You are on page 1of 49

KOZI YA MSINGI YA WAVUMBUZI

[MASTERGUIDE MAFUNZONI]

MAGESA MASATU
KIONGOZI WA TAALUMA
KANDA YA MBEYA MAGHARIBI
SOUTHERN HIGHLAND CONCEFERENCE (SHC)

1
KOZI YA MSINGI YA WAVUMBUZI KWA MASTER GUIDE MAFUNZONI

UTANGULIZI
Katika hatua za awali za uanzishwaji wake, Kanisa la Waadventista Wasabato halikuwa na
muundo maalumu wa huduma za vijana.Pamoja na kuwepo kwa vijana waliofanya kazi kubwa
ya injili kama James white, John Loughborough, na Ellen Harmon.Vijana hawa waliamua
wenyewe kwa msukumo wa Roho Mtakatifu ndani yao kuwashirikisha wengineukweli
walioupata kutoka katika Neno la Mungu. Kanisa lilivyoendelea kukua, Mpango wa Mungu wa
kuwachagua vijana kuwa mkono wake wa msaada ulifunuliwa kwa watu wakie na hivyo Idara
ya huduma za Vijana ikaanza.

Kozi ya msingi ya wavumbuzi imegawanyika katika vipengele 10 navyo ni :


1) Historia,Falsafa na Makusudi ya chama cha wavumbuzi.
2) Muundo wa chama cha wavumbuzi.
3) Uongozi wa chama cha wavumbuzi.
4) Kuwaelewa wavumbuzi.
5) Program za chama cha wavumbuzi.
6) Ufundishaji wa mtaala wa wavumbuzi.
7) Tuzo za wavumbuzi na ufundishaji wake.
8) Familia ya wavumbuzi.
9) Huduma za wavumbuzi.
10) Elimu ya kujikinga na ukimwi.

2
SEHEMU YA KWANZA

HISTORIA, FALSAFA, MAKUSUDI NA MADHUMUNI

HISTORIA YA WAVUMBUZI
Wazo la kuwa na Chama cha wavumbuzi lilianza kwa kuanzishwa madarasa manne (4) ndani ya
chama cha JMV na chama kiliitwa Pre-JMV. Madarasa haya yaliitwa Pre-JMV Classes.
Madarasa haya yaliyoanzishwa mwaka 1930 na aliyekuwa Mkurugenzi wa JMV wa GC ndugu
C. Lester Bond yalikuwa ni Busy bee (nyuki wa Shughuli), Sunbeam (Mwali wa Jua), Builder
(Mjenzi), na Helping hand(Mkono wa Msaada).
Madarasa yalikuwa na masomo ya kujifunza Biblia, masomo ya afya, kanuni za maburudisho,
viumbe vya asili na mtoto kujitambua yeye ni nani na mchango wake katika familia yake.
Mwisho wa mwaka vijana hawa walihitimishwa kwa kupewa pini maalumu, skafu na slides.
Lengo lilikuwa ni kukuza nguvu ya uhusiano kati ya watoto na wazazi na kuwezesha kuwepo
kwa maendeleo ya mtoto kiroho, kiakili , kimwili na kijamii.
 Mwaka 1939 - Konfensi kuu ya ulimwengu (GC) iliidhinisha rasmi wazo hili la kuwa na
madarasa ya haya ya Nyuki wa Shughuli, Mwali wa Jua, Mjenzi na Mkono wa
Msaada.Madarasa haya yalifundishwa kama sehemuya mtaala wa shule za kanisa hasa
kipengele cha mambo ya kiroho au ibada.
 Mwaka 1972 - Washington Conference ilifadhili chama cha watoto kilichoitwa
“Beavers”“ chini ya uongozi wa Carolee Riegel .
 Mwaka 1975 - North-eastern Conference ilitolewa taarifa ya kuwa pia na programu za
vyama vya watoto.
 Mwaka 1979 - Jina la Pre-JMV lilibadilishwa na kuitwa Adventurers (Wavumbuzi).
 1980’s - Hadi kufikia miaka hii conference nyingi zilikuwa na vyama vya watoto
vikiendelea kufanya kazi ya malezi na makuzi.
 Mwaka 1988 - Division ya North America, Idara ya watoto ilitoa mwaliko kwa Conference
mbalimbali na wataalamu wa watoto kusoma na kutathmini wazo la kuwa na chama cha
wavumbuzi.
 Mwaka 1989 - Kamati ya wajumbe 20 ilikutana kuhuisha mtaala wa wavumbuzi na
kutengeneza tuzo za wavumbuzi, na kuandaa mwongozo wa kuongoza chama cha
wavumbuzi.
3
Kamati hii iliwahusisha wakuu wa shule ya sabato, walimu, waratibu wa huduma za watoto
katika Conference na union, wataalamu wa mambo ya watoto na familia. Chini ya Mwenyekiti
ndugu Norman Middag, Kamati hii ilkwa na wajumbe wafuatao; Debra Brill, Terry Dodge,
Sarah Fanton, Merril Fleming, Joyce Fortner, Donna Habenicht, Jasmine Hoyt, Noelene
Johnsson, Kathie Klocko, Barbra Manspeaker, Kathy Martin, Dixie Plata, Julia Raglin, Toin
ShobeHarrison, Emily Tillman, Claude Thomas, Ruth Walker, Al Williamson na Bob Wong.
Mtaalamu wa Wavumbuzi uliandikwa na Teresa Reeve.

 Mwaka 1989 - Chama cha Wavumbuzi kinatambulika rasmi na Konferensi kuu baada
ya mtaala, mwongozo na tuzo kukamilika.
 Mwaka 1990 - Programu za wavumbuzi kwa majaribio zinaanza katika Division ya America
Kaskazini (North America (NAD).
 Mwaka 1991 - Mwongozo mpya wa utawala wa wavumbuzi (administrative manual), na
tuzo za wavumbuzi (adventurer award) ukaanza. Mwongozo wa tuzo ulitolewa katika lugha
nne(4).
 Mwaka 1992 - Programu za Wavumbuzi zinapitishwa rasmi na Konferensi Kuu ya
Ulimwengu kutumika katika makanisa yote katika ulimwengu wa Kanisa la Waadventista
Wasabato.
 Mwaka 1993 - Chama cha Wavumbuzi kinatambulika rasmi katika Division ya America
Kaskazini(NAD) baada ya programu zake kuidhinishwa na GC
 Mwaka 2000 - Konferensi Kuu ya Ulimwengu inapiga kura ya kumwezesha Mkurugenzi wa
Wavumbuzi kuwa sehemu ya wajumbe wa Baraza la Kanisa.
 Mwaka 2016 -Madarasa mawili (2) ya little lamb –miaka 4 na Eager Beaversmiaka 5
yanaongezwa katika huduma za wavumbuzi
 Mwaka 2016 - Nembo mpya ya wavumbuzi, na skafu, inaanzishwa kuonyeshwa umuhimu
wa huduma za wavumbuzi kushirikiana na wazazi kwa ukaribu.
 Mwaka 2021 - Mwongozo mpya wa Mkurugenzi wa Wavumbuzi unatolewa na Konferensi
kuu (Adventurer Director’s Manual), jina Early Bird limepitishwa kutumika badala ya Eager
Beavers kwa watoto wa miaka 5.

4
FALSAFA NA MAKUSUDI YA CHAMA CHA WAVUMBUZI
I. FALSAFA
Chama cha wavumbuzi ni huduma inayodhaminiwa na Kanisa la Waadventista Wasabato iliyo
wazi kwa watoto wa miaka 4-9. Ni maahli ambapo kanisa, shule, familia zinaungana pamoja
kuisaidia kukua katika hekima na kimo kwa mtoto akimpendeza Mungu na wanadamu Luka
2:52.
Programu zao zimeundwa kumsaidia mzazi katika jukumu lake muhimu la kuwa Mwalimu wa
kwanza na mwinjilisti kwa mtoto wake. Kupitia programu za wavumbuzi kanisa, familia na
shule zaweza kufanya kazi pamoja kumwezesha mtoto kukua akiwa na furaha.
Huduma za wavumbuzi ni huduma za kifamilia. Falsafa kuu ya wavumbuzi ni kujenga huduma
ya mahusiano ya kifamilia kwa kuhakikisha ya kuwa wazazi wanahusishwa na kuunga mkono
Shughuli za wavumbuzi.

II: MAKUSUDI
Chama cha wavumbuzi kinatayarisha programu mbalimbali ili kumwezesha mtoto kukabiliana
na changamoto za kuwa mfuasi wa Kristo na hivyo chama kitahakikisha kufanya yafuatayo:-
a) Kuendeleza tabia ya kristo ndani ya mtoto
b) Kupata uzoefu wa furaha na kupata utosherevu wa kufanya vitu vizuri
c) Kuonyesha pendo lao kwa Yesu katika hali halisi
d) Kujifunza michezo mizuri na kuimarisha uwezo wao wa kuwa na wengine
e) Kugundua uwezo waliopewa na MUNGU na kujifunza namna ya kuutumia kwa faida yao na
kuwahudumia wengine
f) Kugundua ufahamu wao waone kitu gani kinafanya familia kuwa imara
g) Kugundua Dunia/ulimwengu wa Mungu jinsi ilivyoumbwa na kwa nini
h) Kukuza uungwaji mkono wa wazazi kwa mafunzo ya watoto wao.

III. MADHUMUNI YA CHAMA CHA WAVUMBUZI

Chama cha Wavumbuzi kinatoa furaha na njia za ubunifu kwa watoto.

1. Kujenga tabia ya KRISTO ndani yao.


5
2. Kuizoea furaha na kuridhika kwa kufanya mambo mema
3. Kuonesha upendo wao kwa YESU kwa njia za asili
4. Kujifunza michezo mizuri na kuimarisha uwezo wao na kuwa karibu na wengine
5. Kugundua vipawa walivyopewa na MUNGU, kujua namna ya kuvitumia ili kuwasaidia
wao binafsi na wengine pia.
6. Kugundua dunia/ ulimwengu wa MUNGU
7. Kuimarisha uelewa wao juu ya mambo yanayoifanya familia kuwa imara
8. Kuendeleza msaada kwa wazazi kwa njia ya mafunzo ya watoto.

