hapatakuwepo na migongano yo yote.

 Ni heshima na adabu kuu kwa kikundi kidogo kutoa taarifa kwa


viongozi wa Kanisa juu ya kile wanachokifanya.
KIKUNDI KIDOGO—NIA na ROHO MOJA

—KWA KIKUNDI KIDOGO—

Panga wasaa na matukio kwa minajili ya kubarizi


Hili laweza fanyika kwa wanakikundi wao kwa wao ama wanakikundi
wanawaalika wageni wengine wasio wanakikundi, mathalani wenzi
wao, marafiki zao au hata familia zao kwa ajili ya kufurahi pamoja
katika mandhari tulivu iliyosheheni viumbe asili katika mazingira hayo.
Hii husaidia kuondoa tofauti ndogondogo na kurejeshana kama
wanakikundi na inasaidia kudumisha mahusiano ya pamoja kwa
ushirika katika Kristo.

—KWA KIKUNDI KIDOGO—

Tengeneza mtandao wa ushiriki


Ni muhimu kuwa na mtandao wa shime, vyanzo na mafunzo.
Kutafanya kikundi kiwe hai kila wakati. Ni sharti upatikanaji wa
rasilimali uwe rahisi; iwe rasilimali fedha au rasilimali watu kwa ajili ya
ufanikishaji wa mipango na malengo ya kikundi.

—KWA KIKUNDI KIDOGO—

KUWA MTU MUHIMU DUNIANI

Sote twahitaji mamlaka; mamlaka ni uwezo wa kuongoza na kutawala


hali za maisha na hatima yake. Hili ni tumaini kuu na wajibu wa kila
mwanadamu. Ni wajibu wa kila mtu kumtambua mwenye mamlaka
na uweza wa kutatua matatizo, kuleta uthabiti wa maisha na
kudumisha maisha ya amani na yenye ustawi. Mamlaka ni uwezo wa
kushawishi na kuongoza hali za maisha yaani mabadiliko katika
maisha. Machafuko katika ulimwengu wetu na hali mbaya ya maisha
ya mwanadamu vinafunua ukosefu wa mamlaka inayoweza kutatua
mahitaji yetu.
KIKUNDI KIDOGO—NIA na ROHO MOJA

Tukiwa wale tuliokabidhiwa sayari dunia, twahitaji Nguvu Kuu toka


juu Yenye mamlaka Itakayotupatia mahitaji yetu. Pale ufalme
unapolitawala koloni, jukumu la kwanza ni kuhakikisha koloni
lifanane na ufalme-taifa tawala katika mitazamo ya akili, mtindo wa
maisha, sifa zake na utamaduni. Lakini mustakabali wa badiliko
hautokei papo kwa hapo. Maendeleo hasa yanahitajika. Mkuu wa
taifa tawala humwagiza gavana kurithisha kwa koloni kaida za taifa
tawala. Hivyo koloni halihitaji uwepo kimwili wa mkuu wa ufalme-
taifa ili kubadilika.
Alipoumba dunia na mwanadamu, Mfalme wa milele alikusudia
kupanua umiliki wake na wa serikali yake. Hakuhitaji uwepo wake
kimwili kwenye koloni-dunia kutawala ama kuliongoza bali aliumba
watu na kuwakabidhi kuitawala dunia. Kwa sababu mwanadamu
aliumbwa kwa mfano na sura ya Mungu, hana budi kuwa karibu na
Muumba wake kwa ajili ya ufanisi wa kazi aliyopatiwa huyo
mwanadamu na uwezo wa kufanya jaribio la maisha. Mwanadamu
akapuliziwa pumzi ya uhai itakayomfanya awe karibu na Mungu
wake. Ni kwa kuumbiwa sura ya Mungu ndivyo kutatuwezesha
kuibadili dunia iliyochafuka kuwa mbingu ndogo.
Kwa nasibu, mpango wa ufalme wa mbinguni wa kupanua usuli wa
mbinguni duniani uliingiliwa na mwovu ibilisi. Ibilisi akaharibu
kenyekenye mpango wa ufalme wa mbinguni na ukaribu wa
mwanadamu kwa Muumba wake. Baya zaidi tulilopata ni kukosa
Roho ya Mfalme. Maagano yote mawili katika Biblia hufunua mpango
mpya wa Mfalme katika koloni lake sayari dunia.
Kwa watu Wake, yaani koloni lake, Mfalme alipanga kuwa angelikuja
hapa duniani kama mwanadamu ili kurejesha sura na mfano wa
Mungu. Ufalme wa Mungu uko ndani yetu (Luka 17:21). "Ufalme
wako uje” (Mathayo 6:9)
Mungu anatawala viumbe vyote (Zaburi 103:19) na anatawala
maishani mwetu ikiwa tutajikabidhi kwake (Luka 17:21); hivyo ufalme
wa Mungu ni Kristo kuishi na kutawala mioyoni mwetu. Aidha,
KIKUNDI KIDOGO—NIA na ROHO MOJA

