Professional Documents
Culture Documents
NGAZI YA SEKONDARI
IDARA YA ELIMU
1
••
•
•
UTANGULIZI
Muhtasari huu ni toleo la Tanzania Union la Mtaala wa kujifunza Biblia (2001). Ni kozi ya
Biblia ya muda wa miaka kumi na tatu iliyobuniwa kukidhi mahitaji ya masomo na vipindi vya
dini kuanzia Shule za awali, hadi elimu ya Sekondari (Kidato cha nne). Kidato cha tano na cha
sita watajifunza mada hizi hizi lakini kwa upana zaidi.
Kozi itafundishwa katika mfumo wa kuendelea kwa mzunguko kama pia. Maana yake ni
mviringo unaoendelea, kwa sababu mada zinazofundishwa hutegemeana moja kwa nyingine na
hurudiwa katika ngazi tofauti kwa kujifunza kwa undani na upana zaidi.
Mtaala huu umekusudiwa kutumika katika kufundisha vijana Waadventista wanaosoma katika
Shule zisizo za kanisa. Kiuhalisia ni vigumu kutoa wakufunzi wa kutosha kufundisha wanafunzi
katika shule hizo zisizo za kanisa maana ni nyingi, inashauriwa Mwalimu / Mkufunzi aunganishe
Madarasa, mfano darasa la 1 na 2, 3 na 4, 5, 6 na 7; pia kidato cha 1 na 2, na 3 na 4.
Inaposhindikana kukawa na mwalimu mmoja basi aunganishe wanafunzi wote wa Sekondari na
atumie taaluma yake kuhakikisha kuwa wanafunzi katika level zote wanamuelewa.
Sehemu ya kidato cha tatu na cha nne cha muhtasari huu kinakamilisha mada ambazo
zimelengwa mahsusi kuwaandaa wanafunzi kwa ajili ya mitihani ya Taifa ya somo la Biblia
(Bible Knowledge).
• Maandiko Matakatifu ndicho kiwango kikamilifu cha kweli hivyo yapaswa kupewa nafasi
ya juu katika Elimu. “kupata elimu yenye thamani inayoligana na jina, lazima tupokee
ufahamu wa Mungu Muumbaji na Kristo Mkombozi kama walivyofunuliwa katika Neno
takatifu” (Education uk.27).
• Mtaala katika Shule zetu ni lazima kiini chake kiwe ni Mungu, Biblia ikiwa ndicho kitabu
cha mwongozo katika kazi ya Elimu.
• Muhtasari umejaribu kuingiza mambo yahusuyo maadili na thamani za Kiafrika kwa
kuchukua mfano na vielelezo vya mambo hayo kutoka jamii mbalimbaliza kiafrika.
• HOJA: “Mlee mtoto katika njia impasayo, naye hataiacha aata atakapokuwa Mzee”
(Methali 22:6).
- Ni kazi ya Wazazi wanaowajibika na kujali, shule makanisani na walimu kufanya kazi
kwa mshikamano katika juhudi ya kutoa mafundisho sahihi ya Kikristo kwa ajili ya
vijana. Mafundisho yatakayowawezesha kuwa watendakazi pamoja na Kristo na
kuwaandaa kwa marejeo yake mara ya pili.
2
“kuwa na jeshi la namna hiyo la watendakazi kama vijana wetu, walifunzwa vyema,
inawezekana kueleza jinsi ya uharaka wa ujumbe wa mwokozi aliye sulubiwa,
aliyefufuka na anayekuja haraka unavyoweza kupelekwa kwa ulimwengu “Ellen
White 1943 uk 555.
MALENGO:
Lengo la kwanza na la mbele kabisa kwa mwalimu lapaswa kuongoza maisha ambayo yatafaa
kuwa vielelezo vya kanuni za Biblia zifundishwazo kwa wanafunzi. Kila mada yapaswa
imalizike kwa fundisho la Kiroho.
