Professional Documents
Culture Documents
Mbinu Za Kufundisha
Mbinu Za Kufundisha
1
MBINU ZA KUFUNDISHA.
MAELEZO YA SOMO:
Ualimu ni moja ya karama za huduma katika kanisa. Ni ofisi kati ya ofisi tano za kanisa la
Mungu (Efeso 4:11) wengine aliwapa au alitoa wawe Mitume, wengine wawe Manabii,
wengine Wainjilisti, wengine Wachungaji, na wengine Waalimu.
Mwanzilishi wa Kanisa duniani Bwana Yesu Kristo alitumia muda wake mwingi kufundisha
kuliko kuhubiri kwa sababu alikuwa anatengeneza watenda kazi ambao baadaye aliwatumia
huko na huko
1. Darasa la mtu mmoja mmoja mfano Nikodemu, Mwanamke msamaria kisimani.
2. Darasa la watu watatu—hasa wale wanafunzi wa Yesu Petro,Yohana, na Yakobu,
kwenye mlima wa ugeuko, bustani ya Gesthmani.
3. Darasa la watu 12—mfano wanafunzi wake.
4. Darasa la watu wengi akitumia hotuba (Lecture) mfano (Math 5:1-11)
Njia alizotumia Bwana Yesu kufundisha na hotuba, majadiliano—mfano ‘hivi watu husema
mimi ni nani?
Wengine husema wewe ni Nabii….Nanyi mwasema kuwa mimi ni nani?
Njia ya maswali na majibu, mifano, kwa njia ya matendo—mf kuwaosha miguu, kuwachukua
wanafunzi watatu kwenda nao kwenye maombi mlimani.
Kwa njia ya mazoezi kwa wanafunziwake alipowatuma kuhubiri na kukemea pepo, semina—
mf alipoingia hekaluni na kuhojiana na wasomiwa wakati huo, kwa njia ya ishara na maajabu,
pia kwa njia ya maisha yake.
Yesu Kristo aliwapenda wanafunzi wake pia aliwajua (Math 9:35-36, Yoh 2:24)
Pia alikifahamu vizuri kile alichokuwa akifundisha na alifahamu jinsi ya kufundisha
ANGALIZO: Kwa hiyo kufunza au kufundisha ni kipawa maalumu toka kwa Mungu , wala sio
wote waliojaliwa kipawa hiki.
2
a. Mwalimu ni nani:
Mwalimu ni yule aliye na kipawa cha kutoa/ kugawia maarifa na ujuzi kwa mtu au
watu wasiojua na kufikia mahali pa kujua.
Mwalimu ni yule anayefanya akili za watu wengine zipanuke katika kujua mambo
na kukaa katika mpangilio.
Mwalimu ni yule anayezibua ufahamu wa watu wengine na kufikia hali ya
kujiamini.
Yule anayetoa maelekezo, yule anayeboresha kile unachokifahamu.
Kwa kifupi mwalimu ni yule anayefunza na kuwafanya wengine wajifunze kufikia kubadilika
kitabia.
Wanaojifunza tunasema wamejifunza tunapoona tabia zaozimebadilika kuelekea kwenye
maadili mema ya Neno la Mungu.
b. Mwalimu mzuri:
Anawaongoza wanafunzi kutoka eneo wanalojua na kuwapeleka eneo ambalo
hawalijui.
Mwalimu ajiweke kwenye nafasi ya kutaka kujifunza kutoka kwa mwanafunzi na
kumshirikisha mwanafunzi wake kile anachokijua.
Ni yule anayetegemea majibu ya matatizo au maswali yatoke kwa wanafunzi pia.
Mwalimu asiwe ndiye mwenye majibu peke yake na mwanafunzi wake kama
makinda ya ndege katika kupokea chakula.
Mwalimu na mwanafunzi huzungumza sio mwalimu peke yake ndiye
mzungumzaji.
Wanafunzi wapate nafasi ya kueleza uzoefu wao.
