You are on page 1of 59

KITABU: MSAADA KATIKA MAISHA YA KILA SIKU (HELP

IN DAILY LIVING).

Mwandishi___ Ellen G. White(1827_1915)


Ellen G. White -Estate 1964.
© Copyright 2010 by the Ellen G. Whit Estate, Inc.

WAFASRI.......2024.

1.Baraka Z. Jipson...............Wa Rukwa


2.Jackline David.................Wa Dar es salaam
3.Minael Mjema..................Wa Kilimanjaro
4.Marco S. Magembe.........Wa Kagera
5.Daud Benjamin.................Wa Mwanza
6.Silvester Brella.................wa Arusha
7.kalebu poncian...................Wa Njombe
8.Ester G. Sayi.......................wa Simiyu
9.Ayubu Machanya....................wa Dar es salaam
10.Ibrahimu Thomas.............wa Mara
11.Juma P. Masasila..........wa Mwanza
12.Joshua kabadi........wa Kakola(Kahama)
13.Frank Isakary........
14.Deborah.......

Utangulizi mfupi....

Help in daily living, Ni kitabu chenye sura nne tu


kilichopendwa na kusomwa na watu wengi, hizi sura
zimechukuliwa kutoka kwa kitabu cha, The ministry of
healing (Huduma ya uponyaji), Sura hizi zimekuwa ni
msaada sana kwa watu, kwa kuwa zimesheheni ushauri,
maonyo, matumaini, kuleta amani, kuimarisha afya ya
kiakili, kiroho na kijamii, namna ya kukabiliana na
changamoto mbalimbali, upendo na ni mwongozo wa
kupata mibaraka katika maisha ya kila siku, kwa kuwa ni
msaada katika maisha ya kila siku kisome mara kwa mara
kwa kukirudia-rudia ili upate uzoefu zaidi wa Kikristo
hatimaye utaimarika kiroho, kiakili na kijamii pia, utakuwa
na mahusiano mazuri zaidi na Mungu na watu wengine.
Mungu akubariki sana na aendelee kuwa pamoja nawe.
Yaliyomo...

1.sura ya Kwanza: Maisha ya kila siku..............3


2.Sura ya pili: kuishi pamoja na wengine..............17
3.Sura ya tatu: Kuendeleza Tabia ya Kikristo..........36
4.Sura ya nne: Kusonga kuelekea kufikia shabaha........44

SURA YA 1

MAISHA YA KILA SIKU.


Kuna ufasaha wenye nguvu zaidi kuliko ule ufasaha wa
maneno katika maisha tulivu, kutokubadilika kwa maisha
halisi, na mkristo wa kweli, Mtu anaushawishi gani kuliko
kile anachokisema, Maofisa ambao walitumwa na Yesu
walirudi na taarifa ambayo kamwe mwanadamu hajawahi
nena Kama alivyonena, Lakini sababu ya hii ilikuwa
kwamba mwanadamu hajawahi kuishi Kama yeye
alivyoishi. Alikuwa na maisha yake tofauti na yalivyokuwa,
asingeweza kusema kama alivyofanya. Maneno yake
yalikuwa na nguvu ya kusadikisha, kwasababu yalitoka
kwenye moyo safi, mtakatifu, uliojaa upendo na huruma,
wema na ukweli. Ni tabia zetu na uzoefu ndio unaoamua
ushawishi wetu kwa wengine. Ili kuwashawishi wengine
lazima tuijue nguvu ya neema ya Kristo ndani ya mioyo na
maisha yetu wenyewe. Injili tunayoiwasilisha kwa ajili ya
kuokoa roho lazima iwe injili ambayo kwayo roho zetu
zimeokolewa. Ni kwa njia ya imani iliyo hai katika Kristo
Kama mwokozi wa roho, inaweza kufanya ushawishi wetu
uonekane katika ulimwengu wenye mashaka. Kama
tunataka kuwatoa wenye dhambi kwenye mkondo
unaokimbia kwa kasi, miguu yetu wenyewe lazima iwe
imara juu ya mwamba, Yesu Kristo.
Msimamo wa mkristo sio tu ishara ya nje, sio kuvaa
msalaba na taji bali ni kile ambacho kina dhihirisha
muungano wa mwanadamu na Mungu. Kwa uweza wa
neema yake ilionekana katika mabadiliko ya tabia,
ulimwengu unapaswa kusadikishwa kwamba Mungu
amemtuma mwanawe kama mkombozi wake. Hakuna
ushawishi mwingine unaoweza kuzunguka roho ya
mwanadamu, zaidi ya nguvu hiyo ya ushawishi wa maisha
yasiyo na ubinafsi. Hoja yenye nguvu inayounga mkono
hoja ya injili ni mkristo mwenye upendo na anayependeka.

NIDHAMU YA MAJARIBU.
Kuishi maisha kama haya, kutoa ushawishi Kama huo,
gharama kwa kila hatua ya jitihada, kujitolea na nidhamu ni
kwasababu wengi hawaelewi wanavyokata tamaa kwa
urahisi katika maisha ya Kikristo. Wengi huweka wakfu
maisha yao kwa utumishi wa Mungu na hushangaa na
kukatishwa tamaa na hujikuta kukabiliwa na vikwazo,
kuzingirwa na majaribu na kuchanganyikiwa, wanaomba ili
wafanane na tabia ya Kristo, ili wafae kwa kazi ya Bwana,
na wamewekwa kwenye hali ambazo zinaonekana kuibua
uovu wao wote wa asili, makosa yanadhihirishwa ambayo
hawakutazamia kama yatakuwepo. Kama ilivyokuwa kwa
Israeli ya kale wanauliza "ikiwa Mungu anatuongoza
kwanini mambo haya yote yanatupata?". Ni kwa sababu
Mungu anawaongoza ndiyo maana mambo hayo
yanawajia. Majaribu na vikwazo ni njia zilizochaguliwa na
Bwana za nidhamu na alizoziweka kuelekea kwenye
mafanikio. Yeye asomaye mioyo ya watu anawajua
wahusika kuliko wao wenyewe wanavyojijua. Anaona
kwamba wengi wana nguvu na hisia ambazo, zikielekezwa
ipasavyo, zinaweza kutumika katika maendeleo ya kazi
yake. Katika majaliwa yake anawaleta watu hawa katika
nafasi na hali mbalimbali ambazo wanaweza kugundua
katika tabia zao kasoro ambazo zimefichwa kutokana na
ujuzi wao wenyewe, yeye amewapa fursa ya kurekebisha
kasoro hizo na kufaa kwa ajili ya utumishi wake. Mara
nyingi yeye huruhusu moto wa mateso ya kuwashambulia
ili wapate kutakasika. Ukweli ni kwamba Bwana Yesu
anaona ndani yetu Kitu cha thamani ambacho anatamani
kukiendeleza, ikiwa haoni chochote ndani yetu ili aweze
kulitukuza jina lake, asingetumia muda kutusafisha ndani.
Bwana Hatupii mawe yasiyofaa ndani ya tanuru lake, ni
madini ya thamani ambayo yeye husafisha. Mhunzi
huweka chuma kwenye moto ili ajue ni kwa namna gani
chuma kitakuwa. Bwana huruhusu wateule wake kuwekwa
kwenye tanuru la mateso, ili kuthibitisha jinsi walivyo na
kama wanaweza kufaa kwa ajili ya kazi yake. Mfinyanzi
huchukua udongo na kuufinyanga kulingana na mapenzi
yake, huunda udongo na kuufanyia kazi, huugawanya-
gawanya na kuupasua-pasua na kisha kuunganisha tena
pamoja, huuloanisha kisha anaukausha, huruhusu ulale
kwa muda bila kuugusa, wakati unapokuwa kamilifu na
kufaa, huendelea na kazi ya kuufanya kuwa chombo. Yeye
huunda umbo katika uimara na kuking'alisha chombo.
Hukausha kwenye jua na kuoka katika tanuru, hapo
chombo kinakuwa kimefaa kwa matumizi. Ndivyo
mfinyanzi mkuu amelenga kutufinyanga na kutuunda, na
kama vile udongo ulivyo mikononi mwa mfinyanzi,
hatupaswi kufanya kazi ya mfinyanzi, kile tunachoweza
kukifanya ni kujitoa ili kufinyangwa na mfinyanzi mkuu.
"Wapenzi, msione kuwa ni ajabu ule msiba ulio kati yenu,
unaowapata kama moto ili kuwajaribu, kana kwamba ni
kitu kigeni kiwapatacho. Lakini kama mnavyoyashiriki
mateso ya Kristo, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu
wake mfurahi kwa shangwe." 1 Petro 4:12-13.
Katika mwanga kamili wa Mchana na katika kusikia mziki
wa sauti nyingine, ndege aliyefungiwa hataimba wimbo
ambao bwana wake anatafuta kumfudisha, hujifunza vifijo
na lugha hiyo lakini sio wimbo tofauti na toni husika,
bwana wake humweka na kumfungia ndege huyo sehemu
ambayo ataweza kusikia wimbo atakaouimba bwana wake,
katika giza, ndege hujaribu na kujaribu kuimba wimbo huo
mpaka ueleweke, naye huvuma kwa sauti kamilifu, kisha
ndege huletwa kwenye mwanga na baada ya hapo
anaweza kuimba vizuri wimbo huo katika mwanga.
Ndivyo Mungu hushughulika na watoto wake, ana wimbo
wa kutufundisha na wakati tumejifunza katikati ya vivuli
vya mateso, tunaweza kuimba wimbo huo baadaye na
hata milele.

CHAGUO LA MUNGU KATIKA KAZI ZA MAISHA YETU.


Wengi hawajaridhika na kazi zao za maisha, inaweza iwe
kwamba mazingira yao hayafai, muda wao umechukuliwa
na kazi zao za kawaida wanapofikiri juu ya wajibu mkuu.
Mara nyingi juhudi zao zinaonekana kutokuthaminiwa au
kutozaa matunda, hawana uhakika na wakati wao ujao.
Hebu tukumbuke kwamba kazi tunayoifanya, isiwe ni
chaguo letu bali inapaswa kukubaliwa Kama chaguo la
Mungu kwa ajili yetu. Iwe inapendeza au haipendezi
tunapaswa kufanya wajibu wetu, "Lo lote mkono wako
utakalolipata kulifanya, ulifanye kwa nguvu zako; kwa
kuwa hakuna kazi, wala shauri, wala maarifa, wala hekima,
huko kuzimu uendako wewe." Mhubiri 9:10
Ikiwa Bwana anataka sisi tupeleke ujumbe Ninawi,
haitampendeza pale tunapopeleka ujumbe Yafa au
Kapernaum. Ana sababu kutupeleka mahali ambapo
miguu yetu imeelekezwa, katika mahali hapo panaweza
kuwa na mtu anayehitaji msaada kwamba tunaweza
kumsaidia. Yeye aliyemtuma Filipo kwa mwethiopia, Petro
kwa akida wa kirumi, na msichana mdogo kwa Naamani,
Mshami nahodha, ni yeye yuleyule anayewatuma
wanaume na wanawake na vijana leo Kama wawakilishi
wake kwa wale wanaohitaji msaada na mwongozo wa
kiungu.
MIPANGO YA MUNGU ILIYOBORA.
Mara nyingi mipango yetu sio mipango ya Mungu,
anaweza kuona kwamba ni bora kwetu kwasababu zake,
kuzuia nia zetu, kama alivyofanya katika kisa cha Daudi.
Tunaweza kuwa na uhakika wa jambo moja kwamba Yeye
atabariki na kutumia kuendeleza kazi yake ya wale
wanaojitolea kwa hiari wao wenyewe na vyote
wanalivyonavyo kwa utukufu wake. Anaona ni vyema
asiwatimizie matamanio yao, hukataa na kuwapatia ishara
za upendo wake na amana na huduma nyingine. Katika
utunzaji wake wa upendo na maslahi yake kwetu, daima
yeye anatujua kuliko tunavyojijua, huzuia tusiwe na roho ya
ubinafsi, kutafuta kuridhika na kutimiza tamaa zetu
wenyewe. Daima mafunzo haya yanamudu mafunzo
muhimu sana ya kututayarisha kwa kazi ya juu zaidi, na
Mara nyingi mipango yetu hushindwa, lakini mipango ya
Mungu juu yetu hufanikiwa. Huhitaji tuwasilishe mambo
yetu yote kwake, tunapoitwa kujisalimisha na kusalimisha
mambo yetu yote ambayo katika hayo ni mema, tunaweza
kuwa na uhakika kwamba Mungu anafanya kazi nzuri zaidi
juu yetu, katika mafumbo ambayo yanatuumiza na
kutukatisha tamaa, tutawekwa wazi. Tunaona ya kwamba
maombi yetu yasiyojibiwa na matumaini ya kukatisha
tamaa yamekuwa miongoni mwa baraka zetu kuu.
Tunapaswa kuangalia Kila wajibu wetu kwa unyenyekevu
kama sababu takatifu na ni sehemu ya utumishi wa
Mungu, ombi letu kila siku linapaswa kuwa "Bwana
nisaidie kufanya niwezavyo, nifundishe namna ya kufanya
kazi kwa ubora zaidi, nipatie nguvu na furaha. Nisaidie
kuleta katika huduma yangu huduma ya upendo wa
mwokozi."

