Professional Documents
Culture Documents
WA
KARISMATIKI KATOLIKI
TANZANIA
Imeandaliwa na:
TUME YA TEOLOJIA
BARAZA LA MAASKOFU KATOLIKI TANZANIA (TEC)
20 Januari, 2016
1
YALIYOMO
UTANGULIZI
DIBAJI
SURA YA KWANZA
1.0.MAANA YA KARISMATIKI KATOLIKI
1.1.Asili ya neno Karismatiki
1.2. Karismatiki Katoliki ni nini?
1.3. Upyaisho wa Roho Mtakatifu
SURA YA PILI
2.0.HISTORIA YA KARISMATIKI KATOLIKI
2.1. Machimbuko ya Karismatiki Katoliki
2.2. Mchakato Papa Leo XIII
2.3. Mchakato Papa Yohane XXIII
2.4. Mchakato Papa Yohane Paulo VI
2.5. Mchakato Papa Yohane II
2.6. Karismatiki Katoliki Tanzania
SURA YA TATU
3.0.MALENGO YA KARISMATIKI KATOLIKI.
3.1.Tamko Maalumu la kuidhinisha Karismatiki Katoliki
3.2.Wongofu
3.3. Utakaso
3.4.Uadilifu
3.5. Uinjilishaji
3.6.Uchangamanisho
3.7.Uamushaji wa Imani
SURA YA NNE
4.0. MUONEKANO WA KARISMATIKI KATOLIKI
4.1. Kikundi cha Sala
4.2. Malengo ya Kikundi cha Sala
4.3. Aina ya Vikundi vya Sala
4.4. Mkutano wa Sala
4.5. Umuhimu wa Kikundi cha Sala
2
SURA YA TANO
5.0. MAKUZI YA KIROHO
5.1.Sala
5.2.Kujifunza Biblia
5.3. Ushirika (fellowship) (Mdo 2:42-47; 4:32-35)
5.4. Masakramenti
5.5.Matendo ya huruma
5.6. Wajibu wa mkarismatiki katoliki
5.7. Karama za Roho Mtakatifu
5.8.Huduma za Uponyaji
5.9.Huduma ya kuwekwa huru kutoka nguvu za giza
5.10. Baadhi ya Karama za Roho Mtakatifu
SURA YA SITA
6.0. KARISMATIKI LAZIMA MMUHESHIMU BIKIRA MARIA (KKK829)
6.1. Heshima ya majitoleo kwa Bikira Maria
6.2. Kielelezo na Tunu
6.3. Bikira Maria mnyenyekevu
6.4. Bikira Maria Nyota ya Uinjilishaji
6.5. Bikira Maria Mwezeshaji wa Miujiza
6.6. Bikira Maria Mama na MWOMBEZI WETU
6.7. Njia ya kumwendea Bikira Maria
SURA YA SABA
7.0. NAFASI YA MAASKOFU NA MAPADRE
7.1. Uongozi wa Maaskofu
7.2. Huduma ya PADRE KWA Wakarismatiki
7.3. Wajibu wa Padre
SURA YA NANE
8.0. MUUNDO WA UONGOZI
8.1. Kamati Tendaji ya Kikundi Cha Sala
8.2. Kamati Tendaji ya Parokia
8.3. Kamati Tendaji ya Jimbo (KTJ)
8.4. Kamati tendaji ya Taifa ya (KTT)
8.5. Kamati Tendaji ya Taifa ya Huduma (KTH)
8.6. Kamati Tendaji ya Huduma ya Taifa (KHT)
8.7. Askofu Mlezi wa Kitume (AMK)
3
SURA YA TISA
9.0. UCHAGUZI NA MIHULA YA UONGOZI
9.1. Utaratibu wa Uchaguzi
9.2. Sifa za viongozi wa Karismatiki Katoliki
SURA YA KUMI
10.0FAIDA ZA KARISMATIKI KATOLIKI
HITIMISHO
BIBLIOGRAFIA
4
UTANGULIZI
Kwa kipindi kirefu waamini wengi wamesikia, wameshuhudi au wameshiriki katika utume na
huduma za Karismatiki Katoliki. Karismatiki Katoliki ni mkondo unaokua kwa kasi katika kanisa
Katoliki. Hapa kwetu Tanzania waamini wengi wamejiunga na vikundi vya Karismatiki au
wamevutiwa kuijiunga navyo kwa sababu ya mabadiliko wanayoyaona katika maisha yao ya
kiroho yaletwayo na mkondo huu. Kwa upande mwingine, kuna mapungufu na changamoto
kadha wa kadha zinazopelekea mkondo huu kutoeleweka vizuri. Wakati mwingine hujifananisha
na makanisa ya kipendekoste, Kilokole au kisabato na kuweka ukatoliki kando. Hivyo, Maaskofu
wameona ni vyema kutoa mwongozo wa Karismatiki Katoliki Tanzania, ili Majimbo yote
Katoliki yawe na kauli moja ya kuelewa, kuupokea na kuusindikiza mkondo huu.
Karismatiki Katoliki ikiendeshwa katika misingi yake, itakuwa chachu ya uinjilisha ji mpya. Kwa
kifupi Karismatiki Katoliki ni chachu nzuri ya imani na Uamsho mwema wa Mungu na jirani.
Maana kama, Baba Mtakatifi Paulo wa VII alivyowahi kusema mwaka 1975, akizungumzia
Karismatiki Katoliki kwamba, kwa njia ya Roho Mtakatifu Kanisa linakuwa na maajabu ya
Pentekoste ya kudumu.Mmiminiko wa karama za Roho Mtakatifu katika mkondo wa Karismatiki
Katoliki, hufanya Kanisa liwe na ujana wake wote.
Mwongozo huu uwe dira yetu katika kuimarisha imani yetu Katoliki na kustawisha Karismatiki
Katoliki nchini Tanzania. Daima ikumbukwe kwamba Krismatiki siyo mkondo nje ya Kanisa
Katoliki, bali ni Kanisa lenyewe likiwa katika muundo wake wa upyaisho. Hivyo, imani Katoliki
isipindishwe wala kubezwa katika huduma za Kikarismatiki Katoliki.
Nawatakieni nyote muusome kwa makini Mwongozo huu. Pia kila mlezi wa mkondo huu, na kila
Mwanakarismatiki anashauriwa kuusoma kwa kina ili kudumu katika njia salama ya imani
tukiongozwa na tahadhali hii tunayopewa na Mt.Yohane: wapenzi wangu msimsadiki kila mtu
asemaye kwamba ana Roho wa Mungu, bali chunguzeni kwa makini kama huyo mtu anaongozwa
na Roho wa Munguau la, maana manabii wengi wa uongo wamezuka ulimwenguni (1Yoh 4:1).
Napenda niwashukuru Makatibu wangu wa Tume ya Teolojia, Padre Novatus Mrighwa na Padre
Victor Tumaini, kwa kudodosa na kutafiti mkondo wa Karismatiki Katoliki. Ninawashuru Bw.
Eslastus Mtema na Bw. Sebastian Chisunga kwa uzoefu wao wa mkondo wa Karismatiki Katoliki
Tanzania, kwa sadaka zao, kwa ushauri wao na ukaribu wao katika kuaandaa Mwongozo huu. Pia
ninawashururu Pdre Almachius Rwejuna na Sr. Juliana Mathias, STh kwa kuhariri na kuchapa
kazi hii.
5
“Mungu wa matumaini atujaze furahana amani yote katika imani yote, tupate kujaa matumaini
kwa nguvu ya Roho Mtakatifu” (Rum 15:13).
Na ichapwe.
6
DIBAJI
Mkondo na mwamko wa Karismatiki Katoliki unakuwa kwa kasi kubwa ndani ya kanisa Katoliki.
Leo hii waamini wengi wanajihusisha na vikundi vya kikarismatiki na kuonja mabadiliko makubwa katika
maisha yao ya kiroho na kimwili.kwa upande wa pili yamejitokeza mapungufu na changamoto
mbalimbali, kuhusiana nauelewa pamoja na utendaji wa mkondo huu wa karismatiki.Baraza la Maaskofu
Katoliki Tanzania wameliona hili na kuiomba tume ya teolojia kuifanyia utafiti wakina, na kutoa
mwongozo,mintarafu Karismatiki Katoliki Tanzania.lengo kuu la kazi hii ni kuelimisha juu yaufahamu wa
maana,historia, faida,vikundi vya sala, vikundi vya sala changamoto na namna ya Kuboresha utendaji wa
mkondo huu kwa nia ya kudumisha imani, mapendo na matumaini, umoja naamani tukiongozwa na
mafundisho sahihi ya imani katoliki.
Karismatiki katiloliki ni mkondo na mwamko mmoja wapo katika kanisa katoliki ambao unakazia suala la
uwazi zaidi kwa uwapo wa Roho Mtakatifu, nguvu nakarama zake, mabadiliko ya kiroho ya mtu binafsi
nakanisa kwa jumla(mdo 1:8; yoh 15:26-27)mkondo huu uko ndani ya kanisa kwa ajili ya kanisa na
mali ya kanisa.
7
SURA YA KWANZA
8
SURA YA PILI
9
Mkutano wa kwanza wa viongozi wa mkondo huu wa Karismatiki uliitishwa mwaka 1973. Baba
Mtakatifu alitazama Karismatiki kama jumuijya ya watu wanaovutwa kuwa na sala za kina na tafakari,
wanakazia sala na masifu, wana ukarimu mkubwa wa kutoa huduma, na wana upendo mkubwa kwa
Maandiko Matakatifu na kwa jirani. Kutokana na yote hayo, Baba Mtakatifu alikiri kuwa kuna dhihirisho
kubwa la uwapo wa Roho Mtakatifu. Wakati wa uzinduzi wa Sinodi kule Roma mwaka uliofuata 1974,
Papa Paulo wa sita alizungumzia hadharani juu ya miminiko la karama za Roho mtakatifu,katika mkondo
wa karismatiki katoliki amabazo zinalifanya kanisa liwe na hali ya ujana. Kwamba kwa njia ya Roho
Mtakatifu kanisa linakuwa namaajabu ya pentekoste ya kudumu. Kufika mwaka 1975, Karismatiki
Katoliki ilikuwa imeenea kwa kasi kubwa kubwa duniani. Mwaka huohuo katika mkutano wa pili
waviongozi wakarismatiki katoliki, Papa Paulo wa VI alikazia kuwa Karismatiki Katoliki sio mkondo nje
ya kanisa lenyewe, balia ni kanisa lenyewe likiwa katika mkondo wake wa upyaisho.