Kuomba ‘ufalme wako uje’ ni kuomba kwamba Mungu azidi


kuongeza utawala wake kwa kuturejesha kwake na kisha hapo
baadaye atakapokuja mara ya pili, ndipo atausimamisha na kuutwaa
ufalme wake yaani watu ambao walikubali atawale maisha yao na
kufikia ukamilifu wa tabia Yake (Ufunuo 11:15; 20:4)

—KWA KIKUNDI KIDOGO—

DUMISHA CHANZI CHAKO—LINDA NADHIRI


YAKO

“na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu”


Viumbe vya Mungu vinapaswa kuishi ndani ya mazingira ya uumbaji
wa Mungu. Mimea na wanyama sharti vidumu kuwa katika nchi kavu
na majini, vikijipatia vyakula vyake. Mimea na wanyama-samaki
vilivyowekewa kanuni isiyobadilika ya kuishi majini, vikipelekwa nchi
kavu havidumu. Ua likitolewa kwenye tawi lake hunyauka na
kukauka. Ni kanuni isiyobadilika daima pindi kiumbe cho chote
kinapotolewa toka kwenye chanzi chake kuangamia.
Samsoni, Mnadhiri wa Mungu (Waamuzi 13—16).
Alifanywa kuwa nyumba ya Roho wa Bwana. Ilikuwa ni wajibu wa
wazazi wake kulinda uwepo wa Roho wa Bwana asije akamwacha
Samsoni. Ndiyo sababu nywele zake zilisukwa katika idadi ya vishungi
saba, kila kimoja kikibeba kanuni moja, kwamba katika utu uzima
wake atakapovishika vishungi hivyo akumbuke kanuni hizo. Nguvu na
uwezo wote vilitegemea tu kama angetembea katika utii wa kanuni za
Mungu, la asipotii, nguvu zingemtoka na kubaki kama mtu wa
kawaida. Ndiyo maana baada ya kujua nguvu zimemtoka kwa sababu
ya uzinzi, ulevi na uwongo, alitubu. Kunyolewa nywele ilikuwa ni
ishara ya wazi kuwa amekana kanuni zote za imani yake.
KIKUNDI KIDOGO—NIA na ROHO MOJA

"Adui mkubwa wa vipawa vya Rohoni ni tamaa za mwilini.


Wengine, wakati walipokuwa wadogo, wakati miili yao
haijazoezwa tamaa, walikuwa wakiota vitu vinatokea lakini
walipokuwa watu wazima hawakuwa hivyo tena kwa sababu
tamaa za mwilini ziliinuka zaidi ya vipawa vya rohoni. Daima
unapouburudisha mwili, kuna kitu cha rohoni hufa.” Tony Kapola
Wengi wetu tumejifungia katika chanzi kisichokuwa chetu.
Maburudisho ya dunia yametusonga na hatimaye kufunga milango ya
kuibua vipawa vyetu kwa ajili ya Mungu. Wengi waliotekwa na
maburudisho wameshindwa kabisa kujinasua. Leo watoto tunawalea
kwa vibonzo (cartoon) na badala ya kuibua vipawa vya Mungu,
wanaibuka na vipawa vichafu visivyopatana na mbingu.
Leo wengi wametekwa na Tik Tok, Instagram, Facebook n.k. Ni
hakika kuwa kujinasua inawezekana kabisa lakini inagharimu sana
kurejea; ni kwa kupambana vikali. Inahitaji muda wa kutosha kuivunja
minyororo hiyo. Unaweza ukaazimu na kunuia kabisa lakini kujinasua
kwake kunahitaji taabu, muda, saburi, uvumilivu na kujitoa kikamilifu.
Amka na jitambue ewe mtoto wa Mungu, uliyeumbwa kwa Sura na
mfano wa Mungu wa mbinguni. Achana na vipawa bandia vya ibilisi
visivyokupatia hatima njema ya maisha yako. Acha kumaliza bando
zako kwa mitandao michafu. Hukuzaliwa kwa ajili ya maburudisho
bali kwa ajili ya Mungu.