Wanafunzi wataweza
3
••
•
•
f) Kufahamu kwamba kusudi la ibada ni kuwa tunafanana zaidi na yeye aliyetuumba.
g) Kuwa na uzoefu wa mafundisho Makuu 28 ya Waadventista Wasabato.
h) Kufahamu asili ya uasi uliopo katika ulimwengu, mabadiliko yaliyoletwa na uasi huu kwa
watu na tiba yake ipatikanayo katika kumjua Mungu kama kweli ilivyo. Kweli hii ni
uwezo wa Mungu (Warumi 1:16).
i) Kujifunza kwamba kushiriki imani yao na wengine (kushuhudia) ni matokeo ya kawaida
ya ufahamu wao kwa Mungu na kumjua Mungu.
j) Kutambua kwamba, Mungu ambaye ameumba Ulimwengu huru amewapa upendeleo na
Madaraka ya kufanya chaguzi zao wenyewe. Hivyo hudhuhirisha kuwa wanaweza au
hawawezi kupewa dhamana ya Uhuru na Uzima wa Milele.
k) Kutambua ujumbe wa afya kama sehemu muhimu ya mafundisho makuu ya imani ya
Waadventista Wasabato.
l) Kufahamu asili ya mtu kuanguka na kurejeshwa kwa sura ya Mungu (Yoh 3:16).
m) Kufahamu kuwa kila andiko lenye pumzi ya Mungu lafaa kwa mafundisho na maisha
yetu ya kila siku.
MBINU ZA UTENDAJI
Mbinu za kufundisha daima zitakuwa tofauti kulingana na Mwalimu, mada, kundi la Wanafunzi
na daraja lao. Hebu angalia mifano michache ya mbinu ambayo kwa kawaida hutumiwa na
Walimu wengi na kwa viwango flani zimeonekana kuwa zenye kufaa.
A: Mafunzo ya njia wazi: Nikanuni ya kufundisha ambayo mwalimu ni mtoaji mkuu wa habari.
Mwalimu hupitisha kweli kwa mwanafunzi katika njia ya wazi sana kadri iwezekanavyo.
Kinyume na mbinu ya madhara, mbinu ya njia wazi, mwalimu anahakikisha kuwa wakati wa
kutoa mafundisho kunakuwepo na muuingiliano (interaction) – kati ya mwalimu na mwana funzi
ambao utahusisha maswali na majibu, kuangalia upya, mazoezi na usahihishaji wa makosa ya
mwanafunzi.
B. MCHEZO WA KUIGIZA
4
Huu ni mfano wa mafunzo ambapo wanafunzi katika darasa huchaguliwa kuigiza hali
wengine huangalia kwa makini na kuchukua kipengele mahsusi cha mchezo wa
kuigizailiwajibu kama mwalimu alivyoelekeza. Mchezo wa kuigiza kama haukuratibiwa
vizuri unaweza kuishia kuwa maburudisho zaidi kuliko mfano wa mafundisho. Kwa
maneno mengine, wanafunzi wanaweza wasifikie ufahamu uliotarajiwa na mwalimu
kushindwa kutimiza malengo yaliyo kusudiwa.
Mchezo wa kuigiza humweka mwanafunzi katika hali halisi ya matukio au shughuli. Kwa
mfano wanaweza kuigiza hadithi ya Yusufu na ndoto zake, Wanawali kumi, Mwana
mpotevu nk.
- Itakuwa rahisi Kwa wanafunzi wazito kujifunza, kuelewa mada ngumu na kuumba
picha katika akili zao ambayo kamwe hawataisahau kwa urahisi.
- Huwasaidia mtu mmoja mmoja kugundua matatizo ya watu, hisia, mitazamo, thamani
na mkakati ya kutatua tatizo.
- Katika ulimwengu wao wa jamii, wengine watakuwa wamesaidiwa kupata kama mtu
binafsi, stadi zao za vipaji kama waigizaji ambavyo vyaweza kutokea kuwa kazi
baadaye.