2.5. Mchakato: papa Yohane Paulo wa II
Kwa upande wake Baba Mtakatifu Yohane Paulo wa II aliendeleza masimamo wa mtangulizi wake
mintarafu Karismatiki Katoliki. Alitoa mahimizo mbalimbali kwa nyakati tofauti, kabla ya Baraza la
kipapa la walei kutoka tamko rasmi la Kutambua utumishi wa kuratibisha Karismatiki Katoliki
ulimwenguni tarehe 14 septemba 1993, pamoja na tamko na tamko hilo , Baraza la kipapa pia lilipitisha
mwongozo/kanuni (statutes) (regthen Peter stood up publish year……….uk) za Kutambua Karismatiki
Katoliki pamoja na huduma ya chombo cha kulea mkondo hu. Mwongozo huu umeifanya Karismatiki
Katoliki kuwa na msingi imara, na kutambuliwa na kanisa lote, pamoja nakwamba baadhi ya makanisa
mahalia yameshindwa kuelewa na kuushi; hivyo kuwa chanzo cha migogoro na sitofahamu kaika kanisa.
Aidha, hati hii ilifanyiwa marekebisho mwaka 2004iliidhinishwa na mhashamu Askofu Stanslaw Rylko
RAIS WA Baraza la kipapa la walei na Joseph Cremence (katibu wa Baraza) kwa tamko lenye
kumbukumbu na. 863/05/Aic/73 La Tarehe 9 Mei 2005 Vatcano
Tamko hili la kuidhinisha Karismatiki Katoliki ulimwenguni pote na kanuni/ statutes za chombo hiki
zabainisha wazi kuwa Malengo ya Karismatiki Katoliki ni yale yale ya kanisa lenyewe yaani:
3.2. Uongofu
Kustawisha mahusiano binafsi ya kina, makomavu na uendelevu baina ya mtu naYesu Kristo Bwana na
mwokozi. Kuwasaidia wakatoliki kuonja ubatizo katika Roho Mtakatifu. Yaani, kuonja kwa namna ya
binafsi upendo wa Mungu kwa kupokea wokovu unaopitia kwa njia ya mwane wa pekee Yesu Kristo aliye
peke yake Bwana na mwokozi wetu.
3.3. Utakaso
Kukuza na kustawisha upokeaji binafsi wa nafsi, uwapo na nguvu ya Roho Mtakatifu katika namna
inayobadilisha maisha. Neema hizo hupati kung’amuliwa kwa pamoja katika kile kinachoitwa sehemu
mbambali za Dunia, ubatizo katika roho mtakatifu, ujazo au upyaisho wa roho mtakatifu tukio hili
lieleweke kama kupokea binafsi zile neema tupazo katika sakramenti za kumwingiza mtu ktika Ukristo
yaani ubatizo, kipaimara, sakaramenti za kupokea nguvu katika huduma kwa ajili. Kuwasaidia wakatoliki
kuwa wazi, kupokea na kutumia karama za roho mtakatifu. Karama hizi zilisha pokelewa kwa njia ya
ubatizo na kipaimara, na kuwa kama zimelala. Ubatizo katika roho mtakatifu huziamsha na kumwezesha
muhusika kuwa hai katika kuzitumia.
3.4. Uadilifu
Kukuza na kustawisha matumizi ya karama za Roho Mtakatifu (carismata) siyo tu ndani ya karismatiki
katoliki bali pia ndani kanisa lote kwa ujumla. Karama hizi mbambali huonekana kwa wingi miongoni
mwa walei watawa na wakleri. Mkondo huu huamsha ari ya sala za kumshukuru, kusifu na kuabudu na
kujikabidhi kwa maongozi yake Mungu. Karama hizi zikieleweka na kutumika vizuri bila mgongano na
mambo mengine katika maisha ya kanisa, ni chimbuko la nguvu kwa wakristo katika safari yao ya
kuelekea utakatifu na kwa utekelezaji wa utume wao.
3.5. Uinjilishaji
Kukuza kazi ya uinjilishaji kwa nguvu ya roho mtakatifu, kuwainjilisha upya wakristo waliorudi nyuma,
kuwaiimarisha na kuwatia bidii wakristo wakristo wanaendelea na imani, kuwainjilisha walio nje na
kanisa na kuinjilisha tamaduni na mihimili ya miundo ya kijamii. Upyaisho huu hasa unakuza na
kuchochoe ushiriki wa utume wa kanisa kwa kutangaza injili kwa maneno na matendo, kwa kumshuhudia
11
yesu kristo kwa ushuhuda binafsi kwa njia ya kazi za imani na za haki, kama kila mmoja wetu alivyoitwa.
Karismatiki Katoliki inakazia uinjilishaji mpya uliojawa naujasili mpya mbinu mpya na namana mpya
zinazoambatana na mijiza ya kulithibitisha neno linalohubiriwa.
3.6. Uchangamanisho
Kustawisha ukuaji endelevu wa utakatifu kwa njia ya muunganiko sahihi wa msisitizo hii ya kikarismatiki
na maisha kamili ya Kanisa. Hili linatizwa kwa kushirika maisha kamili ya kisakramenti na kiliturujia na
katika kuenzi utajiri wa mapokeo ya kanisa katoliki katika sala maisha ya kiroho na malezi endelevu
katika mafundisho ya imani katoliki kwa kuongozwa na mamalaka ifundishayo ya kanisa (church
magsterium) na kwa kushiriki katika mpango wa kichungaji wa kanisa.
12
SURA YA NNE
Mara nyingi mkondo huu huonekana katika sura ya kikundi cha sala. Kikundi cha sala cha kikarismatiki ni
ushirika huria wa wakatoliki unawapa fursa ya kushirikiana mtindo wa maisha na sala za kikarismatiki.
Mtu anahesabiwa kuwa mkarismatiki baada ya kushiriki semina ya maisha ya kiroho (SMK) kwa
takribani miezi mitatu.
4.1.1 Neema tupatazo kwa ubatizo katika roho mtakatifu (Yohane 1:33,Mdo 1:5, au ujazo wa roho
mtakatifu (Mdo 2:17, 33; 10:45 hutumika kwa Kusaidiana katika kushirikiana na wengine. Kila
atakaye kuishi maisha haya mapya hana budi kujiunga na kikundi cha sala na watu wengine
wanaoishi maisha haya.
4.1.2 Katika karismatiki, Mkutano wa sala hufanyika mara moja au mara mbili kadiri ya uhitaji mahalia
kwa wiki; kwa wale wanaojitahidi kuishi maisha ya kikristo, maadilifu nja ya kina katika
ulimwengu wa le. Kusudi la Awali na msingi katika mkutano huo wa sala, ni kumsifu na kumwadu
mungu katika “roho na kweli” (Yoh 4:24;Efeso 5:18…), kwa shangwe na furaha kwa nyimbo
(zaburi 95:1) karama ya kunena kwa lugha (rum 8:26), sala, kupiga makofi (Zab 47:1), kucheza (2
Sam 6:14), kuinua mikono (Zab 63:4; 134:2) na kutumia kila aina ya vyombo vya mziki (Zab
98:5-6; 150:3-5)
4.1.3 Vipindi vya ukimya na tafakari (kwa ibada) ni lazima viwepo ( Zab 46:10;Papa Benedicti XVI:
neno la Bwana, Verbum domini 66).
1)Kufanya upya na kustawisha maisha ya Kikristo kadri ya Injili, kama ilivyokuwa katika kanisa la
mwanzo
5) Kufanya uinjilishaji katika parokia, wiki za neema, uinjilishaji kwenye jumuiya, uinjilisha nyumba
kwa nyumba, makaongamano n.k.
13
4.3.1 Mkutano wa sala
Tukio kubwa katika uhai wa karismatiki katoliki ni mkutano wa kikundi cha sala. Nijumuiiko la
wakatoliki wakishiriki sala ya vikundi vya mtindo wa kikarismatiki. Mkutano wa sala wa kikarismatiki
hujumuisha;
1.Kumsifu na Kumwabudu Mungu kwa shangwe na furaha (Zab 149:3, 47:1, 66:1-4)
4. Kuchochoa na kutumia karama za roho mtakatifu kama vile kunena kwa lugha unabii, uponyaji n.k.
(1Wak 12 na 14).
Mkutano wa sala huishia na muda wamaombi/ maombezi na kuwawekea mikono kwa kuwahudumia
walio a shida mabalimbali. Katika kutekeleza hayo yote ni mhimu kuangalia kuwa uendesha ji wa kikundi
cha sala usikinzane wala utendaji wa roho mtakatifu usingiliwe (1Tim 5:19). Mwisho wa yote mambo
hayo lazima yafanywe kwa utaratifu unaofaa (1Wak 14:26-33, 40)
4.4.1. Kila mkarismatiki shariti awe mshika wa kikundi cha sala ambako atalelewa na kuwajibika.
4.4.2. Kila mhudumu lazima awe na mahudhurio mazuri kwenye kikundi chake sala. Yeyote asiyekuwa na
mahudhurio mazuri apaswi kuhudumu popote
4.4.3 Kila mhudumu atakapo Jimbo moja kwenda Jimbo lingine atapaswa kuwa na barua ya askofu wake
wa Jimbo lake, baada ya mhudumu huyo kupata uthibitisho kutoka kwa mratibu wa Jimbo atokako.
4.4.4. Kila muhudumu afikapo katika Jimbo alikotumwa, anapaswa kujitambulisha au kutambulishwa kwa
Askofu mahalia kabla ya kuanza huduma.
4.4.5.Ieleweke kuwa kikundi cha sala ndio msingi na utimilifu wa utume wa kikarismatiki
katoliki.uongozi uliopo katika ngazi zote(vigango ,parokia ,jimbo,taifa,kimataifa)upo kwa ajili ya
kikundi cha sala.
4.4.6. Kutakuwapo pia jumuiya agano za kiinjili za kikarismatiki (yaani jamii ya wakarismatiki wanaoishi
pamoja kijumuiya kama vile agape center nk.)kadiri ya karismatiki katoliki jumuiya hizi
zitawajibika kwa uongozi wa Karismatiki jimbo chini ya askofu mahalia.ni muhimu hapa
ieleweke kuwa viongozi wa jumuiya za agano za kiinjili za kikarismatiki,wana haki ya
kuchaguliwa katika uongozi wa kikundi cha sala wanapoishi.