—KWA KIKUNDI KIDOGO—


Uongozi thabiti
Kilicho muhimu zaidi katika uongozi si ujuzi mwingi ama uzoefu na
ukomavu wa kiroho bali ni maisha yaliyoguswa, kutiishwa na
kuhuishwa na Kristo. Siyo mpaka uwe na ujuzi mwingi na
kuzungukwa na bahati/fursa nyingi bali ni kuwa mzuri katika jambo
fulani. Kiongozi ni mtumishi wa anaowaongoza. Ni kule kutojisikia
kuwa uko katika viwango fulani vya kiroho bali kuwa tayari
KIKUNDI KIDOGO—NIA na ROHO MOJA

kuuruhusu mchakato endelevu wa kuelekea ukamilifu katika uweza na


neema vya Bwana.
Kiongozi ni yule:
 Amwonaye kila mtu ya kuwa anastahili na ni wa kuheshimiwa.
 Asiyetumia nguvu za kimwili kuongoza
 Asiyewaambia watu washiriki wenyewe bali hutengeneza mazingira
mazuri ya kila mtu kushiriki
 Anayeamini kuwa katika kila mtu kuna kitu cha thamani.
 Asiye bize bali ana kipaumbele kwa ajili ya watu. Anapatikana
kirahisi.
 Anajitambua kuwa naye ana mapungufu
 Asiyejaribu kufanya kila kitu bali anaamini katika huduma
tegemevu—kwamba wanakikundi wote wamejitolea kikamilifu na
wana vipawa anuwai kwa ajili ya huduma—na kiongozi huyo
hutafuta kuvitumia na kuvidumisha vipawa hivyo katika huduma.

 Ana viashiria vya kuwa na wito: Kiongozi mwenye wito atastahimili


kupitia katika magumu awapo katika utumishi. Ni sharti achaguliwe
kiongozi mkristo anayewiwa, aliye na wito na mwenye kipawa.

 Upatikanaji, utayari na kujitolea kikamilifu huwafanya wengi


kutumiwa na Mungu kama viongozi kuliko wale wenye utajiri wa
vitu, vipawa ama ujuzi ( 1 Korintho 1:26-31). Uongozi ni tunda la
Roho wa Mungu.

 Kiongozi sahihi huchaguliwa na Mungu bali kazi yetu wanadamu ni


kuchunguza kwa maombi ya dhati ni nani aliyechaguliwa na Mungu.
Kuchagua kiongozi siyo kuziba pengo au nafasi. Kiongozi sharti
achunguzwe wito, vipawa na ukidhi wa nafasi hiyo. Ni muhimu kulipa
muda wa kutosha suala hili.

 Kiongozi huibua viongozi wengine: (2 Timotheo 2:2). Utambuzi na


uendelezaji wa viongozi ni nyanja endelevu katika ukuaji wa Kanisa.
KIKUNDI KIDOGO—NIA na ROHO MOJA

Uwapo kiongozi ni nafasi kwako na ni rahisi kutambua viongozi


wanaoibuka.