MAELEZO YA MUHIMU KUHUSU MALEZI


Kushirikisha Wazazi na kuwapa watoto nafasi ya kujifunza na kupata uzoefu. Hivyo basi Chama
cha wavumbuzi kinajitahidi kuweka mazingira ambayo:-
A. Watoto kwa mapenzi yao watatoa mioyo na maisha yao kwa Yesu
B. Watoto kuweza kuwa na mtazamo chanya juu ya faida, furaha na majukumu ya kuishi
maisha ya Kikristo
C. Familia za wavumbuzi zitaweza kupata ufahamu na ujuzi unaotakiwa wa jinsi ya kuishi
kwa ajili ya Kristo leo.
D. Wazazi na Walezi kuwa na ujasiri na ufanisi wa kuwa watenda kazi pamoja na Bwana
katika kuwalea watoto wao
E. Uongozi wa Kanisa utakubali majukumu yake ya kuisaidia kuwajali na kuwatunza
washiriki wake wachanga hawa.
F. Kuongeza na kuimarisha uhusiano kati ya mtoto na mzazi wake, na kumkuza mtoto
Kiroho, Kimwili, Kiakili na Kijamii.
G. Kwamba mtoto aweze kulisaidia kanisa lake anapojitambua yeye ni sehemu ya kanisa
H. Mtoto ajitambue na kujithamini kwamba yeye ni sehemu ya jamii inayomzunguka.

6
SEHEMU YA PILI

MUUNDO WA CHAMA

Muundo wa Chama cha Wavumbuzi kanisa la kiulimwengu.


1. Kanisa mahalia- Linaongozwa na uchaguzi wa maofisa na wakuu wa maidara.
Mkurugenzi wa chama cha Wavumbuzi huchaguliwa kila mwaka au kila baada ya
miaka miwili.

2. Conference/Field – Hufanywa na makanisa mahalia ya eneo Fulani lililopangwa na


inawajibika kwa makanisa yote na kazi ya uinjilisti. Mkurugenzi wa
Conference/Field wa Wavumbuzi huchaguliwa kila baada ya miaka mitano (5)

3. Union – Hufanywa na Conference mbalimbali katika himaya iliyoamrishwa.


Uongozi kila baada ya miaka mitano (5)

4. Division – Huundwa na Union mbalimbali katika eneo maalumu lililotengwa.

5. General Conference – Hufanywa na Division zote zilizopo duniani – Mkurugenzi


huchaguliwa kila baada ya miaka mitano (5)

MUUNDO WA CHAMA CHA WAVUMBUZI:


KANISA DOGO
Kanisa

Wazazi Shule ya Sabato

Mkurugenzi

Mshauri Mshauri

Darasa la I na II Darasa IV na V na
na III 4 hadi 6 VI 7 na 8 na 9

7
KANISA KUBWA

Kanisa

Shule ya sabato

Wazazi Shule

Mkurugenzi

Mkurugenzi Mkurugenzi Mratibu wa


Msaidizi Msaidizi familia

Staff Staff

Darasa la I na II Darasa IV na V na VI
na III 4 hadi 6 7 hadi 9

A: JINSI YA KUANZISHA CHAMA


1. Uwe na njozi - Mpango wa mbele utafanya nini.
2. Soma Biblia, Roho ya unabii, Kanuni ya Kanisa.
3. Soma miongozo ya wavumbuzi.
4. Shauriana na Mchungaji kwa njozi ulizo nazo.
8
5. Ita mkutano wa wazazi zungumza umuhimu wa mtoto kuwa ndani ya chama na hasara ya
kutokuwepo ndani ya chama.
 Taratibu za kujifunza, waone utofauti watakaokuwa nao kwa wengine kwa
kuwa na sare.
 Kutakuwa na ziara mbalimbali, muda wa kukutana na watoto.
6. Andaa mahubiri juu ya malezi ya watoto, onyesha mifano ya watoto wa Biblia.
7. Andaa sherehe za uzinduzi
8. Fanya tathmini

MAHITAJI YA UANACHAMA.

 Awe mtoto wa umri wa miaka 4 hadi 9

 Akubali kushiriki katika shughuli za chama cha wavumbuzi ikiwemo nishani, ziara mbali
mbali na mikutano ya chama.

 Wazazi / walezi wa wavumbuzi wanapaswa kutoa ukubali wa kushiriki shughuli za chama.

 Awe na sare ya chama.

 Atii sharia na taratibu za chama.

 Awe tayari kushiriki miradi ya chama.

FOMU YA USAJILI YA CHAMA CHA WAVUMBUZI.


 Zinapatikana katika ngazi ya konferensi husika

SABABU ZINZO MFANYA MTOTO KUJIUNGA NA CHAMA:


 Kujua shughuli zao.
 Kujishughulisha.
 Kujiandaa kwaajili ya kuvishwa.
 Kufundishwa nidhamu Na heshima Kwa watu wote.
 Kumsaidia mtoto kuwa karibu Na viongozi.
 Kupata ujuzi mbalimbali.
 Kwa sababu wanachama Fulani wanaonekana wa maana katika chama.
9
 Kwa sababu chama kitamsaidia mzazi katika malezi.
 Kwa sababu ya msaada wa kiroho unao tolewa na chama.

MOJA YA MBINU YA KUHAKIKISHA WAZAZI WANATAMANI WATOTO WAO


KUJIUNGA
 Simu: Mfano kutoa taarifa Kwa simu kuhusu watoto wake.
 Barua ya kila mwezi: Kuwasilisha kila alicho kifanya mfano kwenye kambi au katika
madarasa yao.
 Majadiliano: Kwaajili ya maendeleo ya mtoto.

10
SEHEMU YA TATU

UONGOZI:
Viongozi wanao chaguliwa kufanya kazi na vijana tabia zao zinapaswa kuangaliawa.

Kuna viongozi wa aina mbili:


1. Viongozi wanaochaguliwa na Kanisa
i. Mkurugenzi (awe Master Guide)
ii. Mkurugenzi Msaidizi (Master Guide/Mafunzoni)
iii. Katibu/ Katibu Mhazini
iv. Mshauri
v. Mzee wa kanisa/MChungaji
vi. Mzazi anayewakilisha wazazi wengine
2. Viongozi wanaochaguliwa nza wanachama wenyewe
i. Waalimu (viumbe, tuzo, madarasa, michezo n.k)

ii. Washauri

iii. Kiongozi wa kikosi

iv. Waelekezaji

WAJUMBE WA BARAZA LA WA VUMBUZI.


i. Mkurugenzi.
ii. Mkurugenzi msaidizi.
iii. Karani.
iv. Mhazini.
v. Kiongozi wa kikosi.
vi. Mzazi/baba/mama.
vii. Washauli.
viii. Walimu.
ix. Waelimishaji.
x. Mdhamini.
KAZI ZA MAOFISA WA CHAMA CHA WAVUMBUZI.

Kila ofisa wa chama ajiendeleze kwa:

-Kusoma vitabu vinavyo husu watoto na program zao.

11
-Ahudhurie mikutano ya mashauri ya watoto, Semina za watoto zinazoendeshwa na
kanisa,conference, Unioni katika kuwahudumia watoto.

-Kusoma miongozo ya watoto.

-Kukamilisha mafunzo ya kozi ya msingi ili ajue kuwahudumia vyema.

MKURUGENZI WA WAVUMBUZI.

a. Ni mwenyekiti wa chama.

b. Anaandaa program za chama.

c. Awe na mawasiliano na kiongozi wa Conference.

d. Atume taarifa Conference.

e. Abebe majukumu.

f. Awe mshiriki mzuri wa kanisa.

g. Apendezwe na mambo ya watoto.

MAJUKUMU YA MKURUGENZI WA CHAMA.

1.Ni mjumbe wa baraza la kanisa.

2.Kudumisha mahusiano mazuri kati yake na mchungaji au mzee wa kanisa.

3.Ni mwenyekiti wa kamati ya wavumbuzi.

4.Kusimamia shughuli za chama na kupanga program.

5.Kuongoza katika kupanga program zote za mwaka.

6.Kupanga shuguli na mikutano ya chama. Mfano:

-kwata,michezo,ibada,kazi za darasani ,nishani


-Mahali pa kukutania.
-kupanga ratiba ya kila mwezi/wiki.
-Matembezi au ziara na miradi ya mahubiri.
-Kuvisha pini / nishani.
-anahusika katika Mambo yote ya fedha, bajet na ada ya uanachama.
-Nidhamu ya chama. Pamoja na Matangazo.

12
MKURUGENZI MSAIDIZI WA CHAMA.

-Akubali kufanya kazi anazopangiwa na mkurugenzi.

-Atunze kumbukumbu na taarifa zote za chama.

-Ni msaidizi wa majukumu yote ya chama.

-Atashika nafasi ya mkurugenzi kama hayupo.

-Anajibike katika masuala yote ya uongozi.

KAZI ZA MSAIDIZI ANAPASWA KUZIANGALIA.

-Madarasa ya wavumbuzi kuwa yanafundishwa.

-Karani kama hajachaguliwa.

-Mhazini kama hajachaguliwa.

-Maburudisho.

-Nishani na ubunifu. Pamoja na kuzingatia Viumbe asili

-Atarattibu na kusimamia maswala yote yanayohusiana na Nyimbo, Ibada, Usafiri, Mahubiri


pamoja

-Mahusiano na jamii pamoja na Matukio muhimu kila mwezi.

KARANI WA CHAMA.

Ndiye mtunza kumbukumbu zote za chama. Atachukua kazi ya mhazini kama hayupo.

MAJUKUMU YA KARANI.

 Kuchunguza kumbukumbu za vikosi na kuhamisha kuwa kumbukumbu za mwanachama.

 Kutunza alama zote zilizo kusanywa na kikosi kila mwezi.

 Kujaza taarifa ya kila robo inayo kwenda kwa mchungaji.