4.4.7. Kutakuwapo na umoja wa jumuiya za agano za kiinjili za kikarismatiki nchini, ambazo zitakuwa na
14
SURA YA TANO
5.0.MAKUZI YA KIROHO
Ubatizo Katika Roho mtakatifu, au ujzo wa Roho Mtakatifu,ni mwanzo tu wa safari binafsi kuelekea
majitoleo ya kina ya maisha ya Kikristo.hali hii haifikiwi mara moja ,bali inahusisha mwenendo wa
majitoleo binafsi na ukuaji hata mkristoafikie ukaribu mkamilifu baina yake na Mungu na jirani (Mk
12:28-30;17-19)
Mafundisho yanahitajika kuhusu jinsi ya kukua kiroho na kimaadili. Katekesi itazingatia mafundisho ya
kanisa Katoliki kama yanavyopatikana katika Biblia, Katekisimu ya kanisa Katoliki, Mtaguso wa pili wa
Vatcano, mapaokeo ya Matakatifu (Nyaraka na mafundisho toka kwa Mapapa na Maaskofu, ili
kuwawezesha wanakikundi wakue kwa namana bora zaidi katika imani Katoliki. Uwapo wa Roho
Mtakatifu na nguvu zake hazina budi kudhihirika kwa ishara na miujiza, lakini pia kwa kjifia nafsi. Ni
mhimu kuwa mafundisho haya yawasaidie wanakikundi kila mmoja kuubeba msalaba wake (Luk 9:23,
RUM 8;9-14).
5.1. Sala
Sala ndio msingi wa kuimarisha na kudumisha mahusiano binafsi ya kina yna ya upendo kwa Mungu,
jirani na nafsi yako yako mwenyewe. Maisha yenye mafanikio yanahitaji ‘kutenga muda wa ukimya kila
siku’(MUKS kwa wakati unaofaa na kadhalika muda wasala na ibada za jumuiya (misa takatifu, kuabudu
Yesu wa Ekarisiti, sala ya familia na pia pamoja na wengine).
Majitoleo kwa Bikira Maria mbarikiwa na kwa Watakatifu ni sehemu muhimu ya imani ya mkatoliki na
chombo cha sala chenye nguvu.
Kila Mkristo anahitaji kumjua Mungu na kumwelewa yeye na njia zake. Kuijifunza Biblia ni zoezi la
makusudi linalolenga kuzoeza akili. Kimsingi hapa si kwa maana ya kisomi ya kumtafuta kupata shahada
au nembo nyingine za jinsi hiyo, bali kwa mapana yake katika mwendelezo wa kumtafuta kujua mamabo
ya Mungu zaidi, ili tuweze kumpenda vizuri na kumtumikia zaidi. Kuijinza bibilia kwatuwezesha
Kutambua ‘Mungu nji nani, anafanya nini na nini anataka tufanye’ (1 Tim 3:17). Kwa sababu hiyo ni
muhimu kwetu sisi kama wakatoliki kusoma na kujinza bibilia kama inavyohimizwa na mtaguso wa pili
wa Vatcano (DV 26).
5.2.1 Katika neno la Mungu upo uwez na nguvu nyingi kiasi kwamba neno hilo huwa egemeo na nguvu
kwa kanisa na pia uthabiti wa imani na chakula cha kiroho na chemichemi safi na maisha ya kiroho kwa
watoto wa kanisa (DV 21).
Ushirika wa neno ambalo linarejeza karibu kila kitu ambacho wakristo Wanafanya pamoja kama
mwili wa kristo. Ni uthibitisho wa uharisia wa kiroho kwamba tu kina kaka na akina dada wa
familia moja. Katika upweke hatuwezi kuwa wakristo kamaili. Ili tuweze kuonja utimilifu wa
15
maisha ya kikristo inatupasa kuungama na wakristo wengine. Twahitaji utegemezo wa wenzetu,
twahitaji hekima zao na nguvu.
1.Ibada za kilitrujia
2. Mikutano ya sala
5.4. Masakramenti
Kadiri ya mapokeo ya kikatoliki, chombo muhimu zaidi katika makuzi ya kiroho, ni masakramenti. ‘
Kanisa limeweka shariti kwamba kwa waamini kushiriki ibada ya misa takatifu siku za jumapili na
sikukuu zilizoamriwa, na wakiwa wamejiaanda kwa sakramenti ya upatanisho, kanisa linawahimiza sana
waamini wake wapokee Ekaristi takatifu kila siku’, ikiwezekana (Can.1389) kwa sababu hiyo
wakarismatiki, wanahimizwa kupokea sakramenti ya upatanisho mara nyingi, na kushiriki komunio
wakiwa na usafi wa moyo ikiwezekana kila siku (1 Wak 11:23-33)
5. Kuwaponya wagonjwa
6. Kuwatembelea wafungwa
7. Kuwazika wafu
16
1. Kuwashauri wenye mashaka
2. Kuwafundisha wasiojua
4. Kuwaonya wakosefu
5. Kusamehe makosa
6. Kuwavumilia wasumbufu
Wakristo wa mwanzo walijaliana, walihurumiana na Kusaidiana sana katika jumuiya zao za Awali (Mdo
2:43-47,4:32-37)
1. Awe na nia, ari na juhudi za kukua kiroho, amepokea sakramenti za kumuzamisha katika imani,
ubatizo,
Ekaristi na kipaimara, (awe na hati ya ubatizo) kwa matendo anasali kila jumapili na siku za amri, na
kila inapowezekana misa za kila siku, na kupokea ekaristi takatifu kulingana na utaratifu wa kanisa
mahalia.
3. Awe hai katika chama kimojawapo cha kitume (Rejio Maria, Moyo Mtakatifu wa Yesu, Utawa wa
tatu wa
Wafransikani, Virafra, Mtakatifu ana, Wawata, Uwaka, n.k. (angalau kimoja na kushiriki katika
jumuia ndogondo za kikristo. Ampende Bikira Maria na kusali Rozali na kufanya hija kwa vituo vya
hija vilivyojengwa kwa heshima ya Bikira Maria pale penye uwekano.
4. Asiwe na fikra za kulogwa na hataki aingize mwingine katika fikra hizo za ushirikina na uchawi,
kwani Yesu Kristo ana nguvu kuliko uchawi.
6. Awe mtu Mwenye utii kwa viongozi na Hiarakia (viongozi wa kanisa) na viongozi wa kikundi chake
cha sala.
7. Awe nia au ari ya kukua katika upendo, na katika matumizi ya karama za Roho Mtakatifu kwa ajili ya
utukufu wa Mungu Baba na kwa manufaa ya wengine.
8. Awe mtu mwema aliyejaa imani, hekima na Roho mtakatifu (Mdo 6:3)
17
5.7.Karama za Roho Mtakatifu
5.7.1. Wakristo wengi waliotoa wengi waliotoa maisha yao kwa Yesu Kristo, kumfanya Bwana na
mwokozi wamaisha yao binafsi, na kujiunga na vikundi vya sala vya Ki-karismatiki, hushuhudia
mabadiliko mkubwa na ya msingi katika maisha yao. Mabadiliko hayo ya maisha hutokanan na toba ya
kweli, uamuzi wao thabiti wa kumgeukia Bwana Yesu Kristo, na kukubali Kujazwa nguvu za Roho
Mtakatifu. Tukio hilo la Kujazwa nguvu za Roho Mtakatifu huitwa ubatizo wa Roho Mtakatifu. Pato moja
la kubatizwa Roho Mtakatifu ni kupokea karama zake, kwa mfano unabii, uponyaji, miujiza, kunena kwa
lugha mpya n.k. (1 Wak 12; Rum 12;6-8). Hivi ndivyo utendaji wa Roho Mtakatifu umejionyesha kwa
nguvu nyingitangu kanisa la Awali. Tunawajibika kuwa na shukrani kwa Mungu kwa kutumwagia kwa
kutumwagia siku hizi karama na neema zilezile zilizolibariki kanisa tangu siku zake za mwanzokabisa
(taz. Sala ya misa ya pentekoste.).
5.7.2 Jambo la kukumbukwa ni zawadi inayotolewa na Roho Mtakatifu ili Kujenga Kanisa (1Wak 14;12).
“Roho ni mmoja agawiae Karama zake mbalimbali kwa ajili ya manufaa ya kanisa, kadri ya utajiri wake
mwenyewe na hitaji la huduma (LG.7). Kwa karama hizo Roho anawawezesha waamini kwa “… kwa
kuwafanya wafae na kuwa tayari kazi na huduma mbalimbali zenye kuleta manufaa kwa ajili ya
matengenezo ya kanisa na maongezo yake (LG.12)
5.7.3 Miongoni mwa karama hizo ambazo zinaonekana kuwa ngeni kwa watu wengi japo ni za muhimu
na zina msingi dhahiri katika maandiko matakatifu na mapokeo. Karama hizo ni pamoja na:-
2) Karama ya unabii
Karama hii inajidhihirisha katika vikundi vya sala wakati baadhi ya wanakikundi wanapokea ujumbe wa
Mungu kwa ajili ya kuwajenga, kuwatia moyo na kuwafariji wenzao (1Kor 14:3-5). Kila unabii
upokelewe kwa shukrani, lakini lazima upimwe bila kumzimisha Roho Mtakatifu (1 Thes 5:19-21; 1KOR
14:29; 1YOH 4:1)
3. Karama za uponyaji
Katika kanisa karama hizi zimeendelea kuonekana kwa njia ya sakramenti ya mpako wa wagonjwa,
maombezi ya watakatifu na mahali pengi pa matokeo ya pekee kama vile Lurd-Ufaranza na Fatima –
Uureno. Katika Karismatiki Katoliki, karama hizi zinadhihirika kwa njia ya sala ya imani ya Waumini
kama alivyosema Bwana Yesu kabla ya kupaa kwake (Mk 16:17-18). Kutokana na hitaji kubwa la
uponyaji katika jamii, karama hii imetumika sana hata imekuwa huduma kamili ya uponyaji ndani ya
Karismatiki Katoliki. Kwa sababu hiyo, mwongozo huu unatoa maelezo ya kina kuhusu huduma hii.
18
5.8.1.1. Zisifanywe kuwa sehemu ya kujipatia fedha: “Mmepewa bure toeni bure” (Mt 10:8).
5.8.1.2. Zisiwe njia ya kujipatia njia ya kujipatia sifa au Umaarufu. Sifa na utukufu wote uwe kwa
Mungu mponyaji. Ili kuepuka hali ya mtu binafsi kujichukulia utukufu, maombezi ya wagonjwa yafanywe
na timu ya wanakikundi kadhaa kila iwezekanapo.
5.8.1.3. Uponyaji hupatikana kwa imani, lakini kamwe isifikiriwe kutokufaulu kupona kwa mtu fulani
inaonekana upungufu wa imani tu au hali ya dhambi ya muhusika.
Katika Biblia huduma hii ni sehemu ya huduma za uponyaji (Mk 16:17-18). Maandi zaidi yanathibitisha
mpango wa Bwana juu ya kutoa pepo; “Yesu aliwaita wale thenashara, akawapa uwezo na mamalaka juu
ya pepo wote na kuponya maradhi” (Lk 9:1; 17-19) Ifahamike kuwa kuponywa kwa ndani au kiroho ni
sehemu ya huduma za uponyaji. Mara nyingie wakati sala za kuponya zinapotolewa yawezekana sala za
kuwinga pepo zikatakiwa. Hapo mambo mawili lazima yazingatiwe: Hekima ya kichungaji na karama ya
kupapambanua roho (1 Yoh 4:1-6; 1 Kor 12:10). Lazima kutofautisha kati ya sala ya kuwekwa huru
kutoka nguvu za giza (derivarence) na sala ya kuwinga shetani (exorcism).
