Professional Documents
Culture Documents
UONGOZI
UONGOZI
Mungu ameona tangu zamani umuhimu wa uongozi ndiyo maana inamugharimu muda wa kutosha kuandaa viongozi.
Musa aliandaliwa kwa miaka 40, Yusufu, Daudi, wanafunzi wa YESU. (MDO 7:23, 30-34, 1SAM. 16:13, 2SAM.
5:1-3, MWA. 41:41-45
Toka katika kuongoza kondoo hadi watu. Musa, Daudi. ZAB. 78:71-70, KUT. 3:1-
Toka katika kuongoza nyumba, vitu, wafungwa hadi Taifa lote la Misri.
Toka katika kuongoza watu 400, 600, kabila moja la Yuda hadi Israel nzima. 1SAM. 23:13, 1SAM.30:10, 2SAM
5:1-3
Musa aliona vivyo hivyo juu ya uhitaji wa uongozi ndiyo maana akaomba MUNGU ili apate mtu baada yake.
HES. 27:15-21
Tunahitaji kuandaa watu, kuomba MUNGU tukiondoka wawepo watu wa kuongoza.
Kanisani kuna mahitaji makubwa ya uongozi.
Kukosa maongozi kunaleta udhaifu katika kanisa.
Tuna wajibu kuona kanisa linasimama imara na hii itatokea tukiwa na maongozi imara yaliyoandaliwa.
Jamii hazina nguvu, haina afya, isipokuwa kiongozi akiwa na afya.
Kanisa vivyo hivyo haliwezi kuwa na afya bila uthibiti wa viongozi au imara wa viongozi.
Ulimwengu una shida mbalimbali hata kama kuna shida nyingi. Shida kubwa kuliko zote ni kukosa viongozi.
Ukristo ndiyo unakabiliwa Zaidi kuliko kitu chochote, ni kukosa uongozi. Kusimama kwa taifaau kanisa hutegemea
uongozi uliopo.
Ni hamu ya jamii husika kuwa na uongozi imara. HAMU hiyo ipo kanisani pia. Watu wana hamu ya kupata kiongozi
ambaye wangemtegemea, wangemuelewa, ili wapate kuendelea vizuri katika maisha yao ya rohoni, uongozi
utakaowakuza kiroho.
Kuzaliwa.
Kuelimishwa.
Uzoefu wa muda mrefu wa maisha.
Mwito wa MUNGU. Sisi watu wa Kiroho tunaamini hivyo. (Imani ya Wayunani ni kuwa uongozi ni zawadi
toka kwa MUNGU). 1SAM. 16:1, 2SAM. 22:1, DAUDI-2SAM. 23:13, 24:16, ELISHA-2FAL.2:1,
YUSUFU-MWA. 42:16
AINA ZA UONGOZI
Kuna aina kadhaa za uongozi.
Kanisani tunahitaji uongozi wa aina gani? Ni uongozi wa MUNGU.(LK 10:33-35,YN 14:16-18, MDO 13:2, 20:28,
1KOR. 12:4-11, MDO 5:1-11)
MBINU ZA UONGOZI.
Uongozi una kanauni zake.
Uongozi una taratibu zake.
Uongozi una mbinu zake.
Kanuni hizo husaidia kufanikisha uongozi ili uwe bora zaidi. Hivyo ni muhimu tukachunguza mbinu na taratibu hizo
ili tuwe na uongozi ulio bora na kufaa.
Kiongozi mwajibakaji, Mfano MUSA, HES. 14:11-18 hajatawaliwa na ubinafsi, anatafuta faida ya wale
anaowaongoza. 2SAM. 24:16-17 aliye tayari ikibidi kuwajibika.
Nasi tunahitaji kuzitumia mbinu hizo zinazofaa, kwa kujifunza kutoka kwa viongozi waliopita na jinsi walivyofaulu
katika uongozi wao pamoja na maombi, kujazwa na Roho MTAKATIFU na kusoma neno la MUNGU, basi
tutafanikiwa kuwa viongozi bora.