—KWA KIKUNDI KIDOGO—


KUWAELEWA NA KUWASAIDIA WANAKIKUNDI
WENZETU
Katika kikundi, sharti kuwepo na utambuzi wa kila hitaji la
mwanakikundi. Katika maisha haya tunapitia mabadiliko mbalimbali
ya hali za maisha. Kila mtu ni mhitaji, kila mmoja ana mipango na
matarajio yake binafsi hivyo lazima kusaidiana katika hali hizo kama
wanakikundi. Mashaka, hofu na hali zo zote zaweza kuratibiwa na
wanakikundi wenyewe ili kila mwanakikundi afurahie umoja huo.
Nyakati za mabadiliko ya hali za maisha ndiyo fursa ya Mungu
kutufanya kuwa na moyo wa kujaliana.
“Watumishi wa Kristo wangefuata mfano Wake. Alipotembea
huko na huko aliwafariji walioumia, na kuponya wagonjwa.
Halafu mbele yao aliweka ukweli mkuu kuhusu ufalme
wake...unapopoza maumivu ya mwili utapata nafasi ya
kuhudumia mahitaji ya kiroho.” E. G. White, Vielelezo vya
Mafundisho ya Kristo uk. 233.3
"Kristo hachagui malaika ambao kamwe hawajaanguka kuwa
wawakilishi wake, bali wanadamu, watu wenye hisia sawa na
zile za hao wanaotafuta kuwaokoa.” E. G. White, Tumaini la
Vizazi Vyote uk. 296.4
“Sote tumefungwa pamoja katika wando mkubwa wa
ubinadamu, na lo lote tunaloweza kufanya kuwanufaisha na
kuwainua wengine kutaakisi mibaraka kwetu wenyewe.
Sheria ya kutegemeana inafunga kila tabaka katika jamii.” E.
G. White, Wazee na Manabii uk. 534.4
KIKUNDI KIDOGO—NIA na ROHO MOJA

Mtazamo wa kikristo
Mitazamo yetu sisi wanadamu iko mbali mno na mtazamo wa
Mungu. Tuna kawaida ya kurekodi kile tukihisicho, tukionacho. Kwa
kutazama au kusikia, badala ya kujenga taswira, wengi ni wepesi
kurekodi kile wakionacho au wakisikiacho pasipo kwanza kujenga
picha mawazoni. Watu hawa ni wepesi kuchora msitari wa hitimisho.
Mkao usiofaa wa akili na mawazo hupelekea mtu kuwa hivyo
Mtu haamini kama anaweza kufanya vitu vikubwa kwa kujiangalia
katika muonekano mmoja tu lakini ni jinsi gani mtu anakuja kuwa mtu
wa tofauti kabisa na vile alivyokuwa hapo awali! Lakini pia watu
wanavyokutazama wanaona kama vile hauwezi kufanya vitu vikubwa,
hauwezi kuwa vile, hauwezi kuwa pale; je, vipi tukiondoa dhana hiyo
ya kujitazama au kumtazama mtu na kuhitimisha kuwa hawezi kitu?

Mtu hapimwi kwa rangi, kabila, kimo, umri, kiwango cha elimu, cheo,
hadhi bali kwa maudhui ya maumbile ya tabia. Akili ndicho kipimo
kwa mtu. Wengi tunaongozwa na uraibu wa matazamio (uraibu wa
hatima—Destination addiction). Kwamba fulani tukimweka hapo
anaweza na fulani hawezi! Ipo mifano ya kushangaza ya wale ambao
waliwahi kutazamwa katika mtazamo uliozoeleka lakini walikuja
kuwa tofauti zaidi ya vile walivyotazamiwa.
Haidhuru watu wakuangalie na kukutazamia kwa namna fulani;
tunavyokuona sisi wanadamu wenzako ni tofauti na anavyokuona
aliyekuumba. Mungu ni Mungu tu. Hajali umri, uzoefu, jinsia au ya
nyuma, haishangazi humbarikia ye yote yule. Mkristo halisi
humtazama kila mtu kama: Sura ya Mungu: Mwanadamu ameumbwa
kwa mfano na sura ya Mungu (Mwanzo 1:26,27; 5:1).
‘Ijapokuwa aina ya watu iwe na hali mbaya kiasi gani na hata
iwapo watu wanawadharau na kuwatenga mbali, hawawezi
kuwa chini kiasi ambacho Mungu hawaangalii kwa upendo.’
E. G. White, Vielelezo vya Mafundisho ya Kristo uk. 225.3
KIKUNDI KIDOGO—NIA na ROHO MOJA