Mtu anaposhindwa kujitawala katika jambo fulani maishani mwake, anahitaji sala ya kuwekwa huru.
Jambo hili ni zaidi ya kishawishi cha kawaida na pungufu ya hali ya kutawaliwa kabisa na shetani. Sara
hii inaweza kutolewa na Mkristo mwenye karama ya kufungua na kuweka huru. Lakini huduma hii
ifanyike na kikundi kinachotambuliwa na uongozi uongozi husika wa kanisa. Ieleweke kwamba siyo kila
ni mapepo isipokuwa kila kitu kinahitaji kupambanuliwa.
Kuwinga Pepo ni sala rasmi ya Kanisa ambapo “Kanisa linaomba wazi kwa mamalaka ya Jina la Yesu
Kristo kuwa mtu au kina fulani kilindwe dhidi ya yule mwovu na kuondolewa kutoka wake (KKK 1673).
Exorcism “ huelekezwa katika ufukuzaji wa mapepo au kufunguliwa kutoka hodhi ya kipepe kwa njia ya
mamalaka ya kiroho ambayo Yesu alilikasmia Kanisa lake” (KKK 1673).
Kutokana na asili na ugumu wa huduma ya exorcism, “hapana hata mtu mmoja ambaye kisheria aweza
kumwinga mtu pepo bila ruhusa maalumu na halisi toka kwa Askofu Mahalia” (Can. 1172 par 1).
Ruhusu ya kuwinga pepo hutolewa na Askofu Mahalia kwa au mtu yeyote aliyejaliwa uchaji, maarifa,
busala na msimo thabiti wa maisha “. Kwa sababu hiyo kabla mtu hajawinga pepo “ ni muhimu
Kuhakikisha kuwa kuna uwapo wa pepo wala si ugonjwa pekee” (KKK 1673).
Ikiwa ni suala la kutawaliwa kabisa na shetani, suala ambalo hujitokeza mara chache, huduma ya kuwinga
shetani inahitajika. Huduma hii hufanywa na Askofu au Padre aliyeidhinishwa naye.
19
5.10. Baadhi ya Karama za Roho Mtakatifu
5.10.2. Hekima
Hii ni karama ambayo Roho Mtakatifu huitumia kumwongoza mtu kufanya maamuzi sahihi au kuchagua vema na
kuishi maisha ya kweli ya Kikristo. Utambuzi wa fumbo la Kristo kama katika mifano aliyoitoa Yesu, kadharika
mafunuo mengi aliyoyapata Mtakatifu Paulo kuhusu mpango wa Mungu wa Wokovu; ni mifano halisi ya karama
hii. Leo hii Wakatoliki wengi na wote wanaofanya kazi ya kufundisha imani, au wanaoshauri katika nasaha za
Kikristo, wanakiri na pia wanaiona kuwa na thamani maalum, na kwa hivyo huiomba daima. Hekima hii ni ile
itokayo juu mbinguni
(Yak 3:13-18)
5.10.3. Maarifa
Kwa karama hii Roho Mtakatifu humpa mtu uelewa wa kina juu ya fumbo la Imani, au humjuvya kuhusu hakika ya
jambo ambalo asingeweza kulijua ila Mungu Mwenyewe Amelifunua. Karama hii huonekana na kudhihirika katika
maisha ya baadhi ya Watakatifu. Kwa mfano, Yesu alidhihirisha karama pale alipomfunulia yule mwanamke
Msamaria katika kisima cha Yakobo kuwa alishakuwa na waume watano( Yoh 4:18). Mtakatifu Yohane Vianey, pia
Padre Pio walitumia karama hii wakati wa maungamo kuongoza mamia ya waamini wafikie toba ya kweli na
kuanza maisha mapya. Lakini pia yafaa katika huduma ya uponyaji kwa kututambulisha chimbuko la ugonjwa ili
kuomba ipasavyo ( 1Kor 12:6-11).
5.10.4 Imani.
Karama hii humwongoza mtu kuomba kwa uhakika, akitumaini kuwa kile aombacho kitatokea.
Katika Marko 11:23, Yesu alisema, “amin, nawambieni, yeyoteatakayeuambia mlima huu, ng’oka ukatupwe
baharini, wala asione shaka moyoni mwake, ila aamini kwamba hayo asemayo yametukia, yatakuwa yake. Imani
ya jinsi hii humsukuma mtu katika kutenda, kama pale Mtakatifu Petro alipomwambia yule kiwete akisema” kwa
jina la Yesu Kristo wa Nazareti, simama uende” (Mdo 3:6-10). Imani huonekana kwa kuvumilia mateso kwa ajili ya
Mungu ( Ebr 11) pia Imani huonekana katika matendo ( Yak 2:14-26).
5.10.5. Miujiza.
Kwa karama hii Mungu hufanya tendo la” Uweza Wake”. Ni tendo lisilowezekana kibinadamu, kwa kumtumia mtu
Fulani, kama chombo chake cha kudhihirishia” kazi zake za nguvu na uweza”, kama alivyomtumia Petro na Paulo
na pia baadhi ya watakatifu. Muujiza mkubwa zaidi ni ule wa uponyaji war oho na mwili kwa sakramenti za
uponyaji yaani mpako wa wagonjwa ( Yak 5: 14-15). Pia kushiriki Sakrament zinazotupa nguvu hasa Ekaristi
Takatifu.
5.10.6 Unabii
Hii ni karama ambayo kwa Mungu kwa kumtumia mtu Fulani hunena neno au kutoa ujumbe kwa mtu binafsi au
kwa jumuia nzima ya Kikristo. Ni Mungu, anamtumia mtu Fulani kuwaambia watu mawazo yake kuhusu hali
iliyopo au kusudi lake ni nini kuhusu mustakabali wa hali ijayo, au ni kipi Mungu anafikiria watu wake wanahitaji
kujua, au kujilinda kwacho kwa wakati huo. Si lazima ujumbe uandamane na utabiri wa mambo yatakayotokea
baadaye, ingawa hilo laweza kutokea na litokeapo lahitaji upambanuzi wa kikundi cha watu hasa viongozi ili
kuthibitisha ujumbe huo. Katika waraka wa Kwanza wa Mt. Paulo kwa Wakorintho, Mtakatifu Paulo anasema, “
Bali yeye ahutubuye ( atoaye unabii) asema na watu maneno ya kuwajenga, na kuwafariji na kuwatia moyo” ( 1Kor
20
14:3), Kwa hiyo, unabii wa kweli utaleta upendo, furaha, amani, wongofu n.k. “ Msimzimishe Roho, msitweze
unabii, jaribuni mambo yote, lishikeni lililo jema, jitengeni na ubaya wa kila namna” ( 1Thes 5:19-22).
5.10.7. Ndimi
Hii ni karama ambayo kwayo mtu hutamka maneno au sauti kwa lugha ambayo yeye mwenyewe haifahamu ( 1Kor
14). Katika UKK hutumika wakati wa masifu – kumuimbia Mungu sifa, Kuabudu, kuombea watu au hali Fulani. Ni
lugha ibubujikayo toka moyoni, hali ambapo Roho wa Mungu ndani ya mtu huendelea kuomba na hasa pale
muhusika anapokuwa hajui cha kusema ( Rum 8:26-27).
1. Ni aina ya ndimi za kimiujiza, ambapo mtu anenapo wasikiaji humsikia katika lugha zao, kama katika (
Mdo 2:6-11). Aina hii ya ndimi hutokea kwa nadra sana na inakusudiwa kuwa ishara kwa wasioamini (
1Kor 14:22).
2. Ni aina ya ndimi inayo lenga kutoa ujumbe kwao waaminio. Hata hivyo yanayotamkwa ni lugha ambayo
yenyewe kama yenyewe haieleweki (yanayotamkwa si lugha yakueleweka na mtu yeyote). Ili ieleweke
yahitajika karama nyingine ya kiroho, ni ile ambayo Mt. Paulo anayosisitiza ya kafasiri (1Kor 14:13,26,27).
3. Hatimaye ni aina ya tatu. Kimsingi aina hii ya ndimi, ni sala halisi. Ni aina inayoonekana zaidi katika UKK,
na ina sifa mbili: Ni sala ya sauti ( haijakusudiwa kuwa ya ukimya), na tena yenyewe kama yenyewe
haieleweki kwa wanaosikia ( haitumii maneno ya kawaida). Pamoja na hayo, Maandiko Matakatifu
yatuhakikishia kuwa ni sala, maana yaongozwa na Mungu, inaeleweka na Mungu na inavuviwa na Roho wa
Mungu, ili kuwasaidia waamini katika udhaifu wao, kwa maana aghalabu hatujui kuomba ipasavyo;”
Lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa” ( 1Kor 14:2; Rom 8:26). Faida ya
sala hii ya ndimi, humjenga anayesali (1Kor 14:4).
4. Mtakatifu Paulo anawahimiza Wakristo kuomba kwa namna zote mbili. Kwa Roho, yaani bila matunda ya
akili, na kwa akili (1Kor 14:14)……).
Angalizo: Karama hii inahitaji hekima na busara katika matumizi yake. Lazima kuangalia wakati, mahali ulipo, na
watu wanaokuzunguka. Kwani karama haikulengwa kutumika kwa majivuno
( Mt 4:1-11; Mt 27:39-44).
5.10.8. Uponyaji
Ni kipawa anachopewa mtu kwa ajili ya kuponya magojwa na shida mbalimbali kwa ajili ya utukufu wa Mungu.
Kwa binadamu kupata maumivu ya kimwili, kisaikolojia au ya kiroho ni sehemu ya maisha yetu. Mara nyingine
mateso tupatayo huunganishwa na dhambi ( Mwa 3:1-19; Kumb 28:21-22, 27-29), lakini pia mateso huweza
kuwapata wenye haki, kama majaribu kwa waadilifu kitabu cha Ayubu, Mateso saba ya Bikira Maria; kwaajili ya
ukombozi wetu:
1) Unabii wa Simeoni ( Lk 2:34-35).
2) Kukimbilia Misri ( Mt 2:13-15).
3) Kumpoteza Mtoto yesu Hekaluni ( Lk 2:43-49).
4) Kukutana Yesu na Maria kwenye Njia ya Msalaba ( Yoh 19:25-27).
5) Kusulibiwa kwa Yesu ( Mt 27:32-44; Mk 15:21-32; Lk 23:26-43; Yoh 19:16-27).
