Professional Documents
Culture Documents
Kanuni Za Kufasiri Maandiko Hermeneutics
Kanuni Za Kufasiri Maandiko Hermeneutics
HAMETIKI
Kanuni za Kufasiri Maandiko
Msingi wa Kujenga Watendakazi na Viongozi Watumishi
Wanaojizidisha na wenye Maono ya Kuigusa Dunia Nzima.
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
MADA YA KWANZA
UTANGULIZI WA JUMLA WA HERMENEUTICS
1. UTANGULIZI
Neno Hermeneutics linatokana na neno la Kigiriki. Neno hermeneien. hilo linatokana
na neno Hermes mojawapo ya miungu ya Kigiriki aliyekuwa Talishi (messanger).
Mungu huyo alihusika na kusafirisha na kufasili mawasiliano baina ya miungu
Hivyo neno Harmeneus hutumika kumaanisha kuelezea (to explain )au kufasili
(Translate )
1. Pengo la utamaduni.
Utamaduni ni jumla ya mfumo mzima wa maisha. Pengo la utamaduni linahusisha
tofauti zilizopo kati ya utamaduni wa mwandishi na utamaduni wa msomaji. Ili
kuondoa pengo hili kanuni za Hermeneutics zinahitajika
2. Pengo la Kihistoria
Pengo la kihistoria linahusiana na tofauti ya muda toka kipindi cha mwandishi hadi
kipindi cha msomaji.
1
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
3. Pengo la Lugha
Hii ni tofauti iliyopo kati ya maandishi halisi (origin manuscript) ya Biblia na
tafsri mbalimbali za Biblia. Biblia iliandikwa kwa lugha za Kiebrania cha kale,
Kialamu na Kigiriki cha kale. Lugha tatu tofauti zenye tofauti ya kisarufi. Hivyo kuna
uhitaji wa kuondoa pengo hilo kupitia kanuni za kufasiri Maandiko.
4. Pengo la kijiografia.
Pengo la kijografia linahusika na utofauti wa maeneo kati ya eneo la mwandishi na
eneo la msomaji. Jiografia ya eneo moja huweza kubadilika kutokana na mabadiliko ya
tabia ya nchi na sura ya nchi na maendeleo ya shughuri za kibinadamu. Hivyo kuna
maeneo mengi ambayo yametajwa katika Biblia leo hii hayapo ama yamebadilishwa
majina, hayaitwi kwa majina ya zamani. Pia tofuati za hali ya hewa na shughuli
mbalimbali za kiuchumi
5. Pengo la kifalsafa
Pengo la kifalsafa linahusu tofauti ya kimtazamo kuhusu ulimwengu na maisha kwa
ujumla kati ya mwandishi na msomaji wa Biblia. Ili kuweza kufasili Maandiko kwa
usahihi inatakiwa kutazama ufanano kati ya mtazamo wa mwandishi na mtazamo wa
msomaji.
2
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
Kutokana na nukuuu hiyo ni wazi kuwa baadhi ya mafundisho ya Paulo ni vigumu
kuyaelewa na kwamba baadhi ya watu wasio na elimu wameyapotosha. Kwa
kutazama usuli wa kifalsafa unaweza kuhitimsha kwamba baadhi ya watu ambao
hawakuwa na elimu ya kutosha walimwelewa visivyo. Hayo ndiyo matokeo ya utofauti
wa akili baina ya wanadamu
Msisitizo
Paulo alimwandikia Timotheo kwamba
Jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mtendakazi asiye na sababu ya
kutahayari ukilitumia kwa halali neno la kweli. 2Timotheo 2:15
3. MKAZO WA HERMENEUTICS
EKSIJESIA NZURI NDIO MSINGI WA THEOLOGIA
Kwa sababu kila kitu tunachokijua kuhusu Mungu kimefunuliwa kwa upana kupitia
Maandiko Matakatifu, kwa hiyo basi Theolojia yote imejengwa juu ya Fasili ya
Maandiko Matakatifu. Kama tutafasili hovyo Maandiko maana yake ni kwamba
Theolojia itakayojengwa itakuwa potofu na italeta athari hasi katika imani na
mwenendo wa waamini. Hii ni kwa sababu matendo na maneno ni matokeo ya kile
mtu anachoaamini. Hivyo tunapaswa kujihusisha zaidi katika kufasili Maandiko kwa
usahihi ili tuweze kuwa na Theologia sahihi inayoegemea kwenye Biblia. (Bible
centred Theology)
3
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
4. SIFA ZA MFASIRI BORA WA MAANDIKO
Kwa hakika si kila mtu anaweza kufasili Maandiko. Mfasiri bora wa Maandiko hana
budi kuwa na sifa kadha wa kadha. Baadhi ya sifa anazotakiwa kuwa nazo mfasili bora
wa Maandiko ni
1. Awe amezaliwa mara ya pili (ameokoka)
mfasili wa Maandiko ni lazima ase amekutana na Yesu katika maisha yake na awe
amempokea Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yake.Kuokoka ndio mwanzo
wa mahusiano na Mungu na ndio mwanzo wa kuweza kupokea mambo ya kiungu.
Mtu yeyote asiyeokoka kwake Biblia ni kitabu kilichofungwa na hawezi kuielewa
Biblia.