 Kumtaarifu mkurugenzi kwa mwanachama asiyekuwepo na aliye na upungufu wa sare.

 Aandae mahitaji ya chama / vifaa na kutuma conference.

 Kupokea barua na kusaidiana na mkurugenzi.

13
 Kutunza Maktaba ya chama na usomaji vitabu.

MHAZINI WA CHAMA.

-Anachaguliwa na Maofisa wa chama.

-Afanye kazi kwa kushirikiana na mkurugenzi ,karani.

-Atunze kumbukumbu za mapato na matumizi.

-Aelewe namna ya kutumia fedha.

-Atoe taarifa kaw baraza la kanisa juu ya mapato na matumizi.

WAJIBU WAKE.

 Kukusanya na kuandika kumbukumbu za mapato na matumizi. Mfano: ada, misaada, sadaka,


michango, pesa za kambi au ziara mbalimbali.

 Kuwakilisha fedha ya chama kwa muhazini wa kanisa

 Kutunza vizuri kumbukumbu za matumizi, orodha ya mapato na matumizi akielezea kwa


ufupi namna ilivyotuka.

 Kutunza stakabadhi zote za matumizi au malipo.

 Kugawa fedha zinapo hitajika.

 Kuchukua fedha kwa muhazini wa kanisa zinapo hitajika.

 Kutunza fedha za sare.

MSHAURI WA KIKOSI.

-Ni kiongozi wa kikosi cha wavumbuzi.

-Awe Na mahusiano ya karibu na familia za wavumbuzi.

-Ni mmoja katika maofisa wa chama.

-Anapangiwa kikosi cha watu wanne had nane (4-8).

-Anapaswa kufahamu kila mwana kikosi wake.

-Anapaswa afahamu wazazi na walezi wa wanakikosi chake.

-Anapaswa kuwepo katika mikutano ya chama ya kawaida.


14
-Anachaguliwa kutoka kwa washiriki walio batizwa.

MAJUKUIMU YAKE.

 Kuwajibika kuongoza/kufundisha/kufanya kazi karibu na wazazi.

 Kuwatia moyo, na kutoa majaribio kwa kila darasa.

 Kuweka mfano mwema katika mahudhurio mavazi,mahudhurio na usafi.

 Kupiga kwata na vikosi.

 Kukuza uelewa kwa wana kikosi.

 Kumsaidia mwanachama alien a tatizo ili viongozi wengine wafahamu.

 Kuwatia moyo wana chama kushiriki shughuli za chama.

 Kushiriki kupanga mipango ya chama.

 Kuhudhuria vikao vya viongozi.

 Kupanga na kuongoza shughuli za uinjilisti.

MWELIMISHAJI/ WALIMU.

-Majukumu ni kufundisha mambo yote muhimu katika madarasa na onesha misingi yote ya
kanisa.

-Afundishe ujuzi maalumu wa somo kama Biblia,ukuaji binafsi ujuzi, wa ukambikaji,nishani na


ufundi mbalimbali.

-Anapaswa ajifunze mtaala wa wavumbuzi na mahitaji yake yote.

-Anapaswa afanye kazi karibu zaidi na waratibu wa madarasa kila anacho taka kufundisha na
ahakikishe anatimiza matakwa ya madarasa.

SIFA ZA KIONGOZI ANAYEFAA KUWALEA WATOTO.

Kutoka 18:1 -
i. Ampende Mungu kwa kiwango cha juu. (Awe mtu wa Kiroho)
ii. Awapende watoto kwa vitendo.
iii. Awatumikie kwa moyo na Kipawa Kinachotamaniwa na Mbingu.

15
iv. Awe mwenye kutawala hisia, kujiheshimu na kuwa na kiasi.
v. Apende mambo ya nje, kwa kuwa ndizo shughuli za watoto zilizo nyingi.
vi. Ajue tabia za watoto.
vii. Mwenye kujielimisha katika fani mbalimbali, ajifunze kutoka kwa wengine.
(Mwenye kupenda kusoma vitabu na kutafiti mambo)
viii. Mwenye uwezo wa Kuongoza (Kiongozi Bora).
ix. Awe na malengo makubwa aanze na yaliyo rahisi.
x. Agawe Madaraka, anaewandaa wengine kuwa kazini / viongozi
xi. Mwenye uhusiano mzuri na wengine.
xii. Anaekubali mambo mapya.

AHADI: Kwa kuwa YESU ananipenda, nitafanya vema kila wakati.

SHERIA
1. Kuwa mtii
2. Kuwa msafi
3. Kuwa kweli
4. Kuwa mkarimu
5. Kuwa na heshima
6. Kuwa msikivu
7. Kuwa tayari kutoa msaada
8. Kuwa Mchangamfu
9. Kuwafikiria wengine
10. kuwa na kicho

Maana ya Ahadi: Watoto waelekezwe kuutambua upendo wa Yesu kwao ili nao wampende.
Kutambua vile Yesu anavyokupenda husaidia kujitoa kumtumikia.
Maana ya sheria Sheria:
1. Kuwa mtii
- Utii kwa wazazi na utii kwa Mungu
2. Kuwa msafi
- Usafi wa kimwili na usafi kiroho (mf. Kufua nguo, kuoga, kupiga mswaki, kusafisha
mazingira nk. Na kiroho:- kusoma neno la Mungu na maombi na kufanya yale yaliyo mapenzi
ya Mungu.

16
3. Kuwa mkweli
- Ndiyo yako iwe ndiyo na hapana iwe hapana. Kuepuka udanganyifu wa namna zote
4. Kuwa mwema
- Wema unajulikana kutokana na zile huduma za mtu kwa wengine zaidi ya kusema tu. Mf.
Wema wako kwa mwenye kiu ni kumpa maji na sio umwambia maji ni mazuri kwa kukata kiu.
5. Kuwa na heshima
- Amri ya tano kati ya zile kumi inazungumzia jambo hili, Baba na Mama huwakilisha watu
wote. Kuheshimu baba na mama kutaongoza katika kumheshimu Mungu.
6. kuwa msikivu
- Kutulia na kusikiliza mashauri na mafundisho ya wazazi, walimu na viongozi wengine.
7. Kutoa msaada
- Kusaidia wahitaji ni kujiwekea akiba kwa Mungu mbinguni
8. Kuwa na furaha
- Ni kinyume cha huzuni. Huboresha afya na kuongeza siku za kuishi
9. Kuwafikiria wengine
- Kuepuka ubinafsi
10. Kuwa na kicho
- Kutetemeka, kuwa na hofu vinavyosababishwa na kuutambua ukuu wa Mungu sio
kutetemeka na hofu kama za aliyekutana na Nyoka au simba.

17
SEHEMU YA NNE
KUWAELEWA WAVUMBUZI.

Tabia za wavumbuzi zimewekwa katika hali ya Kimwili, Kiroho, Kiakili, Kijamii na Kihisia,
Tutaangalia tabia za jumla.

A: Tabia za jumla za Watoto.

i. Umri wenye shughuli nyingi


ii. Wanapenda mambo ya kukariri na chemsha bongo, kuimba na hadithi nzuri
zinazowasisimua au kuwatia moyo.
iii. Wanapenda Michezo na burudani
iv. Ni watiifu na waaminifu, husema kweli daima, na hawajui kusema uongo.
v. Hupenda kutumwa sana, hufanya kazi kwa kushindana, na kazi zao hupenda
zihakikishwe na mtu mzima.
vi. Hupenda kutembea wenye jinsia moja.Hupenda marafiki
vii. Ni umri wenye kupenda sifa.
viii. Wanatunza kumbukumbu sana, lakini pia huweza kusahau
ix. Ni wadadisi sana wa mambo mbalimbali, ni wafikiriaji wazuri na huuliza maswali.
x. Huamini kila kauli ya Mwalimu
xi. Imani yao iko kwa Mzazi kuliko kwa Mwalimu
xii. Wana ubinafsi, Wana ubaguzi.
xiii. Wanakata tamaa mapema.
xiv. Wanaiga kila kitu. (hawana uwezo wa kupambanua jema na baya)
xv. Wanahisi hatari kwa kuona uhalisia wa mtu au kitu. Mfano mwalimu akikasirika au
kufurahi.
xvi. Ni waoga wa vitu au mambo ambayo hawajayazoea.
xvii. Wanahitaji kupendwa sana na kuthaminiwa

TABIA ZA KIMWILI.(PHYSICAL)
1. Wanapenda kujifunza badala ya kukaa muda murefu ,wana nguvu zisizo mipaka.
2. Wanajifunza kwa kushiriki michezo na shughuli mbalimbali za kutumia nguvu.
3. Wanakua kwa utaratibu mzuri uwiano mzuri.

18
TABIA ZA KIAKILI(MENTAL)
1) Wanapenda kujifunza kwa kutenda na niwadadisi wa vitu vingi.
2) Wanashauku ya kutaka kujua yale yanayo wazunguka.
3) Wanaelewa zaidi vitu wanavyo viona kwa macho.
4) Ni wepesi wa kukariri na ni wepesi wa kufikiri kile wanacho fundishwa.
5) Wanapenda kujifunza mambo tofauti tofauti/mchanganyiko.
6) Wanafurahia hadithi na nyimbo,michezo na maswali vinakuza akili zao.
7) Wanaelewa kile wanachogusa, nusa, ona zaidi.

TABIA ZA KIROHO (SPRICTURAL).


1. Uwezo wao wa kutofautisha mema na mabaya sio mkubwa hivyo wanahitaji msaada
mkubwa.
2. Uwezo wao wa kufanya maamuzi ni mdogo hivyo wanapaswa kuongozwa katika kufanya
maamuzi bora.
3. Wana tabia ya utii pale wanapoelekezwa.
4. Wanamkubali Yesu kama mwokozi wao pale wanapoelekezwa kufanya hivyo.
5. Wana tabia ya umimi.

TABIA ZA KIJAMII (SOCIAL).


1) Wanajifunza namna ya kujihusisha na mengine.
2) Wanapenda kugundua na kufanya mambo yao wenyewe.
3) Wanapenda kutenda na kuongea na wenzao.
4) Wanapenda kujitegemea.
5) Wanaipenda jamii inayowazunguka.