6) Kushushwa mwili wa Yesu toka Msalabani ( Yoh 19:38-40).
7) Kuzikwa kwa Yesu ( Mt 27:57-61; Yoh 19:41-42).
Kwa njia ya mateso yake kristo ya hiari, na matakatifu, binadamu ameponywa na kukombolewa ( rej. 1Pet 2:19-25).
Kwa Mt. Paulo Mtume kuteseka ni faida, “sasa nayafurahia mateso niliyonayo kwa ajili yenu; tena nayatimiliza
21
katika mwili wangu yale yaliyopungua ya mateso ya Kristo, kwa ajili ya mwili wake, yaani, Kanisa lake” ( Kol
1:24). Katika kipindi chote cha historia ya Wokovu, Mungu alidhamiria kuondoa mateso. Yesu aliwapa mamlaka
mitume wake kuponya wagonjwa na kufukuza pepo (Mt 10:7-8)
Kanisa daima limehudumia wagonjwa (Taasisis za Afya: Zahanati, Vituo vya Afya, Hospitali, Vituo vya
Walemavu, Vituo vya kulelea Yatima, Nyuma za wazee n.k), huduma ya kichungaji (ushauri nasaha, maongozi ya
kiroho, n.k) na huduma ya kiroho ( sala na Baraka, Sakramenti ya Upatanisho, Mpako wa Wagonjwa na Ekaristi
Takatifu).
Katika sala yoyote ya uponyaji uangalifu unatakiwa katika kupambanua na kuthibitisha uponyaji:
Kama unahitaji kwanza vipimo na tiba ya hospitali au ushauri nasaha au kumuona daktari wa magonjwa ya akili; na
baadaye sala na maombi.
22
SURA YA SITA
6.1.1. Tangu enzi za kale kabisa Kanisa limekuwa likimheshimu Mbarikiwa Bikira Maria ( KKK,
496 - 498, 500), Mama wa Mungu ( Lk 1:43), aliyetungwa mamba kwa uwezo wa Roho
aliishi bila dhambi maisha yake yote ( Pius IX, Ineffabilis Deus, 1854). Mwishoni mwa uhai
wake alipalizwa mbinguni mwili na roho ( Papa Pius XII, Magnificantissimus Deus, 1950).
6.1.2. Kwa kuwa yu Mama wa Mungu na Mama wa Kanisa (Yoh 19:25-27), tunamtambua kuwa Mstahiwa, nasi
tunamheshimu (Lk 1:48). Mama Maria ni kielelezo cha imani na upendo wa kweli, mfano wa kuigwa wa
Kanisa ambalo waamini wake wanatambua kuwa waweza kukimbilia ulinzi wake wakati wa hatari na
uhitaji kwa njia ya kusali Rosari, na kwenda kuhiji katika makanisa na vituo vilivyojengwa kwa heshima
yake.
6.1.3. Majitoleo halisi kwa Mama Maria ni zawado adhimu ya Roho kwa kila Mkristo. Yeye alimpokea Roho
Mtakatifu alipopashwa Habari ( Lk 1:35), alijazwa Roho Mtakatifu siku ya Pentekoste ( Mdo 2:1-4).
6.1.4. Roho Mtakatifu huvuvia majitoleo halisi kwa Maria, na majitoleo hailisi kwa Maria huchochea utii, usikivu
na welekevu kwa Roho Mtakatifu. Yeye ni muombaji ( Yoh 2:1-12). Tuombe maombezi yake
tunaposherekea sikukuu zake, tusalipo rozari, litania zake, na sala nyingine. Na tufuatishe mema yote
aliyonayo ya imani thabiti nay a kipekee, tumaini, upendo na ujasiri wa utayari wazi wa kupokea na
kutimiza mapenzi ya Mungu.
Bikira Maria Msikivu, Mjitoa Sadaka, Mpole na Mnyenyekevu Jasiri – Lk 1:34-35. Mama Maria aliyemsikiliza
Malaika wa Bwana, pale alipomwambia juu ya huo wito, akauliza swali kwa upole na unyenyekevu mkubwa,
akitaka kujua mambo magumu katika maneno aliyoelezwa na Malaika wa Bwana, “Litakuwaje Neno hilo maana
sijui mume” ( Lk 1:34-35). Alipopewa majibu na Malaika wa Bwana, japo pia yalikuwa magumu akawa mtii,
akapokea wito huo moja kwa moja, bila kuuliza uliza na kujiuliza uliza, wala kutaka muda wa kutafakari maana
tayari alikuwa na mpango mwingine wa maisha yake, ambao ulikuwa kinyume kabisa na mpango anaoelezwa na
malaika wa Bwana, akajibu na kueleza “Tazama mimi ni mjakazi wa Bwana na iwe kwangu kama ulivyosema” ( Lk
1:38).
Malaika akaingia nyumbani mwake akasema, “Salamu uliyepewa Neema Bwana yu pamoja nawe” Maria
akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake, akawaza moyoni, salamu hii ni ya namna gain? Ili bidi Malaika
amtulize “ Usiogope Maria, maana neema kwa Mungu” salamu hii aliiona ni kubwa kwake.
Maria alipokwisha kuelezwa na Elizabeti aliyejaa Roho Mtakatifu “ Heri aliyesadiki kwa maana yatatimizwa
aliyoambiwa na Bwana”. Maria akaanza kumshukuru Mungu kwa wimbo/Magnificant akisema “ Moyo wangu
wamwadhimisha Bwana, na roho yangu imemfurahia Mungu mwokozi wangu kwa kuwa ameutazama unyonge wa
mjakazi wake” ( Lk 1:45-48: 1Sam 2:7-8).
23
6. 4. Bikira Maria Nyota ya Uinjilishaji
“Mwishoni mwa Barua yake ya Kitume, Evangelii Nuntiandi, Papa Paulo VI anatoa cheo “ nyota ya uinjilishaji kwa
Mama wa Mungu: ‘Katika asubuhi ya Pentekoste aliangalia kwa sasa zake mwanzo wa uinjilishaji uliochochewa na
Roho Mtakatifu: tunaomba awe Nyota ya uinjilishaji unaofanywa upya daima na ambao Kanisa, likitii amri ya
Bwana wake, ni lazima liendeleze na kukamilisha, hasa katika nyakati hizi ambazo ni ngumu, lakini zilizojaa
matumaini’ ( EN 82). Kwa hiyo, Maria ni njia ya uhakika ya kumpata Kristo. Uchaji wa kweli kwa Mama wa
Bwana daima unatuhamasisha kuelekeza maisha yetu kufuatana na Roho Mtakatifu na tunu za Injili” (rej. Ecclesia
in America 22-1-1999, no.11).
Bikira Maria daima amekuwa mwezeshaji wa jiujiza kwa maombezi yake kwa mwanae, pale tunapomwomba
atuombee. Mara nyingi, Bikira Maria hutuombea hata pale ambapo hatukumwomba atuombee. Anapoona tu,
tunahangaika na tuna shida Fulani, Maria hasubiri kumwambia Mwanae Yesu Kristo, kama tunavyoona katika
habari ya harusi ya Kana ya Galilaya. Mara tu divai ilipowatindikia hata wakati ambapo Yesu alisema saa yake
haijafika bado, Bikira Maria alimwomba Yesu, na Yesu akafanya sawasawa na ombi lake (Yoh 2:1-12).
Bikira Maria kwa kumtokea Mt. Bernadeta kule Urdi, kwa uwepo wake, amewezesha miujiza mingi. Watu wenye
shida mbalimbali duniani kote huenda huko kwa maombezi ya shida zao, hasa za miujiza, aidha ya uponyaji au
shida mbalimbali nyinginezo, na wengi kila mwaka hupata majibu chanya ya sala na maombi yao.
Bikira Maria ni mama yetu kwa sababu Yesu Kristo, Bwana na mwokozi wetu ni kaka yetu. Ni mzaliwa wa kwanza
wetu, (Rum 8:29; Kol 1:15, 18) naye anamwita Mungu, Baba, ndiye Baba yetu pia. Hivyo, Mama yake ni Mama
yetu, na amelidhihirisha hilo na kulithibitisha pale msalabani alipomkabidhi Yohane kwa niaba yetu, alimwambia
Mama yake “Mama tazama mwanao” kisha akamwambia Yohane “ Tazama Mama yako”. Na tangu saa ile Yohane
alimchukua Bikira Maria nyumbani kwake ( rej. Yoh 19:25-27).
Hata baada ya Bwana wetu Kristo Kufufuka na kupaa mbinguni, Bikira Maria alikuwa bado kitovu cha mitume
akiwapa malezi ya kimama, kwani hakuna aliyemjua Yesu kati yao kuliko Bikira Maria, maana alikuwa ameungana
na Yesu katika mwili na roho. Maria alikuwa na mitume wakti wa Pentekoste, ( Mdo1:14) na hata baada ya
Pentekoste, akiwasaidia kwa sala, ushauri wake, na hasa kwa uwapo wake kwa muda mchache – muda wa siku
kumi tu, - walimpokea Roho Mtakatifu siku ile ya Pentekoste. Tangu hapo Injili ikaanza kuhubiriwa kwa nguvu za
ajabu. Bado hata sasa Bikira Maria amekuwa si kielelezo tu, bali pia amekuwa mwombezi wetu kwa Mwanae
mpaka hivi leo. Hivyo, tusisahau wala tusisite au kuchelewa kumwendea pale tunapokuwa na haja mbalimbali.
1) Kila siku: Matendo ya Furaha (J’tatu na J’mosi), Matendo ya Uchungu ( J’nne na Ijumaa), Matendo ya
Utukufu ( J’tano na Jumapili), Matendo ya Mwanga ( Alhamisi).
2) Miezi ya Rozari ( Mei na Oktoba)
3) Novena za siku tisa
6.7.3. Kusali au kuhudhuria na kushiriki Misa Takatifu kwa siku; Sikukuu na Sherehe zifuatazo:
24
1) Jumamosi za Bikira Maria
2) Sikukuu na Sherehe mbalimbali za Bikira Maria kama ifuatavyo:
Januari 01, - Bikira Maria Mtakatifu, Mama wa Mungu (Sherehe).
Februari 11, - Bikira Maria wa Lurdi: Sikukuu ya kuombea Wagonjwa.
Machi 25, - Kupashwa habari Bikira Maria.
Mei 31, - Bikira Maria kwenda kumwamkia Elizabeti.
Agosti 15, - Bikira Maria kupalizwa Mbinguni (Sherehe).
Septemba 15, - Bikira Maria wa Mateso.
Oktoba 07, - Bikira Maria wa Rozari Takatifu.
