You are on page 1of 18

JUMUIYA YA MTAKATIFU BAKHANJA

1. MBALI KULE NASIKIA

1. Mbali kule nasikia malaika wa mbinguni, wakiimba wengi


pia wimbo huo juu angani
KIITIKIO: Glo ..........ria, ine........excelsis deo,
Glo ............ria, ine.......excelsis deo.
2. Wachunga tuimbieni sababu ya nyimbo hizo, mwenye
kuimbiwa ni nani juu ya nani sifa hizo.
3. Je, hamjui jambo kuu kuzaliwa mwokozi, habari ya wimbo
huu ndiyo kumshukuru mwenyezi.
4. Kweli nasi twende hima, tufike huko aliko tuone mtoto na
mama tuwasalimie huko.

2. TUMWIMBIE MWANA WA MUNGU

KIITIKIO: Tumwimbie tumwimbie mwana wa Mungu,


tumwimbie tumwimbie mwana wa Mungu × 2

1. Neno alifanyika mwili tukauona utukufu wake


2. Mwana wa Mungu amezaliwa pangoni leo amezaliwa
3. Bwana wa mbingu amezaliwa, mfalme wa mbingu
amezaliwa
4. Yesu Masiha amezaliwa, tukamwabudu amezaliwa
5. Kitoto mpenzi amezaliwa, tukamsalimu, amezaliwa
6. Nyoyoni mwetu amezaliwa na tumpokee, amezaliwa
7. Kwa watu wote amezaliwa, mleta amani amezaliwa

1
3. SAUTI ZA MALAIKA
KIITIKIO: sauti za malaika, zinaimba mbinguni zinaimba
mbinguni × 2

Leo kazaliwa sote tukamwone mwokozi wetu × 2

1. Ndani ya pango Bethlehem, kazaliwa mtoto yesu


2. Tukamwabudu mkombozi, yeye ni mwana wa Mungu
3. Ni siku nyingi tumengoja, matumaini yatimia
4. Kaa nasi yesu tuokoe, utupe mwanga wa Dunia
5. Ni furaha pote duniani, masiha wetu kazaliwa

4. LEO AMEZALIWA
KIITIKIO: leo amezaliwa kwa ajili yetu mwokozi ndiye
Kristu Bwana

1. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, mwimbieni Bwana


libarikini jina lake
2. Tangazeni wokovu siku zote wahubirini mataifa utukufu
wake
3. Mbingu zifurahi nchi ishangilie, bahari na ivume navyo vyote
viijazavyo
4. Mashamba yashangilie na vyote vilivyomo, ndipo miti yote
iimbe kwa furaha

2
EPIFANIA
5. FAMILIA TAKATIFU

KIITIKIO: Familia takatifu ni ile ya kumpendeza Mungu,


(hiyo) ni familia inayodumu katika pendo la Mungu × 2

{familia takatifu inajaa upendo na imara, inajaa amani tele


na Baraka za mwenyezi Mungu} × 2

1. Familia takatifu daima huamua na kutenda yaliyo mema, kama


vile familia ya Mama Maria na Yosefu na Bwana Yesu
2. Familia iliyo takatifu daima inakuwa ni ya mapendo, kama vile
familia ya Mama Maria na Yosefu na Bwana Yesu
3. Familia takatifu daima shetani hataweza kuivuruga, kama vile
familia ya Mama Maria na Yosefu na Bwana Yesu
4. Familia takatifu daima huamini kuwa sala ndiyo kimbilio, kama
vile familia ya Mama Maria na Yosefu na Bwana Yesu
TAFAKARI, TENZI ZA ROHONI NA MASIFU
6. BWANA ANAKUJA

KIITIKIO: Bwana anakuja, anakuja kwetu (anakuja),


anakuja na enzi kutuokoa × 2

1. Tutayarishe mapito yetu Bwana anakuja, anakuja na enzi


kutuokoa
2. Navyo vilima visawazishwe Bwana anakuja, anakuja na
enzi kutuokoa
3. Na kila bonde na lifunikwe, Bwana anakuja, anakuja na
enzi kutuokoa
3
7. NIKIZIANGALIA MBINGU

KIITIKIO: Nikiziangalia Mbingu ni kazi ya vidole vyako, mwezi na


nyota za mbinguni ulizoratibisha wewe × 2

1. Naye mtu ni kitu gani, hata naye ukumbuke?


Naye Binadamu ni nani, hata naye umuangalie?