SOMO KUTOKA KWA MAISHA YA MUSA.


Fikiri juu ya uzoefu wa Musa, elimu aliyoipokea huko misri
kama mjukuu wa mfalme na mrithi mtarajiwa wa kiti cha
enzi, alikuwa mkamilifu, hakuna kitu kilipuuzwa ambacho
kilihesabiwa kufanya awe mtu wa hekima, kama wamisri
walivyofahamu hekima, alipokea mafunzo ya kiraia na
kijeshi. Alihisi kwamba alikuwa tayari kikamilifu kwa kazi
ya kuwakomboa Israeli kutoka katika utumwa wao. Lakini
Mungu alihukumu kinyume cha mawazo yake Musa.
Katika utunzaji wake alimchagua Musa, miaka arobani ya
mafunzo nyikani kama mchungaji wa kondoo. Elimu
ambayo Musa alikuwa ameipata huko misri ilikuwa
msaada kwake katika mambo mengine. Lakini elimu ya
thamani zaidi na maandalizi ya kazi yake ya maisha
ilikuwa na yalikuwa yale aliyopokea akiwa ameajiriwa
Kama mchungaji. Kiasilia Musa alikuwa na roho ya haraka,
huko misri jeshi lilifanikiwa chini ya kiongozi na kipenzi
cha mfalme na taifa kwa ujumla, yeye alikuwa amezoea
kupokea sifa nyingi. Alikuwa anewavutia watu kwake,
alitumaini kutimiza kwa uwezo wake mwenyewe kazi ya
kuwakomboa wana wa Israeli. Mambo aliyojifunza
yalikuwa tofauti Kama mwakilishi wa Mungu. Alipokuwa
akiongoza mifugo yake kwenye pori la milima na katika
malisho ya kijani kibichi katika mabonde alijifunza imani
na upole, uvumilivu, unyenyekevu na kujisahau. Alijifunza
kutunza wanyonge, kuwauguza wagonjwa, kuwatafuta
waliopotea, kuwavumilia waasi, kuwachunga wanakondoo
na kuwalea wazee na wanyonge, katika kazi hii Musa
alivutwa karibu na mchungaji mkuu. Aliunganishwa kwa
karibu na mtakatifu wa Israeli. Hakuwa na mpango tena
wa kufanya kazi kubwa, yeye alitafuta kufanya kazi
iliyofanywa kwa uaminifu kwa Mungu kwa malipo yake.
Alitambua uwepo wa Mungu katika mazingira yake. Asili
ya uumbaji, maumbile yalizungumza naye juu ya mambo
yasiyoonekana. Alimjua Mungu binafsi katika kutafakari
juu ya tabia yake, yeye alishiriki zaidi na zaidi kikamilifu
hisia ya uwepo wake, alipata kimbilio katika mikono
salama na milele. Baada ya tukio hili Musa alisikia wito
kutoka mbinguni ili kubadilisha fimbo ya uchungaji wake
na kuwa fimbo ya mamlaka, kuacha kundi lake la kondoo
na kuwaongoza waisraeli. Amri ya kiungu ilimkuta katika
hali ya kutokujiamini, mwongeaji wa taratibu-taratibu na
uoga. Alikuwa akizidiwa na hisia ya kutokuwa na uwezo
wa kuwa mnenaji badala ya Mungu. Lakini alikubali kazi
hiyo na kuweka tumaini lake lote kwa Bwana. Ukuu wa
utume wake aliitwa kutumia nguvu bora za akili yake.
Mungu akabariki utii wake na tayari akawa fasaha na
mwenye matumaini, mwenye kujitawala mwenyewe,
aliyefaa kwa kazi kuu kuliko zote alizopewa mwanadamu.
Juu yake imeandikwa "Wala hajainuka tena katika Israeli
nabii kama Musa, ambaye BWANA alimjua uso kwa uso;"
Kumb 34:10
Hebu wale wanaohisi kuwa kazi yao haithaminiwi, na
wanaotamani nafasi ya uwajibikaji zaidi, Mungu anasema
"Maana siko mashariki wala magharibi, Wala nyikani
itokako heshima. Bali Mungu ndiye ahukumuye; Humdhili
huyu na kumwinua huyu." Zaburi 75:6,7, Kila mtu ana
nafasi yake katika mpango wa mbinguni wa milele, ikiwa
tutajaza mahali hapo inategemea uaminifu wetu katika
kushirikiana na Mungu. Tunahitaji kuwa makini na
kujihurumia, kamwe usijishughulishe na hisia za kujihisi
kwamba wewe si wa kuheshimiwa kama unavyopaswa
kuheshimiwa, kwamba juhudi zako hazithaminiwi, pia
kwamba kazi yako ni ngumu sana. Hebu tukumbuke yale
ambayo Kristo alivumilia kwa ajili yetu sisi, kwa kuwa
hunyamazisha kila wazo la manung'uniko "Je! Unajitafutia
mambo makuu? Usiyatafute;" Yeremia 45:5
Bwana hana nafasi katika kazi yake kwa wale ambao
wanashauku kubwa ya kupata taji kuliko kubeba msalaba,
anataka watu ambao wana nia zaidi ya kufanya wajibu
wao kuliko kupokea thawabu yao, watu wanaotaka kanuni
zaidi kuliko motisha, wale ambao ni wanyenyekevu na
wale ambao wanafanya kazi kwa ajili ya Mungu, anaweza
asifanye onyesho kubwa na kujiona ni wa muhimu lakini
kazi yao ni muhimu zaidi. "Bora hekima, basi jipatie
hekima; Naam, kwa mapato yako yote jipatie ufahamu.
Umtukuze, naye atakukuza; Atakupatia heshima,
ukimkumbatia."Mithali 4:7-8, kwa sababu hawana dhamira
ya kuchukua wenyewe mkononi na kujirekebisha, wengi
huwa katika hali iliyozoeleka katika mwenendo mbaya
lakini haitakiwi kuwa hivyo, wanaweza kusitawisha nguvu
zao za kufanya huduma bora zaidi, na kisha watakuwa
katika uhitaji Kila wakati watathamini yote yenye thamani,
ikiwa Kuna yeyote anayestahili cheo cha juu zaidi, Bwana
ataweka mzigo, si juu yao peke yao, bali juu ya hao ambao
wamejaribiwa wanaojua thamani yao, na wale wanaoweza
kuelewa kusonga mbele, ni waliofanya kazi waliyopewa
siku baada ya siku ambao kwa wakati wake watasikia
mwito wa Mungu "njooni juu zaidi". Wachungaji
walipokuwa wanachunga mifugo yao katika milima ya
Bethlehemu, malaika kutoka mbinguni waliwatembelea.
Ndivyo hata leo mtenda kazi mnyenyekevu kwa Mungu,
akifuata na kufanya kazi ya Mungu, malaika wa Mungu
husimama kando yake, wakisikiliza maneno yake,
wakiangalia jinsi kazi yake inavyofanywa ili kuona ikiwa
majukumu makubwa zaidi yanaweza kukabidhiwa
mikononi mwake.

UJIRA
Kristo alipowaita wanafunzi wake wamfuate yeye
hakuwapatia matazamio ya kujifurahisha katika maisha
haya, hakuwapatia ahadi ya faida au heshima ya kidunia,
wala kuweka sharti lolote juu ya nini wanapaswa kupokea,
Kwa Mathayo alipokuwa ameketi kwenye ofisi ya ushuru,
mwokozi alisema "nifuate. Akaacha vyote, akaondoka,
akamfuata." Luka 5:27,28. Mathayo hakufanya hivyo kabla
ya kutoa huduma, hakusubiri na kudai mshahara fulani
sawa na kiasi alichopokea katika kazi yake ya awali. Bila
kuhoji wala kusita alimfuata Yesu. Ilikuwa inatosha kwake
kuwa pamoja na mwokozi, apate kuungana naye katika
kazi yake ndivyo ilivyokuwa kwa wale wanafunzi walioitwa
hapo awali. Wakati Yesu alipomwambia Petro na wenzake
wamfuate mara wakaacha mashua na nyavu zao, baadhi
ya wanafunzi hawa walikuwa na marafiki waliokuwa
wanawategemea kwa msaada, lakini walipopokea
mwaliko wa mwokozi, hawakupokea kwa kusita na kuuliza
"Nitaishi vipi na kuitunza familia yangu?" Walikuwa watiifu
kwa wito na wakati baadaye Yesu alipowauliza "Je! Hapo
nilipowatuma hamna mfuko, wala mkoba, wala viatu,
mlipungikiwa na kitu? Wakasema la!." Luka22:35. Leo
mwokozi anatuita Kama alivyomwita Mathayo, Yohana na
Petro kwa kazi yake. Ikiwa mioyo yetu itaguswa na upendo
wake, suala la fidia halitakuwa katika akili zetu, tutafurahi
kuwa watendakazi pamoja na Kristo, Na hatutaogopa
kumwamini yeye anayejali. Tukimfanya Mungu kuwa
nguvu yetu tutakuwa na mtazamo mzuri wa wajibu wetu
na matarajio yasiyo na ubinafsi, maisha yetu yatakuwa ya
kuchochewa na kusudi tukufu.