Soma 1wakorintho 2:14
Basi mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mambo ya Roho wa Mungu;
maana kwake huyo ni upuuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa
yatambulikana kwa jinsi ya rohoni.
Mfasili bora wa Maandiko ni lazima awe na uwezo wa kupokea mambo ya kiroho toka
kwa Mungu.
3. Awe mnyenyekevu.
Unyenyekevu ni hali ya kukubaliana na hali ilivyo na kuwa tayari kuchukua hatua.
Mfasili wa Maandiko lazima akubali kunyenyekea mbele za Mungu ili Mungu aweze
kusema nae kupitia Neno lake. Pia anapswa kuwa tayari kujifunza na kuachana na
mtazamo aliokuwa nao kabla ya kuelewa maana ya Maandiko hayo. Lazima aweze
kuchukua hatua sawasawa na Neno la Mungu linavyotaka.
Watu wengi na makanisa mengi leo wamejiundia fasili ya Neno la Mungu na wako
tayari kupinga fasili nyingine yoyote iwapo haiendani na fasili zao bila hata ya
kufanya uchunguzi wa kina.
4
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
4. Bidii na uvumilivu
Wakati mwingine kupata fasili ya Andiko si tukio la mara moja au la muda mfupi.
Inaweza kuchukua muda mrefu na inahitaji kujitoa kikamilifu kufanya uchunguzi na
utafiti. Hivyo mfasili bora wa Maandiko hapaswi kuwa mvivu na mzembe. Ni lazima
awe mchapakazi na asiye kata tama upesi. Hakuna njia ya mkato katika kuyaelewa
Maandiko Matakatifu. Ni lazima kutoa muda kikamilifu kujifunza Neno, kununua
vitabu na vifaa vingine vya kujifunzia na mwisho kuliweka neno katika matendo.
Jografia ya Palestina
i. Uelewa kuhusu jografia ya Palestina itamsaidia mfasili kuelewa baadhi ya
vifungu vya Maandiko.
Mfano Zaburi 133:3
Kama umande wa Hermoni ushukao milimani pa Sayuni.,,,
5
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
Uelewa mzuri kuhusu usemi wa umande wa Hermoni ushukao milimani pa Sayuni
unategemea namna mtu anavyoielewa Jografia ya Palestina.
Historia ya watu wengi wa kale na sasa ni za thamani sana. Mfano habari za dola ya
Ashuru, Misri, Babeli, Uajemi, Uyunani na dola ya Rumi zinatoa mwanga katika
kuielewa Biblia.
iii. Uelewa wa lugha za Biblia
Lugha imekuwa nyenzo au chombo kikuu cha mawasiliano katika zama zote. Kwa
sababu Biblia iliandikwa kwa lugha zingine zisizo zetu, hivyo mfasili wa Maandiko
anapaswa kuwa na maarifa yahusuyo lugha za asili za Biblia ambazo ni Kiebrania,
Kiaramu na Kigiriki.
6
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
MADA YA PILI
HISTORIA YA HERMENEUTICS
1. UTANGULIZI
Katika kipengele hiki tutatalii historia ya Harmeneutics. Harmeneutics ina historia
ndefu na inavutia sana. Historia ya Harmeneutics inakupa kuzifahamu na kuzielewa
mbinu za kufasili Maandiko ambazo ziliundwa miaka mingi iliyopita na zinatumika
hadi sasa. Katika kipengere hiki tutajifunza historia ya Hermeneutics kutoka katika
kipindi cha wayahudi wa kale mpaka kipindi cha sasa.
Malengo
Baada ya kujifunza kipengere hiki utaweza
Kuelezea kila kipindi katika historia ya Hermeneutics
Kuainisha wanazuoni mbalimbali wa Hermeneutics (hermeneutist)
Kutathmini mchango wa kila mwanazuoni wa Hermeneutics katika uundaji wa
sheria na kanuni za kufasili Maandiko
Kuainisha mbinu za hermeneutics zilizotumiwa katika kila kipindi.
7
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
Fasili halisi pia hujulikana kama Peshati. Fasili hii hufanyika msingi wa kategoria
zingine za fasili na haikuandikwa kwa sababu ilichukuliwa kwamba kila mmoja
alikuwa anaifahamu na haikuwa na mkanganyiko.
Fasili Halisi inadai kwamba andiko linamaanisha kile linachosema isipokuwa kama
imeelezwa vingine.
Fasili ya Kimidrashi iliweka mkazo zaidi katika maana mficho na hivyo Eksijesia ya
Kimidrashi ilipoteza maana halisi ya Andiko.
8
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
9
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
THOMAS AQUINAS
Thomas Aquinas alikuwa ni mwanafalsafa, wa kiitalia na mwanatheologia ambaye
kazi zake zimemfanya kuwa mwanazuoni mashuhuri wa falsafa na mojawapo wa
wanatheologia wakuu wa kanisa Katoliki.
Thomas Aquinas alijifunza Falsafa ya Alistote katika chuo kikuu cha Nepali.
Mafundisho hayo yaliweza kumuathiri na kumfanya aweze kuunda mawzo yake ya
kitheologia na kifalsafa.
