Katika jina la Yesu Kristo wa Nazareth , Baba wa mbinguni ninakuinulia mkono wangu wa kuume,mimi……………………………………… (taja jina lako). Nitazame Bwana maana nguvu na uwezo wote unatoka kwenye kiti chako cha enzi.kama ilivyo andikwa katika Zaburi ya 62:11-12 “Mara moja amenena Mungu, mara mbili nimeyasikia haya ya kwamba nguvu zina Mungu. Na fadhila ziko kwako ee Bwana, maana ndiwe umlipaye mtu sawa sawa na haki yake” Baba wa mbinguni, ninapokea nguvu kutoka kwako sasa kwa jina la Yesu. Ninatumia nguvu hizi kufuta, kuvunja,kuharibu na kujitenga mwenyewe kutoka kwenye laana zote za maagano yaliyofanywa dhidi yangu.Nina amuru laana zote pamoja na mapatano na mazindiko yaliyo jificha popote dhidi ya maisha yangu kujidhihilisha sasa katika jina la Yesu. Nina amuru moto wa Roho Mtakatifu na damu ya Yesu kuwa dhihilishia wote. Nina ziharibu nguvu zenu wote kwa jina la Yesu.