MUNGU ATATOA.
Wengi wanaodai kuwa Ni wafuasi wa Kristo wana moyo
wenye wasiwasi na kufadhaika kwasababu wanaogopa
kumtumainia Mungu. Hawataki kujisalimisha kikamilifu,
kwani wao wanajiepusha na matokeo kwamba
kujisalimisha huko kunaweza kuhusisha kutokupata amani.
Kuna wengi ambao mioyo yao inauma sana chini ya mzigo
wa utunzaji kwasababu wanatafuta kufikia kiwango cha
ulimwengu. Wamechagua kuutumikia ulimwengu na
wamekubali mashaka yake, wameiga desturi zake, hivyo
tabia zao zimeharibika na maisha yao kuwa uchovu. Hofu
yao ni kuzima nguvu za maisha. Mungu wetu anawataka
waweke kando nira hii ya utumwa, anawaalika kukubali
nira yake anasema, "Nira yangu ni laini na mzigo wangu Ni
mwepesi" Mtahayo 11:30. Wasiwasi Ni upofu na huwezi
kutambua siku zijazo, bali Yesu yeye anaona mwanzo na
mwisho. Katika kila shida yeye njia yake imetayarishwa
kuleta ahueni, "kwa kuwa BWANA, Mungu, ni jua na ngao,
BWANA atatoa neema na utukufu,. Hatawanyima kitu
chema hao waendao kwa ukamilifu". Zaburi 84:11. Baba
yetu ana njia elfu za kutupatia mahitaji yetu ambazo
hatuzijui, wale ambao wanakubali kanuni moja ya kufanya
huduma ya Mungu kuwa kuu zaidi, watakuta mashaka
yanatoweka na wataona njia iliyowazi mbele ya miguu yao,
utekelezaji kwa uaminifu wa majukumu ya leo ndio
maandalizi bora ya majaribio ya kesho, usikusanye pamoja
wajibu wa kesho na kuongeza kwenye mzigo wa leo. "Basi
msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia
yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake". Mathayo 6:34.
Hebu tuwe na matumaini na ujasiri, kukata tamaa katika
kazi ya Mungu ni dhambi na haina maana kufanya hivyo.
Mungu anajua kila hitaji letu kwa kuwa yupo kila wakati na
mahali popote mfalme wa wafalme. Mungu wetu
anayetunza maagano anaunganisha upole na utunzaji wa
mchungaji mwenye huruma. Nguvu zake ni kamili na ni
ahadi ya utimilifu wa uhakika wa ahadi zake kwa wote
wanaomtumaini. Ana njia ya kuondoa ugumu wa kila
namna, kwamba wale wanaomtumikia na kumheshimu
yeye aliyewaajiri atawaimarisha. Upendo wake uko mbali
na upendo mwingine wowote kama vile mbingu ziko juu ya
dunia. Yeye huangalia watoto wake kwa upendo usio na
kikomo na milele. Katika siu za giza wakati kuonekana
kunapoanza kufifia, uwe na imani kwa Mungu anafanya
mapenzi yake, anafanya mambo yote kuwa vema kwa ajili
ya watu wake. Nguvu ya wale wanao mpenda na
kumtumikia itafanya upya siku kwa siku. Ana uwezo na
yuko tayari kuwapa waja wake wote msaada wanaohitaji.
Atawapatia hekima ambayo mahitaji yao mbalimbali
yanadai. Mtume Paulo alijaribiwa alisema "Naye
akaniambia neema yangu yakutosha; maana uweza wangu
hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu
kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu. Kwa
hiyo napendezwa na udhaifu, na ufidhuli, na misiba, na
adha, na shida, kwa ajili ya Kristo. Maana niwapo dhaifu
ndipo nilipo na nguvu." 2wakorintho 12:9,10.

SURA YA 2

KUISHI PAMOJA NA WENGINE


Kila ushirika wa maisha unahitaji mazoezi ya kujidhibiti,
kuvumiliana, na kusikilizana kwa huruma. Tofauti zetu
katika tabia, mazoea, na elimu huifanya mitazamo yetu
kuhusu mambo kutofautiana. Tunahukumu tofauti.
Uelewa wetu wa ukweli, mawazo yetu kuhusu maisha
hayako sawa katika kila hali. Hakuna wawili ambao uzoefu
wao ni sawa kwa kila jambo. Majaribio ya mmoja siyo
majaribio ya mwingine. Majukumu ambayo mmoja
huyaona kuwa mepesi, kwa mwingine ni magumu na
kuleta mashaka.
Ukweli ni kwamba binadamu ni dhaifu, mjinga, na
anayeweza kukosea, hivyo kila mmoja wetu anapaswa
kuwa makini katika kumtathmini mwenzake. Hatujui
vyema jinsi matendo yetu yanavyoathiri uzoefu wa
wengine. Yale tunayofanya au kusema yanaweza
kuonekana machache kwetu, lakini tukiruhusiwa kuona,
tungegundua kwamba yanategemea matokeo muhimu
zaidi kwa wema au uovu.

KUWAZINGATIA WALIOBEBA MIZIGO


Wengi hawajabeba mzigo mwingi, mioyo yao haijapata
mateso halisi, hawajahisi mashaka na dhiki kwa niaba ya
wengine, hivyo hawawezi kuelewa kazi ya mtu aliyebeba
mzigo mwingi kweli. Hawa hawawezi kuthamini mzigo
wake kama vile mtoto anavyoshindwa kuelewa huduma na
taabu za mzigo wa baba yake. Mtoto anaweza kushangaa
juu ya hofu na mashaka ya baba yake. Haya yanaonekana
kuwa hayana maana kwake. Lakini baada ya miaka ya
uzoefu kuongezwa katika maisha yake, atakapojikuta
mwenyewe akichukua mizigo yake, atatazama nyuma
katika maisha ya baba yake na kuelewa kile kilichokuwa
kisichoeleweka zamani. Uzoefu mbaya umempa maarifa.
Kazi ya waliobeba mizigo wengi haijafahamika, kazi zao
hazijathaminiwa, mpaka kifo kimwangukie. Wakati
wengine wanachukua mizigo aliyoacha, na kukabiliana na
matatizo aliyokutana nayo, wanaweza kuelewa jinsi imani
na ujasiri wake ulivyofanyiwa majaribio. Mara nyingi,
makosa waliyokuwa wepesi kulaumu hupotea katika
macho yao. Uzoefu huwafundisha huruma. Mungu
huwaruhusu watu kuwekwa katika nafasi za majukumu.
Wanapotenda makosa, ana uwezo wa kusahihisha au
kuwaondoa. Tunapaswa kuwa makini kutoruhusu mikono
yetu ichukue kazi ya kuhukumu ambayo ni ya Mungu.
Mwenendo wa Daudi kwa Sauli una somo. Kwa amri ya
Mungu, Sauli alipakwa mafuta kuwa mfalme juu ya Israeli.
Kwa sababu ya kutotii, Bwana alitangaza kwamba ufalme
ungechukuliwa kutoka kwake; na bado ni namna gani
Daudi alivyokuwa mpole na mwenye heshima kwa Sauli!
Katika kujaribu kumuua Daudi, Sauli alienda jangwani na,
bila ya kuandamana na mtu yeyote, aliingia pangoni
ambapo Daudi na wanaume wake wa vita walikuwa
wamefichwa. "Na watu wa Daudi wakamwambia, Tazama
siku ambayo Bwana alikuambia, ... nitamtia adui yako
mikononi mwako, ili uweze kumtendea kama
itakavyokuwa vema kwako.... Naye akawaambia watu
wake, Bwana asiruhusu nifanye jambo hili kwa bwana
wangu, mpakwa mafuta wa Bwana, kuleta mkono wangu
juu yake, nikimwua, kwa sababu yeye ni mpakwa mafuta
wa Bwana. " Mwokozi anatuamuru, "Msihukumu, msije
mkahukumiwa. Kwa hukumu mliyohukumu, mtahukumiwa;
na kwa kipimo kile mpimiacho, kitapimwa kwenu tena."
Kumbuka kwamba karibuni rekodi ya maisha yako
itapitiwa mbele ya Mungu. Kumbuka pia kwamba
amesema, "Hauwezi kujitetea, Ewe mwanadamu, yeyote
wewe unayehukumu: ... kwa maana wewe unayehukumu
unatenda mambo yaleyale." 1 Samweli 24: 4-6; Mathayo 7:
1, 2; Warumi 2: 1.

UVUMILIVU KATIKA UOVU


Hatuna uwezo wa kuruhusu roho zetu ziharibike kwa
sababu ya kosa lolote halisi au lililodhaniwa kufanywa
kwetu. Nafsi yetu ni adui ambaye tunapaswa kuogopa
zaidi. Hakuna aina yoyote ya uovu unaokuwa na athari
mbaya zaidi kwa tabia kuliko hisia za kibinadamu
zisizodhibitiwa na Roho Mtakatifu. Hakuna ushindi
mwingine tutakaoupata utakaokuwa na thamani kama
ushindi uliopatikana juu ya nafsi.
Hatupaswi kuruhusu hisia zetu kuumizwa kirahisi.
Tunapaswa kuishi, siyo kwa kulinda hisia zetu au sifa zetu,
bali kwa kuokoa roho. Tunapojihusisha na wokovu wa
roho, tunakoma kujali tofauti ndogo ambazo mara nyingi
hujitokeza katika uhusiano wetu na wenzetu. Lolote
wengine wanavyofikiria juu yetu au kututendea, halipaswi
kuvuruga umoja wetu na Kristo, ushirika wa Roho. "Kwa
maana ni sifa gani kustahimili, mtendapo dhambi na
kupigwa makofi? Lakini kustahimili, mtendapo mema na
kupata mateso, huu ndio wema hasa mbele za Mungu." 1
Petro 2:20.
Usijilipize kisasi. Kadiri uwezavyo, epusha sababu zote za
kueleweka vibaya. Epuka kuonekana kama mbaya. Fanya
yote unayoweza, bila kusitisha kanuni, kusuluhisha na
wengine. "Basi ukileta sadaka yako madhabahuni, na huku
ukikumbuka ya kuwa ndugu yako ana neno juu yako,iache
sadaka yako mbele ya madhabahu, uende zako, upatane
kwanza na ndugu yako, kisha urudi uitoe sadaka yako."
Mathayo 5:23, 24.
Ikiwa maneno yasiyovumilika yamezungumzwa kwako,
kamwe usijibu kwa roho ile ile. Kumbuka kwamba "jawabu
laini hupunguza ghadhabu." Methali 15:1. Na kuna nguvu
ya ajabu katika kimya. Maneno yaliyosemwa kujibu mtu
mwenye hasira mara nyingi huwa yanachochea tu. Lakini
hasira ikikutana na kimya, kwa roho yenye upole na
uvumilivu, haraka inakufa.
Chini ya dhoruba ya maneno ya kulaumu na kusuta, weka
akili ikizingatia neno la Mungu. Acha akili na moyo wako
ujazwe na ahadi za Mungu. Ikiwa unatendwa vibaya au
kulaumiwa kwa makosa, badala ya kujibu kwa hasira, rudia
kwako mwenyewe ahadi za thamani:
"Usishindwe na mabaya, bali shinda mabaya kwa mema."
Warumi 12:21.
"Umkabidhi Bwana njia yako; pia umtumaini yeye; naye
atatenda." Na atatoa haki yako kama nuru, na hukumu
yako kama mchana. "Zaburi 37: 5, 6.
"Hakuna kitu kilichofunikwa, ambacho hakitafunuliwa;
wala hakuna kilichofichwa, ambacho hakitajulikana." Luka
12: 2.
"Umeufanya ubinadamu uwe wa kutembea juu ya vichwa
vyetu; tulipitia moto na maji; lakini ulituleta kutoka huko
mpaka mahali pa utajiri." Zaburi 66:12.
Tuna tabia ya kutafuta huruma na kutiwa moyo kwa
wenzetu, badala ya kumtazamia Yesu. Kwa rehema na
uaminifu wake, Mungu mara nyingi huruhusu wale ambao
tunaweka imani yetu kushindwa, ili tuweze kujifunza
upumbavu wa kumtumaini mwanadamu na kufanya mwili
wetu kuwa mkono wetu.
Tuamini kabisa, kwa unyenyekevu, na bila ubinafsi katika
Mungu. Anajua maumivu tunayoyahisi hadi ndani kabisa
ya nafsi zetu, lakini ambayo hatuwezi kuelezea. Wakati
mambo yote yanapoonekana giza na kushindwa
kufahamika, kumbuka maneno ya Kristo, "Lile nililolitenda
hutolijua sasa; lakini utalifahamu baadaye." Yohana 13:7.
Jifunze historia ya Yusufu na ya Danieli. Bwana hakuzuia
njama za watu waliotaka kuwadhuru; lakini Aliweka mbinu
hizi zote kufanya kazi kwa wema kwa watumishi Wake
ambao katikati ya majaribu na migogoro walihifadhi imani
na uaminifu wao.
Maadam tuko duniani, tutakutana na athari hasi. Kutakuwa
na vichocheo vya kujaribu utulivu; na ni kwa kukabiliana na
haya kwa roho sahihi ndio neema za Kikristo zinakua.
Ikiwa Kristo anakaa ndani yetu, tutakuwa wavumilivu,
wema, na wenye subira, wenye furaha katikati ya vikwazo
na hasira. Siku baada ya siku na mwaka baada ya mwaka
tutashinda nafsi, na kukua katika ujasiri wa kishujaa. Hii ni
kazi yetu iliyotengwa; lakini haiwezi kufanyika bila msaada
kutoka kwa Yesu, uamuzi thabiti, kusudi lisilopingika,
uangalifu endelevu, na maombi yasiyokoma. Kila mmoja
ana mapigano binafsi ya kupigana. Hata Mungu
mwenyewe hawezi kufanya tabia zetu kuwa za adilifu au
maisha yetu kuwa yenye manufaa, isipokuwa tufanye kazi
pamoja naye. Wale wanaokataa kupambana wanapoteza
nguvu na furaha ya ushindi.