Mwalimu asifikiri kuwa yeye ndiye chanzo cha kila kitu, bali ajue vitu vingine
vitoke kwa wanafunzi.
Mwalimu hupanga mambo akishirikisha wanafunzi wake.
Anawapenda wanafunzi, anawajua, anajua anachofundisha na jinsi ya kukifundisha
Aishi kama anavyofundisha—matendo husema zaidi kuliko maneno (Luka
24:19, Yoh 18:38)
ANGALIZO
Mwalimu mzuri ni yule anayeshirikisha na yeye anakuwa mwezeshaji. (Facilitator)
3
Aonyeshe mwelekeo wake kwa wale anaowafundisha.
Awe na uhusiano mzuri na Mungu wake.
Awe na ujuzi wa kutosha namna ya kutumia vifaa vya kufundishia na chumba cha
darasa lake.
Wajibu wake mkuu ni kufaulisha mpango wa kufundisha kanisani.
Chukua muda mrefu kuwafundisha waanini kanisani mpaka wanakuwa watenda
kazi wazuri.
Uweze kuzaa waalimu, wachungaji, wainjilisti , mitume na manabii Math 28:19-20
Kwenda itika kuwafanya mataifa kuwa wanafunzi wa Yesu Kristo, kuwafanya wayashike yote
niliyowafundisha.
Malengo ya somo ni muhimu ili kuweza kupanga, kufunza na kukagua/ Tathmini hatimaye
kutoa taarifa ya mafanikio au mapungufu.
1. Kusudi kubwa la kufundisha ni kuwafikia wengine kupitia mafundisho au elimu ya Neno
la Mungu.
2. Uinjilisti na elimu ya Neno la Mungu ni sawa na mabawa mawili ya ndege inayoruka.
3. Uinjilisti ndiyo lengo kuu la kufundisha Neno la Mungu.
4. Uinjilisti ndiyo lengo la msingi la Ukristo wetu.
5. Kuwafanya wanafunzi wa Bwana Yesu Kristo.
Kusudi la pili la kufundisha ni kufikia kiwango cha kujua umuhimu wa ubatizi katika maji
mengi na kasha ubatizo katika Roho Mtakatifu na kubatizwa.
Math 28:19.
Aina za malengo:
a. Kuongeza elimu, kuwa na kweli nyingi za Biblia ni muhimu kwa mwanafunzi wa Biblia,
Ni vema mwanafunzi kuielewa Biblia na kujua ili waweze kujitoa kwa njia sahihi kwa
Kristo Yesu.
Kiini cha injili ni ukweli wa kihistoria wa maisha ya Kristo- Kifo chake na kufufuka
kwake.
b. Kubadilisha mielekeo yao na mitazamo.
Eneo hili hushughulikia hasa hisia na shauku za wanafunzi, wanafunzi haitoshi kujua
ubaya wa dhambi, kinachotakiwa ni wao kufikia hatua ya kuichukia hiyo dhambi na
kuiacha kabisa—pia wafike mahali pa kuhusiana vema wao kwa wao kama watoto wa
Mungu.
4
c. Kubadilisha tabia:
Kubadilisha mwelekeo unatakiwa uendelee kiasi cha kubadilisha tabia yote au haiba yote
ya mwanafunzi, kubadilika tabia kabisa ni hatua ya maana sana katika ufundishaji wetu
wa Neno la Mungu (Math 5:20)
Haki ya wanafunzi wako lazima izidi ya wale wa dini tu.—hawa huonyesha mielekeo
kama imebadilika, imekuwa sahihi lakini tabia zao ni kama mtu yule yule wa zamani
(Luka 11:28, Yak 2:20)
Roho Mtakatifu akiwa namba moja wa kubadilisha tabia ya mtu.
5
NJIA FAIDA HASARA WATU
WANAO
PENDELEWA
MHADHARA -Mwalimu humaliza somo -Wanafunzi hawashiriki Vijana na watu
HOTUBA haraka. kikamilifu. wazima.