MCHANGANUO WAKE KWA UMRI.


Miaka 0-1.
 Hufurahia hadithi fupi za biblia
 Anatambua picha za Yesu.
 Huwa na utii.
 Huwa wakali.
 Huinamisha kichwa kwa ombi.

Miaka 2&3.
 Wanapenda kusikia hadithi fupifupi.
 Hujifunza mambo kwa kusema wenyewe.
19
 Ni umri mzuri wa kukuza tabia.
Miaka 4&5.
 Humpenda Mungu sana.
 Huwahi sana kwenye vipindi vya S.S kwa wakati.
 Hufurahia taratibu za kujifunza biblia.
 Hutambua lililo jema na baya.
 Huwa na imani kuhusu Mungu.

Miaka 6&7.
 Hutaka kumpenda Mungu.
 Huwa na utambuzi wa kuelewa jambo.
 Husikita pale anapofanya baya.
 Hupenda kufanya vyema shuleni na nyumbani.
 Ana bidii katika kuabudu.

Miaka 8&9.
 Hutamani kumwabudu Mungu.
 Huelewa hitaji la wokovu katika maisha yao.
 Hupenda kusoma biblia, kuomba na kuombea wengine.
 Hujisikia furaha, mwamifu anapowajibika kanisani.
 Hujifunza kufanya maamuzi.

Mwalimu unapaswa kufanya nini:

i. Wafundishe kuzitumia nguvu walizonazo kwa kufanya majukumu unayowapatia. Mfano,


kuimba kwa vitendo, kukariri mafungu, kufanya kazi za kanisa n.k
ii. Wafundishe hadithi za Biblia kwa bidii na uwashawishi wazitumie maishani.
iii. Kuwa rafiki yao.
iv. Wape nafasi ya kuonesha wanayojifunza mbele za wazazi wao
v. Watie moyo katika kazi zao wanazofanya na uwaelekeze kwa umakini na upendo.
vi. Kuza talanta na vipaji vyao

SIFA ZA MWALIMU ANAYEFAURU:


1. Anayewajari watoto.
2. Asiyebagua watoto.
3. Anayefundisha mtoto na siyo darasa.
20
4. Anayejichanganya na watoto.
5. Anaye wapenda watoto wote.
6. Anaye wafurahia watoto.
7. Anaye andaa vitendea kazi mapema vya somo/hadithi.
8. Anaye wafahamu watoto na mazingira watokamo.
9. Anaye wapongeza watoto.
10. Pia anaye watia moyo watoto.
MALEZI YA WAVUMBUZI

Malezi ya wavumbuzi yana misingi yake katika biblia Torati 6:4-9, Waebrania 4:7 hivyo
fundisha kufuata maelekezo ya biblia na miongozo ya wavumbuzi, hata mwendo wako uwe
kielelezo kwa hawa watoto maana wanajifunza kutoka kwako na kuigiza kile unacho kifanya,
unachotamka ili kisiwe tabia kwake.

B: JINSI YA KUSHUGHULIKIA WATOTO WENYE MATATIZO MAALUM

Kuna makundi maalum manne ya watoto:


I. WATOTO WENYE MATATIZO YA AKILI ILYOVIA/ ILIYODUMAA:
Sababu:-

 Lishe duni.
 Malezi ya Wazazi.
 Upweke.
 Kutothaminiwa

Jinsi ya kuwasaidia:-

 Fanya urafiki nao.


 Waketishe karibu nawe unapofundisha
 Usiende polepole wala haraka mno unapofundisha.
 Wapangie muda wa ziada wa mafundisho kwa ajili yao.

II. WATOTO WATUKUTU.


Sababu:
i. Mifarakano katika familia

21
ii. Kuachana au kusambaratika kwa familia.
iii. Malezi mabovu
Jinsi kuwasaidia:-

 Fanya urafiki nao


 Waketishe karibu nawe.
 Waombee watoto ukiwa nao.
 Shirikiana na wazazi/walezi katika kuwasaidia

III. WALIOPATA HASARA KUBWA

SABABU:

Sababu
 Kufiwa na Wazazi (ni yatima)
Jinsi ya kuwasaidia:-
 Uwe nao karibu.
 Elewa mahitaji yao.
 Wapatie nafasi ya utumishi. (mfano; kuomba, kutumwa kazi, kuongoza ibada n.k)

IV. WATOTO WALIO WEPESI KUELEWA/ WENYE VIPAJI

Sababu:

 Ndivyo walivyozaliwa ama kulelewa


Jinsi ya Kuwasaidia.

 Kuza vipaji vyao:


 Watawanye darasani.
 Watumie kuwasaidia wenzao.
 Mshirikishe katika mipango.
C: NIDHAMU KWA MTOTO

Ni hali ya kumfanya awe na furaha na mwanadamu kamili hapo baadaye, ni Maadili


yanayomsaidia mtoto kujitawala na kujitambua. Nidhamu inatakiwa iwe ile ya kumfanya
mvumbuzi awe na furaha maana asie na nidhamu hafai katika chama cha wavumbuzi.
22
Ili awe na Nidhamu:-

• Uwe mfano wa tabia.

• Jenga Mazingira yenye kuleta utulivu ili uvute usikivu wa Mtoto.

• Wabadilishie Mahali pa kujifunzia, na Waalimu wa Kufundisha.

• Maandalizi ya Mwalimu [Vifaa, soma mtaala uuelewe vizuri na uwe mbunifu].

• Weka malengo, washirikishe, utekelezaji wake liambie Kanisa.

• Kusahihisha makosa wakati wote na ukemee kwa mamlaka.


Namna ya kuadhibu:

1. Ongea na mtoto kama mzazi wake


2. Mweleze kosa lake
3. Usimseme mbele ya wenzake
4. Inapobidi mwadhibu mbele ya wenzake kuleta fundisho
5. Lengo la kuadhibu ni kuongoa Roho na si kuingamiza
6. Mtie moyo kwamba YESU anampenda, kwa kuwa anawapenda wadhambi
7. Omba naye

NB:
Adhabu unayoitoa kwa wavumbuzi iwe inamuonyesha upendo wa Yesu na iwe ni ya upendo
siyo ya kigaidi.
Mafungu ya Biblia: Mithali 22:6, Waamuzi 13:3-5, Mithali 1:10, Kumbukumbu la Torati 6:4-9,
Mithali 16:25, Mithali 23:13-14, Mithali 22:15, Mithali 13:24, Mithali 19:18

MAMBO 10 YA MSINGI YA MSINGIYA MAHITAJI YA WAVUMBUZI:


No. HITAJI. NJIA YA KUHIFADHI HITAJI. BIBLIA INASEMA NINI.
1. FARAJA. -Tiamoyo katika mazingira aliyomo Warumi 12:15
hatakama ni mazito. Lia na wanao lia.
-Onyesha kuguswa kama ni
furaha ,furahi kama ni sikitiko sikitika
pia.

23
2. USIKIVU {KUJALI} -Wasikilize vijana wako. 1Wakorintho 12:25
-Tengeneza ratiba ya kuwa nao. Mtunzane.
-Weka nyuma masumbufu na matatizo
yako.
3. PONGEZA. -Wapongeze hata kwa kidogo walicho
fanya.
-Pongeza kwa kundi au mtu mmoja.
-Wape zawadi.
4. UNGA MKONO. Tembea nao kwa kila safari. Wagalatia 6:2
-Omba nao. Tusaidiane kubeba mizigo.
-Unga mkono kwa mema wanayo tenda.
5. TIA MOYO. -Ongea nao maneno ya kutia moyo. 1Wathesolanike5:11
Tianeni moyo mmoja na mwenzake.
6. UPENDO. -Onyesha kuwapenda kwa maneno na Warumi 16:16
matendo.
-Wape msaada pale panapo wezekana.
7. HESHIMU. -Onesha hekima kwa namna unavyo 1Petro 2:17
mjali kila mmoja. Uwaheshimu watu wote.
-Ondoa mawazo na lugha mbaya mfano
matusi, kijiweni n.k.
-Uwe tayari kukubali pale ulipo kosea.
8. USALAMA. -Onesha wanapokuwa na kiongozi wao 1Yohana4:18
wanakuwa na amani. Upendo hufukuza hofu.
-Ondoa hofu.
9. KUTHIBITISHWA -Thibitisha mambo mema wanayo fanya Warumi 14:18.
juu ya tabia yao njema.
10. SHUKURU. -Onesha ulivyo guswa na kile walicho
kifanya.

24
SEHEMU YA TANO
PROGRAM ZA CHAMA
Nukuu:E.G.White (Test Ministers Pg498) “kuna hitaji zaidi kuwajibika kwa mtu binafsi, zaidi ya
kufikiri, kupanga, zaidi ya uwezo wa kufikiri uletwe katika kazi ya Bwana kwa sababu kazi ya
Bwana ni kamilifu kila dakika.”
(Massege to young People) “Tunapo tamani kuwa wakamilifu kama Baba yetualivyo mkamilifu
tunapaswa kuwa waaminifu kwa kufanya mambo madogo vile ambavyo no bora kufanya vyote
katika ubora.”
YALIYOMO KATIKA MRADI WA PROGRAMU.
-Bajeti.
-Ratba.
-Taarifa ya kila mwezi .
-Baraza la kanisa.
-Sare.
-Kumbu kumbu.
-Ufanisi.
-Vyanzo vya fedha.
Ada ya uanachama.
Michango.
Bajeti ya kanisa.
-Kuongoza maisha ya vijana katika maisha ya umilele ni kazi ya muhimu waliyo pewa
wanadamu na inapaswa ipangwe vyema.
-Kiongozi panga programu zenye uwiano juu ya kukuza maisha ya mvumbuzi kiroho, kiakili na
kimwili.
-Mipango ioneshwe kufuatwa kwa uangalifu.
-Programu yenye makusudio ipangwe kwa mwaka mzima, robo, mwezi na wiki.