HESABU BARAKA ZA MUNGU, SI MAJARIBU


Hatuhitaji kuweka rekodi yetu ya majaribu na matatizo,
machungu, na huzuni. Mambo haya yote yameandikwa
katika vitabu, na mbingu itawajibika kwa hayo. Wakati
tunahesabu mambo yasiyopendeza, mambo mengi
ambayo ni mazuri kufikiria yanapita kutoka katika
kumbukumbu, kama fadhili ya rehema ya Mungu
kutuzunguka kila wakati na upendo ambao malaika
wanastaajabu, kwamba Mungu alimtoa Mwanawe kufa
kwa ajili yetu. Ikiwa kama wafanyakazi wa Kristo mnahisi
kwamba mna machungu na majaribu makubwa kuliko
wale wengine, kumbukeni kwamba kwa ajili yenu kuna
amani ambayo haijulikani kwa wale wanaopuuza mizigo
hii. Kuna faraja na furaha katika huduma ya Kristo. Wacha
ulimwengu uone kwamba maisha pamoja naye
hayashindwi.
Ikiwa haujisikii mchangamfu na furaha, usizungumze juu
ya hisia zako. Usitie kivuli juu ya maisha ya wengine. Dini
isiyo na joto, isiyo na jua kamwe haivuti nafsi kwa Kristo.
Inawafukuza kutoka kwake na kuwapeleka kwenye nyavu
ambazo Shetani ametandaza kwa miguu ya wanaopotea.
Badala ya kufikiria kukata tamaa kwako, fikiria nguvu
unazoweza kudai kwa jina la Kristo. Acha mawazo yako
yashikilie mambo yasiyoonekana. Acha mawazo yako
yaongozwe kwa ushahidi wa upendo mkubwa wa Mungu
kwako. Imani inaweza kustahimili majaribu, kushinda
majaribu, kubeba kuvunjika moyo. Yesu anaishi kama
mwombezi wetu. Yote ni yetu ambayo upatanisho wake
unahakikisha.
Fikiria si kwamba Kristo anathamini wale wanaoishi kwa
ajili yake tu? Je, fikiria si kwamba yeye huwaona wale
ambao, kama yule mpendwa Yohana akiwa uhamishoni,
wanateseka kwa ajili yake katika mahali pagumu na
magumu? Mungu hatomruhusu mmoja wa wafanyakazi
wake wa kweli aachwe peke yake, kupambana dhidi ya
changamoto kubwa na kushindwa. Anawahifadhi kama
kito cha thamani kila mtu ambaye maisha yake
yamefichwa na Kristo ndani yake. Kuhusu kila mmoja wa
aina hiyo, anasema: "Mimi ... nitakufanya kuwa kama
muhuri: kwa maana nimekuteua." Hagai 2:23.
Kisha zungumza juu ya ahadi; zungumza juu ya nia ya
Yesu ya kutubariki. Hatusahau hata kwa muda mfupi
mmoja. Wakati, licha ya hali zisizofurahisha, tunapumzika
kwa imani katika upendo wake, na kujifunga naye, hisia ya
uwepo wake itatia moyo wa utulivu wa kina. Kuhusu yeye
mwenyewe Kristo alisema: "Sifanyi kitu kwa uwezo wangu;
lakini kama Baba yangu alivyonifundisha, ndivyo
ninavyosema mambo haya. Na yeye aliyenituma yu
pamoja nami; Baba hajaniondoa peke yangu; kwa sababu
mimi daima hufanya mambo yanayompendeza yeye."
Yohana 8: 28, 29.
Uwepo wa Baba ulimzunguka Kristo, na hakuna
kilichompata isipokuwa kile ambacho upendo usio na
kikomo uliruhusu kwa baraka ya ulimwengu. Hapa ndipo
chanzo chake cha faraja kilipo, na ni kwa ajili yetu. Yule
ambaye amejazwa na Roho wa Kristo anakaa ndani ya
Kristo. Kila kitu kinachomfikia kinatoka kwake Mwokozi,
ambaye anamzunguka na uwepo wake. Hakuna kitu
kinachoweza kumgusa isipokuwa kwa idhini ya Bwana.
Taabu zetu zote na huzuni, majaribu yetu yote na dhiki,
huzuni zetu zote na machungu, mateso yetu yote na
upungufu wetu, kwa ufupi, vitu vyote vinafanya kazi
pamoja kwa wema wetu. Uzoefu wote na mazingira ni
mafundi wa Mungu ambapo hutuletea mema.

USITAMKE UOVU
Tukiwa na ufahamu wa uvumilivu mkubwa wa Mungu
kwetu, hatutapatikana tukihukumu au kulaumu wengine.
Wakati Kristo alipokuwa akiishi duniani, jinsi ambavyo
wenzake wangeshangaa, ikiwa, baada ya kumfahamu,
wangemsikia akisema neno moja la kulaumu, la
kushutumu, au la kukosa uvumilivu. Tusiwasahau kamwe
wale wanaompenda wanapaswa kumwakilisha katika
tabia.
"Kwa upendo wa kindugu mpendane, kwa heshima
mkiwatanguliza wenzenu." "Si kulipa ubaya kwa ubaya, au
matusi kwa matusi: lakini badala yake baraka; mkijua
kwamba mmeitwa, mpate kurithi baraka." Warumi 12:10; 1
Petro 3:9.

HESHIMA
Bwana Yesu anahitaji kutambuliwa kwa haki za kila mtu.
Haki za kijamii za watu, na haki zao kama Wakristo,
zinapaswa kuchukuliwa kwa uzingatiaji. Wote wanapaswa
kushughulikiwa kwa ustadi na upole, kama wana wa kiume
na wa kike wa Mungu.
Ukristo utamfanya mtu kuwa mtu mwema. Kristo alikuwa
mwenye heshima, hata kwa watesaji wake; na wafuasi
wake wa kweli watadhihirisha roho ile ile. Angalia Paulo
alipopelekwa mbele ya watawala. Hotuba yake mbele ya
Agripa ni mfano wa ukunjufu wa kweli pamoja na
ushawishi wa kuvutia. Injili haihamasishi upole wa
kawaida unaotawala ulimwengu, bali heshima inayotokana
na wema wa kweli wa moyo.
Kutenda kwa uangalifu zaidi wa mambo ya nje ya maisha
haitoshi kuzuia malalamiko yote, hukumu kali, na maneno
yasiyofaa. Utakatifu wa kweli hautafichuliwa kamwe
kama mtu binafsi anachukuliwa kama lengo kuu. Upendo
lazima ukae moyoni. Mkristo anayeendelea kwa ukamilifu
hupata motisha za matendo yake kutoka kwa upendo wa
kina wa moyo wake kwa Bwana wake. Kutoka kwa mizizi
ya mapenzi yake kwa Kristo huchipua nia isiyojipenda kwa
ndugu zake. Upendo humpa mmiliki wake neema, maadili,
na upendezi wa tabia. Huangaza uso na kudhibiti sauti;
inatengeneza na kuinua kiumbe kizima.

UMUHIMU WA MAMBO MADOGO


Maisha yanajengwa kwa kiasi kikubwa, si kwa kujitolea
sana na mafanikio ya kushangaza, bali kwa mambo
madogo. Mara nyingi ni kupitia mambo madogo ambayo
yanaweza kuonekana kuwa si ya maana sana ndipo mema
makubwa au maovu yanapoingia katika maisha yetu. Ni
kwa kushindwa kwetu kuvumilia vipimo vinavyotujia katika
mambo madogo ndio tabia zinavyoundwa, na tabia
zinavyopotoshwa; na pale vipimo vikubwa vinapokuja,
vinatukuta hatuko tayari. Ni kwa kufuata kanuni katika
vipimo vya kila siku ndipo tunapopata nguvu ya kusimama
imara na waaminifu katika nafasi zenye hatari zaidi na
ngumu zaidi.

KUJIDHIBITI
Hatujawai kuwa peke yetu. Tumchague au la, tunae
mwandamizi. Kumbuka kuwa popote ulipo, ufanyapo
lolote, Mungu yupo. Hakuna kitu kinachosemwa au
kufanyika au kufikiriwa kinachoweza kuepuka kujua kwake.
Kila neno au tendo lako una shahidi - Mungu mtakatifu,
anaye chukia dhambi. Kabla ya kusema au kutenda, kila
wakati fikiria hili. Kama Mkristo, wewe ni mwanachama wa
familia ya kifalme, mtoto wa Mfalme wa mbinguni.
Usiseme neno, usifanye kitendo, ambacho kitaihujumu "ile
jina la thamani ambayo mmeitwa." Yakobo 2:7.
Jifunze kwa makini tabia ya uungu-ubinadamu, na daima
ujiulize, "Yesu angefanya nini kama angekuwa mahali
pangu?" Hii inapaswa kuwa kipimo cha wajibu wetu.
Usijitie mwenyewe bure katika jamii ya wale ambao kwa
sanaa zao wangepunguza azma yako ya kufanya mema,
au kuleta doa kwenye dhamiri yako. Usifanye kitu
chochote miongoni mwa wageni, barabarani, kwenye
magari, nyumbani, ambacho kingeonekana kidogo cha
uovu. Fanya kitu kila siku kuboresha, kizuri, na kuenzi
maisha ambayo Kristo ameununua kwa damu yake
mwenyewe.

ACHA SHERIA IONGOZE


Daima tenda kutokana na mwongozo, siyo tamaa ya
ghafla. Dhibiti mwenendo wa asili yako kwa unyenyekevu
na upole. Usiruhusu mchezo au maneno yasiyofaa.
Usiruhusu mizaha isiyo na maana itoke kwenye midomo
yako. Hata mawazo hayana ruhusa ya kufanya fujo.
Lazima yadhibitiwe, yakamatwe na kutiishwa kwa Kristo.
Yawekwe kwenye mambo matakatifu. Kisha, kwa neema
ya Kristo, yawe safi na ya kweli.
Tunahitaji hisia thabiti ya nguvu ya kustawisha ya mawazo
safi. Ulinzi pekee kwa roho yoyote ni mawazo sahihi.
Kama mtu "anavyofikiria moyoni mwake, ndivyo alivyo."
Methali 23:7. Nguvu ya kujizuia huimarika kwa mazoezi.
Kile ambacho kwa mara ya kwanza kinaonekana kuwa
kigumu, kwa marudio ya mara kwa mara kinakuwa rahisi,
mpaka mawazo na matendo sahihi yanakuwa ya kawaida.
Ikiwa tutataka, tunaweza kuacha kila kitu ambacho ni cha
bei rahisi na cha hafifu, na kufikia kiwango kikubwa;
tunaweza kuheshimiwa na watu na kupendwa na Mungu.