C. MASIMULIZI YA VISA
Hii ni mbinu ya kufaa sana katika ufundishaji wa Biblia hasa kwa madarasa ya Shule za
awali na ngazi ya Msingi. Hivyo Mwalimu sharti afanye maandalizi ya kina ya mada, na
kupanga vizuri ili kufanya kisa kuwa hai na cha kusisimua. Matumizi ya lugha rahisi na
vielelezo vilivyochukuliwa kutokana na maisha na shughuli za mahali palepale ni
muhimu sana. “kutoka kinacho fahamika kwenda kwa kisichofahamika”.
Mara chache kwa visa vilivyo rahisi mwalimu angeweza kuwapa wanafunzi kazi ya
kusoma kutoka katika Biblia zaidi kisha kuelezea kisa kwa Wanafunzi wengine darasani.
D. “KAZI MRADI”
“Kazi mradi” zinaweza kufanywa na mtu mmoja mmoja au katika vikundi. Hapa
mwalimu sharti atoe maelekezo sahihi yanayoeleweka akieleza ni nini cha kufanya.
5
••
•
•
• Kwaya.
Zote hizi ni shughuli zinazoweza kutajirisha uzoefu wa Kiroho, na ili kufanikiwa mwalimu
atapaswa kuwa na utaratibu na mipango inayofaa.
E. MIJADALA NA PANALI
Itafaa zaidi ikiwa madaraja ya mijadala au Paneli yatafanyika baada ya kusoma mada
iliyokusudiwa kwa ajili ya maandalizi, ni muhimu kua mwalimu atoe maswali bayana ya mjadala
na asimamie vikundi vya mjadala.
F. UCHORAJI NA UFINYANZI
Mbinu ya uchoraji picha za rangi au ufinyanzi wa mambo ni ya kufaa sana naya kupendeza, hasa
kwa wanafunzi wa shule za awali na za msingi.
6
3) Fundisha fungu la kukariri kila somo na ni vizuri likawa fupi na wazi kulingana na umri
wa watoto unaowafundisha. Kumbusha kila mara mafungu ya kukariri
waliyokwishajifunza, wasaidie wakariri kwa ufasaha kabisa.
4) Waulize maswali wanafunzi wako na wewe pia uwape nafasi wakuulize maswali,
kuwapima iwapo wamelifahamu somo ulilofundisha vizuri.
5) Somo lifundishwe kwa lugha iliyo rahisi kwa watoto kuelewa.
6) Omba Mungu akuongoze na kukupatia hekima ya kujua namna ya kulitoa somo na
kulifundisha; nakukmbusha tena kila mara kabla ya kuanza somo anza kwa maombi ili
masomo haya yatakaswe kwa ajili ya maisha matakatifu ya mwalimu mwenyewe na
wanafunzi.
KIDATO CHA KWANZA MUHULA WA KWANZA
MALENGO:
Wanafunzi wanatakiwa kufahamu vitabu vya Biblia, 39 Viko katika Agano la kale na 27
Agano jipya.
Neno la Mungu-Biblia ni la pekee sana, Biblia ni kitabu kilichopendwa sana kuliko vitabu
vingine, lakini pia kimechukiwa sana, watu wamekufa kwa sababu ya Biblia, wengine
wameua na kuuawa kwa sababu yake, vita vimeamshwa kwa ajili ya Biblia. Biblia ndio
humdhihirisha Mungu alivyo, ni Maandiko matakatifu, yaliyovuviwa na Roho wa Mungu
(2.Tim3:16)
MALENGO:
7
••
•
•
1. mwanafunzi ataweza kuelezea dunia/ulimwengu ulivyoumbwa akitofautisha na
dhana za uibukaji.
2. Mwanafunzi aelewe uumbaji wa Mungu na kumtambua Mungu kama muumbaji
wa kila kitu na kuwa wakili mwaminifu kwa uumbaji wake.
• Uumbaji wa mwanadamu, mwanamume na mwanamke (mtu)
(Creation of the universe and of a man)
• Asili ya mwanadamu
• Kuanguka kwa mwanadamu- dhambi yaingia ulimwenguni (The beginning of sin and
suffering)
• Mpango wa Mungu kwa mwanadamu aliyeanguka
• MWANZO 1-3, PATRIARCHS AND PROPHETS UK 2, NA 58-61
MALENGO:
1.Mwanafunzi atatambua kwamba mshahara wa dhambi ni mauti na kifo cha Yesu ndio
njia ya kutukomboa.