UNAPOPANGA PROGRAMU TAFAKARI YAFUATAYO:


-Mategemeo ya kiongozi kwa mwaka ujao.
25
-Watoto Na wazazi wanayegemea nini mwaka ujao.
-Mipango iwe maalumu kwa mwaka mzima. Mfano:siku ya wavumbuzi, Siku ya shukurani,
Likizo, Siku ya kuvishwa pini, Makambi, Siku ya maburudisho.
-Vitu mbalimbali vya kushangaza mfano viumbe vya asili.
-Maendeleo ya wastani katika mtaala wa wavumbuzi.
-Tafuta mawazo kwa wakurugenzi wa konferensi.
-Anza na maliza kwa wakati.
-Uwe mbunifu programu zikidhi mahitaji ya chama.
-Onesha uchangamfu katika programu za wavumbuzi.
-Panga semina kwa wazazi.
MAMBO YA KUZINGATIA.

1. Programu zisilete usumbufu kwa wazazi.

2. Usilete mifadhaiko isiyo ya lazima kwa watoto.

3. Programu zote zipendeze kwa wazazi.

4. Wape programu kulingana na kiwango cha umri wao.


SHUGHULI ZA CHAMA.
1. Mikutano ya chama.
2. Safari za nje ya chama.
3. Shughuli za viumbe vya asili.
4. Sanaa.
5. Michezo.
6. Matukio ya Confenrence/Field.
7. Mikutano ya wazazi.
8. Shughuli mbalimbali zilizo pangwa.

MFANO WA MIPANGO YA ZIARA ZA NJE.


1. Kwanza robo ya kwanza.
 Kituo cha wa toto ya tima.
 Kituo cha zima moto.
 Jumba la kuokea mikate.
26
 Ofisi za miji.
2. Robo ya pili.
 Tembelea Maktaba.
 Hospitali.
 Kituo cha umeme.
 Kituo cha mabasi.
3. Robo ya tatu.
 Kituo cha TV.
 Kiwandani.
4. Robo ya nne.
 Polisi.
 Maeneo ya kihistoria.

RATIBA.
Mfano ratiba lazima izingatie
i. Kugundua.
ii. Neno.
iii. Mahudhurio.

SHUGHULI ZA WATOTO NA WAZAZI.


Kusudi kuu la Programu hii ni kuimarisha mahusiano kati ya wazazi na watoto kwa kushilikisha
uzoefu wa maisha kwa kila mvumbuzi.

SHEREHE ZA UZINDUZI WA CHAMA


{INDUCTION DAY}
Uzinduzi wa chama pamoja na Baraka za Familia ni huduma ambazo husimama peke yake
ambayo inaweza kuwa hufanyika jioni kwa kuingizwa katika muundo wa kifupi kama sehemu
ya ibada ya kanisa la Sabato.

27
Mpango huo unakusudiwa:
• Kueleza nini Adventurers inahusu
• Kueleza majukumu ya kila darasa
• Kueleza Ahadi na Sheria
• Kuthibitisha nafasi ya mtoto katika familia yao
• Kuombea kila mtoto katika klabu ya Wavumbuzi
• Changamoto Wageni na familia zao kuwa “dhabihu iliyo hai” kwa ajili ya Yesu Kristo
NB
Vilabu vingine hufanya haya kama hafla mbili tofauti. Wale wanaowafanya kando mara nyingi
hutumia Baraka ya Familia kama tukio la utangulizi na Usajili inapatikana baada ya huduma.
VITU VYA KUANDAA
1. Meza
2. Bendera ya vyama
3. Bendera ya taifa
4. Bango la ahadi na sheria
5. Nembo ya wavumbuzi
6. Mishumaa
 Mshumaa mmoja mweupe
 Mishumaa ya madarasa ya wavumbuzi kwa rangi zake
 Mshumaa mmoja kwa ajili ya ahadi
 Mishumaa kumi kwaajili sheria meupe

MANENO YA UTANGULIZI
Chama cha wavumbuzi Ni maahli ambapo kanisa, shule, familia zinaungana pamoja kuisaidia
kukua katika hekima na kimo kwa mtoto akimpendeza Mungu na wanadamu na pia Huduma za
wavumbuzi ni huduma za kifamilia. Falsafa kuu ya wavumbuzi ni kujenga huduma ya
mahusiano ya kifamilia kwa kuhakikisha ya kuwa wazazi wanahusishwa na kuunga mkono
Shughuli za wavumbuzi.

28
Namna ya kufanya induction ceremony

 Mkurugenzi atawasha mshumaa kuashiria Roho Mvumbuzi na kusema maneno yafuatayo

“Mshumaa huu unawashwa ili kuweka roho ya uvumbuzi ndani yake na pia uwakilisha roho
mtakatifu kwa kila mvumbuzi kwenye darasa lake. Pia kuhakikisha Roho mtakatifu akae ndani
yetu na kutusaidia kutumiza malengo ambayo yatatufikisha katika uzima wa milele.” Lakini
nuru hii peke yake haijakamilika wala haitoshi.

Kwa kutambulisha nuru za ziada nimwite sasa Mkurugenzi Msaidizi (anamtaja kwa jina lake).
ambapo ataelezea/wataeleza madarasa ya wavumbuzi.

Madarasa ya wavumbuzi

 katika kuanza kwa madarasa ya wavumbuzi na huku mkurugenzi akiwasha kila mshumaa
unaowakilisha darasa husika, mkurugenzi au mkurugenzi Msaidizi anafafanua Madarasa
sita kama ifuatavyo:

(Wavumbuzi sita wanaweza kuwasilisha yafuatayo pia.)

1. Kondoo mdogo

 Mimi ni kondoo mdogo ninajifunza kuwa Yesu ni rafiki yangu na ananitaka kuwa mtoto
bora kwa kila mtu [maneno ya mwanachama]

 Ni darasa ambalo hujifunza kuhusu habari za yesu na hujifunza zaidi namna ya kuwa
mtoto bora (miaka 4 na rangi ya darasa hili ni light blue)

2. Ndege wa awali

 Mimi ni ndege wa awali ninakuwa kwa haraka ninafuata maelezo ambayo Yesu
ananifundisha namna ya kufuata [maneno ya mwanachama]

 Ni Darasa ambalo wanachama wake wanakuwa kwa haraka na ni darasa ambalo


linajifunza namna ya kumfuata Yesu katika maisha yao na kujua jinsi ya kupenda
unaotokana na kristo pamoja na familia. (miaka 5 na rangi ya darasa hili ni kijani)

3. Nyuki wa shughuli

 Mimi ni nyuki wa shughuli ninashughuli nyingi na ninapenda kufanya bora kwa vile
Yesu anapenda mimi niwe hivyo [maneno ya mwanachama]

29
 Ni darasa lenye shughuli nyingi na linajifunza namna bora ambayo Yesu anaweza
kumtumia katika shughuli hizo kwa kufanya yanayompendeza Mungu. (miaka 6 na
rangi ya darasa hili ni njano)

4. Mwali wa jua

 Mimi ni mwali wa jua ninapenda kuuliza maswali mengi kuhusu Yesu na kujifunza
kuhusu Yesu na niangaze kwa watu kila siku [maneno ya mwanachama]

 Ni darasa ambalo lina maswali mengi na pia hujifunza kuhusu Yesu na namna
anavyoweza kuangaza katika maisha yao. (miaka 7 na rangi ya darasa hili ni orange)

5. Mjezi

 Mimi ni mjenzi ninapenda kukariri mafungu ya biblia na pia ninapenda kujifunza


namna ya kuomba, Mungu amenifanya kuwa mjenzi wa hekalu la ufalme wake
[maneno ya mwanachama]

 Ni darasa ambalo hujifunza kuhusu visa na ni umri ambao unajifunza namna bora ya
kuufanya mwili wake kuwa hekalu la kristo na pia hujifunza namna ya kulitunza
kanisa la Mungu (miaka 8 na rangi ya darasa hili ni blue)

6. Mkono wa msaada

 Mimi ni mkono wa msaada kwa kutumia mkono wangu huu Yesu unifundishe
kuwasaidia wengine. [maneno ya mwanachama]

 Ni darasa ambalo hujifunza namna ya njema ya kuwasaidia wengine kwa ajili ya


ufalme wa Mungu na wengi wapate kuokolewa. Pia hujifunza jinsi ya kuwa msaada
kwa wengine. (miaka 9 na rangi ya darasa hili ni damu ya mzee au maroon)

NB

MKURUGENZI

Mkurugenzi atasema yafuatayo:-

 Mishumaa hii inawakilisha ubora wote na mafanikio ya mafunzo yaliyomo ndani ya


program za Wavumbuzi. Ni ishara au alama ya ukamilifu wote wa juu ambapo utafutanjia

30
unatakiwa kufikia na ukuaji na mafanikio ambayo kila mtafuta njia atapatia uzoefu kama
mwanachama wa chama cha Wavumbuzi.

 Sasa na tuendelee na sherehe ya uwashaji wa Mishumaa ya ahadi ya Wavumbuzi.


(mvumbuzi mmoja anatembea kwenda mbele ya mkurugenzi wanapiga saluti na kupokea
Mshumaa mkubwa na anawasha mshumaa alionao wa ahadi na anapourudisha kuusimika
mahali pake mezani atasema maneno haya kulingana na ahadi.)

Ahadi ya wavumbuzi

“Mimi Ninamwakilisha ahadi ya wavumbuzi inayosema Kwa kuwa yesu ananipenda


nitafanya vyema kila wakati na atatoa maaana ya ahadi hiyo”

Maana ya Ahadi:

Natambua upendo wa Yesu kwangu kwa jinsi alivyojitoa kwa ajili yangu na pia nitamwonesha
jinsi nami ninvyompenda.

NB

Mkurugenzi Msaidizi

Mkurugenzi msaidizi atasema maneno yafuatayo:-

 Kwa niaba ya Chama cha Wavumbuzi Ulimwenguni ninakubali Ahadi za Wavumbuzi na


mwakilishi wao kwamba watayaishi na kushika ahadi za Wavumbuzi.