ONGEA NA SEMA VEMA KUHUSU WENGINE


Fanya mazoea ya kusema vema kuhusu wengine. Tilia
mkazo sifa njema za wale unaoshirikiana nao, na uone
kidogo iwezekanavyo makosa yao na mapungufu yao.
Ukijaribiwa kulalamika kuhusu kile ambacho mtu fulani
amesema au kufanya, sifia kitu katika maisha au tabia ya
mtu huyo. Jifunze kuwa na shukrani. Msifu Mungu kwa
upendo wake wa ajabu kwa kutupa Kristo kufa kwa ajili
yetu. Kamwe haisaidii kufikiria malalamiko yetu. Mungu
anatuita tuifikirie rehema yake na upendo wake usio na
kifani, ili tuweze kuwa na hamu ya kumsifu.
Wafanyakazi wa dhati hawana muda wa kuhangaika juu ya
makosa ya wengine. Hatuwezi kumudu kuishi kwa
makosa au mapungufu ya wengine. Kusema mabaya ni
laana yenye pande mbili, ikiwa na uzito zaidi kwa msemaji
kuliko kwa msikilizaji. Yule ambaye anatapanya mbegu za
ugomvi na mgawanyiko anavuna katika roho yake
mwenyewe matunda mauti. Tendo la kutafuta uovu kwa
wengine hulea uovu kwa wale wanaotafuta. Kwa
kujishughulisha na makosa ya wengine, tunabadilika kuwa
sura ile ile. Lakini kwa kumtazama Yesu, kuzungumza juu
ya upendo wake na ukamilifu wa tabia yake,
tunabadilishwa kuwa sura yake. Kwa kutafakari wazo kuu
aliloweka mbele yetu, tutainuliwa katika angahewa safi na
takatifu, hata uwepo wa Mungu. Tunapoishi hapa,
mwanga unatoka kwetu ambao unamulika wote walio na
uhusiano nasi.
Badala ya kukosoa na kuhukumu wengine, sema,
"Ninapaswa kufanya kazi ya wokovu wangu mwenyewe.
Ikiwa nitashirikiana na yule anayetamani kuokoa roho
yangu, lazima nijiangalie kwa makini. Lazima niondoe kila
uovu katika maisha yangu. Lazima nishinde kila kasoro.
Lazima nifanyike kuwa kiumbe kipya katika Kristo. Kisha,
badala ya kuwadhoofisha wale wanaopambana na uovu,
naweza kuwaimarisha kwa maneno ya kutia moyo.
Tunakuwa wakati mwingine wenye kutokujali kuhusu
wenzetu. Mara nyingi tunasahau kwamba wafanyakazi
wenzetu wanahitaji nguvu na furaha. Jitahidi
kuwahakikishia kuhusu masilahi na huruma yako.
Wasaidie kwa maombi yako, na waambie kwamba
unafanya hivyo.
SUBIRA KWA WALIOPOTOKA
Si wote wanaodai kuwa wafanyakazi wa Kristo ni
wanafunzi wa kweli. Miongoni mwa wale
wanaojitambulisha kwa jina lake, na hata kuhesabiwa kati
ya wafanyakazi wake, wapo wale ambao hawamwakilishi
yeye kwa tabia. Hawa hawatawaliwi na kanuni zake. Watu
hawa mara nyingi husababisha mkanganyiko na
kukatishwa tamaa kwa wafanyakazi wenzao ambao ni
wachanga katika uzoefu wa Kikristo; lakini hakuna haja ya
kudanganywa. Kristo ametupa mfano kamili. Anatuamuru
tumfuate yeye.
Mpaka mwisho wa nyakati kutakuwa na magugu kati ya
ngano. Wakati watumishi wa mwenye nyumba, kwa bidii
yao kwa heshima yake, walipoomba ruhusa ya kung'oa
magugu, bwana alisema: "Hapana; isije ikawa wakati
mnapokusanya magugu, mnamng'oa pia ngano pamoja
nao. Acheni wote wakue pamoja hata wakati wa mavuno."
Mathayo 13:29, 30.
Kwa rehema na uvumilivu mrefu, Mungu huwavumilia kwa
subira wakaidi na hata wale wenye moyo wa udanganyifu.
Miongoni mwa mitume waliochaguliwa na Kristo
alikuwemo Yuda msaliti. Je, basi, iwe sababu ya
kushangazwa au kukatishwa tamaa kwamba kuna wale
wenye mioyo ya udanganyifu miongoni mwa wafanyakazi
wake leo? Ikiwa yeye ambaye anasoma moyo angeweza
kumvumilia na yule ambaye alijua angekuwa msaliti wake,
kwa uvumilivu gani tunapaswa kuvumilia wale walio na
makosa.
Na si wote, hata kati ya wale wanaoonekana kuwa na
kasoro zaidi, ni kama Yuda. Petro, mwenye pupa, mwenye
haraka, na mwenye kujiamini mwenyewe, mara nyingi
alionekana kuwa na hasara kubwa zaidi kuliko Yuda. Mara
nyingi alikaripiwa na Mwokozi. Lakini maisha ya huduma
na dhabihu yalikuwa yapi! Ushuhuda gani unaotoa kuhusu
nguvu ya neema ya Mungu! Kadiri tuwezavyo, tunapaswa
kuwa kwa wengine kile ambacho Yesu alikuwa kwa
wanafunzi wake alipokuwa anatembea nao na
kuzungumza nao duniani.
Jichukulieni kama wamishonari, kwanza kabisa, kati ya
wafanyakazi wenzako. Mara nyingi inahitaji muda na
juhudi kubwa kumshinda mtu mmoja kwa Kristo. Na
wakati roho inapotoka dhambini kuelekea kwenye haki,
kuna furaha mbele ya malaika. Je, mnadhani kwamba
roho watumishi wanaowachunguza hawa wana furaha
kuona jinsi wanavyoshughulikiwa kwa kutojaliwa na
baadhi ambao wanadai kuwa Wakristo? Ikiwa Yesu
angelitutendea sisi kama tunavyowatendea mara nyingi
wenzetu, ni nani kati yetu angeokolewa?
Kumbukeni kwamba hamwezi kusoma mioyo. Hamjui ni
nini kinachowachochea kufanya vitendo ambavyo kwenu
vinaonekana kuwa sahihi. Wapo wengi ambao hawajapata
elimu sahihi; tabia zao zimevurugika, ni ngumu na
zimepinda, na zinaonekana kuwa na matatizo kwa kila
namna. Lakini neema ya Kristo inaweza kuwabadilisha.
Kamwe msiwatupilie mbali, kamwe msiwapeleke kwenye
kukata tamaa au kukata tamaa kwa kusema,
"Umenisikitisha, na sitajaribu kukuimarisha." Maneno
machache yaliyosemwa haraka chini ya kuchokoza - tu
wanachostahili - yanaweza kukata nyuzi za ushawishi
ambazo zingepaswa kufunga mioyo yao na yetu.

ATHARI YA MAISHA YA KIKRISTO YENYE UWIANO


Maisha yenye uwiano, uvumilivu wenye subira, roho isiyo
na ghadhabu chini ya kero, ni hoja ya kipekee na wito wa
heshima. Ikiwa umepata fursa na faida ambazo
hazijawapata wengine, chukua hili kwa uzito, na kuwa
mwalimu mwenye hekima, makini, na mpole daima.
Ili kuweza kupata muhuri wa wazi na imara kwenye
mshumaa, hupitishi muhuri juu yake kwa haraka au kwa
ghasia; bali unaweka muhuri kwa upole kwenye mshumaa
wa plastiki na kwa utulivu na kwa umakini unautia chini
mpaka ukae kwenye kalibu. Kwa njia kama hiyo shughulika
na roho za binadamu. Uendelezo wa athari ya Kikristo ni
siri ya nguvu yake, na hii inategemea uimara wako wa
kufichua tabia ya Kristo. Saidia wale waliofanya makosa
kwa kuwaambia juu ya uzoefu wako. Onyesha jinsi,
unapofanya makosa makubwa, uvumilivu, upendo, na
msaada kutoka kwa wafanyakazi wenzako ulivyokupa
ujasiri na tumaini.
Hadi hukumu hutajua kamwe athari ya njia ya fadhili na
upole kuelekea wasio na uaminifu, wasiokuwa na mantiki,
wasiofaa. Tunapokutana na ukosefu wa shukrani na uasi
wa uaminifu wa imani, tunachochea kuonyesha dharau au
hasira yetu. Hili ni jambo ambalo wanaokosa wanatarajia;
wamejiandaa kwa hilo. Lakini uvumilivu wa fadhili
unawashangaza na mara nyingi huamsha hamu yao ya
maisha yenye heshima zaidi.
“Ndugu, mtu akipatikana katika kosa, ninyi mlio wa kiroho,
mnawarejesha watu wa namna hiyo kwa roho ya upole;
ukifikiri juu yako mwenyewe, usije ukajaribiwa pia.
Funikeni mzigo wa kila mmoja, nanyi mtatimiza hivyo
sheria ya Kristo.” Wagalatia 6:1, 2.
Wote wanaojitangaza kuwa watoto wa Mungu wanapaswa
kukumbuka kwamba kama wamishonari watakuwa katika
mawasiliano na madarasa yote ya akili. Kuna wale walio
tasa na wale wenye utu, wanyenyekevu na wenye kiburi,
waumini na wanaoshuku, walioelimika na wasioelimika,
matajiri na maskini. Akili hizi tofauti haziwezi
kushughulikiwa kwa njia ile ile; lakini wote wanahitaji
wema na huruma. Kwa mawasiliano ya kila mmoja akili
zetu zinapaswa kupokea upole na usafi. Tunategemeana
kwa kila mmoja, tumeunganishwa kwa karibu na vifungo
vya ndugu kibinadamu. "Mbingu zinavyotujenga kila
mmoja kwa mwingine kuitegemeana, Bwana au mtumishi
au rafiki, Kila mmoja kwa mwingine kutegemeana, Mpaka
udhaifu wa mtu mmoja unavyo kuwa nguvu ya wote."
Ni kwa njia ya mahusiano ya kijamii ambapo Ukristo
unakuja kuwa katika mawasiliano na dunia. Kila mtu
ambaye amepokea mwanga wa ki_Mungu anapaswa
kumwaga nuru katika njia yenye giza ya wale
wasiofahamu njia bora. Nguvu ya kijamii, iliyotakaswa na
Roho ya Kristo, lazima itumiwe katika kuwaleta watu kwa
Mwokozi. Kristo hataki kufichwa moyoni kama hazina
inayotamaniwa, takatifu na tamu, kufurahiwa pekee na
mmiliki. Tunapaswa kuwa na Kristo ndani yetu kama
kisima cha maji, kikiota hadi uzima wa milele, kurejesha
wote wanaokuja katika mawasiliano nasi.

SURA YA 3

KUENDELEZA TABIA YA KIKIRSTO


Maisha ya Kikristo ni zaidi ya watu
wanavyochukulia.Hayahusishi tu mambo kama ustaarabu
, upole na wema. Vitu hivi ni vya muhimu, lakini inahitajika
pia nguvu ya ujasiri na uvumilivu. Njia ambayo Kristo
alipitia ni njia nyembamba, yenye kujikana nafsi. Kuingia
katika njia hiyo na kuweza kusonga mbele katika magumu
na kukatishwa tamaa kunahitaji watu wasio wanyonge.

NGUVU YA TABIA
Watu thabiti wanahitajika, watu ambao hawatasubiri kila
kizuizi kuondolewa katika njia yao na njia yao kuwa safi,
watu ambao watatoa hamasa na kuamsha ari za wengine
waliokata tamaa, watu ambao mioyo yao ina upendo wa
Kristo na ambao mikono yao ipo tayari kufanya kazi ya
Bwana wao.Baadhi ya watu ambao wanajiingiza katika
huduma ya kimisionari ni dhaifu, sio jasiri, hawana roho wa
Mungu na ni wepesi wa kukata tamaa. Hawana msukumo
na kazi hiyo. Hawana sifa chanya za tabia zinazotoa
uwezo wa kufanya jambo fulani—roho na nguvu isiyokata
tamaa. Wale ambao wangepata mafanikio lazima wawe
na ujasiri na matumaini. Wanapaswa kusitawisha sio tu
sifa tulivu, bali pia sifa tendaji. Wakati wakiwa na jukumu
la kutoa jawabu la upole linalogeuza hasira, wanapaswa
kuvaa roho ya kishujaa kuweza kukataa maovu. Kwa
upendo unaostahimili kila kitu, wanahitaji nguvu ya tabia
ambayo itafanya ushawishi wao kuwa na nguvu
chanya.Wengine hawana uimara wa tabia. Malengo yao na
mipango yao haina uendelezo wala ufafanuzi
unaoeleweka. Matumizi yake ni madogo sana katika
ulimwengu huu. Wanapaswa kuacha udhaifu huu, kukosa
maamuzi na uzembe. Ni lazima tuwe na uadilifu thabiti,
uadilifu ambao hauwezi kubembelezwa, kuhongwa, au
kutishwa.