2.Mwanafunzi ataelewa kwamba kufufuka kwa Kristo kulileta tumaini kuwa anazo nguvu
dhidi ya kifo na atatufufua atakaporudi mara ya pili.
MALENGO:
1.Mwanafunzi ataweza kujua umuhimu wa kuwa mwaminifu katika matoleo kwa Mungu.
8
• Kaini na Habili- sadaka inayokubalika Zaka na sadaka –uwakili wa umilikaji mali.
• Utoaji sadaka wa mapokeo kwa mababu na kwa Mungu
• MWANZO 4:1-16, PATRIARCHS AND PROPHETS UK 71-79
• Mwanafunzi afahamu kwamba mfumo wa kutoa sadaka za kuteketezwa ulitolewa na
Mungu mara baada ya mwanadamu kuanguka na kufukuzwa bustanini.
• Kaini alikuwa amefundishwa kuwa damu ya mwana wa Mungu ndiyo ingesafisha dhambi
zake. Aliamua kuwa mkaidi.
• Wakazi wa madunia mengine walimwangalia Kaini akitenda dhambi ya kuua!! Je
ukitambua kwamba viumbe vya mbinguni vinakuangalia je jambo hili laweza kukusaidia
usifanye dhambi?
MASWALI:
2.Nini madhara ya uzinzi? Je janga la ukimwi limekuwa na matokeo gani katika jamii.
9
••
•
•
MALENGO:
2.Mwanafunzi ataweza kuakisi uhalisia wa Maisha ya Esau na Yakobo katika Maisha yake.
10
•
Isaka amuoa Rebeka
Familia ya Isaka, Esau na Yakobo.
Jukumu la wazazi wa mapokeo ya kiafrika katika ndoa za vijana wao na binti zao
MWANZO 23:1-24, PATRIARCHS AND PROPHETS UK 171-176
Isaka alikuwa na Umri wa miaka 37 wakati wa kifo cha Mamake Sarah.
Sarah alifia Kirjath – arba (mji huu baadaye uliitwa Hebron.
• Katika panjo la Machpela walizikwa Sarah, Abraham, Isaka, Rebeka, Lea na Yakobo.
• Mibaraka ya kuwa na kiasi; Miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu, tunapaswa kulitunza
• Kuishi vizuri bila matumizi ya madawa ya kulevya, vichocheo, nk
• Afya ya jumla- maji, mazoezi na mlo;
Mwili wa Mwanadamu asilimia 75 ni maji, lakini maji hupotea tunapotoa jasho na
uchfu mwingine mwilini. Unatakiwa kunywa glass sita hadinane kwa siku. Maji
hutumika pia kusafisha mwili.
Mazoezi huongeza nguvu mwilini, yanaufanya mwili kuwa imara, huondoa
misongo (stress), huimarisha afya ya ngozi, hupunguza uwezekano wa kupata
magonjwa ya moyo na saratani. Mazoezi si jambo la kuchagua lakini ni la lazima.
Soma Mithali 6:6-13, 14:23)
• Kumbuka mavazi yetu yanatakiwa kuwa ya kawaida tu yasiyo na vikorombwezo vingi,
yawe safi na nadhifu.
MALENGO:
MALENGO:
1.Mwanafunzi ataweza kuelezea namna Yusufu alivyomtegemea Mungu katika hali zote.
11
2.Mwanafunzi atajifunza kuwa na uwezo wa kushinda majaribu kwa kumwamini na
kumtegemea Mungu.
MUHULA WA PILI
MALENGO:
12
2.Mwanafunzi ataelewa kwamba Mungu anatoa ulinzi hata tunapokuwa katika shida na
magumu ya dunia hii.
13
• Makazi katika Kaanani
• Vita wakati wa uongozi wa Yoshua
• Hotuba ya mwisho ya Yoshua na kifo chake.
MALENGO:
1.Mwanafunzi atatambua kwamba zipo nyakati Mungu anaruhusu maamuzi yetu ili
tujifunze.