2. Umemfanya punde mdogo, ni mdogo kuliko Mungu, umemvika


taji yako taji ya utukufu na heshima.

3. Umemtawaza juu ya kazi, ni kazi ya vidole vyako, umeviweka vitu


vyote chini ya miguu yako Ee Bwana

8. UTUKUFU NA UKUU
KIITIKIO: Utukufu na Ukuu una yeye Bwana, hata milele na milele
×2
1. Ee mwana Kondoo, astahili kupokea enzi na utajiri
2. Ee mwana Kondoo, astahili kupokea pia heshima
3. Ewe Mungu wangu, mpitie mfalme hukumu pia na haki yako
4. Atawaamua, atawaamua watu wako kwa haki

9. AMKA KINANDA
KIITIKIO: Ee Mungu wangu, moyo wangu u thabiti, nitaimba,
nitaimba, nitaimba zaburi × 2
Amka ewe kinanda, amka ewe kinubi, nitaamka alfajiri
nitamuimbia Bwana × 2
1. Ee Mungu nitakushukuru kati ya watu, nitakuimbia zaburi kati ya
mataifa

2. Kwa maana fadhili zake ni za milele, na uaminifu wako hata juu


mawinguni

4
10. BWANA NDIYE MCHUNGAJI WANGU
KIITIKIO: Bwana ndiye mchungaji wangu, Bwana ndiye mchungaji
wangu, sitapungukiwa na kitu, sitapungukiwa na kitu, sitapungukiwa
na kitu × 2
1. Bwana ndiye mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu, katika malisho
ya majani mabichi hunilaza kando ya maji ya utulivu huniongoza
2. Hunuhuisha nafsi yangu na kuniongoza katika njia za haki kwa ajiri ya
jina lake, nijapopita kati ya bonde la uvuvi wa mauti sitaogopa
mabaya.
3. Waandaa meza mbele yangu, machoni pa watesi wangu, umenipaka
mafuta kichwani pangu na kikombe changu kinafurika.
4. Hakika wema na fadhili zitanifuata siku zote za maisha yangu maisha
yangu, nami nitakaa nyumbani mwa bwana milele

11. MPIGIENI MUNGU MAKELELE


KIITIKIO: Mpigieni Mungu kelele za shangwe, nchi yote imbeni
utukufu wake, tukuzeni sifa zake Mungu Mkuu
Mwambieni Mungu , matendo yako yanatisha kama nini, tukuzeni sifa
zake Mungu Mkuu × 2
Nchi yote itakusujudia na kukuimbia, naam, italiimbia jina lako njoni. Njoni
tazameni matendo ya Mungu, kageuza bahari kuwa nchi kavu, katika mto
walivuka kwa miguu.
Mwambieni Mungu, matendo yako yanatisha kama nini, tukuzeni sifa
zake Mungu Mkuu × 2
Huko ndiko tulikomfurahia, mtawala milele, naam atawala kwa uweza wake
njoni, njoni sikieni ninyi wenye kumcha, nami nitatangaza alichonitendea
na ahimidiwe Bwana Mungu Mkuu.
Mwambieni Mungu, matendo yako yanatisha kama nini, tukuzeni sifa
zake Mungu Mkuu × 2

5
12. KARIBU MOYONI MWANGU
KIITIKIO: karibu moyoni mwangu (Bwana) karibu nakukaribisha
(sana), karibu moyoni mwangu karibu karibu Bwana × 2.
1. Karibu moyoni mwangu, karibu uungane nami, karibu moyoni
mwangu karibu karibu Bwana.
2. Unipe uzima wako, inipe tumaini lako, karibu moyoni mwangu
karibu karibu Bwana.
3. Uniimarishe Bwana, katika njia yenye haki, karibu moyoni
mwangu karibu karibu bwana.