UTAMADUNI WA KIAKILI
Mungu anatamani kila nafasi tunayoipata tuitumie katika
kujiandaa na kazi yake. Anategemea tuweke nguvu zetu
zote katika utendaji wake na kuweka mioyo yetu tayari
kwa kufanya kazi ya Mungu.Wengi wetu tuna sifa za
kufanya mambo makubwa katika kazi ya Mungu lakini
tunatimiza vichache kwasababu tunafanya kwa uchache.
Maelfu ya watu huishi katika haya maisha kama vile
hawajui lengo la kuishi, hawana viwango vya juu
walivyojiwekea kuvifikia. Kristo alilipa deni kubwa kwa ajili
yetu, na kutokana na deni hilo alilotulipia basi anatamani
sisi tuwe watu tunaojithamini. Usiwe mtu wa kuridhishwa
na viwango dhaifu. Sisi hatupaswi kuwa watu wa hivyo na
hata Mungu hajataka tuwe watu wa hivyo. Mungu
ametupa uwezo wa kufikiri, sio kubaki bila shughuli au
kupotoshwa kwa mambo ya kidunia na ya uchafu, bali
tuendelezwe kwa upeo wa juu, tuliosafishwa, tuliotakaswa,
tuliokuzwa, na kutumika katika kuendeleza maslahi ya
ufalme Wake.Hakuna anayepaswa kukubali kuwa mashine
tu inayoongozwa na akili ya mtu mwingine. Mungu
ametupa uwezo wa kufikiri na kufanya, na ni kwa kufanya
kwa umakini, ukimtazama yeye kwa hekima kwamba
utaweza kuvumilia matatizo. Simama katika tabia na hisia
za kipekee alizokupatia Mungu. Usiwe kivuli cha mtu
mwingine. Tarajia kwamba Bwana atafanya kazi yake
kupitia wewe hivyo hivyo ulivyo.Kamwe usifikiri kwamba
tayari umeshajifunza vya kutosha , na hivyo ukae na
kutuliza juhudi zako. Akili inayofanya kazi ndio kipimo cha
kuwa mtu. Unapaswa kuendelea kujifunza kila siku kwa
maisha yako yote, kila siku unapaswa kusoma na
kutendea kazi yale uliyojifunza. Kumbuka kwamba katika
nafasi yoyote utakayokuwepo unazaa matunda ya
muendelezo wa tabia yako. Chochote kile utakachokifanya,
kifanye kwa usahihi, kwa uangalifu; uishinde ile hali ya
kutaka kurahisisha kazi.

UNAFANYEJE KAZI?
Ile roho na misingi unayoitumia katika kufanya kazi zako
za kila siku, inapaswa iwe hivyo hivyo kwa maisha yako
yote. Wale wanaotamani kiasi maalum kisichobadilika
cha mshahara uliowekwa na ambao wanatamani kuwa na
matokeo mazuri katika kazi zao bila kukutana na
changamoto zozote sio ambao Mungu anawaita katika
shamba lake. Wale ambao wanajifunza namna ya kutumia
kwa uchache nguvu zao, akili na maadili sio watu ambao
kwao Mungu atawashushia baraka zale tele. Mfano wao ni
wa kuambukiza. Wapo tu kwa ajili ya maslahi binafsi. Wale
wanaohitaji kuwekewa uangalizi na kufanya majukumu tu
ambayo anakuwa amewekewa kwa ratiba ya siku hiyo si
miongoni wa wale Mungu atakaowatangaza kuwa ni
wema na waaminifu. Wanahitajika watumishi
watakaodhihirisha uwezo, uadilifu,na bidii, wale waliopo
tayari kufanya chochote kinachohitajika kufanywa.Wengi
wanakuwa hawana tija kwa kukwepa majukumu kwa
kuogopa kushindwa. Hivyo wanashindwa kupata elimu
hiyo ambayo ni matokeo ya uzoefu, na kusoma ambayo
kwayo faida zilizopatikana haziwezi kuwapata wao. Mtu
anaweza kubadili mazingira, lakini mazingira hayapaswi
kumbadilisha mtu. Tunapaswa kuchukulia mazingira kama
kifaa katika kufanya kazi zetu. Tunapaswa kuzoea
mazingira lakini hatupaswi kuruhusu mazingira yatuzoee.
Watu mashuhuri ni wale ambao walipingwa, kudhalilishwa
na kukataliwa. Kwa kuziweka nguvu zao katika vitendo,
vikwazo wanavyokutana navyo vinawathibitishia kuwa
kuna baraka chanya katika hilo wanalolifanya.
Wanajijengea kujitegemea. Migogoro na kuchanganyikiwa
inawapa jitihada za kumwamini Mungu, na nikwa uthabiti
huo unaokuza nguvu.

NIA KATIKA HUDUMA.


Kristo hakutoa huduma dumavu. Hakupima kazi yake kwa
masaa. Muda wake, moyo wake, roho na nguvu alivitoa
kazini kwa manufaa ya wanadamu. Alijitaabisha nyakati za
mchana, na nyakati ndefu za usiku alikesha akiomba
neema na ustahimilivu aweze kufanya kazi kubwa. Kwa
vilio na machozi alituma maombi yake mbinguni kuwa asili
ya ubinadamu iweze kutiwa nguvu ili aweze kuvumilia
changamoto zote atakazokutana nazo katika huduma
yake ya kumkomboa mwanadamu. Kwa watumishi wake
anasema, "nimewapa ninyi mfano, kwamba mfanye kama
nilivyofanya." Yohana 13:15

"Upendo wa Kristo" Paulo alisema "hutubidisha"


2Wakorintho 5:14. Hii ndiyo ilikuwa kanuni inayotumika ya
mwenendo wake, ilikuwa nia yake ya nguvu. Iwapo bidii
yake katika njia ya wajibu ilionyesha kuchoka kwa muda,
mtazamo mmoja kwenye msalaba ulimfanya ajifunge
upya viuno katika akili yake na kusonga mbele katika njia
ya kujikana nafsi. Katika utumishi wake kwa ajili ya
wapendwa wake alitumia muda wake mwingi kuwafunulia
wengi juu ya upendo usio na kikomo wa kafara ya Kristo
kwa watu wake.
Ilikuwa ya maana kiasi gani, ilikuwa ya mguso kiasi gani
kauli hii: _“Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu
Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa
alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa
umaskini wake." 2 Wakorintho 8:9._ Maisha ya dharau na
kudhalilishwa hakuona ni kitu mpaka alipofanikisha
kumkomboa mwanadamu. Hapakuwa na wakati
aliopumzika toka alipotoka kwenye kiti cha enzi mbinguni
hadi msalabani. Upendo wake kwa mwandamu ulimfanya
akubali kila dharau na mateso ya kila namna. Paulo
anatuonya kwamba: "Kila mtu asiangalie mambo yake
mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.
Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia
ndani ya Kristo Yesu; ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna
namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na
Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; bali alijifanya
kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa
ana mfano wa wanadamu;tena, alipoonekana ana umbo
kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti,
naam, mauti ya msalaba." Wafilipi 2:4-8

Paulo alikuwa na shauku kubwa kwamba kufedheheshwa


kwa Kristo kunapaswa kuonekana na kutambuliwa.
Alishawishika kuamini kwamba kama watu wangetambua
thamani ya kafara iliyofanya na Mfalme wa mbinguni,
ubinfsi ungeondoka mioyoni mwao. Mtume huyu alitumia
muda mwingine kuelezea nukta baada ya nukta ili tuweze
kuelewa ukubwa wa kile alichofanya mkombozi kwa ajili
ya wadhambi. kwanza anapeleka fikra zetu katika nafasi
aliyokuwa nayo Kristo mbinguni kwa baba yake, akiwaza
namna atakavyoacha utukufu wake na kujishusha hadi
chini kuishi maisha ya mwanadamu na kubeba dharau
zote hadi kufa kifo cha aibu, kifo cha msalaba. Hivi
tunaweza kuelezea juu ya upendo huu wa Mungu wa ajabu
pasipo kuonyesha shukrani na upendo, na hisia ya kina ya
ukweli kwamba tupo hivi tulivyo leo kwasabu upendo wake
kwetu? Bwana kama huyo hatakiwi kutumikiwa kwa
kununa wala ubinafsi. Petro anasema, “Nanyi mfahamu
kwamba mlikombolewa si kwa vitu viharibikavyo, kwa
fedha au dhahabu..” 1 Petro 1:18_ . Loo, kama haya
yangetosha kununua wokovu wa mwanadamu, ni rahisi
kiasi gani kutimizwa na yule ambaye anasema kwamba ;
_“Fedha ni mali yangu, na dhahabu ni mali yangu, asema
Bwana wa majeshi.”Hagai 2:8. Lakini mdhambi angeweza
tu kuokolewa kwa damu ya thamani ya mwana wa Mungu.
Wale ambao hawatambui umuhimu wa kafara hii ya
thamani, hujizuia wenyewe kutoka kwa huduma ya Kristo,
hivyo basi wataangamia katika ubinafsi wao.

KUSUDI MOJA
Katika maisha ya Kristo, kila kitu alichofanya kilikuwa
chini ya mpango kazi wake aliokuja kuukamilisha. Na
ibada sawa, kujinyima sawa na kujitolea , utiifu uleule
katika neno la Mungu, udhihirike kwa wanafunzi wake pia.
Kila mmoja anayempokea Kristo kama mwokozi wake
binafsi atatamani kupendelea kufanya kazi ya Mungu.
Akitafakari kile mbingu kilichofanya kwa ajili yake, moyo
wake utaondoka ukiwa umejawa na upendo na shukrani
kubwa. Ana shauku ya kuonyesha shukrani zake kwa
kujitolea uwezo wake katika kazi ya Mungu. Anatamani
kuonyesha upendo wake kwa Kristo na kwa kile
alichofanya kwa ajili yake. Mtumishi mwema wa Mungu
atafanya vizuri katika kazi yake kwani kwa kufanya hivyo
atakuwa anamtukuza Bwana wake. Atafanya kwa usahihi
kwa ajili ya kufikia matakwa ya Mungu. Atajitahidi
kuboresha uwezo wake wote. Atafanya kila awezalo kwa
ajili ya Mungu. Tamanio lake kuu itakuwa ni Kristo aweze
kupokea heshima na huduma kamilifu. kuna picha
inayowakilisha fahali aliyesimama kati ya jembe na
madhabahu yenye maandishi; "Tayari kwa lolote", tayari
kufanya kazi kwenye mtaro au kutolewa kwenye
madhabahu ya dhabihu. Huu ndio msimamo wa mtoto wa
kweli wa Mungu, nia ya kwenda mahali ambapo kazi inaita,
kujikana nafsi, kutoa dhabihu kwa ajili ya Mkombozi.