-Mwalimu hufuata mpangilio wa -Ni vigumu kutathmini.
somo lake bila bugudha. -Wanafunzi huchoka
-Mwalimu hutawala somo na haraka.
kuepuka kwenda nje ya somo. -Wanafunzi hulala
-Hufundisha watu wengi kwa darasani
mara moja.
HADITHI NA -Hufahamu kweli ambazo haziko -Kutajua hadithi nyingi. Watoto na watu
MIFANO wazi. -Kutoa hadithi nje ya wazima
-Hukazia mambo muhimu ya somo.
somo. -Kutumia lugha
-Huvuta usikivu wa wasikilizaji. isiyoendana na hadithi.
-Ni rahisi kuiga katika maisha ya
kila siku.
USHUHUDA -Hujenga wengine. -Wengi hawana karama Watu wote
-Hutia moyo wengine. ya kushuhudia. hupenda
-Huleta ujasiri wa kusonga -Kuficha ukweli ulio
mbele. -kutokea au kuongeza.
MUZIKI -Hufurahisha -Huficha ukweli Watu wote hasa
-Huvuta usikivu wa watu. uliotokea au kuongeza. watoto.
PICHA -Huvuta usikivu. -Uhaba wa picha Watoto hasa na
-Huona vitu vinavyofanania na -Ugumu wa kuchora. watu wazima.
somo, hivyo husababisha uelewa.
MICHORO Ya halisi Muda wa kuchora ni
adimu
MWANASESERE Kuvuta usikivu Ni vigumu Kwa watoto
-Huelewesha zaidi (msaada kwa kumwakilisha Mungu.
mwalimu Ni vigumu kutengeneza
na kutumia
MAJADILIANO. Hushirikisha kila mwanafunzi . Mtu mmoja mjanja Zaidi hutumika
Hujenga moyo wa kujianini. kuhadithia kipindi kwa kwa watu wazima
Hoja nyingi hupatikana. nje ya somo.
Waoga hubakia
kusikiliza wengine.
Mwalimu asipokua
makini huweza kuingia
hoja potofu.
Hutumia muda mwingi.
MAISHA YA Ni rahisi kuiga Ikiwa mwalimu haishi Kwa watu wote
MWALIMU kama anavyofundisha.
6
2. Njia ya vikundi.
3. Michezo ya kuigiza.
4. Safari za kujifunza.
5. Project au kwa njia ya vitendo.
6. Mafunzo ya Biblia.
Muhtasari.
a. Njia ya majadiliano-kila mshiriki anahimizwa kusema.
b. Vikundi-huleta habari kutokana na aina nyingi za ujuzi.
c. Michezo ya kuigiza-huleta uhai mpya wa kweli za Biblia.
d. Safari za kujifunza- wanafunzi hujifunza moja kwa moja kwenye ujuzi wa kujifunza.
e. Project/ vitendo—pia huwahusisha wanafunzi kwenye utafiti au kwenye utumishi wenye
manufaa wa kikristo.
Project- kwa kufanya utafiti
Kwa kutumia mifano, kushuhudia, kuhubiri, nk.
f. Mafunzo ya Biblia- huwatia wanafunzi bidii ya kutafuta ukweli mpya na matumizi ya
sehemu za maandiko.
7
e. Somo liwe na motisha kwa wanafunzi—yaani somo likutane na mahitaji ya
wanafunzi.
3. Sheria ya Lugha.
Lugha ya kufundishia iwe inafahamika kwa watu wote wawili— mwalimu na
mwanafunzi—Lugha ya kufundishia ni vyema isiwe na misamiati migumu.
4. Sheria ya somo.
Anza somo lako kutoka eneo wanalolielewa wanafunzi na kisha wapeleke eneo
lisiloeleweka, kwa kutumia ufahamu ulio wazi kwao kama msingi wa somo jipya.
a. Husisha somo kwa masomo yaliyopita (marudio ya somo kabla ya somo jipya)
b. Endelea kwa hatua za juu zaidi hatua kwa hatua ya kuelewa wanafunzi.
c. Fundisha kwa kutumia mifano ili kurahisisha kuelewa.