MKURUGENZI

Sasa tutaendelea na uwashaji wa Mishumaa ya Sheria ya Chama cha Wavumbuzi inayoashiria


sheria ya wavumbuzi (wavumbuzi wanane wanatembea kwenda mbele ya mkurugenzi wanapiga
saluti na kupokea Mshumaa mkubwa na kila mtu anawasha mshumaa alionao wa sheria na
anapourudisha kuusimika mahali pake mezani atasema maneno haya kulingana na sheria
aliyopewa na watasema kwa mfuatano mmoja baada ya mwingine kutoka.)

Sheria za wavumbuzi

Mvumbuzi atasema maneno yafuatayo:-

“Mimi Ninamwakilisha sheria ya ___________ na pia atatoa ufafanuzi wa maana ya moja kati
ya sheria zifuatazo kulingana na mshumaa aliouwasha.”

31
Maana ya sheria Sheria:

1) Kuwa mtii

 Utii kwa wazazi na utii kwa Mungu

2) Kuwa msafi

 nitakuwa msafi wa kimwili na msafi kiroho kwa kutunza mwili wangu

3) Kuwa mkweli

 Ndiyo yako iwe ndiyo na hapana iwe hapana. Kuepuka udanganyifu wa namna zote

4) Kuwa mwema

 Wema unajulikana kutokana na zile huduma za mtu kwa wengine zaidi ya kusema tu.

5) Kuwa na heshima

 Amri ya tano kati ya zile kumi ya Kuwa heshimu baba na mama na watu wote, pia
hutaongoza katika kumheshimu Mungu.

6) kuwa msikivu

 Kutulia na kusikiliza mashauri na mafundisho ya wazazi, walimu na


viongozi wengine.

7) Kuwa tayari Kutoa msaada

 Kusaidia wahitaji ni kujiwekea akiba kwa Mungu mbinguni

8) Kuwa na furaha

 kila siku nitakuwa mwenye furaha na pia husaidia kuboresha afya na kuongeza siku za
kuishi

9) Kuwafikiria wengine

 Kuepuka ubinafsi

10) Kuwa na kicho mbele za Mungu

32
 Kutetemeka, kuwa na hofu vinavyosababishwa na kuutambua ukuu wa Mungu sio
kutetemeka na hofu kama za aliyekutana na Nyoka au simba.

NB

MKURUGENZI MSAIDIZI

Mkurugenzi msaidizi atasema maneno yafuatayo baada ya mishumaa kuwashwa:-

“Kwa niaba ya Chama cha Watafutanjia Ulimwenguni ninakubali KIAPO cha Wavumbuzi na
wawakilishi wao kwamba watayaishi kiapo na kwa kanuni za sheria za Wavumbuzi”.

 Kisha mkurugenzi atawataka wanachama wa klabu kusimama, kisha wanachama wote


wanatamka kiapo cha kufuata ahadi na sheria za wavumbuzi.

Utaratibu wa uwashaji mshumaa kwa wavumbuzi

1. Wanachama wapya (simama)

2. Wavumbuzi wanachama wanaoendelea (simama)

3. Hebu sasa wote tuinue mikono ya kulia juu iliyobeba mishumaa ya ahadi ya kujiweka wakfu
kwa kiapo tunapokariri tena ahadi na sheria za watafutanjia.

Kwa kila mwanachama mkurugenzi atafanya yafuatayo

Kufuatia utaratibu wa kurudiwa kwa Ahadi na Sheria za Wavumbuzi, mkurugenzi anasema,

"Tunatangaza __________________________ (Jina la mwanachama) kukubalika katika


ushirika wa ________________ klabu ya wavumbuzi ya _________ Conference/Misheni ya
Waadventista Wasabato. [Sasa unaletewa mshumaa, (naibu mkurugenzi akimkabidhi
mwanachama mshumaa mweupe au wa rangi ya darasa) ambao sasa unaweza kuwashwa
kutoka kwenye mshumaa wa ‘Roho ya uvumbuzi’, na kuuweka kwenye kinara kwenye
sehemu ya mbele ya meza.]

MKURUGENZI (......atasema)

“Nuru yenu sasa imeangazwa katika nuru ambayo tayari inaangaza katika chama, katika kanisa
lenu na nje ya mipaka ya eneo lenu na ninawaapisha kwa dhati mbele ya wengine kupitia kusudi
ya chama cha wavumbuzi kwamba wote waweze kuona kazi yenu nzuri na kumtukuza Mungu

33
baba yetu wa juu Mbinguni na tunakuamuru mbele ya Wavumbuzi hawa nuru yako iangaze
mbele ya wengine katika Roho ya Mvumbuzi”.

NB

Kama kuna mwanachama mpya baada ya kiapo na kuwasha mshumaa mkurugenzi atasema
maneno yafuatayo, "_________________" (jina la mwanachama mpya), sasa wewe ni
mwanachama kamili wa Klabu ya wavumbuzi"

Ombi kwa ajili ya kuweka wakfu kwamba Mungu akupe nguvu za kuishi kulingana na
maadili ya juu ya klabu yetu na kuwa mwanachama mwaminifu na mwaminifu wa klabu.

Baada ya ombi la kuwekwa wakfu wavumbuzi wazazi wa wavumbuzi wataitwa mbele


wakiwa pamoja na watoto wao na kuwekwa wakfu katika jukumu zima la kusaidia
huduma za wavumbuzi kanisani

 Pia ombi maalumu kwa kanisa la kuhakikisha huduma za wavumbuzi vinakuwa hai kanisa
mahalia na pia kusaidia katika malezi ya watoto hao.

MWISHO

Mwanachama mpya

1. Mwanachama mpya atajisajili kwa mkurugenzi na kupokea mkono wa ushirika na kuvishwa


skafu ya chama cha wavumbuzi.

2. Kisha, naibu mkurugenzi, mshauri, watampa mkono wa kumkaribisha katika chama cha
wavumbuzi

3. Katibu wa chama anampa mwanachama kadi la uanachama.

4. Wataimba Wimbo wa wavumbuzi, na taa huwashwa, ambayo huleta sherehe ya kuanzishwa


kwa klabu.

KUANDAA PROGRAMU ZA AC

Kuwaandaa watoto kujenga urafiki na Yesu,Kuwaelekeza katika umilele.

• Programu za mwaka(ndefu).

34
• Programu za robo au kila wiki.
• Programu za madarasa, kuonana na wazazi au ziara mbalimbali, mahubiri na uvishaji pini.

Ili kufanikisha program hizi:-

• Viongozi wawe na mipango.


• Watekeleze kalenda ya matukio.
• Washirikishe wakuu wa Kanisa katika Mipango.

MASWALI YA KUJIULIZA KABLA YA KUWEKA MALENGO YA CHAMA.

Nataka kukamilisha nini?

Nitakamilisha kwa njia ipi?

Lini nitakamilisha?

Nani atasimamia kukamilisha?

Hatua zipi za mawasiliano zichukuliwe?

MASWALA YA KIFEDHA.

Chama cha wavumbuzi kinapata fedha toka Kwa kanisa Na ada ya uwanachama. Fedha lazima
zifuate utaratibu wote wa kanisa.

NAMNA YA KUPANGA BAJETI YA WAVUMBUZI.

Nani wanaipanga- Baraza la wavumbuzi.

Lini- Wakati wa mkutano wao wa mwanzo wa mwaka au mwisho.

Mambo gani Yahusike?

Tafakari yafuatayo:

a) Unafanya kitugani mwakani.

b) Itaghalimu kiasi gani.

c) Bajeti yako ihusishe

 Tuzo za wavumbuzi.
 Vyeti vya kuhitimu.
35
 Vitu vya Sanaa.
 Miradi ya injili.
 Matukio ya konferensi.
 Matembezi.
 Mikutano na wazazi.
 Bima.
d) Vyanzo vya mapato.

 Ada za uana chama.

 Michango mbalimbali.

 Bajeti ya kanisa.

 Msaada wa mzazi.
FALSAFA YA PROGRAM ZA WAVUMBUZI
Tofauti iliyopo kwa wavumbuzi na watafutanjia ni kwamba program za wavumbuzi zinahitaji
muda mfupi. Program zinazofundishwa kwa kutumia uzoefu na mtaala wa Wavumbuzi, hukuza
utii na uwajibikaji kupitia Nyanja za Kimwili, Kiakili, kiroho, na Kijamii
I: KIMWILI

 Stadi au kazi za nyumbani kama kutandika kitanda, kuosha vyombo, Usafi wa


nyumbani, kufua nguo, kupiga pasi, kupika, kupanga meza, kutunza bustani.
 Pia atumie ujuzi huo katika ziara za mafunzo, na picnic za familia
II: KIAKILI:
 Program iwe rahisi, isiwe ya mashindano, isiyoumiza kichwa.
 iwapatie uzoefu wa kuona uwe mwingi zaidi.
III. KIJAMII:

 Iwasaidie wavumbuzi kupeana vitu mfano mwanasesere, chakula n.k


 Wafundishe kujifunza kukubali matokeo, na waishi na wenzao vizuri bila kuzingatia
kilichotokea.
 Kuwa wenye adabu na ukarimu
IV. KIROHO:

 Kukariri mafungu, Chemsha Bongo.


 Kuelewa hadithi za Biblia
 kuimba nyimbo.
V. UINJILISTI:
 kutembelea wagonjwa nyumbani mwao, kuhudumia wazee na kujua kushukuru.

36
SEHEMU YA SITA
MTAALA WA WAVUMBUZI.
MALENGO YA MTAALA WA WAVUMBUZI.

 Watoto watoe maisha yao kwa Yesu.


 Watoto wapate mtazamo chanya katika kuishi maisha ya kikristo.

 Watoto wapate tabia au mtaji na maarifa kwaajili ya Yesu.

 Mfundishe habari za Yesu.

 Mfundishe mafungu ya kukariri na nyimbo

 Mfundishe kuwa na kicho mbele za Mungu maana hatayaacha Mithali 18:18, Kutayarisha
njia uk 168 sehemu ya kwanza.

NAMANA YA KUFUNDISHA MTAALA WA WAVUMBUZI.