10
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
Aquinas anatambuliwa kuwa mtu mashuhri sana katika kipindi zama za kati. Thomas
Aquinas aliacha kushadadia mbinu ya fasili ya sitiari na kuanza kutetea mbinu ya
uhalisia na matumizi ya mbinu ya sarufi na historia (usuli) kama msingi wa milango
mingine ya fasili ya Maandiko.
Alisisitiza kwamba msomaji wa Biblia anapaswa kutambua kwamba Biblia ina maana
ya kimafumbo (symbolic meaning) kwa sababu mambo ya kimbingu hayawezi
kuelezwa kwa maneno ya kidunia bila kutumia lugha ya ishara (mafumbo).
Kwa majibu wa Thomas Aquinas mfasili anapaswa kushughulikia maana halisi
11
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
na shauku ya kujifunza kuhusu mambo ya kale. Kwa namna moja au nyingine
walijifunza kuhusu mambo ya Ugiriki ya kale, Rumi ya kale n.k.
Wakati huo wa renaissance kuliibuka wasanii wengi sana wengi wao walikuwa
waandishi, wengine wanafalsafa. Watu walijifunza mambo ya hisabati na sayansi
mbalimbali. Kipindi hiki cha Renaisance kilianzia Italia na kisha muda mfupi kilienea
ulaya nzima. Pia renaissance ilipelekea kuzaliwa kwa falsafa ya ubinadamu
(humanismic philosophy) ambayo iliweka mkazo wa uthamani wa kila mtu.
Wanahumanist wa renaissance waliamini kwamba kulikuwa na uwezekano wa
kuboresha jamii kupitia elimu. Elimu hii ilijikita katika kufundisha kutoka katika
matini za kale na iliweka mkazo katika masomo mbalimbali. Baadhi ya masomo
yaliyohusika ni Ushairi, Historia, Uhutubishaji (rhetoric) na falsafa.
Mmojawapo wa wanazuoni wa ubinadamu (humanistic) wa kipindi hiki ni Erasmus.
Erasmus alianzisha mafunzo ya lugha za Biblia kwa kuandika toleo la Kigiriki la
Agano Jipya. Pia ndugu Reuchlin alitafsiri sarufi ya kiebrania na misamiati (lexicon).
Uvumbuzi wa matini za kale na elimu iliyofuata vilisababisha wanazuoni kutupilia
mbali mbinu ya sitiari ya kufasiri Maandiko. Wanazuoni walianza kuweka mkazo
kwamba maandiko yana mlango mmoja tu wa fasili. Wafasili mashuhuri wa kipindi
cha matengenezo ya Kanisa ni Martn Luther na John Calvin
MARTIN LUTHER
Martin Luther alikuwa mwanatheologia na mwanamangenezo ya kanisa wa Ujerumani.
ushawishi wake ulikuwa mkubwa uliogusa Nyanja zote, kidini, kisiasa, kiuchumi na
kijamii. Luther anatambuliwa kama mtu mashuhuri katika historia ya Ulaya.
Hermeneutics ya Luther inaweza kueleweka kwa kuchunguza mtazamo wake kuhusu
Biblia. Mtazamo wake wa kwanza ni kwamba Biblia haipaswi chukukuliwa au
kutazamwa kama vitabu vingine. Imani na roho ya kuangaziwa ni muhimu kwa
msomaji.
Jambo la pili, Luther alidai kwamba kanisa halitakiwa kuipangia Biblia cha
kufundisha bali Biblia ndiyo inatakiwa kusema nini kanisa lifundishe.
Baada ya hapo Luther alipinga mbinu ya fasili ya sitiari.
Katika fasili Luther alidai kwamba katika kuelewa maana ya Andiko lazima kutokane
na uelewa wa uhalisi wa Maandiko ya Biblia. Aliendelea kusema kwamba msomaji ni
lazima azingatie hali ya kihistoria, sarufi na mkutadha wa aya anayokusudia kuifasili.
Luther alisema kwamba Biblia ni kitabu kilichowazi na kinachoelewa kwa urahisi
(Bible is clear book and simpe to understand).
12
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
Baada ya kuachana na mbinu ya sitiari Luther alikumbana na changamoto ya kupata
njia nyingine ya kulifanya Agano la Kale kueleweka kwa Wakristo wa wakati huo.
Maana mpaka kipindi hiki mbinu ya sitiari ilikuwa ni mbinu pekee iliyokuwa
inatumiwa katika kufasili Agano la Kale.
Ili kujaza pengo hilo Luther aliunda kanuni ya Kristolojia (Christological principle).
Kanuni hii baadae ilifanyika kanuni ya Hermeneutics ya Martin Luther.
Kanuni hii ilimsababishia Luther kumwona Yesu katika aya nyingi za Agano la Kale
hususani Zaburi.
Pia kanuni hii ilimwezesha kuonesha umoja wa Biblia bila kusababisha mkangayiko
wa fasili ya Maandiko ya Agano kale.
JOHN CALVIN
John Calvin alikuwa ni mwanatheologia, padre, humanist na mwanamatengenezo ya
kanisa wa kule ufaransa. John Calvin anatambuliwa kama mwanaeksijesia mkuu kama
Luther. Calvin aliiona mbinu ya sitiari kama chombo cha shetani cha kuficha maana
halisi ya Maandiko.