13. HIVI NDIVYO WOTE WENYE KUMCHA BWANA

KIITIKIO: hivi ndivyo wote wenye kumcha Bwana


watakavyobarikiwa naye

1. Amchaye Bwana atasitawi, kama mwerezi wa lebanoni


2. Heri Yule amchae Bwana na kupendezwa na amri zake.
3. Wazao wake watakuwa hodari, kizazi cha waadilifu kitabarikiwa
4. Mwenye haki atakumbukwa milele, pembe yake itakuzwa milele.

14. ZAENI MATUNDA MEMA


KIITIKIO: Bwana akiyapokea, yatabarikiwa vyema, zaeni
matunda mema, zaeni ya heri.
1. Zaeni matunda mema, zaeni matunda yale, zaeni yenye Baraka
zaeni ya heri
2. Safisha mwenendo wako, safisha matendo yako, safisha na bwana
Yesu, safisha yote.
3. Fanyeni kazi kidugu, fanyeni kazi kwa bidii, fanyeni kazi na
Bwana Yesu, fanyeni wote.
4. Tolea matunda yako, pamoja na moyo wako, naye Bwana Mungu
wako atakubariki.

6
5. Baraka za Mungu Baba, Baraka za Mungu mwana na za Roho
mtakatifu ziwe nanyi nyote.

15. HUO NDIYO NI MWANZO

KIITIKIO: huo ndio ni mwanzo, wa ufalme wa Mungu.

1. Umpende Mungu kwa moyo wote, maana ndiye Baba yako


2. Umtendee mwenzako, upendavyo kutendewa wewe
3. Ujikane kila siku, uchukue vema msalaba wako
4. Heri ukiwa masikini moyoni, maana ufalme wa mbingu ni wako
5. Heri ukiona huzuni maana utatulizwa
6. Heri ukiona njaa na kiu ya kupata utakatifu, maana utashibishwa.
7. Heri ukiwa na huruma maana utahurumiwa

7
BIKIRA MARIA:

16. ISHARA KUBWA IMEONEKANA MBINGUNI


KIITIKIO: Ishara kubwa imeonekana Mbinguni × 2

Mwanamke aliyevikwa juu(pia) na mwezi chini ya miguu yake, na


taji la nyota kumi na mbili juu ya kichwa chake × 2

1. Tufurahishie sote katika Bwana, tunapoadhimisha sikukuu kwa


heshima ya Bikira Maria.
2. Mataifa wafurahia kupalizwa kwake mbinguni/ na wanamsifu
mwana wa Mungu.
3. Atukuzwe Baba na Mwana na roho mtakatifu/kama mwanzo na
sasa na siku zote na milele Amina

17. SISI WANA WA DUNIA


KIIITIKIO: Sisi wana wa Dunia tukumbuke maneno aliyosema
Bikira Maria, alipowatokea watoto wa Fatima, Lucia, Francisi na
Yasinta. Alisema tusali, tusali Rozari, tupate amani. Na tuwaombee,
wale wakosefu, wasio na mwombezi. Na wasio mwamini yesu
mwokozi wamuamini ili waokoke.

1. Mama yetu anahuzunishwa sana, na matendo yetu maovu, anajua


adhabu yetu ijayo, hivyo anaona huruma sana.
2. Atusihi tuache dhambi kwa dhati, tuache kumkosea Yesu,
tuyatubu makosa yetu yote ili BWANA atupatie huruma.