2.Atafahamu kwamba Mungu anaruhusu viongozi hata wenye tabia zisizofaa kututawala.
MUHULA WA KWANZA
14
• Kisa cha Ahabu na Eliya
• Kisa cha Ahabu na Nabothi
• Kisa cha nabii Elisha
• Wafalme wengine wa Israeli na Yuda.
• Sababu za uasi
• Matokeo ya uasi
• Mpango na ahadi za Mungu kuokoa waisraeli wa kimwili na kiroho
• KUMBUKUMBU 9, YOHANA 3:16
MALENGO:
15
1.Mwanafunzi ataelewa jinsi Mungu alivyowaokoa watu wake kutoka kwa maangamizi.
16
Hila ya Hamani
Msaada wa Esta
• Hamani atundikwa/ anyongwa
• Tarumbeta za wayahudi na ukuu wa Mordekai
Jina la asili la kiebrania la Esther ni Hadasa. Mungu amemtumia msichana/binti tena mwenye
sura nzuri na jasiri kuliokoa taifa lake wakati wa zahama. Tunajifunza kwamba wanawake na
wanaume wanao wajibu au sehemu ya kufanya katika mpango wa wokovu wa watu wake.
Katika Kitabu cha Esther neno au jina Mungu halijatajwa, lakini kazi yake inaonekana. •
Mwanafunzi ataweza kuelezea historia ya kanisa tangu uumbaji hadi kanisa la masalio.
MALENGO:
Mwanafunzi ataweza kutambua kanisa la masalio katika kipindi cha kufungwa historia ya
ulimwengu.
ZOEZI:
17
MUHULA WA PILI
MALENGO:
MALENGO:
• Kifo ni nini?
• Chanzo cha kifo
• Hali ya mfu
• Mwisho wa kifo ni lini?
• Ufufuo- Lazaro afufuliwa
• Imani ya Kiafrika kabla ya Ukristo juu ya kifo na hali ya wafu
• Ufufuo wa mwisho
• 1.THESALONIKE 4:16, MATENDO 2:34, 1.KORINTHO 15:6, YOHANA 11:11-14, ZABURI
6:5,
• SDA BELIEVE FUNDISHO LA 26.
• Wanafunzi watambue kwamba kifo ni usingizi tukisubiri ufufuo. Mathayo 9:24 Wafu hawajui
neno lolote. Mhubiri 9:5
Hakuna kazi wala huduma inayofanyika makaburini na wala hawamtukuzi Mungu huko!!
Mhubiri 9:10
• Madai kwamba wafu huenda peponi ni umizimu ulioanzishwa na Shetani mwenyewe aliposema
`` Hamtakufa hakika`` Mwanzo 3:4
18
• Maandiko matakatifu yamekataza kabisa zoezi lolote lile la kujifanya unawasiliana na
wafu au ulimwengu wa roho. Yeyote yule anayejidai anawasiliana na ndugu zake
waliokufa, anawasiliana na roho za Shetani.
• Kuna fufuo mbili
(a) Ufufuo wa kwanza wa watakatifu unatokea mara Kristo anaporudi mara ya pili
(b) Ufufuo wa pili ni wale waovu ambao unatokea baada ya miaka 1000 ambao unaambatana na
hukumu.
TAKATIFU
MALENGO:
1.Mwanafunzi atafahamu kwamba kuna huduma ya patakatifu mbinguni kwa ajili yetu.
3.Mwanafunzi ataweza kuelezea jinsi huduma katika hema takatifu ilivyofanyika hapa duniani.
19
MALENGO:
2.Mwanafunzi atatambua kwamba analo jukumu la kuwaandaa wengine kwa ajili ya marejeo ya
Kristo.