SURA YA 4

KUSONGA KUELEKEA KUFIKIA SHABAHA

Tunahitaji daima ufunuo mpya wa Kristo, uzoefu wa kila


siku unaopatana na mafundisho Yake. Mafanikio ya juu na
matakatifu yamo ndani ya uwezo wetu. Kusudi la Mungu
kwetu ni ukuaji daima katika ujuzi na wema. Sheria yake ni
mwangwi wa sauti yake, ikitoa mwaliko kwa wote, “Njooni
juu zaidi. muwe watakatifu, watakatifu zaidi.” Kila siku
tunaweza kusonga mbele katika ukamilifu wa tabia ya
Kikristo. Wale wanaojishughulisha na huduma kwa ajili ya
Bwana wanahitaji uzoefu wa juu zaidi, wa kina, mpana,
kuliko ambavyo wengi wamefikiria kuwa nao. Wengi
ambao tayari ni wanafamilia katika familia kubwa ya
Mungu wanajua kidogo ni nini inamaanisha kuutazama
utukufu wake na kubadilishwa kutoka utukufu hadi
utukufu. Wengi wana mtazamo mdogo wa ubora wa
Kristo, na mioyo yao inasisimka kwa furaha. Wanatamani
hisia kamili zaidi ya upendo wa Mwokozi. Hebu wathamini
kila tumaini la nafsi kwa Mungu. Roho Mtakatifu hufanya
kazi na wale ambao watafanya kazi, huwafinyanga wale
ambao watafinyangwa, huwatengeneza wale
watakaotengenezwa. Jipeni utamaduni wa mawazo ya
kiroho na ushirika mtakatifu. Mmeona lakini miale ya
kwanza ya mapambazuko ya utukufu wake. Kwa kadiri
mnavyoendelea kumjua Bwana, Mtajua kwamba “Njia ya
wenye haki ni kama nuru ing’aayo ikizidi kung’aa hata
mchana mkamilifu” Mithali 4:18 , R.V “Hayo
nimewaambia,” Kristo alisema, “ili furaha yangu iwe ndani
yenu, na furaha yenu itimizwe.” Yohana 15:11. Mbele zake,
Kristo aliona matokeo ya utume Wake. Maisha yake
duniani, yaliyojaa taabu na kujitoa kafara yalifarijiwa na
wazo kwamba hangepitia uchungu huu bure. Kwa kutoa
uhai wake kwa ajili ya wanadamu angerudisha katika
ubinadamu sura ya Mungu. Angetuinua kutoka mavumbini,
aturekebishe tabia mfano wa tabia yake, na kuifanya kuwa
nzuri kwa utukufu wake mwenyewe.
Kristo aliona taabu ya nafsi yake na akaridhika. Alitazama
anga la umilele na akaona furaha ya wale ambao kwa
fedheha yake wangepokea msamaha na uzima wa milele.
Alijeruhiwa kwa makosa yao, alichubuliwa kwa maovu yao,
adhabu ya amani yao ilikuwa juu yake, na kwa kupigwa
kwake waliponywa. Alisikia kelele za waliokombolewa.
Alisikia waliokombolewa wakiimba wimbo wa Musa na wa
Mwanakondoo. Ingawa ubatizo wa damu lazima kwanza
upokelewe, ingawa dhambi za ulimwengu zilikuwaziilemee
nafsi yake isiyo na hatia, ingawa kivuli cha ole isiyoelezeka
kilikuwa juu yake; bado kwa furaha iliyowekwa mbele yake
alichagua kustahimili msalaba na aliidharau aibu. Furaha
hii wafuasi wake wote wanapaswa kuishiriki. Ingawa
maisha baada ya kifo ni makuu na yenye utukufu, thawabu
yetu si yote ya kuhifadhiwa kwa ajili ya wakati wa
ukombozi wa mwisho. Hata hapa tupo kwa imani kuingia
katika furaha ya Mwokozi. Kama Musa, tunapaswa
kuvumilia katika kumwona asiyeonekana. Kanisa sasa liko
vitani. Sasa tunakabiliwa na ulimwengu katika giza, karibu
kabisa kutolewa kwa ibada ya sanamu. Lakini siku inakuja
ambapo vita vitakuwa vimepiganwa, ushindi umepatikana.
Mapenzi ya Mungu ni kufanyika duniani kama vile
mbinguni. Mataifa ya waliokombolewa hawatajua sheria
nyingine isipokuwa sheria ya mbinguni. Wote watakuwa
familia yenye furaha, yenye umoja, iliyovikwa mavazi ya
kifahari mavazi ya sifa na shukrani - vazi la haki ya Kristo.
Viumbe vyote, katika uzuri wake wa kupita vitamtolea
Mungu zawadi ya sifa na kuabudu. Ulimwengu utaoshwa
katika nuru ya mbinguni. Mwanga wa mwezi utakuwa
kama mwanga wa jua, na mwanga wa jua utakuwa
mkubwa mara saba kuliko ulivyo sasa. Miaka itasonga
kwa furaha. Nyota za asubuhi zitaimba pamoja, wana wa
Mungu watapiga kelele kwa furaha, wakati Mungu na
Kristo wataungana kusema, “Hapatakuwa na dhambi tena,
wala mauti haitakuwapo tena.” Maono haya ya utukufu
ujao, matukio yanayoonyeshwa na mkono wa Mungu,
yanapaswa kuwa ya wakfu mkubwa kwa watoto Wake.

KUTATHMINI MAMBO YA WAKATI NA UMILELE

Simama kwenye kizingiti cha umilele na usikie ukaribisho


wa neema wanaopewa wale ambao katika maisha haya
wameshirikiana na Kristo, kuona kama fursa na heshima
kuteseka kwa ajili ya Kristo. Pamoja na Malaika, wanatupa
taji zao miguuni pa Mwokozi, wakisema, “Anastahili
Mwana-Kondoo aliyechinjwa kuupokea uweza na utajiri, na
hekima, na nguvu, na heshima, na utukufu, na baraka.
Heshima, na utukufu, na uweza una yeye aketiye juu ya kiti
cha enzi, na yeye Mwana-Kondoo hata milele na milele.”
Ufunuo 5:12, 13 . Hapo waliokombolewa wakawasalimia
wale walioelekeza kwa Mwokozi aliyeinuliwa.
Wakaungana katika kumsifu Yeye aliyekufa ili wanadamu
wapate uzima huo kipimo na uzima wa Mungu. Mapigano
yamekwisha. Dhiki na ugomvi umefika kikomo. Nyimbo za
ushindi zimejaza mbingu yote pale waliokombolewa
wakisimama kukizunguka kiti cha enzi cha Mungu. Wote
wanachukua mzigo wa furaha, “Anastahili Mwana-Kondoo
aliyechinjwa” na ametukomboa kwa Mungu. “Kisha
nikaona, na tazama, mkutano mkubwa sana ambao
hapana mtu awezaye kuuhesabu, watu wa kila taifa, na
kabila, na jamaa, na lugha, wamesimama mbele ya kile kiti
cha enzi, mbele ya Mwana-Kondoo, wamevikwa mavazi
meupe, wana matawi ya mitende mikononi mwao; wakalia
kwa sauti kuu, wakisema, Wokovu una Mungu wetu
aketiye katika kiti cha enzi, na Mwana-Kondoo.” Ufunuo
7:9, 10. “Hawa ndio wanatoka katika dhiki ile iliyo kuu; nao
wamefua mavazi yao, na kuyafanya meupe katika damu
ya Mwanakondoo. Kwa hiyo wako mbele ya kiti cha enzi
cha Mungu, nao wanamtumikia mchana na usiku katika
hekalu lake , na yeye aketiye katika kiti cha enzi atatanda
hema yake juu yao.. Hawataona njaa tena, wala
hawataona kiu tena; wala jua halitawapiga, wala hari iliyo
yote. Kwa maana Mwana-Kondoo aliye katikati ya kiti cha
enzi, atawachunga, naye atawaongoza kwenye
chemchemi za maji yenye uhai, na Mungu atayafuta
machozi yote katika macho yao." "Wala mauti
haitakuwapo tena, wala maombolezo, wala kilio, wala
maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya
kwanza yamekwisha kupita.” Ufunuo 7:14-17; Ufunuo 21:4.
Tunahitaji kuweka mbele yetu daima maono haya ya
mambo yasiyoonekana. Hivyo ndivyo tutaweza kuweka
thamani halisi ya mambo ya milele na mambo ya wakati.
Ni vitu hivi ndivyo vitatupa uwezo wa kuwashawishi
wengine kwa ajili ya maisha ya juu.

KATIKA MLIMA PAMOJA NA MUNGU


“Njooni kwangu mlimani,” Mungu anatualika. Musa, kabla
hajawa mtumishi wa Mungu katika ukombozi wa Israeli,
iliteuliwa miaka arobaini ya ushirika pamoja naye katika
upweke mlimani. Kabla ya kubeba ujumbe wa Mungu kwa
Farao, alizungumza na malaika kwenye kichaka
kinachowaka moto. Kabla ya kupokea sheria ya Mungu
kama mwakilishi wa watu wake, aliitwa mlimani, na
kuuona utukufu wa Mungu. Kabla ya kutekeleza hukumu
juu ya waabudu sanamu, alifichwa katika ufa wa jabali. na
Bwana akasema, Nitapitisha wema wangu wote mbele
yako” “mwingi wa huruma na fadhili, si mwepesi wa hasira,
mwingi wa rehema na kweli; ... wala si mwenye
kumhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe.” Kutoka
33:19; Kutoka 34:6, 7, A.R.V. Kabla hajaweka chini mzigo
wake kwa ajili ya Israeli, kwa maisha yake, Mungu
alimwita kwenye kilele cha mlima Pisga na kutandaza
mbele zake utukufu wa nchi ya ahadi. Kabla wanafunzi wa
Yesu hawajaanza kazi yao, waliitwa wapande mlimani
pamoja na Yesu. Kabla nguvu na utukufu wa Pentekoste,
ulikuja usiku wa ushirika na Mwokozi, mkutano katika
mlima huko Galilaya, tukio la kuagana juu ya Mizeituni, na
ahadi ya malaika, na siku za sala na ushirika katika
chumba cha juu. Wakati wa kujiandaa kwa ajili ya jaribu
kubwa au kwa kazi muhimu Yesu aliamua kujitenga
milimani na kukaa usiku kucha katika maombi kwa Baba
yake. Usiku wa maombi ulitangulia kuwekwa wakfu kwa
mitume na Mahubiri ya Mlimani, kugeuka sura, na
uchungu wa jumba la hukumu na msalaba, na utukufu wa
ufufuo.