18. TUNAKIMBILIA ULINZI WAKO

Tunakimbilia ulinzi wako mzazi mtakatifu wa Mungu, usitunyime


tukiomba katika shida zetu, utuokoe siku zote kila tuingiapo hatarini,
ewe Bikira mtukufu mwenye Baraka. Amina

8
19. NIONGOZE VEMA MARIA MWEMA
1. Nahangaika hapa duniani maisha hayana furaha, najua wazi hapa
si nyumbani bali njia ya kupita.
KIITIKIO: niongoze vema maria mwema, bondeni huku niliko,
nifike kwa usalama, mbinguni kwa Yesu mwanao.
2. Vita na shori vyote vyanisonga, mashaka mengi yanijia mwili na
roho havina kinga hatari imezidia.
3. Mama Maria ndiwe jibu langu hapa safarini unisaidie uniombee
kwa mwanao Yesu anikinge anilinde.
4. Kwa kuwa Yesu ni mwokozi wangu nakusihi Mama, nakusihi
sana, uzifikishe kwake shida zangu anionee huruma.
5. Kumbuka Mama, Yesu alisema, Mama yangu mwema, nawe
yohana huyo ndiye Mama, huyo ndiye Mama yako.

20. EE MAMA YETU MARIA


KIITIKIO: Ee mama yetu Maria twaomba sana Ee Mama
usituache gizani kwa mwanao tuombee × 2
1. Mama yetu Maria, utusikilize sisi wana wako tunaosumbuka
2. Maisha yetu Mama hayana furaha, tujaze neema, tupate faraja
3. Utuombee kwake mwanao mpendwa, atutie nguvu tushinde maovu
4. Dunia ina giza, dunia ngumu bila nguvu yake hatuwezi kitu
5. Tuombee Maria, tuombee Mama, ili wanawako tufike mbinguni
KWARESMA
21. NITAONDOKA
KIITIKIO: Nitaondoka nitaenda kwa Baba yangu (nakumwambia),
Baba Baba nimekosa juu ya mbingu na mbele yako × 2
1. Tufuate mfano wa mwana mpotevu, alipoamua makosa yake
alisema
2. Tufuate mfano wa Simon Petro, aliyemkana Bwana Yesu naye
akatubu

9
3. Ee Mungu wangu nisaidie mimi, ninapofahamu makosa yangu
nami nisamehe

22. ASIREGEE MOYOWE


1. Asiregee moyowe asitoke machozi, akikumbuka munguwe kwa
yake makombozi. Mtoa roho msalabani mtakatifu mwenyewe, kwa
sababu kupenda ni nani mfunga moyowe.
2. Bustani mle Gethsemani, amwomba Mungu Baba, je Mungu amtu
ana nini nguvu zake ni za haba Bwana waziona dhambi za
Binadamu, mwili wako umetona kama jasho la damu.
3. Salamu rabi salam anena Yuda mbaya, mwenye moyo wake
mgumu am’busu pasi haya. Aliwaambia basi nitakaye m’busu
ndiye mtwaeni na kwa upesi Yuda nani ni siye.
4. Yuda nani siyo yeye aliyetenda dhambi, tukimkosa Mungu Baba
kumdharau naye Mama, tukimsikitisha roho tu, vipofu kama Yuda
tunapata neema yake itokayo kwake Yesu.

23. HUO NI MSALABA


KIITIKIO: huo ni msalaba uliotuokoa twende tukauabudu kwa
heshima

1. Msalaba mtakatifu kwa nia twakusifu wewe ukombozi wetu


wafuta dhambi zetu
2. Uzima tunda lako matumaini kwako furaha na amani twaomba
msalabani
3. Ee Yesu mkombozi na pia kwa msalaba wako utupe neema zako

24. INGEKUWA HERI


KIITIKIO: ingekuwa heri leo msikie sauti yake, msifanye
migumu mioyo yenu × 2
1. Njoni tumwimbie tumfanye shangwe mwamba wa wokovu wetu,
tuje mbele zake kwa shukrani, tumfanyie shangwe kwa zaburi.