—KWA KIKUNDI KIDOGO—

SOTE TUKO SAWA ILA HATUFANANI

Katika mwingiliano wetu sisi kwa sisi hatuna budi kukumbuka


kwamba wote hatufanani katika vipaji au silika. Watendakazi
hutofautiana katika mipango na mawazo. Vipawa mbalimbali,
vikiungana, ni muhimu kwa mafanikio ya kazi. Tukumbuke
kwamba wengine wanaweza kujaza nafasi fulani kwa mafanikio
zaidi kuliko wengine. Mtendakazi ambaye amepewa hekima na
uwezo unaomfaa kwa ajili ya kukamilisha kazi fulani maalum
hapaswi kuwalaumu wengine kwa kutoweza kufanya kile
ambacho yeye, pengine, anaweza kukifanya kwa urahisi. Je,
hakuna mambo ambayo watendakazi wenzake wanaweza
kuyafanya kwa mafanikio zaidi kuliko yeye? E. G. White, Letter
116, 1903 (Evangelism, 103) 2ATH 615.1
Kila uhusiano katika maisha unahitaji kujidhibiti, uvumilivu, na
huruma. Tunatofautiana sana katika silika, mwenendo wa tabia,
elimu, kiasi kwamba njia zetu za kutazama mambo hutofautiana.
Tunatofautiana katika kupima mambo. Uelewa wetu wa ukweli,
mawazo yetu kuhusu mwenendo wa maisha, havifanani katika
mambo yote. Hakuna watu wawili ambao uzoefu wao unafanana
katika kila jambo. Majaribu ya huyu si majaribio ya yule.
Majukumu ambayo fulani huyaona ni marahisi, kwa mwingine ni
magumu na ya kufadhaisha. E. G. White, The Ministry of Healing,
483 (1905). 2ATH 615.2
Vumilianeni—Ni sharti tuvumiliane, tukikumbuka udhaifu
wetu. Wahurumieni wengine, mkifanya jambo la kipekee; wengine
wakiokoa kwa hofu, toka kwenye moto. Wote hawawezi
kufanana katika kuhudumiana. Wote hawawezi kuhusishwa
kwenye wajibu wa mwingine. Fursa lazima ifanywe kulingana na
silika na akili. Mungu anajua jinsi ya kushughulika nasi. Lakini
moyo wangu unateseka nilivyoona ndugu akishughulika na ndugu
KIKUNDI KIDOGO—NIA na ROHO MOJA

na namna mmoja anavyodakia maneno ya mwingine na


kumfanya mwingine kuwa mkosaji. E. G. White, 2ATH 632.5
Utofauti wa hulka na tabia mara nyingi huonekana katika familia
moja, kwa kuwa ni katika utaratibu wa Mungu kwamba watu
wenye hulka tofauti tofauti wanapaswa kukaa pamoja. Inapokuwa
hivyo, kila mwanafamilia katika kaya anapaswa kujali kwa dhati
mahitaji na heshima kama haki ya wenzake. Kwa njia hii kujaliana
na kuvumiliana kutadumu, chuki itayeyushwa, na mienendo
mibaya ya tabia italainishwa. Upatanifu utalindwa, na muunganiko
wa hulka tofauti tofauti utakuwa faida kwa kila mmoja. E. G.
White, The Signs of the Times, Septemba 9, 1886 (Child Guidance,
205) 2ATH 616.1
Upatanifu na muunganiko uliopo kati ya watu wenye tabia
mbalimbali ndio ushahidi wenye nguvu zaidi tunaopaswa kuwa
nao ambao Mungu amemtuma Mwana Wake ulimwenguni
kuokoa wenye dhambi. Ni fursa yetu kuwa na ushahidi huu. Lakini
ili kufanya hivi, ni sharti tujiweke chini ya amri ya Kristo. Tabia
zetu lazima zifinyangwe kupatana na tabia Yake, nia zetu sharti
zisalimishwe kwenye mapenzi Yake. Kisha tutafanya kazi pamoja
bila mgongano. E. G. White, Testimonies for the Church 8:242,
243 (1904) 2ATH 619.4