Calvin alianzisha msemo mashuhuri unaodai kwamba “Maandiko Hufasiri Maandiko
(Scripture enterprates Scriptue). Usemi huu unaashiria kwamba Calvin aliweka mkazo
katika kujifunza mkutadha, sarufi, maneno na usambamba wa aya badala ya kuleta
maana katika Maandiko.
Alidai kwamba kazi ya kwanza ya mfasili ni kumwacha mwandishi aseme
alichokusudia kukisema badala ya kuleta kile msomaji anachoona kwamba mwandishi
alitakiwa kukisema. John Calvin hakumwona Yesu katika kila aya ya Maandiko.
Kanuni za Hermeneutcs za John Calvin na Martin Luther ndio kanuni za sasa za
kufasili Maandiko za waprotestanti.
13
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
Pia katika kipindi hiki zilizuka falsafa na nadharia (empiricism) zilizodai kwamba
maarifa ya kweli yanaweza kupatikana kwa milango mitano ya fahamu pekee (five
senses).
Hivyo baadhi ya wananadharia walilitazama kanisa kama kitu kilichokuwa kinyume na
nadharia ya milango mitano ya fahamu. Hii ni kwa sababu kanisa lilijikita katika imani
na ufunuo. Hivyo basi waradhinishaji (rationalist) walianza kulishambulia kanisa na
Biblia kwa ujumla.
Mlengo huu ulizaa Theolojia ya Kiliberal ambayo ilianza katika kipindi cha
Harmeneutics ya kisasa (morden hernmeneutics).
14
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
kilichoitwa nuru ya ndani (inward light) na baadae walipelekea kila mtu kufasili
Maandiko kwa mtazamo wake mwenyewe. Wakati mwingine walipuuza Maandiko
na kushikilia hisia zao na mitazamo yao.
15
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
MADA YA TATU
KANUNI ZA KUFASIRI MAANDIKO
1.0. UTANGULIZI
Katika mada hii tutajadili baadhi ya kanuni za msingi za kufasiri Maandiko.Inatarajiwa
kuwa baada ya kuchunguza kanuni hizi kwa kina mwanafunzi atakuwa na uwezo wa
kufasiri Maandiko au Biblia kwa ufasaha na hivyo ataweza kuhubiri Neno la Mungu
kwa usahihi
sawasawa na Biblia inavyosema katika kitabu cha 2Timotheo 2:15
“Jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mtendakazi asiye na sababu ya
kutahayari. Ukitumia kwa halali neno la kweli"
1. KANUNI YA MKUTADHA
Kanuni ya msingi ya Maandiko ni kanuni ya mkutadha
Dhana ya mkutadha
Katika mawanda mapana neno Mkutadha uhusisha mazingira ya wakati Andiko hilo
lilipoandikwa. Hii uhusisha utamaduni na historia vikiunganishwa pamoja na
mkutadha wa matini yenyewe.
Wazo kuu katika kanuni hii ni kwamba kifungu cha Maandiko kinaweza kueleweka
kwa kuangalia vifungu vilivyokitangulia na vifungu vinavyofuata baada ya kifungu
hicho.
16
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
Kutokana na maelezo hayo tunaweza tengeneza kanuni ya mfuatano. Unapotaka
kupata maana ya Msitari chunguza mistari iliyotangulia na mistari inayofuata baada ya
mstari huo.
Mstari au kifungu kilichochukuliwa nje ya mkutadha wake daima kitaleta fasili isiyo
sahihi na kupelekea kuzaliwa kwa fundisho potofu na hatimaye imani potofu.
1. Mkutadha wa Andiko
Kuna aina kuu nne za mikutadha ya Andiko ambayo ni
i. Biblia nzima
ii. Agano Jipya au Agano la Kale
iii. Kitabu
iv. Aya
Kujibu maswali hayo kunakupa kuelewa mazingira yote kwa ujumla na hivyo
kuweza kufasili andiko kwa usahihi.
2. Mkutadha wa Kihistoria
Aina hii ya mkutadha inahusu uhusiano wa kifungu cha Andiko na historia halisi ya
mazingira kifungu hicho kilimoandikwa. Hapa unachunguza tarehe ya kuandikwa
kitabu na matukio yaliyotukia katika kipindi hicho katika Historia. Pia unachunguza
mwandishi wa kitabu na mazingira yake. Kufahamu hali halisi ya kihistoria ya wakati
huo inakupa kufahamu kwanini mwandishi alisema kile alichokisema na kwa namna
alivyosema.
Kweli kuu ya kanuni hii - ni kwamba Andiko haliwezi kumaanisha kile ambacho
hakikumaanishwa kwa wasomaji au wasikilizaji halisi wa mwanzo (japokuwa inaweza
tokea katika mazingira fulani hasa katika unabii 1Petro 1:10-12
3. Mkutadha wa Kiutamaduni
Kila kifungu fulani cha Maandiko kiliandikwa katika mazingira fulani ya
kiutamaduni. Katika kipindi cha uandishi wa Maandiko kulikuwa na kuhusika
kwa kiasi kikubwa na mambo ya kitamaduni ambapo yalitofautiana eneo na
eneo na kizazi na kizazi.
Mkutadha wa kiutamaduni uhusisha vitu anuai kama vile siasa, dini, uchumi,
sheria, ujenzi, kilimo, vyakula na mambo mengine mbalimbali ya kijamii.