10
2. Njoni tuabudu tusujudu, tupige magoti mbele za Bwana
aliyetuumba. Kwa maana ndiye Mungu wetu, na sisi tu watu wa
malisho yake, na Kondoo za mkono wake.
3. Ingekuwa heri leo msikie sauti yake, msifanye migumu mioyo
yenu, kama vile huko meriba/kama siku ya masa jangwani, hapo
waliponijaribu Baba zenu, wakanipima wakayaona matendo
yangu.

25. KWELI NI HUZUNI

1. Kweli ni ajabu, ya kifo chake Bwana Yesu, kilikuwa cha maumivu


akasema moyoni namaliza kazi kwa huzuni
KIITIKIO: kweli ni huzuni kwa kifo chake Bwana Yesu,
alivyowambwa pale juu mtini, akasema moyoni
namaliza kazi kwa huzuni.
Akalia kwa huzuni, hata mwisho alikufa, pale juu msalabani
akakata roho kwa huzuni × 2

2. Kweli ni ajabu, kwa kifo chake Bwana Yesu, kilivyokuwa cha


maumivu, alisema moyoni, namaliza kazi kwa huzuni
3. Kweli miujiza, siku ile ya mateso yake, giza likafunika nchi,
tetemeko la nchi ikawa mashaka kwa watu wote.
4. Yesu alisema, Na ninyi mtateswa hivi, nami nitakuwa na ninyi,
hata muwe kifoni, nitawafufua mautini.

26. BWANA KAMA WEWE UNGEHESABU MAOVU

KIITIKIO: Bwana kama wewe ungehesabu maovu yetu// nani


angesimama, nani angesimama, nani angesimama
mbele yako × 2
1. Lakini kwako kuna msamaha, ili wewe uogopwe nimemngoja
Bwana Roho yangu na neno lake nimelitumaini.
2. Nafsi yangu inamngoja Bwana, kuliko walinzi waingojavjo
asubuhi, naam walinzi waingojavyo asubuhi.
11
27. JIWE WALILOKATAA WAASHI
KIITIKIO: Jiwe walilolikataa waashi (ni jiwe imara) limekuwa
Jiwe kuu la pembeni (la pembeni) limekuwa
jiwekuu La pembeni × 2
1. Bwana Mungu ndiye aliyefanya jambo hili, nalo ni la ajabu sana
kwetu
2. Hii ndiyo siku aliyofanya Bwana Mungu.
3. Utuokoe sisi sote Ee Bwana Mungu, tuishangilie kwa furaha
4. Abarikiwe ajae kwa jina lake Bwana, aleta Baraka toka mbinguni
5. Wewe ndiwe mungu wangu name nakushukuru, nitakutukuza Ee
Mungu wangu
6. Mshukuruni mwenyezi Mungu kwakuwa ni mwema, na fadhili
zake ni za milele.

28. ALELUYA KRISTU PASAKA WETU


KIITIKIO: Aleluya aleluya aleluya aleluya aleluya aleluya
aleluya×2
1. Kristu pasaka wetu amekwisha kutolewa sadaka.
Basi na tuifanye karamu katika Bwana.
MIITO
29. NIMTUME NANI
KIITIKIO:Nimtume nani, (unitume mimi nitume Bwana × 2)
Nitakwenda kutangaza neno lako wewe mataifa wasikie
wakufuate wewe unitume mimi nitume bwana.
1. Ungali tumboni mwa Mama yako nilikutakasa/ nalikuita ili uwe
mtume wangu.
2. Utakwenda kutangaza neno langu/ usiogope kwa ajili ya hao.

12
30. BWANA NIMEAMUA MIMI
KIITIKIO: Bwana nimeamua mimi, kufanya kazi yako × 2
Nitaingia shambani, shambani mwako Bwana,
nijalie Bwana nivune mavuno mema × 2
NAMNA YA KUSALI ROZALI YA HURUMA YA MUNGU
Tumia rozari ya kawaida.
Anza “baba yetu.......... salamu maria ............ × 3 “nasadiki ............