USHIRIKA NA MUNGU KATIKA MAOMBI


Sisi, pia, lazima tuwe na nyakati zilizotengwa kwa ajili ya
kutafakari na maombi na kupokea nguvu mpya ya kiroho.
Hatuthamini nguvu na ufanisi wa maombi jinsi
tunavyopaswa. Maombi na imani zitafanya kile ambacho
mamlaka za dunia haziwezi kufanya. Ni mara chache sana
sisi, katika mambo yote, kuwa katika nafasi sawa mara
mbili. Tunaendelea kupita katika matukio mapya na
majaribu mapya, ambapo uzoefu wa zamani hauwezi
kuwa mwongozo wa kutosha. Ni lazima tuwe na nuru
inayoendelea ambayo inatoka kwa Mungu. Kristo huwa
anatuma ujumbe kwa wale wanaosikiliza sauti yake. Usiku
ule wa uchungu huko Gethsemane, wanafunzi waliolala
hawakusikia sauti ya Yesu. Walikuwa na hisia hafifu ya
uwepo wa malaika, lakini walipoteza nguvu na utukufu wa
tukio hilo. Kutokana na usingizi mzito na kuzubaa
walishindwa kuona ushahidi ambao ungeimarisha roho
zao kwa matukio ya kutisha mbele yao. Kwa hivyo hata leo
watu ambao wanahitaji sana mafundisho ya Mungu mara
nyingi hushindwa kuyapokea, kwa sababu hawajajiweka
katika ushirika na mbingu. Majaribu ambayo tunakumbana
nayo kila siku hufanya maombi kuwa ni lazima. Hatari
huzunguka kila njia. Wale ambao wanatafuta kuokoa
wengine kutoka kwa uovu na uharibifu huwa hasa kwenye
majaribu. Kwa kukutana mara kwa mara pamoja na uovu,
wanahitaji kumshikilia Mungu kwa nguvu wasije wao
wenyewe kuharibiwa.Hatua fupi na ndogo za maamuzi
huwashusha watu kutoka juu na katika utakatifu hadi
kiwango cha chini. Maamuzi ya muda mfupi
yanayofanywa yanaweza na yakadilisha hali ya mtu ya
milele. Kushindwa kuzuia jaribu moja kunaacha nafsi bila
ulinzi. Tabia moja mbaya, ikiwa haitapingwa vikali,
itaimarisha katika minyororo ya chuma, kumfunga mtu
mzima. Sababu kwa nini wengi huachwa peke yao mahali
pa majaribu ni kwamba hawamweki Bwana daima mbele
yao. Tunaporuhusu ushirika wetu pamoja na Mungu
kuvunjwa, ulinzi wetu huondoka. Sio kila malengo yako
yote mazuri na nia njema itakuwezesha kustahimili uovu.
Lazima muwe wanaume na wanawake wa maombi.
Maombi yenu lazima yasiwe hafifu, ya muda Fulani tu,
nyakati fulani za kufaa, bali yawe ya bidii, uvumilivu, na ya
kudumu. Sio lazima kila wakati kuinama na kupiga magoti
ili kuomba. Jenga tabia ya kuzungumza na Mwokozi
unapokuwa peke yako, unapokuwa unatembea, na
unapokuwa na shughuli nyingi za kila siku. Hebu kila moyo
uinuliwe daima katika maombi ya kimyakimya kwa
msaada, kwa mwangaza, kwa nguvu, kwa maarifa. Hebu
kila pumzi iwe ni ombi. Kama watumishi wa Mungu lazima
tuwafikie wanadamu mahali walipo, wamezungukwa na
giza, wamezama katika uovu, na kuchafuliwa na ufisadi.
Tunapoweka akili zetu juu ya Yeye aliye jua letu na ngao
yetu, uovu unaotuzingira hautaleta doa kwenye mavazi
yetu. Tunapofanya kazi ya kuokoa roho zinazoangamia
hatutaaibishwa tukimfanya Mungu kuwa tumaini letu.
Kristo miyoni mwetu, Kristo maishani mwetu, huu ndio
usalama wetu. Mazingira ya uwepo wake yatajaza roho
kuchukia kila kitu kiovu. Nafsi zetu zitahusishwa na Roho
yake ambayo katika mawazo na makusudi tutakuwa kitu
kimoja pamoja naye. Ilikuwa ni kwa njia ya imani na
maombi Yakobo aliweza kutoka kuwa mtu dhaifu na
mdhambi na kuwa mkuu na Mungu. Ni kwa hivyo ili mpate
kuwa wanaume na wanawake walio juu na kusudi takatifu,
la maisha matukufu, wanaume na wanawake ambao kwa
mazingatio yoyote hawataweza kuyumbishwa kutoka
kwenye ukweli, uadilifu, na haki. Wote wanasukumwa na
wajibu waa haraka, mizigo, na majukumu, lakini kadiri
msimamo wako na mzigo wako unavyozidi kuwa mzito
zaidi, ndivyo unavyomhitaji Yesu zaidi. Ni kosa zito
kupuuza ibada ya hadhara ya Mungu. Mapendeleo ya
utumishi wa ki_Mungu hayapaswi kuchukuliwa kwa
urahisi. Wale wanaowahudumia wagonjwa mara nyingi
hawawezi kujinufaisha na mapendeleo hayo, lakini
wanapaswa kuwa waangalifu wasijiepushe na nyumba ya
ibada isivyo lazima. Katika kuwahudumia wagonjwa, zaidi
ya kuhudumia tu biashara ya kidunia, mafanikio
yanategemea roho ya kujiweka wakfu na kujitoa ambako
kazi hufanya iwezekane. Wale wanaobeba majukumu
wanahitaji kujiweka ambapo watavutiwa sana na Roho wa
Mungu. Unapaswa kuwa na wasiwasi mkubwa zaidi kwa
msaada wa Roho Mtakatifu na kwa ajili ya maarifa ya
Mungu kuliko wengine kwa vile nafasi yako ya uaminifu ni
ya kuwajibika zaidi kuliko wengine. Hakuna kitu
kinachohitajika zaidi katika kazi yetu kuliko matokeo ya
kivitendo ya ushirika na Mungu. Kwa maisha yetu ya kila
siku tunapaswa kuonyesha tuna amani na pumziko ndani
ya Mwokozi. Amani yake ndani ya mioyo itaangaza usoni.
Itaipa sauti nguvu ya kushawishi. Ushirika na Mungu
utakuza tabia na maisha. Watu watatutambua sisi kama
wanafunzi wa kwanza, kwamba tumekuwa pamoja na
Yesu. Hii itampa mfanyakazi nguvu ambayo hakuna kitu
kingine kinachoweza kutoa. Lazima asikubali kunyimwa
nguvu hii. Ni lazima tuishi maisha mara dufu—maisha ya
fikira na vitendo, ya maombi ya kimya kimya na kufanya
kazi kwa bidii. Nguvu inayopokelewa kwa njia ya ushirika
na Mungu na kuunganishwa na juhudi za dhati katika
kuifundisha akili kuwa na fikira za kina na kujitunza,
huandaa mtu kwa ajili ya majukumu ya kila siku na
huifanya roho kuwa na amani chini ya hali zote, hata
ikijaribiwa.

MSHAURI WA KI_MUNGU

Wengi wanapokuwa na shida hufikiri kwamba wanapaswa


kuwaomba na kuwakimbilia marafiki wa kidunia,
wakiwambia mashaka yao, na kuomba msaada. Katika
hali ya majaribu kutokuamini hujaza mioyo yao, na njia
huwa kama giza. Na nyakati zote anasimama karibu nao
Mshauri mkuu wa vizazi vyote, akiwaalika kuweka imani
yao Kwake. Yesu, Mbeba mizigo mkuu, anasema, “Njooni
kwangu, nami nitawapumzisha.” Je, tutageuka kutoka
kwake kwenda kwa wanadamu wasio na uhakika, ambao
wanamtegemea Mungu kama sisi?, Unaweza kuhisi
upungufu wa tabia yako na udogo wa uwezo wako
ukilinganisha na ukuu wa kazi. Lakini kama ulikuwa na
akili kubwa zaidi aliyopewa mwanadamu, haitatosha kwa
kazi yako. “Pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo
lote,” asema Bwana wetu na Mwokozi. Yohana 15:5.
Matokeo ya yote tunayofanya yamo mikononi mwa Mungu.
Chochote kinachoweza kutokea, Mshikilie Yeye kwa ujasiri
thabiti na wa kudumu. Katika biashara zako, katika
mikusanyiko ya kupata burudani, na katika muungano wa
maisha, vyama vyote unavyounda unapaswa uingie kwa
maombi ya dhati, na ya unyenyekevu. Utaonyesha
kwamba unamheshimu Mungu, na Mungu atakuheshimu.
Ukiwa umekata tamaa Omba. Unapokufa moyo, funga
midomo yako kwa nguvu kwa watu; wala usifuate kivuli
cha njia ya wengine; lakini mwambie Yesu kila kitu. Inua
mikono yako juu unapohitaji msaada. Katika udhaifu wako
shikilia nguvu isiyo na kikomo. Omba unyenyekevu,
hekima, ujasiri, ongezeko la imani, ili uweze kuona nuru
katika nuru ya Mungu na kufurahia upendo wake.

KUWEKA WAKFU; AMINI

Tunapokuwa wanyenyekevu na wenye toba tunasimama


ambapo Mungu anaweza na atajidhihirisha kwetu.
Anafurahia tunapohimiza rehema na baraka zilizopita
kama sababu kwa nini anapaswa kutupa baraka kubwa
zaidi. Atatimiza zaidi ya matarajio ya wale ambao
wanamtumaini kikamilifu. Bwana Yesu anajua kile tu
ambacho Watoto wake wanahitaji, ni nguvu zipi za Ki-
Mungu zinazotufaa kwa baraka za kibinadamu; na
Anatupatia juu yetu yote tutakayotumia katika kuwabariki
wengine na kuzikuza nafsi zetu. Lazima tuwe na imani
ndogo katika kile sisi wenyewe tunaweza kufanya, na
kuamini zaidi kile ambacho Bwana anaweza kufanya kwa
ajili yetu na kupitia sisi. Hujishughulishi na kazi yako
mwenyewe; bali unafanya kazi ya Mungu. Salimisha
mapenzi yako na njia zako Kwake. Usitegemee hata mara
moja, usijifanyie mwafaka na nafsi yako pekee. Jua ni nini
maana ya kuwa huru katika Kristo. Kusikia tu mahubiri ya
Sabato baada ya Sabato, kuipitia Biblia mara kwa mara, au
ufasili wa aya kwa aya wa Biblia, hautatunufaisha sisi au
wale wanaotusikia, Mpaka pale tutakapoleta kweli za
Biblia katika uzoefu wetu binafsi. Uelewa, na matakwa,
upendo, lazima yatolewe kwa udhibiti wa neno la Mungu.
Ndipo kupitia kazi ya Roho Mtakatifu maagizo ya neno
yatakuwa kanuni za maisha. Unapomwomba Bwana
akusaidie, mheshimu Mwokozi wako kwa kuamini
kwamba unapokea baraka zake. Nguvu zote, hekima zote
ziko chini ya amri yetu. Tunapaswa kuomba tu. Tembea
daima katika nuru ya Mungu. Jipatanishe mchana na
usiku juu ya tabia yake. Ndipo utaona uzuri Wake na
kufurahia wema wake. Moyo wako utakua kwa hisia ya
upendo wake. Utainuliwa kana kwamba umebebwa kwa
mikono ya milele. Kwa nguvu na nuru ambayo Mungu
anatoa, unaweza kuelewa zaidi na kutimiza zaidi kuliko
vile ulivyofikiria hapo awali kuwa inawezekana.

“KAENI NDANI YANGU.”


Kristo anatuagiza hivi: “Kaeni ndani yangu, nami ndani
yenu. Kama vile tawi lisivyoweza kuzaa peke yake,
lisipokaa ndani ya mzabibu; kadhalika nanyi, msipokaa
ndani yangu. Akaaye ndani yangu, nami ndani yake, huyo
huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya
neno lo lote... Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu
yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi
mtatendewa. Hivyo hutukuzwa Baba yangu, kwa vile
mzaavyo sana; nanyi mtakuwa Wanafunzi wangu. “Kama
vile Baba alivyonipenda Mimi, nami nilivyowapenda ninyi;
kaeni katika pendo langu...“Si ninyi mlionichagua Mimi,
bali ni Mimi niliyewachagua ninyi, nami nikawaweka
mwende mkazae matunda, na matunda yenu yapate
kukaa; ili kwamba lo lote mmwombalo Baba kwa jina
langu awapeni. Yohana 15:4-16. “Tazama, nasimama
mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na
kuufungua mlango, nitaingia kwake. nami nitakula pamoja
naye, na yeye pamoja nami.” Ufunuo 3:20. "Yeye ashindaye
nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa, nami nitampa jiwe
jeupe, na juu ya jiwe hilo limeandikwa jina jipya asilolijua
mtu ila yeye analipokea." Ufunuo 2:17. “Na yeye
ashindaye,...Nami nitampa ile nyota ya Asubuhi” “Nami
nitaandika juu yake jina la Mungu Wangu, na jina la mji wa
Mungu Wangu: …….na jina langu mwenyewe, lile jipya.”
Ufunuo 2:26-28; 3:12.
“NATENDA NENO MOJA TU.”

Yeye ambaye tumaini lake liko kwa Mungu atakuwa


pamoja na Paulo na ataweza kusema, “Nayaweza mambo
yote katika yeye anitiaye nguvu.” Wafilipi 4:13 , R.V. Bila
kujali makosa au kushindwa kwa wakati uliopita,
tunaweza, kwa msaada wa Mungu, kuyashinda. Pamoja
na mtume tunaweza kusema: “Natenda neno moja tu,
nikiyasahau yaliyo nyuma, nikiyachuchumulia yaliyo mbele,
nakaza mwendo, niifikilie mede ya thawabu ya mwito
mkuu wa Mungu katika Kristo Yesu.” Wafilipi 3:13, 14.

MWISHO.

You might also like