Kristo anaporudi kama Mfalme wa wafalme anawachukua wateule kwenda nao mbinguni;
Wenye haki waliolala wanafufuliwa na kupaa juu mbinguni waovu wanaangamizwa na
Shetani anabaki peke yake kuzimu (bottomless pit), asipate wa kudanganya tena. Nchi/dunia
inabaki ukiwa na wakati huu watakatifu wanatawala na Kristo kule mbinguni wanapewa kazi
ya kuhukumu ulimwengu Baada ya miaka elfu watakatifu wanashuka katika Yerusalemu
mpya
MUHULA WA KWANZA
20
WIKI 3 UUMBAJI
• Uumbaji au uibukaji
• Hadithi za mapokeo kuhusu uumbaji
• Asili ya binadamu
• Maana na kusudi la uumbaji
• Uumbaji na Sayansi
• MWANZO 1, SDA BELIEVE FUNDISHO LA 6 NA 7
MALENGO:
• Mwanzo wa dhambi
• Nafasi ya Lusifa- malaika mkuu
• Jinsi dhambi ilivyoingia katika dunia yetu
• Pambano kuu
• ISAYA 14:13, UFUNUO 12:7-9, SDA BELIEVE FUNDISHO LA 8, PATRIARCHS AND
PROPHETS 34-38, PAMBANO KUU 284-290.
• Agano jipya
• Maisha, kifo na ufufuo wa Kristo
• Uzoefu wa wokovu
• SDA BELIEVE FUNDISHO LA 9 NA 10.
21
• Nuhu anaambiwa kutengeneza Safina na kuhubiri
• Ulimwengu uliharibiwa na gharika
• Nuhu aokolewa na familia yake pamoja na wanyama waliochaguliwa kutoka kila jamii ya
wanyama wenye namna moja
• Upinde wa mvua na ahadi za Mungu
• MWANZO 6-10
Abraham anaitwa kuacha nchi yake na pia kuacha familia yake na nyumba ya Baba yake, na kamwe
asirudi kwa ndugu zake hao tena damu yake. Hii ilikuwa ni jaribio kali sana.
Nchi ya Kanaani aliyoahidiwa Abraham inaunganisha Palestina, hadi Phoenicia mpaka Syria kusini.
Abraham alikuwa na umri wa miaka 75 alipotoka Haran, kwao.
22
WIKI 14 YUSUFU
23
KUTOKA 19, WAEBRANIA 8, KUTOKA 33-34, PATRIARACHS AND PROPHETS
287-295
• Uasi na adhabu
• Kufanywa upya kwa agano
MUHULA WA PILI
MALENGO:
1.Mwanafunzi ataweza kuelezea jinsi Mungu anavyoandaa viongozi kwa ajili ya watu
wake.
2. Atajua sifa nzuri za kiongozi mzuri zinazomwandaa pia kuwa kiongozi wa mfano.
24
• Samson- kuzaliwa kwake na Mungu alivyomtumia dhidi ya Wafilisti.
• Samson na mwanamke wa Timna, Samson na Delila na kifo cha Samsoni.
• Kuja kwa WAFILISTI.
• Makabila ya Yuda na Simon yateka Adonibezek, Yerusalemu na Hebron Makabila ya
Efrahim na Manasse yateka Bethel.
• WAAMUZI 1-6,8-9,11-16, 1.SAMWELI 1,2,4-8, Waamuzi 21:25
MALENGO:
• Wazazi wa Yesu
• Tangazo la kuzaliwa kwa Yesu
• (The birth of Jesus is announced; Luke 1:26-56, and Luke 2:1-52)
• Wachungaji wa kondoo na wenye hekima toka mashariki
• Kukimbilia Misri na kurudi Nazareth (The escape to Egypty and the return from Egypty)
• Maisha ya Yesu kama mtoto
• MATHAYO 1,2, TUMAINI LA VIZAZI VYOTE 21,24,28,33,41.
NYONGEZA:
Nini maana ya jina Imanuel.
Yesu alizaliwa na kukua na kuishi kama mwanadamu, akaishi na wanadamu ili
aweze kuwakomboa wanadamu wote.
Nazareth ni mji ambamo Yesu alikulia. Ni mji wa nyumbani kwa Yusufu na
Mariamu. Katika mji huu Yesu alitumia miaka yake 30 kuishi huko, hivyo watu
humwita Yesu Mnazareti.