Kwenye punje kubwa Sali hivi:-

Baba wa milele, nakutolea mwili na damu, roho na umungu wa


mwanao mpenzi sana bwana wetu yesu kristu, kwa kulipiza dhambi
zetu na dhambi za dunia nzima.

Kwenye punje ndogo 50 Sali hivi:-

K. kwa ajili ya mateso makali ya bwana wetu yesu kristu,

W. utuhurumie sisi na dunia nzima.

Mwisho Sali:

Mungu mtakatifu, mtakatifu mwenye enzi, mtakatifu uishie milele


utuhurumie sisi na dunia nzima. × 3

LITANIA YA HURUMA YA MUNGU

Bwana utuhurumie,

Kristu utuhurumie,

Bwana utuhurumie,

Kristu utusikie,
Kristu utusikilize

13
Baba wa mbinguni Mungu Utuhurumie

Mwana mkombozi wa dunia Mungu, “

Roho mtakatifu Mungu, “

Utatu mtakatifu Mungu mmoja “

Huruma ya Mungu iliyo sifa kuu ya muumba wetu Tunakutumainia

Huruma ya Mungu iliyo kilele cha ukamilifu wa mwokozi wetu “


Huruma ya Mungu iliyo upendo usiopimika wa Roho mtakasa “
Huruma ya Mungu fumbo lisilofahamika la utatu mtakatifu “
Huruma ya Mungu iliyo ishara ya uwezo mkuu wa Mungu mwenyezi “
Huruma ya Mungu iliyofumbuliwa katika kuziumba Roho za Malaika
mbinguni Tunakutumainia
Huruma ya Mungu iliyotuumba na kutuamuru tuwepo bila kutokana na
chochote “
Huruma ya Mungu inayotujalia maisha ya kutokufa “
Huruma ya Mungu inayotukinga na adhabu tunazostahili “
Huruma ya Mungu inayotuinua tutoke katika taabu, unyonge na
maumivu ya dhambi zetu “
Huruma ya Mungu inayotufanya wenye haki katika neno aliyejifanya
mtu “
Huruma ya Mungu inayofurika kutoka katika majeraha ya Kristu “
Huruma ya Mungu inayobubujika kutoka ndani ya moyo mtakatifu wa
Yesu “
Huruma ya Mungu iliyotupatia Bikira Maria mtukufu awe kwetu
“Mama wa huruma” “
14
Huruma ya Mungu iliyoonyeshwa katika kuanzishwa kanisa katoliki “
Huruma ya Mungu inayopatikana katika mafumbo ya Sacramenti
takatifu “
Huruma ya Mungu inayotolewa kwa wanadamu wote kwa njia ya
Sacramenti ya ubatizo na kitubio “
Huruma ya Mungu inayotolewa katika sakramenti ya Ekaristi na
Upadrisho “
Huruma ya Mungu inayoonyeshwa kwetu pale inapotuita na kutuingiza
katika kuwatakatifuza wenye haki “
Huruma ya Mungu inayotimilika katika ukamilifu wa watu watakatifu “
Huruma ya Mungu chemchemi ya afya kwa wagonjwa na wote
wanaoteseka “
Huruma ya Mungu iliyofaraja ya wote wenye uchungu moyoni “
Huruma ya Mungu iliyotumaini la Roho zinazosumbuliwa na mkato wa
tamaa “
Huruma ya Mungu iliyo mwenzi wa daima na popote wa watu wote “
Huruma ya Mungu inayowahi kutuletea neema zake “
Huruma ya Mungu iliyo amani kwa wanaokufa “
Huruma ya Mungu iliyo burudisho na faraja yao marehemu toharani “
Huruma ya Mungu iliyo furaha mbinguni kwa watakatifu wote “
Huruma ya Mungu iliyo taji la watakatifu wote “
Huruma ya Mungu chemchemi ya miujiza isiyokauka “