Novemba 21, - Kutolewa Bikira Maria Hekaluni
Desemba 08, - Bikira Maria Mkingiwa dhambi ya asili ( Sherehe)
6.7.4. Kuhiji kwenye vituo vilivyojengwa kwa heshima yake Bikira Maria, Mfano
25
SURA YA SABA
Uongozi wa Maaskofu ni muhimu katika kuiwezesha Karismatiki Katoliki kukua na kustawi katika ushirika na
utume wa Kanisa. Huduma ya Karismatiki Katoliki katika Jimbo lolote lazima ipate baraka na kibali cha Askofu wa
Jimbo mahalia. Papa Yohane Paulo wa II alipozungumza na viongozi wa Karismatiki Katoliki ulimwenguni, alisifu
juhudi zinazofanywa na Maaskofu za kutia moyo Karismatiki, kuipa maelekezo na kusaidia jumuiya ya Kikristo
kuelewa vizuri zaidi nafasi ya mkondo huu ndani ya Kanisa. Yote haya wamekuwa wakiyafanya ili kuwezesha
mwamko huu kuwa wazi zaidi kwa tunu mbalimbali za upendo wa Mungu zilizomo ndani ya Kanisa. Pia alisema,
“hata kama Maaskofu hawavutiwi na mitindo ya sala ya Kikarismatiki ambayo ninyi mmeona inajeng,
watakubaliana kwa dhati na matamanio yenu ya kufanywa upya kiroho kwenu wenyewe na kwa Kanisa kwa
ujumla. Hivyo watawapeni maongozi yapasayo bila pingamizi kwani huo ndio wajibu waliopewa na Kanisa.” ( Mei
7, 1981. Taz. Pia Christifideles Laici no. 31).
Kuhusu Mapadre, Papa Yohane Paulo wa II alisema hivi: “Padre hataweza kutoa huduma kwa Wakarismatiki
asipoukubali na kuukaribisha mkondo huu katika mawazo ya moyo wake. Awe na hamu ya kukua katika vipaji vya
Roho Mtakatifu na moyo wa kushirikiana na kila mkristo katika kukuza vipaji hivyo.” ( Mei 7, 1981. Taz. Pia
Christifideles Laici no. 31). Hivyo Padre anawajibu wa kutia moyo na kutoa ushauri wa kichungaji hata kama yeye
binafsi si Mkarismatiki.
Kadili ya Mtaguso Mkuu, Maelezo ya Hati 16 za Vatikano II; TMP Book Department, Taborauk. 212-213; uk 187
na 25, wajibu wa Padre ni:
2) Padre anapaswa kuwashauri walei na utume wao katika Kanisa bila kuwakatisha tama, na anapaswa
kuwasaidia, kuyasikiliza mashauri yao, kutambua ujuzi wao na ufundi wao katika mahitaji ya Kanisa la siku
hizi.
3) Mara kwa mara Padre ashiriki katika ibada zao, mikutano yao ili kuwasaidia kwa kuwapatia Sakramenti
mbalimbali kwa mfano: Kitubio, Ekaristi, Mpako wa Wagonjwa, kutoa mafundisho na kuwatia moyo.
4) Wote wafurahi wanapoona vipawa vyao kutoka kwa Mungu na hamu yao ya maisha ya roho na kulitumikia
Kanisa inatimia.
26
SURA YA NANE
1) Mratibu wa Kikundi
2) Mratibu Msaidizi
3) Katibu
4) Katibu Msaidizi
5) Mhazini
6) Mhazini Msaidizi
7) Waratibu wa Kamati za Huduma
27
8.1.4. Uongozi katika Huduma za Kikundi
Kila Kikundi cha Sala kitakuwa na timu mbalimbali za kutoa huduma. Kila timu ya kutoa huduma ( yaani Timu ya
Huduma) itaongozwa na viongozi sita:
1) Mratibu
2) Mratibu Msaidizi
3) Katibu
4) Katibu Msaidizi
5) Mweka Hazina
6) Mweka Hazina Msaidizi
1) Paroko ndiye Mlezi wa vikundi vyote Parokiani. Paroko aonapo inafaa anaweza kuteua Mlezi wa
Kumwakilisha.
8.1.7. Vikao
1) Kamati ya Huduma ya Kikundi itakutana mara moja kwa wiki kusali pamoja; kuombeana na kuombea
mambo mbalimbali, kutathmini matukio ya wiki yaliyotangulia, na kupanga matukio ya wiki inayofuata.
2) Kikao cha kutathmini Mkutano wa Sala na kupanga unaofuata, kifanywe siku ya Mkutano kabla na mara
baada ya mkutano. Kikao hiki kihudhuriwe na wajumbe wote wa Kamati Tendaji, wahudumu wa Mkutano
wa Sala wa siku hiyo, na wale wa Mkutano unaofuata ambao wataombewa siku hiyo.
3) Kamati itakutana mara moja kwa mwezi kupanga utaratibu wote wa huduma kwa mwezi mzima.
4) Mkutano Mkuu wa Kikundi utafanyika mara moja kwa mwaka. Mkutano huo utahudhuriwa wa
wanakikundi wote. Katika mkutano huo viongozi watatoa taarifa ya maendeleo, mapato na matumizi na
kupokea maoni na ushauri wa wanakikundi.
5) Viongozi wa kila Timu ya Huduma ya Kikundi, watakutana angalau kila baada ya wiki mbili, kwa ajili ya
kuombea huduma husika, na kila mwezi kutathmini na kupanga mwenendo mzima wa huduma katika
kikundi.
Parokia zenye zaidi ya Kikundi kimoja cha Sala zitakuwa na Kamati Tendaji ya Parokia – KTP
1) Mratibu wa Parokia
2) Mratibu Msaidizi
3) Katibu
4) Katibi Msaidizi
5) Mhazini
6) Mhazini Msaidizi
7) Waratibu wa Kamati za Huduma
29
8.3. Kamati Tendaji ya Jimbo (KTJ)
1) Katika kila Jimbo ambamo mna vikundi vya sala kuundwe KTJ.
2) Uchaguzi wa Viongozi ufanywe na utambulishwe kwa Askofu Mahalia.
3) Padre Mlezi atateuliwa na Askofu Mahalia.
1) Mratibu wa Jimbo
2) Mratibu Msaidizi wa Jimbo
3) Katibu wa Jimbo
4) Katibu Msaidizi wa Jimbo
5) Mhazini.
6) Mhazini Msaidizi.
7) Waratibu wa Huduma ya Kijimbo
8) Mjumbe / Wajumbe kutoka Jumuiya za Kikarismatiki.
8.3.3. Mujukumu
KTT ndiyo Kiungo Ritibisha cha Juuu katika Upyaisho Karismatiki Katoriki Tanzania ( UKKT). Utume wake ni
kuendeleza UKKT hata ienee kila pembe ya nchi kwa tendo la Roho Mtakatifu. UKKT iko chini ya uongozi wa
Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC). Kiutendaji Baraza la Maaskofu litateua Askofu kuwa Mlezi wa mkondo huo,
akishirikiana na Kamati Tendaji ya Taifa kuratibisha shughuli zote za Karismatiki nchini.
1) Mratibu wa Taifa
2) Mratibu Msaidizi wa Taifa
3) Katibu Mkuu
4) Katibu Mkuu Msaidizi
5) Mhazini.
6) Mhazini Msaidizi.
7) Waratibu wa Kamati za Huduma.
8) Wajumbe waalikwa
1) Kujenga mahusiano ya karibu kati ya mamlaka ya Kanisa ( Maskofu) na UKKT kwa lengo la kushirikisha
kikamilifu ndani ya maisha ya Kanisa.
2) Kuhakikisha kuwa masuala yote ya kichungaji na kiteolojia hayapotoshwi katika vikundi vya sala nchini
kote kwa kushirikiana na Mshauri wa Kitume au Mlezi.
30
3) Kujenga na kuimarisha umoja wa Vikundi vya Sala na Jumiya za Kikarismatiki nchini, kwa njia ya
mikutano, matukio, na huduma mbalimbali.
4) Kuandaa na kusimamia maono kwa ajili ya Upyaisho na kuhakikisha vikundi vya sala na Jumuiya za
Kikarismatiki zinaendelea vyema.
5) Kuwa kiungo cha mawasiliano nchini kote na kwa mamlaka ya Kanisa kutoa taarifa zinazohusu Upyaisho;
kuandaa taarifa za maendeleo kwa ujumla.
6) Kushughulika na mialiko kwa viongozi wa Upyaisho au wawezeshaji kutoka ndani na nje ya nchi kwa ajili
ya kujiimarisha.
7) Itaendesha shughuli zote za siku kwa siku za UKKT ( Upyaisho Karismatiki Katoliki Tanzania) chini ya
uongozi wa Mratibu wa Taifa.
8) Itatayarisha na kupanga kwa niaba ya KTH ( Kamati ya Taifa ya Huduma) mikutano, matukio na ratiba zote
za Kitaifa.
9) Ni kitovu cha mawasiliano cha UKKT na Mataifa ya nje na huduma mbalimbali za Kikristo za ndani na nje
hasa ICCRS ( International Charismatic Renewal Services) iliyoko Vatikano, Roma; AFSCI ( Africa Sub-
Committee of International Charismatic Renewal Services) n.k.
10) Itatunza kumbukumbu mbalimbali na za mahesabu yote ya fedha na mara kwa mara kufanya ukaguzi wa
mahesabu hayo na kuyawasilisha kwa KTH au mamlaka nyingine za Kanisa.
11) Itaandaa mizania ya hesabu, taarifa ya mapato na matumizi ya mwaka na bajeti ya mwaka.
12) Kutoa taarifa za mipango, kazi na maendeleo ya Karismatiki Katoriki kwa Baraza la Maaskofu na KTH.
14) Itasimamia na kudumisha nidhamu na utii, na kuchukua hatua za kinidhamu kila inapobidi
31
Kamati hii ya Taifa ya Huduma ( KTH) itakutana mara moja kwa mwaka kwa ajili ya Mkutano Mkuu. Na wakati
wowote ikitokea dharura.
1) Kuchagua na kupendekeza majina matatu kwa Baraza la Maaskofu ili mmoja achaguliwe kuwa Mratibu wa
Taifa
2) Kuchagua Kamati Tendaji ya Taifa kwa nafasi zilizobaki
3) Kupokea taarifa za mipango- kazi mapato na matumizi ya fedha na maendeleo ya majimbo.
4) Kujadili na kutoa maamuzi juu ya ajenda zote zinazotolewa na KTT na wajumbe mbalimbali.
5) Kuiagiza na kuishauri KTT juu mwelekeo na maendeleo ya Karismatiki nchini.
1) Atakuwa kiungo cha moja kwa moja kati ya Baraza la Maaskofu na UKKT.
2) Atahudhuria Mikutano ya KTT na KTH anapokuwa na nafasi.