18
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
4. Mkutadha wa kiuhalisia
Mkutadha wa kiuhalisia uhusisha mtindo wa uandishi wa kitabu au kifungu. Kuna aina
mbalimbali za mitindo ya uandishi iliyotumika katika Uandishi wa Biblia. Kila mtindo
wa uandishi una kanuni zake za ufasili. Hivyo ili uweze kufasili kwa usahihi kifungu
au Andiko ni muhimu ujue mtindo wa uandishi uliotumika.
Kutajwa kwa kitu mara ya kwanza katika Maandiko hubeba maana thabiti
itakayoendelezwa katika Biblia nzima.
19
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
Kwa mfano katika kitabu cha Mwanzao 3:7
Hii ndio maana ya majani ya mtini mahali popote yanapotajwa katika Biblia. Kwa
mfano kwa mara ya mwisho majani ya mtini yametajwa katika Mathayo 21:18-20, na
Marko 11:12-14, na Marko 13:28-29.
Katika Injili ya Mathayo na Marko tunakuta mtini wenye majani bila matunda. Yesu
aliulaani na ukayauka.
Ili kuweza kuelewa jambo hili tunapaswa kukumbuka kanuni ya mtajo wa kwanza na
kurudi katika kitabu cha Mwanzo 3.
20
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
Mbegu ambayo inaendelea kukua ndani yake katika mtajo mwendelezo katika
Maandiko.
Kanuni ya matajo wa kwanza inaweza kutumika katika maneno, dhana, mifano, watu,
mahali na dhamira.
Kanuni ya mtajo mwendelezo inatambua kwamba Mungu amefunua kweli yake kwa
mwanadamu kwa njia ya mwendelezo, amefunua kweli yake hatua kwa hatua.
Hii ina maana kwamba maudhui mengi ya Biblia huanza na mbegu, mbegu hupandwa,
humwagiliwa maji na kukua na kuwa mti mkubwa wenye matunda.
Mbegu ya kweli fulani iliyopandwa katika vitabu vya mwanzo vya Biblia hukua kwa
kadri inavyoendelea kutajwa katika Agano la Kale na Agano Jipya. Maudhui
yaliyoanza katika kitabu cha Mwanzo hukuzwa katika sehemu zingine za Biblia na
kuishia katika kitabu cha ufunuo.
Mfano
Uzao wa mwanamke akawa ni Kristo na Kanisa lake Wagalatia 3:16, 19, 29.
Kuumbwa kwa Mbingu na Nchi kunapelekea kuumbwa kwa Mbingu mpya na
Nchi mpya Ufunuo 21:1.
Mti wa uzima (Mwanzo 3) unatoa njia kwa mti wa uzima Ufunuo 22:2, 14.
21
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
Ili uweze kuwa na fasili sahihi ni lazima uwe na kila kitu ambacho Mungu amesema
kuhusu jambo hilo.
Unaposoma wazo fulani, tukio fulani au mtu fulani, soma kila Andiko katika Biblia
linalozungumzia jambo hilo au mtu huyo. Matokeo ya usomaji huu hutoa msingi mzuri
ambao kwa usahihi huakisi fundisho zima la Biblia (Bible doctrine).
Kama kifungu kimoja unachokisoma kinasema kwamba Mungu ni Moto ulao, basi
unaweza kuwa na mtazamo mmoja tu kuhusu Mungu. Waebrania 12:29.
Lakini ukisoma kwa undani utangundua kuwa Mungu wetu ni nuru, pendo, roho n.k.
22
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
Kuna watu ambao wanaweka mkazo katika mambo madogo na kuyapuuza mambo
makubwa. Mafarisayo walikuwa ni sehemu ya watu hawa.
Yesu alisema walichuja mbu na kumeza ngamia. Mathayo 23:24.
Mfano kuna mistari mingi sana katika Biblia inayohusu maombi. Na ndio maana
kanisa la kwanza liliyapa maombi kipaumbele.
Unaweza kushangaa kuona mtu anachukua sehemu ndogo tu ya mafundisho na kuipa
uzito mkubwa na kuifanya msingi katika ushirika na huduma.
23
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
Je! Mstari huu unaongezea nini katika kuelewa dhana hii?
Je! Ni kipengere gani katika dhana hii ambacho mstari huu unasisitiza?
Je! Mstari huu unarekebisha mtazamo wangu wa jumla kuhusu somo
hili?
Thomas Watson aliwahi kuandika kwamba. Hakuna kitu kinachoweza kukata almasi
isipokuwa almasi yenyewe. Hakuna kinachoweza kufasili Maandiko isipokuwa
Maandiko yenyewe.
24
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
Williamu Curnall aliwahamasisha waamini kulinganisha Andiko na Maandiko.
Alisema kwamba Mafundisho potofu huwa kama mashahidi wawili wa uongo daima,
mashahidi wa uongo huwa hawakubaliani wenyewe kwa wenyewe. Maana hutoa
taarifa zinazokanganya.
Uzuri wa kutumia kanuni hii ni kwamba Biblia hujibu maswali yake yenyewe.