6. Sheria ya kujifunza:
Kujifunza ninini?
Jibu:
Ni kuwaza na kuingiza kwenye fahamu ya mtu wazo jipya la kweli au kufanya sanaa au
ujuzi mpya kuwa sehemu ya maisha ya mtu, ili kufaulu kufanya haya ni lazima
mwanafunzi awe na tabia ya:-
a. Kurudia rudia yale aliyojifunza.
b. Kuyatafsiri- kutambua kuwa wamepata ujuzi huo ni pale wanafunzi watakapoanza
kutoa maoni yao juu ya ukweli walioupata.
Hapa swali la kwa nini? Liweze kutumika na kujibiwa mbali na maswali mengine ya
nani, nini, wapi na kwa vipi?
8
c. Kuyatumia katika maisha yao, Elimu ni nguvu ya kubadili maisha ya mtu. Mtu
aliyesoma kama hawezi kuishi sawasawa na elimu yake, huyo hakusoma na hana haki
kujivuna kuwa amesoma.
Angalizo.
9
Vitabu hivi visiwe jawabu la mwisho kuhuso Biblia kwa sababu walioandika ni watu tena watu
wa karne yetu-wasomi.
MAANDALIZI YA MWALIMU
1. Kusoma hayo yaliyotajwa hapo juu.
2. Kukusanya vielelezo- hadithi, picha, mifano, ili yakusaidie kupanga masomo yako ya
mbele.
a. Panga masomo na kuyaandaa kabla ya kufikia muda wa kufundisha ikiwa ni pamoja
na zana/ vielelezo vya kufundishia.
b. Kutana na mahitaji ya kila mwanafunzi.
Ujue mahitaji ya darasa lako
Mjali kila mwanafunzi wa darasa lako.
Mfano : andaa picha za kutosha au picha kubwa, ramani/ mchoro utakaomwezesha
kila mwanafunzi kujifunza.
c. Kutana na mahitaji yako binafsi.
Mwalimu anatakiwa kukua kiroho na kiakili.
Hivyo mwalimu hana budi awe msomaji wa vitabu kwa utaratibu.
Kuwa mwombaji na kuombea kazi yako ya ualimu.
10
Lengo: Mwalimu anahitaji msaidizi wakati mwingine hueleza mambo ambayo mwalimu halisi
asingeeleza.
UTAFITI
Watafiti wa ualimu wamegundua viwango vya mwanafunzi vya kukumbuka.
Anaposikia hukumbuka 10% yale aliyosikia.
Anapoona anakumbuka 50% yale aliyoyaona.
Anapofanya anakumbuka 90% yale aliyoyafanya.
Anaposema hukumbuka 70% yale aliyoyasema.
Hivyo ni muhimu ziwepo kazi za mikono zitakazofanywa na wanafunzi ili fundisho lako lipate
kueleweka na kukumbukwa na wanafunzi.
11
NJIA ZA KUPANGA SOMO.
A. Hutegemea akili za mwalimu. Akili bora inatakiwa.
1. Chukua habari tu zinazofaa kufundishwa.
2. Uunganishaji wa habari toka maeneo tofauti tofauti, toka vyanzo tofauti.
3. Fundisha toka yanayojulikana kuelekea yasiyojulikana.
b. Kusudi la somo likishawekwa bayana ni rahisi kuamua mambo gani yatiliwe mkazo.
Kwa mfano: Mwalimu lazima awe makini Ukweli anaoutaka ukae ndani ya akili za
wanafunzi
Kichwa cha somo.
Sehemu za Biblia zinatakiwa kukumbukwa.
Vidokezo vya somo.