3) Atakuwa Mshauri Mkuu wa KTT wakati wote juu ya mambo yote yanayohusu Karismatiki.
32
SURA YA TISA
9.1.2. Muhula wa uongozi ni miaka mitatu na kiongozi anaweza kuchaguliwa kwa mihula mitatu tu.
9.1.3. Kama kuna ulazima mtu anaweza kuchaguliwa tena katika uongozi baada ya kupita mihula
Karismatiki Katoliki inahitajika uongozi kwa lengo la kuratibu na kurahisisha shughuli mbalimbali za kikarismatiki
katika vikundi vya sala. Hii ni pamoja na mikutano ya sala, semina, mafungo, huduma mbalimbali, na kuwakilisha
Karismatiki Katoriki katika mifumo ya Kanisa (ngazi ya Kigango, Parokia, Jimbo na Taifa). Kufanikiwa kwa
Vikundi vya Sala kunategemea sana uongozi imara unaotokana na ujuzi na uaminifu kwa mafundisho sahihi ya
Kanisa na uelewa wa kutosha wa Karismatiki Katoliki. Kutokana na hayo, kiongozi wa kikundi cha sala awe na sifa
anazotaja Mtume Paulo katika barua zake kwa Timotheo na Tito ( 1 Tim 3:13; Tito 1:5-9). Mbali na sifa hizo, pia
awe na sifa zifuatazo:
3) Awe Mwajibikaji
Kiongozi lazima ajue namna ya kupanga na kutekeleza wajibu wake. Awe na wakati wa kutosha kuhudumia
familia yake, kazi zake za kila siku na za kikundi chake cha sala na asiwe na shughuli nyingi mno. Kujitoa
katika mambo mengi mno kunamfanya kiongozi kushindwa katika yote, na hivi kusababisha hasara katika
Kanisa.
7) Awe na Nidhamu
Moja ya mambo yanayoimarisha Karismatiki Katoliki ni hali ya nidhamu, kuwajibika, heshima na kujali
uongozi uliopo katika Kanisa. Nidhamu inayotakiwa ni ile yenye uwiano kati ya utii kwa upande mmoja na
uhuru na wajibu wa Mkristo kwa upande mwingine.
34
SURA YA KUMI
1) Kueneza Injili (Unabii, Ukuhani na Ufalme) – kuamsha hamu ya Wakatoliki katika kuielewa imani yao na
kuiishi vizuri zaidi katika maisha yao ya kila siku.
2) Kuamusha na kukuza moyo was ala. Mkondo huu unasaidia kuondoa roho ya uvuguvugu katika maisha ya
kiroho
3) Kutakatifuza malimwengu, uwapo wake unasaidia kukemea maovu yaliyokithiri katika dunia ya leo, kama
utoaji mamba na matumizi ya vithibiti mamba, michepuko, ndoa za jinsia moja, unyanyasaji wa kijinsia,
ulevi sugu na utumiaji wa madawa ya kulevya, rushwa, ufisadi, udanganyifu, na mengineyo.
4) Kuchoche ari ya kupenda kusoma Biblia na kusikiliza Neno la Mungu. Kwa muda mrefu wazo la walei ni
kuwa, kazi ya kulisoma Neno la Mungu ni ya Padre, Katekista au Mtawa.
5) Kuchochea, kulea na kuwezesha miito ya Upadre, Utawa, na maisha ya Ndoa. Hii ni kwa njia ya maisha
yao ya sala (mafundisho) na kutolea mali zao kwa ukarimu
6) Kuyafikia kwa ukaribu zaidi maisha ya maskini na wahitaji wa aina mbalimbali, hasa wagonjwa,
walemavu, wazee, wanyanyapaliwa, wapweke, yatima, wajane na wengineo.
7) Kuchochea ujasiri wa kumshuhudia Kristo katika maisha ya kila siku. Kwa kufanya hivyo wanawavuta
Wakatoliki kutoshawishiwa na makundi mengine na pia kuwarudisha kundini wale walioanguka.
8) Kuchochea moyo wa ukarimu wa kujitolea na kutoa kwa hali na mali, kwa ajili ya maendeleo ya kiroho na
kimwili ya Kanisa na jamii kwa ujumla.
9) Kuwaalika Mapadre kuhubiri kwenye Makongamano au Mikutano mbalimbali ya Injili ili kuwapa jukwaa
la kufundisha kwa mapana zaidi Neno la Mungu.
10) Kuwapa Wakatoliki fursa ya kutambua Karama zao na kuzitumia kwa kulijenga Kanisa lao.
11) Kuwasaidia Wakriso kuwa wakomavu na hivyo kushinda changamoto za maisha ya kuhimili mateso kwa
ajili ya utukufu wa Mungu.
35
SURA YA KUMI NA MOJA.
11.1.1. Licha ya faida zake mbalimbali na kukubali kwake na Kanisa, mkondo huu unaonekana
1) Baadhi ya kutokuwa na uwiano au kiasi, katika misisitizo ya maombi ya miujiza, maajabu, kuponya
wagonjwa na kufukuza mashetani ( badala ya maisha ya upendo ufuasi na utakatifu.
2) Kutokuwa wanyenyekevu kwa kujiona wanajua Maandiko Matakatifu kuliko wengine nap engine
kupotosha tafsiri halisi ya Maandiko Matakatifu.
3) Baadhi yao kuonekana wanatafuta umaarufu kwa kujisifia matendo ambayo wametendewa na Mungu au
yale ambayo Mungu ametenda kwa kuwatumia wao.
4) Baadhi yao kutopenda kufuata mashauri, maagizo au maongozi ya mapadre wao kwa kujiona wakamilifu na
hata kuwa wepesi kuwahukumu mapadre na waamini wengine na kutopenda kuishirikiana nao.
5) Baadhi yao kupuuza mafundisho ya msingi ya mapokeo ya Kanisa, kama vile nafasi ya Mama Bikira Maria,
Watakatifu, Rosari, Sakramenti ya Kitubio matumizi ya sanamu na vielelezo na hata mafundisho kuhusu
Toharani.
6) Baadhi yao kuchanganya ibada za kikatoliki na ulokole hali inayojionesha katika mahubiri, nyimbo,
misamiati na namna ya kusalimiana.
7) Baadhi yao kupotosha ukweli kuwa kuwa pombe ni dhambi, badala ya kulezea madhara ya pombe au
dhammbi ya ulevi ili kuwataka watu wawe na kiasi ( 1 Tim 4:4; Efe 5:23).
8) Baaadhi yao kutokuwa na kiasi katika utoaji wa mali na muda wao, kwa Mungu/ Karismatiki hata
kusababisha matatizo nap engine matengano katika familia na ndoa zao.
9) Kukazia mno mambo ya uponyaji, na kuona mateso lazima yatokane na laana na mapepo, bila ya kutambua
kuwa, mateso pia huwa ni njia ambayo Mungu huitumia kumuongoza mtu katika kufikia utakatifu.
10) Baadhi yao huzingatia zaidi vionjo vya nje vya kiibada kuliko vya ndani, kama vile kunena kwa lugha na
kuomba kwa makelele, kama ushahidi wa mtu kuwa na Roho Mtakatifu.
36
11.2. Changamoto
11.2.1. Mapungufu hapo juu, pamoja na mengineyo, yanatokana na changamoto mbalimbali. Hizi
1) Kukosekana kwa mwongozo toka kwa wachungaji wa Makanisa Mahalia wanaoifahamu vizuri Karismatiki
Katoliki na nafasi yake katika Kanisa.
2) upungufu wa taarifa na mafundisho sahihi, mintarafu Karismatiki Katoliki. Changamoto hii husababisha
uelewa mbovu na upotoshaji.
3) Matumizi ya mamlaka na nguvu kubwa kupita kiasi kwa baadhi ya Mapadre kupambana, kuwatisha, na
kuwakatisha tama Wakarismatiki. Hali hii huweza kusababisha upotoshaji zaidi unaoweza kuleta mpasuko
katika Kanisa Mahalia.
4) Baadhi ya wachungaji kukosa muda wa kuwa karibu na Wakarismatiki, na hivyo kuwa kama kondoo wasio
na mchungaji. Hali hii huwapa nafasi ya kujiamulia mambo kadiri wanavyojisikia kuwa ni sawa. Matokeo
yake wakati mwingine ni mafarakano ( Mk 14:27).
5) Utamaduni wa mtazamo hasi na mila potofu juu ya magonjwa. Mwelekeo wakuyahusisha magonjwa
mbalimbali na ushirikina, laana, na mapepo. Wanasahau kuwa magonjwa yapo ya kisaikolojia, kibailojia
nay a kurithi.
6) Vikundi / kikundi kutokuwa na mlezi / walezi wenye ufahamu mzuri wa mkondo huu wa maisha ya kiroho
kwa ujumla.
7) Mtazamo hasi wa watu kuwa Karismatiki ni mkusanyiko wa watu wenye shida, ambao wanatafuta majibu
ya haraka.
37
SURA YA KUMI NA MBILI
12.1.1. Kutokana na mapungufu na changamoto kadhaa zilizoanishwa hapo juu, hatua kadhaa
zaweza kuchukuliwa. Lengo kubwa likiwa ni kuleta uelewa mzuri na kuboresha huduma za
1) Mwongozo huu wa Karismatiki Katoliki Kitaifa ufuatwe na uheshimiwe ili utendaji wa mkondo huu
(Karismatiki Katoliki) uendane na mafundisho sahihi ya Imani Katoriki.
2) Mapadre na Makanisa Mahalia wawe karibu na Wakarismatiki. Ukaribu wao utasaidia kujua nini
kinachoendelea na kutoa maelekezo pale taratibu zinapokiukwa.
4) Wahudumu wote, hususani wahubiri, watambulike rasmi na Kanisa. Wawe wamepitia mafunzo maalumu
ya Elimu ya Biblia, Katekisimu ya Kanisa Katoliki, maisha ya Kiroho na Saikolojia katika chuo
kinachotambuliwa na Kanisa Katoliki, kila inapowezekana.
5) Kuwa na msimamo mmoja wa Maaskofu , mintarafu Karismatiki Katoliki kwa kumteua mmoja wao kuwa
Mlezi.
6) Uwepo utaratibu / mwongozo wa namna ya kuendesha shughuli zao, hususani za kiibada na kipaumbele
kipewe kwa adhimisho la Misa Takatifu. Aidha, uwepo ufuatiliaji wa karibu kuhakikisha kuwa utaratibu
unaheshimiwa.
7) Mkazo zaidi uwekwe katika maandalizi na malezi ya Mapadre watarajiwa katika kuwaandaa kukabiliana na
changamoto mbalimbali katika utume wao.
8) Msisitizo katika kuheshimu nafasi ya Mamlaka – funzi, Hierakia, na Baraza la Walei katika Kanisa
Mahalia.