—KWA KIKUNDI KIDOGO—


Ushirika wa pamoja katika Roho
Ili kila mmoja katika kikundi aweze kukua katika Kristo, sharti kuwepo
na mpangilio na muundo mzuri wa kikundi; ili hata vipaji zaidi
viibuliwe na ili kila mwanakikundi aonekane kujitolea kikamilifu
kwenye huduma. Uwepo wa Mungu sharti uonekane katika kikundi.
Ni muhimu kwa wanakikundi kuwa na maslahi ya pamoja, ikiwemo
kushiriki pamoja mambo mbalimbali ya kiroho na kimwili; kuwa
wenza.
KIKUNDI KIDOGO—NIA na ROHO MOJA

Utofauti wetu katika hali mbalimbali ndio msingi wa kuwa na ushirika


mmoja. Tunatofautiana hadhi kwenye jamii, vyeo, historia, umiliki,
mahitaji na tamaduni, lakini je, ni kipi kinachotuunganisha?—ni Kristo
ndani yetu. Jifunze zaidi katika Yohana 15. Kwa kuwa twakutania
sehemu moja, yaani katika Kristo, utofauti wa duniani hauna nafasi
wala nguvu.
"Kadhalika na sisi, tulipokuwa watoto, tulikuwa
tukitumikishwa na kawaida za kwanza za dunia. Hata
ulipowadia utimilifu wa wakati, Mungu alimtuma
Mwanawe...kusudi awakomboe hao waliokuwa chini ya
sheria, ili sisi tupate kupokea hali ya kuwa wana. Na kwa
kuwa ninyi mmekuwa wana, Mungu alimtuma Roho wa
Mwanawe mioyoni mwetu, aliaye, Aba, yaani, Baba. Kama
ni hivyo, wewe si mtumwa tena bali u mwana; na kama u
mwana, basi, u mrithi kwa Mungu.” Galatia 4:4–7 (Rumi
8:14–16; 1 Yohana 3:1).

—KWA KIKUNDI KIDOGO—


Kuitatua migogoro kwa upendo
Katika maisha, kwa sababu bado tungali duniani, migongano na
kutofautiana haviepukiki. Kutofautiana ndio sehemu ya mwito wetu
katika kuwa wanafunzi katika shule ya Kristo. Ndiyo kiashiria cha
ukuaji na ukomavu wa mwanadamu. Hatupaswi kuiweka migogoro
katika mitazamo hasi.
Migongano inaweza kusababishwa na viwango vya elimu, desturi na
mazoea, uzoefu uliopita, hali ya mtu, itikadi za kitamaduni, kidini n.k.
Kuna tofauti katika mafundisho na namna ya kutafsiri Biblia, tofauti ya
silika na hulka vya mtu, utofauti wa kiumri au mtu fulani
hukumtazamia kuwa angekuja kuwa hivi alivyo leo. Aidha, kama kuna
ajenda za siri hasa kunapokuwapo na wanandugu katika kikundi
(kikabila au wa damu).
KIKUNDI KIDOGO—NIA na ROHO MOJA

Sharti kuitatua migogoro katika kikundi ili uhusiano usichafuliwe ndani


ya kikundi. Pia, katika mchakato wa kutatua tatizo, iwe mara chache
sana kutumia mbinu ya kimadaraka bali mara nyingi itumike mbinu
patanishi. Kila upande unaokinzana sharti uridhike na suluhisho. Hapa
ni hekima na busara zaidi vya kimungu vyahitajika na sio akili au
uzoefu wa kibinadamu tu. Kupiga kura ya wengi wape haifai katika
kikundi kidogo.

—KWA KIKUNDI KIDOGO—

“NGUVU INAYOKUTAWALA” NA THAMANI


YA KUJITAWALA

Kuna wale wanaoamini kuwa upole ni udhaifu, lakini maana halisi ya


upole ni “nguvu itawalayo.” Ukiwa na roho ya upole utakuwa mtu na
kiongozi usiyejionyesha (show-off). Hauhitaji kujionyesha kuwa wewe
ni nani na una nini. Si lazima ujitambulishe, “mimi ni mheshimiwa
fulani” au “mimi ni profesa...nina PhD”
Mtu mpole hutenda kazi kimyakimya akitekeleza majukumu yake bila
kuangalia ni nani anayemtazama. Ni mtu ambaye hapendi wengine
wamwone anachokifanya na wakati huo hafanyi kwa siri bali
hadharani ila ni kimyakimya.