Jambo la kuzingatia katika kanuni ya mtajo mlinganisho ni kwamba tunafasili kifungu
kisichowazi kwa kutumia kifungu kilichowazi. (tunafasili kifungu kinachoeleweka kwa
kutumia kifungu kisichoeleweka).
Katika maeneno matatu (3) tunaona wale waliojazwa Roho Mtakatifu walinena kwa
lugha.
1. Mwanzo wa ujazo wa Roho Mtakatifu Mdo 2:4
“Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine kama Roho
alivyowajalia kutamka”.
2. Kumwagwa kwa Roho Mtakatifu katika nyumba ya Kornelio Mdo 10:46
“Kwa maana waliwasikia wakisema kwa lugha na kumwadhimisha Mungu”.
25
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
3. Kujazwa kwa Roho Mtakatifu wanaume kule Efeso Mdo 19:6
“Na Paulo, alipokwisha kuweka mikono yake juu yao, Roho Mtakatifu akaja juu yao;
wakaanza kunena kwa lugha, na kutabiri”.
Katika tukio la nne haioneshi kwa uwazi ni ishara gani iliyotokea, japokuwa kwa
hakika kuna kitu cha tofauti kilitokea. Katika tukio hili ni Wasamaria waliojazwa Roho
Mtakatifu. Mdo 8:14-21.
“Hata Simoni alipoona watu wanapewa Roho Mtakatifu kwa kuwekewa mikono ya
mitume, akataka kuwapa fedha akisema, Mdo 8:18.
Katika tukio hili, kunena kwa lugha hakutajwi kwa wazi, japokuwa mtu anaweza
kushangaa ni nini Simoni alichokiona? Kwa hakika kuna kitu cha tofauti ambacho
Simoni mchawi alikiona na kikamvutia hadi kutaka kutoa hongo kwa Petro.
Je kweli kwamba mtume Paulo anathibitisha kwamba watu walio hai wanaweza
kuwasaidia wafu kwa kubatizwa kwa niaba yao mahali pao?
Jambo hili haliwezi si la kuumiza kichwa kwa sababu kuna shahidi mmoja au mstari
mmoja tu katika Biblia unaozungumzia fundisho hili.
26
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
Je! Mashahidi wenigne wa pili na watatu wako wapi? Kunapoibuka jambo kama hili
katika Biblia lenye utata mashahidi watatu ni:-
1. Agizo la Yesu katika Injili
2. Matumizi (practice) yake katika kanisa la kwanza katika kitabu cha Matendo ya
Mitume
3. Ufahamu wa kitheolojia kama ulivyowekwa wazi katika nyaraka mbalimbali za
mitume
Kama tukitumia kanuni hii katika ubatizo na ushirika mtakatifu ni rahisi kutambua
mashahidi wawili au watatu. Kwa hakika tukitumia kanuni hii katika ibada ya
kuosha/kutawaza miguu na ubatizo kwa ajili ya wafu tutakosa mashahidi
wawili/watatu.
Fasili ya Andiko hili haiwezi kuumiza kichwa kwa sababu inaelekea kupingana na
Biblia nzima.
Biblia inafundisha kwamba kifo ni mwisho Webrania 9:27
“Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa ni hukumu”
Biblia inafundisha kwamba hakuna nafasi nyingine ya kutengeneza baada ya
kufa
Luka 16:19-31, Ezekieli 18:19-32.
Biblia inafundisha kwamba hatima yetu ya milele inategemea nini tunafanya
wakati tukiwa hai 1Wakorintho 3:10-15.
Katika Korintho kulikuwa na tatizo la wamini katika kuyaacha mafundisho ya dini zao.
Pamoja na kuokoka bado walishikilia mfundisho ya dini zao za kipagani. Waliingia
kanisani pamoja na mafundisho yao.
6. KANUNI YA UCHAGUZI
Hii inahusish uchaguzi wa Mungu juu ya mtu fulani au taifa fulani kwa kusudi lake.
Aina za uchaguzi
1. Uchaguzi wa muda au kipindi fulan. Mungu huchagua mtu fulani, kundi fulani
au taifa fulani kutimiza kusudi lake mahususi katika kipindi fulani
2. Uchaguzi wa kila mmoja wetu, akiwa na utashi (making free will) na uwezo
wa kufanya uchaguzi utakaoamua hatima yake ya milele
Uchaguzi na ukombozi
1. Uchaguzi ni tendo huru la Mungu. Mungu hakutakiwa kumuokoa yeyote kwa
sababu sisi sote tulikuwa tumepoteza nafasi yetu ya kukubalika mbele za Mungu
2. Kile Mungu anafanya kwetu ni kwa sababu ya neema yake iliyo kuu Rumi (:11,
11:5-6. Kwa hakika hatukustahili kabisa. Ni Mungu ambaye ameamua kutuokoa
kutokana na upendo na neema yake.
3. Uchaguzi (predestination) umejikita katika maarifa (foreknowledge) ya Mungu
juu ya mambo yajayo. 1Petro 1:1-2 Mungu anachagua wale ambao aliwajua tangu
zamani kuwa watamkubali Kristo.