12
MPANGO WA SOMO:
a. Jina la somo
b. Tarehe.
c. Andiko la somo
d. Mstari wa kukumbukwa (mstari wa msingi)
e. Kweli kuu.
f. Lengo la somo.
g. Vidokezo vya somo.
h. Jinsi utakavyoshughulika na darasa (unda hali bora ya kusoma darasani)
i. Maendeleo ya darasa (njia za kufundisha, vifaa vya macho na masikio — mfano:
Projecti, maswali na mafafanuzi.
j. Mwitikio (jambo ambalo wanafunzi wanaweza kufanya kuonyesha uelewa wao.
k. Kazi za nyumbani kwaajili ya somo litakalofuata— mfano: kusoma mistari fulani ya
Biblia au kumweleza mhusika katika habari itakayokuja katika somo linalofuata.
13
wakati mwingine husababishwa na kujua kidogo na kutomshirikisha Roho mtakatifu
katika kazi ya ufundishaji.
4. Mwalimu ahakikishe anafanya maandalizi ya somo lake— Mwalimu anatakiwa kuwa
hodari katika kuwaongoza wanafunzi katika somo/ masomo yale anayofundisha kwa
uzuri na mvuto wa kutosha.
Angalizo:
Wanafunzi wanaweza wakawa sababu pia ya kutofanikisha somo lako:
Shida za wanafunzi binafsi:
Kufanya mambo kinyume, kutotulia darasani, matendo ya kutokuwajali wengine,
kutokuwa makini na masomo.
5. Kuboresha nidhamu:
a. Kuelewa kusudi la nidhamu—ambayo hulenga kukuza vipawa vilivyo vyema—
Mfano kuwaongoza wanafunzi kumjua Mungu zaidi, Kusababisha kuwa
wanyenyekevu na uadilifu kwa wanafunzi wote.
Hulenga kurithisha maadili mema toka kizazi hadi kizazi.
Hulenga wanafunzi kumfanania Yesu Kristo ambaye ndiye chanzo cha utaratibu,
Kumbuka ni wa utaratibu. Hufanya sahihi, Kwa wakati sahihi na Kwa watu sahihi.
Kitakachofanya wanafunzi wafanye sahihi kwa wakati sahihi, kwa watu sahihi ni
NIDHAMU chini ya uongozi wa Roho mtakatifu.
b. Weka msingi wa nidhamu, kuwapenda wanafunzi-Kuwajali-kukutana na mahitaji yao
katika mafunzo, Kukuza uwezo wako, Uwe wazi kwa wanafunzi nini unachowataka
wafanye na tabia gani inayotakiwa.
c. Usiwabague wanafunzi— kama wapo wenye shida shughulikia msingi wa shida hiyo
ikiwezekana uimalize— Shida za darasa ni pamoja na utulivu, kuasi, zogo nk.
Shida za ndani, roho zao au ukristo wao haujakaa vizuri.
d. Himiza sana uhusiano mwema—wanafunzi lazima wapendwe na kukubaliwa jinsi
walivyo, Mtu akibadilika ndani huwa mtu mzuri sana, onyesha shauku kubwa ya
kuwasaidia.
e. Waalimu wa kutosha ni moja ya kudumisha nidhamu ya wanafunzi—Mwalimu
mmoja asiwe na wanafunzi wengi kiasi kwamba hushindwa kuwasaidia wengine na
kusababisha zogo.
f. Mwalimu ni lazima kuwaombea wanafunzi wako (panga, fanya bidii, kufundisha na
kuwaombea kwa uaminifu)
g. Mwalimu ni vizuri kupima na kukagua uelewa wa wanafunzi kupitia:
Majaribio, Maswali, Kazi za nyumbani, Projecti, Mitihani nk.
Angalizo
1. Ufundishaji mzuri husababisha maisha ya wanafunzi.
2. Kumjali mwanafunzi, mpango wa ufundishaji kila unapofundisha na nguvu za
Roho mtakatifu na bidii ya mwalimu, ni muhimu sana katika ufundishaji.
3. Kushirikisha elimu kwa vitendo husaidia sana katika swala zima la kujifunza.
14