15
Mwanakondoo wa Mungu uliyetuonyesha huruma yako kuu katika
kuikomboa Dunia kwa msalaba wako mtakatifu. UTUSAMEHE EE
BWANA
Mwanakondoo wa Mungu unayejitolea kwetu kwa mapendo na huruma
katika kila adhimisho la sadaka ya misa takatifu UTUSIKILIZE
BWANA
Mwanakondoo wa Mungu unayeondoa dhambi za dunia kwa njia ya
huruma yako isiyo na mwisho UTUHURUMIE
V. Bwana utuhurumie
R. Kristu utuhurumie
W.Bwana utuhurumie
V.Huruma anana za Bwana zi juu ya kazi zake zote
R. Huruma za Bwana nitaziimba milele.

TUOMBE
Ee mungu uliye na huruma isiyo na mwisho, na hazina za wema na
upendo wako hazina mipaka. Tunakusihi ututazame sisi watu wako
huku duniani na kutuongezea huruma yako tena na tena, ili itusaidie
tusije tukakata tama hata mara moja, hadhuru tukumbane na majaribu
makubwa kiasi gani, bali tuweze daima kuzielekea na kuzishika amri
zako. Kwa matumaini na kutimiza mapenzi yako matakatifu, ambayo
ndiyo huruma yenyewe. Tunaomba hayo kwa njia ya bwana wetu yestu
kristu mwanao, mfalme wa amani na huruma, aishie na kutawala nawe,
na roho mtakatifu, kwa pamoja mkituonyesha huruma, daima na milele.
AMINA

16
ENYI WATU WOTE PIGENI MAKOFI – Na S. B. Mutta
Enyi watu wote pigeni makofi, enyi watu wote pigeni makofi, mpigieni
bwana mungu wetu, mshangilieni kwa vigelegele × 2
1. Enyi watu pigeni makofi, mpigieni mungu, pigeni kelele kwa sauti
ya shangwe
2. Kwa kuwa bwana aliye juu ni mwenye kuogopwa, ndiye mfalme
mkuu wa dunia yote
3. Bwana atawatiisha watu wote wan chi yetu na mataifa chini ya
miguu yake.
BWANA NI NURU YANGU – Na Deo Mhumbira
Bwana ni nuru yangu, na wokovu wangu, nimwogope nani, bwana
ni ngome ya uzima wangu, nimhofu nani × 2
1. Watesi wangu na adui zangu, walijikwaa wakaanguka, jeshi
lijapokupigana name, moyo wangu, hautaogopa.
2. Vita vijaponitokea, hata hapo, nitatumaini, neon moja nalitoka kwa
bwana, nalo ndilo nitalitafuta.
3. Nikae nyumbani kwa bwana, siku zota, za maisha yangu,
niutazame uzuri wa bwana, na kutafakari, hekaluni mwake.
EE BWANA TWAKUOMBA UPOKEE – Paschal F. Mwarabu
Ee bwana twakuomba upokee vipaji vyetu × 2
Hivyo vyote ni mali yako, tumepata kwa wema wako pokea × 2
1. Mkate divai twakutolea, twakuomba baba upokee.
2. Mawazo pia matendo yetu, twakuomba baba upokee
3. Sadaka zetu uzibariki, pia nasi baba tubariki.

17
AULAYE MWILI WANGU – Na Stan Mujwahuki
Aulaye mwili wangu, na kuinywa damu yangu (asema bwana)
hukaa ndani yangu name hukaa ndani yake × 2
1. Aulaye mwili wangu, na kuinywa damu yangu ana uzima wa
milele.
2. Njoni enyi wenye njaa, njoni enyi wenye kiu, njoni kwangu
niwashibishe.
3. Aniaminiye mimi, na kuyashika nisemayo, nitamfufua siku ya
mwisho.
4. Mlapo chakula hiki, mnywapo kikombe hiki, mwatangaza kifo cha
bwana.
5.

18

You might also like