-Kuwa na mtaala wa wavumbuzi ni kuona mawazo yanayo hitajika kwa wanao fundishwa.

-Muongozo una namna ya kumsaidia mzazi au mwalimu namna ya kuongoza wavumbuzi.

-Muongozo unatoa maelezo ya namna ya kuunda programu za wavumbuzi.

MTAZAMO WA JUMLA

Kuwatazamisha vijana Kwa mambo tofauti na watoto wa ulimwengu wanavyo ishi na kila lengo
limegawanyika katika mambo matatu.
Mtaala wa Wavumbuzi umegawanyika katika Mambo makubwa matano yenye vipengele vitatu
kila moja;

1. Mahitaji ya Msingi:-
• Utayari (Umri).
• Majukumu(Kutumika).
• Vichocheo(shime au tia moyo).
2. Mungu wangu:-
• Mtoto aone kuwa Mungu ni wake
 (Kumwonyesha mfano wa Uumbaji, Wokovu ni wake, kuja kwa Yesu
mara ya pili).
• Ujumbe wa Mungu kwangu (Akariri Mafungu)
• Kile ambacho Mungu anataka nitende (kwenda Kanisani, kutoa sadaka).
37
3. Mimi mwenyewe.
• Ajigundue kuwa yeye ni wa pekee.
• Agundue kuwa yeye anaweza kufanya uamuzi wa busara.
• Agundue kuwa yeye anaweza kutunza mwili wake (Usafi, Mazoezi, Kiasi na
muda wa kulala). Kuheshimiana Kijinsia.
4. Familia Yangu:-
• Ajue kuwa ni mmoja wa familia,nini sehemu yake nyumbani.
• Ajue kuwa familia inajali kila mmoja ili aondoe ubinafsi.
• Kusaidia kujijali (Usalama wake, wasifunge mlango mpaka arudi)kujijali na
uwakili.
5. Ulimwengu wangu:-
▪ Aelewe kuwa ulimwengu aliomo ana Marafiki,wazuri na wabaya.
▪ Kuna watu wengine hawafanani (weupe na weusi) wapole na wakorofi, Kanisani na
Barabarani na Shuleni.

▪ Asili ya ulimwengu huu.

ZINGATIA YAFUATAYO:-
1. Panga kwaajili ya mafanikio.
 Elewa ubunifu.(Usizidishe dk 20 Katika kufundisha,wabadilishie kazi.)
 Soma vyema mtaala ili uelewe.
 Pitia kile unachoenda kufundisha.
 Shughulika na changamoto maalumu.

2. Tengeneza kalenda na ifanyia kazi.


 Tambua mahitaji muhimu ya darasa lake.
 Chagua njia sahihi ya kuwasilisha kazi zako.
 Tambua kinachoenda kufundishwa.

3. Hitaji linafundishwa lini na linaenda na kalenda.


 Litafundishwa wapi.
 Ni habari gani wanayopaswa kufahamu.
 Je utafundishaje.

4. Vyanzo.
 Uwe na vifaa vinavyo hitajika ilio ufanyanye mambo mazuri.
 Ni lazima uwe na miongozo ya ziada na kiada.

38
JINSI YA KUWAFUNDISHA
• Kulipenda neno la Mungu.
• Kulipenda kanisa la Mungu.( Kulijali).
• Waandaliwe kwa huduma(nyumbani na kanisani, kutenda kazi.

Anamsikia Mzazi:-

• Kuwashirikisha Wazazi ili kurahisisha ufundishaji.


• Washirikishe wazazi kile utakachofundisha (sheria).
• Wape wazazi vitu vya kufuatilia.
• Wape uhuru wazazi wajieleze tatizo alilonalo mtoto.
• Waambie wazazi matatizo waliyonayo watoto.

HATUA ZA UFUNDISHAJI:-
1. Anza na Mpango mzuri.
2. Uwe na ratiba ionyeshe mada na vipengele.
3. Ni mara moja au mbili kwa wiki nani Dk 20 tu.
Mfano:-

Mada Kuu Mada Muda Kazi Idadi ya watoto Tathmini


ndogondogo
Kurudi kwa Yesu Dalili Dk 20au Zoezi 25 Somo
Matayarisho limeeleweka

4. Elewa mahitaji yao:-


• Yaelewe vizuri na jinsi yanavyoweza kutosheleza Malengo yako.
• Katika robo hii unataka wapate nini (lengo).
5. Fikiria watoto wako.
• Je mahitaji yao ni nini, Wanapen delea nini.
• Je ni mambo gani ambayo wameshayafahamu.
• Anza na mambo rahisi au yaliyojulikana.
• Je hitaji hilinninalowafundisha litawasaidiaje.
6. Amua kile ambacho ni lazima kifundishwe :-
• Weka kipaumbele,tafuta ambacho ni cha muhimu.
• Panga hatua uwasaidie.
7. Panga kazi ya darasa:
• Rudia uone una vipindi vingapi na utatumia muda gani kumaliza mada.
8. Panga ratiba.
• Hakikisha kuwa kila kipindi kiwaongezee watoto kuelewa.
39
Kumbuka:

 Watoto ni wepesi kuchoka, kipindi kisizidi dakika 30, na unapofundisha zitumie kwa
kuchanganya mambo, nyimbo, mazoezi kidogo n.k

 Mwalimu hakikisha unafahamu mahitaji ya madarasa yote na vifaa vyake.

 Mtaala unatoa maelekezo ya madarasa ya wavumbuzi.


 Rangi za madarasa ya wavumbuzi
- Miaka 4 - KONDOO MDOGO - Rangi Nyekundu [Damu Ya Mzee]
- Miaka 5 - NDEGE WA AWALI - Rangi Light Blue
- Miaka 6 - NYUKI WA SHUGHULI - Rangi Ya Njano
- Miaka 7 - MWALI WA JUA - Rangi Ya Kijani
- Miaka 8 - MJENZI - Rangi Light Nyekundu
- Miaka 9 - MKONO WA MSAADA - Rangi Ya Dark Blue

Inapendekeza kuwa Kanisa lianzishe shule ya chekechea.

40
SEHEMU YA SABA
TUZO NA UFUNDISHAJI WAKE
Tuzo za Wavumbuzi ni ujuzi au Elimu inayotolewa kwa Wavumbuzi ili kupanua ufahamu wao
katika mambo mbali mbali. Kiongozi au mwalimu wa Tuzo za Wavumbuzi anatakiwa awe
mbunifu ili kufanya tuzo hizi kuwa na manufaa kwa watoto. Atie moyo kila mtoto kufanya
vizuri. Mwalimu lazima azifahamu vizuni na namna ya kuzifundisha. Tuzo zimegawanyika
katika makundi sita ambayo ni Tuzo za kiroho, Tuzo za kijamii, tuzo za viumbe vya asili, tuzo
za ufundi [sanaa za mikono], tuzo za maburudisho pamoja na tuzo za nyumbani.

Baadhi ya Tuzo hizo ni:-


1. Artist - Uchoraji
2. Astronomer - Unajimu
3. Basket maker - (Kutengeneza vikapu)
4. Bible 1 - Kujifunza Biblia I
5. Bible II - Kujifunza Biblia II
6. Computer skills -Ujuzi wa computer
7. Environmentalist -Utunzaji wa mazingira
8. Friend of animals -Rafiki wa Wanyama
9. Friend of nature -Rafiki wa asili
10. Road safety -Usalama barabarani
11. Trees -Miti
12. Cyclist -Uendeshaji wa Baskeli
13. Fitness fun -Mazoezi
14. Friend of Jesus -Rafiki wa Yesu
15. Gardener -Bustani

NB
 Hizi ni baadhi tu kati ya nyingi zipatazo karibu hamsini (50).
 Mwalimu lazima awe mbunifu katika ufundishaji wa tuzo hizo na kuwafanya wafurahie.
41
MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI UNAFUNDISHA
1. Mruhusu avijaribu vitu vinavyo mzunguka.
2. Tumia nyimbo, hadithi, maigizo na michezo katika ufundishaji.
3. Mfundishe kuwa Yesu ni mwokozi wake kwa kuomba.
4. Mwalimu kuwa mbunifu.

NDANI YA MTAALA KUNA NINI?


-Maelekezo ya mahitaji.
-Maelezo ya msingi.
-Namna ya kufundisha.
-Tathmin.
NAMNA YA KUFUNDISHA.

1. Amsha hamu.
 kwa kutumia picha, hadithi, vitu halisi au matendo, kadiri inavyowezekana
wafanye watoto wagundue wenyewe, alika wageni, mjadala na picha.

2. Washirikishe katika kutenda, ndivyo anavyoelewa haraka ni njia ya kupima uelewa wao
(zoezi).
 Nyimbo za vitendo, Michezo na maswali.
3. Fanya tathmini kagua kazi zao.

4. Kusanya Maarifa:- Vitabu rejea [ziada na kiada]


 Ziada visivyo katika Miongozo,
 Kiada vilivyo katika Miongozo,
 Hudhuria semina mbalimbali zinazohusu mambo ya vijana.
5. Fundisha mtoto na siyo darasa,
 Hakikisha kuwa unalitawala darasa lako.