9) Elimu zaidi ya ujumla, mintarafu mafundisho ya Imani Katoliki. Msisitizo katika uelewa wa dhati wa
Katekisimu ya Kanisa Katoliki.
10) Awepo Mlezi Mkuu Kitaifa ( Askofu) au chombo maalumu cha kitaifa kitakachoratibu na kufuatilia
huduma za Kikarismatiki. Aidha, kila jimbo liwe na Mlezi ( Padre) ambaye atafuatilia kwa karibu mkondo
huu kijimbo.
38
11) Semina za malezi endelevu ya ufahamu wa Karismatiki, kijimbo na kiparokia. Hizi zitawasaidia
Wakarismatiki na wale wanaopenda kuwa sehemu ya mkondo huu kutokumbatia mwelekeo wa kilokole na
siasa kali.
12) Wachungaji wafundishwe zaidi kwa njia ya maisha yao na kuwa karibu na mkondo wao, wasikilize
matatizo yao. Umbali na kutojali kwa baadhi ya Mapadre kunawafanya waamini wao kutafuta njia mbadala.
13) Mafundisho na semina za Kikarismatiki vilenge zaidi katika kuwaimarisha waamini, kuwarudisha kundini
Wakatoliki walioanguka na kuwaongoa watu madhehebu mengine.
14) Wanakikundi wapya wapewe mafundisho ya kina mintarafu maana, mwongozo, na utume mzima wa
Karismatiki ndani ya Kanisa Katoliki.
15) Ili kurahisisha ufuatiliaji, ni vema shughuli zote za Kikarismatiki ziwe zinafanyika katika maeneo ya
Parokia.
16) Kuachwa kwa nyimbo na vitendo vinavyowafanya Wakarismatiki wakati mwingine wadhaniwe kuwa
waamini wa madhehebu mengine. Ni muhimu kwao kutambua na kukumbuka daima kuwa wao ni
Wakatoliki, bila kuwachukia au kuwadharau watu wa madhehebu mengine; tukikumbuka kuwa sisi sote ni
watu wa kundi moja chini ya mchungaji mmoja.
17) Waamini waelimishwe kuwa si kila tatizo sugu au ugonjwa usiotibika ni kazi ya shetani / mapepo. Itolewe
Katekesi ya mateso, kifo na ufufuo wake katika muungano wa mateso, kifo na ufufuko wa Kristo.
18) Mkarismatiki aelewe na kuthamini matumizi ya Rozari, Msalaba wenye sanamu ya Yesu na heshima
itolewayo na Kanisa Katoliki kwa Bikira Maria na Watakatifu.
19) Waamini watambue umuhimu wa kuomba na kupokea Baraka kutoka kwa Mapadre wao na siyo wao
kupeana baraka.
1) Kabla ya kuanza mkutano au sala, kiongozi wa Karismatiki awafahamishe waamini hasara na majanga ya
kutaja jina la anayedhaniwa kuwa mbaya wake au mshiriki / mlozi / mchawi wake. Ikitokea akawepo wa
mwelekeo wa kutaja jina la mlozi aondolewe mara moja na kusikilizwa binafsi na Mkarismatiki mwenye
uwezo wa kutunza siri aliyeteuliwa rasmi kushughulikia kesi za aina hiyo.
2) Anayehitaji kuombewa, asali na wanaosali kumwombea, ili pamoja nao nia yake ya uongofu, yaani, kupona
kiroho na kimwili ifanikiwe ( re. Yak 5:13).
3) Nyimbo, Sala, ishara, maneno na vitendo vinavyowafanya waamini wadhaniwe kuwa ni wa madhehebu
mengine viachwe. Nyimbo, Sala (mf. Sala ya Uje Roho Mtakatifu uzieenee nyoyo za waamini wako…..,
Baba yetu…., Salamu Maria….., Atukuzwe Baba….n.k.), ishara ( mf. Ishara ya Msalaba) na matendo mf.
Maadhimisho ya Sakramenti saba na hasa Sakramenti ya Kitubio, Ekaristi na Mpako wa Wagonjwa) ya
Kikatoliki kulingana na maelezo ( Rubrics) ya Liturujia lazima vionekane wazi katika ibada zao. Itumike
39
Biblia Takatifu yenye vitabu vya Deuterokanoni au yenye Imprimatur / “Ichapwe” ikiwa na jina la Askofu
toka Kanisa Katoliki. Biblia zenyewe ni: (1) “BIBLIA TAKATIFU” yenye utangulizi wa Mahashamu
Tarcisiuc J. Ngalalekumtwa, Askofu wa Iringa; (2) “BIBLIA Habari njema kwa Watu Wote yenye
Vitabu vya Deuterokanoni” yenye ikibali ya Mhashamu C.C.Davies, Askofu wa Ngong, Kenye; (3)
“BIBLIA YA KIAFRIKA” yenye ikibali ya Mhashamu Jude Thaddaeus S.Ruwa’ichi OFMcap, Askofu
wa Dodoma; (4) “THE NEW JERUSALEM BIBLE.” Ni muhimu waamini wakati wote kutambua kuwa
wao ni Wakatoliki.
4) Waamini waelimishwe kuwa si kila tatizo lisiloisha au ugonjwa usiotibika chanzo chake ni shetani.
Katekesi ya mateso, kifo na ufufuko wake katika muunganiko na mateso, kifo na Ufufuko wa Kristo,
itolewe ( rejea 7.1.19).
5) Mkarismatiki ajongee daima Sakramenti ya Kitubio / Upatanisho na kuungama dhambi ( rej. 1Yoh 1:8-10)
kwa Padre.
6) Wagonjwa wawaite Mapadre wawaombee na kuwapa Mpako Mtakatifu na Komunyo – pamba ( rej. Yak
5:14-16)
7) Mkarismatiki aelewe na kuthamini matumizi ya Rozari, Msalaba wenye sanamu ya Yesu na heshima
itolewayo na Kanisa Katoliki kwa Bikira Maria ( rejea 7.1.18).
8) Waamini wajue umuhimu wa kuomba na kupewa Baraka kutoka kwa Mapadre wao na si wao kutoleana
baraka
( rejea 7.1.19).
9) Mkarismatiki asichapishe kitabu chochote kuhusu imani Katoliki bila ikibali ya maandishi au ruhusa ya
kuchapwa yaani Imprimatur toka kwa askofu yeyote Mkatoliki.
Ili Utume wa Karismatiki uendelee vizuri, kwa ajili ya kuimarisha imani, upendo, umoja, amani na maendeleo ya
kiroho na kimwili katika Majimbo na baina ya Majimbo Katoliki Tanzania, utaratibu huu uzingatiwe:
1) Kila anayetaka kutoa huduma ya Kikarismatiki ya kuwinga mapepo na uponyaji wa kimijiza, lazima
aonyeshe kwa Askofu wa Jimbo husika barua ya Askofu Mkatoliki inayomruhusu kutoa huduma ya namna
hiyo ( kulingana na maelekezo ya Askofu Mahalia).
2) Kiongozi wa Karismatiki asialikwe kuendesha shughuli za Kikarismatiki ndani ya Jimbo lisilo lake bila
barua au kibali cha askofu wa Jimbo husika.
3) Shughuli za Kikarismatiki katika Parokia zisiendeshwe bila Paroko kuwa na ruhusa ya Askofu inayoruhusu
shughuli hizo kufanyika parokiani mwake ( kwa kadiri ya maelekezo ya Askofu Mahalia).
40
HITIMISHO
Kwa ujumla wake, malengo ya uanzishwaji wa mkondo huu ni mazuri. Tatizo kubwa linakuwa ni katika utekelezaji
wake. Inapotumiwa vema, Karismatiki Katoliki ni chachu nzuri ya imani.
Imewasaidia Wakatoliki wengi kubaki katika imani yao, badala ya kukimbilia katika madhehebu mengine. Utafiti
umeonyesha kuwa ni vigumu sana kumshawishi anayeijua vema na kujiunga mkono Karismatiki Katoliki kulipa
kisogo Kanisa na kuukimbilia ulokole au madhehebu mengine! Kinyume chake, mkondo huu umesaidia sana
kuwarudisha na kuwavuta wengi katika Imani Katoliki. Karismatiki Katoliki inasaidia kuboresha na kuipa liturujia
mvuto zaidi. Kwa ujumla, wana karismatiki wamekuwa mstari wa mbele katika suala zima la utamadunisho.
Ukaribu huu watakiwa kukua na kuongezeka siku kwa siku, ukijengwa katika shina na msingi wa upendo; hata
mkristo afikie kipawa cha ‘kufahamu pamoja na watakatifu wote jinsi ulivyo upana, na urefu, na kimo, na kina; na
kuujua upendo wake Kristo upitao ufahamu kwa jinsi ulivyo mwingi, apate kutimilika kwa utimilifu wote wa
Mungu’ Ni mchakato wa ukaribu utakaojengwa katika ulinganifu wa ongezeko la ufahamu na maarifa ya kumjua
Mungu, na kiwango cha imani.
Utafiti unaonyesha kuwa maeneo ambayo Mapadre wamekuwa karibu nao, Karismatiki Katoliki imefanya vizuri, na
kuwa kweli ‘Upyaisho’ katika Kanisa. Kinyume chake, sehemu ambazo Mapadre wamejitenga nayo na hata kuipiga
vita, madhara yake yamekuwa makubwa katika Kanisa.
Bila shaka, kubwa kuliko yote, ni vurugu na kupelekea mpasuko katika Kanisa (Mk 14:27). Kwa ujumla lengo
msingi la Karismatiki Katoliki ni kuwaelekeza watu waweze kuufikia wokovu. Yote kwa yote, kwa asili Kanisa
zima linategemewa kuwa Karismatiki kwa vile Roho Mtakatifu yu ndani yake, akitenda kazi daima.
41
BIBLIOGHAFIA
1. Centrem Ignatianum Spiritualitatis, Jesuits and the Charismatic Renewal, Vol. XV, Rome 1984.
2. HATI ZA MTAGUSO MKUU WA VATIKANO II
3. KAMATI YA HUDUMA YA KARISMATIKI KATOLIKI TAIFA, Maadili, Dar es Salaam, 2006.
4. Mwongozo wa Karismatiki Katoliki Tanzania, Toleo la Tatu, Dar es Salaam 2006
5. LENGUEJU Alex Victor, Semina za Maisha ya Kiroho: Masomo ya Walimu, Dar es Salaam, 2005.
6. MWAKYANJALA B., Historia ya Upyaisho wa Kikarismatiki Katoliki, Dar es Salaam, 2005
7. NATIONAL CONFERENCE OF CATHOLIC BISHOPS, A Pastoral Statement on the Catholic
Charismatic Renewal, United States Catholic Conference Inc.., Washington, 1985.
42