ANGALIZO:-
28
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
Hakuna kifungu chochote katika Biblia kinachosema kwamba Mungu
alimchagua mtu fulani kwaajili ya kwenda Jehanam
MUHIMU
Unapochunguza kifungu fulani cha Maandiko
1. Unapaswa kujiuliza swali ikiwa kuna mstari katika kifungu hicho ambao
una muunganiko (connection) na kusudi la Mungu la uchaguzi. Kanuni hii
si lazima ifanye kazi kwa kila mstari na kila kifungu na inafanya kazi kwa
kifungu kile kinachoelezea kweli kuhusu kanuni ya uchaguzi inapokuwa
imehusika.
2. Kanuni ya uchaguzi inakwenda sambamba na kanuni ya Agano. kwa hiyo
kanuni hizi mbili ni lazima zizingatiwe kwa pamoja katika matumizi.
Maandiko
Malaki 1:2-3 “.... Je Esau si ndugu yake Yakobo ? Ila nimempenda Yakobo bali
memchukua Esau
Mwanzo 25:19-34 Hata kabla ya kuzaliwa kwao (Esau na Yakobo) Bwana
alimwambia Rebeka akisema” mataifa mawili yako katika tumbo lake na
kabila mbili za watu na watu hao watafarakana tangu tumboni. Kabila moja
litakuwa hodali kuliko la pili, na mkubwa atamtumikia mdogo.
Warumi 9:6-24
11 Kwa maana kabla hawajazaliwa wale watoto, wala hawajatenda neno jema
wala baya, ili lisimame kusudi la Mungu la kuchagua, si kwa sababu ya
matendo bali kwa sababu ya nia yake aitae.
29
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
13 Kama ilivyoandikwa nimempenda Yakobo bali Esau nimemchukia.
HITIMISHO
7. KANUNI YA AGANO
Dhana ya Agano:-
Aina hiii ya Agano hutumia maneno kama “ Ikiwa, Kama, iwapo na nita, ndipo
n.k
30
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
Sehemu Kuu Mbili katika Maagano Mungu aliyofanya na mwanadamu:-
Unaposoma kifungu cha habari katika Biblia ni muhimu kutambua muundo wa agano
wa Biblia. Unapaswa kutambua agano ambalo lilikuwa likifanya kazi katika kipindi
hicho andiko hilo lilipoandikwa au kutolewa. unahitaji kujua namna agano hilo
31
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
lilivyoathiri maisha ya watu wakati huo. unatakiwa kujua namna agano hilo
lilivyohusiana na maagano mengine . Huu ndio ufungua wa kufungua habari nyingi.
Mambo ya kuzingatia
iii. Kubaini kategoria ya agano yaani kutambua kama agano nila masharti au si
la masharti.
iv. Kutambua kama agano hilo limetimizwa katika Agano Jipya. Mfano ahadi
ya Agano la Daudi imetimizwa na Yesu Kristo na katika Kanisa katika
Agano Jipya. 2Samweli 7:14-17, Isaya 9:7, Yeremia 33: 17, Luka 1:32.
v. Kufasiri Agano kwa mtazamo wa msalaba wa Yesu na Agano Jipya.
Maagano yote yana kipengere cha alama (symbol) karibu vipengere vya
kila agano yanaonesha au kuelekeza utimizo wake katika agano jipya.
Mfano , damu ya Agano kwa hakika inaelekeza kwa Yesu Kristo na damu
yake aliyoimwaga pale kalvari.
Ili uweze kutoa fasili sahihi ya mistari hii ni lazima urejelee kwenye agano la Edeni.
Hii ni kwa sababu chini ya Agano hili mti wa uzima umetajwa kwa mara ya kwanza.
Adamu na Hawa walipoteza haki ya kula matunda ya mti wa uzima
waliposhindwa kutii masharti ya agano la Edeni walipokula matunda ya mti wa ujuzi
wa mema na mabaya ambao walikatazwa wasile. Hivyo hawakushinda kwa sababu
hawakutekeleza amri yake na wakapoteza haki ya mti wa uzima. (mwanzo 2:8-17,
3:22-24.
32
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
Mpango wa Mungu utakapokuwa umetimia kikamilifu ushindi utakujua tena juu ya
kile kilichopotea
Agano la Adamu
Warumi 12:20
ili kuweze kutambua matmizi kamili ya mstari huu ni lazima msitari uchunguzwe kwa
nuru ya Agano la Adamu. Baada ya kuingia kwa dhambi katika maisha ya
mwanadamu, Mungu alimwambia nyoka (shetani) Nitaweka uadui kati yako na
huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake, huo utakuponda kichwa na
wewe utauponda kisigino. (mwanzo 3:15).
Agano la Nuhu
Ufunuo 4:3
Mstari huu unapaswa kufasiliwa kwa kuhusishwa na agano la Nuhu. Upinde wa mvua
wa kwanza uliwekwa mawinguni kuwa ukumbusho kwa Mungu na mwanadamu kuwa
Mungu hangeangamiza dunia tena kwa maji. (mwanzo9:17)
Upinde wa mvua katika kiti cha enzi unaonesha kwamba Mungu anatunza mhuri wa
Agano la Nuhu daima mbele zake akithibitisha uaminifu wake kwa ahadi yake.