Bethlehemu ni mji ambamo Yesu Kristo alizaliwa na matukio mengine
yaliyohusisha kuzaliwa kwake, mfano Mamajusi (Wisemen) kutoka mashariki
walitembelea/walikuja Bethlehemu, mauaji ya watoto wachanga yaliyotangazwa
na Herode (Herod the Great)
Mfalme Herode alikufa mara tu baada ya kuua watoto wachaanga kule
Bethlehemu.
4.BC WIKI
7 UBATIZO
MALENGO:
25
1.Mwanafunzi ataweza kuelezea nafasi ya Yohana Mbatizaji katika huduma ya Yesu.
• Hotuba mlimani
• Uwezo dhidi ya maradhi na pepo wachafu Uwezo wa kusamehe dhambi.
• MATHAYO 4-7, TUMAINI LA VIZAZI VYOTE 31. MATHAYO 8-9
Wasaidie wanafunzi kuzifahamu heri zote tisa na watie moyo kuwa vijana wapole,
wapatanishi, wenye moyo safi, wenye rehema, n.k
Hebu angalia uwezo wa Yesu
1. Yesu anamponya mtu mwenye ukoma kwa kumgusa
2. Yesu amponya mtumishi wa akida aliyepooza huko Kapernaumu.
3. Yesu amponya mama mkwe wa Petro aliyekuwa na homa
4. Yesu akemea upepo katika bahari akiwa na wanafunzi wake
5. Yesu atoa pepo kwa watu wawili katika nchi ya Wagerasi, pepo watoka na
kuwaingia nguruwe,wateketea baharini
6. Alitoa wengi wenye pepo na wasioweza na aliwasamehe.
26
• Dalili ya badiliko
• Dalili ya imani
• Yesu achangamana na watoza ushuru na wadhambi
• MATHAYO 9
Wanafunzi waweze kuwataja kwa majina wanafunzi wa Yesu: Simon Peter, Andrea,
Yakobo, Yohana, Filipo, Bartholomayo, Tomaso, Mathayo,, Yakobo wa Alfayo,
Thadayo, Simon Mkananayo, na Yuda Isakariote.
MALENGO:
1.Mwanafunzi atafahamu kwamba Yesu anao uwezo wa kutenda miujiza hata leo
MALENGO:
27
1.Mwanafunzi ataweza kufahamu mafundisho na imani za Mafarisayo na Masadukayo na
jinsi walivyotofautiana.
MALENGO:
• Ndoa ya kwanza
• Ndoa leo zikoje
• Ndoa ya wake wengi, sababu yake ni nini
• Uasherati na uzinzi
• Ndoa katika mtazamo wa kiafrika
• SDA BELIEVE FUNDISHO LA 23, MWANZO 2:18-25.
Maswali: Taja mtu wa kwanza kuoa wake zaidi ya mmoja- Lameki (Ada na Sila).
Vijana wanapaswa kuja kwamba Mungu anachukia Uasherati na Uzinzi, Hii ni sababu
mojawapo iliyosababisha Mungu akachukia na kupunguza umri wa wanadamu kuishi hapa
duniani; soma Mwanzo 6:1-3.
ANGALIA KIAMBATANISHO B
28
KIDATO CHA NNE
MUHULA WA KWANZA
WIKI 1 FAMILIA
• Maana ya Kibiblia
• Jukumu la baba,mama,na watoto
• Familia katika mtazamo wa kiafrika
• SDA BELIEVE FUNDISHO LA 23, EDUCATION UK 20.
• Ombi la mama
• Uponyaji wa watu wawili vipofu
• Kuingia Yerusalemu kwa ushindi
• Kutakasa hekalu
• Mtini uliolaaniwa
• Mamlaka ya Yesu yatiliwa shaka
• Mpangaji mwovu
• MATHAYO 20,21
• Vazi la harusi
• Kodi kwa kaisari
• Kuwanyamazisha masadukayo
• Changamoto- Kristo ni mwana wa nani?
• Masuto
• Ole saba: Taja ole Saba.