6. Tathmini darasa na jiulize maswali haya.


 Je somo hili limewasaidia watoto.
 Je kusudi la somo hili limewasaidia watoto.
 Je ni vitu gani nilivyofanya.
 Alika Mwalimu au mtu akusikilize na akupe tathmini na urekebishe ulipokosea.
42
Unapofundisha Zingatia:-

i. Fundisha dini,
 Kichwani mwake awe Yesu tu.
 Jinsi ya Kumheshimu Mungu,
 tangu utoto ajue namna ya kuomba na kupiga magoti.
 Tafuta muda ambao akili hazijachoka
 Fundisho liwe fupi. (Dk 20).
 Lifanye somo liwe fupi na la Kupendeza kwa kulingana nao na kufanana nao.
 Badilisha mtindo wa ibada au kujifunza Usiwe na staili ileile tu kila siku, ili
wasione ibada kama kitu kisicho na maana.
Dini ipi wanapaswa kufundishwa;
Yakobo 1:27,
Mathayo 22: 37 – 40,
Kumbukumbu la Torati 6: 4 - 9
ii. Wafundishe kuishi maisha ya kiasi.
 Tabia ya umimi (changu) kujipendelea iondoke.
iii. Kuepuka mazoea mabaya.
 Umri huu wanaingia katika mazoea mabaya kirahisi kwani hawawezi kupambanua
mema na mabaya.
 Aina ya chakula vinywaji vinachangia kuwa na mazoea mabaya, hivyo
watenganishiwe.
iv. Wafundishwe kujihusisha na kanisa
 (Waebrania 10:25).
v. Jenga mahusiano mazuri kati ya Mzazi, Kanisa na mwalimu.
 (Watembelee)
vi. Fundisha heshima na utii.
 Picha ya watoto ndio itakayodhihirisha tabia ya Mwalimu.
 Kutoka 20:12, Mambo ya walawi 19:32.
vii. Wafundishe watoto kufanya kazi kwa juhudi,
 Kuwaacha watoto kukua kivivu ni dhambi
 Wajifunze kukunja nguo zao
 Kunyoosha nguo zao.
 Kuosha vyombo.
 Wajifunze kupika.
 Kufagia nyumba, uwanja nk.

43
 Kutunza bustani za maua, mboga nk.
 Wafundishe kutoa zaka na sadaka
viii. Zungumza na Wazazi katika kazi ya malezi ya watoto.
 Mithali 14:23; 16:26
 Kutoka 20:8,
 2Wathesalonike 3:10 - 12
ix. Wafundishe watoto kujali elimu
 Mithali 4:13
x. Wafundishe waache mazoea mabaya na kuyaepuka mfano:-
 Vinywaji visivyofaa na vinavyofaa kwa mkristo
 Vyakula vinavyofaa na visivyofaa
 Michezo inayofaa na isiyofaa kutazwa

NB:
Wafundishe kwa moyo maana umebeba maisha ya baadae ya hawa wavumbuzi.

44
SEHEMU YA NANE
FAMILIA YA WAVUMBUZI.
Chama hiki cha wavumbuzi ili kuwasaidia na kuwaunga mkono wazazi/walezi katika jukumu la
kulea mtoto/watoto na kuwafanya watoto wampokee Yesu maishani mwao.
MAWAKALA WANAOCHANGIA MALEZI YA MTOTO

Mawakala hawa wanaweza kuchochea malezi mazuri ama malezi mabaya.

MZAZI/MLEZI
SHULE
(NYUMBANI)
MTOTO
JAMII
KANISA
(MITAANI)

• Jedwali linaloonesha uhusiano wa mawakala wa malezi ya mtoto

AINA ZA WAKALA WA WATOTO.


Mungu ametuweka kuwa wakala kwa watoto hawa na zipo aina zifuatazo za wakala wa watoto:-
 Wazazi (baba na mama): Mwalimu wa kwanza na baba na mama , mwalimu ni wapili na
nimsaidizi.
 Kanisa: Kupitia waalimu
 Jamii: Wale wote wanaomzunguka mtu.
 Shule: Mzazi au mlezi unapaswa kutambua kuwa mtoto huwa na tabia tofauti tofauti
kulingana na mazingira hivyo tammbua kuwa wokovu wa mtoto uko mikononi mwako.

NUKUU:
kutayarisha njia uk, 210. Inasema
“umri wa miaka 0-9 ni mzuri wa kumpandikiza mtoto tabia unayoitaka awenayo”

45
MTANDAO WA FAMILIA YA WAVUMBUZI.
1. Mahusiano ya malezi.
 Ulimwengu wa wavumbuzi kitovu chake ni familia, ili kuyaongoza maisha ya watoto
kwa Mungu ushirikiano wa wazazi na familia unahitajiwa uratibeshwe kwa hali zote.
2. Vyanzo vya jamii katika mahusiano ya malezi.
 Pia ni muhimu au washiriki wanapaswa kufahamu nini watoto hawa wanachojifunza
jamii/washiriki pia ni chanzo kizuri cha malazi ya vijana hawa.
3. Mtandao wa Programu.
 Kunapaswa kuwepo mtandao mzuri wa kazi ya wavumbuzi na wazazi kuhusu program
zinazoendelea.

MTANDAO WA FAMILIA YA WAVUMBUZI KAMA UTARATIBU WA KUUNGA


MKONO
a) Lengo
 Kutoa mafundisho kunafaidisha familia na kutoa vifaa vya kufundishia.
b) Kujihusisha kwa familia.
 Wazazi wanakaribishwa na kuombwa kuchukua sehemu katika shughuli za chama,
kando ya mikutano ya kawaida ya wazazi wanakaribishwa na kuithamini mikutano hiyo
ushirika na vijana kutoa mvuto wao na msaada.
c) Mtandao wa familia ya wavumbuzi
 Katika eneo hili kuna mashauri kwa wazazi kusaidia kazi ya wavumbuzi wazazi ambao
inachukuliwa kuwa ni aliyezaa, malezi baraza la kanisa, idara ya familia na kaya, shule
sabato watoto, idara ya watoto zinapaswa kuunga mkono wazazi kukuza tabia ya
wavumbuzi. Sehemu hii inatoa mawazo halisi namna ya kumsaidia kiongozi kupanga
vitu vya kuvutia na kufanya mikutano ya wazazi iwe ya kupendeza.
d) Vyanzo vya jumuia
 Jumuia inapaswa iwe na mtazamo chanya kwa chama cha wavumbuzi watambue kuwa
hapa ndipo mwanzo mkuu wa kujenga tabia ya watoto, walione na kuliwekea umuhimu
kuliko program zote.

46
JAMBO LA KUFANYA KUSAIDIA KATIKA MALEZI:-

• Uwe na vikao au na mikutano na wazazi.


• Katika ziara uwe na wazazi au walezi wao,
• Wapange wavumbuzi katika umri wao ndipo wanapoanza kuvumbua vitu
mbalimbli, na ikumbukwe kwamba kwao kila kitu ni kigeni.
• Kumbukumbu la Torati 4:6-9;
• Waebrania 11:7.
Umri miaka 0-9

 Ni umri unaofaa kumjengea mtoto tabia.


 Wazazi na Kanisa ndio walimu.

 Kila kitu kwao ni kipya.

MADARASA YA WAVUMBUZI

No: JINA LA DARASA UMRI MAELEZO


1. KONDOO MDOGO MIAKA 4 Wana shughuli nyingi

2. NDEGE WA AWALI MIAKA 5 Ni umri ambao wanakua kwa haraka

3. NYUKI WA SHUGHULI MIAKA 6 Wana shughuli nyingi, si watulivu

4. MWALI WA JUA MIAKA 7 Wanaanza kuchomoza

5. MJENZI MIAKA 8 Kujenga tabia

6. MKONO WA MSAADA MIAKA 9 Anaelewa mambo anaweza


kutumika/kutumwa

47
SEHEMU YA TISA
HUDUMA ZA WAVUMBUZI
SARE ZA CHAMA.
 Sare zinafanya chama kuwa halisi na kionekane kuwa kipo hai.
 Inafanya wana chama wakipende chama na kuwaleta pamoja.
 Inaleta changamoto na wito kwa wale ambao bado hawajajiunga.
 Ni kichocheo cha kujenga moyo wa chama.
 Sare inapaswa kuwa safi kwani program za wavumbuzi ni za thamani.

SARE INA PASWA IVALIWE KWENYE MATUKIO YAFUATAYO.


1) Mikutano ya kawaida ya chama.
2) Programu maalumu.(Siku za wavumbuzi,uvishaji wa pini)
3) Huduma mbalimbali za kijamii na kikanisa. Mfano: Kugwa chakula, kupokea
wgeni,kutembelea wagonjwa,msaada wa huduma ya kwanza.

AINA ZA SARE:
1. Official Uniform/Sare za kiofisi
(Huvaliwa na wanachama,walimu, na wakurugenzi wakati wa program.)
2. Sare za kazi.
(Huvaliwa wakati wa shughuli mbalimbali na mafunzo kama Hiking,safari,ziara,kazi za
kijamii.)
3. Staff Uniform/Sare za viongozi.
(Huvaliwa na wakurugenzi)
Sare ya daraja la kwanza wavumbuzi wavulana na wasichana.
Wasichana- Sketi za nevy-blue na shati jeupe la mikono mifupi.
Wavulana- Kaptula au suluari za nevy-blue na shati jeupe la mikono mifupi kora za kawaida.
Viatu vyeusi na soksi nyeupe
Skafu pamoja na slide
Mkanda wa tuzo ni rangi ya Nevy blue.
SARE YA MAOFISA WA WAVUMBUZI.
Wanawake- Sketi nevy blue na shati jeupe mikono mifupi.
Wanaume- Suruali za nevy blue na shati jeupe mikono mifupi.
48
Wanawake & Wanaume sare ndani ya chama mkanda mweusi tai ya nevy blue au skafu za
wavumbuzi.
Mkanda- Mkanda huvaliwa wakati maalumu,Nishani za AY zisivaliwe kwenye mkanda wa
wavumbuzi, Tuzo pekee ndizo zina kaa kwenye mkanda.
Nembo- Patch ya wavumbuzi inavaliwa bega la kulia
Nembo ya dunia ya wavumbuzi inavaliwa bega la kushoto
Crescent ya chama inawekwa kulia juu kidogo ya Patch.
Tuzo za wavumbuzi zinavaliwa katika mkanda.
Pini za madarasa zinavaliwa katika mfuko wa hati au Blauzi upande wa kushoto kuanzia kulia.
SARE ZA KAZI.
Sare za wavumbuzi za kazi ni Shati la light blue au T-shart ya Blue.
Kanisa linaweza kubuni sare ya kazi kwa wavumbuzi lakini iwe nembo ya chama
NB
Nembo ya chama cha wavumbuzi.
 Msalaba
 Mtoto
 Wazazi
 Viumbe vya asili [mazingira]

EMBLEM
Adventurer World Logo Adventurer emblem

END

49

You might also like