THAMANI YA KUJITAWALA
Unapokuwa kiongozi au mtu mwenye kipawa chako unajiweka katika
nafasi ya kuonekana na wengi, na kujaribiwa ni rahisi mno. Wengi
walio maarufu wanashindwa kujitawala hasira zao, misisimko yao n.k
Soma Yakobo 1:12–16 na 1 korintho 10:13
Kaa chini na fikiria udhaifu wako uko wapi. Kuujua udhaifu wako ni
salama. Ukijijua itakuwa rahisi kwako kuishi na watu. Daima
KIKUNDI KIDOGO—NIA na ROHO MOJA

utawajibu watu kwa upole na uungwana. Jinsi gani unavyoitikia pale


watu wanaposema vile ambavyo hukutarajia au pale mambo
yanaposhindwa kwenda vile ulivyotaka?
Wakati majaribu hayazuiliki kukufikia, wewe kiongozi, mwenye
kipawa ama mwenye wadhifa wowote, inakupasa kuamsha nguvu ya
ndani na kunuia kujizuia. Nguvu hii haitoki kwingine tofauti na kwa
Mungu. Nguvu ya Roho wa Mungu inapaswa ipate maskani kwako.
Ni kwa kiasi gani uko imara, thabiti, usiyeyumbishwa na chochote?
Nguvu ya ndani inaweza kuwa ni masharti na misimamo au viapo
alivyojiwekea mtu kuwa hatavivunja kamwe, haijalisha hali yoyote.
Hivi vitampa nguvu kukabiliana na jaribu.
“20 Je! Umemwona mtu mwenye kuhamaki katika maneno?
Afadhali kumtumaini mpumbavu kuliko yeye. 22 Mtu wa
hasira huchochea ugomvi; Na mtu mwenye ghadhabu huasi
sana.” Mithali 29:20, 22.
Kwa kutojitawala hasira na misisimko yako au ahadi nyingi, unaweza
ukakosea na ikachukua pengine muda mchache tu ukasamehewa lakini
mtu asikuamini tena! Uaminifu na misimamo uliyoijenga kwa miaka
20, inaweza kupuuzwa kwa sekunde 20 tu kwa kushindwa kujitawala.

—KWA KIKUNDI KIDOGO—


Jitayarishe kuwa peke yako. Chukua muda wa kuwa peke yako
na stahimili kusimama peke yako

Kwa kuwa mna njozi kama kikundi, na mnaona mwisho tangu


mwanzo, ni sharti muuishi mchakato wa kufikia malengo yenu. Mna
wajibu mkubwa kufikia lengo. Mnafanya kazi nyuma ya pazia ambapo
hamna mwingine anayeona ila ninyi tu.
KIKUNDI KIDOGO—NIA na ROHO MOJA

Suala hili linahitaji maamuzi mazito. Kwa sababu ya uzito wa kazi, sharti
kuna muda mnapaswa kuwa peke yenu ili kuchakata wajibu wenu,
kuhuisha roho zenu, akili na mwili.
“Lakini habari zake zikazidi kuenea, wakakutanika makutano
mengi wamsikilize na kuponywa magonjwa yao. Lakini Yeye
alikuwa akijiepua akaenda mahali pasipokuwa na watu,
akaomba.” Luka 5:15, 16

Je, huwa mnapata muda wa kuwa peke yenu na Mungu?