Agano la Ibrahimu
W agalatia 3:29
Haiwezekani kufasili mstahi huu kwa usahihi pasipo kutazama vitu vinavyohusika
katika Agano la Ibrahimu. kama ilivyoelezwa hapo awali. Ibrahimu alitakiwa kuwa
baba wa vizazi viwili ambavyo ni uzao wa kiroho na uzao wa kimwili ( Mwanzo
13:16, 15:5). Uzao wa kimwili ulihusika na urithi wa nchi, watoto, na milki.(mwanzo
12:1-3, 22:16-18)
33
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
Ahadi ya kiroho (uzao wa kiroho) ilihusika na masihi na huduma yake kwa mataifa
yote ya dunia. Ahadi hii inahusisha kuhesabiwa haki kwa imani na kumpokea Roho
Mtakatifu. (wagalatia 3:8). Hivyo basi mstari huu unaeleza kwamba mtu ambaye ni
mali ya Yesu amekuwa uzao wa Ibrahimu na anamahusiano ya kimaagano na
Mungu. akiwa mrithi wa ahadi ya Agano la Ibrahimu kupitia Yesu Kristo.
Agano la Musa
Wakolosai 2:16-17
Agano la Daudi
Luka 1: 32-33.
Uzao (Seed)
Nyumba (House)
Kiti cha enzi (Throne)
Kingdom ( Ufalme)
Mistari ya Injili ya Luka iliyotajwa hapo juu ilitabiri kwamba vitu hivi vinne
vingepata utimizo wake katika Bwana wetu Yesu Kristo mwana wa Daudi au wa uzao
wa Daudi.
Agano Jipya
Yeremia 31;31-33
A. Wakorintho 10:5-11
Si kila kitu kilichotokea katika kipindi cha agano la kale kimeandikwa kwaajili
yetu katika Biblia. Kwa hakika hakuna historia nzima ya mtu yeyote katika
Biblia. Mungu aliamua kuandika matukio ambayo aliamua yeye kulingana na
kusudi lake takatifu. Lengo lake ni kutusaidia sisi kuingia katika mpango wake
kamilifu kwaajili ya maisha yetu na kututayarisha kuwa tayari wakati Bwana
Yesu atakaporudi.
B. Yohana 21:24-25
Si kila kitu alichokifanya Yesu Kristo akiwa hapa duniani kimeandikwa katika Biblia
yaani katika Agano Jipya. Yale ambayo yameandikwa yametolewa kwetu kwa lengo
la kutufunza sisi njia ya wokovu. Tukitazama matukio mbalimbali ya maisha ya Yesu
yaliyoandikwa katika Biblia tunaweza kupata kanuni ya kweli isiyobadilika
kulingana na wakati kupita. (Timeless Principle).
C. Warumi 15:4
Kwa kuwa yote yaliyotangulia kuandikwa, yaliandikwa ili kutufundisha sisi;
ili kwa saburi na faraja ya Maandiko tupate kuwa na tumaini.
D. 2Timeotheo 3:14-17
Biblia imetolewa kwetu ili kutufanya tuwe na hekima, kukuza imani,
kutufundisha sisi namna ya kuishi na kutuandaa kwaajili ya maisha na
huduma. tunapokea haya kutoka katika Neno tunapochunguza kweli
isiyobadilika kulingana na wakati kupita ambayo inapatikana katika matukio
mbalimbali yaliyoandikwa katika Biblia.
35
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
II. Nini kweli ya Kimaadili au Kanuni ya Kimaadili.
Kamusi zinafasili neno hili “maadili kwa namna mbalimbali kama ifuatavyo
Kamusi inaelezea neno Moralize kama kupata maadili kutoka katika kitu
fulani. au kufanya maadili kuakisi kuhusu kitu fulani au kuelejea jambo
fulani kwa mtazamo wa kimaadili.
Tunahitaji kutumia kanuni hii katika kufasili Maandiko kwa sababu si kila
kweli isiyobadilika kutokana na wakati kupita imeelezwa kwa uwazi katika
Biblia Mithali 25:2
Je twaweza kujifunza kitu fulani kutoka kwa waamuzi mbalimbali katika Biblia
? au kwa wafalme mbalimbali waliotawala katika Israeli na Yuda ?
36
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
vipi kuhusu mafunzo tunayoyapata kutoka katika maisha ya Ayubu, kitabu
cha Ruthu, na Esta ? Tunaweza kujifunza nini kutokana na kifo cha Sauli
mfalme wa kwanza wa taifa la Israeli? 1Mambo ya Nyakati 10:13-14
Basi Sauli alikufa kwa sababu ya kosa lake alilomkosa Bwana, kwa sababu ya
neno la Bwana asilolishika. Na tena kwa kutaka ushauri kwa mwenye pepo wa
utambuzi, aulize kwake, asiulize kwa Bwana, kwa hiyo akamuua, na ufalme
akamgeuzia Daudi mwana wa Yese.
37
By Rev. Dr. Erick L. Mponzi (Dip. Min, BEDCP, B.Th, M.Min, ThD)
Njia mojawapo za kumsadia mfasili ili kuweza kuelewa kanuni ya kimaadili
ya fasili ni kutumia kiambatisho cha orodha ya sifa za wahusika katika
mada hii. Unapokuwa unasoma kifungu unawza kujiuliza maswali. Je!
kifungu hiki kinatufundisha kitu chochote kuhusina na tahadhari , umakini
au upatikanaji n.k ?
38