• MATHAYO 22 NA 23
• Dalili za mwisho
• Hekalu labomolewa
• Kuja kwa Mwana wa Adamu
• Kuja mara ya pili kwa Kristo
29
• SDA BELIEVE FUNDISHO LA 25.
WIKI 6 : UWAJIBIKAJI
• Bwana Harusi
• Hukumu
• Wanawali kumi
• Talanta
• Kondoo na mbuzi
• MATHAYO 25
WA KIKRISTO MALENGO:
2.Atajifunza kufanya maandalizi kwa ajili ya kumkaribisha Roho Mtakatifu katika maisha
yake.
30
• Roho mtakatifu aja siku ya Pentekosti;
• Petro ahutubia kusanyiko
• Ushirika wa waumini(fellowship)
31
•
• MATENDO 2 NA 3.
• Mitume wateswa
• Saba wachaguliwa
• Stefano akamatwa
• Hotuba ya Stefano mbele ya Sanhedrin
• Stefano apigwa mawe
• Mathayo alikufa kwa kuuawa na upanga mbali kidogo na mji wa Ethiopia • Marko alifia
Alexandria baada ya kukokotwa kikatili kwenye barabara za mji.
• Luka alitundikwa juu ya mti wa mizeituni nchini Ugiriki
• Yohana alitiwa katika pipa la mafuta lichemkalo lakini kwa muujiza wa Bwana hakufa,
baadae akapelekwa katika kisiwa cha Patmo ileafie huko, hakufa. Baadae alikuwa akiwa
mzee tu wa siku.
• Petro alisulibiwa Rumi kichwa chini miguu juu
• Yakobo wa Zebedayo alikatwa kichwa huko Jerusalemu
• Yakobo wa Alfayo alitupwa toka kwenye kinara kirefu cha kanisa halafu akapigwa rungu
lenye msumari hadi akafa
• Batholomayo alichunwa ngozi akiwa hai, hadi kufa
• Andrea alifungwa kwenye msalaba hadi akafa
32
•
33
•
MUHULA WA PILI
Kijana Timotheo alitoka katika wilaya ya Derbe-Listra (Lystra). Maana ya jina hili ni
“aliyeheshimiwa na Mungu”. Alikuwa na umri kati ya miaka 18-20. Ni kijana ambaye
alikuwa tayari kukabiliana na changamoto mbalimbali za maisha na utume na akamruhusu
Kristo amtumie. Mama yake aliitwa Yunisi (Eunice).
Vijana wana nafasi ya kumtumikia Mungu pia, Mfano mzuri ni Timotheo.
SWALI; Ni nini kilisababisha Paulo na Sila watupwe gerezani huko Filipi? Baada ya
kumtoa kijakazi mmoja pepo ambaye kupitia kwa mapepo hayo alitengeneza faida
nyingi kwa ajili ya familia yake, waliona wamepata hasara.
• MATENDO 16
34
WIKI 5-6 KAZI YA INJILI HUKO THESALONIKE
• Bera, Ikonia, Prisila, Akila, Apolo, na Athene Paulo katika Efeso na fujo kutokea.
• MATENDO 17-19
Paulo akiwa Thesalonike aliingia katika sinagogi la Wayahudi na kufundishana nao neno la
Mungu Sabato tatu; mafungu haya yanaonyesha kwamba Mitume waliendelea kuitunza
Sabato. Tatizo walilokumbana nalo hawa mitume ni kuhubiri habari za Yesu, tena kama
Mfalme.
Paulo alipofika Athene- Ugiriki alichukia sana kuona masanamu, Hii inatupa picha kuwa
Ibada ya kuabudu sanamu ilikuwepo hata wakati wa Yesu na mitume; wanaabudu mungu
asiyejulikana.
MALENGO:
• Kushuhudia
• Muda na uwezo
• Zaka na sadaka
• Matumizi ya zaka
• Mibaraka ya uwakili
• SDA BELIEVE FUNDISHO LA 21
35
• MATENDO 23-26
36
MATHAYO 13, LUKE 10:38-42, LUKE 18:1-14, LUKA 19.
REJEA
37