Kama kikundi si tu msimame peke yenu, bali pia mwe na huo uwezo
wa kusimama peke yenu. Yesu aliachwa na wanafunzi wote katika saa
nzito ya uhitaji wa wanafunzi wake lakini aliweza kusimama peke yake.
Yusufu akiwa gerezani aliitwa kufasiri maono ya mnyweshaji na
mwokaji aliokuwa nao gerezani. Kwa mnyweshaji, Yusufu alitamka
jema lijalo kwa mnyweshaji, bali kwa mwokaji alitabiri kifo (Mwanzo
40). Mungu ndiye aliyetoa tafsiri kupitia kwa Yusufu, naye Yusufu
alikuwa amefungiwa katika dhamiri ya kutokudanganya wala kuogopa,
ndiyo maana alitafsiri ndoto vile Mungu alivyoitoa.
Ikiwa Yusufu angetafuta ukubali kwa marafiki zake hao ili waendelee
kumpenda, angejaribiwa kudanganya au kuuficha ukweli kwa namna
fulani. Lakini Yusufu alitafuta kwanza ukubali kwa Mungu, naye
akafanya ilivyo sahihi kwake. Mara nyingine ni sharti kuwa kinyume na
ukubali wa watu, marafiki au hata ndugu. Mkijaribiwa kusalimisha
dhamiri zenu au kuingia mapatano basi ni rahisi kwenu kuongozwa na
wengine na sio nyie wenyewe.
KIKUNDI KIDOGO—NIA na ROHO MOJA

—KWA KIKUNDI KIDOGO—


Namna ya kuanza
Kikundi kidogo chaweza kuanza na wazo la mtu au watu wachache
ambao wana:
 Maslahi ya pamoja
 Nia ya kina ya hitaji hilo
 Njozi au maono
Kikundi kitaundwa ikiwa kuna mmoja au wachache wana kiu, imani na
kunuia ambako kutaongozwa na Roho wa Mungu. Vikundi vingi
vimeanza kwa sababu ya wachache tu waliohisi hitaji kuu la kutumika
kikamilifu. Suala si idadi bali ni ubora. Hakuna kumsubiri fulani kwa ajili
ya kuianza hatua ya kwanza bali jitihada katika kufanya kile
tunachoweza.
Siyo mpaka uwe na ujuzi mwingi na kuzungukwa na bahati bali ni
kuwa mzuri katika jambo fulani, juhudi na kuwa katika mahali sahihi na
wakati sahihi.
Hebu tujifunze mandhari ya ushindi wa Daudi dhidi ya Goliati (I
Samwel 17:1-52). Wafilisti walikuwa maadui wakubwa wa taifa la
Israeli. Kila siku asubuhi na jioni hadi kwa siku 40 walikuwa
wakitishiana, Sauli mfalme akitafuta mtu wa kuwashinda wafilisti.
Daudi, kijana mdogo kati ya ndugu zake wanane anafika eneo la vita;
ndugu zake wanamkasirikia kulingana na umri wake. Daudi, hata hivyo
ameiona na kuikubali changamoto. Tatizo hasa ameliona. Licha ya umri
mdogo na kutokuwa na uzoefu wa vita, ameona kuwa anayetukanwa
ni Mungu na si vinginevyo.

Hatua za kuzingatia hapa:


 Badiliko: likaanza kwa njozi, yaani kutambua tatizo lenyewe na
uzito wake.
KIKUNDI KIDOGO—NIA na ROHO MOJA

 Maamuzi: Anaamua kukabiliana na tatizo (1 Samweli 17:31,32)


 Kunuia: Akaona wivu kwa ajili ya Mungu (hasira takatifu), yaani
kutukanwa Mungu wake. Hatua hii ilimfanya aibue kipawa chake.
Sio umri wala uzoefu wa vita bali changamoto ndiyo ilimsaidia
kuibua kipawa chake; yaani kuwa vizuri katika jambo fulani (na si
mambo yote). Badiliko toka kuwa mchunga kondoo na kuwa
mpiganaji lilikuwa limeshakamilika.
 Kujiamini: Mungu (mtoa vipawa) akamfanya kuwa tegemeo lake
na si yeye (1 Samweli 17:37)

Hivyo, Daudi alikuwa:


i. Sahihi na maamuzi yake
ii. Alinuia: Wengi hukosoa, wachache tu ndio huchukua hatua.
iii. Alijiamini: Tegemeo thabiti lilimpatia Daudi ushindi. Sauli
akamvalisha Daudi mavazi ya kivita lakini kwa kuwa Daudi
hakuwa na uzoefu nayo, mavazi hayo yalikuwa mzigo kwake
hivyo akayavua. Aliamini katika kile alichonacho kwa wakati huo;
kile alicho na uzoefu nacho—kombeo (I Samwel 17:38-40)

You might also like